TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 10541
Pakua: 2598


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10541 / Pakua: 2598
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

Mwandishi:
Swahili

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ مُوسَىٰ إِنَّهُ كَانَ مُخْلَصًا وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥١﴾

51. Na mtaje Musa katika Kitabu, hakika yeye alikuwa ni Mwenye kutakaswa na alikuwa Mtume Nabii

وَنَادَيْنَاهُ مِن جَانِبِ الطُّورِ الْأَيْمَنِ وَقَرَّبْنَاهُ نَجِيًّا ﴿٥٢﴾

52. Na tulimwita upande wa kuume wa Tur na tukamkurubisha kunong’ona naye.

وَوَهَبْنَا لَهُ مِن رَّحْمَتِنَا أَخَاهُ هَارُونَ نَبِيًّا ﴿٥٣﴾

53. Na tukampa kutokana na rehema zetu nduguye, Haruna, awe Nabii

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِسْمَاعِيلَ إِنَّهُ كَانَ صَادِقَ الْوَعْدِ وَكَانَ رَسُولًا نَّبِيًّا ﴿٥٤﴾

54. Na mtaje katika Kitabu, Ismail, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii.

وَكَانَ يَأْمُرُ أَهْلَهُ بِالصَّلَاةِ وَالزَّكَاةِ وَكَانَ عِندَ رَبِّهِ مَرْضِيًّا ﴿٥٥﴾

55. Na alikuwa akiwaamrisha watu wake swala na zaka na alikuwa mbele ya Mola wake mwenye kuridhiwa.

وَاذْكُرْ فِي الْكِتَابِ إِدْرِيسَ إِنَّهُ كَانَ صِدِّيقًا نَّبِيًّا ﴿٥٦﴾

56. Na mtaje katika Kitabu, Idris, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii

وَرَفَعْنَاهُ مَكَانًا عَلِيًّا ﴿٥٧﴾

57. Na akamwinua mahali pa juu

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مِّنَ النَّبِيِّينَ مِن ذُرِّيَّةِ آدَمَ وَمِمَّنْ حَمَلْنَا مَعَ نُوحٍ وَمِن ذُرِّيَّةِ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْرَائِيلَ وَمِمَّنْ هَدَيْنَا وَاجْتَبَيْنَا إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُ الرَّحْمَـٰنِ خَرُّوا سُجَّدًا وَبُكِيًّا ﴿٥٨﴾

58. Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha miongoni mwa manabii katika uzao wa Adam na katika wale tuliowapandisha pamoja na Nuh na katika uzao wa Ibrahim na Israil na katika wale tuliowaongoa na tukawateua. Wanaposomewa Aya za Mwingi wa rehema huanguka kusujudu na kulia.

MUSA, ISMAIL NA IDRIS

Aya 51-58

MAANA

Na mtaje Musa katika Kitabu, hakika yeye alikuwa ni Mwenye kutakaswa na alikuwa Mtume Nabii.

Neno kutakaswa limefasiriwa kutokana na neno mukhlaswa kwa maana ya kuwa Mwenyezi Mungu amemtakasa na kila lisilopendeza na akamteua Yeye Mwenyewe. Ikiwa litasomwa, Mukhliswa, litakuwa na maana yakuwa kauli za Musa na vitendo vyake vyote ni vya ikhlasi.

Maana ya Mtume na Nabii ni moja, tofauti iko katika matamshi. Mtume au Mjumbe kwa kuwa anachukua ujumbe wa Mungu na Nabii (lenye maana ya kuzindua na kutoa habari), kwa maana ya kuwa anawazindua na kuwapa habari wale anaowapelekea ujumbe.

Wengine wamesema kuwa Mtume ni yule anayepokea wahyi na kuufikisha na Nabii ni yule anayepokea wahyi tu, lakini haufikishi, Utafiti huu hauna faida yoyote.

Na tulimwita upande wa kuume wa Tur na tukamkurubisha kunong’ona naye.

Tur ni mlima ambao Mwenyezi Mungu alizungumza na Musa. Makusudio ya kuumeni ni kuumeni kwa Musa; Kwa sababu mlima hauna kuume wala kushoto.

Makusudio ya kuumkurubisha kunong’na naye, ni kumkurubisha kihadhi sio ukaribu wa mahali. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu alimtukuza Musa kwa unabii na utume na kuzungumza naye moja kwa moja bila ya kuweko mjumbe mwengine.

Maneno yalikuwa yakimjia Musa kuumeni kwake; kama vile watu walivyo na mazoweya ya kusema: Nimesikia sauti kuumeni kwangu au kushotoni mwangu.

Na tukampa kutokana na rehema zetu nduguye, Haruna, awe Nabii

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anaashiria, kwa Aya hii, jambo lilokwishapita, nalo ni kuwa Mwenyezi Mungu alipomwamrisha Musa kwenda kwa Firauni, Musa alimuomba Mwenyezi Mungu kwa kusema: Na nipe waziri katika watu wangu, Harun ndugu yangu, niongeze nguvu zangu kwaye (20:30)

KUTEKELEZA AHADI

Na mtaje katika Kitabu, Ismail, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii. Na alikuwa akiwaamrisha watu wake swala na zaka na alikuwa mbele ya Mola wake mwenye kuridhiwa.

Maana yako wazi haihitajiki tafsiri, Ni jambo zuri tukizungumzia ahadi kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu: “Alikuwa ni mkweli wa ahadi” Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu Ismail kwamba yeye anapoahidi kitu hutekeleza.

Wafasiri wamesema kuwa Ismail siku moja aliahidiana na sahibu yake amngojee mahali, Yule mtu akachelewa, akamngoja siku tatu au zaidi.

Ni sawa riwaya hii iwe sahihi au la, lakini inaonyesha kwamba ni juu ya mtu kufanya bidii, kadiri atakavyoweza kutekeleza ahadi yake.

