TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 10581
Pakua: 2614


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10581 / Pakua: 2614
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

Mwandishi:
Swahili

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

Sura Ya Ishirini: Surat Twaha. Imeshuka Makka, ina Aya 135

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

طه ﴿١﴾

1. Twaha

مَا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْقُرْآنَ لِتَشْقَىٰ ﴿٢﴾

2. Hatukukuteremshia Qur’an ili upate mashaka.

إِلَّا تَذْكِرَةً لِّمَن يَخْشَىٰ ﴿٣﴾

3. Ispokuwa ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.

تَنزِيلًا مِّمَّنْ خَلَقَ الْأَرْضَ وَالسَّمَاوَاتِ الْعُلَى ﴿٤﴾

4. Uteremsho utokao kwa aliyeumba ardhi na mbing zilizo juu.

الرَّحْمَـٰنُ عَلَى الْعَرْشِ اسْتَوَىٰ ﴿٥﴾

5. Mwenyezi Mungu ametawala juu ya Arshi.

لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَمَا تَحْتَ الثَّرَىٰ ﴿٦﴾

6. Ni vyake vilivyo katika mbingu na katika ardhi na vilivyo baina yao na vilivyo chini ya mchanga.

وَإِن تَجْهَرْ بِالْقَوْلِ فَإِنَّهُ يَعْلَمُ السِّرَّ وَأَخْفَى ﴿٧﴾

7. Na ukiinua sauti kwa kusema, basi yeye anajua siri na yanayofichika. zaidi.

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ لَهُ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Mwenyezi Mungu hapana Mola ila Yeye, Anamajina mazuri.

Twaha

Aya 1 – 8

Twaha

wametofautiana katika makusudio ya Twaha. Ikasemekana ni jina katika majina ya Mwenyezi Mungu. Kauli hiyo ameichagua Tabariy, pale aliposema: hii ndio maana ya sawa; kwa sababu maana ya Twaha katika Lugha ya Akka ni Ewe mtu!

Wafasiri wengi wamesema kuwa tamko la Twaha ni herufi za kuendeleza, kama ilivyo Alif Lam Mim na Kaf Ha Ya Ayn Swad.

Katika Tafsir Arraziy imeelezwa kuwa Imam Jaffer As-swadiq(a.s) amesema: herufi twa ni twahara ya watu wa nyumba ya Mtume (Ahlu bayt) na herufi Ha ni hidaya (uongofu) yao.

Si mbali kuwa tafsiri hii inayonasibishwa kwa Imam Jaffer Asswadiq ndio sababu ya wale wanaosema kuwa Twaha ni miongoni mwa majina ya Mtume(s.a.w.w) . Kwa sababu yeye ndio chimbuko la kwanza la utwahara wa watu wa nyumba yake na hidaya yao.

Hatukukuteremshia Qur’an ili upate mashaka; isipokuwa ni mawaidha kwa wenye kunyenyekea.

Mtume(s.a.w.w) alikuwa akijituma na kufuatisha na ibada na pia alikuwa akifanya juhudi na kutaabika huku akiwasikitikia makafiri na ukafiri wao. Mwenyezi Mungu akampoza na kujitaabisha huku na akamwambia:

Kwa nini unajitia mashaka na kujibebsha mzigo mzito wa ibada nyingi na kusononeka na upinzani wa anayepinga mwito wako? Mimi sikukuteua wala kuiteremsha Qur’an kwa hili la kupata tabu; isipokuwa nimekuteremshia ili uongoke nayo wewe na wanaokufuata katika waumini na uwaawidhie kwayo makafiri iwe ni hoja juu yao.

فَلَا تَذْهَبْ نَفْسُكَ عَلَيْهِمْ حَسَرَاتٍ ﴿٨﴾

“Basi roho yako isitoke kwa kuwasikitikia” (35:8)

Kwa hiyo ni neema na rehema kutoka kwa wanaoamini na balaa kwa wenye kupinga na kuasi.

Uteremsho utokao kwa aliyeumba ardhi na mbingu zilizo juu

Aliyeitermsha Qur’an ndiye aliyeumba ulimwengu; ulimwengu ni kitabu cha Mwenyezi Mungu kinachozongumza kwa lugha ya hali na Qur’an ni Kitabu chake kinachozungumza kwa lugha ya makala. Vyote hivyo viwili vina kheri ya watu na wema wao, basi ni kwa nini kushuka Qur’an kuwe ni nyenzo ya kukutaabisha ewe Muhammad?

Unaweza kuuliza : Qur’an ilishuka kwa Mtume(s.a.w.w) ili aweze kuitumia na kuwaongozea watu, imeelezwa katika hiyo Qur’an:

وَمَا جَعَلَ عَلَيْكُمْ فِي الدِّينِ مِنْ حَرَجٍ ﴿٧٨﴾

“Wala hakuwawekea mambo mazito katika dini ” (22:78).

