TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 11157
Pakua: 2127


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11157 / Pakua: 2127
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

فَلَمَّا ذَهَبَ عَنْ إِبْرَاهِيمَ الرَّوْعُ وَجَاءَتْهُ الْبُشْرَىٰ يُجَادِلُنَا فِي قَوْمِ لُوطٍ ﴿٧٤﴾

74. Basi hofu ilipomwondokea Ibrahim na ikawa ile bishara imemfikia, alianza kujadiliana nasi juu ya watu wa Lut.

إِنَّ إِبْرَاهِيمَ لَحَلِيمٌ أَوَّاهٌ مُّنِيبٌ ﴿٧٥﴾

75. Hakika Ibrahim alikuwa mpole, mwenye huruma, mwepesi wa kurejea (kwa Mungu).

يَا إِبْرَاهِيمُ أَعْرِضْ عَنْ هَـٰذَا إِنَّهُ قَدْ جَاءَ أَمْرُ رَبِّكَ وَإِنَّهُمْ آتِيهِمْ عَذَابٌ غَيْرُ مَرْدُودٍ ﴿٧٦﴾

76. Ewe Ibrahim! Achana nayo haya. Hakika amri ya Mola wako imekwishakuja, na hakika wao itawafikia adhabu isiyorudishwa.

IBRAHIM ANAJADILI KUHUSU WATU WA NUH

Aya 74-76

MAANA

Basi hofu ilipomwondokea Ibrahim na ikawa ile bishara imemfikia, alianza kujadiliana nasi juu ya watu wa Lut.

Baada ya kujua Ibrahim hali halisi ya wageni wake na madhumuni yao alitulia, na akajawa na furaha yeye na mkewe, Sarah, kwa habari ya kupata mtoto na mjukuu. Lakini hakufurahishwa na habari ya adhabu ya watu wa Lut. Akawa anajadiliana naao.

Kundi kubwa la wafasiri, akiwemo Arrazi na mwenye Tafsir Al-Manar, wamesema kuwa Ibrahim hakujadili kuhusu watu wa Lut; isipokuwa alijadili kuhusu Lut akihofia kupatwa na adhabu. Wafasiri hao wametoa dalili kwa kauli yake Mwenyezi Mungu:

قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطًا قَالُوا نَحْنُ أَعْلَمُ بِمَن فِيهَا لَنُنَجِّيَنَّهُ وَأَهْلَهُ إِلَّا امْرَأَتَهُ كَانَتْ مِنَ الْغَابِرِينَ ﴿٣٢﴾

Akasema: Humo yumo Lut. Wakasema: Sisi twajua zaidi aliyemo humo, kwa hakika tutamuokoa yeye na watu wake ila mkewe aliye miongoni mwa watakaobaki nyuma. (29:32).

Lakini ilivyo, Aya hii waliyoitolea ushahidi, haina uhusiano wowote na mjadala wa wa Ibrahim; isipokuwa ni kutolea habari tu kwamba humo yumo Lut; na ndio maana wakasema tunajua sana.

Ayah hii tunayoifasiri inazungumzia mjadala kuhusu watu wa Lut sio kwa Lut peke yake. Kuongezea kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na hakika wao itawafikia adhabu isiyorudishwa.

Dhamir katika hakika wao na itawajia inawarudia watu wa Lut ambao ibrahim amewajadili. Lakini wafasiri wakasema kuwa kuwajadili watu wa Lut ni kumkosea Adabu Mwenyezi Mungu, na Ibrahim ni Maasum, kwa hiyo hapana budi iwe ni kujadili Lut pekee.

Nasi tunasema:

Kwanza : hakuna tofauti katika kumjadili Lut peke yake au kaumu yake. Kujadili ni kujadili tu.

Pili : Mjadala ulikuwa unahusiana na kuondolewa adhabu waja wa Mungu au kuchelweshwa. Kwa hiyo hilo si dhambi; bali ni kinyume cha hivyo. Kwa sababu mjadala huu hauna kupingana wala kuzozana; isipokuwa ni kutaka hurumma kutoka kwa mwenye nguvu kwenda kwa mnyonge. Ombi hili linafahamisha upole na hurumma.

Ndio maana Mwenyezi Mungu akamsifu kuwa niMpole, mwenye hurumma mwepesi wa kurejea (kwa Mungu) baada ya kuwahurumia watu wa Lut

Tatu : Ibrahim alijadili kuhusu watu wa Lut ili awe na yakini kwamba wao wameasi kiasi ambacho hakuna tamaa ya kuongoka kwao; sawa na alivyosema:

قَالَ أَوَلَمْ تُؤْمِن قَالَ بَلَىٰ وَلَـٰكِن لِّيَطْمَئِنَّ قَلْبِي ﴿٢٦٠﴾

Akasema: Huamini? Akasema: Kwa nini! (naamini) Lakini upate kutulia moyo wangu. (2:260).

Hili linasisitizwa na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Ewe Ibrahim! Achana nayo haya. Hakika amri ya Mola wako imekwishakuja, na hakika wao itawafikia adhabu isiyorudishwa.

Yaani usiniulize ewe ibrahim katika mambo yanayohusu watu wa Lut, kwa vile wao wataangamia tu, kwa sababu ya kuendelea kwao na shirk na ufisadi na kutokuwepo tama ya kutubia.

وَلَمَّا جَاءَتْ رُسُلُنَا لُوطًا سِيءَ بِهِمْ وَضَاقَ بِهِمْ ذَرْعًا وَقَالَ هَـٰذَا يَوْمٌ عَصِيبٌ ﴿٧٧﴾

77. Na wajumbe wetu walipomfikia lut, aliwahuzunikia na akawaonea dhiki. Na akasema: Hii ni siku ngumu.

وَجَاءَهُ قَوْمُهُ يُهْرَعُونَ إِلَيْهِ وَمِن قَبْلُ كَانُوا يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ قَالَ يَا قَوْمِ هَـٰؤُلَاءِ بَنَاتِي هُنَّ أَطْهَرُ لَكُمْ فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَلَا تُخْزُونِ فِي ضَيْفِي أَلَيْسَ مِنكُمْ رَجُلٌ رَّشِيدٌ ﴿٧٨﴾

78. Na wakamjia kaumu yake mbiombio na kabla ya haya walikuwa wakifanya maovu. Akasema: Enyi kaumu yangu! Hawa binti zangu wao wametakasika zaidi kwenu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu. Wala msinifedheheshe mbele ya wageni wangu. Hivi hakuna mtu muongofu miongoni mwenu.

