TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI30%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 25 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 16597 / Pakua: 3728
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI Juzuu 20

Mwandishi:
Swahili

1

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

Sura Ya Ishirini Na Tisa: Surat A’nkabut. Imesemekana kuwa imeshuka Makka, ina Aya 69.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

الم ﴿١﴾

1. Alif Laam Miim.

أَحَسِبَ النَّاسُ أَن يُتْرَكُوا أَن يَقُولُوا آمَنَّا وَهُمْ لَا يُفْتَنُونَ ﴿٢﴾

2. Je, wanadhani watu wataachwa waseme tumeamini nao wasijaribiwe?

وَلَقَدْ فَتَنَّا الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ فَلَيَعْلَمَنَّ اللَّـهُ الَّذِينَ صَدَقُوا وَلَيَعْلَمَنَّ الْكَاذِبِينَ ﴿٣﴾

3. Hakika tuliwajaribu waliokuwa kabla yao. Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio wakweli na kwa yakini atawatambulisha waongo.

أَمْ حَسِبَ الَّذِينَ يَعْمَلُونَ السَّيِّئَاتِ أَن يَسْبِقُونَا سَاءَ مَا يَحْكُمُونَ ﴿٤﴾

4. Au wanadhani wanaotenda maovu kwamba watatushinda? Ni mabaya wanayohukumu.

مَن كَانَ يَرْجُو لِقَاءَ اللَّـهِ فَإِنَّ أَجَلَ اللَّـهِ لَآتٍ وَهُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٥﴾

5. Mwenye kutaraji kukutana na Mwenyezi Mungu, basi hakika miadi ya Mwenyezi Mungu itafika. Naye ni mwenye kusikia mwenye kujua.

وَمَن جَاهَدَ فَإِنَّمَا يُجَاهِدُ لِنَفْسِهِ إِنَّ اللَّـهَ لَغَنِيٌّ عَنِ الْعَالَمِينَ ﴿٦﴾

6. Na anayefanya juhudi basi hakika anafanya juhudi kwa ajili ya nafsi yake. Hakika Mwenyezi Mungu si mhitaji wa walimwengu.

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُكَفِّرَنَّ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَلَنَجْزِيَنَّهُمْ أَحْسَنَ الَّذِي كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٧﴾

7. Na wale ambao wameamini na wakatenda mema, kwa hakika tutawaondolea maovu yao, na tutawalipa mazuri ya waliyokuwa wakiyatenda.

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ حُسْنًا وَإِن جَاهَدَاكَ لِتُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا إِلَيَّ مَرْجِعُكُمْ فَأُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٨﴾

8. Na tumemuusia mtu kuwatendea wema wazazi wake wawili. Na wakikushikilia unishirikishe mimi na yale usiyokuwa na ujuzi nayo, basi usiwatii. Kwangu mimi ndio marejeo yenu, na nitawaambia mnayoyatenda.

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَنُدْخِلَنَّهُمْ فِي الصَّالِحِينَ ﴿٩﴾

9. Na wale ambao wameamini na wakatenda mema kwa hakika tutawaingiza katika wema.

IMANI, JIHADI NA SUBIRA

Aya 1 – 9

MAANA

Alif Laam Miim.

Umepita mfano wake katika Juz. 1 (2:1).

Wasidhani watu wataachwa waseme tumeamini nao wasijaribiwe?

Imani sio tamko la kusemwa, bali hapana budi liamambatane na mitihani na majaribu ya aina ya raha na tabu. Mwenye kuvumilia tabu na asitoke kwenye dini yake na akashukuru raha na kunyenyekea, wala cheo na mali isimfanye jeuri na kupetuka mipaka, huyo ndiye mumin wa kweli. Vinginevyo atakuwa sio mumin chochote.

Hivi ndivyo inavyofahamisha dhahiri ya Aya. Tukiiunganisha na Aya nyingine zinazohusiana na maudhui haya, tunapata muhtasari wa kuwa kuna jambo ambalo haliepukani na imani kwa hali yoyote. Nalo ni kuitikia muumini mwito wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kimatendo sio kimatamshi; yaani afanye bidii yake yote kutii amri ya Mungu na makatazo yake na kuambatana hayo na tabia yake na matendo yake. Anapopata mtihani na msukosuko wowote, basi umzidishe imani na unyenyekevu, kwa sababu anamfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu.

Tazama Juz. 2 (2: 153 – 157), kifungu cha ‘Thamani ya Pepo,’ Juz. 2 (2:211 – 212), kifungu cha ‘Hakuna imani bila ya takua’ na Juz. 5 (4: 135 – 136) kifungu cha ‘Baina ya dini na watu wa dini.’

Hakika tuliwajaribu waliokuwa kabla yao.

Wafuasi wa Mitume waliotangulia tuliwajaribu kwa shida, wakavumilia na wakawa na subira ya uungwana na wakazidi kushikamana na dini yao na ikhlasi kwa Mola wao na mitume yao.

Tafsiri inayofafanua zaidi Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Ni manabii wangapi waliopigana pamoja nao waumin wengi, nao hawakulegea kwa yale yaliyowasibu katika njia ya Mwenyezi Mungu, wala hawakudhoofika, wala hawakudhalilika. Na Mwenyezi Mungu anawapenda wanaosubiri.” Juz. 4 (3:146).

Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio wa kweli na kwa yakini atawatambulisha waongo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamtahini mja wake kwa kumpa mbele ya dunia na nyuma yake, ili vidhihiri vitendo vyake vitakavyomfanya astahiki thawabu na adhabu. Kwa sababu yeye ambaye, imetukuka hekima yake, hamhisabu mtu kutokana na maandalizi yake ya kheri au ya shari; isipokuwa anamhisabu kwa matendo yake ambayo yanadhihirika.

Au wanadhani wanaotenda maovu kwamba watatushinda?

Waovu wanafikiria kuwa Mwenyezi Mungu hawezi kuwapata? Itakuwaje naye ni muweza wa kila kitu? Ni nani atakayeweza kuwazuia naye na hali yeye hana mpinzani wala mshirika aliye sawa naye?

Ni mabaya wanayohukumu kwamba wao wataponyoka na utawala wa Mwenyezi Mungu na hukumu yake.

Mwenye kutaraji kukutana na Mwenyezi Mungu, basi hakika miadi ya Mwenyezi Mungu itafika.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja wenye kukufuru siku ya mwisho sasa anataja mwenye kumwamini. Akamwambia mumin huyu:

Thibiti kwenye imani yako, kwani saa itafika tu hakuna shaka, basi ifanyie kazi.

Naye ni mwenye kusikia, Mwenye kujua.

Anasikia unayoyasema na anajua unayoyadhamiria na kuyafanya na atakulipa yaliyopita.

Na anayefanya juhudi basi hakika anafanya juhudi kwa ajili ya nafsi yake.

Tafsiri ya Aya hii ni ile Aya isemayo:

فَمَنْ أَبْصَرَ فَلِنَفْسِهِ وَمَنْ عَمِيَ فَعَلَيْهَا ﴿١٠٤﴾

“Basi atakayefungua macho ni faida yake mwenyewe; na atakayeyapofua ni hasara yake mwenyewe.” Juz. 7 (6:104).

Hakika Mwenyezi Mungu si mhitaji wa walimwengu , haumnufaishi utiifu wa mwenye kutii, wala haumdhuru uasi wa mwenye kuasi.

Na wale ambao wameamini na wakatenda mema, kwa hakika tutawaondolea maovu yao, na tutawalipa mazuri ya waliyokuwa wakiyatenda.

Mwenye kuamini baada ya kukufuru, akawa mwema baada ya kuwa mfisadi, basi Mwenyezi Mungu atamsamehe na kumghufiria yaliyopita. Zaidi ya hayo atapata thawabu kutokana na imani yake na wema wake; sawa na ambaye hana dhambi.

Katika msingi huu wa heri kuna heri zote za utu. Kwa sababu unafungua mlango wa matumaini ya wenye dhambi na makosa na kupata msukumo wa kutubia na kujing’oa kwenye uovu. Hakuna njia nzuri kuliko hii ya kuisafisha jamii na dhulma na ufisadi.

TENA KUWATENDEA WEMA WAZAZI WAWILI

Na tumemuusia mtu kuwatendea wema wazazi wake wawili. Na wakikushikilia unishirikishe mimi na yale usiyokuwa na ujuzi nayo, basi usiwatii. Kwangu mimi ndio marejeo yenu, na nitawaambia mnayoyatenda.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameamrisha kuwatendea wema wazazi wawili na kuwatii katika kila kitu isipokuwa katika lile ambalo haliridhii Mwenyezi Mungu Mtukufu; kwani hakuna kumtii kiumbe kwa kumuasia muumba.

Tumelizungumzia kwa ufafanuzi hilo katika Juz. 15 (17:23). Na katika vitabu vya Hadith, kuna kisa kinachofahamisha kuwa kuwatendea wema wazazi wawili kunanufaisha wakati wa shida na pia kwamba dua bora ya kumwelekea Mwenyezi Mungu wakati wa shida ni matendo mema.

Imepokewa kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba watu watatu walingia kwenye pango lililokuwa njiani, wakalala humo. Likaanguka jiwe kubwa kutoka mlimani likawazibia mlango. Baada ya kufikiria sana hawakupata njia isipokuwa kuelekea kwenye dua kumuomba Mwenyezi Mungu peke yake awaokoe na maangamizi haya.

Kisha akakumbuka kila mmoja tendo jema alilolitenda: Wa kwanza, akakumbuka jinsi alivyowatendea wema wazazi wake wawili na kuwapatia raha. Basi jiwe likasogea kidogo. Wa pili akakumbuka kumtekelezea haja mwanamke aliyekuwa na dharura bila ya kufanya naye tendo chafu. Jiwe likasogea tena. Wa tatu akasema kuwa alikuwa na mfanyakazi aliyeondoka bila ya kuchukua mshahara wake. Ule mshahara akauhifadhi na ukazaa, ukawa na wanyama wengi sana, basi akampa mshahara wake na ile ziyada. Hapo jiwe likamalizika kufunguka na wakatoka kwenye pango.

Riwaya hii iwe ni sahihi au la, lakini kisa kinauelezea Uislamu na uhakika wake, kwa sababu unadhibiti njia ya uokovu duniani na akhera kwa matendo mema, sio kwa kauli na kujionyesha.

Na wale ambao wameamini na wakatenda mema, kwa hakika tutawaingiza katika wema.

Unaweza kuuliza : Kuna tofauti gani kati ya Aya hii na ile iliyotangulia, isemayo: Na wale ambao wameamini na wakatenda mema, kwa hakika tutawaondolea maovu yao, na tutawalipa mazuri ya waliyokuwa wakiyatenda?

Jibu : Kuingizwa katika kundi la watu wema; kama vile mashahidi na mawalii, ni daraja ya juu zaidi sana kuliko kusamehewa na kulipwa. Ni sawa na kumwambia aliyefanya uovu kisha akatengenea na kuwa mwenye ikhlasi: Nimekusamehe na nitakufanyia wema fulani. Zaidi ya hayo nitakuweka kwenye idadi ya wateuliwa walio bora.

وَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ آمَنَّا بِاللَّـهِ فَإِذَا أُوذِيَ فِي اللَّـهِ جَعَلَ فِتْنَةَ النَّاسِ كَعَذَابِ اللَّـهِ وَلَئِن جَاءَ نَصْرٌ مِّن رَّبِّكَ لَيَقُولُنَّ إِنَّا كُنَّا مَعَكُمْ أَوَلَيْسَ اللَّـهُ بِأَعْلَمَ بِمَا فِي صُدُورِ الْعَالَمِينَ ﴿١٠﴾

10. Na katika watu kuna wanaosema: Tumemwamini Mwenyezi Mungu, lakini wanapoudhiwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu wanayafanya maudhi ya watu kama ni adhabu ya Mwenyezi Mungu. Na itakapokuja nusra kutoka kwa Mola wako lazima watasema: Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi. Kwani Mwenyezi Mungu hayajui yaliyomo vifuani mwa walimwengu?

وَلَيَعْلَمَنَّ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَلَيَعْلَمَنَّ الْمُنَافِقِينَ ﴿١١﴾

11. Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha wale ambao wameamini na kwa yakini atawatambulisha wanafiki.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا اتَّبِعُوا سَبِيلَنَا وَلْنَحْمِلْ خَطَايَاكُمْ وَمَا هُم بِحَامِلِينَ مِنْ خَطَايَاهُم مِّن شَيْءٍ إِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿١٢﴾

12. Na wale ambao wamekufuru waliwaambia walioamini: Fuateni njia yetu nasi tutayabeba makosa yenu. Wala wao hawatabeba katika makosa yao chochote kile. Hakika hao ni waongo.

وَلَيَحْمِلُنَّ أَثْقَالَهُمْ وَأَثْقَالًا مَّعَ أَثْقَالِهِمْ وَلَيُسْأَلُنَّ يَوْمَ الْقِيَامَةِ عَمَّا كَانُوا يَفْتَرُونَ ﴿١٣﴾

13. Na kwa hakika wataibeba mizigo yao na mizigo mingine pamoja na mizigo yao, na kwa hakika wataulizwa siku ya Kiyama juu ya waliyoyazua.

KATIKA WATU KUNA WANAOSEMA, TUMEAMINI

Aya 10 – 13

IMANI AU SARABI?

MAANA

Na katika watu kuna wanaosema: Tumemwamini Mwenyezi Mungu. Lakini wanapoudhiwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu wanayafanya maudhi ya watu kama ni adhabu ya Mwenyezi Mungu.

Aya hii inaleta picha ya uhakika ya baadhi ya watu tunaowajua na kuishi nao. Shetani amewapambia watu hawa kwa hila na wasiwasi wake, mpaka wakamsadiki, wakajiona ni katika watu wa takua na imani; kumbe hawaitakidi wala kuona kitu chochote isipokuwa manufaa na masilahi yao.

Hakuna kitu kinachofahamisha zaidi kuwa imani zao ni njozi na sarabi, kuliko kule kuhofia kwao watu japo kwa kitu kidogo tu. Wanawahofia itakapodhihiri haki na usawa kwa kauli au kwa vitendo; sawa na mawalii na wenye takua wanavyomhofia Mwenyezi Mungu.

Imetangulia ishara ya kundi hili katika Aya isemayo:

فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيْهِمُ الْقِتَالُ إِذَا فَرِيقٌ مِّنْهُمْ يَخْشَوْنَ النَّاسَ كَخَشْيَةِ اللَّـهِ أَوْ أَشَدَّ خَشْيَةً ﴿٧٧﴾

“Walipolazimishwa kupigana, mara kundi moja katika wao wakawaogopa watu kama kumwogopa Mwenyezi Mungu au kwa hofu zaidi.” Juz. 5 (4:77).

