TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA Juzuu 19

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA33%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 14 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 8924 / Pakua: 3824
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA Juzuu 19

Mwandishi:
Swahili

1

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA

كَذَّبَتْ ثَمُودُ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٤١﴾

141. Thamud waliwakadhibisha mitume.

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَالِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٤٢﴾

142. Alipowaambia ndugu yao Swaleh: Je, hamna takua?

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٤٣﴾

143. Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٤٤﴾

144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٤٥﴾

145. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

أَتُتْرَكُونَ فِي مَا هَاهُنَا آمِنِينَ ﴿١٤٦﴾

146. Je, mtaachwa salama katika haya yaliyopo hapa?

فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿١٤٧﴾

147. Katika mabustani na chem- chem?

وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ ﴿١٤٨﴾

148. Na mimea na mitende yenye makole yalioiva?

وَتَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا فَارِهِينَ ﴿١٤٩﴾

149. Na mnachonga majumba mlimani kwa ustadi

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٥٠﴾

150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ ﴿١٥١﴾

151. Wala msitii amri za waliopituka mipaka.

الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ ﴿١٥٢﴾

152. Ambao wanafanya ufisadi katika ardhi wala hawaiten- genezi.

قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ﴿١٥٣﴾

153. Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa tu.

مَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿١٥٤﴾

154. Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi. Basi lete ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

قَالَ هَـٰذِهِ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ﴿١٥٥﴾

155. Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalum.

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٥٦﴾

156. Wala msimguse kwa ubaya isije ikawashika adhabu ya siku kubwa.

فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا نَادِمِينَ ﴿١٥٧﴾

157. Lakini wakamuua wakawa wenye kujuta.

فَأَخَذَهُمُ الْعَذَابُ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٥٨﴾

158. Basi ikawashika adhabu. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٥٩﴾

159. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

SWALEH

Aya 141 – 159

MAANA

Kisa cha Swaleh kimetangulia katika Juz. 8 (7: 73 – 79) na Juz. 12 (11: 61 -68).

Thamud waliwakadhibisha mitume. Alipowaambia ndugu yao Swaleh: Je, hamna takua? Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

Zimetangulia Aya hizi kwa herufi zake katika sura hii Aya 105 – 110, na pia katika sehemu iliyopita bila ya mabadiliko yoyote isipokuwa jina tu la Thamud na Swaleh. Tumesema huko kuwa siri ya hilo ni kuwa risala ya mitume wote ni moja.

Je, mtaacha salama katika haya yaliyopo hapa katika mabustani na chemchem na mimea na mitende yenye makole yalioiva? Na mna chonga majumba mlimani kwa ustadi

Kabila la Thamud lilizama katika anasa na strehe – matunda, mito, makasri, wanyama n.k. Wakiwa wameghafilika na kila kitu isipokuwa matamanio yao na ladha zao. Ndipo ndugu yao Swaleh akawaonya na mwisho mbaya na akawaambia, Je, mmemsahau Mwenyezi Mungu na yeye hajawasahau? Je, mmejiaminisha na matukio ya ghafla?

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini wala msitii amri za waliopituka mipaka ambao wanafanya ufisadi katika ardhi wala hawaitengenezi.

Makusudio ya waliopituka mipaka, walio wafisadi, ni viongozi ambao ndio chimbuko la balaa zote; isipokuwa wachache sana. Hakuna dini wala misimamo, katika ufahamu wao, isipokuwa masilahi yao na masilahi ya jamaa zao.

Wafisadi hawa, katika kaumu ya Swaleh, walikuwa tisa; kama ilivyoelezwa katika Aya nyingine: kwenye juzuu hii. “Na walikuwako mjini watu tisa wakifanya ufisadi katika ardhi wala hawafanyi la masilahi” (25:48).

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa tu.

Umerogwa na mchawi mpaka umekuwa hujui unalolisema. Hivi ndivyo wasemavyo vijana wengi wa kileo wanapoambiwa swalini na fungeni.

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi, unakula chakula na kutembea sokoni, sasa vipi unateremshiwa wahyi zaidi yetu sisi?

Basi lete ishara ukiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Walisema haya wakiwa wameazimia kuendelea na ukafiri wao na inadi yao, hata kama wataletewa dalili elfu na moja; vinginevyo maombi yao yangelikuwa ya haki na ya sawa.

Akasema: Huyu ngamia jike; awe na zamu yake ya kunywa na nyinyi muwe na zamu yenu ya kunywa katika siku maalum. Wala msimguse kwa ubaya isije ikawashika adhabu ya siku kubwa.

Walimuomba awaletee muujiza unaofahamisha utume wake, akawaletea ngamia kwa njia isiyo ya kawaida na akawawekea sharti la maji kwa zamu; siku moja yao na siku moja ya ngamia na kwamba wasimdhuru isije ikawafikia adhabu,

lakini wakamuua wakawa wenye kujuta, Basi ikawashika adhabu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7: 77 – 78).

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٦٠﴾

160. Kaumu ya Lut waliwakadhibisha mitume.

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٦١﴾

161. Alipowaambia ndugu yao Lut: Je, hamna takua?

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٦٢﴾

162. Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٦٣﴾

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٤﴾

164. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

أَتَأْتُونَ الذُّكْرَانَ مِنَ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٥﴾

165. Je, katika viumbe wote mnawaendea wanaume?

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ ﴿١٦٦﴾

166. Na mnaacha alichowaumbia Mwenyezi Mungu katika wake zenu? Bali nyinyi ni watu mnaoruka mipaka.

قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا لُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمُخْرَجِينَ ﴿١٦٧﴾

167. Wakasema: Kama hutakoma ewe Lut bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa.

قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ الْقَالِينَ ﴿١٦٨﴾

168. Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.

رَبِّ نَجِّنِي وَأَهْلِي مِمَّا يَعْمَلُونَ ﴿١٦٩﴾

Mola wangu! Niokoe na ahli zangu kwa wayatendao.

فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ﴿١٧٠﴾

Basi tukamuokoa na ahli zake wote.

إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ﴿١٧١﴾

171. Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma.

ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ ﴿١٧٢﴾

Kisha tukwaangamiza wale wengine.

وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ ﴿١٧٣﴾

173. Na tukawanyesheza mvua, basi ni uovu mno wa mvua ya waliyoonywa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٧٤﴾

174. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٧٥﴾

175. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

LUT

Aya 160-175

MAANA

Kisa cha Lut kimetangulia katika Juz. 8 (7:80 –84) na Juz. 12 (11:82– 87).

Kaumu ya Lut waliwakadhibisha mitume. Alipowaambia ndugu yao Lut: Je, hamna takua?

Ni ndugu yao katika kuwa pamoja na makazi; si katika dini wala nasabu. Kwa kuwa yeye alikuja hapo na ami yake, Ibrahim(a.s) kutoka Babel (Babylon) kupitia Misr hadi Palestina. Lut alikaa katika bonde la Jordan na Ibrahim akakaa katika nyanda za juu kaskazini. Hapo ilikuwa ni karne kumi na tisa kabla ya kuzaliwa Nabii Isa (19 B.C.)

Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya sura hii na pia sehemu iliyopita.

“Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

Lut alianza kama alivyoanza Nuh, Hud na Swaleh(a.s ) . Kwa sababu risala ya wote ni moja. Soma katika sura hii Aya zinazomzungumzia kila mmoja katika wao.

Je, katika viumbe wote mnawaendea wanaume?

Mnafanya kitendo hiki cha fedheha kwa wanaume katika wanadamu?

Na mnaacha alichowaumbia Mwenyezi Mungu katika wake zenu?

Kwa hiyo mnahalifu hukumu ya maumbile na kanuni, tabia na lengo la kumbwa mume na mke.

Tendo lenu halikubaliwi hata na wanyama na wadudu. Lakini bunge la Uingereza limeruhusu ulawiti. Hiyo ni dalili kuwa Uingereza ni duni zaidi kuliko wanyama katika hulka yake na thamani yake. Sio mbali kuwa hii ni natija ya historia yake ndefu ya ukoloni unaochukiwa. Kwa sababu utaghuti na uadui una mwisho mbaya.

Bali nyinyi ni watu mnaoruka mipaka.

Mmepituka mipaka yote kwa hawa, usafihi, uasi na ujeuri wenu.

Wakasema: Kama hutakoma ewe Lut bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaotolewa.

Umetangulia mfano wake katika Aya 116 ya Sura hii.

Akasema: Hakika mimi ni katika wanaokichukia hiki kitendo chenu.

Katika maana yake ni; Aya 216 ya sura hii! “Na ikiwa watakuasi basi sema mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yatenda.”

Mola wangu! Niokoe na ahli zangu kwa wayatendao. Basi tukamuokoa na ahli zake wote. Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma. Kisha tukwaangamiza wale wengine. Na tukawanyesheza mvua, basi ni uovu mno wa mvua ya waliyoonywa.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:83 – 84) na Juz. 14 (15:59 – 60).

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya Sura hii na pia sehemu iliyopita.

كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٧٦﴾

176. Watu wa mwituni waliwakadhibisha mitume.

إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾

177. Alipowaambia Shua’yb: Je, hamna takua?

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٧٨﴾

178. Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٧٩﴾

179. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٨٠﴾

180. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ ﴿١٨١﴾

181. Timizeni kipimo sawasawa wala msiwe miongoni mwa wanaopunja.

وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ ﴿١٨٢﴾

182. Na pimeni kwa mizani iliyo sawa.

وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ ﴿١٨٣﴾

183. Wala msiwapunguzie watu vitu vyao, Wala msifanye ufisadi katika nchi mkafanya vurugu.

وَاتَّقُوا الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالْجِبِلَّةَ الْأَوَّلِينَ ﴿١٨٤﴾

184. Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.

قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ﴿١٨٥﴾

185. Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa tu.

وَمَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ ﴿١٨٦﴾

186. Na wewe si chochote ila ni mtu kama sisi, na kwa hakika tunakuona ni katika waongo.

فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿١٨٧﴾

187. Basi tuangushie kipande cha mbingu, ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

قَالَ رَبِّي أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١٨٨﴾

188. Akasema: Mola wangu anajua zaidi mnayoyatenda.

فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ الظُّلَّةِ إِنَّهُ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٨٩﴾

189. Basi wakamkadhibisha, ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٩٠﴾

190. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٩١﴾

191. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

SHUA’YB

Aya 176 – 191

MAANA

Kisa cha Shua’yb kimetangulia katika Juz. 8 (7: 85) na Juz. 12 (11:84 – 95).

Watu wa mwituni waliwakadhibisha mitume. Alipowaambia Shua’yb: Je, hamna takua?

Wafasiri wamesema kuwa watu wa mwituni ni watu waliokuwa karibu na Madyan kwenye miti mingi.

Alipowaambia Shua’yb: Je, hamna takua?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakusema ndugu yao Shua’yb, kama alivyosema ndugu yao Hud, Swaleh na Lut, kwa sababu Shua’yb si mtu wa hapo kinasabu wala hana uhusiano wowote na watu wa mwituni, isipokuwa ujirani. Mwenyezi Mungu alimtuma kwao; kama alivyomtuma kwa watu wake wa Madyan.

Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

Aya hizi zimetanguliwa kwa herufi zake kupitia mdomoni mwa Nuh, Hud, Swaleh na Lut. Hayo ni maneno ya kila Nabii.

Timizeni kipimo sawasawa wala msiwe miongoni mwa wanaopunja. Na pimeni kwa mizani iliyo sawa. Wala msiwapunguzie watu vitu vyao, Wala msifanye ufisadi katika nchi mkafanya vurugu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7: 85) na Juz. 12 (11:84)

Na mcheni aliyewaumba nyinyi na vizazi vilivyotangulia.

Yaani mhofie adhabu ya Mwenyezi Mungu aliyewaumba nyinyi na wale waliotangulia.

Wakasema: Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa tu.

Imetangulia kwa herufi zake katika Aya 153 ya sura hii.

Wewe si chochote ila ni mtu kama sisi, na kwa hakika tunakuona ni katika waongo.

Yaani wewe unakusudia uwongo katika madai yako ya utume, kwa dalili ya kuwa wewe ni mtu unayekula chakula na kutembea sokoni. Lau wahyi ungeliwashukia watu basi watu wote wangelikuwa Mitume.

Ibn Hisham katika kitabu Al-Mughni, katika kuelezea watu wasiofaliwa na maneno yoyote, anasema: “Mtu mmoja alimwambia mwengine: ‘Baba yako amemfanyaje punda wako?’ Akasema: ‘Amemuuzo’ akiwa na maana amemuuza. Yule muulizaji akasema kwa mshangao: kwa nini umeweka o kwenye herufi ya mwisho? yule akajibu: si wewe umeweka o kwenye herufi ya mwisho!” Mtu wa namna hii utamwambiaje?

Basi tuangushie kipande cha mbingu, ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Aliwahadharisha na adhabu wakamdharau na wakasema iko wapi hiyo adhabu unayotutisha nayo, basi teremsha kipande cha mbingu kiwe ni adhabu, ukiwa ni mkweli wa madai yako.

Akasema: Mola wangu anajua zaidi mnayoyatenda na amri ni yake peke yake, akitaka ataileta haraka au ataicheleweshwa. Basi wakamkadhibisha, ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakubainisha kivuli hicho. Wafasiri wanasema ni mawingu waliyoyafanya kivuli kutokana na joto lililowapata, kisha yakawanyeshea mvua ya moto iliyowaunguza wote.

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya Sura hii na pia sehemu iliyopita.

8

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA

وَإِنَّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٩٢﴾

192. Na hakika hiyo ni uteremsho wa Mola wa walimwengu wote.

نَزَلَ بِهِ الرُّوحُ الْأَمِينُ ﴿١٩٣﴾

193. Ameiteremsha Roho mwaminifu.

عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ الْمُنذِرِينَ ﴿١٩٤﴾

194. Juu ya moyo wako, ili uwe katika waonyaji.

بِلِسَانٍ عَرَبِيٍّ مُّبِينٍ ﴿١٩٥﴾

195. Kwa ulimi wa kiarabu ulio wazi.

وَإِنَّهُ لَفِي زُبُرِ الْأَوَّلِينَ ﴿١٩٦﴾

197. Na hakika hiyo iko katika vitabu vya kale.

أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿١٩٧﴾

198. Je haikuwa kwao ni ishara kwamba wanayajua haya maulama wa wana wa Israil?

وَلَوْ نَزَّلْنَاهُ عَلَىٰ بَعْضِ الْأَعْجَمِينَ ﴿١٩٨﴾

198. Lau tungeliitermsha juu ya mmoja wa wasiokuwa waarabu.

فَقَرَأَهُ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا بِهِ مُؤْمِنِينَ ﴿١٩٩﴾

199. Na akawasomea wasingelikuwa wenye kuiamini.

كَذَٰلِكَ سَلَكْنَاهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ ﴿٢٠٠﴾

200. Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ حَتَّىٰ يَرَوُا الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ﴿٢٠١﴾

201. Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu.

فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿٢٠٢﴾

202. Basi itawafikia ghafla na hali hawaitambui.

فَيَقُولُوا هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ ﴿٢٠٣﴾

203. Na watasema: Je sisi tutapewa muda?

أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ ﴿٢٠٤﴾

204. Basi je wanahimiza adhabu yetu?

أَفَرَأَيْتَ إِن مَّتَّعْنَاهُمْ سِنِينَ ﴿٢٠٥﴾

205. Unaonaje, kama tukiwastarehesha kwa miaka.

ثُمَّ جَاءَهُم مَّا كَانُوا يُوعَدُونَ ﴿٢٠٦﴾

206. Kisha yawafikie waliyokuwa wakiahidiwa.

مَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يُمَتَّعُونَ ﴿٢٠٧﴾

207. Hayatawafaa yale waliyostareheshewa.

وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ ﴿٢٠٨﴾

208. Wala hatukuuangamiza mji wowote ila ulikuwa na waonyaji.

ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَالِمِينَ ﴿٢٠٩﴾

209. Kuwa ni ukumbusho wala hatukuwa sisi ni wenye kudhulumu.

وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ ﴿٢١٠﴾

210. Wala mashetani hawakuteremka nayo.

وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ ﴿٢١١﴾

211. Wala haiwapasi wala hawaiwezi.

إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ ﴿٢١٢﴾

121. Hakika wao wametengwa na kusikia.

AMEITERMSHA ROHO MWAMINIFU

Aya 192 – 212

MAANA

Na hakika hiyo ni uteremsho wa Mola wa walimwengu wote. Ameiteremsha Roho mwaminifu juu ya moyo wako, ili uwe katika waonyaji.

Hiyo ni Qur’an. Roho mwaminifu ni Jibril(a.s) na maneno yanelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) .

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja visa vya mitume katika Aya zilizotangulia, sasa anamtaja Muhammad na Qur’an na kwamba Jibril ameitermsha kwa Mtume mtukufu ili apambane na makafiri na wapinzani kwa Aya zake na ubainifu wake. Jibril ameitwa roho kwa sababu ameiteremsha Qur’an ambayo ni uongofu na ponyo kwa roho:

هُوَ لِلَّذِينَ آمَنُوا هُدًى وَشِفَاءٌ ﴿٤٤﴾

“Hiyo ni uwongofu na ponyo kwa wenye kuamini.” (41:44).

Na ameitwa mwaminifu kwa sababu ni mtiifu kwa Mwenyezi Mungu, akiwa na biidii ya kuufikisha ujumbe wake kwa mitume, kama ulivyo. Yeye vile vile anaujua huo ujumbe na malengo yake.

Kwa ulimi wa kiarabu ulio wazi.

Katika Juz. 12 (12:2) tumebainisha sababu za kushuka Qur’an kwa lugha ya kiarabu, tazama huko.

Na hakika hiyo iko katika vitabu vya kale.

Yaani vitabu vya Mwenyezi Mungu vilivyotangulia, vilimbashiria Muhammad(s.a.w.w) na Qur’an. Huko nyuma tulithibitisha dalili za kiakili na kinakili kwamba Qur’an ni wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Katika dalili za kiakili ni kwamba Qur’an iliwashinda wapinzani hata kuleta mfano mmoja tu wa Sura zake. Walijaribu wakashindwa. Na kwamba inatolea habari mambo ya ghaibu na yakatokea. Pia hiyo Qur’an inachukua njia nyingi za tafsiri. Wala hakuna siri ya hili ila ni kwa kuwa inatoka kwa ambaye amekizunguka kila kitu kwa ujuzi. Tazama Juz. 1 (2: 23) Juz. 5 (4:53 na 82) na Juz. 18 (24:55).

Ama dalili za kinukuu, miongoni mwazo ni Tawrat na Injili za asili, zilizoleta bishara ya Muhammad. Tazama Juz. 9 (7: 157). Vile vile vitabu vingine vya mbinguni vilitoa habari ya kuja Muhammad. Tazama Juz. 1 (2:46).

Je, Haikuwa kwao ni ishara kwamba wanayajua haya maulama wa wana wa Israil?

Maulama wa kiyahudi, kabla ya kutumwa Mtume(s.a.w.w) , walikuwa wakimbashiria Muhammad; wakiwazungumzia waarabu kuhusiana naye na kutaja sifa zake kwa makuraishi na wengineo. Alipokuja wakasilimu baadhi ya Mayahudi waliokuwa wakimzungumzia; kama vile Abdallah bin Salaam na wenzake. Vile vile wakasilimu jamaa katika waarabu na wakampinga mayahudi wengine na vigogo katika makuraishi.

Aya hii inawaambia wale waliomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) baada ya kusikia hadith ya mayahudi kumhusu. Inawaambia, vipi mnamkadhibisha na hali mmewasikia maulama wa kiyahudi kabla, wakimtolea habari, wakikiri kuwa ametajwa katika Tawrat? Ushahidi wao huo hauwatoshi kuwa ni dalili ya ukweli wa Muhammad(s.a.w.w) ?