Na kwamba atakayeacha ahadi, haifai kumwamini na kitu chochote; bali inafaa tumpe sifa ya urongo na udanganyifu; hata kama kutekeleza ahadi kuna hasara ya kimaada, kwa sababu hasara ya kidini ni kubwa zaidi.

Kuna riwaya inayosema kuwa kutekeleza ahadi ni katika alama ya dini na kwamba dini ni maingiliano. Kuna kauli mashuhuri inayosema: ‘Asiyekuwa na ahadi hana dini’

Nimesoma maneno kuhusu ahadi nikaokota baadhi yake kama ifuatavyo:-

• “Mwenye kuacha ahadi kwa sababu ya matatizo atakuwa anajaribu kukikmbia kujituhumu, lakini hali halisi itamtuhumu.

• Kutekeleza ahadi ni tamko zuri katika masikio na ni zuri katika maisha.

• Makusudio ya kutekeleza ahadi nikuwatekelezea ahadi watu wa nyum- bani na marafiki na kuitumikia nchi na mwisho kwa watu wote.

• Utekelezaji ahadi unakufanya upende maisha na kuhalifu kunakufanya uchukie maisha.

• Maana ya kutekeleza ahadi kwa ajili ya watu wa nyumbani na marafiki ni kufanya kazi kwa ajili yao bila ya malipo na kutekeleza ahadi kwa ajili ya nchi ni kujitolea muhanga”

Na mtaje katika Kitabu, Idris, Hakika yeye alikuwa mkweli wa ahadi na alikuwa Mtume, Nabii Mwenyezi Mungu amemsifu kwa ukweli na utume na akamwinua mahali pa juu.

Makusudio ya mahali hapa ni cheo. Imesekana kuwa Mwenyezi Mungu alimwinua mpaka mbingu ya nne, wengine wakasema ni ya saba, kwa kudhania tu. Katika tafsiri imeelezwa kuwa Idris ni babu wa baba yake Nuh, na kwam- ba yeye ndiye wa kwanza kushona nguo, kuandika kwa kalamu, kuangalia nyota na taaluma ya hisabu, Hatujui wafasiri wameyatoa wapi haya.

Mwanafasihi mashuhuri aitwayeTawfiki amandika tamthilia aliyoiita Izyis, Akasema kuwa Izyis huyu ndiye mke wa Ozyrys ambaye aliteswa na mfalme Typhoon. Ikasemekana kuwa Ozyrys huyu ndiye Idris aliyeashiri- wa na Qur’an. Lakini kauli zote hizi ni mawazo na hisia tu.

Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaneemesha miongoni mwa manabii katika uzao wa Adam na katika wale tuliowapandisha pamoja na Nuh na katika uzao wa Ibrahim na Israil na katika wale tuliowaongoa na tukawateua. Wanaposomewa Aya za Mwingi wa rehema huanguka kusujudu na kulia.

Amesema Razi na Tabrasiy: makusudio ya kizazi cha Adam ni Idris, kwa sababu yeye ndiye aliyewatangulia wote na yuko karibu zaidi na Adam kuliko Nuh.

Makusudio ya kizazi cha waliopandishwa pamoja na Nuh ni Ibrahim, kwa sababu yeye ni katika kizazi cha Sam. Makusudio ya kizazi cha Ibrahim ni Is-haq, Ismail, na Ya’qub, Israil ndiye Ya’qub. Miongoni mwa kizazi chake ni Musa, Harun, Zakariya, Yahya na Isa kwa upande wa mama.

Wote hao na wengineo ni wale aliwaongoza Mwenyezi Mungu na kuwateua kwa utume, wanamnyenyekea Mwenyezi Mungu na kuhofia ghadhabu yake na adhabu yake pamoja na kuwa wao wanamfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu na kutenda kwa amri yake. Basi inatakikana yule mwenye kujasiri kumuasi Mungu atubie na ahisi hofu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.

فَخَلَفَ مِن بَعْدِهِمْ خَلْفٌ أَضَاعُوا الصَّلَاةَ وَاتَّبَعُوا الشَّهَوَاتِ فَسَوْفَ يَلْقَوْنَ غَيًّا ﴿٥٩﴾

59. Wakafuata baadae wazawa wabaya walioiacha swala na wakafuata matamanio. Basi watakujakuta malipo ya ubaya

إِلَّا مَن تَابَ وَآمَنَ وَعَمِلَ صَالِحًا فَأُولَـٰئِكَ يَدْخُلُونَ الْجَنَّةَ وَلَا يُظْلَمُونَ شَيْئًا ﴿٦٠﴾

60. Ispokuwa waliotubu, wakaamini na wakatenda mema, Hapo basi wataingia (Bustani) Peponi wala hawatadhulumiwa chochote.

جَنَّاتِ عَدْنٍ الَّتِي وَعَدَ الرَّحْمَـٰنُ عِبَادَهُ بِالْغَيْبِ إِنَّهُ كَانَ وَعْدُهُ مَأْتِيًّا ﴿٦١﴾

61. Bustani za milele ambazo Mwingi wa rehema aliwaahidi waja wake kwa ghaibu, Hakika Yeye ahadi yake itafika.

لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا إِلَّا سَلَامًا وَلَهُمْ رِزْقُهُمْ فِيهَا بُكْرَةً وَعَشِيًّا ﴿٦٢﴾

62. Hawatasiki humo upuuzi isipokuwa salama tu na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni

تِلْكَ الْجَنَّةُ الَّتِي نُورِثُ مِنْ عِبَادِنَا مَن كَانَ تَقِيًّا ﴿٦٣﴾

63. Hiyo ndiyo Bustani (Pepo) tutakayowarithisha katika waja wetu waliokuwa na takua

وَمَا نَتَنَزَّلُ إِلَّا بِأَمْرِ رَبِّكَ لَهُ مَا بَيْنَ أَيْدِينَا وَمَا خَلْفَنَا وَمَا بَيْنَ ذَٰلِكَ وَمَا كَانَ رَبُّكَ نَسِيًّا ﴿٦٤﴾

64. Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu na yaliyoko baina ya hayo, Na Mola wako si mwenye kusahau.

