TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 14294
Pakua: 2499


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 25 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 14294 / Pakua: 2499
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

Mwandishi:
Swahili

18

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

أَلَمْ تَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ سَخَّرَ لَكُم مَّا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَأَسْبَغَ عَلَيْكُمْ نِعَمَهُ ظَاهِرَةً وَبَاطِنَةً وَمِنَ النَّاسِ مَن يُجَادِلُ فِي اللَّـهِ بِغَيْرِ عِلْمٍ وَلَا هُدًى وَلَا كِتَابٍ مُّنِيرٍ ﴿٢٠﴾

20. Je, hamuoni kwamba Mwenyezi Mungu amevifanya viwatumikie vilivyomo mbinguni na kwenye ardhi na akawakamilishia neema zake zilizo dhahiri na siri? Na katika watu wapo wanaojadiliana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu wala uongofu wala Kitabu chenye nuru.

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّبِعُوا مَا أَنزَلَ اللَّـهُ قَالُوا بَلْ نَتَّبِعُ مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءَنَا أَوَلَوْ كَانَ الشَّيْطَانُ يَدْعُوهُمْ إِلَىٰ عَذَابِ السَّعِيرِ ﴿٢١﴾

21. Na wanapoambiwa: Fuateni aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu; husema: ‘Bali tutafuata yale tuliyowakuta nayo baba zetu.’ Je, hata kama shetani anawaita kwenye adhabu ya moto?

وَمَن يُسْلِمْ وَجْهَهُ إِلَى اللَّـهِ وَهُوَ مُحْسِنٌ فَقَدِ اسْتَمْسَكَ بِالْعُرْوَةِ الْوُثْقَىٰ وَإِلَى اللَّـهِ عَاقِبَةُ الْأُمُورِ ﴿٢٢﴾

22. Na ausalimishaye uso wake kwa Mwenyezi Mungu naye akawa anafanya wema, basi huyo hakika amekwishakama- ta kishikilio madhubuti. Na mwisho wa mambo yote ni wa Mwenyezi Mungu.

وَمَن كَفَرَ فَلَا يَحْزُنكَ كُفْرُهُ إِلَيْنَا مَرْجِعُهُمْ فَنُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٢٣﴾

23. Na mwenye kukufuru, isikuhuzunishe kufuru yake. Marejeo yao ni kwetu, ndipo tutawaambia yale waliyoyafanya. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

نُمَتِّعُهُمْ قَلِيلًا ثُمَّ نَضْطَرُّهُمْ إِلَىٰ عَذَابٍ غَلِيظٍ ﴿٢٤﴾

24. Tunawastarehesha kwa uchache kisha tutawasukuma kwenye adhabu ngumu.

وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ اللَّـهُ قُلِ الْحَمْدُ لِلَّـهِ بَلْ أَكْثَرُهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٥﴾

25. Na ukiwauliza ni nani aliyeumba mbingu na ardhi na akalitiisha jua na mwezi, bila shaka watasema ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdulillah (sifa njema ni za Mwenyezi Mungu) Bali wengi wao hawafahamu.

لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ ﴿٢٦﴾

26. Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na ardhini. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye mkwasi, Msifiwa.

وَلَوْ أَنَّمَا فِي الْأَرْضِ مِن شَجَرَةٍ أَقْلَامٌ وَالْبَحْرُ يَمُدُّهُ مِن بَعْدِهِ سَبْعَةُ أَبْحُرٍ مَّا نَفِدَتْ كَلِمَاتُ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴿٢٧﴾

27. Na lau miti yote iliyomo ardhini ikawa ni kalamu na bahari na ikaongezewa bahari nyingine saba, (kuwa wino) maneno ya Mwenyezi Mungu yasingemalizika. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo, Mwenye hekima.

مَّا خَلْقُكُمْ وَلَا بَعْثُكُمْ إِلَّا كَنَفْسٍ وَاحِدَةٍ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ بَصِيرٌ ﴿٢٨﴾

28. Hakukuwa kuumbwa kwenu wala kufufuliwa kwenu ila ni kama nafsi moja tu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.

KISHIKILIO MADHUBUTI

Aya 20 – 28

MAANA

Je, hamuoni kwamba Mwenyezi Mungu amevifanya viwatumikie vilivyomo mbinguni na kwenye ardhi na akawakamilishia neema zake zilizo dhahiri na siri?

