TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE Juzuu 14

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 9062
Pakua: 2218


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 9062 / Pakua: 2218
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE Juzuu 14

Mwandishi:
Swahili

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE

ضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا عَبْدًا مَّمْلُوكًا لَّا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَمَن رَّزَقْنَاهُ مِنَّا رِزْقًا حَسَنًا فَهُوَ يُنفِقُ مِنْهُ سِرًّا وَجَهْرًا هَلْ يَسْتَوُونَ الْحَمْدُ لِلَّـهِ بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٧٥﴾

75. Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mtumwa mwenye kumilikiwa asiyeweza kitu, na mwengine tuliyemruzuku riziki njema inayotoka kwetu, naye anatoa katika riziki hiyo kwa siri na kwa dhahiri, Je, wanalingana sawa? Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu; bali wengi wao hawajui.

وَضَرَبَ اللَّـهُ مَثَلًا رَّجُلَيْنِ أَحَدُهُمَا أَبْكَمُ لَا يَقْدِرُ عَلَىٰ شَيْءٍ وَهُوَ كَلٌّ عَلَىٰ مَوْلَاهُ أَيْنَمَا يُوَجِّههُّ لَا يَأْتِ بِخَيْرٍ هَلْ يَسْتَوِي هُوَ وَمَن يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَهُوَ عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٧٦﴾

76. Na Mwenyezi Mungu anapiga mfano wa watu wawili. Mmoja wao ni bubu hawezi chochote, naye ni mzigo kwa bwana wake, Popote anapomuelekeza haleti kheri. Je, huyo anaweza kuwa sawa na yule anayeamrisha uadilifu, naye yuko juu ya njia iliyonyooka?

وَلِلَّـهِ غَيْبُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا أَمْرُ السَّاعَةِ إِلَّا كَلَمْحِ الْبَصَرِ أَوْ هُوَ أَقْرَبُ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٧٧﴾

77. Mwenyezi Mungu ana siri zote za mbingu na ardhi. Wala halikuwa jambo la saa (ya kiyama) ila kama kupepesa kwa jicho au karibu zaidi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.

MWENYE UWEZA NA MWENYE KUSHINDWA

Aya 75 – 77

MAANA

Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa mtumwa mwenye kumilikiwa asiyeweza kitu, na mwengine tuliyemruzuku riziki njema inayotoka kwetu, naye anatoa katika riziki hiyo kwa siri na kwa dhahiri, Je, wanalingana sawa?

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja, katika Aya iliyotangulia, kwamba washirikina wamemfanyia Mungu mfano, hapa anataja mifano miwili ya kuwafahamisha washirikina kwamba Mwenyezi Mungu hana wa kufanana naye.

Kwa ufupi mfano wa kwanza unaoelezwa na Aya hii, ni kuwa mfano wenu enyi washirikina katika kumfanya Mungu kuwa ni sawa na masanamu unafanana na anayemfanya mtumwa asiyemiliki chochote na kushindwa kufanya chochote kuwa ni sawa na aliye huru ambaye ni tajiri tena mkarimu anatoa kwa siri na kwa dhahiri bila ya kumwogopa yeyote.

Ikiwa akili na maumbile zinaakataa usawa huu, basi imekuwaje nyinyi kumfanya sawa Mwenyezi Mungu Mwenye uweza wa kila kitu na masana- mu yasiyioweza chochote?

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu.

Hii ni jumla iliyoingia kati, ikiwa na maana kuwa hakuna yeyote anayestahiki sifa, shukrani na kuabudiwa isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Bali wengi wao hawajui kuwa sifa njema zinaamstahiki Mungu tu sio mwengine.

Na Mwenyezi Mungu anapiga mfano wa watu wawili. Mmoja wao ni bubu hawezi chochote, naye ni mzigo kwa bwana wake, Popote anapomuelekeza haleti kheri. Je, huyo anaweza kuwa sawa na yule anayeamrisha uadilifu, naye yuko juu ya njia iliyonyooka?

Huu ni mfano wa pili. Kwa ufupi ni kuwa bubu anayeshindwa na kila kitu hawezi kuwa sawa na anayetamka. Kwa hiyo vipi nyinyi washirikina mnafanya ni sawa katika ibada baina ya mwenye kuwa na sifa zote za ukamailifu na ambaye si chochote?

Mwenyezi Mungu ana siri zote za mbingu na rdhi.

Kila siri mbele ya Mwenyezi Mungu inajulikana na kila ghaibu kwake inaonekana. Punde tu imetangulia Aya ya 73 ya sura hii isemayo: ‘Hakika Mwenyezi Mungu anajua na nyinyi hamjui.’

Wala halikuwa jambo la saa (ya kiyama) ila ni kama kupepesa kwa jicho au karibu zaidi.

Hii ni ibara nyingine ya: “Hakika amri yake anapotaka kitu ni kukiambia kuwa na kikawa”. Ndani yake mna makemeo na kumuhofisha yule anayehalifu na akawa na inadi.

Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.

Wala hakuna yeyote anayeweza kumzuia akitaka kuwaangamiza washirikina na viumbe wote

وَاللَّـهُ أَخْرَجَكُم مِّن بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ لَا تَعْلَمُونَ شَيْئًا وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ لَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿٧٨﴾

Na Mwenyezi Mungu amewatoa matumboni mwa mama zenu hamjui kitu, na amewajaalia usikizi na uoni na nyoyo ili mpate kushukuru.

