TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU Juzuu 13

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 12982
Pakua: 2190


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 17 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 12982 / Pakua: 2190
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU Juzuu 13

Mwandishi:
Swahili

12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

وَقَالَ الشَّيْطَانُ لَمَّا قُضِيَ الْأَمْرُ إِنَّ اللَّـهَ وَعَدَكُمْ وَعْدَ الْحَقِّ وَوَعَدتُّكُمْ فَأَخْلَفْتُكُمْ وَمَا كَانَ لِيَ عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا أَن دَعَوْتُكُمْ فَاسْتَجَبْتُمْ لِي فَلَا تَلُومُونِي وَلُومُوا أَنفُسَكُم مَّا أَنَا بِمُصْرِخِكُمْ وَمَا أَنتُم بِمُصْرِخِيَّ إِنِّي كَفَرْتُ بِمَا أَشْرَكْتُمُونِ مِن قَبْلُ إِنَّ الظَّالِمِينَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢٢﴾

22. Na shetani atasema itakapokatwa hukumu: “Hakika Mwenyezi Mungu aliwaahidi ahadi ya kweli nami nikawaahidi sikuwatimizia. Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa niliwaita mkaniitikia. Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe, Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu wala nyinyi hamuwezi kuwa watetezi wangu, Mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha, Hakika madhalimu wana adhabu chungu.

وَأُدْخِلَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا بِإِذْنِ رَبِّهِمْ تَحِيَّتُهُمْ فِيهَا سَلَامٌ ﴿٢٣﴾

23. Na wale ambao wameamini na wakatenda mema wataingizwa katika Mabustani (Pepo) ambayo hupita mito chini yake.

MIADI YA MWENYEZI MUNGU

Aya 22-23

HOTUBA YA SHETANI

Tumezungumzia kwa ufafanuzi kuhusu fikra ya Iblisi na Shetani, mwan- zoni mwa Juzuu ya kwanza na katika Juz.5 (4:38) na katika Aya nyingine zinazozungumzia shetani tumezungumzia kwa ujumla.

Hapa tunarudia kwa upana zaidi; kwa sababu Aya tuliyo nayo ndiyo iliyowazi zaidi kuonyesha dalili za kuweko shetani na kwamba ni hakika yenye kuthibiti; ingawaje haikueleza vile alivyo. Tutaeleza njia zinazoambatana na Aya hii, kama ifuatavyo:

1- Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemtaja shetani, katika Kitabu chake Kitakatifu, kwa ibara mbali mbali. Mara nyingine anasema, Mtukufu, kuwa shetani ni katika aina ya watu na majini; kama pale aliposema:

شَيَاطِينَ الْإِنسِ وَالْجِنِّ يُوحِي بَعْضُهُمْ إِلَىٰ بَعْضٍ زُخْرُفَ الْقَوْلِ غُرُورًا ﴿١١٢﴾

“Mashetani watu na majini Baadhi yao wanawapa wenzao maneno ya kupambapamba kuwahadaa.” Juz.8 (6:112).

Aya hii inaashira kwamba kila kauli ambayo dhahiri yake ni rehema na undani wake ni adhabu, basi hiyo ni kazi ya shetani, hata ikiwa imesemwa na nani.

Mara nyingine anasema Mwenyezi Mungu kuwa shetani ana askari na ana kabila; kama ilivyo katika Aya hizi:

وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ ﴿٩٥﴾

“Na majeshi ya ibilisi yote” (26:95)

يَا بَنِي آدَمَ لَا يَفْتِنَنَّكُمُ الشَّيْطَانُ كَمَا أَخْرَجَ أَبَوَيْكُم مِّنَ الْجَنَّةِ يَنزِعُ عَنْهُمَا لِبَاسَهُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوْآتِهِمَا إِنَّهُ يَرَاكُمْ هُوَ وَقَبِيلُهُ مِنْ حَيْثُ لَا تَرَوْنَهُمْ ﴿٢٧﴾

“Enyi wanaadamu! shetani asiwatie katika fitina, kama alivyowatoa wazazi wenu katika Bustani (Pepo) akiwavua nguo zao ili kuwaonyesha tupu zao. Hakika yeye na kabila lake anawaona, na nyinyi hamuwaoni, Juz.8 (7:27).

Aya hizi zinafahamisha kuwa mashetani hawana idadi kwa wingi na kwamba wao hawaonekani kwa macho wala kuguswa kwa mkono.

Mara ya tatu Mwenyezi Mungu anasema mashetani wana marafiki na wasimamizi; kama ilivyo katika Aya hizi:

وَمَن يَكُنِ الشَّيْطَانُ لَهُ قَرِينًا فَسَاءَ قَرِينًا ﴿٣٨﴾

“Na ambaye shetani amekuwa ndiye rafiki yake, basi ana rafiki mbaya, Juz,5 (4:38).

فَقَاتِلُوا أَوْلِيَاءَ الشَّيْطَانِ ﴿٧٦﴾

“Basi piganeni na marafiki wa shetani” Juz.5 (4:76)

Tamko hili peke yake linafahamisha kuwa kupigana jihadi na wapotufu ni lazima na wajib, wajapokuwa ni waislamu. Mara ya nne, Mwenyezi Mungu, ambaye imetukuka hekima yake na maneno yake, anasema:

هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ ﴿٢٢١﴾ تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ ﴿٢٢٢﴾

“Je, niwaambie nani wanawashukia Mashetani? Wanamshukia kila mzushi mkubwa mwingi wa dhambi (26: 221-222).

Inafahamisha Aya hii kuwa Mashetani ni wale waongo wazushi.

Ama wadhifa wa shetani na askari wake, kama ulivyoelezwa, ni kupoteza na kudanganya ili kuzuia njia ya haki na kheri, kwa nguvu na kulazimisha; isipokuwa ni kwa wasiwasi, kupambapamba na kudanganya.

