TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA42%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 11910 / Pakua: 4676
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ مُوسَىٰ إِنَّهُ كَانَ مُخْلَصًا وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥١﴾

51. Na mtaje Musa katika Kitabu, hakika yeye alikuwa ni Mwenye kutakaswa na alikuwa Mtume Nabii

وَنَادَيْنَاهُ مِن جَانِبِ الطُّورِ الْأَيْمَنِ وَقَرَّبْنَاهُ نَجِيًّا ﴿٥٢﴾

52. Na tulimwita upande wa kuume wa Tur na tukamkurubisha kunong’ona naye.

وَوَهَبْنَا لَهُ مِن رَّحْمَتِنَا أَخَاهُ هَارُونَ نَبِيًّا ﴿٥٣﴾

53. Na tukampa kutokana na rehema zetu nduguye, Haruna, awe Nabii

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِسْمَاعِيلَ إِنَّهُ كَانَ صَادِقَ الْوَعْدِ وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥٤﴾

54. Na mtaje katika Kitabu, Ismail, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii.

وَكَانَ يَأْمُرُ أَهْلَهُ بِالصَّلَاةِ وَالزَّكَاةِ وَكَانَ عِندَ رَبِّهِ مَرْضِيًّا ﴿٥٥﴾

55. Na alikuwa akiwaamrisha watu wake swala na zaka na alikuwa mbele ya Mola wake mwenye kuridhiwa.

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِدْرِيسَ إِنَّهُ كَانَ صِدِّيقًا نَّبِيًّا ﴿٥٦﴾

56. Na mtaje katika Kitabu, Idris, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii

وَرَفَعْنَاهُ مَكَانًا عَلِيًّا ﴿٥٧﴾

57. Na akamwinua mahali pa juu

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مِّنَ النَّبِيِّينَ مِن ذُرِّيَّةِ آدَمَ وَمِمَّنْ حَمَلْنَا مَعَ نُوحٍ وَمِن ذُرِّيَّةِ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْرَائِيلَ وَمِمَّنْ هَدَيْنَا وَاجْتَبَيْنَا إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُ الرَّحْمَـٰنِ خَرُّوا سُجَّدًا وَبُكِيًّا ﴿٥٨﴾

58. Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha miongoni mwa manabii katika uzao wa Adam na katika wale tuliowapandisha pamoja na Nuh na katika uzao wa Ibrahim na Israil na katika wale tuliowaongoa na tukawateua. Wanaposomewa Aya za Mwingi wa rehema huanguka kusujudu na kulia.

MUSA, ISMAIL NA IDRIS

Aya 51-58

MAANA

Na mtaje Musa katika Kitabu, hakika yeye alikuwa ni Mwenye kutakaswa na alikuwa Mtume Nabii.

Neno kutakaswa limefasiriwa kutokana na neno mukhlaswa kwa maana ya kuwa Mwenyezi Mungu amemtakasa na kila lisilopendeza na akamteua Yeye Mwenyewe. Ikiwa litasomwa, Mukhliswa, litakuwa na maana yakuwa kauli za Musa na vitendo vyake vyote ni vya ikhlasi.

Maana ya Mtume na Nabii ni moja, tofauti iko katika matamshi. Mtume au Mjumbe kwa kuwa anachukua ujumbe wa Mungu na Nabii (lenye maana ya kuzindua na kutoa habari), kwa maana ya kuwa anawazindua na kuwapa habari wale anaowapelekea ujumbe.

Wengine wamesema kuwa Mtume ni yule anayepokea wahyi na kuufikisha na Nabii ni yule anayepokea wahyi tu, lakini haufikishi, Utafiti huu hauna faida yoyote.

Na tulimwita upande wa kuume wa Tur na tukamkurubisha kunong’ona naye.

Tur ni mlima ambao Mwenyezi Mungu alizungumza na Musa. Makusudio ya kuumeni ni kuumeni kwa Musa; Kwa sababu mlima hauna kuume wala kushoto.

Makusudio ya kuumkurubisha kunong’na naye, ni kumkurubisha kihadhi sio ukaribu wa mahali. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu alimtukuza Musa kwa unabii na utume na kuzungumza naye moja kwa moja bila ya kuweko mjumbe mwengine.

Maneno yalikuwa yakimjia Musa kuumeni kwake; kama vile watu walivyo na mazoweya ya kusema: Nimesikia sauti kuumeni kwangu au kushotoni mwangu.

Na tukampa kutokana na rehema zetu nduguye, Haruna, awe Nabii

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anaashiria, kwa Aya hii, jambo lilokwishapita, nalo ni kuwa Mwenyezi Mungu alipomwamrisha Musa kwenda kwa Firauni, Musa alimuomba Mwenyezi Mungu kwa kusema: Na nipe waziri katika watu wangu, Harun ndugu yangu, niongeze nguvu zangu kwaye (20:30)

KUTEKELEZA AHADI

Na mtaje katika Kitabu, Ismail, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii. Na alikuwa akiwaamrisha watu wake swala na zaka na alikuwa mbele ya Mola wake mwenye kuridhiwa.

Maana yako wazi haihitajiki tafsiri, Ni jambo zuri tukizungumzia ahadi kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu: “Alikuwa ni mkweli wa ahadi” Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu Ismail kwamba yeye anapoahidi kitu hutekeleza.

Wafasiri wamesema kuwa Ismail siku moja aliahidiana na sahibu yake amngojee mahali, Yule mtu akachelewa, akamngoja siku tatu au zaidi.

Ni sawa riwaya hii iwe sahihi au la, lakini inaonyesha kwamba ni juu ya mtu kufanya bidii, kadiri atakavyoweza kutekeleza ahadi yake.

Na kwamba atakayeacha ahadi, haifai kumwamini na kitu chochote; bali inafaa tumpe sifa ya urongo na udanganyifu; hata kama kutekeleza ahadi kuna hasara ya kimaada, kwa sababu hasara ya kidini ni kubwa zaidi.

Kuna riwaya inayosema kuwa kutekeleza ahadi ni katika alama ya dini na kwamba dini ni maingiliano. Kuna kauli mashuhuri inayosema: ‘Asiyekuwa na ahadi hana dini’

Nimesoma maneno kuhusu ahadi nikaokota baadhi yake kama ifuatavyo:-

• “Mwenye kuacha ahadi kwa sababu ya matatizo atakuwa anajaribu kukikmbia kujituhumu, lakini hali halisi itamtuhumu.

• Kutekeleza ahadi ni tamko zuri katika masikio na ni zuri katika maisha.

• Makusudio ya kutekeleza ahadi nikuwatekelezea ahadi watu wa nyum- bani na marafiki na kuitumikia nchi na mwisho kwa watu wote.

• Utekelezaji ahadi unakufanya upende maisha na kuhalifu kunakufanya uchukie maisha.

• Maana ya kutekeleza ahadi kwa ajili ya watu wa nyumbani na marafiki ni kufanya kazi kwa ajili yao bila ya malipo na kutekeleza ahadi kwa ajili ya nchi ni kujitolea muhanga”

Na mtaje katika Kitabu, Idris, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii Mwenyezi Mungu amemsifu kwa ukweli na utume na akamwinua mahali pa juu.

Makusudio ya mahali hapa ni cheo. Imesekana kuwa Mwenyezi Mungu alimwinua mpaka mbingu ya nne, wengine wakasema ni ya saba, kwa kudhania tu. Katika tafsiri imeelezwa kuwa Idris ni babu wa baba yake Nuh, na kwam- ba yeye ndiye wa kwanza kushona nguo, kuandika kwa kalamu, kuangalia nyota na taaluma ya hisabu, Hatujui wafasiri wameyatoa wapi haya.

Mwanafasihi mashuhuri aitwayeTawfiki amandika tamthilia aliyoiita Izyis, Akasema kuwa Izyis huyu ndiye mke wa Ozyrys ambaye aliteswa na mfalme Typhoon. Ikasemekana kuwa Ozyrys huyu ndiye Idris aliyeashiri- wa na Qur’an. Lakini kauli zote hizi ni mawazo na hisia tu.

Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha miongoni mwa manabii katika uzao wa Adam na katika wale tuliowapandisha pamoja na Nuh na katika uzao wa Ibrahim na Israil na katika wale tuliowaongoa na tukawateua. Wanaposomewa Aya za Mwingi wa rehema huanguka kusujudu na kulia.

Amesema Razi na Tabrasiy: makusudio ya kizazi cha Adam ni Idris, kwa sababu yeye ndiye aliyewatangulia wote na yuko karibu zaidi na Adam kuliko Nuh.

Makusudio ya kizazi cha waliopandishwa pamoja na Nuh ni Ibrahim, kwa sababu yeye ni katika kizazi cha Sam. Makusudio ya kizazi cha Ibrahim ni Is-haq, Ismail, na Ya’qub, Israil ndiye Ya’qub. Miongoni mwa kizazi chake ni Musa, Harun, Zakariya, Yahya na Isa kwa upande wa mama.

Wote hao na wengineo ni wale aliwaongoza Mwenyezi Mungu na kuwateua kwa utume, wanamnyenyekea Mwenyezi Mungu na kuhofia ghadhabu yake na adhabu yake pamoja na kuwa wao wanamfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu na kutenda kwa amri yake. Basi inatakikana yule mwenye kujasiri kumuasi Mungu atubie na ahisi hofu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

فَخَلَفَ مِن بَعْدِهِمْ خَلْفٌ أَضَاعُوا الصَّلَاةَ وَاتَّبَعُوا الشَّهَوَاتِ فَسَوْفَ يَلْقَوْنَ غَيًّا ﴿٥٩﴾

59. Wakafuata baadae wazawa wabaya walioiacha swala na wakafuata matamanio. Basi watakujakuta malipo ya ubaya

إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ وَلَا يُظْلَمُونَ شَيْئًا ﴿٦٠﴾

60. Ispokuwa waliotubu, wakaamini na wakatenda mema, Hapo basi wataingia (Bustani) Peponi wala hawatadhulumiwa chochote.

جَنَّاتِ عَدْنٍ الَّتِي وَعَدَ الرَّحْمَـٰنُ عِبَادَهُ بِالْغَيْبِ إِنَّهُ كَانَ وَعْدُهُ مَأْتِيًّا ﴿٦١﴾

61. Bustani za milele ambazo Mwingi wa rehema aliwaahidi waja wake kwa ghaibu, Hakika Yeye ahadi yake itafika.

لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا إِلَّا سَلَامًا وَلَهُمْ رِزْقُهُمْ فِيهَا بُكْرَةً وَعَشِيًّا ﴿٦٢﴾

62. Hawatasiki humo upuuzi isipokuwa salama tu na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni

تِلْكَ الْجَنَّةُ الَّتِي نُورِثُ مِنْ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيًّا ﴿٦٣﴾

63. Hiyo ndiyo Bustani (Pepo) tutakayowarithisha katika waja wetu waliokuwa na takua

وَمَا نَتَنَزَّلُ إِلَّا بِأَمْرِ رَبِّكَ لَهُ مَا بَيْنَ أَيْدِينَا وَمَا خَلْفَنَا وَمَا بَيْنَ ذَٰلِكَ وَمَا كَانَ رَبُّكَ نَسِيًّا ﴿٦٤﴾

64. Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu na yaliyoko baina ya hayo, Na Mola wako si mwenye kusahau.

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴿٦٥﴾

Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake. Basi muabudu Yeye na uwe na subira kwa ibada yake, Je, unamjua somo yake?

WAKAJA BAADA YAO WALIO WABAYA

Aya 59 – 65

MAANA

Wakafuata baadae wazawa wabaya walioiacha swala na wakafuata matamanio.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwataja Mitume watakatifu, anaashiria waovu waliowafuatilia, akawapa wasifu wa kuwacha ibada ya mwingi wa rehema na kumfuata shetani. Maana haya yanafupika kwenye ibara hii: ‘Bora ni waliopita, wabaya ni waliokuja’

Basi watakujakuta malipo ya ubaya, Shari na adhabu ikiwa ni malipo ya maasi yao na inadi yao.

Ispokuwa waliotubu, wakaamini na wakatenda mema, Hapo basi wataingia Bustani (Peponi) wala hawatadhulumiwa chochote.

Tafsiri nzuri ya Aya hii ni kauli ya Mtume mtukufu(s.a.w.w) :“Mwenye kutubia dhambi ni kama asiye na dhambi” , Umetangulia mfano wake katika Juz; 7 (6:54).

Bustani za milele, Zipo daima, neema yake haikatiki wala hakimwi mkaaji wake.

Ambazo Mwingi wa rehema aliwaahidi waja wake kwa ghaibu.

Makusudio ya waja wake hapa ni waumini wenye ikhlasi. Kwa ghaibu ni kuwa wao waliamini Pepo ikiwa iko ughaibuni, Mwenyezi Mungu ame- wasifu waumini kuwa wanaoamini ghaibu katika Aya kadhaa.

Hakika Yeye ahadi yake itafika.

Yaani Mwenyezi Mungu havunji ahadi.

Hawatasikia humo upuuzi isipokuwa salama tu na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni.

Katika maisha ya dunia ni upuuzi uwongo na matusi, lakini Peponi ni kauli njema na riziki isiyokoma. Asubuhi na jioni ni fumbo la kudumu, kwa sababu Peponi hakuna asubuhi wala jioni.