أَلَمْ يَرَوْا إِلَى الطَّيْرِ مُسَخَّرَاتٍ فِي جَوِّ السَّمَاءِ مَا يُمْسِكُهُنَّ إِلَّا اللَّـهُ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٧٩﴾

79. Je, hawaoni ndege waliowezeshwa katika anga ya mbingu? Hawazuii isipokuwa Mwenyezi Mungu, Hakika katika haya kuna ishara kwa watu wanaoamini.

وَاللَّـهُ جَعَلَ لَكُم مِّن بُيُوتِكُمْ سَكَنًا وَجَعَلَ لَكُم مِّن جُلُودِ الْأَنْعَامِ بُيُوتًا تَسْتَخِفُّونَهَا يَوْمَ ظَعْنِكُمْ وَيَوْمَ إِقَامَتِكُمْ وَمِنْ أَصْوَافِهَا وَأَوْبَارِهَا وَأَشْعَارِهَا أَثَاثًا وَمَتَاعًا إِلَىٰ حِينٍ ﴿٨٠﴾

80. Na Mwenyezi Mungu amewafanyia majumba yenu yawe ni maskani. Na akawafanyia kutokana na ngozi za wanyama wenu nyumba mnazoziona nyepesi siku ya kusafiri kwenu na siku ya kutulia kwenu. Na katika sufu zao na manyoya yao na nywele zao mnatengeneza vyombo na vifaa vya kutumia kwa muda.

وَاللَّـهُ جَعَلَ لَكُم مِّمَّا خَلَقَ ظِلَالًا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ الْجِبَالِ أَكْنَانًا وَجَعَلَ لَكُمْ سَرَابِيلَ تَقِيكُمُ الْحَرَّ وَسَرَابِيلَ تَقِيكُم بَأْسَكُمْ كَذَٰلِكَ يُتِمُّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكُمْ لَعَلَّكُمْ تُسْلِمُونَ ﴿٨١﴾

81. Mwenyezi Mungu amewafanyia vivuli katika alivyoviumba na amewafanyia makazi katika milima na amewafanyia nguo za kuwakinga na joto na nguo za kuwakinga na vita vyenu. Ndio hivyo anatimiza neema zake kwenu ili mpate kusilimu.

فَإِن تَوَلَّوْا فَإِنَّمَا عَلَيْكَ الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿٨٢﴾

82. Na kama wakikengeuka, basi juu yako ni kufikisha tu ujumbe ulio wazi.

يَعْرِفُونَ نِعْمَتَ اللَّـهِ ثُمَّ يُنكِرُونَهَا وَأَكْثَرُهُمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٣﴾

Wanazijua neema za Mwenyezi Mungu kisha wanazikanusha, Na wengi wao ni makafiri.

MWENYEZI MUNGU AMEWATOA MATUMBONI MWA MAMA ZENU HAMJUI KITU

Aya 78 – 83

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja katika Aya hizi baadhi ya dalili za kuweko Muumbaji mwenye kupangilia mambo vizuri, Wakati huo huo dalili hizo ni katika neema za Mwenyezi Mungu kwa waja wake. Dalili hizo ni hizi zifuatazo:

PAMOJA NA WENYE MAADA

Na Mwenyezi Mungu amewatoa matumboni mwa mama zenu hamjui kitu na amewajaalia usikizi na uoni na nyoyo ili mpate kushukuru.

Mtu anatoka tumboni mwa mama yake hajui chochote, lakini Mwenyezi Mungu ana zana za maarifa za hisia ambazo ni usikizi na uoni na zana za maarifa ya kiakili ambazo ni akili na maumbile.

Wanaoamini maada wanasema kuwa maada pofu na kiziwi imejianzishia hiyo yenyewe usikizi, uoni na akili. Sisi tunawajibu hivi: Kwanza, asiye nacho hawezi kutoa kitu. Pili, ikiwa maisha na utambuzi unahusika na maada tu basi itabidi usikizi, uoni na moyo uwe ni maada; Kwa sababu kuenea sababu kunapeleka kuenea msababishaji.

Wakisema kuwa kwenye maada kuna aina maalum inayohusika nayo; Kwa namna ambayo inakuwa ni lazima mwili usikie uone na utambue, nasi tutawaambia: ama mseme kwamba maada hiyo yenyewe ndiyo iliyoleta uhai na utambuzi au mseme hapana. Mkisema ndio, itakuwa ni lazima maada iwe na uhai na utambuzi. Mkisema hapana, itakuwa ni lazima maada yote isiwe na uhai kabisa.

Yote mawili hayawezekani; Kwa sababu imeshuhudiwa waziwazi kwamba baadhi ya maada zimeganda na nyingine ziko hai na utambuzi. Na mgawanyiko huu unajulisha kuwa nyuma ya maada kuna nguvu yenye ujuzi na hekima; ndiyo ambayo imeleta uhai, na utambuzi kwenye baadhi ya maada na kuleta kutofautiana kwenye hizo maada.

ULIMWENGU NI MKUBWA KULIKO MAROKETI

Je, hawaoni ndege waliowezeshwa katika anga ya mbingu? Hawazuii isipokuwa Mwenyezi Mungu, Hakika katika haya kuna ishara kwa watu wanaoamini.

