7
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU
أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَسَالَتْ أَوْدِيَةٌ بِقَدَرِهَا فَاحْتَمَلَ السَّيْلُ زَبَدًا رَّابِيًا وَمِمَّا يُوقِدُونَ عَلَيْهِ فِي النَّارِ ابْتِغَاءَ حِلْيَةٍ أَوْ مَتَاعٍ زَبَدٌ مِّثْلُهُ كَذَٰلِكَ يَضْرِبُ اللَّـهُ الْحَقَّ وَالْبَاطِلَ فَأَمَّا الزَّبَدُ فَيَذْهَبُ جُفَاءً وَأَمَّا مَا يَنفَعُ النَّاسَ فَيَمْكُثُ فِي الْأَرْضِ كَذَٰلِكَ يَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ ﴿١٧﴾
17. Ameteremsha maji kutoka mbinguni na mabonde yakamiminika maji kwa kadiri yake na mvo ukachukua mapovu yaliyokusanyika juu yake. Na katika vile wanavyoyeyusha katika moto kwa kutaka mapambo au vyombo vingine hutokea povu mfano wake. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyopiga mfano wa haki na batili, Ama povu linakwenda bure; ama kinachowafaa watu hukaa kwenye ardhi, Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyopiga mifano.
لِلَّذِينَ اسْتَجَابُوا لِرَبِّهِمُ الْحُسْنَىٰ وَالَّذِينَ لَمْ يَسْتَجِيبُوا لَهُ لَوْ أَنَّ لَهُم مَّا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ مَعَهُ لَافْتَدَوْا بِهِ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ سُوءُ الْحِسَابِ وَمَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿١٨﴾
18. Waliomwitikia Mola wao watapata wema na wasiomwitikia, hata wange-likuwa na vilivyomo ardhini vyote na mfano wake, hakika wangelivitoa kujikombolea. Hao wana hisabu mbaya kabisa na makao yao ni Jahannam, na hapo ni mahali pabaya mno.
Aya 17-18
Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amefananisha baina ya mumin na kafir, akapiga mifano miwili: Kwanza, baina ya kipofu na mwenye kuona - kumfananisha kafiri na upofu na mumin na kuona. Pili, baina ya giza na nuru - kumfananisha kafiri na giza na mumin na nuru.
Katika Aya tuliyo nayo hivi sasa, amefananisha haki na batili akaleta mifano miwili vile vile: Kwanza, baina ya maji yanayokaa ardhini na kuwapatia watu heri na uhai. Pili, mapovu ambayo yanashuka kwenye maji kisha yanachukuliwa na mumbu na kwenda na upepo. Amefananisha haki na maji yenye kunufaisha, na batili akifananisha na mapovu yasiyokaa. Haya ndiyo aliyoyakusudia Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliposema:
Ameteremsha maji kutoka mbinguni na mabonde yakamiminika maji kwa kadiri yake na mvo ukachukua mapovu yaliyokusanyika juu yake.
Makusudio ya kadiri yake ni kwamba kila bonde linachukua maji ya mvua kwa kiasi chake cha upana na kina yanayozidi yanaminika kwengine.
Ama mfano mwingine wa haki na batili alioufananisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni madini yanayoyeyushwa motoni ili yatengenezwe vipambo kama dhahabu na fedha au vifaa kama chuma risasi na shaba na povu linazimika kwenye madini yaliyoyeshwa ambayo yanapotea; kama yanavy- opotea mapovu yanayochukuliwa na mvo. Kwa hiyo haki ni kama myeyuko wa madini ulio na manufaa na batili ni povu linalotokana na myeyuko ambalo halina manufaa. Hiyo ndiyo maana ya kauli yake:
Na katika vile wanavyoyeyusha katika moto kwa kutaka mapambo au vyombo vingine hutokea povu mfano wake.
Yaani kwenye madini pia hutokea povu lisilokuwa na manufaa sawa na povu la mvo.
Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyopiga mfano wa haki na batili.
Yaani Mwenyezi Mungu analeta mfano na picha ya haki kwa ubainifu kati- ka picha ya maji na madini ambayo hupatiwa manufaa na batili katika picha ya povu lisilokuwa na manufaa.