قَالُوا لَقَدْ عَلِمْتَ مَا لَنَا فِي بَنَاتِكَ مِنْ حَقٍّ وَإِنَّكَ لَتَعْلَمُ مَا نُرِيدُ ﴿٧٩﴾

79. Wakasema: Umekwishajua hatuna haki juu ya binti zako, na hakika unajua tunayoyataka.

قَالَ لَوْ أَنَّ لِي بِكُمْ قُوَّةً أَوْ آوِي إِلَىٰ رُكْنٍ شَدِيدٍ ﴿٨٠﴾

80. Akasema: Lau ningelikuwa na nguvu kwenu au nategemea kwenye nguzo yenye nguvu!

HUZUNI YA LUT

Aya 77- 80

MAANA

Na wajumbe wetu walipomfikia Lut, aliwahuzunikia na akawaonea dhiki.

Ujumbe uliondoka kwa Ibrahim(a.s) kuelekea kwa Lut(a.s) .

Katika Juz.8 (7:80) tulitaja kuwa Lut ni mtoto wa ndugu yake Ibrahim na kwamba yeye alikuwa mashariki mwa Jordan na kaumu yake ndio watu wa kwanza kuwaingilia kimwili wanaume badala ya wanawake. Na hili walikuwa wakilifanya dhahiri bila ya uficho wowote. Mwenye kukataa walikuwa wakimshika kwa nguvu; hata kama ni mgeni mheshimiwa.

Kwa hiyo walipokuja wajumbe wa Mwenyezi Mungu kwa Lut, kwa sura za kibinadamu, alihofia watu wake wasiwakosee heshima, huku akiwa hawezi kuwazuia.

Basi akawa anaona uchunguNa akasema: Hii ni siku ngumu.

Na wakamjia kaumu yake mbiombio.

Yaani walikuja nyumbani kwa Nuh haraka wakidhani kuwa siku hii ni kama nyinginena kabla ya haya walikuwa wakifanya maovu hawakufkiria mwisho wake.

Akasema: Enyi kaumu yangu! Hawa binti zangu wao wametakasika zaidi kwenu.

Makusudi ya binti zake ni binti wa umma wake; kwa sababu mtume ni kama mzazi kwa umma wake. Maana ni kuwa oweni wanawake na mstarehe kwa halali na wema na muache ulawiti kwa sababu hiyo ni kazi ya shetani.Basi mcheni Mwenyezi Mungu.

Anawahofisha na Mungu, na hilo wanalipuuza watu wa ufuska na uovu.

Wala msinifedheheshe mbele ya wageni wangu. Ikiwa hamumuogopi Mwenyezi Mungu basi angalau muone haya, msinifedheheshe mbele ya wageni.Hivi hakuna mtu muongofu miongoni mwenu? mwenye akili atakayewazuia hayo mnayotaka?

Wakasema: Umekwishajua hatuna haki juu ya binti zako Yaani hatuwataki.Na hakika unajua tunayoyataka.

Yaani unajua kuwa sisi hatupendelei mabinti, tunataka wanaume na unajua kuwa sisi hatutishwi na huyo Mungu wako. Binadamu anafikia kiwango hiki cha kiburi akiwa amejiachia, akipinga misimamo na kukosa majukumu.

Kuna watu leo walio mfano wa kaumu Lut katika ushenzi na kiburi tena ni wengi. Miongoni mwao wamo walezi na waalimu wa mashule na vyuo vikuu.

Na sisi hatuna shaka kwamba kuna watu wa dini ambao ni waovu mara elfu kuliko hao. Lakini la kusisitiza ni kuwa lau kusingelikuweko na watu wanaolingania kwenye dini na misimamo, basi ulimwengu ungelikuwa mbaya kuliko ulivyo hivi sasa.

Akasema: Lau ningelikuwa na nguvu kwenu au nategemea kwenye nguzo yenye nguvu!

Baada ya Lut kukata tamaa na watu wake, alitamani lau angelikuwa na nguvu za kuwazuia au kupata msadizi. Alitamani hivi akiwa hajui kwamba nusura ya Mwenyezi Mungu iko nyumbani kwake na kwamba umebakia wakati mchache sana wa kuangamia wafisadi.

قَالُوا يَا لُوطُ إِنَّا رُسُلُ رَبِّكَ لَن يَصِلُوا إِلَيْكَ فَأَسْرِ بِأَهْلِكَ بِقِطْعٍ مِّنَ اللَّيْلِ وَلَا يَلْتَفِتْ مِنكُمْ أَحَدٌ إِلَّا امْرَأَتَكَ إِنَّهُ مُصِيبُهَا مَا أَصَابَهُمْ إِنَّ مَوْعِدَهُمُ الصُّبْحُ أَلَيْسَ الصُّبْحُ بِقَرِيبٍ ﴿٨١﴾

81. Wakasema: Ewe Lut! Hakika sisi ni wajumbe wa Mola wako. (Hawa) hawatakufikia. Basi ondoka pamoja na watu wako wa nyumbani katika sehemu ya usiku. Wala yeyote katika nyinyi asigeuke nyuma, isipokuwa mke wako, kwani yeye yatamsibu yatakayowasibu. Hakika miadi yao ni asubuhi, je asubuhi si karibu?

فَلَمَّا جَاءَ أَمْرُنَا جَعَلْنَا عَالِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهَا حِجَارَةً مِّن سِجِّيلٍ مَّنضُودٍ ﴿٨٢﴾

82. Basi ilipofika amri yetu tuliigeuza juu chini. Na tukawateremshia mvua ya mawe ya udongo mkavu yaliyopandana.

مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ وَمَا هِيَ مِنَ الظَّالِمِينَ بِبَعِيدٍ ﴿٨٣﴾

83. Yaliyotiwa alama kwa Mola wako. Na hayo hayako mbali na wenye kudhulumu.

HAWATAKUFIKIA

Aya 81-83

MAANA

Wakasema: Ewe Lut! Hakika sisi ni wajumbe wa Mola wako. Hawa hawatakufikia.

Arrazi anasema: Malaika walipoona wasiwasi na huzuni ya Lut walimpa bishara zifuatazo:

1. Kwamba wao ni wajumbe wa Mwenyezi Mungu.

2. Makafiri hwatafikia lile walilolikusudia.

3. Mwenyezi Mungu atawaangamiza.

4. Mwenyezi Mungu atamwokoa yeye na watu wake kutokana na adhabu.

5. Kwamba yeye Lut yuko kwenye Nguzo yenye nguvu, kwa sababu Mungu atamwokoa na watu madhalimu.

Basi ondoka pamoja na watu wako wa nyumbani katika sehemu ya usiku. Wala yeyote katika nyinyi asigeuke nyuma, isipokuwa mke wako, kwani yeye yatamsibu yatakayowasibu.

