TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 10525
Pakua: 2556


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10525 / Pakua: 2556
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA Juzuu 16

Mwandishi:
Swahili

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

وَمَا أَعْجَلَكَ عَن قَوْمِكَ يَا مُوسَىٰ ﴿٨٣﴾

83. Ni lipi lililokuharakisha ukaawaacha watu wako ewe Musa?

قَالَ هُمْ أُولَاءِ عَلَىٰ أَثَرِي وَعَجِلْتُ إِلَيْكَ رَبِّ لِتَرْضَىٰ ﴿٨٤﴾

84. Akasema: Hao hapo nyuma yangu wananifuatia. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu, ili uridhie.

قَالَ فَإِنَّا قَدْ فَتَنَّا قَوْمَكَ مِن بَعْدِكَ وَأَضَلَّهُمُ السَّامِرِيُّ ﴿٨٥﴾

85. Akasema: Hakika sisi tumewatia mtihani watu wako baada yako na msamaria amewapoteza.

فَرَجَعَ مُوسَىٰ إِلَىٰ قَوْمِهِ غَضْبَانَ أَسِفًا قَالَ يَا قَوْمِ أَلَمْ يَعِدْكُمْ رَبُّكُمْ وَعْدًا حَسَنًا أَفَطَالَ عَلَيْكُمُ الْعَهْدُ أَمْ أَرَدتُّمْ أَن يَحِلَّ عَلَيْكُمْ غَضَبٌ مِّن رَّبِّكُمْ فَأَخْلَفْتُم مَّوْعِدِي ﴿٨٦﴾

86. Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na kusikitika. Akasema: “Enyi watu wangu! Kwani Mola wenu hakuwaahidi ahadi nzuri? Je ahadi imerefuka? Au mmetaka iwafikie ghadhabu kutoka kwa Mola wenu, ndio maana mkavunja ahadi yangu?

قَالُوا مَا أَخْلَفْنَا مَوْعِدَكَ بِمَلْكِنَا وَلَـٰكِنَّا حُمِّلْنَا أَوْزَارًا مِّن زِينَةِ الْقَوْمِ فَقَذَفْنَاهَا فَكَذَٰلِكَ أَلْقَى السَّامِرِيُّ ﴿٨٧﴾

87. Wakasema: “Hatukuvunja ahadi yako kwa hiyari yetu, lakini tulibebeshwa mizigo ya vipambo vya watu. Basi tukaitupa na kadhalika Msamaria akatupa.

فَأَخْرَجَ لَهُمْ عِجْلًا جَسَدًا لَّهُ خُوَارٌ فَقَالُوا هَـٰذَا إِلَـٰهُكُمْ وَإِلَـٰهُ مُوسَىٰ فَنَسِيَ ﴿٨٨﴾

88. Akawaundia ndama, kiwiliwili chenye sauti, Wakasema: Huyu ndiye Mungu wenu na Mungu wa Musa, lakini amemsahau.

أَفَلَا يَرَوْنَ أَلَّا يَرْجِعُ إِلَيْهِمْ قَوْلًا وَلَا يَمْلِكُ لَهُمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا ﴿٨٩﴾

89. Je, hawakuona kuwa hakuwarudishia neno, wala hakuweza kuwadhuru wala kuwafaa?.

MSAMARIA NA NDAMA

Aya 83 – 89

MAANA

Baada ya kuangamia Firauni na Mwenyezi Mungu (s.w.t) kumwahidi Musa kuwa atamteremshia Tawrat na kumpa muda wake, Musa alikwenda kwa Mola wake kuichukua na kumwachia uongozi nduguye Haruna kwa Wana wa Israil, Hapo waliitumia fursa ya kuondoka Nabii wao Musa, wakaabudu ndama. Yakahakikika yale Aliokuwa wakiyawazia hapo mwanzo, pale walipowaona watu:

يَعْكُفُونَ عَلَىٰ أَصْنَامٍ لَّهُمْ قَالُوا يَا مُوسَى اجْعَل لَّنَا إِلَـٰهًا كَمَا لَهُمْ آلِهَةٌ قَالَ إِنَّكُمْ قَوْمٌ تَجْهَلُونَ ﴿١٣٨﴾

“Waliokuwa wakiyaabudu masanamu yao; wakaema: “Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu.” Akasema: “Hakika nyinyi ni watu wafanyao ujinga.” Juz.9 (7:138).

Yametangulia maelezo ya hayo katika Juz; 1 (2:51) na Juz 9 (7: 148). Aya hii tuliyo nayo na zinazofuatia hadi ya 98, zote zinazungumzia maudhui haya na yanayoambatana nayo.

Ni lipi lililokuharakisha ukaawaacha watu wako ewe Musa?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamuuliza kuhusu haraka yake huku akijua sababu, Anataka kumfahamisha yaliyoowatokea watu wake-kuabudu ndama.

Akasema: Hao hapo nyuma yangu wananifuatia. Na nimefanya haraka kukujia, Mola wangu, ili uridhie.

Dhahiri ya maneno inafahamisha kuwa Musa alitakiwa aje na watu wake, lakini akaja peke yake, ndio akajibu kuwa wao wanakuja bila ya kuchelewa, nimewatangulia ili kukuridhisha. Alisema haya akiwa hajui waliyoyazua watu wake baada yake.

Akasema Mwenyezi Mungu: Hakika sisi tumewatia mtihani watu wako baada yako na msamaria amewapoteza.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatia mtihani ili idhihirike hakika yao Waisrail. Namna ya mtihani ni kuwa Mwenyezi Mungu amewakataza kuabudu ndama kupitia kwenye ulimi wa Musa na shetani akawaamrisha kuabudu ndama kupitia ulimi wa Msamaria; wakamwasi Mungu na wakatii shetani. Ikadhihiri hakika yao ya udhaifu wa imani na ukafiri wao; sawa na afanyavyo muovu anapopata nafasi.

Musa akarudi kwa watu wake kwa ghadhabu na kusikitika.

Umetangulia mfano wake katika Juz. Juz.9 (7:150).

Akasema: Enyi watu wangu! Kwani Mola wenu hakuwaahidi ahadi nzuri?”