Hiyo ndiyo Pepo tutakayowarithisha katika waja wetu waliokuwa na takua.

Neni ‘tutawarithisha’ linatambulisha kuwa Pepo ni ya wenye takua. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Hao ndio warithi ambao watarithi Firdausi. Humo watadumu” (23: 11)

Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu na yaliyoko baina ya hayo.

Katika Tafsiri Tabariy na Tabrasi, imeelezwa kwamba wahyi ulichelewa kushuka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Aliposhuka Jibril, Mtume akamuuliza ni lipi lililokuzuia hata usitutembelee mara kwa mara, kama ulivyokuwa ukifanya? Ikashuka Aya hii, dhahiri yake inaafikiana na Aya hii, hasa kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na Mola wako si mwenye kusahau.

Maana ni kuwa amri ya kuteremshwa wahyi ni ya Mwenyezi Mungu peke yake. Yeye ndiye mmiliki wa kila kitu na ujuzi wake umekizunguka kila kitu na kila mahali, kilipokuwa na kitakapokuwa.

Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘yaliyoko mbele yetu’ ni ishara ya yatakayokuja, na ‘yaliyoko nyuma yetu’ ni yaliyopita na ‘yaliyoko baina ya hayo’ ni yaliyoko sasa.

Mola wa mbingu na Ardhi na vilivyo baina yake.

Ambaye ni Mola wa ulimwengu itakuwa muhali kwake kusahahu.

Basi muabudu Yeye na uwe na subira kwa ibada yake.

Hii ni amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Mtume wake kwamba aendelee na na umuhimu wake wa kufikisha (tabligh) mwito, kwa sababu hiyo ni katika ibada kubwa, na kuvumilia maudhi katika njia yake.

Je, unamjua somo yake?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hana kifani na chochote, katika sifa zake za utukufu na ukamilifu. Basi anayekuwa hivyo anawajibikiwa na kuabudiwa na kutiiwa.

وَيَقُولُ الْإِنسَانُ أَإِذَا مَا مِتُّ لَسَوْفَ أُخْرَجُ حَيًّا ﴿٦٦﴾

66. Na mtu husema: Hivi nitakapokufa, ni kweli nitatolewa niwe hai?

أَوَلَا يَذْكُرُ الْإِنسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِن قَبْلُ وَلَمْ يَكُ شَيْئًا ﴿٦٧﴾

67. Je, hakumbuki mtu ya kwamba tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote?

فَوَرَبِّكَ لَنَحْشُرَنَّهُمْ وَالشَّيَاطِينَ ثُمَّ لَنُحْضِرَنَّهُمْ حَوْلَ جَهَنَّمَ جِثِيًّا ﴿٦٨﴾

68. Basi naapa kwa Mola wako! Hakika tutawakusanya na mashetani. Kisha tutawahud hurisha kandokando ya Jahanna mnao wamepiga magoti

ثُمَّ لَنَنزِعَنَّ مِن كُلِّ شِيعَةٍ أَيُّهُمْ أَشَدُّ عَلَى الرَّحْمَـٰنِ عِتِيًّا ﴿٦٩﴾

69. Kisha Kwa hakika tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao waliozidi kumwasi Mwingi wa rehema

ثُمَّ لَنَحْنُ أَعْلَمُ بِالَّذِينَ هُمْ أَوْلَىٰ بِهَا صِلِيًّا ﴿٧٠﴾

70. Tena hakika sisi tunawajua vizuri wanaostahiki kuunguzwa humo.

وَإِن مِّنكُمْ إِلَّا وَارِدُهَا كَانَ عَلَىٰ رَبِّكَ حَتْمًا مَّقْضِيًّا ﴿٧١﴾

71. Hakuna Miongoni mwenu ila ni mwenye kuifikia. Ni hukumu ya Mola wako, ni lazima itimizwe.

ثُمَّ نُنَجِّي الَّذِينَ اتَّقَوا وَّنَذَرُ الظَّالِمِينَ فِيهَا جِثِيًّا ﴿٧٢﴾

72. Kisha tutawaokoa wale wenye takua na tutawaacha madhalimu hapo wamepiga magoti.

KWELI NITATOLEWA HAI?

Aya 66 –72

MAANA

Na mtu husema: hivi nitakapokufa, ni kweli nitatolewa niwe hai? Je hakumbuki mtu ya kwamba tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote?

Kwa ufupi ni kuwa, hakuna kitu mbele ya mwenye kupinga ufufuo anachopima nacho isipokuwa kustaajabu; vipi utarudi uhai baada ya kumuondokea binadamu? Jibu ni kuwa ataurudisha mara ya pili yule aliyeuleta kwanza: ‘tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote’. Maana ya Aya hii yamekaririka katika Aya kadhaa, Angalia Juz; 1 (2:28-29), Juz; 2 (4:87) na Juz. 13 (13:5).

Basi naapa kwa Mola wako! Hakika tutawakusanya na mashetani.

Tutawakusanya hao wanaopinga ufufuo, Makusudio ya kukusanywa ni kutolewa kwao makaburini mwao wakiwa madhalili, wamedharaulika pamoja na wale waliowapoteza

Kisha tutawahudhurisha kandokando ya Jahannam nao wamepiga magoti.

Baada ya kutoka makaburini mwao na hali mbaya hiyo, Malaika watawakalisha wakiwa wamepiga magoti, kandokando ya Jahannam ili waiangalie, wazidi machungu na masikitiko.

Kisha kwa hakika tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao waliozidi kumwasi Mwingi wa rehema.

Baada ya kuizunguka Jahannam wakiwa wamepiga magoti, wakiwa ni makundi mbali mabali, Mwenyezi Mungu kwanza atachukua kiongozi kutoka kila kundi na kuwatupa katika Jahannam, kisha wanaowafuatia. Kila mmoja atawekwa mahali pake panapomstahiki katika adhabu ya kuungua

Tena hakika sisi tunawajua vizuri wanaostahiki kuunguzwa humo

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua maovu anayoyafanya kisiri na kidhahiri na atamlipa anavyostahili.

Mwenye madhambi makubwa adhabu yake ni kubwa, kisha anayefuatia na mwingine anayefuatia “Na watakuta waliyoyafanya yamehudhurishwa” Juz; 15 (18: 49).

Hakuna miongoni mwenu ila ni mwenye kuifikia. Ni hukumu ya Mola wako, ni lazima itimizwe. Kisha tutuwaokoa wale wenye takua na tutawaacha madhalimu hapo wamepiga magoti.

Makusudio ya kufikia hapa ni kuona na kushuhudia, kwa sababu waumini wataepushwa na moto; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الَّذِينَ سَبَقَتْ لَهُم مِّنَّا الْحُسْنَىٰ أُولَـٰئِكَ عَنْهَا مُبْعَدُونَ ﴿١٠١﴾

“Hakika wale ambao wema wetu umewatangulia wataepushwa nao” (21:101).

Pia kwamba kuadhibiwa mtiifu kunapingana na uadilifu wa Mungu. Maana ni kuwa hakuna yeyote kati ya mwema na muovu ila atauona waziwazi. Muovu atauona kisha aungie hali amepiga magoti na mwema atauona na aupite hali ya kushukuru neema ya kuokoka na mwako wake:

فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ﴿١٨٥﴾

“Mwenye kuepushwa na moto akatiwa Peponi, basi huyo amefuzu” Juz, 4 (3:185)

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَيُّ الْفَرِيقَيْنِ خَيْرٌ مَّقَامًا وَأَحْسَنُ نَدِيًّا ﴿٧٣﴾

73. Na wanaposomewa Aya zetu zilizowazi, waliokufuru huwaambia walioamini: lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lililo bora barazani

وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هُمْ أَحْسَنُ أَثَاثًا وَرِئْيًا ﴿٧٤﴾

74. Na karne ngapi tuliziangamiza zilizokuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa mandhari?

قُلْ مَن كَانَ فِي الضَّلَالَةِ فَلْيَمْدُدْ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ مَدًّا حَتَّىٰ إِذَا رَأَوْا مَا يُوعَدُونَ إِمَّا الْعَذَابَ وَإِمَّا السَّاعَةَ فَسَيَعْلَمُونَ مَنْ هُوَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضْعَفُ جُندًا ﴿٧٥﴾

75. Sema: aliye katika upotofu basi Mwingi wa rehema atampa muda mpaka ayaone aliyoahidiwa –Ama ni adhabu au ni saa. Hapo ndipo watajua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu

وَيَزِيدُ اللَّـهُ الَّذِينَ اهْتَدَوْا هُدًى وَالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ خَيْرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابًا وَخَيْرٌ مَّرَدًّا ﴿٧٦﴾

76. Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wale walioongoka, Na mema yenye kubaki ni bora katika malipo mbele ya Mola wako na yana mwisho mwema.

LIPI KATI YA MAKUNDI MAWILI

Aya 73-76

MAANA

Na wanaposomewa Aya zetu zilizowazi, waliokufuru huwaambia walioamini: lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lililo bora barazani?

Aya za Mwenyezi Mungu zilizo wazi ni dalili, makundi mawili ni waumi- ni na washirikina. Maana ni kuwa Mtume na maswahaba wanawapa washirikina hoja ya mantiki, kiakili na kimaumbile na wao wanajibu kwa mantiki ya tumbo na falsafa yake.

FALSAFA YA TUMBO

Epikouros alikuwa ni mwanafalsafa wa kiyunani (ugiriki) katika wanafunzi wa Aristatle, alikuwa na madhehebu yake peke yake yaliyotofautiana na wenzake na pia wale waliomtangulia.

Kwa ufupi anasema ladha ndio kheri kuu na machungu ndio shari kuu na kwamba thamani ya fadhila inategemea ladha za kimaana; kama ukweli, maisha ya utulivu na raha na pia ladha za kihisia; kama chakula na kinywaji...

Katika mwongozo wa falsafa hii anasema: Mtu asisukumwe na hawa yake na upendeleo wake kwenye ladha fupi itakayofuatiwa na machungu marefu.

Kwa maneno mengine ni kuwa, kwake yeye Epikouros – akiwa haamini ufufuo- ni kwamba kheri yote inakuwa kwenye ladha ya kidunia; ni sawa iwe kwenye tumbo au kwengineko. Kama itakutana na machungu basi linalozingatiwa ni wingi, lile lenye ladha nyingi litakuwa ni kheri na lenye machungu mengi basi ni shari.

Kuna falsafa ya kale inayoaifikiana na Epikouros kwamba kheri yote iko kwenye ladha ya dunia. Yeye anasema kheri iko kwenye ladha ya kimaana na kihisia pamoja nayo anasema kheri iko kwenye ladha ya tumbo na mengineyo ya hisia.

Miongoni mwa wenye falsafa hii ni Firauni na washirikina wa kiquraysh. Firauni alipinga utume wa Musa(a.s) , akaleta sababu ya kupinga kwake kwa kusema:

“Au mimi si bora kulio huyu aliye mnyonge wala hawezi kusema wazi. Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu...” (43: 52 – 53)

Akasema tena:

فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

“Mimi Ndiye Mola wenu Mkubwa” (79:24).

Kisha akaendela:

أَلَيْسَ لِي مُلْكُ مِصْرَ وَهَـٰذِهِ الْأَنْهَارُ تَجْرِي مِن تَحْتِي ﴿٥١﴾

“Kwani ufalme wa Misri si wangu na hii mito inapita chini yangu?” (43:51).

Makurishi nao, kama Firauni, walikanusha utume wa Muhmmad (s.a.w.) na wakatoa hoja kwa kusema:

لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْهِ كَنزٌ ﴿١٢﴾

“Mbona hakuteremshiwa hazina?” Juz;12 (11:12)

Falsafa hii haihusiki na Firauni na washirikina wa Makka tu, wala na watanuzi na wenye utajiri; isipokuwa inahusika na kila anayemuheshimu mtu na akampima kwa mali yake, basi yeye ni katika walioamini falsafa ya tumbo.

Miongoni mwa niliyoyasoma ni maneno ya kibaraka mmoja aliyesema: “Hawa wanaoilaumu Marekani na majeshi yake na wanavyowapiga wakombozi kila mahali na vile wanavyopora mali za wanyonge kila mahali, wamesahau au wanajitia kusahahu kuwa Marekani ina nguvu za kielimu na mali; na kwamba mwenye nguvu mpishe.”

Nilikuwa nikidhania kuwa falsafa ya tumbo ilikwisha kwenye zama za dhulma, lakini makala haya nilyoyasoma yamenifanya nitambue kuwa falsafa hii imekita mizizi kwenye nafsi za wapiga debe wa ukoloni na vibaraka wake.

Na karne ngapi tuliziangamiza zilizokuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa mandhari?

Umetangulia mfano wake katika Juz.7 (6:6)

Sema: aliye katika upotofu basi Mwingi wa rehema atampa muda mpaka ayaone aliyoahidiwa – ama ni adhabu au ni saa. Hapo ndipo watajua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake awaambie wale wanaoona kheri iko kwenye tumbo tu, kwamba hayo wanayojifaharisha nayo katika nafasi ya maisha waliyo nayo, kuwa ni mtihani wa Mwenyezi Mungu anowajaribu nao waja wake na anawapa muda mwingi.