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴿٦٥﴾

Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake. Basi muabudu Yeye na uwe na subira kwa ibada yake, Je, unamjua somo yake?

WAKAJA BAADA YAO WALIO WABAYA

Aya 59 – 65

MAANA

Wakafuata baadae wazawa wabaya walioiacha swala na wakafuata matamanio.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwataja Mitume watakatifu, anaashiria waovu waliowafuatilia, akawapa wasifu wa kuwacha ibada ya mwingi wa rehema na kumfuata shetani. Maana haya yanafupika kwenye ibara hii: ‘Bora ni waliopita, wabaya ni waliokuja’

Basi watakujakuta malipo ya ubaya, Shari na adhabu ikiwa ni malipo ya maasi yao na inadi yao.

Ispokuwa waliotubu, wakaamini na wakatenda mema, Hapo basi wataingia Bustani (Peponi) wala hawatadhulumiwa chochote.

Tafsiri nzuri ya Aya hii ni kauli ya Mtume mtukufu(s.a.w.w) :“Mwenye kutubia dhambi ni kama asiye na dhambi” , Umetangulia mfano wake katika Juz; 7 (6:54).

Bustani za milele, Zipo daima, neema yake haikatiki wala hakimwi mkaaji wake.

Ambazo Mwingi wa rehema aliwaahidi waja wake kwa ghaibu.

Makusudio ya waja wake hapa ni waumini wenye ikhlasi. Kwa ghaibu ni kuwa wao waliamini Pepo ikiwa iko ughaibuni, Mwenyezi Mungu ame- wasifu waumini kuwa wanaoamini ghaibu katika Aya kadhaa.

Hakika Yeye ahadi yake itafika.

Yaani Mwenyezi Mungu havunji ahadi.

Hawatasikia humo upuuzi isipokuwa salama tu na watapata humo riziki zao asubuhi na jioni.

Katika maisha ya dunia ni upuuzi uwongo na matusi, lakini Peponi ni kauli njema na riziki isiyokoma. Asubuhi na jioni ni fumbo la kudumu, kwa sababu Peponi hakuna asubuhi wala jioni.

Hiyo ndiyo Pepo tutakayowarithisha katika waja wetu waliokuwa na takua.

Neni ‘tutawarithisha’ linatambulisha kuwa Pepo ni ya wenye takua. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Hao ndio warithi ambao watarithi Firdausi. Humo watadumu” (23: 11)

Wala hatuteremki ila kwa amri ya Mola wako. Ni yake Yeye yaliyoko mbele yetu na yaliyoko nyuma yetu na yaliyoko baina ya hayo.

Katika Tafsiri Tabariy na Tabrasi, imeelezwa kwamba wahyi ulichelewa kushuka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Aliposhuka Jibril, Mtume akamuuliza ni lipi lililokuzuia hata usitutembelee mara kwa mara, kama ulivyokuwa ukifanya? Ikashuka Aya hii, dhahiri yake inaafikiana na Aya hii, hasa kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na Mola wako si mwenye kusahau.

Maana ni kuwa amri ya kuteremshwa wahyi ni ya Mwenyezi Mungu peke yake. Yeye ndiye mmiliki wa kila kitu na ujuzi wake umekizunguka kila kitu na kila mahali, kilipokuwa na kitakapokuwa.

Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘yaliyoko mbele yetu’ ni ishara ya yatakayokuja, na ‘yaliyoko nyuma yetu’ ni yaliyopita na ‘yaliyoko baina ya hayo’ ni yaliyoko sasa.

Mola wa mbingu na Ardhi na vilivyo baina yake.

Ambaye ni Mola wa ulimwengu itakuwa muhali kwake kusahahu.

Basi muabudu Yeye na uwe na subira kwa ibada yake.

Hii ni amri kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Mtume wake kwamba aendelee na na umuhimu wake wa kufikisha (tabligh) mwito, kwa sababu hiyo ni katika ibada kubwa, na kuvumilia maudhi katika njia yake.

Je, unamjua somo yake?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hana kifani na chochote, katika sifa zake za utukufu na ukamilifu. Basi anayekuwa hivyo anawajibikiwa na kuabudiwa na kutiiwa.

وَيَقُولُ الْإِنسَانُ أَإِذَا مَا مِتُّ لَسَوْفَ أُخْرَجُ حَيًّا ﴿٦٦﴾

66. Na mtu husema: Hivi nitakapokufa, ni kweli nitatolewa niwe hai?

أَوَلَا يَذْكُرُ الْإِنسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِن قَبْلُ وَلَمْ يَكُ شَيْئًا ﴿٦٧﴾

67. Je, hakumbuki mtu ya kwamba tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote?

فَوَرَبِّكَ لَنَحْشُرَنَّهُمْ وَالشَّيَاطِينَ ثُمَّ لَنُحْضِرَنَّهُمْ حَوْلَ جَهَنَّمَ جِثِيًّا ﴿٦٨﴾

68. Basi naapa kwa Mola wako! Hakika tutawakusanya na mashetani. Kisha tutawahud hurisha kandokando ya Jahanna mnao wamepiga magoti

ثُمَّ لَنَنزِعَنَّ مِن كُلِّ شِيعَةٍ أَيُّهُمْ أَشَدُّ عَلَى الرَّحْمَـٰنِ عِتِيًّا ﴿٦٩﴾

69. Kisha Kwa hakika tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao waliozidi kumwasi Mwingi wa rehema

ثُمَّ لَنَحْنُ أَعْلَمُ بِالَّذِينَ هُمْ أَوْلَىٰ بِهَا صِلِيًّا ﴿٧٠﴾

70. Tena hakika sisi tunawajua vizuri wanaostahiki kuunguzwa humo.

وَإِن مِّنكُمْ إِلَّا وَارِدُهَا كَانَ عَلَىٰ رَبِّكَ حَتْمًا مَّقْضِيًّا ﴿٧١﴾

71. Hakuna Miongoni mwenu ila ni mwenye kuifikia. Ni hukumu ya Mola wako, ni lazima itimizwe.

ثُمَّ نُنَجِّي الَّذِينَ اتَّقَوا وَّنَذَرُ الظَّالِمِينَ فِيهَا جِثِيًّا ﴿٧٢﴾

72. Kisha tutawaokoa wale wenye takua na tutawaacha madhalimu hapo wamepiga magoti.

KWELI NITATOLEWA HAI?

