TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 14255
Pakua: 2444


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 25 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 14255 / Pakua: 2444
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

Mwandishi:
Swahili

19

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Sura Ya Thelathini Na Mbili: Surat As-Sajda. Ina Aya 30. Mwenye Majmaul-bayan anasema: Imeshuka Makka isipokuwa Aya tatu zimeshuka Madina; kuanzia 18 – 20.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

الم ﴿١﴾

1. Alif Laam Miim.

تَنزِيلُ الْكِتَابِ لَا رَيْبَ فِيهِ مِن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٢﴾

2. Ni uteremsho wa Kitabu kisicho na shaka ndani yake, kinachotoka kwa Mola wa walimwengu wote.

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ بَلْ هُوَ الْحَقُّ مِن رَّبِّكَ لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّا أَتَاهُم مِّن نَّذِيرٍ مِّن قَبْلِكَ لَعَلَّهُمْ يَهْتَدُونَ ﴿٣﴾

3. Au wanasema amekizua? Bali hicho ni haki itokayo kwa Mola wako, ili uwaonye watu wasiofikiwa na mwonyaji kabla yako, huenda wakaongoka.

اللَّـهُ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ ثُمَّ اسْتَوَىٰ عَلَى الْعَرْشِ مَا لَكُم مِّن دُونِهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا شَفِيعٍ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ ﴿٤﴾

4. Mwenyezi Mungu ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake katika siku sita. Kisha akatawala kwenye Arshi. Hamna walii wala mwombezi isipokuwa Yeye. Basi je hamkumbuki?

يُدَبِّرُ الْأَمْرَ مِنَ السَّمَاءِ إِلَى الْأَرْضِ ثُمَّ يَعْرُجُ إِلَيْهِ فِي يَوْمٍ كَانَ مِقْدَارُهُ أَلْفَ سَنَةٍ مِّمَّا تَعُدُّونَ ﴿٥﴾

5. Hulipanga jambo kutoka mbinguni hadi ardhini, kisha linapanda kwake katika siku ambayo kipimo chake ni miaka elfu kwa mnavyohisabu.

ذَٰلِكَ عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿٦﴾

6. Huyo ndiye Mjuzi wa mambo ya ghaibu na ya dhahiri, Mwenye uwezo, Mwenye kurehemu.

الَّذِي أَحْسَنَ كُلَّ شَيْءٍ خَلَقَهُ وَبَدَأَ خَلْقَ الْإِنسَانِ مِن طِينٍ ﴿٧﴾

7. Ambaye ametengenza vizuri umbo la kila kitu. Na akaanzisha umbo la mtu kwa udongo.

ثُمَّ جَعَلَ نَسْلَهُ مِن سُلَالَةٍ مِّن مَّاءٍ مَّهِينٍ ﴿٨﴾

8. Kisha akajaalia uzao wake utokane na kizazi cha maji hafifu.

ثُمَّ سَوَّاهُ وَنَفَخَ فِيهِ مِن رُّوحِهِ وَجَعَلَ لَكُمُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَالْأَفْئِدَةَ قَلِيلًا مَّا تَشْكُرُونَ ﴿٩﴾

9. Kisha akamlinganisha sawa na akampulizia roho yake. Na amewajaalia kusikia na kuona na nyoyo. Ni uchache mnavyoshukuru.

AMETENGENEZA VIZURI UMBO LA KILA KITU

Aya 1 – 9

MAANA

Alif Laam Miim.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1).

Ni uteremsho wa Kitabu kisicho na shaka ndani yake, kinachotoka kwa Mola wa walimwengu wote.

Ushahidi wa hilo tumeuleza kwenye Aya kadhaa; kama vile Juz. 1 ( 2:23 – 25), Juz. 5 (4:80 – 82) na Juz. 18 (24:55 – 57).

Au wanasema amekizua? Bali hicho ni haki itokayo kwa Mola wako, ili uwaonye watu wasiofikiwa na mwonyaji kabla yako, huenda wakaongoka.

Wapenda anasa wanaojitia kwenye upotevu, katika vigogo wa kikuraishi, walisema: “Qur’an ni utungo wa Muhammad.” Mwenyezi Mungu (s.w.t.) akasema, kuwarudi, kuwa hapana bali ni wahyi wa Mwenyezi Mungu na Muhammad amewajia na yale ambayo hajawaletea yeyote kabla yake wala hatawaletea yeyote baada yake.

Amewajia na kheri ya dunia na akhera akawakataza dhulma na ufisadi mlio nao, ili mpate mawaidha na muache kabla hayajawafikia majanga. Ilitakiwa mumshukuru Muhammad kwa fadhila hii badala ya kumpangia njama za kiuadui na kumfanya ni mwongo mzushi.

Mwenyezi Mungu ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake katika siku sita. Kisha akatawala kwenye arshi. Hamna walii wala mwombezi isipokuwa Yeye. Basi je hamkumbuki?

Siku sita ni kinaya cha mikupuo au mara. Makusdio ya Arshi ni utawala. Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:54), Juz. 11 (10:3) na Juz. 19 (25:59). Katika Juz. 8 (54:56) tumeeleza kauli zilizosemwa kuhusu siku sita na rai yetu.

Hulipanga jambo kutoka mbinguni hadi ardhini, kisha linapanda kwake katika siku ambayo kipimo chake ni miaka elfu kwa mnavyohisabu.

Makusudio ya kupanga jambo ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameumba ulimwengu, kila kiumbe akakipa sifa kwa namna inavyotaka hekima yake. Akamwajibishia kiumbe ambaye amempa uweza na utambuzi kulazimiana na njia aliyomwongoza.

Makusudio ya ‘kupanda kwake katika siku’ ni kuwa matendo ya viumbe yatakwenda kwake Siku ya Kiyama. Miaka elfu ni kinaya cha kurefuka zama.

Maana ni kuwa viumbe wote wamezungukwa na mipangilio ya Mungu na ulinzi wake. Yeye ndiye aliyewaleta na akawapangilia vizuri: “ambaye amekipa kila kitu umbo lake kisha akakiongoza” Juz. 16 (20:50). Ni Yeye atakayekimaliza na kukirudisha, na matendo yatapelekwa kwake siku ambayo itakuwa ndefu na nzito kwa waasi na wakosefu.

Huyo ndiye Mjuzi wa mambo ya ghaibu na ya dhahiri, Mwenye uwezo Mwenye kurehemu.