Huko nyuma tulisema kuwa hakuna yoyote anayeifuata haki ila ataitolea thamani kwa nafsi yake na vitu vyake. Vinginevyo watu wa haki na wanaoinusuru, wasingekuwa na ubora wowote. Tazama Juz. 2 (2: 153 – 157), kifungu cha ‘Thamani ya Pepo.’

Kuna Hadith isemayo: “Mwenye kumwogopa Mwenyezi Mungu huogopewa na kila kitu, na asiyemwogopa Mwenyezi Mungu haogopewi na chochote.”

Na itakapokuja nusra kutoka kwa Mola wako lazima watasema: Hakika sisi tulikuwa pamoja nanyi.

Wao wako pamoja na dini ikiwa ni biashara yenye masilahi, na wao ni maadui wa dini ikiwa itawataka wajitolee muhanga japo kidogo. Kauli fasaha zaidi katika maana haya ni ile ya Bwana wa mashahidi, Husein bin Ali(a.s) pale aliposema:“Watu ni watumwa wa dunia na dini wameilamba kwa ndimi zao tu, inachukulika yanapokuwa mazuri maisha yao. Wapatwapo na misukosuko, wenye dini wanakuwa wachache.”

Umetangulia mfano wake katika Juz. 5 (4:141).

Kwani Mwenyezi Mungu hayajui yaliyomo vifuani mwa walimwengu?

Mnataka kumhadaa Mwenyezi Mungu na kumfanyia hila na yeye ni mjuzi wa mnayoficha na mnayoyadhihirisha?

Kwa yakini Mwenyezi Mungu atawatambulisha wale ambao wameamini na kwa yakini atawatambulisha wanafiki.

Umetangulia mfano wake katika Aya 3 ya sura hii na Juz. 4 (4:154).

Na wale ambao wamekufuru waliwaambia walioamini: Fuateni njia yetu nasi tutayabeba makosa yenu.

Washirikina wa Makka waliwaambia wale walioitikia mwito wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) : Vipi mnamfuata Muhammad na kuvumilia mengi kwa ajili yake? Mwacheni na mrudi kwenye dini yetu. Ikiwa mnahofia adhabu ya Mwenyezi Mungu baada ya mauti, kama anavyowahofisha Muhammad, basi sisi tutawabebea. Walisema hivi wakikusudia kuwa ufufuo baada ya mauti ni porojo.

Wala wao hawatabeba katika makosa yao chochote kile. Hakika hao ni waongo.

Kwa sababu kila mtu atalipwa kwa matendo yake, hatabeba mzigo wa wengine au kuulizwa kwa niaba yake:

قُل لَّا تُسْأَلُونَ عَمَّا أَجْرَمْنَا وَلَا نُسْأَلُ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢٥﴾

“Sema: hamtaulizwa kwa makosa tuliyoyafanya, wala sisi hatutaulizwa kwa mnayoyatenda nyinyi.” (34:25).

Na kwa hakika wataibeba mizigo yao na mizigo mingine pamoja na mizigo yao.

Kila anayempoteza mwingine atabeba dhambi zake na dhambi za kupoteza; kwa sababu amesababisha kupatikana upotevu na kuenea. Ama yule anayemfuata mpotevu atabeba dhambi zake bila ya kupungua, kwa sababu aliitikia upotevu kwa hiyari yake.

Kwa maneno mengine ni kuwa mpotezaji ana dhambi mbili: Moja kwa upotevu wake na nyingine ni kwa kupoteza. Na mfuasi ana dhambi moja ya kupotea kwa hiyari yake.

Na kwa hakika wataulizwa siku ya Kiyama juu ya waliyoyazua ya kudai kwao kuwa Mwenyezi Mungu ana mshirika, kusema kwao kuwa Mtume(s.a.w.w) ni mchawi, kuwaambia waumini kuwa watawabebea dhambi zao n.k.

وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوْمِهِ فَلَبِثَ فِيهِمْ أَلْفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمْسِينَ عَامًا فَأَخَذَهُمُ الطُّوفَانُ وَهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٤﴾

14. Na hakika tulimtuma Nuhu kwa kaumu yake, akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini. Basi tufani iliwachukua hali ya kuwa wao ni madhalimu.

فَأَنجَيْنَاهُ وَأَصْحَابَ السَّفِينَةِ وَجَعَلْنَاهَا آيَةً لِّلْعَالَمِينَ ﴿١٥﴾

15. Tukamwokoa yeye na watu wa safina na tukaifanya kuwa ni ishara kwa walimwengu wote.

NUH

Aya 14 – 15

MAANA

Na hakika tulimtuma Nuhu kwa kaumu yake, akakaa nao miaka elfu kasoro miaka hamsini. Basi tufani iliwachukua hali ya kuwa wao ni madhalimu. Tukamwokoa yeye na watu wa safina na tukaifanya kuwa ni ishara kwa walimwengu wote.

Dhahiri ya Aya inafahamisha kwa uwazi kuwa Nuhu aliishi miaka 950 na akili hailikitai hilo. Kwa hiyo ni wajibu kulisadiki. Ama kutafuta visababu kwamba siku hizo watu walikuwa wachache ndio maana umri ukarefushwa, kama walivyosema baadhi ya wafasiri, hilo haifai kulitegemea katika kufasiri wahyi.

Katika Kamusi ya Kitabu Kitakatifu imeelezwa kuwa jina la Nuhu ni Samiy na maana yake ni raha na baba yake ndiye aliyemuita hivyo.

Lakini ni lazima ieleweke kuwa jina Samiy linatokana na Sam bin Nuhu, sasa vipi mzazi anasibishwe kwa mwana? Na katika Uk. 448 wa kamusi hiyo hiyo imeelezwa kuwa Sam ni mtoto wa Nuhu na kwamba alizaliwa akiwa Nuhu ana miaka 500. Kamusi haikuasharia tarehe ya wakati wa Nuhu; pengine ni kwa kukosekana rejea. Yametangulia maneno kuhusu Nuhu(a.s) katika Aya kadha; zikiwemo: Juz. 8 (7:59 – 64) na Juz.12 (11:25 – 26).

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI

وَإِبْرَاهِيمَ إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ اعْبُدُوا اللَّـهَ وَاتَّقُوهُ ذَٰلِكُمْ خَيْرٌ لَّكُمْ إِن كُنتُمْ تَعْلَمُونَ ﴿١٦﴾

16. Na Ibrahim pale alipowaambia watu wake: Muabuduni Mwenyezi Mungu na mcheni Yeye. Hayo ni kheri kwenu ikiwa mnajua.

إِنَّمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَوْثَانًا وَتَخْلُقُونَ إِفْكًا إِنَّ الَّذِينَ تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ لَا يَمْلِكُونَ لَكُمْ رِزْقًا فَابْتَغُوا عِندَ اللَّـهِ الرِّزْقَ وَاعْبُدُوهُ وَاشْكُرُوا لَهُ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿١٧﴾

17. Hakika nyinyi mnaabudu masanamu kinyume na Mwenyezi Mungu na mnazua uzushi. Hakika mnao waabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu hawamilikii riziki yoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu na mumwabudu na mumshukuru; kwake mtarudishwa.

وَإِن تُكَذِّبُوا فَقَدْ كَذَّبَ أُمَمٌ مِّن قَبْلِكُمْ وَمَا عَلَى الرَّسُولِ إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿١٨﴾

18. Na kama mkikadhibisha basi zimekwisha kadhibisha umma kabla yenu. Na si juu ya Mtume ila kufikisha.

IBRAHIM

Aya 16 – 18

MAANA

Na Ibrahim pale alipowaambia watu wake: Muabuduni Mwenyezi Mungu na mcheni Yeye. Hayo ni kheri kwenu ikiwa mnajua. Hakika nyinyi mnaabudu masanamu kinyume na Mwenyezi Mungu na mnazua uzushi. Hakika mnaowaabudu kinyume cha Mwenyezi Mungu hawamilikii riziki yoyote. Takeni riziki kwa Mwenyezi Mungu na mumwabudu na mumshukuru; kwake mtarudishwa. Na kama mkikadhibisha basi zimekwisha kadhibisha umma kabla yenu. Na si juu ya Mtume ila kufikisha.

Hakika mwito wa Ibrahim(a.s) ni mwito wa kila Nabii – Ikhlasi katika kila jambo na kuiondoa shirki kwa sura zake zote, kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ndiye mwanzilishi na ndiye mrejeshaji; mkononi mwake ndio kuna madhara na manufaa. Mwenye kukadhibisha na akaukataa mwito huu atakuwa amejidhulumu nafsi yake.

Katika kamusi ya Kitabu Kitakatifu, imeelezwa kuwa Ibrahim ni mwana wa Tarih kutokana na kizazi cha Sam bin Nuhu, yeye anatoka katika mji ulio baina ya mito miwili: mto Dijla na mto Furat na kwamba yeye alikaa hapo miaka 75, kisha akahama pamoja na mkewe na Lut hadi ardhi ya Kanani. Mtungaji wa Kamusi hiyo anasema: “Haiwezekani kuainisha kwa mpangilio tarehe aliyoishi Ibrahim, lakini yeye alizaliwa, kulingana na tarehe aliyoielezea Ashir, kuwa ni kwenye mwaka 1996 kabla ya Kuzaliwa Nabii Isa.”

Yametangulia maelezo kuhusu Ibrahim katika Juz. 7 (6:74 – 84 , Juz. 16 (19:41 – 50) na Juz. 17 (21:52 – 72).

أَوَلَمْ يَرَوْا كَيْفَ يُبْدِئُ اللَّـهُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ إِنَّ ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ ﴿١٩﴾

19. Je, hawaoni jinsi Mwenyezi Mungu anavyoanzisha uumbaji na kisha akaurudisha. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni rahisi.

قُلْ سِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَانظُرُوا كَيْفَ بَدَأَ الْخَلْقَ ثُمَّ اللَّـهُ يُنشِئُ النَّشْأَةَ الْآخِرَةَ إِنَّ اللَّـهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٢٠﴾

20. Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyoanzisha kuumba, kisha Mwenyezi Mungu ndiye atakayeumba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu.

يُعَذِّبُ مَن يَشَاءُ وَيَرْحَمُ مَن يَشَاءُ وَإِلَيْهِ تُقْلَبُونَ ﴿٢١﴾

21. Humwadhibu amtakaye, Na humrehemu amtakaye; na kwake mtapelekwa.

وَمَا أَنتُم بِمُعْجِزِينَ فِي الْأَرْضِ وَلَا فِي السَّمَاءِ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ اللَّـهِ مِن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ ﴿٢٢﴾

22. Wala nyinyi si wenye kushinda ardhini wala mbinguni. Wala hamna mlinzi wala msaidizi isipokuwa Mwenyezi Mungu.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا بِآيَاتِ اللَّـهِ وَلِقَائِهِ أُولَـٰئِكَ يَئِسُوا مِن رَّحْمَتِي وَأُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢٣﴾

23. Na wale ambao wamezikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu na kukutana naye. Hao wamekata tamaa na hao watakaopata adhabu chungu.

فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوْمِهِ إِلَّا أَن قَالُوا اقْتُلُوهُ أَوْ حَرِّقُوهُ فَأَنجَاهُ اللَّـهُ مِنَ النَّارِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٢٤﴾

24. Basi halikuwa jawabu la watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto! Mwenyezi Mungu akamwokoa na moto. Hakika katika halo kuna ishara kwa watu wanaoamini.

وَقَالَ إِنَّمَا اتَّخَذْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ أَوْثَانًا مَّوَدَّةَ بَيْنِكُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا ثُمَّ يَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُ بَعْضُكُم بِبَعْضٍ وَيَلْعَنُ بَعْضُكُم بَعْضًا وَمَأْوَاكُمُ النَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّاصِرِينَ ﴿٢٥﴾

25. Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi baina yenu katika maisha ya dunia. Kisha siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi na mtalaniana nyinyi kwa nyinyi. Na makazi yenu ni motoni wala hamtapata wa kuwanusuru.

فَآمَنَ لَهُ لُوطٌ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّي إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ {26 }

26. Akamwamini Lut na akasema: Hakika mimi ninahamia kwa Mola wangu. Hakika Yeye ni mwenye nguvu mwenye hekima.

وَوَهَبْنَا لَهُ إِسْحَاقَ وَيَعْقُوبَ وَجَعَلْنَا فِي ذُرِّيَّتِهِ النُّبُوَّةَ وَالْكِتَابَ وَآتَيْنَاهُ أَجْرَهُ فِي الدُّنْيَا وَإِنَّهُ فِي الْآخِرَةِ لَمِنَ الصَّالِحِينَ ﴿٢٧﴾

27. Na tulimtunukia yeye Is-haq na Ya’qub na tukajaalia katika kizazi chake Unabii na Kitabu na tukampa ujira wake katika dunia. Naye hakika katika Akhera, bila shaka atakuwa katika wema.

MWENYEZI MUNGU NDIYE MWANZILISHI NA MRUDISHAJI

Aya 19 – 27

MAANA

Je, hawaoni jinsi Mwenyezi Mungu anavyoanzisha uumbaji na kisha akaurudisha. Hakika hayo kwa Mwenyezi Mungu ni rahisi.

Maana ya hawaoni ni hawajui. Maana yanafupika kwa kauli ya Imam Ali(a.s) :“Namstaajabu anayepinga uumbaji wa mwisho naye anaona uuum- baji wa kwanza.”

Wajihi wa kuungana maumbo haya mawili ni kwa kisababishi ambacho ni uweza wa aliyeyafanya. Kwani aliyeweza kukifanya kitu bila ya kuweko kitu, vile vile anaweza kukifanaya baada ya kutawanyika; bali huko kukufanya ni kwepesi zaidi. Tunasema hivi tukijua kuwa kwa Mwenyezi Mungu hakuna jepesi wala zito, na kwamba yeye anafanya kikubwa na kidogo kwa neno ‘Kuwa.’ Maelezo haya tumeyakariri kwa kukaririka Aya. Angalia Juz.1 (2:28 – 29), Juz. 5 (4:85 – 87) na Juz. 13 (13:5 – 7).

QUR’AN NA FIKRA

Sema: Tembeeni katika ardhi na tazameni jinsi alivyoanzisha kuumba, kisha Mwenyezi Mungu ndiye atakayeumba umbo la baadaye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Muweza juu ya kila kitu.

