1. Elimu ni nini?
2."Sema, Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.. ." (39:9) Ni kwasababu gani wanaojua hawawi sawa na wasiojuwa?
3. Unatoa maoni gani iwapo wanaojua na wasiojua wakawa sawa kiutendaji?
4. Toa maelezo yenye ushahidi wa Qur-an kuonyesha kuwa:
(a) Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa binaadamu na Mola wake.
(b) Kutafuta elimu ni amri ya kwanza kwa binaadamu.
5. Onyesha kwa ushahidi wa Qur-an kuwa katika Uislamu mgawanyiko wa elimu katika "elimu ya dini" na "elimu ya dunia" haukubaliki.
6."Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba." (96:1)
Kusoma kwa jina la Mola wako maana yake nini?
7. "....Soma na Mola wako ni karimu sana.Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu.Amemfundisha mwanaadamu mambo aliyokuwa hayajui". (96:3-5)
Orodhesha njia tano anazozitumia Allah (SW) katika kuwasiliana na wanaadamu.
8. Elimu yenye manufaa kwa binaadamu ni ile.................................
9. Eleza sababu tatu zinazopelekea elimu kupewa nafasi ya kwanza katika Uislamu.