TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO Juzuu 15

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO22%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 19 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 17073 / Pakua: 4163
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO Juzuu 15

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

وَآتِ ذَا الْقُرْبَىٰ حَقَّهُ وَالْمِسْكِينَ وَابْنَ السَّبِيلِ وَلَا تُبَذِّرْ تَبْذِيرًا ﴿٢٦﴾

26. Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia, wala usifanye ubadhirifu.

إِنَّ الْمُبَذِّرِينَ كَانُوا إِخْوَانَ الشَّيَاطِينِ وَكَانَ الشَّيْطَانُ لِرَبِّهِ كَفُورًا ﴿٢٧﴾

27. Hakika wabadhirifu wamekuwa ni ndugu wa mashetani, na shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake.

وَإِمَّا تُعْرِضَنَّ عَنْهُمُ ابْتِغَاءَ رَحْمَةٍ مِّن رَّبِّكَ تَرْجُوهَا فَقُل لَّهُمْ قَوْلًا مَّيْسُورًا ﴿٢٨﴾

28. Na ikiwa unajipurukusha nao kwa kutaraji rehema ya Mola wako, basi sema nao maneno laini.

وَلَا تَجْعَلْ يَدَكَ مَغْلُولَةً إِلَىٰ عُنُقِكَ وَلَا تَبْسُطْهَا كُلَّ الْبَسْطِ فَتَقْعُدَ مَلُومًا مَّحْسُورًا ﴿٢٩﴾

29. Wala usiufanye mkono wako umefungwa shingoni mwako, wala usiunyooshe wote kabisa, utabaki mwenye kulaumiwa, mwenye kuishiwa.

إِنَّ رَبَّكَ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ إِنَّهُ كَانَ بِعِبَادِهِ خَبِيرًا بَصِيرًا ﴿٣٠﴾

30. Hakika Mola wako humkunjulia riziki amtakaye na humpimia amtakaye. Hakika Yeye kwa waja wake ni mwenye habari, aonaye.

وَلَا تَقْتُلُوا أَوْلَادَكُمْ خَشْيَةَ إِمْلَاقٍ نَّحْنُ نَرْزُقُهُمْ وَإِيَّاكُمْ إِنَّ قَتْلَهُمْ كَانَ خِطْئًا كَبِيرًا ﴿٣١﴾

31. Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa kuishiwa, sisi tutawaruzuku nyinyi na wao Hakika kuwaua ni hatia kubwa.

وَلَا تَقْرَبُوا الزِّنَىٰ إِنَّهُ كَانَ فَاحِشَةً وَسَاءَ سَبِيلًا ﴿٣٢﴾

32. Wala msiikurubie zinaa; Hakika hiyo ni uchafu na njia mbaya.

وَلَا تَقْتُلُوا النَّفْسَ الَّتِي حَرَّمَ اللَّـهُ إِلَّا بِالْحَقِّ وَمَن قُتِلَ مَظْلُومًا فَقَدْ جَعَلْنَا لِوَلِيِّهِ سُلْطَانًا فَلَا يُسْرِف فِّي الْقَتْلِ إِنَّهُ كَانَ مَنصُورًا ﴿٣٣﴾

33. Wala msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuiua), ila kwa haki. Na aliyeuliwa kwa kudhulumiwa, basi tumempa madaraka walii wake, lakini asipetuke mpaka katika kuua, kwani hakika yeye anasaidiwa.

وَلَا تَقْرَبُوا مَالَ الْيَتِيمِ إِلَّا بِالَّتِي هِيَ أَحْسَنُ حَتَّىٰ يَبْلُغَ أَشُدَّهُ وَأَوْفُوا بِالْعَهْدِ إِنَّ الْعَهْدَ كَانَ مَسْئُولًا ﴿٣٤﴾

34. Wala msiikurubie mali ya yatima isipokuwa kwa njia bora zaidi, mpaka afikie kukomaa kwake; Na tekelezeni ahadi. Hakika ahadi itasailiwa.

وَأَوْفُوا الْكَيْلَ إِذَا كِلْتُمْ وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ ذَٰلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلًا ﴿٣٥﴾

35. Na timizeni kipimo mnapopima, na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni kheri kweni na hatima njema.

وَلَا تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولَـٰئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْئُولًا ﴿٣٦﴾

36. Wala usifuatilie ambalo huna ujuzi nalo. Hakika masikio na macho na moyo, hivyo vyote vitasailiwa.

وَلَا تَمْشِ فِي الْأَرْضِ مَرَحًا إِنَّكَ لَن تَخْرِقَ الْأَرْضَ وَلَن تَبْلُغَ الْجِبَالَ طُولًا ﴿٣٧﴾

37. Wala usitembee katika Ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala kufikia urefu wa milima.

كُلُّ ذَٰلِكَ كَانَ سَيِّئُهُ عِندَ رَبِّكَ مَكْرُوهًا ﴿٣٨﴾

38. Hayo yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako.

ذَٰلِكَ مِمَّا أَوْحَىٰ إِلَيْكَ رَبُّكَ مِنَ الْحِكْمَةِ وَلَا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتُلْقَىٰ فِي جَهَنَّمَ مَلُومًا مَّدْحُورًا ﴿٣٩﴾

39. Hayo ni katika hekima alizokupa wahyi Mola wako. Usimfanye mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, usije ukalaumiwa, uliyetupwa.

WASIA 10

Aya 26 – 39

MAANA

1.Na mpe jamaa wa karibu haki yake na maskini na mwana njia wala usifanye ubadhirifu.

Amenukuu Tabrasi katika Majmaul-bayan kutoka kwa Assadiy, ambaye ni miongoni mwa wafasiri wakubwa, kwamba makusudio ya jamaa wa karibu ni jamaa wa Mtume(s.a.w.w) .

Abu Hayan Al-andalusi amenukuu kutoka kwa Imam Ali bin Husein(a.s) kwamba yeye amesema: “Hao ni jamaa wa Mtume(s.a.w.w) , Mwenyezi Mungu ameamrisha kuwapa haki yao kutoka katika hazina.

Amesema Abu Bakar Al-mua’firi Al-maliki katika Ahkamul-qur’an: “Anaingia katika jamaa wa karibu jamaa wa Mtume kuingia kwa kutangulia na kwa njia ya aula tu. Lakini hakika Aya ni ya ndugu wa mtu walio karibu zaidi. Ama jamaa wa karibu wa Mtume Mwenyezi Mungu amebainisha kuwahusu wao na akaeleza kwamba kuwapenda ndio ujira wa Mtume kwa yale aliyotuongoza.”

Imesemekana kuwa makusudio ya jamaa wa karibu ni yule ambaye ana haki ya kumtunza na kurithi, masikini ni muhitajia na mwananjia ni msafiri aliyekatikiwa njiani asiyekuwa na uwezo wa gharama za kurudi kwao. Hawa wawili wana haki ya zaka; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

إِنَّمَا الصَّدَقَاتُ لِلْفُقَرَاءِ وَالْمَسَاكِينِ وَالْعَامِلِينَ عَلَيْهَا وَالْمُؤَلَّفَةِ قُلُوبُهُمْ وَفِي الرِّقَابِ وَالْغَارِمِينَ وَفِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَابْنِ السَّبِيلِ فَرِيضَةً مِّنَ اللَّـهِ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ حَكِيمٌ ﴿٦٠﴾

“Hakika sadaka ni ya (hawa) tu: Mafukara na masikini na wanaozitumikia na wanaotiwa nguvu nyoyo zao na kuwakomboa watumwa na wenye madeni na katika njia ya Mwenyezi Mungu na mwana njia.” Juz.10 (9:60).

Hakika wabadhirifu wamekuwa ni ndugu wa mashetani, na shetani ni mwenye kumkufuru Mola wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameleta ibara ya wabadhirifu kuwa ni ndugu wa shetani, kwa sababu ubadhirifu ni jambo linalochukiwa na Mwenyezi Mungu na kila linalochukiwa na Mwenyezi Mungu linapendeza kwa shetani.

Hakuna anayetofautiana na wenzake kuwa maana ya ubadhirifu ni kutoa mali kwenye njia isiyokuwa yake na kuiweka mahali pasipokuwa pake, iwe kwa uchache au kwa wingi. Kwa ibara ya watu wa mantiki ni kwamba ubadhirifu ni katika aina si katika idadi.

Unaweza kuuliza kuwa : kauli ya isiyokuwa njia yake na pasipokuwa mahali pake inafanana na maneno yenye kutatiza ambayo yanahitaji ufafanuzi na maelezo; basi ni ipi hiyo njia yake na mahali pake?

Jibu : kila mwenye kutumia mali yake katika mambo yanayomletea madhara au yasiyokuwa na manufaa yoyote, basi huyo ni mwenye israfu, mbadhirifu na safihi, kikawaida na kisharia; isipokuwa mali anayoitoa kwa ajili ya kuvuta sigara. Tumedokeza kuhusu matumizi mabaya na kuzuiliwa kutumia matumizi ya kimali kwa mwenye kufanya hivyo, katika Juz. 4 (4:5).

WAKO WAPI WAADILIFU?

Swali la pili linaweza kuja hivi: Mtu ametumia mali yake kwa kunywa pombe, kula nyama ya nguruwe na mengineyo katika yaliyoharamishwa ambayo yanamletea manufaa ya sasa na madhara ya muda ujao. Mtu huyu watu wengi hawamuoni kuwa ni mbadhirifu wala safihi; sasa je, sharia ya kiislamu inawajibisha kuzuiliwa matumizi ya kimali, kwa vile yeye ni safihi mwenye kufanya israfu?

Jibu : Mtu mwenye akili anayo ruhusa ya kutumia mali yake bila ya kuiingiliwa; awe mumin au kafiri, fasiki au mwadilifu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Mkiwaona wana uwekevu, basi wapeni mali zao” Juz. 4 (4:6) na wala hakusema mkiwaona wana uwekevu wa dini au uadilifu. Imepokewa Hadith Mutawatur kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba yeye amesema: “Watu wamesalitiwa na mali zao,” na wala hakusema waumini au waadilifu.

Kwa hiyo sharti pekee la kusihi matumizi haya ni uwekevu katika mali si katika dini. Lau ingelikuwa uadilifu na uongofu ni sharti la kusihi matumizi ya mtu katika mali yake, basi nidhamu ingeliharibika na maisha yangesimama, kwa sababu watu wa duniani wako kama tunavyowajua, tutawatoa wapi watu wa dini na waadilifu?

Hanafi, Malik na Hambali wako katika rai yetu hii. Ama Shafii, wamesema kuwa uongofu ndio unaofaa katika dini na mali, kama ilivyoelezwa katika kitab Al-mughni cha Ibn Abi quddama.

Na ikiwa unajipurukusha nao kwa kutaraji rehema ya Moa wako, basi sema nao maneno laini.

Wakusema nao hapa ni jamaa wa karibu, masikini na msafiri aliyeishiwa njiani. Maana ni kuwa, akikuuliza kitu katika mali na wala usipate cha kumpa na ukamuomba Mwenyezi Mungu amtosheleze yeye na akutosheleze wewe kutokana na fadhila yake na rehema yake, basi sema naye kwa kauli laini kwa kumpa maneno mazuri yatakyompa matumaini na matarajio katika moyo wake. Kuna Hadith isemayo: “ Ikiwa hamna wasaa wa kuwapa watu mali zenu basi mnao wasaa wa kuwapa maadili yenu” Mshairi naye anasema: Kutamka kuwe kwema ikiwa hali si njema.