Wakishukuru Mwenyezi Mungu atawapa thawabu na marejeo mazuri na wakizidi ukafiri na uasi basi atawasalitia ambaye atawatesa katika maisha haya ya duniani au atawaadhibu Mwenyezi Mungu huko Akhera. Huko watajua ni nani wenye hali mbaya, waumini walio mafukara au makafiri walio matajiri?

Lau mtu atamiliki kila kinacho chomozewa na jua, miliki hiyo si chochote kulinganisha na adhabu ya chini ya Jahannam. Amesema Amirul-mu’min, Aliy(a.s) : “Heri siyo kheri ikiwa baada yake ni moto; na shari si shari ikiwa baada yake ni Pepo, Na kila neema isiyokuwa Pepo ni kazi bure na kila balaa isiyokuwa moto ni nafuu.”

Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wale walioongoka

Hilo ni kwa kuwafahamisha hakika yao na sehemu za makosa na za sawa. Hii ni hidaya na neema kubwa.

Na mema yenye kubaki ni bora katika malipo mbele ya Mola wako na yana mwisho mwema.

Mema yanayobakia ni elimu na mambo ya manufaa. Hayo mawili ni bora kuliko mali na jaha. Kwa sababu yanadumu na kubakia manufaa yake na thawabu zake hazikatiki, lakini jaha na mali zinaisha na kuangamia.

أَفَرَأَيْتَ الَّذِي كَفَرَ بِآيَاتِنَا وَقَالَ لَأُوتَيَنَّ مَالًا وَوَلَدًا ﴿٧٧﴾

77. Je, umemuona aliyezikana ishara zetu na akasema: Hakika mimi nitapewa mali na watoto.

أَطَّلَعَ الْغَيْبَ أَمِ اتَّخَذَ عِندَ الرَّحْمَـٰنِ عَهْدًا ﴿٧٨﴾

78. Kwani yeye amepata habari za ghaibu au amechukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

كَلَّا سَنَكْتُبُ مَا يَقُولُ وَنَمُدُّ لَهُ مِنَ الْعَذَابِ مَدًّا ﴿٧٩﴾

79. Hapana! Tutaandika anayoyo asema na tutamkunjulia muda wa adhabu.

وَنَرِثُهُ مَا يَقُولُ وَيَأْتِينَا فَرْدًا ﴿٨٠﴾

80. Na tutamrithi hayo anayoyasema na atatufikia akiwa peke yake.

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لِّيَكُونُوا لَهُمْ عِزًّا ﴿٨١﴾

81. Na wamechukua miungu mingine ili iwape nguvu.

كَلَّا سَيَكْفُرُونَ بِعِبَادَتِهِمْ وَيَكُونُونَ عَلَيْهِمْ ضِدًّا ﴿٨٢﴾

82. Sivyo kabisa! Wataikataa ibada yao na watakuwa ndio dhidiyao.

أَلَمْ تَرَ أَنَّا أَرْسَلْنَا الشَّيَاطِينَ عَلَى الْكَافِرِينَ تَؤُزُّهُمْ أَزًّا ﴿٨٣﴾

83. Kwani huoni kwamba tume-watuma mashetani kwa makafiri wawachochee kwa uchochezi.

فَلَا تَعْجَلْ عَلَيْهِمْ إِنَّمَا نَعُدُّ لَهُمْ عَدًّا ﴿٨٤﴾

84. Basi usiwafanyie haraka, Sisi tunawahisabia siku.

يَوْمَ نَحْشُرُ الْمُتَّقِينَ إِلَى الرَّحْمَـٰنِ وَفْدًا ﴿٨٥﴾

85. Siku tutakayowakusanya wenye takua kuwa ni wageni wa Mwingi wa rehema.

وَنَسُوقُ الْمُجْرِمِينَ إِلَىٰ جَهَنَّمَ وِرْدًا ﴿٨٦﴾

86. Na tutawachunga wahalifu kuwapeleka Jahannam hali ya kuwa na kiu

لَّا يَمْلِكُونَ الشَّفَاعَةَ إِلَّا مَنِ اتَّخَذَ عِندَ الرَّحْمَـٰنِ عَهْدًا ﴿٨٧﴾

87. Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale waliochukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

JE, UMEMUONA ALIYEZIKANA ISHARA ZETU

Aya 77 – 87

MAANA

Je, umemuona aliyezikana ishara zetu na akasema: Hakika mimi nitapewa mali na watoto.

Imeelezwa katika Hadith na tafsiri kwamaba A’si bin Wail, mzazi wa Amru bin Al’as, aliposikia kuhusu utume, alisema kwa stihzai: Bila shaka mimi huko akhera nitapewa mali na watoto.

Lakini dhahiri ya tamko la Aya linaonyesha kuwa kuna mzandiki fulani aliyesema hivi; ama kuwataja watu majina, hiyo si katika njia ya Qur’an. Mfano wa Aya hii ni kauli ya yule mwenye kitalu aliyesema:

وَلَئِن رُّدِدتُّ إِلَىٰ رَبِّي لَأَجِدَنَّ خَيْرًا مِّنْهَا مُنقَلَبًا ﴿٣٦﴾

“Na kama nitarudishwa kwa Mola wangu bila shaka nitapata marejeo bora zaidi Kuliko haya”Juz;15 (18:36).

Ameirudi Mwenyezi Mungu kauli hii kwa kusema:

Kwani yeye amepata habari za ghaibu au amechukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

Amepata wapi habari hizi? Au yeye ana funguo za siri au amechukua ahadi na Mwenyezi Mungu katika hilo?

Hapana ! si hivi wala hivyo; isipokuwa yeye ni kafiri muovu.Tutaandika anayoyasema na tutamkunjulia muda wa adhabu Tumezihifadhi kauli zake na tutamzidishia adhabu zaidi ya kufuru yake na uzushi wake.

Na tutamrithi hayo anayoyasema na atatufikia akiwa peke yake, akiwa mtupu na pia tutamnyng’anya mali na watoto alio nao, pale anapokufa na kuangamia na tutamfufua siku ya kiyama akiwa peke yake mtupu; sawa na tulivyomuumba mara ya kwanza.

Na wamechukua miungu mingine ili iwape nguvu. Sivyo kabisa! Kwa sababu mwenye kutaka nguvu kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, basi Mungu humvisha vazi la udhalili.

Wataikataa ibada yao na watakuwa ndio dhidi yao

Yaani hao wanawaabudu wataikataa ibada yao na watakuwa dhidi yao. Tafsiri inayofafanua zaidi Aya hii ni kauli ya Imam Ali(a.s), katika Nahjulbalagha: Sio mbali anayefuatwa atajitenga na mfuasi na kiongozi na anayeongozwa watafarikiana kwa chuki na watalaaniana watakapokutana.

Mwenyezi Mungu naye amesema:

تَبَرَّأْنَا إِلَيْكَ مَا كَانُوا إِيَّانَا يَعْبُدُونَ ﴿٦٣﴾

“Tunajitenga nao mbele yako, Hawakuwa wakituabudu sisi” (28:63);bali walikuwa wakiabudu hawa zao na malengo yao.

Kwani huoni kwamba tumewatuma mashetani kwa makafiri wawa- chochee kwa uchochezi.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) haingilii kati baina yao na mashetani wanowapa wasiwasi na kuwahadaa na maasi, wala hajiingizi, kwa uweza wake wa kufanya, kumzuia shetani; isipokuwa amewabainishia njia ya kheri na shari na kuwapa uwezo kamili wa kutenda na kuwaacha; anawakataza hili na kuwaamrisha lile; kisha anawaachia hiyari katika watakayoyatenda na kuyaacha.

Kama angeliwanyanyag’anya utashi, basi wangelikuwa wao na miti ni sawa.

Basi usiwafanyie haraka. Sisi tunawahisabia siku.

Yaani, ewe Muhammad, usiwe na haraka ya kuangamia makafiri, kwani maangamizi yao yatakuja tu, lakini Mwenyezi Mungu anawangoja mpaka muda uliotajwa, ili avidhibiti vitendo vyao, kisha aje awalipe, wanayostahili. Kwani hakuna kheri ya kurefuka maisha isipokuwa kwa yule anayeamini na akatenda amali njema, lakini mwenye kukufuru na akafanya maovu, basi maisha yake ni balaa:

وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ خَيْرٌ لِّأَنفُسِهِمْ إِنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ لِيَزْدَادُوا إِثْمًا وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴿١٧٨﴾

“Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa ni kheri kwa nafsi zao, Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika dhambi na wana adhabu idhalilishayo.”Juz.4 (3:178).

Siku tutakyowakusanya wenye takua kuwa ni wageni wa Mwingi wa rehema.

Neno lililotumika katika kufasiri wageni limetokana na neno la kiarabu wafd lenye maana ya wageni wa heshima. Maana ni kuwa wale wanaomtii Mwenyezi Mungu, kesho watakuwa ni wageni wenye kutukuzwa.

Na tutawachunga wahalifu kuwapeleka Jahannam halia ya kuwa na kiu

Waumini watapata makaribisho ya heshima na wahalifu watapata makaribisho ya dharau, kuchungwa kama wanyama wanavyochungwa kwenda kunywa maji; ndivyo wahalifu nao watachungwa kupelekwa kwenye Jahannam.

Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale waliochukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

Kila mwenye kutekeleza ahadi ya Mwenyeezi Mungu na wala asimfanyie hiyana kwenye dogo wala kubwa, basi Mwenyezi Mungu amempa ahadi ya kufuzu na kuokoka na uombezi:

وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ ﴿٤٠﴾

“Na tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu”Juz;1(2:40)

وَقَالُوا اتَّخَذَ الرَّحْمَـٰنُ وَلَدًا ﴿٨٨﴾

88. Na wanasema Mwingi wa rehema anamwana.

لَّقَدْ جِئْتُمْ شَيْئًا إِدًّا ﴿٨٩﴾

89. Hakika mmeleta Jambo la kuchusha.

تَكَادُ السَّمَاوَاتُ يَتَفَطَّرْنَ مِنْهُ وَتَنشَقُّ الْأَرْضُ وَتَخِرُّ الْجِبَالُ هَدًّا ﴿٩٠﴾

90. Zinakurubia mbingu kutatuka kwa hilo na ardhi kupasuka na milima kuanguka vipande vipande

أَن دَعَوْا لِلرَّحْمَـٰنِ وَلَدًا ﴿٩١﴾

91. Kwa kudai kwao kuwa Mwingi wa rehema ana mwana.

وَمَا يَنبَغِي لِلرَّحْمَـٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا ﴿٩٢﴾

92. Hahitajii Mwingi wa rehema kuwa na mwana.

إِن كُلُّ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِلَّا آتِي الرَّحْمَـٰنِ عَبْدًا ﴿٩٣﴾

93. Hakuna yeyote aliyemo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Mwingi wa rehema kuwa ni mtumwa.

لَّقَدْ أَحْصَاهُمْ وَعَدَّهُمْ عَدًّا ﴿٩٤﴾

94. Hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa.

وَكُلُّهُمْ آتِيهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَرْدًا ﴿٩٥﴾

95. Na kila mmoja kati yao atam fikia siku ya Kiyama peke yake

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَيَجْعَلُ لَهُمُ الرَّحْمَـٰنُ وُدًّا ﴿٩٦﴾

96. Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.

فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ الْمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِ قَوْمًا لُّدًّا ﴿٩٧﴾

97. Hakika tumeifanya nyepesi, kwa ulimi wako ili uwabashirie kwayo wenye takua na uwaonye kwayo wabishi

وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هَلْ تُحِسُّ مِنْهُم مِّنْ أَحَدٍ أَوْ تَسْمَعُ لَهُمْ رِكْزًا ﴿٩٨﴾

98. Na karne ngapi tumeziangamiza kabla yao, Je, unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?

WANASEMA MWINGI WA REHEMA AMEJIFANYIA MWANA

Aya 88 – 98

MAANA

Na wao wanasema Mwingi wa rehema ana mwana. Hakika mmeleta jambo la kuchusha, Zinakurubia mbingu kutatuka kwa hilo na ardhi kupasuka na milima kuanguka vipande vipande kwa kudai kwao kuwa Mwingi wa rehema ana mwana.

Mwenyezi Mungu amewakemea sana wale waliomfanya Mwenyezi Mungu kuwa ana watoto wa kiume na mabinti na akawapa kiaga kwenye Aya kadhaa; miongoni mwazo ni: Juz.1 (2:116), Juz.5 (4:48), Juz. 6 (4:171) na Juz. 7 (6:101).

Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akataja hapa kauli yao hii kwa mfumo huu wa kutisha. Nao unafahamisha kuwa mtu anamchezea ambaye hachezewi na yeyote aliye mbinguni wala ardhini.

Binadamu anamchezea Muumba wake naye anaishi kwenye himaya yake, na anamnasibisha mambo ambayo kuyasikia tu yanaweza yakaipasua mbingu na ardhi na kuangusha milima.

Unaweza kuuliza : kwanini hasira yote hii ya kilimwengu kwa sababu tu ya maneno ya kijinga na ya udhaifu wa akili?

Jibu : Hasira yote hii, haiko kwa mtu au kikundi cha watu maalum; isipokuwa imetokana na shirki hii ambayo sasa imekuwa ni dini na itikadi wanayoifuata mamilioni, kizazi baada ya kizazi na mifano hii ya mungu mwan na mungu mama.

