TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 11171
Pakua: 2131


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11171 / Pakua: 2131
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI Juzuu 12

Mwandishi:
Swahili

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA MBILI

وَقَالَ الَّذِي اشْتَرَاهُ مِن مِّصْرَ لِامْرَأَتِهِ أَكْرِمِي مَثْوَاهُ عَسَىٰ أَن يَنفَعَنَا أَوْ نَتَّخِذَهُ وَلَدًا وَكَذَٰلِكَ مَكَّنَّا لِيُوسُفَ فِي الْأَرْضِ وَلِنُعَلِّمَهُ مِن تَأْوِيلِ الْأَحَادِيثِ وَاللَّـهُ غَالِبٌ عَلَىٰ أَمْرِهِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢١﴾

21. Na yule aliyemnunua kule Misri alimwambia mkewe: Mtengenezee makazi ya heshima, huenda akatufaa au tukamfaya mtoto. Na kama hivyo tulimkalisha Yusuf katika nchi ili tumfundishe kufasiri mambo. Na mwenyezi Mungu ndiye mshindi katika jambo lake, lakini watu wengi hawajui.

وَلَمَّا بَلَغَ أَشُدَّهُ آتَيْنَاهُ حُكْمًا وَعِلْمًا وَكَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿٢٢﴾

22. Na alipofikilia kukomaa kwake, tulimpa hukumu na elimu. Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

ALIYEMNUNUA

Aya 21 -22

MAANA

Na yule aliyemnunua kule Misri alimwambia mkewe: “Mtengenezee makazi ya heshima, huenda akatufaa au tukamfaya mtoto.”

Yusuf alinadiwa sokoni na akanunuliwa na Aziz (mheshimiwa). Hii ni lakabu ya waziri mkuu wa mfalme. Linalotufahamisha kuwa yeye ndiye aliyemnunua ni kauli yake Mwenyezi Mungu kwnye Aya 30 katika sura hii: “Na wanawake wa mjini wakawa wanasema: Mke wa muheshimiwa anamtaka mtumishi wake pasipo kutakiwa naye”

Waziri alitambua werevu na akili ya Yusuf, akamwambia mkewe amuweke makazi ya kiheshima. Kwa maana ya kuwa akishakuwa mkubwa, aje asimamie mambo yao au wamfanye ni mtoto wao.

Kwa sababu mheshimiwa alikuwa mgumba, hana mtoto; kama walivyosema wafasiri wengi. Na Aya inaashiria hilo pale iliposema: “Au tumfanye mtoto”

Na kama hivyo tulimkalisha Yusuf katika nchi ili tumfundishe kufasiri mambo.

Mwenyezi Mungu alimneemesha Yusuf kwa kumwokoa na vitimbi vya ndugu zake, kumtoa kisimani, kumjaalia kuwa katika nyumba ya mheshimiwa, kumweka kwenye moyo wa mwenye nyumba na kumfundisha hakika ya mambo, ikiwa ni pamoja na kutabiri ndoto.

Neema zote hizi zilimwinua Yusuf mbele za watu na kumfanya awe ni tegemeo la watu wote na mwenye kuheshimiwa. Vile vile kuwekwa kuwa ndiye mweka hazina wa nchi ya Misr na kuambiwa na mfalme: “Hakika wewe leo kwetu ni mwenye heshima mwenye kuaminika”

Na mwenyezi Mungu ndiye mshindi katika jambo lake.

Ndugu zake Yusuf walimtakia shari na Mwenyezi Mungu alimtakia kheri.

إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

“Hakika amri yake anapotaka chochote hukiambia ‘Kuwa,’ basi kinakuwa” (36:82).

Lakini watu wengi hawajui.

Kuwa amri ni ya Mwenyezi Mungu peke yake na kwamba mwenye kujifanya jeuri na kughurika na nguvu zake na uwezo wake, Mwenyezi Mungu atampatiliza kwa mashiko ya mwenye nguvu mwenye uweza.

Na alipofikilia kukomaa kwake, tulimpa hukumu na elimu.

Kukomaa hapa ni kukomaa kimwili na kiakili. Ahglab, hali hii huaanzia kwenye umri wa miaka thelathini na kuendelea hadi arobaini. Katika muda huu yanatimia maandalizi ya utume na kuanza wahyi. Makusudio ya hukumu hapa ni hekima; yaani kila kitu kukiweka mahali pake na kupatia.

Maana ni kuwa, baada ya Yusuf kukomaa, Mwenyezi Mungu alimpa elimu na kumwezesha kuitumia.

Imesemekana kuwa makusudio ya elimu hapa ni utume. Hilo haliko mbali. Kwa sababu Yusuf ni katika mitume.