UISLAMU NA NADHARIA YA MAADILI

2.Wala usiufanye mkono wako umefungwa shingoni mwako, wala usiunyooshe wote kabisa, utabaki mwenye kulaumiwa, mwenye kuishiwa.

Kipimo na uwiano ndio msingi wa kila kitu katika Uislam kiitikadi, kisharia na kimaadili; sio ki ulahidi na kiidadi ya waungu. Na si kwa kuondoa milki ya mtu wala kuweka milki ya utaghuti na wala sio udikteta wa kikundi cha watu au wa mtu mmoja wala si utawala wa kila anayetaka, sio utawa wala sio kuzama kwenye matamanio. Kila kitu kinakuwa na uhalali na uharamu:

وَكُلُّ شَيْءٍ عِندَهُ بِمِقْدَارٍ ﴿٨﴾

“Na kila kitu kwake, ni kwa kipimo” Juz; 13 (13:8).

Kusema kwake ni kwa kipimo ni kuwa na nidhamu inayoafikiana na hekima na masilahi, hakuna kupetuka mpaka wala kupetusha mipaka; wala hivi hivi au kombokombo. Kila kitu kina mpaka wake mbele ya Mwenyezi Mungu ambayo ni wajibu kwa kila mtu asimame kwenye mipaka hiyo bila ya kuikeuka. Kwa mfano mipaka ya hukumu na utawala ni uadilifu; mipaka ya kumiliki ni kutomdhuru mtu au watu; mipaka ya matumizi ni kutofanya uchoyo wala kufanya ubadhirifu na matendo mengineyo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameuletea ibara uchoyo kwa kufunga mkono shingoni, kwa sababu mchoyo anazuia mkono wake kutoa. Na kauli yake: ‘wala usiunyooshe wote kabisa’ anakusudia mkono ambao hauzuii kitu. Mwisho wa wote hawa wawili ni mmoja – kuishiwa na lawama.

Mwenye israfu atauma mkono wa kuishiwa, kujuta na kulaumiwa mbele ya Mwenyezi Mungu, watu na yeye mwenyewe, pale atakapokuwa mikono mitupu; wakati ambapo bakhili analaumiwa na kila mtu, na kuishiwa kwake kesho ni zaidi kuliko mbadhirifu. Jambo bora zaidi ni wastani.

Unaweza kuuliza : Je, hii ina maana Uislamu unakubaliana na nadharia ya Socrates inayosema: Kila ubora ni kati ya mabaya mawili. Kwa hiyo ushujaa ni wastani baina ya kujitutumua na woga, ukarimu ni baina ya israfu na uchoyo, unyenyekvu ni baina ya kutahayari na kukosa haya nk?

Jibu : Hapana! Kwani Uislam unapanga ubora na kuweka sharia ya hukumu kwa misingi ya masilahi ya mtu mmoja mmoja hadi watu wengi. Kila jambo ambalo linaendeleza maisha basi ni wajibu wa lazima kwa kiongozi na wajibu wa kutosheana (kifaya) kwa raia.

Na kila lenye manufaa kwa upande fulani basi ni bora; bali ni ibada ya wajibu kwa kila mwenye uweza au suna kulingana na kiwango cha manufaa. Mwenyezi Mungu anasema:

وَأَمَّا مَا يَنفَعُ النَّاسَ فَيَمْكُثُ فِي الْأَرْضِ ﴿١٧﴾

“Ama kinachowafaa watu hukaa kwenye ardhi” Juz; 13 (13:17).

Mtume(s.a.w.w) amesema: “Bora ya watu ni yule wanayenufaika naye.” Dalili wazi zaidi ya hakika hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu: “Ambao wanamfuata Nabii asiyesoma wala kuandika ambaye wanamkuta ameandikwa kwao katika Tawrat na Injili ambaye anawaamrisha mema na anawakataza maovu, na anawahalalishia vizuri na kuwaharamishia vibaya, na kuwaondolea mizigo yao na minyororo iliyokuwa juu yao.” Juz.9 (7:157).

Msingi huu wa Qur’an – masilahi - unaweza kulingana na nadharia ya wastani kwenye vitu vyenye wastani; kama vile ukarimu kuwa baina ya uchoyo na israfu. Lakini unatofautiana katika vitu visivyo na wastani; kama vile uaminifu ni dhidi ya hiyana, wala hakuna jingine la kuleta wastani kuwa ni baina ya uaminifu na hiyana; Tumezungumzia kuhusu maadili katika Juz. 6 (5:79).

Hakika Mola wako humkunjulia riziki amtakaye na humpimia amtakaye. Hakika Yeye kwa waja wake ni mwenye habari aonaye.

Makusudio ya kumpimia ni kuifanya finyu. Kila kitu kiko mikononi mwake, riziki na zisizokuwa riziki. Kwa sababu Yeye ni mmliki wa milki zote, lakini hekima yake imetaka na kupitisha kutomruzuku yeyote isipokuwa kwa sababu za kiulimwengu ambazo ameziumba na kuziwekea njia za kuchuma mali n.k. Angalia Juz. 6(5: 66) na Juz; 13 (13: 26).

3.Wala msiwaue watoto wenu kwa kuogopa kuishiwa, sisi tutawaruzuku nyinyi na wao pia. Hakika kuwaua ni hatia kubwa.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (6: 151).

4.Wala msiikurubie zinaa. Hakika hiyo ni uchafu na njia mbaya.

Imekuwa ni uchafu kwa vile mwishilio wake ni kuvurugika na kuchanganyika nasaba. Inatosha zina kuwa ni uovu kwa vile ni katika sifa mbaya za kushutumiwa.

5.Wala msiiue nafsi ambayo Mwenyezi Mungu ameharamisha (kuiua), ila kwa haki.

Umetangulia mfano wake katika katika Juz. 8 (6: 151).

Na aliyeuliwa kwa kudhulumiwa, basi tumempa madaraka walii wake, lakini asipetuke mpaka katika kuua, kwani hakika yeye anasaidiwa.

Kila aliyeuawa bila ya kufanya kosa linalowajibisha kuuliwa basi ameuawa kwa dhulma. Walii wa aliyeuawa ni ndugu zake kwa upande wa baba. Ikiwa hawako basi ni hakimu wa sharia. Kupetuka mpaka katika kuua ni kuua wawili kwa mmoja; kama walivyokuwa wakifanya wakati wa jahilia.

Maana ni kuwa ndugu wa aliyeuawa kwa dhulma wana haki ya kuua aliyeua au kuchukua fidiya; kama ilivyoelezwa katika Hadith tukufu: “Mwenye kuua basi watu wa aliyeuawa wana hiyari mbili: wakipenda wataua na wakipenda watachukua fidiya.”

Kwa vile ndugu wa aliyeuawa wana haki hiyo, basi ni wajibu wa hakimu na kila mwislamu kusaidia kutimizwa haki hii; Yametangulia maelezo kuhusu haya katika Juz. 2 (2:178).

6.Wala msiikurubie mali ya yatima isipokuwa kwa njia bora zaidi, mpaka afikie kukomaa kwake.

Imekwishapita Aya kama hii kwa herufi zake katika Juz. 8 (6: 152).

7.Na tekelezi ahadi; Hakika ahadi itasailiwa.

Kila aliloliamrisha Mwenyezi Mungu na kulikataza ni wajibu kutekelezwa; ikiwa ni pamoja na mapatano ya bei, ajira n.k. Kwa maelezo zaidi angalia Juz. 6 (5:1).

Na timizeni kipimo mnapopima na pimeni kwa mizani zilizo sawa. Hayo ni kheri kwenu na hatima njema.

Kukamilisha kipimo ni wajibu wa kisharia na kidesturi; wala hauhusiki na dini kuliko dini nyingine au desturi kuliko desturi nyingine. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehimiza kukamilisha kipimo kwa mifumo mbalimbali; kama vile: pimeni kwa mizani zilizo sawa, timizeni kipimo na mizani, wala msipunguze na wala msipetuke mipaka. Siri ya hilo ni kwamba ustawi wa jamii hauwezi kuwa bila ya usawa wa vipimo.

KUSEMA BILA YA UJUZI

9.Wala usifuatilie ambalo huna ujuzi nalo. Hakika masikio na macho na moyo, hivyo vyote vitasailiwa.

Neno kufuatilia limefasiriwa kutokana na neno la kiarabu Qafwa lenye maana ya kufatilia athari ya jambo. Miongoni mwa majina ya Mtume(s.a.w.w) ni Almuqfi (mfuatiliaji) kwa vile yeye ni mtume wa mwisho.

Kusema jambo bila ya ujuzi ni vibaya hata kwa yule asiyemwamini Mungu na siku ya mwisho. Mwenyezi Mungu ametaja masikio, macho na moyo akikusudia mwenye vitu hivyo vitatu.

Na kwamba Yeye Mwenyezi Mungu ataviuliza na kuviadhibu ikiwa vitawekewa vitu visivyovijua; kama vile lau mtu atasema nimesikia naye hakusikia, nimeona naye hakuona au ni ninaitakidi na kuazimia naye hana itikadi wala maazimio yoyote.

Hakuna tofauti baina ya anayekusudia uongo na anayekurupuka kusema jambo bila ya kulithibitisha. Kwani kusema kwa dhana na shubha ni kusema bila ya ujuzi. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema:

إِنَّ الظَّنَّ لَا يُغْنِي مِنَ الْحَقِّ شَيْئًا ﴿٣٦﴾

“Hakika dhana haifai kitu mbele yake haki” Juz; 11 (10:36)

إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا الظَّنَّ ﴿١١٦﴾

“Hawafuati ila dhana na hawakuwa ila wenye kuzua tu.” Juz; 8 (6: 116)

Mwenyezi Mungu amelinganisha dhana na kuzua.

Kutokana na Aya hii yanajitokeza mambo yafuatayo:

(i) Kubatilika na uharamu wa Taqlid (kufuata) kwa yule mwenye uwezo wa kuchambua hukumu kutoka kwenye rejea zake. Kwa sababu ameacha elimu yake na akaumia elimu ya mwingine. Hii ni rai ya Shia Imamia. Zaydiya, Muu’tazila, Ibin Hazm, Sheikh Muhammad Abduh, Sheikh Shaltut na wengineo. Tumezungumza kwa ufafanuzi kuhusu taqlid katika Juz. 8 (2:259).

(ii) Uharamu wa kutoa hukumu kwa kutumia qiyas (kukisia) na istihsan (kuchukulia kuwa ni vizuri).

Qiyas ni kulinganisha jambo ambalo halikutajwa katika hukumu na jigine lililotajwa kutokana na kuwa na sababu moja.

Kwa mfano sharia kusema kuwa nyanya wa upande wa mama anarithi na ikanyamazia nyanya wa upande wa baba. Tukasema kuwa huyu pia atarithi kwa kukisia kuwa yeye pia ni nyanya.

Istihsan ilivyosimuliwa kutokana na Abu Hanifa ni kutoa hukumu kwa atavyoonelea mujtahidi kuwa ni vizuri bila ya kuweko dalili yoyote isipokuwa anavyoonelea yeye tu.