Kwa ajili hii, tunasema na tunaendelea kusema kwamba jambo lolote linalompambia mtu kufanya uovu na kumuhimiza shari na ufisadi kwa njia ya hadaa na shauku, basi hilo ni shetani aliyefukuzwa na ibilisi mlaanifu ni sawa iwe ni mtu, mali, jaha, kitabu, gazeti, wasiwasi, mazungumzo ya ndani ya nafsi au kitu chochote kingine kinachoonekana au kisichoonekana.

Hii ndio picha ya shetani iliyoakisi katika akili zetu, tukiwa tunafuatilia na kuzifikiria Aya za Mwenyezi Mungu katika Kitabu chake, tukiziamini pamoja na mitume wa Mwenyezi Mungu.

Mengineyo yasiyokuwa hayo, katika aina na ufafanuzi, tunaiachia elimu ya Mwenyezi Mungu; wala sisi hatukalifiwi nayo au kuulizwa nayo. La wajibu kwetu ni kutohadaika, kutojiingiza katika matamanio na kuacha kuwasikiliza wadanganyifu na wapotevu. Kikitutokea kitu katika hayo, basi tumkumbuke Mwenyezi Mungu kwa ahadi na miadi yake: “Na kama uchochezi wa shetani ukikuchochea, basi jikinge kwa Mwenyezi Mungu; hakika yeye ndiye asikiaye na ajuaye, Hakika wale wanye takua zinapowagusa pepesi za shetani huzinduka, Juz.9 (7:200-201), Rudia huko.

2- Katika nafsi ya binadamu kuna matamanio na silika, navyo ni vitenda- kazi vinavyopelekea kumuasi Mwenyezi Mungu na kuhalifu amri zake, kwa sababu vinakuja kutoka ndani sio nje na kutoka batini sio dhahiri. Kwa hiyo ikiwa ndani mwa mtu hamna nguvu kubwa na ngumu itakayomzuia kupondokea kwa ashetani na kudhibiti ukaidi wake, basi mtu bila shaka atakuwa amepigwa mwereka na matamanio.

3-Na shetani atasema itakapokatwa hukumu.

Kila kitu, isipokuwa Mwenyezi Mungu, kina mwanzo na mwisho. Inawezekana mwanzo wenyewe ukaonekana, kwa dhahiri, ni heri na mwisho ukaonekana, kiuhakika, ni shari na kinyume chake. Kwa ajili hii haifai kukihukumu kitu kwa dhahiri yake na mwanzo wake, maadamu mwisho wake uko kwenye elimu ya ghaibu.

Watu walimfurahia Qarun alipowatokea na kipambo chake na wakasema: Hakika yeye ni mwema na mtu adhimu. Ardhi ilipommeza yeye na nyumba yake, walisema ni mtu mbaya na muovu.

Dunia ni mwanzo na Akhera ni mwisho. Huko zitafunuka pazia na vifuniko; atajulikana kila mtu mwishilio wake, ambapo hakutakuwa na kombokombo wala kufungwafungwa. Hiyo ndiyo maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘Itakapokatwa hukumu’

4-Hakika Mwenyezi Mungu aliwaahidi ahadi ya kweli nami nikaawahidi sikuwatimizia.

Ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ufufuo, hisabu na malipo:

فَوَرَبِّكَ لَنَسْأَلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٩٢﴾ عَمَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٩٣﴾

Kwa haki ya Mola wako! Tutawauliza wote yale waliyokuwa wakiyatenda (15:92-93).

Ama ahadi ya shetani ni kupinga ahadi ya Mwenyezi Mungu kuwa haku- na hisabu wala ufuo wala Pepo na moto. “Hakuna kingine ila maisha yetu ya dunia, wala sisi hatutafufuliwa, Jz.7 (7:29).

Haya ndiyo anayoyasema shetani kuwaambia marafiki zake hapa duniani, palipo na kupindisha pindisha mambo na kudanganya, lakini huko Akhera hakuna kitu isipokuwa haki na uadilifu; hata shetani mwenyewe ataji- tokeza wazi na uongo wake, akiri mwenyewe kwa kauli yake kuwa mwanzo alikuwa akiwafundisha watu uongo na uzushi.

5-Na sikuwa na mamlaka juu yenu, isipokuwa niliwaita mkaniitikia.

Kabisa! Shetani anakubali mwenyewe kuwa hana uwezo wala nguvu yoy- ote isipokuwa vitimbi na hadaa. Wala hawamwitikii isipokuwa wale wad- haifu wa akili, nafsi na imani. Kauli yake hiyo shetani ni ile aliyoambiwa na Mwenyezi Mungu:

إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْغَاوِينَ ﴿٤٢﴾

Hakika waja wangu wewe hutakuwa na mamlaka nao, isipokuwa wale wapotofu waliokufuata (15:42).

6-Basi msinilaumu mimi, bali jilaumuni wenyewe.

Ikiwa ni ole wake yule aliyekufurishwa na Namrudi, itakuwaje kwa yule aliyekufurishwa na Iblisi? Ikiwa watu wanajilinda na shetani itakuwaje yule anyemtaka huyo shetani amlinde.

Huu ndio mwisho wa yule anayeidharau haki na watu wema kusaidia ufisadi na wafisadi na mwenye kufuata mlio. Tumewaona wengi katika mashetani watu wakiwahadaa walio wadhaifu, wanawaghuri kwa kueneza vurugu. Hata yakiwapata yale waliyoyafanya wenyewe, mashetani wao huwaambia yale yale atakayowaambia Ibilisi wafuasi wake siku ya hisabu na malipo.