Na hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

Yusuf alitenda wema kwa uvumilivu wake na twaa yake kwa Mwenyezi Mungu, naye akamlipa mema kwa sababu yeye Mwenyezi Mungu hapotezi ujira wa yeyote mwenye kutenda jambo.

وَرَاوَدَتْهُ الَّتِي هُوَ فِي بَيْتِهَا عَن نَّفْسِهِ وَغَلَّقَتِ الْأَبْوَابَ وَقَالَتْ هَيْتَ لَكَ قَالَ مَعَاذَ اللَّـهِ إِنَّهُ رَبِّي أَحْسَنَ مَثْوَايَ إِنَّهُ لَا يُفْلِحُ الظَّالِمُونَ ﴿٢٣﴾

23. Na bibi mwenye nyumba aliyokuwemo (Yusuf) alimshawishi kinyume cha nafsi yake. Na akafunga milango akasema: Njoo. Akasema: Najikinga kwa Mwenyezi Mungu. Hakika yeye ni Bwana wangu ameyatengeneza vizuri makazi yangu. Hakika waliodhulumu hawatengenekewi.

AKAMWAMBIA NJOO

Aya 23

MAANA

Na bibi mwenye nyumba aliyokuwemo (Yusuf) alimshawishi kinyume cha nafsi yake.

Neno alimshawishi linamaanisha kuwa alimfanyia vitimbi Yusuf ili atake vile anavyotaka yeye. Neno hili peke yake, linaonyesha kutojiheshimu. Lakini baadhi ya wafasiri wamechafua kurasa kuonyesha picha ya mke wa waziri kumvutia Yusuf kwa uzuri wake na ulimbwende wake. Na hayo hayana chimbuko lolote isipokuwa hadith za kiisrail. Amesema kweli mwenye Al-Manar: “Wapokezi wa kiisrail wamepokea riwaya zinazohusiana na Yusuf na mke wa waziri mambo ya ufedhuli ya uongo.

Mfano wa maneno hayo haujulikani kuwa unatoka kwa Mwenyezi Mungu, au kwa riwaya sahihi. Na hakuna yeyote anayedai hivyo”[3]

MTU NA MALI NA MAMBO YA KIJINSIYA NA AKAFUNGA MILANGO

Alijiuliza Mustafa Sadiq Arrafiy: kwanini ametumia neno waghallaqat, ambayo pia inakuwa kwenye mfumo wa kutilia mkazo jambo, na hakusema waaghlaqat? Na akajibu: “Hii inafahamisha kuwa yeye alipokata tamaa na kuona kuwa anataka kwenda zake, alikikuwa kama aliyepagawa akifikiria kufuli moja kama ni nyingi akakimbia kwenye mlango mmoja hadi mwingine, akiupigisha mkono wake, kama ambaye anajaribu kuziba milango sio kuufunga tu.”

Sisi hatuoni tofauti yoyote baina ya matamko hayo. Na hiyo inafahamisha tu uhodari wa Rafiy katika fasihi na uweza wake wa kutoa kitu kutoka kusiko na kitu.

Vyovyote iwavyo, ni kuwa Yusuf aliishi pamoja na mke wa waziri kwa muda mwingi akiwa ni barobaro mbichi, mwenye kuvutia. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa mke wa waziri kuvutiwa naye wala si ajabu kwa Yusuf kuziepuka mbinu zake pamoja na kuwa matamanio mara nyingi yanashinda akali.

Kwani binadamu sio mtumwa wa matamanio yake ya kijinsia tu; kama asemavyo Freud; na wala si mtumwa wa mali na uchumi; kama asemavyo Marks. Ispokuwa anakuwa kwenye misukumo mingi, ikiwemo mambo ya kijinsia, mali, umashuhuri, utawala, dini, desturi kupenda nchi na mambo mazuri n.k. Kwa binadamu kuna misukumo miwili inayopingana:

Kheri inayomwongoza kwenye njia ya uongofu na shari inayompeleka kwenye njia ya maangamivu. Mara nyingine mvutano huu unaendelea kwa muda mfupi na mara nyingine kwa muda mrefu mpaka upande mmoja ushinde mwingine. Au hata unaweza kuendelea hadi mwisho, huku binadamu akiwa yuko huku na huku.

Mke wa waziri alipambana na mivutano miwili: Matamanio yake ya kinya- ma yaliyomfanya amtongoze Yusuf na kwa upande mwingine hadhi nakibri kinamkataza kujidhalilisha mbele ya aliyenunuliwa kwa thamani ndogo. Akabakia yuko katikati kiasi cha muda. Kisha akashindwa akanasa kwenye mtego wa matamanio ya kijinsia ambayo yanaonyeshwa na kauli yake: “Njoo.” Kauli hii si rahisi kuisema mwanamke ila yule aliyeshindwa kabisa, kiasi cha kuwa kama wazimu.