Rejea Kitabu Allami’ fi usulilfiqh cha Abu Is-haq, Ibrahim bin Ali bin Yusuf Fayruz Abadiy, uk; 65 chapa ya 1939. Mwenya kitabu hicho ametoa mfano wa mwenye kusema:

‘Nikifanya jambo fulani basi mimi ni Myahudi’ akifanya jambo hilo itabidi atoe kafara kwa kuchukulia kuwa ni kama aliyeapa kwa kusema: ‘Wallahi nikifanya jambo fulani basi mimi ni Myahudi.’

Kila mwenye kujasiri kutoa fatwa na kubainisha halali na haramu na yeye si kufu wa kufanya hivyo, basi atakuwa amesema uongo na kumzulia Mwenyezi Mungu na Mtume wake na atakuwa ni katika wale waliokusudiwa na ile Aya isemayo:

تَاللَّـهِ لَتُسْأَلُنَّ عَمَّا كُنتُمْ تَفْتَرُونَ ﴿٥٦﴾

“Wallahi! Hakika mtaulizwa hayo mliyokuwa mkiyazua” Juz; 14 (16:56)

Na kauli ya Mtume Mtukufu(s.a.w.w) : “Mwenye kunisemea uongo kwa makusudi basi na ajichagulie makazi yake motoni” Kumsemea uongo Mwenyezi Mungu na Mtume ni kutoa riwaya kutokana nao au kunasibisha halali na haramu kwao.

Siku hizi mamufti wazushi wamekuwa wengi walioifanya dini kuwa ni njia ya kutafutia riziki na pazia ya kuwa wahaini na vibaraka. Wengine wameanzisha vyama vya kutumikia uzayuni na ukoloni, lakini vina majina ya kiislamu na waislamu ili kuwahadaa na kuwapoteza watu.

Sheikh mmoja aliniuliza kuhusu wake wa Habil na Qabil kuwa je, hao ni katika hurilaini wa peponi au sio? Nikamjibu kuwa masuala haya yanaju- likana kwa kunakili sio kwa kiakili, na nukuu yake haitumiwi isipokuwa ikiwa ni ya Qur’an au Hadith mutawatir wala hakuna nukuu yoyote ya hilo. Kwa hiyo inatupasa tunyamaze yale aliyoyanyamazia Mwenyezi Mungu.

Akasema: Itakuwaje? Je, tuseme tumeshindwa tutakapoulizwa? Nikamwambia: Je, tunatakikana tujue kila kitu kwa vile sisi tuna vilemba vya ushekhe?

Wala usitembee katika Ardhi kwa maringo. Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala kufikia urefu wa milima.

Mjinga anaweza kuwa na kiburi na kujifanya mkubwa anapomiliki ghururi za dunia; kama vile jaha na mali. Lakini likimtokea jambo la ghafla katika mambo yaliyojificha, basi anakuwa mnyonge na kudangana hana la kufanya. Mwenye akili ni yule anayejijua, akafikiri na kuzingatia.

Kauli yake Mwenyezi Mungu‘Wala usitembee katika Ardhi kwa maringo’ ni kukataza kiburi na kuamrisha kunyenyekea. Kauli yake:‘Hakika wewe huwezi kuipasua ardhi wala kufikia urefu wa milima’ ni fumbo la kushindwa mtu na kwamba yeye ni mdhaifu wa kufikia anayoyataka; kama alivyo mdhaifu wa mwili wake kuweza kufikilia jabali kwa urefu na kuweza kuipasua ardhi kwa wayo wake.

Hayo yote ubaya wake ni wenye kuchukiza mbele ya Mola wako.

Hayo ni kuishiria yaliyotangulia kutajwa katika yale aliyoyaamrisha Mwenyezi Mungu na kuyakataza. Makusudio ya ubaya wake ni yale aliyoyakataza hasa. Maana ni kuwa vitu vyote hivi ambavyo amevikataza Mwenyezi Mungu anavichukia, na mwenye kuvifanya ni mwenye kughadhibikiwa na Mwenyezi Mungu na mwenye kustahili adhabu.

Hayo ni katika hekima alizokupa wahyi Mola wako.

Hayo ni ishara ya maamrisho na makatazo yaliyotanglia kutajwa. Hekima ni kukiweka kitu mahali pake; Hakuna mwenye shaka kwamba hukumu zake zote Mwenyezi Mungu ziko mahali pake. Na kwamba mwenye kuichukua atakuwa ameichukua kwa haki, heri na uadilifu.

Usimfanye mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, usije ukalaumiwa uliyetupwa.

Imetangulia Aya hii pamoja na tafsiri yake katika Sura hii Aya 22. Mwenyezi Mungu ameanzia na kukataza shirki na akamalizia nako, kwa sababu tawhid ndio kianzio na lengo la Uislamu, dini ya Mwenyezi Mungu iliyo ya haki. Kwa kuwa hukumu zote zinatoka kwake, basi hakuna halali ila aliyoiamrisha wala haramu ila aliyoiharamisha.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

أَفَأَصْفَاكُمْ رَبُّكُم بِالْبَنِينَ وَاتَّخَذَ مِنَ الْمَلَائِكَةِ إِنَاثًا إِنَّكُمْ لَتَقُولُونَ قَوْلًا عَظِيمًا ﴿٤٠﴾

40. Je, mola wenu amewachagulia waototo wa kiume na yeye akajichukulia watoto wa kike katika Malaika? Hakika nyinyi mnasema kauli kubwa.

وَلَقَدْ صَرَّفْنَا فِي هَـٰذَا الْقُرْآنِ لِيَذَّكَّرُوا وَمَا يَزِيدُهُمْ إِلَّا نُفُورًا ﴿٤١﴾

41. Hakika tumekwishabainisha katika Qur’an ili wapate kukumbuka, lakini haiwazidishii isipokuwa kuwa mbali.

قُل لَّوْ كَانَ مَعَهُ آلِهَةٌ كَمَا يَقُولُونَ إِذًا لَّابْتَغَوْا إِلَىٰ ذِي الْعَرْشِ سَبِيلًا ﴿٤٢﴾

42. Sema lau kama wangelikuwa pamoja naye miungu mingine, kama wasemavyo, basi wangelitafuta njia ya kumfikia Mwenye Arshi.

سُبْحَانَهُ وَتَعَالَىٰ عَمَّا يَقُولُونَ عُلُوًّا كَبِيرًا ﴿٤٣﴾

43. Ametakasika na ametukuka juu kabisa na hayo wanayoyasema.

تُسَبِّحُ لَهُ السَّمَاوَاتُ السَّبْعُ وَالْأَرْضُ وَمَن فِيهِنَّ وَإِن مِّن شَيْءٍ إِلَّا يُسَبِّحُ بِحَمْدِهِ وَلَـٰكِن لَّا تَفْقَهُونَ تَسْبِيحَهُمْ إِنَّهُ كَانَ حَلِيمًا غَفُورًا ﴿٤٤﴾

44. Zinamtakasa zote mbingu saba na ardhi na vilivyomo ndani yake. Na hapana kila kitu ila kinamtakasa kwa sifa zake, lakini nyinyi hamfahamu kutakasa kwake. Hakika Yeye ni Mpole Mwenye maghufira.

JE, MOLA WENU AMEWACHAGULIA WAVULANA?

Aya 40 – 44

MAANA

Je, mola wenu amewachagulia waototo wa kiume na yeye akajichukulia watoto wa kike katika Malaika?

Qur’an inazingatiwa kuwa ni hoja isiyokuwa na ubishi, katika yote iliyoyasema na kuyasajili; Aya hii inaelezea vile washirikina walivyokuwa wakiitakidi kwamba Mwenyezi Mungu ana mabinti katika aina ya malaika. Vile vile walikuwa wakiitakidi kwamba mtoto wa kiume ni bora kuliko wa kike; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: “Na mmoja wao akibashiriwa msichana uso wake unasawijika naye amejaa chuki.” Juz; 14 (16:58).

Kwa hiyo basi wao walijinasibishia ubora na uduni wakamnasibishia Mungu. Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawatahayariza na ujinga huu, akawaambia:

Hakika nyinyi mnasema kauli kubwa , kwa sababu Yeye Mwenyezi Mungu hana mshirika wala aliyeshabihiana naye. Lau angelikuwa na mtoto angelikuwa huyo mtoto wake atamrithi na kushabihiana naye, lau angelikuwa na mzazi angelikuwa mzazi wake ni mshirika wake kwenye utukufu na enzi, bali huyo mzazi angelikuwa ni mtukufu zaidi yake, kwa sababu yeye ndiyo sababu ya kupatikana kwake.

Pengine mantiki ya wajahili ni kwamba siri iliyowafanya wamnasibishie Mungu mabinti na wao watoto wa kiume, ni kuwa Mwenyezi Mungu hahofii ufukara kwa sababu ya kuwa na watoto wengi wala aibu ya kuwa na mabinti.

Hakika tumekwishabainisha katika Qur’an ili wapate kukumbuka, lakini haiwazidishii isipokuwa kuwa mbali.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameweka dalili na hoja za kupatikana kwake na umoja wake na akazifafanua kwa kupiga mifano na mifumo mbalimbali ili wafahamu na waelewe, lakini wao wameng’ang’ania njozi na kuiga. Wakazidi inadi na kuwa mbali.

Razi anasema: “Hakika Mwenyezi Mungu amekithirisha kutaja dalili katika Qur’an; kwa sababu Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alitaka washirikina wazifahamu na kuziamini; Hii inafahamisha kwamba Yeye, aliyetukuka, anafanya vitendo vyake kwa hekima na inafahamisha kuwa Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alitaka imani kwa kila mmoja ni sawa aamini au asiamini.”

Kauli hii ya Razi inapingana na aliyoyaelezea mara kwa mara kwamba vitendo vya Mwenyezi Mungu havina sababu ya malengo, na kwamba Yeye ndiye aliyetaka kafiri awe kafiri; kama ilivyo kwa madhehebu ya Ashaira. Lakini Mwenyezi Mungu anataka kuinusuru haki na kuidhihirisha hata kwenye ulimi wa yule anayeipinga bila ya kujitambua.

Sema lau kama wangelikuwa pamoja naye miungu mingine, kama wasemavyo, basi wangelitafuta njia ya kumfikia Mwenye Arshi.

Watu wa tafsiri wametaja maana mbili za Aya hizi:

Kwanza: Ikisemwa kuwa kuna miungu wengine pamoja na Mwenyezi Mungu basi msiwahesabu hao waungu kuwa ni nyota, binadadamu, mawe au vitu vingine. Kwa sababu hivi vyote vimeumbwa na Mwenyezi Mungu, vinamwabudu na kujikurubisha kwake.

Basi mambo yakiwa hivi ni juu yenu enyi washirikiakina kumwabudu Mwenyezi Mungu; kama ambavyo vile manvyoviabudu vinamwabudu Yeye tu.

Maana au tafsiri ya pili ambayo ina nguvu zaidi ni: Lau kungelikuwa na waungu wengine, basi wangelipingana na Mwenyezi Mungu na wangelitafuta nji ya kufikia kwenye madaraka. Hakuna mwenye shaka kwamba kupingana na kuzozana viongozi kunaleta vurugu na ghasia; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

لَوْ كَانَ فِيهِمَا آلِهَةٌ إِلَّا اللَّـهُ لَفَسَدَتَا فَسُبْحَانَ اللَّـهِ رَبِّ الْعَرْشِ عَمَّا يَصِفُونَ ﴿٢٢﴾

“Lau wangelikuwemo humo miungu wengine isipokuwa Mwenyezi Mungu, bila shaka hizo mbingu na ardhi zingelifisidika,” (21:22).