Aya 66 –72

MAANA

Na mtu husema: hivi nitakapokufa, ni kweli nitatolewa niwe hai? Je hakumbuki mtu ya kwamba tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote?

Kwa ufupi ni kuwa, hakuna kitu mbele ya mwenye kupinga ufufuo anachopima nacho isipokuwa kustaajabu; vipi utarudi uhai baada ya kumuondokea binadamu? Jibu ni kuwa ataurudisha mara ya pili yule aliyeuleta kwanza: ‘tulimuumba kabla na hali hakuwa chochote’. Maana ya Aya hii yamekaririka katika Aya kadhaa, Angalia Juz; 1 (2:28-29), Juz; 2 (4:87) na Juz. 13 (13:5).

Basi naapa kwa Mola wako! Hakika tutawakusanya na mashetani.

Tutawakusanya hao wanaopinga ufufuo, Makusudio ya kukusanywa ni kutolewa kwao makaburini mwao wakiwa madhalili, wamedharaulika pamoja na wale waliowapoteza

Kisha tutawahudhurisha kandokando ya Jahannam nao wamepiga magoti.

Baada ya kutoka makaburini mwao na hali mbaya hiyo, Malaika watawakalisha wakiwa wamepiga magoti, kandokando ya Jahannam ili waiangalie, wazidi machungu na masikitiko.

Kisha kwa hakika tutawatoa katika kila kundi wale miongoni mwao waliozidi kumwasi Mwingi wa rehema.

Baada ya kuizunguka Jahannam wakiwa wamepiga magoti, wakiwa ni makundi mbali mabali, Mwenyezi Mungu kwanza atachukua kiongozi kutoka kila kundi na kuwatupa katika Jahannam, kisha wanaowafuatia. Kila mmoja atawekwa mahali pake panapomstahiki katika adhabu ya kuungua

Tena hakika sisi tunawajua vizuri wanaostahiki kuunguzwa humo

Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua maovu anayoyafanya kisiri na kidhahiri na atamlipa anavyostahili.

Mwenye madhambi makubwa adhabu yake ni kubwa, kisha anayefuatia na mwingine anayefuatia “Na watakuta waliyoyafanya yamehudhurishwa” Juz; 15 (18: 49).

Hakuna miongoni mwenu ila ni mwenye kuifikia. Ni hukumu ya Mola wako, ni lazima itimizwe. Kisha tutuwaokoa wale wenye takua na tutawaacha madhalimu hapo wamepiga magoti.

Makusudio ya kufikia hapa ni kuona na kushuhudia, kwa sababu waumini wataepushwa na moto; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الَّذِينَ سَبَقَتْ لَهُم مِّنَّا الْحُسْنَىٰ أُولَـٰئِكَ عَنْهَا مُبْعَدُونَ ﴿١٠١﴾

“Hakika wale ambao wema wetu umewatangulia wataepushwa nao” (21:101).

Pia kwamba kuadhibiwa mtiifu kunapingana na uadilifu wa Mungu. Maana ni kuwa hakuna yeyote kati ya mwema na muovu ila atauona waziwazi. Muovu atauona kisha aungie hali amepiga magoti na mwema atauona na aupite hali ya kushukuru neema ya kuokoka na mwako wake:

فَمَن زُحْزِحَ عَنِ النَّارِ وَأُدْخِلَ الْجَنَّةَ فَقَدْ فَازَ ﴿١٨٥﴾

“Mwenye kuepushwa na moto akatiwa Peponi, basi huyo amefuzu” Juz, 4 (3:185)

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَيُّ الْفَرِيقَيْنِ خَيْرٌ مَّقَامًا وَأَحْسَنُ نَدِيًّا ﴿٧٣﴾

73. Na wanaposomewa Aya zetu zilizowazi, waliokufuru huwaambia walioamini: lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lililo bora barazani

وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هُمْ أَحْسَنُ أَثَاثًا وَرِئْيًا ﴿٧٤﴾

74. Na karne ngapi tuliziangamiza zilizokuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa mandhari?

قُلْ مَن كَانَ فِي الضَّلَالَةِ فَلْيَمْدُدْ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ مَدًّا حَتَّىٰ إِذَا رَأَوْا مَا يُوعَدُونَ إِمَّا الْعَذَابَ وَإِمَّا السَّاعَةَ فَسَيَعْلَمُونَ مَنْ هُوَ شَرٌّ مَّكَانًا وَأَضْعَفُ جُندًا ﴿٧٥﴾

75. Sema: aliye katika upotofu basi Mwingi wa rehema atampa muda mpaka ayaone aliyoahidiwa –Ama ni adhabu au ni saa. Hapo ndipo watajua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu

وَيَزِيدُ اللَّـهُ الَّذِينَ اهْتَدَوْا هُدًى وَالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ خَيْرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابًا وَخَيْرٌ مَّرَدًّا ﴿٧٦﴾

76. Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wale walioongoka, Na mema yenye kubaki ni bora katika malipo mbele ya Mola wako na yana mwisho mwema.