Malaika walimtaka Lut atoke na watu wake wa nyumbani na kutoangalia nyuma yeyote. Huenda hekima ya hilo ilikuwa ni kutoona muangaliaji jinsi mji wake unavyoangamia asishikwe na hurumma akahuzunika.

Ama mkewe alimwacha, kwa amri ya Mwenyezi Mungu, pamoja na makafiri kwa sababu yeye ni miongoni mwao. Kwa hiyo naye alikuwa na laana ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu zake.

Hakika miadi yao ni asubuhi, je asubuhi si karibu?

Haya ni katika maneno ya kuashiria jibu la anayeharakisha adhabu.

Basi ilipofika amri yetu tuliigeuza juu chini.

Dhamiri ya tuliiegeuza ni ya ardhi ya vijiji vya kaumu ya Lut. Baadhi ya tafsiri zinasema kuwa umbali wake na Baytul maqdis ni mwendo wa siku tatu

Na tukawateremshia mvua ya mawe ya udongo mkavu yaliyopandana, yaliyotiwa alama kwa Mola wako.

Mahali pengine Mwenyezi Mungu anasema:

لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ ﴿٣٣﴾

“Tuwatupie mawe ya udongo” (51:33).

Yaliyopandana inaweza kuwa ni kupandana hayo yenyewe au kupandana kwa mfululizo wa kushuka. Alama ni alama maalumu ya kumfikia yule anayestahiki. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu aliteremsha adhabu mbili kwa kaumu ya Lut: Mvua ya mawe na kuzama ardhini.

Na hayo hayako mbali na wenye kudhulumu.

Wafasiri wanasema kuwa wenye kudhulumu hapa ni makafiri wa Makka, kwamba Mwenyezi Mungu aliwaahidi kuwa wao, yatawapata yaliyowapata watu wa Lut, kama wataendelea kumkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) .

Maana haya hayako mbali, pamoja na kujua kuwa kila dhalimu aliyeko mashariki au magharibi anaweza kushukiwa na adhabu kutoka mbinguni au kuadhibiwa ardhini. Kwani mapinduzi yoyote yanayotokea au yatakayotokea, basi matokeo yake ni adhabu kwa dhulma na watu wake na kwa ufisadi na wasaidizi wake.

وَإِلَىٰ مَدْيَنَ أَخَاهُمْ شُعَيْبًا قَالَ يَا قَوْمِ اعْبُدُوا اللَّـهَ مَا لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرُهُ وَلَا تَنقُصُوا الْمِكْيَالَ وَالْمِيزَانَ إِنِّي أَرَاكُم بِخَيْرٍ وَإِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ مُّحِيطٍ ﴿٨٤﴾

84. Na kwa Wamadian (tulimpeleka) ndugu yao Shuaib. Akasema: Enyi watu wangu! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, hamna Mungu mwingine zaidi yake. Wala msipunguze kipimo na mizani. Mimi ninawaona mko katika kheri; na mimi nawahofia na adhabu ya siku izungukayo.

وَيَا قَوْمِ أَوْفُوا الْمِكْيَالَ وَالْمِيزَانَ بِالْقِسْطِ وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ ﴿٨٥﴾

85. Enyi watu wangu! Timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu wala msiwatilie kasoro watu vitu vyao. Wala msifanye ufisadi katika nchi mkafanya vurugu.

بَقِيَّتُ اللَّـهِ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُم مُّؤْمِنِينَ وَمَا أَنَا عَلَيْكُم بِحَفِيظٍ ﴿٨٦﴾

86. Alivyowabakishia Mwenyezi Mungu ni bora kwa ajili yenu ikiwa nyinyi ni waumini. Wala mimi si mlinzi wenu.

SHUAIB

Aya 84-86

MAANA

Na kwa Wamadian (tulimpeleka) ndugu yao Shuaib. Akasema: Enyi watu wangu! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, hamna Mungu mwingine zaidi yake.

Imepita tafsiri ya Aya hii kwa herufi zake katika Juz. 8 (7:85).

Wala msipunguze kipimo na mizani.

Hili ni katazo la kupunja; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾ الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ﴿٢﴾

“Ole wao wanopunja. Ambao wanapojipimia kwa watu hutaka watimiziwe. Na wanapowapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.” (83:1-2)

Mimi ninawaona mko katika kheri.

Makusudio ya kheri hapa ni riziki nyingi.

Na mimi nawahofia na adhabu ya siku izungukayo.

Hii ni kuwaonya na adhabu, kama wataendelea na maasi

Enyi watu wangu! Timizeni kipimo na mizani kwa uadilifu.

Baada ya kuwakataza kupunguza sasa anawaamrisha kutimiza vipimo. Maana zote mbili ni sawa. Hatufahamu lengo lake zaidi ya kuwa ni kusisitiza tu.

Wala msiwatilie kasoro watu vitu vyao.

Vitu ni kila kitu; kama vile haki ya kimaada (yakuonekana) na ya kimaana (isyoonekana). Kwa hiyo ni haramu kumpunguzia mtu kitu au jambo lolote; kama ilimu yake na hulka yake.

Wala msifanye ufisadi katika nchi mkafanya vurugu.

Katika Aya hii kuna maneo mawili (ta’thaw na Mufsidin) yenye maana moja, ya ufisadi. Kwa hiyo ikawa ni lazima kufanya T’awil (tafsir inayowakilisha). Ama kutafsir Ta’athaw kwa maana ya juhudi; yaani msifanye juhudi ya kuleta ufisadi; au kutafsir Mufisidin kwa maana ya kuleta vurugu; kama vile vita na umwagaji damu, bila ya sababu inayowajibisha. Lakini vita vyenyewe vikiwa ni vya kuondoa ufisadi, basi itakuwa kuacha kupigana ndio ufisadi. Hapo Ndipo jihadi inakuwa ndio twaa bora. Taawili hii ni bora kuliko ile ya kwanza.

Alivyowabakishia Mwenyezi Mungu ni bora kwa ajili yenu ikiwa nyinyi ni waumini.

Halali ni njema na yenye kubaki hata ikiwa chache na haramu ni uovu, ni shari na inakwisha hata ikiwa nyingi. Tukichunguza sababu ya vita leo, tutaona ni kujilundikia mali wachache na kunyimwa wengi.

Imetokea sadfa kusoma magazeti ya leo 24-12-1968, kwamba jamaa huko London walifanya maandamano kuelekea makao ya mfalme, Birmingham (Birmingham Palace) wakimtaka malkia aiache ikulu yake, inayoweza kukaliwa na watu elfu, ambapo London pekee ina watu elfu sita wasio na makazi.

Wala mimi si mlinzi wenu wa kuwazuia na maasi kwa nguvu.

