TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 11144
Pakua: 2126


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11144 / Pakua: 2126
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

Mwandishi:
Swahili

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

قَالُوا يَا نُوحُ قَدْ جَادَلْتَنَا فَأَكْثَرْتَ جِدَالَنَا فَأْتِنَا بِمَا تَعِدُنَا إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿٣٢﴾

32. Wakasema: Ewe Nuh! Umejadiliana nasi na umezidisha kutujadili basi tuletee unayotuahidi ukiwa ni miongoni mwa wakweli.

قَالَ إِنَّمَا يَأْتِيكُم بِهِ اللَّـهُ إِن شَاءَ وَمَا أَنتُم بِمُعْجِزِينَ ﴿٣٣﴾

33. Akasema: Mwenyezi Mungu atawaletea akipenda na wala nyinyi si wenye kumshinda.

وَلَا يَنفَعُكُمْ نُصْحِي إِنْ أَرَدتُّ أَنْ أَنصَحَ لَكُمْ إِن كَانَ اللَّـهُ يُرِيدُ أَن يُغْوِيَكُمْ هُوَ رَبُّكُمْ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٣٤﴾

34. Wala nasaha yangu haitawafaa kitu nikitaka kuwapa nasaha ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kuwapoteza. Yeye ndiye Mola wenu; na kwake mtarejeshwa.

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ قُلْ إِنِ افْتَرَيْتُهُ فَعَلَيَّ إِجْرَامِي وَأَنَا بَرِيءٌ مِّمَّا تُجْرِمُونَ ﴿٣٥﴾

35. Au wanasema ameizua? Sema: ikiwa nimeizua, basi kosa hilo ni juu yangu, na mimi sihusiki na makosa myatendayo.

EWE NUH UMEZIDISHA MAJADILIANO NASI

Aya 32-35

MAANA

Wakasema: Ewe Nuh! Umejadiliana nasi na umezidishi kutujadili basi tuletee unayotuahidi ukiwa ni miongoni mwa wakweli.

Nuh(a.s) alipowaziba mdomo watu wake kwa hoja na dalili, walipata dhiki na wakawa hawana pa kutokea, basi wakaona njia pekee, iliyobaki, ya upinzani ni kuomba adhabu.

Walipoiomba, Akasema: Mwenyezi Mungu atawaletea akipenda na wala nyinyi si wenye kumshinda.

Washirikina wa Makka walimwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu, kama walivyosema watu wa Nuh. Tazama Juz.9 (8:32).

Wala nasaha yangu haitawafaa kitu nikitaka kuwapa nasaha.

Mwenyezi Mungu alitaka kuwanasihi bali alikithirisha kuwanasihi, lakini kuna faida gani ikiwa nyoyo zimesusuwaa na wala hazipondokei kwenye uongofu,ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kuwapoteza.

Mwenyezi Mungu haumbi upotevu kwa mtu. Lau ingelikuwa hivyo basi angekuwa ameuondoa utu wake. Lakini desturi ya Mwenyezi Mungu, katika maumbile yake, imepitisha kuwa mwenye kufuata, njia ya upotevu, kwa matakwa yake, atakuwa katika wapotevu tu. Sawa na na aliyejinyonga kwa hiyari yake.

Ni kwa maana hii ndio ikafaa kunasibishwa upotevu kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t). Yametangulia maelezo katika Juz.11 (10:78) kifungu cha‘uongofu na upotevu’

Yeye ndiye Mola wenu; na kwake mtarejeshwa

Wala hakuna kuhepa kukutana naye, hisabu yake na malipo yake.

Au wanasema ameizua? Sema: ikiwa nimeizua, basi kosa hilo ni juu yangu, na mimi sihusiki na makosa myatendayo.

Dhahiri ya mfumo wa maneno inafahamisha kuwa dhamiri katika ‘wanasema’ inawarudia watu wa Nuh na uliozuliwa ni wahyi; kwa maana ya kuwa: Sema ewe Nuh kuwaambia watu wako: Ikiwa mimi ni mwongo wa ninayoyasema, kama mnavyodai, basi mimi peke yangu ndiye nitakayebeba majukumu na dhambi ni zangu na adhabu. Na ikiwa ninasema kweli, basi nyinyi ndio wenye majukumu, na adhabu ya kukadhibisha itawashukia peke yenu.

