11%

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

وَلَئِن شِئْنَا لَنَذْهَبَنَّ بِالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ ثُمَّ لَا تَجِدُ لَكَ بِهِ عَلَيْنَا وَكِيلًا ﴿٨٦﴾

86. Na tungelipenda, tungeliyaondoa tuliyokupa wahyi; kisha usingelipata wakili wa haya juu yetu.

إِلَّا رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ إِنَّ فَضْلَهُ كَانَ عَلَيْكَ كَبِيرًا ﴿٨٧﴾

87. Isipokuwa rehema itokayo kwa Mola wako. Hakika fadhila yake kwako ni kubwa.

قُل لَّئِنِ اجْتَمَعَتِ الْإِنسُ وَالْجِنُّ عَلَىٰ أَن يَأْتُوا بِمِثْلِ هَـٰذَا الْقُرْآنِ لَا يَأْتُونَ بِمِثْلِهِ وَلَوْ كَانَ بَعْضُهُمْ لِبَعْضٍ ظَهِيرًا ﴿٨٨﴾

88. Sema: Lau wangelikusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur’an, basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao.

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا لِلنَّاسِ فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ مِن كُلِّ مَثَلٍ فَأَبَىٰ أَكْثَرُ النَّاسِ إِلَّا كُفُورًا ﴿٨٩﴾

89. Na hakika tumewaeleza watu katika hii Qur’an kwa kila mfano, lakini watu wengi wamekataa isipokuwa kukanusha tu.

TUNGELIPENDA TUNGELIONDOA

Aya 86- 89

MAANA

Na tungelipenda, tungeliyaondoa tuliyokupa wahyi.

Razi anasema, katika kufasiri Aya hii, kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) baada ya kubainisha, katika Aya iliyotangulia, kuwa yeye amewapa elimu kidogo tu, hapa anabainisha kwamba yeye lau angelitaka kuwaondolea hiki kidogo, angeliweza, Na hilo ni kwa kufuta kuhifadhika kwake moyoni na maandishi yake ya vitabuni.

Kisha usingelipata wakili wa haya juu yetu, utakayemtegemea akutetee kukurudishia tulichokichukua kwako.Isipokuwa rehema itokayo kwa Mola wako ; Hiyo pekee ndiyo inayoweza kukurudishia ambacho tungekichukua kwako.

Hakika fadhila yake kwako ni kubwa kutokana na elimu aliyokupa na ubwana juu ya watu wote.

Sema: lau wangelikusanyika watu na majini ili walete mfano wa hii Qur’an, basi hawaleti mfano wake, hata wakisaidiana wao kwa wao.

Umepita mfano wake katika Juz 1 (2: 23).

Hakika tumewaeleza watu katika hii Qur’an kwa kila mfano, katika yanayohusiana na itikadi, sharia na maadili. Na tukaweka hoja mkataa na dalili wazi, lakini watu wengi wamekataa isipokuwa kukanusha tu, na kuwa mbali na haki. Kwa sababu iko chungu na ni nzito, hawawezi kuivumilia isipokuwa wenye takua.

وَقَالُوا لَن نُّؤْمِنَ لَكَ حَتَّىٰ تَفْجُرَ لَنَا مِنَ الْأَرْضِ يَنبُوعًا ﴿٩٠﴾

90. Na walisema: hatutakuamini mpaka utuchimbulie katika ardhi hii chemchemi.

أَوْ تَكُونَ لَكَ جَنَّةٌ مِّن نَّخِيلٍ وَعِنَبٍ فَتُفَجِّرَ الْأَنْهَارَ خِلَالَهَا تَفْجِيرًا ﴿٩١﴾

91. Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu na utupitishie mito kati yake ikimiminika.

أَوْ تُسْقِطَ السَّمَاءَ كَمَا زَعَمْتَ عَلَيْنَا كِسَفًا أَوْ تَأْتِيَ بِاللَّـهِ وَالْمَلَائِكَةِ قَبِيلًا ﴿٩٢﴾

92. Au utuangushie mbingu vipande vipande, kama ulivyodai, au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika ana kwa ana.