Ama Yusuf alikuwa na msukumo mmoja tu, unaomwongoza; na wala hakuna hata chembe ya msukumo mwingine katika moyo wake. Nao ni kumcha Mwenyezi Mungu na radhi yake. Hiyo peke yake ndiyo ladha yake na starehe yake, akasema:

Najikinga kwa Mwenyezi Mungu. Hakika yeye ni Bwana wangu ameyatengeneza vizuri makazi yangu. Hakika waliodhulumu hawatengenekewi.

Yaani najilinda kumwasi Mwenyezi Mungu. Vipi nimuasi na hali yeye amenipa hisani na fadhila nyingi; pale aliponitoa kisimani na akaufanya moyo wa waziri unipende na kuniweka kwenye daraja ya mwanawe. Na vipi nijidhulumu kwa kumwasi Mwenyezi Mungu na hali Mungu hawaongozi madhalimu? Hivi ndivyo ifanyavyo imani ya kweli. Inamlinda mtu na yaliyoharamu na kumpa ushindi katika kupambana na shetani na chama chake.

Wafasiri wengi wamesema kuwa dhamiri ya yeye ni bwana wangu inamrudia waziri kwa maana ya kuwa yeye ni mlezi wangu vipi nitamfanyia hiyana? Lakini mfumo wa maneno unaerejesha dhamiri kwa Mwenyezi Mungu kutokana na kuwa karibu na neno: “Najilinda kwa Mwenyezi Mungu,” kuongezea kuwa msukumo wa kujizuia Yusuf ni kumwofia Mwenyezi Mungu, sio waziri.

Kama tutakadiria kuwa dhamir inarudia kwa waziri, basi makusudio yatakuwa ni kumtahayariza kuwa anavyotakikana ni kuwa na heshima na mumewe ambaye amemfanya awe na daraja ya juu.

وَلَقَدْ هَمَّتْ بِهِ وَهَمَّ بِهَا لَوْلَا أَن رَّأَىٰ بُرْهَانَ رَبِّهِ كَذَٰلِكَ لِنَصْرِفَ عَنْهُ السُّوءَ وَالْفَحْشَاءَ إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُخْلَصِينَ ﴿٢٤﴾

24. Na hakika (mke) alimtamani naye alimtamani kama asingeona dalili ya Mola wake. Hivyo ndivyo ilivyokuwa ili tumwepushie uovu na uchafu. Hakika yeye ni katika waja wetu waliotakaswa.

وَاسْتَبَقَا الْبَابَ وَقَدَّتْ قَمِيصَهُ مِن دُبُرٍ وَأَلْفَيَا سَيِّدَهَا لَدَى الْبَابِ قَالَتْ مَا جَزَاءُ مَنْ أَرَادَ بِأَهْلِكَ سُوءًا إِلَّا أَن يُسْجَنَ أَوْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢٥﴾

25. Na wote wawili wakakimbilia mlangoni na mwanamke akairarua kanzu yake kwa nyuma. Wakamkuta bwana wake mlangoni. Akasema: Hapana malipo ya mwenye kukusudia uovu kwa mkeo isipokuwa kufungwa gerezani au kupewa adhabu iumizayo.

قَالَ هِيَ رَاوَدَتْنِي عَن نَّفْسِي وَشَهِدَ شَاهِدٌ مِّنْ أَهْلِهَا إِن كَانَ قَمِيصُهُ قُدَّ مِن قُبُلٍ فَصَدَقَتْ وَهُوَ مِنَ الْكَاذِبِينَ ﴿٢٦﴾

26. Akasema (Yusuf): Yeye ndiye aliyenitaka bila ya mimi kumtaka. Na shahidi, aliyekuwa katika jamaa za mke, akatoa ushahidi, ikiwa kanzu yake imechanwa mbele, basi mke ni mkweli na yeye (Yusuf) ni katika waongo.

وَإِن كَانَ قَمِيصُهُ قُدَّ مِن دُبُرٍ فَكَذَبَتْ وَهُوَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿٢٧﴾

27. Na ikiwa kanzu yake imechanwa nyuma basi mke ni muongo na yeye Yusuf ni katika wakweli.

فَلَمَّا رَأَىٰ قَمِيصَهُ قُدَّ مِن دُبُرٍ قَالَ إِنَّهُ مِن كَيْدِكُنَّ إِنَّ كَيْدَكُنَّ عَظِيمٌ ﴿٢٨﴾

28. Basi mume alipoona kanzu imechanywa nyuma, alisema: Hii ni katika vitimbi vyenu (wanawake). Hakika vitimbi vyenu ni vikuu.