Qur’an imekataza kuiga na ikaamrisha kufanya utafiti na uchunguzi. Imewasifu wataalamu na wenye kufanya jitihada. Hakuna mwenye shaka kwamba utafiti na uchunguzi ni katika alama za uhai na njia ya kuuen- deleza na kutatua matatizo yake, ikiwa utafiti na uchunguzi utaambatana na subira na kuamua kufikia kwenye malengo hata kama kutakuwa na vikwazo vya namna gani.

Subira na imani inashinda nguvu zote. Binadamu wa zama hizi ameamua kufika mwezini; akajitahidi na akafanya bidii mpaka akakanyaga kwenye uso wa mwezi kwa unyayo wake. Kesho au kesho kutwa atakanyaga mirikh na sayari nyinginezo.

Kwa hiyo, hakuna nguvu isiyoshindwa na binadamu isipokuwa nguvu ya muumba tu. Ndio maana ikasemwa: hakuna zaidi ya binadamu isipokuwa muumba wake.

Kama mtu ataniuliza: Ni kiwango gani cha binadamu? Nitamjibu: Kiwango chake ni kuwa hakuna kiwango cha nguvu zake na maandalizi yake. Ujinga na kuiga ndiko kunakoingilia kati baina ya mtu na mkabala wake na kumtenganisha na nafsi yake na uhalisi wake.

Ndio maana Qur’an ikaharamisha kuiga na kuamrisha kuchunguza na kufuata akili katika hukumu zake zote na kukupa jina la nuru uongofu na dalili.

Unaweza kuuliza : Ni kweli Qur’an imekataza kuiga na kuamrisha kufanya utafiti na uchunguzi, pia ikawasifu wataalamu.

Lakini mfumo au sababu iliyowajibisha kushuka Aya inayohusiana na maudhui haya inafahamisha wataalamu wa dini ndio waliosifiwa kuwa watu wa elimu ya Mwenyezi Mungu na kujua halali yake na haramu yake na kwamba Yeye ameamrisha kuchunguza na kufikiri katika kuumbwa vilivyoko ili mtu aishilie kwa hilo kwenye imani ya Mungu na Siku ya Mwisho, aweze kufuzu kwa kupata pepo na neema zake na kuokoka na moto na ukali wake.

Mfano mzuri wa hayo ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ ﴿٦٣﴾ أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ ﴿٦٤﴾ لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ ﴿٦٥﴾

“Je, mmeona mnayolima. Je, nyinyi mmeiotesha au tumeiotesha sisi? Lau tungelitaka tungeifanya makapi mkabaki mnastaajabu.” (56:63 – 65).

Ni mwenye akili gani atakayeweza kusema kuwa Aya hii inahimiza elimu ya kilimo?

Jibu :Kwanza : kuna Aya zilizobariki na kusifu kila linalowanufaisha watu; kama vile kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَأَمَّا مَا يَنفَعُ النَّاسَ فَيَمْكُثُ فِي الْأَرْضِ ﴿١٧﴾

“Ama povu linakwenda bure; ama kinachowafaa watu hukaa kwenye ardhi.” Juz. 13 (13:17).

Hakuna kitu kinachowafaa zaidi watu kama elimu; bali hakuna maisha bila elimu katika zama hizi. Zaidi ya hayo kuna Aya kadhaa zinazohimiza kufanya amali njema na kuwazingatia watendaji wake kuwa ni viumbe bora. Mwenyezi Mungu anasema:

إِنَّ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ هُمْ خَيْرُ الْبَرِيَّةِ ﴿٧﴾

“Hakika wale ambao wameamini na wakatenda mema, hao ndio bora ya viumbe” (98:7)

Na elimu inajitokeza kuwa ni katika matendo mema.

Pili : Ni kweli kuwa sababu za kushuka Aya zilizoamrisha utafiti na uchunguzai au nyingi katika hizo ni kumrudi yule anayemkufuru Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, lakini sababu ya kushuka hailifungi neno na sababu hiyo hiyo peke yake.

Tatu : Elimu yenye manufaa ni nzuri katika mtazamo wa akili. Ndio, elimu ina daraja mbali mbali, zinazopimwa kutokana na faida na manufaa yake.

Elimu ya sharia ya kiislamu na sharia yake ndiyo iliyo na manufaa zaidi kidunia na akhera. Kidunia ni kwa kuwa inaelekeza kila kitu kwenye heri ya watu na masilahi yao. Ama kiakhera, hiyo ndio njia ya kuokoka na hasira za Mwenyezi Mungu na adhabu yake.

Ndio maana waislamu wakamwita mwanachuoni wa kidini: ‘Mwanachuoni huru’ na ‘Mwanachuoni aliyefungwa’ kuwa ni yule wa kidunia.

Nne : wameafikiana mafakihi wa kiislamu kwa kauli moja kwamba kila elimu inayohitajika katika maisha basi ni wajib kifaya.

Kuna hadith isemayo: “ Hakuna Mwislamu yoyote aliyepanda mti au kupanda mbegu, akala humo ndege au mnyama au mtu, ila huwa ni kama sadaka, “Tafuteni elimu katika machimbuko yake ya kidini na kidunia” na “Tafuteni elimu hata kama ni China.”

Kimsingi ni kuwa elimu ya dini inatafutwa katika Kitabu na Sunna sio China!

Humwadhibu amtakaye, katika wanaostahiki adhabu,Na humrehemu amatakaye, katika wanaostahiki rehema.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu ni mwadilifu na hakimu, atailipa kila nafsi iliyoyachuma.

Na kwake mtapelekwa . Mtarudishwa siku ya Kiyama kwa hisabu na malipo.

Wala nyinyi si wenye kushinda ardhini wala mbinguni.

Yaani wala aliyeko mbinguni. Katika Nahjul-balagha imeelezwa: “Hamshindi anayemtafuta wala hamponyoki anayemkimbia.”

Wala hamna mlinzi wala msaidizi isipokuwa Mwenyezi Mungu.

Hakuna wa kuzuia hukumu yake wala kumkimbia.

Na wale ambao wamezikanusha Ishara za Mwenyezi Mungu na kukutana naye. Hao wamekata tamaa na hao watakaopata adhabu chungu.

Kukata tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu ni natija ya kumkana Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho na malipo ya mwenye kukata tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu, kwa ukafiri na inadi, ni kuonja adhabu ya kuungua.

Basi halikuwa jawabu la watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto! Mwenyezi Mungu akamwokoa na moto.

Zinarudi simulizi za Ibrahim(a.s) na sera yake pamoja na watu wake ambao walijaribu kuepukana naye na mwito wake kwa kumuua au kumchoma.

Haya ndio mantiki ya mataghuti kila wakati na mahali. Wanashindwa na hoja wazi basi wanahofia vyeo vyao. Kwa hiyo wanakuwa hawana jingine isipokuwa dhulma waliyo nayo. Hapo wanaanza kutoa amri ya: Wafungeni, waadhibuni, wanyang’anyeni mali, vunjeni majumba, nyongeni, chomeni n.k.

Hapa ndio unaingia uokovu wa Mwenyezi Mungu. Unaweza kuwa ni kwa kuokoka mdhulumiwa kutoka mikononi mwa dhalimu, kuadhibiwa dhalimu na Mwenyezi Mungu au kupitia kwa wanamapinduzi, wakombozi. Umepita mfano wake katika Juz. 17 (21:68).

Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wanaoamini.

Yaani wanaonufaika na maonyo, kuwaidhika na mazingatio, kuitafuta haki kwa ajili ya haki ili waiamini na kutenda kwa ikhlasi.

Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Mwenyezi Mungu kwa mapenzi baina yenu katika maisha ya dunia.

Ibrahim aliwaambia watu kuwa nyinyi mnayaabudu haya masanamu mkiwa na yakini kuwa hayadhuru wala hayanufaishi, lakini mmeyatukuza kwa kuwaiga mnaowapenda katika maisha haya na kesho haya mapenzi yatabadilika kuwa uadui na chuki.

Kisha siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi.

Imam Ali(a.s) anasema:“Mfuatwa atajitenga na mfuasi, na kiongozi na muongozwa; watafarikiana kwa chuki na watalaaniana wakati wa kukutana.”

Na makazi yenu ni motoni wala hamtapata wa kuwanusuru.

Huu ndio mwisho wa kila mwenye kuipinga haki awe mfuasi au mwenye kufuatwa.

Akamwamini Lut na akasema: “Hakika mimi ninahamia kwa Mola wangu. Hakika Yeye ni mwenye nguvu mwenye hekima.”

Lut ni mtoto wa nduguye Ibrahim. Kundi katika wafasiri wamesema: “Hakuongoka yoyote katika kaumu ya Ibrahim au kumwamini isipokuwa Lut peke yake.” Yakushangaza ni yale yaliyoandikwa katika Biblia Mwanzo: (19:30 – 38)

Imeelezwa kuwa mabinti wawili wa Lut walimlewesha baba yao pombe, wakalala naye na wakashika mimba. Mkubwa akazaa mtoto wa kiume aliyemwita Moabu na mdogo pia akazaa mtoto wa kiume aliyemwita Binamu.

Na tulimtunukia Is-ahq na Ya’qub na tukajaalia katika kizazi chake Unabii na Kitabu na tukampa ujira wake katika dunia. Naye hakika katika Akhera, bila shaka atakuwa katika wema.

Aliyetunukiwa ni Ibrahim(a.s) . Aya hii ni dalili ya wazi kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakutuma mtume baada yake ila anatokana na uti wake wa mgongo.

Tukiiunganisha Aya hii na Hadith isemayo: “Jambo hili liko kwa makuraish... Watu wanawafuata makuraishi Maimamu ni katika makraishi...” tunapata natija ya kuwa mitume wote na maimamu wanatokana na kizazi cha Ibrahim. Kwa sababu nasaba ya Kuraishi inakomea kwake.

Umepita mfano wake katika Juz. 16 (19: 49) na Juz. 17 (21: 72 - 73).

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

وَلَمَّا دَخَلُوا عَلَىٰ يُوسُفَ آوَىٰ إِلَيْهِ أَخَاهُ قَالَ إِنِّي أَنَا أَخُوكَ فَلَا تَبْتَئِسْ بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٦٩﴾

69. Walipoingia kwa Yusuf alimkumbatia ndugu yake akasema: Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.

فَلَمَّا جَهَّزَهُم بِجَهَازِهِمْ جَعَلَ السِّقَايَةَ فِي رَحْلِ أَخِيهِ ثُمَّ أَذَّنَ مُؤَذِّنٌ أَيَّتُهَا الْعِيرُ إِنَّكُمْ لَسَارِقُونَ ﴿٧٠﴾

70. Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: “Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.”

قَالُوا وَأَقْبَلُوا عَلَيْهِم مَّاذَا تَفْقِدُونَ ﴿٧١﴾

71. Wakasema na hali wamewaelekea: “Mmepoteza nini?”

قَالُوا نَفْقِدُ صُوَاعَ الْمَلِكِ وَلِمَن جَاءَ بِهِ حِمْلُ بَعِيرٍ وَأَنَا بِهِ زَعِيمٌ ﴿٧٢﴾

72. Wakasema: “Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

قَالُوا تَاللَّـهِ لَقَدْ عَلِمْتُم مَّا جِئْنَا لِنُفْسِدَ فِي الْأَرْضِ وَمَا كُنَّا سَارِقِينَ ﴿٧٣﴾

73. Wakasema: “Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi si wezi.”

قَالُوا فَمَا جَزَاؤُهُ إِن كُنتُمْ كَاذِبِينَ ﴿٧٤﴾

74. Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

قَالُوا جَزَاؤُهُ مَن وُجِدَ فِي رَحْلِهِ فَهُوَ جَزَاؤُهُ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الظَّالِمِينَ ﴿٧٥﴾

75. Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.”

فَبَدَأَ بِأَوْعِيَتِهِمْ قَبْلَ وِعَاءِ أَخِيهِ ثُمَّ اسْتَخْرَجَهَا مِن وِعَاءِ أَخِيهِ كَذَٰلِكَ كِدْنَا لِيُوسُفَ مَا كَانَ لِيَأْخُذَ أَخَاهُ فِي دِينِ الْمَلِكِ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ نَرْفَعُ دَرَجَاتٍ مَّن نَّشَاءُ وَفَوْقَ كُلِّ ذِي عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴿٧٦﴾

76. Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake, Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme, isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu, Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao, Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi.

MIMI NI NDUGUYO, USIHUZUNIKE

Aya 69-76

Maana

Walipoingia kwa Yusuf, alimkumbatia ndugu yake akasema: “Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.”

Watu wa tafsiri akiwemo Tabari, Razi, Tabrasi na Abu Hayani al-andalusi, wametaja ufafanuzi wa Aya hii ambao hauna dalili katika Qur’an, lakini unaoana nayo na kunasibiana nayo. Kwa ajili hii tutafupiliza kauli zao, kama ifuatavyo:

Ndugu wa Yusuf walipofika Misr aliwaalika kwenye chakula na akawaweka wawili wawili, kwa lengo la kuwa yeye abakie na ndugu yake Bin-yamin akae naye kwenye meza yake ya chakula; sawa na alivyofanya Muhammad(s.a.w.w) baina ya maswahaba zake wawili wawili kuwa ndugu na akambakisha Ali awe wake yeye.

Baada ya chakula, Yusuf aliwapangia vyumba vya kulala wawili wawili na ndugu yake Bin-yamini akalala naye chumba kimoja. Walipokuwa peke yao akamwambia: “Je, unapenda mimi niwe ndugu yako?” Akamjibu ni nani anaweza kuwa na ndugu mfano wako? Lakini wewe hukuzaliwa na Ya’qub wala Rahel. Basi akamkumbatia na kumwambia: “Mimi nimezaliwa na Ya’qub na Rahel. Basi mimi ni ndugu yako, Wala usuhuzunike na waliyotufanyia ndugu zetu.” Bin-Yamin akafurahi sana na akamshukuru Mwenyezi Mungu.

Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.

Yusuf alitaka kumtenga Bin-yamin na ndugu zake na kubaki naye, lakini hakuwa na njia ila kufanya ujanja. Katika sharia ya watu wa Ya’qub ni mwizi kufanywa mtumwa. Ndio watumishi wakaweka chombo cha kupimia kwenye mzigo wa Bin-yamin, kwa amri ya Yusuf. Akanadi mnadi kuwa nyinyi wana wa Ya’qub! Ni wezi, kwa hiyo msiendelee na msafara hadi tuangalie mambo yenu.