Vile vile imesema:

أَوْ نَتَوَفَّيَنَّكَ فَإِنَّمَا عَلَيْكَ الْبَلَاغُ وَعَلَيْنَا الْحِسَابُ ﴿٤٠﴾

“Basi ni juu yako kufikisha na juu yetu ni hisabu”Juz ;13(13:40)?

Ilikuwaje kwa Mtume kujitaabisha kwa ibada na masononeko?

Jibu : yule aliye mtukufu huiona ndogo kheri anayoifanya hata kama ni kubwa, huifanya kubwa dhambi yake hata kama ni ndogo na hujituhumu kwa uzembe kadiri anavyojitahidi.

Na Mtume(s.a.w.w) ni mtukufu zaidi ya viumbe wote. Utukufu wake unategemea na kumjua kwake Mungu, kumtii na kufanya juhudi ya kulingania mwito wa njia yake.

Kwa ajili hii anaji- tuhumu na anajiona bado hajatimiza haki ya Mungu kadiri atakavyofanya ibada na kutoa mwito wa haki; hasa pale inapokuwa haujatoa matunda ya kuwaongoza makuraish.

Mwenyezi Mungu ametawala juu ya Arshi.

Hili ni fumbo la kutawalia mambo na kuyapangilia vizuri, Umetangulia mfano wake, katika Juz; 8 (7:54).

Ni vyake vilivyo katika mbingu na katika ardhi na vilivyo baina yao na vilivyo chini ya mchanga

Makusudio ya mchanga hapa ni ardhi. Aya hii ni ubainfu na tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu, ameumba ardhi na mbingu na ametawala kwenye Arsh.

Kwa sababu mwenye kuumba na kupangilia ndiye mmiliki. Hakuna yeyote anayemiliki kitu isipokuwa ni katika milki yake.

Na ukiinua sauti kwa kusema, basi yeye anajua siri na yanayofichika zaidi.

Yanayofichika zaidi ni yale yanayopita moyoni bila ya kuyatamka. Ufafanuzi zaidi wa tafisri ya yanayofichika ni kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿١٥٤﴾

“Na Mwenyezi Mungu anayajua yaliyomo vifuani”Juz; 4(3:154)

Mwenyezi Mungu hapana Mola ila Yeye, Ana majina mazuri.

Majina yote ya Mwenyezi Mungu ni mazuri, kwa sababu yanaleta ibara ya maana nzuri na sifa nzuri. Angalia kifungu cha: ‘Je, majina ya Mwenyezi Mungu ni hayo hayo au yana kiasi’ Juz. 9 (7: 178 – 181)

وَهَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ مُوسَىٰ ﴿٩﴾

9. Je, imekujia hadith ya Musa?

إِذْ رَأَىٰ نَارًا فَقَالَ لِأَهْلِهِ امْكُثُوا إِنِّي آنَسْتُ نَارًا لَّعَلِّي آتِيكُم مِّنْهَا بِقَبَسٍ أَوْ أَجِدُ عَلَى النَّارِ هُدًى ﴿١٠﴾

10. Pale alipoona moto, akawaambia watu wake: ngojeni! Mimi nimeona moto, huenda nikawaletea kijinga kutoka huko au nikapata uongofu.

فَلَمَّا أَتَاهَا نُودِيَ يَا مُوسَىٰ ﴿١١﴾

11. Basi alipoufikia akaitwa: Ewe Musa!

إِنِّي أَنَا رَبُّكَ فَاخْلَعْ نَعْلَيْكَ إِنَّكَ بِالْوَادِ الْمُقَدَّسِ طُوًى ﴿١٢﴾

12. Hakika Mimi ndiye Mola wako, basi vua viatu vyako; kwani hakika wewe uko katika bonde takatifu la Tuwa

وَأَنَا اخْتَرْتُكَ فَاسْتَمِعْ لِمَا يُوحَىٰ ﴿١٣﴾

13. Nami nimekuteua, basi sikiliza unayopewa wahyi

إِنَّنِي أَنَا اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنَا فَاعْبُدْنِي وَأَقِمِ الصَّلَاةَ لِذِكْرِي ﴿١٤﴾

14. Hakika Mimi ndiye Mwenyezi Mungu, Hapana Mungu isipokuwa mimi, Basi niabudu mimi na usimamishe swala kwa ajili ya kunikumbuka

إِنَّ السَّاعَةَ آتِيَةٌ أَكَادُ أُخْفِيهَا لِتُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا تَسْعَىٰ ﴿١٥﴾

