8
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
DUA YA 45
ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KUUAGA MWEZI WA RAMADHANI
Oh Allah! Ewe ambaye hapendi alipwe, Ewe ambaye hajutii kwa sababu ya kutoa. Ewe ambaye hamlipi mja wake sawa kwa sawa. Huruma zako ndio mwanzo, Msamaha wako ni ufadhili, Adhabu yako ni uadilifu, Hukumu yako ni uchaguzi mwema. Ukitoa huutii doa utowaji wako kwa masimbulizi. Ukiziwiya (kutoa) hauwi uziwiyaji wako uchokozi. Wamshukuru anayekushukuru na wewe ndiye uliyempa ilhamu ya kushukuru wamlipa mwenye kukuhimidi na wewe ndiye uliyemfundisha kukuhimidi wamsitiri ambaye lau ungependa ungemfedhehesha. Wamfanyia hisani ambae lau ungependa ungemnyima. Wote hao wawili wastahiki kutoka kwako fedheha na kunyimwa, isipokuwa wewe umefanya msingi wa matendo yako kufadhili. Umepitisha uwezo wako katika msamaha. Umemlaki aliye kuasi kwa huruma umempa muhula mwenye kukusudia kujidhulumu nafsi yake. Unawangoja kurejea kwa saburi yako. Unaacha kuwa harakia kwenye toba ili mwangamiaji asije angamia kwa sababu yako mwenye kuangamia miongoni mwao. Na asije kuwa na hali mbaya kwa neema zako mwenye hali mbaya wao isipokuwa kwa ajili ya udhuru wako mrefu kwake, na baada ya mfululizo wa hoja dhidi yake. Ikiwa ni ukarimu wa msamaha wako Ewe Mkarimu! Na ni tendo la huruma Ewe mpole. Wewe ndie uliyefungua mlango wa msamaha wako kwa waja wako, na umeuita "TOBA" na umeweka juu ya mlango huo dalili kwa ufunuo wako ili wasiupotee ndipo ulisema - jina lako limebarikiwa: (Tubuni kwa Mungu toba isiyo ya kurudi nyuma huwenda Mola wenu akakuondoleeni maovu yenu na akakuingizeni katika Jannah ambazo chini yake mito yatiririka. Siku ambayo Mungu hatomwaibisha huyu Nabii na walioamini pamoja naye nuru yao yakimbia (pita) mbele yao na kuliani kwao wakisema Mola wetu tutimiziye nuru yetu na tughofirie kwa hakika wewe umuweza juu ya kila kitu). Basi ni udhuru gani atakuwa nao mwenye kughafilika kuingia nyumba ile baada ya mlango kufunguliwa na kuwepo dalili?
Na wewe ndiye ambaye ulijizidishia bei dhidi yako mwenyewe kwa faida ya waja wako ukiwatakia faida yao kwa biashara yao na wewe. Na kufuzu kwao kwa kukufika wewe na ziada kutoka kwako. Ukasema jina lako limebarikiwa na uko ngazi ya juu (mwenye kuleta tendo jema atapata malipo yaliyo sawa na mema kumi, na mwenye kuleta tendo ovu moja hatolipwa ila sawa na malipo ya ovu hilo moja) na umesema: (mfano wa ambao watoao mali zao katika njia ya Mungu ni mfano wa punje moja imetoa masuke saba katika kila suke kuna punje mia moja Mungu humzidishia amtakaye). Na ulisema: (nani ambaye atamkopesha Mungu mkopo mzuri? Naye atamzidishia zidisho jingi. Na ulizoteremsha fano wao katika Qur'ani miongoni mwa aya zielezazo miongoni mwa ongezeko la malipo ya matendo mema. Na wewe ndiye uliyewajulisha kwa kauli yako toka ghaibu yako na himizo lako ambalo lina hadhi yao ndani yake, lau ungelificha kwao macho yao yasingelidiriki. Masikio yao yasingelisikia. Akili zao zisingelifikia. hivyo basi ulisema: (Nikumbukeni nitawakumbuka nishukuruni wala musinikufuru) na ulisema: (mukiwa wenye kushukuru nitawazidishieni lakini mkikufuru (kuacha shukrani) hakika adhabu yangu ni kali). Na ulisema: (Niombeni nitakujibuni hakika wanaofanya kibri kuniabudu mimi wataingia Jehannam wakiwa duni) umeiita DU'A yako Ibada, na kuacha kukuomba ni kibri, na umekamia mwenye kuacha kukuomba ataingia jehannam akiwa duni.
