12%

10

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S) KATIKA KUJIKINGA NA VITIMBI VYA MAADUI NA KUONDOWA MACHUNGU YAO

Mola wangu uliniongoza nikabeuwa. Uniwaidhi moyo wangu ukawa mgumuUlinitaribu kwa uzuri nimeasi. Baadaye nilitambuwa uliyo amrisha uliponitambulisha. Nikaomba ghofirani ukaondowa nikarudia ukasitiri. Zako Mola wangu ni sifa njema. Nimetosha katika bonde za kuangamiza nimejiweka kwenye hatari ya dhahbu zako na ni mashukio ya adhabu zako. Njia yangu kwako ni Tawheed. Nasababu zangu za kufika kwako ni kuwa sija kushirikisha na kitu chochote sijaambatanisha pamoja na wewe Mungu nimekimbilia kwako na nafsi yangu. Kwako ndio kimbilio la mtenda maovu aliyepoteza hadhi ya nafsi yake na kuomba kimbilio. Kiasi gani cha aduwi amechoomowa kwa ajili yangu upanga wa uaduwi wake! Na amechongowa makali ya ncha ya upanga wake kwa ajili yangu! Na kunowa kwa ajili yangu bapa la makali yake. Ameichanganya sumu yake iuwayo kwa ajili yangu. Na kuelekeza kwangu mishale yake iliyonyooka irukayo. Wala halikulala jicho lake linichungalo. Na kisiri siri akakusudia kunifanyia makuruuhi. Ana nitakia mimi uchungu wa chuki yake umeona O Mungu wangu udhaifu wangu kuibeba mizigo mizito na kushindwa kwangu kupata ushindi dhidi ya aliyenikusudia kwa kupigana naye. Na upeka wangu mbele ya idadi kubwa ya aliye na uaduwi na mimi. Anivizia kwa balaa ambalo sikuliwazia fikrani mwangu.

Ulianza kunisaidia kwa nusura yako uliimarisha mgongo wangu kwa nguvu zako. Uliyafanya butu makali yake. Baada ya mkusanyiko mwingi umemfanya abakiye peke. Umekiinua kisigino changu juu yake na kumfanya aliyonilenga yamrudie ulimrudisha nyuma. Hakuzituliza ghadhabu zake. Hakukoza kiu chake. Ameuma kidole chake. Aligeuza mgongo na kukimbia mpango wake haukutimia. Ni mara ngapi mdhalimu amenifanyia udhalimu kwa vitimbi vyake amenitegea mtego wake. Akaniwekea uangalizi wa walinzi wake akaniwinda uwindaji wa mnyama mkali awindapo windo lake.

Naye unidhihirishia tabasamu ya mwenye kujipendekeza. Huku akiniangalia kwa ghadhabu kali ulipoona Ewe Mungu wangu! Umebarikiwa na umetukuka ubaya wa fikra zake za siri na ubaya wa aliyo nayo. Ulimtupa kichwa chini ndani ya shimo lake mwenyewe. Na umemtumbukiza katika maporomoko aliyochimba. Alidogeshwa dhahili baada ya kujitukuza kwake ndani ya tanzi la mtego wake ambao alipanga anione nimenasa humo. Kama si Rehema zako yangenifika yaliyomfika. Wangapi miongoni mwa hasidi amenisonga koo kwa maumivu makubwa sana. Kwa ukali wake amenihuzunisha amenikata kwa ncha ulimi wake alinifanyia kijicho heshima yangu ilikuwa lengo lake ili kuiharibu. Amenivisha utepe wa aibu ambao ungalipo. Amenifanyia vitimbi ameniknga na hila zake. Hivyo basi nikakuita Oh Mungu wangu nikiomba msaada kwako. Nikiwa na uhakika wa haraka ya jibu lako. Nikijua kuwa hatendewi vibaya mwenye kukimbilia kwenye kivuli cha hifadhi yako. Hatofadhaika mwenye kukimbilia kwenye ngome ya ushindi wako. Ukanihifadhi na ukali wake kwa uwezo wako. Kiasi gani cha mawingu makuruhi umeniondolea mbali. Na mawingu ya neema umenyeshesha rehema zake juu yangu. Vijimto vya rehema umevitiririsha na halki njema umenivika nayo macho ya misiba umeyapofowa. Mfululizo wa mfuniko wa majonzi umeitanduwa. Dhana nzuri ngapi umeithibitisha na ukosefu umesawazisha ugonjwa umeuponya. Umasikini umeubadilisha. Yoote hayo ni neema na ufadhili kutoka kwako. Na katika hali yoote hiyo umeendelea ushupavu kutoka kwangu wa kukuasi. Matendo yangu maovu hayatakuzuiya kutimiza ihsani ufanyayo.