Umuhimu wangu ni kuwanasihi na kufikisha tu, na nimekwishatekeleza kwa ukamilifu na nimeondokana na majukumu. Shuaib (a.s.) ndiye anayesema hivyo.

قَالُوا يَا شُعَيْبُ أَصَلَاتُكَ تَأْمُرُكَ أَن نَّتْرُكَ مَا يَعْبُدُ آبَاؤُنَا أَوْ أَن نَّفْعَلَ فِي أَمْوَالِنَا مَا نَشَاءُ إِنَّكَ لَأَنتَ الْحَلِيمُ الرَّشِيدُ ﴿٨٧﴾

87. Wakasema: Ewe Shuaib! Je, Swala yako inakuamuru tuyaache waliyokuwa wakiyaabudu baba zetu au kufanya tupendavyo katika mali zetu? Hakika wewe ndiwe mpole, mwongofu!

قَالَ يَا قَوْمِ أَرَأَيْتُمْ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٍ مِّن رَّبِّي وَرَزَقَنِي مِنْهُ رِزْقًا حَسَنًا وَمَا أُرِيدُ أَنْ أُخَالِفَكُمْ إِلَىٰ مَا أَنْهَاكُمْ عَنْهُ إِنْ أُرِيدُ إِلَّا الْإِصْلَاحَ مَا اسْتَطَعْتُ وَمَا تَوْفِيقِي إِلَّا بِاللَّـهِ عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْهِ أُنِيبُ ﴿٨٨﴾

88. Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa nina dalili iliyo wazi itokayo kwa Mola wangu na ameniruzuku riziki njema itokayo kwake? Wala sipendi kuwakhalifu nikafanya yale ninayowakataza. Sitaki ila kutengeneza kiasi ninavyoweza. Na taufiki yangu haiko ila kwa Mwenyezi Mungu. Kwake ninategemea na kwake naelekea.

وَيَا قَوْمِ لَا يَجْرِمَنَّكُمْ شِقَاقِي أَن يُصِيبَكُم مِّثْلُ مَا أَصَابَ قَوْمَ نُوحٍ أَوْ قَوْمَ هُودٍ أَوْ قَوْمَ صَالِحٍ وَمَا قَوْمُ لُوطٍ مِّنكُم بِبَعِيدٍ ﴿٨٩﴾

89. Na enyi watu wangu! Kupingana nami kusije kukawapelekea yakawasibu kama yaliyowasibu kaumu ya Nuh au kaumu ya Hud au kaumu ya Swaleh, na kaumu ya Lut si mbali nanyi.

وَاسْتَغْفِرُوا رَبَّكُمْ ثُمَّ تُوبُوا إِلَيْهِ إِنَّ رَبِّي رَحِيمٌ وَدُودٌ ﴿٩٠﴾

90. Na muombeni maghufira Mola wenu kisha mtubie kwake. Hakika Mola wangu ni Mwenye kurehemu, Mwenye upendo.

HISTORIA YA UKOMUNISTI NA UBEPARI

Aya 87-90

MAANA

Wakasema: Ewe Shuaib! Je, Swala yako inakuamuru, tuyaache waliyokuwa wakiyaabudu baba zetu au kufanya tupendavyo katika mali zetu?

Kila asiyemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, huifanya swala ni ya kudharau na kuifanyia stizai pamoja na hao wanaoswali. Bila shaka yoyote Shuaib alikuwa ni katika wanaoswali.

Alipowaamuru watu wake kutupilia mbali masanamu, na kumwabudu Mwenyezi Mungu peke yake na kuwakataza chumo la haramu, ndio wakaanza kumdharau na kusema: Hivi swala yako ya kipuuzi unayoiswali ndiyo inakufanya utuamrishe tuache ada zetu tulizowakuta nazo mababa zetu na mababu zetu jadi na jadi; tena unatukataza tuache kuchumma mali vile tupendavyo?

Hakika wewe ndiwe mpole, mwongofu!

Yaani, kweli wewe una akili kwa haya uyasemayo?

Aya hii inakusanya mambo yafuatayo:-

1. Risala ya mitume haiko kwenye nembo peke yake, bali inakusanya maisha ya kijamii na kumpangia binadamu uhuru wake na matumizi yake na kumwekea mipaka ya kutomwingilia mwingine, vilevile kumzuia kufanya tendo lolote baya litakaloleta madhara kwa mtu binafsi na kwa jamii. Dalili wazi juu ya hilo ni kauli yake Mwenyezi Mungu katika Aya 85 ya sura hii: “wala msiwatilie kasoro watu vitu vyao. Wala msifanye ufisadi katika nchi mkafanya vurugu”

2. Aya imefahamisha kuwa maadui wakubwa wa mitume na wenye kuswali ni wale wanaotafuta mali kwa hadaa na utapeli na kutumia vipato vya watu vile wanavyotaka; kama yanavyofanya mashirika mengi ya ulanguzi na unyonyaji.

3. Vilevile Aya inafahamisha kwamba ubepari una mizizi ya kihistoria.

Ushahidi wa hilo ni mwingi sana. Kwa mfano huu ubepari unaotaka kila mtu awe na uhuru wa kupata utajiri vile atakavyo, iwe ni kwa uporaji au kwa lolote lile. Hilo linafafanuliwa na kauli ya waliomdodosa Shuaib: “Au kufanya tupendavyo katika mali zetu” Makusudio sio kula na kuvaa watakavyo; isipokuwa ni kuwatumia watu katika kupata mali vile wapendavyo.

Kama ambavo historia imeonyesha kuwa siasa za Ubepari zilianza zamani, vilevile inafahimisha historia kuwa Ukomonisti nao ulianza zamani. Imeelezwa katika uchunguzi wa mwanahistoria W.L. Dewarnet kwamba watafiti walipata ubao wa Sumeria ambao tarehe yake inarudi kwenye mwaka 2100, kabla ya kuzaliwa Nabii Issa, ukisema kuwa Serikali ndiyo inayopanga mwelekeo wa kiuchumi.

Katika Babilon, mnamo mwaka wa 1750, kabla ya kuzaliwa Nabii Issa, Sheria ya Hamurabi ndiyo iliyokuwa ikipanga bei za kila kitu. Na katika zama za Batholomeo, serikali ndiyo iliyokuwa ikimiliki ardhi na kuongoza kilimo na mengimeyo.

Uislamu haukubaliani na siasa za ubepari wala za ukomonisti kwa maana yake yaliyo mashuhuri; isipokuwa unakubaliana na kila linalotatua matati- zo ya maisha bila ya kuwapunguzia watu vitu vyao. Angalia kifungu, ‘Tajiri ni wakili sio mweneyewe’ katika kufasiri Juz. 4 (3:182)

Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa ni dalili iliyo wazi itokayo kwa Mola wangu?