Hakuna mwenye shaka kwamba dalili hii ni tosha kwa mwenye kuitafuta haki kwa njia ya haki, lakini vigogo ambao walipinga utume wa Muhammad(s.a.w.w) walifanya hivyo kwa sababu ya masilahi yao; sio kwa sababu ya udhaifu wa hoja na dalili:

وَمَا تُغْنِي الْآيَاتُ وَالنُّذُرُ عَن قَوْمٍ لَّا يُؤْمِنُونَ ﴿١٠١﴾

“Na dalili na maonyo hayawafai watu wasioamini.” Juz. 11 (10:101).

Lau tungeliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa waarabu na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuiamini.

Wao hawaiamini haki na ubainifu wake, iwe imekuja na mwarabu au asiyekuwa mwarabu. Kwa sababu haki na elimu kwao ni masilahi; vinginevyo si chochote kwao. Tumelikariri hilo mara nyingi pamoja na uwazi wake.

Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu.

Yaani wakosefu wanapoisikia haki au Qur’an wanaipinga na kuikanusha. Kwa maneno mengine ni kuwa mbengu inaota vizuri kwenye ardhi iliyo na rutuba, lakini ikiwa ardhi si nzuri, basi uotaji wake utakuwa hauna manufaa:

وَالْبَلَدُ الطَّيِّبُ يَخْرُجُ نَبَاتُهُ بِإِذْنِ رَبِّهِ وَالَّذِي خَبُثَ لَا يَخْرُجُ إِلَّا نَكِدًا ﴿٥٨﴾

“Na mji mzuri hutoa mimea yake kwa idhini ya Mola wake. Na ule ulio mbaya hautoi ila kwa taabu tu.” Juz. 8 (7:58).

Kadhalika haki inaleta matunda na athari ikisadifu kuwa kwenye nafsi safi na haileti chochote ikiwa kwenye nafsi chafu. Maana ni kuwa Qur’an haina athari yoyote katika nafsi zao isipokuwa upinzani na kukadhibisha.

Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu. Basi itawafikia ghafla na hali hawaitambui.

Wakosefu hawaiamini Qur’an. Yaani wao hawaiamini haki hata ikiwa na dalili kiasi gani ila ikiwafikia adhabu kwa ghafla. Na wakionywa kabla wanaifanyia masihara. Ilivyo ni kwa kunyenyekea wakati wa kuona adhabu ni unafiki na ni kulazimishwa sio hiyari.

Na watasema: Je sisi tutapewa muda?

Waliiharakia adhabu kabla ya kuiona na wakamwambia Mtume wao ilete ukiwa ni katika wakweli. Walipoiona kwa macho walijuta na wakatamani lau wangelipewa muda ili waamini na watii. Ndivyo alivyo mpotevu; anatamani kurudi au kupewa muda baada ya kupita wakati.

Basi je wanahimiza adhabu yetu?

Haya ni maneno ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuwajibu wale waliomwambia Mtume wao. Tuangushie kipande cha mbingu na tuletee yale uliyotuahidi. Maana yake ni kuwa vipi mnaiharakia adhabu na ikiwafikia hamuiwezi wala kuikwepa.

Unaonaje, kama tukiwastarehesha kwa miaka, kisha yawafikie waliyokuwa wakiahidiwa, hayatawafaa yale waliyostareheshewa?

Wakosefu watatamaani kupewa muda watakapoiona adhabu, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawajibu kwamba kupewa muda hakufai kitu hata kama muda utakuwa mrefu kiasi gani. Bali kila muda unavyokuwa mrefu ndio madhambi yanazidi na kuongezeka na kuzidi adhabu yao.

Wala hatukuuangamiza mji wowote ila ulikuwa na waonyaji.

Aya hii iko katika maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَمَا كُنَّا مُعَذِّبِينَ حَتَّىٰ نَبْعَثَ رَسُولًا ﴿١٥﴾

“Wala sisi hatuadhibu mpaka tupeleke Mtume.” Juz. 15 (17:15).

Kuwa ni ukumbusho wala hatukuwa sisi ni wenye kudhulumu katika kuangamiza miji, wakati ambapo tulituma waonyaji wa hiyo adhabu, na wakumbushaji wa twaa ya Mwenyezi Mungu wakiwa na dalili. Wakawakadhibisha ndio ikastahiki adhabu.

Wala mashetani hawakuteremka nayo wala haiwapasi wala hawaiwezi.

Watu wa wakati wa ujahili walikuwa wakiitakidi ukuhani; kwamba kila kuhani ana shetani wake anayemletea habari za ghaibu. Iliposhuka Qur’an wakasema kuwa inatoka kwa shetani kwenda kwa makuhani ambao nao wanampelekea Muhammad(s.a.w.w) ; au yeye mwenyewe ni kuhani anayeteremkiwa na shetani.

Ndipo Mwenyezi Mungu akayajibu madai haya, kuwa Qur’an ni uongofu, mwanga na ni ubainifu ulio wazi. Ni wapi na wapi ukuhani na ushetani kulinganisha na uongofu na ubainifu? Wao ni dhaifu na ni duni zaidi. Zaidi ya hayo ni kuwa hakika wao wametengwa na kusikia.

Wamezuiliwa kusikia Qur’an pale Mwenyezi Mungu anapompa Jibril kuileta kwa Muhammad(s.a.w.w) . Ikiwa mashetani wameshindwa kuleta hata Aya moja mfano wake na pia kusikiliza japo tamko moja, basi watainukuu vipi kwa makuhani na kuitolea habari?

فَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ ﴿٢١٣﴾

213. Basi usimwombe Mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

214. Na uwonye jamaa zako walio karibu.

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

215. Na inamisha bawa lako kwa wanokufuata katika waumini.

فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢١٦﴾

216. Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyafanya.

وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ ﴿٢١٧﴾

217. Na mtegemee Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ ﴿٢١٨﴾

218. Ambaye anakuona unaposimama.

وَتَقَلُّبَكَ فِي السَّاجِدِينَ ﴿٢١٩﴾

219. Na mageuko yako katika wale wanaosujudu.

إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٢٢٠﴾

220. Hakika yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

WAONYE JAMAA ZAKO WA KARIBU

Aya 213 – 220

MAANA

Basi usimwombe Mungu mwingine pamoja na Mwenyezi Mungu ukawa miongoni mwa watakaoadhibiwa.

Dhahiri ya mfumo wa maneno inaonyesha yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , lakini makusudio ni kutoa habari kuwa kila atakayemuomba Mungu mwingine zaidi ya Mwenyezi Mungu basi atakuwa ni mwenye kuadhibiwa kwa hali yoyote atakayokuwa.

Na uwonye jamaa zako walio karibu.

Mtume(s.a.w.w) ni mwenye kuamrishwa kuwaonya watu wote:

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ ﴿١﴾ قُمْ فَأَنذِرْ ﴿٢﴾

“Ewe uliyejigubika! Simama uonye.” (74:1 – 2),

عَجَبًا أَنْ أَوْحَيْنَا إِلَىٰ رَجُلٍ مِّنْهُمْ أَنْ أَنذِرِ النَّاسَ وَبَشِّرِ الَّذِينَ آمَنُوا ﴿٢﴾

“Kwamba tumempa wahyi mmoja wao, kuwa uwaonye watu na uwape bishara wale walioamini.” Juz. 11 (10:2).

Amehusisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja jamaa wa Mtume(s.a.w.w) , kwa sababu mwenye kutaka kutengeneza kwanza anajianza yeye mwenyewe, kisha jamaa zake, ndio wafuatie wengine. Jamaa zake wakimsadiki na kumwamini watamsaidia kueneza mwito wake.

Maneno ya Waislamu yamekuwa mengi kuhusiana na Aya hii. Jamaa katika Sunni wamesema kuwa iliposhuka Aya hii Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alisema: “Ewe Fatima bint Muhammad! Ewe Swafiya bint Abdul Muttwalib! Enyi wana wa Abdillah! Fanyeni amali, kwani mimi siwatoshelezei chochote kwa Mwenyezi Mungu.

Shia na jamaa wengie wa kisunni; akiwemo: Ahmad bin Hambal, An-Nasai, As-Suyutwi, Abu Na’im Al-Baghwi, Atha’alabi, mwenye kitabu Assiratul-halabiya, mwenye kitabu Kanzul-u’mmal na wengineo, wamesema kuwa, iliposhuka Aya hii, Mtume(s.a.w.w) aliwaita watu wa ukoo wa Abdul-Muttwalib. Wakati huo walikuwa ni watu arobaini, wakiwemo maami zake: Abu Twalib, Hamza, Abbas na Abu Lahab.

Alikuwa amewaandalia karamu. Baada ya kula na kunywa, akasema: “Enyi wana wa Abdul-Muttwalib! Nimewaletea kheri ya duniani na Akhera na Mwenyezi Mungu ameniamrisha nitoe mwito wa hilo. Basi ni nani atakayenisaidia kwenye jambo hili, awe ndugu yangu, wasii wangu na khalifa wangu kwenu?”

Wakanyamaza wote, isipokuwa Ali(a.s) akasema:“Mimi ewe Nabii wa Mwenyezi Mungu.” Basi akamshika shingoni na akasema: “Hakika huyu ni ndugu yangu, wasii wangu na khalifa wangu kwenu. Basi msikilizeni na mumtii [1]

Tukio hili alilitaja Muhammad Haykal katika kitabu chake Hayatu Muhammad, chapa ya kwanza na akaliondoa katika chapa ya pili.

Abu Hayyan Al-Andalusi katika Bahrul-muhit, anasema: “Zimepokewa Hadith kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kuhusiana na hilo.” Anaashiria Hadith zilizomtaja Imam Ali na zile ambazo hazikumtaja. Wala hakuna kupingana baina ya Hadith hizi.

Kwa sababu kuzichanganya pamoja ni jambo linalowezekana na la karibu sana. Mtume(s.a.w.w) aliwaandalia chakula watu arobaini katika jamaa zake na kuwaambia ni nani atakayenisaidia … kisha pia akawaambia mimi siwatoshelezi lolote kwa Mwenyezi Mungu.