Hivyo basi wamekutaja kwa ukarimu wako. Na wamekushukuru kwa fadhila zako na wamekuomba kwa amri yako. Na wametoa sadaka wakitaka ziada yako. Na katika yote hayo umekuwa uokozi wao kwa kuepukana na ghadhabu zako na kufuzu kwao kupata ridhaa zako. Lau kiumbe mwenyewe angemwongoza kiumbe mwingine mfano wa yale uliyowaongoza waja wako angekuwa asifike kuwa ni muhisani na angesifika kuwa ni mwema na angehimidiwa na kila ulimi. Sifa njema ni zako. Kipatikanacho katika mwenendo wa sifa zako hapana tamko libakialo kwa sifa usifiwazo na maana ya sifa ya kuelekea wewe. Oh yule ambaye amesifika kwa waja wake kwa hisani na ufadhili. Na amewaeneza ukarim na umbuji wingi ulioje wa neema zako zilizotuenea? Ukarimu wako mwingi mno kwetu umetufanya makhsusi kwa wema wako. Umetuongoza kwenye dini yako ambayo umeichagua. Na mila yako uliyoiridhia, na njia yako uliyoirahisisha. Na umetuoneysha ukaribu kwako, nafika kwenye ukarimu wako. Oh Allah! Miongoni mwa teule mno katika nyadhifa hizo na zilizo makhsusi sana miongoni mwa faradhi hizo ni mwezi wa Ramadhani ambao umeufanya kuwa makhsusi kwa kuulinganisha na miezi mingine. Umeuchagua toka zama zote na nyakati zote. Umeupenda kuliko nyakati zote za mwaka kwa sababu umeteremsha humo Qur'an na nuru. Humo umezidisha imani na umewajibisha humo (mwezi wa Rama...) Funga, na umependezewa humo kisimamo cha sala Na umeutukuza kwa Laylatul-qadir ambayo ni bora kuliko usiku elfu moja. Kisha umetupendelea sisi kwayo kuliko umma zingine. Kwa ubora wake umetuchagua mbali na watu wa mila. Tumefunga kwa amri yako mchana wake tumesimama tukisal usiku wake tukijishughulisha kuufunga na kusali humo. Kwa vile umetuonesha kwa ajili yake rehema zako. Kwa ajili yake tumekuwa na sababu kuelekea thawabu zako. Na wewe uko daraja la juu zaidi kuliko kile kwa ajili yake watakiwa. Umkarimu uombwacho kwa fadhila zako.
Ukaribu kwa mwenye kujaribu kuupata ukaribu wako. Mwezi huu umetusimamishia msimamo wa sifa njema, umesuhubiana na sisi usuhuba wa mtu mwema. Umetufidisha faida bora ya viumbe wa ulimwengu. Kisha umetuacha ulipotimia wakati wake na kukatika kwa muda wake na kutimiza idadi yake. Nasi tu wenye kuuaga uwagaji wa ambaye kujitenga nae kwake kwa umiza juu yetu. Kumetusononesha na kutuacha peka, kutoweka kwake, mbali na sisi, kwa ajili yake umetulazimu ulinzi ulihifadhika. na heshima yenye kuangaliwa, na haki tekelezwa. Hivyo twasema: Assalaamu Alayka Ewe mwezi wa Mungu mkubwa kabisa Ewe Iddi ya wapenzi wake (Mungu). Assalaamu Alayka, Ewe wakati ulio bora kuwa nao miongoni mwa nyakati. Ewe mbora wa miezi katika siku na saa Assalaamu Alayka mwezi matumaini yamekurubia. Kazi njema humo zimetawanywa. Assalaamu Alayka Ewe rafiki ambaye thamani yake iliyopo imetukuka. Kutoweka kwake kwa tia simanzi. Machungu ya kutengana naye kwake yatazamiwa. Assalaamu Alayka msuhuba ambaye ujaji wake huleta raha hufurahisha ambaye aondokapo huleta kitwea. Assalaamu Alayka jirani ambaye nyoyo hulainika kwa ajili yake. Dhambi mwake zimepungua. Assalaamu Alayka msaidizi asaidiae dhidi ya shetani. Mwezi arahisishaye njia za ihsani. Assalaamu Alayka wengi walioje wakombolewa wa Mungu ndani yako.