أَوْ يَكُونَ لَكَ بَيْتٌ مِّن زُخْرُفٍ أَوْ تَرْقَىٰ فِي السَّمَاءِ وَلَن نُّؤْمِنَ لِرُقِيِّكَ حَتَّىٰ تُنَزِّلَ عَلَيْنَا كِتَابًا نَّقْرَؤُهُ قُلْ سُبْحَانَ رَبِّي هَلْ كُنتُ إِلَّا بَشَرًا رَّسُولًا ﴿٩٣﴾

93. Au uwe na nyumba ya dhahabu au upae mbinguni, Na hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie Kitabu tukisome. Sema: ametakasika Mola wangu! Kwani mimi ni nani, isipokuwa ni mwanadamu Mtume?

وَمَا مَنَعَ النَّاسَ أَن يُؤْمِنُوا إِذْ جَاءَهُمُ الْهُدَىٰ إِلَّا أَن قَالُوا أَبَعَثَ اللَّـهُ بَشَرًا رَّسُولًا ﴿٩٤﴾

94. Na nini kilichowazuia watu kuamini ulipowajia utume, isipokuwa walisema: je, Mwenyezi Mungu hupeleka mwanadamu kuwa Mtume?

قُل لَّوْ كَانَ فِي الْأَرْضِ مَلَائِكَةٌ يَمْشُونَ مُطْمَئِنِّينَ لَنَزَّلْنَا عَلَيْهِم مِّنَ السَّمَاءِ مَلَكًا رَّسُولًا ﴿٩٥﴾

95. Sema: Lau ingelikuwa duniani kuna Malaika wanaotembea kwa utulivu, basi bila ya shaka tungeliwateremshia Malaika kuwa Mtume wao.

قُلْ كَفَىٰ بِاللَّـهِ شَهِيدًا بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ إِنَّهُ كَانَ بِعِبَادِهِ خَبِيرًا بَصِيرًا ﴿٩٦﴾

96. Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi. Hakika Yeye anawajua vyema waja wake na anawaona.

KUFIKIRIA MALI

Aya 90-96

KUJIPENDA

Kila mmoja wetu anajipenda; awe mwana mume au mwanamke, mzee au mtoto, mwenye takua au muovu n.k. Ni binadamu gani asiyekuwa na shauku na maisha yake na kutetea heshima yake na uhalisi wake? Lau si hivyo uhai usingeendelea kuwako wala tusingeendelea, Hakuna tofauti katika kujipenda huko baina ya watu; isipokuwa tofauti iko katika aina zifutazo:-

Kuna yule anayekuwa kwenye msingi wa maumbile na akili. Hili linafa- hamika kutokana na jinsi mtu anavyoheshimu haki za wengine, kutosheka na alichoandikiwa kilichotokana na jasho lake na kusaidiana na kila mwenye kutumai kheri na manufaa ya watu kwa namna moja au nyingine; bali hata kujitolea juu ya hilo.

Kwani mwenye kutoa na kujitolea kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, atakuwa amejipenda, atake asitake, kwa sababu Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa mwenye kufanya wema, vile vile jamii inamsifu na kumtukuza yule mwenye kujitolea kwa ajili ya hiyo jamii.

Na kuna yule anayejipenda kwa kutumia yale yanayopituka akili, dini na uhalisi. Hili linafahamika kutokana na tamaa ya mtu ambaye haioni umuhimu wala manufaa ya mwingine isipokuwa wake.

Hili halikubaliki na mantiki yoyote; hata ya yahisia na ya kuonekana; sawa na alivyosema Mwenyezi Mungu: “Wana nyonyo, lakini hawafahamu kwazo, na wana macho, lakini hawaoni kwayo, na wanayo masikio, lakini hawasikii kwayo. Hao ni kama wanyama bali wao ni wapotevu zaidi, Hao ndio walioghafilika.” Juz; 9 (7: 179). Hawa wako kila mahali na kila wakati; miongoni mwao ni wale aliowaashira Mwenyezi Mungu kwa kuli zake zifuatazo:-

1. Na walisema: hatutakuamini mpaka utuchimbulie katika ardhi hii chemchem.

wapenda raha katika washirikina walitoa pendekezo kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kuwa awachimbulie chemchem au mto, wao sio watu wengine, kwa ajili ya chumo na faida. Kuna mapokezi yanayosema kuwa vijoho na wapenda anasa walisema: Ewe Muhammad! Hii ardhi ya Makka ni finyu, basi yaondoe majabali yake na utuchimbulie chemchem ili tunufaike na ardhi.