مَّا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ وَأُمُّهُ صِدِّيقَةٌ كَانَا يَأْكُلَانِ الطَّعَامَ ﴿٧٥﴾

“Masih mwana wa Maryam hakuwa ila ni Mtume, Wamepita kabla yake Mitume, Na mama yake ni mkweli, Wote wawili walikuwa wakila chaku- la”Juz; 6 (5:75).

Hahitajii Mwingi wa rehema kuwa na mwana.

Kwa sababu mwana anafanana na mzazi wake, na Mwenyezi Mungu hana aliyefanana naye. Na kwa sababu kuwa na mtoto ni kumuhitajia, na Mwenyezi Mungu amejitosheleza na walimwengu wote

Hakuna yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Mwingi wa rehema kuwa ni mtumwa.

Hakuna yeyote aliyeko chini au juu ila huwa ni mja wa Mwenyezi Mungu anayemilikiwa. Kimsingi ni kwamba mwenye kumilikiwa sio mtoto na mmliki sio baba.

Hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa na kila mmoja kati yao atamfikia siku ya Kiyama peke yake.

Waliodhibitiwa ni walio mbinguni na ardhini na atakyefikiwa ni Mwenyezi Mungu. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu hapotewi na kujua kitu chochote katika ardhi wala katika mbingu na kwamba kila mmoja atakwenda kwa Mwenyezi Mungu siku ya kiyama akiwa peke yake, hana wa kumnusuru wala kumsaidia au kujisaidia yeye mwenyewe kwa wingi au uchache, sikwambii tena kumsadia mwenginewe. Ambaye atamjia Mwenyezi Mungu katika hali kama hiyo, anawezaje kuwa mtoto wake?

Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.

Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anatia mapenzi katika nyoyo za waja wake kwa watu wenye imani na ikhlasi, si kwa chochote ila kwa kuthamini fadhila na hulka njema.

Muhammad bin Ahmad Alkalabiy, mwenye kitabu Attas-hil anasema: Inasemekana kuwa Aya hii ilishukwa kwa Aliy bin Abi Twalib. Sheikh Almaraghi, mmoja wapo wa masheikh wa Al-Azhar, anasema: ‘Ibin Mardaywyh na Dilamiy wamepokea kutoka kwa Baraa, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alimwambia Aliy: Sema ewe Mola wangu nijalie ahadi kwako na unijaalie mapenzi katika nyoyo za waumini’ ndipo ikashuka Aya hii”.

WANASWARA NA BANI HASHIM

Amesema Abu Hayani Al-andalusi katika tafsir yake Albahrul-Muhit: “Aya hii ilishuka kwa Aliy bin Abi Twalib na amesema Muhammad Alhanafiya: huwezi kumpata mumin ila anampenda Aliy. Maajabu ni yale aliyotueleza Imam wa lugha Ridhad Din, Abu Abdillah Muhammad bin Aliy bin Yusuf Al-Answariy Ashatibiy kuhusu aliyosema, ibn Is-haq Mnaswara:

• Uday na Taym kwa ubaya kamwe sitothubutu kuwataja

• Lakini naona ni vibaya Ali kulaumiwa na waja

• Mimi ni mpenzi wa dhuriya ya Hashimu na wanawe pamoja

• Naswira watukufu kupambiya kwa nini imekuwa ni kioja

• Tawaambiya huku kiusiya moyo wangu umekwisha wachuja

• Kupenda nifuraha nawambiya hata wanyama pia wangoja.

Hakika tumeifanya nyepesi, kwa ulimi wako ili uwabashirie kwayo wenye takua na uwaonye kwayo wabishi.

Yaani Mwenyezi Mungu ameteremsha Qur’an kwa lugha ya kiarabu ili iwe wepesi kuijua na kufahamu maana yake na iwe ni habari njema kwa mwenye kumcha Mwenyezi Mungu na onyo kwa mwenye kukufuru na akafanya uovu. Umepita mfano wake katika Juz. 12 (12:2)

Na karne ngapi tumeziangamiza kabla yao, Je, unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?

Yaani Mwenyezi Mungu amewaangamiza mpaka wa mwisho wao. Umetangulia mfano wake katika Aya ya 84 ya sura hii; na Juz, 15 (17:17).

MWISHO WA SURA YA KUMI NA TISA

15

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Sura Ya Sitini Na Nane: Surat Al- Qalam. Imeshuka Makka. Imesemekana kuwa baadhi imeshuka Madina. Ina Aya 52.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

ن وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ ﴿١﴾

1. Nun. Naapa kwa kalamu na yale wanayoandika.

مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ ﴿٢﴾

2. Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.

وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ ﴿٣﴾

3. Na kwa hakika wewe una ujira usiokatika.

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ ﴿٤﴾

4. Na hakika wewe una tabia tukufu.

فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ ﴿٥﴾

5. Karibu utaona, na wao wataona.

بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ ﴿٦﴾

6. Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ ﴿٧﴾

7. Hakika Mola wako ndiye anayemjua zaidi aliyepotea njia yake na Yeye ndiye anaye­wajua zaidi walioongoka.

فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ ﴿٨﴾

8. Basi usiwatii wanaokadhibisha.

وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ ﴿٩﴾

9. Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ ﴿١٠﴾

10. Wala usimtii kila mwingi wa kuapa aliye dhalili.

هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ ﴿١١﴾

11. Msingiziaji, apitae akifitini.

مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ﴿١٢﴾

12. Mwenye kuzuia heri, mwenye kudhulumu, mwingi wa mad­hambi.

عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ ﴿١٣﴾

13. Mwenye roho ngumu, juu ya hayo, ni mwanaharamu.

أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ ﴿١٤﴾

14. Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٥﴾

15. Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni ngano za watu wa kale!

سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ ﴿١٦﴾

16. Tutamtia doa juu ya pua.

WEWE SI MWENDAWAZIMU

Aya 1- 16

MAANA

Nun . kwa kukadiria maneno ya kuwa hii ni sura ya Nun. Hii sio kama mianzo mingineyo ya herufi zinazoanziwa sura, tulizozizungumzia katika Juz. 1 (2:1).

Kuna aliyesema kuwa ni samaki, mwingine akasema ni chombo cha wino, watatu akasema ni wino, wa nne akasema ni nun ya neno rahman, na jamaa wa kisufi wakasema kuwa ni nafsi. Kauli zote hizi zinahitajia dalili.

Naapa kwa kalamu na yale wanayoandika.

Wametofautiana kuhusu kalamu: Kuna waliosema ni kalamu iliyotumika kwenye lawh mahfud[ (ubao maalum uliohifadhiwa). Mwingne akasema ni kila kalamu, na kwamba herufi aliY na la` kwenye neno hili ni ya jinsi, ambayo inamaanisha kuenea.

Hii ndio kauli iliyo dhahiri; kwamba makusudio sio kalamu hasa, bali ni nyenzo yoyote ya kuandikia; kama inavyoashiria kauli inayofuatia inayosema: “Na yale wanayoyaandika.”

Kwa hiyo basi kalamu itakuwa ni kinaya cha chombo cha kuandikia, vyovyote kitakavyokuwa, kilichopo au kitakachogunduliwa karibuni au baadaye. Tumedokeza faida za ubainifu katika Juz. 27 (55:4), kwamba manufaa ya ubainifu ni sawa na manufaa ya maji na hewa.

Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) . Hakuna yeyote anayed­hania kuwa Muhammad(s.a.w.w) ni mwenda wazimu. Wale waliompa sifa hiyo walikusudia kuwa ana jinni linalompa wahyi; kama wanavyodai kwamba kila mshairi ana jinni linalomfundisha ushairi.

Hilo linaashiriwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwasimulia:

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ﴿٣٦﴾

“Na wakisema: Hivi tuiache miungu miungu yetu kwa ajili ya huyu mshairi mwendawazimu?” Juz. 23 (37:36).

Na kwa hakika wewe una ujira usiokatika.

Neno ‘usiokatika’ tumelifasiri kutokana na neno mamnun, ambalo pia lina maana ya kusimbuliwa au maana zote mbili pamoja (kukatika na kusimbuliwa).

Kimsingi ni kuwa malipo yanapimwa kwa natija ya kazi na athari yake. Bado athari za Muhammad(s.a.w.w) , mwito wake na ukuu wake unaendela hadi leo, kuanzia mashariki mwa ardhi hadi magharibi yake na utaendelea hadi siku ya mwisho. Kwa hiyo si kioja kupata karama ya milele kutoka kwa Mola wake.

Na hakika wewe una tabia tukufu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakumsifu yeyote katika mitume wake na wasi­fa huu isipokuwa Muhammad.

Maana yake yanafupilizwa na kauli yake Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) : “Mola wangu amenifunza maadili akayafanya mazuri mafunzo yangu,” yaani Mwenyezi Mungu ameelekeza kwa Muhammad(s.a.w.w) maadili yale yale aliyoumba kwa ajli ya nafsi.

Vile vile Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuwahi kuapa kwa maisha ya mtu isipokuwa kwa maisha ya Muhammad(s.a.w.w) ; pale aliposema:

لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِي سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ ﴿٧٢﴾

“Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao wakiman­gamanga.”

Juz. 14 (15:72).

Ama wasifu wa Muhammad(s.a.w.w) kuwa ni mwisho wa manabii, Maana yake ni kuwa Muhammad alifikia ukomo wa sifa za mtu zisizofikiwa na yeyote kwa ukamilifu. Ni muhali kuja baada yake atakayekuwa bora zaidi kuliko yeye au kuja na sharia bora zaidi ya sharia zake; bali hakuna kium­be yeyote kuanzia wa mwanzo hadi wa mwisho anayefanana naye. Hilo linaashiriwa na kauli yake Mtume(s.a.w.w) : “Mimi ni bwana wa watu wote, wala sisemi kwa kujifaharisha.”

Hii ni kwa kuwa sharia na utume umeishilizwa kwake. Ibn Al-arabiy anasema, katika Futuhat: kuwa Mwenyezi Mungu ameumba viumbe aina kwa aina, akafanya walio bora. Walio bora katika viumbe ni mitume, na katika mitume kuna wateule ambao ni ulul-az` na katika wao kuna mteule zaidi naye ni Muhammad(s.a.w.w) .

Karibu utaona, na wao wataona, ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

Hili ni onyo na kiaga, kwamba hivi karibuni itakubainikia wewe na maadui zako kwamba wao ndio wajinga, wapotevu na wendawazimu zaidi katika watu, na kwamba wewe ndiwe ulie juu, mwenye akili na mtukufu wa maadili zaidi ya watu wengine na kwamba ndiwe mtukufu wao zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu.

Hakika Mola wako ndiye anayemjua zaidi aliyepotea njia yake na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

Mwenyezi Mungu anajua cheo chako ewe Muhammad(s.a.w.w) na uongo­fu na anajua nafasi ya wahasimu wake ya upotevu na mbele yao kuna hisabu na malipo. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 14 (16:125).

Basi usiwatii wanaokadhibisha.

Washirikina walijaribu kila njia kumzuia Mtume(s.a.w.w) na mwito wake, wakajaribu kumbembeleza kwa cheo na mali, akakataa. Wakatamani lau watakubaliana naye kufanya vile watakavyo, Mwenyezi Mungu akamkataza hilo. Lengo la kumkataza ni kuwakatisha tamaa na wajue kuwa hakuna mjadala wala makubaliano katika twaa ya Mwenyezi Mungu na amri yake. Katazo hili linafanana na anayekutaka mkubaliane naye kwenye dini yako, ukiwa unataka kumkatisha tamaa kabisa, na kumwambia: Mwenyezi Mungu amenikataza hilo.

Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

Washirikina walitamani Mtume(s.a.w.w) apunguze baadhi ya yale anayowalingania na wao waache baadhi ya yale aliyowakataza, ijapokuwa ni kwa njia ya kupakaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili kusiwe na mvu­tano baina ya pande mbili.

Mfumo wa maneno unafahamisha kuwa aliyetoa maoni hayo anasifika na sifa aliyoiashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kusema:Wala usimtii kila mwingi wa kuapa aliye dhalili . Anakithirisha viapo bila ya sababu jambo linalomsababisha kuwa dhalili anayedharauliwa.Msingiziaji anawatia ila sana watu.Apitaye akifitini . Anajaribu kuwavuruga watu kwa kunukuuu ya huku akiyapeleka kule.

Mwenye kuzuia heri , yeye haifanyi na anazuia wengine wasiifanye.Mwenye kudhulumu , haki za watu.Mwingi wa madhambi na makosa.Mwenye roho ngumu, juu ya hayo, ni mwanaharamu, asiyejua nasaba yake. Hii ni sifa mbaya zaidi ya zote zinazofikiriwa na akili.

Wafasiri wengi wamesema kuwa aliyekusudiwa na ushenzi huu ni Walid bin Al-mughira, aliyekuwa ni miongoni mwa vigogo wa kikuraishi, mwenye mali nyingi na watoto; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:Ati kwa kuwa ana mali na watoto! Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni ngano za uwongoza watu wa kale!

