TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 11031
Pakua: 2045


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11031 / Pakua: 2045
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

Mwandishi:
Swahili

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

Surah Ya Kumi na Mbili: Surat Yusuf

Sura hii imeshuka Makka. Tabrasi akimnukuu Ibn Abbas, anasema kuwa kuna aya nne zilizoshuka Madina ambazo ni: 1,2,3,8.Ina Aya 111.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

الر تِلْكَ آيَاتُ الْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿١﴾

1. Alif laam raa. Hizo ni Aya za Kitabu kinachobainisha

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لَّعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿٢﴾

2. Hakika sisi Tumeiteremsha Qur’ani kwa kiarabu ili mpate kutia akilini.

نَحْنُ نَقُصُّ عَلَيْكَ أَحْسَنَ الْقَصَصِ بِمَا أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ هَـٰذَا الْقُرْآنَ وَإِن كُنتَ مِن قَبْلِهِ لَمِنَ الْغَافِلِينَ ﴿٣﴾

3. Sisi tunakusimulia simulizi nzuri sana kwa kukupa wahyi Qur’ani hii. Na hakika kabla ya haya ulikuwa miongoni mwa wasio na habari.

AYA ZA KITABU KINACHOBAINISHA

Aya 1-3

MAANA

Alif laam raa.

Umetangulia mfano wake katika mwanzo wa sura Baqara. Juz. 1 (2:1)

Hizo ni Aya za Kitabu kinachobainisha.

Hizo ni ishara ya Aya za sura hii na Kitabu kinachobainisha ni Qur’ani. Mwenyezi Mungu amekisifu kuwa ni chenye kubainisha, kwa sababu kinauweka wazi utume wa Muhammad(s.a.w.w) na kinadhihirisha uongofu

Hakika sisi Tumeiteremsha Qur’ani kwa kiarrabu ili mpate kutia akilini.

Maana yako ya wazi kwamba Mwenyezi Mungu ameiteremsha kwa lugha ya kiarabu ili watambue siri yake na utukufu wake, wayafahamua maana yake na wayatumie. Unaweza kuuliza: Muhammad ametumwa kwa watu wote kama inavyose-ma Qur’ani:

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا ﴿٢٨﴾

“Na hatukukutumua ila kwa watu wote uwe mbashiri na muonyaji” (34:28).

Na kuteremshwa Qur’ani kwa lugha ya kiarabu kunafahamisha kuwa yeye ni wa Waarabu tu, si wa wengine. Sasa tutazioanishaje Aya mbili hizi?

Jibu :Kwanza : kuteremshwa Qur’ani kwa Lugha ya kiarabu hakummaaanishi kuwa waarabu peke yao ndio wanaokalifiwa na hukumu zake na mafunzo yake. Qura’ni yenyewe na wale wanaoiamini wanaisadikisha Tawrat iliyoteremshiwa Musa(a.s) na Injil iliyoteremshiwa Issa(a.s) na lugha ya vitabu hivyo siyo lugha ya Qur’ani wala ya wale wanayoiamini.

Pili : lugha ni nyenzo na maana ndio lengo. Haiwezekani kuwa maana yahusike na kaumu fulani tu. Kwani watu wote wanaamini ukaumu wa binadamu. Kwa maneno mengine lugha inahusika na watu fulani, lakini maana yanawaenea wote, hayana kundi fulani wala jinsi fulani.

Tatu ; ikiwa Mtume hatatumwa kwa lugha ya watu wake basi ataleta ujumbe kwa lugha gani na hakuna lugha inayozungumzwa na wote? Hapa ndipo inafichuka siri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَمَا أَرْسَلْنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا بِلِسَانِ قَوْمِهِ لِيُبَيِّنَ لَهُمْ ﴿٤﴾

“Na hatukumtumma Mtume yeyote ila kwa lugha ya watu wake ili apate kuwabainishia.” (14:4).

Sisi tunakusimulia simulizi nzuri sana kwa kukupa wahyi Qur’ani hii.

Makusudio ya simulizi ni habari za mitume zilizokuja katika Qur’ani Tukufu, nazo ni habari nzuri sana kutokana na mafunzo na hekima zili- zomo ndani yake.

Na hakika kabla ya haya ulikuwa miongoni mwa wasio na habari.