Hakika uliombwa ukatowa usipo ombwa ulianza (kutowa) uliombwa ufadhili wako haukutowa kwa unyimivu. Umekataa Oh Mungu wangu isipokuwa kufanya ihsani na ufadhili na kuneemesha. Nimekataa kila kitu isipokuwa kujitosa katika yaliyoharamisha. Na kuvuka mipaka yako. Na kutotiliya mananni makamio yako. Yako ni sifa njema Oh Mungu wangu! muweza asiye shindwa. Na saburi hafanyi haraka. Hiki ni kisimamo cha mwenye kutambuwa wingi wa neema na umeikabili kwa kiwango cha chini ya vile inavyobidi. Na amejishuhudiya binafsi kutowajibika. Oh Allah mimi najikurubisha kwako kupitia daraja ya juu ya Muhammad na kwa mwanga wa daraja ya juu ya Aali. Naelekea kwako kupitia wao wawili unilinde kutokana na shari fulani na fani. Hakika hayo hayakutii dhiki katika utajiri wako. Wala haikupi taabu katika nguvu zako na wewe ni muweza juu ya kila kitu. Basi nipe Oh Mungu wangu katika rehema zako na taufiki yako ya kudumu ambayo nitaifanya ngazi niipandayo ili kuifikia ridhaa yako. Ili niwe na amani mbali na adhabu yako. Oh Mwingi wa rehema kuliko wote wenye kurehemu.

NA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA HALI YA WOGA

Oh Allah hakika wewe umeniumba katika hali sawa bila dosari. Umenikuza nilipokuwa mdogo, uliniruzuku vya kutosha. Oh Allah hakika mimi nimekuta katika uliyoteremsha kitabuni mwako na umewabashiria hayo waja wako umesema: Oh! Waja wangu ambao wamezifuja nafsi zao, musikate tamaa na rehema za Allah. hakika Mungu hughofiria dhambi zote. Na yametangulia toka kwangu katika uliyoyajuwa na ambayo wewe ni mjuzi zaidi kuliko mimi. Aibu iliyoje kwa yale ambayo kitabu chako kimeyahifadhi dhidi yangu. Lau kama si sehemu ambazo nina matumaini ya msamaha wako ambao umeenea kila kitu ningejitupa chini (nikikata tamaa). Lau kama yeyote angeweza kumkimmbia Mola wake ningekuwa na haki zaidi ya kukukimbia. Na wewe hakifichiki kwako chenye kujificha kiwe ardhini au mbinguni ila utakileta. Wewe ni mwenye kujaza tosha na wewe ni mhasibu tosha. Oh Allah! hakika wewe utanitafuta endapo nitakimbi utanipata endapo nitapiga mbio hivyo basi mimi ni huyo ni mbele yako mnyenyekevu dhalili mwenye kujitweza. Ukiniadhibu ninastahiki, nayo Oh! Mola wangu ni uadilifu kutoka kwako. Na ukinisamehe toka zamani nimeingizwa katika msamaha wako. Na umenivika hali njema yako. Hivyo basi nakuomba Oh Allah! kwa majina yako yaliyo katika hazina na kwa utukufu wako uliyo nyuma ya pazia, ikiwa hautoihurumia nafsi hii yenye mashaka na hii mifupa iliyo sumbuka ambayo haiwezi joto la jua lako, itawezaje joto kali la moto wako ambayo haiwezi kuvumilia sauti ya radi yako. Vipi itaweza kuivumilia sauti ya ghadhabu yako. Hivyo basi nihurumie. Oh Allah! mimi ni mtu mnyonge, thamani yangu ndogo, kuniadhibu kwako hakuuzidishii ufalme wako uzito hata kama ule wa chembe ya vumbi.. Lau kama kuniadhibu kwako mimi kungezidisha chochote katika ufalme wako, ningekuomba niiivumiliye (adhabu), na ningependa iwe yako. Lakini mamlaka yako Allahumma ni Mtukufu mno, na ufalme wako ni wa kudumu mno kuliko ule wa kuongezwa na utii wa watii au upunguzwe na maasi ya watenda dhambi. Nihurumiye Ewe mwenye rehema zaidi ya woote wenye kurehemu. Nivumiliye Ewee mwenye enzi na ukarimu. Nirejelee, hakika wewe ni mwingi wa kukubali toba mwenye huruma kuliko wote.