Wafasiri wamesema kuwa Aya hii ni ya kukataza kumtii mshenzi huyu. Lakini lililo karibu zaidi na usawa ni kuwa huko kuwa na mali na watoto kumemfanya athubutu kusema Qur’an ni simulizi za watu wa zamani; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الْإِنسَانَ لَيَطْغَىٰ ﴿٦﴾ أَن رَّآهُ اسْتَغْنَىٰ ﴿٧﴾

“Hakika mtu hupituka mipaka kwa kujiona ametajirika.” (96:6-7).

Sikwambii tena akiwa na nguvu na watu.Tutamtia doa juu ya pua yake. Waarabu wanatumia kutaja pua kwa ajili ya utukufu na udhalii. Wanasema kwa utukufu: ana pua ya kunusa. Kwenye udhalili wanasema: pua yake ikio mchangani.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) atamfedhehesha mjeuri huyu ambaye amejitukuza kwa mali na watoto, atamdhalilisha muda wote, atam laani kwa lugha iliyosajiliwa kwenye Kitabu chake na atamfedhehesha Akhera mbele ya ushuhuda, kwa kusawijika uso na alama nyinginezo za kuakisi madhambi yake.

إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ ﴿١٧﴾

17. Hakika tumewajaribu kama tulivyowajaribu wenye sham­ba, walipoapa kwamba watal­ivuna itakapokuwa asubuhi.

وَلَا يَسْتَثْنُونَ ﴿١٨﴾

18. Wala hawakusema: Inshaallah!

فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ ﴿١٩﴾

19. Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako, nao wamelala!

فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ ﴿٢٠﴾

20. Likawa kama limefyekwa.

فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ ﴿٢١﴾

21. Wakaitana asubuhi.

أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ ﴿٢٢﴾

22. Ya kwamba raukeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ ﴿٢٣﴾

23. Basi walikwenda na huku wakinong’onezana.

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ ﴿٢٤﴾

24. Ya kuwa leo asiliingie hata maskini mmoja.

وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ ﴿٢٥﴾

25. Na walirauka, nao wana nguvu za kunyima.

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ ﴿٢٦﴾

26. Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ ﴿٢٧﴾

27. Bali tumenyimwa!

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ ﴿٢٨﴾

28. Akasema Mbora wao: Je, Sikuwambia, kwa nini hamumsabihi Mwenyezi Mungu?

قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ ﴿٢٩﴾

29. Wakasema: Ametakasika Mola wetu! Hakika tulikuwa madhalimu.

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ ﴿٣٠﴾

30. Basi wakakabiliana kulau­miana wao kwa wao.

قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ ﴿٣١﴾

31. Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ ﴿٣٢﴾

32. Asaa Mola wetu akatubadil­ishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٣٣﴾

Kama hivyo inakuwa adhabu, na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi, laiti wangelijua!

LIKAWA KAMA LIMEFYEKWA

Aya 17 – 33

MAANA

Hakika tumewajaribu kama tulivyowajaribu wenye shamba.

Waliojaribiwa ‧ katika neno tumewajaribu - ni washirikina wa kikuraishi waliomkadhibisha Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) ambao Mwenyezi Mungu amewaashiria katika Aya ya nane ya surua hii. ‘Basi usiwatii wanaokadhibisha.’ Akiwemo yule mwenye kupituka mipaka mwenye dhambi ambaye, kama walivyosema wafasri, ni Walid bin Almughira, kigogo wa makuraishi msemaji wa wakadhibishaji akielezea ufidhuli na jeuri yao juu ya haki.

Aya hizi tulizo nazo zinampigia mfano yeye na wao, kwamba kulikuwa na watu waliokuwa na shamba lililojaa mazao, lakini wao walikuwa mabahili kwa mafukara na masikini.

Mazao yalipokomaa na kukurubia kuvunwa walipanga njama na kuapa kuwa wavune shamba asubuhi na mapema, mafukara wakiwa hawana habari. Waliazimia hivyo bila ya kuyaunganisha maazimio yao na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Waliambiana kuwa wawanyime wahitaji kile walichopewa na Mwenyezi Mungu, wakiwa wamesahau mipangilio ya Mwenyezi Mungu na uweza wake.

Usiku huo huo walioazimia kuvuna, Mwenyezi Mungu alilitermshia shamba janga la mbinguni lilioharibu mazao yote kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Walipoamka asubuhi na kwenda shambani walipigwa na butwaa, wakaan­za kulaumiana wenyewe kwa wenyewe, kila mmoja akimwambia mwen­zake: “Wewe ndiye sababu ya haya.” Miongoni mwao alikuwako mtu mwema aliyewapa nasaha kabla, lakini hawakumsikiliza, ndio akawaambia: Kwani sikuwaaambia, lakini mkakataa. Basi tubieni kwa Mola ili mpate kufaulu. Wakatubia kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na wakam­womba msamaha na kutaka wahurumiwe na kuneemeshwa kutoka shambani mwao.

Lengo la kupiga mfano huu, ni kupata funzo kila aliyeneemeshwa na Mwenyezi Mungu; hasa watu wa Makka akiwemo yule mshenzi. Wapokezi wa Hadith wanasema watu wa Makka walipatwa na kahati na njaa kwa vile walimkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) , ndipo akawaombea majanga na Mwenyezi Mungu akaitikia maombi yake. Kahati iliendelea kiasi cha miaka saba mpaka wakawa wanakula mizoga na mifupa. Pia wapokezi wanasema Mwenyezi Mungu aliingamiza mali ya Walid.

Haya ndio makusudio ya Aya kwa ujumla wake. Ufuatao ni ufufanuzi wa Aya moja moja:-

Walipoapa kwamba watalivuna itakapokuwa asubuhi.

Wenye shamba waliapa kuwa watalivuna mafukara wakiwa hawana habari.

Wala hawakusema: Inshaallah!

Yaani hawakusema tutavuna asubuhi Mungu akipenda.

Tumefasiri wala hawakusema inshaallah! Kutokana na maneno ya kiarabu yastathnuua ambayo tafsiri yake ya moja kwa moja ni ‘hawakutenga au hawakutoa.’ Kwa hiyo baadhi ya wafasiri wakasema maana ni hawakutenga kitu kwa ajili ya masikini. Kila moja kati ya tafsiri mbili hizi inafaa. Vile vile zinaweza kwenda kwa pamoja.

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako, nao wamelala! Likawa kama limefyekwa.

Wenye shamba walilala raha mustarehe wakiwa na imani ya kulivuna shamba lao asubuhi na mapema, lakini usiku huo likafikwa na janga.

Neno kufyekwa, tumelifasiri kutokana na neno Asswarim, ambalo maana yake nyingine ni weusi, kwa maana ya kuungua na kuwa jeusi kama usiku wa giza

Wakaitana asubuhi, ya kwamba raukeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

Ilipofika asubuhi waliitana ili wawahi kwenda shamba bila ya masikini kujua.

Basi walikwenda na huku wakinong’onezana. Ya kuwa leo asiliingie hata masikini mmoja.

Walifanya haraka wakidhamiria kwa siri kuwa masikini asionje hata chembe ya mazao.

Hakuna mwenye shaka kuwa huu ni uchoyo. Ikiwa hawa shamba lilikuwa lao na mazao ni yao hawakuiba, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu aliwaghadhabikia na kuwaandalia adhabu; je, itakuwaje kwa yule aliyepituka mipaka kwenye maisha ya watu akawanyang’anya vyakula vyao, akawaua na kuwafukuza kwenye miji, kama wanavyofanya wakoloni hivi sasa katika mashariki ya dunia na magharibi yake?

Na walirauka, nao wana nguvu za kunyima.

Waliingia shambani mwao wakiwa na dhamira kabisa ya kuwanyima mafukara, wakiwa na mawazo kwamba shamba na mazao yake yako mikononi mwao. Hawakujua kuwa mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao.

Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea! Bali tumenyimwa!

Walipofika shamba yaliwashangaza waliyoyaona na wakakubali kuwa wamepotea na kusema: sisi ndio tuliokosa fadhila za Mwenyezi Mungu na thawabu zake, na tunastahili ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake na sio mafukara na masikini.

Miongoni mwao alikuwa mtu mwema aliyekuwa akiaamrisha mema na kuwakataza maovu, lakini hawakusikiliza nasaha zake. alipoona yaliyowafika:

Akasema Mbora wao: Je, Sikuwambia, kwa nini hamumsabi­hi Mwenyezi Mungu?

Yaani hamumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kauli wala kwa vitendo kwa kutoa. alisema hivi kwa kuwahurumia. Kisha akawaamuru kutubia:Wakasema: Ametakasika Mola wetu! Hakika tulikuwa madhalimu wa nafsi zetu kwa kumuasi Mwenyezi Mungu.

Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

Kila mmoja anamtupia lawama mwinziwe; kama ilivyo hali ya washiriki­na, wanapofikwa na yale yaliyofanywa na mikono yao.

Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Walirudia akili zao na wakacha kulaumiana, wakakiri dhambi zao kwam­ba wao walikuwa katika upotevu, wakijiombea kufa kwa kusema ‘Ole wetu’ na kumwomba msamaha Mwenyezi Mungu, wakasema:Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

Hii ni dua na matarajio yao kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) awasamehe yaliyopita na awabadilishie yaliyo bora kuliko yaliyopita. Na Mwenyezi Mungu anakubali toba kutoka kwa waja wake, anawasamehe mengi na anaitikia maombi ya anayemuomba kwa ukweli na ikhlasi.

Kama hivyo inakuwa adhabu, na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi, laiti wangelijua!

Razi anasema hii iko wazi haihitaji tafsir, lakini sheikh Maraghi amekataa isipokuwa kuifasiri kwa kusema: “Yaani adhabu ya Akhera ni kali na inau­miza zaidi kuliko adhabu ya duniani.”

16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴿٣٤﴾

34. Hakika wenye takua watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao.

أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ ﴿٣٥﴾

35. Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ﴿٣٦﴾

36. Mna nini? Mnahukumu vipi?

أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ ﴿٣٧﴾

37. Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ ﴿٣٨﴾

38. Kuwa mtapata humo mnayo yachagua?

أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ ﴿٣٩﴾

39. Au mna viapo juu yetu vinavyofika Siku ya Kiyama ya kuwa mtapata mnayo­jihukumia?

سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ ﴿٤٠﴾

40. Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?

أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ ﴿٤١﴾

41. Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao waki­wa wanasema kweli.

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ ﴿٤٢﴾

42. Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusu­judu, lakini hawataweza.

خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ ﴿٤٣﴾

43. Macho yao yatanyenyekea fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa salama.

KWANI TUTAWAFANYA WAISLAMU KAMA WAKOSEFU?

Aya 34 – 43

MAANA

Hakika wenye takua watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao.

Katika Aya zilizotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaahidi wakosefu adhabu kubwa, na katika Aya hii anawaahidi wanaomcha Mwenyezi Mungu kuwa na milki ya daima na neema ya kudumu. Namna hii Mwenyezi Mungu analinganisha mwisho wa wakosefu na wa wenye takua; kwa kuvutia na kuhadharisha.

Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu? Mna nini? Mnahukumu vipi?

Makusudio ya waislamu hapa sio kila mwenye kusema: Lailaha ilallah muhammadur-rasulullah[ (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu); bali makusudio ni wanaom­cha Mwenyezi Mungu. Kwa sababu mazungumzo hapa yanahusiana na wao na yale waliyo nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu ya Pepo yenye neema.

Unaweza kuuliza : hatudhani kama kuna yeyote anayehukumu kuwa wenye takua wako sawa na wakosefu; sasa kuna haja gani ya Mwenyezi Mungu kusema: mnahukumu vipi?

Jibu : Ni kweli kuwa hakuna anayehukumu kuwa wakosefu na wenye takua wako sawa, lakini mara nyingi wakosefu wanajiona kuwa ni wacha Mungu na kwamba wao wanastahiki malipo na tahawabu wanazostahiki wenye takua.

Basi ndio Mwenyezi Mungu akalipinga hilo na kuwaambia, vipi mnajifanya mko sawa na wenye takua na kati yenu na wao kuna umbali wa mashriki na magharibi? Linalofahamisha maana haya kuwa ndio makusudio ni maswali haya yafuatayo:

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma? Kuwa mtapata humo mnayoyachagua?

Je, mna Kitabu kutoka mbinguni au ardhini mnachokisoma kwamba nyi­nyi duniani mtapata mnachokipenda na Akhera mpate mnachokitamani? Wasifu uko sawa na ule wa mayahudi na wanaswara: “Na Mayahudi na Manaswara wanasema: Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi vyake.” Juz. 6 (5:18).

Makusudio ya Aya tunayoifasiri ni ya vigogo wa kikuraishi. Ingawaje wao hawakudai kuwa na Kitabu, lakini lengo ni kuwanyamazisha, kwamba hakuna dalili wa mfano wa dalili kuwa wako sawa na wenye takua na kwamba wao watapata wanayoyataka.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 22 (35:30) na Juz. 25 (43:21)

Au mna viapo juu yetu vinavyofika Siku ya Kiyama ya kuwa mtapata mnayojihukumia?

Je, Mwenyezi Mungu amewaapia kiapo kizito na kuwapa ahadi msisitizo kuwa atawaingiza Peponi pamoja na wanaomcha Mungu? Kwamba hatabadilisha ahadi mpaka siku ya Kiyama?

Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?

Yaani waulize wewe Muhammad! Ni nani aliyeahidiana nao kutekelezewa madai yao?

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanase­ma kweli.

Makusudio ya washirika hapa ni masanamu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: “Sema: nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika.” Juz. 22 (34:27).

Maana ni kuwa haya nawalete hao washrikina waungu wanaowaabudu ili washuhudie kwamba wao watapata Pepo pamoja na wenye takua.

Msawali yote aliyoyaelekeza Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa washirikina ni kuwa hakuna kitu kinachofahamisha kwa karibu wala mbali kwamba washirikina wana chochote. Aina hii ya hoja ni katika nyenzo nzuri sana ya kumnyamazisha hasimu, wakati huo ikielimisha na kuleta uhakika.

Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza.

Waarabu wanaiita siku ngumu na yenye shida kuwa siku ya kufunuka muundi. Ndio maana siku ya Kiyama imeitwa hivyo. hakuna atakayetaki­wa kusujudi siku hiyo wala kufanya ibada nyingineyo, kwa sababu hiyo ni siku ya hisabu na malipo sio siku ya taklifa na matendo. Kwa hiyo basi kutakiwa kusujudi ni kwa njia ya kutahayariza, sio kwa sharia na taklifa.

Kwa hiyo makusudio ya kutoweza kusujudi siku hiyo ni kwamba hakutawafaa kitu kwa sababu siku hiyo ni ya malipo sio ya kufanya amali. Maana ni kuwa wale ambao wamepituka mipaka au wakafanya uzembe duniani walipokuwa na uwezo wa kufanya, watatahayarizwa na kuadhibi­wa siku ya Kiyama ambayo hakuna hila wala njia ya kuwakurubisha kwa Mwenyezi Mungu.

Macho yao yatanyenyekea.

Kunyenyekea ni sifa ya moyo, lakini Mwenyezi Mungu Mtukufu ameileta kwa kinaya cha udhalili wao na utwevu wao uliodhahiri machoni mwao. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:fedheha itawafunika , ni tafsiri na ubainifu wa hilo.

Na hakika walikuwa dunianiwakiitwa wasujudu, lakini walikataa kwa kiburi.walipokuwa salama, bila ya kizuizi chochote. Baada ya kuiona adhabu sasa ndio wanataka kusujudi, lakini wakati umekwishapita.

فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَـٰذَا الْحَدِيثِ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٤٤﴾

44. Basi niache na wanaokad­hibisha maneno haya! Tutawavuta kidogo kidogo kwa mahali wasipopajua.

وَأُمْلِي لَهُمْ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ ﴿٤٥﴾

45. Na ninawapa muda; hakika hila zangu ni imara.

أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ ﴿٤٦﴾

46. Au wewe unawaomba ujira, kwa hiyo wanalemewa na gharama?

أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ ﴿٤٧﴾

47. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wanaandika?

فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ ﴿٤٨﴾

48. Basi ingojee hukumu ya Mola wako, wala usiwe kama sahibu wa samaki, aliponadi naye amezongwa.

لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ ﴿٤٩﴾

49. Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufuk­weni naye ni mwenye kulau­miwa.

فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿٥٠﴾

50. Lakini Mola wake alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ ﴿٥١﴾

51. Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ ﴿٥٢﴾

52. Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

NIACHENI NA WANAOKADHIBISHA

Aya 44 - 52

MAANA

Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya!

Wanaokadhibisha ni washirikina wa kiarabu. Maneno ni Qur’an. Neno ‘niache na’ ni lakutangaza vita nao kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwam­ba Mwenyezi Mungu Yeye mwenyewe atatekeleza kuwaadhibu; apumue Nabii na wale walio pamoja naye kutokana nao na shari yao, kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akabainisha, vipi na kwa njia gani atawatesa pale aliposema:

Tutawavuta kidogo kidogo kwa mahali wasipopajua. Na ninawapa muda; hakika hila zangu ni imara.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anawapa muda wala hawafanyii haraka. Vile vile anawapa mali na watoto na kuwatoa kwenye hali nzuri hadi kwenye hali nzuri zaidi katika dhahiri ya maisha ya dunia, lakini wao kwa undani, wanagurishwa kutoka kwenye hali mbaya hadi kwenye hali mbaya zaidi; mpaka wakifikia kujiona kuwa wako katika ngome madhubuti, ndipo Mwenyezi Mungu huwapatiliza kwa mpatilizo wa mwenye nguvu mwenye uweza. Ili hilo liwe ni la kuumiza zaidi na kutia uchungu moyoni.

Mwenyezi Mungu amekuita huku kuvuta kidogo kidogo kuwa ni hila kwa sababu kunafanana na hila kwa dhahiri; vinginevyo ni kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kutakata na hila na vitimbi. Vipi isiwe hivyo na hali hakimbilii kwake ila mwenye kushindwa, na Mwenyezi Mungu husema kukiambia kitu ‘kuwa kikawa.’ Zaidi ya haya lengo la kutajwa vitimbi ni asihadaike mtu na dunia ikimkabili na kumpa tabasamu. Anatakikana awe na hadhari na yanayojificha.

Au wewe unawaomba ujira, kwa hiyo wanalemewa na gharama? Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wanaandika?

Je, unawataka mali inayokuwa na uzito kwao kuitoa, au wamejua ilimu ya siri kwa hiyo wakafuta yale wanayotakiwa kuamini. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 27 (40-41).

Basi ingojee hukumu ya Mola wako, wala usiwe kama sahibu wa samaki, aliponadi naye amezongwa.

Sahibu wa samaki ni Nabii Yunus ambaye alipata dhiki na watu wake na akawaacha kwa hasira. Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:97), Juz. 17 (21:87) na.Juz. 23 (37:140). Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuusia Nabii wake mtukufu(s.a.w.w) kuwa na subira na adha ya watu wake, wala asifanye haraka, kama alivyofanya Yunus, aliyemezwa na samaki, akanadi akiwa tumboni mwa samaki:

أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾

“Hapana Mola isipokuwa wewe, umetakasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.” Juz. 17 (21:87).

Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Yunus alimwomba Mola wake akiwa tumboni mwa samaki, akamwitikia dua yake kwa kumuhurumia, akatemwa na samaki akiwa si mwenye kulau­miwa. Lau si dua yake na kuhurumiwa na Mola wake angelikuwa katika wenye kulaumiwa; bali angelibakia tumboni mwa samaki hadi siku ya ufu­fuo. Ilivyo hasa nikuwa kulaumiwa hapa ni kwa sababu ya kuacha lilo bora sio kwa sababu ya dhambi na uasi.

Lakini Mola wake alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu kwa Yunus ni kwamba Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alimtoa tumboni mwa samaki, akiwa radhi naye, na akamrudisha kwa watu wake akiwa Nabii; kama alivyokuwa hapo mwanzo; wakanufaika naye na kwa mawaidha yake.

Lau angelibakia kati­ka tumbo la samaki hadi siku ya ufufuo, unabii wake usingelikuwa na athari yoyote. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “akamfanya mion­goni mwa watu wema,” ni kuwa atamfufua kesho pamoja na manabii.

Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wana­posikia mawaidha

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Maana ni kuwa washirikina wanaposikia Qur’an kutoka kwa Muhammad(s.a.w.w) wanamtazama kwa mtazamo wa kiuadui na chuki, na miguu ya Mtume(s.a.w.w) inakurubia kuteleza kutokana na mtazamo wao mkali kama mshale. Razi anasema: “Waarabu wanasema: Amenitazama kwa kwa mtazamo unaokaribia kuniangusha na kunila. Mshairi anasema: wakikutana macho huyazungusha, mtazamo wa nyoyo kuziangusha

Na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Walimtazama Mtume kwa mtazamo mkali, vile vile wakamtupia maneno makali, kama kusema kwao: Yeye ni mwendawazimu mwenyezi Mungu (s.w.t) amewarudi, mwanzo mwanzo mwa sura hii tuliyo nayo, kwa kuse­ma: “Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.”

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Makusudio ya ukumbusho ni ukumbusho wa heri na mwongozo wa njia yake. Maana ni kuwa Qur’an ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu aliouteremsha kwa Muhammad(s.a.w.w) ili awaongoze watu wote, kila mahali na kila wakati.

MWISHO WA SURA YA SITINI NA NANE: SURAT AL- QALAM

15

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Sura Ya Sitini Na Nane: Surat Al- Qalam. Imeshuka Makka. Imesemekana kuwa baadhi imeshuka Madina. Ina Aya 52.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

ن وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ ﴿١﴾

1. Nun. Naapa kwa kalamu na yale wanayoandika.

مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ ﴿٢﴾

2. Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.

وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ ﴿٣﴾

3. Na kwa hakika wewe una ujira usiokatika.

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ ﴿٤﴾

4. Na hakika wewe una tabia tukufu.

فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ ﴿٥﴾

5. Karibu utaona, na wao wataona.

بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ ﴿٦﴾

6. Ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ ﴿٧﴾

7. Hakika Mola wako ndiye anayemjua zaidi aliyepotea njia yake na Yeye ndiye anaye­wajua zaidi walioongoka.

فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ ﴿٨﴾

8. Basi usiwatii wanaokadhibisha.

وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ ﴿٩﴾

9. Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ ﴿١٠﴾

10. Wala usimtii kila mwingi wa kuapa aliye dhalili.

هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ ﴿١١﴾

11. Msingiziaji, apitae akifitini.

مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ﴿١٢﴾

12. Mwenye kuzuia heri, mwenye kudhulumu, mwingi wa mad­hambi.

عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ ﴿١٣﴾

13. Mwenye roho ngumu, juu ya hayo, ni mwanaharamu.

أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ ﴿١٤﴾

14. Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٥﴾

15. Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni ngano za watu wa kale!

سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ ﴿١٦﴾

16. Tutamtia doa juu ya pua.

WEWE SI MWENDAWAZIMU

Aya 1- 16

MAANA

Nun . kwa kukadiria maneno ya kuwa hii ni sura ya Nun. Hii sio kama mianzo mingineyo ya herufi zinazoanziwa sura, tulizozizungumzia katika Juz. 1 (2:1).

Kuna aliyesema kuwa ni samaki, mwingine akasema ni chombo cha wino, watatu akasema ni wino, wa nne akasema ni nun ya neno rahman, na jamaa wa kisufi wakasema kuwa ni nafsi. Kauli zote hizi zinahitajia dalili.

Naapa kwa kalamu na yale wanayoandika.

Wametofautiana kuhusu kalamu: Kuna waliosema ni kalamu iliyotumika kwenye lawh mahfud[ (ubao maalum uliohifadhiwa). Mwingne akasema ni kila kalamu, na kwamba herufi aliY na la` kwenye neno hili ni ya jinsi, ambayo inamaanisha kuenea.

Hii ndio kauli iliyo dhahiri; kwamba makusudio sio kalamu hasa, bali ni nyenzo yoyote ya kuandikia; kama inavyoashiria kauli inayofuatia inayosema: “Na yale wanayoyaandika.”

Kwa hiyo basi kalamu itakuwa ni kinaya cha chombo cha kuandikia, vyovyote kitakavyokuwa, kilichopo au kitakachogunduliwa karibuni au baadaye. Tumedokeza faida za ubainifu katika Juz. 27 (55:4), kwamba manufaa ya ubainifu ni sawa na manufaa ya maji na hewa.

Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) . Hakuna yeyote anayed­hania kuwa Muhammad(s.a.w.w) ni mwenda wazimu. Wale waliompa sifa hiyo walikusudia kuwa ana jinni linalompa wahyi; kama wanavyodai kwamba kila mshairi ana jinni linalomfundisha ushairi.

Hilo linaashiriwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu akiwasimulia:

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ﴿٣٦﴾

“Na wakisema: Hivi tuiache miungu miungu yetu kwa ajili ya huyu mshairi mwendawazimu?” Juz. 23 (37:36).

Na kwa hakika wewe una ujira usiokatika.

Neno ‘usiokatika’ tumelifasiri kutokana na neno mamnun, ambalo pia lina maana ya kusimbuliwa au maana zote mbili pamoja (kukatika na kusimbuliwa).

Kimsingi ni kuwa malipo yanapimwa kwa natija ya kazi na athari yake. Bado athari za Muhammad(s.a.w.w) , mwito wake na ukuu wake unaendela hadi leo, kuanzia mashariki mwa ardhi hadi magharibi yake na utaendelea hadi siku ya mwisho. Kwa hiyo si kioja kupata karama ya milele kutoka kwa Mola wake.

Na hakika wewe una tabia tukufu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakumsifu yeyote katika mitume wake na wasi­fa huu isipokuwa Muhammad.

Maana yake yanafupilizwa na kauli yake Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) : “Mola wangu amenifunza maadili akayafanya mazuri mafunzo yangu,” yaani Mwenyezi Mungu ameelekeza kwa Muhammad(s.a.w.w) maadili yale yale aliyoumba kwa ajli ya nafsi.

Vile vile Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuwahi kuapa kwa maisha ya mtu isipokuwa kwa maisha ya Muhammad(s.a.w.w) ; pale aliposema:

لَعَمْرُكَ إِنَّهُمْ لَفِي سَكْرَتِهِمْ يَعْمَهُونَ ﴿٧٢﴾

“Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao wakiman­gamanga.”

