TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA42%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11905 / Pakua: 4655
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea. Hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka kwa lugha ya kiswahili hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasayansi kama kina Enstein, wasanii kama Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146), Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama. Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu Jabal amil 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa.” Kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

قَالَ أَلَمْ أَقُل لَّكَ إِنَّكَ لَن تَسْتَطِيعَ مَعِيَ صَبْرًا ﴿٧٥﴾

75. Akasema: Sikukuambia kuwa wewe hutaweza kuvumilia kuwa pamoja nami?

قَالَ إِن سَأَلْتُكَ عَن شَيْءٍ بَعْدَهَا فَلَا تُصَاحِبْنِي قَدْ بَلَغْتَ مِن لَّدُنِّي عُذْرًا ﴿٧٦﴾

76. Akasema: Nikikuuliza tena kitu baada ya haya usifuatane nami kwani umekwishapata udhuru kwangu

فَانطَلَقَا حَتَّىٰ إِذَا أَتَيَا أَهْلَ قَرْيَةٍ اسْتَطْعَمَا أَهْلَهَا فَأَبَوْا أَن يُضَيِّفُوهُمَا فَوَجَدَا فِيهَا جِدَارًا يُرِيدُ أَن يَنقَضَّ فَأَقَامَهُ قَالَ لَوْ شِئْتَ لَاتَّخَذْتَ عَلَيْهِ أَجْرًا ﴿٧٧﴾

77. Basi wawili hao wakaondoka, mpaka wakawafikia watu wa mji mmoja, wakawaomba watu wake wawape chakula, nao wakakataa kuwakaribisha. Hapo wakakuta ukuta unataka kuanguka akausimamisha, Akasema (Musa): Ungelitaka ungelichukua ujira kwa haya.

قَالَ هَـٰذَا فِرَاقُ بَيْنِي وَبَيْنِكَ سَأُنَبِّئُكَ بِتَأْوِيلِ مَا لَمْ تَسْتَطِع عَّلَيْهِ صَبْرًا ﴿٧٨﴾

78. Akasema: “Huku ndio kufarikiana baina yangu na wewe. Nitakueleza taawili ya yale uliyokuwa huwezi kuyavumilia.

أَمَّا السَّفِينَةُ فَكَانَتْ لِمَسَاكِينَ يَعْمَلُونَ فِي الْبَحْرِ فَأَرَدتُّ أَنْ أَعِيبَهَا وَكَانَ وَرَاءَهُم مَّلِكٌ يَأْخُذُ كُلَّ سَفِينَةٍ غَصْبًا ﴿٧٩﴾

79. Ama ile jahazi iikuwa ni ya maskini wafanyao kazi baharini. Nilitaka kuitia kasoro, kwani nyuma yao kulikuwa na mfalme anayenyang’anya majahazi yote.

وَأَمَّا الْغُلَامُ فَكَانَ أَبَوَاهُ مُؤْمِنَيْنِ فَخَشِينَا أَن يُرْهِقَهُمَا طُغْيَانًا وَكُفْرًا ﴿٨٠﴾

80. Ama yule kijana wazazi wake walikuwa waumini, tukahofia asiwahangaishe kwa uasi na kufuru.

فَأَرَدْنَا أَن يُبْدِلَهُمَا رَبُّهُمَا خَيْرًا مِّنْهُ زَكَاةً وَأَقْرَبَ رُحْمًا ﴿٨١﴾

81. Basi tulitaka Mola wao awabadilishie aliye bora zaidi kuliko huyo kwa kutakasika na aliye karibu zaidi kwa huruma.

وَأَمَّا الْجِدَارُ فَكَانَ لِغُلَامَيْنِ يَتِيمَيْنِ فِي الْمَدِينَةِ وَكَانَ تَحْتَهُ كَنزٌ لَّهُمَا وَكَانَ أَبُوهُمَا صَالِحًا فَأَرَادَ رَبُّكَ أَن يَبْلُغَا أَشُدَّهُمَا وَيَسْتَخْرِجَا كَنزَهُمَا رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ وَمَا فَعَلْتُهُ عَنْ أَمْرِي ذَٰلِكَ تَأْوِيلُ مَا لَمْ تَسْطِع عَّلَيْهِ صَبْرًا ﴿٨٢﴾

82. Na ama ukuta ulikuwa ni wa vijana wawili mayatima kule mjini, na chini yake ilikuwako hazina yao, na baba yao alikuwa ni mtu mwema. Basi Mola wako alitaka wafikie kukomaa na wajitolee hazina yao. Nirehema itokayo kwa Mola wako. Hayo sikuyatenda kwa amri yangu, Hiyo ndiyo tafsiri ya ambayo hukaweza kuyavu milia.

HUWEZI KUVUMILIA

Aya 75 – 82

MAANA

Juzuu ya 15, imeishia na Aya ya kuuliwa kijana na mshangao wa Musa kwa tendo hilo. Kwenye Aya hii swahibu wa Musa anamkumbusha kuhusu walivyoahidiana:

Akasema: “Sikukuambia kuwa wewe hutaweza kuvumilia kuwa pamoja nami?

Anamkumbusha tena lile sharti na Musa naye anaomba tena msamaha akasema:Nikikuuliza tena kitu baada ya haya usifuatane nami.

Hapo mwanzo yule mtu alimuwekea sharti Musa, hivi sasa Musa anajiwekea mwenyewe sharti kwamba asisuhubiane naye tena kama atamuuliza, na waumini wanalazimiana na masharti yao; sikwambii tena mitume.

Kwani umekwishapata udhuru kwangu; Sababu zote zitakuwa zimekwisha.

Basi wawili hao wakaondoka, mpaka wakawafikia watu wa mji mmoja.

Huu ni ushahidi wa tatu wa kuwa ni wachache wanaovumilia. Ushahidi wa kwanza na wa pili umekwishapita kwenye Juzuu ya 15. Inasemekana mji huo walioufikia ni Antioch. Katika riwaya iliyopokewa kwa Imam Jafar As-Swadiq, inasema kuwa ni Nazarethi[1] .

Wakawaomba watu wake wawape chakula, lakini nao wakakataa kuwakaribisha.

Wafasiri wanasema kuwa Mwenyezi Mungu amesema walikataa kuwakaribisha, badala ya walikataa kuwapa chakula, kwa vile watu wa mji ule walikuwa wabaya sana. Kwani hakuna anayemkataa mgeni ila mtu mbaya, hasa ikiwa mgeni ni wa mbali.

Hapo wakakuta ukuta unataka kuanguka, akausimamisha.

Hapo, ni hapo kwenye mji. Aliyeusimamisha, ni yule mja mwema. Kutaka kuanguka, ni kukurubia kuanguka. Maana ni kuwa Musa na mwenzake walikuta ukuta unakaribia kuanguka, yule mwenzake akautengeneza bila ya malipo yoyote.

Ndipo Musa akastaajabu na akasema: Ungelitaka ungelichukua ujira kwa haya.

Unafanya kazi ya bure tu kwa watu waliokataa hata kutukaribisha tukiwa na shida. Kutoboa jahazi na kuua kijana ni mifano miwili yenye dhahiri ya ubaya na kusimamisha ukuta ni kinyume cha mifano hiyo miwili.

Akasema: Huku ndio kufarikiana baina yangu na wewe. Nitakueleza taawili ya yale uliyokuwa huwezi kuyavumilia.

Mja mwema alitoa sharti kwa Musa la kutoulizwa, Musa akakubali, lakini pamoja na hayo akauliza, Alipokumbushwa akaomba msamaha, Tena akauliza baada ya msamaha. Alipokumbushwa mara ya pili akajiwekea sharti yeye mwenyewe la kutofuatana naye kama atauliza tena. Lakini bado akauliza, ingawaje alikuwa na hamu sana ya kufuatana naye.

Musa hana lawama yoyote katika yote aliyoyauliza; Kwa sababu nafsi yake inaweza kuvumilia mambo ya kheri na mazuri, lakini yale anayoyaona ni mabaya, hakuweza wala hataweza kuvumilia; hata kama hilo litapelekea kuvunja masharti na maelewano. Ni kipimo gani cha masharti kinachoweza kupimwa kuacha mema na kukataza mabaya.

Imani sahihi haiwezi kuzuiwa na kitu chochote, si msukumo wa nafsi wala mengineyo. Hakuna kitu kigumu zaidi kuliko imani sahihi; na atakayeshindwa na kitu chochote katika hivyo basi hana imani sahihi; hata akiswali, kufunga na kuhiji Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu.

Huku ndio kufarikiana baina yangu na wewe , ushike njia yako nami nishike yangu, Hivyo ndivyo alivyomwambia Musa. Lakini kabla ya kutengana, yule mja mwema alimwambia Musa hekima ya yale aliyoyapinga, kama ifuatavyo:

Ama lile jahazi lilikuwa ni la maskini wafanyao kazi baharini. Nilitaka kulitia kasoro, kwani nyuma yao kulikuwa na mfalme anayenyang’anya majahazi yote.

Mwenye akili anavumilia madhara kwa ajili ya kuondoa madhara makubwa; kama anavyosema mshairi: “Nimevumilia nusu shari kihofia shari yote.”

Kuanzia hapa ndio mafaqihi wakaafikiana kuwa dhara kubwa inakingwa na dhara hafifu na yakiingiliana maovu mawili litaangaliwa lile lenye madhara zaidi kwa lile lililo na machache. Kutokana na kawaida hii wametoa hukumu nyingi, kama vile kuruhusiwa kukata kiungo ikiwa kitamletea mtu maangamizi.

Ama yule kijana wazazi wake walikuwa waumini, tukahofia asiwahangaishe kwa uasi na kufuru. Basi tulitaka Mola wao awabadilishie aliye bora zaidi kuliko huyo kwa kutakasika na aliye karibu zaidi kwa huruma.

Imepokewa riwaya kutoka kwa Imam Jafar As-Swadiq(a.s) kuwa huyo kijana aliuawa katika rika la balehe na alikuwa kafiri. Akifanya juhudi kuwaingiza wazazi wake kwenye ukafiri, sawa na wanavyofanya baadhi ya vijana wa kileo.

Tumewahi kuwona maulama wengi wa kidini waliokuwa ni tegemeo kubwa la watu, lakini mara tu walipobalehe vijana wao, wakabomoa yote waliyojenga baba zao kwa muda mrefu.

Kuna kauli mashuhuri ya Imam Ali(a.s) :“Zubeir aliendelea kuwa nasi mpaka alipokuwa na kijana wake Abdullah”

Ahmad Amin wa Misr, katika kitabu Hayati (maisha yangu), anasema: “Hivi sasa mimi na uzee wangu ninakubali kila ambalo nilikuwa nikilikataa na huwa ninaacha misimamo niliyokuwa nayo kwa sababu ya watu na mazungumzo yao na wingi wa watoto.”

• Udogo sikutaka Hawa nafsi yangu

• Zama zikakatika kawa na mvi zangu

• Hawa zikanishika kinyume matakwa yangu

• Laitani ngezalika nao ukubwa wangu

• Udogo wa marika kupinga nafsi yangu

Na ama ukuta ulikuwa ni wa vijana wawili mayatima kule mjini, na chini yake ilikuwako hazina yao, na baba yao alikuwa ni mtu mwema. Basi Mola wako alitaka wafikie kukomaa na wajitolee hazina yao. Ni rehema itokayo kwa Mola wako. Hayo sikuyatenda kwa amri yangu, Hiyo ndiyo tafsiri ya ambayo hukaweza kuyavumilia.”

Kwa ufupi ni kuwa ukuta ulikua wa watoto wawili na chini yake kulikuwa na dafina yao. Mwenyezi Mungu akataka kuilinda mali hiyo isipotee, kwa kubakia ukuta, mpaka wawe wakubwa au wawe na akili, kisha wajitolee mali yao wao wenyewe; na mzazi wao alikuwa mtu mwema “Na wema wa mtu mumini, Mwenyezi Mungu huufanya kwa mtoto wake na mtoto wa mtoto wake.”

Funzo la kisa hiki ni kwamba mtu asijione ni yeye tu na asifanye haraka kujiamulia jambo kwa kuangalia upande mmoja, bali ni lazima aangalie pande zote kwa undani na kulinganisha kisha aangalie ulio bora zaidi; kwani masilahi huwa yanasigana na madhara.

Hakuna jambo lolote la manufaa isipokuwa lina baadhi ya madhara ndani yake; kama ambavyo hakuna jambo lolote ila lina baadhi ya manufaa. Siku zote mazingatio ni kwa lililo na wingi.

وَيَسْأَلُونَكَ عَن ذِي الْقَرْنَيْنِ قُلْ سَأَتْلُو عَلَيْكُم مِّنْهُ ذِكْرًا ﴿٨٣﴾

83. Na wanakuuliza kuhusu Dhul-qarnain, Waambie nitawasimulia baadhi ya habari zake.

إِنَّا مَكَّنَّا لَهُ فِي الْأَرْضِ وَآتَيْنَاهُ مِن كُلِّ شَيْءٍ سَبَبًا ﴿٨٤﴾

84. Hakika sisi tulimmakinisha katika ardhi na tukampa sababu ya kila kitu.

فَأَتْبَعَ سَبَبًا ﴿٨٥﴾

85. Basi akafuata sababu.

حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ مَغْرِبَ الشَّمْسِ وَجَدَهَا تَغْرُبُ فِي عَيْنٍ حَمِئَةٍ وَوَجَدَ عِندَهَا قَوْمًا قُلْنَا يَا ذَا الْقَرْنَيْنِ إِمَّا أَن تُعَذِّبَ وَإِمَّا أَن تَتَّخِذَ فِيهِمْ حُسْنًا ﴿٨٦﴾

86. Hata alipofika machweo ya jua aliona linatua kwenye chemchem yenye matope meusi, Na hapo akawakuta watu, tukasema: Ewe Dhul-qarnain! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.

قَالَ أَمَّا مَن ظَلَمَ فَسَوْفَ نُعَذِّبُهُ ثُمَّ يُرَدُّ إِلَىٰ رَبِّهِ فَيُعَذِّبُهُ عَذَابًا نُّكْرًا ﴿٨٧﴾

87. Akasema: “Ama aliyedhulumu, basi tutamwadhibu adhabu na kisha atarudishwa kwa Mola wake amuadhibu adhabu isiyojulikana.

وَأَمَّا مَنْ آمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَلَهُ جَزَاءً الْحُسْنَىٰ وَسَنَقُولُ لَهُ مِنْ أَمْرِنَا يُسْرًا ﴿٨٨﴾

88. Na ama mwenye kuamini na akatenda mema tutamlipa malipo mazuri na tutamwambia lililo jepesi katika amri yetu.

ثُمَّ أَتْبَعَ سَبَبًا ﴿٨٩﴾

89. Kisha akafuata sababu.

حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ مَطْلِعَ الشَّمْسِ وَجَدَهَا تَطْلُعُ عَلَىٰ قَوْمٍ لَّمْ نَجْعَل لَّهُم مِّن دُونِهَا سِتْرًا ﴿٩٠﴾

90. Mpaka alipofika mawiyo ya jua aliona linawachomozea watu tusiowawekea sitara ya kuwakinga nalo.

كَذَٰلِكَ وَقَدْ أَحَطْنَا بِمَا لَدَيْهِ خُبْرًا ﴿٩١﴾

91. Kama hivyo tulizijua vizuri habari zake.

ثُمَّ أَتْبَعَ سَبَبًا ﴿٩٢﴾

92. Kisha akafuata sababu.

DHUL-QARNAIN

Aya 83 – 92

MAANA

Na wanakuuliza kuhusu Dhul- qarnain, Waambie nitawasimulia baadhi ya habari zake.

Wametofautiana kuhusu Dhul-qarnaini huyu kuwa ni nani? Ikasemekana kuwa alikuwa miongoni mwa Malaika, lakini hili ni jambo la kushangaza, Ikasemekana alikuwa Mtume.

Imepokewa kutoka kwa Imam Ali(a.s) kwamba yeye alikuwa ni mja mwema. Hakuna shaka ya wema wake, kwani vitendo vyake na kauli zake, alizozisajili Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika kitabu chake, zinatoa ushahidi wa ubora wake na wema wake.

