20%

15

MAFUNZO 150 KWA MAISHA BORA

SOMO LA 14 1: LITABAKIA JINA TU KUTOKEA ISLAM

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Itawafikia watu zama ambapo herufi na maandishi kutokea Qur'an Tukufu na jina kutokea Islam yatakuwa yamebakia miongoni mwao. Misikiti ya Waislamu itakuwa ikiimarishwa kimajengo lakini yatakuwa yameteketea kwa mtazamo wa mwongozo na hidaya. 146

Maelezo mafupi: Sisi hatuwezi kusema kuhusu ubashiri huu wa kiajabu iwapo umekwisha dhihirika siku hizi au itahusika maishani mbele, lakini kwa hakika sisi tunashuhudia baadhi ya mifano yake hapa na pale na inashangaza kuwa Waislamu wanalalamikia kurudi nyuma kama kwamba kwao jina la Islam na mapicha ya Qur'an Tukufu tu vinatosha. Wao kamwe hawakuitumia Qur'an Tukufu kama ni Kitabu kifundishacho kwa ajili ya kumwelimisha mwanadamu na wala hawakuichukulia Islam kama ni shule yenye mpango wa kufundishia kiakili na kimatendo. Je wewe umeshashuhudia jamii halisi ya Kiislamu ambayo imerudi au kubakia nyuma au jamii ambayo haikutukuzwa au kuheshimiwa ulimwenguni ?

SOMO LA 14 2: KUTAMBUA UWEREVU NA UJAHILI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Ulimi ni utambulisho wa kukadiria kiasi cha ujahili na kupima uwerevu na busara. 147

Maelezo mafupi: Kwa hakika ulimi ni dirisha muhimu la nafsi na utu wake na kupima upeo wa fahamu za kila mtu. Ulimi ambao hufunua pazia kwa kupitia mizunguko yake ya kawaida na hivyo hudhihirisha vile ilipo na ilivyo nafsi ya mtu. Kwa misingi hii, mafunzo mengi mno ya Dini ya Islam yanazungumzia na kusisitiza usahihishwaji wa ulimi na maonyo na tahadhari zinakaa zikitolewa na hata viongozi wetu na ingawaje kusahihishwa kwa kikamilifu kwa ulimi hauwezekani bila ya kuirekebisha nafsi na akili na fahamu, lakini sisi tunaweza kudhibiti matokeo yanayoumiza kwa kutokwenda kwa ulimi katika mkondo sahihi kwa kukaa kimya au kujidhibiti na hiyo ndiyo njia ya kujiepusha na maovu yatokanayo na ulimi.

SOMO LA 14 3: ZAIDI YA NEEMA

imam hadi(a.s.) amesema:

"Yeyote yule anayeshukuru msaada, kuneemeka kwake kwa kushukuru kwake ni zaidi ya neema kwa ajili ya msaada, kwa sababu misaada ni mambo ya maisha ya humu duniani na shukurani ni mtaji wa humu duniani na Aakhera." 148

Maelezo mafupi: Tukichukulia ukweli huu kuwa shukrani si shukrani kwa mdomo tu, bali ni shukrani kwa uhakika na vile vile kwa kutumia msaada mahala panapostahiki, basi hapo ndipo inasemwa kuwa shukrani kwa msaada ina matokeo katika neema na mali yake kiasi kwamba msaada wenyewe si jambo kubwa kwa kulinganishwa nayo. Kwa kutumia misaada kwa uridhisho wa Allah swt na mahitaji ya waja Wake kwa hakika ni rasilimali na mtaji mkubwa kwa kuheshimika humu duniani na vile vile kwa neema kubwa huko Aakhera, wakati ambapo msaada unaweza kuwa ni neema cha kitu tu. Hivyo, shukurani ina thamani zaidi na zaidi ya msaada wenyewe.

SOMO LA 14 4: KUHUISHA SIRA ZA MA'ASUMIIN A.S.