Insemekana kuwa Aya ii ni jumla ya maneno iliyoingia kati, katika kisa cha Nuh; na kwamba ilishuka kwa washirikina wa kiquraish, kwa sababu walimtilia shaka Muhammad(s.a.w.w) katika kuwaelezea kisa hiki. Ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha awaambie: Sio lawama lenu uzushi wangu, ni langu mimi peke yangu. Maana haya yenyewe yanafaa, lakini yako mbali na dhahiri ya maneno.

وَأُوحِيَ إِلَىٰ نُوحٍ أَنَّهُ لَن يُؤْمِنَ مِن قَوْمِكَ إِلَّا مَن قَدْ آمَنَ فَلَا تَبْتَئِسْ بِمَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ﴿٣٦﴾

36. Akaletewa wahyi Nuh kuwa hataamini katika watu wako isipokuwa yule aliyekwishaamini. Basi usisikitike kwa waliyokuwa wakiyatenda.

وَاصْنَعِ الْفُلْكَ بِأَعْيُنِنَا وَوَحْيِنَا وَلَا تُخَاطِبْنِي فِي الَّذِينَ ظَلَمُوا إِنَّهُم مُّغْرَقُونَ ﴿٣٧﴾

37. Na unda jahazi mbele ya macho yetu na kwa wahyi wetu wala usinizungumzie kuhusu wale waliodhulumu, hakika wao watagharikishwa.

وَيَصْنَعُ الْفُلْكَ وَكُلَّمَا مَرَّ عَلَيْهِ مَلَأٌ مِّن قَوْمِهِ سَخِرُوا مِنْهُ قَالَ إِن تَسْخَرُوا مِنَّا فَإِنَّا نَسْخَرُ مِنكُمْ كَمَا تَسْخَرُونَ ﴿٣٨﴾

38. Na akawa anaunda jahazi na kila wakimpita wakuu wa kaumu yake wakimkejeli. Akasema: Ikiwa nyinyi mnatukejeli, hakika nasi tutawakejeli, kama mnavyotukejeli.

فَسَوْفَ تَعْلَمُونَ مَن يَأْتِيهِ عَذَابٌ يُخْزِيهِ وَيَحِلُّ عَلَيْهِ عَذَابٌ مُّقِيمٌ ﴿٣٩﴾

39. Mtakuja jua ni nani itakayemfikia adhabu ya kumfedhehesha na itakaye mteremkia adhabu ya kudumu.

AKALETEWA WAHYI NUHU

Aya 36-39

MAANA

Akaletewa wahyi Nuh kuwa hataamini katika watu wako isipokuwa yule aliyekwi shaamini. Basi usisikitike kwa waliyokuwa wakiyatenda.

Mwenyezi Mungu alimpa habari Nuh kwamba kazi yake imekwisha, baada ya kutekeleza ujumbe kwa njia sahihi na kumpa hoja kila mpinzani; na kwamba hakuna yeyote atakayemwitikia baada ya sasa.

Mwenyezi Mungu alimpoza Nuh, kwani alikuwa anaungulika na kuwa na kuwa na huzuni, kwa sababu ya watu wake kuendelea na ushirikina.

Na unda jahazi mbele ya macho yetu na kwa wahyi wetu wala usinizungumzie kuhusu wale waliodhulumu, hakika wao watazamishwa.

Mbele ya macho yetu ni fumbo la kuhifadhi kwake na kuchunga kwake Mwenyezi Mungu. Na makusudio ya wahyi wetu ni amri na maelekezo yake. Baada ya Mwenyezi Mungu kumwamrisha kuunda jahazi, alimkataza kutawasali naye kuhusu wale waliojidhulumu, kwa sababu neno la adhabu limekwisha wathibitikia wote.

Na akawa anaunda jahazi na kila wakimpita wakuu wa kaumu yake wakimkejeli kwa vile anaitengeza kwenye nchi kavu mbali na maji. Walimkejeli na kumcheka kwa vile walikuwa na yakini kuwa hakuna chochote zaidi ya wanavyoona. Hivi ndivyo alivyo mjinga anategemea mambo ya nje tu wala hafikirii vizuri au kuzingatia.