Muumba wa kila kitu na msimamizi wa kila kitu. Ni Mjuzi wa ya lililokuwa na litakalokuwa, liwe dogo au kubwa, la dhahiri au la kujificha. Ni Mwenye nguvu kwa uweza wake na ufalme wake na Mwenye huruma kwa viumbe wake na waja wake.

Ambaye ametengenza vizuri umbo la kila kitu.

Kila kiumbe kilichopatikana kwa nidhamu kamili basi ni kizuri na kimepangika, kikifahamisha uwezo wa mtengenezaji na utukufu wake. Hakuna kitu chochote kilichopo ila utaona nidhamu na uwiano unaofahamisha kuweko mjuzi mwenye hekima:

مَّا تَرَىٰ فِي خَلْقِ الرَّحْمَـٰنِ مِن تَفَاوُتٍ فَارْجِعِ الْبَصَرَ هَلْ تَرَىٰ مِن فُطُورٍ ﴿٣﴾

“Hutaona tofauti yoyote katika uumbaji wa Mwingi wa rehema. Hebu rudisha jicho, je unaona kosa lolote” (67:3).

Na akaanzisha umbo la mtu kwa udongo.

Makusudio ya mtu hapa ni baba wa watu, Adam.

Kisha akajaalia uzao wake utokane na kizazi cha maji hafifu ambayo ni manii. Kisha akamlimganisha sawa katika umbile zuri na akampulizia roho yake.

Hiki ni kinaya cha uhai. Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:2) na Juz. 18 (23:12 – 14).

Amewajaalia kusikia na kuona na nyoyo. Ni uchache mnavyoshukuru.

Neema ya ubainifu inatokana na neema ya usikizi uoni na utambuzi. Ama matamanio ya chakula ni kwa ajili ya kuishi na matamanio ya jinsia ni kwa ajli ya kubakia. Hakuna matamanio yoyote kwa mtu isipokuwa yana faida na hekima.

وَقَالُوا أَإِذَا ضَلَلْنَا فِي الْأَرْضِ أَإِنَّا لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ بَلْ هُم بِلِقَاءِ رَبِّهِمْ كَافِرُونَ ﴿١٠﴾

10. Na husema: Ati tutakapopotea ardhini, kweli tutakuwa kwenye umbo jipya? Bali wao wanakanusha kukutana na Mola wao.

قُلْ يَتَوَفَّاكُم مَّلَكُ الْمَوْتِ الَّذِي وُكِّلَ بِكُمْ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُمْ تُرْجَعُونَ ﴿١١﴾

11. Sema, atawafisha malaika wa mauti aliyewakilishwa kwenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu.

وَلَوْ تَرَىٰ إِذِ الْمُجْرِمُونَ نَاكِسُو رُءُوسِهِمْ عِندَ رَبِّهِمْ رَبَّنَا أَبْصَرْنَا وَسَمِعْنَا فَارْجِعْنَا نَعْمَلْ صَالِحًا إِنَّا مُوقِنُونَ ﴿١٢﴾

12. Na ungeliwaona wakosefu wanavyoinamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao. Mola wetu! Tumeona na tumesikia, turejeshe tutatenda mema, kwani hakika sisi tuna yakini.

وَلَوْ شِئْنَا لَآتَيْنَا كُلَّ نَفْسٍ هُدَاهَا وَلَـٰكِنْ حَقَّ الْقَوْلُ مِنِّي لَأَمْلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ الْجِنَّةِ وَالنَّاسِ أَجْمَعِينَ ﴿١٣﴾

13. Na lau tungelitaka tungeipa kila nafsi muongozo wake. Lakini imehakikika kauli kutoka kwangu: Kwa hakika nitaijaza Jahannam kwa wote majini na watu.

فَذُوقُوا بِمَا نَسِيتُمْ لِقَاءَ يَوْمِكُمْ هَـٰذَا إِنَّا نَسِينَاكُمْ وَذُوقُوا عَذَابَ الْخُلْدِ بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿١٤﴾

14. Basi onjeni kwa sababu ya kusahau mkutano wa siku yenu hii, hakika sisi tumewasahau. Na onjeni adhabu yenye kudumu kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.

WAKOSEFU WANAINAMISHA VICHWA VYAO.

Aya 10-14

MAANA

Na husema: Ati tutakapopotea ardhini, kweli tutakuwa kwenye umbo jipya?”

Hii ni sawa na kauli yao:

أَإِذَا كُنَّا تُرَابًا أَإِنَّا لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ كَفَرُوا بِرَبِّهِمْ ﴿٥﴾

“Ati tutakapokuwa mchanga, kweli tutakuwa katika umbo jipya?” Juz.13(13:5)

Bali wao wanakanusha kukutana na Mola wao.

Unaweza kuuliza : Washirikina walitangaza waziwazi kufuru yao ya kukutana na Mwenyezi Mungu waziwazi. Sasa kuna haja gani ya kusema wanakanusha kukutana na Mola wao? Si ni sawa na kumwambia aliyetangaza ukafiri kuwa wewe ni kafiri?

Jibu : makusudio ni kuwa wao hawakuipinga akhera kwa ujuzi, bali ni kwa ujinga na kuiga; sawa na kumwambia aliyetangaza ukafiri: wewe ni mjinga.

Sema, atawafisha malaika wa mauti aliyewakilishwa kwenu; kisha mtarejeshwa kwa Mola wenu.

Yaani, ewe Muhammad! Waambie waliokufuru kuwa nyinyi mtakufa tu, hilo halina shaka. Baada ya mauti hakika itawafunukia na mtajua kuwa bila shaka saa ya Kiyama itakuja na kwamba Mwenyezi Mungu atawafufua walio katika makaburi.

Na ungeliwaona wakosefu wanavyoinamisha vichwa vyao mbele ya Mola wao.

Walipinga ufufuo na wakawafanyia maskhara waliouamini, waliowapa mwito wake na kuwahadhari na mwisho mbaya. Watapofufuliwa na kusimama mbele ya Mola wao kwa ajili ya hisabu watainamisha vichwa vyao kwa kuona haya na majuto na kusema:

Mola wetu! Tumeona na tumesikia, turejeshe tutatenda mema, kwani hakika sisi tuna yakini.

Umetangulia mfano wake katika Juz.7 (6:27) na Juz. 18 (23:99 – 100).