Neema za Mwenyezi Mungu ni nyingi sana; kama alivyozisifu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kauli yake: “Na mkihisabu neema za Mwenyezi Mungu hamuwezi kuzidhibiti.” Juz. 13 (14:34).

Ni nani atakayeweza kudhibiti na kuyajua yaliyo katika mbingu na ardhi zaidi ya aliyeumba hiyo mbingu na ardhi? Wafasiri wametoa mfano wa neema ya dhahiri kuwa ni zile zinazohisiwa na hisia tano na neema za siri kuwa ni nguvu za nafsi na utashi wake. Mulla Sadra anasema katika Juz. 3 ya kitabu chake Al-asfar:

“Watu walio bora wanashindwa kujua mambo ya mbingu na ya ardhi na hawajui hekima yake; bali wengi hawajui hakika ya nafsi ambayo ndiyo mtu mwenyewe. Mambo wanayohusiana nayo yaliyofichika ni mengi zaidi ya yaliyo dhahiri. Ikiwa mtu hajui nafsi yake na mwili wake, vipi ataweza kujua mwili na roho. Nasi, kwa kushindwa huku, hatuna ila kutaamali na kufikiria maajabu ya uumbaji na maumbile ya kushangaza.”

Na katika watu wapo wanaojadiliana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu wala uongofu wala Kitabu chenye nuru.

Aya hii, pamoja na ufupi wake, imekusanya sababu tatu za maarifa: Kwanza ni hisia na majaribio yaliyoashiriwa na neno ‘ilimu.’ Pili, ni akili ilyokusudiwa kwenye neno uwongofu. Tatu ni wahyi ulioletewa ibara ya Kitabu chenye nuru.

Aya hii Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 17 (22:8).

Na wanapoambiwa: Fuateni aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu; husema: Bali tutafuata yale tuliyowakuta nayo baba zetu.’ Je, hata kama shetani anawaita kwenye adhabu ya moto?

Umetangulia mfano wake katika Juz. 2 (2:170).

NI NANI MWENYE KUSHIKILIA KISHIKILIO MADHUBUTI?

Na ausalimishaye uso wake kwa Mwenyezi Mungu naye akawa anafanya wema, basi huyo hakika amekwishakamata kishikilio madhubuti. Na mwisho wa mambo yote ni wa Mwenyezi Mungu.

Kishikilio madhubuti ni kinaya cha Qur’an, kamba ya Mungu ni radhi zake na mengineyo anayosalimika nayo mtu na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake. Kila mwenye kusifika na sifa mbili basi atakuwa ameshikilia mpini ulio imara:

Kwanza : ni kumwamini Mwenyezi Mungu kwa kufanya aliyoyaamrisha katika ibada; kama vile Swaumu na Swala. na kuacha aliyoyakataza; kama vile zina, uwongo na pombe.

Pili : ni kuwa mwema. Mwema ni yule ambaye wema wake unaenea kwa wengine wala hajifanyii yeye pekee na watu wake tu. Anashirikiana na watu katika machungu yao anatenda kwa ajili ya kuwakomboa wanaodhulumiwa na kukandamizwa na kwa ajili ya haki na uadilifu popote ulipo na utakapokuwa. Kwa ufupi ni kuwa wema ni sawa na maji twahara; hayo yenyewe ni twahara na yanatwaharisha kingine.

Kwa hiyo basi inatubainikia kuwa watakaosalimika na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake ni wale waumini wanaofanya wema. Ama mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu na akamwabudu wala asi- wafanyie wema wengine kwa kusaidiana nao kwenye manufaa ya wote au akafanya wema na asimwamini Mwenyezi Mungu, wote hawa wawili hawana amani ya adhabu ya Mwenyezi Mungu na ghadhabu yake. Kwa sababu watakuwa hawakukamata kishikilio madhubuti.

Kuna Hadith nyingi zinazohusiana na maudhui hii; miongoni mwazo ni hizi zifuatazo:

“Asiyetilia umuhimu mambo ya waislamu basi yeye si mwislamu.”

“Imani ya mja haiwi kweli mpaka ampendelee ndugu yake lile analojipendelea yeye mwenyewe.”