Ama povu ambalo linachukuliwa na mvo au kuzimika kwenye madini yanapoyeyeshwalinakwenda bure bila ya manufaa.
Ama kinachowafaa watu hukaa kwenye ardhi nayo ni maji na madini hukaa ardhini kwa ajili ya heri na uhai
Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyopiga mifano ya haki na batili na mingineyo.
Mara nyingi maana yanakuwa magumu kufahamika na watu wengi. Mifano ni nyenzo nzuri ya kufafanua na kuweka wazi, mbali ya kuwa mfano unaongezea uzuri wa ubainifu.
Mwenyezi Mungu amepiga mifano mingi katika Aya nyingi za ubainifu; kama vile ukafiri na imani kuupigia mfano wa giza na nuru au upofu na uoni. Vile vile mfano wa haki, katika Aya hii, kwa maji na madini, na wa batili kuwa povu.
Aya hii inaleta picha halisi ya Uislamu, Au kwa ufasaha zaidi, inaleta picha ya Mwislamu wa kweli, kuwa ni yule ambye watu wananufaika naye kwa manufaa yenye kudumu; sawa na yule aliyeihuisha ardhi baada ya kufa; na kama madini magumu yanayojengewa viwanda na viwanda vinazalisha zana na vifaa mbali mbali na kuleta maendeleo, vya mbali vikaletwa karibu. Kukawa na majeshi, wakatembea angani, ardhi ikalimwa na dunia ikajaa heri, amani na raha.
Natija ya hayo ni kwamba kila mwenye kunufaisha, akaleta utengeneo na katenda kwa ajili ya maisha ya binadamu mwenzake awe na uhuru, amani na raha, hakika mtu huyo atakuwa kwenye malengo ya Uislam, hata kama si Mwislamu. Kwa sababu yeye ni sawa na madini aliyoyatolea mfano wa haki Mwenyezi Mungu. Na kwamba kila mwenye kutenda kwa ajili ya uovu wa mtu. Yeye hana uislamu kitu, hata kama atafunga maisha na kuunganisha swala za usiku na alfajiri.
Waliomwitikia Mola wao watapata wema.
Yaani watapata wema kwa sababu ya kumwitikia Mola wao kwenye mwito wa kutenda kwa ajili ya manufaa ya watu na kwa ajili ya maisha bora. Ama makusudio ya wema ni ujira na thawabu na kwamba watu wa haki watanufaisha, kama maji yanavyonufaisha ardhi.
Na wasiomwitikia - nao ni wale wasiokuwa na maana, kama mapovu-hata wangelikuwa na vilivyomo ardhini vyote na mfano wake, hakika wangelivitoa kujikombolea. Hao wana hisabu mbaya kabisa na makao yao ni Jahannam, na hapo ni mahali pabaya mno.
Umetangulia mfano wake katika Juz.3 (3:91) na Juz,11(10:54).
أَفَمَن يَعْلَمُ أَنَّمَا أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ الْحَقُّ كَمَنْ هُوَ أَعْمَىٰ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿١٩﴾
19. Je, anayejua kwamba yaliyoteremshwa kutoka kwa Mola wako ni haki, ni sawa na aliye kipofu? Wanaozingatia ni wenye akili tu.
الَّذِينَ يُوفُونَ بِعَهْدِ اللَّـهِ وَلَا يَنقُضُونَ الْمِيثَاقَ ﴿٢٠﴾
20. Wale ambao wanatimiza ahadi ya Mwenyezi Mungu wala hawavunji maagano.
وَالَّذِينَ يَصِلُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيَخْشَوْنَ رَبَّهُمْ وَيَخَافُونَ سُوءَ الْحِسَابِ ﴿٢١﴾
21. Na wale ambao huyaunga aliyoamrisha Mwenyezi Mungu yaungwe na humwogopa Mola wao na huihofu hisabu mbaya.
وَالَّذِينَ صَبَرُوا ابْتِغَاءَ وَجْهِ رَبِّهِمْ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً وَيَدْرَءُونَ بِالْحَسَنَةِ السَّيِّئَةَ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عُقْبَى الدَّارِ ﴿٢٢﴾
22. Na ambao husubiri kwa kutaka radhi ya Mola wao na wakasimamisha Swala na wakatoa kwa siri na kwa uwazi katika vile tulivyowaruzuku na wakayaondoa maovu kwa wema, Hao ndio watakaopata malipo ya nyumba.
جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا وَمَن صَلَحَ مِنْ آبَائِهِمْ وَأَزْوَاجِهِمْ وَذُرِّيَّاتِهِمْ وَالْمَلَائِكَةُ يَدْخُلُونَ عَلَيْهِم مِّن كُلِّ بَابٍ ﴿٢٣﴾
23. Nayo ni Bustani (Pepo) za Milele wataziingia wao na walio wema miongoni mwa baba zao wake zao na vizazi vyao, Na Malaika wanawaingilia kila mlango.
سَلَامٌ عَلَيْكُم بِمَا صَبَرْتُمْ فَنِعْمَ عُقْبَى الدَّارِ ﴿٢٤﴾
24. (wakisema): Assalaam alaykum kwa sababu ya mlivyosubiri. Basi ni mema mno malipo ya nyumba.
وَالَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهْدَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مِيثَاقِهِ وَيَقْطَعُونَ مَا أَمَرَ اللَّـهُ بِهِ أَن يُوصَلَ وَيُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ أُولَـٰئِكَ لَهُمُ اللَّعْنَةُ وَلَهُمْ سُوءُ الدَّارِ ﴿٢٥﴾
25. Na wale wanaovunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kuifunga na wanakata aliyoamrisha Mwenyezi Mungu yaungwe na wanafanya ufisadi katika nchi. Hao ndio walio na laana na wana nyumba mbaya.
YALIYOTEREMSHWA KUTOKA KWA MOLA WAKO NI HAKI
Aya 19-25
Je, anayejua kwamba yaliyoteremshwa kutoka kwa Mola wako ni haki, ni sawa na aliye kipofu? wanaozingatia ni wenye akili tu.
Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kufananisha ukafiri na upofu, tena akafananisha haki kwa maji na batili kwa povu, sasa anafananisha mwenye kumwamini Muhammad na kuona na mwenye kumkana kwa upofu.
Mwenyezi Mungu ameeleza uhakika huu kwa njia ya swali ili kumsuta na kumtahayariza.
Wanaozingatia ni wenye akili tu wanasikiliza sauti kwa akili na yule asiyetia akilini isipokuwa yanayoafiki hawaa yake, ni sawa na asiye na akili.
Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja sifa za wenye akili ambazo zinafahamisha makusudio ya wenye akili kuwa ni waumini wenye takua; kama ifuatavyo:
1.Wale ambao wanatimiza ahadi ya Mwenyezi Mungu.
Kila lililo na dalili basi hilo ni ahadi ya Mwenyezi Mungu na ni juu ya binadamu kutekeleza, lakini maibilisi wanapotosha uhakika kwa mapenzi yao kisha wananasibisha hawa zao hizi za kishetani kwa Mwenyezi Mungu na haki. Mwenyezi Mungu ametakata na yale wanayomzushia.
Wala hawavunji maagano, Hii ni kutilia mkazo kauli yake ‘wanatimiza’ ambapo wanalazimiana na utekelezaji ahadi bila ya kuvunja.
2.Na wale ambao huyaunga aliyoamrisha Mwenyezi Mungu yaungwe.
Wafasiri wametaja kauli kadhaa katika kufasiri aliyoamrisha Mwenyezi Mungu yaungwe, Kauli iliyo karibu zaidi ya roho ya Uislamu na misingi yake, ni ile ya yule aliyesema: Makusudio ya aliyoamrisha yaungwe, ni msaada wa mtu kwa nduguye mtu, kusaidiana naye kuondoa madhara na kuleta manufaa kwa karibu au mbali.
3.Na humwogopa Mola wao na huihofu hisabu mbaya kimatendo sio kinadharia na kimaneno. Imam Ali anasema: “Mambo mema yanafahami- ka kwa imani na imani inafahamika kwa mambo mema.”
4.Na ambao husubiri kwa kutaka radhi ya Mola wao. Wanapigana jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanavumilia majeraha na maumivu; hawataki malipo wala shukrani isipokuwa radhi ya Mwenyezi Mungu peke yake.