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUSIHI NA KUNYENYEKEA

Oh Mungu wangu nakuhimidi na wewe ni mwenye kustahiki kuhimidiwa, kwa ihisani yako kwangu, na wingi wa neema zako kwangu, na kwa wingi wa utowaji wako kwangu, na kwa uliyonifadhili katika rehema zako. Umenikamilishia neema zako.Umenitendea mema kwa kiwango nashindwa kutekeleza shukurani yake. Lau kama si ihisani yako kwangu, na wingi wa neema zako kwangu, nisingeifikia hadhi yangu, wala nisingeiweka nafsi yangu sawa. Lakini wewe ulianza kunihisani na uliniruzuku vya kutosha katika mambo yangu yote. Uliniondolea taabu ya balaa. Uliziwiya kwa ajili yangu maamuzi yako yakuogofya.

Mungu wangu, balaa ngapi zitaabishazo umeniondolea. Neema ngapi za ukarimu umeniletea karibu. Matendo yako mangapi ya ukarimu kwangu! Wewe ndiye ambaye ulinijibu wakati wa dharura ombi langu. Na ulidogesha nilipojikwaa mtelezo wangu na ulinichukulia kutoka kwa maaduwi niliodhulumiwa. Oh! Mungu wangu sijakukuta bakhili nikuombapo. Wala mwenye kujikunja nilipo kutaka, bali nilikukuta mwenye kusikiliza DU'A yangu. Na mpaka wa matakwa yangu. Nimekuta neema zako kwangu nyingi. Katika kila jambo miongoni mwa mambo yangu. Na kila zama katika zama zangu wewe kwangu ni mwenye kuhimidiwa na matendo mema yako kwangu yenye kuheshimiwa. Nafsi yangu, ulimi wangu, akili yangu, vya kuhimidi himidi ifikiye tekelezo na hakika ya kushukuru. Himidi iwe kiwango cha ridhaa zako kwangu. Niokowe toka kwenye makasiriko yako. Oh! Mwokozi wangu nijikwaapo, lau si kama sitara yako aibu yangu, ningekuwa miongoni mwa wenye kufedheheka. Oh! Muungaji wangu mkono kwa msaada kama si msaada wako kwangu ningekuwa miongoni mwa wenye kushindwa. Oh! We ambaye wafalme wamemwekea kongwa ya udhalili shingoni mwao wakiogopa adhabu zake.