Pia imesemekana kuwa ni Alexandre wa Macedonia (The great Alexandre), mwanafunzi wa Aristotle. Lakini hili nalo ni la kushangaza zaidi, kwa sababu Alexandre alikuwa ni mwabudu masanamu na Dhul-qar-nain alikuwa akimwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Amenukuu Razi na Abu Hayyani Al-Andalusi (Mhispania), kutoka kwa Abu Rayhan Al-Biruni, kuwa Dhul-qarnaini alikuwa ni mwarabu wa Yemen kutoka kabila la Himayr na jina ake ni Abu Bakr.

Vilevile wametofautiana, kuwa kwa nini aliitwa Dhul-qarnain (mwenye pembe mbii)? Ikasemekana ni kwa kuwa yeye aikuwa ni mtukufu wa wazazi wawili.

Ikasemekana kuwa ni kwa vile alikuwa na misokoto miwili ya nywele. Pia ikasemekana ni kwa vile yeye alimiliki mashariki na magharibi na mengineyo katika kauli za kutofautiana.

Ni ajabu kwa wafasiri kujishughulisha na kuwashughulisha watu kwa jambo lisilokuwa na faida yoyote ya kidunia wala akhera. Tangu lini Qur’an ikajishughulisha na majina na sababu zake? Kama hilo lingekuwa na faida basi Qur’an isingelinyamazia.

Ni kwa ajili hii ndio sisi tukatosheka na dhahiri ya Qur’an na tunasema: watu walimuuliza Mtume mtukufu(s.a.w.w) kuhusu mtu aliyeitwa Dhul-qarnain, Mwenyezi Mungu akamwamrisha awaambie waulizaji kuwa nitawaambia baadhi ya habari zake.

Hakika sisi tulimmakinisha katika ardhi na tumpa sababu ya kila kitu

Makusudio ya kummakinisha hapa ni nguvu na utawala. Na sababu ni nyenzo zinazomfikisha mtu kwenye yale anayoyataka; kama vile elimu, uwezo, afya, mali, watu na zana. Zaidi ya hayo ni tawfiki ya Mungu na msaada wake, Nyenzo zote hizi alikuwa nazo Dhul-qarnain. Kwa hiyo akawa ni mwenye nguvu, Hii ndiyo maana ya kummakinisha katika ardhi. Aya inafahamisha waziwazi kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) analeta vitu kwa sababu zake.

Basi akafuata sababu

Mwenyezi Mungu alimwandalia njia naye akazitumia katika kheri na matendo mema. Miongoni mwazo ni kwenda kwake magharibi ambako amekuashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika kauli yake:

Hata alipofika machweo ya jua aliona linatua kwenye chemchem yenye matope meusi.

Makusudio ya machweo ya jua ni miji ya magharibi, Ni wazi kuwa jua haliwezi kuingia kwenye chemchem. Kwa hio makusudio ni chemchem yenye matope meusi ya bahari ambayo yanaonekana na watu kama Jua linatua ndani yake. Bahari hii ni miongoni mwa bahari za miji ya magharibi, lakini ni bahari gani hiyo? Mwenyezi Mungu ndiye mjuzi zaidi wa hilo. Sheikh Maraghi anasema ni bahari ya Atlantic.

Na hapo akawakuta watu, tukasema: Ewe Dhul-qarnain! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.

Makusudio ya hapo ni hapo kwenye chemchem. Dhahiri ya Aya, ikiwa peke yake, inafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwachia Dhul-qarnain afanye atakavyo kwa watu wa mji huo, akitaka atawaadhibu na akitaka awafanyie hisani.

Na ilivyo hasa ni kuwa jambo hilo haliafikiani na uadilifu wake Mwenyezi Mungu Mtukufu, kafiri na washirikina, ikiwa watang’ang’ania kufru na shirk, tutapata kuwa watu aliowakuta Dhul-qar-nain huko magharibi walikuwa ni makafiri na kwamba yeye aliwelezea imani wakaikataa.

Unaweza kuuliza : kuwa je, inafaa kuwafanyia wema makafiri?

Jibu : Inafaa ikiwa hawakutupiga vita kwenye dini yetu wala hawakututoa majumbani mwetu. Mwenyezi Mungu anasema:

لَّا يَنْهَاكُمُ اللَّـهُ عَنِ الَّذِينَ لَمْ يُقَاتِلُوكُمْ فِي الدِّينِ وَلَمْ يُخْرِجُوكُم مِّن دِيَارِكُمْ أَن تَبَرُّوهُمْ وَتُقْسِطُوا إِلَيْهِمْ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ ﴿٨﴾

“Mwenyezi Mungu hawakatazi kuwafanyia wema na uadilifu wale ambao hawakupigana nanyi kwa ajili ya dini wala hawakuwafukuza katika miji yenu; Hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wafanya uadilifu.” (60:8).

Akasema (Dhul-qarnain): Ama aliyedhulumu, basi tutamwadhibu adhabu na kisha atarudishwa kwa Mola wake amuadhibu adhabu isiyojulikana. Na ama mwenye kuamnini na akatenda mema tutamli- pa malipo mazuri na tutamwambia lililo jepesi katika amri yetu.

Hii ndio desturi ya hukumu Dhul-qarnain na utawala wake. Kwa ufupi ni kuwa, upanga ni kwa mwenye kuasi na wema ni kwa mtiifu. Hakika mali, elimu, na utawala ni neema kubwa anayowapa mtihani Mwenyezi Mungu kwayo waja wake.

Basi neema hiyo huwazidisha washari ukafiri na kupitua mipaka, lakini watu wazuri huifanya neema hiyo kuwa ni nyenzo ya kumtii Mwenyezi Mungu na kumridhisha, kama alivyofanya Dhul-qar- nain.

Kisha akafuata sababu, Yaani akafuata njia, Dhul-qarnain alirejea kutoka magharibi na akaelekea mashariki ambako Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekuashria kwa kauli yake:

Mpaka alipofika mawiyo ya jua aliona linawachomozea watu tusiowawekea sitara ya kuwakinga nalo.

Makusudio ya mawiyo ya jua hapa ni upande wa mashariki, na sitara ni jengo na mfano wake, kama hema, vibanda na mapango. Maana ni kuwa Dhul-qarnain alipowasili miji ya mashariki aliwakuta watu wanaishi kwenye nchi iliyo wazi ikifikiwa na jua, wakiishi maisha ya kiporini, kama wanyama.

Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa nchi hiyo ilikuwa ufuoni mwa Afrika mashariki, Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakutaja alichofanya Dhul-qarnain huko; kuwa je alimfanyia wema mwenye kuamini na aka- tenda mema na kumwadhibu mwenye kunga’ang’ania ukafiri na inadi au aliwaacha kama walivyo? Mwenyezi Mungu ni mjuzi zaidi.

Kama hivyo tulizijua vizuri habari zake.

Yaani hii ndiyo habari ya Dhul-qarnain, tunaijua yote.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ بَيْنَ السَّدَّيْنِ وَجَدَ مِن دُونِهِمَا قَوْمًا لَّا يَكَادُونَ يَفْقَهُونَ قَوْلًا ﴿٩٣﴾

93. Hata alipofikia baina ya milima miwili, alikuta nyuma yake watu ambao takriban hawakuwa wakifahamu kauli.

قَالُوا يَا ذَا الْقَرْنَيْنِ إِنَّ يَأْجُوجَ وَمَأْجُوجَ مُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ فَهَلْ نَجْعَلُ لَكَ خَرْجًا عَلَىٰ أَن تَجْعَلَ بَيْنَنَا وَبَيْنَهُمْ سَدًّا ﴿٩٤﴾

94. Wakasema: Ewe Dhul-qar-nain! Hakika Juju na Majuju wanafanya ufisadi katika nchi. Basi je, tukulipe ujira ili utujengee baina yetu na wao ngome?

قَالَ مَا مَكَّنِّي فِيهِ رَبِّي خَيْرٌ فَأَعِينُونِي بِقُوَّةٍ أَجْعَلْ بَيْنَكُمْ وَبَيْنَهُمْ رَدْمًا ﴿٩٥﴾

95. Akasema: Yale Mola wangu aliyoniwezesha ni bora. Lakini nisaidieni kwa nguvu nijenge kizuizi baina yenu na wao.

آتُونِي زُبَرَ الْحَدِيدِ حَتَّىٰ إِذَا سَاوَىٰ بَيْنَ الصَّدَفَيْنِ قَالَ انفُخُوا حَتَّىٰ إِذَا جَعَلَهُ نَارًا قَالَ آتُونِي أُفْرِغْ عَلَيْهِ قِطْرًا ﴿٩٦﴾

96. Nileteeni vipande vya chuma, Hata alipojaza baina ya nafasi iliyo kati ya milima miwili, akasema: Vuvieni. Hata alipokifanya moto akasema: Nileteeni shaba iliyoyeyuka niimwagie.

فَمَا اسْطَاعُوا أَن يَظْهَرُوهُ وَمَا اسْتَطَاعُوا لَهُ نَقْبًا ﴿٩٧﴾

97. Hawakuweza kuukwea wala hawakuweza kuutoboa.

قَالَ هَـٰذَا رَحْمَةٌ مِّن رَّبِّي فَإِذَا جَاءَ وَعْدُ رَبِّي جَعَلَهُ دَكَّاءَ وَكَانَ وَعْدُ رَبِّي حَقًّا ﴿٩٨﴾

98. Akasema: Hii ni rehema itokayo kwa Mola wangu, Itakapofika ahadi ya Mola wangu atauvunja vunja. Na ahadi ya Mola wangu ni ya kweli.

وَتَرَكْنَا بَعْضَهُمْ يَوْمَئِذٍ يَمُوجُ فِي بَعْضٍ وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَجَمَعْنَاهُمْ جَمْعًا ﴿٩٩﴾

99. Na siku hiyo tutawaacha wakisongana. Na parapanda itapuziwa na wote watakusanywa pamoja.

وَعَرَضْنَا جَهَنَّمَ يَوْمَئِذٍ لِّلْكَافِرِينَ عَرْضًا ﴿١٠٠﴾

100. Na siku hiyo tutawaonyesha wazi makafiri Jahannam waione.

JUJU NA MAJUJU

Aya 93 – 100

MAANA

Kisha akafuata sababu.

Dhul-qarnaini alirejea mji wa tatu ulioko katika Bahari nyeusi, unaokaliwa na Slaves[2] -kama ilivyosemekana - ambao Mwenyezi Mungu ameuashiria kwa kauli yake:

Hata alipofikia baina ya milima miwili, alikuta nyuma yake watu ambao takriban hawakuwa wakifahamu kauli.

Watu aliowakuta huko walikuwa hawafahamu lugha yake wala hakufaamu lugha yao, lakini walielewana kwa ishara au kwa mkalimani; kama anavyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Wakasema: “Ewe Dhul-qar-nain! Hakika Juju na Majuju wanafanya ufisadi katika nchi. Basi je, tukulipe ujira ili utujengee baina yetu na wao ngome?

Sheikh Maraghi anasema katika Tafsir yake: “Juju ni wa Tatars, na Majuju ni wa Mongoli. Asili yao wanatokana na baba mmoja anayeitwa Turk. Miji yao inaanzia Tibet na China hadi kwenye Bahri iliyoganda. Miongoni mwao ni Changez Khan na Halako.

Kisha akanukuu Maraghi Jarida la Al-Muqtatif la mwaka 1888, kwamba jengo la ukuta wa Dhul-qarnain liko nyuma ya Amou–Daria sehemu za Balkh. Jina lake hivi sasa ni mlango wa chuma na liko karibu na mji wa Tirmidh.

Mtaalamu mmoja wa kijerumani Cyllid Burger, amelitaja katika safari zake zilizokuwa mwanzoni mwa karne ya 15. Vilevile amelitaja mwana historia wa Kihispania Clavijo katika safari zake za mwaka 1402 A.D.

Vyovyote iwavyo ni kwamba watu walimtaka Dhul-qarnain awajengee ngome itakayowakinga na Juju na Majuju waliokuwa wakiishambulia nchi yao, wakiwapa adhabu mbaya ya kuwaua, kuwateka na kupora. Wakajiwekea sharti la kumlipa katika mali zao ikiwa atawajenega ngome.

Akasema: Yale Mola wangu aliyoniwezesha na akanipa utawala na malini bora kuliko yale aliyowapa Mwenyezi Mungu. Nyinyi wenyewe mna haja kubwa ya mali yenu, basi itumieni kwenye masilahi yenu.

Lakini nisaidieni kwa nguvu nijenge kizuizi baina yenu na wao.

Makusudio ya nguvu hapa ni wafanyikazi na vifaa vya ujenzi.

Nileteeni vipande vya chuma. Hata alipojaza baina ya nafasi iliyo kati ya milima miwili.

Yaani alipoletewa vyuma alivipanga mpaka vikajaza nafasi iliyo baina ya milima miwili, kisha wakamletea kuni akawasha moto akaweka mifuoakasema: Vuvieni. Hata alipokifanya (chuma)moto akasema: Nileteeni shaba iliyoyeyuka niimwagie.

Wakamletea, akamwagia kwenye vyuma vilivyo moto, vikashikana, ukawa mlima wa chuma.

Hawakuweza kuukwea hao Juju na Majuju, kutokana na urefu na kutelezawala hawakuweza kuutoboa kutokana na ugumu wake na maki yake.

Akasema: Hii ni rehema itokayo kwa Mola wangu.

Aliyesema ni Dhul-qarnain, akimshukuru Mola wake (s.w.t) kwa rehema na neema hii aliyoitimiza mikononi mwake, Hivi ndivyo anavyokuwa mumin mwenye ikhlasi. Anamnyenyekea Mwenyezi Mungu na kushukuru kila zinapokuwa neema za Mwenyezi Mungu kupitia kwake.

Kujengwa kwa ngome hii ni usadikisho wa mfano kuwa katika historia ya binadamu kulikuwa na kusaidiana baina ya mataifa makubwa na yale madogo yanayoendelea; baina ya taifa lililo na nyenzo za maendeleo na lile lisilokuwa nazo.

Nguvu za Amerika zinafanana sana na nguvu za Dhul-qarnaini, kwa vile haziwezi kukabiliwa na yoyote, lakini kuna tofauti kubwa ya matokeo na natija. Wakati nguvu zote za Dhul-qarnain zilkuwa ni utawala wa kheri ya ubinadamu na ufanisi wake, lakini nguvu za Amerika ni za kuhami uovu wa uzayuni na kutawala nyenzo zote, masoko yote kwa masilahi ya ukoloni na kuwadumaza watu kwa kila namna.

Ushahidi wa hayo hauna idadi. Kuanzia kuusaidia uzayuni dhidi ya waarabu na ubaguzi wa rangi ndani ya Amerika hadi Rhodesia,[3] mapinduzi ya kijeshi katika nchi za kiafrika[4] na kuwapiga vita wapigania ukombozi huko Kongo na kila mahali, Ama huko Vietnam ndio haisemeki. Wamekusanya majeshi na kutumia kila walicho nacho, lakini ukakamavu wa wananchi wa Vietnam umetoa somo kwa Amerika, ambalo hawatalisahau maisha.

Kwa hiyo kila ushindi wanaoupata Amerika wajue huo ni wa muda tu, utaondoka kwa upinzani wa wananchi ambao unazidi siku baada ya siku.

Itakapofika ahadi ya Mola wangu atauvunja vunja.

Yaani huo mlima atauvunja vunja, Maana ni kuwa utakapokurubia wakati wa kutokea Juju na Mjuju nyuma ya ukuta, Mwenyezi Mungu ataleta sababu za kuvunjika kwake.

Na ahadi ya Mola wangu ni kweli haina shaka.

Shekh Maraghi anasema: “Ahadi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ilifika kwa kutoka Changez Khan wakafanya ufisadi katika ardhi”.

Katika Tafsir Ar-Razi imeelezwa kuwa maana ya ahadi hapa ni siku ya Kiyama. Katika Tafsir At-Twabariy imeelezwa ni baada ya kuuliwa Dajjal.

Ama sisi tunapondokea kwenye kauli ya Maraghi, kwa sababu iko karibu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Na siku hiyo tutawaacha wakisongana wao kwa wao.