Kwa sababu yalitokea karne zilizopita nayo hayajulikani kiujumla. Hii ni dalili mkataa kwamba ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ رُوحًا مِّنْ أَمْرِنَا مَا كُنتَ تَدْرِي مَا الْكِتَابُ وَلَا الْإِيمَانُ ﴿٥٢﴾

“Na kama hivyo tulikupa wahyi roho (Qur’ani) kwa amri yetu. Hukuwa ukijua Kitabu ni nini wala imani.” (42:52).

Mwenye kuisoma vizuri Qur’ani, akayazingatia maana yake ataishia kuamini kwamba hakuna anayeweza kujua yote isipokuwa yule ambaye kila kitu amekizunguka kwa ujuzi wake.”

إِذْ قَالَ يُوسُفُ لِأَبِيهِ يَا أَبَتِ إِنِّي رَأَيْتُ أَحَدَ عَشَرَ كَوْكَبًا وَالشَّمْسَ وَالْقَمَرَ رَأَيْتُهُمْ لِي سَاجِدِينَ ﴿٤﴾

4. Yusuf alipomwambia baba yake: Ewe baba yangu! Hakika mimi nimeota nyota kumi na moja na jua na mwezi nimeota zikinisujudia.

قَالَ يَا بُنَيَّ لَا تَقْصُصْ رُؤْيَاكَ عَلَىٰ إِخْوَتِكَ فَيَكِيدُوا لَكَ كَيْدًا إِنَّ الشَّيْطَانَ لِلْإِنسَانِ عَدُوٌّ مُّبِينٌ ﴿٥﴾

5. Akasema: Ewe mwanagu! Usiwasimulie ndugu zako ndoto yako wasije wakakufanyia vitimbi. Hakika Shetani ni adui aliye dhahiri kwa mtu.

وَكَذَٰلِكَ يَجْتَبِيكَ رَبُّكَ وَيُعَلِّمُكَ مِن تَأْوِيلِ الْأَحَادِيثِ وَيُتِمُّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَعَلَىٰ آلِ يَعْقُوبَ كَمَا أَتَمَّهَا عَلَىٰ أَبَوَيْكَ مِن قَبْلُ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْحَاقَ إِنَّ رَبَّكَ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴿٦﴾

6. Na kadhalika Mola wako atakuteua na atakufundisha tafsiri ya mambo. Na atatimiza neema yake juu yako na juu ya ukoo wa Ya’qub; kama alivyowatimizia hapo zamani baba zako Ibrahim na Is-haq. Hakika Mola wako ni Mjuzi, Mwenye hekima.

NYOTA KUMI NA MBILI

Aya 4-6

MAANA

Yusuf alipomwambia baba yake: Ewe baba yangu! Hakika mimi nimeota nyota kumi na moja na jua na mwezi nimeota zikinisujudia.

Yusuf ni mtoto wa Ya’qub mtoto wa Is-haq mtoto wa Ibrahim Khalil(a.s ) . Ya’qub ndiye Israil. Maana ya Israil, wakati huo, ilikuwa ni Abdullah (Mtumishi wa Mwenyezi Mungu), lakini wakati huu ni mtumishi wa ukoloni na jeshi lake.

Siku moja Yusuf aliota ndoto aliyomsimulia baba yake Ya’qub. Nayo ni kwamba yeye aliona usingizini nyota kumi na moja na jua na mwezi zikimsujudia. Hapo baba yake akajua kuwa ndoto hii ni ya kweli, akapata bishara ya mustakbali wa mwanawe.

Kuna tafsiri zisemazo kuwa umri wa Yusuf wakati huo ulikuwa ni miaka saba; wala hatujui rejea sahii za kipimo hiki. Lakini ukweli ni kuwa yeye, wakati huo, alikuwa ni kijana mwenye haiba na mwenye sura nzuri, akipigiwa mfano kwa uzuri wake; kama itakavyobainika katika masimulizi ya kisa.

Nyota kumi na moja ni ndugu zake na jua na mwezi ni baba na mama yake. Hayo yanafahamika kutokana na kauli yake itakayokuja mbele kwenye Aya 100: “Hii ndiyo tafsir ya ile ndoto yangu” Ufafanuzi unafuatia.

Akasema ewe mwanagu! Usiwasimulie ndugu zako ndoto yako wasije wakakufanyia vitimbi. Hakika Shetani ni adui aliye dhahiri kwa mtu.