Oh! Mwenye stahiki ya kutukuzwa. Oh! Mwenye majina mema. Nakuomba unisamehe na unighofiriye siko mweupe bila dhambi, ili niweze kutowa udhuru. Wala sina nguvu, niwe na weza kupata ushindi wala sina kimbilio niweze kukimbilia. Ninakuomba uniokowe toka kwenye kujikwaa kwangu. Najitenga mbele yako na dhambi zangu ambazo zimeniweka pabaya na zimenizunguka na kunihilikisha. Kutokana nazo nimekimbilia kwako Mola wangu mwenye kutubu nikubaliye toba yangu. Najikinga kwako nipe kinga. Nikiomba hifadhi usiniache. Nikiomba usininyime. Nikishikilia usiniache. Nikiomba usinirudishe mikono mitupu. Nimekuomba Ewe Mola wangu niko hali mbaya mnyonge. Mwenye hofu mwoga. Mwenye kutapatapa fakiti. Nimedharurika kwako. Nakulalamikia Ewe Mola wangu, udhaifu wa nafsi yangu kutoharakia kwenye kile ulichowaahidi marafiki zako. Nakujiepusha na ulicho wahadharisha maadui zako. Na kukithiri mayonzi yangu na wasiwasi wa nafsi yangu. Mola wangu hujanifedhehesha kwa ajili ya fikra zangu za siri, wala hujanihilikisha kwa maovu yangu, nakuita wanijibu japo nipo goigoi unaponiita. Nakuomba nipendapo haja zangu. Popote niwapo naweka siri zangu kwako. Simwombi yeyote bali ni wewe tu. Simtumainii yeyote asiyekuwa wewe. Labeika Labeika. Wamsikia anayekunung'unikia, wampokea akutegemeaye. Wamwokoa mwenye kuomba hifadhi kwako. Wamfariji akimbiliyae kwako. Mola wangu usininyime mwisho mwema na mwanzo mwema kwa uchache wa shukrani wangu. Nighofirie ujuayo katika dhambi zangu. Ukiadhibu ni kwa kuwa mimi ni dhalimu, mzembe, mwenye kupuuza, mwenye dhambi, mwenye kuachwa mvivu. Mwenye kughafirika na hisa yake binafsi. Ukinisamehe ni kwa sababu wewe ni mwenye huruma mno kuliko wenye huruma wote.

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUMSIHI ALLAH (s.w.t)

Oh Allah! ambaye hakifichiki kitu chochote kwake katika ardhi au mbinguni. Vipi kifichike kwako Ewee Mola wangu ambacho wewe umekiumba? Vipi usijuwe idadi ya ambacho wewe umekiumba! Au vipi kisionekane kwako ambacho wewe wakimiliki. Oh Allah! Hapana kirudishacho ghadhabu zako isipokuwa huruma zako. Wala kiirudishacho kasiriko lako ispokuwa msamaha wako. Wala hakuna atowaye kimbilio la kuepuka adhabu ila ni Rehema zako. Hakuna kitakachoniokoa kutoka kwako isipokuwa kunyenyekea kwako mbele yako. Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad na utupe kutoka kwako Ewe Mola wangu Faraja kwa nguvu ambazo kwayo wa Huisha wafu wa waja. Na kwayo unarudisha uhai wa wafu na wala usinihilikishe Ewe Mola wangu katika majonzi kabla hujanijibu na kunijulisha jibu katika duwa yangu. Nionjeshe utamu wa kuwa na hali njema mpaka mwisho wa muda wangu. Usimpe fursa kunisimanga aduwi yangu, wala usiiweke shingo yangu chini ya uwezo wake usimpe mamlaka juu yangu. Oh Mungu! Wangu ukiniinuwa ni nani atanitweza? ukinitweza ni nani ataniinuwa? Ukinipa heshima ni nani atakayenidunisha ukinidunisha ni nani atakayenipa heshima? Ukiniadhibu ninani atakayenihurumia? Ukinihilikisha ni nani atakayekupinga katika mja wako au akuulize kuhusu mambo yalee? Nijuavyo ni kwamba hapana dhulma katika hukumu yako, wala haraka katika malipizi yako. Kwa kuwa hufanya haraka aogopaye kukosa na ni hakika kabisa kuwa aihitajie dhuluma ni yule ambaye ni dhaifu. Na hakika umetukuka Ewe Mola wangu! Umbali na hayo utukufu wa juu kabisa. Oh Allah mrehemu Muhammad na Aali wake. Usinifanye kuwa shabaha ya mabalaa wala nisiwe lengo la kisasi chako nipe muda nipe raha. Niondoshee kujikwaa kwangu Watambuwa udhaifu wangu na uhaba wa hila yangu na maombi yangu kwako. Na maombi yangu kwako na jikinga kwako Oh Allah dhidi ya ghadhabu yako hii leo. Mrehemu Muhammad na Aali wake ni kinge na kuomba amani ili niwe mbali na adhabu yako. Mrehemu Muhammad na Aali wake, na unipe amani. Nakuomba mwongozo basi mrehemu Muhammad na Aali wake na ni ongoze. Naomba kwako msaada basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unisaidiye na kuomba rehema, basi mrehemu Muhammad na aali wake na unirehemu. Nakuomba kujitosheleza basi mrehemu Muhammad na Aali wake na unitosheleze. nakuomba riziki basi mrehemu Muhammad na Aali wake na uniruzuku. Nakuomba mssada basi mrehemu muhammad na Aali wake na unisaidie. Nakuomba msamaha kwa yaliyopita katika dhambi zangu mrehemu Muhammad na Aali wake na unisamehe. Nihifadhi basi mrehemu Muhammad Na Aali wake na unihifadhi. Kwa kuwa sitorudia kitu ulichokichukia kutoka kwangu ukipenda hivyo. Yaa Rabbi yaa Rabbi Oh Mola wangu! Oh Mola wangu! Yaa Hannaan yaa Hannan mpenda wote ya Dhal-Jalaal Wal-Ikram Oh Mwenye Ufalme na ukarimu.Mrehemu Muhammad na Aali zake na nijibu kwa yote niliyokuomba na nimeyataka kutoka kwako na nilio kulondea agiza, gadiria, nihukumiye nipitishiye. Nipe kizuri katika ukipitishacho, nibariki nacho. Nifadhili nacho, Nifanye niwe na furaha na unipacho nizidishie fadhila zako na wasaa kwa uliyo nayo. Kwani wewe ni mwenye wasaa mpaji na unganisha hayo na heri ya Ahera na Neema Zake. Ewe Mwenye Rehema sana miongoni mwa wenye kurehemu (hapo omba upendayo na utamsalia Mtume Muhammad na Ahli wake mara 1000 elifu moja. Hivi ndivyo alivyokuwa afanya amani iwe juu yake).