Inasemekana kuwa watu wa Nuh walikuwa hawajui jahazi wala manufaa yake; ndio wakamkejeli na kustaajabu. Lakini ni maarufu kuwa Wafoeniki ndio watu wa mwanzo mwanzo kuunda majahazi.

Abu Hayyan Al-andalusiy, katika tafsir yake, Albahrul muhit, akimnukuu Ibn Abbas, anasema kuwa Nuh alikata mbao za kutengenezea Safina, kutoka katika msitu wa milima ya Lebanon. Hili linafahamisha kwamba, misitu ya mili- ma ya Lebanon, ilikuwa maarufu tangu zamani na kwamba Wafoniki walikuwa wakikata mbao za majahazi yao kwenye msitu huo.

WAUMINI NA WENYE KEJELI

Akasema: Ikiwa nyinyi mnatukejeli, hakika nasi tutawakejeli, kama mnavyotukejeli. Nanyi mtakuja jua ni nani itakayemfikia adhabu ya kumfedhehesha na itakaye mteremkia adhabu ya kudumu.

Hawakujua hakika ya jahazi (Safina) na lengo lake, hawakujua siku zimeficha majanga gani. Hilo likawapelekea dharau na kejeli. Lakini Nuh alikuwa na hakika na alifanyalo, kwamba yeye anafanya kwa uangalizi, kuwa ataokoka yeye na walio pamoja naye na kwamba mwisho wa wenye kejeli ni gharka tu.

Vijana wetu wa leo wanafanana sana na wale waliokufuru katika watu wa Nuh. Wale walikejeli Safina ya Nuh na hawa wanawakejli waumini, wakisema: Mpaka sasa, karne ya ishirini, bado watu wanaswali na kufunga tu; sawa na walivyosema wale makafiri: Jahazi kwenye nchi kavu kusiko na bahari wala maji? Hawakujua siri na hakika ya Safina, wakamkejeli Nuh. Na vijana wa leo hawajui siri ya saum na swala, ndio wanawadharau wafungaji na waswaliina. Je, vijana wanaokejeli dini, watasalimika kupatwa na yaliyowapata watu wa Nuh na Safina yake?

حَتَّىٰ إِذَا جَاءَ أَمْرُنَا وَفَارَ التَّنُّورُ قُلْنَا احْمِلْ فِيهَا مِن كُلٍّ زَوْجَيْنِ اثْنَيْنِ وَأَهْلَكَ إِلَّا مَن سَبَقَ عَلَيْهِ الْقَوْلُ وَمَنْ آمَنَ وَمَا آمَنَ مَعَهُ إِلَّا قَلِيلٌ ﴿٤٠﴾

40. Ikawa inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuh akamwita mwanawe naye alikuwa mbali: Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri.

وَقَالَ ارْكَبُوا فِيهَا بِسْمِ اللَّـهِ مَجْرَاهَا وَمُرْسَاهَا إِنَّ رَبِّي لَغَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٤١﴾

41. Na akasema: Pandeni humo kwa Bismillahi, Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, kwenda kwake na kusimama kwake. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu.

وَهِيَ تَجْرِي بِهِمْ فِي مَوْجٍ كَالْجِبَالِ وَنَادَىٰ نُوحٌ ابْنَهُ وَكَانَ فِي مَعْزِلٍ يَا بُنَيَّ ارْكَب مَّعَنَا وَلَا تَكُن مَّعَ الْكَافِرِينَ ﴿٤٢﴾

42. Ikawa inakwenda nao katika mawimbi kama milima. Na Nuh akamwita mwanawe naye alikuwa mbali: Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri.

قَالَ سَآوِي إِلَىٰ جَبَلٍ يَعْصِمُنِي مِنَ الْمَاءِ قَالَ لَا عَاصِمَ الْيَوْمَ مِنْ أَمْرِ اللَّـهِ إِلَّا مَن رَّحِمَ وَحَالَ بَيْنَهُمَا الْمَوْجُ فَكَانَ مِنَ الْمُغْرَقِينَ ﴿٤٣﴾

43. Akasema: Nitakimbilia mlimani unilinde na maji. Akasema: Leo hapana wa kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu. Na wimbi likaingia kati yao akawa miongoni mwa waliogharikishwa.