Makusudio ya kuwezeshwa hapa ni kuwezeshwa kuruka angani; na kuzuwiya ni kuzuiwa wasianguke; mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu:

أَوَلَمْ يَرَوْا إِلَى الطَّيْرِ فَوْقَهُمْ صَافَّاتٍ وَيَقْبِضْنَ مَا يُمْسِكُهُنَّ إِلَّا الرَّحْمَـٰنُ ﴿١٩﴾

“Kwani hawaoni ndege walioko juu yao wanavyozikunjua mbawa na kuzikunja, hawazuii isipokuwa Mwingi wa rehema” (67:19).

Ni wazi kuwa Mwenyezi Mungu anapitisha mambo kwenye sababu zake, Inaeleweka kwamba Mwenyezi Mungu akilitaka jambo huliandalia sababu.

Kwa hiyo maana ya kauli yake Mungu: ‘Hawazuii isipokuwa Mwingi wa rehema’ ni kwamba Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu amewaumbia ndege mbawa mbili na akaziwekea vitu vinavyowezesha kuruka angani baina ya mbingu na ardhi:

فَقَدَّرَهُ تَقْدِيرًا ﴿٢﴾

“Na ameumba kila kitu akakikadiria kwa kipimo (chake)”, (25:2).

إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ ﴿٤٩﴾

“Hakika sisi kila kitu tumekiumba kwa kipimo,” (54:49).

Kwa hiyo kuumba, kukadiria na mpangilio ni dalili wazi kuwa kuna Muumbaji mwenye kupangilia vizuri.

Kuna wanouliza, kuwa : binadamu amevumbua ndege inayokwenda kwa kasi zaidi ya sauti, akatengeneza roketi inayokata maelfu ya maili kwa muda wa saa, ikaweza kufika hadi mwezini. Tena binadamu huyo akatengeneza satelaiti inazozunguuka ardhini na mwezini na kuzungumza na wataalamu kwa lugha zao kutoka huko iliko. Sasa ndege wanoruka angani ni kitu gani mbele ya uvumbuzi huu?

Jibu : Ajabu ya mtu na akili zake kuuliza swali kama hili. Anashangazwa na ugunduzi huu akisahau yule aliyeifanya akili iliyoweza kugundua vitu hivyo? Lau mtu atafanya insafu akajiangalia yeye mwenyewe na akili yake, ataiona ni kubwa zaidi kuliko kuvumbua maroketi, madege n.k.

Bali lau atafanya insafu akaangalia ulimwengu, atauona ni mkubwa kuliko kuumbwa binadamu aliyevumbua maroketi na masatalaiti. Mwenyezi Mungu anasema:

لَخَلْقُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ أَكْبَرُ مِنْ خَلْقِ النَّاسِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٥٧﴾

“Hakika kuumba mbingu na ardhi ni kukubwa zaidi kuliko kuwaumba watu, lakini watu wengi hawajui” (40:57)

na kuumba mtu ni kukubwa mara nyingi zaidi kuliko kutengeneza maroketi.

Zaidi ya hayo mazungumzo tangu mwanzo yalikuwa juu ya mnyama ndege aliye hai. Ama ndege za kutengeneza, roketi na satalaiti ni katika vitu visivyo na uhai. Kwa hiyo kuvilinganisha na vyenye uhai si mahali pake. Ni wazi kuwa wataalamu wa maroketi wakichanganyika na wataalamu wa kijini hawawezi kuumba nzi hata ubawa wake:

لَن يَخْلُقُوا ذُبَابًا وَلَوِ اجْتَمَعُوا لَهُ وَإِن يَسْلُبْهُمُ الذُّبَابُ شَيْئًا لَّا يَسْتَنقِذُوهُ مِنْهُ ﴿٧٣﴾

“Hawataumba hata nzi ijapokuwa watajumuika kwa hilo, Na nzi akiwapokonya kitu hawawezi kukipata kwake” (22:73).

Kwa hakika Mwenyezi Mungu ametegemeza kuzuiya ndege angani kwake moja kwa moja kwa vile yeye ndiye sababu ya kwanza na akamapa viungo vya kurukia.

Ashaira wamekana kuweko sababu za kimaumbile kwa aina zote na wakasema, kila vitendo vinategemezwa kwa Mwenyezi Mungu moja kwa moja bila ya kuingia kati kitu chochote kwa namna yoyote ile; ni sawa vitendo hivyo vijitokeze kwenye ndege au wadudu, wanyama au binadamu, au hata kwenye maumbile mengine.

Kwa hiyo, kwa upande wao, hakuna uhusiano wowote baina ya kuungua na moto, au kuondoka kiu na kunywa maji, wala baina ya kushiba na kula. Mwenyezi Mungu ndiye anayeunguza wakati wa kugusa moto, ndiye anayeondoa kiu wakati wa kunywa maji na pia ndiye anayeshibisha wakati wa kula, sio kuwa moto wenyewe ndio uliounguza, au maji kuondoa kiu au kuwa chakula ndio kilichoondoa njaa.

Kujibu hoja hiyo inatosha tu kusema kuwa hilo linapingana na hisia na dhamira. Na kwamba linapelekea kuwa mtu ni sawa na mnyama na vitu visiyo na harakati; hawezi kusifika kwa wema wala ubaya na kuwa ni mwenye hatia au asiye na hatia.

Kwa hiyo hatastahiki sifa wala lawama au thawabu wala adhabu; Kwa sababu Mungu ndiye mtendaji na mtu ni chombo tu; sawa na chombo cha kuwekea maji

Na Mwenyezi Mungu amewafanyia majumba yenu yawe ni maskani.

Makusudio ya maskani hapa ni utulivu kutokana na neno la kiarabu sakan; yaani kutulia majumbani, majumba haya ni yale yanayojengwa kwa miti, mawe simiti n.k.

