6%

ZOEZI

1. Elimu ni nini?

2."Sema, Je wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.. ." (39:9) Ni kwasababu gani wanaojua hawawi sawa na wasiojuwa?

3. Unatoa maoni gani iwapo wanaojua na wasiojua wakawa sawa kiutendaji?

4. Toa maelezo yenye ushahidi wa Qur-an kuonyesha kuwa:

(a) Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa binaadamu na Mola wake.

(b) Kutafuta elimu ni amri ya kwanza kwa binaadamu.

5. Onyesha kwa ushahidi wa Qur-an kuwa katika Uislamu mgawanyiko wa elimu katika "elimu ya dini" na "elimu ya dunia" haukubaliki.

6."Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba." (96:1)

Kusoma kwa jina la Mola wako maana yake nini?

7. "....Soma na Mola wako ni karimu sana.Ambaye amemfundisha mwanaadamu kwa kalamu.Amemfundisha mwanaadamu mambo aliyokuwa hayajui". (96:3-5)

Orodhesha njia tano anazozitumia Allah (SW) katika kuwasiliana na wanaadamu.

8. Elimu yenye manufaa kwa binaadamu ni ile.................................

9. Eleza sababu tatu zinazopelekea elimu kupewa nafasi ya kwanza katika Uislamu.