Imetangulia Aya kama hii katika Aya 28 ya sura hii.

Na ameniruzuku riziki njema itokayo kwake?

Baada ya Shuaib kuwaamrisha watu wake wachume kihalali na kuwakataza haramu, aliwapa hoja ya riziki aliyoruzukiwa na Mwenyezi Mungu, inayotosheleza mahitaji yake yote, pamoja nakuwa yeye yuko mbali na haramu.

Kwa hiyo basi sababu za riziki nzuri sio haramu. Ni jambo lisilowezekana kwa Mwenyezi Mungu afungue mlango wa riziki kisha awanyime waja wake. Kauli yake: Na ameniruzuku riziki njema, inaonyesha alikuwa na maisha mazuri.

Wala sipendi kuwakhalifu nikafanya yale ninayowakataza.

Lau angelifanya hivyo wao wangelikuwa na hoja juu yake. Na katika sharti za mtume ni kuwa sifa zake zote ziwe ni za kuvutia sio za kufukuza. Na ilivyo ni kuwa anayesema asiyoyafanya basi atakimbiwa.

Sitaki ila kutengeneza kiasi ninavyoweza.

Na mtengenezaji huwaonya watu kwa vitendo vyake kabla ya maneno yake. Na kuendeleza mwito wake huku akivumlia adha na mashaka. Ndio maana Shuaib na mitume wengineo walikuwa wakila kutokana na kazi ya mikono yao na walikuwa wakivumilia adha kutoka kwa makafiri na wapinzani.

Na taufiki yangu haiko ila kwa Mwenyezi Mungu. Kwake ninategemea na kwake naelekea.

Yaani kwamba yeye ataendelea kutekeleza risala yake kwa hali yoyote itakavyokuwa, akiwa anamtegemea Mwenyezi Mungu, kutaka msaada wake na kumrejea yeye katika mambo yake.

Na enyi watu wangu! Kupingana nami kusije kukawapelekea yakawasibu kama yaliyowasibu kaumu ya Nuh au kaumu ya Hud au kaumu ya Swaleh, na kaumu ya Lut si mbali nanyi.

Yaani uadui wenu kwangu usije ukawasababishia adhabu. Kwani hakuna watu waliomfanyia uadui mtume wao ila huwashukia wao adhabu. Ushahidi wa hayo ni mitume waliotajwa. Ni kama mfano wa anayeambiwa: Usimuudhi baba yako usije ukapatwa na hasira za Mwenyezi Mungu.

Na muombeni maghufira Mola wenu kisha mtubie kwake.

Umepita mfano wake pamoja na tafsir yake katika Aya ya 52 na 61 ya Sura hii.

Hakika Mola wangu ni Mwenye kurehemu Mwenye upendo.

Mwenye kurehemu anayemtaka maghufira na Mwenye upendo kwa kuwaneemesha waja wake, kuwapa nasaha na kuapa muda ili wapate kurejea.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

قَالُوا يَا شُعَيْبُ مَا نَفْقَهُ كَثِيرًا مِّمَّا تَقُولُ وَإِنَّا لَنَرَاكَ فِينَا ضَعِيفًا وَلَوْلَا رَهْطُكَ لَرَجَمْنَاكَ وَمَا أَنتَ عَلَيْنَا بِعَزِيزٍ ﴿٩١﴾

91. Wakasema: Ewe Shuaib! Hatufahamu mengi ya hayo unayoyasema; na sisi tunakuona kwetu ni mdhaifu. na lau si jamaa zako, bila shaka tungelikurujumu. Wala wewe si Mtukufu kwetu.

قَالَ يَا قَوْمِ أَرَهْطِي أَعَزُّ عَلَيْكُم مِّنَ اللَّـهِ وَاتَّخَذْتُمُوهُ وَرَاءَكُمْ ظِهْرِيًّا إِنَّ رَبِّي بِمَا تَعْمَلُونَ مُحِيطٌ ﴿٩٢﴾

92. Akasema: Enyi watu wangu! Kwani jamaa zangu ni watukufu zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu? Na Yeye mmemuweka nyuma ya migongo yenu? Hakika Mola wangu ni mwenye kuyazunguka yote mnayoyatenda.

وَيَا قَوْمِ اعْمَلُوا عَلَىٰ مَكَانَتِكُمْ إِنِّي عَامِلٌ سَوْفَ تَعْلَمُونَ مَن يَأْتِيهِ عَذَابٌ يُخْزِيهِ وَمَنْ هُوَ كَاذِبٌ وَارْتَقِبُوا إِنِّي مَعَكُمْ رَقِيبٌ ﴿٩٣﴾

93. Enyi watu wangu! Fanyeni muwezavyo, mimi ninafanya. Karibuni mtajua ni nani itakayemfika adhabu itakayomfedhehesha na nani aliye mwongo. Na ngojeni nami ninangoja pamoja nanyi.

وَلَمَّا جَاءَ أَمْرُنَا نَجَّيْنَا شُعَيْبًا وَالَّذِينَ آمَنُوا مَعَهُ بِرَحْمَةٍ مِّنَّا وَأَخَذَتِ الَّذِينَ ظَلَمُوا الصَّيْحَةُ فَأَصْبَحُوا فِي دِيَارِهِمْ جَاثِمِينَ ﴿٩٤﴾

94. Ilipofika amri yetu tulimwokoa Shuaib na walioamini pamoja naye, kwa rehema itokayo kwetu. Na ukelele ukawaangamiza wale waliodhulumu, wakapambaukiwa wameanguka kifudifudi katika majumba yao.

كَأَن لَّمْ يَغْنَوْا فِيهَا أَلَا بُعْدًا لِّمَدْيَنَ كَمَا بَعِدَتْ ثَمُودُ ﴿٩٥﴾

95. Kama kwamba hawakuwemo humo. Ehee! (watu wa) Madyan wamepotelea mbali; kama walivyopotelea mbali (watu wa) Thamud.

LAU SI JAMAA YAKO TUNGEKURUJUMU

Aya 91-95

MAANA

Wakasema: Ewe Shuaib! Hatufahamu mengi ya hayo unayoyasema.

Walifahamu vizuri amri, makatazo makemeo na ahadi alizowaambia, isipokuwa walikusudia, kwa kauli yao hii, kwamba vitisho na ahadi walizopewa na Shuaib si lolote kwao.

Kwa vile eti wao ni wasafi. Ibada yao ya masanamu ni safi kwa sababu waaliifanya mababu zao; na kupunja katika vipimo ni kusafi kwa vile ni demokrasia. Kwa hiyo madai ya Shuaib kwao ni kuvuruga amani ya uhuru wao.