2.Au uwe na kitalu cha mitende na mizabibu na utupitishie mito kati yake ikimiminika.

Yaani kama hutatuchimbulia chemchem, basi angalu jichimbulie wewe, ili uwe unafanana na hadhi ya juu, Lakini ukiwa huna kitu basi wewe unatakikana uwasikilize walio nacho. Kwamba mali peke yake ndiyo itakayomfanya aliye nayo awe anafaa kuwa kiongozi na bwana mkubwa. Hawakujua kuwa risala ya Muhammad(s.a.w.w) ni utajiri mkubwa wa mtu, uhai wake, na kwamba Muhammad ni rehema kwa watu wa ardhini itakayowaokoa na ufukara, ujinga, dhulma na utaghuti. Wapi na wapi wanaoabudu mali na kupigana vikumbo na tamaa waweze kujua rehema na kheri?

3.Au utuangushie mbingu vipande vipande, kama ulivyodai, au utuletee Mwenyezi Mungu na Malaika ana kwa ana.

Walitaka wachimbuliwe chemchem yao au yake; kam sio hivyo au vile, basi awalete adhabu kutoka mbinguni au Mwenyezi Mungu mwenyewe aje na malaika kushuhudia kuwa Yeye ni Mtume.

Hii vile vile inatokana na fikra yao kwamba anayestahiki uongozi ni tajiri, sio fukara. Dalili ya hilo ni kule kuweka sharti la kumwamini Muhammad na jambo wanaloliona kuwa haliwezekani. Ni wazi kuwa kulazimisha jambo lisilowezekana maana yake ni kung’ang’ania matakwa yao ya kuchimbuliwa chemchem ardhini; sawa na kusema: Sifanyi hivi mpaka ngamia apite kwenye tundu ya sindano.

4.Au uwe na nyumba ya dhahabu.

Yaani iliyojengwa kwa dhahabu au iliyopambwa nayo. Hii vile vile inatokana na fikra ya mali.

Au upae mbinguni.

Nalo hili linafungamana na jambo lisilowezekana. Maana yake ni kung’ang’ania kuwa mali ndio kitu pekee cha kumweka mtu kwenye cheo.

Na hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie Kitabu tukisome.

Baadhi ya wafasiri wapya wanasema: “Unadhihiri utoto wa kuhafamu na kufikria; kama unavyodhihiri ukaidi wa kipumbavu.” Lakini hapana huo si utoto wala si upumbavu; isipokuwa hilo linatokana na ufisadi, kujibagua, uporaji, unyang’anyi na kuabudu mali. Kitu kinachofahamisha hilo zaidi ni kule kupendekeza na kuweka sharti la kumfuata Mtume awe na nyumba ya dhahabu kuwa ndio muabudiwa wao wa kwanza na ndio mfano wao mkuu.

Sema: Ametakasika Mola wangu! Kwani mimi ni nani, isipokuwa ni mwanadamu Mtume?

Anayefuata amri ya yule aliyemtuma na kukatazika kwa makatazo yake:

وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأْتِيَ بِآيَةٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ ﴿٣٨﴾

“Haiwi kwa Mtume kuleta muujiza isipokuwa kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.” Juz; 13 (13:38).

Na nini kilichowazuia watu kuamini ulipowajia utume, isipokuwa walisema: je, Mwenyezi Mungu hupeleka mwanadamu kuwa Mtume?