وَقِيلَ يَا أَرْضُ ابْلَعِي مَاءَكِ وَيَا سَمَاءُ أَقْلِعِي وَغِيضَ الْمَاءُ وَقُضِيَ الْأَمْرُ وَاسْتَوَتْ عَلَى الْجُودِيِّ وَقِيلَ بُعْدًا لِّلْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٤٤﴾

44. Na ikasemwa: Ewe ardhi! meza maji yako na ewe mbingu! Jizuie. Na maji yakadidimia chini na amri ikapitishwa, na Jahazi ikasimama juu ya Judi. Na ikasemwa: wapotelee mbali watu madhalimu!

MAFURIKO

Aya 40-44

LUGHA

Neno tannur (tanuri) katika lugha ya kiarabu lina maana nyingi; miongoni mwazo ni ardhi, na ndiyo iliyokusudiwa hapa.

MAANA

Hata ilipokuja amri yetu na ikafurika tanuri.

Maana ni kuwa, ilipokuja amri ya Mwenyezi Mungu na maji yakawa yanabubujika kutoka ardhini

Tulisema: Pakia humo wawili wawili, dume na jike kutoka kila aina.

Neno kila linategemea kile kinachoelzewa. Kwa mfano katika kaule yake Mwenyezi Mungu: Nichake kila kitu, inamaanisha kuwa vitu vyote ni vyake. Na kauli yake kuhusu Bilqis:

وَأُوتِيَتْ مِن كُلِّ شَيْءٍ ﴿٢٣﴾

Na amepewa kila kitu, (27:23),

Inahusu vitu vya wakati wake au mji wake. Kwa hiyo basi maana ya kila aina katika Aya hii tuliyonayo ni kiasi kile atakachoweza kukichukua Nuh(a.s) . Katika Safina (jahazi ) miongoni mwa viumbe na wala sio aina yote ya viumbe.

Vinginevyo ingelibidi urefu na upana wa Safina uwe mamia ya maili.

Na watu wako wa nyumbani isipokuwa yule ambaye limempitia neno.

Yaani pakia ndani ya Safina watu wa nyumbani isipokuwa wale ambao tumekukataza kuwachukua.

Wafasiri wanasema kuwa watoto wa Nuh aliowachukuwa ni: Ham, Sam na Yafith. Ama yule ambaye aliandikiwa kuangamia katika watu wake wa nyumbani ni mmoja wa watoto wake ambaye Mwenyezi Mungu amemwashiria kwa kusema: Akawa katika waliozama ambaye inasemekana jina lake ni Kanani.

Mke wa Nuh pia alikuwa ni miongoni mwa waliozama, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu:

ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا لِّلَّذِينَ كَفَرُوا امْرَأَتَ نُوحٍ وَامْرَأَتَ لُوطٍ ﴿١٠﴾

“Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa waliokufuru kwa mke wa Nuh na mke wa Lut” (66:10).

Na walioamini; na hawakuamini pamoja naye isipokuwa wachache tu.

Yaani chukua kikundi kidogo cha watu walioamini pamoja nawe.

Na pandeni humo kwa Jina la Mwenyezi Mungu (Bismillah) kuwa ndio kwenda kwake na kuthibiti kwake.

Nuh alifuata amri ya Mwenyezi Mungu, akwaita wauminii katika watu wake wa nyumbani na swahaba zake wapande Safina; na yeye pamoja na waliokuwa naye wasome Bismillah katika kwenda na kutua.

Nimeona baadhi ya tafsir za kisufi wakisema kuwa makusudio ya Safina hapa ni sharia na makusudio ya mawimbi ni hawa za nafsi na matamanio yake. Nikawa najiulza: wametoa wapi masheikh hawa tafsir ya kukiita Kitabu cha Mwenyezi Mungu na ujumbe wake kuwa ni Safina?

Ikawa inakwenda nao katika mawimbi kama milima.