Tumefafanua hayo katika kufasiri, Juz; 5 (5:48).

Ametakasika na ametukuka juu kabisa na hayo wanayoyasema.

Amejivua Mwenyezi Mungu (s.w.t) na kauli ya madhalimu na washiriki- na kwamba Yeye ana washirika na watoto.

KILA KITU KINAMTAKASA (KINAMSABBIH)

Zinamtakasa zote mbingu saba na ardhi na vilivyomo ndani yake. Na hapana kila kitu ila kinamtakasa kwa sifa zake.

Ndio! Kila kitu kinamtaksa na kumsifu Mwenyezi Mungu Mtukufu, hilo halina shaka. Tasbih au utakasho wa kitu unatofautiana na kitu kingine kulingana na kilivyo hicho kitu.

Mwenye akili anamtakasa na kumsifu Mwenyezi Mungu kwa ulimi wake, vitu vingine vinamtakasa kwa lugha ya hali. Kwa maneno mengine vinamtakasa na kumsifu kwa jinsi vilivyopatikana umbile lake na mpangilio wake, kuwa yuko mpangiliaji mzuri aliyevifanya viwe hivyo vilivyo; sawa na unavyojulisha mchoro mzuri kuwa mchoraji ni hodari aliye bingwa.

Lugha ya hali ina nguvu na ni fasaha zaidi kuliko lugha ya maneno. Kwa sababu ya maneno inahitajia dalili, lakini ya hali hiyo yenyewe ni dalili inayopeleka kwenye elimu na yakini; Yamekwisha tangulia maelezo ya hayo katika kufasiri Juz; 13 (13:15).

Lakini nyinyi hamfahamu kutakasa kwake; Hakika Yeye ni Mpole Mwenye maghufira.

Hawawezi kufahamu walahidi na washirikina tasbihi zao, kwa sababu ya kujiweka mbali kwao na utukufu wa Mwenyezi Mungu katika kuumba kwake au kwa sababu ya kuzembea kuchunguza na kutambua siri na maajabu ya ulimwengu.

Anasema Ibn Arabi katika kitabu Alfutuhatil-makkiyya Juz; 4: “Mwenyezi Mungu ana ishara aina kwa aina: Kuna zile zinazotambulika kwa kutumia akili, zinazotambulika kwa usikizi na zile zinazotambulika kwa kuona. Kwa hiyo ni juu ya kila mtu kutumia vyombo hivi kuweza kujua ishara za Mwenyezi Mungu ambazo amezitaja katika kitabu chake. Akishajua na kuamini kwazo na akatenda kwa mujibu wake basi atakuwa ni miongoni mwa watu wa Qur’an na watu mahususi wa Mwenyezi Mungu.”

Kisha akaendelea kusema Ibn Arabi: “Chukua kupatikana kote kuwa ni Kitabu kinachotamka haki” Hii ni kama kauli ya mmoja wa wataalamu wa elimu ya Mwenyezi Mungu: “Hakika Mwenyezi Mungu ana vitabu viwili: kimoja kinatamka kwa lugha ya makala, hicho ni Qur’an na kingine kinatamka kwa lugha ya hali nacho ni ulimwengu.”

وَإِذَا قَرَأْتَ الْقُرْآنَ جَعَلْنَا بَيْنَكَ وَبَيْنَ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ حِجَابًا مَّسْتُورًا ﴿٤٥﴾

45. Na unaposoma Qur’an tunaweka baina yako na ya wale wasioamini Akhera pazia linalowafunika.

وَجَعَلْنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ أَكِنَّةً أَن يَفْقَهُوهُ وَفِي آذَانِهِمْ وَقْرًا وَإِذَا ذَكَرْتَ رَبَّكَ فِي الْقُرْآنِ وَحْدَهُ وَلَّوْا عَلَىٰ أَدْبَارِهِمْ نُفُورًا ﴿٤٦﴾

46. Na tunaweka vifuniko juu ya nyoyo zao wasije wakaifahamu na tunaweka kwenye masikio yao uziwi, Na unapomtaja Mola wako peke yake katika Qur’an, basi wao hugeuka nyuma wakaenda zao.

نَّحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَسْتَمِعُونَ بِهِ إِذْ يَسْتَمِعُونَ إِلَيْكَ وَإِذْ هُمْ نَجْوَىٰ إِذْ يَقُولُ الظَّالِمُونَ إِن تَتَّبِعُونَ إِلَّا رَجُلًا مَّسْحُورًا ﴿٤٧﴾

47. Sisi tunajua vyema kabisa sababu wanayosikilizia wanapokusikiliza, na wanaponon’gona, wanaposema hao madhalimu: nyinyi hamfuati isipokuwa mtu aliyerogwa.

انظُرْ كَيْفَ ضَرَبُوا لَكَ الْأَمْثَالَ فَضَلُّوا فَلَا يَسْتَطِيعُونَ سَبِيلًا ﴿٤٨﴾

48. Tazama vipi wanavyokupigia mfano, Basi wamepotea, kwa hiyo hawawezi kuipata njia.

UNAPOSOMA QUR’AN

Aya 45 – 48

MAANA

Na unaposoma Qur’an tunaweka baina yako na ya wale wasioamini Akhera pazia linalowafunika.

Kuna kauli nyingi katika kufasir Aya hii; Yenye nguvu zaidi ni ile isemayo kuwa jamaa katika washirikina walikuwa – Muhammad anaposoma Qur’an – wanajaribu kumzuia kwa kumuudhi, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamwambia endelea kusoma Qur’an na kutoa mwito wa Mwenyezi Mungu wala usichoke.

Na tunaweka vifuniko juu ya nyoyo zao wasije wakaifahamu na tunaweka kwenye masikio yao uziwi.

Hili ni fumbo la inadi ya washirikina. Ama kunasibisha vifuniko na uziwi kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t), tumekuzungumzia kwa ufafanuzi katika kufasiri Juz; 7 (6:25). Hiyo ni mfano wa Aya hii kinukuu na kimaana.

Na unapomtaja Mola wako peke yake katika Qur’an, basi wao hugeuka nyuma wakaenda zao.

Walikuwa washirikina, inaposomwa Qur’an, wanapomsikia Mtume wa Mwenyezi Mungu akisema: Lailaha illallah (hapana Mungu isipokuwa Mwenyezi Mungu) basi wanaachana naye na kwenda zao huku wakisema:

أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ﴿٥﴾ وَانطَلَقَ الْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ امْشُوا وَاصْبِرُوا عَلَىٰ آلِهَتِكُمْ ﴿٦﴾

“Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu. Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nenedeni zenu na dumuni na miungu yenu.” (38: 5-6).

Sio siri kuwa upinzani huu ni kwa vile tu tamko la tawhid linakusanya msingi wa kusema: “Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu ni yule mwenye takua zaidi” (49: 13). Sio utabaka na ubaguzi.

Sisi tunajua vyema kabisa sababu wanayosikilizia wanapokusikiliza, na wanaponon’gona, wanaposema hao madhalimu: Nyinyi hamfuati isipokuwa mtu aliyerogwa.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusema: ‘na tunaweka kwenye masikio yao uziwi’ sasa anasema: Sisi tunajua vizuri kwamba wewe wakati unaposoma Qur’an washirikina hawakusikilizi kwa moyo safi, bali wanakusikiliza kwa kwa roho ya chuki, inadi na kiburi, kisha wanaambiana na pia kuwaambia wengine, kuwa Muhammad ni mchawi ameingiwa na jini linalozungumza hekima na ufasaha huu kwenye ulimi wake; itakuwaje azungumze hivi naye hajui kusoma wala kuandika, tena hana hazina ya dhahabu au fedha wala hana shamba la mitende na mizabibu.

Hii ndio fikra yao ya kitabaka, kwamba mwenye mali tu ndio anayeweza kuwa na cheo kitukufu kiwe cha dini au cha kawaida: “Na walisema: kwa nini hii Qur’an haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii” (43:31) Ama akili, ukweli na uaminfu kwao hauna maana.

Tazama vipi wanavyokupigia mfano.

Walizidi mno kwa Muhammad(s.a.w.w) kwa vile kuwa ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na kutamka maneno ya Mwenyezi Mungu; mara wakamwita mwendawazimu, mara mchawi, mara kuhani na mara nyingine wakamwita mshairi.

Muhammad ambaye ametumwa kukamilisha tabia njema, amekuwa mchawi na mwendawazimu? Kwa nini amekuwa hivyo? Kwa vile yeye anatamka haki na kuitolea mwito na wala hakukubaliana na matamanio ya wabatilifu na wafisadi. Zaidi ya hayo hana farasi wala mali.

Kwa ufupi ni kwamba watu wa matamanio na matakwa, hisia zao ziko upande mmoja tu, matamanio na masilahi yao binafsi. Hawasikii wala hawaoni isipokuwa kwayo tu; kiasi cha kuhalalisha yote kwenye hawa zao na matamanio. Kwa hali hii ndio tunapata tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana kifuniko” Juz, 1 (2:7) na tafsiri ya kila Aya iliyo na maana haya katika maneno ya Mtukufu Aliyetukuka.

Basi wamepotea, kwa hiyo hawawezi kuipata njia, ya kuwakadhibisha wenye haki, isipokuwa uzushi, upotevu, ulaghaii, uadui, njama na rushwa.

وَقَالُوا أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا وَرُفَاتًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ خَلْقًا جَدِيدًا ﴿٤٩﴾

49. Na wakasema: je, tutakapokuwa mifupa na mapande yaliyosagika, je tutafufuliwa kuwa viumbe wapya?

قُلْ كُونُوا حِجَارَةً أَوْ حَدِيدًا ﴿٥٠﴾

50. Sema: kuweni hata mawe au chuma.

أَوْ خَلْقًا مِّمَّا يَكْبُرُ فِي صُدُورِكُمْ فَسَيَقُولُونَ مَن يُعِيدُنَا قُلِ الَّذِي فَطَرَكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ فَسَيُنْغِضُونَ إِلَيْكَ رُءُوسَهُمْ وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هُوَ قُلْ عَسَىٰ أَن يَكُونَ قَرِيبًا ﴿٥١﴾

51. Au umbo lolote mnaloliona kubwa katika vifua vyenu, Watasema: Ni nani atakayeturudisha tena? Sema: Ni huyo aliyewaumba mara ya kwanza. Watakutikisia vichwa vyao Na watasema: lini hayo? Sema: asaa yakawa karibu.

يَوْمَ يَدْعُوكُمْ فَتَسْتَجِيبُونَ بِحَمْدِهِ وَتَظُنُّونَ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا ﴿٥٢﴾

52. Siku atakayowaita nanyi mkamwitikia kwa kumsifu. Na mkadhani kuwa hamkukaa ila muda mchache tu.

TUTAKAPOKUWA MIFUPA NA MAPANDE YALIYOSAGIKA

Aya 49 – 52

MAANA

Na wakasema: je, tutakapokuwa mifupa na mapande yaliyosagika, je tutafufuliwa kuwa viumbe wapya?