7-Mimi siwezi kuwa mtetezi wenu wala nyinyi hamuwezi kuwa watetezi wangu

Yaani shetani kesho atawaambia wafuasi wake: mimi siwatoshelezi na kitu chochte, wala nyinyi pia hamnitoshelezi. Mimi na nyinyi hatuna mawasiliano yoyote.

Mimi nilikataa tangu zamani kunishirikisha.

Ibilisi anawaambia wale wale waliotikia mwito wake: mlinitii katika yale niliyowalingalia, mkanifanya ni mshirika wa Mwenyezi Mungu katika wajibu wa twaa, na mimi ninajiepusha na shirki na yale mliyoyashirikisha; hata kama mtanifanya ni mshirika wa Mwenyezi Mungu.

Hakika madhalimu wana adhabu chungu.

Hii ni jumla nyingine inayoanza, si katika maneno ya Ibilisi, ikiwa na maana ya kutoa miadi. Inawezekana kuwa ni mwishilio wa hotuba ya Ibilisi.

Ajabu ni yaliyoelezwa na baadhi ya wafasiri kwamba Ibilisi atatoa hotuba yake hii kwa watu wa motoni kwenye mimbari atakyowekewa huko! Kama ni hivyo basi, itabidi awekewe spika kubwa, kwa sababu wasikilizaji, ambao ni jeshi lake, ni wengi kuliko idadi ya mchanga.

Na wale ambao wameamini na wakatenda mema wataingizwa katika Mabustani (Pepo) ambayo hupita mito chini yake.

Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja wapotevu na adhabu yao, sasa anataja waongofu wenye msimamo na malipo yao; kama iilvyo kawaida ya Qur’an. Umepita mfano wake katika Juz. 11 (10:9).

أَلَمْ تَرَ كَيْفَ ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا كَلِمَةً طَيِّبَةً كَشَجَرَةٍ طَيِّبَةٍ أَصْلُهَا ثَابِتٌ وَفَرْعُهَا فِي السَّمَاءِ ﴿٢٤﴾

24. Je, hukuona jinsi Mwenyezi Mungu alivyopiga mfano wa neno zuri; kama mti mzuri, mizizi yake ni imara na matawi yake yako mbinguni.

تُؤْتِي أُكُلَهَا كُلَّ حِينٍ بِإِذْنِ رَبِّهَا وَيَضْرِبُ اللَّـهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ﴿٢٥﴾

25. Hutoa matunda yake kila wakati kwa idhini ya Mola wake. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano ili wapate kukumbuka.

وَمَثَلُ كَلِمَةٍ خَبِيثَةٍ كَشَجَرَةٍ خَبِيثَةٍ اجْتُثَّتْ مِن فَوْقِ الْأَرْضِ مَا لَهَا مِن قَرَارٍ ﴿٢٦﴾

26. Na mfano wa neno ovu ni kama mti muovu uliong’olewa juu ya ardhi, hauna uimara.

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ وَيُضِلُّ اللَّـهُ الظَّالِمِينَ وَيَفْعَلُ اللَّـهُ مَا يَشَاءُ ﴿٢٧﴾

27. Mwenyezi Mungu huwaimarisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika Akhera, na anawapoteza madhalimu; na Mwenyezi Mungu hufanya apendavyo.

NENO JEMA NA NENO OVU

AYA 24-27

MAANA

Je, hukuona jinsi Mwenyezi Mungu alivyopiga mfano wa neno zuri, kama mti mzuri.

Imesemekana kuwa maana ya neno zuri hapa ni tamko la Tawhidi: La ilaa-ha illa llah ‘Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hapana mwenye shaka kuwa Tawhid ndio msingi wa haki na chimbuko lake.

Ni kutokana na Tawhid na ikhlasi ya Mwenyezi Mungu peke yake ndio tunaweza kulifasiri neno zuri kwa kila neno linalowanufaisha watu na kuwapatia kheri na utengeneo kwa namna moja au nyingine; ni sawa liwe ni neno la dini au sharia, elimu au falsafa na hata fasihi na fani. Mtu yeyote ambaye watu watanufaika na kauli yake au kitendo chake atakuwa, kwa upande huu, anakutana na misingi ya Uislamu na dini, kwa namana yoyote atakavyokuwa.

Kauli na neno bora zaidi ni neno la mapinduzi na kelele za hasira mbele ya mtawala jeuri na wale wanaomsaidia, miongoni mwa vibaraka na wanoji- weka nyuma. Kwa sababu wao ndio asili ya ugonjwa na chimbuko la balaa.

Amesema Imam Ali(a.s) :“Haikuwa kazi yoyote nzuri na jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu katika kuamrisha mema na kukataza mabaya ila ni kama upumuo katika lindi la bahari na kwamba kuamrisha mema na kukataza maovu hakukurubiwi na ajali wala hakupungukiwi na riziki na bora yake kabisa ni tamko la usawa mbele ya kiongozi jeuri.”

Kwa sababu kiongozi huyo ndio chimbuko la kila uovu; Kwa hiyo mwenye kumkabili na akampinga atakuwa ameupiga vita uovu wote.

Kuna Hadith kadha za Mtume Mtukufu(s.a.w.w) zenye maana ya kauli hii ya Imam Ali, Kila kitokacho kwa Ali Amirul-muminin ni miali ya jua la Muhammad bwana wa viumbe wote.

Hakuna kitu kinachofahamisha kuwa makusudio ya neno zuri ni neno lenye faida na manufaa kuliko kufananishwa kwake na mti mzuri ambaomizizi yake ni imara haungolewi na kimbungana matawi yake yako mbinguni uko mbali na mabalaa ya dunia na uchafu wake.

Hutoa matunda yake kila wakati kwa idhini ya Mola wake sio kuwa mara nyingine unakuwa mkarimu na mara nyingine unakuwa bakhili; kama mfanya biashara wa nipe nikupe, Huu unatoa tu wakati wote.

Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano ili wapate kukumbuka.