Baba yake alihofia ndugu zake wakisikia aliyomsimulia na wakafahamu alivyofahamu yeye wasije wakadhihirisha chuki yao kwake na wasighilibiwe na Shetani kwa kumfanyia vitimbi vya kumwangamiza. Kwa vile alijua wivu wao kwake kutokana na kumpenda sana na kutukuza kwake. Kwa hiyo akamnasihi asiwasimule ndoto yake. Tutaizungumzia ndoto mahali pake, inshaallah.

Na kadhalika Mola wako atakuteua na atakufundisha tafsiri ya mambo.

Kukuteua ni kukuchagua wewe si mwingine na kukujaza aina za karama. Imesemekana makusudio ya kutafsiri mambo ni kutafsiri ndoto, kwa vile Yusuf alikuwa na kiwango cha juu cha kutafsiri ndoto, lakini dhahiri ya neno inaenea zaidi ya hivyo. Linalonasibiana na utume wa Yusuf ni kuwa tafsri ya mambo ni fumbo la kujua hakika ya mambo na kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) atamfundisha ambayo hakuwa akiyajua.

Na atatimiza neema yake juu yako na juu ya ukoo wa Ya’qub; kama alivyowatimizia hapo zamani baba zako Ibrahim na Is-haq.

Nema za Mwenyezi Mungu hazihisabiki na ukamilifu wake ni unabii na utume. Na amewaneemesha nao Ibrahim babu wa Ya’qub na Is-haq babu wa Yusuf na Ya’qub mwenyewe. Pia na atamneemesha nao Yusuf baada ya ndoto hii na wengineo katika wajukuu wa Ya’qub.

Hakika Mola wako ni Mjuzi Mwenye hekima.

Anamjua anayemchagua na kumteua kwa ujumbe na ana hekima katika uteuzi huo na katika mambo yote.

لَّقَدْ كَانَ فِي يُوسُفَ وَإِخْوَتِهِ آيَاتٌ لِّلسَّائِلِينَ ﴿٧﴾

7. Kwa hakika katika Yusuf na ndugu zake kuna ishara kwa wanaouliza.

إِذْ قَالُوا لَيُوسُفُ وَأَخُوهُ أَحَبُّ إِلَىٰ أَبِينَا مِنَّا وَنَحْنُ عُصْبَةٌ إِنَّ أَبَانَا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٨﴾

8. Waliposema: Hakika Yusuf na nduguye wanapendwa zaidi na baba yetu kuliko sisi na hali sisi ni kikundi imara. Hakika baba yetu yumo katika upotevu dhahiri.

اقْتُلُوا يُوسُفَ أَوِ اطْرَحُوهُ أَرْضًا يَخْلُ لَكُمْ وَجْهُ أَبِيكُمْ وَتَكُونُوا مِن بَعْدِهِ قَوْمًا صَالِحِينَ ﴿٩﴾

9. Muuweni Yusuf au mtupeni nchi ya mbali, uso wa baba yenu utawaelekea nyinyi. Na baada ya haya mtakuwa ni watu wema.

قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ لَا تَقْتُلُوا يُوسُفَ وَأَلْقُوهُ فِي غَيَابَتِ الْجُبِّ يَلْتَقِطْهُ بَعْضُ السَّيَّارَةِ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ ﴿١٠﴾

10. Akasema msemaji kati yao: Msimuue Yusuf, lakini mtumbukizeni ndani ya kisima, watamuokota baadhi ya wasafiri, ikiwa nyinyi ni wenye kufanya.

قَالُوا يَا أَبَانَا مَا لَكَ لَا تَأْمَنَّا عَلَىٰ يُوسُفَ وَإِنَّا لَهُ لَنَاصِحُونَ ﴿١١﴾

11. Wakasema: Ewe baba yetu! Mbona hutuamini kwa Yusuf na hakika sisi ni wenye kumnasihi.

أَرْسِلْهُ مَعَنَا غَدًا يَرْتَعْ وَيَلْعَبْ وَإِنَّا لَهُ لَحَافِظُونَ ﴿١٢﴾

12. Mpeleke kesho pamoja nasi afaidi na acheze, na bila shaka sisi tutamhifadhi.

قَالَ إِنِّي لَيَحْزُنُنِي أَن تَذْهَبُوا بِهِ وَأَخَافُ أَن يَأْكُلَهُ الذِّئْبُ وَأَنتُمْ عَنْهُ غَافِلُونَ ﴿١٣﴾

13. Akasema: Kwa hakika inanihuzunisha kwamba nyinyi mwende naye, na ninahofia asije mbwa mwitu akamla nanyi mmeghafilika naye.