Katika hali hii, inayofanana na kukata roho, Nuh alimwangalia mwanawe kwa masikitiko akimpa mwito wa kumwamini Mungu na kuokoka, kabla ya kuvuta pumzi za mwisho.

Na Nuh akamwita mwanawe naye alikuwa mbali: Ewe mwanangu! Panda pamoja nasi wala usiwe pamoja na makafiri.

Maskini! Hurumma za mzazi, mwanawe akiguswa na shida yoyote naye inamgusa moyoni mwake na rohoni mwake. Nuh alikuwa na uhakika kuwa mwanawe ataangamia ikiwa atang’ang’ania kumshirikisha Mwenyezi Mungu, hivyo akamtaka amwamini Mwenyezi Mungu na apande Safina pamoja nao, lakini hakuna kuokoka kwa mwenye inadi. Upuuzaji wa ujana ukampofusha kujua mwisho mbaya,akasema: Nitakimbilia mlimani unilinde na maji.

Ujinga na ghururi ulimpa picha kuwa tatizo ni maji tu na kwamba ataweza kulitatua tatizo hilo kwa kupanda mlimani; hakujua kwamba hayo ni matakwa ya Mwenyezi Mungu na hasira zake kwa washirikina.

Akasema: Leo hapana wa kulindwa na amri ya Mwenyezi Mungu.

Nuh akamjibu kuwa tatizo sio maji; isipokuwa ni matakwa ya Mwenyezi Mungu ambayo hayana kimbilio. Atakayeokoka ni yule aliyerehemiwa na Mwenyezi Mungu na atakyeangamia ni yule aliyekasirikiwa na Mwenyezi Mungu.

Na wimbi likaingia kati yao akawa miongoni mwa waliogharikishwa.

Wimbi lilikuja katikati ya mazungumzo ya mzazi na mwanawe. Yaliyomfika Nuh(a.s) na mwanawe yanawafika wazazi wengi na watoto wao wanaojifanya wajuaji; kisha mwisho wao unakuwa kama wa mtoto wa Nuh.

Na ikasemwa: Ewe ardhi! meza maji yako na ewe mbingu! Jizuie. Na maji yakadidimia chini na amri ikapitishwa, na Jahazi ikasimama juu ya Judi.

Mwenyezi Mungu aliamrisha ardhi imeze maji na akaamrisha mbingu isimamiishe kumimina na mambo yakaishia kwa kuokoka waumini na kuangamia washirikina. Safina nayo ikatua Judiy mlima uloko Muosal, Lebanon; kama inavyosemekana.

Na ikasemwa: wapotelee mbali watu madhalimu!

Ambao wameikadhibisha haki. Neno ‘potolea mbali’ ni dua ya kuwekwa mbali na rehema. Kama kauli yake Mwenyezi Mungu:

فَسُحْقًا لِّأَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴿١١﴾

“ Kuangamia ni kwa watu wa motoni” (67:11).

وَنَادَىٰ نُوحٌ رَّبَّهُ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ابْنِي مِنْ أَهْلِي وَإِنَّ وَعْدَكَ الْحَقُّ وَأَنتَ أَحْكَمُ الْحَاكِمِينَ ﴿٤٥﴾

45. Na Nuh alimwomba Mola wake akasema: Ewe Mola wangu! Hakika mwanangu ni katika watu wangu, na hakika ahadi yako ni haki na wewe ni hakimu bora wa mahakimu wote.

قَالَ يَا نُوحُ إِنَّهُ لَيْسَ مِنْ أَهْلِكَ إِنَّهُ عَمَلٌ غَيْرُ صَالِحٍ فَلَا تَسْأَلْنِ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنِّي أَعِظُكَ أَن تَكُونَ مِنَ الْجَاهِلِينَ ﴿٤٦﴾

46. Akasema: Ewe Nuh! Huyo si katika watu wako. Hakika yeye ni mwendo usio mwema. Basi usiniombe usilo na ujuzi nalo mimi ninakuwaidhi usije ukawa miongoni mwa wasiojua.