Na inamisha bawa lako kwa wanokufuata katika waumini.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 14 (15:88).

Na ikiwa watakuasi basi sema: Mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyafanya.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , awaambie wale jamaa zake aliowaonya. ‘Aliye karibu na Mwenyezi Mungu na Mtume wake ni yule aliyekurubishwa na takua. Na aliye mbali na Mwenyezi Mungu na Mtume wake ni yule aliyewekwa mbali na maasi, kwa namna yoyote atakavyokuwa’

Na mtegemee Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu na uachane nao wakikuasi; wala roho isikutoke juu yao, na uelekee kwa Mwenyezi Mungu peke yake katika mambo yako yote.

Ambaye anakuona unaposimama kwenye tahajjud (Swala za usiku wa manane)na mageuko yako katika wale wanaosujudu.

Shia Imamiyya wanasema kuwa mababa wote wa Mtume walikuwa wakimpwekesha Mwenyezi Mungu. Miongoni mwa dalili zao katika hilo ni Aya hii; walipofasiri mgeuko kwa maana ya mgeuko wake katika migongo ya wanaompwekesha Mungu; yaani kupitia mifupani mwao.

Tamko la Aya linakubaliana na maana haya na pia linakubaliana na tafsiri ya anayesema kuwa Mungu anakuona ukiwa pamoja na wanaoswali. Dhahiri ya mfumo wa maneno inafahamisha tafsiri hii zaidi kuliko ile.

Hakika yeye ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Anasikia kauli na anajua siri na vitendo vyote na kuvilipa. Vikiwa ni kheri basi ni kheri na vikiwa ni shari basi ni shari.

هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ ﴿٢٢١﴾

221. Je niwaambie ambao mashetani wanawashukia?

تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ ﴿٢٢٢﴾

222. Wanamshukia kila mzushi mkubwa, mwingi wa dhambi.

يُلْقُونَ السَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَاذِبُونَ ﴿٢٢٣﴾

223. Wanawapa masikio na wengi wao ni waongo.

وَالشُّعَرَاءُ يَتَّبِعُهُمُ الْغَاوُونَ ﴿٢٢٤﴾

224. Na washairi ni wapotofu ndio wanaowafuata.

أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِي كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ ﴿٢٢٥﴾

225. Je huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde?

وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ ﴿٢٢٦﴾

226. Na kwamba wao wanasema wasiyoyatenda?

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَذَكَرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا وَانتَصَرُوا مِن بَعْدِ مَا ظُلِمُوا وَسَيَعْلَمُ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَيَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ ﴿٢٢٧﴾

227. Isipokuwa wale ambao wameaamini na wakatenda mema na wakamtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi na wakajitetea wanapodhulumiwa. Na punde watajua waliodhulumu ni mgeuko gani watakaogeuka.

WASHAIRI WANAFUATWA NA WAPOTOFU

Aya 221 – 227

MAANA

Qur’an inawapiga vita wabatilifu, lakini kabla ya chochote, kwanza inawapiga vita kwa mantiki ya kiakili iliyo salama na inawajadili kwa njia nzuri, huku ikiwalingania kwenye haki kwa hekima na mawaidha mazuri; ikifafanua kwa kila aina ya mfumo na kuwaomba, kwa upole na ulaini kabisa, walete hoja zao:

لَّوْلَا يَأْتُونَ عَلَيْهِم بِسُلْطَانٍ بَيِّنٍ ﴿١٥﴾

“Kwa nini hawawaletei dalili bayana?” Juz. 15 (18:15).

Wanapoleta hoja dhaifu, Qur’an huibatilisha na kubainisha udhaifu uliopo. Washirikina na watu wengi wanaojali masilahi yao tu, wamesema mengi kuhusiana na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Miongoni mwa madai yao ni kuwa Qur’an inatokana na shetani na pia kudai kuwa Muhammad(s.a.w.w) ni mshairi. Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawajibu kwa haya yafuatayo:

Je niwaambie ambao mashetani wanawashukia? Wanamshukia kila mzushi mkubwa, mwingi wa dhambi.

Hili ni jibu la kauli yao kuwa Qur’an ni katika wahyi wa shetani. Njia ya kujibu ni kuwa shetani anaingiza wasiwasi na ubatilifu kwa waongo na wenye madhambi mfano wao: “Mashetani watu na majini. Baadhi yao wanawapa wenzao maneno ya kupambapamba kuwahadaa.” Juz. 8 (6:112).

Shetani hana njia kwa wa kweli na waaminifu, kama vile mitume na viongozi wema. Zaidi ya hayo ni kuwa ni kuwa Qur’an ni haki na kheri na mawazo ya shetani ni shari na uzushi.

Wanawapa masikio na wengi wao ni waongo.

Makusudio ya kuwapa masikio hapa ni kuwasikiliza. Wanaosikilizwa ni makafiri. Maana ni kuwa wale ambao wanawasikiliza mashetani na kuchukua kutoka kwao uwongo na ubatilifu ndio makafiri. Na makafiri wengi ni waongo katika mazungumzo yao na kauli zao. Muhammad(s.a.w.w) ni mkweli katika kauli zake zote na vitendo vyake vyote; vipi aambiwe amesikiliza na kupokea kutoka kwa shetani?

Na washairi ni wapotofu ndio wanaowafuata. Je huwaoni kwamba wao wanatangatanga katika kila bonde na kwamba wao wanasema wasiyoyatenda?

Hii ni kuwajibu washirikina waliosema kuwa Muhammad ni mshairi. Njia ya kubainisha ni kuwa kuna tofauti kubwa baina ya washairi na Muhammad kwa njia hizi zifuatazo:

Kwanza : wale waliomfuata Muhammad(s.a.w.w) walimfuata kwa kumwamini na kumwadhimisha. Na pia kumwamini Mwenyezi Mungu wakitarajia biashara isiyofilisika.

Ndio maana walimfidia kwa roho zao na wakapigana na mababa zao na watoto wao kwa ajili yake. Lakini washairi wao wanaishi katika njozi na kufikirika tu. Wakale walisema: “ushairi ni njozi ” wala hakuna anayewafuata hawa isipokuwa wale wanaoelekeana nao.

Pili : washairi wengi hapo zamani walikuwa wakiwasaidia viongozi madhalimu. Mshairi alikuwa akitumia kipawa chake na akili yake kutunga shairi au nyimbo itakayoimbwa mbele ya viongozi madhalimu. Sasa hili ni wapi na wapi na risala ya Muhammad(s.a.w.w) ambayo hiyo yenyewe ni mapinduzi dhidi ya dhulma na ufisadi?

Tatu, kwamba washairi wengi wanasema sana na kutenda kidogo, wala hakiwapi umuhimu kitu isipokuwa hawa na malengo yao tu ndio yanayowapa msukumo yakiwalekeza popote yanapoelekea. Lakini Muhammad(s.a.w.w) yeye hatamki kwa hawa yake wala hafuati isipokuwa wahyi kutoka kwa Mola wake. Sasa vipi ataambiwa ni mshairi:

وَمَا عَلَّمْنَاهُ الشِّعْرَ وَمَا يَنبَغِي لَهُ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْآنٌ مُّبِينٌ ﴿٦٩﴾

“Wala hatukumfundisha mashairi, wala hayatakikani kwake. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur’an inayobainisha.” (36:69).

Unaweza kuuliza : Je hii haifahamishi kuwa Uislamu unapiga vita mashairi, kutokana na Qur’an kuyashutumu?

Jibu : Hapana! Qur’an haikushutumu shairi kama shairi au washairi kama washairi; isipokuwa imewashutumu washairi wanaoipinga haki na kufuata kombokombo. Ama washairi wanaoelezea matumaini ya wanyonge na kuwa pamoja na wanaodhulumiwa, kuusaidia uadilifu na uhuru wa binadamu na kupinga utaghuti, ujinga na kurudi nyuma, hawa wako katika safu ya wapigania jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu.

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) aliulizwa unasemaje kuhusu washairi? Akasema: “Hakika muumini ni mpigania jihadi kwa upanga wake na ulimi wake. Naapa kwa yule ambaye nafsi yangu iko mikononi mwake, wao ni kama kwamba wanarusha mikuki.”

Aina ya mashairi ambayo ni mikuki katika nyoyo za madhalimu ndiyo aliyoikusudia Mtume(s.a.w.w) katika kauli yake: “Hakika katika shairi kuna hekima.” Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema: “Amemfundisha ubainifu.” (55:4).

Hakuna mwenye shaka kuwa ushairi ni fani ya hali ya juu ya ubainifu na fasihi, kama ambavyo ni utajiri wa lugha na hazina yake yenye thamani.

Ndio maana Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawavua washairi wema na wapigania jihadi kwa kusema:

Isipokuwa wale ambao wameaamini na wakatenda mema na wakamtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi na wakajitetea wanapodhulumiwa.

Yaani washairi wakiitetea haki na na watu wake kutokana na wachokozi na maadui na wakautetea uhuru wa ubinadamu na heshima yake.

Hii ni nukuu iliyo wazi kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwamba shairi la kimapinduzi dhidi ya dhulma na uonevu ni katika umuhimu wa dini, imani na matendo mema.

Katika maana ya Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t):

لَّا يُحِبُّ اللَّـهُ الْجَهْرَ بِالسُّوءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلَّا مَن ظُلِمَ ﴿١٤٨﴾

“Hapendi Mwenyezi Mungu maneno ya kutangaza uovu ila kwa mwenye kudhulumiwa.”

Juz. 6 (4:148).

Na punde watajua waliodhulumu ni mgeuko gani watakaogeuka.

Huu ni ukemeo na kiaga cha mwisho mbaya kwa kila mwenye kudhlumu na kuonea.

Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu Mola wa viumbe wote na rehema na amani zimshukie Muhammad na kizazi chake kitakatifu.

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA

فَجُمِعَ السَّحَرَةُ لِمِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ﴿٣٨﴾

38. Basi wakakusanywa wachawi wakati wa siku maalum.

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلْ أَنتُم مُّجْتَمِعُونَ ﴿٣٩﴾

39. Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika?