15. Hakika Saa (kiyama) itakuja, nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyoyafanya

فَلَا يَصُدَّنَّكَ عَنْهَا مَن لَّا يُؤْمِنُ بِهَا وَاتَّبَعَ هَوَاهُ فَتَرْدَىٰ ﴿١٦﴾

16. Kwa hiyo asikukengeushe nayo yule asiyeiamni na akafuata hawa yake ukaangamia.

HADITHI YA MUSA

Aya 9-16

KUKARIRIKA KISA

Mwenyezi Mungu amekitaja kisa cha Musa, katika Kitabu chake, mara nyingi, Siri - kama tulivyogundua tukifasiri Aya za Dhikr Tukufu – ni kwamba Mwenyezi Mungu ametaja maovu mengi ya Wana wa Israil na Musa akiwakataza na kuwahadharisha, ndio ikawa kutajwa kwao ndio kutajwa kwake. Hii ni kuongezea kisa chake na Shuaib na Firauni, kusuhubiana kwake na mja mwema ambaye aliitoboa safina, kumuua kijana na kujenga ukuta. Vilelele kuzaliwa kwake na kuwekwa kwenye kisanduku katika maji hadi kumua kwake Firaun nk.

Badhi ya wafasiri wamesema: “Mwenyezi Mungu alikariri kisa cha Musa pamoja na Firauni, kwa sababu hikaya ya Musa tangu kuanza kutungwa mimba yake mpaka mwisho wa uhai wake, ni somo, nasaha, onyo, bishara na maliwazo kwa Mtume na waumini.

Ndani yake mna ishara zinazofahamisha elimu ya Mwenyezi Mungu, uweza wake, hekima yake na jinsi Musa alivyowachukua watu wake waliokuwa wapumbavu kuliko watu wote.”

Hii ndio dunia ya Musa: wakati wa kuzaliwa kwake aliwekwa kwenye kisanduku na akatupwa majini, akalelewa yatima katika nyumba ya Firaun, akafukuzwa akawa hana kitu akila mimea ya ardhi, akawa mchungaji kon- doo kisha akawa mtume akipata ugumu kutoka kwa watu wake.

Kwa hiyo si nyongeza kisa chake kikikaririka kutajwa na kuzungumziwa katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, maadamu maisha yake yote na kisa chake ni somo na mawaidha. Aya hizi tulizo nazo hivi sasa zinazungumzia kuanza kushuka wahyi kwa Musa na kuzungumza na Mwenyeezi Mungu.

Je imekujia hadith ya Musa?

Huu ni mfano wa kusema: ‘unayo habari?’ au ‘una habari gani?’ Makusudio ni kutanabahi msikilizaji asikilize vizuri simulizi. Na hii ifuatayo ndio hadith ya kuanza wahyi kwa Musapale alipoona moto, akawaambia watu wake: ngojeni! Mimi nimeona moto, huenda nikawaletea kijinga kutoka huko au nikapata uongofu.

Katika Aya 14 na zilizo baada yake Mwenyezi Mungu amekieleza kisa cha Musa. Anaelezea kwamba Musa alipofikia umri wa kukomaa aliwaona watu wawili wakipigana, mmoja ni wa upande wa Firaun na mwingine upande wa mayahudi. Huyu wa upande wa mayahaudi alitaka msaada kwa Musa. Musa akampiga ngumi ikamuua.

Musa akakimbia kutoka Misr kwenda Madyan ambako Shuayb alimuoza mmoja wa mabinti zake kwa kuchunga wanyama wake kwa muda wa miaka minane au miaka kumi:

فَلَمَّا قَضَىٰ مُوسَى الْأَجَلَ وَسَارَ بِأَهْلِهِ آنَسَ مِن جَانِبِ الطُّورِ نَارًا قَالَ لِأَهْلِهِ امْكُثُوا إِنِّي آنَسْتُ نَارًا لَّعَلِّي آتِيكُم مِّنْهَا بِخَبَرٍ أَوْ جَذْوَةٍ مِّنَ النَّارِ لَعَلَّكُمْ تَصْطَلُونَ ﴿٢٩﴾

“Basi alipotimiza muda wake na akasafiri na ahali zake, aliona moto upande wa Mlima Tur. Akwaambia ahali zake: ngojeni! Mimi nimeona moto, labda nitawaletea kutoka habari au kijinga cha moto ili mpate kuota” (28:29)

Musa alitokea Madyan kuelekea Misr akiwa na mkewe. Njiani alihitajia moto. Wapokezi wanasema: Musa alipotea njia katika usiku wa kusi kukiwa na baridi na giza. Mkono ukashindwa kupekecha moto na huku mkewe akiwa na uchungu wa kuzaa.

Wakati akiwa amedangana hana la kufanya mara akaona moto kwa mbali, akafurahi na akawaambia watu wake, huenda faraja inakuja katikati ya dhiki, kaeni niende kwenye moto nitawaletea moto muote au nipate habari za faraja.