5.Na wakasimamisha Swala ambayo mwanzo wake ni Takbira ihram: Mungu ni mkubwa zaidi (Allahu akbar) hakuna mkubwa zaidi yake vyovyote atakavyo kuwa. Na Mwisho wake swala ni Tahlil na Salaam: Hakuna Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu (lailalaha illallah) Hakuna anayeabudiwa isipokuwa Yeye; hakuna mali wala jaha au hisabu zinazoweza kuabudiwa wala hakuna nguvu inayonyenyekewa isipokuwa nguvu yake Mwenyezi Mungu pekee yake bila ya kuwa na mshirika.
6.Na wakatoa kwa siri na kwa uwazi katika vile tulivyowaruzuku, Mali ndiyo ugomvi. Angalia tulivyoielezea katika mwanzo wa Juz.4 (3:92).
7.Na wakayaondoa maovu kwa wema, Hao ndio watakaopata malipo ya nyumba.
Makusudio ya wema hapa ni msamaha na uovu ni haki maalum inayokuwa baina ya wawili; kama kisasi. Mwenyezi Mungu anasema: “Mmeandikiwa kisasi katika waliouawa; muungwana kwa muungwana na mtumwa kwa mtumwa na mwanamke kwa mwanamke, Na anayesamehewa na ndugu yake chochote, basi ni kufuatana kwa wema na kulipa kwa ihsani.” Juz.2 (2:178)
Ama haki ya Mwenyezi Haina kusameheana,
وَلَا تَأْخُذْكُم بِهِمَا رَأْفَةٌ فِي دِينِ اللَّـهِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّـهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ﴿٢﴾
“Wala isiwashike kwa ajili yao huruma katika hukumu ya Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi mnamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho.” (24:2).
Nayo ni Bustani (Pepo) za Milele wataziingia wao na walio wema miongoni mwa baba zao wake zao na vizazi vyao.
Wema wote wataingia peponi, Iwapo duniani walikuwa na udugu na upenzi basi furaha itazidi kwa kuunganishwa tena na kukumbuka enzi zao walipokuwa duniani. Iwapo matendo yao yatatofautiana, basi udugu na urafiki utakatika siku hiyo:
فَرِيقٌ فِي الْجَنَّةِ وَفَرِيقٌ فِي السَّعِيرِ ﴿٧﴾
Kundi moja litakuwa Peponi na kundi jingine litakuwa Motoni. (42:7).
Na Malaika wanawaingilia kila mlango (wakisema): Assalaam alaykum kwa sababu ya mlivyosubiri. Basi ni mema mno malipo ya nyumba.
Maana ya Assalaamu alykum! Ni: Amani iwe juu yenu. Kauli yake Mwenyezi Mungu kwa sababu ya mlivyosubiri, inaashiria kwamba Pepo ni haramu isipokuwa kwa mwenye kufanya jihadi akasubiri, akavumilia tabu na mashaka ya jihadi, Imam Ali(a.s) anasema:“Pepo imezungukwa na machukivu na moto umezungukwa na matamanio. Na jueni kuwa hakuna yeyote anayemtii Mwenyezi Mungu ila hujiwa na machukivu,Na hakuna yeyote aliyemwasi Mwenyezi mungu ila hujiwa na matamanio.”
Na wale wanaovunja ahadi ya Mwenyezi Mungu baada ya kuifunga.
Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwataja wema na sifa zao na malipo mema aliyowaandalia, sasa anawataja wafisadi. Kwa ibara ya kuunganisha ni kuwa baada ya kutaja wanamapinduzi dhidi ya ufisadi anataja wapinzani wao.
Ni kawaida makundi mawili hayo kupingana, Watenda mema hutekeleza ahadi ya Mwenyezi Mungu, wakatenda kulingana na akili na dhamiri na kila linalofahamishwa na dalili. Wafisadi wanavunja ahadi yake Mwenyezi Mungu na hutenda kulingana na mawazo ya kishetani wakiichanganya haki na batili na wakiificha haki na hali wanajua
Na wanakata aliyoamrisha Mwenyezi Mungu yaungwe.
Wanawatawalisha mataghuti wakosaji na kuwasaidia kuwakandamiza watu wema kinyume na aliyoamrisha Mwenyezi Mungu na kuyakataza.