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ السَّحَرَةَ إِن كَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ﴿٤٠﴾

40. Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakaoshinda.

فَلَمَّا جَاءَ السَّحَرَةُ قَالُوا لِفِرْعَوْنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجْرًا إِن كُنَّا نَحْنُ الْغَالِبِينَ ﴿٤١﴾

41. Basi walipokuja wachawi wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa tutashinda?

قَالَ نَعَمْ وَإِنَّكُمْ إِذًا لَّمِنَ الْمُقَرَّبِينَ ﴿٤٢﴾

42. Akasema: Ndio, hapo nanyi hakika mtakuwa miongoni mwa wanaokurubishwa.

قَالَ لَهُم مُّوسَىٰ أَلْقُوا مَا أَنتُم مُّلْقُونَ ﴿٤٣﴾

43. Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa.

فَأَلْقَوْا حِبَالَهُمْ وَعِصِيَّهُمْ وَقَالُوا بِعِزَّةِ فِرْعَوْنَ إِنَّا لَنَحْنُ الْغَالِبُونَ ﴿٤٤﴾

44. Wakatupa kamba zao na fimbo zao na wakasema: Kwa nguvu za Firauni hakika sisi bila shaka ni wenye kushinda.

فَأَلْقَىٰ مُوسَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ تَلْقَفُ مَا يَأْفِكُونَ ﴿٤٥﴾

45. Musa akatupa fimbo yake, mara ikavimeza walivyovibuni.

فَأُلْقِيَ السَّحَرَةُ سَاجِدِينَ ﴿٤٦﴾

46. Wachawi wakapomoka kusujudu.

قَالُوا آمَنَّا بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٤٧﴾

47. Wakasema: Tumemwamini Mola wa Walimwengu.

رَبِّ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ﴿٤٨﴾

48. Mola wa Musa na Harun.

قَالَ آمَنتُمْ لَهُ قَبْلَ أَنْ آذَنَ لَكُمْ إِنَّهُ لَكَبِيرُكُمُ الَّذِي عَلَّمَكُمُ السِّحْرَ فَلَسَوْفَ تَعْلَمُونَ لَأُقَطِّعَنَّ أَيْدِيَكُمْ وَأَرْجُلَكُم مِّنْ خِلَافٍ وَلَأُصَلِّبَنَّكُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٤٩﴾

49. Akasema Firauni: Je, mmemwamini kabla sijawaruhusu. Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliyewafundisha uchawi, lakini punde mtajua. Nitawakata mikono yenu na miguu yenu kwa kubadilisha, kisha nitawasulubu nyote.

قَالُوا لَا ضَيْرَ إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا مُنقَلِبُونَ ﴿٥٠﴾

50. Wakasema: Haidhuru, hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu.

إِنَّا نَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لَنَا رَبُّنَا خَطَايَانَا أَن كُنَّا أَوَّلَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٥١﴾

51. Hakika sisi tunatumai Mola wetu atughufirie makosa yetu kwa kuwa ndio wa kwanza kuamini.

WALIFIKA WACHAWI

Aya 38 – 51

MAANA

Basi wakakusanywa wachawi wakati wa siku maalum.

Siku yenyewe ni sikukuu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

قَالَ مَوْعِدُكُمْ يَوْمُ الزِّينَةِ وَأَن يُحْشَرَ النَّاسُ ضُحًى ﴿٥٩﴾

“Akasema: Miadi yenu ni siku ya sikukuu na watu wakusanywe kabla ya adhuhuri.” Juz. 16 (20:59).

Na watu wakaambiwa: Je, mtakusanyika ili mshuhudie mapambano haya? Watu hawahitaji kuhimizwa kwenye mambo haya; hao wenyewe watashindana kufika. Na hili ndilo alilolitaka Musa, ili haki idhihirike na batili ibatilike machoni mwa watu.

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakaoshinda.

Waliosema haya kwa watu ni Firauni na wakuu wake. Dhahiri ya kauli yao hii inaashiria kuwa wana shaka na dini ya wachawi na kwamba wao wanitafuta haki ili waifuate, lakini haya sio makusudio yao. Kwa sababu wao na wachawi wako kwenye dini moja. Makusudio yao ni kuwa huenda tutabaki kwenye uthabiti wa dini yetu wala hatutamfuta Musa.

Basi walipokuja wachawi wakamwambia Firauni: Je, tutapata ujira ikiwa tutashinda? Akasema: Ndio, hapo nanyi hakika mtakuwa miongoni mwa wanaokurubishwa. Musa akawaambia: Tupeni mnavyotaka kutupa. Wakatupa kamba zao na fimbo zao na wakasema:

“Kwa nguvu za Firauni hakika sisi bila shaka ni wenye kushinda. Musa akatupa fimbo yake, mara ikavimeza walivyovibuni. Wachawi wakapomoka kusujudu.Wakasema: Tumemwamini Mola wa Walimwengu. Mola wa Musa na Harun.

Akasema Firauni: Je, mmemwamini kabla sijawaruhusu. Hakika yeye ndiye mkubwa wenu aliyewafundisha uchawi, lakini punde mtajua. Nitawakata mikono yenu na miguu yenu kwa kubadilisha, kisha nitawasulubu nyote. Wakasema: Haidhuru, hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu. Hakika sisi tunatumai Mola wetu atughufirie makosa yetu kwa kuwa ndio wa kwanza kuamini.

Aya hizi zote zimetajwa katika Juz. 9 (7: 113 – 126); wala hakuna tofauti baina ya hapa na huko, isipokuwa katika baadhi ya ibara tu; kwa mfano kule imesemwa: ‘wakaja wachawi’ na hapa ikasemwa; ‘walipokuja wachawi,’ n.k.

وَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنْ أَسْرِ بِعِبَادِي إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ ﴿٥٢﴾

52. Na tulimpelekea wahyi Musa kwamba nenda na waja wangu wakati wa usiku, kwa hakika mtafuatwa.

فَأَرْسَلَ فِرْعَوْنُ فِي الْمَدَائِنِ حَاشِرِينَ ﴿٥٣﴾

53. Basi Firauni akawatuma mjini wakusanyao.

إِنَّ هَـٰؤُلَاءِ لَشِرْذِمَةٌ قَلِيلُونَ ﴿٥٤﴾

54. Hakika hawa ni kikundi kidogo.

وَإِنَّهُمْ لَنَا لَغَائِظُونَ ﴿٥٥﴾

55. Nao wanatuudhi.

وَإِنَّا لَجَمِيعٌ حَاذِرُونَ ﴿٥٦﴾

56. Na sisi ni wengi wenye kuchukua hadhari.

فَأَخْرَجْنَاهُم مِّن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿٥٧﴾

58. Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem.

وَكُنُوزٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ ﴿٥٨﴾

58. Na mahazina na vyeo vya heshima.

كَذَٰلِكَ وَأَوْرَثْنَاهَا بَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿٥٩﴾

59. Hivyo ndivyo! Na tukawarithisha wana wa Israil.

فَأَتْبَعُوهُم مُّشْرِقِينَ ﴿٦٠﴾

60. Kisha wakawafuata walipotokewa na jua.

فَلَمَّا تَرَاءَى الْجَمْعَانِ قَالَ أَصْحَابُ مُوسَىٰ إِنَّا لَمُدْرَكُونَ ﴿٦١﴾

61. Yalipoonana makundi mawili, watu wa Musa wakasema: Hakika tumepatikana.

قَالَ كَلَّا إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهْدِينِ ﴿٦٢﴾

62. Akasema: Hapana! Hakika Mola wangu yuko pamoja nami, ataniongoza.

فَأَوْحَيْنَا إِلَىٰ مُوسَىٰ أَنِ اضْرِب بِّعَصَاكَ الْبَحْرَ فَانفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرْقٍ كَالطَّوْدِ الْعَظِيمِ ﴿٦٣﴾

63. Tulimpelekea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana na kila sehemu ikawa kama milima mkubwa.

وَأَزْلَفْنَا ثَمَّ الْآخَرِينَ ﴿٦٤﴾

64. Na tukawajongeza hapo wale wengine.

وَأَنجَيْنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُ أَجْمَعِينَ ﴿٦٥﴾

65. Na tukamwokoa Musa na waliokuwa pamoja naye wote.

ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ ﴿٦٦﴾

66. Kisha tukawazamisha hao wengine.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿٦٧﴾

67. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿٦٨﴾

68. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

KUGHARIKI FAIRAUNI NA WATU WAKE

Aya 52 – 68

MAANA

Na tulimpelekea wahyi Musa kwamba nenda na waja wangu wakati wa usiku, kwa hakika mtafuatwa.

Mwenyezi Mungu alimwamrisha Musa atoke na wana wa Israil kutoka ardhi ya Misri usiku na akampa habari kwamba Firauni atawafuata ili awarudishe.

Basi Firauni akawatuma mjini wakusanyao.

Firauni alipojua kuwa Musa na watu wake wametoka aliwakusanyia watu ili awarudishe kwenye utawala wake na awape adhabu ya utoro.

Akasema: Hakika hawa ni kikundi kidogo nao wanatuudhi na sisi ni wengi wenye kuchukua hadhari.

Ni nani huyo Musa na watu wake. Wao si chochote kwetu; wanajaribu kutukasirisha na kutufanyia jeuri, na sisi tunawachunga. Basi watapata adhabu ya matendo yao. Lakini juu ya mipango ya Firauni kuna mipango ya Mwenyezi Mungu. Imam(a.s) anasema:Mambo yanakuwa kwa makadirio ili maangamizi yawe kwa mpangilio.

Basi tukawatoa katika mabustani na chemchem na mahazina na vyeo vya heshima.

Firauni na jeshi lake alitoka ili amwadhibu Musa na watu wake, lakini Mungu akawaadhibu wao na akawatoa katika yale waliyokuwa wakiyamilikii na kustarehe nayo; yakiwemo makasri ya ghorofa, mito inayotiririka, miti iliyojaa matunda kochokocho, mahazina yaliyojificha, mabembea, mabwawa ya kuogelea na sehemu za kupunga upepo. Yote haya na mengineyo waliyaacha bila ya kurudi.