يُوسُفُ أَعْرِضْ عَنْ هَـٰذَا وَاسْتَغْفِرِي لِذَنبِكِ إِنَّكِ كُنتِ مِنَ الْخَاطِئِينَ ﴿٢٩﴾

29. Yusuf! Achana nayo haya. Na wewe mwanamke omba msamaha kwa dhambi zako, hakika wewe ni miongoni mwa wakosaji.

ALIMTAMANI NAYE AKAMTAMANI

Aya Ya 24-29

LUGHA

Amesema Tabrasi, katika Majmaul-bayan kuwa neno hamma (lililofasiriwa kwa maana ya kutamani) lina maana nyingi. Miongoni mwanzo ni kuazimia, kupitia na mawazo bila ya kuazimia, kutamani kitu nk.

Na hakika (mke) alimtamani naye alimtamani kama asingeona dalili ya Mola wake.

Tumezungumzia, katika Juz.1 (2:35-39) na 124. Vile vile Juz.5 (4:58-59), kuhusu isma (kuhifadhiwa na dhambi) ya mitume na kwamba mitume wote ni wenye kuhifadhiwa na dhambi. Hapo linakuja swali, kuwa Yusuf ni mwenye kuhifadhiwa na dhambi kwa sababu yeye ni mtume. Na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Naye alimtamani, inaonyesha azma mbaya ya kuitikia matamanio ya mke wa waziri. Imekuwaje?

Wafasiri wamejibu kwa majibu ya kufedhehesha, wengine wakatoka nje ya dhahiri ya maneno. Jawabu lililo karibu zaidi na dhahiri ya maneno na heshima ya mitume ni lile lisemalo kuwa katika Aya kuna kutangulizwa maneno na kuja nyuma. Asili yake ni: Na hakika (mke) alimtamani naye kama asingeona dalili ya Mola wake angelimtamani. Yaani hakumtamani kabisa; kama vile kusema: alikuwa amekwisha yule kama si fulani.

Ubainifu wa pili ni: Mambo yote yalikuwa tayari. Mwanamke amejileta mwenyewe; kijana naye amekamilika kuwa mwanamume, wako peke yao, hakuna wa kuwasikia wala wa kuwaona. Lakini kulikuwa na kizuizi kimoja tu, kilichomzuia Yusuf, chenye nguvu kuliko makemeo yoyote na kikubwa zaidi ya kila anayesikia na anayeona.

Nacho ni kujua kwake halali ya Mwenyezi Mungu na haramu yake na yakini yake kwamba Mwenyezi Mungu yuko karibu naye zaidi kuliko kuliko mshipa wa shingo; na kwam- ba yeye Mungu anajua zaidi kilicho moyoni na kilichojificha.

Hiyo ndiyo dalili iliyomzuia Yusf na kufikiria haram na inayomzuia kila mwenye kumwamini kikwelikweli Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, awe mtume au sio mtume.

Kuna wengine wamesema kuwa Yusuf haikumdhihirikia dalili ya Mola wake ila alipomtamani. La hasha! Haiwi hivyo kwa mitume na wakweli. Hakika dalili ya Mwenyezi Mungu, haiondoki kwa wauminii wakweli.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa ili tumwepushie uovu na uchafu. Hakika yeye ni katika waja wetu waliotakaswa.

Uovu ni vitimbi vya mke wa waziri na uchafu ni zina. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaomcha ambao wanamkimbilia kwake wakiwa ni wenye ikhlasi; anawalinda na kuwahifadhi na kila anayewakusudia uovu au anyejaribu kuwaingiza kwenye upotevu; sawa na alivyofanya Yusuf, alikimbilia kwa Mola wake, huku akisema:

“ Na kama hutaniondolea vitimbi vyao nitawaelekea na nitakuwa miongoni mwa wajinga Basi Mola wake akamwitikia na akamuondoshea vitimbi vyao. Kama Hakika yeye ni msikizi Mjuzi”

Na wote wawili wakakimbilia mlangoni, na mwanamke akairarua kanzu yake kwa nyuma.

Yusuf alijaribu kumponyoka kwa kutoka pale nyumbani. Mwanamke naye akamfuatia nyuma, kama ngamia mkali, akamuwahi kabla ya kufika mlangoni, akamvuta kanzu yake kwa nyuma hadi ikachanika. Mara mume naye akaingia.

Wakamkuta bwana wake mlangoni.

Mwenye Tafsir Al-Manar anasema: “Wanawake wa Misri walikuwa wakiwaita waume zao bwana (sayyid) na hilo linaendela hadi leo.

Mume alipoingia nyumbani alimkuta Yusuf mlangoni alipomuona Yusuf amesimama mlangoni, huku kanzu yake ikiwa imeraruka; kabla ya kuuliza habari yoyote Akasema:

Hapana malipo ya mwenye kukusudia uovu kwa mkeo isipokuwa kufungwa gerezani au kupewa adhabu iumizayo.