Al-Imam 'Ali ar-Ridha (a.s) amesema:

Yeyote yule akaaye katika kikao au mkusanyiko ambapo huisha sira zetu, basi moyo wake hautakufa pale patakapo kufa nyoyo zingine. 149

Maelezo mafupi: Inafahamika wazi wazi kutokana na kauli ya hapo juu kuwa wajibu mkuu wa lazima juu ya wafuasi wa Ahlul Bayt(a.s) ya wananyumba ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni kuhuisha katika mikutano na mikusanyiko yao, kwa kujua imani na akida zao, kuelewa maana na ujumbe halisi kutokana na kauli na semi zao na kujizoesha na kufuata maamrisho yao na ni kusema kwamba mikutano na mikusanyiko yao iwe daima ni mikutano ya kusahihishana na kuwa tayari kwa maisha vile ipasavyo, na wala isiwe mikutano na mikusanyiko yao kwa ajili ya kuupoteza muda kwa starehe tu, kujiombea maslahi yao ya kibinafsi na kujifikiria mwenyewe na matatizo yake mwenyewe na matakwa yake mwenyewe bila kujali maslahi ya binadamu wengineo, imani na jamii kwa ujumla. Kwa hakika iwapo mikutano na mikusanyiko itakapokuwa vile tulivyofundishwa na Ahlul Bayt(a.s) basi nyoyo zetu zitahuika na vile vile fikara zetu zitakuwa njema zenye kuzaa matunda.

SOMO LA 14 5: SIRI NI AMANA

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati mtu asemapo jambo lolote na kujitazama mwenyewe, basi mazungumzo yake hayo ni amana na siri kwetu (na inatubidi sisi kuitunza). 150

Maelezo mafupi: Kuamini katika Dini ya Islam ina sura nyingi, ikiwemo uaminifu katika kuweka na kutunza siri za watu. Jambo ili lina umuhimu mno katika Dini ya Islam kiasi kwamba kutoa siri za watu kumesemwa kuwa ni mojawapo ya Madhambi Makuu. Kwa ajili ya kutaka kuthibitisha jambo fulani kuwa siri, si lazima kwa msemaji kusema na kuomba na kusisitiza kuwapo kwa siri na kuitunza kwake. Na badala yake, ishara ndogo inatosheleza kuelewa uhakika huu. Iwapo mtu akijitazama mwenyewe na kujichambua mbele ya mtu mwingine basi inatosheleza kwake yeye kuweka mazungumzo ya ndugu yake Mwislamu kama siri yake.

SOMO LA 14 6: ALAMA ZA IMANI YA DINI YA ISLAM

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati matendo yako mema yanapokufurahisha na matendo yako maovu yanapokuhuzunisha, basi wewe ni Mumin. 151

Maelezo mafupi: Dini ya Islam inasema kuwa kila mtu huzaliwa akiwa katika maumbile yaliyo halisi na safi, imani halisi na mapenzi ya mema. Maovu na maasi ndiyo yanayokuja kuathiri nafsi yake na kuibadilisha na kuigeuza kabisa. Hata hivyo, hadi pale mwanadamu anapokuwa akipenda mema na kuchukia mabaya, nafsi yake ya imani na hali ya uhalisi wake bado unakuwapo hai ndani mwake. Watu walio waovu ambao wanakuwa wamekerwa kwa matendo yao maovu, na hujisikia fahari katika hali hiyo na au wanapojitolea mhanga, uwema, usamehevu na uadilifu huwa ni kero kwao, kwa hakika wao ni makafiri.

SOMO LA 14 7: SHARTI LA KWANZA KWA AJILI YA KILA KAZI

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amemwambia Kumail ibn Ziyad:

Hakuna harakati wala kazi hadi pale utakapohitaji maarifa yake, uzoefu na elimu ya kutekeleza hivyo. 152

Maelezo mafupi: Iwapo sisi tutatafakari juu ya 'harakati zozote' zile, ndipo hapo sisi tutakuwa na uzoefu kwa mikakati na mipango ya Kiislamu na tutatambua hapo kuwa Dini ya Islam si mfuatilio wa 'ibada na dua tu na au inakosa mipango ya kimatendo. Badala yake inayo mipango na mikakati ya maisha ya mtu binafsi na vie vile masuala ya kijamii na vile vile hatua za maendeleo ya kibinadamu, jambo la kwanza ni akili na elimu ya uhakika. Islam inachukulia harakati na jitihada zote zisizo na matunda, ambazo zina elimu kidogo au mwongozo mdogo.