“Mtu anayependeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu ni yule anayewafaa zaidi watu.”

Kauli yake Mtume mtukufu(s.a.w.w) :“Hakika nimetumwa kukamilisha maadili mema,” ni ushahidi tosha kuwa risala ya uislamu ni risala ya kiutu. Ndio maana baadhi ya wajuzi wakamwelezea mwislamu kuwa ni ‘Mtu ambaye manufaa yake yanaenea kwa jamii ya uma wake wote na sio mtu finyu wa manufaa ya nafsi yake.”

Na mwenye kukufuru, isikuhuzunishe kufuru yake. Marejeo yao ni kwetu, ndipo tutawaambia yale waliyoyafanya. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

Unahuzunikia nini na kupata uchungu kwa sababu ya kufuru ya anayekufuru ewe Muhammad! Wewe umekwishafikisha na ukatekeleza risala kwa ukamilifu. Achana nao hao wakosefu na dunia yao. Sisi tunawajua zaidi na marejeo yao na hisabu yao ni kwetu.

Tunawastarehesha kwa uchache kisha tutawasukuma kwenye adhabu ngumu.

Hizo ni siku chache tu wanacheza nazo na zinacheza nao, kisha iwazingire adhabu kali bila ya kujitambua.

Umetangulia mfano wake katika Aya nyingi; miongoni mwazo ni Juz. 4 (3:176).

Na ukiwauliza ni nani aliyeumba mbingu na ardhi na akalitiisha jua na mwezi, bila shaka watasema ni Mwenyezi Mungu. Sema: Alhamdulillah (sifa njema ni za Mwenyezi Mungu). Bali wengi wao hawafahamu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (23:84) na katika Juzuu hii tuliyo nayo (29: 61).

Ni vya Mwenyezi Mungu vilivyomo mbinguni na ardhini. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mkwasi, Msifiwa.

Sifa njema na ufalme ni wake peke yake, wala hakuna Mkwasi ila yule anayetosheka naye

Na lau miti yote iliyomo ardhini ikawa ni kalamu na bahari na ikaongezewa bahari nyingine saba, (kuwa wino) maneno ya Mwenyezi Mungu yasingemalizika. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye uwezo Mwenye hekima.

Bahari saba ni kinaya cha wingi. Makusudio ya maneno ya Mwenyezi Mungu ni uweza wake wa kuvileta vyote vilivyoko wakati wowote anaotaka.

Maana ni kuwa lau tungelikadiria bahari kuwa ni wino na miti ikawa ni kalamu za kuandikia uweza wa Mwenyezi Mungu basi wino na kalamu zingelikwisha na uweza wa Mwenyezi Mungu ungelibakia bila ya kuwa na kikomo.

Kwa manenno mengine ni kuwa uweza wa Mwenyezi Mungu hauna mpaka. Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (18:109).

Ibn Al-arabi anasema katika Futahatil – Makkiyya: “Bahari na Miti ni katika jumla ya maneno ya Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo kama bahari ni wino isingeweza kujiandika isipokuwa hiyo yenyewe tu. Kalamu na mengineyo yangelibakia bila ya kitu cha kuandikia. Hii ni kwa vile amabavyo tayari viko. Je, kwa vile ambavyo haviko lakini vinawezekana kuwako?”

Anakusudia kuwa lau bahari ingelikuwa wino na tukataka kuandika maajabu na siri za bahari tu basi wino ungelikwisha. Ikiwa wino umekwisha kalamu hazitaweza kuandika tena siri na maajbu ya vitu vilivyobaki, zikiwemo hizo kalamu zenyewe.

Na hii ni kwa vile vitu ambavyo tayari vipo. Je, vile amabavyo havipo vinavyopatikana kwa neno ‘kuwa’ wakati wowote anaotaka?

Hakukuwa kuumbwa kwenu wala kufufuliwa kwenu ila ni kama nafsi moja tu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona.

Asiyekuwa Mwenyezi Mungu anaweza baadhi ya vitu na vingine vinamshinda. Na vile anavyoviweza kuna vile visivyohitajia juhudi yoyote, kuna vinavyohitajia juhudi kidogo na vile vinavyohitajia juhudi kubwa.