Na akawafanyia kutokana na ngozi za wanyama wenu nyumba mnazoziona nyepesi siku ya kusafiri kwenu na siku ya kutulia kwenu.

Baada ya Mwenyezi Mungu kutaja majumba yaliyojengwa, sasa anataja majumba ya kutembea nayo; kama vile mahema. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametaja ngozi na wala hakuaja katani n.k., kwa sababu ngozi ndiyo iliyokuwa ikitumika zaidi katika nchi za uarabuni. Vyovyote itakavyokuwa nyumba, itakuwa inafahamisha kupatikana aliyeiumba na kuitengeneza.

Imenipendeza ibara ya mwanafasihi mmoja na fasaihi yake, ninamnukuu: “kila kilicho juu yako kikakufunika basi ni paa, kila kilicho chini yako basi ni sakafu na kila kinachokusitiri katika pembe nne basi ni kuta, Vyote hivyo ukivipangilia na ukavishikanisha basi hiyo ni nyumba.”

HESHIMA YA NYUMBA KATIKA SHARIA

Aina zote za nyumba ni katika neema za Mwenyezi Mungu. Haijui thamani yake ila yule asiyekuwa nayo. Nyumba ina heshima zake katika sharia ya kiislamu; miongoni mwazo ni kutoingia mtu bila ya hodi na kukaribishwa. Mwenyezi Mungu anasema:

فَلَا تَدْخُلُوهَا حَتَّىٰ يُؤْذَنَ لَكُمْ وَإِن قِيلَ لَكُمُ ارْجِعُوا فَارْجِعُوا ﴿٢٨﴾

“Basi msiyaingie mpaka mpewe idhini na mkiambiwa rudini basi rudini” (24:28).

Wanafiqh wanasema kuwa mwenye kuchungulia nyumba ya mtu kutoka tunduni au kwenye mwanya wa mlango n.k., mwenye nyumba anayo haki ya kumkemea, akiendela anayo haki ya kumpiga au kumrushia jiwe n.k., akipata madhara mchunguliaji basi ni shauri yake, mwenye nyumba hana lawama yoyote.

Kuna Hadith ya Mtume(s.a.w.w) isemayo:“Mwenye kukuchungulia ukimtupia jiwe na jicho lake likapofuka basi huna lawama.” Imam Jafar As- swadiq(a.s) amesema:“Tupu ya muumini ni haramu kwa muumini Mwenye kumchungulia muumini katika nyumba yake, basi macho yake ni halali yake katika hali hiyo.”

Na katika sufu zao na manyoya yao na nywele zao mnatengeneza vyombo na vifaa vya kutumia kwa muda.

Makusudio ya vyombo hapa ni mahitaji ya mtu, kama vile matandiko, mavazi n.k. Vifaa ni kila kinachomnufaisha mtu katika mahitaji yake. Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘kwa muda’ ni ishara ya kuwa vitu vyote vya maisha ya hapa duniani ni vya muda sio vya kudumu.

VIPI NEEMA YA DHAHABU NYEUSI

Mwenyezi Mungu amewafanyia vivuli katika alivyoviumba.

Kivuli ni kile anachojikinga mtu na joto la Jua.

Na amewafanyia makazi katika milima.

Chochote anachokihitajia mtu ni katika neema akikipata; hata wingu litakalomkinga na jua, bali hata pango katika milima.

Na amewafanyia nguo za kuwakinga na joto.

Vilevle za kuwakinga na baridi. Hazikutajwa kwa sababu ya kujulikana kwa kutajwa moja.

Na nguo za kuwakinga na vita vyenu . Hizi ni deraya n.k.

Ndio hivyo anatimiza neema zake kwenu ili mpate kusilimu.

Makusudio ya kusilimu hapa ni kutii na kuinyenyekea haki kwa kuifuata na kuitumia.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amewapa watu neema ya majumba, vifaa, mavazi ya kawaida, mavazi ya vita, vivuli na mapango, ili waweze kumshukuru na kumcha Yeye na wasilete ufisadi katika nchi.

Ikiwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa waarabu wa wakati wa giza, vivuli, miti, mawingu na mapango ya milima na akazingatia kuwa hizo zote ni katika kutimiza neema zake, na akawataka washukuru kwa hayo na wainyenyekee haki tena akawahadharisha wale watakaoasi.

Ikiwa ni hivyo, itakuwaje kwa neema hii ya dhahabu nyeusi inayotiririka katika miji ya Waarabu? Itakuwaje majumba yanayopasua mawingu wanayoyajenga kwayo? Vipi vifaa wanavyomiliki, zikiwemo ndege gari n.k.?

Mwenyezi Mungu aliwaneemesha waliopita kwa wanyama; kama ngamia, nyumbu baghala na punda. Vilevile kwa majumba ya mawe, ngozi, vifaa vya sufu na manyoya ya wanyama na nguo za kuwakinga na joto na baridi; bali hata mapango. Pia naye amewataka washukuru na wakumbuke.

Je, vipi wale wenye kustarehe hivi leo wakikaa kwenye majumba ya ghorofa wakiibadilisha hewa vile watakavyo – baridi au joto na pembeni mwao kuna mahema ya wakimbizi na huku wanadai kuwa wao wanamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho?

Na kama wakikengeuka, basi juu yako ni kufikisha tu ujumbe ulio wazi na hisabu ni juu yetu sisi. Wewe umekwishamaliza kazi yako kwa ukamilifu na sisi tutawalipa hisabu yao na malipo yao.