Kwani tunafahamu kuwa Juju na Majuju wataenea katika ardhi baada ya kuharibika ngome na wataharibu maisha ya watu. Mwenyezi Mungu anasema:

حَتَّىٰ إِذَا فُتِحَتْ يَأْجُوجُ وَمَأْجُوجُ وَهُم مِّن كُلِّ حَدَبٍ يَنسِلُونَ ﴿٩٦﴾

“Mpaka watakapofunguliwa Juju na Majuju wakawa wanateremka kutoka kila mlima.” (21:96).

Zaidi ya hayo ni kwamba lau ingelikuwa makusudio ya ahadi yake ni Kiyama au baada ya kufa Dajjal, ingelikuwa ngome bado ipo; na kama ipo basi ingelionekana, hasa kwa kuzingatia kuwa elimu imefanya dunia hivi sasa, pamoja na wakazi wake, ni kama familia moja inayoishi kwenye nyumba moja.

Na parapanda itapuziwa na wote watakusanywa pamoja.

Hii ndiyo siku ya mwisho kwa wale wa mwanzo na wa mwisho. Katika Tafsir Attwabariy imeelezwa kuwa Mtume(s.a.w.w) aliulizwa kuhusu Parapanda, akasema ni pembe itakayopuziwa.

Baada ya hayo yote, tunapenda kujulisha kuwa tuliyoyaeleza au kuyanukuu kutoka kwa wengine kuhusiana na Juju na Majuju, ni kwa njia ya kuleta karibu ufahamisho sio uhakika hasa.

Kwa vile hatukupata rejea za kutegemewa; Kwa sababu hiyo basi tutuatosheka na dhahiri ya Qur’an Tukufu na kuwaachia ufafanuzi wenzetu wengine.

الَّذِينَ كَانَتْ أَعْيُنُهُمْ فِي غِطَاءٍ عَن ذِكْرِي وَكَانُوا لَا يَسْتَطِيعُونَ سَمْعًا ﴿١٠١﴾

101. Wale ambao macho yao yalikuwa kwenye pazia ya kunitaja, Na wakawa hawawezi kusikia.

أَفَحَسِبَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَن يَتَّخِذُوا عِبَادِي مِن دُونِي أَوْلِيَاءَ إِنَّا أَعْتَدْنَا جَهَنَّمَ لِلْكَافِرِينَ نُزُلًا ﴿١٠٢﴾

102. Je, wanadhani waliokufuru kuwafanya waja wangu ndio walinzi badala yangu? Hakika sisi tumeiandaa Jahannamu iwe ni mashukio ya makafiri.

قُلْ هَلْ نُنَبِّئُكُم بِالْأَخْسَرِينَ أَعْمَالًا ﴿١٠٣﴾

103. Sema: je, tuwaambie wale wenye hasara mno ya vitendo?

الَّذِينَ ضَلَّ سَعْيُهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَهُمْ يَحْسَبُونَ أَنَّهُمْ يُحْسِنُونَ صُنْعًا ﴿١٠٤﴾

104. Ambao juhudi yao katika maisha ya dunia imepotea bure, nao wanadhani kuwa wanafanya kazi nzuri?

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ رَبِّهِمْ وَلِقَائِهِ فَحَبِطَتْ أَعْمَالُهُمْ فَلَا نُقِيمُ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَزْنًا ﴿١٠٥﴾

105. Hao ndio ambao wamezikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kukutana naye; Kwa hiyo vitendo vyao vimepomoka; nawala siku ya Kiyama hatutawapa uzito wowote.

ذَٰلِكَ جَزَاؤُهُمْ جَهَنَّمُ بِمَا كَفَرُوا وَاتَّخَذُوا آيَاتِي وَرُسُلِي هُزُوًا ﴿١٠٦﴾

106. Hiyo Jahanamu ndiyo malipo yao kwa walivyokufuru na wakazifanyia kejeli ishara zangu na Mitume wangu.

JAHANNAMU NA WALIOHASIRIKA

Aya 101 – 106

MAANA

Na siku hiyo tutawaonyesha wazi Jahannam makafiri waione.

Wenye makosa, kesho, watashuhudia kwa macho yao Jahannam kabla ya kuingizwa humo, ili wachomeke kwa aina mbili za moto: Moto wa hofu na moto wa kuungua.

Wale ambao macho yao yalikuwa kwenye pazia ya kunitaja.

Kutajwa huwa kunasikiwa na masikio. Kwa hiyo hapa maana ya pazia ya macho ni mfundo wa makafiri kwa Mtume na waumini, na kwamba wao walikuwa hawawezi kumwangalia Mtume(s.a.w.w) wala waumini.

Na wakawa hawawezi kusikia utajo wa Mungu kutoka kwa Mtume wake Mtukufu.

Kwa maneno mengine ni kuwa wakosefu hawawezi kusikiza haki wala kuwatazama watu wa haki. Haya ndiyo tunayoyashuhudia kwa macho, ikiwa ni matokeo ya mzozo baina ya haki na batili na kheri na shari.

Je wanadhani waliokufuru kuwafanya waja wangu ndio walinzi badala yangu?

Makusudio ya waja wangu hapa ni viumbe ambao washirikina wali- wafanya ndio walinzi wao badala ya Mwenyezi Mungu. Hapa kuna maneno yanayokadiriwa kuwa: Je, wana dhani hawa kuwa tumeghafilika nao?Hapana! Hakika sisi tumeiandaa Jahannamu iwe ni mashukio ya makafiri.

Mashukio ni mahali anapoandaliwa mgeni, vile vile linatumika neno hilo kwa maana ya nyumba. Maana ni kuwa tumewaandalia Jahannam kuwa ndio tosha yao. Hii ni sawa na kumwambia yule unayemdharau: unadhani mimi sikuwezi wewe nawe ni kama hiki kiatu?

THAMANI YA MTU

Sema je, tuwaambie wale wenye hasara mno ya vitendo? Ambao juhudi yao katika maisha ya dunia imepotea bure, nao wanadhani kuwa wanafanya kazi nzuri?

Ufupi wa maana ni kuwa mwenye hasara zaidi katika watu na mwenye kuhangaika bure, ni yule mjinga sana anayeuona ujinga wake kuwa ni elimu, shari yake kuwa ni kheri na uovu wake kuwa ni wema.

Hapana mwenye shaka kuwa huyo ni mwenye hasara duniani, kwa vile yeye anaishi asivyokuwa. Vile vile huko akhera, kwa vile atakutana na Mola wake akiwa na ujinga, ghururi na matendo maovu. Aya inaashiria kuwa thamani ya mtu haiwezi kupimwa kwa kuiona yeye mwenyewe; Kwa sababu mgomvi hawezi kujihukumu. Wala pia haiwezi kupimwa kwa mtazamo wa watu.

Ispokuwa mtu hupimwa kwa kipimo cha Qur’an na misingi yake na kushikamana na mafunzo yake na hukumu zake. Hupimwa kwa ukweli na uadilifu, kuinusuru haki na watu wake na kujitolea kwa hali na mali. Qur’an imejaa aina nyingi za mafunzo haya; kama vile kauli zake Mwenyezi Mungu Mtukufu zifuatazo: “...Na kuweni pamoja na wa kweli” Juz; 11 (9:119)

قَوَّامِينَ بِالْقِسْطِ ﴿١٣٥﴾

“....Kuweni Imara kwa uadilifu” Juz;. 5 (4:135)

كُونُوا أَنصَارَ اللَّـهِ ﴿١٤﴾

“...Kuweni wasaidizi wa Mwenyezi Mungu (61:14)

كُونُوا رَبَّانِيِّينَ ﴿٧٩﴾

“...Kuweni watumishi wa Mwenyezi Mungu”Juz.3 (3:79)

وَجَاهِدُوا بِأَمْوَالِكُمْ وَأَنفُسِكُمْ فِي سَبِيلِ اللَّـهِ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿٤١﴾

“...Na mpiganie jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu kwa mali zenu na nafsi zenu Juz.10 (9:41)

إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ ﴿١٣﴾

“Hakika mtukufu wenu zaidi, kwa Mwenyezi Mungu, ni yule mwenye takua zaidi katika nyinyi” (49:13)

Unaweza kuuliza : Mkosaji anaweza kujiona kuwa amepatia na kwamba amefanya vizuri. Je atakuwa ni miongoni mwa waliohasirika; pamoja na kujua kuwa hakuna mwenye isma (kuhifadhiwa na madhambi) isipokuwa yule mwenye isma?

Jibu : Wenye kukosea wako aina mbili: Wa kwanza ni yule mwenye kukosea baada ya kutafiti na kuhakikisha; sawa na wanavyofanya wale wanaojitahidi, kiasi ambacho natija inayopatikana inaweza kuwa sawa na ya mtaalmu.

Hapana mwenye shaka kuwa mkoseaji huyu hawezi kuwa ni katika wale ambao juhudi zao zimepotea bure, au kuwa ni aibu ukoseaji wake; bali huyu analipwa thawabu kutokana na juhudi yake; kama ilivyoelezwa katika Hadith. Lakini kwa sharti awe na nia ya kujikosoa, yatakapofichuka makosa.

Aina ya pili, ni kukosea kulikotokana na kujiamini kwa juujuu, kulikotokana na mawazo, bila ya kufanya utafiti, kwa vile hajui misingi ya utafiti na elimu, Au anaweza kuwa anaijua, lakini asiitumie au aitumie nusunusu, aitumie kabla ya kuikamilisha. Huyu ndiye aliye miongoni mwa wale waliopata hasara katika kazi zao, hilo halina shaka. Kwa sababu Mwenyezi Mungu ameamrisha kuwa na mazingatio na uthabiti na akakataza pupa na kusema bila ya ujuzi.

Baada ya hayo somo tunalolipata kutokana na Aya hii, ni kuwa tusijidanganye, tukajipa sifa tusizo nazo wala kujidanganya kwa maneno.

Vile vile ni wajibu tujihisabu nafsi zetu zinapokuwa na ghururi na kujitukuza, kabla hajatuhisabu Mwenyezi Mungu na watu. Pia rai zetu na kauli zetu tusizione kuwa ndio sawa mia kwa mia. Makosa yanatokea kwa yeyote.

Hao ndio ambao wamezikanusha ishara za Mwenyezi Mungu na kukutana naye.

Mfumo wa maneno unafahamisha kuwa makusudio ya wale waliokanusha ishara za Mola wao na kukutana naye ndio wale ambao juhudi yao katika maisha ya dunia imepotea bure; ni sawa wawe wameamini ufufuo au wameukanusha. Linalozingatiwa ni imani na matendo kwa pamoja; sio imani peke yake.

Kwa hiyo vitendo vyao vimepomoka na wala siku ya kiyama hatutawapa uzito wowote.

Yaani hatutawathamini, kwa sababu hakuna heshima mbele ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kwa yule mwenye takua.

Hiyo Jahanamu ndiyo malipo yao kwa walivyokufuru na wakazifanyia kejeli ishara zangu na Mitume wangu.

Walimkufuru Mwenyezi Mungu na wakaifanyia masikhara haki na watu wake. Moto ndio mwisho na ukomo wa ufisadi na upotevu.

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ كَانَتْ لَهُمْ جَنَّاتُ الْفِرْدَوْسِ نُزُلًا ﴿١٠٧﴾

107. Hakika wale ambao wameamini wakatenda mema, mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi.

خَالِدِينَ فِيهَا لَا يَبْغُونَ عَنْهَا حِوَلًا ﴿١٠٨﴾

108. watadumu humo; hawatataka kuondoka.

قُل لَّوْ كَانَ الْبَحْرُ مِدَادًا لِّكَلِمَاتِ رَبِّي لَنَفِدَ الْبَحْرُ قَبْلَ أَن تَنفَدَ كَلِمَاتُ رَبِّي وَلَوْ جِئْنَا بِمِثْلِهِ مَدَدًا ﴿١٠٩﴾

109. Sema: Lau bahari ingelikuwa ndio wino kwa maneno ya Mola wangu, basi bahari ingemalizika kabla ya kumalizika maneno ya Mola wangu, hata tungeleta mfano wake kuongezea.

قُلْ إِنَّمَا أَنَا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ فَمَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ رَبِّهِ فَلْيَعْمَلْ عَمَلًا صَالِحًا وَلَا يُشْرِكْ بِعِبَادَةِ رَبِّهِ أَحَدًا ﴿١١٠﴾

110. Sema: hakika mimi ni binadamu kama nyinyi tu, nimeletewa wahyi kwamba Mungu wenu ni Mungu mmoja. Mwenye kutarajia kukutana na Mola wake, basi na atende matendo mema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake.

WALIOAMNI NA WAKATENDA MEMA

Aya 108 – 110

MAANA

Hakika wale ambao wameamini wakatenda mema, mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo za Firdausi.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwahidi makafiri moto, sasa anatoa ahadi ya Pepo kwa waumini. Firdausi ni katika Pepo ya daraja ya juu. Mtume Mtukufu(s.a.w.w) amesema: “Mkimuomba Mwenyezi Mungu muombeni Firdausi.”

Watadumu humo; hawatataka kuondoka.

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawalipa wema yale ambayo hawatataka mengine, tosha kabisa! Yanatosheleza yote wanayoyataka. Aya inaashiria kuwa hakuna tamaa huko Akhera; vinginevyo ingelikuwa hakuna kutosheka. Kwani mwenye tamaa hatosheki.

Sema: Lau bahari ingelikuwa ndio wino kwa maneno ya Mola wangu, basi bahari ingemalizika kabla ya kumalizika maneno ya Mola wangu, hata tungeleta mfano wake kuongezea.

Bahari ni jina la jinsi, linaenea kwenye bahari zote. Makusudio ya kabla ya kumalizika maneno, ni kuwa hayamaliziki na mfano wake ni mfano wa bahari. Maana ni kuwa lau tuchukulie kuwa bahari zote ni wino wa kuandika maneno ya Mwenyezi Mungu zisingetosha na maneno ya Mwenyezi Mungu yangelibakia bila ya kikomo.

Aya nyingine yenye maana hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu: “Na lau miti yote iliyomo ardhini ikawa ni kalamu na bahari (ikawa wino) na ikaongezewa bahari nyingine saba, maneno ya Mwenyezi Mungu yasingelimalizika.” (31:27).

Makusudio ya maneno ya Mwenyezi Mungu hapa sio matamshi yanayotokana na herufi wala si amri ya kitendo inayotokana na ibara ya ‘kuwa na kikawa,’ kwa sababu amri hii haiingii kwenye mahisabu: “Na amri haikuwa ila ni moja tu, kama kupepesa jicho.” (54:51).

Isipokuwa makusudio ya maneno yake hapa, ni kuweza kuvileta vitu vyote, wakati wowote atakao; ni sawa iwe ni kwa kuviambia kuwa na vikawa au aviambie muda ujao, wa karibu au mbali. Uwezo huu hauna kikomo wala mwisho, lakini bahari, miti na mifano yake ina kikomo; na kila chenye kikomo kinakwisha.

Kwa maneno mengine ni kuwa kila kitu kilichopo kitakwisha na kukoma, isipokuwa uwezo wa Mwenyezi Mungu wa kukifanya hicho kitu utabakia.

Tutaifafanua zaidi fikra hii kwa mfano huu: Mtu akiwa na maarifa ya kilimo, maarifa yake haya atakuwa nayo tu wakati wote atakaokuwa hai, lakini kile atakochokilima kitaisha. Uweza wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hauishi kwa vile hauna kikomo ni wa milele, lakini viumbe vyake vimepatikana na kila chenye kupatikana kina mwisho.

Sema: Hakika mimi ni binadamu kama nyinyi tu, sina tofauti na nyinyi isipokuwanimeletewa wahyi kwamba Mungu wenu ni Mungu mmoja.

Ibn Abbas anasema: “Mwenyezi Mungu, kwa Aya hii, amemfundisha Mtume wake unyenyekevu, akamwamrisha aseme yeye mwenyewe kuwa ni binadamu kama wengine, isipokuwa Mwenyezi Mungu amemtukuza kwa wahyi.”

Nasi tunaongezea kauli ya Ibn Abbas: Na ili waislamu wasimfanye Muhammad(s.a.w.w) kama wanaswara (wakristo) walivyomfanya Isa(a.s) .

Mwenye kutarajia kukutana na Mola wake, kwa hisabu, thawabu na adhabu,basi na atende matendo mema, wala asimshirikishe yeyote katika ibada ya Mola wake.