Lakini Mwenyezi Mungu ni muweza wa kila kitu na kila kitu kwake ni sawa, kiwe kidogo au kikubwa. Kwa hiyo kwake yeye kumuumba mtu mmoja ni sawa na kuumba watu wote. Vile vile kuwafufua na hisabu yao.

Imam Ali(a.s) anasema:“Hakuna kitu kilichoanza kuumbwa kwake ila ni kwa uweza wake aliye mmoja mwenye kushinda nguvu zote ambaye kwake ni marejeo ya mambo yote. Bila ya kukizuia kingelikwisha. Hachoki kukitengenza kitu chochote anapokitengeneza. Wala haoni uzito wa kuumba anachokiumba baada ya kutokuweko.”

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى وَأَنَّ اللَّـهَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٢٩﴾

29. Je, huoni kwamba huuingiza usiku katika mchana na huuingiza mchana katika usiku. Na amelitiisha jua na mwezi, vyote hupita mpaka wakati uliowekwa. Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyafanya.

ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّـهَ هُوَ الْحَقُّ وَأَنَّ مَا يَدْعُونَ مِن دُونِهِ الْبَاطِلُ وَأَنَّ اللَّـهَ هُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٣٠﴾

30. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye wa kweli, na kwamba wale wanaowaomba badala yake ni batili, na hakika Mwenyzi Mungu ndiye aliye juu, Mkubwa.

أَلَمْ تَرَ أَنَّ الْفُلْكَ تَجْرِي فِي الْبَحْرِ بِنِعْمَتِ اللَّـهِ لِيُرِيَكُم مِّنْ آيَاتِهِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ ﴿٣١﴾

31. Je, huoni kwamba majahazi hupita baharini kwa neema za Mwenyezi Mungu, ili awaonyeshe ishara zake. Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mwenye subira nyingi, mwenye shukrani.

وَإِذَا غَشِيَهُم مَّوْجٌ كَالظُّلَلِ دَعَوُا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ فَلَمَّا نَجَّاهُمْ إِلَى الْبَرِّ فَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ وَمَا يَجْحَدُ بِآيَاتِنَا إِلَّا كُلُّ خَتَّارٍ كَفُورٍ ﴿٣٢﴾

32. Na wimbi linapowafunika kama vivuli, humuomba Mwenyezi Mungu kwa kumsafia dini. Lakini anapowaokoa wakafika nchi kavu, wapo baadhi yao huenda mwendo wa wastani. Wala hazikanushi ishara zetu ila kila mhaini mkuu, kafiri mkubwa.

HUUINGIZA USIKU KATIKA MCHANA

Aya 29 - 32

MAANA

Je, huoni kwamba huuingiza usiku katika mchana na huuingiza mchana katika usiku.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (3:26) na Juz. 17 (22:61).

Na amelitiisha jua na mwezi, vyote hupita mpaka wakati uliowekwa. Na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyafanya.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (13:2).

Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye wa kweli, na kwamba wale wanaowaomba badala yake ni batili, na hakika Mwenyzi Mungu ndiye aliye juu, Mkubwa.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 17 (22:62).

Je, huoni kwamba majahazi hupita baharini kwa neema za Mwenyezi Mungu, ili awaonyeshe ishara zake.

Miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu ni kusahilisha mawasiliano. Miongoni mwa mawasiliano hayo ni majahazi ambayo yanahitajia maji, upepo na mbingu. Sababu hizi zote zunaishia kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mwenye subira nyingi mwenye shukrani, anayevumilia machungu na kuchunguza ishara za Mwenyezi Mungu katika maumbile yake na kushukuru Mungu wake.

Na wimbi linapowafunika kama vivuli, humuomba Mwenyezi Mungu kwa kumsafia dini. Lakini anapowaokoa wakafika nchi kavu, wapo baadhi yao huenda mwendo wa wastani. Wala hazikanushi ishara zetu ila kila mhaini mkuu, kafiri mkubwa.