Imetangulia Aya hii katika Juz.3 (3:20) na Juz.13 (13:40),Wanazijua neema za Mwenyezi Mungu kisha wanazikanusha . Makusudio ya kuzijua ni kwamba wao wanazitumia. Na kuzikanusha ni kwamba wao wanazitegemeza neema hizo kwa asiyestahiki. Yaani wanakula riziki ya Mwenyezi Mungu na wanamwabudu mwingine.

Na wengi wao ni makafiri.

Inafaa kulitumia neno wengi kwa maana yake ya dhahiri na inafaa pia kulitumia kwa maana ya wote. Makusudio hapa ni kila ambaye imemfikia risala ya Muhammad(s.a.w.w) na akaikanusha kwa inadi.

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA NNE

وَيَوْمَ نَبْعَثُ مِن كُلِّ أُمَّةٍ شَهِيدًا ثُمَّ لَا يُؤْذَنُ لِلَّذِينَ كَفَرُوا وَلَا هُمْ يُسْتَعْتَبُونَ ﴿٨٤﴾

84. Siku tutakapomwinua shahidi kwa kila umma, kisha hawataruhusiwa wale ambao wamekufuru wala hawataachiliwa kutaka radhi.

وَإِذَا رَأَى الَّذِينَ ظَلَمُوا الْعَذَابَ فَلَا يُخَفَّفُ عَنْهُمْ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ ﴿٨٥﴾

85. Na wale ambao wamedhulumu watakapoiona adhabu hawatapunguziwa wala hawatangojewa.

وَإِذَا رَأَى الَّذِينَ أَشْرَكُوا شُرَكَاءَهُمْ قَالُوا رَبَّنَا هَـٰؤُلَاءِ شُرَكَاؤُنَا الَّذِينَ كُنَّا نَدْعُو مِن دُونِكَ فَأَلْقَوْا إِلَيْهِمُ الْقَوْلَ إِنَّكُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿٨٦﴾

86. Na wale ambao wameshirikisha watakapowaona wale ambao wamewashirikisha watasema: Mola wetu! Hawa ndio washirikishwa wetu ambao tulikuwa tukiwaomba badala yako, Ndipo wale watakapowatupia kauli: Hakika nyinyi ni waongo.

وَأَلْقَوْا إِلَى اللَّـهِ يَوْمَئِذٍ السَّلَمَ وَضَلَّ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ ﴿٨٧﴾

87. Na siku hiyo watasalimu amri mbele ya Mwenyezi Mungu na yatapotea waliyokuwa wakiyazua.

الَّذِينَ كَفَرُوا وَصَدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ زِدْنَاهُمْ عَذَابًا فَوْقَ الْعَذَابِ بِمَا كَانُوا يُفْسِدُونَ ﴿٨٨﴾

88. Wale ambao wamekufuru na kuzuilia watu njia ya Mwenyezi Mungu tutawazidishia adhabu juu ya adhabu kwa walivyokuwa wafisadi.

وَيَوْمَ نَبْعَثُ فِي كُلِّ أُمَّةٍ شَهِيدًا عَلَيْهِم مِّنْ أَنفُسِهِمْ وَجِئْنَا بِكَ شَهِيدًا عَلَىٰ هَـٰؤُلَاءِ وَنَزَّلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ تِبْيَانًا لِّكُلِّ شَيْءٍ وَهُدًى وَرَحْمَةً وَبُشْرَىٰ لِلْمُسْلِمِينَ ﴿٨٩﴾

89. Na siku tutakapomwinua katika kila umma akiwashudia kutokana na wao na tukakuleta wewe uwe shahidi juu ya hawa na tumekuteremshia Kitabu hiki kubainisha kila kitu na uongofu na bishara kwa Waislamu.

TUTAPOMWINUA SHAHIDI

Aya 84 -89

MAANA

Siku tutakapomwinua shahidi kwa kila umma, kisha hawataruhusiwa wale ambao wamekufuru wala hawatachiliwa kutaka radhi.

Haya ni makemeo na kiaga kwa wale aliowaashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya iliyotangulia kwa kusema kwake: “Wanazijua neema za Mwenyezi Mungu kisha wanazikanusha”

Njia ya makemeo hayo ni kuwa Mwenyezi Mungu atawakusanya watu kesho na atamleta kila mtume ashuhudie au awe shahidi wa umma wake. Atakpotoa ushahidi Mwenyezi Mungu ataichukua kauli yake na wala hawataruhusiwa kuipinga kauli hiyo na kutoa udhuru. Mwenyezi Mungu anasema:

هَـٰذَا يَوْمُ لَا يَنطِقُونَ ﴿٣٥﴾ وَلَا يُؤْذَنُ لَهُمْ فَيَعْتَذِرُونَ ﴿٣٦﴾

Hii ni siku ambayo hawtazungumza, Wala hawatapewa ruhusa kutoa udhuru, (77:35-36).

Makusudio ya kutoachiliwa kutaka radhi ni kuwa hawatatakiwa kuomba msamaha kwa kauli wala vitendo. Kwa sababu Akhera ni nyumba ya hisabu na malipo, sio nyumba ya matendo na kuomba msamaha.

Na wale ambao wamedhulumu watakapoiona adhabu hawatapunguziwa wala hawatangojewa.