Mke aliyasema haya kwa utulivu bila ya kuonyesha fadhaiko lolote. Anasema hapana malipo ya mwenye kukusudia uovu, nayeye mwenyewe ndiye muovu anayeutuhumu wema na usafi. Hii inatukumbusha wale ambao leo wameanzisha vita huko Vietnam, Mashariki ya kati, Kongo na kwengineko.

Na wanawapa silaha mabeberu ili wawamalize wanyonge huko Angola, Afrika kusini, Rhodesia (sasa ni Zimbwabwe), Latin Amerika na kwengineko. Wanaweka vituo vya kijeshi ardhini kote, mashariki na magharibi vikiwa na kila aina ya silaha za maangamizi.

Wanayafanya yote hayo kwa madai ya kuhifadhi amani na kuchunga haki za binadamu. Kwa hiyo hakuna ajabu kwa mwanamke huyo kuficha uongo wake kwa mumewe ili afiche makosa yake.

Akasema (Yusuf): Yeye ndiye aliyenitaka bila ya mimi kumtaka.

Nimejizuia naye na nikamkimbia akanipata hapa mlangoni akaifanyia hivi nguo yangu.

Na shahidi, aliyekuwa katika jamaa za mke, akatoa ushahidi.

Wafasiri wamerefusha maneno kuhusu shahidi huyu. Wengine wamesema ni binamu yake, wengine wakasema ni katika jamaa za mume na wengine wakasema alikuwa mtoto mchanga. Ama sisi tunasimama kwenye dhahiri ya wahyi amabo unafahamisha kuwa shahidi alikuwa ni katika jamaa za mke na alikuwa ni baleghe, kutokana kauli yake:

Ikiwa kanzu yake imechanwa mbele, basi mke ni mkweli na yeye Yusuf ni katika waongo na ikiwa kanzu yake imechanwa nyuma basi mke ni muongo na yeye Yusuf ni katika wakweli.

Haya ndiyo yaliyosemwa na wahyi. Ama kuwa shahidi alikuwa nani, alitoa vipi huo ushahidi, alikuja tu yeye mwenyewe au aliitwa na mengineyo, haya yamenyamaziwa na wahyi. Kuna hadith isemayo: “Mwenyezi Mungu ameyanyamazia mambo, basi msijikalifishe nayo.”

Basi mume alipoona kanzu imechanywa nyuma, alisema: Hii ni katika vitimbi vyenu (wanawake). Hakika vitimbi vyenu ni vikuu.

Mume alikinai na akawa na yakini ya ukweli wa Yusuf(a.s) na uongo wa mkewe, lakini akaona asitri aibu. Akatosheka na kusema: Hakika vitimbi vyenu ni vikuu.

Wasifu huu unawapendeza wanawake, kwa sababu unaonyesha werevu wao na kwamba wanaume hawawezi kwa kwa hila na vitimbi.

Unaweza kuuliza : Hapa imesemwa kuwa vitimbi vya wanawake ni vikuu na katika Juz.5 (4:76), imesemwa kuwa vitimbi vya shetani ni dhaifu; je maana yake ni kuwa mwanamke ana nguvu kuliko shetani?

Jibu : Vitimbi vya wanawake ni sehemu ya vitimbi vya shetani. Mkusudio ya kuwa vitimbi vya shetani ni dhaifu ni kuwa shetani hana nguvu kwa waja wa Mwenyezi Mungu; isipokuwa yule mwenye kumfuata katika wapotevu. Na makusudio ya kuwa vitimbi vya wanawake ni vikuu ni kuwa wao ndio askari wa shetani wenye nguvu zaidi. Imepokewa kutokana na iblis kwamba yeye amesema: “Ninapochachiwa na laana za watu wema huwaendea wanawake kujiliwaza…”

Kisha waziri akasema:Yusuf! Achana nayo haya. Yaani yafiche haya wala usimwambie mtu. Na akamwambia mkewe:Na wewe mwanamke omba msamaha kwa dhambi zako, hakika wewe ni miongoni mwa wakosaji.

Hii ni dalili mkataa kwamba mume alikuwa na hakika kuwa Yusuf hakuwa na makosa, na mkewe ndiye mwenye makosa. Abu Hayan Al-andalusi (mhispania) katika tafsir yake Albahrul-muhit anasema: “Waziri hakuwa na wivu mwingi na hii ni tabia ya watu wa Misr” Naye mwenye tafsir Al- Manar akamjibu: “Haya ni maneno ya kujisemea yasiyokuwa ya kielimu sahihi.” Nasi tunaongeza kuwa hiyo imesababishwa na hawa na ubinafsi.

Neno wakosaji hapa kwa kiarabu limetumika kwa khatwiin dhamiri inay- otumika kwa wote wanaume na wanawake kwa sababu makosa yanatokea kwa wote.