Kila mwenye kufanya amali kwa ajili ya mwengine atakuwa amemshirikisha Mwenyezi Mungu kwenye ibada; ni sawa aseme waungu ni wengi au asiseme.

Tofauti ni kuwa kauli ni shirki ya waziwazi na riya ni shirki ya kificho. Kuna Hadith inayosema:

“Mwenye kuswali kwa riya amefanya shirki na mwenye kufunga kwa riya amefanya shirk”

Fananisha mengine kwenye swala na saumu.

MWISHO WA SURA YA KUMI NA NANE

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

41. Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi.

وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

42. Na mumtakase asubuhi na jioni.

هُوَ الَّذِي يُصَلِّي عَلَيْكُمْ وَمَلَائِكَتُهُ لِيُخْرِجَكُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ وَكَانَ بِالْمُؤْمِنِينَ رَحِيمًا ﴿٤٣﴾

43. Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake, ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru. Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

تَحِيَّتُهُمْ يَوْمَ يَلْقَوْنَهُ سَلَامٌ وَأَعَدَّ لَهُمْ أَجْرًا كَرِيمًا ﴿٤٤﴾

44. Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا ﴿٤٥﴾

45. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji.

وَدَاعِيًا إِلَى اللَّـهِ بِإِذْنِهِ وَسِرَاجًا مُّنِيرًا ﴿٤٦﴾

46. Na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake, na taa iangazayo.

وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ بِأَنَّ لَهُم مِّنَ اللَّـهِ فَضْلًا كَبِيرًا ﴿٤٧﴾

47. Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

وَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَالْمُنَافِقِينَ وَدَعْ أَذَاهُمْ وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٤٨﴾

48. Wala usiwatii makafiri na wanafiki na acha udhia wao na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَكَحْتُمُ الْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ طَلَّقْتُمُوهُنَّ مِن قَبْلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمْ عَلَيْهِنَّ مِنْ عِدَّةٍ تَعْتَدُّونَهَا فَمَتِّعُوهُنَّ وَسَرِّحُوهُنَّ سَرَاحًا جَمِيلًا ﴿٤٩﴾

49. Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakayoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

NDIYE ANAYEWAREHEMU

Aya 41 – 49

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi na mumtakase asubuhi na jioni.

Hii ni amri ya kudumu kwenye Swala tano na kumkumbuka, Mwenyezi Mungu wakati wote, kwa kumbukumbu nzuri.

Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.

Kuswalia kukitoka kwa Mwenyezi Mungu, maana yake ni maghufira na rehema na kukitoka kwa mwenginewe ni kuombea maghufira na rehema. Kwa hiyo inampasa kila mtu kumswalia na kumwombea amani kila mwenye kuamini na katenda mema.

Ni vizuri kudokeza kwamba Sunni, aghlabu wakimtaja sahaba mtukufu au imam mkuu husema: Radhiallah anh (Mwenyezi Mungu awe radhi naye). Shia wao husema: Alayhissalam (amani ishuke juu yake). Chimbuko la kauli zote mbili ni moja – Qur’an. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: “Awe radhi nao Mwenyezi Mungu na wao wawe radhi naye.” Juz. 7 (5:119) na akasema:“Amani kwa Ilyasin” (37:130) na amesema kwenye Aya hii tuliyo nayo: “Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.”

Katika Tafsir Ruhul-bayan imeelezwa: “Bani Israil walimuuliza Musa: “Mola wetu naye anaswali? Basi hili likawa zito kwa Musa.” Hilo si ajabu kwa Waisrail.

Ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru.

Makusudio ya viza hapa ni viza vya moto; na nuru ni nuru ya neema; yaani Mwenyezi Mungu na malaika wake wanawaswalia waumini ili wawe mbali na adhabu ya moto na waingie kwenye raha. Imesekana kuwa makusudio ya viza ni ukafiri na nuru ni nuru ya imani, lakini hii haiafikiani na kauli yake Mwenyezi Mungu inayofuatia:

Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

Vile vile haiafikiani na kuwa Mwenyezi Mungu na malaika wake hawarehemu makafiri ili awatoe kwenye imani.

Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:10) Juz. 13 (14:23).

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake.

Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad(s.a.w. w ) kulingania haki na akamsheheneza hoja za kutosha, kumpa habari njema ya pepo yule mtiifu na kumwonya na adhabu chungu yule mwenye kuasi. Kesho atakuwa shahidi wa huyu kwamba alipinga na akatupilia mbali na atakuwa shahidi wa yule kwamba alisikia na akatii.

Kwenye Nahjul-balagha kuna maelezo haya: “Alimtuma kuwa ni mlingania kwenye haki na shahidi kwa viumbe. Akafikisha ujumbe wa Mola wake bila ya kubweteka wala kuzembea, na akapigana jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na maadui zake bila ya kudhoofika wala kutafuta visababu. Ni imamu wa mwenye takua na busara ya mwenye kutaka kuongoka.

Na taa iangazayo inayowaongoza wanaohangaika kwenye ufukwe wa salama.

Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Umepita mfano wake katika Juz.11 (9-112)

Wala usiwatii makafiri na wanafiki.

Imetangulia neno kwa neno katika Juzuu iliyopita mwanzo wa sura hii tuliyo nayo.

Na acha udhia wao.

Mtume hakuwaudhi, ispokuwa washirikina ndio waliomuudhi, kiasi cha kufikia kusema: “Hakuudhiwa Nabii mfano wa nilivyoudhiwa mimi.” Kwa hiyo maana ni, achana nao, usikushughulishe ujinga na upumbavu wao.

Na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

Kwenye Nahjul-balagha imesemwa: “ Mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu anamtoshea na mwenye kumwomba atampa na mwenye kumkopesha atamlipa, na mwenye kumshukuru atampa jaza yake.

Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakyoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

Kabla ya kuwagusa ni kabla ya kuwaingilia. Cha kuwaliwaza kisharia ni kitu anachokitoa mtaliki akiwa hajamwingilia na hakutaja mahari yake. Ikiwa ametaja itakuwa ni wajibu kutoa nusu ya mahari. Tazama Juz. 2 (2:236 – 237).

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَحْلَلْنَا لَكَ أَزْوَاجَكَ اللَّاتِي آتَيْتَ أُجُورَهُنَّ وَمَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ مِمَّا أَفَاءَ اللَّـهُ عَلَيْكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَمَّاتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ خَالَاتِكَ اللَّاتِي هَاجَرْنَ مَعَكَ وَامْرَأَةً مُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلنَّبِيِّ إِنْ أَرَادَ النَّبِيُّ أَن يَسْتَنكِحَهَا خَالِصَةً لَّكَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ قَدْ عَلِمْنَا مَا فَرَضْنَا عَلَيْهِمْ فِي أَزْوَاجِهِمْ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ لِكَيْلَا يَكُونَ عَلَيْكَ حَرَجٌ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٠﴾

50. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao, na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu, na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe, na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine. Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

تُرْجِي مَن تَشَاءُ مِنْهُنَّ وَتُؤْوِي إِلَيْكَ مَن تَشَاءُ وَمَنِ ابْتَغَيْتَ مِمَّنْ عَزَلْتَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكَ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن تَقَرَّ أَعْيُنُهُنَّ وَلَا يَحْزَنَّ وَيَرْضَيْنَ بِمَا آتَيْتَهُنَّ كُلُّهُنَّ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي قُلُوبِكُمْ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَلِيمًا ﴿٥١﴾

51. Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye. Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako. Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote. Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

لَّا يَحِلُّ لَكَ النِّسَاءُ مِن بَعْدُ وَلَا أَن تَبَدَّلَ بِهِنَّ مِنْ أَزْوَاجٍ وَلَوْ أَعْجَبَكَ حُسْنُهُنَّ إِلَّا مَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ رَّقِيبًا ﴿٥٢﴾

52. Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza; isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume. Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu.

TUMEKUHALALISHIA WAKE ZAKO

Aya 50 – 52

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya hii ametaja aina ya wanawake walio halali kwa Mtume(s.a.w. w ) na kumwachia hiyari ya kumlalia na kutomlalia anayemtaka. Kisha akamharamishia kuzidisha wale aliokuwa nao au kubadilisha mwingine. Wakati huo alikuwa na wake tisa. Ufuatao ni ufafanuzi:

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao.

Makusudio ya ujira hapa ni mahari. Na kuwapa hayo mahari kunakuwa ni lazima. Aya inaashiria kuwa Mtume anaweza kuoa idadi yoyote anayoitaka. Haya ni katika mambo yanayomuhusu yeye tu.

Unaweza kuuliza : kufunga ndoa kunaswihi hata kama mahari hayakuta- jwa, kwa nini basi Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufunga uhalali kwa mahari?

Jibu : Ulazima hapa ni wa kuyatoa hayo mahari sio kuyataja kwenye ndoa. Ikiwa mahari hayakutajwa kwenye ndoa, basi ni lazima kutoa mahari kifani; yaani yanayofana na mwingine wa aina yake. Mahari ya mtume, wakati huo, yalikuwa ni Dirhamu 500. wamekadiria Dirhamu moja kuwa ni sawa na Lira 25 za dhahabu.

Na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka waliowatekwa nyara na waislamu kati- ka vita na washirikina, ambao wanaitwa masuria. Mwenyezi Mungu amemuhalishia Mtume wake na umma wake, wanawake hawa.

Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe.

Unaweza kuuliza : Mabinti wa ami, wa shangazi, wajomba na wa khalat (dada wa mama) si wanaingia katika aina ya kwanza ya wanawake, sasa kuna haja gani ya kuhusishwa kutajwa?

Jibu : Inawezekana kuwa makusudio ya kutajwa ni kuwa inavyopendeza ni kuwa hadhi ya Mtume ni kuoa makuraishi aliohama nao kutoka mji wa ukafiri hadi mji wa Uislamu. Ama waumimi wengine ni bora kutowaoa.

Swali la pili : Watu wa sira wamesema kuwa Mtume alikuwa na ami tisa: Abbas, Hamza, Abu Twalib, Zabeir, Harith, Hijla, Muqawwam, Dhirar na Abu Lahab. Na shangazi sita: Swafiya, Ummu Hakim al-baydhau, Atika, Umayma, Arwa na Barra (Assiratu nnabaawiya cha Ibn Hisham).

Na wakasema: “Mtume hakuwa na wajomba wala khalat (mama wadogo au wakubwa), kwa sababu mama yake Amina bint Wahb(a.s) hakuwa na kaka wala dada.” (Tafsir Ruuhul-bayan).

Sasa kuna wajihi gani wa Mwenyezi Mungu kusema: ‘Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako?’

Jibu : Makusudio ya wajomba na khalat wa Mtume ni ukoo wa mama yake unaoitwa Bani Zuhra, ambao walikuwa wakisema: “Sisi ni wajomba zake Mtume.”

Na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine.

Katika mambo yanayomuhusu Mtume tu ni kumuoa mwanamke, akitaka, ikiwa atajitoa mwenye kwa Mtume bila ya mahari, kwa masharti ya kuwa mumini. Ndio! Inajuzu kwa mwinginewe kuoa kwa mahari, kisha mke asamehe mahari, kama anavyosamehe mtu yoyote mali yake kwa mwingine.

Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomi- likiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu, ameweka idadi ya wake waungwana na akaharamisha mwanamke kujitoa mwenyewe bila mahari. Lakini akaliruhusu hilo kwa Mtume ili isiwe dhiki juu yake.

Vile vile kufahamisha utukufu wa cheo chake na juhudi zake. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye anayejua zaidi li lilo na masilahi zaidi kwa watu, akiwa anawahurumia na kuwaghufuria.

Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye.

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amempa uhuru Mtume wake mtukufu katika idadi ya wanawake na katika Aya hii amempa hiyari ya kuongeza au kupunguza zamu ya yeyote anayemtaka.

Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako.

Yaani anaweza kumrudia aliyemaliza zamu naye na kumwacha aliyekuwa kwenye zamu yake. Kwa ibara ya wanaoimudu lugha ni, anaweza kumtanguliza wa mwisho na kumweka mwisho wa kwanza.

Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote.

‘Hivyo’ ni huko kuachiwa hiyari Mtume(s.a.w.w) . Maana ni kuwa wao wakijua kuwa hiyari ni yako sio yao ya zamu sawa, basi kila mmoja ataridhia na vile utakavyokuwa kwake kwa siku kidogo au nyingi kwa kujua kuwa ziada hiyo imetokana na wewe wala si wajibu kwako. Pamoja na hayo, lakini Mtume alikuwa akikaa siku sawa baina ya wake zake.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu ya kupondokea zaidi kwa baadhi ya wake zenu kuliko wengine. Mwenyezi Mungu hayachukulii mapenzi yaliyo moyoni au chuki; isipokuwa anachukulia matendo. Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza.

Wafasiri wametaja maana tatu za Aya hii; iliyo karibu zaidi na maana ya dhahiri ni ile isemayo kuwa Mwenyezi Mungu baada ya kumhalalishia Mtume wanawake aliowaishiria katika Aya iliyotangulia, amewajibisha katika Aya hii kutosheka na alio nao ambao walikuwa tisa na akaharamishiwa kumwacha yeyote katika wao na kuweka mwingine mahali pake, hata kama atakuwa amempendeza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ijapo uzuri wao utakupendeza’ inafahamisha kuwa mwanamume anaruhusiwa kumwangalia mwanamke anayetaka kumuoa.

Na ndio mafakihi wakalitolea fatwa hilio kwa kutegemea Aya hii na Hadith za Mtume mtukufu(s.a.w. w ) .

Isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume, aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka.

Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu, hata kilicho siri na kwenye dhamiri:

وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ﴿٤﴾

“Naye yu pamoja nanyi popote mlipo.” (57:4).

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتَ النَّبِيِّ إِلَّا أَن يُؤْذَنَ لَكُمْ إِلَىٰ طَعَامٍ غَيْرَ نَاظِرِينَ إِنَاهُ وَلَـٰكِنْ إِذَا دُعِيتُمْ فَادْخُلُوا فَإِذَا طَعِمْتُمْ فَانتَشِرُوا وَلَا مُسْتَأْنِسِينَ لِحَدِيثٍ إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ يُؤْذِي النَّبِيَّ فَيَسْتَحْيِي مِنكُمْ وَاللَّـهُ لَا يَسْتَحْيِي مِنَ الْحَقِّ وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ وَمَا كَانَ لَكُمْ أَن تُؤْذُوا رَسُولَ اللَّـهِ وَلَا أَن تَنكِحُوا أَزْوَاجَهُ مِن بَعْدِهِ أَبَدًا إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمًا ﴿٥٣﴾

53. Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo. Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki. Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao. Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

إِن تُبْدُوا شَيْئًا أَوْ تُخْفُوهُ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٥٤﴾

54. Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

لَّا جُنَاحَ عَلَيْهِنَّ فِي آبَائِهِنَّ وَلَا أَبْنَائِهِنَّ وَلَا إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ أَخَوَاتِهِنَّ وَلَا نِسَائِهِنَّ وَلَا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ وَاتَّقِينَ اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدًا ﴿٥٥﴾

55. Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

MKISHAKULA TAWANYIKENI

Aya 53 – 55

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo.

Yaani msikae kabisa si kwa mazungumzo wala kwa jambo jingine. Yametajwa mazungumzo kwa vile mara nyingi mtu anakaa kwa kupiga gumzo.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa baadhi ya maswahaba walikuwa wakiingia nyumba ya Mtume(s.a.w. w ) bila ya idhini kama ilivyo ada ya kijahiliya; na kwamba wakiona chakula kinapikwa basi wanakingoja na baada ya kula walikuwa wakipiga gumzo.

Hakuna mwenye shaka kwamba aina hii ya upuzi na kukosa adabu inamuudhi binadamu yeyote, awe Mtume au si Mtume. Ni kwa ajili hii Mtume(s.a.w. w ) aliwafundisha adabu mswahaba na wengineo kuwa wasiingie nyumba yoyote bila ya idhini ya wenyewe - hayo yamedokezwa kwenye Juz. 18 (24:28) – na kwamba wasiende kula ila wakiitwa, tena chakula kiwe kimeandaliwa na wakishamaliza kula wasingoje tena.

