NAHJUL BALAGHA
JUZUU YA PILI
MTARJUMI: HARUNA PINGILI
“Japo Mwenyezi Mungu amwachie muda dhalimu mshiko wake hautomkosa, naye yuamchunga kwenye mapito ya njia zake, na mahali pa mkwamo wa koo mapitio ya mate yake[221] , naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mkononi mwake, hawa watu (Mu’awiya na kundi lake) watapata ushindi dhidi yenu[222] ,
si kwa sababu wana haki zaidi kuliko mliyonayo bali ni kwa sababu ya haraka yao ya kutekeleza batili yao na ugoigoi wenu mbali na haki yangu (kuifuata). Umma huwa waogopa dhulma ya niliwaiteni kwa siri na kwa wazi hamkuitika, nilikunasihini hamkukubali.
“Mkiwa mpo kama hampo, mko watumwa kama mabwana![223] Ninakusomeeni nukta za hekima mnazikwepa, na ninakuonyeni kwa mawaidha yafikayo (masikioni) mnafarakana mbali nayo, nawahimizeni kwenda jihadi dhidi ya watu waovu, wala sijafikia mwisho wa kauli yangu nawaona mnatawanyika mfano wa mikono ya Sabaa - Ayaadiy sab’a.[224] “Munarejea kwenye makazi yenu mkiwa hamuwaidhiki. Nakunyoosheni asubuhi, mwarejea kwangu jioni mkiwa mmepindama kama upinde, mnyooshaji amehemewa na mnyoshwaji amekuwa mgumu.
“Enyi kaumu ambao miili yao ipo hadhiri hali akili zao zimeghibu, na ambao utashi wao uko tofauti. Watawala wao wamepatwa na balaa. Sahibu yenu yuamtii Mungu, na ninyi mnamuasi, na sahibu wa watu wa Sham yuamuasi Mungu na hali wao wanamtii! Ningependa, wallahi lau Muawiya hangenibadilishia ninyi ubadilishaji wa dinari na dirham, angewachukua kutoka kwangu kumi kati yenu na angenipa mimi mtu mmoja kutoka wao!
“Enyi Watu wa Kufa! nimepata uzoefu kwenu wa matatu na mawili mengine: Mko viziwi hali mkiwa na masikio, na mko mabubu hali mkiwa mwasema, vipofu mlio na macho. Sio wasaidizi wa kweli wakati wa mapambano wala sio ndugu wa kuaminika kwenye balaa! Mikono yenu iingie mchanga!( – yaani mikono yenu isiwe na kheri! - hili ni neno la kumlaani mtu). Enyi mlio mfano wa ngamia ambao mchungaji wake ameghibu! Kila wakusanywapo upande mmoja wanatawanyika upande mwingine.
Wallahi nawaona kwa maoni yangu, endapo vita vitakuwa vikali na hali ya mambo ikiwa inayumba mtamkimbia mwana wa Abi Talib ukimbiaji wa mwanamke akiwa uchi mbele, kwa hakika mimi nipo katika mwongozo wa wazi kutoka kwa Mola wangu Mlezi, na (niko) katika njia ya Nabii wangu, na niko katika njia ya wazi nikiokota cha kuokota[225] .
“Waangalieni Ahlul-bayt wa Nabii wenu, na jiambatisheni na mwendo wao, na fuateni nyayo zao, hawatokutoweni nje ya mwongozo, na hawato kutumbukizeni kwenye maangamizi, wakikaa kaeni wakiinuka inukeni, msiwatanguliye mtapotea, wala msibaki nyuma yao mtaangamia.
Kwa kweli nimewaona sahaba za Muhammad(s.a.w.w) simuoni yeyote kati yenu anashabihiana nao, kwa kweli walikuwa wanaianza asubuhi wakiwa na nywele timtim na wakiwa wamejaa vumbi kichwani (na mwilini)[226] .
Wamepitisha usiku katika hali sijda na qiamu, wakibadili kati ya paji zao za uso na mashavu yao ( yaani mara wakisujudu kwa paji la uso na mara nyingine kwa mashavu yao). Na walikuwa wanasimama mfano wa aliyesimama juu ya kaa la moto kwa ajili ya kukumbuka marejeo yao, kana kwamba kati ya macho yao kuna goti la mguu wa mbuzi kutokana na sijda zao ndefu. Atajwapo Mungu macho yao hutiririsha machozi mpaka yalowesha kosi (kola zao), walikuwa wana yumba kama uyumbavyo mti siku ya upepo mkali, wakiogopa adhabu, na wakiwa na matarajio ya thawabu.”.
Na Miongoni Mwa Maneno Yake(a.s) - Ibn Qutaybah ameeleza katika al-Imama was-Siyasah, jalada la kwanza, uk. 151.
“Wallahi wataendelea hivi (Ufafanuzi: Usemi hapa ukadiriwe hivi: Wangali bado ni madhalimu) mpaka wafikie kiasi cha kuwa hawatoacha alichokiharamisha Mungu ila watakihalalisha, wala ahadi ila wataitangua na hata haitobakia nyumba ya matofali wala ya manyoya ila dhulma yao itaingia, na ubaya wa matendo yao utawafanya duni.
Mpaka watakuja kusi-mama waliaji wawili walie: Mliaji analia kwa ajili ya dini yake, na mliaji alia kwa ajili ya dunia yake, mpaka iwe nusura ya mmoja wenu kwa mwingine mfano wa nusura ya mtumwa kwa bwana wake, akiwa yupo anamtii, na anapoghibu humsengenya.