Basi alipoufikia akaitwa: Ewe Musa! Hakika Mimi ndiye Mola wako Musa(a.s) alikurubia kile alichofikiria kuwa ni moto; mara ukawa ni nuru adhimu inayoangaza zaidi ya jua; huku sauti ya kuogofya ikisema:

Hakika mimi ndiye Mola wako, basi vua viatu vyako kwa adabu na kun- yenyekea. Kwanihakika wewe uko katika bonde takatifu la Tuwa, mahali palipotwahara palipobarikiwa, ilipojionyesha nuru ya Mungu na katika anga yake ikainuka sauti ya utukufu na ukamilifu.

Musa aliona nuru na akasikia sauti; hakuna kitu kingine zaidi ya hivyo. Imam Aliy(a.s) anasema:

“Hakika Mwenyezi Mungu (s.w.t) haidirikiwi na hisia wala kukisiwa na watu…ambaye alizungumza na Musa na akamuonyesha ishara zake tukufu bila ya viungo wala zana yoyote.

Nami nimekuteua, basi sikiliza unayopewa wahyi.

Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) hawateui kwa wahyi wake isipokuwa wale wasafi walio na uaminifu nao. Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:144). Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akabainisha kuwa dini aliyompia wahyi Musa inasimamia kwenye misingi mitatu:

Umoja wa Mungu:Hakika mimi ndiye Mwenyezi Mungu, hapana Mungu isipokuwa mimi.

Ikhalsi ya Mungu katika ibada:Basi niabudu mimi na usimamishe swala kwa ajili ya kunikumbuka Ufufuo:Hakika saa (kiyama) itakuja, nimekaribia kuificha, ili kila nafsi ilipwe kwa iliyoyafanya.

Makusudio ya kukurubia kuificha ni kuificha. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameficha kujulikana saa ya kiyama kwa waja wake, ili watarajie kufika kwake wakati wowote, waweze kuwa na hofu nayo na waifanyie kazi, kisha walipwe malipo yao bila ya kudhulumiwa kitu.

Kwa hiyo asikukengeushe nayo yule asiyeiamni na akafuata hawa yake ukaangamia.

Dhamiri ya ‘nayo’ inarudia kwenye hiyo saa, sio swala, kwa sababu ndiyo iliyo karibu na jumla hiyo, Inawezekana kurudia kwenye zote mbili. Maana ni kuwa ewe Musa, shikilia kuamini ufufuo, hisabu na malipo na uyayafanyie kazi wala usifuate hawaa za wapinzani usije ukaangamia kama watavyoangamia wao. Tumeshawahi kudokeza kuwa inafaa kwa mkuu kumkataza aliye chini yake, hata kama ni maasumu; kuongezea kuwa kukataza kitu hakufahamishi kuwa kuna uwezekanao wa aliyekatazwa kukifanya.

وَمَا تِلْكَ بِيَمِينِكَ يَا مُوسَىٰ ﴿١٧﴾

17. Nnini hicho kilicho mkononi mwako wa kuume ewe Musa?

قَالَ هِيَ عَصَايَ أَتَوَكَّأُ عَلَيْهَا وَأَهُشُّ بِهَا عَلَىٰ غَنَمِي وَلِيَ فِيهَا مَآرِبُ أُخْرَىٰ ﴿١٨﴾

18. Akasema: Hii ni fimbo yangu; ninaiegemea na ninawaangushia majani mbuzi na kondoo wangu; tena inanifaa kwa matumizi mengine.

قَالَ أَلْقِهَا يَا مُوسَىٰ ﴿١٩﴾

19. Akasema: Itupe ewe Musa!

فَأَلْقَاهَا فَإِذَا هِيَ حَيَّةٌ تَسْعَىٰ ﴿٢٠﴾

20. Akaitupa mara ikawa nyoka anayekwenda mbio.

قَالَ خُذْهَا وَلَا تَخَفْ سَنُعِيدُهَا سِيرَتَهَا الْأُولَىٰ ﴿٢١﴾

21. Akasema: ichukue wala usihofu! Tutairudisha hali yake ya kwanza

وَاضْمُمْ يَدَكَ إِلَىٰ جَنَاحِكَ تَخْرُجْ بَيْضَاءَ مِنْ غَيْرِ سُوءٍ آيَةً أُخْرَىٰ ﴿٢٢﴾

22. Na uambatanishe mkono wako na ubavu wako, utatoka mweupe pasipokuwa na ubaya wowote. Hiyo ni ishara nyingine.

لِنُرِيَكَ مِنْ آيَاتِنَا الْكُبْرَى ﴿٢٣﴾

23. Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa.

اذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَىٰ ﴿٢٤﴾

24. Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepetuka mpaka.

قَالَ رَبِّ اشْرَحْ لِي صَدْرِي ﴿٢٥﴾

25. Aksema: Ewe Mola wangu! Nikunjulie kifua changu

وَيَسِّرْ لِي أَمْرِي ﴿٢٦﴾

26. Na unifanyie wepesi jambo langu.

وَاحْلُلْ عُقْدَةً مِّن لِّسَانِي ﴿٢٧﴾

27. Na ulifungue fundo lilo katika ulimi wangu.

يَفْقَهُوا قَوْلِي ﴿٢٨﴾

28. Wapate kufahamu kauli yangu.

وَاجْعَل لِّي وَزِيرًا مِّنْ أَهْلِي ﴿٢٩﴾

29. Na nipe waziri katika watu wangu

هَارُونَ أَخِي ﴿٣٠﴾

30. Harun Ndugu yangu.

اشْدُدْ بِهِ أَزْرِي ﴿٣١﴾

31. Niongeze nguvu zangu kwaye

وَأَشْرِكْهُ فِي أَمْرِي ﴿٣٢﴾

32. Na umshirikishe katika jambo langu.

كَيْ نُسَبِّحَكَ كَثِيرًا ﴿٣٣﴾

33. Ili tukutakase sana

وَنَذْكُرَكَ كَثِيرًا ﴿٣٤﴾

34. Na tukukumbuke sana

إِنَّكَ كُنتَ بِنَا بَصِيرًا ﴿٣٥﴾

35. Hakika wewe unatuona.

NA NINI HICHO KILICHO MKONONI MWAKO WA KUUME EWE MUSA?

Aya 17 – 35

MAANA

Na nini hicho kilicho mkononi mwako wa kuume ewe Musa?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamuuliza Musa amueleze kilicho mkononi mwake, huku akiwa anajua zaidi kuliko huyo Musa mwenyewe, Kwa hiyo hapo kuna siri, Ndio kuna siri kubwa kwenye fimbo hii, aliyotaka kuidhi- hirisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa Musa, ambayo ni kugeuka fimbo kuwa nyoka.

Ikiwa tone la manii lina viini vya binadamu, yai lina viini vya kuku na mbengu kuwa na viini vya mimea, lakini mti huu mkavu hauna viini vyovyote vya nyoka, hata hivyo umegeuka nyoka! Hii ndio siri ya muujiza; na hapa ndio tunapata tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ ﴿٩٥﴾

“Humtoa aliye hai katika maiti” Juz; 7 (6:95)

Razi anasema: Anayetaka kutoa kitu kikuu kutokana na kidogo, kwanza hukionyesha hadharani kile kidogo huku akiseam: nini hiki? Nao waseme: ni kadha, Hapo ndio anaanza kazi yake. Ndio hivi alivyofanya Mwenyezi Mungu (s.w.t) na Musa.

Alimuuliza kuhusu fimbo, alipokiri kuwa ni mti tu mkavu, Mwenyezi Mungu akaugeuza nyoka mkubwa, akaipigia bahari ikapasuka na jiwe likatoka chemchem.

Jambo la kushangaza ni kwamba Sheikh Maraghi alinukuu ibara hii ya Razi bila ya kuashiria chimbuko lake; kama ilivyo kawaida yake, katika tafsiri yake kuanzia mwanzo hadi kwenye Aya hii. Na ninadhani inayofu- atia pia ni hivi hivi; sawa na mpangilio wa Nidhamuddin Naysabury, katika tafsiri yake Gharaibulqur’an wa raghaibulfurqan.

Akasema: Hii ni fimbo yangu; ninaiegemea na ninawaangushia majani mbuzi na kondoo wangu; tena inanifaa kwa matumizi mengine.

Tumesoma elimu ya maani na bayan, katika kitabu Al-mutawwal cha Taftazaniy. Tulipofika kwenye mlango wa kufupisha, kurefusha na kulinganisha sawa, mwenye kitabu alitaja faida za kurefusha; zikiwa ni pamoja na: kufafanua, kusisitiza kwa kukaririka na ladha ya elimu. Kisha Ustadh akapiga mfano wa mazungumzo pamoja na mpendwa, kutokana na riwaya ya baadhi ya wategemezi.

Kwa ufupi ni kwmba mpokezi aliota ndoto ya kuonana na Muhammad(s.a.w.w) na Musa bin Imran(a.s) . Akamsikia Musa akimlaumu Muhammad huku akimwambia: miongoni mwa mambo uliyasema ni: Ulama wa uma wangu ni kama manabii wa Bani Israil. Hii ndio hadhi yetu kwako ewe Abulqasim sawa na ulama wa uma wako?