LIPI KATI YA MAKUNDI MAWILI

Aya 73-76

MAANA

Na wanaposomewa Aya zetu zilizowazi, waliokufuru huwaambia walioamini: lipi katika makundi mawili lenye cheo kizuri na lililo bora barazani?

Aya za Mwenyezi Mungu zilizo wazi ni dalili, makundi mawili ni waumi- ni na washirikina. Maana ni kuwa Mtume na maswahaba wanawapa washirikina hoja ya mantiki, kiakili na kimaumbile na wao wanajibu kwa mantiki ya tumbo na falsafa yake.

FALSAFA YA TUMBO

Epikouros alikuwa ni mwanafalsafa wa kiyunani (ugiriki) katika wanafunzi wa Aristatle, alikuwa na madhehebu yake peke yake yaliyotofautiana na wenzake na pia wale waliomtangulia.

Kwa ufupi anasema ladha ndio kheri kuu na machungu ndio shari kuu na kwamba thamani ya fadhila inategemea ladha za kimaana; kama ukweli, maisha ya utulivu na raha na pia ladha za kihisia; kama chakula na kinywaji...

Katika mwongozo wa falsafa hii anasema: Mtu asisukumwe na hawa yake na upendeleo wake kwenye ladha fupi itakayofuatiwa na machungu marefu.

Kwa maneno mengine ni kuwa, kwake yeye Epikouros – akiwa haamini ufufuo- ni kwamba kheri yote inakuwa kwenye ladha ya kidunia; ni sawa iwe kwenye tumbo au kwengineko. Kama itakutana na machungu basi linalozingatiwa ni wingi, lile lenye ladha nyingi litakuwa ni kheri na lenye machungu mengi basi ni shari.

Kuna falsafa ya kale inayoaifikiana na Epikouros kwamba kheri yote iko kwenye ladha ya dunia. Yeye anasema kheri iko kwenye ladha ya kimaana na kihisia pamoja nayo anasema kheri iko kwenye ladha ya tumbo na mengineyo ya hisia.

Miongoni mwa wenye falsafa hii ni Firauni na washirikina wa kiquraysh. Firauni alipinga utume wa Musa(a.s) , akaleta sababu ya kupinga kwake kwa kusema:

“Au mimi si bora kulio huyu aliye mnyonge wala hawezi kusema wazi. Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu...” (43: 52 – 53)

Akasema tena:

فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

“Mimi Ndiye Mola wenu Mkubwa” (79:24).

Kisha akaendela:

أَلَيْسَ لِي مُلْكُ مِصْرَ وَهَـٰذِهِ الْأَنْهَارُ تَجْرِي مِن تَحْتِي ﴿٥١﴾

“Kwani ufalme wa Misri si wangu na hii mito inapita chini yangu?” (43:51).

Makurishi nao, kama Firauni, walikanusha utume wa Muhmmad (s.a.w.) na wakatoa hoja kwa kusema:

لَوْلَا أُنزِلَ عَلَيْهِ كَنزٌ ﴿١٢﴾

“Mbona hakuteremshiwa hazina?” Juz;12 (11:12)

Falsafa hii haihusiki na Firauni na washirikina wa Makka tu, wala na watanuzi na wenye utajiri; isipokuwa inahusika na kila anayemuheshimu mtu na akampima kwa mali yake, basi yeye ni katika walioamini falsafa ya tumbo.

Miongoni mwa niliyoyasoma ni maneno ya kibaraka mmoja aliyesema: “Hawa wanaoilaumu Marekani na majeshi yake na wanavyowapiga wakombozi kila mahali na vile wanavyopora mali za wanyonge kila mahali, wamesahau au wanajitia kusahahu kuwa Marekani ina nguvu za kielimu na mali; na kwamba mwenye nguvu mpishe.”

Nilikuwa nikidhania kuwa falsafa ya tumbo ilikwisha kwenye zama za dhulma, lakini makala haya nilyoyasoma yamenifanya nitambue kuwa falsafa hii imekita mizizi kwenye nafsi za wapiga debe wa ukoloni na vibaraka wake.

Na karne ngapi tuliziangamiza zilizokuwa na mapambo mazuri zaidi na wazuri zaidi kwa mandhari?

Umetangulia mfano wake katika Juz.7 (6:6)

Sema: aliye katika upotofu basi Mwingi wa rehema atampa muda mpaka ayaone aliyoahidiwa – ama ni adhabu au ni saa. Hapo ndipo watajua ni nani mwenye makao mabaya na mwenye askari dhaifu.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake awaambie wale wanaoona kheri iko kwenye tumbo tu, kwamba hayo wanayojifaharisha nayo katika nafasi ya maisha waliyo nayo, kuwa ni mtihani wa Mwenyezi Mungu anowajaribu nao waja wake na anawapa muda mwingi.

Wakishukuru Mwenyezi Mungu atawapa thawabu na marejeo mazuri na wakizidi ukafiri na uasi basi atawasalitia ambaye atawatesa katika maisha haya ya duniani au atawaadhibu Mwenyezi Mungu huko Akhera. Huko watajua ni nani wenye hali mbaya, waumini walio mafukara au makafiri walio matajiri?

Lau mtu atamiliki kila kinacho chomozewa na jua, miliki hiyo si chochote kulinganisha na adhabu ya chini ya Jahannam. Amesema Amirul-mu’min, Aliy(a.s) : “Heri siyo kheri ikiwa baada yake ni moto; na shari si shari ikiwa baada yake ni Pepo, Na kila neema isiyokuwa Pepo ni kazi bure na kila balaa isiyokuwa moto ni nafuu.”

Na Mwenyezi Mungu huwazidishia uwongofu wale walioongoka

Hilo ni kwa kuwafahamisha hakika yao na sehemu za makosa na za sawa. Hii ni hidaya na neema kubwa.

Na mema yenye kubaki ni bora katika malipo mbele ya Mola wako na yana mwisho mwema.