Hufananisha maana ya ndani kwa maana ya dhahiri ili watu wafahamu njia ya uongofu wapate kuifuata na njia ya uongofu wapate kuiepuka.

Na mfano wa neno ovu ni kama mti muovu.

Kila neno linalodhuru watu wala lisiwanufaishe; hilo ni lenye kulaaniwa; ni sawa liwe linatokana na Mwislamu au asiyekuwa Mwislamu; awe wa hali ya juu au mlalahoi. Bali kunyamazia batili kunahisabika ni katika madhambi makubwa. Kuna hadithi inayosema: “Mwenye kunyamazia haki ni shetani bubu.”

Ghandi alimwandikia Taghore “Hakika wewe ni mshairi adhimu lakini unacheza na nyumba inaungua nyimbo nzuri nzuri hazimshibishi mwenye njaa wala kumponyesha mgonjwa”

Ulion’golewa juu ya ardhi, hauna uimara.

Huu ni mfano sahii kabisa wa batili na watu wake wanojifanya wakubwa na wajinga wakidhaniwa kuwa wao ni watu wazito kumbe ni kama mti tu uliosimama bila ya mizizi, mara moja unaweza ukalala chini unapopigwa na upepo.

Mwenyezi Mungu huwaimarisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia na katika Akhera.

Makusudio ya wale walioamini sio waliosema tumemwamini Mungu na siku ya mwisho tu, kisha wasiisimamishe haki na kuipinga batili; isipokuwa makusudio ya wale walioamini ni wale aliowakusudia Mwenyezi Mungu katika kauli yake: “Hakika waumini ni wale tu walio mwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho; kisha wasiwe na sahaka na wakapigania njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zao na nafsi zao” (49:15)

Lakini wakidai tu kumwamini Mwenyezi Mungu kisha wasiizuie dhulma na ufisadi kwa ushujaa, basi hao ni wenye shaka sio waumini.

Maana ya kuwaimarisha kwa kauli thabiti katika maisha ya dunia ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa habari katika Kitabu chake kupitia Mtume wake kuwa wao wako katika ulinzi wa Mwenyezi Mungu na kwamba Yeye ndiye mlezi wao na msimamizi wao, mwenye kuwahifadhi na kuwanusuru; kama alivyo washujaisha na kuwasifu kwa ukweli na ikhlasi na mengineyo katika fadhila. Ama kuwaimarisha katika maisha ya akhera kwa kauli thabiti ni kauli YakeMwenyezi Mungu:

يَا عِبَادِ لَا خَوْفٌ عَلَيْكُمُ الْيَوْمَ وَلَا أَنتُمْ تَحْزَنُونَ ﴿٦٨﴾

Enyi waja wangu! Hamna hofu leo wala nyinyi si wenye kuhuzunika” (43:68).

Na anawapoteza madhalimu kwa kufuru yao na utwaghuti wao.

Mara nyingi Qur’an hutumia neno dhulma kwa maana ya kufuru na shirki, lakini makusudio ya dhulma hapa ni kuidhulumu mtu nafsi yake kwa kufuru na kumdhulumu mwingine kwa uadui na uzushi; kama ambavyo makusudio ya upotevu hapa ni adhabu; sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu:

كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّـهُ مَنْ هُوَ مُسْرِفٌ مُّرْتَابٌ ﴿٣٤﴾

Hivyo ndivyo humpoteza Mwenyezi Mungu yule aliyepita kiasi mwenye shaka (40:34).

Na Mwenyezi Mungu hufanya apendavyo katika kumpa thawabu mtiifu na kumwadhibu mfisadi, wala hakuna mwenye kuzuia matakwa yake.

Nikiwa kwenye tafsiri ya Aya hii, nimesoma makala katika gazeti la Al-Ahram la Misr la tarehe 2, February 1969, yenye kichwa cha maneno: “Je ubinadamu utashuhudia kummalizika vita vya Atomic na kuanza vita vya sumu?” Miongoni mwa yaliyomo katika makala hiyo ni: “Imejitokeza silaha mpya hatari zaidi na yenye nguvu kulio silaha za nyuklia.

Silaha hiyo ni ya sumu na kwamba athari yake ni mtu anapoigusa chembe tu, basi viungo vyake vinanywea, macho yanamtoka na kufa papo hapo. Na kwamba Amerika na Uingereza tayari ina viwanda vya kutengeneza silaha hizi na kuzihifadhi mpaka pale zitakapohitajika. Wakati mataifa yakitafuta muafaka wa kummaliza silaha za nyuklia, huku mataifa mawili haya yanatafuta silaha hatari zaidi, kama badili ya mabomu ya Atomic na Haidrojeni.”

Je, imani inaweza kuwa pamoja na nia na maazimio ya kutumia silaha hizi? Je swala za wale wanaowaunga mkono wenye nia hizo na maazimio hayo zitawafaa mbele ya Mwenyezi Mungu?

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ بَدَّلُوا نِعْمَتَ اللَّـهِ كُفْرًا وَأَحَلُّوا قَوْمَهُمْ دَارَ الْبَوَارِ ﴿٢٨﴾

28. Je, hukuwaona wale waliobadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru? Na wakawafikisha watu wao kwenye nyumba ya maangamivu?

جَهَنَّمَ يَصْلَوْنَهَا وَبِئْسَ الْقَرَارُ ﴿٢٩﴾

29. Nayo ni Jahannam watakayoiingia, Ni mahala pabaya pa kukaa.

وَجَعَلُوا لِلَّـهِ أَندَادًا لِّيُضِلُّوا عَن سَبِيلِهِ قُلْ تَمَتَّعُوا فَإِنَّ مَصِيرَكُمْ إِلَى النَّارِ ﴿٣٠﴾

30. Na walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika ili wapoteze katika njia yake, Sema: Stareheni! Kwani hakika marejeo yenu ni motoni.