Anaashira kwa hili, kwamba Mwenyezi Mungu amewaahidi kuteremshiwa Tawrat kwa Mtume wao, ndani yake mna upambanuzi wa kila wanayoyahitajia katika kujua halali na haramu na kwamba Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t.) atawamilikisha makao ya wafasiki; kama ilivyoelezwa katika Juz. 9 (7:145):

وَكَتَبْنَا لَهُ فِي الْأَلْوَاحِ مِن كُلِّ شَيْءٍ مَّوْعِظَةً وَتَفْصِيلًا لِّكُلِّ شَيْءٍ فَخُذْهَا بِقُوَّةٍ وَأْمُرْ قَوْمَكَ يَأْخُذُوا بِأَحْسَنِهَا سَأُرِيكُمْ دَارَ الْفَاسِقِينَ ﴿١٤٥﴾

“Na tukamwandikia katika mbao kila kitu mawaidha na ufafanuzi wa kila jambo, Basi yashike kwa imara na uwaamrishe watu wako washike mazuri yake zaidi, Nitawaonyesha makao ya wafasiki.”

Je ahadi imerefuka?

Yaani muda wa kutokuwepo Musa umekuwa mrefu?

Au mmetaka iwafikie ghadhabu kutoka kwa Mola wenu.

Yaani mimi sikuwa mbali nanyi kwa muda mrefu, kwa nini basi mkamshirikisha Mwenyezi Mungu? Au mlitaka iwafikie ghadhabu yake na adhabu yake?.

Hii inaonyesha kuwa wao wanaamini maadamu Musa amewasimamia kwenye vichwa vyao, akiondoka wanageuka na kuipotoa dini kwa hawa zao, kama ilivyotokea.

Ndio maana mkavunja ahadi yangu.

Mmegeuka kwenye dini ya Mwenyezi Mungu baada ya kuniahidi kuwa mtakuwa thabiti.

Wakasema: Hatukuvunja ahadi yako kwa hiyari yetu.

Huku ni kukubali wazi kwamba wao walikufuru, kurtadi na kuvunja ahadi. Udhuru wao pekee ni kwamba wao ni kama wanoendeshwa hawawezi kujizuia na kufuru na hiyana; ni kama kwamba wao wametengenezwa hivyo, Hivi ndivyo inavyodhihiri hakika ya waisraili kwenye ndimi zao kuongezea vitendo vyao.

Lakini tulibebeshwa mizigo ya vipambo vya watu.

Vipambo vya watu ni vipambo vya wanawake wa watu wa Firauni. Wafasiri wamesema kuwa Waisraili walipojua kuwa wataipituka bahari na kwamba Mwenyezi Mungu atamwangamiza Firauni majini, waliwafanyia hila wanawake wa watu wa Firauni; wakawaazima vipambo vyao kwa kutoa visingizio vya harusi na mengineyo. Hili haliko mbali na tabia za kiisraili na hila zao za kuchuma mali kwa mbinu yoyote.

Basi tukaitupa na kadhalika Msamaria akatupa.

Tabari anasema katika Tafsiri yake: “Bani Israil walitupa vipambo walivyokuwa navyo ndani ya shimo, naye Msamaria akatupa alivyokuwa navyo, Vyote akavifua kwenye umbo la ndama” akawaundia ndama, kiwiliwili chenye sauti.

Umepita mfano wake katika Juz. 9 (7:148).

Wakasema: Huyu ndiye Mungu wenu na Mungu wa Musa, lakini amemsahau.

Waliosema ni Msamaria na wenzake wakikusudia kuwa huyo ni Mungu wa wa viumbe vyote akiwemo Musa lakini amemsahu na kwenda kumtafua milimani, hajui kuwa ni mgeni wetu na tunaye majumbani mwetu.

Hii inaashiria kuwa kila anayesema kuwa Mungu ana kiwiliwili yuko pamoja na waabudu ndama atake asitake.

Je, hawakuona kuwa hakuwarudishia neno, wala hakuweza kuwad- huru wala kuwafaa.

Vipi atakuwa ndama ni Mola wao na wamemtengeneza kwa mikono yao? Hasikii maneno yao wala harudishi jawabu; hawawaletei manufaa wala hawazuii na madhara. Baadhi ya wafasiri wamesema: Zaidi ya hayo hawezi kupiga pembe wala teke.

Katika Tafsir Razi, imelezwa kuwa Myahudi mmoja alimwambia Imam Ali(a.s) :“Hamkuzika Mtume wenu mpaka mlipohitalifiana.”

Imam akasema:“Hatukuhitalifiana naye, bali tulihitalifiana kuhusiana naye, nanyi hata maji ya bahari hayajakauka miguuni mkaanza kumwambia Nabii wenu, tutengenezee mungu kama walivyo na mungu wao.”

Kama ingelifaa kufasiri Qur’an kwa rai na taawili ya hisia basi tungesema kuwa kutengeneza ndama kutokana na dhahabu na kumfanya ni mungu wao ni nembo ya kwamba wao tangu zamani wana maumbile ya kuabudu mali na kwamba hiyo ndio mungu wao wa pekee asiyekuwa na mshirika.

Historia yao ya zamani na ya sasa inafahamisha hilo waziwazi. Wao wanahalalisha kila kitu kwa ajili ya mali, hata kumwaga damu na umalaya.

وَلَقَدْ قَالَ لَهُمْ هَارُونُ مِن قَبْلُ يَا قَوْمِ إِنَّمَا فُتِنتُم بِهِ وَإِنَّ رَبَّكُمُ الرَّحْمَـٰنُ فَاتَّبِعُونِي وَأَطِيعُوا أَمْرِي ﴿٩٠﴾

90. Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihani tu kwa kitu hiki. Na kwa hakika Mola wenu ni Mwingi wa rehema. Basi nifuateni na mtii amri yangu.