Makusudio ya wale ambao wameadhulumu ni kila dhalimu; ni sawa awe amemdhulumu Muumba wake kwa kumkanusha au amemdhulumu mwingine kwa kumfanyia ubaya; au awe amejidhulumu yeye mwenyewe kwa kujiingiza kwenye majanga. Yeye ataadhibiwa tu kwa sababu ya dhul- ma. Atapata malipo yanayolingana na kosa, hatapunguziwa wala kuzidishiwa tena bila ya kuchelewa.

Na wale ambao wameshirikisha watakapowaona wale ambao wamewashirikisha watasema: Mola wetu! Hawa ndio washirikishwa wetu ambao tulikuwa tukiwaomba badala yako, Ndipo wale watakapowatupia kauli: Hakika nyinyi ni waongo.

Watakaotupa kauli ni wale walioshirikishwa, wakiwatupia washirikina. Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa Mwenyezi Mungu atawafufua wale waliokuwa wakiabudiwa, wawe ni masanamu au kitu kingine, ili awape hoja wale waliokuwa wakiwafanya wengine kuwa ni waungu. Na kwamba washirikina watakapowaona hao waungu wao waliokuwa wakiwaabudu, watamwambia Mwenyezi Mungu: hawa ndio tuliokuwa tukiwashirikisha nawe. Na hao waungu wajibu kwa maneno au kwa kihali kuwa, nyinyi washirikina ni waongo na wazushi kwa kutufanya sisi ni washirika wa Mwenyezi Mungu.

Sio mbali kuwa masimulizi haya ya kauli ya washirikina ni fumbo la kufichuka uhakika kesho na kwamba hakutakuwa na nafasi ya uwongo wala kudanganya.

Na siku hiyo watasalimu amri mbele ya Mwenyezi Mungu.

Yaani washirikina na waungu wao watasalimu amri na kunyenyekea amri ya Mwenyezi Munguna yatapotea waliyokuwa wakiyazua. Kila mzushi katika maisha haya utamrudia uzushi wake kwa hizaya na adhabu siku hiyo ngumu.

Wale ambao wamekufuru na kuzuilia watu njia ya Mwenyezi Mungu tutawazidishia adhabu juu ya adhabu kwa walivyokuwa wafisadi.

Walifanya ufisadi kwa kukufuru kwao haki na wakafanya ufisadi kwa kuizuilia haki kwa hiyo wanastahiki adhabu mara mbili. Moja kwa ajili ya ufisadi na nyingine kwa ajili ya kufisidisha:

وَمَا هُم بِحَامِلِينَ مِنْ خَطَايَاهُم مِّن شَيْءٍ ﴿١٢﴾

“Na hakika wataibeba mizigo yao pamoja na mizigo mingine” (29:12)

Na siku tutakapomwinua katika kila umma akiwashudia kutokana na wao.

Yametangulia maana ya Aya hii katika Aya 84 ya sura hii, Hapa imerudia kuwakema wale waliomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) .

Na tukakuleta wewe uwe shahidi juu ya hawa.

Neno ‘wewe’ hapa ni Muhammad(s.a.w.w) na ‘hawa’ ni umma wake.Unaweza kuuliza kwamba : Muhammad(s.a.w.w) ni Mtume wa Mwenyezi

Mungu kwa watu wote kwa nukuu ya Aya hii:

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٨﴾

Na hatukukutumma ila kwa watu wote uwe mbashiri na muonyaji, lakini watu wengi hawajui (34:28).

Kwa hiyo ikiwa risala ya Muhammad ni kwa watu wote, inatakikana ushahidi wake pia uwe kwa watu wote huko akhera, lakini kama ikiwa ushahidi wake huko akhera ni kwa umma wake tu, basi itabidi risala yake hapa duniani iwe kwa umma wake tu?

Jibu : hakuna uhusiano wa ushahidi wake kwa umma wote huko akhera na kuenea risala yake hapa duniani. Kwa sababu risala ya Uislamu inafikishwa na umma wa Muhammad(s.a.w.w) baada yake kwa umma zote wakati wote na mahali pote. Mtume anatoa ushahidi juu ya umma wake kwamba hawakufikisha risala kwa vizazi vingne.

Na tumekuteremshia Kitabu hiki kubainisha kila kitu.

Maneno anaambiwa Muhammad, Makusudio ya kitabu hiki ni Qur’an, ndani yake mna ubainifu wa kila kitu unaoamabatana na itikadi, sharia, maadili, mazingatio na mawaidha.na uongofu kwa anayeutakana bishara kwa Waislamu.

Makusudio ya bishara hapa ni Pepo na Mwislamu ni kila mwenye kusalimu amri ya haki na akaitumia.

إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ يَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ ﴿٩٠﴾

90. Hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha uadilifu na hisani na kuwapa jamaa na anakataza uchafu na uovu na dhulma. Anawapa mawaidha ili mpate kukumbuka.

وَأَوْفُوا بِعَهْدِ اللَّـهِ إِذَا عَاهَدتُّمْ وَلَا تَنقُضُوا الْأَيْمَانَ بَعْدَ تَوْكِيدِهَا وَقَدْ جَعَلْتُمُ اللَّـهَ عَلَيْكُمْ كَفِيلًا إِنَّ اللَّـهَ يَعْلَمُ مَا تَفْعَلُونَ ﴿٩١﴾

91. Na tekelezeni ahadi ya Mwenyezi Mungu mnapoahidi; wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha, ilhali mmekwishamfanya Mwenyezi Mungu ndiye mdhamini wenu, Hakika Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyafanya.