قَالَ رَبِّ إِنِّي أَعُوذُ بِكَ أَنْ أَسْأَلَكَ مَا لَيْسَ لِي بِهِ عِلْمٌ وَإِلَّا تَغْفِرْ لِي وَتَرْحَمْنِي أَكُن مِّنَ الْخَاسِرِينَ ﴿٤٧﴾

47. Akasema: Ewe Mola wangu! Hakika mimi ninajikinga kwako kukuomba nisilo na ujuzi nalo. Na kama hutanisamehe na kunirehemu nitakuwa katika waliohasirika.

قِيلَ يَا نُوحُ اهْبِطْ بِسَلَامٍ مِّنَّا وَبَرَكَاتٍ عَلَيْكَ وَعَلَىٰ أُمَمٍ مِّمَّن مَّعَكَ وَأُمَمٌ سَنُمَتِّعُهُمْ ثُمَّ يَمَسُّهُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٤٨﴾

48. Ikasemwa: Ewe Nuh! Shuka kwa salama itokayo kwetu na baraka juu yako na juu ya umma zilizo pamoja nawe; na zitakuwepo umma tutakazozistarehesha kisha zishikwe na adhabu chungu itokayo kwetu.

تِلْكَ مِنْ أَنبَاءِ الْغَيْبِ نُوحِيهَا إِلَيْكَ مَا كُنتَ تَعْلَمُهَا أَنتَ وَلَا قَوْمُكَ مِن قَبْلِ هَـٰذَا فَاصْبِرْ إِنَّ الْعَاقِبَةَ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٤٩﴾

49. Hizo ni habari za ghaibu tunazokupa wahyi. Hukuwa ukizijua wewe wala watu wako kabla ya hii. Basi subiri! Hakika mwisho ni wa wacha Mungu.

NUHU AKAMWOMBA MOLA WAKE

Aya Ya 45-49

MAANA

Na Nuh alimwomba Mola wake akasema: Ewe Mola wangu! Hakika mwanangu ni katika watu wangu, na hakika ahadi yako ni haki na wewe ni hakimu bora wa mahakimu wote.

Katika Aya ya 40 Mwenyezi Mungu alimwamrisha Nuh kuchukua watu wake wa nyumbani, isipokuwa yule aliyemkataza; na hakumkataza wala kumwamrisha kumchukua mwanawe, bali alinyamaza kwa hekima yake. Nuh akadhani kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawaokoa watu wake wote wa nyumbani, waasi na watiifu.

Ndio maana akamwomba Mola atekeleze ahadi yake kwa mwanawe, kwa sababu ni katika watu wake.

Unaweza kuuliza : Nuh ni mtume na mtume ni maasumu (aliyehifadhiwa na dhambi) itakuwaje adhanie kinyume?

Jibu : Kudhania kinyume hakuharibu isma (kuhifadhiwa na dhambi) ikiwa hakuna kitendo, kwa vile kunafanana na mawazo tu yanayopita kichwani kisha yanaondoka, kama vile hayakuwepo. Hata tukikadiria kuwa maasum amedhania kinyume na hali halisi, basi Mwenyezi Mungu atamfichulia na atamhifadhi na makosa. Hayo tumekwisha yafafanua katika Juz.5 (4:105).

Akasema: Ewe Nuh! Huyo si katika watu wako. Hakika yeye ni mwendo usio mwema.”

Yaani ana mwendo usiokuwa mwema. Mwenyezi Mungu anamwambia Nuh kuhusu mwanawe kuwa nimekuamrisha uchukue watu wako katika Safina ispkokuwa niliokukataza. na yey- ote katika wao niliyekukataza basi ni kwa hekima niliyoipitisha na matakwa yangu yametaka mwanao awe ni miongoni mwa watakaoazama, kwa vile mwendo wake si mzuari. Hakika watu wa Mtume ni wale wema hata kama wako mbali kinasaba na madui zao ni waovu hata kama wako karibu kinasaba.

Maana haya yanatiliwa mkazo na kauli yake Mwenyezi Mungu: “Hakika watu wanaomkurubia zaidi Ibrahimu ni wale waliomfuata” Juz.3 (3:68).

Na hapo ndipo alipochukua Imam Ali(s.a) kauli yake: “ Hakika mpenzi wa Muhammad ni yule anayemtii Mwenyezi Mungu hata kama yuko mbali naye kidamu na adui wa Muhammad ni yule anaye muasi Mwenyezi Mungu hata kama yuko karibu naye kiudugu”.