قَالُوا لَن نَّبْرَحَ عَلَيْهِ عَاكِفِينَ حَتَّىٰ يَرْجِعَ إِلَيْنَا مُوسَىٰ ﴿٩١﴾

91. Wakasema: Hatutaacha kumwabudu mpaka Musa atakaporejea kwetu.

قَالَ يَا هَارُونُ مَا مَنَعَكَ إِذْ رَأَيْتَهُمْ ضَلُّوا ﴿٩٢﴾

92. Akasema (Musa): Ewe Harun! Ni nini kilichokuzuia ulipowaona wamepotea.

أَلَّا تَتَّبِعَنِ أَفَعَصَيْتَ أَمْرِي ﴿٩٣﴾

93. Hata usinifute? Je,umeasi amri yangu?

قَالَ يَا ابْنَ أُمَّ لَا تَأْخُذْ بِلِحْيَتِي وَلَا بِرَأْسِي إِنِّي خَشِيتُ أَن تَقُولَ فَرَّقْتَ بَيْنَ بَنِي إِسْرَائِيلَ وَلَمْ تَرْقُبْ قَوْلِي ﴿٩٤﴾

94. Akasema: Ewe mwana wa mama yangu! Usinishike ndevu zangu, wala kichwa change; Kwa hakika niliogopa usije ukasema umewafarikisha Wana wa Israil na hukungojea kauli yangu.

قَالَ فَمَا خَطْبُكَ يَا سَامِرِيُّ ﴿٩٥﴾

95. Akasema: Una nini wewe Msamaria?

قَالَ بَصُرْتُ بِمَا لَمْ يَبْصُرُوا بِهِ فَقَبَضْتُ قَبْضَةً مِّنْ أَثَرِ الرَّسُولِ فَنَبَذْتُهَا وَكَذَٰلِكَ سَوَّلَتْ لِي نَفْسِي ﴿٩٦﴾

96. Akasema: Nimeyaona wasiyoyaona wao na nikashika sehemu chache ya mwendo wa Mtume kisha nikaitupa, na hivyo ndivyo ilivyonielekeza nafsi yangu.

قَالَ فَاذْهَبْ فَإِنَّ لَكَ فِي الْحَيَاةِ أَن تَقُولَ لَا مِسَاسَ وَإِنَّ لَكَ مَوْعِدًا لَّن تُخْلَفَهُ وَانظُرْ إِلَىٰ إِلَـٰهِكَ الَّذِي ظَلْتَ عَلَيْهِ عَاكِفًا لَّنُحَرِّقَنَّهُ ثُمَّ لَنَنسِفَنَّهُ فِي الْيَمِّ نَسْفًا ﴿٩٧﴾

97. Akasema (Musa): Basi ondoka na kwa hakika utakuwa katika maisha ukisema: ‘Usiniguse’ Na hakika una miadi kwako isiyovunjwa, Na mtazame huyo mungu wako uliyeendelea kumwabudu; hakika tutamuunguza kisha tutamtawanya baharini atawanyike.

إِنَّمَا إِلَـٰهُكُمُ اللَّـهُ الَّذِي لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ وَسِعَ كُلَّ شَيْءٍ عِلْمًا ﴿٩٨﴾

98. Hakika Mungu wenu ni Mwenyezi Mungu tu, hapana mungu mwingine ispokuwa Yeye, ujuzi wake umeenea kila kitu.

MUSA AMLAUMU HARUN

Aya 90 – 98

MAANA

Na hakika Harun alikwisha waambia kabla yake: Enyi watu wangu! Hakika nyinyi mmetiwa mtihani tu kwa kitu hiki. Na kwa hakika Mola wenu ni Mwingi wa rehema. Basi nifuateni na mtii amri yangu.

Musa alipokwenda mlimani, alimwambia ndugu yake Harun: “Shika mahali pangu katika watu wangu na utengeneze wala usifuate njia ya wafisadi.” Juz; 9 (7:142). Harun akatengeneza, kama alivyoamrishwa na ndugu yake; akatoa nasaha na kuwahadharisha wana wa Israil kutokana na Msamaria na ndama wake. Miongoni mwa maneno Aliowaambia ni: ‘Ni jambo gani lililowahadaa na ndama huyu mpaka mkashindwa na mtihani wake, mkamwelekea badala ya Muumba wa mbingu na ardhi? Basi nifu- ateni nitawaongoza njia ya uwongofu.

Basi halikuwa jawabu la watu wake ispokuwawakasema: Hatutaacha kumwabudu mpaka Musa atakaporejea kwetu, tuone rai yake kwenye hili. Kama kwamba wanamgonja amlaumu Harun kwenye hilo na awaunge mkono wao.

Kila mwenye kuathirika na mali kuliko dini yake na dhamiri yake, au akamfuata mpotezaji kwenye upotevu wake, basi yeye ni katika wafuasi wa Msamaria na chama chake. Mwenyezi Mungu amewatia mtihani waja wake kila wakati kwa ndama mwenye kutoa sauti Aliyetengenezwa kwa dhahabu au kuwa bendera inayofuta upepo.

Akasema (Musa): Ewe Harun! Ni nini kilichokuzuia ulipowaona wamepotea, hata usinifute? Je, umeasi amri yangu?

Hii kwa dhahiri inaonyesha ni lawama kwa Harun, lakini kiuhakika ni lawama na kuwatahariza wale walioabudu ndama. Kwa sababu Musa alijua fika kwamba ndugu yake Harun hakumukhalifu wala hatamkhalifu kwenye jambo lolote; na kwamba yeye alitekeleza wajibu wake kwa ukamilifu, kwa sabu yeye ni mshirika wake katika utume na kuwa ni maasumu.

Akasema: Ewe mwana wa mama yangu! Usinishike ndevu zangu, wala kichwa changu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (7:150).

Kwa hakika niliogopa usije ukasema umewafarikisha Wana wa Israil na hukungojea kauli yangu.

Musa alimwambia Harun: “Kwa nini hukuwaacha wana wa Israil na kuun- gana nami ulipowaona wanakuasi wewe na kumfuata Msamaria?” Harun akamjibu: “Niliona nikiwaaacha itatokea fitna ya umwagikaji damu baina ya makundi mawili, lililo na imani na lile lilioritadi, hapo ndio utakuwa unaweza kunilaumu na ukaniambaia: umewaacha ili yatokee yaliotokea? Kwa ufupi ni kuwa aliyepo ndiye anayeona hali ilivyo.Musa akakinai na akasema:

“Mola wangu! Nisamehe mimi na ndugu yangu na utuingize katika rehe- ma yako na wewe ni mwenye kurehemu kushinda wote wenye kurehemu.” Juz; 9 (7:151).

Kisha akamwelekea Msamaria na akasema: Una nini wewe Msamaria?

Yaani, ni jambo gani lililokuacha ukafanya uliyoyafanya?