Mpaka itakuwa mwenye shida kubwa mno kati yenu ni yule mwenye kuwa na dhana njema mno kwa Mungu miongoni mwenu.
Mungu akikutunukieni amani na salama ikubali- ni, na akikupeni mtihani vuteni subira, “..... Na kwa hakika mwisho mwema ni wa wachamungu.”(7:128).
Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - an-Nuuriy ameieleza katika al-Mustadrak Jz. 1, uk. 411, na as-Saduq katika Man la Yahdhurul-Faqih, Jz. 1, uk. 270.
“Tunamhimidi kwa yaliyotokea, na tunamuomba msaada kwa ajili ya mambo yetu yatakayokuwa, tunamuomba usalama katika dini, kama tunavyomuomba usalama kuihusu miili[227] .
“Nakuusieni kujiweka mbali na dunia hii ambayo ni yenye kukuacheni japo muwe hampendi kuiacha, na ni yenye kuichakaza miili yenu japo mupende kuifanya upya. Kwa kuwa mfano wake na ninyi ni kama wasafiri[228] , wamesafiri waliokwenda kiasi fulani cha masafa kisha wakawa kana kwamba wao haraka wameikata safari, wameikusudia alama, na mara moja kana kwamba wameifikia. Ukaribu ulioje wa masafa kwenye lengo endapo mtu atalielekea na kulifikia! Ukaribu wa masafa ulioje wa kwenye lengo ikiwa mtu yualielekea na kulifikia!
Hatua fupi ilioje ya mtu aliye na siku moja tu ambayo hawezi kuizidisha, hali ikiwa amtakaye mwenye haraka yaani mauti amfuata, anasumbua duniani mpaka aitoke apende asipende! Hivyo basi msihusudiane kugombania utukufu wa dunia na fahari yake, na wala msifurahiye mapambo na neema zake, na wala msiyahuzunikie madhara yake na shida ya madhara yake.
“Kwa hakika utukufu wake na fahari yake vinaelekea kukatika, mapambo yake na neema zake vitatoweka, madhara yake na shida zake zinakwisha, na kila muda humo waelekea mwisho, na kila aliye hai humo aelekea mwisho.
Je ninyi kutokana na athari za waliokuwa mwanzo hamuonyeki! Na katika babu zenu wa mwanzo kuna ufunguzi wa macho na zingatio, endapo mtakuwa mnatia akilini! Je hamuoni kuwa waliopita miongoni mwenu hawarejei, na walioendelea kuishi hawatobaki milele! Si mwaona wana wadunia wanaingiwa na jioni na wanaingiwa na asubuhi wakiwa katika hali nyingi mtawanyiko: Kuna aliyekwisha kuwa mauti analiliwa, na mwingine ahaniwa, na aliyetupika chini amekumbwa na balaa, na mwenye kumtembelea mgonjwa, na mwingine anatapia nafsi yake, na ambaye aitafuta dunia na mauti yamtafuta yeye, na kuna aliyeghafilika wala haghafilikiwi, na katika athari za waliopita hupita waliobakia! Lo! Mkumbukeni mbomoa raha, na anayeyatia uchungu matamanio, na mkata matumaini, pindi yavamiwapo matendo mabaya, na muombeni msaada Allah (swt) ili kutekeleza wajibu wa haki Yake, na neema Zake na hisani Zake zisizo na idadi.”.
“Mstahiki wa sifa ni Allah Mwenye kueneza fadhila Zake kwa viumbe, na Mwenye kuwanyooshea mkono wake wa ukarimu. Tunamtukuza katika mambo Yake yote, na tunamuomba msaada ili kuzichunga haki Zake.
Na tunashuhudia kuwa hakuna mungu mwingine, isipokuwa Yeye na kuwa Muhammad ni mja Wake na mjumbe Wake, amemtuma kudhihirisha amri Yake na kuitangaza, na awe mwenye kutamka utajo Wake.
Na alitekeleza kwa uaminifu, na alifariki akiwa ndani ya uongofu; na alituachia bendera ya haki[229] , mwenye kuitangulia atakuwa ametoka[230] , na mwenye kubaki nyuma yake atakuwa amenyauka, na mwenye kujiambatisha nayo atakuwa amejiunga na haki.
Dalili yake ni umakini wa usemaji[231] , asimama taratibu, ana haraka akienda. Hivyo basi endapo ninyi mtamlainishia shingo zenu (yaani mkimtii), na mkamuishiria kwa vidole vyenu[232] , 4mauti itamjia na itaenda naye, na mtabaki baada yake ma’sha’Allaahu, mpaka Mungu amtoe kwa ajili yenu mmoja ambaye atakukusanyeni, na kuuweka pamoja mparaganyiko wenu, msimtumainie asiyekuja wala msikate tamaa na aliyegeuza mgongo[233] kwa kuwa aliyegeuza mgongo huenda ukamteleza mguu wake mmoja, na ukathibiti mwingine, na ikarudi miwili mpaka ikathibiti yote.
“Juweni! Kuwa mfano wa Aali Muhammad(s.a.w.w) , ni mfano wa nyota za mbinguni, ikizama nyota yachomoza nyota. Kama kwamba neema za Mungu zimekukamilikieni, na amekuonesheni kile mlichokuwa mwakitarajia.[234] ”