Hivyo ndivyo! Na tukawarithisha wana wa Israil.

Tabari anasema: “Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwarithisha wana wa Israil majumba ya Firauni na watu wake.” Abu Hayyani Al-Andalusi naye amesema katika kitabu Al-bahrul-Muhit: “Haya ndio maana ya dhahiri, kwa sababu Aya ya kurithishwa wana wa Israil, imekuja moja kwa moja baada ya Aya ya kuwatoa.”

Wengine wamesema kuwa Mwenyezi Mungu aliwarithisha wana wa Israil mfano wa alivyokuwa Firauni na watu wake. Kwa sababu Waisrail hawakurudi Misri baada ya kuitoka.

Vyovyote iwavyo Aya inaeleza kuwa Mwenyezi Mungu hawaachi madhal- imu na dhulma yao na kwamba yeye anawaadhibu mikononi mwa wenye ikhlasi au kwa sababu yoyote. Haya ndiyo tunayoyaamini na kuyakubali. Ama uchunguzi wa historia na mfano wake tunawaachia wataalamu wake, ila ikiwa tuna yakini nayo.

Kisha wakawafuata walipotokewa na jua.

Firauni alitoka na jeshi lake la wapanda farasi na wendao kwa miguu kumtafuta Musa na watu wake wakawapata lilipochomoza jua.

Yalipoonana makundi mawili, kundi la Musa na la Firauni, watu wa Musa wakasema : Hakika tumepatikana.

Walisema hivyo kwa hofu na fazaa, kuwa adui amekwishatufikia hatuna la kufanya.

Akasema: Hapana! Hakika Mola wangu yuko pamoja nami, ataniongoza. Tulimpelekea wahyi Musa tukamwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana na kila sehemu ikawa kama milima mkubwa.

Musa aliwaambia watu wake kuwa msimuogope Firauni na nguvu zake. Hakika Mwenyezi Mungu ana nguvu zaidi na yuko pamoja nami, nanyi mtaona.

Hakumaliza maneno yake, mara Mwenyezi Mungu akamwamrisha kupiga bahari kwa fimbo yake. Alipoipiga ikapasuka njia kumi na mbili kulingana na koo za waisrail. Maji yakainuka baina ya njia moja na nyingine kama mlima. Musa na watu wake wakavuka hadi ng’ambo ya pili.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:77).

Na tukawajongeza hapo wale wengine. Na tukamwokoa Musa na waliokuwa pamoja naye wote. Kisha tukawazamisha hao wengine.

Makusudio ya wengine ni kundi la Firauni. Maana ni kuwa baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwavusha wana wa Israil upande wa pili na wakawa wameokoka, kundi la Firauni nalo liliwasili. Wakaona muuujiza mkubwa – maji ya bahari yamesimama kama jabali na kutengeneza njia. Firauni akawaambia watu wake: Tazameni bahari ilivyoitikia matakwa yangu na kunifungulia njia ya kuwafuata walionitoroka.

Kisha wakajitoma na wakaenda kwa amani na utulivu. Hawakufika katikati, bahari ikawafunika wote, baada ya kuhadharishwa na kupewa muda mrefu, lakini walizama kwenye upotevu wao.

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara ya muujiza, mazingatio na mawaidha, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Wengi wao hapa wanakusudiwa wana wa Israil waliookolewa na Mwenyezi Mungu mikononi mwa Firauni, kwa kuchukilia dhahiri ya mfumo wa maneno ulivyo.

Na wala sio walioangamia, kama wasemavyo baadhi ya wafasiri. Dalili ya kuwa makusudio ni wana wa Israil ni kuwa wafuasi wa Firauni wote wlikuwa makafiri, bila ya kubaki; hasa wale aliokuwa nao. Na wana wa Israili, walipookolewa na Mungu kutoka kwa Firauni, walimwambia Musa: Tunataka sanamu tuliabudu badala ya Mwenyezi Mungu:

وَجَاوَزْنَا بِبَنِي إِسْرَائِيلَ الْبَحْرَ فَأَتَوْا عَلَىٰ قَوْمٍ يَعْكُفُونَ عَلَىٰ أَصْنَامٍ لَّهُمْ قَالُوا يَا مُوسَى اجْعَل لَّنَا إِلَـٰهًا كَمَا لَهُمْ آلِهَةٌ ﴿١٣٨﴾

“Na tukawavusha bahari wana wa Israil na wakawafikia waliokuwa wakiyaabudu masanamu yao; wakasema: Ewe Musa! Hebu nasi tufanyie waungu kama hawa walivyo na waungu.” Juz. 9 (7:138).

Kwa hiyo maana yanakuwa kwamba Waisraili walishuhudia muujiza wa kupasuka bahari na miujiza mingineyo, lakini bado waliendelea kung’ang’ania ukafiri wao na jeuri yao.

وَاتْلُ عَلَيْهِمْ نَبَأَ إِبْرَاهِيمَ ﴿٦٩﴾

69. Na wasomee habari za Ibrahim.

إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَا تَعْبُدُونَ ﴿٧٠﴾

70. Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

قَالُوا نَعْبُدُ أَصْنَامًا فَنَظَلُّ لَهَا عَاكِفِينَ ﴿٧١﴾

71. Wakasema: Tunaabudu masanamu nasi tutaendelea kuyanyenyekea.

قَالَ هَلْ يَسْمَعُونَكُمْ إِذْ تَدْعُونَ ﴿٧٢﴾

72. Akasema: Je yanawasikia mnapoyaita?

أَوْ يَنفَعُونَكُمْ أَوْ يَضُرُّونَ ﴿٧٣﴾

73. Au yanawafaa au yanawadhuru?

قَالُوا بَلْ وَجَدْنَا آبَاءَنَا كَذَٰلِكَ يَفْعَلُونَ ﴿٧٤﴾

Wakasema: Bali tumewakuta mababa zetu wakifanya hivyo hivyo.

قَالَ أَفَرَأَيْتُم مَّا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ ﴿٧٥﴾

75. Akasema: Je, mmewaona mnaowaabudu?

أَنتُمْ وَآبَاؤُكُمُ الْأَقْدَمُونَ ﴿٧٦﴾

76. Nyinyi na baba zenu wa zamani?

فَإِنَّهُمْ عَدُوٌّ لِّي إِلَّا رَبَّ الْعَالَمِينَ ﴿٧٧﴾

77. Hakika hao ni maadui zangu isipokuwa Mola wa walimwengu wote.

الَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهْدِينِ ﴿٧٨﴾

78. Ambaye ameniumba naye ananiongoza.

وَالَّذِي هُوَ يُطْعِمُنِي وَيَسْقِينِ ﴿٧٩﴾

79. Na ambaye ananilisha na kuninywesha.

وَإِذَا مَرِضْتُ فَهُوَ يَشْفِينِ ﴿٨٠﴾

80. Na ninapougua basi yeye ananiponya.

وَالَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحْيِينِ ﴿٨١﴾

81. Na ambaye atanifisha kisha atanihuisha.

وَالَّذِي أَطْمَعُ أَن يَغْفِرَ لِي خَطِيئَتِي يَوْمَ الدِّينِ ﴿٨٢﴾

82. Na ambaye ndiye ninayemtumai kunighufuria makosa yangu siku ya malipo.

رَبِّ هَبْ لِي حُكْمًا وَأَلْحِقْنِي بِالصَّالِحِينَ ﴿٨٣﴾

83. Mola wangu! Nitunukie hukumu na uniunganishe na wema.

وَاجْعَل لِّي لِسَانَ صِدْقٍ فِي الْآخِرِينَ ﴿٨٤﴾

84. Na unijaalie kutajwa kwa wema na wengine.

وَاجْعَلْنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ النَّعِيمِ ﴿٨٥﴾

85. Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

وَاغْفِرْ لِأَبِي إِنَّهُ كَانَ مِنَ الضَّالِّينَ ﴿٨٦﴾

86. Na umghufirie baba yangu, kwani alikuwa miongoni mwa wapotevu.

وَلَا تُخْزِنِي يَوْمَ يُبْعَثُونَ ﴿٨٧﴾

87. Wala usinihizi siku watakapofufuliwa.

يَوْمَ لَا يَنفَعُ مَالٌ وَلَا بَنُونَ ﴿٨٨﴾

88. Siku ambayo haitafaa mali wala wana.

إِلَّا مَنْ أَتَى اللَّـهَ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ﴿٨٩﴾

89. Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo uliosalimika.

IBRAHIM

Aya 69 – 89

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekitaja kisa cha Ibrahim kwa kukigawa kulingana na mnasaba ulivyo.

Katika Aya hizi Mwenyezi Mungu (s.w.t) amerudia majibizano baina ya Ibrahim na watu wake, kwa mfumo mwingine unaotofautiana na ule ulio katika Juz. 17 (21:51).

Na wasomee habari za Ibrahim.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kuwa awasomee makuraishi ambao wanadai kuwa ni kizazi cha Ibrahim na wako kwenye dini yake.

Alipomwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?

Katika Juz.7 (6:74) tumetaja tofauti za wafasiri kuhusu baba aliyeambiwa maneno haya na Ibrahim, kuwa je, ni baba yake hasa au ni baba wa kimajazi au ni ami yake?

Wakasema: Tunaabudu masanamu nasi tutaendelea kuyanyenyekea.

Tutadumu kuyaabudu na kuyatukuza. Kukubali kwao kuabudu masanamu kunajulisha kuwa neno sanamu halikuwa linamaanisha shutuma katika ufahamu wao, kama tunavyofahamu sisi; bali neno hilo lilikuwa likimaanisha utukufu na ukuu.

Akasema: Je yanawasikia mnapoyaita? Au yanawafaa au yanawadhuru?

Ni kawaida anayeabudiwa asikie, aone, adhuru na kunufaisha. Je, haya mnayoyaabudu yana sifa hizi? Swali hapa ni la kupinga.

Wakasema: Bali tumewakuta mababa zetu wakifanya hivyo hivyo.