Baadhi ya wafasiri wamesema makusudio ya mwenye kwenda mwendo wa wastani hapa ni mwenye kuficha ukafiri wake. Razi akasema ni kafiri wa wastani. Lakini usawa hasa ni yule ambaye hakuidhulumu nafsi yake kwa kuipeleka kwenye hasira za Mwenyezi Mungu na adhabu wala hakuwa ni katika waliotangulia kwenye heri:

فَمِنْهُمْ ظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ وَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ وَمِنْهُمْ سَابِقٌ بِالْخَيْرَاتِ بِإِذْنِ اللَّـهِ ﴿٣٢﴾

“Kati yao yupo aliyejidhulumu nafsi yake na yupo wa wastani na yupo aliyetangulia katika mambo ya kheri” (35:32).

Makusudio ya mhaini mkuu hapa ni yule anayevunja ahadi ya umbile aliloumbiwa nalo kila mwenye kuzaliwa.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11(10:22-23) na Juzuu hii tuliyo nayo (29:65-66)

يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمْ وَاخْشَوْا يَوْمًا لَّا يَجْزِي وَالِدٌ عَن وَلَدِهِ وَلَا مَوْلُودٌ هُوَ جَازٍ عَن وَالِدِهِ شَيْئًا إِنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ الْحَيَاةُ الدُّنْيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِاللَّـهِ الْغَرُورُ ﴿٣٣﴾

33. Enyi watu! Mcheni Mola wenu na iogopeni siku ambayo mzazi hatamfaa mwanawe wala mwana hatamfaa mzaziwe kwa lolote. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Basi yasiwadanganye maisha ya dunia wala asiwadanganye na Mwenyezi Mungu mdanganyifu.

إِنَّ اللَّـهَ عِندَهُ عِلْمُ السَّاعَةِ وَيُنَزِّلُ الْغَيْثَ وَيَعْلَمُ مَا فِي الْأَرْحَامِ وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿٣٤﴾

34. Hakika ujuzi wa Saa uko kwa Mwenyezi Mungu na huiteremsha mvua na anavijua vilivyo ndani ya matumbo ya uzazi. Na haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho, wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, mwenye habari.

UJUZI WA SAA UKO KWA MWENYEZI MUNGU

Aya 33 – 34

MAANA

Enyi watu! Mcheni Mola wenu na iogopeni siku ambayo mzazi hatamfaa mwanawe wala mwana hatamfaa mzaziwe kwa lolote. Hakika ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Basi yasiwadanganye maisha ya dunia wala asiwadanganye na Mwenyezi Mungu mdanganyifu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameamrisha takua kwa sababu ni njia ya kuokoka na siku ambayo mtu atawakimbia wanawe na mama yake na baba yake. Siku hii itakuja bila ya shaka yoyote. Mwenye kuhadaika ni yule anayeghurika na mambo ya batili na uwongo.

KWA NINI MUNGU AKAMUUMBA MTU?

Nilisoma mwandishi mmoja akisema: “Miongoni mwa maswali ambayo hayana majibu ni swali hili: Kwa nini Mungu amemuumba mtu?”

Bila shaka kila mmoja anatamani lau angelijua jawabu la swali hili, kwa sababu linafungamana na kuweko mtu na hakika yake moja kwa moja. Sio siri kwamba mimi nimesoma majibu mengi sana ya swali hili kutoka kwa wataalamu, wanafalsafa na wengineo katika waliopita na wa sasa, lakini sikukinai kabisa; igawaje mimi nilipoulizwa swali hili mara nyingi nilijibu kama walivyojibu, kwa vile sina jibu jingine zaidi ya hayo waliyoyasema.

Nilipoingilia kufasiri Aya za Qur’an yenye hekima, nilisahau swali hili na sikuyahifadhi majibu ya wataalamu. Kwa sababu Tafsir Al-Kashif imeninyang’anya kila kitu; hata kumbukumbu yangu pia. Hakuna kitu isipokuwa busara inayoniongoza kwenye maana ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu na malengo yake na mfungamano wake na maisha.

Nilipoendela kidogo tu na tafsiri nilipata jawabu lilio wazi wazi, katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, lisilokubali shaka wala taawili. Si uzushi kwamba Muumba wa kitu ndiye anayejua zaidi analolitaka kwa alichokiumba.

Basi nikapata katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu Aya zinazofahamisha kwa uwazi kuwa mtu ameumbiwa akhera sio dunia ili akaishi maisha yasiyokuwa na tabu wala matatizo yoyote.