Akasema:Nimeyaona wasiyoyaona wao na nikashika sehemu chache ya mwendo wa Mtume kisha nikaitupa, na hivyo ndivyo ilivyonielekeza nafsi yangu.

Imesemekana kuwa makusudio ya mtume hapa ni mjumbe Jibril; na sehe- mu chache ya mwendo ni mchanga alioukanyaga kwa unyayo wake au kwa kwato za farasi wake. Pia imesemekana kuwa makusudio ya mtume ni Musa na sehemu ya mwendo wake ni desturi yake.

Vile vile imesemekana kuwa Msamria ni muongo na kwamba yeye hakuona chochote katika sehemu ya mwendo wa Mtume; ispokuwa alitaka kujitoa kwa alioyafanya.

Kauli hii ina nguvu kuliko ile ya mguu wa Jibril au farasi wake. Mwenye kutengeneza ndama kwa mkono wake na akataka aabudiwe badala ya Mwenyezi Mungu kusema uongo na uzushi kwake ni jambo jepesi. Ama sauti inawezekana kutengenezwa kwa ndama kwa namna ambayo upepo ukiingia unatoa sauti; kama tulivyoeleza katika Juz. 9 (7: 148).

Vyovyote iwavyo, dhahiri ya maana inayofahamishwa na Qur’an ni kwamba Msamaria ndiye aliyefanya ufisadi, akawapoteza wana wa Israil katika kuabudu ndama. Ama jinsi alivyofanya, hatuna lazima nako kukujua wala hakuna uhusiano wowote na itikadi yetu na maisha yetu.

Akasema (Musa): Basi ondoka na kwa hakika utakuwa katika maisha ukisema: Usiniguse.

Haya ndiyo malipo yako duniani – kutengwa na watu wote, hutachanganyika na watu wala hakuna atakayetaka kuchanganyika na wewe kwa kauli wala vitendo, Ama adhabu yako huko Akhera, itakuwa chungu zaidi. Inasemekana kuwa Msamaria aliishi mwituni na wanyama.

Na hakika una miadi kwako isiyovunjwa.

Hakuna kukimbia wala kuihepa nayo ni kukutana na Mungu na kuhisabi- wa yale uliyoyazua na malipo yako ni adhabu na kuungua na moto.

Na mtazame huyo Mungu wako uliyeendelea kumwabudu; hakika tutamuunguza kisha tutamtawanya baharini atawanyike.

Huu ndio mwisho wa kila mzushi mwenye vitimbi, kuhizika na utwevu.

Hakika Mungu wenu ni Mwenyezi Mungu tu, hapana mungu mwingine ispokuwa Yeye, ujuzi wake umeenea kila kitu.

Yeye peke yake ndiye Mungu wa haki, hakuna muabudiwa ispokuwa Yeye, rehema yake imeenea kwenye kila kitu; na hakuna kitu chochote ispokuwa kinamwabudu na kumsabihi kwa kusifu.

WAISRAIL WANASHANGAZA

Ni vizuri tumalizie Aya hii kwa yale yalioelezwa katika Tafsir ya Razi. Ninamnukuu: “Ameseam Abul-Qasim Al-Ansariy, amesema: “Wachawi walikuwa ni washirikina, lakini walipoona muujiza mmoja tu wa fimbo kugeuka nyoka, walimwamini Mwenyezi Mungu na Musa, wakavumilia adhabu kali kwa ajili ya imani yao hiyo, wala hawakurudi nyuma. Lakini Wana wa israil waliiona fimbo ilivyovunjilia mbali uchawi, wakawaona wachawi walivyokubali kushindwa; kisha wakaona miujiza mingine tisa, zaidi ya hayo wakaona bahari ilivyopasuka njia kumi na mbili. Pamoja na yote hayo, baada ya kutoka baharini na kuona watu wengine wakiabudu ng’ombe nao wakamwambia Musa tufanyie Mungu kama wao na waliposikia sauti ya ndama tu wakaanza kumwabudu.”

Wakati nikifasiri Aya zinazohusianan na wana wa israil, nimekuwa nikitamani sana, kuundwe kamati ya wataalamu wa maumbile ya binadamu wafanye utafiti juu ya waisral na tabia zao. Wachunguze historia yao na:

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SITA

كَذَٰلِكَ نَقُصُّ عَلَيْكَ مِنْ أَنبَاءِ مَا قَدْ سَبَقَ وَقَدْ آتَيْنَاكَ مِن لَّدُنَّا ذِكْرًا ﴿٩٩﴾

99. Namna hivi tunakuhadithia katika habari za yaliotangulia, Na hakika tumekuletea kutoka kwetu mawaidha.

مَّنْ أَعْرَضَ عَنْهُ فَإِنَّهُ يَحْمِلُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وِزْرًا ﴿١٠٠﴾

100. Atakayejitenga nayo basi hakika siku ya Kiyama atabeba mzigo.

خَالِدِينَ فِيهِ وَسَاءَ لَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ حِمْلًا ﴿١٠١﴾

101. Watadumu humo. Ni mzigo muovu kwao kuubeba siku ya Kiyama!

يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ وَنَحْشُرُ الْمُجْرِمِينَ يَوْمَئِذٍ زُرْقًا ﴿١٠٢﴾

102. Siku itakayopulizwa parapanda na tutawakusanya wahalifu siku hiyo wakiwa buluu.

يَتَخَافَتُونَ بَيْنَهُمْ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا عَشْرًا ﴿١٠٣﴾

103. Watanong’onezana wao kwa wao: ‘Hamkukaa ila siku kumi tu.

نَّحْنُ أَعْلَمُ بِمَا يَقُولُونَ إِذْ يَقُولُ أَمْثَلُهُمْ طَرِيقَةً إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا يَوْمًا ﴿١٠٤﴾

104. Sisi tunayajua zaidi watakayoyasema, atakaposema mbora wao kwa mwendo: ‘Nyinyi hamkukaa ila siku moja tu.’

وَيَسْأَلُونَكَ عَنِ الْجِبَالِ فَقُلْ يَنسِفُهَا رَبِّي نَسْفًا ﴿١٠٥﴾

105. Wanakuuliza kuhusu milima. Sema: Mola wangu ataivurugavuruga.

فَيَذَرُهَا قَاعًا صَفْصَفًا ﴿١٠٦﴾

106. Ataiwacha tambarare iliyo sawa sawa.

لَّا تَرَىٰ فِيهَا عِوَجًا وَلَا أَمْتًا ﴿١٠٧﴾

107. Hutaona humo mabonde wala miinuko.

يَوْمَئِذٍ يَتَّبِعُونَ الدَّاعِيَ لَا عِوَجَ لَهُ وَخَشَعَتِ الْأَصْوَاتُ لِلرَّحْمَـٰنِ فَلَا تَسْمَعُ إِلَّا هَمْسًا ﴿١٠٨﴾

108. Siku hiyo watamfuata muitaji asiye na upotofu, na sauti zote zitamnyenyekea Mwingi wa rehma. Basi hutasikia ila mnong’ono.