HUKUMU KWA USHAHIDI WA MAZINGIRA

Makusudio ya shahidi katika neno: ‘Na akashuhudia shahidi’ sio kuwa ni sharia kuchukua ushahidi wa aina hii; isipokuwa ni ujuzi wa kujua mambo yasiyojulikana. Kuchanika kanzu kunajulikana wazi na ni kawaida mtu akishikwa kwa nyuma, kanzu yake itachanika kwa nyuma, na akishikwa kwa mbele itachanika kwa mbele. Hapo anajulikana mkweli na muongo. Kwa mnasaba huu tunaashiria kuwa kuna aina tatu za kujua uhakika wa mambo:

1. Mambo yasiyokubalika kiakila; kwa mfano, mtu mwenye umri wa miaka arubaini kudai kuwa yeye ni mzazi wa mtu aliye na umri kama wake. Au kudai kuwa amerithi jengo fulani na inajulikana kwamba baba yake alikufa fukara. Madai kama haya na mfano wake, hayahitaji nukuu ya sharia katika kuyapinga.

2. Yanayotumika na kutegemewa na sharia; kama, kukiri makosa, ushahidi wa mwenyewe, ushahidi wa waadilifu wawili. Aina hii huitwa ‘ubainifu wa kisharia’ na katika sheria za kutungwa, wanaita: ‘ushahidi wa kikanuni.’ Wameafikiana wote kuwa ni wajibu kwa kadhi kuhukumu kulingana na nukuu za kisharia. Iwe ana uhakika au la.

3. Ushahidi wa kimazingira. Kutoa hukumu kwa ijtahadi yake na werevu wake kwa kulinganisha hali na mambo yanayoyazunguka madai. Kila madai yana mambo yake na hali zake na kila kadhi ana fahamu yake na ijtihadi yake. Miongoni mwa ulinganisho ni: ikiwa kanzu ime chanika kwa mble. Vile vile yale yaliyonasibishwa kwa Nabii Suleiman bin Daud(a.s) , au Imam Ali(a.s) alipohukumu baina ya wanawake wawili waliokuwa wakigombania mtoto mmoja, kila mmoja akisema ni wake; akasema nipeni kisu nimpasue katikati, mmoja akakataa na mwengine akakubali, akampa mtoto yule aliyekataa.

La kushangaza katika niliyoyasoma kuhusiana na maudhui haya ni kauli ya Shatibi katika Kitabu almuwafiqat Juzuu ya pili uk. 267 suala la 11: “Abu bakar alitekeleza wasia wa ndoto” Yaani mtu alikufa na hakuwahi kuusia katika uhai wake, kisha akaufikisha wasia wake kwa anayemtaka kwenye usingizi na Abu bakar akaupitisha wasia huo.

وَقَالَ نِسْوَةٌ فِي الْمَدِينَةِ امْرَأَتُ الْعَزِيزِ تُرَاوِدُ فَتَاهَا عَن نَّفْسِهِ قَدْ شَغَفَهَا حُبًّا إِنَّا لَنَرَاهَا فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٣٠﴾

30. Na wanawake wa mjini wakawa wanasema: Mke wa mheshimiwa anamtaka mtumishi wake pasipo kutamaniwa naye. Hakika amegubikwa na mapenzi. Sisi hakika tunamuona yuko katika upotevu uliodhahiri.

فَلَمَّا سَمِعَتْ بِمَكْرِهِنَّ أَرْسَلَتْ إِلَيْهِنَّ وَأَعْتَدَتْ لَهُنَّ مُتَّكَأً وَآتَتْ كُلَّ وَاحِدَةٍ مِّنْهُنَّ سِكِّينًا وَقَالَتِ اخْرُجْ عَلَيْهِنَّ فَلَمَّا رَأَيْنَهُ أَكْبَرْنَهُ وَقَطَّعْنَ أَيْدِيَهُنَّ وَقُلْنَ حَاشَ لِلَّـهِ مَا هَـٰذَا بَشَرًا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا مَلَكٌ كَرِيمٌ ﴿٣١﴾

31. Aliposikia vitimbi vyao. Aliwaita na akawawekea matakia, na akampa kila mmoja wao kisu. Akasema: Tokea mbele yao. Walipomuona wakaona ni kitu kikubwa na wakakata mikono yao Na wakasema: “Hasha lillahi! Huyu si mtu, hakuwa huyu ila ni Malaika mtukufu.