Hii ndio hoja ya mwenye kutilia shaka ufufuo, tangu zamani hadi sasa, kuwa itakuwaje mtu arudi kuwa hai baada ya kuwa vumbi linalotifuka?

Jibu : Yule aliyeweza kuumba kitu na kukifanya kiwepo baada ya kuwa hakipo, basi ni wazi kuwa anaweza kukikusanya baada ya kutawanyika. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameitaja shaka hii na jawabu lake kwenye Aya kadhaa; miongoni mwazo ni ile iliyo katika sura Yasin:

وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِيَ خَلْقَهُ قَالَ مَن يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ ﴿٧٨﴾ قُلْ يُحْيِيهَا الَّذِي أَنشَأَهَا أَوَّلَ مَرَّةٍ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ ﴿٧٩﴾

“Akasema: ni nani huyo atakayeihuisha mifupa nayo imekwisha mung’unyika? Sema: atahiuisha huyohuyo aliyeiumba mara ya kwanza na Yeye ni mjuzi wa kila kuumba” (36: 78 – 79).

Tumelifafanua suala hili katika Juz; 13 (13:5).

Sema: kuweni hata mawe na chuma au umbo lolote mnaloliona kubwa katika vifua vyenu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawaambia wale wanaokanusha ufufuo kuwa hata kama mtakuwa mawe au chuma au kitu kikubwa zaidi ya hivyo tutawaumba tu kuwa watu hai.

Anayeweza kuumba kutokana na chuma au jiwe au kitu kigumu zaidi ya hivyo, basi ni muweza zaidi wa kumrudishia uhai yule aliyempa uhai mwanzo. Kwa sababu kuvikusanya vitu baada ya kutawanyika ni rahisi zaidi kuliko kuvianzisha upya.

Kwa ufupi ni kuwa kumfufua mtu baada ya kufa ni wepesi zaidi kuliko kukifanya chuma kuwa mtu, Anayeweza hivi basi hashindwi kufanya vile.

Watasema: Ni nani atakayeturudisha tena kwenye uhaai baada ya kuwa mavumbi yanayopeperuka. Jibu la swali hili ni:

Sema: Ni huyo aliyewaumba mara ya kwanza.

Mwenye kurudisha ndiye yule aliyeanza; Kuanza na kurudisha ni kumoja tu; bali kurudisha ni wepesi zaidi, kwa sababu ni kurudisha ilivyokuwa. Tunasema hivi, kama mfano tu, tukijua kuwa Mwenyezi Mungu anaumba vichache na vingi na pia vidogo na vikubwa kwa neno.

كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

“Kuwa! Na kikawa” (36:82).

Watakutikisia vichwa vyao kwa stihzai na kukadhibishaNa watasema: lini hayo? Makusudio ya swali hili ni kuona kuwa haiwezekani.

Sema: asaa yakawa karibu. Makusudio ya karibu hapa ni kuhakikika na kutokea, kwani ‘Kila lijalo liko karibu.’

Siku atakyowaita nanyi mkamwitikia kwa kumsifu.

Makusudio ya Siku ni siku ya Ufufuo, kuitwa ni kupuziwa parapanda, kuitikia ni fumbo la kutoka kwao makaburini na kumsifu ni kutii na kufuata:

وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ ﴿٥١﴾

“Na itapulizwa parapanda mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao” (36:51).

Na mkadhani kuwa hamkukaa ila muda mchache tu.

Watu watakapotoka makaburini watadhani kuwa wao hawakukaa duniani isipokuwa siku moja au sehemu ya siku:

قَالَ كَمْ لَبِثْتُمْ فِي الْأَرْضِ عَدَدَ سِنِينَ ﴿١١٢﴾ قَالُوا لَبِثْنَا يَوْمًا أَوْ بَعْضَ يَوْمٍ فَاسْأَلِ الْعَادِّينَ ﴿١١٣﴾

“Atasema: mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka? Watasema tulikaa siku moja au sehemu ya siku,” (23:112- 113).

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

إِنَّ هَـٰذَا الْقُرْآنَ يَهْدِي لِلَّتِي هِيَ أَقْوَمُ وَيُبَشِّرُ الْمُؤْمِنِينَ الَّذِينَ يَعْمَلُونَ الصَّالِحَاتِ أَنَّ لَهُمْ أَجْرًا كَبِيرًا ﴿٩﴾

9. Hakika hii Qur’an inaongoza kwenye yaliyonyooka kabisa na inawabashiria waumini ambao wanatenda mema kwamba watapata malipo makubwa.

وَأَنَّ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ أَعْتَدْنَا لَهُمْ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿١٠﴾

10. Na kwamba wale wasioamini Akhera tumewaandalia adhabu chungu.

وَيَدْعُ الْإِنسَانُ بِالشَّرِّ دُعَاءَهُ بِالْخَيْرِ وَكَانَ الْإِنسَانُ عَجُولًا ﴿١١﴾

11. Na mtu huomba shari kama vile aombavyo kheri. Na mtu amekuwa ni mwenye pupa.

وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ وَالنَّهَارَ آيَتَيْنِ فَمَحَوْنَا آيَةَ اللَّيْلِ وَجَعَلْنَا آيَةَ النَّهَارِ مُبْصِرَةً لِّتَبْتَغُوا فَضْلًا مِّن رَّبِّكُمْ وَلِتَعْلَمُوا عَدَدَ السِّنِينَ وَالْحِسَابَ وَكُلَّ شَيْءٍ فَصَّلْنَاهُ تَفْصِيلًا ﴿١٢﴾

12. Na tumeufanya usiku na mchana kuwa ni ishara mbili, Tena tukaifuta ishara ya usiku. Na tukaifanya ishara ya mchana ni ya kuangazia ili mtafute fadhila itokayo kwa Mola wenu na mpate kujua idadi ya miaka na hisabu, Na kila kitu tumekifafanua wazi wazi.

QUR’ANI INAONGOZA KWENYE YALIYONYOOKA

Aya 9 -12

MAANA

Hakik hii Qur’an inaongoza kwenye yaliyonyooka kabisa na inawabashiria waumini ambao wanatenda mema kwamba watapata malipo makubwa.

Yaliyonyooka kabisa ni mila au njia ambayo imenyooka. Neno hili lina maana ya kuenea masilahi zaidi kwenye kila kitu, wakati wowote, mahali popote na kwa mtu yeyote.

Aya hii ni madai yaliowazi yaliyosajiliwa na Qur’an anayoyaamini kila Mwislamu - kwamba Uislamu ndio dini bora zaidi ya dini zote. Dalili ya usahihi wa madai haya na ukweli wake ni Qur’an kutokana na itikadi yake, sharia yake na mafunzo yake mengine kuongezea sera ya mwenye ujumbe huo, Muhammad Bin Abdillah(s.a.w.w) ambaye ameijaza ardhi elimu, imani, wema na uadilifu baada ya kuwa na ujahili, kufuru na ufisadi.

Maulama wamethibitisha hakika hii na wakatunga mamia ya vitabu katika kufasiri maneno ya Mwenyezi Mungu na hadithi za Mtume wa Mwenyezi Mungu na sera yake, itikadi sharia na maadili ya kiislamu ambayo yamethibitika katika nyanja mbalimbali, Tumetaja baadhi katika juzuu zilizotangulia za tafsiri hii. Tutaonyesha baadhi ya mifano ya misingi hiyo kama ifuatavyo:

1. Uislamu Ni Dini Ya Maumbile

Kila msingi katika misingi ya Uislamu, kila tawi katika sharia yake na kila hukumu katika hukumu zake, imejikita kwenye umbile safi: “Ndilo umbile alilowaumbia watu. Hapana mabadiliko katika uumbaji wa Mwenyezi Mungu, Hiyo ndiyo dini iliyonyooka, lakini watu wengi hawajui.”

Aya inaonyesha wazi kwamba Uislamu unaitikia matakwa ya maumbile ya binadamu na kunyoosha mikono yake kwa kila jipya lenye faida; ni sawa liwe limekuja kutoka mashariki au magharibi. Amesema Imam Ali(a.s) : “Hekima ni adimu kwa Mumin. Chukua hekima hata kama ni kutoka kwa wanafiki.” Akasema tena: “Angalia kauli usiangalie aliyesema” Kuna hadith nyingi zenye maana haya.

2. Imani Ya Uislamu Kwenye Elimu

Uislamu unaamini elimu na kusimamia kwake maisha katika pande zote. Mwenyezi Mungu anasema katika sura hii tuliyo nayo Aya 36: “Wala usifuatilie ambalo huna ujuzi nalo.” Amesema tena:

قُلْ هَاتُوا بُرْهَانَكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿١١١﴾

Sema: Leteni dalili zenu kama nyinyi ni wasema kweli.” Juz.1 (2:111)

فَاسْأَلُوا أَهْلَ الذِّكْرِ إِن كُنتُمْ لَا تَعْلَمُونَ ﴿٤٣﴾

“Basi waulizeni wenye ukumbusho ikiwa nyinyi hamjui” Juz,14(16:43).

Mtume(s.a.w.w) amesema: “Wino wa mulama utapimwa na damu ya mashahidi siku ya kiyama.” Imam Ali naye amesema: “Elimu ni dini, inafuatwa dini kwayo.”

Maana ya kuamini elimu ni kuamini maendeleo na kufanya mambo kwa ajili ya maisha yaliyo bora na ya ukamilifu.

3. Kuiachia Huru Akili

Uislamu unatoa mwito wa kufikiri, kutaamali na kuchunguza maumbile haya kwa kutafiti kuweza kujua siri zake, faida zake na manufaa yake. Vilevile kujua mafungamano ya mtu na muumba wake. Pia Uislamu unatoa mwito kwa dini, elimu na falsafa, kutilia umuhimu mambo yanayoonekana na maarifa ya hisia; jambo ambalo wamekuwa nalo waislamu tangu mwanzo, kisha likaenda kwa wazungu. Ikawa msingi wa elimu ya majaribio uko kwao:

أَوَلَمْ يَنظُرُوا فِي مَلَكُوتِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا خَلَقَ اللَّـهُ مِن شَيْءٍ ﴿١٨٥﴾

Je, hawatazami ufalme wa mbingu na ardhi na alivyoviumba Mwenyezi Mungu. Juz. (7:185).

4. Uhuru Wa Kufikiri

Uislamu unatoa uhuru wa kusema na kufikiri, kiasi ambacho Mwenyezi Mungu aliwaruhusu watumishi wake, Malaika, wamuhoji huku wakisema:

قَالُوا أَتَجْعَلُ فِيهَا مَن يُفْسِدُ فِيهَا وَيَسْفِكُ الدِّمَاءَ ﴿٣٠﴾

Utaweka humo watakaofanya uharibifu humo na kumwaga damu? Juz; 1 (2:30).

Pia aliruhusu Ibrahim(a.s) amjadili kuhusu watu wa Lut:

فَلَمَّا ذَهَبَ عَنْ إِبْرَاهِيمَ الرَّوْعُ وَجَاءَتْهُ الْبُشْرَىٰ يُجَادِلُنَا فِي قَوْمِ لُوطٍ ﴿٧٤﴾

“Basi hofu ilipomwondokea Ibrahim na ikawa ile bishara imemfikia, alianza kujadiliana nasi juu ya watu wa Lut.” Juz; 12 (11:74).