SOMO LA 14 8: UMUHIMU WA WAGENI

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) amesema:

Wakati Allah swt anapowatakia watu kheri na ukarimu, basi huwazawadia. Wao waliuliza: "Je ni zawadi ipi hiyo?" Kwa hayo Mtume (s.a.w.w) alijibu: "Mgeni." 153

Maelezo mafupi: Hayo ni ya kweli kabisa. Kwa hakika mgeni ni zawadi kutoka Allah swt , zawadi yenye heshima na thamani kubwa mno. Lakini katika ulimwengu ambamo mapenzi yote yameshapotea, mgeni hathaminiwi. Na badala yake ngeni anachukuliwa kusumbua na kutokupendwa. Hivyo, ni kwa nadra tu hutokea kwa mtu kumwalika mtu mwingine au kutembelewa isipokuwa kwa maada tu, kibiashara na uhusiano wa kisiasa. Wakati ambapo katika nchi za Kiislamu na familia ambazo bado utamaduni wa Kiislam upo hai, basi kwao mgeni huheshimiwa na kutukuzwa kama ni zawadi kutokea Allah swt hata kama hatakuwa na uhusiano wowote wa kijamaa pamoja nao.

SOMO LA 1 4 9: HESHIMA NA MAPENZI

Al-Imam Ja'afer as-Sadiq(a.s) amesema:

Yeyote asiyewaheshimu wakubwa na wala kuwahurumia na kuwapenda wadogo, basi huyo si miongoni mwetu. 154

Maelezo mafupi: Jamii za binadamu ni kama msafara mkubwa ambao daima upo katika mwendo. Watoto wachanga huzaliwa na mama zao, na watoto hao hukua na wakubwa huwa wazee na wazee hufa na hakuna mtu ambaye asiyepitia msafara huu. Humu ndani, watu wazima ndio kwa kawaida wanakuwa na uzoefu zaidi na kuwa na mtazamo wa undani zaidi na wamekuwa ndio vianzio vya huduma mbalimbali katika maisha yao lau wao wangalikuwa watu wenye kutuonya kuhusu matendo yetu iwapo ni mema au mabaya, na mahisabu yote yanaonyesha kuwa wao waheshimiwe na vijana na mabarobaro waelewe heshima zao.

Na kwa kuwa watoto bado ni wapya na mwazoni mwa maisha yao, lazima wapendwe na misingi ya ukuaji wao lazima ijengwe na wakubwa kwa moyo halisi, na kwa hakika hivyo ndivyo ilivyo njia na utamaduni wa kibinadamu na jamii inayoendelea kimaendeleo.

SOMO LA 150: JICHUKULIE NJIA HII KWA AJILI YAKO

Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema:

Chochote kile kutokea kheri utakachokituma, kitahifadhiwa kwa ajili yako, na chochote kile utakachokiahirisha wewe, kitawafaidia wengineo ( na uwajibisho huo utakuwa mzigo juu yako). 155

Maelezo mafupi: Mali na utajiri unapatikana katika ulimwengu wetu wa leo kuliko kabla ilivyokuwapo bila ya kujali madhumuni muhimu na falsafa ya mali. Wale ambao hulimibikiza mali kama vichaa, na ambao hawajali ni njia zipi za halali, haraamu, haki au kudhulumu, kamwe hawafikirii kuwa wao kamwe hawataambatana pamoja na mali yao, na wala kuila yote kwa pamoja. Kwa hakika mzigo mzito upo juu ya mabega ya wenye kuimiliki mali hiyo; kulimbikiza, kuiacha na kuondoka na hatimaye kubeba wajibu wote juu yao.