قَالَتْ فَذَٰلِكُنَّ الَّذِي لُمْتُنَّنِي فِيهِ وَلَقَدْ رَاوَدتُّهُ عَن نَّفْسِهِ فَاسْتَعْصَمَ وَلَئِن لَّمْ يَفْعَلْ مَا آمُرُهُ لَيُسْجَنَنَّ وَلَيَكُونًا مِّنَ الصَّاغِرِينَ ﴿٣٢﴾

32. Akasema (yule bibi): Huyu ndiye mliyekua mkinilaumia. Hakika nilimtaka kinyume cha nafsi yake, lakini akakataa. Na akitofanya ninayomwamrisha basi hapana shaka atafungwa gerezani na atakuwa miongoni mwa madhalili.

قَالَ رَبِّ السِّجْنُ أَحَبُّ إِلَيَّ مِمَّا يَدْعُونَنِي إِلَيْهِ وَإِلَّا تَصْرِفْ عَنِّي كَيْدَهُنَّ أَصْبُ إِلَيْهِنَّ وَأَكُن مِّنَ الْجَاهِلِينَ ﴿٣٣﴾

33. Akasema: Ewe Mola wangu! Gereza linapendeza zaidi kwangu kuliko haya wanayoniitia. Na kama hutanion- dolea vitimbi vyao nitawaelekea na nitakuwa miongoni mwa wajinga.

فَاسْتَجَابَ لَهُ رَبُّهُ فَصَرَفَ عَنْهُ كَيْدَهُنَّ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٣٤﴾

34. Basi Mola wake akamwitikia na akamuondoshea vitimbi vyao; hakika yeye ni Msikizi, Mjuzi.

ثُمَّ بَدَا لَهُم مِّن بَعْدِ مَا رَأَوُا الْآيَاتِ لَيَسْجُنُنَّهُ حَتَّىٰ حِينٍ ﴿٣٥﴾

35. Kisha ikawadhihirikia baada ya kuona ishara ya kuwa wamfunge kwa muda.

MKE WA MHESHIMIWA NA WANAWAKE WA MJINI

Aya 30-35

LUGHA

Kugubikwa ni kufunikwa kabisa, yaani moyo wake ulifunikwa.

Na wanawake wa mjini wakawa wanasema: Mke wa mheshimiwa anamtaka mtumishi wake pasipo kutamaniwa naye. Hakika amegubikwa na mapenzi. Sisi hakika tunamuona yuko katika upotevu uliodhahiri.

Ilienea habari mjini, hasa kwa wanawake kwamba mke wa mheshimiwa amesalitika kimapenzi na mtumishi wake na akamtaka, lakini akakataa. Hilo ni kosa lisilosamehewa.

Aliposikia vitimbi vyao.

Yaani maneno yao. Yameeitwa vitimbi kwa vile hawakukusudia njia ya haki, bali ni kule kuenea tu. Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa pengine walimlaumu kwa kumwambia wazi wazi mwanamume, na kwamba ilitakikana watumie mbinu. Kauli hii inaweza kufaa kwa Malaya sio kwa wanaojihesimu.

Aliwaita na akawawekea matakia, na akampa kila mmoja wao kisu.

Alitaka kuwafanyia vitimbi, kama wao walivyomfanyia. Kwa hiyo akawaandalia karamu ya kukata na shoka, akawekea mito laini na chakula chenye ladha na kila mmoja akampa kisu cha kukatia nyama. Kutumia visu wakati huo kunafahamisha kuwa walikuwa wameendelea. Katika Tafsir Attabariy anasema: Kazi ya kisu katika karamu ni ya kukatia kinacholiwa tu. Kwa hiyo kikitajwa kisu ndio kimetajwa kinacholiwa.

Akasema kumwambia Yusuf:Tokea mbele yao. Walipomuona wakaona ni kitu kikubwa na wakakata mikono yao kutokana na mshangao mkubwa.

Baadhi ya wafasiri wanasema maana ya kukata hapa ni kujijeruhi. Lakini dhahiri ya neno kukata ni kukata tu, na mfano wa matukio haya hufasiriwa vingine ikiwa iko haja ya kufanya hivyo kwa sababu ya mikanganyo na sio kwa nukuu iliyo wazi.

Na wakasema: Hasha lillahi Huyu si mtu, hakuwa huyu ila ni Malaika mtukufu.

Alie katika umbo la binadamu, kutokana na haiba yake na uzuri, ambao ulimletea aina za balaa na mitihani.

Akasema yule bibi: Huyu ndiye mliyekua mkinilaumia.

Aliasema haya kwa uhuru ule wanaopigania wanawake wa sasa uhuru bila ya majukumu; hata katika kuvunja heshima na uharibifu. Sisi pia tunapigania uhuru wa wanaume na wanawake, lakini katika mipaka ya majukumu kikauli na kivitendo.

Hakika nilimtaka kinyume cha nafsi yake, lakini akakataa. Na akitofanya ninayomwamrisha basi hapana shaka atafungwa gerezani na atakuwa miongoni mwa madhalili.