Wakashangaa watoto wa Ya’qub kwa mshtukizo huu.

Wakasema na hali wamewaelekea: Mmepoteza nini?

Walisema hivi wakiwa na yakini kuwa hawana hatia yoyote. Na hii ni mara yao ya kwanza kusikia tuhuma hii.

Wakasema watumishi wa Yusuf:

Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

Mdhamini huyu ndiye aliyewaambia nyinyi ni wezi, kama walivyosema wafasiri, na akadhamini kwa sharti ya kuwa mtu aliye na hicho chombo akirudishe yeye mwenyewe.

Aya hii inaingia kwenye milango miwili ya Fiqh: Jaala, ambayo ni kutangaza zawadi kwa atakayeleta kilichopotea na Dhamana ambayo ni kutekeleza ahadi; kama vile kauli ya alisema: ‘Na mimi ni mdhamini.’ Yaani nadhamini kutekeleza ahadi ya shehena ya ngamia, Kuna hadithi isemayo: “Mdhamini ni mwenye kugharimika.”

Wakasema watoto wa Ya’qub:Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi sio wezi.

Walibishana wakajadiliana na kuleta hoja za kutokuwa na hatia na usafi wao; miongoni mwa waliyoyasema ni: Vipi mnatutuhumu na mnajua nasabu yetu na sera yetu katika safari yetu ya kwanza na hii ya pili kwamba hatukuja kufanya ufisadi au hiyana; isipokuwa tumekuja kuwanunulia chakula watu wetu.

Kwenye tafsiri nyingi imeelezwa kuwa watoto wa Ya’qub, kwenye safari yao ya kwanza, walipokuta bidha zao zimerudishwa walidhani kuwa zimesahaulika, kwa hiyo hawakuzitumia, bali walizirudisha Misr. Kwa hiyo wakawa mashuhuri kwa wema na uamnifu wao.

Kauli hii ya wafasiri haiku mbali; bali inaashiria kauli ya watoto wa Ya’qub: Wallah mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya uharibifu katika nchi hii

Unaweza kuuliza : Imekuwaje kwa Yusuf kufanya njama hizi za kuwaelekezea tuhuma ndugu zake na hali anajua kuwa hawana hatia?

Jibu : Kwanza, tukio hili ni maalum, lina sababu zake, haifai kulipima na matukio mengine. Pili, aliyelengwa na tuhuma za wizi ni Bin-yamin, ndugu wa Yusuf kwa baba na mama, na hilo lilikuwa kwa makubaliano yao na kuridhika kwake, kwa hekima iliyotaka hivyo; wakati huohuo hilo halipingi msingi wowote katika misingi ya sharia; kama vile kuhalalisha haramu au kuharamisha halali.

Zaidi ya hayo, tendo la watoto wa Ya’qub la kumtoa Yusuf kwa baba yake na kumtupa kisimani kwa lengo la kumuua ni zaidi ya wizi.

Swali la pili : Vipi Yusuf kumtenganisha nduguye na baba yake na kumzidishia baba yake majonzi juu ya majonzi?

Jibu : Kila alilolifanya Yusuf lilikuwa kwa maslahi ya ndugu yake na baba yake; akiwa na uhakika kuwa baba yake atamkubalia na hata kumshukuru atakapojua uhakika wake. Na lilifanyika hilo. Kimsingi ni kuwa mambo hupimwa kwa matokeo yake sio kwa mfumo wake. Katika hali nyingine mitume hawatuhumiwi katika upande wa haki.

Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

Watumishi waliwaambia watoto wa Ya’qub ili waseme wenyewe kwamba mwizi atachukuliwa mateka au mtumwa, kama malipo ya tendo lake hilo. Ili iwe ni hoja juu yao pale Yusuf atakapomchukua ndugu yake.

Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.

Kusema ‘basi huyo ndiye malipo yake’ ni kuzidisha ufafanuzi; sawa na kusema: malipo ya muuaji ni kuuliwa, hayo ndiyo malipo yake.

Ndugu wa Yusuf walisema hiyo ndiyo sharia yetu, ambaye mtamkuta nalo mtamchukua mtumwa au mateka. Walisema hivyo wakiwa na uhakika kuwa wao hawana hatia

Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake.

Mtafutaji alianza na mizigo yao kabla ya ndugu yao madogo, ili kuificha hila. Mpaka alipoishia kwenye mzigo wa Bin-yamin akalitoa na akawaonyesha; wakapigwa na butwa na wakawa na wakati mgumu, lakini ni wapi haya na waliyomfanyia Yusuf katika giza la shimo akiwa peke yake?

Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf.

Yaani tulimpa wahyi wa mpango huu, ili ndugu zake waseme wenyewe, kuwa waziri amchukue nyara au mtumwa. Imeitwa hila kwa sababu dhahiri yake sio hali halisi; na ilijuzu kisharia, kwa sababu haikuhalalisha haramu wala kuharamisha halali.

Hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme.

Yaani sharia na hukumu ya mfalme. Maana ni kuwa lau si mipango hii ingelikuwa uzito kwa Yusuf kumchukua ndugu yake, kwa sababu sharia ya mfalme wa Misr sio kuchukua mateka, bali ni kumfunga au kupigwa, na Yusuf hakutaka kumdhuru ndugu yake. Hayo ndio makusudio ya kauli yake:

Isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu.

Kwa ufupi ni kuwa hekima ilikuwa ni kutosema Yusuf kuwa yule ni ndugu yake na wakati huo huo asipatwe na sharia ya mfalme ya kufungwa au kupigwa; bali apatwe na hukumu ya watu wa Ya’qub.

Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao Kwa elimu na utume kama tulivyomfanyia Yusuf juu ya ndugu zake.

Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi mpaka ishie kwa aliye juu zaidi.

Hiyo ni ishara kuwa ndugu wa Yusuf walikuwa ni maulama, lakini Yusuf alikuwa na elimu zaidi na mkamilifu zaidi.

قَالُوا إِن يَسْرِقْ فَقَدْ سَرَقَ أَخٌ لَّهُ مِن قَبْلُ فَأَسَرَّهَا يُوسُفُ فِي نَفْسِهِ وَلَمْ يُبْدِهَا لَهُمْ قَالَ أَنتُمْ شَرٌّ مَّكَانًا وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا تَصِفُونَ ﴿٧٧﴾

77. Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.” Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia; akasema: “Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi; na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema.

قَالُوا يَا أَيُّهَا الْعَزِيزُ إِنَّ لَهُ أَبًا شَيْخًا كَبِيرًا فَخُذْ أَحَدَنَا مَكَانَهُ إِنَّا نَرَاكَ مِنَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٧٨﴾

78. Wakasema: “Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

قَالَ مَعَاذَ اللَّـهِ أَن نَّأْخُذَ إِلَّا مَن وَجَدْنَا مَتَاعَنَا عِندَهُ إِنَّا إِذًا لَّظَالِمُونَ ﴿٧٩﴾

79. Akasema: “Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.”

فَلَمَّا اسْتَيْأَسُوا مِنْهُ خَلَصُوا نَجِيًّا قَالَ كَبِيرُهُمْ أَلَمْ تَعْلَمُوا أَنَّ أَبَاكُمْ قَدْ أَخَذَ عَلَيْكُم مَّوْثِقًا مِّنَ اللَّـهِ وَمِن قَبْلُ مَا فَرَّطتُمْ فِي يُوسُفَ فَلَنْ أَبْرَحَ الْأَرْضَ حَتَّىٰ يَأْذَنَ لِي أَبِي أَوْ يَحْكُمَ اللَّـهُ لِي وَهُوَ خَيْرُ الْحَاكِمِينَ ﴿٨٠﴾

80. Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona. Akasema mkubwa wao: “Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf? Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

KAMA AMEIBA BASI NDUGUYE PIA ALIIBA ZAMANI

Aya 77-80

MAANA

Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.

Ndugu zake Yusuf ndio waliosema hivyo, wakimkusudia Bin-yamin na Yusuf. Hizo ni tuhuma walizombadika nazo Yusuf. Hakuna ishara yoyote katika Aya yoyote kwamba Yusuf kuanzia utotoni aliwahi kuiba yai au kuku au kuiba sanamu ya babu yake mzaa mama yake, au mkanda wa shangazi yake n.k.

Lakini Qur’an imesajili waziwazi uwongo wa ndugu zake Yusuf, pale waliposema kuwa ameliwa na mbwa mwitu. Kuongezea hasadi na chuki yao iliyowapelekea kufanya waliyoyafanya. Kwa hiyo basi wao ni waongo katika kumnasibishia kwao Yusuf wizi alipokuwa mtoto.

Kusema hivi, ingawaje ni natija ya uchambuzi, lakini ndio mantiki ya sawa, au angalau ndio kauli ya karibu na maana.

Wafasiri wameichukulia kauli ya nduguze Yusuf kuwa ni ya kweli, kama kwamba uwongo unastahili. Wakawa wanafanya utafiti wa hicho alichokiiba Yusuf. Kuna aliyesema kuwa aliiba yai akampa mwenye njaa; mweingine akasema ni kuku.

Wa tatu akasema aliiba sanamu la babu yake mzaa mama yake na akalivunja. Wa nne akasema kuwa alikuwa akilelewa na shangazi yake, bint wa Is-haq, alipokuwa na baba yake, akataka kumchukua, kwa hiyo akamtuhumu kuiba mkanda wa mume wa shangazi yake ili abaki naye kama mtumwa; kwa vile adhabu ya mwizi ilikuwa ni kufanywa mtumwa.

Wafasiri wengi wako juu ya kauli hii ya mwisho, Lakini jambo la ajabu ni kuwa hakuna hata mmoja wao aliyezinduka kuwa hukumu ya watoto sio ya wakubwa katika sharia zote, Ajabu zaidi ni kauli ya baadhi ya Masufi kwamba ndugu zake Yusuf walimtuhumu na wizi wa kuiba roho ya baba yake!

Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia.

Aliapuuza maneno yao kwa upole na ukarimu; kama asemavyo mshairi: Nampitia mlaumu akinitusi Namsamehe nasema hanihusi

Akasema: Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi.

Haya aliyasema kisirisiri, kwa dalili ya kauli yake: “Wala hakuwadhihirishia.”

Na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema ya kuninasibishia wizi mimi na ndugu yangu, kwamba ni uwongo na uzushi.

Wakasema: Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

Baada ya mambo kudhihirika na kwamba hukumu ni kuchukuliwa mtumwa ndugu yao Bin-yamin, walielekea kutaka kuhurumiwa kwa kusamehewa au kuchukuliwa fidia ya mmoja wao badala yake. Walibembeleza sana kwa kutumia wema wa Yusuf na uzee wa baba yao na cheo chake na jinsi anavyompenda sana mwanawe Bin-yamin.

Walifanya hivyo sio kwa kumpenda ndugu yao, bali ni kujitoa kwenye lawama kutokana na ahadi waliyoichukua kwa baba yao.

Akasema: Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.

Yusuf alikataa ombi lao na matarajio yao na akashikilia kumchukua ndugu yake, kwa jambo ambalo Mwenyezi Mungu alitaka kulitimiza baada ya kupita mtihani na balaa.

Yusuf alitumia ibara ya ndani sana na yenye hekima ya kumwepusha ndugu yake na wizi, alposema: Yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, ambapo ndugu zake walifahamu: ‘aliyeiba mali yetu.’ Na tofauti hapo ni kubwa sana.

Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona.

Baada ya kukata tamaa watoto wa Ya’qub ya kumpata ndugu yao walijitenga ili washauriane jinsi watakavyomwambia baba yao.

Akasema mkubwa wao: Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Baadhi ya wafasiri wanasema kuwa makusudio ya mkubwa wao ni mkubwa kiakili si kimiaka. Wengine wakasema ni kiakili na kimiaka.

Kauli hii ndiyo inayokuja haraka akilini, Vyovyote iwavyo ni kwamba mkubwa huyo aliwaambia ndugu zake mtafanyaje mtakapofika kwa baba yenu bila ya Bin-yamin nanyi mliapa kuwa mtamrudisha?

Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf?

Anaashiria walivyomtupa shimoni na baba yao alivyokuwa mkali.

Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

Mkubwa wao aliamua abakie karibu na ndugu yake kwa kumwonea haya baba yake na kwamba hataondoka kwenye nchi aliyo Bin-yamin mpaka apewe idhini na baba yake au apate faraja yoyote, kutoka kwa Mwenyezi Mungui hata kama ni mauti. Muda haukuwa mrefu ikaja faraja kwa wote; kama yatakavyokuja maelezo.

ارْجِعُوا إِلَىٰ أَبِيكُمْ فَقُولُوا يَا أَبَانَا إِنَّ ابْنَكَ سَرَقَ وَمَا شَهِدْنَا إِلَّا بِمَا عَلِمْنَا وَمَا كُنَّا لِلْغَيْبِ حَافِظِينَ ﴿٨١﴾

81. Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba, na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibuu.

وَاسْأَلِ الْقَرْيَةَ الَّتِي كُنَّا فِيهَا وَالْعِيرَ الَّتِي أَقْبَلْنَا فِيهَا وَإِنَّا لَصَادِقُونَ ﴿٨٢﴾

82. Na waulize watu wa mji tuliokuwako na msafara tuliokuja nao, Na hakika sisi tunasema kweli.

قَالَ بَلْ سَوَّلَتْ لَكُمْ أَنفُسُكُمْ أَمْرًا فَصَبْرٌ جَمِيلٌ عَسَى اللَّـهُ أَن يَأْتِيَنِي بِهِمْ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ ﴿٨٣﴾

83. Akasema: “Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani. Basi subira ni njema. Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja, Hakika Yeye ni Mjuzi, Mwenye hekima.

وَتَوَلَّىٰ عَنْهُمْ وَقَالَ يَا أَسَفَىٰ عَلَىٰ يُوسُفَ وَابْيَضَّتْ عَيْنَاهُ مِنَ الْحُزْنِ فَهُوَ كَظِيمٌ ﴿٨٤﴾

84. Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf! Na macho yake yakawa meupe kwa huzuni naye akawa anaizuia.

قَالُوا تَاللَّـهِ تَفْتَأُ تَذْكُرُ يُوسُفَ حَتَّىٰ تَكُونَ حَرَضًا أَوْ تَكُونَ مِنَ الْهَالِكِينَ ﴿٨٥﴾

85. Wakasema: “Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.”

قَالَ إِنَّمَا أَشْكُو بَثِّي وَحُزْنِي إِلَى اللَّـهِ وَأَعْلَمُ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٨٦﴾

86. Akasema: “Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

يَا بَنِيَّ اذْهَبُوا فَتَحَسَّسُوا مِن يُوسُفَ وَأَخِيهِ وَلَا تَيْأَسُوا مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٧﴾

87. Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

HATUTOI USHAHIDI ILA TUNAYOYAJUA

Aya 81-87

MAANA

Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibu.