Furaha iliyoje kwa wenye kuchunga heshima yako kwa msaada wako. Assalaamu Alayka umekuwa mfutaji mno wa dhambi. Umesitiri sana wa aina mbali mbali za aibu. Assalaamu Alayka umekuwa na uvumilivu kwa watenda dhambi wa tisha mno mioyoni mwa waumini. Assalaamu Alayka mwezi ambao siku hazishindani nao. Assalaamu Alayka mwezi ambao amani katika kila jambo. Assalaamu Alayka mwezi ambao kuwa pamoja nao kwake hakuchukizi, wala kuchanganyika pamoja nao kwake hakulaumiki. Assalaamu Alayka kama ulivyoingia kwetu kwa baraka nyingi na umetoa uchafu wa makosa. Assalaamu Alayka si muagwa achukizaye wala hakichoshi kilichoachwa na saumu yake. Assalaamu Alayka mtafutwa kabla ya wakati wake. Na muhuzunikiwa kabla ya kwisha kwake. Assalaamu Alayka maovu mangapi yamezuiliwa yasitufike kwa wewe. Mema mangapi tumebubujishiwa kwa sababu yako. Assalamu Alayka wa Alaa Laylatil Qadr ambayo ni bora kuliko miezi elfu moja. Assalamu Alayka tulipupia sana jana tutakuwa na shaka sana na wewe kesho. Assalaamu Alayka na juu ya fadhila zako zilizo haramishwa kwetu na juu ya baraka zako zilizopita ambazo hivi sasa tumepokonywa. Oh Allah! Sisi ni wana, mwezi huu ambao umetuboresha kwako (kwa huo mwezi). Na kwa huruma yako umetupa taufiki. walipokosa kuujua wakati wake. Na wamenyimwa fadhila zake kwa ajili ya uovu wao. Na wewe ndiye mfadhili wa elimu zake ambazo umetupendelea maarifa yake.
Umetuongoza kwenye utekelezaji wa sunna zake. Kwa tawfiki yako tumebeba jukumu la kuufunga na kusali kwa kiwango kidogo sana. Tumetekeleza humo kidogo sana miongoni mwa kingi. Oh Allah! sifa njema zote ni zako. Twakiri maovu. Twatambua kuzembea. Katika nyoyo zetu kuna fundo la majuto kwako. Ulimini mwetu kuna ukweli wa kukuomba udhuru. Tupe thawabu kwa yaliyotupata ingawaje tumezembea. Huenda tutaifikia kwayo fadhila itakiwayo na kwayo tufanikiwe aina mbali mbali za vifaa vilivyohifadhiwa. Wajibisha kwa ajili yetu udhuru wako kwa tuliyoshindwa kutekeleza ipasavyo miongoni mwa haki zako. Umri wetu tulio nao ufikishe mwezi wa Ramadhani ujao tukiufikia tusaidiye kufanya ibada unayostahiki. Tufanye tuwe twatekeleza yapasayo (ndani ya) mwezi huu yastahikiyo katika utii. Tutunukiye Amali njema itayotekeleza haki yako katika miezi miwili miongoni mwa miezi ya Dahar. Oh Allah! Tuliyoyatenda katika mwezi wetu huu miongoni mwa dhambi ndogo au kubwa. Au dhambi tumeangukia Emo na kosa tulilotenda makusudi au kwa kusahau. Tumejidhulumu nafsi zetu. Au tumemvunjia heshima mtu mwingine. Mswaliye Muhammad na Aali zake. Na utusitiri kwa sitira yako. Tusamehe kwa msamaha wako wala usituweke mbele ya macho ya wasimbuliaji. Wala usitukunjulie ndimi za wa umbuwaji. Tutumikishe kwa yatakayokuwa ndiyo punguzo na kafara ya usilolikubali kutoka kwetu. Kwa huruma yako isiyokwisha na fadhila yako isiyopanguliwa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake uuponye msiba wetu kwa mwezi wetu. Utubariki siku ya Iddi yetu na siku yetu ya kwanza kufunguliwa.