Mema yanayobakia ni elimu na mambo ya manufaa. Hayo mawili ni bora kuliko mali na jaha. Kwa sababu yanadumu na kubakia manufaa yake na thawabu zake hazikatiki, lakini jaha na mali zinaisha na kuangamia.

أَفَرَأَيْتَ الَّذِي كَفَرَ بِآيَاتِنَا وَقَالَ لَأُوتَيَنَّ مَالًا وَوَلَدًا ﴿٧٧﴾

77. Je, umemuona aliyezikana ishara zetu na akasema: Hakika mimi nitapewa mali na watoto.

أَطَّلَعَ الْغَيْبَ أَمِ اتَّخَذَ عِندَ الرَّحْمَـٰنِ عَهْدًا ﴿٧٨﴾

78. Kwani yeye amepata habari za ghaibu au amechukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

كَلَّا سَنَكْتُبُ مَا يَقُولُ وَنَمُدُّ لَهُ مِنَ الْعَذَابِ مَدًّا ﴿٧٩﴾

79. Hapana! Tutaandika anayoyo asema na tutamkunjulia muda wa adhabu.

وَنَرِثُهُ مَا يَقُولُ وَيَأْتِينَا فَرْدًا ﴿٨٠﴾

80. Na tutamrithi hayo anayoyasema na atatufikia akiwa peke yake.

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لِّيَكُونُوا لَهُمْ عِزًّا ﴿٨١﴾

81. Na wamechukua miungu mingine ili iwape nguvu.

كَلَّا سَيَكْفُرُونَ بِعِبَادَتِهِمْ وَيَكُونُونَ عَلَيْهِمْ ضِدًّا ﴿٨٢﴾

82. Sivyo kabisa! Wataikataa ibada yao na watakuwa ndio dhidiyao.

أَلَمْ تَرَ أَنَّا أَرْسَلْنَا الشَّيَاطِينَ عَلَى الْكَافِرِينَ تَؤُزُّهُمْ أَزًّا ﴿٨٣﴾

83. Kwani huoni kwamba tume-watuma mashetani kwa makafiri wawachochee kwa uchochezi.

فَلَا تَعْجَلْ عَلَيْهِمْ إِنَّمَا نَعُدُّ لَهُمْ عَدًّا ﴿٨٤﴾

84. Basi usiwafanyie haraka, Sisi tunawahisabia siku.

يَوْمَ نَحْشُرُ الْمُتَّقِينَ إِلَى الرَّحْمَـٰنِ وَفْدًا ﴿٨٥﴾

85. Siku tutakayowakusanya wenye takua kuwa ni wageni wa Mwingi wa rehema.

وَنَسُوقُ الْمُجْرِمِينَ إِلَىٰ جَهَنَّمَ وِرْدًا ﴿٨٦﴾

86. Na tutawachunga wahalifu kuwapeleka Jahannam hali ya kuwa na kiu

لَّا يَمْلِكُونَ الشَّفَاعَةَ إِلَّا مَنِ اتَّخَذَ عِندَ الرَّحْمَـٰنِ عَهْدًا ﴿٨٧﴾

87. Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale waliochukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

JE, UMEMUONA ALIYEZIKANA ISHARA ZETU

Aya 77 – 87

MAANA

Je, umemuona aliyezikana ishara zetu na akasema: Hakika mimi nitapewa mali na watoto.

Imeelezwa katika Hadith na tafsiri kwamaba A’si bin Wail, mzazi wa Amru bin Al’as, aliposikia kuhusu utume, alisema kwa stihzai: Bila shaka mimi huko akhera nitapewa mali na watoto.

Lakini dhahiri ya tamko la Aya linaonyesha kuwa kuna mzandiki fulani aliyesema hivi; ama kuwataja watu majina, hiyo si katika njia ya Qur’an. Mfano wa Aya hii ni kauli ya yule mwenye kitalu aliyesema:

وَلَئِن رُّدِدتُّ إِلَىٰ رَبِّي لَأَجِدَنَّ خَيْرًا مِّنْهَا مُنقَلَبًا ﴿٣٦﴾

“Na kama nitarudishwa kwa Mola wangu bila shaka nitapata marejeo bora zaidi Kuliko haya”Juz;15 (18:36).

Ameirudi Mwenyezi Mungu kauli hii kwa kusema:

Kwani yeye amepata habari za ghaibu au amechukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

Amepata wapi habari hizi? Au yeye ana funguo za siri au amechukua ahadi na Mwenyezi Mungu katika hilo?

Hapana ! si hivi wala hivyo; isipokuwa yeye ni kafiri muovu.Tutaandika anayoyasema na tutamkunjulia muda wa adhabu Tumezihifadhi kauli zake na tutamzidishia adhabu zaidi ya kufuru yake na uzushi wake.

Na tutamrithi hayo anayoyasema na atatufikia akiwa peke yake, akiwa mtupu na pia tutamnyng’anya mali na watoto alio nao, pale anapokufa na kuangamia na tutamfufua siku ya kiyama akiwa peke yake mtupu; sawa na tulivyomuumba mara ya kwanza.

Na wamechukua miungu mingine ili iwape nguvu. Sivyo kabisa! Kwa sababu mwenye kutaka nguvu kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu, basi Mungu humvisha vazi la udhalili.

Wataikataa ibada yao na watakuwa ndio dhidi yao

Yaani hao wanawaabudu wataikataa ibada yao na watakuwa dhidi yao. Tafsiri inayofafanua zaidi Aya hii ni kauli ya Imam Ali(a.s), katika Nahjulbalagha: Sio mbali anayefuatwa atajitenga na mfuasi na kiongozi na anayeongozwa watafarikiana kwa chuki na watalaaniana watakapokutana.