Wafasiri, akiwemo Tabrasi na Razi, wameiangalia Aya hii kuwa haiungani na Aya zilizotangulia na wakasema katika kuifasiri: Hakika washirikina wa Makka hawakumwamini Muhammad(s.a.w.w) kwa sababu wao walikuwa wakiitakidi kuwa mjumbe ni lazima awe ni katika jinsia ya malaika, si katika jinsia ya watu. Lakini tafsiri hiyo iko mbali sana kutokana na njia zifuatazo:-

Washirikina wa kikuraishi walikuwa wakiamini utume wa Ibrahim na kwamba wao wanatokana na kizazi chake.

Kauli ya washirikina: ‘Hatutakuamini mpaka utuchimbulie,’ inafahamisha kuwa wanaamini risala ya binadamu; isipokuwa walitoa sharti la kuwa Mtume awe tajiri: “Na walisema: kwanini hii Qur’an haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii” (43:31) Makusudio ya mtu mkubwa ni Walidi bin Mughira, katika viongozi wa Makka au Urwa bin Masud katika viongozi wa Taif.

Lau ingelikuwa tafsiri kama wanavyosema, basi washirikina wangelikuwa na udhuru katika kupinga kwao utume wa Muhammad (s.a.w.), kwa sababu watakuwa wanafanya lile wanaloliitakidi, na Mwenyezi Mungu amewasifu kwenye Aya nyingi kuwa wanadhihirisha yale waliyoyaficha:

بَلْ بَدَا لَهُم مَّا كَانُوا يُخْفُونَ مِن قَبْلُ ﴿٢٨﴾

“Bali yamewadhihirikia waliyokuwa wakiyaficha zamani,” Juz, 7 (6:28)

“Na wakazikataa kwa dhulma na kujitia uluwa na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nazo.” (27:19).

Kwa ufupi ni kuwa maana sahihi ya Aya ni kwamba washirikina wali- poshindwa na hoja ya utume wa Muhammad, walikimbilia ubabaishaji na kujaribu kuwapoteza wajinga wasiokuwa na akili.

Ndio wakasema kama mbinu tu za kuhadaa, kuwa Mwenyezi Mungu hamtumi Mtume binadamu, isipokuwa Malaika tu. Walisema haya wakiwa wanajua kwamba wao ni waongo. Ndio maana Mwenyezi Mungu akasema ‘Ispokuwa walisema’ na wala hakusema walidhani n.k. Hii inafahamisha kuwa kupinga kwao ni kiasi cha inadi tu ya kauli si ya itikadi.

Sema: Lau ingelikuwa duniani kuna Malaika wanaotembea kwa utulivu, Yaani wanaotembea kama wanadamubasi bila ya shaka tun- geliwateremshia Malaika kuwa Mtume wao.

Hekima ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) inataka apeleke Mtume kwa viumbe wake kutokana na jinsi yao. Wakiwa ni watu basi mtume wao atatokana na wao na wakiwa ni Malaika basi watakuwa hivyo hivyo. Kwa sababu jinsia inapendelea zaidi kwenye jinsia yake:

لَقَدْ مَنَّ اللَّـهُ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ إِذْ بَعَثَ فِيهِمْ رَسُولًا مِّنْ أَنفُسِهِمْ ﴿١٦٤﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu amewaneemesha waumini kwa kuwaletea Mtume miongoni mwao” Juz. 4 (3:164).

Washirikina wanajua hilo, lakini wanafanya vitimbi na hadaa. Umetangulia mfano wake katika Juz.7 (6:9).

Unaweza kuuliza: Jibril ni Malaika naye alikuwa mjumbe wa Mungu kwa Muhammad ambaye ni mtu, imekuwaje? Jibu: baina ya hawa wawili kuna aina fulani ya kukurubiana katika jinsi; kwamba kila mmoja wao ni mjumbe kutoka kwa Mungu.

Sema: Mwenyezi Mungu anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi. Hakika Yeye anawajua vyema waja wake na anawaona.

Mwenyezi Mungu ni shahidi wa Muhammad kwa miujiza aliyoidhihirisha mikononi mwake, historia inashuhudia heri ya utu iliyopatikana kutokana naye na risala yake inashuhudia kwamba yeye ni rehema kwa viumbe na lolote katika sera ya Muhammad ni hoja tosha ya ukweli wake na utukufu wake.