Hii ni kukubali kuwa wao ni waigaji. Wala hilo si ajabu. Katika karne ya ishirini, zama za kutembea angani, tumeona wafuasi wakiwaiga viongozi wao na wakitoa dalili kwa kauli zao na kuzichukulia kuwa ni msingi, bila ya kuhakisha na kuchunguza.

Akasema: Je, mmewaona mnaowaabudu nyinyi na baba zenu wa zamani? Hakika hao ni maadui zangu isipokuwa Mola wa walimwengu wote.

Ikiwa nyinyi mnawaiga baba zenu, basi mimi simwigi yeyote na ninatangaza kujitenga kwangu na uadui wangu kwa hao waungu wenu; wala siabudu isipokuwa Mola wa walimwengu wote. Yeye ndiye walii wangu duniani na akhera. Yakiwa masanamu ni miungu, kama mnavyodai, basi na waniteremshie hasira zao, mimi napingana nao.

Ambaye ameniumba naye ananiongoza.

Mwenyezi Mungu amenipa akili nami naitumia kuniongoza kwenye haki. Ninaifuata na ninaitumia vizuri; wala simuigi yoyote; kama mnavyodai.

Na ambaye ananilisha na kuninywesha.

Kwa kuzifanya nyepesi sababu kwangu mimi na kwa viumbe vyake vyote.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameiumba ardhi hii na akaweka kila wanayoyahitajia na akasema: Yeye ndiye aliyeidhalisha ardhi kwa ajili yenu, basi tembeeni katika pande zake na kuleni katika riziki zake. Na kwake yeye ndio kufufuliwa.

Na ninapougua basi yeye ananiponya kutokana na madawa aliyoyaumba.

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema, “Hakika kila ugonjwa una dawa, dawa ikifika kwenye ugonjwa hupona kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.” Kuna Hadithi nyingine isemayo: Hakika Mwenyezi Mungu ameteremsha ugonjwa na dawa, basi fanyeni dawa wala msifanye dawa kwa haramu.

Na ambaye atanifisha kisha atanihuisha na ambaye ndiye ninayemtumai kunighufuria makosa yangu siku ya malipo.

Uhai, mauti na maghufira yako mikononi mwa Mwenyezi Mungu, hilo halina shaka. Na Ibrahim(a.s) ni mwenye kuhifadhiwa na makosa na hatia (maasumu). Katika isma ya kila maasumu ni kuikuza hofu yake kwa Mwenyezi Mungu.

Mola wangu! Nitunukie hukumu.

Makusudio ya hukumu hapa, sio utawala bali ni hekima na kukata hukumu:

وَآتَيْنَاهُ الْحِكْمَةَ وَفَصْلَ الْخِطَابِ ﴿٢٠﴾

“Na tukampa hekima na kukata hukumu.” (38:20).

Na uniunganishe na wema.

Unipe tawfiki ya kufuata nyao zao na kutenda matendo yao.

Na unijaalie kutajwa kwa wema na wengine.

Makusudio ya wengine ni umma utakaokuja baadaye. Maana ni nijaalie kutajwa kwa wema baina ya watu baada yangu. Mwenyezi Mungu aliitikia dua yake; ambapo dini zote za mbinguni zimeafikiana kumtukuza na kumwadhimisha Nabii Ibrahim(a.s) .

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema.

Ni nani anayestahiki hizo zaidi kuliko Ibrahim.

Na umghufirie baba yangu, kwani alikuwa miongoni mwa wapotevu.

Angalia tafsiri ya “Na haikuwa Ibrahim kumtakia msamaha baba yake ila ni kwa sababu ya ahadi aliyofanya naye, lakini ilipopambanukia kuwa yeye ni adui wa Mwenyezi Mungu, alijiepusha naye.” Juz. 11 (9:114).

Wala usinihizi siku watakapofufuliwa.

Dua hii ni katika aina ya dua za mitume na viongozi wema.Siku ambayo haitafaa mali wala wana. Isipokuwa mwenye kuja kwa Mwenyezi Mungu na moyo uliosalimika.

Kutokana na maafa ya ukafiri, unafiki, mifundo, ria na maafa mengineyo na maradhi.

Moyo ukiwa salama na uchafu, basi viungo vyote huwa salama: ulimi utasalimika na uwongo, kusengenya, kusikiliza upuzi na ubatilifu. Vile vile mkono unasalimika na kufanya haramu na tupu kutokana na zina na uovu.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TISA

وَأُزْلِفَتِ الْجَنَّةُ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٩٠﴾

90. Na Bustani (Pepo) itasogezwa kwa wenye takua.

وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِلْغَاوِينَ ﴿٩١﴾

91. Na Jahannam itadhihirishwa kwa wapotofu.

وَقِيلَ لَهُمْ أَيْنَ مَا كُنتُمْ تَعْبُدُونَ ﴿٩٢﴾

92. Na wataambiwa, wako wapi mliokuwa mkiwaabudu.

مِن دُونِ اللَّـهِ هَلْ يَنصُرُونَكُمْ أَوْ يَنتَصِرُونَ ﴿٩٣﴾

93. Badala ya Mwenyezi Mungu? Je, watawasaidia au kujisaidia wenyewe?

فَكُبْكِبُوا فِيهَا هُمْ وَالْغَاوُونَ ﴿٩٤﴾

94. Basi watavurumizwa humo wao na wapotofu.

وَجُنُودُ إِبْلِيسَ أَجْمَعُونَ ﴿٩٥﴾

95. Na majeshi ya Ibilisi yote.

قَالُوا وَهُمْ فِيهَا يَخْتَصِمُونَ ﴿٩٦﴾

96. Watasema na hali ya kuwa wanazozana humo:

تَاللَّـهِ إِن كُنَّا لَفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٩٧﴾

97. Wallah! Hakika tulikuwa katika upotevu ulio wazi.

إِذْ نُسَوِّيكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٩٨﴾

98. Tulipowafanya sawa na Mola wa walimwengu wote.

وَمَا أَضَلَّنَا إِلَّا الْمُجْرِمُونَ ﴿٩٩﴾

99. Na hawakutupoteza ila wakosefu.

فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ ﴿١٠٠﴾

100. Basi hatuna waombezi.

وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ ﴿١٠١﴾

101. Wala rafiki wa dhati.

فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٠٢﴾

102. Laiti tungepata kurejea tena tungelikuwa katika waumi- ni.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٠٣﴾

103. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٠٤﴾

104. Na hakika Mola wako ndiye mwenye nguvu mwenye kurehemu.

PEPO KWA WENYE TAKUA NA MOTO KWA WAPOTEVU

Aya 90 – 104

MAANA

Na Bustani (Pepo) itasogezwa kwa wenye takua

Bila shaka iko karibu na mwenye kuongoka na akamcha Mungu na iko mbali na mwenye kupotea.

Na Jahannam itadhihirishwa kwa wapotofu.

Ataidhihirisha Mwenyezi Mungu kwa wale walioikana na kuikadhibisha.

Na wataambiwa wako wapi mliokuwa mkiwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu? Na mkiwatarajia kwa siku hii, huku mkisema kuwa mliwabudu ili wawakurubishe kwa Mwenyezi Mungu?

Je, watawasaidia au kujisaidia wenyewe?

Hakika wao hawawezi kuwasaidia wala kujisaidia wenyewe.

Basi watavurumizwa humo wao na wapotofu na majeshi ya Ibilisi yote.

Wao ni hao waungu wao na wapotofu ni wale walioabudu. Mwanajeshi wa Ibilisi ni kila mpotofu na mpotoshaji. Mwenyezi Mungu atawachanganya wote kisha awatupe kwenye shimo la Jahannam.

Watasema na hali ya kuwa wanazozana humo: Wallah! Hakika tulikuwa katika upotevu ulio wazi, tulipowafanya sawa na Mola wa walimwengu wote. Na hawakutupoteza ila wakosefu.

Wapotofu kesho watasema, baada ya kupitwa na wakati, kuwaambia waungu wao na mashetani wao, kwamba nyinyi ndio mliokuwa viongozi wetu wa upofu na upotevu, wakati tulipowaabudu na kuwafanya mko sawa na Mwenyezi Mungu. Na wakosefu ndio waliokuwa kikwazo, ambao ni viongozi wa manufaa na masilahi, asili ya ufisadi na balaa.

Basi hatuna waombezi wala rafiki wa dhati.

Kesho hakuna uombezi wala ugombezi. Hakuna kitakachomfaa mtu isipokuwa moyo ulio salama na amali njema. Na muovu ni yule asiyekuwa na mawili hayo.

Laiti tungepata kurejea tena tungelikuwa katika waumini.

Baada ya kukata tamaaa na kila kitu ndio wanatamani kurudi duniani ili waamiini na kutenda. Mwenyezi Mungu anasema:

وَلَوْ رُدُّوا لَعَادُوا لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿٢٨﴾

“Na kama wangelirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.” Juz. 7 (6:28)

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya sura hii.

كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٠٥﴾

105. Kaumu ya Nuh waliwakadhibisha mitume.

قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٠٦﴾

106. Alipowaambia ndugu yao Nuh: Je, hamna takua?

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٠٧﴾

107. Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٠٨﴾

108. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٠٩﴾

109. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١١٠﴾

110. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ ﴿١١١﴾

111. Wakasema: Je, tukuamini na hali wanaokufuata ni walio duni?

قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١١٢﴾

112. Akasema: Nayajuaje waliyokuwa wakiyafanya?

إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي لَوْ تَشْعُرُونَ ﴿١١٣﴾

113. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wangu. Lau mngelitambua.

وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١٤﴾

114. Wala mimi si mwenye kuwafukuza waumini.

إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿١١٥﴾

115. Sikuwa mimi ila ni muonyaji aliye dhahiri.

قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ ﴿١١٦﴾

116. Wakasema: Kama hutakoma ewe Nuh bila shaka utapigwa mawe.

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ ﴿١١٧﴾

117. Akasema: Mola wangu! Hakika kaumu yangu wamenikadhibisha.

فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١٨﴾

118. Basi amua baina yagu mimi na wao uamuzi. Na uniokoe na walio pamoja nami katika waumini.

فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ﴿١١٩﴾

119. Basi tukamuokoa na walio pamoja naye katika jahazi iliyosheheni.

ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ ﴿١٢٠﴾

120. Kisha tukawagharikisha baadaye waliobaki.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٢١﴾

121. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٢٢﴾

122. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

NUH

Aya 105 – 122

MAANA

Kaumu ya Nuh waliwakadhibisha mitume.