Haya hayahusiki na nyumba ya Mtume peke yake; isipokuwa Mwenyezi Mungu amemtaja yeye kwa vile ndio sababu ya kushuka Aya. Mara nyingi tumesema kuwa sababu ya kushuka Aya haiifungi na hilo lililoishukia.

Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki.

Makusudio ya haki aliyokuwa akiistahi Mtume ni haki yake ya kiutu – kuwatoa wapuuzi nyumbani kwake. Mtume aliwanyamazia kwa kuwaonea haya; ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akatanabahisha kwamba kubaki kwao baada ya chakula kunamuudhi Mtume, vile vile kuingia kwao nyumbani kwake bila ya idhini yake.

Kuna Hadith isemayo: “Haya ni tawi la imani na asiyekuwa na haya hana dini.” Kuna Hadith nyingine isemayo:“Hakukubakia katika mifano ya mitume isipokuwa kauli ya watu: Kama huna haya basi fanya utakavyo.”

Katika maelezo ya wasifu wa Mtume(s.a.w. w ) ni kuwa yeye alikuwa na haya kuliko mwanamwali kwenye ushungi wake. Katika Nahjul-balagha imesemwa:“Hakuna imani kama haya na subira.” Farazdaq katika kumsifu Imam Zaynul-abdin anasema:

Hufumba macho kwa haya kwa haiba yake. Hazungumzi ila kuonekana tabasamu yake Maajabu ni yale yaliyoandikwa kwenye kitabu Muhadharatul-udabai cha Asfahaniy:

“Doezi mmoja alilaumiwa kwa kudoea kwake, akasema akijitetea: “Ala! Ikiwa bani Israil walimdoea Mungu, je sisi tusidoee watu?”

Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize ni nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.

Yaani mnapowaomba haja wakeze Mtume. Kutaja chombo cha chumbani ni kutolea mfano tu, sio kuhusisha na kuondoa hukumu kwa vingine. Hilo linafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.” Inayotambulisha kuwa kuchanganyika na kuondoa pazia baina ya wanawake na wanaume kunaleta ufisadi na fitna.

Maana yake ni kuwa kuchanganyika ni haramu, au angalau ni bora kuacha. Hapa inatubainikia kuwa kuchanganyika ni sababu ya kuleta matamanio ya kijinsiya, na wala sio kumtia adabu mwanamke na kumkandamiza; kama wanavyodai wale wasemao: “Mungu amesema hivyo na mimi nasema hivi” Ni nani aliye mkweli zaidi kwa mazungumzo kuliko Mwenyezi Mungu?

Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

Hukumu hii inamuhusu Mtume tu peke yake. Kwa sababu wakeze wako katika daraja ya mama wa waumini. Imeelezwa katika Tafsir Arrazi na Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy: “Hakika Aya hii ilishuka pale aliposema Twalha bin Abdallah Attaymiy:“Akifa Muhammad(s.a.w. w ) nitamuoa Aisha.”

Hilo linataliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Hilo ni karipio kwa yule aliyedhamiria kuoa wake za Mtume baada yake.

Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuamrisha kuzungumza na wanawake nyuma ya pazia (hijabu) hapa anavua wale ambao hawawezi kuoana nao, ambao ni: baba, mtoto, kaka, mtoto wa kaka na mtoto wa dada, mtumwa na wanawake. Lakini Mwenyezi Mungu amesema wanawake wao, yaani wanawake wenzao walio waumini, kwa sababu wasiokuwa waumini watawasifia wanaume zao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (24:31).

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

56. Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeami- ni! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

إِنَّ الَّذِينَ يُؤْذُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَأَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا مُّهِينًا ﴿٥٧﴾

57. Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾

58. Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

MSWALIENI MTUME

Aya 56 – 58

MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

Makusudio ya Mwenyezi Mungu kumsalia Mtume ni kumridhia kumrehe- mu na kumsifu kwa kila kheri, swala ya malaika ni kumsifu, na kutoka kwa waumini ni kumwombea dua ya kuwa na daraja ya juu. Imam Ar-Ridha(a.s) aliulizwa kuhusu maana ya kauli ya Mwenyezi Mungu: malaika na waumini humswalia Mtume, akasema:“Swala kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni rehema, kutoka kwa malaika ni kumsifu na kutoka kwa waumni ni kumwombea.”

Kuswaliwa huku hakuhusiki na risala ya Muhammad(s.a.w. w ) peke yake. Kila mtu anayetumia desturi ya risala ya Muhammad(s.a.w. w ) , kuifundisha au kuijulisha au kutaja fadhila yoyote katika fadhila zake basi atakuwa amemswalia, awe mumin au sio mumin, akitaka hilo au asitake.

Imam Ja’far As-Sadiq(a.s) anasema: “Mtu kumswalia Muhammad(s.a.w. w ) ni kama kusema:“Subhanallah walhamdulillah walailaha illaha wallahu akbar” (Kutakasika ni kwa Mwenyezi Mungu na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu na hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mkubwa).

Imam hapa anakusudia kuwa thawabu za kumswalia Mtume ni sawa na thawabu za tasbih, tahmid, tahlil na takbir. Imepokewa Hadith kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w. w ) , amesema:“Bakhili wa kweli ni yule ambaye nikitajwa mbele yake haniswalii” .

VIPI TUTAMSWALIA MTUME?

Katika Sahih Al-Bukhariy Juz. 8, mlango wa kumswalia mtume, Tafsir At- Tabariy, Tafsir Ar-Raziy, Tafsir Al-Maraghi na wafasiri wengineo, pia katika vitabu vya Hadith, kuna maelezo haya: “Mtume aliulizwa: Vipi tutakuswalia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?Akasema: semeni:

Allahumma swalli a’la muhammdi wa a’la aali Muhammad, kama swal-layta a’la Ibrahima wa a’laa aali Ibrahim, Innaka hamidum majiid Allahumma barik ala muhammdi wa a’la ali Muhammad, kama barakta a’la Ibrahima wa a’la ali Ibrahim, Innaka hamidum majid.

(Ewe Mwenyezi Mungu mswalie Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyomswalia Ibrahim na kizazi cha Ibrahim, hakika wewe ni mwenye kusifiwa mwenye kutukuzwa. Ewe Mwenyezi Mungu mbariki Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyombariki Ibrahim na kizazi cha Ibrahim. Hakika wewe ni Mwenye kusifiwa Mwenye kutukuzwa. )

Katika tafsir Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy, amesema: “Inatakikana mwenye kuswali aseme: Allhumma swali a’la Muhammad wa a’la AliMuhammad” kwa kulirudia neno ‘a’la’; kwani Sunni wanaweka neno hilo kabla ya aali, kuwapinga Shia ambao hawaliweki neno hilo.

Sisi hatuoni tofauti yoyote baina ya anayesema: neno hilo na asiyelisema. Ama kuhusu ile Hadith isemayo:“Mwenye kutenganisha baina yangu na kizazi changu, hatapata shafaa yangu,” Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi usahihi wake.

Imam Shafii naye amesema katika shairi lenye maana hii: Enyi watu wa nyumba ya Mtume pendo lenu ni faradhi kutoka kwa Mwenyezi Mungu amelieleza katika Qur’an. Inawatosha kuwa ni cheo kikuu kwamba nyinyi asiyewaswalia hana Swala

Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

Makusudio ya kumuudhi Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kumghadhabisha, na sababu yenye kuwajibisha hilo ni kumpinga, kumnasibishia mshirika au mtoto, au kuasi hukumu miongoni mwa hukumu zake. Na kuumuudhi Mtume(s.a.w. w ) ni kupinga utume wake au kupuuza mwenendo wake.

Laana kutoka kwa Mungu ni kwa kuwekwa mbali na rehema yake na kutoka kwa watu ni shutuma na kuombewa mabaya. Katika Nahjul-balagha imeelezwa:“Mwenyezi Mungu amewalaani wanaoamrisha mema na kuacha kuyatenda na wanaokataza maovu na wanayoyatenda.”

Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

Pasi na wao kufanya, yaani kufanya kosa linalostahili udhia. Kuudhi kunakuwa ni kwa kusengenya, vitimbi, uzushi n.k. Kuna Hadith zisemazo:

“Mwislamu ni yule ambaye watu wamesalimika na mkono wake na ulimi wake.”

“Utukufu wa mumin ni kwa kujizuia na kuwaudhi watu.”

“Aliye dhalili zaidi katika watu ni yule anayewadharau watu.”

Imam Ali(a.s) anasema: Mwenye hali mbaya zaidi katika watu ni yule asiyemwaamini yeyote kwa dhana zake mbaya, na asiyeaminiwa na yeyote kwa vitendo vyake vibaya.”

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ قُل لِّأَزْوَاجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَاءِ الْمُؤْمِنِينَ يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِن جَلَابِيبِهِنَّ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يُعْرَفْنَ فَلَا يُؤْذَيْنَ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٩﴾

59. Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie jalbab zao. Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

لَّئِن لَّمْ يَنتَهِ الْمُنَافِقُونَ وَالَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْمُرْجِفُونَ فِي الْمَدِينَةِ لَنُغْرِيَنَّكَ بِهِمْ ثُمَّ لَا يُجَاوِرُونَكَ فِيهَا إِلَّا قَلِيلًا ﴿٦٠﴾

60. Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

مَّلْعُونِينَ أَيْنَمَا ثُقِفُوا أُخِذُوا وَقُتِّلُوا تَقْتِيلًا ﴿٦١﴾

61. Wamelaaniwa! Popote waonekanapo, na wakamatwe na wauliwe kabisa.

سُنَّةَ اللَّـهِ فِي الَّذِينَ خَلَوْا مِن قَبْلُ وَلَن تَجِدَ لِسُنَّةِ اللَّـهِ تَبْدِيلًا ﴿٦٢﴾

62. Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

WAJIBU WA HIJABU

Aya 59 – 62

LUGHA

Kuna kauli nyingi kuhusu neno Jalbab: kuna wanaosema kuwa ni nguo inayomfunika mwanamke kutoka kichwani hadi nyayoni. Wengine wakasema ni ushungi unaofunika kichwa cha mwanamke na uso wake. Kauli hii ndio aliyo nayo mwenye Majmaul-Bayan.

MAANA

Zimekwishatangulia Aya mbili zinazofahamisha wajibu wa hijabu kwa wanawake:

Ya kwanza ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Wala wasidhihirishe uzuri wao ila kwa waume zao.” Juz. 18 (24: 31). Ya pili ni ile Aya ya 53, katika Sura hii tuliyo nayo: “Na mnapowaomba chombo cha nyum- bani, basi waulizeni nyuma ya mapazia.”

Aya iliyo wazi zaidi ya hizi mbili ni hii tuliyo nayo, isemayo:

Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie nguo zao.

Kusema kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘wajiteremshie nguo zao’ inaenea kusitiri na kufunika sehemu zote za mwili, kikiwemo kichwa na uso. Hilo linatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe.

Waislamu, mwanzoni walikuwa wakitoka bila ya kujitanda, kama ilivyokuwa desturi ya kijahiliya, ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamtaka Mtume wake mtukufu, katika Aya hii, awaamrishe wake zake kujisitiri na kuvaa hijabu. Na amri inafahamisha wajibu. Kwa hiyo hijabu ni wajibu.

Hata hivyo uso na viganja viwili havimo kwenye wajibu huu, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ﴿٣١﴾

“Wala wasionyeshe uzuri wao, isipokuwa unaodhihirika.” Juz. 18 (24:31).

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana kutokana na kujistahi na kujichunga. Kwani hijabu ni kinga baina ya mwanamke na tamaa ya watu wenye shakashaka na mafasiki,wasiudhiwe kwa kuangaliwa na mafasiki.

Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Anasamehe yaliyopita na anamuhurumia mwenye kutubia na kurejea nyuma.

Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

Wanafiki walificha ukafiri na wakadhihirisha imani. Wanaoeneza fitna ni watu katika wananfiki waliokuwa wakieneza propaganda dhidi ya Mtume(s.a.w. w ) na maswahaba na wakawatia shaka wale wadhaifu wa imani ambao Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewaletea ibara ya wenye mardhi nyoyoni mwao. Aya inatoa onyo la kuuawa na kufukuzwa wanafiki, waeneza fitna na wale watakaowasikiliza, ikiwa hawatajizuia na upotevu na ufisadi wao.

VITA VYA NAFSI

Siku hizi kueneza fitna kunaitwa ‘vita vya nafsi.’ Nguvu ya shari imetafuta njia nyingi sana za kueneza uongo na mambo ya ubatilifu kwa kila nyenzo. Kuanzia magazeti, radio, runinga, sinema, hotuba, vipeperushi, shule, vyuo, vitabu n.k.

Vyombo hivi vimekaririka masikioni mwa watu kila siku, kiasi ambacho uhakika haupati nafasi kwa watu na wenye ikhlasi, isipokuwa kwa mwamko mkamilifu na elimu itakayotangulia propaganda za wakoloni na wazayuni.

Nimesoma kwenye gazeti linaloitwa Akhabar Al-yawm la Misr, la 13/12/69, kwamba Israil ina magazeti ya propaganda yanayofikia 890 ulimwenguni kwa ajili ya kueneza habari za uongo. Zaidi ya hayo wametawala vyombo vingi vya habari ulimwenguni, kwa njia isiyokuwa ya moja kwa moja; kama vile runinga, radio n.k.

Kwenye mahisabu haya hayaingii magazeti ya Beiruti yenye uhusiano mkubwa na wakoloni na wazayuni.

Kwa vyovyote iwavyo, Alhamdu lillah, Israil imehisi mapigo kutoka kwa waarabu na kwamba propaganda zao zilizotengenezwa na Marekani, na kutangazwa na vibaraka, zimeanza kujulikana.

Wamelaaniwa! Popote waonekanapo na wakamatwe na wauliwe kabisa.

Wamelaaaniwa na kila ulimi, kwa sababu dini yao ni pesa na matendo yao ni udanganyifu, uwongo na hadaa. Hawana dawa isipokuwa kuuawa popote walipo; kama kiungo kilichoharibika, kisipokatwa kitaharibu mwili wote.

Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya desturi ya Mwenyezi Mungu hapa ni hukumu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa mpotevu anayepoteza, ambayo ni kuuliwa ambako amekuwekea sharia, ambaye imetukuka hekima yake, tangu zamani. Hukumu hii itabakia milele bila ya mabadiliko wala mageuzi.

يَسْأَلُكَ النَّاسُ عَنِ السَّاعَةِ قُلْ إِنَّمَا عِلْمُهَا عِندَ اللَّـهِ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّ السَّاعَةَ تَكُونُ قَرِيبًا ﴿٦٣﴾

63. Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

إِنَّ اللَّـهَ لَعَنَ الْكَافِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمْ سَعِيرًا ﴿٦٤﴾

64. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka.

خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا لَّا يَجِدُونَ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا ﴿٦٥﴾

65. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru.

يَوْمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمْ فِي النَّارِ يَقُولُونَ يَا لَيْتَنَا أَطَعْنَا اللَّـهَ وَأَطَعْنَا الرَّسُولَا ﴿٦٦﴾

66. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

وَقَالُوا رَبَّنَا إِنَّا أَطَعْنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَاءَنَا فَأَضَلُّونَا السَّبِيلَا ﴿٦٧﴾

67. Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia.

رَبَّنَا آتِهِمْ ضِعْفَيْنِ مِنَ الْعَذَابِ وَالْعَنْهُمْ لَعْنًا كَبِيرًا ﴿٦٨﴾

68. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ آذَوْا مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ اللَّـهُ مِمَّا قَالُوا وَكَانَ عِندَ اللَّـهِ وَجِيهًا ﴿٦٩﴾

69. Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

WANAKUULIZA KUHUSU SAA

Aya 63 – 69

MAANA

Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

Makusudio ya saa ni Kiyama Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:187).

Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

Makafiri na waasi kesho watasukumwa kwenye adhabu ya moto, hawatakuwa na msaidizi wala udhuru. Watauma vidole vyao kwa kujutia walivyomuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, lakini ‘majuto ni mjukuu.’

Umetangulia mfano wake katika Juz. 19 (25:27).

Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

Makusudio ya mabwana na wakubwa ni viongozi wa dini na dunia. Laana ni kufedheheka. Wadhaifu watawageuzia adhabu na watamtaka Mwenyezi Mungu awaongezee adhabu.