يَوْمَئِذٍ لَّا تَنفَعُ الشَّفَاعَةُ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَـٰنُ وَرَضِيَ لَهُ قَوْلًا ﴿١٠٩﴾

109. Siku hiyo uombezi hautafaa ila wa aliyemruhusu Mwingi wa rehema na akamridhia kusema.

يَعْلَمُ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُمْ وَلَا يُحِيطُونَ بِهِ عِلْمًا ﴿١١٠﴾

110. Anayajua yalio mbele yao na yalio nyuma yao, wala wao hawawezi kumjua Yeye vilivyo.

وَعَنَتِ الْوُجُوهُ لِلْحَيِّ الْقَيُّومِ وَقَدْ خَابَ مَنْ حَمَلَ ظُلْمًا ﴿١١١﴾

111. Zitanyenyenyekea nyuso kwa Aliye hai, Mwangalizi Mkuu, Na hakika ameharibikiwa mwenye kubeba dhulma.

وَمَن يَعْمَلْ مِنَ الصَّالِحَاتِ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَا يَخَافُ ظُلْمًا وَلَا هَضْمًا ﴿١١٢﴾

112. Na mwenye kutenda mema naye ni mumin, hatahofu dhulma wala kupunjwa.

KAMA HIVYO TUNAKUSIMULIA

Aya 99 – 112

MAANA

Namna hivi tunakuhadithia katika habari za yaliotangulia.

Mwenyezi Mungu anaashiria kisa cha Musa(a.s) na habari zake, Maneno hayo anaambiwa Muhammad(s.a.w.w) . Neno ‘katika’ ni kuelezea baadhi; yaani tunakusimulia baadhi ya habari za umma uliotangulia, kama ulivyosikia. Nazo ni mazingatio na mawaidha kwa watu. Wakati huo huo zinafahamisha ukweli wako na utume wako. Kwa sababu ni habari za ghaibu.

Na hakika tumekuletea kutoka kwetu mawaidha.

Makusudio ya mawaidha hapa ni Qur’an. Imeitwa hivyo kwa sababu ndani yake kuna utajo wa Mwenyezi Mungu na sifa zake, mitume na habari zao, akhera na mambo yake, imani na ukafiri, kheri na shari, halali na haramu, kuumbwa mbingu na ardhi na mengineyo.

Atakayejitenga nayo basi hakika siku ya Kiyama atabeba mzigo.

Kila mwenye kuipinga Qur’an kwa kauli na vitendo au kwa vitendo bila ya kauli, basi atakuwa amejitenga nayo na atakuwa ameibebesha nafsi yake mzigo mzito. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema: “Hakuiamini Qur’an yule anayehalalisha yaliyo haramu” Yatakuja maelezo zaidi kwenye Aya ya 124 ya Sura hii, inshaallah.

Watadumu humo.

Yaani humo mwenye mizigo, Adhabu kuiita mizigo ni katika kutumia sababu kwa msabibishi.

Ni mzigo muovu kwao kuubeba siku ya Kiyama!

Yaani mzigo wa madhambi walioubebesha nafsi zao kwa sababu ya kujtenga kwao na Qur’an.

Siku itakayopulizwa parapanda.

Hiki ni kinaya cha kufufuliwa walioko makaburini.

Na tutawakusanya wahalifu siku hiyo wakiwa buluu.

Hii pia ni kinaya cha kufazaika kwao na hali mbaya watakayokuwa nayo. Ya kushangaza ni yale niliyoyasoma katika Tafsir Al-Bahru-Muhit ya Abu Hayan Al-Andalusi, akisema: “Makusudio ya ubuluu ni ubuluu wa macho, na macho ya buluu yanachukiza sana kwa waarabu kwa sababu maadui zao waroma wana macho ya buluu.” Mfasiri huyu alikuwa karibu na wakati wa vita vya msalaba (Crusade).

Watanong’onezana wao kwa wao: Hamkukaa ila siku kumi tu.

Miongoni mwa sifa za wahalifu siku ya Kiyama nikuwa wao kutokana na vituko watakavyopambana navyo, watasahau muda wa kukaa kwao katika maisha ya dunia.

Kwa hiyo wataambiana kwa lugha ya maneno au kwa lugha ya hali kwa sauti ya chini: Hatukukaa ispokuwa siku kumi au masaa kadhaa au kitambo kidogo tu.

Unaweza kuuliza : Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya hii, amewazungumzia kuwa watasema tumekaa siku kumi, katika Sura Kahf, Aya 19 amesema, siku moja au sehemu ya siku; na katika Sura Rum, Aya 55, watasema kuwa hawakukaa ispokuwa saa moja. Je, kuna wajihi gani wa kuchanganya Aya zote hizo?

Razi amejibu kuwa baadhi ya wahalifu wataona ni siku moja wengine kumi. Tuonavyo sisi ni kuwa neno kumi, siku au saa katika Aya sio kuzungumzia kauli halisi ya wahalifu; ispokuwa ni kinaya cha vile watakavyowazia uchache wa muda na kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) hayo ameyaletea ibara ya kumi, mara nyingine siku na hata saa. Mwenyezi Mungu ameyaashiria haya kwa kauli yake: “Siku atakayowaita nanyi mkamwitikia kwa kumsifu. Na mkadhani kuwa hamkukaa ila muda mchache tu.” Juz.15 (17:52).

Sisi tunayajua zaidi watakayoyasema, atakaposema mbora wao kwa mwendo: Nyinyi hamkukaa ila siku moja tu.