قُل لِّعِبَادِيَ الَّذِينَ آمَنُوا يُقِيمُوا الصَّلَاةَ وَيُنفِقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ يَوْمٌ لَّا بَيْعٌ فِيهِ وَلَا خِلَالٌ ﴿٣١﴾

31. Waambie waja wangu walioamini wasimamishe Swala na watoe katika tulivyowaruzuku kwa siri na kwa dhahiri, kabla ya kuwajia siku isiyokuwa na biashara wala urafiki.

WALIBADILISHA NEEMA YA MUNGU KWA KUFURU

Aya 28 -31

MAANA

Je, hukuwaona wale waliboadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru? Na wakawafikisha watu wao kwenye nyumba ya maangamivu? Nayo ni Jahnnam watakayoiingia ni mahala pabaya pa kukaa.

Dhamiri ya wakawafikisha inawarudia viongozi wa kufuru na upotevu. Makusudio ya neema ya Mwenyezi Mungu ni imani na uwongofu. Maana ni kuwa, je, hustajabu ewe Muhammad au ewe msikilizaji na msomaji, hali ya viongozi wa kufuru na upotevu ambao wamehiyari upotevu kuliko uon- gofu na moto kuliko neema, wakiingia humo wao na wafuasi wao, wakawa ndio kuni zake.

Mfano wa Aya hii ni kama kauli yake Mwenyezi Mungu:

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ اشْتَرَوُا الضَّلَالَةَ بِالْهُدَىٰ فَمَا رَبِحَت تِّجَارَتُهُمْ وَمَا كَانُوا مُهْتَدِينَ ﴿١٦﴾

“Hao ndio walionunua upotofu kwa uongofu, lakini biashara yao haikupa- ta faida wala hawakuwa ni wenye kuongoka.” Juz.1 (2:16)

Tabariy amenukuu, katika kufasiri Aya hii, kwamba Umar bin Al-Khatab alisema: “Wale ambao wamebadilisha neema ya Mwenyezi Mungu kwa kufuru ni koo mbili ovu katika maqurayshi: Bani Mughira na Bani Umayya. Ama Bani Mughira mliwatosha siku ya Badr na Bani Umayya watajifurahisha muda mchache tu.”

Na walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika ili wapoteze katika njia yake.

Walimfanyia Mwenyezi Mungu washirika, wakiwapenda kama kumpenda Mungu na kuwaabudu kama kumwabudu Mungu.

Ilivyo hasa ni kuwa wao walifanya hivyo kwa kukusudia kuongoka si kwa kukusudia kupoteza njia. Kwa hiyo neno kwa ‘ili’ hapa halina maana ya kuwa ndio lengo bali ni matokeo. Maana yanakuwa kwamba washirikina waliabudu masanamu kwa kukusudia kuongoka nayo na kujikurubisha kwa Mwenyezi Mungu, lakini natija ikawa ni kupotea, kuangamia na kuwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu. Neno ‘ili’ hapa liko sawa na mfano wa kusema: Amekuja mwenyewe ili afe.

Sema: Stareheni! Kwani hakika marejeo yenu ni motoni.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha mtume wake kuwahadharisha washirikina na mwisho mbaya na kuwaambia kuwa starehe za dunia ni chache hata kama zinawapendeza na Akhera ni ya mwenye takua. Lakini lugha ya haki inafaa kitu kwa wale ambao hawatingishwi na lolote zaidi ya faida na chumo?

Waambie waja wangu walioamini wasimamishe Swala ambayo mwenye kuiswali inamkumbusha Mungu na kumhadharisha na adhabu na mateso na kumkataza dhambi na makosa

Na watoe katika tulivyowaruzuku kwa siri na kwa dhahiri.

Zaka ni ndugu yake swala. Swala inamkumbusha Mungu na zaka inamkurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Umepita mafano wake katika Juz 3 (2:74).

Kabla ya kuwajia siku isiyokuwa na biashara wala urafiki.

Biashara hapa ni fumbo la fidia. Maana ni kuwa mwenye kutoa mali yake katika njia ya Mwenyezi Mungu atanufaika nayo huko akhera na mwenye kuifanyia ubakhili atakuwa na hasara na adhabu wala haitamfaa siku hiyo ambapo hakutakuwa na fidia wala urafiki, Umepita mfano wake katika Juzuu hii tuliyo nayo (13:18).

13

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

اللَّـهُ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَأَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجَ بِهِ مِنَ الثَّمَرَاتِ رِزْقًا لَّكُمْ وَسَخَّرَ لَكُمُ الْفُلْكَ لِتَجْرِيَ فِي الْبَحْرِ بِأَمْرِهِ وَسَخَّرَ لَكُمُ الْأَنْهَارَ ﴿٣٢﴾

32. Mwenyezi Mungu ndiye ambaye ameziumba mbingu na ardhi na akateremsha maji kutoka mbinguni. Na kwayo akatoa matunda kuwa riziki kwa ajili yenu. Na akafanya yawatumikie majahazi yanayopita baharini kwa amri yake, na akaifanya mito iwatumikie.

وَسَخَّرَ لَكُمُ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ دَائِبَيْنِ وَسَخَّرَ لَكُمُ اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ ﴿٣٣﴾

33. Na akalifanya liwatumikie Jua na Mwezi daima. Na akaufanya usiku na mchana uwatumikie.

وَآتَاكُم مِّن كُلِّ مَا سَأَلْتُمُوهُ وَإِن تَعُدُّوا نِعْمَتَ اللَّـهِ لَا تُحْصُوهَا إِنَّ الْإِنسَانَ لَظَلُومٌ كَفَّارٌ ﴿٣٤﴾

34. Na akawapa kila mlichomuomba, Na mkihisabu neema za Mwenyezi Mungu hamuwezi kuzidhibiti. Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru.