Mwenyezi Mungu naye amesema:

تَبَرَّأْنَا إِلَيْكَ مَا كَانُوا إِيَّانَا يَعْبُدُونَ ﴿٦٣﴾

“Tunajitenga nao mbele yako, Hawakuwa wakituabudu sisi” (28:63);bali walikuwa wakiabudu hawa zao na malengo yao.

Kwani huoni kwamba tumewatuma mashetani kwa makafiri wawa- chochee kwa uchochezi.

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) haingilii kati baina yao na mashetani wanowapa wasiwasi na kuwahadaa na maasi, wala hajiingizi, kwa uweza wake wa kufanya, kumzuia shetani; isipokuwa amewabainishia njia ya kheri na shari na kuwapa uwezo kamili wa kutenda na kuwaacha; anawakataza hili na kuwaamrisha lile; kisha anawaachia hiyari katika watakayoyatenda na kuyaacha.

Kama angeliwanyanyag’anya utashi, basi wangelikuwa wao na miti ni sawa.

Basi usiwafanyie haraka. Sisi tunawahisabia siku.

Yaani, ewe Muhammad, usiwe na haraka ya kuangamia makafiri, kwani maangamizi yao yatakuja tu, lakini Mwenyezi Mungu anawangoja mpaka muda uliotajwa, ili avidhibiti vitendo vyao, kisha aje awalipe, wanayostahili. Kwani hakuna kheri ya kurefuka maisha isipokuwa kwa yule anayeamini na akatenda amali njema, lakini mwenye kukufuru na akafanya maovu, basi maisha yake ni balaa:

وَلَا يَحْسَبَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا أَنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ خَيْرٌ لِّأَنفُسِهِمْ إِنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ لِيَزْدَادُوا إِثْمًا وَلَهُمْ عَذَابٌ مُّهِينٌ ﴿١٧٨﴾

“Wala wasidhanie kabisa wale waliokufuru kwamba muda tunaowapa ni kheri kwa nafsi zao, Hakika tunawapa muda na wanazidi tu katika dhambi na wana adhabu idhalilishayo.”Juz.4 (3:178).

Siku tutakyowakusanya wenye takua kuwa ni wageni wa Mwingi wa rehema.

Neno lililotumika katika kufasiri wageni limetokana na neno la kiarabu wafd lenye maana ya wageni wa heshima. Maana ni kuwa wale wanaomtii Mwenyezi Mungu, kesho watakuwa ni wageni wenye kutukuzwa.

Na tutawachunga wahalifu kuwapeleka Jahannam halia ya kuwa na kiu

Waumini watapata makaribisho ya heshima na wahalifu watapata makaribisho ya dharau, kuchungwa kama wanyama wanavyochungwa kwenda kunywa maji; ndivyo wahalifu nao watachungwa kupelekwa kwenye Jahannam.

Hawatakuwa na mamlaka ya uombezi ila wale waliochukua ahadi kwa Mwingi wa rehema.

Kila mwenye kutekeleza ahadi ya Mwenyeezi Mungu na wala asimfanyie hiyana kwenye dogo wala kubwa, basi Mwenyezi Mungu amempa ahadi ya kufuzu na kuokoka na uombezi:

وَأَوْفُوا بِعَهْدِي أُوفِ بِعَهْدِكُمْ وَإِيَّايَ فَارْهَبُونِ ﴿٤٠﴾

“Na tekelezeni ahadi yangu nitatekeleza ahadi yenu”Juz;1(2:40)

وَقَالُوا اتَّخَذَ الرَّحْمَـٰنُ وَلَدًا ﴿٨٨﴾

88. Na wanasema Mwingi wa rehema anamwana.

لَّقَدْ جِئْتُمْ شَيْئًا إِدًّا ﴿٨٩﴾

89. Hakika mmeleta Jambo la kuchusha.

تَكَادُ السَّمَاوَاتُ يَتَفَطَّرْنَ مِنْهُ وَتَنشَقُّ الْأَرْضُ وَتَخِرُّ الْجِبَالُ هَدًّا ﴿٩٠﴾

90. Zinakurubia mbingu kutatuka kwa hilo na ardhi kupasuka na milima kuanguka vipande vipande

أَن دَعَوْا لِلرَّحْمَـٰنِ وَلَدًا ﴿٩١﴾

91. Kwa kudai kwao kuwa Mwingi wa rehema ana mwana.

وَمَا يَنبَغِي لِلرَّحْمَـٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا ﴿٩٢﴾

92. Hahitajii Mwingi wa rehema kuwa na mwana.

إِن كُلُّ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِلَّا آتِي الرَّحْمَـٰنِ عَبْدًا ﴿٩٣﴾

93. Hakuna yeyote aliyemo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Mwingi wa rehema kuwa ni mtumwa.

لَّقَدْ أَحْصَاهُمْ وَعَدَّهُمْ عَدًّا ﴿٩٤﴾

94. Hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa.

وَكُلُّهُمْ آتِيهِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فَرْدًا ﴿٩٥﴾

95. Na kila mmoja kati yao atam fikia siku ya Kiyama peke yake

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ سَيَجْعَلُ لَهُمُ الرَّحْمَـٰنُ وُدًّا ﴿٩٦﴾

96. Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.

فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ الْمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِ قَوْمًا لُّدًّا ﴿٩٧﴾

97. Hakika tumeifanya nyepesi, kwa ulimi wako ili uwabashirie kwayo wenye takua na uwaonye kwayo wabishi

وَكَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّن قَرْنٍ هَلْ تُحِسُّ مِنْهُم مِّنْ أَحَدٍ أَوْ تَسْمَعُ لَهُمْ رِكْزًا ﴿٩٨﴾

98. Na karne ngapi tumeziangamiza kabla yao, Je, unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?

WANASEMA MWINGI WA REHEMA AMEJIFANYIA MWANA

Aya 88 – 98

MAANA

Na wao wanasema Mwingi wa rehema ana mwana. Hakika mmeleta jambo la kuchusha, Zinakurubia mbingu kutatuka kwa hilo na ardhi kupasuka na milima kuanguka vipande vipande kwa kudai kwao kuwa Mwingi wa rehema ana mwana.