Lakini hekima ya Muumba imetaka kuwe na mfungamano baina ya maisha mema ya akhera aliyoumbiwa mtu na kuisadiki imani kwa haki na ikhlasi na kuihami; kama ambavyo hekima yake Mtukufu imetaka kuwa asiyeamini mfungamano huu au akauamini kinadhariya bila ya kuufanyia kazi, kuwa atahisabiwa hisabu nyepesi na ataadhibiwa adhabu chungu.

Kwa sababu yeye hakujua au alijitia kutojua lengo aliloumbiwa na akaiacha njia ya sawa kwa uchaguzi wake mbaya baada ya kuongozwa na Mwenyezi Mungu na kuamrishwa kuifuata.

Kwa maneno mengine ni kuwa, ilivyo hasa maisha ya mtu yanabaki kwa kubakia muumba wake na kwamba Yeye amemuweka kwenye nyumba ya dunia kwa muda tu, mpaka wakati maalum kisha agure kwenye nyumba ya kudumu. Naye amemwamrisha kuzishughulikia nyumba zote mbili pamoja, na afanye ihtiyat ya lile linalowezekana kumtokea katika nyumba ya kwanza na lile litakalotokea katika nyumba ya pili ambalo halina shaka.

Ikiwa atafuata amri na akatii basi atakuwa amejichagulia amani na kufaulu; sawa na msafiri mwenye maandalizi kamili ya safari yake. Na atakyepinga na kuasi basi atakuwa amejichagulia mwisho mbaya; sawa na anayesafiri mji wa mbali ugenini bila ya maandalizi yoyote. Tazama Juz. 20 (28:77).

Hebu sasa tutaje baadhi ya Aya zinazofahamisha kuwa lengo la kumbwa mtu ni maisha ya pili; kama ifuatavyo:

1. Kuna zile zinazoisifia dunia kuwa ni upuuzi, mchezo, starehe zinazodanganya na mahali pa kujifaharisha na kujigamba na kwamba dunia itaondoka na kuisha; na kuisifia akhera kuwa ni nyumba ya Mwenyezi Mungu, ya kheri, ya maisha na kuridhiwa.

Vipi Mwenyezi Mungu (s.w.t) amuumbe mtu na ampe siri, ugunduzi na uwezo wa kuleta maendeleo kuweza kuigeuza historia ya mtu, mbingu na ardhi kwa ajili ya mchezo na starehe zenye ghururi na maisha yanayofanana na ndoto; na hali Yeye amesema: “Hakika tumewatukuza wanaadamu.”?

Juz. 15 (17:70). Hakuna kitu kinachooafikiana na kutukuzwa watu na hekima ya Mungu isipokuwa maisha yatakayobakia kwa kubakia muumbaji wake.

2. Aya zinazofahamisha kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamjaribu na kumtahini mtu – pamoja na kuwa anamjua zaidi – ili ifichuke siri yake na hakika yake na vijitokeze vitendo vyake vitakavyomfanya astahiki thawabu au adhabu huko mwisho, akhera. Miongoni mwa Aya hizo ni: “Hakika tumevifanya vilivyo katika ardhi kuwa ni pambo lake ili tumjaribu ni nani kati yao mwenye vitendo vizuri zaidi” Juz. 15 (18:7)

وَمَا كَانَ لَهُ عَلَيْهِم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يُؤْمِنُ بِالْآخِرَةِ مِمَّنْ هُوَ مِنْهَا فِي شَكٍّ ﴿٢١﴾

“Naye – Iblisi – hakuwa na mamlaka juu yao ila ni kwa sababu ya (kuwajaribu) tumjue ni nani mwenye kuamini akhera na ni nani anayetilia shaka” (34:21).

3. Lengo sio kutangaza na kuweka wazi tu bali ni “ili awalipe waliotenda ubaya kwa waliyoyatenda na waliotenda mema awalipe kwa memea” (53:31).

Kwa vile malipo haya hayathibiti duniani, basi lazima kuweko na siku nyingine; vinginevyo itakuwa ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kukuza mambo tu. Mwenyezi Mungu ametakata na wayasemayo wajinga.

4. Aya zinazofahamisha kubakia Peponi kwa mwenye kuamini na kufanya wema na kubaki motoni mwenye kukufuru na kufanya uovu.