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUJIDHALILISHA KWA MUNGU MWENYE ENZI MTUKUFU

Oh Mola wangu zimeninyamazisha dhambi zangu maneno yangu yamekatika sina hoja nimekuwa mateka wa balaa yangu. Niko rehani kwa matendo yangu. Mwenye kutaradadi katika makosa yangu nimechanganyikiwa katika makusudio yangu. Nimezuilika. Nimejikwamisha binafsi mahali pa madhalili wenye dhambi. Mahali pa wenye hali mbaya wanaothubutu dhidi yako, ambao waifanyao ahadi yako nyepesi. Sub'haanaka-utakatifu ni wako. Ni ufedhuli ulioje nimekufanyia! Kudanganyika gani nimejidanganya nafsi yangu Mola wangu uhurumiye mtelezo wangu ulioniweka fudi fudi. Na kuteleza kwa nyayo yangu nitendee kwa upole wako kulingna na kutojuwa kwangu. Na kwa ih'sani yako juu ya uovu wangu. Mimi ni mwenye kukiri dhambi yangu.Mwenye kutambuwa makosa yangu. Huu mkono wangu na paji langu la uso. Najitoa kwa malipizi nafsi yangu, zihurumie mvi zangu na kwisha kwa siku zangu. Na kukurubia muda wangu, udhaifu wangu taabu yangu, na uchache wa hila yangu Mola wangu nihurumie pindi athari yangu ikatikapo duniani. Na kufutika kwa viumbe utajo wangu nikawa miongoni mwa waliosahaulika kama ambaye amekwisha sahauliwa. Mola wangu nihurumie libadilikapo umbo langu na hali yangu uozapo mwili wangu na kutawanyika viungo vyangu. Oh! mghafala ni wangu kwa yaliyotakiwa kwangu. Oh Mola wangu! nihurumie siku ya kukusanywa kwangu na kufufuka kwangu. Jaalia siku ile kisimamo changu niwe pamoja na mawalii wako. Matokeo yangu yawe pamoja na wapenzi wako. Makazi yangu yawe karibu yako. OhMola wa ulimwengu.