Na wanafanya ufisadi katika nchi kwa kuidhihirisha dhulma na kuleta fitina vurugu, kuwapoteza wasio na hatia, kuleta utengano, kuleta maangamizi na kila aina ya ufisadi na upotevu.
Hao ndio walio na laana na wana nyumba mbaya.
Ikiwa matendo yao ni kinyume cha watendao mema, basi vile vile ni kawaida malipo yao yawe tofauti. Wema watapata pepo na nyumba yenye neema na waovu watapata Jahannam na mahali pabaya.
اللَّـهُ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ وَفَرِحُوا بِالْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَمَا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا فِي الْآخِرَةِ إِلَّا مَتَاعٌ ﴿٢٦﴾
26. Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na humkunjia. Wamefurahia maisha ya dunia na maisha ya dunia kwa kulingana na Akhera si kitu ila ni starehe.
وَيَقُولُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْهِ آيَةٌ مِّن رَّبِّهِ قُلْ إِنَّ اللَّـهَ يُضِلُّ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي إِلَيْهِ مَنْ أَنَابَ ﴿٢٧﴾
27. Na husema wale ambao wamekufuru: “Kwa nini hakuteremshiwa Ishara kutoka kwa Mola wake?” Sema: Mwenyezi Mungu humpoteza amtakaye na humuongoza anayeelekea kwake.
الَّذِينَ آمَنُوا وَتَطْمَئِنُّ قُلُوبُهُم بِذِكْرِ اللَّـهِ أَلَا بِذِكْرِ اللَّـهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ ﴿٢٨﴾
28. Wale ambao wameamini na zikatua nyoyo zao kwa kumdhukuru Mwenyezi Mungu. Ehe! Kwa kumdhukuru Mwenyezi Mungu nyoyo zinatua.
الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ طُوبَىٰ لَهُمْ وَحُسْنُ مَآبٍ ﴿٢٩﴾
29. Wale ambao wameamini na wakafanya matendo mema, raha ni yao na marejeo mazuri.
Aya 26-29
Katika Juz.6 (5:66) Tumelielezea suala hili. Pia katika Juz, 7 (5:100), tumefafanua zaidi katika kifungu ‘Je riziki ni bahati au majaliwa’ Hivi sasa tunarudia maudhui haya kwa mfumo mwingine kwa kuangalia umuhimu wake.
Mtu ana sifa nyingi, zikiwemo za kidhati na ulazima anazokuwa nazo bila ya kubanduka; kwa mfano kuwa mrefu au mfupi kuwa ni mtoto wa tajiri au fukara. Nyingine, sio za dhati ni za kutafuta; mfano kuwa mkulima, mfanyabiashara, tabibu au mwajiriwa n.k.
Utajiri nao una sababu zake; zikiwemo nasabu; yaani urithi, Huo unatambuliwa na kukubaliwa na dini, hata kama haukupatikana kwa jasho. Sababu nyingine ni ulanguzi na unyang’anyi; kama vile riba, ghushi, wizi, biashara ya haramu n.k. Huu ni haramu, hilo halina shaka. Sababu nyingine ya utajiri ni jasho la mtu na bidii; kama vile ukulima, viwanda n.k. Sababu hii ndio bora zaidi kiakili na kisharia.
Kwa hiyo basi, inatubainikia kuwa ufukara na utajiri unatokana na sanaa ya ardhini sio ya mbinguni. Lakini wako wanaotoka nje ya hayo na kuziita sababu za hayo kuwa ni tawfiki ya Mungu, wengine wakaita bahati, lakini hakuna hata mmoja wao anayethubutu kusema kuwa kadhaa na kadari inaingilia juhudi za mtu na kazi yake na kwamba inawaunga mkono wengine kwa kuwasaidia na kuwaacha wengine. Hakuna anayeweza kuthibitisha hilo. Vinginevyo ingelikuwa sababu zote ni bure tu, na kufanya kazi kungelikuwa ni maneno tu yasiyokuwa na maana.
Unaweza kuuliza : Kauli yako hii si inapingana na kauli ya Mwenyezi Mungu.
Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na humkunjia.