Hii ni kauli ya mkubwa wao akiwausia ndugu zake kuwa waseme ukweli kwa baba yao. Wampe habari kuwa wamewaona watumishi wa waziri wakitoa chombo cha kupimia cha mfalme katika mzigo wa Binyamin, Na kwamba waziri aling’ang’ania kumchukua, Hayo ndiyo tuliyoyashuhudia.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyo nyuma ya hayo, Na lau tungelijua ghaibuu, basi tusingemchukua wala kukupa ahadi ya kurudi naye, Tumefanya bidii sana. Tunaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na kwako.

Na waulize watu wa mji tuliokuwako.

Yaani waulize watu wa Misr, jambo hili la wizi limeenea kwao.

Na msafara tuliokuja nao.

Yaani vile vile uliza msafara tuliokuja nao kutoka Misr ambao uko jirani yako katika nchi ya Kanaan.

Na hakika sisi tunasema kweli kwa haya tunayokusimulia. Mara hii walikuwa wakisema kwa kujiamini kwa sababu walikuwa na uhakika wa wanayoyasema kinyume na mara ya kwanza walipokuja na damu ya uwongo kwenye kanzu ya Yusuf.

Akasema: Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani.

Walipomweleza baba yao aliwaambia mmefanyia vitimbi kama mlivyomfanyia ndugu yake, Yusuf.

Wafasiri wamejiuliza kuwa vipi Ya’qub aliwatuhumu wanawe kwa vitimbi kabla ya kuthibitisha na yeye ni mtume ma’asum?

Kisha wakajbu kwa njia nyingi zisizotegemea msingi wowote. Njia nzuri zaidi waliyoitaja ni ile kuwa makusudio ya Ya’qub ni kuwa nafsi zenu zimewapa picha ya kuwa Bin-yamin ni mwizi na hali yeye si mwizi.

Tuonavyo sisi ni kuwa Ya’qub aliwatuhumu na vitimbi kwa kuchukulia walivyomfanyia Yusuf, lakini yeye hakuchukulia moja kwa moja, kwa kukosa dalili ya uwongo wao. Vile vile hakuwachukulia hatua yoyote kwa dhana, Kwa sababu dhana haitoshelezi kitu.

Hiyo haipingani na cheo cha utume. Kwa sababu mtume hajui ghaibu, naye ni kama mtu mwingine anadhania na kuchukulia uwezekano. Tofauti ni kuwa kwake yeye dhana haina athari yoyote, kama afanyavyo asiyekuwa ma’sum.

Subira ni njema.

Yaani ‘subira yavuta heri, Haya aliwahi kuyasema zamani alipopotea Yusuf na sasa anayasema kwa Bin-yamin.

Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja.

Yaani Yusuf, Bin-yamin na kaka yao aliyebakia Misr karibu na ndugu yake. Neno ‘huenda‘ ni mwangaza wa matumaini; hasa likiwa linatoka kwa anayeamini ghaibu kikwelikweli; kama mitume na wasadikishao. Katika Nahjulbalagha imeelezwa: “Haiwi kweli imani ya mja mpaka yawe yaliyo kwa Mwenyezi Mungu ni ya kutegemewa zaidi kuliko yaliyo mikononi mwake” Kuna Hadith nyingi zenye maana haya.

Hakika yeye ni Mjuzi Mwenye hekima.

Anajua huzuni yangu na machungu yangu na anapanga mambo kwa hekima yake.

Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf!

Alijitenga na watu ili aomboleze peke yake, ambapo huzuni na kilio kilizidi kwa kumkosa mwanawe, Bin-yamin (Benjamin)na macho yake yakawa meupe kwa huzuni.

Yaliathirika kwa sababu ya kulia.

Naye akawa anaizuia.

Yaani anameza uchungu kwa mwili na mishipa yake.

Wakasema: Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.

Yaani wanawe walimwambia bado unamkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au ufe bure, kwa sababu Yusuf amekwenda harudi tena.

Akasema: Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu, sio kwenu kwa sababu ni udhalili na usafihi kumshtakia ambaye haondoi dhara. Imam Ali(a.s) anasema:“Allah Allah! Na kumshatakia ambaye hawezi kuondoa mashaka yenu, wala hawezi kupunguza kwa rai yake yale mliyokwishayapitisha”

Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

Yaa’qub ameteseka kwa kumkosa Yusuf, lakini wakati huo huo bado anamtegemea Mwenyezi Mungu na kumwekea dhana nzuri wala hakati tamaaa na rehema yake huku akiamini kuwa mwisho wa subra ni faraja (baada ya dhiki faraja); kama ilivyofahamisha kauli yake kuwaambia wanawe “Wala msikate tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu.”

Tukiunganisha kumtegemea kwake Mwenyezi Mungu katika ndoto ya Yusuf udogoni mwake natija ni kuwa Yaa’qub ana matumaini ya uhai wa Yusuf hadi atakapokuwa mkubwa, lakini hajui yuko wapi na ana hali gani, Yuko utumwani au kwenye uhuru, Huo ndio ulikuwa wasiwasi wake.

HAKUNA KUNGOJA MEMA YAJE YENYEWE WALA MABAYA

Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

Nendeni mkatafute wala msikate tama, Amekutanisha matumaini na kutenda. Maana yake ni kuwa. Ikiwa hakutakuwa na matendo basi Aya itakwenda kinyume; na uvivu utaambatana na kukata tamaa na yatakuwa matarajio bila ya kufanya kitu ni ujinga na upumbavu. Neno tafuteni linawajibisha kutenda kwa hisia zote dhahiri na batini.

Ndivyo alivyo mwenye akili akitokewa na janga lolote anajitahidi kuondoa visababishi vyake, ni sawa viwe ni ufisadi au uzembe.

Na anapopatwa na mazuri huhofia asijisahau akapetuka mpaka kwa utajiri au cheo kikamletea kiburi. Kwa hiyo hujikinga kwa takua:

فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

“Hawaaminishi hila ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara.” Juz. 9 (7:99).

Kwa ufupi ni kuwa mwenye kutaraji mabaya ni yule asemaye hakuna faida ya kujisumbua, na mvivu ni yule mwenye kutaraji mazuri yaje yenyewe.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

وَلَمَّا دَخَلُوا عَلَىٰ يُوسُفَ آوَىٰ إِلَيْهِ أَخَاهُ قَالَ إِنِّي أَنَا أَخُوكَ فَلَا تَبْتَئِسْ بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٦٩﴾

69. Walipoingia kwa Yusuf alimkumbatia ndugu yake akasema: Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.

فَلَمَّا جَهَّزَهُم بِجَهَازِهِمْ جَعَلَ السِّقَايَةَ فِي رَحْلِ أَخِيهِ ثُمَّ أَذَّنَ مُؤَذِّنٌ أَيَّتُهَا الْعِيرُ إِنَّكُمْ لَسَارِقُونَ ﴿٧٠﴾

70. Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: “Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.”

قَالُوا وَأَقْبَلُوا عَلَيْهِم مَّاذَا تَفْقِدُونَ ﴿٧١﴾

71. Wakasema na hali wamewaelekea: “Mmepoteza nini?”

قَالُوا نَفْقِدُ صُوَاعَ الْمَلِكِ وَلِمَن جَاءَ بِهِ حِمْلُ بَعِيرٍ وَأَنَا بِهِ زَعِيمٌ ﴿٧٢﴾

72. Wakasema: “Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

قَالُوا تَاللَّـهِ لَقَدْ عَلِمْتُم مَّا جِئْنَا لِنُفْسِدَ فِي الْأَرْضِ وَمَا كُنَّا سَارِقِينَ ﴿٧٣﴾

73. Wakasema: “Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi si wezi.”

قَالُوا فَمَا جَزَاؤُهُ إِن كُنتُمْ كَاذِبِينَ ﴿٧٤﴾

74. Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

قَالُوا جَزَاؤُهُ مَن وُجِدَ فِي رَحْلِهِ فَهُوَ جَزَاؤُهُ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الظَّالِمِينَ ﴿٧٥﴾

75. Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.”

فَبَدَأَ بِأَوْعِيَتِهِمْ قَبْلَ وِعَاءِ أَخِيهِ ثُمَّ اسْتَخْرَجَهَا مِن وِعَاءِ أَخِيهِ كَذَٰلِكَ كِدْنَا لِيُوسُفَ مَا كَانَ لِيَأْخُذَ أَخَاهُ فِي دِينِ الْمَلِكِ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ نَرْفَعُ دَرَجَاتٍ مَّن نَّشَاءُ وَفَوْقَ كُلِّ ذِي عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴿٧٦﴾

76. Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake, Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme, isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu, Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao, Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi.

MIMI NI NDUGUYO, USIHUZUNIKE

Aya 69-76

Maana

Walipoingia kwa Yusuf, alimkumbatia ndugu yake akasema: “Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.”

Watu wa tafsiri akiwemo Tabari, Razi, Tabrasi na Abu Hayani al-andalusi, wametaja ufafanuzi wa Aya hii ambao hauna dalili katika Qur’an, lakini unaoana nayo na kunasibiana nayo. Kwa ajili hii tutafupiliza kauli zao, kama ifuatavyo:

Ndugu wa Yusuf walipofika Misr aliwaalika kwenye chakula na akawaweka wawili wawili, kwa lengo la kuwa yeye abakie na ndugu yake Bin-yamin akae naye kwenye meza yake ya chakula; sawa na alivyofanya Muhammad(s.a.w.w) baina ya maswahaba zake wawili wawili kuwa ndugu na akambakisha Ali awe wake yeye.

Baada ya chakula, Yusuf aliwapangia vyumba vya kulala wawili wawili na ndugu yake Bin-yamini akalala naye chumba kimoja. Walipokuwa peke yao akamwambia: “Je, unapenda mimi niwe ndugu yako?” Akamjibu ni nani anaweza kuwa na ndugu mfano wako? Lakini wewe hukuzaliwa na Ya’qub wala Rahel. Basi akamkumbatia na kumwambia: “Mimi nimezaliwa na Ya’qub na Rahel. Basi mimi ni ndugu yako, Wala usuhuzunike na waliyotufanyia ndugu zetu.” Bin-Yamin akafurahi sana na akamshukuru Mwenyezi Mungu.

Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.

Yusuf alitaka kumtenga Bin-yamin na ndugu zake na kubaki naye, lakini hakuwa na njia ila kufanya ujanja. Katika sharia ya watu wa Ya’qub ni mwizi kufanywa mtumwa. Ndio watumishi wakaweka chombo cha kupimia kwenye mzigo wa Bin-yamin, kwa amri ya Yusuf. Akanadi mnadi kuwa nyinyi wana wa Ya’qub! Ni wezi, kwa hiyo msiendelee na msafara hadi tuangalie mambo yenu.

Wakashangaa watoto wa Ya’qub kwa mshtukizo huu.

Wakasema na hali wamewaelekea: Mmepoteza nini?

Walisema hivi wakiwa na yakini kuwa hawana hatia yoyote. Na hii ni mara yao ya kwanza kusikia tuhuma hii.

Wakasema watumishi wa Yusuf:

Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

Mdhamini huyu ndiye aliyewaambia nyinyi ni wezi, kama walivyosema wafasiri, na akadhamini kwa sharti ya kuwa mtu aliye na hicho chombo akirudishe yeye mwenyewe.

Aya hii inaingia kwenye milango miwili ya Fiqh: Jaala, ambayo ni kutangaza zawadi kwa atakayeleta kilichopotea na Dhamana ambayo ni kutekeleza ahadi; kama vile kauli ya alisema: ‘Na mimi ni mdhamini.’ Yaani nadhamini kutekeleza ahadi ya shehena ya ngamia, Kuna hadithi isemayo: “Mdhamini ni mwenye kugharimika.”

Wakasema watoto wa Ya’qub:Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi sio wezi.

Walibishana wakajadiliana na kuleta hoja za kutokuwa na hatia na usafi wao; miongoni mwa waliyoyasema ni: Vipi mnatutuhumu na mnajua nasabu yetu na sera yetu katika safari yetu ya kwanza na hii ya pili kwamba hatukuja kufanya ufisadi au hiyana; isipokuwa tumekuja kuwanunulia chakula watu wetu.

Kwenye tafsiri nyingi imeelezwa kuwa watoto wa Ya’qub, kwenye safari yao ya kwanza, walipokuta bidha zao zimerudishwa walidhani kuwa zimesahaulika, kwa hiyo hawakuzitumia, bali walizirudisha Misr. Kwa hiyo wakawa mashuhuri kwa wema na uamnifu wao.

Kauli hii ya wafasiri haiku mbali; bali inaashiria kauli ya watoto wa Ya’qub: Wallah mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya uharibifu katika nchi hii

Unaweza kuuliza : Imekuwaje kwa Yusuf kufanya njama hizi za kuwaelekezea tuhuma ndugu zake na hali anajua kuwa hawana hatia?

Jibu : Kwanza, tukio hili ni maalum, lina sababu zake, haifai kulipima na matukio mengine. Pili, aliyelengwa na tuhuma za wizi ni Bin-yamin, ndugu wa Yusuf kwa baba na mama, na hilo lilikuwa kwa makubaliano yao na kuridhika kwake, kwa hekima iliyotaka hivyo; wakati huohuo hilo halipingi msingi wowote katika misingi ya sharia; kama vile kuhalalisha haramu au kuharamisha halali.

Zaidi ya hayo, tendo la watoto wa Ya’qub la kumtoa Yusuf kwa baba yake na kumtupa kisimani kwa lengo la kumuua ni zaidi ya wizi.

Swali la pili : Vipi Yusuf kumtenganisha nduguye na baba yake na kumzidishia baba yake majonzi juu ya majonzi?

Jibu : Kila alilolifanya Yusuf lilikuwa kwa maslahi ya ndugu yake na baba yake; akiwa na uhakika kuwa baba yake atamkubalia na hata kumshukuru atakapojua uhakika wake. Na lilifanyika hilo. Kimsingi ni kuwa mambo hupimwa kwa matokeo yake sio kwa mfumo wake. Katika hali nyingine mitume hawatuhumiwi katika upande wa haki.

Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

Watumishi waliwaambia watoto wa Ya’qub ili waseme wenyewe kwamba mwizi atachukuliwa mateka au mtumwa, kama malipo ya tendo lake hilo. Ili iwe ni hoja juu yao pale Yusuf atakapomchukua ndugu yake.

Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.

Kusema ‘basi huyo ndiye malipo yake’ ni kuzidisha ufafanuzi; sawa na kusema: malipo ya muuaji ni kuuliwa, hayo ndiyo malipo yake.

Ndugu wa Yusuf walisema hiyo ndiyo sharia yetu, ambaye mtamkuta nalo mtamchukua mtumwa au mateka. Walisema hivyo wakiwa na uhakika kuwa wao hawana hatia

Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake.

Mtafutaji alianza na mizigo yao kabla ya ndugu yao madogo, ili kuificha hila. Mpaka alipoishia kwenye mzigo wa Bin-yamin akalitoa na akawaonyesha; wakapigwa na butwa na wakawa na wakati mgumu, lakini ni wapi haya na waliyomfanyia Yusuf katika giza la shimo akiwa peke yake?

Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf.

Yaani tulimpa wahyi wa mpango huu, ili ndugu zake waseme wenyewe, kuwa waziri amchukue nyara au mtumwa. Imeitwa hila kwa sababu dhahiri yake sio hali halisi; na ilijuzu kisharia, kwa sababu haikuhalalisha haramu wala kuharamisha halali.

Hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme.

Yaani sharia na hukumu ya mfalme. Maana ni kuwa lau si mipango hii ingelikuwa uzito kwa Yusuf kumchukua ndugu yake, kwa sababu sharia ya mfalme wa Misr sio kuchukua mateka, bali ni kumfunga au kupigwa, na Yusuf hakutaka kumdhuru ndugu yake. Hayo ndio makusudio ya kauli yake:

Isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu.

Kwa ufupi ni kuwa hekima ilikuwa ni kutosema Yusuf kuwa yule ni ndugu yake na wakati huo huo asipatwe na sharia ya mfalme ya kufungwa au kupigwa; bali apatwe na hukumu ya watu wa Ya’qub.

Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao Kwa elimu na utume kama tulivyomfanyia Yusuf juu ya ndugu zake.

Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi mpaka ishie kwa aliye juu zaidi.

Hiyo ni ishara kuwa ndugu wa Yusuf walikuwa ni maulama, lakini Yusuf alikuwa na elimu zaidi na mkamilifu zaidi.

قَالُوا إِن يَسْرِقْ فَقَدْ سَرَقَ أَخٌ لَّهُ مِن قَبْلُ فَأَسَرَّهَا يُوسُفُ فِي نَفْسِهِ وَلَمْ يُبْدِهَا لَهُمْ قَالَ أَنتُمْ شَرٌّ مَّكَانًا وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا تَصِفُونَ ﴿٧٧﴾

77. Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.” Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia; akasema: “Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi; na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema.

قَالُوا يَا أَيُّهَا الْعَزِيزُ إِنَّ لَهُ أَبًا شَيْخًا كَبِيرًا فَخُذْ أَحَدَنَا مَكَانَهُ إِنَّا نَرَاكَ مِنَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٧٨﴾

78. Wakasema: “Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

قَالَ مَعَاذَ اللَّـهِ أَن نَّأْخُذَ إِلَّا مَن وَجَدْنَا مَتَاعَنَا عِندَهُ إِنَّا إِذًا لَّظَالِمُونَ ﴿٧٩﴾

79. Akasema: “Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.”

فَلَمَّا اسْتَيْأَسُوا مِنْهُ خَلَصُوا نَجِيًّا قَالَ كَبِيرُهُمْ أَلَمْ تَعْلَمُوا أَنَّ أَبَاكُمْ قَدْ أَخَذَ عَلَيْكُم مَّوْثِقًا مِّنَ اللَّـهِ وَمِن قَبْلُ مَا فَرَّطتُمْ فِي يُوسُفَ فَلَنْ أَبْرَحَ الْأَرْضَ حَتَّىٰ يَأْذَنَ لِي أَبِي أَوْ يَحْكُمَ اللَّـهُ لِي وَهُوَ خَيْرُ الْحَاكِمِينَ ﴿٨٠﴾

80. Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona. Akasema mkubwa wao: “Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf? Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

KAMA AMEIBA BASI NDUGUYE PIA ALIIBA ZAMANI

Aya 77-80

MAANA

Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.

Ndugu zake Yusuf ndio waliosema hivyo, wakimkusudia Bin-yamin na Yusuf. Hizo ni tuhuma walizombadika nazo Yusuf. Hakuna ishara yoyote katika Aya yoyote kwamba Yusuf kuanzia utotoni aliwahi kuiba yai au kuku au kuiba sanamu ya babu yake mzaa mama yake, au mkanda wa shangazi yake n.k.

Lakini Qur’an imesajili waziwazi uwongo wa ndugu zake Yusuf, pale waliposema kuwa ameliwa na mbwa mwitu. Kuongezea hasadi na chuki yao iliyowapelekea kufanya waliyoyafanya. Kwa hiyo basi wao ni waongo katika kumnasibishia kwao Yusuf wizi alipokuwa mtoto.

Kusema hivi, ingawaje ni natija ya uchambuzi, lakini ndio mantiki ya sawa, au angalau ndio kauli ya karibu na maana.

Wafasiri wameichukulia kauli ya nduguze Yusuf kuwa ni ya kweli, kama kwamba uwongo unastahili. Wakawa wanafanya utafiti wa hicho alichokiiba Yusuf. Kuna aliyesema kuwa aliiba yai akampa mwenye njaa; mweingine akasema ni kuku.

Wa tatu akasema aliiba sanamu la babu yake mzaa mama yake na akalivunja. Wa nne akasema kuwa alikuwa akilelewa na shangazi yake, bint wa Is-haq, alipokuwa na baba yake, akataka kumchukua, kwa hiyo akamtuhumu kuiba mkanda wa mume wa shangazi yake ili abaki naye kama mtumwa; kwa vile adhabu ya mwizi ilikuwa ni kufanywa mtumwa.

Wafasiri wengi wako juu ya kauli hii ya mwisho, Lakini jambo la ajabu ni kuwa hakuna hata mmoja wao aliyezinduka kuwa hukumu ya watoto sio ya wakubwa katika sharia zote, Ajabu zaidi ni kauli ya baadhi ya Masufi kwamba ndugu zake Yusuf walimtuhumu na wizi wa kuiba roho ya baba yake!

Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia.

Aliapuuza maneno yao kwa upole na ukarimu; kama asemavyo mshairi: Nampitia mlaumu akinitusi Namsamehe nasema hanihusi

Akasema: Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi.

Haya aliyasema kisirisiri, kwa dalili ya kauli yake: “Wala hakuwadhihirishia.”

Na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema ya kuninasibishia wizi mimi na ndugu yangu, kwamba ni uwongo na uzushi.

Wakasema: Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

Baada ya mambo kudhihirika na kwamba hukumu ni kuchukuliwa mtumwa ndugu yao Bin-yamin, walielekea kutaka kuhurumiwa kwa kusamehewa au kuchukuliwa fidia ya mmoja wao badala yake. Walibembeleza sana kwa kutumia wema wa Yusuf na uzee wa baba yao na cheo chake na jinsi anavyompenda sana mwanawe Bin-yamin.

Walifanya hivyo sio kwa kumpenda ndugu yao, bali ni kujitoa kwenye lawama kutokana na ahadi waliyoichukua kwa baba yao.

Akasema: Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.

Yusuf alikataa ombi lao na matarajio yao na akashikilia kumchukua ndugu yake, kwa jambo ambalo Mwenyezi Mungu alitaka kulitimiza baada ya kupita mtihani na balaa.

Yusuf alitumia ibara ya ndani sana na yenye hekima ya kumwepusha ndugu yake na wizi, alposema: Yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, ambapo ndugu zake walifahamu: ‘aliyeiba mali yetu.’ Na tofauti hapo ni kubwa sana.

Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona.

Baada ya kukata tamaa watoto wa Ya’qub ya kumpata ndugu yao walijitenga ili washauriane jinsi watakavyomwambia baba yao.

Akasema mkubwa wao: Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Baadhi ya wafasiri wanasema kuwa makusudio ya mkubwa wao ni mkubwa kiakili si kimiaka. Wengine wakasema ni kiakili na kimiaka.

Kauli hii ndiyo inayokuja haraka akilini, Vyovyote iwavyo ni kwamba mkubwa huyo aliwaambia ndugu zake mtafanyaje mtakapofika kwa baba yenu bila ya Bin-yamin nanyi mliapa kuwa mtamrudisha?

Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf?

Anaashiria walivyomtupa shimoni na baba yao alivyokuwa mkali.

Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

Mkubwa wao aliamua abakie karibu na ndugu yake kwa kumwonea haya baba yake na kwamba hataondoka kwenye nchi aliyo Bin-yamin mpaka apewe idhini na baba yake au apate faraja yoyote, kutoka kwa Mwenyezi Mungui hata kama ni mauti. Muda haukuwa mrefu ikaja faraja kwa wote; kama yatakavyokuja maelezo.

ارْجِعُوا إِلَىٰ أَبِيكُمْ فَقُولُوا يَا أَبَانَا إِنَّ ابْنَكَ سَرَقَ وَمَا شَهِدْنَا إِلَّا بِمَا عَلِمْنَا وَمَا كُنَّا لِلْغَيْبِ حَافِظِينَ ﴿٨١﴾

81. Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba, na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibuu.

وَاسْأَلِ الْقَرْيَةَ الَّتِي كُنَّا فِيهَا وَالْعِيرَ الَّتِي أَقْبَلْنَا فِيهَا وَإِنَّا لَصَادِقُونَ ﴿٨٢﴾

82. Na waulize watu wa mji tuliokuwako na msafara tuliokuja nao, Na hakika sisi tunasema kweli.

قَالَ بَلْ سَوَّلَتْ لَكُمْ أَنفُسُكُمْ أَمْرًا فَصَبْرٌ جَمِيلٌ عَسَى اللَّـهُ أَن يَأْتِيَنِي بِهِمْ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ ﴿٨٣﴾

83. Akasema: “Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani. Basi subira ni njema. Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja, Hakika Yeye ni Mjuzi, Mwenye hekima.

وَتَوَلَّىٰ عَنْهُمْ وَقَالَ يَا أَسَفَىٰ عَلَىٰ يُوسُفَ وَابْيَضَّتْ عَيْنَاهُ مِنَ الْحُزْنِ فَهُوَ كَظِيمٌ ﴿٨٤﴾

84. Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf! Na macho yake yakawa meupe kwa huzuni naye akawa anaizuia.

قَالُوا تَاللَّـهِ تَفْتَأُ تَذْكُرُ يُوسُفَ حَتَّىٰ تَكُونَ حَرَضًا أَوْ تَكُونَ مِنَ الْهَالِكِينَ ﴿٨٥﴾

85. Wakasema: “Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.”

قَالَ إِنَّمَا أَشْكُو بَثِّي وَحُزْنِي إِلَى اللَّـهِ وَأَعْلَمُ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٨٦﴾

86. Akasema: “Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

يَا بَنِيَّ اذْهَبُوا فَتَحَسَّسُوا مِن يُوسُفَ وَأَخِيهِ وَلَا تَيْأَسُوا مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٧﴾

87. Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

HATUTOI USHAHIDI ILA TUNAYOYAJUA

Aya 81-87

MAANA

Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibu.

Hii ni kauli ya mkubwa wao akiwausia ndugu zake kuwa waseme ukweli kwa baba yao. Wampe habari kuwa wamewaona watumishi wa waziri wakitoa chombo cha kupimia cha mfalme katika mzigo wa Binyamin, Na kwamba waziri aling’ang’ania kumchukua, Hayo ndiyo tuliyoyashuhudia.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyo nyuma ya hayo, Na lau tungelijua ghaibuu, basi tusingemchukua wala kukupa ahadi ya kurudi naye, Tumefanya bidii sana. Tunaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na kwako.

Na waulize watu wa mji tuliokuwako.

Yaani waulize watu wa Misr, jambo hili la wizi limeenea kwao.

Na msafara tuliokuja nao.

Yaani vile vile uliza msafara tuliokuja nao kutoka Misr ambao uko jirani yako katika nchi ya Kanaan.

Na hakika sisi tunasema kweli kwa haya tunayokusimulia. Mara hii walikuwa wakisema kwa kujiamini kwa sababu walikuwa na uhakika wa wanayoyasema kinyume na mara ya kwanza walipokuja na damu ya uwongo kwenye kanzu ya Yusuf.

Akasema: Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani.

Walipomweleza baba yao aliwaambia mmefanyia vitimbi kama mlivyomfanyia ndugu yake, Yusuf.

Wafasiri wamejiuliza kuwa vipi Ya’qub aliwatuhumu wanawe kwa vitimbi kabla ya kuthibitisha na yeye ni mtume ma’asum?

Kisha wakajbu kwa njia nyingi zisizotegemea msingi wowote. Njia nzuri zaidi waliyoitaja ni ile kuwa makusudio ya Ya’qub ni kuwa nafsi zenu zimewapa picha ya kuwa Bin-yamin ni mwizi na hali yeye si mwizi.

Tuonavyo sisi ni kuwa Ya’qub aliwatuhumu na vitimbi kwa kuchukulia walivyomfanyia Yusuf, lakini yeye hakuchukulia moja kwa moja, kwa kukosa dalili ya uwongo wao. Vile vile hakuwachukulia hatua yoyote kwa dhana, Kwa sababu dhana haitoshelezi kitu.

Hiyo haipingani na cheo cha utume. Kwa sababu mtume hajui ghaibu, naye ni kama mtu mwingine anadhania na kuchukulia uwezekano. Tofauti ni kuwa kwake yeye dhana haina athari yoyote, kama afanyavyo asiyekuwa ma’sum.

Subira ni njema.

Yaani ‘subira yavuta heri, Haya aliwahi kuyasema zamani alipopotea Yusuf na sasa anayasema kwa Bin-yamin.

Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja.

Yaani Yusuf, Bin-yamin na kaka yao aliyebakia Misr karibu na ndugu yake. Neno ‘huenda‘ ni mwangaza wa matumaini; hasa likiwa linatoka kwa anayeamini ghaibu kikwelikweli; kama mitume na wasadikishao. Katika Nahjulbalagha imeelezwa: “Haiwi kweli imani ya mja mpaka yawe yaliyo kwa Mwenyezi Mungu ni ya kutegemewa zaidi kuliko yaliyo mikononi mwake” Kuna Hadith nyingi zenye maana haya.

Hakika yeye ni Mjuzi Mwenye hekima.