Ijaaliye kuwa miongoni mwa siku ya kheri mno imetupitia yenye kuleta msamaha sana na yenye kufuta mno dhambi. Tughofiriye zilizojificha katika dhambi zetu na zilizotangazika. Oh Allah! tutowe kwa kutoweka mwezi huu makosa yetu tuvuwe kwa kutoweka kwake maovu yetu. Tufanye miongoni mwa watu wenye heri mno kwa huwo (mwezi). Na wenye hisa kubwa mno humo na wenye hadhi mno humo. Oh Allah! mwenye kuchunga haki ya mwezi huu kwa haki, na kuhifadhi heshima yake kwa haki, na kutekeleza mipaka yake kwa haki. Na kuchelea dhambi zake kwa haki yake. Au akajikurubisha kwako kwa ujikurubishaji uwajibishao ridhaa yako kwake na huruma yako ikamwelekea juu yake. Tupe sisi mfano wake kutoka kwenye ukwasi wako. Tupe na sisi zaidi yake kwa fadhila zako. Hakika fadhila zako hazipunguwi kwa hakika hazina zako hazipunguwi bali huzidi. Ni kweli kabisa kuwa chimbuko la hisani zako hazishi. Upaji wako ni upaji wapendeza sana. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake, tuandikie ujira mfano wa ujira wa mwenye kuufunga au amekuabudu ndani yake mpaka siku ya Kiyama.
Oh Allah! Hakika twatubu kwako siku ya kwanza ya kufuturu kwetu ambayo umeifanya kwa waumini kuwa ni Idi na furaha. Na kwa watu wa mila yako wakati wa mkusanyiko na mjumuiko kutokana na kila dhambi tumeitenda au ovu tumelitanguliza, au fikra ya shari tumeificha iwe toba ya asiyeficha dhamira ya kurudi kwenye dhambi wala harejei baada yake kwenye makosa. Toba ya nasuha iliyeepukana na shaka na wasiwasi. Ikubali kutoka kwetu tu iridhiye tuimarishe juu yake. Oh Allah! Turuzuku kuogopa adhabu za kamio na shauku ya thawabu iliyo ahidiwa ili tuipate ladha ya kile tukuombacho kwa ajili yake na huzuni ya tukuombeacho kimbilio kwa ajili yake. Tujaaliye tuwe miongoni mwa walio tubu kwako. Ambao umewajibisha mapenzi yako. Oh! Umwadilifu mno wa waadilufu, Oh Allah! Wavumilie baba zetu na mama zetu na watu wote wa Dini yetu waliotangulia kati yao na watakaopita mpaka siku ya Kiyama. Oh Allah! Mrehemu Muhammad Nabii wetu na Aali Zake kama ulivyowarehemu malaika wako waliokurubishwa. Na umswali yeye na Aali zake. Kama ulivyowasalia Manabii wako wajumbe. Mswaliye yeye na Aali zake kama ulivyowasalia waja wako wema na bora zaidi kuliko hivyo Ewe Bwana wa Ulimwengu Swala Baraka zake zitufikie. Nafu yake ihifike, kwayo DU'A zetu zijibiwe. Hakika wewe u umkarimu mno wa waombwao. Na umtoshelezaji mno wa wanaotegemewa. Na umpaji mno wa waombwao fadhila yake. Na u muweza juu ya kila kitu.
Akimaliza kusali husimama kuelekea Qibla na siku ya Ijumaa husema: Ewe! Unayemrehemu asiyerehemewa na waja. Ewe ambaye humkubali asiyekubaliwa na nchi. Ewe ambaye hawadharau wenye haja kwake. Ewe ambaye hamtowi matumaini mwenye kumsihi sana. Ewe ambaye hawakabili kwa kutowakubalia wenye msimamo mgumu kwake. Ewe ambaye akusanyae kidogo apewacho na ashukurue kidogo atendewacho. Ewe ashukuruye kidogo na hulipa kikubwa. Ewe ambaye humsogelea kwa amwendaye karibu yake. Ewe ambaye humwita kwake mwenye kumtumbia mgongo! Oh we! ambaye haibadilishi neema wala aharakii kulipizi. Oh We! ambaye huzalisha jema ili likuwe na hufumbia macho ovu ili asamehe hurudi tumaini kutoka kwake na haja yake bila kufikia uelewa na kiwango cha ukaribu wako. Vyombo vya haja vimejaa upaji wako sifa zimeshindwa kufikia sifa zako katika kukusifu. Ujuu wa juu kabisa ni wako uko juu kabisa kuliko kila aliyejuu. Utukufu mkubwa kabisa juu ya utukufu wote. Kila mtukufu kwako ni mdogo kila kitukufu kwenye utukufu wako ni kinyonge. Wameshindwa kupata waya tarajiayo wa mwenoeaye asiyekuwa wewe. Wamehasirika wajipelekao mbele isipokuwa kwako. Wamepotea wakaao ispokuwa na wewe wamekuwa wa kiwa wenye kukimbilia isipokuwa waliokimbilia fadhila zako. Mlango wako uko wazi kwa waronga - Rongao. Upaji wako kwa ajili ya waombao msaada wako ukaribu na waombao msaada. Wenye matumaini hawa katishwi tamaa wajiletao kwako hawatokwi na matumaini na upaji wako. Hawapatwi na hali mbaya kwa ajili ya lipizi lako wenye kuomba ghofirani.
