50%

AKIDA

MSAMIATI

Adilisha: tendea haki, wema na uadilifu.

Daawa: utangazaji wa mafundisho ya dini ya Kiislamu;

Tablighi: Uhubiri.

Mwanadaawa: mtu anayetangaza mafundisho ya dini ya Kiislamu;

Mubalighi; mhubiri.

Dhahania: mawazo.

hasi: -a kukana; -a kinyume kabisa.

Irfani: mafundisho au imani inayohusiana na maarifa ya hakika ya Mwenyezi Mungu yapatikanayo kwa njia ya mtu kujisahau nafsi yake na kumwabudu Mwenyezi Mungu tu; usufii; uwalii.

Maada: asili au dhati ya kila kitu; meta.

Maadili: (elimu inayohusiana na) tabia njema au mwenendo sahihi wa mtu; akhlak.

Hekima, kauli; fani ya utumiaji wa akili.

Maono: fikra, ufahamu au uonaji wa kimoyomoyo (wa dini moja au mfumo mmoja wa kiitikadi) juu ya ulimwengu mzima,viumbe na vitu; nadharia.

Metafizikia: elimu ihusikanayo na asili ya mwanzo wa uhai, Uungu, n.k.

Nara: matamko mafupi au mwito maalum wa kikundi cha watu, chama au dini ambao unatolewa aghlab katika medani za vita, mikutano, misafara, n.k. kwa lengo la kutia shime, kuhamasisha au kutangaza shabaha yake, n.k. Pia shaari.

Radiamali: jambo au kitendo kinachofanywa kurudia kitendo fulani kilichotendewa.

Shaari:taz.nara.

Shirki: hali ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na kiumbe au kitu chochote katika ibada, uumbaji na tadbiri Yake ya ulimwengu; ushirikina.

Stadhaafika:kuwa katika hali ya kukandamizwa kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni.

Ustadhaafu: hali ya kustadhaafika.

Mustadhaafu:(wastadhaafu/mustadhaafina): mtu mwenye kukandamizwa kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni; mnyonge; mwenye kudhoofishwa au kustadhaafishwa.

Takabari (stakabari); fanya jeuri au kiburi na kuona wengine si kitu; kandamiza watu kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni. Utakabari (ustakabari): hali ya kutakabari au kustadhaafisha. Mtakabari/mstakabari (watakabari/ was-takabari): mtu mwenye kukandamiza watu kiuchumi, kisiasa, kiitikadi au kitamaduni.

Taghuti:(ma-) kitu au kiumbe ambacho ni sababu ya uasi au uvunjaji wa sheria za Mwenyezi Mungu, k.v. miungu, masanamu, mashetani, viongozi madhalimu, utawala wa haramu, n.k.; mtu yeyote anayefuatwa bila ya idhini ya Mwenyezi Mungu; mtu anayependelea mambo yenye kukiuka mipaka (sheriaya Mwenyezi Mungu).

Tasnifu: ithibati (thesis).

Tawhidi:Umoja na Upweke wa Mwenyezi Mungu katika dhati, sifa, vitendo na ibada Zake.