Na lau tungelitaka tungeipa kila nafsi muongozo wake.

Razi anasema: “ Hii ni wazi kuwa madhehebu yetu yako sahihi pale tunaposema: Mwenyezi Mungu hakutaka imani kutoka kwa kafiri na hakutaka kwake isipokuwa kufuru.”

Nasi tunamwambia Razi: Ikiwa Mwenyezi Mungu ndiye aliyetaka kufuru kwa kafiri, na hakuna anayerudisha matakwa yake, basi kwa nini atamwadhibu. Vipi na Yeye ndiye aliyesema: “Wala hatukuwadhulumu, bali wao ndio waliokuwa madhalimu” (43:76).

Usahihi ni kuwa makusudio ya matakwa ya Mwenyezi Mungu hapa ni matakwa ya kiuumbaji ambayo ni kusema ‘kuwa.’

Yaani lau Mwenyezi Mungu angelitaka kuwalazimisha uongofu wangeliongoka. Na kama angelifanya hivyo, basi kusingekuwa na thawabu wala adhabu. Hayo tumeyaeleza mara kadhaa. Tazama Juz. 6 (5:49 – 50).

Lakini imehakikika kauli kutoka kwangu: Kwa hakika nitaijaza Jahannam kwa wote majini na watu.

Imehakikika kauli kutoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwamba ataijaza Jahannam kwa wafisadi na wale walioasi kwa hiyari na matakwa yao wenyewe. Ama wale ambao walimwitikia Mola wao wana maghufira na malipo makubwa. Kuna Hadith Qudsi inayosema: “Nimeiumba Pepo kwa anayenitii hata kama ni mtumwa Muhabeshi; na moto kwa anayeniasi hata kama ni bwana wa kikuraishi.”

Basi onjeni kwa sababu ya kusahau mkutano wa siku yenu hii, hakika sisi tumewasahau. Na onjeni adhabu yenye kudumu kwa yale mliyokuwa mkiyatenda.

Hakuna yoyote aliyefuata matamanio yake na hawa yake ila atamsahau Mwenyezi Mungu na hisabu na ataikufuru haki na dhamiri. Na kesho malaika wa adhabu watamwambia mkosaji huyu: umelewa utamu wa dunia basi leo onja uchungu wa akhera. Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:51) na Juz. 10 (9:67).

إِنَّمَا يُؤْمِنُ بِآيَاتِنَا الَّذِينَ إِذَا ذُكِّرُوا بِهَا خَرُّوا سُجَّدًا وَسَبَّحُوا بِحَمْدِ رَبِّهِمْ وَهُمْ لَا يَسْتَكْبِرُونَ ﴿١٥﴾

15. Hakika wanaoziamni Aya zetu ni wale tu ambao wanapokumbushwa hizo huanguka kusujudu na humsabihi kwa kumsifu Mola wao, nao hawatakabari.

تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ ﴿١٦﴾

16. Mbavu zao zinaachana na vitanda kumwomba Mola wao kwa hofu na tumaini, na hutoa katika yale tuliyowaruzuku.

فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٧﴾

17. Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika yanayofurahisha maisha. Ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda.

أَفَمَن كَانَ مُؤْمِنًا كَمَن كَانَ فَاسِقًا لَّا يَسْتَوُونَ ﴿١٨﴾

18. Je, aliye mumin ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.

أَمَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فَلَهُمْ جَنَّاتُ الْمَأْوَىٰ نُزُلًا بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٩﴾

19. Ama wale ambao wameamini na wakatenda mema watakuwa na bustani za makao. Ndipo pa kufikia kwa waliyokuwa wakiyatenda.

وَأَمَّا الَّذِينَ فَسَقُوا فَمَأْوَاهُمُ النَّارُ كُلَّمَا أَرَادُوا أَن يَخْرُجُوا مِنْهَا أُعِيدُوا فِيهَا وَقِيلَ لَهُمْ ذُوقُوا عَذَابَ النَّارِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ﴿٢٠﴾

20. Na ama wale ambao wamefanya ufuska, basi makazi yao ni motoni; kila wakitaka kutoka humo watarudishwa humo humo. Na wataambiwa: Onjeni adhabu ya moto ambayo mlikuwa mkiikadhibisha.

وَلَنُذِيقَنَّهُم مِّنَ الْعَذَابِ الْأَدْنَىٰ دُونَ الْعَذَابِ الْأَكْبَرِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢١﴾

21. Na kwa hakika tutawaonjesha adhabu hafifu kabla ya adhabu kubwa, labda watarejea.

وَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن ذُكِّرَ بِآيَاتِ رَبِّهِ ثُمَّ أَعْرَضَ عَنْهَا إِنَّا مِنَ الْمُجْرِمِينَ مُنتَقِمُونَ ﴿٢٢﴾

22. Ni nani dhalimu mkubwa kuliko yule anayekumbushwa kwa ishara za Mola wake kisha akazikataa. Hakika sisi ni wenye kuwachukulia kisasi wakosefu.

MUUMIN ANAWEZA KUWA SAWA NA FASIKI?

Aya 15 – 22

MAANA

Hakika wanaoziamni Aya zetu ni wale tu ambao wanapokumbushwa hizo huanguka kusujudu na humsabihi kwa kumsifu Mola wao.

Makusudio ya waumini hapa ni wale wanaoijua haki na kuitumia na kujitolea muhanga kwa ajaili yake; wanamwabudu Mwenyezi Mungu usiku na mchana kwa kumtegemea Yeye na kumfanyia ikhlasi peke yake, asiyekuwa na mshirika. Ama tasbihi, rukui na sujudi kwa msukumo wa chumo na kibiashara kwa dini, yote hayo ni unafiki sio ibada na ni uzandiki sio imani.

Nao hawatakabari; yaani waumini wanaikaribisha haki na kuacha masilahi yao binafsi kwa ajili ya haki; kwa sabu hiyo ndiyo dini yao na masilahi yao.

Ni wajibu kusujudi kwa mwenye kuisoma Aya hii au kuisikiliza na imesemekana hata mwenye kuisikia pia bila ya kukusudia.

Mbavu zao zinaachana na vitanda kumwomba Mola wao kwa hofu na tumaini.