Mwenye kuichunguza historia ataona kwamba aghlabu umma wa kijinga unaongozwa na mataghuti na waovu. Lakini watu wenye mwamko na maarifa hawaamini kuweka masilahi yao isipokuwa kwa waaminifu wenye ikhlasi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:38).

Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

Waliomuudhi Musa(a.s) ni Wana wa Israil, hilo halina shaka; ambapo walimsifu sifa zisizokuwa za mitume.

Aya hii inaashiria kwamba badhi ya swahaba walimuudhi Mtume mtukufu(s.a.w.w) na wakambandika mambo asiyokuwa nayo, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawakataza waislamu hilo.

Kuna riwaya inayosema kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) siku moja aliapa, basi mtu mmoja katika Answar akasema: “Kiapo hiki hakikusudiwa radhi ya Mwenyezi Mungu.” Hapo uso wa Mtume ukaiva wekundu na akasema:“Amrehemu Musa, hakika aliudhiwa zaidi ya hivi na akasubiri.”

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾

70. Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa.

يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا ﴿٧١﴾

71. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu. Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

إِنَّا عَرَضْنَا الْأَمَانَةَ عَلَى السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَالْجِبَالِ فَأَبَيْنَ أَن يَحْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحَمَلَهَا الْإِنسَانُ إِنَّهُ كَانَ ظَلُومًا جَهُولًا ﴿٧٢﴾

72. Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanadamu akaichukua. Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana,

لِّيُعَذِّبَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْمُشْرِكِينَ وَالْمُشْرِكَاتِ وَيَتُوبَ اللَّـهُ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٣﴾

73. Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na washirikina wanaume na washirikina wanawake; na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

TULIZITOLEA AMANA

Aya 70 – 73

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu.

Kauli ya sawa ni kusema haki na ukweli, bila ya kuficha kitu; hata kama inamuhusu mwenyewe. Makusudio yake hapa ni ile inayowanufaisha watu kwa kulinganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu ‘Atawatengenezea amali zenu;’ ambapo Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejaalia kauli ya haki ni sababu ya matendo mema; kwa mfano kumwongoza aliyepotea kwenye njia ya heri na amani, kumsaidia aliyedhulumiwa kwa neno la usawa au kauli ambayo italeta suluhu baina ya watu wawili na mengineyo yanay- owanufaisha watu kwa namna moja au nyingine.

Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

Atafuzu duniani kwa kufaulu na kuwa na sera nzuri na katika Akhera atafuzu kwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu zake.

Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanaadamu akaichukua.

Wafasiri wametofautiana kuhusu maana ya amana. Kuna waliosema kuwa ni taklifa na twaa. Wengine wakasema ni tamko la Lailaha illahha (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu). Kuna waliosema ni viungo vya mwanadamu; kama masikio yake, macho yake, mikono yake na miguu yake. Kwamba ni juu yake kuvitumia kwa ajili ya lengo lilioumbiwa. Pia kuna wale waliosema kuwa ni amana katika mali.

Tuonavyo sisi maana yake ni kujitolea muhanga kwa ajili ya manufaa ya jamii, si kwa lololote isipokuwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na ya ubinadamu.

Kwa sababu kujitolea huku ni kuzito na kukubwa kiasi ambacho maumbile yenye nguvu zaidi, kama mbingu, ardhi na majabali yangelikataa kubeba, kama yangelikuwa na hisia.

Kwa hiyo lengo la kutaja mbingu na ardhi ni kuashiria ukubwa wa kuji- tolea huku, na kwamba binadamu ni kiumbe pekee anayeweza kupingana na nafsi yake na matamanio yake.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu:Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana, maana yake ni kuwa binadamu atajidhulumu yeye mwenyewe na mwingine ikiwa ataifanyia hiyana amana hii na kutojua mwisho muovu utakotokana na hiyana yake hiyo.

Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake ambao wanajionyesha kuwa wanatekeleza amana, lakini kumbe ni wahaini.

Na washirikina wanaume na washirikina wanawake. Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa vile kosa la ushirikina haliwezi kufutwa hata na kujitolea muhanga.

Na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Yaani anawaghufiria wenye kutubia na kuwahurumia wanyonge. Ewe Mwenyezi Mungu mrehemu Muhammad na kizazi chake, rehema ambayo atatuombea nayo siku tutakapohitajia.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA TATU: SURAT AL-AHZAB

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اذْكُرُوا اللَّـهَ ذِكْرًا كَثِيرًا ﴿٤١﴾

41. Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi.

وَسَبِّحُوهُ بُكْرَةً وَأَصِيلًا ﴿٤٢﴾

42. Na mumtakase asubuhi na jioni.

هُوَ الَّذِي يُصَلِّي عَلَيْكُمْ وَمَلَائِكَتُهُ لِيُخْرِجَكُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ وَكَانَ بِالْمُؤْمِنِينَ رَحِيمًا ﴿٤٣﴾

43. Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake, ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru. Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

تَحِيَّتُهُمْ يَوْمَ يَلْقَوْنَهُ سَلَامٌ وَأَعَدَّ لَهُمْ أَجْرًا كَرِيمًا ﴿٤٤﴾

44. Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ شَاهِدًا وَمُبَشِّرًا وَنَذِيرًا ﴿٤٥﴾

45. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji.

وَدَاعِيًا إِلَى اللَّـهِ بِإِذْنِهِ وَسِرَاجًا مُّنِيرًا ﴿٤٦﴾

46. Na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake, na taa iangazayo.

وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ بِأَنَّ لَهُم مِّنَ اللَّـهِ فَضْلًا كَبِيرًا ﴿٤٧﴾

47. Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

وَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَالْمُنَافِقِينَ وَدَعْ أَذَاهُمْ وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٤٨﴾

48. Wala usiwatii makafiri na wanafiki na acha udhia wao na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا نَكَحْتُمُ الْمُؤْمِنَاتِ ثُمَّ طَلَّقْتُمُوهُنَّ مِن قَبْلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ فَمَا لَكُمْ عَلَيْهِنَّ مِنْ عِدَّةٍ تَعْتَدُّونَهَا فَمَتِّعُوهُنَّ وَسَرِّحُوهُنَّ سَرَاحًا جَمِيلًا ﴿٤٩﴾

49. Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakayoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

NDIYE ANAYEWAREHEMU

Aya 41 – 49

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mkumbukeni Mwenyezi Mungu kwa wingi na mumtakase asubuhi na jioni.

Hii ni amri ya kudumu kwenye Swala tano na kumkumbuka, Mwenyezi Mungu wakati wote, kwa kumbukumbu nzuri.

Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.

Kuswalia kukitoka kwa Mwenyezi Mungu, maana yake ni maghufira na rehema na kukitoka kwa mwenginewe ni kuombea maghufira na rehema. Kwa hiyo inampasa kila mtu kumswalia na kumwombea amani kila mwenye kuamini na katenda mema.

Ni vizuri kudokeza kwamba Sunni, aghlabu wakimtaja sahaba mtukufu au imam mkuu husema: Radhiallah anh (Mwenyezi Mungu awe radhi naye). Shia wao husema: Alayhissalam (amani ishuke juu yake). Chimbuko la kauli zote mbili ni moja – Qur’an. Mwenyezi Mungu Mtukufu amesema: “Awe radhi nao Mwenyezi Mungu na wao wawe radhi naye.” Juz. 7 (5:119) na akasema:“Amani kwa Ilyasin” (37:130) na amesema kwenye Aya hii tuliyo nayo: “Yeye ndiye anayewaswalia na malaika wake.”

Katika Tafsir Ruhul-bayan imeelezwa: “Bani Israil walimuuliza Musa: “Mola wetu naye anaswali? Basi hili likawa zito kwa Musa.” Hilo si ajabu kwa Waisrail.

Ili awatoe vizani na kuwatia kwenye nuru.

Makusudio ya viza hapa ni viza vya moto; na nuru ni nuru ya neema; yaani Mwenyezi Mungu na malaika wake wanawaswalia waumini ili wawe mbali na adhabu ya moto na waingie kwenye raha. Imesekana kuwa makusudio ya viza ni ukafiri na nuru ni nuru ya imani, lakini hii haiafikiani na kauli yake Mwenyezi Mungu inayofuatia:

Naye ni mwenye kuwarehemu waumini.

Vile vile haiafikiani na kuwa Mwenyezi Mungu na malaika wake hawarehemu makafiri ili awatoe kwenye imani.

Maamkuzi yao siku ya kukutana naye yatakuwa ni Salaam na amewaandalia malipo yenye heshima.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:10) Juz. 13 (14:23).

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekutuma uwe shahidi na mbashiri na muonyaji na mlinganiaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake.

Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad(s.a.w. w ) kulingania haki na akamsheheneza hoja za kutosha, kumpa habari njema ya pepo yule mtiifu na kumwonya na adhabu chungu yule mwenye kuasi. Kesho atakuwa shahidi wa huyu kwamba alipinga na akatupilia mbali na atakuwa shahidi wa yule kwamba alisikia na akatii.

Kwenye Nahjul-balagha kuna maelezo haya: “Alimtuma kuwa ni mlingania kwenye haki na shahidi kwa viumbe. Akafikisha ujumbe wa Mola wake bila ya kubweteka wala kuzembea, na akapigana jihadi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na maadui zake bila ya kudhoofika wala kutafuta visababu. Ni imamu wa mwenye takua na busara ya mwenye kutaka kuongoka.

Na taa iangazayo inayowaongoza wanaohangaika kwenye ufukwe wa salama.

Wape bishara waumini ya kwamba wanafadhila kubwa kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Umepita mfano wake katika Juz.11 (9-112)

Wala usiwatii makafiri na wanafiki.

Imetangulia neno kwa neno katika Juzuu iliyopita mwanzo wa sura hii tuliyo nayo.

Na acha udhia wao.

Mtume hakuwaudhi, ispokuwa washirikina ndio waliomuudhi, kiasi cha kufikia kusema: “Hakuudhiwa Nabii mfano wa nilivyoudhiwa mimi.” Kwa hiyo maana ni, achana nao, usikushughulishe ujinga na upumbavu wao.

Na mtegemee Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa mlinzi.

Kwenye Nahjul-balagha imesemwa: “ Mwenye kumtegemea Mwenyezi Mungu anamtoshea na mwenye kumwomba atampa na mwenye kumkopesha atamlipa, na mwenye kumshukuru atampa jaza yake.

Enyi ambao mmeamini! Mkiwaoa wanawake waumini kisha mkawaacha kabla ya kuwagusa, basi hamna eda juu yao mtakyoihisabu. Hivyo wapeni cha kuwaliwaza na waacheni muachano mzuri.

Kabla ya kuwagusa ni kabla ya kuwaingilia. Cha kuwaliwaza kisharia ni kitu anachokitoa mtaliki akiwa hajamwingilia na hakutaja mahari yake. Ikiwa ametaja itakuwa ni wajibu kutoa nusu ya mahari. Tazama Juz. 2 (2:236 – 237).

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِنَّا أَحْلَلْنَا لَكَ أَزْوَاجَكَ اللَّاتِي آتَيْتَ أُجُورَهُنَّ وَمَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ مِمَّا أَفَاءَ اللَّـهُ عَلَيْكَ وَبَنَاتِ عَمِّكَ وَبَنَاتِ عَمَّاتِكَ وَبَنَاتِ خَالِكَ وَبَنَاتِ خَالَاتِكَ اللَّاتِي هَاجَرْنَ مَعَكَ وَامْرَأَةً مُّؤْمِنَةً إِن وَهَبَتْ نَفْسَهَا لِلنَّبِيِّ إِنْ أَرَادَ النَّبِيُّ أَن يَسْتَنكِحَهَا خَالِصَةً لَّكَ مِن دُونِ الْمُؤْمِنِينَ قَدْ عَلِمْنَا مَا فَرَضْنَا عَلَيْهِمْ فِي أَزْوَاجِهِمْ وَمَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ لِكَيْلَا يَكُونَ عَلَيْكَ حَرَجٌ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٠﴾

50. Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao, na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu, na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe, na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine. Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

تُرْجِي مَن تَشَاءُ مِنْهُنَّ وَتُؤْوِي إِلَيْكَ مَن تَشَاءُ وَمَنِ ابْتَغَيْتَ مِمَّنْ عَزَلْتَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيْكَ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن تَقَرَّ أَعْيُنُهُنَّ وَلَا يَحْزَنَّ وَيَرْضَيْنَ بِمَا آتَيْتَهُنَّ كُلُّهُنَّ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ مَا فِي قُلُوبِكُمْ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَلِيمًا ﴿٥١﴾

51. Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye. Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako. Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote. Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

لَّا يَحِلُّ لَكَ النِّسَاءُ مِن بَعْدُ وَلَا أَن تَبَدَّلَ بِهِنَّ مِنْ أَزْوَاجٍ وَلَوْ أَعْجَبَكَ حُسْنُهُنَّ إِلَّا مَا مَلَكَتْ يَمِينُكَ وَكَانَ اللَّـهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ رَّقِيبًا ﴿٥٢﴾

52. Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza; isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume. Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu.

TUMEKUHALALISHIA WAKE ZAKO

Aya 50 – 52

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya hii ametaja aina ya wanawake walio halali kwa Mtume(s.a.w. w ) na kumwachia hiyari ya kumlalia na kutomlalia anayemtaka. Kisha akamharamishia kuzidisha wale aliokuwa nao au kubadilisha mwingine. Wakati huo alikuwa na wake tisa. Ufuatao ni ufafanuzi:

Ewe Nabii! Hakika sisi tumekuhalalishia wake zako ambao umewapa ujira wao.

Makusudio ya ujira hapa ni mahari. Na kuwapa hayo mahari kunakuwa ni lazima. Aya inaashiria kuwa Mtume anaweza kuoa idadi yoyote anayoitaka. Haya ni katika mambo yanayomuhusu yeye tu.

Unaweza kuuliza : kufunga ndoa kunaswihi hata kama mahari hayakuta- jwa, kwa nini basi Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameufunga uhalali kwa mahari?

Jibu : Ulazima hapa ni wa kuyatoa hayo mahari sio kuyataja kwenye ndoa. Ikiwa mahari hayakutajwa kwenye ndoa, basi ni lazima kutoa mahari kifani; yaani yanayofana na mwingine wa aina yake. Mahari ya mtume, wakati huo, yalikuwa ni Dirhamu 500. wamekadiria Dirhamu moja kuwa ni sawa na Lira 25 za dhahabu.

Na uliowamiliki kwa mkono wako wa kuume katika aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka waliowatekwa nyara na waislamu kati- ka vita na washirikina, ambao wanaitwa masuria. Mwenyezi Mungu amemuhalishia Mtume wake na umma wake, wanawake hawa.

Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako waliohama pamoja nawe.

Unaweza kuuliza : Mabinti wa ami, wa shangazi, wajomba na wa khalat (dada wa mama) si wanaingia katika aina ya kwanza ya wanawake, sasa kuna haja gani ya kuhusishwa kutajwa?

Jibu : Inawezekana kuwa makusudio ya kutajwa ni kuwa inavyopendeza ni kuwa hadhi ya Mtume ni kuoa makuraishi aliohama nao kutoka mji wa ukafiri hadi mji wa Uislamu. Ama waumimi wengine ni bora kutowaoa.

Swali la pili : Watu wa sira wamesema kuwa Mtume alikuwa na ami tisa: Abbas, Hamza, Abu Twalib, Zabeir, Harith, Hijla, Muqawwam, Dhirar na Abu Lahab. Na shangazi sita: Swafiya, Ummu Hakim al-baydhau, Atika, Umayma, Arwa na Barra (Assiratu nnabaawiya cha Ibn Hisham).

Na wakasema: “Mtume hakuwa na wajomba wala khalat (mama wadogo au wakubwa), kwa sababu mama yake Amina bint Wahb(a.s) hakuwa na kaka wala dada.” (Tafsir Ruuhul-bayan).

Sasa kuna wajihi gani wa Mwenyezi Mungu kusema: ‘Na mabinti wa ami zako, na mabinti wa shangazi zako, na mabinti wa wajomba zako na mabinti wa khalat zako?’

Jibu : Makusudio ya wajomba na khalat wa Mtume ni ukoo wa mama yake unaoitwa Bani Zuhra, ambao walikuwa wakisema: “Sisi ni wajomba zake Mtume.”