Bali alimruhusu hata Iblis kutoa hoja mbele yake:

قَالَ أَنَا خَيْرٌ مِّنْهُ خَلَقْتَنِي مِن نَّارٍ وَخَلَقْتَهُ مِن طِينٍ ﴿١٢﴾

“Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye, umeniumba kwa moto naye umemuumba kwa udongo” Juz, 8 (7:12).

5. Wigo Mpana

Mafunzo yote ya kiislam yanaenea kwa wote; hayahusiki na mtu wala kikundi wala hayabagui:

إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ﴿١٣﴾

“Hakika mtukufu wenu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mwenye takua zaidi” (49:13)

Hadith inasema: “Nyote mmetokana na Adam, na Adama ametokana na mchanga”.

6. Jihadi

Uislamu umelazimisha jihadi ya hali na mali dhidi ya dhulma na ufisadi kwa kila mwenye uwezo. Mwenyezi Mungu anasema:

“Nendeni mkiwa wepesi na wazito, na mpiganie jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu, Hilo ni kheri kwenu mkiwa mnamjua.” Juz; 10 (9:41).

Imam Ali(a.s) anasema:“Wallah! Lau si Mwenyezi Mungu kuchukua ahadi kwa Maulama kwamba wasiafiki kuvimbiwa kwa dhalim wala kufa njaa kwa aliyedhulumiwa, ningelitupilia mbali kamba yake na ningelim- nywesha wa mwisho wake kwa glasi ya wa mwanzo wake na dunia yenu hii kwangu ingelikuwa ya upuzi kuliko kamasi za mbuzi.”

Ustadh Muhammad Sa’d Jalal, katika Jarida la Al-katib la Misr anasema, ninamnukuu: “Makusudio ya Imam (Ali) ni kuwa lau si ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa maulama kutokubali tofauti mbaya baina ya watu katika kula; ambapo wengine wanavimbiwa kwa kula ili wengine wawe na njaa, basi asingeli- fanya juhudi ya kuitaka haki yake ya ukhalifa ambayo ndiyo nyenzo ya kuthibitika uadilifu wa kuzuia tofauti iliyotajwa. Kwa hiyo jihadi yake haikuwa kwa ajili ya kutamani utawala na manufaa ya nafsi yake; isipokuwa ilikuwa ni kwa ajili ya kutekeleza hukumu ya uadilifu wa kijamii katika kugawa utuajiri kwa waislamu wote kwa namna ambayo hatakuweko mwenye kuvimbiwa kwa kula wala mwenye utapia mlo.”

7. Mali Ni Ya Mwenyezi Mungu

Vyote vilivyomo ulimwenguni ni mali ya Mwenyezi Mungu na binadamu ni wakala wa vile vilivyomo mikononi mwake. Kwa hiyo ni juu yake kutotumia ila kwa idhini na amri ya yule mwenyewe anayemuwakilisha: “Ni vyake vilivomo mbinguni na vilivyo katika ardhi na viliomo baina yao na viliyomo chini ya ardhi” (20:6) (57:7) Angalia Juz; 4 (180).

8. Uislamu Na Maisha

Uislamu unalenga binadamu aishi katika uwiano unaokwenda sambamba na nidhamu ya ulimwengu na mahitaji ya maisha:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّـهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ ﴿٢٤﴾

Enyi mlioamini! Mwitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapowaita kwenye lile litakalowapa uhai, juz.9 (8:24).

Angalia maelezo yake huko, Hivi karibuni kimetoka kitabu kipya cha mwandishi Wilfred Smith, Anasema katika kitabu hicho: “Waislamu wana uwezo, kulingana na dini yao, wa kuleta maendeleo pamoja na mahitaji ya sayansi na kuchangia katika kutengeneza jamii itakayoongozwa na maendeleo ya kijamii kwa uadilifu na heshima.”

Na kwamba wale wasioamini Akhera tumewaandalia adhabu chungu.

Hakuna tofauti baina ya anayemkufuru Mwenyezi Mungu na anayekufuru siku ya mwisho. Kwa sababu kukataa kurudishwa viumbe baada ya kufa, maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu hawezi hilo; na hivyo hasa ni kufuru.

Imam Ali(a.s) anasema:“Namstaajabu yule anayemtilia shaka Mwenyezi Mungu naye anaona umbile lake; na namstaajabu yule anayekanusha ufufuo wa Akhera naye anaona ufufuo wa kwanza.”

Na mtu huomba shari kama vile aombavyo kheri.

Katika maisha haya kuna huzuni na furaha, tamu na chungu, Hakuna kimo- jawapo kinachodumu. Ni kuanzia hapa ndio ikasemwa: ‘siku ni mbili: kuna siku yako na siku ya kwako.’ Lakini baadhi ya watu wanapopatwa na jambo baya lolote wanalalamika na mishipa kuwasimama, wakidhani kuwa wako kwenye matatizo makubwa yasiyotatulika. Kwa hiyo wanajiombea shari, kama wanavyojiombea heri. Na hii ni aina ya ujinga na upumbavu. Lau wangelingojea siku kidogo tu, matatizo yangeliondoka pamoja na siku zinavyokwenda

Na mtu amekuwa ni mwenye pupa katika kujiombea shari bila ya kuwa na subira na uvumilivu.

Makusudio ya mtu hapa ni baadhi sio watu wote. Kwenye Nahjul-balagha kuna msemo huu: “Msilifanyie haraka lile linalokuwa kwa kungojewa, Wala msione kuchelewa litakalokuja kesho, Ni mangapi yaliyopatikana yakidhaniwa hayatapatikana?”

Na tumeufanya usiku na mchana kuwa ni ishara mbili.

Ni dalili mbili za kuweko Mwenyezi Mungu; Kwa sababu zinafuatana kulingana na kanuni thabiti na nidhamu ya kudumu kwenye maelfu ya miaka; hakuna hata mwaka mmoja uliotufautiana na mwingine. Yote hayo, na mengine mfano wake, ni dalili mkataa ya kuweko mpangiliaji mzuri na mhandisi mwenye ujuzi wa hali ya juu sana.

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawapa mwito wataalamu na wenye fikra kumwamini Yeye kupitia kufikiria vizuri na kuzingatia maumbile ya mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake, jinsi vilivyopangiliwa kwa utaalamu wa hali ya juu; kama vile kufuatana usiku na mchana na mengineyo yanayoonekana ulimwenguni.

Ama wale watu wa kawaida anawalingania kwa kukumbuka neema zake:

فَلْيَعْبُدُوا رَبَّ هَـٰذَا الْبَيْتِ ﴿٣﴾ الَّذِي أَطْعَمَهُم مِّن جُوعٍ وَآمَنَهُم مِّنْ خَوْفٍ ﴿٤﴾

Basi na wamwabudu Mola wa nyumba hii, ambaye amewaliwasha kutokana na njaa na akawasalimisha na hofu (106: 3-4).

Tunasema hivi huku tukijua kuwa miito yote miwili (kufikiria maumbile na neema) inaweza kuwa pamoja.

Tena tukaifuta ishara ya usiku.

Kusema ishara ya usiku ni kubainisha; maana yake ni hiyo hiyo ishara ambayo ni usiku.

Unaweza kuuliza kuwa : dhahiri ya neno kufuta ni kuondoka kabisa na inajulikana usiku upo kwa hisia na kuona?

Makusudio ya kufuta hapa ni kuondoka athari ya kiutendaji. Kwa sababu watu wanatulia kinyume na mchana ambapo watu wanafanya kazi na kuhangaika huku na huko. Kwa hiyo linalofutwa hapa ni ule utulivu. Mwenyezi Mungu anasema:

وَجَعَلَ اللَّيْلَ سَكَنًا ﴿٩٦﴾

Ameufanya usiku kuwa mapumziko na utulivu, Juz. 6 (6:96)

وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا ﴿١٠﴾ وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا ﴿١١﴾

Na tukaufanya usiku kuwa ni sitara na mchana kuwa ni wakati wa maisha (78:10–11).

Na tukaifanya ishara ya mchana ni ya kuangazia kila kitu kionekane ili mtafute fadhila itokayo kwa Mola wenu.

Usiku ni wa utulivu na kupumzika na mchana ni wa kutafuta riziki kwa mkono na kutoka jasho, sio kwa kughushi, hila, hiyana na kuwa kibaraka ili mtafute fadhila kutoka kwa ofisi za mabalozi na za upelelezi. Fadhila ya Mwenyezi Mungu inatolewa kwa kila mwenye kuitaka; nayo ni bora na ni yenye kubaki, tena ni safi na twahara.

“Ewe Mola tujaalie tutosheke na halali yako tusiwe na haja na haramu yako na tutosheke na twa yako tusiwe na haja na maasi yako na fadhila yako tusiwe na haja ya kumuomba asiyekuwa Wewe”

Na mpate kujua idadi ya miaka na hisabu.

Tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi katika Juz; 10 (9:36).

Na kila kitu tumekifafanua waziwazi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametubainishia halali na haramu, akatuwekea hoja, dalili na mawaidha. Mwema ni yule aliyejikomboa na matamanio na akajikwamua na hawa ya nafsi yake.

وَكُلَّ إِنسَانٍ أَلْزَمْنَاهُ طَائِرَهُ فِي عُنُقِهِ وَنُخْرِجُ لَهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ كِتَابًا يَلْقَاهُ مَنشُورًا ﴿١٣﴾

13. Na kila mtu tumemfungia ndege wake shingoni mwake, Na siku ya Kiyama tutamtolea kitabu atakachokikuta kimekunjuliwa.

اقْرَأْ كِتَابَكَ كَفَىٰ بِنَفْسِكَ الْيَوْمَ عَلَيْكَ حَسِيبًا ﴿١٤﴾

14. Soma kitabu chako! Nafsi yako leo inakutosha kukuhisabu.

مَّنِ اهْتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهْتَدِي لِنَفْسِهِ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيْهَا وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ وَمَا كُنَّا مُعَذِّبِينَ حَتَّىٰ نَبْعَثَ رَسُولًا ﴿١٥﴾

15. Anayeongoka hakika anaongoka kwa faida ya nafsi yake tu, na anayepotea anapotea kwa hasara ya nafsi yake tu. Wala mbebaji hatabeba mzigo wa mwingine, Wala sisi hatuadhibu mpaka tupeleke Mtume.

NDEGE SHINGONI

Aya 13 – 15

LUGHA

Makusudio ya ndege hapa ni matendo ya mtu ya kheri na shari. Waarabu walikuwa wakiona ni bahati njema ndege anayekuja upande wa kuume kwa sababu mtu anaweza kumpiga na wakiona ni kisirani ndege akitokea upande wa kushoto, kwa sababu hawezi kumpiga.

Ndio likaazimwa neno ndege kwa matendo ya heri na shari [6] .1 Shingoni mwake ni fumbo la kuwa nayo; kama vile amefunga koja au mkufu.

MAANA

Aya hizi tatu zinatofautiana kimatamshi, lakini zinashabihiana kimaana, Kauli yake Mwenyezi Mungu: Na kila mtu tumemfungia ndege wake shingoni mwake ni fumbo la kuwa mtu peke yake ndiye mwenye jukumu la matendo yake. Na kauli yake:

Na siku ya Kiyama tutamtolea kitabu atakachokikuta kimekunjuliwa.