Muhammad akataka kumthibitishia, akamwambia: hivi sasa nitakukutan- isha na mmoja wa ulama wa uma wangu ili umjaribu uone usahihi wa niliyoyasema, Musa akamwambia sawa. Akamkutanisha na mwanachuoni Ardabeliy. Musa akamuuliza: waitwaje? Akajibu: Mimi ni Ahmad na baba yangu jina lake ni Muhammad, ninatoka Ardabeliy, nimesoma Najaf na mwalimu wangu ni Shahiduthani.

Musa akamwambia: ni yanini yote hayo? Nimekuuliza jina lako tu, wewe waniambia jina lako, la baba yako, mji wako na mwalimu wako! Ardabeliy akamwambia: wewe si uliulizwa na Mwenyezi Mungu kuhusu kilicho mikononi mwako na ukasema:“Hii ni fimbo yangu; ninaiegemea na ninawaangushia majani mbuzi na kondoo wangu; tena inanifaa kwa matumizi mengine na ingetosha kusema hii ni fimbo yangu tu.”

Hapo Musa akamgeukia Muhammad na kumwambia huku akiomba msamaha: wewe unajua zaidi uliyoyasema.

Ustadh aliongezea riwaya hii kwa kusema: namna hii mtu hurefusha maneno pamoja na yule anayempenda si kwa lolote ila ni kwa kumfungulia moyo na bashasha. Miongoni mwa hayo ni kauli ya malenga mashuhuri anayeitwa Mutanabbi: Maswali mengi hutokana na shauku na mengi majibu ni kwa kutunuku

Akasema: itupe ewe Musa! Akiatupa mara ikawa nyoka anayekwenda mbio, Akasema: ichukue wala usihofu! Tutairudisha hali yake ya kwanza.

Musa alipatwa na hofu kutokana na mandhari haya yakutisha na akarudi nyuma; kama inavyofahamisha Aya isemayo:

فَلَمَّا رَآهَا تَهْتَزُّ كَأَنَّهَا جَانٌّ وَلَّىٰ مُدْبِرًا وَلَمْ يُعَقِّبْ يَا مُوسَىٰ لَا تَخَفْ إِنِّي لَا يَخَافُ لَدَيَّ الْمُرْسَلُونَ ﴿١٠﴾

“Alipoiona inayumba kama nyoka akageuka kurudi nyuma wala hakungoja. Ewe Musa! Usikhofu hakika hawakhofu mbele yangu mitume (27:10).

Yaani Mitume hawaogopi kwa yale ninayowaamrisha, kwa vile wanajua kuwa siwaamrishi isipokuwa kheri wala siwakatazi isipokuwa shari, Mara tu, Musa alipoweka mkono wake kwenye nyoka iligeuka fimbo.

Na uambatanishe mkono wako na ubavu wako, utatoka mweupe pasipokuwa na ubaya wowote. Hiyo ni ishara nyingine, Ili tukuonyeshe baadhi ya ishara zetu kubwa.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t) Amesema uambatanishe mkono na ubavu wako. Na mahali pengine akasema:

وَأَدْخِلْ يَدَكَ فِي جَيْبِكَ ﴿١٢﴾

“Na ingiza mkono wako kwenye uwazi wa vazi lako” (27:12).

Pasipokuwa na ubaya wowote ni kutokuwako madhara.

Mkono wa Musa ulikuwa wa rangi ya kahawiya, kwa sbabu yeye alikuwa wa rangi hiyo. Alipouingiza mkono wake na akautoa, ulitoa mwanga kama wa jua. Umetangulia mfano wa Aya hii katika Juz. 9 (7:108).

Nenda kwa Firauni; kwani hakika yeye amepetuka mpaka.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha Musa kumkemea Firauni na dhulma yake, akiwa ni mwenye nguvu na uwezo; kiasi cha kujigamba na kusema:

أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ ﴿٢٤﴾

“Mimi ndiye Mola wenu Mkuu” (79:24),

مَا عَلِمْتُ لَكُم مِّنْ إِلَـٰهٍ غَيْرِي ﴿٣٨﴾

“Simjui kwa ajili yenu Mungu asiyekuwa mimi” (28: 38) tena akmwambia Musa:

قَالَ أَلَمْ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدًا وَلَبِثْتَ فِينَا مِنْ عُمُرِكَ سِنِينَ ﴿١٨﴾

“Je hatukukulea kwetu ukiwa mtoto na ukakaa kwetu miaka ya umri wako?” (26:18).

Musa alikulia katika kasri ya Firauni kama yatima; kisha akawa mkimbizi akila majani. Imam Aliy(a.s) anasema katika Nahjulbalagha: Rangi ya kijani ya majani ilikuwa ikionekana kwenye ngozi ya tumbo lake kwa wembamba wake na kutenga na nyama yake.