Hayo ndiyo maneno ya wanyang’anyi kila mahali na kila wakati. Wanaua na kunyang’anya mali za watu; ukiwaambia wanasema tunataka kuleta amani na demokrasia na wewe unataka kuleta vurugu, kusababisha vita na kuvuruga amani. Kwa sababu amani, wanavyotaka wao, ni kuupigia magoti uovu wao na kusujudia masanamu yao.

Na sisi tunakuona kwetu ni mdhaifu Hakuna wakutuzuia kukukamata, kwa hiyo bora unyamaze. Na lau si jamaa zako, bila shaka tungelikurujumu.

Unaweza kuuliza : imekuwaje kusema kuwa Shuaib ni mdhaifu, lakini watu wake wana nguvu; kwani nguvu za watu wa mtu si ndio nguvu zake?

Jibu : Hakuna kufanana kati ya nguvu mbili; huenda nguvu za watu wa mtu ni dhidi yake sio za kumsaidia yeye. Makuriash walikuwa ndio maadui wakubwa zaidi wa Muhammad mkuraishi.

Baadhi ya wafasiri wanasema kuwa kauli ya lau si jamaa zako, ina maana ya lau si kuwaheshimu jamaa zako. Tamko la Aya linakubaliana na maana haya.

Akasema: Enyi watu wangu! Kwani jamaa zangu ni watukufu zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu?

Ni ajabu gani ya ujinga huu na upotevu?

إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ ﴿٢٨﴾

“Hakika wanomwogopa Mwenyezi Mungu miongoni mwa waja wake ni wale tu wenye elimu” (35: 28).

Na Yeye mmemuweka nyuma ya migongo yenu?

Yaani mmemsahau na kumpuuza.

Enyi watu wangu! Fanyeni muwezavyo, mimi ninafanya niwezavyo.

Huu ni mfano wa kauli yake:

لِّي عَمَلِي وَلَكُمْ عَمَلُكُمْ أَنتُم بَرِيئُونَ مِمَّا أَعْمَلُ وَأَنَا بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٤١﴾

“Mimi nina amali yangu na nyinyi mna amali yenu. Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.” Juz. 11 (10:41).

Na pia kauli yake:

لَكُمْ دِينُكُمْ وَلِيَ دِينِ ﴿٦﴾

“Mna dini yenu nami ninadini yangu” (109:6).

Karibuni mtajua ni nanai itakayemfika adhabu itakayomfedhehesha na nani aliye mwongo. Na ngojeni nami ninangoja pamoja na nyinyi.

Hili ni karipio kutoka kwa Shuaib kwa watu wake kuwa watashukiwa na adhabu. Na hakuna dalili kubwa zaidi, inayofahamisha utume wake, kuliko kuamini ghaibu hii.

Ilipofika amri yetu tulimwokoa Shuaib na walioamini pamoja naye, kwa rehema itokayo kwetu. Na ukelele ukawaangamiza wale waliodhulumu, wakapambaukiwa wameanguka kifudifudi katika majumba yao. Kama kwamba hawakuwemo humo. Ehee! (watu wa) Madyan wamepotelea mbali; kama walivyopotelea mbali (watu wa) Thamud.

Umekwishapita mfano wa Aya hii katika Aya 66-67 ya Sura hii.

وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا مُوسَىٰ بِآيَاتِنَا وَسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ﴿٩٦﴾

96. Na hakika tulimtumma Musa pamoja na Ishara zetu na dalili zilizo wazi

إِلَىٰ فِرْعَوْنَ وَمَلَئِهِ فَاتَّبَعُوا أَمْرَ فِرْعَوْنَ وَمَا أَمْرُ فِرْعَوْنَ بِرَشِيدٍ ﴿٩٧﴾

97. Kwa Firauni na waheshimiwa wake, lakini wao walifuata amri ya Firauni na amri ya Firauni haikuwa yenye uongofu.

يَقْدُمُ قَوْمَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَأَوْرَدَهُمُ النَّارَ وَبِئْسَ الْوِرْدُ الْمَوْرُودُ ﴿٩٨﴾

98. Siku ya Kiyama atawatangulia watu wake na atawaingiza motoni. Ni pabaya mno mahala pa kufikiwa.

وَأُتْبِعُوا فِي هَـٰذِهِ لَعْنَةً وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ بِئْسَ الرِّفْدُ الْمَرْفُودُ ﴿٩٩﴾

99. Na wamefuatishiwa laana katika (dunia) hii na siku ya Kiyama ni kibaya mno watakachopewa.

MUSA

Aya 96-99

MAANA

Alipomaliza, Mwenyezi Mungu (s.w.t), kutaja yaliyowapata watu wa Nuh, Hud, Swaleh, Lut, Na wa Shuaib, ameashiria kwa Firaun na kaumu yake. Na lengo ni mazingatio na mawaidha.

Kwa muhtasari Aya hizi nne zinazungumzia kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimtumma Mussa(a.s) kwa Firauni na watu wake kwa hoja na dalili zilizo wazi. Miongoni mwazo ni fimbo na mkono, lakini Firauni aling’angania ukafiri na utaghuti; kama alivyowalazimisha watu wake wamfuate na wafuate amri zake.

Mwisho wa wafuasi na anyefuatwa ukawa ni laana na maangamizi hapa duniani na Akhera.

Lau Firaun asingepata wafuasi na wasaidizi, basi asingeweza kujasiri na kusema:

أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

“Mimi ndiye Mola wenu mkubwa” (79:24) na

مَا عَلِمْتُ لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرِي ﴿٣٨﴾

“Simjiu kwa ajili yenu Mungu asiyekuwa mimi” (28:38)

Mfisadi na mpotezaji yoyote hawezi kujitokeza ila baada ya kupata wafuasi.

Tabia ya binadamu iko hivyo wakati wowote, linalobadilika ni jina na mfumo tu. Zamani kulikuwa na Firauni na Namrud, leo ni majeshi ya ushirika na mashirika kama vile ARAMCO n.k. Ama wafuasi na wasaidizi ni wale wanaokabidhiwa majukumu na kuonekana ndio watukufu baina ya watu.

ذَٰلِكَ مِنْ أَنبَاءِ الْقُرَىٰ نَقُصُّهُ عَلَيْكَ مِنْهَا قَائِمٌ وَحَصِيدٌ ﴿١٠٠﴾

100. Hizo ni habari za miji tunazokusimulia, mingine bado ipo na mingine imefyekwa.

وَمَا ظَلَمْنَاهُمْ وَلَـٰكِن ظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ فَمَا أَغْنَتْ عَنْهُمْ آلِهَتُهُمُ الَّتِي يَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مِن شَيْءٍ لَّمَّا جَاءَ أَمْرُ رَبِّكَ وَمَا زَادُوهُمْ غَيْرَ تَتْبِيبٍ ﴿١٠١﴾

101. Nasi hatukuwadhulumu, lakini wao wamejidhulumu wenyewe. Na miungu yao waliyokuwa wakiiabudu badala ya Mwenyezi Mungu, haikuwafaa kitu ilipofika amri ya Mola wako, na haikuwazidishia isipokuwa maangamizi.