Mwenyezi Mungu amewakemea sana wale waliomfanya Mwenyezi Mungu kuwa ana watoto wa kiume na mabinti na akawapa kiaga kwenye Aya kadhaa; miongoni mwazo ni: Juz.1 (2:116), Juz.5 (4:48), Juz. 6 (4:171) na Juz. 7 (6:101).

Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akataja hapa kauli yao hii kwa mfumo huu wa kutisha. Nao unafahamisha kuwa mtu anamchezea ambaye hachezewi na yeyote aliye mbinguni wala ardhini.

Binadamu anamchezea Muumba wake naye anaishi kwenye himaya yake, na anamnasibisha mambo ambayo kuyasikia tu yanaweza yakaipasua mbingu na ardhi na kuangusha milima.

Unaweza kuuliza : kwanini hasira yote hii ya kilimwengu kwa sababu tu ya maneno ya kijinga na ya udhaifu wa akili?

Jibu : Hasira yote hii, haiko kwa mtu au kikundi cha watu maalum; isipokuwa imetokana na shirki hii ambayo sasa imekuwa ni dini na itikadi wanayoifuata mamilioni, kizazi baada ya kizazi na mifano hii ya mungu mwan na mungu mama.

مَّا الْمَسِيحُ ابْنُ مَرْيَمَ إِلَّا رَسُولٌ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِ الرُّسُلُ وَأُمُّهُ صِدِّيقَةٌ كَانَا يَأْكُلَانِ الطَّعَامَ ﴿٧٥﴾

“Masih mwana wa Maryam hakuwa ila ni Mtume, Wamepita kabla yake Mitume, Na mama yake ni mkweli, Wote wawili walikuwa wakila chaku- la”Juz; 6 (5:75).

Hahitajii Mwingi wa rehema kuwa na mwana.

Kwa sababu mwana anafanana na mzazi wake, na Mwenyezi Mungu hana aliyefanana naye. Na kwa sababu kuwa na mtoto ni kumuhitajia, na Mwenyezi Mungu amejitosheleza na walimwengu wote

Hakuna yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Mwingi wa rehema kuwa ni mtumwa.

Hakuna yeyote aliyeko chini au juu ila huwa ni mja wa Mwenyezi Mungu anayemilikiwa. Kimsingi ni kwamba mwenye kumilikiwa sio mtoto na mmliki sio baba.

Hakika amewadhibiti na amewahisabu sawa sawa na kila mmoja kati yao atamfikia siku ya Kiyama peke yake.

Waliodhibitiwa ni walio mbinguni na ardhini na atakyefikiwa ni Mwenyezi Mungu. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu hapotewi na kujua kitu chochote katika ardhi wala katika mbingu na kwamba kila mmoja atakwenda kwa Mwenyezi Mungu siku ya kiyama akiwa peke yake, hana wa kumnusuru wala kumsaidia au kujisaidia yeye mwenyewe kwa wingi au uchache, sikwambii tena kumsadia mwenginewe. Ambaye atamjia Mwenyezi Mungu katika hali kama hiyo, anawezaje kuwa mtoto wake?

Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema Mwingi wa rehema atawajaalia mapenzi.

Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anatia mapenzi katika nyoyo za waja wake kwa watu wenye imani na ikhlasi, si kwa chochote ila kwa kuthamini fadhila na hulka njema.

Muhammad bin Ahmad Alkalabiy, mwenye kitabu Attas-hil anasema: Inasemekana kuwa Aya hii ilishukwa kwa Aliy bin Abi Twalib. Sheikh Almaraghi, mmoja wapo wa masheikh wa Al-Azhar, anasema: ‘Ibin Mardaywyh na Dilamiy wamepokea kutoka kwa Baraa, kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alimwambia Aliy: Sema ewe Mola wangu nijalie ahadi kwako na unijaalie mapenzi katika nyoyo za waumini’ ndipo ikashuka Aya hii”.

WANASWARA NA BANI HASHIM

Amesema Abu Hayani Al-andalusi katika tafsir yake Albahrul-Muhit: “Aya hii ilishuka kwa Aliy bin Abi Twalib na amesema Muhammad Alhanafiya: huwezi kumpata mumin ila anampenda Aliy. Maajabu ni yale aliyotueleza Imam wa lugha Ridhad Din, Abu Abdillah Muhammad bin Aliy bin Yusuf Al-Answariy Ashatibiy kuhusu aliyosema, ibn Is-haq Mnaswara:

• Uday na Taym kwa ubaya kamwe sitothubutu kuwataja

• Lakini naona ni vibaya Ali kulaumiwa na waja

• Mimi ni mpenzi wa dhuriya ya Hashimu na wanawe pamoja

• Naswira watukufu kupambiya kwa nini imekuwa ni kioja

• Tawaambiya huku kiusiya moyo wangu umekwisha wachuja

• Kupenda nifuraha nawambiya hata wanyama pia wangoja.

Hakika tumeifanya nyepesi, kwa ulimi wako ili uwabashirie kwayo wenye takua na uwaonye kwayo wabishi.

Yaani Mwenyezi Mungu ameteremsha Qur’an kwa lugha ya kiarabu ili iwe wepesi kuijua na kufahamu maana yake na iwe ni habari njema kwa mwenye kumcha Mwenyezi Mungu na onyo kwa mwenye kukufuru na akafanya uovu. Umepita mfano wake katika Juz. 12 (12:2)

Na karne ngapi tumeziangamiza kabla yao, Je, unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao?

Yaani Mwenyezi Mungu amewaangamiza mpaka wa mwisho wao. Umetangulia mfano wake katika Aya ya 84 ya sura hii; na Juz, 15 (17:17).

MWISHO WA SURA YA KUMI NA TISA