Mtume aliyetumwa kwao ni mmoja ambaye ni Nuh, lakini mwenye kumkadhibisha Mtume mmoja ni kama amewakadhibisha mitume wote, kwa vile aliyewatuma ni mmoja na ujumbe ni mmoja.

Alipowaambia ndugu yao Nuh: Je, hamna takua?

Mwenye kuishika takua atakuwa katika amani na atasalimika na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake.

Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

Alijisifu kwa uaminifu ambao waliujua kwake akiwa mdogo na mtu mzima; sawa na makuraishi walivyomjua Muhammad(s.a.w.w) kwa ukweli na uaminifu katika hali zake zote.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii. Kwa sababu ninawaita kwenye lile ambalo lina kheri yenu ya dunia na akhera.

Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:90) na Juz. 12 (11:29).

Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

Hakuna sababu ya kukaririka jambo la takua (kumcha Mungu) isipokuwa ni jambo muhimu na la msingi.

Wakasema: Je, tukuamini na hali wanaokufuata ni walio duni.

Walimtia ila Nuh, si kwa lolote ila ni kwa kuwa mafukara walimwamini na kwao, hawana thamani. Kwa hiyo utume wa Nuh hauna thamani. Kwa maneno mengine ni kuwa wapenda anasa hawaoni kuwa ufukara ni maisha. Vipi wataamini waliloliamini mafukara? Hivi ndivyo wafanyavyo wapenda anasa; wanakuwa vipofu wa haki na wanakuwa na kiburi.

Akasema: Nayajuaje waliyokuwa wakiyafanya? Hisabu yao haiko ila kwa Mola wangu.

Nuh aliwaambia wale waliomjadili kuhusu ufukara, kuwa thamani ya mtu ni matendo yake na malengo yake, sio kwa cheo na mali. Na mimi sijui kuwa wao walimfanyia ubaya mtu yoyote kwa kauli au vitendo. Siri iko kwa Mwenyezi Mungu. Yeye peke yake ndiye anayejua na kuhisabu.

Lau mngelitambua kwamba thamani ya mtu ni kwa matendo sio kwa mali na dhahiri ni ya watu na batini ni ya Mwenyezi Mungu.

Wala mimi si mwenye kuwafukuza waumini. Sikuwa mimi ila ni muonyaji aliye dhahiri.

Umetangulia mfano wake katika Juz. Juz. 12 (11: 29).

Wakasema: Kama hutakoma ewe Nuh bila shaka utapigwa mawe.

Wameshindwa kuijadili haki wakakimbilia vitisho na mabavu. Hii ndio tabia ya wasiofuta haki, kila mahali na kila wakati.

Akasema: Mola wangu! Hakika kaumu yangu wamenikadhibisha. Basi amua baina yagu mimi na wao uamuzi.

Walipompa vitisho vya kutumia nguvu, alimuomba msaada Mwenyezi Mungu na nguvu zake. Na kwa unyenyekevu akamuomba Mwenyezi Mungu ahukumu, baina yake na yao, hukumu itakayomnusuru mwenye haki na kumwadhibu mwenye batili.

Na uniokoe na walio pamoja nami katika waumini pale itakapowashukia adhabu makafiri.

Basi tukamuokoa na walio pamoja naye katika jahazi iliyosheheni walioamini katika watu wake na wengineo na viumbe wengine wa kiume na wa kike. Kisha tukawagharikisha baadaye waliobaki.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:64) na Juz. 12 (11:40).

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini . Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu. Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya Sura hii.

كَذَّبَتْ عَادٌ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٢٣﴾

123. A’d waliwakadhibisha mitume.

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٢٤﴾

124. Alipowaambia ndugu yao Hud: Je, hamna takua?

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٢٥﴾

125. Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٢٦﴾

126. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٢٧﴾

127. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ ﴿١٢٨﴾

128. Je, mnajenga juu ya kila muinuko ishara ya kufanyia upuuzi?

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ ﴿١٢٩﴾

129. Na mnajenga ngome ili mkae milele.

وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ ﴿١٣٠﴾

130. Na mnaposhika kwa nguvu mnashika kwa nguvu kwa ujabari.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٣١﴾

131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

وَاتَّقُوا الَّذِي أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ ﴿١٣٢﴾

132. Na mcheni ambaye amewapa mnayoyajua.

أَمَدَّكُم بِأَنْعَامٍ وَبَنِينَ ﴿١٣٣﴾

133. Amewapa wanyama na watoto wa kiume.

وَجَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿١٣٤﴾

134. Na mabustani na chemchemi.

إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٣٥﴾

135. Hakika ninawahofia adhabu ya siku kubwa.

قَالُوا سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ الْوَاعِظِينَ ﴿١٣٦﴾

136. Wakasema: Ni mamoja kwetu ukitupa mawaidha au kutokuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

إِنْ هَـٰذَا إِلَّا خُلُقُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٣٧﴾

137. Haya si chochote ila ni hulka ya wa kale.

وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ﴿١٣٨﴾

138. Wala sisi hatutaadhibiwa.

فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَاهُمْ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٣٩﴾

139. Basi wakamkadhibisha na tukawahilikisha. Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini.

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٤٠﴾

140. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Hud

Aya 123 – 140

MAANA

Kisa cha Hud kimetangulia katika Juz. 8 (7:65 – 72) na Juz. 12 (11:50 – 60).

A’d waliwakadhibisha mitume. Alipowaambia ndugu yao Hud: Je, hamna takua? Hakika mimi kwenu ni Mtume mwaminifu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii. Na siwataki ujira juu yake, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.

Zimetangulia Aya kwa herufi zake katika sehemu iliyopita ya Sura hii Aya 105 – 110, bila ya mabadiliko yoyote isipokuwa jina tu. Kule imesemwa kaumu ya Nuh na hapa ni Hud na A’d.

Siri ya hilo ni kuwa risala ya mitume wote ni moja, ikilingania kwenye umoja wa Mwenyezi Mungu na kutii amri yake na makatazo yake.

Je, mnajenga juu ya kila muinuko ishara ya kufanyia upuuzi?

Makusudio ya ishara hapa ni jengo. Kila jengo linalotekeleza haja ya maisha hilo ni la kheri na ni katika dini. Kwa sababu dini ya Mwenyezi Mungu ni dini ya maisha. Ama jengo lisilokuwa na faida zaidi ya kujionyesha na kujifaharisha, hilo ni shari kidini na kiakili. Aina hii ndio inayokusudiwa hapa kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu ‘ya kufanyia upuuzi’ kwa sababu upuuzi ni ule usiohitajika.

Na mnajenga ngome ili mkae milele.

Makusudio ya ngome hapa ni jengo lisilokuwa na manufaaa yoyote.

Na mnaposhika kwa nguvu mnashika kwa nguvu kwa ujabari. Basi mcheni Mwenyezi Mungu na mnitii.

Kutumia nguvu kwa ujabari ni kudhulumu kwa hali ya juu, na inakuwa kubwa dhulma kwa kumdhulumu mnyonge. Lililothibiti katika dini ya Mwenyezi Mungu ni kuwa dhulma ni miogoni mwa madhambi makubwa; bali ni sawa na kumkufuru Mungu.

Tumelithibitisha hilo huko nyuma kwa nukuu ya Qur’an.

Aya hii ilishuka wakati ambao hakukuwa na silaha za maangamizi wala hakukuwa na matajiri wanaotoa mamilioni ya pesa ili waangamizwe wanawake kwa ujumla. Ilishuka wakati ambao kutumia nguvu kulikuwa ni kwa kutumia mkono zaidi - upanga mshale na mkuki.

Ikiwa Mwenyezi Mungu amesifu kuwa ni ubaya na uovu mkubwa kutumia nguvu kwa kiganja cha mkono, basi atawalipa nini wale wanaowanyeshea wanyonge mvua ya makombora, mabomu ya sumu na silaha za nuklia? Au wale ambao wameijaza ardhi na anga kwa vikosi vya majeshi. Wameijaza maroketi ya kijeshi; si kwa lolote ila wanataka kuhukumu roho za waja na nyenzo za nchi kulingana na hawa zao na masilahi yao tu.

Na mcheni ambaye amewapa mnayoyajua. Amewapa wanyama na watoto wa kiume na mabustani na chemchemi. Hakika ninawahofia adhabu ya siku kubwa.

Hud aliwalingania kwenye twaa ya Mwenyezi Mungu na akawakumbusha neema yake juu yao na anavyowapa muda na pia akawahadharisha na mwisho mbaya wa dhulma. Lakini hilo halikuwazidisha kitu isipokuwa kiburi nawakasema: Ni mamoja kwetu ukitupa mawaidha au kutokuwa miongoni mwa watoao mawaidha sisi hatutakuamini. Mawaidha yako hayatatuzidishia isipokuwa kuachana nawe.

Haya si chochote ila ni hulka ya wa kale wala sisi hatutaadhibiwa.

Haya ni ishara ya dini yao na masanamu yao wanayoyaabudu; na kwamba wao hawatayaacha kwa sababu wameyarithi kutoka jadi na jadi. Hiyo ndiyo hoja yao; hawana zaidi ya ‘tumewakuta nayo baba zetu na sisi tunafuata nyayo zao.’

Basi wakamkadhibisha na tukawahilikisha.

Hud aliwaonya watu wake kwa dalili na hoja, lakini hawakujali, wakawa miongoni mwa walioangamia.

Hakika bila shaka katika hayo ipo ishara, lakini wengi wao si wenye kuamini. Na hakika Mola wako ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

Imetangulia kwa herufi zake, katika Aya 67 na 68 ya Sura hii na pia sehemu iliyopita.


4

5

6