Mbora wao kwa mwendo ni yule mwenye sera nzuri na mwenye kujua hakika ya mambo. Maana ni kuwa wakati wanapoambiana kuwa tumekaa siku kumi tu, huyo mbora wao atawaambia: Maisha mliyokuwa nayo mkishindana, si chochote ispokuwa ni kama ndoto tu, hayawezi kuhisabiwa kwa wakati wala kwa siku. Maisha ya uhakika hasa ni haya tuliyo nayo hivi sasa, ambayo hayana muda wala mwisho.

Wanakuuliza kuhusu milima, Sema: Mola wangu ataivurugavuruga. Ataiwacha tambarare iliyo sawasawa, Hutaona humo mabonde wala miinuko.

Muulizaji alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kuwa vipi milima itakavyokuwa siku ya kiyama? Mwenyezi Mungu akamwambia mtume wake Mtukufu: mjibu Aliyeuliza sawali hili kuwa Mwenyezi Mungu ataing’oa na ataigeuza kuwa ni mavumbi yatakayotawanyika angani na pale ilipokuwa patakuwa tambarare bila ya mabonde wala miinuko.

Siku hiyo watamfuata muitaji asiye na upotofu.

Siku hiyo ni siku ya Kiyama, watakofuata ni viumbe na muitaji ni yule atakayewaita viumbe kwenye mkusanyiko, hisabu na malipo. Maana ni kuwa mwito utakuwa wa haki na utaitikiwa na wote, hakuna atakayeweza kuuhalifu: “Siku atakapoita muitaji kuliendea jambo linalochusha; macho yao yatainama; watatoka makaburini kama nzige waliotawanyika; wanamkimbilia muitaji na makafiri watasema: Hii ni siku ngumu. (54:6-9).

Na sauti zote zitamnyenyekea Mwingi wa rehma. Basi hutasikia ila mnong’ono.

Makusudio ya sauti ni wenye sauti hizo, Na mnong’ono unafahamisha unyenyekevu.

Siku hiyo uombezi hautafaa ila wa aliyemruhusu Mwingi wa rehema na akamridhia kusema.

Hii iko katika maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Wala hawaombei ila yule Aliemridhia” (21:28). Tumeazungumzia shafaa kwa urefu katika Juz; 1 (2:97).

Anayajua yalio mbele yao na yalio nyuma yao wala wao hawawezi kumjua Yeye vilivyo.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (2:255).

Zitanyenyenyekea nyuso kwa Aliye hai, Mwangalizi Mkuu.

Makusudio ya nyuso ni walio na nyuso hizo. Maana ni kuwa viumbe wote kesho watasalimu amri mbele ya Aliye hai, asiyekufa na Msimamizi wa kila jambo wala hakuna kinachosimamiwa ila kwa ajili yake.

Na hakika ameharibikiwa mwenye kubeba dhulma.

Mwenye hasara zaidi katika watu kesho ni yule mwenye kuwadhulumu watu na akaingilia heshima na uhuru wao. Na mwenye faida mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule mwenye kufanya kwa ajili ya kheri ya binadamu na masilahi kwa njia ya kheri na ya ubinadamu.

Na mwenye kutenda mema naye ni mumin, hatahofu dhulma wala kupunjwa.

Hii ni sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu: “Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni mumin tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa mazuri zaidi waliyokuwa wakiyafanya.” Juz; 14 (16: 97).

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلْنَاهُ قُرْآنًا عَرَبِيًّا وَصَرَّفْنَا فِيهِ مِنَ الْوَعِيدِ لَعَلَّهُمْ يَتَّقُونَ أَوْ يُحْدِثُ لَهُمْ ذِكْرًا ﴿١١٣﴾

113. Namna hiyo tumeiteremsha Qur’an kwa lugha ya kiarabu na tumekariri humo maonyo ili wawe na takua au iwaletee makumbusho.

فَتَعَالَى اللَّـهُ الْمَلِكُ الْحَقُّ وَلَا تَعْجَلْ بِالْقُرْآنِ مِن قَبْلِ أَن يُقْضَىٰ إِلَيْكَ وَحْيُهُ وَقُل رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا ﴿١١٤﴾

114. Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa haki, Wala usiifanyie haraka hii Qur’an kabla haujamalizika wahyi wake, Na sema: Mola wangu! Nizidishie elimu.

وَلَقَدْ عَهِدْنَا إِلَىٰ آدَمَ مِن قَبْلُ فَنَسِيَ وَلَمْ نَجِدْ لَهُ عَزْمًا ﴿١١٥﴾

115. Na hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau wala hatukuona kwake azma.

وَإِذْ قُلْنَا لِلْمَلَائِكَةِ اسْجُدُوا لِآدَمَ فَسَجَدُوا إِلَّا إِبْلِيسَ أَبَىٰ ﴿١١٦﴾

116. Na tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu wote ispokuwa Iblisi alikataa.

فَقُلْنَا يَا آدَمُ إِنَّ هَـٰذَا عَدُوٌّ لَّكَ وَلِزَوْجِكَ فَلَا يُخْرِجَنَّكُمَا مِنَ الْجَنَّةِ فَتَشْقَىٰ ﴿١١٧﴾

117. Tukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo, Basi asiwatoe katika Bustani (Pepo) hii, mkaingia mashakani.

إِنَّ لَكَ أَلَّا تَجُوعَ فِيهَا وَلَا تَعْرَىٰ ﴿١١٨﴾

118. Hakika humo hutakuwa na njaa wala hutakuwa uchi.

وَأَنَّكَ لَا تَظْمَأُ فِيهَا وَلَا تَضْحَىٰ ﴿١١٩﴾

Na kwamba wewe hutapata kiu humo wala hutapata joto.

فَوَسْوَسَ إِلَيْهِ الشَّيْطَانُ قَالَ يَا آدَمُ هَلْ أَدُلُّكَ عَلَىٰ شَجَرَةِ الْخُلْدِ وَمُلْكٍ لَّا يَبْلَىٰ ﴿١٢٠﴾

120. Lakini shetani alimtia wasi- wasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujulishe mti wa kuishi milele na ufalme usiokoma?