قَالُوا لَئِنْ أَكَلَهُ الذِّئْبُ وَنَحْنُ عُصْبَةٌ إِنَّا إِذًا لَّخَاسِرُونَ ﴿١٤﴾

14. Wakasema: Ikiwa mbwa mwitu atamla na sisi ni kundi imara, basi hakika sisi tutakuwa kwenye hasara.”

فَلَمَّا ذَهَبُوا بِهِ وَأَجْمَعُوا أَن يَجْعَلُوهُ فِي غَيَابَتِ الْجُبِّ وَأَوْحَيْنَا إِلَيْهِ لَتُنَبِّئَنَّهُم بِأَمْرِهِمْ هَـٰذَا وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿١٥﴾

15. Basi walipokwenda naye na wakakubaliana wamtumbukize ndani ya kisima. Na tukampa wahyi bila shaka utakuja waambia jambo lao hili na hali hawatambui.

YUSUF NA NDUGUZE

Aya 7-15

MASILAHI KULIKO UDUGU

Binadamu ni mtumwa wa hisia zake, ni vigumu kuepukana nazo au kujipu- rukusha nazo. Kwa nini? Kwani inawezekana kukiepusha kitu na dhati yake? Kitu cha kwanza cha hisia hizi ni masilahi; yaani kutaka raha na kufukuza machungu. Maamuzi ya kufanya au kuacha jambo yanategemea masilahi.

Ama udugu si chochote ikiwa hauna raha au kuweka mbali machungu. Kwa hiyo kiwango cha pendo la mtu kwa jamaa zake linapimwa kwa masilahi haya. Mfano mzuri wa hilo ni kwamba huzuni na masikitiko ya kumpoteza ndugu yanakuja kutokana na kiwango cha alivyokuwa akinufaika naye wakati alipokuwa hai; kama ambavyo ndugu anaweza kuwa adui mkubwa akiwa anasababisha machungu au kuharibu raha na ladha.

Ni akina mama wangapi wamewaua watoto wao kwa sababu ya starehe tu?[2] Ni watoto wangapi wamewaua wazazi wao kwa sababu ya kuharakisha mirathi? Qabil alimuua Habil nao ni ndugu waliotokamana na tone moja la manii na wakawa katika mfuko mmoja wa uzazi.

Wana wa israil walimtupa Yusuf kwenye shimo bila ya kuwa na hurumma ya udugu na damu moja.

Ndio Ali, Amirul mumin(a.s) akasema:“ Udugu una haja kubwa zaidi ya mapenzi kuliko mapenzi kwenye udugu.” Hata mapenzi na urafiki chimbuko lake ni ladha ya roho, lakini mara nyingi mtu anjisahau na kusahau uhalisi wake, akaufanya udugu utokane na masilahi.

Kwa hiyo si dharura masilahi yawe ndiyo yanaupeleka utu. Kwani mtu safi aliye na ikhlas anaamini kwa kauli na vitendo kwamba masilahi yake ni masilahi ya jamii. Kwa hiyo anaumia ikiwa jamii inaumia na anafurahi ikiwa inafuraha. Anaona heri ni kuisimamisha haki na uadilifu.

Ama asiyekuwa hivyo basi haoni umuhimu ila umuhimu wake wala maisha isipokuwa maisha yake tu; kama walivyofanya wana wa israil kwa Yusuf ili wapate kupendwa wao na baba yao, lakini matokeo yake ni kuadhibiwa kwa kunyimwa na Mwenyezi Mungu hilo walilolitaka, wakastahiki hasira ya Mwenyezi Mungu na ya mtume wake Ya’qub na Yusuf akapata utukufu na cheo, wakasimama mbele yake wakiwa dhalili huku wakikiri makosa yao na kuomba msamaha kwa kusema: “Wallahi Mwenyezi Mungu amekufadhilisha wewe kuliko sisi na hakika sisi tulikuwa wenye makosa” Aya 91 ya sura hii.