Na mwanamke mumin akijitoa mwenyewe kwa Nabii ikiwa Nabii anataka kumuoa. Ni halali kwako wewe tu, si kwa waumini wengine.

Katika mambo yanayomuhusu Mtume tu ni kumuoa mwanamke, akitaka, ikiwa atajitoa mwenye kwa Mtume bila ya mahari, kwa masharti ya kuwa mumini. Ndio! Inajuzu kwa mwinginewe kuoa kwa mahari, kisha mke asamehe mahari, kama anavyosamehe mtu yoyote mali yake kwa mwingine.

Tunajua tuliyowafaradhishia wao kuhusu wake zao na wale waliomi- likiwa na mikono yao ya kuume. Ili isiwe dhiki juu yako. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Mwenyezi Mungu, ameweka idadi ya wake waungwana na akaharamisha mwanamke kujitoa mwenyewe bila mahari. Lakini akaliruhusu hilo kwa Mtume ili isiwe dhiki juu yake.

Vile vile kufahamisha utukufu wa cheo chake na juhudi zake. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye anayejua zaidi li lilo na masilahi zaidi kwa watu, akiwa anawahurumia na kuwaghufuria.

Unamwakhirisha umtakaye katika wao na na unamsogeza kwako umtakaye.

Katika Aya iliyotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) amempa uhuru Mtume wake mtukufu katika idadi ya wanawake na katika Aya hii amempa hiyari ya kuongeza au kupunguza zamu ya yeyote anayemtaka.

Na unayemtaka katika uliyemtenga si vibaya kwako.

Yaani anaweza kumrudia aliyemaliza zamu naye na kumwacha aliyekuwa kwenye zamu yake. Kwa ibara ya wanaoimudu lugha ni, anaweza kumtanguliza wa mwisho na kumweka mwisho wa kwanza.

Hivyo itakuwa ni karibu zaidi kuburudika macho yao wala wasihuzunike na wawe radhi juu ya kile unachowapa wao wote.

‘Hivyo’ ni huko kuachiwa hiyari Mtume(s.a.w.w) . Maana ni kuwa wao wakijua kuwa hiyari ni yako sio yao ya zamu sawa, basi kila mmoja ataridhia na vile utakavyokuwa kwake kwa siku kidogo au nyingi kwa kujua kuwa ziada hiyo imetokana na wewe wala si wajibu kwako. Pamoja na hayo, lakini Mtume alikuwa akikaa siku sawa baina ya wake zake.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyomo nyoyoni mwenu ya kupondokea zaidi kwa baadhi ya wake zenu kuliko wengine. Mwenyezi Mungu hayachukulii mapenzi yaliyo moyoni au chuki; isipokuwa anachukulia matendo. Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mpole.

Hawakuhalalikii wanawake baadaye wala kuwabadilisha kwa wake wengine, ijapo uzuri wao utakupendeza.

Wafasiri wametaja maana tatu za Aya hii; iliyo karibu zaidi na maana ya dhahiri ni ile isemayo kuwa Mwenyezi Mungu baada ya kumhalalishia Mtume wanawake aliowaishiria katika Aya iliyotangulia, amewajibisha katika Aya hii kutosheka na alio nao ambao walikuwa tisa na akaharamishiwa kumwacha yeyote katika wao na kuweka mwingine mahali pake, hata kama atakuwa amempendeza.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ijapo uzuri wao utakupendeza’ inafahamisha kuwa mwanamume anaruhusiwa kumwangalia mwanamke anayetaka kumuoa.

Na ndio mafakihi wakalitolea fatwa hilio kwa kutegemea Aya hii na Hadith za Mtume mtukufu(s.a.w. w ) .

Isipokuwa uliyemmiliki kwa mkono wako wa kuume, aliokupa Mwenyezi Mungu katika mateka.

Na Mwenyezi Mungu ni Mchungaji wa kila kitu, hata kilicho siri na kwenye dhamiri:

وَهُوَ مَعَكُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ ﴿٤﴾

“Naye yu pamoja nanyi popote mlipo.” (57:4).

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَدْخُلُوا بُيُوتَ النَّبِيِّ إِلَّا أَن يُؤْذَنَ لَكُمْ إِلَىٰ طَعَامٍ غَيْرَ نَاظِرِينَ إِنَاهُ وَلَـٰكِنْ إِذَا دُعِيتُمْ فَادْخُلُوا فَإِذَا طَعِمْتُمْ فَانتَشِرُوا وَلَا مُسْتَأْنِسِينَ لِحَدِيثٍ إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ يُؤْذِي النَّبِيَّ فَيَسْتَحْيِي مِنكُمْ وَاللَّـهُ لَا يَسْتَحْيِي مِنَ الْحَقِّ وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ ذَٰلِكُمْ أَطْهَرُ لِقُلُوبِكُمْ وَقُلُوبِهِنَّ وَمَا كَانَ لَكُمْ أَن تُؤْذُوا رَسُولَ اللَّـهِ وَلَا أَن تَنكِحُوا أَزْوَاجَهُ مِن بَعْدِهِ أَبَدًا إِنَّ ذَٰلِكُمْ كَانَ عِندَ اللَّـهِ عَظِيمًا ﴿٥٣﴾

53. Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo. Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki. Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao. Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

إِن تُبْدُوا شَيْئًا أَوْ تُخْفُوهُ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٥٤﴾

54. Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

لَّا جُنَاحَ عَلَيْهِنَّ فِي آبَائِهِنَّ وَلَا أَبْنَائِهِنَّ وَلَا إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ إِخْوَانِهِنَّ وَلَا أَبْنَاءِ أَخَوَاتِهِنَّ وَلَا نِسَائِهِنَّ وَلَا مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُنَّ وَاتَّقِينَ اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ شَهِيدًا ﴿٥٥﴾

55. Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

MKISHAKULA TAWANYIKENI

Aya 53 – 55

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Msiingie majumba ya Mtume ila mkipewa ruhusa ya kwenda kula, sio kungojea kiive. Lakini mtakapoitwa, basi ingieni. Na mkisha kula, tawanyikeni wala msiweke mazungumzo.

Yaani msikae kabisa si kwa mazungumzo wala kwa jambo jingine. Yametajwa mazungumzo kwa vile mara nyingi mtu anakaa kwa kupiga gumzo.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa baadhi ya maswahaba walikuwa wakiingia nyumba ya Mtume(s.a.w. w ) bila ya idhini kama ilivyo ada ya kijahiliya; na kwamba wakiona chakula kinapikwa basi wanakingoja na baada ya kula walikuwa wakipiga gumzo.

Hakuna mwenye shaka kwamba aina hii ya upuzi na kukosa adabu inamuudhi binadamu yeyote, awe Mtume au si Mtume. Ni kwa ajili hii Mtume(s.a.w. w ) aliwafundisha adabu mswahaba na wengineo kuwa wasiingie nyumba yoyote bila ya idhini ya wenyewe - hayo yamedokezwa kwenye Juz. 18 (24:28) – na kwamba wasiende kula ila wakiitwa, tena chakula kiwe kimeandaliwa na wakishamaliza kula wasingoje tena.

Haya hayahusiki na nyumba ya Mtume peke yake; isipokuwa Mwenyezi Mungu amemtaja yeye kwa vile ndio sababu ya kushuka Aya. Mara nyingi tumesema kuwa sababu ya kushuka Aya haiifungi na hilo lililoishukia.

Hakika hayo yanamuudhi Nabii, naye anawastahi nyinyi. Lakini Mwenyezi Mungu hastahi kwa haki.

Makusudio ya haki aliyokuwa akiistahi Mtume ni haki yake ya kiutu – kuwatoa wapuuzi nyumbani kwake. Mtume aliwanyamazia kwa kuwaonea haya; ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akatanabahisha kwamba kubaki kwao baada ya chakula kunamuudhi Mtume, vile vile kuingia kwao nyumbani kwake bila ya idhini yake.

Kuna Hadith isemayo: “Haya ni tawi la imani na asiyekuwa na haya hana dini.” Kuna Hadith nyingine isemayo:“Hakukubakia katika mifano ya mitume isipokuwa kauli ya watu: Kama huna haya basi fanya utakavyo.”

Katika maelezo ya wasifu wa Mtume(s.a.w. w ) ni kuwa yeye alikuwa na haya kuliko mwanamwali kwenye ushungi wake. Katika Nahjul-balagha imesemwa:“Hakuna imani kama haya na subira.” Farazdaq katika kumsifu Imam Zaynul-abdin anasema:

Hufumba macho kwa haya kwa haiba yake. Hazungumzi ila kuonekana tabasamu yake Maajabu ni yale yaliyoandikwa kwenye kitabu Muhadharatul-udabai cha Asfahaniy:

“Doezi mmoja alilaumiwa kwa kudoea kwake, akasema akijitetea: “Ala! Ikiwa bani Israil walimdoea Mungu, je sisi tusidoee watu?”

Na mnapowaomba chombo cha nyumbani, basi waulize ni nyuma ya mapazia. Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.

Yaani mnapowaomba haja wakeze Mtume. Kutaja chombo cha chumbani ni kutolea mfano tu, sio kuhusisha na kuondoa hukumu kwa vingine. Hilo linafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Hilo linasafisha zaidi nyoyo zenu na nyoyo zao.” Inayotambulisha kuwa kuchanganyika na kuondoa pazia baina ya wanawake na wanaume kunaleta ufisadi na fitna.

Maana yake ni kuwa kuchanganyika ni haramu, au angalau ni bora kuacha. Hapa inatubainikia kuwa kuchanganyika ni sababu ya kuleta matamanio ya kijinsiya, na wala sio kumtia adabu mwanamke na kumkandamiza; kama wanavyodai wale wasemao: “Mungu amesema hivyo na mimi nasema hivi” Ni nani aliye mkweli zaidi kwa mazungumzo kuliko Mwenyezi Mungu?

Haiwafalii nyinyi kumuudhi Nabii wala kuwaoa wake zake kabisa. Hakika hilo ni kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu.

Hukumu hii inamuhusu Mtume tu peke yake. Kwa sababu wakeze wako katika daraja ya mama wa waumini. Imeelezwa katika Tafsir Arrazi na Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy: “Hakika Aya hii ilishuka pale aliposema Twalha bin Abdallah Attaymiy:“Akifa Muhammad(s.a.w. w ) nitamuoa Aisha.”

Hilo linataliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Mkidhihirisha chochote au mkikificha, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Hilo ni karipio kwa yule aliyedhamiria kuoa wake za Mtume baada yake.

Hapana ubaya kwao kwa baba zao, wala watoto wao, wala kaka zao, wala watoto wa kaka zao, wala watoto wa dada zao, wala wanawake wao, wala wale waliomilikiwa na mikono yao ya kuume. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwenye kushuhudia kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuamrisha kuzungumza na wanawake nyuma ya pazia (hijabu) hapa anavua wale ambao hawawezi kuoana nao, ambao ni: baba, mtoto, kaka, mtoto wa kaka na mtoto wa dada, mtumwa na wanawake. Lakini Mwenyezi Mungu amesema wanawake wao, yaani wanawake wenzao walio waumini, kwa sababu wasiokuwa waumini watawasifia wanaume zao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (24:31).

إِنَّ اللَّـهَ وَمَلَائِكَتَهُ يُصَلُّونَ عَلَى النَّبِيِّ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا صَلُّوا عَلَيْهِ وَسَلِّمُوا تَسْلِيمًا ﴿٥٦﴾

56. Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeami- ni! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

إِنَّ الَّذِينَ يُؤْذُونَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ لَعَنَهُمُ اللَّـهُ فِي الدُّنْيَا وَالْآخِرَةِ وَأَعَدَّ لَهُمْ عَذَابًا مُّهِينًا ﴿٥٧﴾

57. Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

وَالَّذِينَ يُؤْذُونَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ بِغَيْرِ مَا اكْتَسَبُوا فَقَدِ احْتَمَلُوا بُهْتَانًا وَإِثْمًا مُّبِينًا ﴿٥٨﴾

58. Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

MSWALIENI MTUME

Aya 56 – 58

MAANA

Hakika Mwenyezi Mungu na malaika wake wanamswalia Nabii. Enyi ambao mmeamini! Mswalieni na mumsalimu kwa salamu.

Makusudio ya Mwenyezi Mungu kumsalia Mtume ni kumridhia kumrehe- mu na kumsifu kwa kila kheri, swala ya malaika ni kumsifu, na kutoka kwa waumini ni kumwombea dua ya kuwa na daraja ya juu. Imam Ar-Ridha(a.s) aliulizwa kuhusu maana ya kauli ya Mwenyezi Mungu: malaika na waumini humswalia Mtume, akasema:“Swala kutoka kwa Mwenyezi Mungu ni rehema, kutoka kwa malaika ni kumsifu na kutoka kwa waumni ni kumwombea.”

Kuswaliwa huku hakuhusiki na risala ya Muhammad(s.a.w. w ) peke yake. Kila mtu anayetumia desturi ya risala ya Muhammad(s.a.w. w ) , kuifundisha au kuijulisha au kutaja fadhila yoyote katika fadhila zake basi atakuwa amemswalia, awe mumin au sio mumin, akitaka hilo au asitake.

Imam Ja’far As-Sadiq(a.s) anasema: “Mtu kumswalia Muhammad(s.a.w. w ) ni kama kusema:“Subhanallah walhamdulillah walailaha illaha wallahu akbar” (Kutakasika ni kwa Mwenyezi Mungu na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu na hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mkubwa).

Imam hapa anakusudia kuwa thawabu za kumswalia Mtume ni sawa na thawabu za tasbih, tahmid, tahlil na takbir. Imepokewa Hadith kutoka kwa Mtume mtukufu(s.a.w. w ) , amesema:“Bakhili wa kweli ni yule ambaye nikitajwa mbele yake haniswalii” .

VIPI TUTAMSWALIA MTUME?

Katika Sahih Al-Bukhariy Juz. 8, mlango wa kumswalia mtume, Tafsir At- Tabariy, Tafsir Ar-Raziy, Tafsir Al-Maraghi na wafasiri wengineo, pia katika vitabu vya Hadith, kuna maelezo haya: “Mtume aliulizwa: Vipi tutakuswalia ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu?Akasema: semeni:

Allahumma swalli a’la muhammdi wa a’la aali Muhammad, kama swal-layta a’la Ibrahima wa a’laa aali Ibrahim, Innaka hamidum majiid Allahumma barik ala muhammdi wa a’la ali Muhammad, kama barakta a’la Ibrahima wa a’la ali Ibrahim, Innaka hamidum majid.

(Ewe Mwenyezi Mungu mswalie Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyomswalia Ibrahim na kizazi cha Ibrahim, hakika wewe ni mwenye kusifiwa mwenye kutukuzwa. Ewe Mwenyezi Mungu mbariki Muhammad na kizazi cha Muhammad, kama ulivyombariki Ibrahim na kizazi cha Ibrahim. Hakika wewe ni Mwenye kusifiwa Mwenye kutukuzwa. )

Katika tafsir Ruhul-bayan ya Ismail Haqiy, amesema: “Inatakikana mwenye kuswali aseme: Allhumma swali a’la Muhammad wa a’la AliMuhammad” kwa kulirudia neno ‘a’la’; kwani Sunni wanaweka neno hilo kabla ya aali, kuwapinga Shia ambao hawaliweki neno hilo.

Sisi hatuoni tofauti yoyote baina ya anayesema: neno hilo na asiyelisema. Ama kuhusu ile Hadith isemayo:“Mwenye kutenganisha baina yangu na kizazi changu, hatapata shafaa yangu,” Mwenyezi Mungu ndiye anayejua zaidi usahihi wake.

Imam Shafii naye amesema katika shairi lenye maana hii: Enyi watu wa nyumba ya Mtume pendo lenu ni faradhi kutoka kwa Mwenyezi Mungu amelieleza katika Qur’an. Inawatosha kuwa ni cheo kikuu kwamba nyinyi asiyewaswalia hana Swala

Hakika wale ambao wanamuudhi Mwenyezi Mungu na Mtume wake Mwenyezi Mungu amewalaani duniani na Akhera, na amewaandalia adhabu ya kufedhehesha.