Unaweza kuuliza : Utaichukulia vipi kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu inayosema: “Sikuumba majini na watu ila waniabudu” (51:56); ambapo inafahamisha waziwazi kuwa lengo la kuumbwa mtu ni kumwabudu Mwenyezi Mungu katika maisha haya ya dunia na wala sio kupewa maisha bora akhera?

Jibu : Makusudio ya ibada hapa ni kila tendo linalomridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na kujikurubisha kwake. Hakuna mwenye shaka kwamba kumridhisha Mwenyezi Mungu ni njia pekee ya maisha mema ya kudumu. Kwa hiyo maana yanakuwa, sikuumba majini na watu ila wafanye matendo mema yatakayowasababishia kuishi maisha mema ya milele huko akhera. Kwa maneno mengine ni kuwa Aya hii inarudufu kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَقَضَىٰ رَبُّكَ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا إِيَّاهُ ﴿٢٣﴾

“Na Mola wako amepitisha kuwa msimwabudu yoyote ila Yeye tu” Juz. 15 (17:23)

na pia kaulu Yake:

وَمَا أُمِرُوا إِلَّا لِيَعْبُدُوا اللَّـهَ مُخْلِصِينَ لَهُ الدِّينَ ﴿٥﴾

“Na hawakuamrishwa ila wamwabudu Mwenyezi Mungu kwa kumsafia dini” (98:5).

Na natija ya usafi wa dini ni maisha ya kudumu na pepo.

Zaidi ya hayo kuna Aya kadhaa amabazo zimeifunga pepo kwa kutenda matendo mema na ya kheri duniani na kuufunga moto na kufanya shari na ufisadi duniani.

Miongoni mwa Aya hizo ni: “Na aliyekuwa kipofu katika dunia hii, basi Akhera atakuwa kipofu na aliyepotea zaidi njia.” Juz. 15 (17:72).

“Je, mwadhani mtaingia Peponi na hali Mwenyezi Mungu hajawajua wale waliofanya jihadi miongoni mwenu na kuwajua wale waliofanya subira?” Juz. 4 (3:142). Makusudio ya jihadi hapa ni jihadi ya kuihami haki na watu wake na kufa shahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu na makusudio ya subira ni uthabiti dhidi ya wabatilifu na wapetuka mipaka; na wala sio subira ya kujisalimisha kwenye nguvu ya shari na uovu na kuwa dhalili na ufukara.

Baada ya kutubainikia kuwa lengo la kuumbwa mtu ni maisha yatakayobaki na kwamba kupata neema zake ni mpaka mtu afanye heri na wema hapa duniani; na kupata moto ni mpaka mtu afanye shari na ufisadi, tutakuwa tumejua kwamba tafsiri yoyote ya kuelezea lengo la kuumbwa mtu itakayokwenda kinyume na hakika hii basi hiyo itakuwa mbali na usawa na uhalisi wa mambo.

Inatosha kuwa ni dalili ya yote hayo kauli yake Mwenyezi Mungu: “Je, mnadhani kuwa tuliwaumba bure na kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?” Juz. 18 (23:115).

Yaani lau Mwenyezi Mungu asingelimuumba mtu kwa ajili ya akhera basi ingelikuwa Mwenyezi Mungu, ambaye imetukuka hekima yake, anafanya mambo bure tu.

UJUZI WA SAA, MVUA NA VILIVYO MATUMBONI

Hakika ujuzi wa saa uko kwa Mwenyezi Mungu na huiteremsha mvua na anavijua vilivyo ndani ya matumbo ya uzazi. Na haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho, wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, mwenye habari.

Unaweza kuuliza : Ujuzi wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hauna kikomo; kama alivyosema: “Hakifichikani kwake kilicho na uzito wa chembe katika mbingu wala aradhini” (34:3) Na akasema tena “Na ziko kwake funguo za ghaibu; hakuna azijuaye ila Yeye; anajua kilichomo nchi kavu na kilichomo baharini; na halianguki jani ila analijua wala punje katika giza la ardhi; wala kibichi au kikavu, ila kimo katika Kitabu kinachobainisha.” Juz. 7 (6:59).