فَأَكَلَا مِنْهَا فَبَدَتْ لَهُمَا سَوْآتُهُمَا وَطَفِقَا يَخْصِفَانِ عَلَيْهِمَا مِن وَرَقِ الْجَنَّةِ وَعَصَىٰ آدَمُ رَبَّهُ فَغَوَىٰ ﴿١٢١﴾

121. Basi wakaula wote na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustani. Na Adam akamuasi Mola wake na akapotea njia.

ثُمَّ اجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَتَابَ عَلَيْهِ وَهَدَىٰ ﴿١٢٢﴾

122. Kisha Mola wake akamteua na akamkubalia toba yake naakamwongoa.

TUMEITERMSHA QUR’AN KWA LUGHA YA KIARABU

Aya 113 – 122

MAANA

Namna hiyo tumeiteremsha Qur’an kwa lugha ya kiarabu na tumekariri humo maonyo ili wawe na takua au iwaletee makumbusho.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameteremsha Qur’an kwa mja wake Muhammad(s.a.w.w) kwa lugha ya kiarabu na akawahadharisha waja na hisabu yake na adhabu yake, kwa mifumo mbalimbali, ili wapate kumcha na kumtii kwenye hukumu zake zote au awamkumbuke yeye wanapofanya madhambi ili watubu na wamwombe msamaha. Au hapa, ni kwa maana ya na; kama mfano ukisema: “Kuwa mwana wa chuoni au mwenye zuhudi.” Kwa sababu kukumbuka kuko pamoja na takua; kama ambavyo zuhudi iko pamoja na elimu.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Juz. 12 (12:2). Huko tumejibu kwa ufafanuzi swali la mwenye kuuliza, kwa nini Qur’an imeteremshwa kwa lugha ya kiarabu pamoja na kuwa Muhammad (s.a.w.) ametumwa kwa watu wote?

WASIFU WA QUR’AN

Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameitaja Qur’an, katika kitabu chake kitukufu, kwa sifa nyingi, zikiwemo hizi zifuatazo:

1. Ya kiarabu; kama ilivyo katika Aya hii na ile ya Juz. 12 (12:2).

2. Ukumbusho:

إِنَّا نَحْنُ نَزَّلْنَا الذِّكْرَ ﴿٩﴾

“Na hakika sisi tumeuteremsha ukumbusho huu” Juz; 14 : (15:9).

3. Nuru:

قَدْ جَاءَكُم مِّنَ اللَّـهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

“Hakika imekwishawafikia nuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu” Juz. 6: (5:15).

4. Upambanuzi:

إِنَّهُ لَقَوْلٌ فَصْلٌ ﴿١٣﴾

“Hakika hiyo ni kauli ya upambanuzi” (86:13).

5. Uongofu: “Hicho ni kitabu, hakina shaka ndani yake, ni uongofu kwa wenye takua.” Juz; 1 (2:2).

6. Hekima:

وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ ﴿٢﴾

“Naapa kwa Qur’an yenye hekima” (36:2).

وَالْقُرْآنِ الْمَجِيدِ ﴿١﴾

“Naapa kwa Qur’an Tukufu” (50:1).

7. Roho:

رَفِيعُ الدَّرَجَاتِ ذُو الْعَرْشِ يُلْقِي الرُّوحَ مِنْ أَمْرِهِ عَلَىٰ مَن يَشَاءُ مِنْ عِبَادِهِ لِيُنذِرَ يَوْمَ التَّلَاقِ ﴿١٥﴾

“Hupeleka Roho kwa amri yake juu ya amtakaye katika waja wake, ili kuonya kwa siku ya makutano” (40:15).

8. Haki:

إِنَّهُ الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٧﴾

Hakika hiyo ni haki itokayo kwa Mola wako, Lakini watu wengi hawaamini, Juz; 12 (11:17).

9. Habari kubwa:

قُلْ هُوَ نَبَأٌ عَظِيمٌ ﴿٦٧﴾ أَنتُمْ عَنْهُ مُعْرِضُونَ ﴿٦٨﴾

“Sema: Hiyo ni habari kubwa ambayo nyinyi mnaipuuza.” (38:67–68).

10. Ponyo:

قُلْ هُوَ لِلَّذِينَ آمَنُوا هُدًى وَشِفَاءٌ ﴿٤٤﴾

“Sema: hiyo ni uongofu na ponyo kwa wenye kuamini” (41:44).

11. Rehema:

وَإِنَّهُ لَهُدًى وَرَحْمَةٌ لِّلْمُؤْمِنِينَ ﴿٧٧﴾

Na hakika hiyo ni uwongofu na rehema kwa waumini, (27:77).

12. Uteremsho:

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٨٠﴾

Ni uteremsho utokao kwa Mola wa walimwengu wote (56:80).

13. Bishara na onyo:

قُرْآنًا عَرَبِيًّا لِّقَوْمٍ يَعْلَمُونَ ﴿٣﴾ بَشِيرًا وَنَذِيرًا ﴿٤﴾

Ni Kitabu kilichopambanuliwa Aya zake, cha kusomwa kwa kiarabu kwa watu wanaojua, kinachotoa bishara na kuonya (41:3 – 4).

14. Nguvu na utukufu:

وَإِنَّهُ لَكِتَابٌ عَزِيزٌ ﴿٤١﴾

“Na hakika ni Kitabu chenye nguvu na utukufu.” (41:41).

15. Adhimu:

وَلَقَدْ آتَيْنَاكَ سَبْعًا مِّنَ الْمَثَانِي وَالْقُرْآنَ الْعَظِيمَ ﴿٨٧﴾

Na hakika tumekupa Aya saba zinazorudiwa rudiwa na Qur’an Adhimu, Juz; 14 (15:87).

16. Ubainifu:

وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿٢﴾

Naapa kwa Kitabu kinachobainisha (43:2).

Hakika bora zaidi inayofahamisha sifa hizi ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameteremsha Qur’an kwa Mtume wake, kwa ajili tu ya kuwaongoza watu kwenye wema, amani na utulivu wao.

Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa haki.

Imam Ali(a.s) anasema, akilingania Mola wake:“Kutakata ni kwako! Ni utukufu ulioje wa tunayoyaona katika uumbaji wako! Na udogo ulioje wa hayo katika uweza wako! Na ni vituko vilioje wa tuvionavyo katika ufalme wako! Na ni uduni ulioje wa tusivyoviona katika ufalme wako! Na ueneaji ulioje wa neema zako katika dunia! Na ni udogo ulioje wa neema hizo kulinganisha na neema za Akhera!”