وَكَذَٰلِكَ أَخْذُ رَبِّكَ إِذَا أَخَذَ الْقُرَىٰ وَهِيَ ظَالِمَةٌ إِنَّ أَخْذَهُ أَلِيمٌ شَدِيدٌ ﴿١٠٢﴾

102. Na ni kama hivyo kushika kwa Mola wako anapoishika miji inapokuwa imedhulumu. Hakika kushika kwake ni kuchungu, kukali.

HABARI ZA MIJI

Aya 100-102

MAANA

Hizo ni habari za miji tunazokusimulia, mingine bado ipo na mingine imefyekwa.

Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja sehemu ya visa katika umma zilizopita pamoja na mitume yao, alimwambia mtume mtukufu(s.a.w.w) kwamba baadhi ya umma hizo athari zake bado zipo na nyingine athari zake hazipo.

Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa ambazo athari zake zimebakia ni miji ya Aa’d na Thamud, na zile ambazo hazikubakia athari zake ni miji ya Nuh. Ama sisi tunawachia wataalamu wa mambo ya kale.

Kwa hali yoyote iwayo, ni kuwa ubainifu wa kisa hiki kwa ulimi wa Muhammad(s.a.w.w) ni dalili mkataa ya utume wake na kwamba ni wahyi wa kutoka kwa Mwenyezi Mungu sio njozi wala nukuu ya yaliyosemekana.

Nasi hatukuwadhulumu, lakini wao wamejidhulumu wenyewe kwa kumkadhibisha kwao mtume wa Mwenyezi Mungu na kung’ang’ania kwao shirki na ufisadi. Maana haya yamekaririka katika Katika Qur’ani kwa karibu Aya ishirini.

Na miungu yao waliyokuwa wakiiabudu badala ya Mwenyezi Mungu, haikuwafaa kitu ilipofika amri ya Mola wako, na haikuwazidishia isipokuwa maangamizi.

Miungu yao ni masanamu yao. Maana yanaupishwa na kauli yake:

وَيَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَنفَعُهُمْ وَلَا يَضُرُّهُمْ ﴿٥٥﴾

“Na wanaabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu yasiyowafaa wala kuwadhuru” (25:55)

Na ni kama hivyo kushika kwa Mola wako anapoishika miji inapokuwa imedhulumu.

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t). Atawaangamiza makafiri, madhlimu kama mfano wa tufani, tetemeko na ukelele wa adhabu.

Hakika kushika kwake ni kuchungu, kukali, lakini ni baada ya onyo na hoja kupitia mitume wakionya ana kwa ana.

Tumesema ana kwa ana, kwa sababu hivi sasa ukafiri na ufisadi ni mwingi kuliko hapo zamani, na maonyo yapo, ya kiakili, vitabu vya mbinguni na hadith za Mtume, lakini pamoja na hayo, hakuna matufani wala mitetemeko au mawe ya udongo mkavu.

Hatujui siri ya hilo, isipokuwa kudhani kuwa matakwa ya Mwenyezi Mungu yamehukumia maangamivu ya wale wanaowapinga mitume wao ana kwa ana; na sio wale wanaoasi wahyi na akili. Lakini dhana haitoshelezi kitu haki. Na Mwenyezi ndiye Mjuzi zaidi.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّمَنْ خَافَ عَذَابَ الْآخِرَةِ ذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّجْمُوعٌ لَّهُ النَّاسُ وَذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّشْهُودٌ ﴿١٠٣﴾

103. Hakika katika hayo kuna Ishara kwa yule anayeogopa adhabu ya Akhera. Hiyo ndiyo siku itakayokusanyiwa watu na hiyo ndiyo siku itakayoshuhudiwa.

وَمَا نُؤَخِّرُهُ إِلَّا لِأَجَلٍ مَّعْدُودٍ ﴿١٠٤﴾

104. Na hatuiakhirishi ila kwa muda unaohisabiwa.

يَوْمَ يَأْتِ لَا تَكَلَّمُ نَفْسٌ إِلَّا بِإِذْنِهِ فَمِنْهُمْ شَقِيٌّ وَسَعِيدٌ ﴿١٠٥﴾

105. Siku itakapofika, nafsi yoyote haitasema ila kwa kwa idhini yake. Katika wao kuna waovu na wengine ni wema.

فَأَمَّا الَّذِينَ شَقُوا فَفِي النَّارِ لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَشَهِيقٌ ﴿١٠٦﴾

106. Ama wale waovu watakuwa motoni watachachatika na kukorama.

خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ إِنَّ رَبَّكَ فَعَّالٌ لِّمَا يُرِيدُ ﴿١٠٧﴾

107. Watadumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipokuwa apendavyo Mola wako. Hakika Mola wako hufanya atakavyo.

وَأَمَّا الَّذِينَ سُعِدُوا فَفِي الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ السَّمَاوَاتُ وَالْأَرْضُ إِلَّا مَا شَاءَ رَبُّكَ عَطَاءً غَيْرَ مَجْذُوذٍ ﴿١٠٨﴾

108. Ama wale wema watakuwa Peponi watadumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipokuwa apendavyo Mola wako. Ni kipawa kisicho na ukomo.

فَلَا تَكُ فِي مِرْيَةٍ مِّمَّا يَعْبُدُ هَـٰؤُلَاءِ مَا يَعْبُدُونَ إِلَّا كَمَا يَعْبُدُ آبَاؤُهُم مِّن قَبْلُ وَإِنَّا لَمُوَفُّوهُمْ نَصِيبَهُمْ غَيْرَ مَنقُوصٍ ﴿١٠٩﴾

109. Basi usiwe na shaka na wanayo yaabudu hao. Hawaabudu ila kama walivyoabudu baba zao zamani. Na hakika sisi tutawatimizia fungu lao bila ya kupunguzwa.

SIKU ITAKAYOSHUHUDIWA

Aya 103 – 109

MAANA

Hakika katika hayo kuna ishara kwa yule anayeogopa adhabu ya Akhera. Hiyo ndiyo siku itakayokusanyiwa watu na hiyo ndiyo siku itakayoshuhudiwa.

Hayo ni ishara ya kuadhibu kwake Mwenyezi Mungu vijiji. Yaani katika kuadhibu huku kuna mazingatio kwa mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na ni waadhi kwa anayeogopa adhabu ya siku watakayoishuhudia viumbe wote, pale atakapowakusanya kwa ajili ya hisabu na malipo.