Juz. 14 (15:72).

Ama wasifu wa Muhammad(s.a.w.w) kuwa ni mwisho wa manabii, Maana yake ni kuwa Muhammad alifikia ukomo wa sifa za mtu zisizofikiwa na yeyote kwa ukamilifu. Ni muhali kuja baada yake atakayekuwa bora zaidi kuliko yeye au kuja na sharia bora zaidi ya sharia zake; bali hakuna kium­be yeyote kuanzia wa mwanzo hadi wa mwisho anayefanana naye. Hilo linaashiriwa na kauli yake Mtume(s.a.w.w) : “Mimi ni bwana wa watu wote, wala sisemi kwa kujifaharisha.”

Hii ni kwa kuwa sharia na utume umeishilizwa kwake. Ibn Al-arabiy anasema, katika Futuhat: kuwa Mwenyezi Mungu ameumba viumbe aina kwa aina, akafanya walio bora. Walio bora katika viumbe ni mitume, na katika mitume kuna wateule ambao ni ulul-az` na katika wao kuna mteule zaidi naye ni Muhammad(s.a.w.w) .

Karibu utaona, na wao wataona, ni nani kati yenu aliyepandwa na wazimu.

Hili ni onyo na kiaga, kwamba hivi karibuni itakubainikia wewe na maadui zako kwamba wao ndio wajinga, wapotevu na wendawazimu zaidi katika watu, na kwamba wewe ndiwe ulie juu, mwenye akili na mtukufu wa maadili zaidi ya watu wengine na kwamba ndiwe mtukufu wao zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu.

Hakika Mola wako ndiye anayemjua zaidi aliyepotea njia yake na Yeye ndiye anayewajua zaidi walioongoka.

Mwenyezi Mungu anajua cheo chako ewe Muhammad(s.a.w.w) na uongo­fu na anajua nafasi ya wahasimu wake ya upotevu na mbele yao kuna hisabu na malipo. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 14 (16:125).

Basi usiwatii wanaokadhibisha.

Washirikina walijaribu kila njia kumzuia Mtume(s.a.w.w) na mwito wake, wakajaribu kumbembeleza kwa cheo na mali, akakataa. Wakatamani lau watakubaliana naye kufanya vile watakavyo, Mwenyezi Mungu akamkataza hilo. Lengo la kumkataza ni kuwakatisha tamaa na wajue kuwa hakuna mjadala wala makubaliano katika twaa ya Mwenyezi Mungu na amri yake. Katazo hili linafanana na anayekutaka mkubaliane naye kwenye dini yako, ukiwa unataka kumkatisha tamaa kabisa, na kumwambia: Mwenyezi Mungu amenikataza hilo.

Wanatamani lau ungelainisha ili nao wakulainishie.

Washirikina walitamani Mtume(s.a.w.w) apunguze baadhi ya yale anayowalingania na wao waache baadhi ya yale aliyowakataza, ijapokuwa ni kwa njia ya kupakaka mafuta kwa mgongo wa chupa ili kusiwe na mvu­tano baina ya pande mbili.

Mfumo wa maneno unafahamisha kuwa aliyetoa maoni hayo anasifika na sifa aliyoiashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kusema:Wala usimtii kila mwingi wa kuapa aliye dhalili . Anakithirisha viapo bila ya sababu jambo linalomsababisha kuwa dhalili anayedharauliwa.Msingiziaji anawatia ila sana watu.Apitaye akifitini . Anajaribu kuwavuruga watu kwa kunukuuu ya huku akiyapeleka kule.

Mwenye kuzuia heri , yeye haifanyi na anazuia wengine wasiifanye.Mwenye kudhulumu , haki za watu.Mwingi wa madhambi na makosa.Mwenye roho ngumu, juu ya hayo, ni mwanaharamu, asiyejua nasaba yake. Hii ni sifa mbaya zaidi ya zote zinazofikiriwa na akili.

Wafasiri wengi wamesema kuwa aliyekusudiwa na ushenzi huu ni Walid bin Al-mughira, aliyekuwa ni miongoni mwa vigogo wa kikuraishi, mwenye mali nyingi na watoto; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:Ati kwa kuwa ana mali na watoto! Anaposomewa Aya zetu, husema: Hizi ni ngano za uwongoza watu wa kale!

Wafasiri wamesema kuwa Aya hii ni ya kukataza kumtii mshenzi huyu. Lakini lililo karibu zaidi na usawa ni kuwa huko kuwa na mali na watoto kumemfanya athubutu kusema Qur’an ni simulizi za watu wa zamani; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الْإِنسَانَ لَيَطْغَىٰ ﴿٦﴾ أَن رَّآهُ اسْتَغْنَىٰ ﴿٧﴾

“Hakika mtu hupituka mipaka kwa kujiona ametajirika.” (96:6-7).

Sikwambii tena akiwa na nguvu na watu.Tutamtia doa juu ya pua yake. Waarabu wanatumia kutaja pua kwa ajili ya utukufu na udhalii. Wanasema kwa utukufu: ana pua ya kunusa. Kwenye udhalili wanasema: pua yake ikio mchangani.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) atamfedhehesha mjeuri huyu ambaye amejitukuza kwa mali na watoto, atamdhalilisha muda wote, atam laani kwa lugha iliyosajiliwa kwenye Kitabu chake na atamfedhehesha Akhera mbele ya ushuhuda, kwa kusawijika uso na alama nyinginezo za kuakisi madhambi yake.

إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ ﴿١٧﴾

17. Hakika tumewajaribu kama tulivyowajaribu wenye sham­ba, walipoapa kwamba watal­ivuna itakapokuwa asubuhi.

وَلَا يَسْتَثْنُونَ ﴿١٨﴾

18. Wala hawakusema: Inshaallah!

فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ ﴿١٩﴾

19. Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako, nao wamelala!

فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ ﴿٢٠﴾

20. Likawa kama limefyekwa.

فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ ﴿٢١﴾

21. Wakaitana asubuhi.

أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ ﴿٢٢﴾

22. Ya kwamba raukeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ ﴿٢٣﴾

23. Basi walikwenda na huku wakinong’onezana.

أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ ﴿٢٤﴾

24. Ya kuwa leo asiliingie hata maskini mmoja.

وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ ﴿٢٥﴾

25. Na walirauka, nao wana nguvu za kunyima.

فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ ﴿٢٦﴾

26. Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea!

بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ ﴿٢٧﴾

27. Bali tumenyimwa!

قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ ﴿٢٨﴾

28. Akasema Mbora wao: Je, Sikuwambia, kwa nini hamumsabihi Mwenyezi Mungu?

قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ ﴿٢٩﴾

29. Wakasema: Ametakasika Mola wetu! Hakika tulikuwa madhalimu.

فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ ﴿٣٠﴾

30. Basi wakakabiliana kulau­miana wao kwa wao.

قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ ﴿٣١﴾

31. Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ ﴿٣٢﴾

32. Asaa Mola wetu akatubadil­ishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ ﴿٣٣﴾

Kama hivyo inakuwa adhabu, na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi, laiti wangelijua!

LIKAWA KAMA LIMEFYEKWA

Aya 17 – 33

MAANA

Hakika tumewajaribu kama tulivyowajaribu wenye shamba.

Waliojaribiwa ‧ katika neno tumewajaribu - ni washirikina wa kikuraishi waliomkadhibisha Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) ambao Mwenyezi Mungu amewaashiria katika Aya ya nane ya surua hii. ‘Basi usiwatii wanaokadhibisha.’ Akiwemo yule mwenye kupituka mipaka mwenye dhambi ambaye, kama walivyosema wafasri, ni Walid bin Almughira, kigogo wa makuraishi msemaji wa wakadhibishaji akielezea ufidhuli na jeuri yao juu ya haki.

Aya hizi tulizo nazo zinampigia mfano yeye na wao, kwamba kulikuwa na watu waliokuwa na shamba lililojaa mazao, lakini wao walikuwa mabahili kwa mafukara na masikini.

Mazao yalipokomaa na kukurubia kuvunwa walipanga njama na kuapa kuwa wavune shamba asubuhi na mapema, mafukara wakiwa hawana habari. Waliazimia hivyo bila ya kuyaunganisha maazimio yao na matakwa ya Mwenyezi Mungu. Waliambiana kuwa wawanyime wahitaji kile walichopewa na Mwenyezi Mungu, wakiwa wamesahau mipangilio ya Mwenyezi Mungu na uweza wake.

Usiku huo huo walioazimia kuvuna, Mwenyezi Mungu alilitermshia shamba janga la mbinguni lilioharibu mazao yote kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Walipoamka asubuhi na kwenda shambani walipigwa na butwaa, wakaan­za kulaumiana wenyewe kwa wenyewe, kila mmoja akimwambia mwen­zake: “Wewe ndiye sababu ya haya.” Miongoni mwao alikuwako mtu mwema aliyewapa nasaha kabla, lakini hawakumsikiliza, ndio akawaambia: Kwani sikuwaaambia, lakini mkakataa. Basi tubieni kwa Mola ili mpate kufaulu. Wakatubia kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu na wakam­womba msamaha na kutaka wahurumiwe na kuneemeshwa kutoka shambani mwao.

Lengo la kupiga mfano huu, ni kupata funzo kila aliyeneemeshwa na Mwenyezi Mungu; hasa watu wa Makka akiwemo yule mshenzi. Wapokezi wa Hadith wanasema watu wa Makka walipatwa na kahati na njaa kwa vile walimkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) , ndipo akawaombea majanga na Mwenyezi Mungu akaitikia maombi yake. Kahati iliendelea kiasi cha miaka saba mpaka wakawa wanakula mizoga na mifupa. Pia wapokezi wanasema Mwenyezi Mungu aliingamiza mali ya Walid.

Haya ndio makusudio ya Aya kwa ujumla wake. Ufuatao ni ufufanuzi wa Aya moja moja:-

Walipoapa kwamba watalivuna itakapokuwa asubuhi.

Wenye shamba waliapa kuwa watalivuna mafukara wakiwa hawana habari.

Wala hawakusema: Inshaallah!

Yaani hawakusema tutavuna asubuhi Mungu akipenda.

Tumefasiri wala hawakusema inshaallah! Kutokana na maneno ya kiarabu yastathnuua ambayo tafsiri yake ya moja kwa moja ni ‘hawakutenga au hawakutoa.’ Kwa hiyo baadhi ya wafasiri wakasema maana ni hawakutenga kitu kwa ajili ya masikini. Kila moja kati ya tafsiri mbili hizi inafaa. Vile vile zinaweza kwenda kwa pamoja.

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako, nao wamelala! Likawa kama limefyekwa.

Wenye shamba walilala raha mustarehe wakiwa na imani ya kulivuna shamba lao asubuhi na mapema, lakini usiku huo likafikwa na janga.

Neno kufyekwa, tumelifasiri kutokana na neno Asswarim, ambalo maana yake nyingine ni weusi, kwa maana ya kuungua na kuwa jeusi kama usiku wa giza

Wakaitana asubuhi, ya kwamba raukeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

Ilipofika asubuhi waliitana ili wawahi kwenda shamba bila ya masikini kujua.

Basi walikwenda na huku wakinong’onezana. Ya kuwa leo asiliingie hata masikini mmoja.

Walifanya haraka wakidhamiria kwa siri kuwa masikini asionje hata chembe ya mazao.

Hakuna mwenye shaka kuwa huu ni uchoyo. Ikiwa hawa shamba lilikuwa lao na mazao ni yao hawakuiba, lakini pamoja na hayo Mwenyezi Mungu aliwaghadhabikia na kuwaandalia adhabu; je, itakuwaje kwa yule aliyepituka mipaka kwenye maisha ya watu akawanyang’anya vyakula vyao, akawaua na kuwafukuza kwenye miji, kama wanavyofanya wakoloni hivi sasa katika mashariki ya dunia na magharibi yake?

Na walirauka, nao wana nguvu za kunyima.

Waliingia shambani mwao wakiwa na dhamira kabisa ya kuwanyima mafukara, wakiwa na mawazo kwamba shamba na mazao yake yako mikononi mwao. Hawakujua kuwa mkono wa Mwenyezi Mungu uko juu ya mikono yao.

Basi walipoliona, wakasema: Hakika tumepotea! Bali tumenyimwa!

Walipofika shamba yaliwashangaza waliyoyaona na wakakubali kuwa wamepotea na kusema: sisi ndio tuliokosa fadhila za Mwenyezi Mungu na thawabu zake, na tunastahili ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake na sio mafukara na masikini.

Miongoni mwao alikuwa mtu mwema aliyekuwa akiaamrisha mema na kuwakataza maovu, lakini hawakusikiliza nasaha zake. alipoona yaliyowafika:

Akasema Mbora wao: Je, Sikuwambia, kwa nini hamumsabi­hi Mwenyezi Mungu?

Yaani hamumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kauli wala kwa vitendo kwa kutoa. alisema hivi kwa kuwahurumia. Kisha akawaamuru kutubia:Wakasema: Ametakasika Mola wetu! Hakika tulikuwa madhalimu wa nafsi zetu kwa kumuasi Mwenyezi Mungu.

Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

Kila mmoja anamtupia lawama mwinziwe; kama ilivyo hali ya washiriki­na, wanapofikwa na yale yaliyofanywa na mikono yao.

Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

Walirudia akili zao na wakacha kulaumiana, wakakiri dhambi zao kwam­ba wao walikuwa katika upotevu, wakijiombea kufa kwa kusema ‘Ole wetu’ na kumwomba msamaha Mwenyezi Mungu, wakasema:Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

Hii ni dua na matarajio yao kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) awasamehe yaliyopita na awabadilishie yaliyo bora kuliko yaliyopita. Na Mwenyezi Mungu anakubali toba kutoka kwa waja wake, anawasamehe mengi na anaitikia maombi ya anayemuomba kwa ukweli na ikhlasi.

Kama hivyo inakuwa adhabu, na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi, laiti wangelijua!

Razi anasema hii iko wazi haihitaji tafsir, lakini sheikh Maraghi amekataa isipokuwa kuifasiri kwa kusema: “Yaani adhabu ya Akhera ni kali na inau­miza zaidi kuliko adhabu ya duniani.”

16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ ﴿٣٤﴾

34. Hakika wenye takua watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao.

أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ ﴿٣٥﴾

35. Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ﴿٣٦﴾

36. Mna nini? Mnahukumu vipi?

أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ ﴿٣٧﴾

37. Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ ﴿٣٨﴾

38. Kuwa mtapata humo mnayo yachagua?

أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ ﴿٣٩﴾

39. Au mna viapo juu yetu vinavyofika Siku ya Kiyama ya kuwa mtapata mnayo­jihukumia?

سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ ﴿٤٠﴾

40. Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?

أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ ﴿٤١﴾

41. Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao waki­wa wanasema kweli.

يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ ﴿٤٢﴾

42. Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusu­judu, lakini hawataweza.

خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ ﴿٤٣﴾

43. Macho yao yatanyenyekea fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipokuwa salama.

KWANI TUTAWAFANYA WAISLAMU KAMA WAKOSEFU?

Aya 34 – 43

MAANA

Hakika wenye takua watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao.

Katika Aya zilizotangulia Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaahidi wakosefu adhabu kubwa, na katika Aya hii anawaahidi wanaomcha Mwenyezi Mungu kuwa na milki ya daima na neema ya kudumu. Namna hii Mwenyezi Mungu analinganisha mwisho wa wakosefu na wa wenye takua; kwa kuvutia na kuhadharisha.

Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu? Mna nini? Mnahukumu vipi?

Makusudio ya waislamu hapa sio kila mwenye kusema: Lailaha ilallah muhammadur-rasulullah[ (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu); bali makusudio ni wanaom­cha Mwenyezi Mungu. Kwa sababu mazungumzo hapa yanahusiana na wao na yale waliyo nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu ya Pepo yenye neema.

Unaweza kuuliza : hatudhani kama kuna yeyote anayehukumu kuwa wenye takua wako sawa na wakosefu; sasa kuna haja gani ya Mwenyezi Mungu kusema: mnahukumu vipi?

Jibu : Ni kweli kuwa hakuna anayehukumu kuwa wakosefu na wenye takua wako sawa, lakini mara nyingi wakosefu wanajiona kuwa ni wacha Mungu na kwamba wao wanastahiki malipo na tahawabu wanazostahiki wenye takua.

Basi ndio Mwenyezi Mungu akalipinga hilo na kuwaambia, vipi mnajifanya mko sawa na wenye takua na kati yenu na wao kuna umbali wa mashriki na magharibi? Linalofahamisha maana haya kuwa ndio makusudio ni maswali haya yafuatayo:

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma? Kuwa mtapata humo mnayoyachagua?

Je, mna Kitabu kutoka mbinguni au ardhini mnachokisoma kwamba nyi­nyi duniani mtapata mnachokipenda na Akhera mpate mnachokitamani? Wasifu uko sawa na ule wa mayahudi na wanaswara: “Na Mayahudi na Manaswara wanasema: Sisi ni wana wa Mwenyezi Mungu na vipenzi vyake.” Juz. 6 (5:18).

Makusudio ya Aya tunayoifasiri ni ya vigogo wa kikuraishi. Ingawaje wao hawakudai kuwa na Kitabu, lakini lengo ni kuwanyamazisha, kwamba hakuna dalili wa mfano wa dalili kuwa wako sawa na wenye takua na kwamba wao watapata wanayoyataka.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 22 (35:30) na Juz. 25 (43:21)

Au mna viapo juu yetu vinavyofika Siku ya Kiyama ya kuwa mtapata mnayojihukumia?

Je, Mwenyezi Mungu amewaapia kiapo kizito na kuwapa ahadi msisitizo kuwa atawaingiza Peponi pamoja na wanaomcha Mungu? Kwamba hatabadilisha ahadi mpaka siku ya Kiyama?

Waulize: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?

Yaani waulize wewe Muhammad! Ni nani aliyeahidiana nao kutekelezewa madai yao?

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanase­ma kweli.

Makusudio ya washirika hapa ni masanamu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu: “Sema: nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika.” Juz. 22 (34:27).

Maana ni kuwa haya nawalete hao washrikina waungu wanaowaabudu ili washuhudie kwamba wao watapata Pepo pamoja na wenye takua.

Msawali yote aliyoyaelekeza Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa washirikina ni kuwa hakuna kitu kinachofahamisha kwa karibu wala mbali kwamba washirikina wana chochote. Aina hii ya hoja ni katika nyenzo nzuri sana ya kumnyamazisha hasimu, wakati huo ikielimisha na kuleta uhakika.

Siku utakapowekwa wazi muundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza.

Waarabu wanaiita siku ngumu na yenye shida kuwa siku ya kufunuka muundi. Ndio maana siku ya Kiyama imeitwa hivyo. hakuna atakayetaki­wa kusujudi siku hiyo wala kufanya ibada nyingineyo, kwa sababu hiyo ni siku ya hisabu na malipo sio siku ya taklifa na matendo. Kwa hiyo basi kutakiwa kusujudi ni kwa njia ya kutahayariza, sio kwa sharia na taklifa.

Kwa hiyo makusudio ya kutoweza kusujudi siku hiyo ni kwamba hakutawafaa kitu kwa sababu siku hiyo ni ya malipo sio ya kufanya amali. Maana ni kuwa wale ambao wamepituka mipaka au wakafanya uzembe duniani walipokuwa na uwezo wa kufanya, watatahayarizwa na kuadhibi­wa siku ya Kiyama ambayo hakuna hila wala njia ya kuwakurubisha kwa Mwenyezi Mungu.

Macho yao yatanyenyekea.

Kunyenyekea ni sifa ya moyo, lakini Mwenyezi Mungu Mtukufu ameileta kwa kinaya cha udhalili wao na utwevu wao uliodhahiri machoni mwao. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:fedheha itawafunika , ni tafsiri na ubainifu wa hilo.

Na hakika walikuwa dunianiwakiitwa wasujudu, lakini walikataa kwa kiburi.walipokuwa salama, bila ya kizuizi chochote. Baada ya kuiona adhabu sasa ndio wanataka kusujudi, lakini wakati umekwishapita.

فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَـٰذَا الْحَدِيثِ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٤٤﴾

44. Basi niache na wanaokad­hibisha maneno haya! Tutawavuta kidogo kidogo kwa mahali wasipopajua.

وَأُمْلِي لَهُمْ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ ﴿٤٥﴾

45. Na ninawapa muda; hakika hila zangu ni imara.

أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ ﴿٤٦﴾

46. Au wewe unawaomba ujira, kwa hiyo wanalemewa na gharama?

أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ ﴿٤٧﴾

47. Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wanaandika?

فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ ﴿٤٨﴾

48. Basi ingojee hukumu ya Mola wako, wala usiwe kama sahibu wa samaki, aliponadi naye amezongwa.

لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ ﴿٤٩﴾

49. Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufuk­weni naye ni mwenye kulau­miwa.

فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿٥٠﴾

50. Lakini Mola wake alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ ﴿٥١﴾

51. Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanaposikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ ﴿٥٢﴾

52. Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

NIACHENI NA WANAOKADHIBISHA

Aya 44 - 52

MAANA

Basi niache na wanaokadhibisha maneno haya!

Wanaokadhibisha ni washirikina wa kiarabu. Maneno ni Qur’an. Neno ‘niache na’ ni lakutangaza vita nao kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwam­ba Mwenyezi Mungu Yeye mwenyewe atatekeleza kuwaadhibu; apumue Nabii na wale walio pamoja naye kutokana nao na shari yao, kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akabainisha, vipi na kwa njia gani atawatesa pale aliposema:

Tutawavuta kidogo kidogo kwa mahali wasipopajua. Na ninawapa muda; hakika hila zangu ni imara.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anawapa muda wala hawafanyii haraka. Vile vile anawapa mali na watoto na kuwatoa kwenye hali nzuri hadi kwenye hali nzuri zaidi katika dhahiri ya maisha ya dunia, lakini wao kwa undani, wanagurishwa kutoka kwenye hali mbaya hadi kwenye hali mbaya zaidi; mpaka wakifikia kujiona kuwa wako katika ngome madhubuti, ndipo Mwenyezi Mungu huwapatiliza kwa mpatilizo wa mwenye nguvu mwenye uweza. Ili hilo liwe ni la kuumiza zaidi na kutia uchungu moyoni.

Mwenyezi Mungu amekuita huku kuvuta kidogo kidogo kuwa ni hila kwa sababu kunafanana na hila kwa dhahiri; vinginevyo ni kuwa Mwenyezi Mungu ni mwenye kutakata na hila na vitimbi. Vipi isiwe hivyo na hali hakimbilii kwake ila mwenye kushindwa, na Mwenyezi Mungu husema kukiambia kitu ‘kuwa kikawa.’ Zaidi ya haya lengo la kutajwa vitimbi ni asihadaike mtu na dunia ikimkabili na kumpa tabasamu. Anatakikana awe na hadhari na yanayojificha.

Au wewe unawaomba ujira, kwa hiyo wanalemewa na gharama? Au wanayo ilimu ya ghaibu, nao wanaandika?

Je, unawataka mali inayokuwa na uzito kwao kuitoa, au wamejua ilimu ya siri kwa hiyo wakafuta yale wanayotakiwa kuamini. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 27 (40-41).

Basi ingojee hukumu ya Mola wako, wala usiwe kama sahibu wa samaki, aliponadi naye amezongwa.

Sahibu wa samaki ni Nabii Yunus ambaye alipata dhiki na watu wake na akawaacha kwa hasira. Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:97), Juz. 17 (21:87) na.Juz. 23 (37:140). Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuusia Nabii wake mtukufu(s.a.w.w) kuwa na subira na adha ya watu wake, wala asifanye haraka, kama alivyofanya Yunus, aliyemezwa na samaki, akanadi akiwa tumboni mwa samaki:

أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾

“Hapana Mola isipokuwa wewe, umetakasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.” Juz. 17 (21:87).

Kama isingelimfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

Yunus alimwomba Mola wake akiwa tumboni mwa samaki, akamwitikia dua yake kwa kumuhurumia, akatemwa na samaki akiwa si mwenye kulau­miwa. Lau si dua yake na kuhurumiwa na Mola wake angelikuwa katika wenye kulaumiwa; bali angelibakia tumboni mwa samaki hadi siku ya ufu­fuo. Ilivyo hasa nikuwa kulaumiwa hapa ni kwa sababu ya kuacha lilo bora sio kwa sababu ya dhambi na uasi.

Lakini Mola wake alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

Miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu kwa Yunus ni kwamba Yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu alimtoa tumboni mwa samaki, akiwa radhi naye, na akamrudisha kwa watu wake akiwa Nabii; kama alivyokuwa hapo mwanzo; wakanufaika naye na kwa mawaidha yake.

Lau angelibakia kati­ka tumbo la samaki hadi siku ya ufufuo, unabii wake usingelikuwa na athari yoyote. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “akamfanya mion­goni mwa watu wema,” ni kuwa atamfufua kesho pamoja na manabii.

Na waliokufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wana­posikia mawaidha

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Maana ni kuwa washirikina wanaposikia Qur’an kutoka kwa Muhammad(s.a.w.w) wanamtazama kwa mtazamo wa kiuadui na chuki, na miguu ya Mtume(s.a.w.w) inakurubia kuteleza kutokana na mtazamo wao mkali kama mshale. Razi anasema: “Waarabu wanasema: Amenitazama kwa kwa mtazamo unaokaribia kuniangusha na kunila. Mshairi anasema: wakikutana macho huyazungusha, mtazamo wa nyoyo kuziangusha

Na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

Walimtazama Mtume kwa mtazamo mkali, vile vile wakamtupia maneno makali, kama kusema kwao: Yeye ni mwendawazimu mwenyezi Mungu (s.w.t) amewarudi, mwanzo mwanzo mwa sura hii tuliyo nayo, kwa kuse­ma: “Kwa neema ya Mola wako wewe si mwendawazimu.”

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Makusudio ya ukumbusho ni ukumbusho wa heri na mwongozo wa njia yake. Maana ni kuwa Qur’an ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu aliouteremsha kwa Muhammad(s.a.w.w) ili awaongoze watu wote, kila mahali na kila wakati.

MWISHO WA SURA YA SITINI NA NANE: SURAT AL- QALAM


4

5

6

7