وَمَن يَهْدِ اللَّـهُ فَهُوَ الْمُهْتَدِ وَمَن يُضْلِلْ فَلَن تَجِدَ لَهُمْ أَوْلِيَاءَ مِن دُونِهِ وَنَحْشُرُهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ عُمْيًا وَبُكْمًا وَصُمًّا مَّأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ كُلَّمَا خَبَتْ زِدْنَاهُمْ سَعِيرًا ﴿٩٧﴾

97. Na anayeongozwa na Mwenyezi Mungu ndiye aliyeongoka na anayempotoa, basi, hutawapatia walinzi wasiokuwa Yeye. Na tutawakusanya Siku ya Kiyama hali ya kukokotwa juu ya nyuso zao wakiwa ni vipofu na mabubu na viziwi. Makazi yao ni Jahannam. Kila moto ukifanya kuzimika tutazidi kuuchochea uwake kwa nguvu.

ذَٰلِكَ جَزَاؤُهُم بِأَنَّهُمْ كَفَرُوا بِآيَاتِنَا وَقَالُوا أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا وَرُفَاتًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ خَلْقًا جَدِيدًا ﴿٩٨﴾

98. Hayo ni malipo yao kwamba wao walizikataa ishara zetu na wakasema: je, tutakapokuwa mifupa na mapande yaliyosagika, je tutafufuliwa kuwa viumbe wapya?

أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ قَادِرٌ عَلَىٰ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُمْ وَجَعَلَ لَهُمْ أَجَلًا لَّا رَيْبَ فِيهِ فَأَبَى الظَّالِمُونَ إِلَّا كُفُورًا ﴿٩٩﴾

99. Kwani hawaoni kwamba Mwenyezi Mungu aliyeumba mbingu na ardhi ni Mwenye kuweza kuumba mbingu mfano wao? Na yeye amewawekea muda usio na shaka yoyote, lakini madhalimu hawataki isipokuwa ukafiri.

قُل لَّوْ أَنتُمْ تَمْلِكُونَ خَزَائِنَ رَحْمَةِ رَبِّي إِذًا لَّأَمْسَكْتُمْ خَشْيَةَ الْإِنفَاقِ وَكَانَ الْإِنسَانُ قَتُورًا ﴿١٠٠﴾

100. Sema, lau mngelikuwa mnamiliki hazina ya rehema ya Mola wangu, basi mngeliizuia kwa kuchelea kuisha. Na mtu ni mchoyo sana.

ALIYEONGOZWA NA MUNGU

Aya 97-100

MAANA

Na anayeongozwa na Mwenyezi Mungu ndiye aliyeongoka na anayem- potoa, basi, hutawapatia walinzi wasiokuwa Yeye.

Hii ni kumwelezea aliye mwema; yaani anayekuwa hivyo mbele ya Mwenyezi Mungu; na wala sio yule watu wanayesema kuwa ni mwema. Kuna Hadith isemayo: “Dhahiri ni ya watu na batini ni ya Mungu.” Katika Nahjulbalagha imeelezwa: ”Utajiri na ufukara ni baada ya kuonekana kwa Mungu.”

Wafisadi na wapotevu hawana wa kuwanusuru wala kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7: 178). Ama adhabu ya wapotevu wanaopoteza, ameiashiria Mwenyezi Mungu kwa kusema:

Na tutawakusanya Siku ya Kiyama hali ya kukokotwa juu ya nyuso zao wakiwa ni vipofu na mabubu na viziwi. Makazi yao ni Jahannam. Kila moto ukifanya kuzimika tutazidi kuuchochea uwake kwa nguvu.

Hili ni fumbo la uchungu wa adhabu na ukali wake kwa yule Mwenye kupinga hisabu na adhabu yake mpaka ajue aliyoyapinga:

كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا أُعِيدُوا فِيهَا وَقِيلَ لَهُمْ ذُوقُوا عَذَابَ النَّارِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ﴿٢٠﴾

“Na wataambiwa: onjeni adhabu ya moto ambayo mlikuwa mkiikadhibisha” (32:20).