Kwa hakika katika Yusuf na ndugu zake kuna ishara kwa wanaouliza.

Makusudio ya ishara hapa ni mazingatio na mafunzo.

Wana wa israil walimtupa Yusuf shimoni, si kwa lolote ila ni kwamba baba yao alikuwa akimpenda na kumhurumia zaidi. Maquraishi walimpiga vita Muhammad na wakafika kikomo cha kumuudhi, naye ni mquraishi mwenzao, kwa sababu tu Mwenyezi Mungu alimfanya bora kuliko wao na kuliko watu wote. Hata hivyo Mwenyezi Mungu alimnusuru Yusuf na ndugu zake na akamnusuru Muhammad na jamaa zake.

Katika hayo kuna mawaidha na mafunzo kwa wenye kutaka kujua uhakika na kufaidika nao.

Waliposema: Hakika Yusuf na nduguye wanapendwa zaidi na baba yetu kuliko sisi na hali sisi ni kikundi imara. Hakika baba yetu yumo katika upotevu dhahiri.

Maana ya Aya hii na inayoifuatia iko wazi, lakini pamoja na hayo tunaifuatilia kila Aya na yale yanayonasibiana nayo. Wana wa israil walipoona baba yao amelemea zaidi kwa Yusuf na ndugu yake, hasadi na chuki iliwachemka na wakaanza kuulizana: Kwa nini huyu mzee ameathirika na hawa watoto wawili na hali sisi ni wakubwa tena ni wengi wenye nguvu tulio na manufaana kumhudumia? Hakika huyu mzee amepotea.

Yusuf na nduguye, Benjamin, mama yao alikuwa mmoja, aliyeitwa Rachel. Mara nyingi hutokea chuki baina ya watoto kutokana na kuoa wake wengi.

Muuweni Yusuf au mtupeni nchi ya mbali uso wa baba yenu utawaelekea nyinyi.

Walikula njama ya kumuua si kwa chochote ila, ni kwa kutaka kuhodhi mapenzi ya baba yao; kama wanavyokiri wenyewe. Hii ndio mantiki ya wenye kuhodhi na kulimbikiza; ‘uwa na ufukuze’ hata kama ni ndugu wa damu, ili upate faida na chumo.

Na baada ya haya mtakua watu wema.

Wafasiri wanasema kuwa makusudi ya wema hapa ni wema wa dini; kwamba wao watatubia baada ya tendo lao hili ovu. Lakini dhahiri ya mfumo wa maneno inafahamisha kuwa makusudio ni kuwa wema kwa baba yao wao peke yao.

Akasema msemaji kati yao: Msimuue Yusuf, lakini mtumbukizeni ndani ya kisima, watamuokota baadhi ya wasafiri, ikiwa nyinyi ni wenye kufanya.

Katika Tawrat, Kitabu cha mwanzo 37:18-22, imesemwa kuwa aliyeyasema haya ni Reuben na ni ya yake ilikuwa ni kumtoa Yusuf kisimani baada ya kuondoka ndugu zake.

Wakasema: Ewe baba yetu! Mbona hutuamini kwa Yusuf na hakika sisi ni wenye kumnasihi, tunampenda na kumtakia kila la heri. Hivi ndivyo alivyo mwenye hadaa na vitimbi, kila mahali na kila wakati, ni mbwa mwitu katika ngozi ya kondoo.

Mpeleke kesho pamoja nasi afaidi na acheze, na bila shaka sisi tutamhifadhi.

Walijua kwamba baba yao anampenda Yusuf na anapenda afurahi na pia walijua jinsi alivyokuwa akimlinda sana. Kwa hiyo wakamwingilia kwa mlango huo huo. Yusuf anacheza huku wao wakimlinda na jambo lolote baya: ‘kikulacho kinguoni mwao.’

Akasema: Kwa hakika inanihuzunisha kwamba nyinyi mwende naye, na ninahofia asije mbwa mwitu akamla nanyi mmeghafilika naye.

Aliwapa udhuru kwamba yeye hawezi kuachana na Yusuf. Hilo likawazidishia chuki. Pia aliwapa udhuru kwamba anahofia asiliwe na mbwa mwitu. Razi anasema juu ya udhuru huu: Ni kama mbaye amewatafutia hoja. Mithali inasema: “Balaa iliponzwa na ulimi”

Wakasema: Ikiwa mbwa mwitu atamla na sisi ni kundi imara, basi hakika sisi tutakuwa kwenye hasara.