وَلَا تَكُونُوا كَالَّتِي نَقَضَتْ غَزْلَهَا مِن بَعْدِ قُوَّةٍ أَنكَاثًا تَتَّخِذُونَ أَيْمَانَكُمْ دَخَلًا بَيْنَكُمْ أَن تَكُونَ أُمَّةٌ هِيَ أَرْبَىٰ مِنْ أُمَّةٍ إِنَّمَا يَبْلُوكُمُ اللَّـهُ بِهِ وَلَيُبَيِّنَنَّ لَكُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ مَا كُنتُمْ فِيهِ تَخْتَلِفُونَ ﴿٩٢﴾

92. Wala msiwe kama mwanamke ambaye ameufumua uzi wake baada ya kuusokota na kuwa mgumu. Mnavifanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganyana baina yenu kwa kuwa kundi moja lina nguvu zaidi kuliko jengine. Hakika Mwenyezi Mungu anawajaribu kwayo na hakika atawabainishia siku ya kiyama yale mliyokuwa mkihitalifiana.

وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَجَعَلَكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَلَـٰكِن يُضِلُّ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ وَلَتُسْأَلُنَّ عَمَّا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٩٣﴾

93. Na lau Mwenyezi Mungu angelitaka bila shaka angeliwafanya umma mmoja, lakini humpoteza anayemtaka na humwongoa anayemtaka. Hakika mtaulizwa kuhusu yale mliyokuwa mkiyafanya.

MWENYEZI MUNGU ANAAMRISHA UADILIFU NA HISANI

Aya 90 – 93

LUGHA

Kwa kawaida kila analojilazimisha nalo mtu kwa hiyari yake ni Ahadi. Ahadi inakuwa ni wajib kuitekeleza ikiwa ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kuambatanishwa na jina lake; mfano kusema: ‘Nimemwahidi Mwenyezi Mungu kufanya jambo fulani’ au ‘Nimejilazimisha ahadi ya Mwenyezi Mungu kufanya jambo fualani’ Kuvunja ahadi hii ni kama kuvunja kiapo, inabidi kutoa kafara; kama ilivyoelezwa katika vitabu vya Fiqh.

MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu anaamrisha uadilifu na hisani na kuwapa jamaa na anakataza uchafu na uovu na dhulma.

Aya imeamrisha mambo matatu mazuri na kukataza matatu maovu. Ama matatu mazuri ni haya yafuatayo:

1. Uadilifu: Mtu mwadilifu ni yule anayewafanyia insafu watu yeye mwenyewe na kuwafanyia yale yaliyo wajibu kuwafanyia.

2. Hisani: Inakusanya kila jambo la kheri. Watu wanafahamu kuwa hisani ni kujitolea mtu kwa mali yake au juhudi yake katika njia ya kheri.

3. Kuwapa jamaa: Huko pia ni kufanya hisani. Mwenyezi Mungu amekuhusisha kukutaja peke yake kwa kukukweza kutokana na ubora wake.

Ama matatu mabaya ni:

1. Uchafu; kama zinaa, ulawiti, pombe, kamari, uwongo na uzushi. Uchafu ulio dhahiri zaidi ni zinaa. Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anasema:

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

“Wala msiikurubie zinaa; hakika hiyo ni uchafu na njia mbaya.” (17:32).

2. Uovu: Ni kila linalopingana na akili na sharia.

3. Dhulma: Ni kuwafanyia uadui watu kwa kauli au vitendo. Hukumu yake kesho mbele ya Mwenyezi Mungu ni sawa na shirki, bali dhulma ni zaidi. Kwa sababu shrki ni kuifanyia uadui haki ya Mwenyezi Mungu ambaye anaweza kuisamehe. Lakini dhulma ni kuifanyia uadui haki ya Mwenyezi Mungu na haki ya watu.

Mara nyingine uchafu unaitwa uovu na uovu unaitwa uchafu. Yote hayo mawili ni dhulma.

Anawapa mawaidha ili mpate kukumbuka.

Makusudio ya mawaidha yake Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni kuamrisha kwake mambo mazuri na kukataza kwake mambo mabaya. Lengo la mawaidha ni kuwa tuwe waumini wenye takua, wema na wasafi. Wapokezi wa Hadith wamepokea kutoka kwa Ibn Mas’ud kwamba Aya hii ndiyo iliyokusanya zaidi mambo ya kheri na ya shari katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu.

Amesema Uthman Bin Madh’un: “Nilisilimu kwa kumstahi Mtume wa Mwenyezi Mungu, Na haukuingia Uisalmu moyoni mwangu mpaka iliposhuka Aya hii. Kwa hiyo nikamwamini Muhammad(s.a.w.w) na nikamwendea ami yake, Abu Twalib, nikampa habari ya jambo langu hilo, akasema: ‘Enyi maquraish! Mfuateni Muhammad mtaongoka; Kwa sababu yeye hawaamuru isipokuwa tabia nejema.

Na tekelezeni ahadi ya Mwenyezi Mungu mnapoahidi.

Kumwahidi Mwenyezi Mungu kunaweza kuwa kwa mambo mawili: Kwanza, kukata mtu katika nafsi yake kumwahidi Mwenyezi Mungu kufanya jambo fulani au kuliacha; kama kusema: ‘Namwahidi Mwenyezi Mungu kuwa nitafanya jambo kadhaa au kuacha jambo kadhaa’

Aina ya pili ni kumwamini Mwenyezi Mungu. Kwa sababu mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu anakuwa amempa ahadi Mwenyezi Mungu kufuata amri yake na kukatazika na makatazo yake.