Jibu : Maisha ya watu yako makundi mawili: kuna wale walio na riziki pana na wale walio na riziki finyu. Kila moja kati ya utajiri na ufukara unatokana na sababu zake maalum ambazo tumekwisha zidokeza. Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na humkunjia’ ni wasifu na kuelezea hali halisi ya watu; kana kwamba anasema watu ni makundi mawili mafukara na matajiri. Mwenyezi Mungu ameutegemeza ufukara na utajiri kwake ili kutanabahisha kuwa Yeye mtukufu ndiye muumba wa ulimwengu ambao una tabu na raha.
Ikiwa mtu atasema kwa nini basi Mwenyezi Mungu asingeumba ulimwengu usiokuwa na dhiki?
Majibu yake yako kwenye Juz, 5 (4:78), ‘Kifungu cha Haiwezekani kuongeza zaidi ya ilivyo’
Wamefurahia maisha ya dunia na maisha ya dunia kwa kulingana na Akhera si kitu ila ni starehe.
Mfano wa Aya hii umekwishapita mara nyingi, ikiwemo ile ya Juz.4 (3:185). Kuongezea na tuliyoyazungumza huko, ni kwamba kuna aina ya watu wanafurahia mali kwa sababu inasitiri aibu yao na uovu wao. Wengi katika wao hawaoni kitu isipokuwa kwenye mali na utajiri. Ni maarufu kwa wamarekani kwamba wao hawaangalii kitu chochote ila kupitia dola (pesa). Hicho ndicho kipimo cha hadhi ya mtu, hata wataalamu na wenye vipaji, thamani yao ni vile vilivyo katika mifuko yao sio vilivyo vichwani mwao.
Na husema wale ambao wamekufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Ishara kutoka kwa Mola wake?.
Umepita mfano wake katika Juz,1 (2: 118), Juz. 7 (6:37), Juz,11 (10:20) na kwa herufi zake hizihizi katika Juzu na sura hii tunayoendela nayo Aya 7.
Sema: Mwenyezi Mungu humpoteza amtakaye na humuongoa anayeelekea kwake.
Angalia kifungu cha ‘Uongofu na upotevu’ kwenye Juz,1 (2: 26) na kifungu ‘Upotevu’ katika Juz.5 (4:88).
Wale ambao wameamini na zikatua nyoyo zao kwa kumdhukuru Mwenyezi Mungu. Ehe! Kwa kumdhukuru Mwenyezi Mungu nyoyo zinatua.
Mwenyezi Mungu (s.w.t) alipotaja watu wa mali na furaha yao inayotokana na kutulizana kwao kwenye maisha yao, anawataja waumini kwamba ni wale wanaotulizana kwa dhikri ya Mwenyezi Mungu. Kutua au kutulizana moyo maana yake ni kuzidi asili ya imani; yaani uthabiti wa imani na utulivu wake. Kuna Aya inayosema:
قَالَ أَوَلَمْ تُؤْمِن قَالَ بَلَىٰ وَلَـٰكِن لِّيَطْمَئِنَّ قَلْبِي ﴿٢٦٠﴾
“(Mwenyezi Mungu) akasema: Huamini? Akasema: Kwa nini! (naami-ni) Lakini upate kutulia moyo wangu.” Juz. 3 (2:260)
وَقَلْبُهُ مُطْمَئِنٌّ بِالْإِيمَانِ ﴿١٠٦﴾
Na hali ya kuwa moyo wake umetulia juu ya imani (16:106).
Makusudio ya Dhikr sio kutamka maneno tu; isipokuwa ni dhikri ambayo inamzidisha yakini ya Mwenyezi Mungu yule mwenye kudhukuru na akawa ana mategemeo ya ahadi na miadi yake Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo dhikri ya matamshi tu na tasbihi sio dhikr ya kiuhakika. Dhikri inayozidisha yakini ni ile aliyoisema Mwenyezi Mungu:
فَاذْكُرُونِي أَذْكُرْكُمْ ﴿١٥٢﴾
Basi nidhukuruni nitawadhukuru Juz 2 (2:152).
Wale ambao wameamini na wakafanya matendo mema, raha ni yao na marejeo mazuri.
Makusudio ya raha ni Pepo. Aya hii inaoana na ile isemayo:
وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ ﴿٢٥﴾
Wabashirie wale walioamini na wakafanya vitendo vizuri, kwamba watapata mabustani yapitayo mito chini yake Juz.1 (2:25).