Wala usiifanyie haraka hii Qur’an kabla haujamalizika wahyi wake

Kuna Hadith isemayo kuwa Nabii wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alikuwa anapoletewa Qur’an na Jibril hufuatilia kuisoma kwa kuhofia kisimpite kitu, ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha asikilize tu wala asifuatishe na kwamba atulie tu wala asiogope kusahau. Usahihi wa Hadith hii unafahamishwa na ile Aya isemayo:

“Usiutikisie, huu wahyi, ulimi wako kwa kuufanyia haraka, Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha, kisha ni juu yetu kuubainisha” (75: 16 – 19).

NIZIDISHE ELIMU

Na sema: Mola wangu! Nizidishie elimu

Elimu aliyomwamrisha Mwenyezi Mungu Mtume wake, kuomba kuzidishiwa ni ile inayomnufaisha mwenye nayo na mwenginewe. Hakuna itikadi wala misimamo, falsafa wala sharia au fasihi na sanaa, zote hizi si lolote mbele ya Mwenyezi Mungu ispokuwa kama zitakuwa ni nyenzo za maisha bora yasiyokuwa na matatizo wala vikwazo vyovyote.

Hata maisha ya Akhera yanafungamana moja kwa moja na kazi itakayon- ufaisha katika maisha ya duniani. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: “Mbora zaidi wa watu mbele ya Mwenyezi Mungu ni yule anayewafaa zaidi watu.” Hakuna mwenye shaka kwamba anayewafaa zaidi watu ni yule anayefanya kwa ajili ya maisha bora na jamii.

Kila kitu, wakati huu, kinafahamisha waziwazi kuwa hakuna maisha bora ispokuwa kwa elimu; bila ya kutofautisha baina ya maisha ya kimaada, kijamii na kiutamaduni.

Kama ambavyo jamii yoyote haiwezi kuishi maisha bora bila ya mitambo ya kuchapisha, viwanda vya nguo, nyenzo za mawasiliano, vifaa vya nyumbani na maengineyo ya lazima; basi vile vile haiwezekani kuishi huru na heshima bila ya elimu ya siasa, uchumi, ya kijamii na elimu nyinginezo zinazofanya kazi ya kumtumikia mtu kwa ajili ya utu.

Hii ndiyo elimu sahihi na ndiyo iliyokusudiwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Na sema: Mola wangu! Nizidishie elimu’ na kauli ya Mtume: “Mwenye kufuata njia ya kutafuta elimu, amefuata njia ya kwenda peponi.”

Yeyote mwenye kufasiri neno elimu kwa maana ya kuhifadhi maandishi na maelezo, basi huyo ni katika wale wanaoamini kuwa elimu ni matamshi na maandishi tu; na dini ni kupiga takbira na kusoma tasbih tu.

Na hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau wala hatukuona kwake azma.

Maagano Alioagana Mwenyezi Mungu na Adam ni kutoukurubuia mti na kwamba asisikilize mwito wa Iblis. Makusudio ya kusahau ni kuacha na azma ni uthabiti.

Na tulipowaambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu wote ispokuwa Iblisi alikataa.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Juz; 1 (2:34), Juz; 8 (7:11), Juz. 14 (15: 30 – 31), na katika Juz. 15 ( 17: 61) na (18:50).

Tukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo, Basi asiwatoe katika Bustani (Pepo) hii, mkaingia mashakani. Hakika humo hutakuwa na njaa wala hutakuwa uchi, Na kwamba wewe hutapata kiu humo wala hutapata joto.

Yaani hutatabika kwenye joto la jua, Neno joto tumelifasiri kutoka neno Dhuha lenye maana ya mchana, Umetumika mchana kwa maana ya joto kwa vile mchana kunakuwa na joto kali.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimuhadharisha Adam kutokana na wasiwasi wa Ibilisi na akamwambia, wewe una hiyari ya mambo mawili; ama unitii mimi na umuasi Ibilisi upate hii Pepo (Bustani) – kama uinavyo – safi na nzuri. Humo hamna njaa, kiu, kukaa uchi wala maradhi, Hamna maumivu wala huzuni, hamna mauti, damu wala machozi, hamna kuhangaika kwenye joto wala baridi, Hamna chochote ispokuwa amani, utulivu na raha.

Au uniasi mimi na kumtii Ibilisi, utoke Peponi uende duniani kwenye taabu, balaa zote, magonjwa na majanga.

Lakini Adam alisahau hadhari hizi; akaandamwa na misukosuko yeye na kizazi chake, kuanzia na kuuliwa Habil hadi uhalifu wa Israil na mengineyo yasiyokuwa na kikomo.

Sio mbali kuwa kutolewa Adam Peponi ni somo na fundisho kwa yule anayefuata matamanio na kwamba malipo yake mbele ya Mwenyezi Mungu ni adhabu, Angalia kifungu ‘Mtaka yote hukosa yote’ Juz; 1 (2: 35–39).

Lakini shetani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujulishe mti wa kuishi milele na ufalme usiokoma? Basi wakaula wote na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Bustani.

Umetangulia mfano wa Aya hii katika Juz; 8 (7:19 – 22).

Na Adam akamuasi Mola wake na akapotea njia.

Unaweza kuuliza : Adam ni nabii na nabii ni maasumu wa makosa, imekuwaje Mwenyezi Mungu (s.w.t) kumnasibishia uasi na upotevu?

Wamelijibu hilo kwa majibu kadhaa; miongoni mwayo ni kuwa makusudio ya kuasi ni kuacha mapendekezo sio wajibu, jambo ambalo halipingani na isma.

Jibu jingine ni kuwa Adam alipokuwa Peponi alikuwa Akhera ambako hakuna tabligh wala taklifa yoyote ya kuhitajia mitume, na kwamba utume wa Adam ulikuwa wa duniani sio wa Akhera.

Kwa hali yoyote iwayo ni kwamba Adam alitubia na akamuomba msamaha Mola wake;kisha Mola wake akamteua na akamkubalia toba yake na akamwongoa.

Tumeuazungumzia hayo kwa ufafanuzi zaidi katika Juz; 1 (2:35–39) kifungu cha ‘isma ya mitume.