Ahadi zote hizi mbili ni wajibu kuzitekeleza. Makusudio ya ahadi kwenye Aya hii ni aina ya kwanza ya ahadi tuliyoieleza.

Wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha.

Makusudio ya kuvidhibitisha hapa ni kuvifunga hivyo viapo, yaani kuapa. Kwa sababu kiapo kinafungika ikiwa si kwa kumwasi Mwenyezi Mungu na wala hakifungiki, kivyovyote, ikiwa ni kwa jili ya kumwasi.

Imesemekana kuwa makusudio ya kuvithibisha hapa ni kuvitilia mkazo na kuvisisitiza. Lakini maelezo haya ni kutatizika. Ambapo maana yake yatakuwa viapo visivyosisitizwa havina wajibu wa kuvitekeleza na inajulikana kuwa kiapo kikitimia basi ni wajibu kukitekeleza, kiwe kimesisitizwa au la.

Ilhali mmekwishamfanya Mwenyezi Mungu ndiye mdhamini wenu.

Kila aliyeapa kwa jina la Mwenyezi Mungu amemfanya Mwenyezi Mungu ni mdhamini kiutekelezaji. Akivunja kiapo basi atakuwa amemfanyia hiyana Mwenyezi Mungu hasa, na atastahiki adhabu.

Hakika Mwenyezi Mungu anayajua mnayoyafanya.

Mwenye kutekeleza ahadi yake na kiapo chake, Mwenyezi Mungu atamlipa thawabu za watiifu na mwenye kuvunja na akafanya hiyana atamwadhibu adhabu ya waasi.

Kwa hakika ilivyo ni kwamba ahadi na kiapo vinafunguka ikiwa kuacha ni bora kuliko kutekeleza. Kwa mfano, mtu akiapa au kumwahidi Mungu kuwa hatakula nyama na ikawa kuacha kula nyama kuna manufaa ya afya yake, basi kiapo au ahadi itafungika.

Na kama baadae, ukimtokea ulazima wa kula nyama, atakula na kiapo au ahadi itafunguka na hatakuwa na chochote. Kuna hadith isemayo: “Ukiona heri yoyote katika kiapo chako basi kiache”

Wala msiwe kama mwanamke ambaye ameufumua uzi wake baada ya kuusokota na kuwa mgumu.

Kila kitu kinachovunjwa baada ya kufungwa basi kimefumuka, kiwe uzi, kamba au kitu chochote.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amepiga mfano wa kuvunja ahadi na uzi uliofumuliwa baada ya kusokotwa.

Inasemekana kuwa huko Makka kulikuwa na mwanamke mmoja mpum- bavu aliyekuwa akisokota sufu yake asubuhi na ikifika jioni anaifumua, na Mwenyezi Mungu akamfananisha na mvunja ahadi.

Vyovyote iwavyo ni kuwa Aya inatilia mkazo kauli yake Mwenyezi Mungu: ”Wala msivunje viapo baada ya kuvithibitisha.”

Mnavifanya viapo vyenu kuwa ni njia ya kudanganyana baina yenu kwa kuwa kundi moja lina nguvu zaidi kuliko jengine.

Yaani msijaalie viapo vyenu kuwa ni nyenzo ya kudanganya na hiyana; kwa kuapa mbele ya wale walio wengi na wenyenguvu zaidi kuliko nyinyi ili wawaamini, wakati nyinyi mnadhamiria kuvunja viapo hivyo na muwaache wale ambao mliapa mbele yao pale mtakapojiona nyinyi mna nguvu zaidi kuliko wao.

Hakika Mwenyezi Mungu anawajaribu kwayo

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawakalifisha waja ili atii mtiifu kwa hiyari yake na aasi muasi kwa hiyari yake; kisha kila mmoja amlipe malipo yake anayostahiki. Tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi katika Juz. 7 (5:94)

Na hakika atawabainishia siku ya Kiyama yale mliyokuwa mkihitali- fiana.

Mwenyezi Mungu atawarudisha waja siku ya kiyama ili ajulikane mtiifu na mbatilifu na amlipe kila mmoja stahiki yake.

Na Mwenyezi Mungu angelitaka bila shaka angeliwafanya umma mmoja.

Yaani kama Mwenyezi Mungu angelitaka kumlazimisha mtu kuamini watu wote wangelikuwa umma mmoja, lakini amemwachia mtu na hiyari yake. Kwani lau angelimnyang’anya uhuru huu na hiyari, angelikuwa sawa na mnyama Tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi katika Juz. 7 (6: 35) na katika Juz. 12 (11:118).

Lakini humpoteza anayemtaka na humwongoa anayemtaka.

Hakuna shaka kwa mwenye akili kwamba Mwenyezi Mungu hapotezi wala kumwongoza yeyote kwa lazima. Lau ingelikuwa hivyo isingelikuwa sawa kumuuliza na kumchukulia hisabu. Naye amesema mara tu baada ya maneno hayo:

Hakika mtaulizwa kuhusu yale mliyokuwa mkiyafanya.

Maana ya Aya ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamzingatia mtu kuwa ni mpotevu baada ya yeye mwenyewe kufuata njia ya upotevu, na anamzingatia ni mwongofu baada ya kufuata njia ya uwongofu; sawa na anavyomuua anayeamua kujinyonga.

Yametangulia maelezo kuhusu uongofu na upotevu katika Juz; 1 (2:26), Juz. 3 (2: 272) na Juz; 5 (4:88).