Unaweza kuuliza kuwa : tufani au tetemeko na mfano wake mara nyingi huzuka kwa sababu za kimaumbile na maumbile hayawezi kumpambanua mwema na muovu. Je, haiwezekani kuwa yaliyowatokea kaumu za mitume ni aina hii?

Jibu : Mtume alikuwa akiwaonya watu wake kwa kuzuka adhabu na kuieleza aina ya adhabu yenyewe na wakati wa kutokea kwake.

Nayo hutokea kama ilivyoelezwa. Kwa hiyo haiwezekani kuipa tafsiri ya ugunduzi wa kielimu, kwani wakati huo hakukuwa na nyenzo zozote za kielimu, wala hatuwezi kuitafsiri kua ni kawaida ya maumbile, kwa sababu Mtume alikuwa akielezea kwa kujiamini; akisema huu ndio uhakika na mtaona.

Kama ambavyo pia haiwezekani tafsiri ya sadfa kutokana na kukaririka. Ikiwa tafsiri zote hizi haziwezekani, basi inabaki tafsiri ya wahyi na matakwa ya Mwenyezi Mungu peke yake.

Na hatuiakhirishi ila kwa muda unaohisabiwa.

Kila kitu mbele ya Mwenyezi Mungu kina muda wake, hautangulii wala kuchelewa. Miongoni mwavyo ni kuisha dunia na kuja Akhera.

Siku itakapofika, nafsi yoyote haitasema ila kwa idhini yake.

Itapewa idhini ya kujitetea kama ilivyo katika mahakama za kidunia.

Katika wao kuna waovu na wengine ni wema.

Uovu wa mtu au wema wake kesho utakuwa kwa matendo yake tu hapa duniani.

Ile kauli ya “Muovu ni muovu tangu tumboni mwa mama yake na mwema ni mwema tangu tumboni mwa mama yake,” inatiliwa mashaka. Kwa sababu dhahiri yake inapingana na uadilifu wake Mwenyezi Mungu na rehema yake; mbali ya kuwa ni hadith Ahaad ambayo ni hoja katika hukumu za kisharia tu; kama halali, haramu, twahara na najisi; sio katika misingi ya itikadi na yanayoambatana nayo.

Kisha akawaelezea wale watakaokuwa waovu kwa kusema:

Ama wale waovu watakuwa motoni watachachatika na kukoroma.

Kimsingi ni kuwa Mwenyezi Mungu humwadhibu mfisadi. Kwa hiyo basi uovu anauchumma mwenyewe mtu; sio kwa kadha na kadari.

kuchachatika na kukoroma ni kuelezea uchungu wa watu wa motoni.

Watadumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipokuwa apendavyo Mola wako.

Wafasiri wamerefusha maneneno sana kuhusu makusudio ya ‘apendavyo Mwenyezi Mungu,’ hapa. Wakataja njia zilizofanya Aya iwe yenye kutatiza na yenyewe siyo ya kutatiza, bali iko wazi.

Kwa ufupi ni kuwa mwenye kuingia Jahannam kwa dhambi yoyote ile, hataweza kutoka humo yeye mwenyewe, si kwa kuombewa wala kwa fidia. Kwa namna hiyo ndiyo inasemwa ni mwenye kudumu. Lakini Mungu akitaka atoke humo atatoka na ataondokewa na wasifa wa kudumu motoni. Kwa sababu matakwa ya Mwenyzi Mungu, hayazuiwi na kitu chochote.

Hakika Mola wako hufanya atakavyo.

Na kila kitu mwisho wake unarejea kwenye matakwa yake wala matakwa yake hayarejei isipokuwa kwake. Kwa hiyo sababu ya kudumu itafanyakazi madamu muumbaji anataka hivyo na asipotaka basi haiwi.

إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

“Hakika amri yake anapotaka chochote ni kukiambia: Kuwa, kikawa” (36:82)

Kama alivyowaelezea walio mashakani kuwa watadumu motoni, vile vile amewaeelezea wenye furaha kuwa ni wenye kudumu Peponi.

Ama wale wema watakuwa Peponi watadumu humo muda wa kudumu mbingu na ardhi, isipokuwa apendavyo Mola wako. Ni kipawa kisicho na ukomo. Yaani hakikatiki.

Unaweza kuuliza kwamba : mwenye kuingia pepeoni hatoki, sasa kuna haja gani ya kukuwekea matakwa ya Mwnyezi Mungu?

Imesemekana kuwa Mwenyezi Mungu atawatoa kutoka pepo moja hadi nyingine mfano wake au nzuri zaidi.

Tuonavyo sisi ni kuwa hilo ni kiasi cha kuashiria uweza wa Mwenyezi Mungu na ukuu wake, na kwamba sababu zinafanya kazi ikiwa hazikugongana na matakwa ya Mwenyezi Mungu.

Kwa hiyo moto utaunguza ikiwa mwenyezi Mungu hakuuambia kuwa baridi na salama.

Basi usiwe na shaka na wanayoyaabudu hao.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) . Na hao ni ishara ya watu wake waliomkadhibisha. Muhammad hakuwa wala hatakuwa na shaka kwamba wao wako kwenye ubatilifu katika ibada yao, lakini lengo ni kuwatahayariza na kuwahadharisha.

Hawaabudu ila kama walivyoabudu baba zao zamani.

Hii ni sababu ya yakini ya kutokuwepo shaka katika kubatilika wanayoaabudu hawa. Kwa sababu ni mfano wa walivyoabudu wa kwanza ambao walipatwa na adhabu kwa sababu ya shirki yao na kuabudu kwao masanamu.

Na hakika sisi tutawatimizia fungu lao bila ya kupunguzwa.

Sawa na tulivyotimiza fungu la adhabu waliyostahaiki mababa zao bila ya kupunguza kitu.

Unaweza kuuliza : Huku sikukatisha tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu? Na Mwenyezi Mungu amesema:

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ ﴿٥٣﴾

“Enyi waja wangu waliojidhulumu msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu” (39:53).

Jibu : Hakika makusudio ya kauli yake, Msikate tamaa ni kuhimiza katika toba na kwamba mwenye kutubia Mwenyezi Mungu humtakabalia toba yake.

Na makusudio ya bila kupunguzwa ni kwamaba mwenye kung’ang’ania shirki na wala asitubie, Mungu atamlipa anavyostahiki.

Sisi hatuna shaka kwamba Mwenyezi Mungu anasamehe na kumhurumia anayewahurumia watu, na anayefanya kwa maslahi ya watu. Ama wale wanaoingilia uhuru na ahaki zao, hawatapunguziwa adhabu wala hawatasaidiwa.