Imam Ali(a.s) naye anasema:“Hakika Mwenyezi Mungu anajua kudondoka kwa tone na kutulia kwake, kusogea kwa chembe na kupita kwake na chakula kinachomtosha mbu.” Sasa kwanini Mwenyezi Mungu (s.w.t) akahusisha kutaja vitu hivi hapa?

Imesemekana kuwa muulizaji alimuuliza Mtume(s.a.w.w) : kuhusu vitu hivi ndipo ikashuka Aya. Razi anasema: Mwenyezi Mungu (s.w.t) alipotaja saa ya Kiyama alinasibisha kutaja vitu hivi.

Sisi tumesema mara nyingi kuwa Qur’an ni Kitabu cha uongofu kinampeleka mtu kwenye jambo moja hadi jingine. Imam Ja’far Sadiq(a.s) amesema:“Hakika Aya inakuwa mwanzo ni jambo jingine na mwisho wake ni jengine; ni maneno yanayoungana yakinyumbuka kwenye njia mabalimbali…” Kwa vyovyote iwavyo nikuwa Aya imekusanya mambo matano:

1.Hakika ujuzi wa Saa uko kwa Mwenyezi Mungu

“Hakuna wa kuidhihirisha kwa wakati wake ila yeye tu.” Juz. 9 (7:187). Hekima katika hilo ni kuwa watu wawe kwenye hadhari, wakitazamia kutokea wakati wowote.

2.Na huiteremsha mvua.

Wafasiri wengi wamesema kuwa makusudio ya kuteremsha mvua ni kuwa ujuzi wa kushuka kwake unahusika na Mwenyezi Mungu tu peke yake.

Usawa ni kulichukulia neno kuteremsha kama lilivyo; kuwa ujuzi wa kuiteremsha unahusika na Mwenyezi Mungu, kwa vile sababu za kushuka kwake zinakomea kwake.

Hii haimzui mtu kujua wakati wa kushuka mvua kutokana na dalili zake. Hata kama tukichukulia kuwa makusudio ya kujua ni kujua wakati wa kushuka kwake.

Kwa sababu mtu anajua wakati wa kushuka kwake baada ya kujitoikeza dalili na alama zake. Lakini hakuna ajuae kuwa dalili na alama hizo zitatokea lini isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Unaweza kuuliza : Wataalamu wanaweza kushusha mvua ya kutengenezwa, sasa itakuwaje kuwa anahusika nayo Mungu tu?

Jibu : Wataalamu wanageuza mawingu kuwa mvua na Mwenyezi Mungu ndiye aliyetengeneza mawingu kisha anayasukuma kutoka mji mmoja hadi mwingine anavyotaka. Tofauti ni kubwa baina ya kukifanya kitu na kukigeuza.

3.Na anavijua vilivyo ndani ya matumbo ya uzazi.

Unaweza kuuliza : Elimu ya kisasa inajua vilevile inajua aliyemo tumboni, kupitia vipimo kuwa ni mume au ni mke?

Jibu : Kipimo kinajua ambacho kimekwishakuwa, lakini hakijui sifa zake na utashi wa aliyemo tumboni; kama vile uzuri na ubaya, werevu na ujinga n.k. Lakini haya yote kwa Mwenyezi Mungu yanajulikana.

Imam Ali(a.s) anasema:“Mwenyezi Mungu (s.w.t) anajua kilicho katika matumbo ya uzazi kuwa kitakuwa mume au mke, mbaya au mzuri, mkarimu au bakhili, mwema au muovu na ambaye atakuwa kuni kwenye moto wa Jahannam au atakayekuwa Peponi pamoja na mitume.”

4.Na haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho kwa sababu kila siku ina mambo mengine.

Baada ya kupita siku nyingi imethibitika nadharia ya mwanafalsafa wa kigiriki, Heraclitus aliyesema: “Wewe huwezi kuingia mto mmoja mara mbili.” akiashiria kuwa mambo ya dhahiri ya kilimwengu na ya kijamii hubadilika mara kwa mara kutoka hali moja hadi nyingine. Kwa hiyo elimu haiwezi kujua litakalomtokea mtu baadaye.

5.Wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani wala wakati gani pia.

Kwa sababu mauti hayazuiliki, yanamchuka mtoto mchanga na kijana mwenye afya na kumwacha mgonjwa na kikongwe.