Mwenye tafsir Al-Manar anasema: “Wallahi sistajabu kwa Yusuf kumkataa mwanamke aliyejileta mwenyewe; isipokuwa kustajabu kwangu ni mtazamo wake Yusuf kwa Mwenyezi Mungu haukuacha nafasi yoyote katika moyo wake wa kibinadamu wa kumwangalia mwanamke huyu aliyeshikwa na nyonda.” Nasi tunaongeza kwenye kauli hii kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amepiga mfano kwa Yusuf wa mumin mwenye ikhlasi ili ajulikane mumin aliye kombo kombo ambaye huipeleka dini vile atakavyo yeye.

Akasema: Ewe Mola wangu! Gereza linapendeza zaidi kwangu kuliko haya wanayoniitia.

Makusudio ya kupendeza hapa sio kuwa ni zuri, isipokuwa ni hiyari tu yaani afadhali. Amesema wanayoniitia, kwa tamko la wengi. Kwa sababu wanawake waliomuona pia walimtamani, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu katka Aya 50 ya sura hii: “Rejea kwa bwana wako na umuulize habari ya wale wanawake waliokata mikono yao. Hakika Mola wangu anajua vizurivitimbi vyao”. Yusuf alihiyari gereza pamoja na uchungu wake na kuacha ladha ili apate mwisho mtamu.

Unaweza kuuliza : Ikiwa mtu atahiyarishwa baina ya zina na kufungwa gerezani na hawezi kuepuka moja ya mawili hayo, je inaruhusiwa kuzini?

Jibu : Hairuhusiwi. Kwa sababu hiyari hapo iko baina ya zina ambayo hiyo yenyewe ni haramu na kufungwa ambako ni haramu kwa dhalimu sio kwa mwenye kufungwa. Ila ikiwa kufungwa kutasababisha dhambi kubwa zaidi ya zina. Kwa hiyo mtu akihiyarishwa baina ya kuzini na kuua, basi atachagua kuzini. Lakini hiyo ni kwa asiyekuwa maasumu. Yeye an hukumu nyingine.

Na kama hutaniondolea vitimbi vyao nitawaelekea na nitakuwa miongoni mwa wajinga.

Vilipozidi vitisho na vivutio, Yusuf alihofia kudhoofika msimamo wake, kwa hiyo akamwelekea Mwenyezi Mungu akiomba kujinasua, huku akisema: Ewe Mola wangu! Yamenishukia nisiyoyaweza isipokuwa kwa msaada wako; na wewe ni muweza wa kuyaondoa. Na kama hutayaondoa nguvu zangu zitadhoofika na uwezo wangu utakuwa mchache.

Basi Mola wake akamwitikia na akamuondoshea vitimbi vyao; kama alivyomwondoshea vya ndugu zake hapo mwanzo. Mja yeyote hamfanyii ikhlasi Mwenyezi Mungu ila humjaalia matokeo na faraja.

وَكَانَ حَقًّا عَلَيْنَا نَصْرُ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٤٧﴾

“Na ililkuwa ni haki juu yetu kuwanusuru wauminii.” (30:47).

Hakika yeye ni Msikizi, Mjuzi.

Anasikia dua ya mwenye kumnyenyekea na anajua ikhlasi ya mwenye kumfanyia ikhlas.

Kisha ikawadhihirikia baada ya kuona ishara ya kuwa wamfunge kwa muda.

Dhamir ya ikawadhihirikia inamrudia mheshimiwa na mkewe na wengineo waliokuwa na maoni kama yao. Imesemekana kuwa inamrudia yeye peke yake na tamko la wengi likafaa kwa vile halikutajwa jina lake.

Makusudio ya ishara ni dalili zinazonyesha usafi wa Yusuf na kutokuwa na hatia. Hatia yake ni usafi wake na kujichunga. Kama angelikuwa mhalifu kama wao wasingempa cheo kikubwa.

Yusuf alikataa matakwa yao kwa hiyo wakamwadhibu kama mwenye hatia. Hivi ndivyo ilivyo katika historia yoyote.

Mtu mzuri anapata tabu katika mazingira ya dhulma, lakini Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaomcha na wakavumilia misukosuko katika njia yake si katika njia yao. Na muovu anampa muda kisha mambo humgeukia.

Na Mwenyezi Mungu humpa nguvu kwa nusra yake mwenye kuamini na akawa na subira; sawa na yaliyomtokea Yusuf pamoja na ndugu zake na mke wa mheshimiwa, pale mwisho ndugu zake walipomwambia:

“Wallahi Mwenyezi Mungu amekufadhilisha wewe kuliko sisi na hakika sisi tulikuwa wenye makosa” Aya: 90. Na mke wa mheshimiwa aliposema: “Sasa haki imedhihiri. Mimi ndiye niliyemtaka kinyume cha nafsi yake na hakika yeye ni katika wakweli” Aya: 51