Maana yake ni kuwa mtu kesho hataweza kuficha kitu chochote katika mambo aliyoyatenda:

يَوْمَ تَجِدُ كُلُّ نَفْسٍ مَّا عَمِلَتْ مِنْ خَيْرٍ مُّحْضَرًا وَمَا عَمِلَتْ مِن سُوءٍ تَوَدُّ لَوْ أَنَّ بَيْنَهَا وَبَيْنَهُ أَمَدًا بَعِيدًا ﴿٣٠﴾

“Siku ambayo kila nafsi itakuta kheri iliyoitenda imehudhurishwa Na iliyoyatenda katika uovu, itapenda lau kungekuwa na masafa marefu baina ya uovu huo na yeye.” Juz. 3(3:30)

Kwa maelezo zaidi angalia huko.

Pia kauli yake Mwenyezi Mungu: Soma kitabu chako! Nafsi yako leo inakutosha kukuhisabu.

Hakuna haja ya shahidi wala mhasibu kesho; Kwa sababu mtu mwenyewe atajishuhudia na atajihisabu. Twabrasi anasema: “Atakuwa anajihisabu mwenyewe kwa sababu Siku ya Kiyama atakapoyaona matendo yake yote yameandikwa na kuona malipo yake pia yameandikwa kwa uadilifu, hayakupunguwa wala kuzidishiwa adhabu hata kidogo, atakiri na kukubali yeye mwenyewe, wala hatakuwa na hoja wala upinzani, Itawadhihirikia watakaofufuliwa kuwa hakuna dhulma.

Anasema Hasan:“Ewe mwanadamu! Amekufanyia insafu yule aliyekufanya ujihisabu mwenyewe.”

Anayeongoka hakika anaongoka kwa faida ya nafsi yake tu, na anayepotea anapotea kwa hasara ya nafsi yake tu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (6: 104) na Juz. 11 (10: 108).

Wala mbebaji hatabeba mzigo wa mwingine. Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (6:164), Wala sisi hatuadhibu mpaka tupeleke Mtume.

Angalia Juz. 2 (2:159) kifungu cha ‘Ubaya wa adhabu bila ya ubainifu’.

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TANO

وَإِذَا أَرَدْنَا أَن نُّهْلِكَ قَرْيَةً أَمَرْنَا مُتْرَفِيهَا فَفَسَقُوا فِيهَا فَحَقَّ عَلَيْهَا الْقَوْلُ فَدَمَّرْنَاهَا تَدْمِيرًا ﴿١٦﴾

16. Tunapotaka kuangamiza mji, huwaamrisha wapenda anasa wake, lakini hufanya maovu humo; basi hapo kauli huhakikika katika mji huo na tukauangamiza maangamizo makubwa.

وَكَمْ أَهْلَكْنَا مِنَ الْقُرُونِ مِن بَعْدِ نُوحٍ وَكَفَىٰ بِرَبِّكَ بِذُنُوبِ عِبَادِهِ خَبِيرًا بَصِيرًا ﴿١٧﴾

17. Na karne ngapi tumeziangamiza baada ya Nuh? Na Mola wako anatosha kuwa ni mwenye habari na mwenye kuona dhambi za waja wake.

مَّن كَانَ يُرِيدُ الْعَاجِلَةَ عَجَّلْنَا لَهُ فِيهَا مَا نَشَاءُ لِمَن نُّرِيدُ ثُمَّ جَعَلْنَا لَهُ جَهَنَّمَ يَصْلَاهَا مَذْمُومًا مَّدْحُورًا ﴿١٨﴾

18. Anayetaka ya upesi upesi (dunia) tutamharakishia humo tunayoyataka kwa tunayemtaka; kisha tunamwekea Jahannam; ataiingia hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa mwenye kufurushwa.

وَمَنْ أَرَادَ الْآخِرَةَ وَسَعَىٰ لَهَا سَعْيَهَا وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَأُولَـٰئِكَ كَانَ سَعْيُهُم مَّشْكُورًا ﴿١٩﴾

19. Na mwenye kutaka ya mwisho (Akhera) na akayahangaikia kwa mahangaikio yake huku akiwa ni mumin, basi hao mahangaikio yao yatakuwa ni yenye kushukuriwa.

كُلًّا نُّمِدُّ هَـٰؤُلَاءِ وَهَـٰؤُلَاءِ مِنْ عَطَاءِ رَبِّكَ وَمَا كَانَ عَطَاءُ رَبِّكَ مَحْظُورًا ﴿٢٠﴾

20. Wote hao tunawasaidia, hawa na hao, katika atia za Mola wako; na atia za Mola wako hazizuiliki.

انظُرْ كَيْفَ فَضَّلْنَا بَعْضَهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ وَلَلْآخِرَةُ أَكْبَرُ دَرَجَاتٍ وَأَكْبَرُ تَفْضِيلًا ﴿٢١﴾

21. Angalia jinsi tulivyowafad- hilisha baadhi yao kuliko wengine. Na Akhera ni yenye daraja kubwa zaidi na fadhila kubwa zaidi.

TUNAWAAMRISHA WAPENDA ANASA WAKE

Aya 16 -21

LUGHA

Neno ‘mutraf,’ambalo tumelifasiri kwa neno wapenda anasa, lina maana ya wale ambao wanastarehe watakavyo.

MAANA

Nilipofikia kufasiri Aya hii (tunawaamrisha watanasi wake), nilikumbuka swali nililoulizwa na mmoja wa mahatibu wa Iraq akisema: Kwa nini unawatukana wapenda anasa kwenye vitabu vyako? Nami nikamuuliza: Kwanini wewe unawatetea? Je, wewe ni mmoja wao? Au ni kwa vile wao ni mawalii wa neema zako? Basi akarudi nyuma na swali lake na akaomba msamaha. Hili limenifanya niieleze Aya hii kwa mfumo ufuatao:

1. Mbali ya neno ‘utajiri,’ neno ‘wapenda anasa’ pamoja na mnyumbuliko wake limekuja mara nane katika Qur’an; kama ilivyoelezwa katika Murshid, Katika Nahjulbalagha neno hili limeelezwa mara nyingi. Halikutajwa neno wapenda anasa ila pamoja na shutuma.

2. Watu wa Lugha wamesema: Neno Taraf katika mnyumbuliko wake linatumika hivi: Amejitanaasi mtu, kwa maana ya kujineemesha. Ameitanasi mali, kwa maana ya kuifuja. Pia neno hilo linakuwa kwa maana ya uovu na kiburi, Haya ndio maelezo yake kilugha. Ama sifa yake iliyotajwa katika Qur’an na kwengineko ni: Kughafilika na Mwenyezi Mungu, kuwafanyia uovu waja wa Mwenyezi Mungu, kuifanyia kiburi amri ya Mwenyezi Mungu na kuwapiga vita mawalii wa Mwenyezi Mungu. Vile vile kujifaharisha kwa wingi, kujiona, unyanyapaa na mengine mengi ya shutuma; isipokuwa yule aliyehurumiwa na Mungu na akajihurumia mwenyewe.

3.Tunapotaka kuangamiza mji, huwaamrisha wapenda anasa wake, lakini hufanya maovu humo; basi hapo kauli huakikika katika mji huo na tukauangamiza maangamizo makubwa.

Linaoamriwa ni uadilifu na twaa; yaani tunawamrisha uadilifu na utiifu. Wafasiri wametaja njia nne katika maana ya Aya hii. Yenye nguvu zaidi ni ile inayosema kuwa Mwenyezi Mungu amelitumia neno wapenda anasa kwa watu wote wa mji, katika mtindo wa kutumia sehemu kwa maana ya yote.

Mfano huu katika maneno ya waarabu unatumika sana, ikiwa hiyo sehemu ni muhimu zaidi; kama jicho katika mwili, wamelitumia kwa mstari wa mbele katika jeshi; kwa sababu jicho ni kiungo muhimu katika mwili [7] 1

Kwa kuwa wapenda raha ni wepesi zaidi na wajasiri wa kufanya maasi kuliko wengine, ndio ikafaa kulitumia neno hilo kwa watu wote wa mji; kama linavyotumika jicho kwa mtu.

Kwa hiyo basi maana ya Aya yanakuwa kwamba Mwenyezi Mungu hawaangamizi watu wa mji ila wakistahili hilo baada ya kuwekewa hoja kwa kutumwa mtume awaamrishe kheri, kuwakataza uovu, kuwahadharisha na uhalifu na maasi. Wakifanya uovu na kutoka kwenye utiifu, basi linahakika neno la adhabu juu yao na Mwenyezi Mungu huwateremshia maangamizi.

Ni kweli maana haya yanawafikiana na matamshi ya Aya, wala hayakataliwi na akili, lakini sisi tutaifasiri kwa njia njingine; kama ifuatavyo: Jamii yoyote iliyo na wapenda anasa, kwa maana tuliyoyataja, basi ni jamii inayoishi kwenye nidhmu ya ufisadi na dhulma. Kwani kuweko kwao ni sawa kabisa na kuweko saratani katika mwili.

Wa kulaumiwa kwanza kabisa kwa kupatikana wafisadi ni jamii yenyewe; kwa vile haikusimama kidete kuwapinga au angalu kutowaunga mkono; bali wanawabatiza majina ya waheshimiwa, kuwatukuza, kuwapa kura na kuwapa uongozi.

Hapa ndio inakuwa jamii yenyewe ni mshiriki kamili wa wapenda anasa na wafisadi katika makosa na madhambi yao yote na wanastahiki maangamivu; sawa na wapenda anasa.

Kuna Hadith isemayo:“Mwenye kuridhia dhulma ni kama mwenye kuifanya” “Mwenye kuinyamazia haki ni kama shetani bubu” Ikiwa mambo ni hayo itakuwaje kwa yule mwenye kuiridhia batili?

Anasema Seyyid Afghani: “Ewe mkulima unayechimba ardhi kwa jembe lako kwa nini usilitumie jembe hilo kuuchimba moyo wa anayekufanya mtumwa?” Tazama Juz; 13 (13:11).

Kwa hakika maangamizi yako aina nyingi; Yanaweza kuwa tufani tetemeko la ardhi, vimondo n.k. Vile vile yanaweza kuwa kwa udhalili na kusalitiwa shari.

Aina hii ni mbaya na ya kufedhesha zaidi. Wameadhibiwa nayo umma wa Muhammad(s.a.w.w) pale walipoacha jihadi, wakawafumbia jicho wafisadi na washari na wakaukubali udhalili na unyonge.

Imam Ali(a.s) anasema:“Hakika kwenye utawala wa kiislamu kuna hifadhi ya mambo yenu, basi upeni utiifu wenu…; Wallahi ni lazima mfanye hivyo au Mwenyezi Mungu atauondoa kwenu utawala wa kiislamu kisha usirudi kwenu kabisa mpaka mambo yarudie kwa wengine wasiokuwa nyinyi.”

Yaani tukiutii Uislamu tutaishi kwenye ngome imara tukiwa na hadhi na heshima; vinginevyo utawala utahama kwenda kwa maadui zetu, kisha usirudi kwetu; Kila ninaposoma onyo hili basi hujisikia natetema.

Na karne ngapi tumeziangamiza baada ya Nuh?