Vitanda ni kinaya cha usingizi. Tukiunganisha Aya hii na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Watu ambao biashara wala kuuza hakuwashughulishi na kumdhukuru Mwenyezi Mungu.” Juz. 18 (24:37), maana yatakuwa: Hakika waumini haiwashughulishi biashara wala usingizi kuacha ibada ya Mwenyezi Mungu, jambo ambalo linaelezea kuhofia kwao adhabu yake na kutumai kwao thawabu zake.

Ibada hiyo ndiyo aliyoikusudia Mwenyezi Mungu aliposema: “Na usi- mamishe Swala, hakika Swala inakataza machafu na maovu.” Kuna Hadith isemayo: Kisimamo cha mja kinamkurubisha kwa Mwenyezi Mungu, kinamkataza dhambi, kinafuta maovu na kufukuza ugonjwa mwilini.” Ama Swala ya kibiashara huwa inaamrisha uovu na ubaya. Kwa sababu ubaya unaelekeza kwenye mfano wake na vile vile wema.

Na hutoa katika yale tuliyowaruzuku.

Wamemwabudu Mwenyezi Mungu kwa nyoyo, miili na mali.

Nafsi yoyote haijui waliyofichiwa katika yanayofurahisha maisha. Ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyatenda.

Makusudio ya nafsi ni nafsi yoyote, iliyokuwa na itakayokuwa katika ardhi au mbingu. Maana ni kuwa hakuna yeyote anayejua uhakika wa thawabu za kufurahisha ambazo Mwenyezi Mungu amewaandalia waumini, wenye kufanya matendo. Mtume anasema katika Hadith: “Mwenyezi Mungu anasema: “Nimewaandalia waja wangu wema ambayo hakuna jicho liliyaona wala sikio lililoyoyasikia, wala moyo uliyoyawazia.”

Je, aliye mumin ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.

Tafsri nyingi; ikiwemo Jamiu ya Tabariy, Bahrul-muhit ya Andalusi, Ruhul-bayan ya Haqi, zimesema kuwa Aya hii ilishuka Madina kuhusiana na Ali bin Abi Twalib na Walid bin U’qba bin Abi Mu’it. Tutanukuu yale ya Tabariy: “Kulipita maneno baina ya Walid na Ali. Walid akasema: “Mimi nina ulimi mpana kuliko wewe, nina meno makali kuliko wewe na ninafaa zaidi kwenye jeshi kuliko wewe.” Ali akamwambia, nyamaza wewe ni fasiki, ndipo ikashuka: ‘Je, aliye mumin ni sawa na aliye fasiki? Hawawi sawa.

Hapana wallah hawawi sawa duniani wala kwenye mauti na akhera pia.

Ama wale ambao wameamini na wakatenda mema watakuwa na bustani za makao. Ndipo pa kufikia kwa waliyokuwa wakiyatenda.

Hii ni kutofautisha baina ya mumin mwenye takua na kafiri muovu; ni sawa na kutofautisha wema na uovu, heri na shari na Pepo iliyoandaliwa wenye takua na moto ulioandaliwa wakosefu.

Na ama wale ambao wamefanya ufuska, basi makazi yao ni motoni; kila wakitaka kutoka humo watarudishwa humo humo. Na wataambiwa: Onjeni adhabu ya moto ambayo mlikuwa mkiikadhibisha.

Waumini watapata Pepo zenye neema na mafasiki watapata moto unaowaka. Umetangulia mfano wake katika Juz. 17 (22:22).

Na kwa hakika tutawaonjesha adhabu hafifu kabla ya adhabu kubwa, labda watarejea.

Makusudio ya adhabu hafifu ni adhabu ya duniani; kama vile kahati, balaa n.k. Anawaonya kwayo na kwa nguvu za hoja, wale walioghafilika na wanaojishughulisha na mambo ya batili na kuiacha haki, ili waonyeke na wapate mawaidha.

Vinginevyo watafikiwa na adhabu kubwa: “Moto wa Jahanam hali ya kudumu humo. Ni tosha yao. Na Mwenyezi Mungu amewalaani. Na wana wao adhabu ya kudumu.” Juz. 10 (9:68).

Kwa hakika ilivyo ni kuwa viongozi na watawala ndio chimbuko la kwanza la ufisadi na uovu. Kuna Hadith zinayosema: “Watawala wakiwa waongo huzuiliwa mvua, na mtawala akiwa jeuri dola inakuwa dhalili.”

Ni nani dhalimu mkubwa kuliko yule anayekumbushwa kwa ishara za Mola wake kisha akazikataa. Hakika sisi ni wenye kuwachukulia kisasi wakosefu.

Mwenye kupata mawaidha kisha asiwaidhike nayo basi huyo ni katika wakosefu wakubwa. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewaonya kwa ulimi wa mitume wake na kwa madhara na shida, lakini nyoyo zao zikasusuwaa na wakaendelea na dhulma na ufisadi. Ndio Mwenyezi Mungu akawalipiza kisasi na Yeye ni mwenye nguvu Mwenye kulipiza kisasi.

وَلَقَدْ آتَيْنَا مُوسَى الْكِتَابَ فَلَا تَكُن فِي مِرْيَةٍ مِّن لِّقَائِهِ وَجَعَلْنَاهُ هُدًى لِّبَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿٢٣﴾

23. Hakika tulimpa Musa Kitabu basi usiwe na shaka ya kukipokea kwake, na tukakifanya ni mwongozo kwa wana wa Israil.

وَجَعَلْنَا مِنْهُمْ أَئِمَّةً يَهْدُونَ بِأَمْرِنَا لَمَّا صَبَرُوا وَكَانُوا بِآيَاتِنَا يُوقِنُونَ ﴿٢٤﴾

24. Na tukawafanya miongoni mwao maimamu wanaoongoza kwa amri yetu waliposubiri, na wakawa na yakini na ishara zetu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَفْصِلُ بَيْنَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ فِيمَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ﴿٢٥﴾

25. Hakika Mola wako ndiye atakayefafanua baina yao Siku ya Kiyama katika lile walilohitalifiana.

أَوَلَمْ يَهْدِ لَهُمْ كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّنَ الْقُرُونِ يَمْشُونَ فِي مَسَاكِنِهِمْ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ أَفَلَا يَسْمَعُونَ ﴿٢٦﴾

26. Je, haikuwabainikia, ni vizazi vingapi tuliviangamiza kabla yao nao wanatembea katika maskani zao. Hakika katika hayo kuna ishara, basi je, hawasikii.

أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا نَسُوقُ الْمَاءَ إِلَى الْأَرْضِ الْجُرُزِ فَنُخْرِجُ بِهِ زَرْعًا تَأْكُلُ مِنْهُ أَنْعَامُهُمْ وَأَنفُسُهُمْ أَفَلَا يُبْصِرُونَ ﴿٢٧﴾

27. Je, hawaoni kwamba tunayapeleka maji kwenye ardhi kame, kisha kwayo tunaitoa mimea wanayokula wanyama wao. Je, hawapati busara.

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْفَتْحُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٨﴾

28. Na wanasema: Ushindi huu utatokea lini, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

قُلْ يَوْمَ الْفَتْحِ لَا يَنفَعُ الَّذِينَ كَفَرُوا إِيمَانُهُمْ وَلَا هُمْ يُنظَرُونَ ﴿٢٩﴾

29. Sema: Siku ya ushindi wale ambao wamekufuru haitafaa imani yao, wala hawatapewa muda.

فَأَعْرِضْ عَنْهُمْ وَانتَظِرْ إِنَّهُم مُّنتَظِرُونَ ﴿٣٠﴾

30. Basi achana nao na ungoje; hakika wao wanangoja.

USIWE NA SHAKA YA KUIPOKEA KWAKE

Aya 23 – 30

MAANA

Hakika tulimpa Musa Kitabu basi usiwe na shaka ya kukipokea kwake, na tukakifanya ni mwongozo kwa wana wa Israil.

Wafasiri wengi wamesema kuwa ‘Kwake’ inarudi kwa Musa; kwa maana ya kuwa Muhammad atakutana na Musa usiku wa Miraji. Ilivyo hasa ni kuwa dhamiri hiyo inarudia kwenye Qur’an; kwa maana ya kuwa, ewe Muhammad! Tumekutermshia Qur’an kama tulivyomteremshia Musa Tawrat. Wala haitakikani kutia shaka katika hilo wewe wala mwingine.

Kuhusu kukatazwa Mtume kutia shaka tumekuelezea mara nyingi. Tazama Juz. 3 (3:59-63).

Na tukawafanya miongoni mwao maimamu wanaoongoza kwa amri yetu waliposubiri, na wakawa na yakini na ishara zetu.

Makusudio ya maimamu hapa ni mitume wa Kiisrail; kama vile Musa, na Isa ambaye nasaba ya upande wa mama yake inafikia kwa Daud. Kila Mtume wa kiisraili alipata aina kwa aina ya adhabu na mateso; bali waisrail waliwaua manabii wao kadhaa:

وَيَقْتُلُونَ النَّبِيِّينَ بِغَيْرِ الْحَقِّ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَوا وَّكَانُوا يَعْتَدُونَ ﴿٦١﴾

“Na wakiwaua Manabii pasipo haki. Basi haya ni kwa sababu ya kuasi kwao na kupituka mipaka.” Juz. 1 (2:61).

Pamoja na yote hayo, waliweza kuvumilia wakawa na subira na wakaendelea kutekeleza risala yao. Kwa hiyo nawe Muhammad vumilia maudhui ya watu wako na uendelee na risala yako.

Hakika Mola wako ndiye atakayefafanua baina yao Siku ya Kiyama katika lile walilohitalifiana.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:113), Juz. 11(10:93) na Juz. 14 (16:124).

Je, haikuwabainikia, ni vizazi vingapi tuliviangamiza kabla yao nao wanatembea katika maskani zao. Hakika katika hayo kuna Ishara, basi je, hawasikii.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20).

Je, hawaoni kwamba tunayapeleka maji kwenye ardhi kame, kisha kwayo tunaitoa mimea wanayokula wanyama wao.

Je, hawapati busara kwa jinsi Mwenyezi Mungu alivyoipa uhai ardhi baada ya kufa kwake na akaotesha humo kila aina za mimea wanayokula watu na wanyama? Kama hivyo atawafufua wafu baada ya kuwa ni mchanga na mifupa

Umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa; kama Juz. 17: (22:5).

Na wanasema: ushindi huu utatokea lini, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

Aya hii ni mfano wa ile isemayo: “Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi mnasema kweli?” Juz. 17 (21:38). Kwa sababu makusudio ya ushindi hapa ni siku itakayohukumiwa kwa haki. Hilo linatiliwa nguvu na kauli inayofuatia:

Sema: Siku ya ushindi wale ambao wamekufuru, na wakaifanyia inadi haki katika maisha ya dunia,haitafaa imani yao huko akhera wakati watakapoiona adhabu. Kwa sababu imani hiyo itakuwa ni kuukimbia moto sio imani ya kweli na yakini.

Wala hawatapewa muda.

Mwenyezi Mungu hawezi kuwapa muda siku ya Kiyama, kwa sababu ali- wapa muda mrefu duniani, lakini hawakuitumia fursa hiyo.

Basi achana nao na ungoje; hakika wao wanangoja.

Wao wanangoja ufikwe na majanga, basi achana nao na ungoje kidogo tu, utaona hukumu ya Mwenyezi Mungu kwako na kwao. Yeye atakunusuru na atawafedhehsha wao:

هُوَ الَّذِي أَرْسَلَ رَسُولَهُ بِالْهُدَىٰ وَدِينِ الْحَقِّ لِيُظْهِرَهُ عَلَى الدِّينِ كُلِّهِ وَلَوْ كَرِهَ الْمُشْرِكُونَ ﴿٣٣﴾

“Yeye ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uongofu na dini ya haki ili ipate kushinda dini zote, ijapokwa washirikina wamechukia.” Juz. 10 (9:33).

20

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Sura Ya Thelathini Na Tatu: Surat Ahzab. Imeshuka Madina, Ina Aya 73.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ اتَّقِ اللَّـهَ وَلَا تُطِعِ الْكَافِرِينَ وَالْمُنَافِقِينَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمًا ﴿١﴾

1. Ewe Nabii! Mche Mwenyezi Mungu wala usiwatii makafiri na wanafiki. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hekima.