Mzee akaghurika na akawaachia Yusuf nao wakawa ni katika watu walio kwenye hasara.

Basi walipokwenda naye na wakakubaliana wamtumbukize ndani ya kisima, walilitekeleza hilo wakidhani kuwa wamepata yale waliyoyataka, lakini Yusuf alimkabidhi Mwenyezi Mungu mambo yake naye akamlinda na ubaya wa hila walizozifanya.

Na tukampa wahyi bila shaka utakuja waambia jambo lao hili na hali hawatambui.

Mwenyezi Mungu alimtuliza moyo Yusuf kwamba wewe utaokoka kutokana na mitihani yako hii na kwamba utawapa habari ya hili walilolifanya bila ya kukutambua.

BAINA YA WATOTO WA ISRAIL NA WATOTO WA MAULAMA

Kwa mnasaba huu mambo yanyonasibiana kati ya watoto wa maulama wa kidini na watoto wa Israil.

Watoto wa Israil walisema: “Hakika baba yetu yumo katika upotevu dhahiri.” Baadhi ya watoto wa mulama nao husema hivyo hivyo ikiwa wameambiwa na baba zao yale yasiyowapendeza hata kama ni maneno ya Mwenyezi Mungu.

Watoto wa Israil walisema: “Muuweni Yusuf au mtupeni nchi (ya mbali) uso wa baba yenu utawaelekea nyinyi”

Watoto wa maulama nao wanafanya hivyo hivyo. Wanawafanyia njama viongozi wazuri waliowaaminifu, wanawazushia mambo na kuwachafua ili nyuso za baba zao ziwaelekee wao. Wanawafanyia kazi mashetani wao kisha wanapata malipo kwa pesa za kigeni. Athari ikiwa kubwa zaidi na malipo nayo yanakuwa makubwa.

Watoto wa Israil walikuja na kanzu ya Yusuf “ina damu ya uongo” Kila siku baadhi ya watoto wa maulama wanakwenda na uzushi wanaowazushia watu wema, ili wao waonekani wazuri na waaminifu.

Watoto wa Isralil walikuja kwa baba yao “usiku wakilia” wakificha vitendo vyao kwa unafiki na machozi ya mamba.

Vile vile baadhi ya watoto wa maulama, mbele ya baba zao wanajifanya ni wacha Mungu wenye ikhlasi kwa uongo na ria.

وَجَاءُوا أَبَاهُمْ عِشَاءً يَبْكُونَ ﴿١٦﴾

16. Wakaja kwa baba yao usiku wakilia.

قَالُوا يَا أَبَانَا إِنَّا ذَهَبْنَا نَسْتَبِقُ وَتَرَكْنَا يُوسُفَ عِندَ مَتَاعِنَا فَأَكَلَهُ الذِّئْبُ وَمَا أَنتَ بِمُؤْمِنٍ لَّنَا وَلَوْ كُنَّا صَادِقِينَ ﴿١٧﴾

17. Wakasema: Ewe baba yetu! Hakika tulikwenda kushindana mbio na tukamwacha Yusuf kwenye vitu vyetu, basi mbwa mwitu akamla. Na wewe hutatuamini, ijapokuwa tunasema kweli.

وَجَاءُوا عَلَىٰ قَمِيصِهِ بِدَمٍ كَذِبٍ قَالَ بَلْ سَوَّلَتْ لَكُمْ أَنفُسُكُمْ أَمْرًا فَصَبْرٌ جَمِيلٌ وَاللَّـهُ الْمُسْتَعَانُ عَلَىٰ مَا تَصِفُونَ ﴿١٨﴾

18. Na wakaja na kanzu yake ina damu ya uongo, bali nafsi zenu zimewashawishi kutenda jambo, lakini subira ni njema. Na Mwenyezi Mungu ndiye wa kuombwa msaada kwa haya mnayoyasema.

وَجَاءَتْ سَيَّارَةٌ فَأَرْسَلُوا وَارِدَهُمْ فَأَدْلَىٰ دَلْوَهُ قَالَ يَا بُشْرَىٰ هَـٰذَا غُلَامٌ وَأَسَرُّوهُ بِضَاعَةً وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِمَا يَعْمَلُونَ ﴿١٩﴾

19. Ukaja msafara. Wakamtuma mchota maji wao. Akatumbukiza ndoo yake. Akasema: Ee habari njema! Huyu hapa mvulana! Wakamficha ili awe bidhaa. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa wanayoyafanya.