Anajua huzuni yangu na machungu yangu na anapanga mambo kwa hekima yake.

Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf!

Alijitenga na watu ili aomboleze peke yake, ambapo huzuni na kilio kilizidi kwa kumkosa mwanawe, Bin-yamin (Benjamin)na macho yake yakawa meupe kwa huzuni.

Yaliathirika kwa sababu ya kulia.

Naye akawa anaizuia.

Yaani anameza uchungu kwa mwili na mishipa yake.

Wakasema: Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.

Yaani wanawe walimwambia bado unamkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au ufe bure, kwa sababu Yusuf amekwenda harudi tena.

Akasema: Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu, sio kwenu kwa sababu ni udhalili na usafihi kumshtakia ambaye haondoi dhara. Imam Ali(a.s) anasema:“Allah Allah! Na kumshatakia ambaye hawezi kuondoa mashaka yenu, wala hawezi kupunguza kwa rai yake yale mliyokwishayapitisha”

Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

Yaa’qub ameteseka kwa kumkosa Yusuf, lakini wakati huo huo bado anamtegemea Mwenyezi Mungu na kumwekea dhana nzuri wala hakati tamaaa na rehema yake huku akiamini kuwa mwisho wa subra ni faraja (baada ya dhiki faraja); kama ilivyofahamisha kauli yake kuwaambia wanawe “Wala msikate tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu.”

Tukiunganisha kumtegemea kwake Mwenyezi Mungu katika ndoto ya Yusuf udogoni mwake natija ni kuwa Yaa’qub ana matumaini ya uhai wa Yusuf hadi atakapokuwa mkubwa, lakini hajui yuko wapi na ana hali gani, Yuko utumwani au kwenye uhuru, Huo ndio ulikuwa wasiwasi wake.

HAKUNA KUNGOJA MEMA YAJE YENYEWE WALA MABAYA

Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

Nendeni mkatafute wala msikate tama, Amekutanisha matumaini na kutenda. Maana yake ni kuwa. Ikiwa hakutakuwa na matendo basi Aya itakwenda kinyume; na uvivu utaambatana na kukata tamaa na yatakuwa matarajio bila ya kufanya kitu ni ujinga na upumbavu. Neno tafuteni linawajibisha kutenda kwa hisia zote dhahiri na batini.

Ndivyo alivyo mwenye akili akitokewa na janga lolote anajitahidi kuondoa visababishi vyake, ni sawa viwe ni ufisadi au uzembe.

Na anapopatwa na mazuri huhofia asijisahau akapetuka mpaka kwa utajiri au cheo kikamletea kiburi. Kwa hiyo hujikinga kwa takua:

فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

“Hawaaminishi hila ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara.” Juz. 9 (7:99).

Kwa ufupi ni kuwa mwenye kutaraji mabaya ni yule asemaye hakuna faida ya kujisumbua, na mvivu ni yule mwenye kutaraji mazuri yaje yenyewe.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA TATU

وَلَمَّا دَخَلُوا عَلَىٰ يُوسُفَ آوَىٰ إِلَيْهِ أَخَاهُ قَالَ إِنِّي أَنَا أَخُوكَ فَلَا تَبْتَئِسْ بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٦٩﴾

69. Walipoingia kwa Yusuf alimkumbatia ndugu yake akasema: Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.

فَلَمَّا جَهَّزَهُم بِجَهَازِهِمْ جَعَلَ السِّقَايَةَ فِي رَحْلِ أَخِيهِ ثُمَّ أَذَّنَ مُؤَذِّنٌ أَيَّتُهَا الْعِيرُ إِنَّكُمْ لَسَارِقُونَ ﴿٧٠﴾

70. Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: “Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.”

قَالُوا وَأَقْبَلُوا عَلَيْهِم مَّاذَا تَفْقِدُونَ ﴿٧١﴾

71. Wakasema na hali wamewaelekea: “Mmepoteza nini?”

قَالُوا نَفْقِدُ صُوَاعَ الْمَلِكِ وَلِمَن جَاءَ بِهِ حِمْلُ بَعِيرٍ وَأَنَا بِهِ زَعِيمٌ ﴿٧٢﴾

72. Wakasema: “Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

قَالُوا تَاللَّـهِ لَقَدْ عَلِمْتُم مَّا جِئْنَا لِنُفْسِدَ فِي الْأَرْضِ وَمَا كُنَّا سَارِقِينَ ﴿٧٣﴾

73. Wakasema: “Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi si wezi.”

قَالُوا فَمَا جَزَاؤُهُ إِن كُنتُمْ كَاذِبِينَ ﴿٧٤﴾

74. Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

قَالُوا جَزَاؤُهُ مَن وُجِدَ فِي رَحْلِهِ فَهُوَ جَزَاؤُهُ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الظَّالِمِينَ ﴿٧٥﴾

75. Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.”

فَبَدَأَ بِأَوْعِيَتِهِمْ قَبْلَ وِعَاءِ أَخِيهِ ثُمَّ اسْتَخْرَجَهَا مِن وِعَاءِ أَخِيهِ كَذَٰلِكَ كِدْنَا لِيُوسُفَ مَا كَانَ لِيَأْخُذَ أَخَاهُ فِي دِينِ الْمَلِكِ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ نَرْفَعُ دَرَجَاتٍ مَّن نَّشَاءُ وَفَوْقَ كُلِّ ذِي عِلْمٍ عَلِيمٌ ﴿٧٦﴾

76. Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake, Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme, isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu, Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao, Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi.

MIMI NI NDUGUYO, USIHUZUNIKE

Aya 69-76

Maana

Walipoingia kwa Yusuf, alimkumbatia ndugu yake akasema: “Hakika mimi ni nduguyo, Basi usihuzunike kwa waliyokuwa wakiyafanya.”

Watu wa tafsiri akiwemo Tabari, Razi, Tabrasi na Abu Hayani al-andalusi, wametaja ufafanuzi wa Aya hii ambao hauna dalili katika Qur’an, lakini unaoana nayo na kunasibiana nayo. Kwa ajili hii tutafupiliza kauli zao, kama ifuatavyo:

Ndugu wa Yusuf walipofika Misr aliwaalika kwenye chakula na akawaweka wawili wawili, kwa lengo la kuwa yeye abakie na ndugu yake Bin-yamin akae naye kwenye meza yake ya chakula; sawa na alivyofanya Muhammad(s.a.w.w) baina ya maswahaba zake wawili wawili kuwa ndugu na akambakisha Ali awe wake yeye.

Baada ya chakula, Yusuf aliwapangia vyumba vya kulala wawili wawili na ndugu yake Bin-yamini akalala naye chumba kimoja. Walipokuwa peke yao akamwambia: “Je, unapenda mimi niwe ndugu yako?” Akamjibu ni nani anaweza kuwa na ndugu mfano wako? Lakini wewe hukuzaliwa na Ya’qub wala Rahel. Basi akamkumbatia na kumwambia: “Mimi nimezaliwa na Ya’qub na Rahel. Basi mimi ni ndugu yako, Wala usuhuzunike na waliyotufanyia ndugu zetu.” Bin-Yamin akafurahi sana na akamshukuru Mwenyezi Mungu.

Alipokwisha watengenezea mahitaji yao akaweka kopo katika mzigo wa ndugu yake. Kisha mnadi akanadi: Enyi wasafiri! Hakika nyinyi ni wezi.

Yusuf alitaka kumtenga Bin-yamin na ndugu zake na kubaki naye, lakini hakuwa na njia ila kufanya ujanja. Katika sharia ya watu wa Ya’qub ni mwizi kufanywa mtumwa. Ndio watumishi wakaweka chombo cha kupimia kwenye mzigo wa Bin-yamin, kwa amri ya Yusuf. Akanadi mnadi kuwa nyinyi wana wa Ya’qub! Ni wezi, kwa hiyo msiendelee na msafara hadi tuangalie mambo yenu.

Wakashangaa watoto wa Ya’qub kwa mshtukizo huu.

Wakasema na hali wamewaelekea: Mmepoteza nini?

Walisema hivi wakiwa na yakini kuwa hawana hatia yoyote. Na hii ni mara yao ya kwanza kusikia tuhuma hii.

Wakasema watumishi wa Yusuf:

Tumepoteza kopo la mfalme na atakayelileta atapata shehena nzima ya ngamia na mimi ni mdhamini.

Mdhamini huyu ndiye aliyewaambia nyinyi ni wezi, kama walivyosema wafasiri, na akadhamini kwa sharti ya kuwa mtu aliye na hicho chombo akirudishe yeye mwenyewe.

Aya hii inaingia kwenye milango miwili ya Fiqh: Jaala, ambayo ni kutangaza zawadi kwa atakayeleta kilichopotea na Dhamana ambayo ni kutekeleza ahadi; kama vile kauli ya alisema: ‘Na mimi ni mdhamini.’ Yaani nadhamini kutekeleza ahadi ya shehena ya ngamia, Kuna hadithi isemayo: “Mdhamini ni mwenye kugharimika.”

Wakasema watoto wa Ya’qub:Wallahi mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya ufisadi katika nchi hii wala sisi sio wezi.

Walibishana wakajadiliana na kuleta hoja za kutokuwa na hatia na usafi wao; miongoni mwa waliyoyasema ni: Vipi mnatutuhumu na mnajua nasabu yetu na sera yetu katika safari yetu ya kwanza na hii ya pili kwamba hatukuja kufanya ufisadi au hiyana; isipokuwa tumekuja kuwanunulia chakula watu wetu.

Kwenye tafsiri nyingi imeelezwa kuwa watoto wa Ya’qub, kwenye safari yao ya kwanza, walipokuta bidha zao zimerudishwa walidhani kuwa zimesahaulika, kwa hiyo hawakuzitumia, bali walizirudisha Misr. Kwa hiyo wakawa mashuhuri kwa wema na uamnifu wao.

Kauli hii ya wafasiri haiku mbali; bali inaashiria kauli ya watoto wa Ya’qub: Wallah mnajua vyema kwamba sisi hatukuja kufanya uharibifu katika nchi hii

Unaweza kuuliza : Imekuwaje kwa Yusuf kufanya njama hizi za kuwaelekezea tuhuma ndugu zake na hali anajua kuwa hawana hatia?

Jibu : Kwanza, tukio hili ni maalum, lina sababu zake, haifai kulipima na matukio mengine. Pili, aliyelengwa na tuhuma za wizi ni Bin-yamin, ndugu wa Yusuf kwa baba na mama, na hilo lilikuwa kwa makubaliano yao na kuridhika kwake, kwa hekima iliyotaka hivyo; wakati huohuo hilo halipingi msingi wowote katika misingi ya sharia; kama vile kuhalalisha haramu au kuharamisha halali.

Zaidi ya hayo, tendo la watoto wa Ya’qub la kumtoa Yusuf kwa baba yake na kumtupa kisimani kwa lengo la kumuua ni zaidi ya wizi.

Swali la pili : Vipi Yusuf kumtenganisha nduguye na baba yake na kumzidishia baba yake majonzi juu ya majonzi?

Jibu : Kila alilolifanya Yusuf lilikuwa kwa maslahi ya ndugu yake na baba yake; akiwa na uhakika kuwa baba yake atamkubalia na hata kumshukuru atakapojua uhakika wake. Na lilifanyika hilo. Kimsingi ni kuwa mambo hupimwa kwa matokeo yake sio kwa mfumo wake. Katika hali nyingine mitume hawatuhumiwi katika upande wa haki.

Wakasema: “Malipo yake yatakuwa ni nini ikiwa nyinyi ni waongo?”

Watumishi waliwaambia watoto wa Ya’qub ili waseme wenyewe kwamba mwizi atachukuliwa mateka au mtumwa, kama malipo ya tendo lake hilo. Ili iwe ni hoja juu yao pale Yusuf atakapomchukua ndugu yake.

Wakasema: “Malipo yake ni yule ambaye litaonekana katika mzigo wake, basi huyo ndiye malipo yake, Hivyo ndivyo tunavyowalipa madhalimu.

Kusema ‘basi huyo ndiye malipo yake’ ni kuzidisha ufafanuzi; sawa na kusema: malipo ya muuaji ni kuuliwa, hayo ndiyo malipo yake.

Ndugu wa Yusuf walisema hiyo ndiyo sharia yetu, ambaye mtamkuta nalo mtamchukua mtumwa au mateka. Walisema hivyo wakiwa na uhakika kuwa wao hawana hatia

Basi akaanza na mizigo yao kabla ya mzigo wa ndugu yake; kisha akalitoa katika mzigo wa ndugu yake.

Mtafutaji alianza na mizigo yao kabla ya ndugu yao madogo, ili kuificha hila. Mpaka alipoishia kwenye mzigo wa Bin-yamin akalitoa na akawaonyesha; wakapigwa na butwa na wakawa na wakati mgumu, lakini ni wapi haya na waliyomfanyia Yusuf katika giza la shimo akiwa peke yake?

Hivyo ndivyo tulivyomfanyia hila Yusuf.

Yaani tulimpa wahyi wa mpango huu, ili ndugu zake waseme wenyewe, kuwa waziri amchukue nyara au mtumwa. Imeitwa hila kwa sababu dhahiri yake sio hali halisi; na ilijuzu kisharia, kwa sababu haikuhalalisha haramu wala kuharamisha halali.

Hakuweza kumchukua ndugu yake katika sharia ya mfalme.

Yaani sharia na hukumu ya mfalme. Maana ni kuwa lau si mipango hii ingelikuwa uzito kwa Yusuf kumchukua ndugu yake, kwa sababu sharia ya mfalme wa Misr sio kuchukua mateka, bali ni kumfunga au kupigwa, na Yusuf hakutaka kumdhuru ndugu yake. Hayo ndio makusudio ya kauli yake:

Isipokuwa alivyotaka Mwenyezi Mungu.

Kwa ufupi ni kuwa hekima ilikuwa ni kutosema Yusuf kuwa yule ni ndugu yake na wakati huo huo asipatwe na sharia ya mfalme ya kufungwa au kupigwa; bali apatwe na hukumu ya watu wa Ya’qub.

Tunawatukuza kwenye vyeo tuwatakao Kwa elimu na utume kama tulivyomfanyia Yusuf juu ya ndugu zake.

Na juu ya kila mwenye elimu yuko ajuaye zaidi mpaka ishie kwa aliye juu zaidi.

Hiyo ni ishara kuwa ndugu wa Yusuf walikuwa ni maulama, lakini Yusuf alikuwa na elimu zaidi na mkamilifu zaidi.