وَاتَّبِعْ مَا يُوحَىٰ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرًا ﴿٢﴾

2. Na fuata uliyoletewa wahyi kutoka kwa Mola wako. Hakika Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda.

وَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّـهِ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ وَكِيلًا ﴿٣﴾

3. Na mtegemee Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni wa kutegemewa.

EWE NABII, MCHE MWENYEZI MUNGU

Aya 1-3

MAANA

Ewe Nabii! Mche Mwenyezi Mungu wala usiwatii makafiri na wanafiki. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye hekima. Na fuata uliyoletewa wahyi kutoka kwa Mola wako. Hakika Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda. Na mtegemee Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anatosha kuwa ni wa kutegemewa.

Katika Aya hizi Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemwamrisha Nabii wake mtukufu, kuwa na takua, kumtegemea Yeye, kuutumia wahyi wake na kutowatii makafiri na wanafiki.

Wafasiri wamejiuliza kuwa Nabii ni maasumu, sasa kuna haja gani ya amri zote hizi na kukatazwa uasi?

Kuna waliojibu kuwa hii ni kusisitiza utiifu na unyenyekevu alio nao Nabii(s.a.w.w) . Wengine wakasema kuwa Abu Sufyan alimtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kutoyatukana masanamu wanayoyaubudu makauraishi. Abu Sufyani wakati huo alikuwa pamoja na kundi la makafiri na wanafiki.

Sisi huko nyuma tumesema mara kwa mara kuwa aliye juu ana uwezo wa kumwamrisha aliye chini na kumkataza maasi hata kama ni maasumu. Hivi sasa tunayaunganisha hayo na haya yafutayo:

Hakuna kitu kizito kwa yule asiyemuogopa Mwenyezi Mungu kuliko tamko la ‘mche Mungu;’ wala hakuna adui mkubwa kuliko atakayelisema tamko hilo kwake. Imenukuliwa kutoka kutoka kwa Abdul-Malik bin Marwani kwamba yeye alipotawala alisema katika hotuba: “Kuanzia leo, atakayeniambia: mche Mungu, nitamkata shingo yake.”

Ama yule mwenye kuhofia kukutana na Mola wake na akaikanya nafsi na matamanio, basi kwake yeye hilo ni tamko la mapenzi na huruma na hutamani lau angelisikia mara kwa mara; hata kama ni maasumu wa makosa na madhambi; bali huko kulipenda na kulisikilza kumetokana na umaasumu na utiifu wake. Mtu adhimu huwa anajituhumu kwa upunguvu kadiri atakavyoweza kujitahidi.

Kwa hiyo basi hakuna haja ya kuleta taawili na tafsiri nyingine. Kuongezea kuwa amri ya takuwa kwa bwana wa watu na majini ni hekima na somo kubwa kwa wenye vyeo na watawala, kwamba kwa vyovyote watakavyokuwa wakubwa, lakini hawako zaidi ya kuamrishwa uadilifu na takua.

Kwenye Nahjul balagha imeelezwa: “Ambaye itakuwa uzito kwake kuambiwa neno la haki au kuelezwa uadilifu basi itakuwa kuyafanya mawili hayo ni uzito zaidi.”

مَّا جَعَلَ اللَّـهُ لِرَجُلٍ مِّن قَلْبَيْنِ فِي جَوْفِهِ وَمَا جَعَلَ أَزْوَاجَكُمُ اللَّائِي تُظَاهِرُونَ مِنْهُنَّ أُمَّهَاتِكُمْ وَمَا جَعَلَ أَدْعِيَاءَكُمْ أَبْنَاءَكُمْ ذَٰلِكُمْ قَوْلُكُم بِأَفْوَاهِكُمْ وَاللَّـهُ يَقُولُ الْحَقَّ وَهُوَ يَهْدِي السَّبِيلَ ﴿٤﴾

4. Mwenyezi Mungu hakumwekea mwanamume nyoyo mbili ndani yake. Wala hakuwafanya wake zenu – mnaowalinganisha migongo yao na migongo ya mama zenu – kuwa ni mama zenu. Wala hakuwafanya watoto wenu wa kupanga kuwa ni wana wenu. Hiyo ni kauli yenu kwa vinywa vyenu tu. Na Mwenyezi Mungu anasema haki, naye huongoza njia.

ادْعُوهُمْ لِآبَائِهِمْ هُوَ أَقْسَطُ عِندَ اللَّـهِ فَإِن لَّمْ تَعْلَمُوا آبَاءَهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ فِي الدِّينِ وَمَوَالِيكُمْ وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُم بِهِ وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥﴾

5. Waiteni kwa baba zao. Hilo ndio uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. Kama hamuwajui mababa zao basi ni ndugu zenu katika dini na rafiki zenu. Si vibaya kwenu kwa mlivyokosea, lakini kwa yale ziliyoyakusudia nyoyo zenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

MWENYEZI MUNGU HAKUMWEKA MTU MMOJA NYOYO MBILI

Aya 4 – 5

MAANA

Mwenyezi Mungu hakumwekea mwanamume nyoyo mbili ndani yake.

Hata mwanamke pia ni kama mwanamume. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuhusu mwanmume hapa kwa sababu amemwamrisha Mtume(s.a.w.w) wake mtukufu kuwa na takua, kwa hiyo ikanasibiana kufuatishia amri hii kuwa mwanamume hawezi kuwa na moyo mmoja wa kumcha Mwenyezi Mungu na mwingine wa kucha watu.

Lengo ni Mwenyezi Mungu (s.w.t) anabainisha kuwa mtu hawezi kuamini mambo mawili yanayopingana kwa wakati mmoja; kwa mfano aamini dini inayokataza dhulma na uchokozi, Uislamu na Ukiristo, na wakati huo huo ahalalishe dhulma na uchokozi.

Ila ikiwa ana nyoyo mbili na nyuso mbili; kama waamerika ambao wameleta kununi mpya, kwamba mmarekani anaweza kuwa ni mwisrail na kupigana na mwarabu kwa jina la Israil na wakati huo bado ni raia wa Marekani.

Au itabidi tuseme kuwa Israil ni kambi ya jeshi la uchokozi la marekani na kwamba urai wa Israil ni jina tu; hata watawala pia; kwa vile ni kikosi tu cha kulinda masilahi ya ukoloni na unyonyaji.

Mtu mmoja alimwambia Imam Ali(a.s ) : “Mimi nakupenda wewe na ninampenda Muawiya.” Imam akamwambia:“Wewe ni chongo, sasa chagua ama uwe kipofu au upone chongo.”

Unaweza kuuliza : Utasemaje kuhusiana na anayesema; mimi ni mwislamu au mkristo kiitikadi, lakini kisiasa ninafuata siasa za mashariki au magharibi. Je inawezekana kuchanganya mawili haya?