Mshairi naye anasema: Mapenzi ya Salmani kwao, udugu walishibana, Lakini Nuh na mwanawe katu hawakuwiyana

Basi usiniombe usilo na ujuzi nalo mimi ninakuwaidhi usije ukawa miongoni mwa wajinga.”

Jambo ambalo hakuwa akilijua Nuh ni alivyopitisha Mwenyezi Mungu tangu mwanzo kuwa mwanawe atakuwa miongoni mwa watakaozama, kwa maslahi fulani; na alipomuomba Mola wake akamwambia usiniombe usilolijua, akasema:

Ewe Mola wangu! Hakika mimi ninajikinga kwako kukuombe nisilo na ujuzi nalo [1] .

Yaani sitakuomba tena kuhusu mototo wangu baada ya kunifahamisha uhakika; bali ninaridhia hukumu yako na ulivyopitisha.

Na kama hutanisamehe na kunirehemu nitakuwa katika waliohasirika.

Hii ni kiasi cha unyeneyekevu wa Nuh tu kwa Mwenyezi Mungu, sio kutubia dhambi iliyofanyika. Ndivyo walivyo Mitume na watu wema. Tumelifafanua hilo katika Juz.4 (4:18) kifungu cha ‘Toba na maumbile.’

Ikasemwa: Ewe Nuh! Shuka kwa Salama itokayo kwetu na baraka nyingi juu yako na juu ya umma zilizo pamoja nawe; na zitakuwepo umma tutakazozistarehesha kisha zishikwe na adhabu chungu itokayo kwetu.

Tufani ilipokwisha na washirikina kuangamia, Mwenyezi Mungu alimwamrisha Nuh ashuke ardhini yeye na wenzake aliokuwa nao kwa salama na baraka za maisha na riziki, waenee huku na huko kisha wazaane na upatikane umma mwingine; kama ilivyokujatokea wakapatikana Ad na Thamud, watastarehe kidogo duniani kisha wakapata adhabu kwa kufru yao na uasi wao.

KIGANO CHA MWEZI 10, MUHARRAM

Kinasema kigano kwamba Nuh alishuka kwenye Safina yake siku ya Ashura(10,Muharram) akafunga kwa ajili ya kumshukuru Mwenyezi Mungu. Naye alikuwa amemaliza chakula.

Akachanganya kofi moja la choroko (pojo), kofi moja la adesi na ngano hadi zikawa nafaka saba akazipika, wakala wote mpaka wakashiba. Basi kiganao hiki kikaenea katika miji na watu wakaifanya ni sunna siku ya Ashura.

Hizo ni habari za ghaibu tunazokupa wahyi. Hukuwa ukizijua wewe wala watu wako kabla ya hii. Basi subiri! Hakika mwisho ni wa wacha Mungu.

Msemo unaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) Baada ya Mwenyezi Mungu kumwelezea kisa cha Nuh, alimwambia kuwa kisa hiki ni wahyi, hukukijua wewe wala maquraish. Kwa hiyo nawe vumilia kwa yatakayokupata kutoka kwa watu wako; kama alivyovumilia Nuh. Kama ambavyo mwisho ulikuwa wake na walioamini pamoja naye, basi vilevile mwisho utakuwa wako na waislam. Kwa sababu siku zote mwisho ni wa wenye kusubiri wenye kumcha Mwenyezi Mungu.

TUFANI IMETHIBITI KWA UMA NYINGINEZO

Masimulizi ya Tufani ya Nuh hayahusiki na vitabu vya dini tu. Watafiti wamegundua mabaki ya mbao zinazoashiria kisa hiki na tarehe yake inarudi kwenye mwaka 2100 kabla ya kuzaliwa Nabii Issa(a.s) .

Wataalamu wengine wasiohusika na dini wamesema kuwa kisa cha Tufani kinajulikana na umma za kale za Wahindi, Wagiriki, Wajapani, Wachina, Wabrazili, watu wa Mexico na wengineo. Wanatofautiana katika masimulizi, lakini wanaafikiana katika madhumuni na kwamaba sababu ilikuwa ni kufuru ya watu na dhulma yao.