NA AKATEREMSHA MAJI KUTOKA MBINGUNI

Aya 32 -34

MAANA

Aya zote hizi tatu umepita mfano wake kama ifuatavyo:

Kuumbwa mbingu na ardhi: Juz. 7 (6:73).

Kutermshwa maji kutoka mbinguni: Juz. 1 (2:22) na Juz. hii tuliyo nayo (13:18).

Kupita majahazi: Juz. 2 (2:164).

Kunufaika na Jua na Mwezi: Juz. hii (13:2). Usiku na mchana Juz. 11(10: 67).

Mwenyezi Mungu ameweka idadi ya neema nyingi kwa waja wake katika Juz. hii na Juz. 8 (6:143144) na nyinginezo nyingi zilizokwisha tangulia pamoja na tafsiri yake na ufafanuzi wake. Mwenyezi Mungu amerudia hapa au kuzidokeza kwa mnasaba wa kubadilisha neema kwa kufuru.

Kwa ufupi Aya hizi tatu zinamaanisha kuwa neema za Mwenyezi Mungu hazihisabiki; kama vile kuumbwa mbingu na ardhi, kuteremshwa maji kuenda majahazi faida za jua, mwezi, usiku na mchana. Vile vile kuwafadhili watu kwa waliyoomba na wasiyoomba, lakini pamoja na neema zote hizo wengi wanamkufuru na kuzikufuru neema zake huku wakiabudu yasiyowanufaisha wala kuwadhuru.

JE MTU ANA MAUMBILE YA HATIA?

Kwa mnasaba wa kauli yake Mwenyezi Mungu:Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru, tunadokeza kwamba wataalamu wa saikolojia wametofautiana kuhusu binadamu, kuwa je, ana maumbile ya kufanya hatia, kwamba yeye amezaliwa kumfanyia uadui ambaye hajamfanyia uadui na kukufuru neema za aliyemfanyia wema (hana shukrani)

Mnamo mwaka 1832 watalamu 528 walikutana huko Amerika wakilijadili suala hili, Wengi wakaonelea kuwa hakuna dalili kuwa mwanadamu anaweza kuepuka kufanya makosa, lakini kundi jingine likapinga.

Sisi tunaamini kuwa binadamu hakuzaliwa kuwa ni mwenye kufanya makosa; vinginevyo angelikuwa hana taklifa yoyote na kuhisabiwa kwake na kuadhibiwa ingelikuwa ni dhulma na uonevu. Vile vile dini na sharia ingelkiuwa ni upuzi na mchezo; kama vile unyoya kwenye mavumo ya upepo. Isipokuwa anakuwa ni mwenye hatia kwa sababu nyingine za nje; kama vile njaa inayofanya awe mwizi, hadaa zinazomfanya awe na hiyana na kuwa kibaraka n.k.

Hapa ndio unapata tofauti baina ya watu katika nafsi zao, Wengine wanakuwa dhaifu mbele ya hadaa na kushindwa na matamnio; kama vile mwenye chakula lakini bado anataka ziada tena kwa hali yoyote; au mwenye mke anayemtosheleza, lakini anazini; au anayeificha haki kwa kupupia cheo au manufaa yoyote katika starehe za dunia. Hakuna mwenye shaka kwamba huyu amefanya dhambi kwa kutaka kwake sio kwa maumbile yake. Hayo ndiyo aliyoyakusudia Mwenyezi Mungu aliposema:

Hakika mtu ni dhalimu mkubwa mwingi wa kukufuru.

Ni wazi kuwa kupondokea haramu hakuifanyi kuwa ni halali, madamu iko nafasi ya kuweza kufanya subira na kushinda mapondokeo haya. Tumetangulia kueleza yanayoambatana na utafiti huu katika kufasiri Juz. 12 (11:9).

وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ رَبِّ اجْعَلْ هَـٰذَا الْبَلَدَ آمِنًا وَاجْنُبْنِي وَبَنِيَّ أَن نَّعْبُدَ الْأَصْنَامَ ﴿٣٥﴾

35. Na Ibrahim aliposema: Ewe Mola wangu! Ujaalie mji huu uwe wa amani na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu.

رَبِّ إِنَّهُنَّ أَضْلَلْنَ كَثِيرًا مِّنَ النَّاسِ فَمَن تَبِعَنِي فَإِنَّهُ مِنِّي وَمَنْ عَصَانِي فَإِنَّكَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿٣٦﴾

36. Ewe Mola wangu! Hakika hayo yamewapoteza watu wengi, Basi atakayenifuata, hakika huyo ni katika mimi na atakayeniasi basi hakika wewe ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

رَّبَّنَا إِنِّي أَسْكَنتُ مِن ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيْرِ ذِي زَرْعٍ عِندَ بَيْتِكَ الْمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُوا الصَّلَاةَ فَاجْعَلْ أَفْئِدَةً مِّنَ النَّاسِ تَهْوِي إِلَيْهِمْ وَارْزُقْهُم مِّنَ الثَّمَرَاتِ لَعَلَّهُمْ يَشْكُرُونَ ﴿٣٧﴾

37. Ewe Mola wetu! Hakika mimi nimeweka baadhi ya dhuria zangu katika bonde lisilokuwa na mmea, kwenye nyumba yako takatifu, ewe Mola wetu, ili wasimamishe Swala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao na uwaruzuku matunda ili wapate kukushukuru.

رَبَّنَا إِنَّكَ تَعْلَمُ مَا نُخْفِي وَمَا نُعْلِنُ وَمَا يَخْفَىٰ عَلَى اللَّـهِ مِن شَيْءٍ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ ﴿٣٨﴾

38. Ewe Mola wetu! Hakika wewe unajua tunayoyaficha na tunayoyafichua, na hapana kitu kinachofichikana mbele ya Mwenyezi Mungu katika ardhi wala mbingu.

الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي وَهَبَ لِي عَلَى الْكِبَرِ إِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ إِنَّ رَبِّي لَسَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٩﴾

39. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliyenipa juu ya uzee wangu Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu ni mwenye kusikia sana dua.

رَبِّ اجْعَلْنِي مُقِيمَ الصَّلَاةِ وَمِن ذُرِّيَّتِي رَبَّنَا وَتَقَبَّلْ دُعَاءِ ﴿٤٠﴾

40. Ewe Mola wangu! Nijaalie niwe mwenye kuisimamisha Swala na katika dhuria zangu pia. Ewe Mola wetu! Na utakabalie dua yangu.

رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَابُ ﴿٤١﴾

41. Ewe Mola wetu! Nighufirie mimi na wazazi wangu wawili na waumini siku ya kusimama hisabu.

EWE MOLA WANGU UJAALIE MJI HUU UWE WA AMANI

AYA 35-41

Na Ibrahim aliposema: Ewe Mola wangu! Ujaalie mji huu uwe wa amani.

Ibrahim na Ismail ndio waliojenga Al-ka’ba Makka. Angalia Juz. 1 (2:127).

Ibrahim na Ismail walimwomba Mola wao awajalie watu wawe na amani, na akawaitikia dua yao. Walikuwa na wanaendelea kuwa maadui wanakutana bila ya kuhofiana. Katika hili Mwenyezi Mungu ameashiria kwa kusema:

أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا جَعَلْنَا حَرَمًا آمِنًا وَيُتَخَطَّفُ النَّاسُ مِنْ حَوْلِهِمْ ﴿٦٧﴾

“Je hawaoni kuwa tumeifanya nchi takatifu iwe ya amani na hali watu wengine wananyakuliwa kwa majirani zao? ” (29:67)

Na uniepushe mimi na wanangu na kuabudu masanamu.

Ni muhali kabisa kwa Ibrahim kuabudu masnamu. Itakuwaje ayaabudu naye aliyavunja kwa mikono yake na akawaambia:

أُفٍّ لَّكُمْ وَلِمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿٦٧﴾ قَالُوا حَرِّقُوهُ وَانصُرُوا آلِهَتَكُمْ إِن كُنتُمْ فَاعِلِينَ ﴿٦٨﴾

Je, mnaabudu badala ya Mwenyezi Mungu yasiyofaa chochote wala kuwadhuru, Kefle yenu! Na mnavyoviabudu badala ya Mwenyezi Mungu, Je, hamtii akili? (21:67-68).

lakini mitume wa Mwenyezi Mungu na manabii wake – pamoja na isma yao – wanaogopa maasi, Hofu hii ndiyo daraja ya juu ya utiifu. Anayejiona ni mtakatifu basi amemfungulia shetani madirisha.

MITUME NA KUITIKIWA DUA

Unaweza kuuliza : kuwa Ibrahim alimuomba Mola wake kuwa watoto wake wawe waumini, asimshirikishe Mwenyezi Mungu hata mmoja wao; na inajulikana kuwa wengi katika kizazi chake walimshirikisha Mwenyezi Mungu, wakaabudu masanamu, wakiwemo maquraish ambao wao ni katika kizazi chake?

Razi amenukuu majibu matano kutoka kwa wafasiri, lakini bado swali liko palepale linataka jawabu.

Tuonavyo sisi ni kuwa dua ni maombi na matarajio; ni sawa iwe inatoka kwa Nabii au mwinginewe. Inaweza kuwa hekima yake Mwenyezi Mungu inataka kuyakubali maombi na wakati mwingine kuyakataa. Wala hiyo haimaanishi kuwa aliyekataliwa maombi hana uzito wowote mbele ya Mungu kuweza kudhuru cheo cha utume na isma yake.

Hapana! Kwani kukataliwa maombi hakummaanishi hasira za mwenye kuombwa kwa muombaji; bali inawezekana kuwa ni mapenzi zaidi kwake na kuchunga masilahi yake. Nuhu(a.s) alimtaka Mwenyezi Mungu kumuokoa mtoto wake kutokana na kuangamia, Mola wake akamjibu kwa kusema: “Basi usiniombe usilo na ujuzi nalo” Juz.12 (11:46).

Kwa maneno mengine ni kuwa dua ya Nabii Ibrahim haina tafsiri nyingine zaidi ya hamu yake na mapenzi. Hakuna mwenye shaka kwamba manabii wana hamu na wanapendelea watu wote waamini na waongoke kwenye haki. Pamoja na hayo Mwenyezi Mungu alimwambia Bwana wa mitume aliyeadhimu:

إِنَّكَ لَا تَهْدِي مَنْ أَحْبَبْتَ وَلَـٰكِنَّ اللَّـهَ يَهْدِي مَن يَشَاءُ ﴿٥٦﴾

Hakika wewe huwezi kumwongoza umpendae, lakini Mwenyezi Mungu humuongoza amtakaye (28:56)

Lau yangehakikia kila wanayoyataka mitume basi asingelipatikana hata kafiri mmoja duniani na mitume wasingelisumbuka; hasa yule bwana wao na wa mwisho wao ambaye alisema: “Hakuudhiwa mtume kama nilivyoudhiwa mimi”

Ewe Mola wangu! Hakika hayo yamewapoteza watu wengi.

Makusudio ya hayo ni ya masanamu. Maana ni kuwa wengi katika watu wamepotea kwa sababu ya ibada ya masanamu; sawa na kusema: mali imempoteza fulani; yaani amepotea kwa sababu yake.