Jibu : Mtu yoyote anayeamini haki kwa ukweli na usafi wa nia, inafaa, bali ni wajibu kumuunga mkono kila kwenye msimamo wa kuinusuru haki na uadilifu; awe ni wa mashariki au magharibi. Wala haijuzu kumuunga mkono tu, hivi hivi, bila ya msingi wowote. Kwa maana hiyo basi haiwezekeni kuchanganya baina ya itikadi ya kiislamu na kuunga mkono tu hivi hivi kwa hali yoyote.

Hii ni katika yanayohusiana na Uislamu. Ama yanayohusiana na itikadi ya kikiristo tunawaachia makasisi walio huru waliotangaza hasira zao kwa baba mtakatifu aliyekataa kukutana nao, lakini wakati huo huo akakutana na viongozi wa kimarekani.

Wakasema katika mateta yao: “Mkutano huu wa Baba mtakatifu na viongozi hawa unaonyesha wazi uhusiano wa nguvu ulioko baina ya kanisa kama tasisi ya dini na siasa za kiuchumi zinazosimamia ukandamizaji na dhulma dhidi ya watu wengi.” Makasisi hawa walitangaza kuwa wangejaribu kuuangamiza uhusiano huu[6] .

Wala hakuwafanya wake zenu – mnaowalinganisha migongo yao na migongo ya mama zenu – kuwa ni mama zenu.

Wakati wa ujahiliya mtu alikuwa akimwacha mkewe kwa kumwambia: Wewe kwangu ni kama mgongo wa mama yangu (Dhihar). Uislamu ukalikataza hilo, kwa sabau mke hawezi kuwa mama kwa kauli hii, na ukawajibisha kafara kwa atakayesema kauli hiyo, yakipatikana masharti yake, ambayo yatabainishwa mwanzoni mwa Juzuu ya 28. (inshaallah).

Wala hakuwafanya watoto wenu wa kupanga kuwa ni wana wenu.

Wakati wa ujahiliya mtu alikuwa akimchukua mtoto wa mwingine kumfanya mwanawe hasa na kumwingiza kwenye ukoo wake, anakuwa na hukumu ya mtoto wake halisi katika kila kitu na watu wakimwita kwa jina la baba aliyemchukua badala ya baba yake. Ndipo Uislamu ukakataza mtindo huu[7] .

Hiyo ni kauli yenu kwa vinwywa vyenu tu.

Na kauli haibadilishi uhalisi wa mambo.

Na Mwenyezi Mungu anasema haki naye huongoza njia.

Kauli ya haki na njia ya sawa ni kuwa mtoto wa kupanga sio mtoto wa kiuhakika; wala mke hawi ni mama kwa dhihari.

Waiteni kwa baba zao waliowazaa sio waliowapanga.Hilo ndio uadilifu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu. yaani hilo la kuwaita kwa ubini wa baba zao.

Kama hamuwajui mababa zao basi ni ndugu zenu katika dini na rafiki zenu.

Neno rafiki limefasiriwa kutokana na neno mawla, pia lina maana ya huria; mtumwa aliyeachwa huru. Mtu alikuwa anaweza kuitwa huria wa fulani.

Wafsiri na watu wa sera wanasema kuwa Zayd Bin Haritha alitekwa nyara akiwa mdogo. Hakim bin Huzam akamnunua kwa ajili ya kumpatia shangazi yake Khadija Bint Khuwalid. Mtume(s.a.w.w) alipomuoa akapewa zawadi na mkewe. Baada ya kushuka wahyi kwa Nabii, akamlingania kwenye Uisalamu na akasilimu. Akamfanya ndugu na ami yake Hamza bin Abu Twalib.

Haritha, Baba yake Zayd, akaja siku moja kwa Mtume(s.a.w.w) na kumwambia, ama uniuzie mwanangu, au mwache huru. Mtume akamwacha huru na kumwambia nenda upendako. Basi akakataa kuachana na Mtume. Ndipo watu wakawa wanamwita Zayd bin Muhammad mpaka iliposhuka Qur’an kubatilisha hilo.

Si vibaya kwenu kwa mlivyokosea, lakini kwa yale ziliyoyakusudia nyoyo zenu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Anayemwita mtu asiyekuwa baba yake kwa kufikiria kuwa ni baba yake, hana lawama; isipokuwa mwenye dhambi ni yule aliyejua na akakusudia: Mtume(s.a.w.w) anasema: “Umma wangu umeondolewa kukosea na kusahau na yale waliyolazimishwa na wasiyoyajua na wasiyoyaweza na wanayokuwa na dharura nayo,” kwa sharti la kutotokea hayo kwa uzembe na kupuuza.

النَّبِيُّ أَوْلَىٰ بِالْمُؤْمِنِينَ مِنْ أَنفُسِهِمْ وَأَزْوَاجُهُ أُمَّهَاتُهُمْ وَأُولُو الْأَرْحَامِ بَعْضُهُمْ أَوْلَىٰ بِبَعْضٍ فِي كِتَابِ اللَّـهِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُهَاجِرِينَ إِلَّا أَن تَفْعَلُوا إِلَىٰ أَوْلِيَائِكُم مَّعْرُوفًا كَانَ ذَٰلِكَ فِي الْكِتَابِ مَسْطُورًا ﴿٦﴾

6. Nabii ni aula kwa waumini kuliko nafsi zao. Na wake zao ni mama zao. Na ndugu wa tumbo ni aula wenyewe kwa wenyewe, katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, kuliko waumini wengine na wahajiri. Ila muwe mnafanya wema kwa marafiki zenu. Hayo yamekwishaandikwa kitabuni.

وَإِذْ أَخَذْنَا مِنَ النَّبِيِّينَ مِيثَاقَهُمْ وَمِنكَ وَمِن نُّوحٍ وَإِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَى ابْنِ مَرْيَمَ وَأَخَذْنَا مِنْهُم مِّيثَاقًا غَلِيظًا ﴿٧﴾

7. Na tulipochukua kwa manabii agano lao na kwako wewe na Nuh na Ibrahim na Isa mwana wa Maryam, na tulichukua kwao agano madhubuti.