Na hayo ni malipo yao kwamba wao walizikataa ishara zetu pamoja na ufafanuzi wa kutokea ufufuo. Walikanusha na wakapinga si kwa chochote ila ni kwa kuona ni mbali hilo.

Na wakasema: je, tutakapokuwa mifupa na mapande yaliyosagika, je tutafufuliwa kuwa viumbe wapya?

Imekwishatangulia Aya hii neno kwa neno katika Aya ya 49 ya Sura hii.

Kwani hawaoni kwamba Mwenyezi Mungu aliyeumba mbingu na ardhi ni Mwenye kuweza kuumba mbingu mfano wao? Na yeye amewawekea muda usio na shaka yoyote, lakini makafiri hawataki isipokuwa ukafiri.

Makusudio ya muda hapa ni muda wa ufufuo na kwamba huo utakuwa tu. Wameukana na hali wanaona kuumbwa kwa mbingu na ardhi huku wakikubali kuwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyeziumba na akazipangilia vizuri kwa uweza wake, lakini wakasema kuwa Mwenyezi Mungu hawezi kuwarudisha tena baada ya kutoweka, kwa vile hilo ni jambo zito.

Ndio Mwenyezi Mungu akawaambia kuwa mwenye kuweza kukifanya kitu bila ya kitu basi ana uweza zaidi kukikusanya kitu hicho baada ya kutawanyika.

Maana ya Aya hii yamekwisha tangulia kwenye Aya nyingi, Angalia Juz.13 (13:5).

Hebu tusome kwa pamoja hoja hizi za kufunga mdomo wa mpinzani wa ufufuo, kwa mfumo usiokuwa na ushabiki; kisha useme: Ole wao wenye kukadhibisha:

“Walisema: Je, tutakapokufa na tukawa mchanga na mifupa ndio tutafu- fuliwa? Tuliahidiwa haya sisi na baba zetu zamani. Hayakuwa haya ila ni ngano za watu wa kale.”

“Sema: Ni ya nani ardhi na mbingu na vilivyomo ndani yake, kama nyinyi mnajua?”

“Watasema ni ya Mwenyezi Mungu.”

“Sema: Basi je, hamkumbuki?”

“Sema ni nani Mola wa mbingu saba na Mola wa Arshi kuu?”

“Watasema ni Mwenyezi Mungu.”

“Sema: Basi Je, hamuogopi?”

“Sema: ni nani ambaye ufalme wa kila kitu umo mikononi mwake, naye ndiye alindaye na halindwi, ikiwa mnajua?”

“Watasema ni vya Mwenyezi Mungu”

“Sema: basi vipi mnadanganywa?” 23: (82 – 89).

Huu ni ushahidi wazi kwamba itikadi ya kiislamu iko kwenye misingi ya elimu na uhuru wa akili na rai, Tazama: Juz; 7 (6:4) “Kifungu hakuna udikteta katika ardhi wala mbingu.”

Sema lau mngelikuwa mnamiliki hazina ya rehema ya Mola wangu, basi mngeliizuia kwa kuchelea kuisha.

Rehema ya Mwenyezi Mungu inaenea kwenye kila jambo, kama vile afya, ufahamu, mali na neema nyinginezo, lakini makusudio yake hapa ni kuhusu mali, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t): “Kuhofia kuisha” na ile Aya ya 90 ya Sura hii.

Ubainifu wake ni kuwa Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake awaambie wapenda anasa kuwa nyinyi mlitaka Mwenyezi Mungu awazidishie mali zenu na utajiri wenu kwa kuchimbua mito ardhini, huku akiwa anajua kwamba nyinyi lau mtamiliki hazina ya mbingu na ardhi ambayo haishi, basi mngeendelea na ubahili wenu na uchoyo kwa kuhofia kuisha. Hili linatilia mkazo tuliyosema kwamba wapenda anasa hawafikirii isipokuwa mali.

Na mtu ni mchoyo sana

Katika Juz. 12 (11: 9) tumesema kuwa Qur’an, haikusudii, kwa wasifu huu, kumueleza binadamu alivyo; isipokuwa ni kutafsiri tabia ya binadamu katika badhi ya hali zake. kwa maelezo zaidi rudia huko.