رَبِّ إِنِّي لِمَا أَنزَلْتَ إِلَيَّ مِنْ خَيْرٍ فَقِيرٌ ﴿٢٤﴾

Mola wangu! Hakika mimi ni muhitaji wa kheri utakayonitermshia” (28:24).

Imam anasema:“Wallah hakumuomba isipokuwa mkate wa kula tu” na Mungu alimwitikia maombi yake, akapata mkate kwa Shuayb kwa kufanya kazi ya kuchunga wanyama wake.

Hii ndiyo dunia ya Musa bin Imran: Wakati wa kuzaliwa kwake aliwekwa kwenye sanduku, akatupwa majini. Akakulia kwenye nyumba ya Firauni akiwa yatima; akawa mkimbizi akila mimea ya ardhi, kisha akawa mchunga mbuzi na kondoo.

Mtu huyu oheahe asiye na chochote anaenda kumkabili kigogo mwenye kila kitu, itawezekana kweli? Ndio iliwezekana! Alikwenda Musa kwa Firauni na wakuu wake na fimbo yake ikameza vyote walivyovizua na mkono wake ulioonyesha ukweli wake na usafi wake. Mbali ya fimbo na mkono Musa aliomba mambo mengine zaidi, kama ifuatavyo:-

Ewe Mola wangu! Nikunjulie kifua changu.

Inajulikana kuwa Musa alikuwa ni mwepesi wa kukasirika kwa jambo linalomchukiza. Haya yametamkwa na Qur’an. Imeeleza kuwa alishika ndevu za nduguye Haruna na kichwa chake, pale wana wa Israil walipoabudu ndama. Akampiga ngumi mtu wa upande wa Firauni na kum- maliza na akahalifu amri ya mja mwema baada ya kumwambia kuwa nitavumilia.

Hakuna mwenye shaka kwamba matatizo aliyopamabana nayo Musa katika maisha yake yameacha athari ya hasira hizi za harakaharka; Kwa kuwa Utume unahitajia uvumilivu wa machukivu na tabu, ndio akamuomba Mola wake awe mpole na mkunjufu.

Na unifanyie wepesi jambo langu.

Yaani unisaidie, ewe Mola wangu, kwa masaada na tawfiki ya kuweza kutekekeleza yale uliyonikalifisha na unifanye niweze kuyabeba. Hakuna kitu cha kheri kinachotimia kwa mtu, isipokuwa kwa tawfiki na msaada wa Mwenyezi Mungu; hata akiwa na nyenzo zote.

Na ulifungue fundo lilo katika ulimi wangu; Wapate kufahamu kauli yangu

Aya hii tukiunganisha na ile isemayo:

وَأَخِي هَارُونُ هُوَ أَفْصَحُ مِنِّي لِسَانًا ﴿٣٤﴾

“Na ndugu yangu Harun ni fasaha zaidi kuliko mimi kwa ulimi” (28:34).

Na pia:

وَلَا يَكَادُ يُبِينُ ﴿٥٢﴾

“Wala hawezi kusema waziwazi” (43:52).

Tukiunganisha Aya zote hizi tatu, tunapata ushahidi wa yule asemaye kwamba Musa alikuwa na kigugumizi. Ama kuwa kigugumizi hiki ni cha maumbile au kilitokana na kaa la moto alilolitia mdomoni, pale alipojaribiwa na Firauni utotoni, ujuzi wake uko kwa Mola wangu.

Kwa hakika Aya hii inaonyesha kuwa ufasaha wa ulimi na kubainisha maneno ni katika sifa kuu na neeema kubwa ya Mwenyezi Mungu kwa mtu:

خَلَقَ الْإِنسَانَ ﴿٣﴾ عَلَّمَهُ الْبَيَانَ ﴿٤﴾

“Amemuumba mtu akamfundisha kusema” (55:3-4).

Imam Aliy(a.s) anasema:“Mtu si mtu lau si ulimi (kuzungumza); isipokuwa mnyama mwenye kupuuzwa au picha”

Na nipe waziri katika watu wangu, Harun ndugu yangu, niongeze nguvu zangu kwaye na umshirikishe katika jambo langu, ili tukutakase sana na tukukumbuke sana, Hakika wewe unatuona.

Katika Majmaul-bayan imeelezwa kuwa Harun alikuwa ni nduguye Musa kwa baba na mama, na alikuwa ni mkubwa wake kwa miaka mitatu. Alikuwa mwenye kimo, mwenye mwili mwangavu, mwenye nyama nyingi na mfasaha wa kuzungumza. Ni kutokana na sifa hizi ndio Musa akamuomba Mola wake amfanye nduguye Harun ni mshirika wake katika utume. Mwenye Majmaul-bayan anasema kuwa alikufa kabla ya kufa nduguye Musa kwa miaka mitatu.