لِّيَسْأَلَ الصَّادِقِينَ عَن صِدْقِهِمْ وَأَعَدَّ لِلْكَافِرِينَ عَذَابًا أَلِيمًا ﴿٨﴾

8. Ili awaulize wakweli juu ya ukweli wao. Na amewandaalia makafiri adhabu chungu.

NABII NI AULA KWA WAUMINI KULIKO NAFSI ZAO

Aya 6 – 8

MAANA

Je, Nabii Ni Hakimu Kwa Amri Yake? Nabii Ni Aula Kwa Waumini Kuliko Nafsi Zao.

Neno aula tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu linalotamkwa hivyo hivyo awla lililonyumbuliwa kutokana na neno wilaya na walii, ambalo maana yake yanatofautiana kulingana na yule anayezungumziwa. Akizungumziwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) basi maana yake ni utawala na nguvu zisizoshindwa na yeyote. Akizungumziwa Nabii(s.a.w.w) inakuwa maana ni utiifu usiopingwa. Haya ndiyo maana yaliyokusudiwa hapa.

Sasa unaweza kuuliza: Si itakuwa maana yake ni kuwa Nabii ni hakimu na mtoa amri tu, mwengine hana uhuru. Tutalinganisha vipi hili na lile la msingi wa uhuru ambao ni haki ya kiasili ya kila mtu?

Jibu : Tutalinganisha uhuru wa mtu na utiifu wa Mwenyezi Mungu. Nabii(s.a.w. w ) anamsemea na kumbainishia Mwenyezi Mungu:

وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَىٰ ﴿٣﴾ إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَىٰ ﴿٤﴾

“Hatamki kwa matamanio. Hayakuwa haya ila ni wahyi uliofunuliwa” 53 (3 – 4).

Kuna Hadith sahihi kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) amesema:“Haamini mmoja wenu mpaka matamanio yake yafuate yale niliyokuja nayo.” Kwa hiyo kufuata na kutii ni aliyokuja nayo kutoka kwa Mwenyezi Mungu sio kutoka kwake.

Zaidi ya hayo uhuru ni kushikamana na njia ya usawa, kutumia haki na kubeba majukumu kwa utashi wake, huku akiipigania haki kwa nguvu zake zote. Lakini mwenye kuwa na msukumo wa mapendeleo bila ya kujali hisabu wala mchungaji, huyo ni mtumwa wa matamanio. Mwana falsafa mmoja mashuhuri alisema: “Uhuru sio kujifadhilisha kiundani kunakoruhusu tujifadhilishe sisi kuliko majukumu; isipokuwa ni uwezo wa kujenga mustakabali.”

Na wake zao ni mama zao.

Wake za mitume wana heshima na uharamu wa kuolewa baada yake sawa na mama, lakini kwenye mambo mengine ni watu kando kama wengine.

Na ndugu wa tumbo ni aula wenyewe kwa wenyewe, katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu, kuliko waumini wengine na wahajiri.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 10 (9:75).

Ila muwe mnafanya wema kwa marafiki zenu

Makusudio ya wema hapa ni wasia, na marafiki wanakuwa ni pamoja na walioachwa huru au ndugu wasiorithi. Maana ni kuwa mirathi ni ya ndugu wa karibu wa maiti, lakini wasia ni wa aliyeusiwa awe wa mbali au wa karibu.

Hayo yamekwishaandikwa kitabuni.

Yaani hukumu imekwishathibiti Kitabuni mbele ya Mwenyezi Mungu na mwenye kuiasi atakuwa miongoni mwa walioangamia.

Na tulipochukua kwa manabii agano lao na kwako wewe na Nuh na Ibrahim na Isa mwana wa Maryam, na tulichukua kwao ahadi ngumu.

‘Kwako wewe,’ anaambiwa Muhammad(s.a.w. w ) . Makusudio ya agano ni kufikisha (Tabligh) risala ya Mwenyezi Mungu kwa ukamilifu wake na kuwa na subira na yatakayowapata katika njia yake. Amehusisha kutaja Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na Muhammad, baada ya kuwataja manabii kwa ujumla kwa vile wao ni bora ya manabii wote, na ametangulizwa Muhammad kwa vile yeye ni mbora wao hao watano.

Katika Juz. 26 (46:35) wameashiriwa mitume Ulul-azmi (wenye ustahamilivu). Sababu ya kuitwa hivyo, kama zilivyopokewa baadhi ya riwaya, ni kuwa kila Nabii baada ya Nuh alikwa akifuata sharia ya Nuh, kisha sharia yake ikafutwa na sharia ya Ibrahim nayo ikafutwa na sharia ya Musa, nayo ikafutwa na Isa, kisha ikafutwa na ya Muhammad (s.a.w.) ambayo haitafutwa hadi Kiyama, kwa vile hakuna Nabii mwingine baada yake.

Na tulichukua kwao agano madhubuti.

Hili ndilo agano la kwanza, na amerudia kulitaja ili alisifu kuwa ni imara na lenye nguvu. Mwenyezi Mungu ameyapa sifa ya maagano madhibuti katika sehemu tatu katika Kitabu chake kitukufu:

Kwanza, ni agano la ndoa aliposema: “Na hali wao wamechukua kwenu agano madhubuti?” Juz. 4 (4:21). Pili ni agano alilochukua na wana wa Israil aliposema: “Na tukachukua kwao agano madhubuti.” Juz. 6 (4:154). Agano la tatu ni hili la Manbii tunalolizungumzia.

Sheikh Mahmud Shaltut, alighafilika kidogo pale aliposema: “Wasifu wa agano madhubuti haukuja katika sehemu yoyote ile katika sehemu zake – yaani Qur’an - isipokuwa katika kufunga ndoa.” Kutokosea ni kwa Mungu.

Ili awaulize wakweli juu ya ukweli wao.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewatuma Manabii na akachukua kwao agano la kufikisha ujumbe ili wakawaulize wakweli, walikusudia nini kwenye ukweli wao. Je, walikusudia radhi ya Mwenyezi Mungu au ni kwa ajili ya kuwaambia watu kuwa wao ni wakweli na mengineyo ya kibinafsi.

Imam Ja’far Sadiq(a.s) anasema: “Mwenyezi Mungu akimuuliza mtu kuhusu ukweli wake ni kwa njia gani aliusema, basi atamlipa kulingana nao, je vipi hali ya muongo?”

Na amewandalia makafiri adhabu chungu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alipowataja mitume sasa anawataja makafiri kwa mkabala wa kuwataja wema.