Riziki yako imekunjuka mpaka kwa wanaokuasi. Huruma yako ya mwendea akupingaye, tabia yako ni kuwatendea hisani waovu desturi yako kuwabakisha wachokozi, mpaka kuwangojea kwako kumewadanganya wasirejee. Kuwapa kwako muhla kunawazuia kukoma. Hakika hukuwafanyia haraka ili warudi kwa amri yako. Mwenye kuwa miongoni mwa wema mulihitimishia. Na mwenye kuwa miongoni mwa anayestahiki hali mbaya wa mwacha bila msaada wako wote hao watakuwa kwenye hukumu yako, na mambo yao yazuilika na amri yako. Mamlaka yao hayadhoofiki kwa muda wao mrefu wote. Dalili yako haikuvunjwa kwa kuacha kuwaharakia! Hoja yako ipo haivunjwi, na ufalme wako uko thabiti haitoweki. Ole wake yule atakayeelemea mbali na wewe. Kuachwa kusiko kuwa na msaada ni kwa yule mwenye kuachwa na wewe shakawa iliyo mbaya sana ni ya aliye danganyika nawe. Atafanyaje ndani ya adhabu yako? Mahangaiko yake marefu yaliyoje ndani ya adhabu yako? Upeo wake wa faraja umbali ulioje? Kukatishwa tamaa kwake kulioje na urahisi wa kutoka? Ni uadilifu kutokana na uamuzi wako hudhulumu katika maamuzi.
Ni usawa wa hukumu yako huwezi muonea. Umesaidia hoja na kuzijaribu nyudhuru. Ulianza na tishio. Umekuwa mpole katika kuhimiza na umefanya mifano. Na umerefusha kutoa muhla. Umechelewesha ukiwa muweza wa kufanya haraka. Umefanya bila haraka hali ukiwa umejaa haraka. Kutoharakia kwako hakukuwa kwa sababu ya kushindwa, wala kutoa muhla kwako ni unyonge wala kujiziwia kwako si mghafala. Wala kungoja kwako si upendeleo, bali ili hoja yako iwe yenye nguvu zaidi na ukarimu wako uwe kamili na ihsani yako iwe ya kutosha. Neema zako ziwe timilifu. Yote hayo yamekuwa na yangali yataendelea kuwa haitokoma. Hoja yako ni kubwa mno kuliko vile vya weza kuelezwa yote. Utukufu wako uko juu zaidi hauwezi kufanyiwa mipaka kwa kiini chake. Neema zako nyingi haziwezi kuhesabiwa zote. Hisani zako nyingi kuliko vile zishukuruwe hata kwa kiasi chake kidogo. Ukimya umenifanya nishindwe kukuhimidi. Kujizuiya kumenifanya nishindwe kukutukuza. Niwezalo kulifanya ni kukiri kushindwa kwangu. Si kwa kupenda Ewe Mola wangu! Bali ni kutoweza, Mimi ni huyu hapa naja tena mbele yako. Nakuomba usaidizi mwema. Mrehemu Muhammad na Aali zake. sikiliza mnong'ono wangu. Kubali duwa yangu, wala usiihitimishe siku yangu kwa kukatishwa matumaini. Wala usinikabili kwa kurudisha ombi langu bila jibu. Uheshimu utokaji wangu kwako. Marejeo yangu ni kwako. Hakika wewe hudhikiki na ulipendalo. Na si mshindwi wa uombwalo We u muweza juu ya kila kitu. Hapana hila wala nguvu isipokuwa kuwezeshwa na Allah Mtukufu mkubwa.