HAKIKA YA UTUME

Kwa vyovyote ilivyo ni kuwa mwenye ujumbe hana budi kuwa na mwen- za msaidizi mwenye ikhlasi na atakayejitolea muhanga. Kwani unabii, katika hakika yake, ni habari inayotoka kwa Mungu anayoinukuu mtu; sio nguvu tekelezi au kusema ‘kuwa’ na ikawa.

Nabii ni mtu asiyeweza kujizuia na madhara wala kujiletea manufaa. Utekelezaji wake unatumia nyenzo zilezile anazozitumia mumin na asiyekuwa mumin.

Hakuna tofauti isipokuwa ni habari za kutoka kwa Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu anamchukua mtu aliye mtukufu zaidi na kumteua mwenye sifa nzuri zaidi. Lakini sifa takatifu hazifanyi mwenye nazo asiwe na haja na desturi ya maumbile. Hapana! Manabii na wasiokuwa manabii, wote wanahitaji nyenzo.

Nabii anahitajia tabibu akiwa mgonjwa; sawa na asiyeamini Mungu na siku ya mwisho anavyohitajia. Vile vile anahitaji nguvu; kama anavyohitajia mtu mwingine. Mitume wote waliudhiwa na wengi wao wakuawa.

Hapa inatubainikia kujiingiza sana hadi kupotea kwa yule anayesema kuwa Muhammad(s.a.w.w) ndiyo hakika ambayo Mwenyezi Mungu ameiumbia viumbe na ni roho ambayo imeenea kwenye viumbe vyote vya juu na vya chini:

وَلَوْ كُنتُ أَعْلَمُ الْغَيْبَ لَاسْتَكْثَرْتُ مِنَ الْخَيْرِ وَمَا مَسَّنِيَ السُّوءُ إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ وَبَشِيرٌ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿١٨٨﴾

“Na lau kama ningelijua ghaibu ningelijizidishia kheri nyingi, wala isingelinigusa dhara. Mimi si chochote ila ni mwonyaji na mtoaji bishara kwa watu wanaoamini.” Juz: 9 (7:188)

Hii ndio hakika ya utume: kuonya na kuleta bishara. Anapopatikana muonyaji na mbashiri akiwa pamoja na msaidizi, basi kuongoza kutakuwa na nguvu ya hoja. Ni kwa ajili hii ndio maana Musa akamuomba Mola wake ampe nguuvu kwa ndugu yake.

Kwa mnasaba huu itakuwa ni vizuri tutaje aliyoyasema W.L. Dewarnet kuhusu Muhammad katika ensaiklopidia yake ya Historia ‘Kisa cha maendeleo katika ulimwengu:’ “Maskani zote alizowahi kuishi Muhammad zilikuwa na upana usiozidi hatua 12 na kwenda juu hatua zisizozidi 8. Dari yake ilikuwa ya miti ya mitende, milango yake ikitokana na manyoya ya mbuzi au ya ngamia. Tandiko lake lilitandikwa ardhini na mto wake ulikwa wa ndifu.

Alikuwa akirekebisha mwenyewe viatu vyake na nguo zake, akiwasha moto, kufagia nyumba, kukama maziwa ya mbuzi, kununua chakula chake sokoni na akila kwa mkono na kuramba vidole vyake. Chakula chake kikuu kilikuwa ni tende na mkate wa shairi. Maziwa na asali ndio ilikuwa anasa yake baadhi ya wakati”

ALIY NA HARUN

Hivyohivyo ilimtokea Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Suyuti, katika Durrilmanthur anasema wakati wa kufasiri: ‘Ewe Mola wangu! Nikunjulie kifua changu “Ametoa Hadith Ibn Mardawyh, Khatib na Ibn Asakir kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alisema:

Ewe Mola wangu! Hakika mimi ninakuomba aliyokuomba ndugu yangu Musa kuwa unikunjulie kifua changu, ufanye wepesi jambo langu na unifungue fundo lilo katika ulimi wangu na nipe waziri katika watu wangu, Aliy ndugu yangu, niongeze nguvu zangu kwaye na umshirikishe katika kazi yangu, ili tukutakase sana na tukukumbuke sana, Hakika wewe unatuona.

Amesema Muslim katika Sahihi yake Juz: 2 uk. 108, chapa ya 1348 AH: Hakika Mtume alimwambia Aliy: Je, huridhii kuwa wewe kwangu uko katika daraja ya Harun na Musa? Katika Juz. 1 ya Musnad Ahmad bin Hambal: Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) aliwaita Hassan wawili (Hassan na Hussein) kwa kumfuata Harun katika kuwaita wanawe Shubbar na Shabir, yenye maana ya Hassan na Hussein.