Makusudio ya karne hapa ni watu. Hii ni hadhari na ahadi kwa wale wanaomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w ) kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni muweza wa kuwafanya kama alivyowafanya wale waliowakadhibisha Mitume waliokuwa kwenye karne zilizopita; kama vile Ad na Thamud:

أَفَأَمِنُوا مَكْرَ اللَّـهِ فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

“Je, wamejiaminisha na hila ya Mwenyezi Mungu? Hawaaminishi hila ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara.” Juz; 9 (7:99).

Imam Ali(a.s) amesema:“Hakika radhi ya Mwenyezi Mungu kwa waliobaki ni moja na uchukivu wa Mwenyezi Mungu kwa waliobaki ni mmoja. Jueni kuwa Yeye hataridhia chochote alichokichukia kwa waliokuwa kabla yenu wala hatachukia chochote alichowaridhia waliokuwa kabla yenu”

Na Mola wako anatosha kuwa ni mwenye habari na mwenye kuona dhambi za waja wake.

Kwa hiyo atamwadhibu anavyostahiki, Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alisema kumwambia Abu dharr:“Hakika mumin anaziona dhambi ni jiwe kubwa analohofia kumwangukia na kwamba kafiri anaona dhambi zake ni kama nzi tu anayepita puani mwake.”

Anayetaka ya upesi upesi (dunia) tutamharakishia humo tunayoyataka kwa tunayemtaka.

Sio kuwa kila alitakalo mtu anapewa na Mungu, Kwani sisi huwa tunataka mambo mengi na hayawi. Ispokuwa makusudio ya Aya ni kuwa mwenye kufanya kwa ajili ya dunia tu, bila ya kuamini chochote isipokuwa manufaa yake, basi atapata matunda ya kazi yake na juhudi yake kwa matakwa ya Mwenyezi Mungu, kwani mja hawezi kufikia jambo lolote kama Mungu akikataa, hata kama atafanya kazi usiku na mchana. Hakika Mwenyezi Mungu hatupi tunayoyataka ila kwa kutaka kwake. Hayo ndio makusudio ya ‘tunayoyataka kwa tunayemtaka’

Kisha tunamwekea Jahannam; ataiingia hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa mwenye kufurushwa.

Kwa vile yeye anaamini masilahi yake tu na haoni umuhimu wowote isipokuwa nafsi yake, wala hafanyi lolote isipokuwa kwa ajili yake.

Na mwenye kutaka ya mwisho (Akhera) na akayahangaikia kwa mahangaikio yake huku akiwa ni mumin, basi hao mahangaikio yao yatakuwa ni yenye kushukuriwa.

Makusidio ya kuyahangaikia kwa mahangaikio yake ni kutaka kheri na kuifanya na kuiamini si kwa chochote isipokuwa kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na kheri. Anayefanya hivi ndiye anayestahiki daraja na cheo mbele ya Mwenyezi Mungu na mbele ya watu.

Ama anayefanya kwa ajili ya faida na biashara basi yake ni Jahannam. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasemama: “Ambaye Hijra yake (kuhama kwake) ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi Hijra yake ni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na ambaye hijra yake ni kwa ajili ya kuipata dunia au mwanamke amuoe, basi Hijra yake ni kwa lile alilololi- hajiria.

Muhtasari wa yote haya ni kuwa Uislamu ni njia inayomuelekeza mtu kufanya kheri na kuiacha shari hiyo yenyewe. Kwa hiyo itakuwa ni lazima kusema ukweli kwa kuwa ni lazima kufanya hivyo na ni lazima kujiepusha na uongo kwa kuwa ni lazima kujiepusha. Mtume(s.a.w.w) ameutolea ibara mwelekeo huu kwa kusema:“Hakika nimetumwa kutimiza tabia njema.” Ilivyo hasa ni kuwa tabia njema haiwi ila ikiwa imetakata na kila uchafu.

Wote hao tunawasaidia, hawa na hao,

Hiyo ni ishara ya makundi yote mawili: wale wanaotenda kwa ajili ya dunia na wale wanaotenda kwa ajili ya akhera.

Katika atia za Mola wako; na atia za Mola wako hazizuiliki.

Atia (vipawa) za Mwenyezi Mungu kwa mtu zinaanzia tangu kuumbwa kwake na kuweko kwake ambako hakupatikani ila kwake tu; kisha sababu za kubakia kwake na kukua kwake. Atia hizi zinamhusu mwema na muovu. Ama atia zake katika akhera zitawahusu wema wanaomcha Mungu tu.

Angalia jinsi tulivyowafadhilisha baadhi yao kuliko wengine.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hawagawanyi watu kwenye tabaka, wala kuto- fautiana katika haki za kibinadamu kwa mtu binafsi au makundi. Vipi iwe hivyo na hali yeye ndiye aliyesema:

إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ﴿١٣﴾

“Hakika mtukufu wenu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mwenye takua zaidi katika nyinyi” (49:13).

Kwa hiyo basi kuzidiana watu katika dunia, katika isiyokuwa haki ya kibinadamu, inafaa; kama vile afya, umri, riziki kupitia kufanya kazi, kurithi au njia nyingine yoyote aliyoihalalisha Mungu. Lakini utajiri unaokuja kwa ulanguzi, hila na uporaji unatokana na shetani, wala haifai kuunasibisha na Mwenyezi Mungu.

Na akhera ni yenye daraja kubwa zaidi na fadhila kubwa zaidi.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja kuwa watu wanatofautiana katika dunia, sasa anasema kuwa huko Akhera pia itakuwako tofauti, lakini huko tofauti ni kubwa sana. Kwani sifa zinazowatofautisha hapa ni utajiri na ufukara, elimu na ujinga, maradhi na siha na umri mrefu na mfupi; kisha wote wanaishia kwenye mauti kwa usawa, hata wema na waovu. Ama sifa watakazotofautiana huko Akhera, ni kuungua katika moto na kuwa kwenye neema na furaha. Wapi na wapi tofauti hii na ile.

لَّا تَجْعَلْ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَقْعُدَ مَذْمُومًا مَّخْذُولًا ﴿٢٢﴾

22. Usimfanye mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, usije ukabaki ni mwenye kukalaumiwa uliyetupwa.

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ وَبِالْوَالِدَيْنِ إِحْسَانًا إِمَّا يَبْلُغَنَّ عِندَكَ الْكِبَرَ أَحَدُهُمَا أَوْ كِلَاهُمَا فَلَا تَقُل لَّهُمَا أُفٍّ وَلَا تَنْهَرْهُمَا وَقُل لَّهُمَا قَوْلًا كَرِيمًا ﴿٢٣﴾

23. Na Mola wako amepitisha kuwa msimwabudu yoyote ila Yeye tu na kuwatendea wema wazazi wawili. Mmoja wao akifikia uzee naye yuko kwako au wote wawili, basi usiwaambie Ah! Wala usiwakemee, Na sema nao kwa msemo wa heshima.

وَاخْفِضْ لَهُمَا جَنَاحَ الذُّلِّ مِنَ الرَّحْمَةِ وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا ﴿٢٤﴾

24. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma na useme: Mola wangu! Warehemu kama walivyonilea utotoni.

رَّبُّكُمْ أَعْلَمُ بِمَا فِي نُفُوسِكُمْ إِن تَكُونُوا صَالِحِينَ فَإِنَّهُ كَانَ لِلْأَوَّابِينَ غَفُورًا ﴿٢٥﴾

25. Mola wenu ni Mjuzi zaidi wa yaliyo katika nafsi zenu, ikiwa nyinyi mtakuwa wema. Hakika Yeye ni Mwenye kughufiria wanaorejea kwake.

USIWAMBIE AH!

Aya 22 – 25

MAANA

Usimfanye mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu, usije ukabaki ni mwenye kulaumiwa uliyetupwa.

Maneno haya anaambiwa kila mtu, sio Mtume(s.a.w.w) kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘mmoja wao akifikia uzee naye yuko kwako au wote wawili; Na inajulikana kuwa Mtume alikuwa yatima.

Na Mola wako amepitisha kuwa msimwabudu yoyote ila Yeye tu na kuwatendea wema wazazi wawili. Mmoja wao akifikia uzee naye yuko kwako au wote wawili, basi usiwaambie Ah! Wala usiwakemee, Na sema nao kwa msemo wa heshima. Na uwainamishie bawa la unyenyekevu kwa kuwaonea huruma na useme: Mola wangu! Warehemu kama walivyonilea utotoni.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekutanisha shukrani ya wazazi wawili na shukrani yake na akawajibisha kuwatendea wema. Kuna Hadith isemayo: “Kuna mtu mmoja alikwenda kwa Mtume(s.a.w.w) akimtaka idhini ya kupigana jihadi pamoja naye. Akamuuliza: je, Wazazi wako wako hai? Akasema: Ndio. Akasema mtume: basi fanya jihad kwao.

Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘kama walivyonilea utotoni,’ ni ishara ya kuwa wao walijitolea nafsi zao kwa ajili yake, wakakesha usiku ili yeye alale, wakawa na njaa ili ashibe yeye na wakawa uchi ili yeye avae. Na hili ni deni shingoni mwake, ni wajibu alilipe atakapokuwa na nguvu na wao kuwa dhaifu, na kuwachukulia kwenye uzee wao sawa na wao walivyomchukulia alipokuwa mdogo, na wao wamemzidi kwa kumtangulia.

Imam Zaynul-abidin(a.s) anasema akiwaombea Mungu wazazi wake: “Ewe Mola wangu! Ni wapi na wapi urefu wa shughuli yao ya kunilea mimi? Ni wapi na wapi shida ya tabu yao ya kunilinda mimi? Ni wapi na wapi kujinyima kwao kwa jili ya kunifurahisha mimi? Ni mbali kwa mbali kabisa na jinsi walivyotekeleza haki yao kwangu; ni mbali kwambali yote hayo na jinsi ninavyowafanyia! Wala mimi sijatekeleza wadhifa wa kuwahudumia.”

Kila mmoja kati ya baba na mama anajitolea kwa nafsi yake na pumzi zake zote kwa ajili ya mtoto, kisha hataki malipo wala shukrani yoyote. Analotamani ni kuwa mtoto wake awe ni mtu mwenye kutajika. Nimepata mtihani wa kuwa baba, lakini wazazi wangu hawakuupata mtihani huo, kwa sababu nilikuwa yatima wa baba na mama.

Ninasema nimepatwa na mtihani huo, kwa sababu mimi sioni raha yoyote katika maisha haya isipokuwa raha ya mwanangu wa kike na kiume. Tabasamu moja tu ya mmoja wao kwangu ni sawa na dunia na vilivyomo ndani yake na hasononeki yoyote kati yao ila huwa ninahisi kuna mkono unatoa roho yangu iliyo mbavuni mwangu.

Mola wenu ni Mjuzi zaidi wa yaliyo katika nafsi zenu, ikiwa nyinyi mtakuwa wema. Hakika Yeye ni Mwenye kughufiria wanaorejea kwake.

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua maazimio, kama anavyojua kauli na vitendo na kumlipa kila mmoja kulingana na nia yake. Mwenye kufanya uovu kisha akatubia sawasawa, basi Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, mwenye kurehemu.

Hiii ni tahadhari kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa yule mwenye kuwaudhi wazazi wake na akawa anawaona ni mzigo kwake, kama ambavyo pia ni hadhari ya kuacha ikhlasi katika kauli na vitendo.


3

4

5

6

7

8

9