Basi atakayenifuata, katika kizazi changu,hakika huyo ni katika mimi kinasabu na kidini.Na atakayeniasi basi hakika wewe ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Atakayemuasi Ibrahim(a.s) basi yuko mbali naye sana hata kama ndiye aliyekaribu zaidi kiudugu kuliko watu wengine; Kwa sababu atakayemuasi atakuwa amemuasi Mwenyezi Mungu.

Lakini, pamoja na hayo, Ibrahim ni mpole mno mwenye kurudi kwa Mwenyezi Mungu; kama alivyomsifu yule aliyemchagua kuwa kipenzi na akamtakasa. Ndio maana hakuwatakia adhabu waasi katika kizazi chake, bali alimwachia Mwenyezi Mungu mambo yao kwa masamaha wake na maghufira yake.

Ilivyo ni kuwa akili haizuwii kusamehewa washirikina, kwa sababu adhabu ya washirikina ni haki ya Mwenyezi Mungu. Akitaka atwaadhibu na akitaka atawasamehe. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu hasamei kufanyiwa mshirika, lakini husamehe yasiyokuwa hayo” Juz.5 (4:48), ni dalili ya kiusikilizaji si dalili ya kiakili, Angalia tafsiri yetu huko, tumefafanua zaidi.

Ewe Mola wetu! Hakika mimi nimeweka baadhi ya dhuria zangu katika bonde lisilokuwa na mmea, kwenye nyumba yako takatifu, ewe Mola wetu, ili wasimamishe Swala.

Aliyasema haya Ibrahim(a.s) pale alipomwacha Ismail na mama yake Makka, pakiwa ni bonde kavu, halina chochote, si maji wala mmea; isipokuwa nyumba tu inayosimamishwa swala ndani yake na kukaririwa talbiya. Ni kwa lengo hili Ibrahim aliiweka baadhi ya famila yake mahali hapa pa kame. Lakini binadamu haishi kwa swala peke yake, bali hana budi apate mkate vile vile, ndipo Ibrahim akasema:

Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao na uwaruzuku matunda ili wapate kukushukuru.

Ikiwa kwenye nyumba ya Mwenyezi Mungu hakuna mmea wala kiwele, basi watu waelekee huko kwa ibada au biashara wakiwa na mkate na matunda, ili familia ya Ibrahim nayo ipate kula na kuweza kuswali na kushukuru.

Musa(a.s) alisema: “Mola wangu! Hakika mimi ni muhitaji wa heri utakyoiteremsha” (28:24). Imam Ali(a.s) anasema:“Wallahi hakumuomba isipokuwa mkate atakokula” Alisema mshairi aliye faqih: Fadhila ni za mkate lau si huo kamwe hata siku hakuna aabaduo.

Ewe Mola wetu! Hakika wewe unajua tunayoyaficha na tunayoyafichua, na hapana kitu kinachofichikana mbele ya Mwenyezi Mungu katika ardhi wala mbingu.

Baada ya Ibrahim kuuomba watu wafike nyumbani kwake wakiwachukulia familia yake mkate na matunda ili wapate nguvu na uchangamfu wa kuabudu, baada ya haya alisema maombi yangu haya si lolote ila ni unyenyekevu na kukiri kuwa wewe ni Muumba Mwenye kuruzuku. Ama haja yetu na masilahi yetu wewe unayajua zaidi kuliko sisi; tuwe tumekuomba au hatukuomba.

Kwa hiyo kauli ya Ibrahim ‘tunayofichua’ maana yake ni tunayoyaomba na maana ya ‘tunayoyaficha’ ni yale tusiyoyaomba.

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu aliyenipa juu ya uzee wangu Ismail na Is-haq. Hakika Mola wangu ni mwenye kusikia sana dua.

Shukrani hii kutoka kwa Ibrahim imechanganya maombi ya msaada wa Mwenyezi Mungu kwa wanawe, Ismaili na Is-haq. Kwa vile Ibrahim amekwishakuwa mzee na muda wake umekurubia, ndipo akawakilisha mambo ya familia yake kwa Mwenyezi Mungu; wala hakuwabainishia kitu au kuwalimbikizia mali watoto wake ili wastarehe na kuwanyima wengine.

Ewe Mola wangu! Nijaalie niwe mwenye kuisimamisha Swala na kati- ka dhuria zangu pia. Ewe Mola wetu! Na utakabalie dua yangu.

Swala ya Ibrahim sio aina ya hii swala tunayoiswali sisi; bali ni katika aina ya swala amabyo Mwenyezi Mungu ameiainisha kwa kusema:

إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ﴿٤٥﴾

Hakika Swala huzuia mambo machafu na maovu (29:45).

Ndio hapa mafakihi wakaigawanya swala katika mafungu mawili: Swala ya kutekeleza wajibu tu, lakini mtekelezaji halipwi kitu; na Swala ya kutekeleza wajibu na mtekelezaji analipwa. Hiyo ni ile ambayo inaleta ikhlasi katika matendo na ukweli katika kuamiliana na watu.

Ewe Mola wetu! Nighufirie mimi na wazazi wangu wawili na waumini siku ya kusimama hisabu.

Tumetangulia kueleza katika Juz, 7 (6:74) tofauti baina ya Sunni na Shia kuhusu imani ya baba wa Ibrahim Al-khalil(a.s) . Miongoni mwa tuliyoyasema ni kuwa mzozo huu na mfano wake ni tasa, na kwamba linalotakikana kwa Mwislamu ni kuitakidi isma ya mitume, Ama kuamini kuwa mababa zao walikuwa waumini si itikadi ya uislamu kabisa.

Lau mtu atasema mimi ninamwamini Mungu na umoja wake, mitume na isma yao na siku ya mwisho na hisabu, lakini sithibitishi wala si kanushi imani ya mababa wa Mitume, Atakayesema hivi, tutamwambia kuwa wewe ni Mwislamu, unastahiki wanyostahiki waislamu nawe unawajibu wa kuwafanyia wanayostahiki waislamu wenzako.