Makusudio ya kumuudhi Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kumghadhabisha, na sababu yenye kuwajibisha hilo ni kumpinga, kumnasibishia mshirika au mtoto, au kuasi hukumu miongoni mwa hukumu zake. Na kuumuudhi Mtume(s.a.w. w ) ni kupinga utume wake au kupuuza mwenendo wake.

Laana kutoka kwa Mungu ni kwa kuwekwa mbali na rehema yake na kutoka kwa watu ni shutuma na kuombewa mabaya. Katika Nahjul-balagha imeelezwa:“Mwenyezi Mungu amewalaani wanaoamrisha mema na kuacha kuyatenda na wanaokataza maovu na wanayoyatenda.”

Na wale ambao wanawaudhi waumini wanaume na waumini wanawake pasi na wao kufanya, hakika wamebeba dhulma kubwa na dhambi kubwa.

Pasi na wao kufanya, yaani kufanya kosa linalostahili udhia. Kuudhi kunakuwa ni kwa kusengenya, vitimbi, uzushi n.k. Kuna Hadith zisemazo:

“Mwislamu ni yule ambaye watu wamesalimika na mkono wake na ulimi wake.”

“Utukufu wa mumin ni kwa kujizuia na kuwaudhi watu.”

“Aliye dhalili zaidi katika watu ni yule anayewadharau watu.”

Imam Ali(a.s) anasema: Mwenye hali mbaya zaidi katika watu ni yule asiyemwaamini yeyote kwa dhana zake mbaya, na asiyeaminiwa na yeyote kwa vitendo vyake vibaya.”

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ قُل لِّأَزْوَاجِكَ وَبَنَاتِكَ وَنِسَاءِ الْمُؤْمِنِينَ يُدْنِينَ عَلَيْهِنَّ مِن جَلَابِيبِهِنَّ ذَٰلِكَ أَدْنَىٰ أَن يُعْرَفْنَ فَلَا يُؤْذَيْنَ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥٩﴾

59. Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie jalbab zao. Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

لَّئِن لَّمْ يَنتَهِ الْمُنَافِقُونَ وَالَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْمُرْجِفُونَ فِي الْمَدِينَةِ لَنُغْرِيَنَّكَ بِهِمْ ثُمَّ لَا يُجَاوِرُونَكَ فِيهَا إِلَّا قَلِيلًا ﴿٦٠﴾

60. Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

مَّلْعُونِينَ أَيْنَمَا ثُقِفُوا أُخِذُوا وَقُتِّلُوا تَقْتِيلًا ﴿٦١﴾

61. Wamelaaniwa! Popote waonekanapo, na wakamatwe na wauliwe kabisa.

سُنَّةَ اللَّـهِ فِي الَّذِينَ خَلَوْا مِن قَبْلُ وَلَن تَجِدَ لِسُنَّةِ اللَّـهِ تَبْدِيلًا ﴿٦٢﴾

62. Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

WAJIBU WA HIJABU

Aya 59 – 62

LUGHA

Kuna kauli nyingi kuhusu neno Jalbab: kuna wanaosema kuwa ni nguo inayomfunika mwanamke kutoka kichwani hadi nyayoni. Wengine wakasema ni ushungi unaofunika kichwa cha mwanamke na uso wake. Kauli hii ndio aliyo nayo mwenye Majmaul-Bayan.

MAANA

Zimekwishatangulia Aya mbili zinazofahamisha wajibu wa hijabu kwa wanawake:

Ya kwanza ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Wala wasidhihirishe uzuri wao ila kwa waume zao.” Juz. 18 (24: 31). Ya pili ni ile Aya ya 53, katika Sura hii tuliyo nayo: “Na mnapowaomba chombo cha nyum- bani, basi waulizeni nyuma ya mapazia.”

Aya iliyo wazi zaidi ya hizi mbili ni hii tuliyo nayo, isemayo:

Ewe Nabii! Waambie wake zako na wake za waumini, wajiteremshie nguo zao.

Kusema kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘wajiteremshie nguo zao’ inaenea kusitiri na kufunika sehemu zote za mwili, kikiwemo kichwa na uso. Hilo linatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana wasiudhiwe.

Waislamu, mwanzoni walikuwa wakitoka bila ya kujitanda, kama ilivyokuwa desturi ya kijahiliya, ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamtaka Mtume wake mtukufu, katika Aya hii, awaamrishe wake zake kujisitiri na kuvaa hijabu. Na amri inafahamisha wajibu. Kwa hiyo hijabu ni wajibu.

Hata hivyo uso na viganja viwili havimo kwenye wajibu huu, kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَلَا يُبْدِينَ زِينَتَهُنَّ إِلَّا مَا ظَهَرَ مِنْهَا ﴿٣١﴾

“Wala wasionyeshe uzuri wao, isipokuwa unaodhihirika.” Juz. 18 (24:31).

Hilo ni karibu zaidi kuweza kujulikana kutokana na kujistahi na kujichunga. Kwani hijabu ni kinga baina ya mwanamke na tamaa ya watu wenye shakashaka na mafasiki,wasiudhiwe kwa kuangaliwa na mafasiki.

Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Anasamehe yaliyopita na anamuhurumia mwenye kutubia na kurejea nyuma.

Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao, na wale wanaoeneza fitna Madina, hawataacha, basi kwa yakini tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda mchache tu.

Wanafiki walificha ukafiri na wakadhihirisha imani. Wanaoeneza fitna ni watu katika wananfiki waliokuwa wakieneza propaganda dhidi ya Mtume(s.a.w. w ) na maswahaba na wakawatia shaka wale wadhaifu wa imani ambao Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewaletea ibara ya wenye mardhi nyoyoni mwao. Aya inatoa onyo la kuuawa na kufukuzwa wanafiki, waeneza fitna na wale watakaowasikiliza, ikiwa hawatajizuia na upotevu na ufisadi wao.

VITA VYA NAFSI

Siku hizi kueneza fitna kunaitwa ‘vita vya nafsi.’ Nguvu ya shari imetafuta njia nyingi sana za kueneza uongo na mambo ya ubatilifu kwa kila nyenzo. Kuanzia magazeti, radio, runinga, sinema, hotuba, vipeperushi, shule, vyuo, vitabu n.k.

Vyombo hivi vimekaririka masikioni mwa watu kila siku, kiasi ambacho uhakika haupati nafasi kwa watu na wenye ikhlasi, isipokuwa kwa mwamko mkamilifu na elimu itakayotangulia propaganda za wakoloni na wazayuni.

Nimesoma kwenye gazeti linaloitwa Akhabar Al-yawm la Misr, la 13/12/69, kwamba Israil ina magazeti ya propaganda yanayofikia 890 ulimwenguni kwa ajili ya kueneza habari za uongo. Zaidi ya hayo wametawala vyombo vingi vya habari ulimwenguni, kwa njia isiyokuwa ya moja kwa moja; kama vile runinga, radio n.k.

Kwenye mahisabu haya hayaingii magazeti ya Beiruti yenye uhusiano mkubwa na wakoloni na wazayuni.

Kwa vyovyote iwavyo, Alhamdu lillah, Israil imehisi mapigo kutoka kwa waarabu na kwamba propaganda zao zilizotengenezwa na Marekani, na kutangazwa na vibaraka, zimeanza kujulikana.

Wamelaaniwa! Popote waonekanapo na wakamatwe na wauliwe kabisa.

Wamelaaaniwa na kila ulimi, kwa sababu dini yao ni pesa na matendo yao ni udanganyifu, uwongo na hadaa. Hawana dawa isipokuwa kuuawa popote walipo; kama kiungo kilichoharibika, kisipokatwa kitaharibu mwili wote.

Ni desturi ya Mwenyezi Mungu iliyokuwa kwa wale waliopita zamani. Wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

Makusudio ya desturi ya Mwenyezi Mungu hapa ni hukumu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa mpotevu anayepoteza, ambayo ni kuuliwa ambako amekuwekea sharia, ambaye imetukuka hekima yake, tangu zamani. Hukumu hii itabakia milele bila ya mabadiliko wala mageuzi.

يَسْأَلُكَ النَّاسُ عَنِ السَّاعَةِ قُلْ إِنَّمَا عِلْمُهَا عِندَ اللَّـهِ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّ السَّاعَةَ تَكُونُ قَرِيبًا ﴿٦٣﴾

63. Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

إِنَّ اللَّـهَ لَعَنَ الْكَافِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمْ سَعِيرًا ﴿٦٤﴾

64. Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka.

خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا لَّا يَجِدُونَ وَلِيًّا وَلَا نَصِيرًا ﴿٦٥﴾

65. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru.

يَوْمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمْ فِي النَّارِ يَقُولُونَ يَا لَيْتَنَا أَطَعْنَا اللَّـهَ وَأَطَعْنَا الرَّسُولَا ﴿٦٦﴾

66. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

وَقَالُوا رَبَّنَا إِنَّا أَطَعْنَا سَادَتَنَا وَكُبَرَاءَنَا فَأَضَلُّونَا السَّبِيلَا ﴿٦٧﴾

67. Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia.

رَبَّنَا آتِهِمْ ضِعْفَيْنِ مِنَ الْعَذَابِ وَالْعَنْهُمْ لَعْنًا كَبِيرًا ﴿٦٨﴾

68. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَكُونُوا كَالَّذِينَ آذَوْا مُوسَىٰ فَبَرَّأَهُ اللَّـهُ مِمَّا قَالُوا وَكَانَ عِندَ اللَّـهِ وَجِيهًا ﴿٦٩﴾

69. Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

WANAKUULIZA KUHUSU SAA

Aya 63 – 69

MAANA

Watu wanakuuliza kuhusu Saa. Sema: Ujuzi wake uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Na nini kitakachokujulisha? Pengine hiyo saa iko karibu.

Makusudio ya saa ni Kiyama Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:187).

Hakika Mwenyezi Mungu amewaandalia makafiri moto unaowaka. Watadumu humo milele. Hawatapata mlinzi wala wa kuwanusuru. Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungelimtii Mwenyezi Mungu na tungelimtii Mtume!

Makafiri na waasi kesho watasukumwa kwenye adhabu ya moto, hawatakuwa na msaidizi wala udhuru. Watauma vidole vyao kwa kujutia walivyomuasi Mwenyezi Mungu na Mtume, lakini ‘majuto ni mjukuu.’

Umetangulia mfano wake katika Juz. 19 (25:27).

Na watasema: Mola wetu! Hakika sisi tuliwatii mabwana zetu na wakubwa wetu, wakatupoteza njia. Mola wetu wape adhabu mara mbili, na walaani laana kubwa.

Makusudio ya mabwana na wakubwa ni viongozi wa dini na dunia. Laana ni kufedheheka. Wadhaifu watawageuzia adhabu na watamtaka Mwenyezi Mungu awaongezee adhabu.

Mwenye kuichunguza historia ataona kwamba aghlabu umma wa kijinga unaongozwa na mataghuti na waovu. Lakini watu wenye mwamko na maarifa hawaamini kuweka masilahi yao isipokuwa kwa waaminifu wenye ikhlasi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:38).

Enyi ambao mmeamini! Msiwe kama wale ambao walimuudhi Musa, lakini Mwenyezi Mungu akamtaksa na waliyoyasema; naye alikuwa ni mwenye heshima mbele ya Mwenyezi Mungu.

Waliomuudhi Musa(a.s) ni Wana wa Israil, hilo halina shaka; ambapo walimsifu sifa zisizokuwa za mitume.

Aya hii inaashiria kwamba badhi ya swahaba walimuudhi Mtume mtukufu(s.a.w.w) na wakambandika mambo asiyokuwa nayo, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawakataza waislamu hilo.

Kuna riwaya inayosema kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) siku moja aliapa, basi mtu mmoja katika Answar akasema: “Kiapo hiki hakikusudiwa radhi ya Mwenyezi Mungu.” Hapo uso wa Mtume ukaiva wekundu na akasema:“Amrehemu Musa, hakika aliudhiwa zaidi ya hivi na akasubiri.”

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ وَقُولُوا قَوْلًا سَدِيدًا ﴿٧٠﴾

70. Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa.

يُصْلِحْ لَكُمْ أَعْمَالَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَمَن يُطِعِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ فَازَ فَوْزًا عَظِيمًا ﴿٧١﴾

71. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu. Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

إِنَّا عَرَضْنَا الْأَمَانَةَ عَلَى السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَالْجِبَالِ فَأَبَيْنَ أَن يَحْمِلْنَهَا وَأَشْفَقْنَ مِنْهَا وَحَمَلَهَا الْإِنسَانُ إِنَّهُ كَانَ ظَلُومًا جَهُولًا ﴿٧٢﴾

72. Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanadamu akaichukua. Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana,

لِّيُعَذِّبَ اللَّـهُ الْمُنَافِقِينَ وَالْمُنَافِقَاتِ وَالْمُشْرِكِينَ وَالْمُشْرِكَاتِ وَيَتُوبَ اللَّـهُ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٧٣﴾

73. Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na washirikina wanaume na washirikina wanawake; na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

TULIZITOLEA AMANA

Aya 70 – 73

MAANA

Enyi ambao mmeamini! Mcheni Mwenyezi Mungu na semeni kauli ya sawa. Atawatengenezea matendo yenu na atawaghufiria dhambi zenu.

Kauli ya sawa ni kusema haki na ukweli, bila ya kuficha kitu; hata kama inamuhusu mwenyewe. Makusudio yake hapa ni ile inayowanufaisha watu kwa kulinganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu ‘Atawatengenezea amali zenu;’ ambapo Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejaalia kauli ya haki ni sababu ya matendo mema; kwa mfano kumwongoza aliyepotea kwenye njia ya heri na amani, kumsaidia aliyedhulumiwa kwa neno la usawa au kauli ambayo italeta suluhu baina ya watu wawili na mengineyo yanay- owanufaisha watu kwa namna moja au nyingine.

Na mwenye kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake, hakika amefuzu kufuzu kukubwa.

Atafuzu duniani kwa kufaulu na kuwa na sera nzuri na katika Akhera atafuzu kwa kupata radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu zake.

Kwa hakika tulizitolea amana mbingu na ardhi na milima na vikakataa kuichukua na vikaiogopa, lakini mwanaadamu akaichukua.

Wafasiri wametofautiana kuhusu maana ya amana. Kuna waliosema kuwa ni taklifa na twaa. Wengine wakasema ni tamko la Lailaha illahha (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu). Kuna waliosema ni viungo vya mwanadamu; kama masikio yake, macho yake, mikono yake na miguu yake. Kwamba ni juu yake kuvitumia kwa ajili ya lengo lilioumbiwa. Pia kuna wale waliosema kuwa ni amana katika mali.

Tuonavyo sisi maana yake ni kujitolea muhanga kwa ajili ya manufaa ya jamii, si kwa lololote isipokuwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na ya ubinadamu.

Kwa sababu kujitolea huku ni kuzito na kukubwa kiasi ambacho maumbile yenye nguvu zaidi, kama mbingu, ardhi na majabali yangelikataa kubeba, kama yangelikuwa na hisia.

Kwa hiyo lengo la kutaja mbingu na ardhi ni kuashiria ukubwa wa kuji- tolea huku, na kwamba binadamu ni kiumbe pekee anayeweza kupingana na nafsi yake na matamanio yake.

Ama kauli yake Mwenyezi Mungu:Hakika yeye ni dhalimu mkubwa, mjinga sana, maana yake ni kuwa binadamu atajidhulumu yeye mwenyewe na mwingine ikiwa ataifanyia hiyana amana hii na kutojua mwisho muovu utakotokana na hiyana yake hiyo.

Ili Mwenyezi Mungu awaadhibu wanafiki wanaume na wanafiki wanawake ambao wanajionyesha kuwa wanatekeleza amana, lakini kumbe ni wahaini.

Na washirikina wanaume na washirikina wanawake. Mwenyezi Mungu atawaadhibu kwa vile kosa la ushirikina haliwezi kufutwa hata na kujitolea muhanga.

Na awapokelee toba waumini wanaume na waumini wanawake. Na Mwenyezi Mungu ni mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Yaani anawaghufiria wenye kutubia na kuwahurumia wanyonge. Ewe Mwenyezi Mungu mrehemu Muhammad na kizazi chake, rehema ambayo atatuombea nayo siku tutakapohitajia.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA TATU: SURAT AL-AHZAB


4

5

6

7