وَشَرَوْهُ بِثَمَنٍ بَخْسٍ دَرَاهِمَ مَعْدُودَةٍ وَكَانُوا فِيهِ مِنَ الزَّاهِدِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na wakamuuza kwa thamani duni kwa pesa za kuhisabiwa, na walikuwa hawana haja naye.

WAKAJA KWA BABA YAO WAKILIA

Aya 16-20

MAANA

Wakaja kwa baba yao usiku wakilia. Kwa kuvunga na kuyafinika waliyoyafanya. Wakasema: Ewe baba yetu! Hakika tulikwenda kushindana mbio na tukamwacha Yusuf kwenye vitu vyetu, basi mbwa mwitu akamla.

Kuna mithali inayosema “Damu ya Yusuf iko mbali na mbwa mwitu.” Imeelezwa kuwa msimulizi mmoja alikuwa akiwasimulia watu kisa cha Yusuf. Alipofika mahali pa mbwa mwitu, akasema mbwa mwitu aliyemla Yusuf anaitwa fulani. Wakasema waliokuwepo: Yusuf hakuliwa na mbwa mwitu! Akasema msimulizi: Basi naliwe hili ni jina la mbwa ambaye hakumla Yusuf.

Na wewe hutatuamini, ijapokuwa tunasema kweli.

Imam Ali(a.s) anasema:“Inatosha kua ni adhabu kwa muongo kuwa akisema ukweli haaminiwi

Na wakaja na kanzu yake ina damu ya uongo.

Maana yako wazi, lakini wafasiri walipokosa la kusema wakatofautiana kuhusu damu, kuwa je, ilkuwa ya paa au ya mwanakondoo. Wengine wamaesema kuwa Ya’qub alipoona kanzu ya mtoto wake ni nzima, alise- ma: Sijawahi kuona mbwa mwitu mpole kuliko huyu aliyemla mwanangu bila ya kuirarua kanzu yake.

Ama sisi tunatosheka na kuwa Ya’qub alisema:Bali nafsi zenu zimewashawishi kutenda jambo, lakini subira ni njema. Na Mwenyezi Mungu ndiye wakuombwa msaada kwa haya mnayoyasema.

Haya ndiyo yaliyoelezwa na wahyi kuhusu jawabu ya Ya’qub kuwaambia wanawe; wala hakuna dalili ya jengine.

Aya inaonyesha kuwa Ya’qub alitambua uongo wao kutokana na husuda yao kubwa kwa Yusuf. Lakini alisubiri na kumwachia mambo yake Mwenyezi Mungu.

Ukaja msafara.

Katika Tawrat Kitabu cha mwanzo imesemwa kwamba msafara wenyewe ulikuwa wa kizazi cha Ismail; yaani waarabu, kwa sababu nasabu yao inaishia kwa Ismail bin Ibrahim(a.s) .

Wakamtuma mchota maji wao. Yaani awaletee maji.Akatumbukiza ndoo yake.

Mchota maji alipomuona Yusuf alisema:Ee habari njema! Huyu hapa mvulana!

Anajipa habari yeye mwenyewe au anawapa jamaa zake. Basi wakamtoa kisimaniwakamficha ili awe bidhaa.

Walimficha na watu ili jamaa zake wasimjue, wakamfanya mtumwa aliye katika jumla ya bidhaa zao za biashara.

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa wanayoyafanya.

Yaani anajua siri yao ya kumfanya mtumwa na hali yeye ni mtu huru.

Na wakamuuza kwa thamani duni kwa pesa za kuhisabiwa.

Wafasiri wengi wamesema kuwa watu wa zama hizo wakipima pesa, kikiwa kitu thamani yake ni kubwa na wakihisabu ikiwa thamani ni ndogo. Na kwamba kusemwa pesa zenye kuhisabiwa ni ishara ya uchache wa thamani waliyouzia.

Na walikuwa hawana haja naye.

Ndio wakafanya haraka kumuuza kwa bei ya kutupa ili waondokane naye wasije wakatuhumiwa wizi.