قَالُوا إِن يَسْرِقْ فَقَدْ سَرَقَ أَخٌ لَّهُ مِن قَبْلُ فَأَسَرَّهَا يُوسُفُ فِي نَفْسِهِ وَلَمْ يُبْدِهَا لَهُمْ قَالَ أَنتُمْ شَرٌّ مَّكَانًا وَاللَّـهُ أَعْلَمُ بِمَا تَصِفُونَ ﴿٧٧﴾

77. Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.” Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia; akasema: “Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi; na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema.

قَالُوا يَا أَيُّهَا الْعَزِيزُ إِنَّ لَهُ أَبًا شَيْخًا كَبِيرًا فَخُذْ أَحَدَنَا مَكَانَهُ إِنَّا نَرَاكَ مِنَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٧٨﴾

78. Wakasema: “Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

قَالَ مَعَاذَ اللَّـهِ أَن نَّأْخُذَ إِلَّا مَن وَجَدْنَا مَتَاعَنَا عِندَهُ إِنَّا إِذًا لَّظَالِمُونَ ﴿٧٩﴾

79. Akasema: “Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.”

فَلَمَّا اسْتَيْأَسُوا مِنْهُ خَلَصُوا نَجِيًّا قَالَ كَبِيرُهُمْ أَلَمْ تَعْلَمُوا أَنَّ أَبَاكُمْ قَدْ أَخَذَ عَلَيْكُم مَّوْثِقًا مِّنَ اللَّـهِ وَمِن قَبْلُ مَا فَرَّطتُمْ فِي يُوسُفَ فَلَنْ أَبْرَحَ الْأَرْضَ حَتَّىٰ يَأْذَنَ لِي أَبِي أَوْ يَحْكُمَ اللَّـهُ لِي وَهُوَ خَيْرُ الْحَاكِمِينَ ﴿٨٠﴾

80. Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona. Akasema mkubwa wao: “Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf? Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

KAMA AMEIBA BASI NDUGUYE PIA ALIIBA ZAMANI

Aya 77-80

MAANA

Wakasema: Kama ameiba, basi ndugu yake pia ameiba zamani.

Ndugu zake Yusuf ndio waliosema hivyo, wakimkusudia Bin-yamin na Yusuf. Hizo ni tuhuma walizombadika nazo Yusuf. Hakuna ishara yoyote katika Aya yoyote kwamba Yusuf kuanzia utotoni aliwahi kuiba yai au kuku au kuiba sanamu ya babu yake mzaa mama yake, au mkanda wa shangazi yake n.k.

Lakini Qur’an imesajili waziwazi uwongo wa ndugu zake Yusuf, pale waliposema kuwa ameliwa na mbwa mwitu. Kuongezea hasadi na chuki yao iliyowapelekea kufanya waliyoyafanya. Kwa hiyo basi wao ni waongo katika kumnasibishia kwao Yusuf wizi alipokuwa mtoto.

Kusema hivi, ingawaje ni natija ya uchambuzi, lakini ndio mantiki ya sawa, au angalau ndio kauli ya karibu na maana.

Wafasiri wameichukulia kauli ya nduguze Yusuf kuwa ni ya kweli, kama kwamba uwongo unastahili. Wakawa wanafanya utafiti wa hicho alichokiiba Yusuf. Kuna aliyesema kuwa aliiba yai akampa mwenye njaa; mweingine akasema ni kuku.

Wa tatu akasema aliiba sanamu la babu yake mzaa mama yake na akalivunja. Wa nne akasema kuwa alikuwa akilelewa na shangazi yake, bint wa Is-haq, alipokuwa na baba yake, akataka kumchukua, kwa hiyo akamtuhumu kuiba mkanda wa mume wa shangazi yake ili abaki naye kama mtumwa; kwa vile adhabu ya mwizi ilikuwa ni kufanywa mtumwa.

Wafasiri wengi wako juu ya kauli hii ya mwisho, Lakini jambo la ajabu ni kuwa hakuna hata mmoja wao aliyezinduka kuwa hukumu ya watoto sio ya wakubwa katika sharia zote, Ajabu zaidi ni kauli ya baadhi ya Masufi kwamba ndugu zake Yusuf walimtuhumu na wizi wa kuiba roho ya baba yake!

Yusuf aliyaweka siri moyoni mwake wala hakuwadhihirishia.

Aliapuuza maneno yao kwa upole na ukarimu; kama asemavyo mshairi: Nampitia mlaumu akinitusi Namsamehe nasema hanihusi

Akasema: Nyinyi mko katika hali mbaya zaidi.

Haya aliyasema kisirisiri, kwa dalili ya kauli yake: “Wala hakuwadhihirishia.”

Na Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayoyasema ya kuninasibishia wizi mimi na ndugu yangu, kwamba ni uwongo na uzushi.

Wakasema: Ewe mheshimiwa! Hakika anaye baba mzee sana, Kwa hiyo mchukue mmoja wetu badala yake, Hakika sisi tunakuona wewe ni katika watu wema.

Baada ya mambo kudhihirika na kwamba hukumu ni kuchukuliwa mtumwa ndugu yao Bin-yamin, walielekea kutaka kuhurumiwa kwa kusamehewa au kuchukuliwa fidia ya mmoja wao badala yake. Walibembeleza sana kwa kutumia wema wa Yusuf na uzee wa baba yao na cheo chake na jinsi anavyompenda sana mwanawe Bin-yamin.

Walifanya hivyo sio kwa kumpenda ndugu yao, bali ni kujitoa kwenye lawama kutokana na ahadi waliyoichukua kwa baba yao.

Akasema: Mwenyezi Mungu apishe mbali kumchukua ila yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, Hivyo basi tutakuwa ni wenye kudhulumu.

Yusuf alikataa ombi lao na matarajio yao na akashikilia kumchukua ndugu yake, kwa jambo ambalo Mwenyezi Mungu alitaka kulitimiza baada ya kupita mtihani na balaa.

Yusuf alitumia ibara ya ndani sana na yenye hekima ya kumwepusha ndugu yake na wizi, alposema: Yule tuliyekuta mali yetu iko kwake, ambapo ndugu zake walifahamu: ‘aliyeiba mali yetu.’ Na tofauti hapo ni kubwa sana.

Walipokata tamaa naye walikwenda kando kunong’ona.

Baada ya kukata tamaa watoto wa Ya’qub ya kumpata ndugu yao walijitenga ili washauriane jinsi watakavyomwambia baba yao.

Akasema mkubwa wao: Je, hamjui kuwa baba yenu amechukua ahadi kwenu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Baadhi ya wafasiri wanasema kuwa makusudio ya mkubwa wao ni mkubwa kiakili si kimiaka. Wengine wakasema ni kiakili na kimiaka.

Kauli hii ndiyo inayokuja haraka akilini, Vyovyote iwavyo ni kwamba mkubwa huyo aliwaambia ndugu zake mtafanyaje mtakapofika kwa baba yenu bila ya Bin-yamin nanyi mliapa kuwa mtamrudisha?

Na hapo zamani mlikosea katika Yusuf?

Anaashiria walivyomtupa shimoni na baba yao alivyokuwa mkali.

Basi sitaondoka nchi hii mpaka baba yangu aniruhusu au Mwenyezi Mungu anihukumie; naye ni mbora wa mahakimu.

Mkubwa wao aliamua abakie karibu na ndugu yake kwa kumwonea haya baba yake na kwamba hataondoka kwenye nchi aliyo Bin-yamin mpaka apewe idhini na baba yake au apate faraja yoyote, kutoka kwa Mwenyezi Mungui hata kama ni mauti. Muda haukuwa mrefu ikaja faraja kwa wote; kama yatakavyokuja maelezo.

ارْجِعُوا إِلَىٰ أَبِيكُمْ فَقُولُوا يَا أَبَانَا إِنَّ ابْنَكَ سَرَقَ وَمَا شَهِدْنَا إِلَّا بِمَا عَلِمْنَا وَمَا كُنَّا لِلْغَيْبِ حَافِظِينَ ﴿٨١﴾

81. Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba, na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibuu.

وَاسْأَلِ الْقَرْيَةَ الَّتِي كُنَّا فِيهَا وَالْعِيرَ الَّتِي أَقْبَلْنَا فِيهَا وَإِنَّا لَصَادِقُونَ ﴿٨٢﴾

82. Na waulize watu wa mji tuliokuwako na msafara tuliokuja nao, Na hakika sisi tunasema kweli.

قَالَ بَلْ سَوَّلَتْ لَكُمْ أَنفُسُكُمْ أَمْرًا فَصَبْرٌ جَمِيلٌ عَسَى اللَّـهُ أَن يَأْتِيَنِي بِهِمْ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ ﴿٨٣﴾

83. Akasema: “Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani. Basi subira ni njema. Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja, Hakika Yeye ni Mjuzi, Mwenye hekima.

وَتَوَلَّىٰ عَنْهُمْ وَقَالَ يَا أَسَفَىٰ عَلَىٰ يُوسُفَ وَابْيَضَّتْ عَيْنَاهُ مِنَ الْحُزْنِ فَهُوَ كَظِيمٌ ﴿٨٤﴾

84. Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf! Na macho yake yakawa meupe kwa huzuni naye akawa anaizuia.

قَالُوا تَاللَّـهِ تَفْتَأُ تَذْكُرُ يُوسُفَ حَتَّىٰ تَكُونَ حَرَضًا أَوْ تَكُونَ مِنَ الْهَالِكِينَ ﴿٨٥﴾

85. Wakasema: “Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.”

قَالَ إِنَّمَا أَشْكُو بَثِّي وَحُزْنِي إِلَى اللَّـهِ وَأَعْلَمُ مِنَ اللَّـهِ مَا لَا تَعْلَمُونَ ﴿٨٦﴾

86. Akasema: “Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

يَا بَنِيَّ اذْهَبُوا فَتَحَسَّسُوا مِن يُوسُفَ وَأَخِيهِ وَلَا تَيْأَسُوا مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴿٨٧﴾

87. Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

HATUTOI USHAHIDI ILA TUNAYOYAJUA

Aya 81-87

MAANA

Rudini kwa baba yenu, na mwambieni: Ewe baba yetu! Hakika mwanao ameiba na hatutoi ushahidi ila tunayoyajua; wala hatukuwa wenye kuhifadhi mambo ya ghaibu.

Hii ni kauli ya mkubwa wao akiwausia ndugu zake kuwa waseme ukweli kwa baba yao. Wampe habari kuwa wamewaona watumishi wa waziri wakitoa chombo cha kupimia cha mfalme katika mzigo wa Binyamin, Na kwamba waziri aling’ang’ania kumchukua, Hayo ndiyo tuliyoyashuhudia.

Na Mwenyezi Mungu anajua yaliyo nyuma ya hayo, Na lau tungelijua ghaibuu, basi tusingemchukua wala kukupa ahadi ya kurudi naye, Tumefanya bidii sana. Tunaomba msamaha kwa Mwenyezi Mungu na kwako.

Na waulize watu wa mji tuliokuwako.

Yaani waulize watu wa Misr, jambo hili la wizi limeenea kwao.

Na msafara tuliokuja nao.

Yaani vile vile uliza msafara tuliokuja nao kutoka Misr ambao uko jirani yako katika nchi ya Kanaan.

Na hakika sisi tunasema kweli kwa haya tunayokusimulia. Mara hii walikuwa wakisema kwa kujiamini kwa sababu walikuwa na uhakika wa wanayoyasema kinyume na mara ya kwanza walipokuja na damu ya uwongo kwenye kanzu ya Yusuf.

Akasema: Bali nafsi zenu zimewashawishi jambo fulani.

Walipomweleza baba yao aliwaambia mmefanyia vitimbi kama mlivyomfanyia ndugu yake, Yusuf.

Wafasiri wamejiuliza kuwa vipi Ya’qub aliwatuhumu wanawe kwa vitimbi kabla ya kuthibitisha na yeye ni mtume ma’asum?

Kisha wakajbu kwa njia nyingi zisizotegemea msingi wowote. Njia nzuri zaidi waliyoitaja ni ile kuwa makusudio ya Ya’qub ni kuwa nafsi zenu zimewapa picha ya kuwa Bin-yamin ni mwizi na hali yeye si mwizi.

Tuonavyo sisi ni kuwa Ya’qub aliwatuhumu na vitimbi kwa kuchukulia walivyomfanyia Yusuf, lakini yeye hakuchukulia moja kwa moja, kwa kukosa dalili ya uwongo wao. Vile vile hakuwachukulia hatua yoyote kwa dhana, Kwa sababu dhana haitoshelezi kitu.

Hiyo haipingani na cheo cha utume. Kwa sababu mtume hajui ghaibu, naye ni kama mtu mwingine anadhania na kuchukulia uwezekano. Tofauti ni kuwa kwake yeye dhana haina athari yoyote, kama afanyavyo asiyekuwa ma’sum.

Subira ni njema.

Yaani ‘subira yavuta heri, Haya aliwahi kuyasema zamani alipopotea Yusuf na sasa anayasema kwa Bin-yamin.

Huenda Mwenyezi Mungu akaniletea wote pamoja.

Yaani Yusuf, Bin-yamin na kaka yao aliyebakia Misr karibu na ndugu yake. Neno ‘huenda‘ ni mwangaza wa matumaini; hasa likiwa linatoka kwa anayeamini ghaibu kikwelikweli; kama mitume na wasadikishao. Katika Nahjulbalagha imeelezwa: “Haiwi kweli imani ya mja mpaka yawe yaliyo kwa Mwenyezi Mungu ni ya kutegemewa zaidi kuliko yaliyo mikononi mwake” Kuna Hadith nyingi zenye maana haya.

Hakika yeye ni Mjuzi Mwenye hekima.

Anajua huzuni yangu na machungu yangu na anapanga mambo kwa hekima yake.

Na akajitenga nao, na akasema: Oh! Masikitiko yangu juu ya Yusuf!

Alijitenga na watu ili aomboleze peke yake, ambapo huzuni na kilio kilizidi kwa kumkosa mwanawe, Bin-yamin (Benjamin)na macho yake yakawa meupe kwa huzuni.

Yaliathirika kwa sababu ya kulia.

Naye akawa anaizuia.

Yaani anameza uchungu kwa mwili na mishipa yake.

Wakasema: Wallahi huachi kumkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au uwe katika wenye kuaangamia.

Yaani wanawe walimwambia bado unamkumbuka Yusuf mpaka uwe mgonjwa au ufe bure, kwa sababu Yusuf amekwenda harudi tena.

Akasema: Majonzi yangu na huzuni yangu ninamshtakia Mwenyezi Mungu, sio kwenu kwa sababu ni udhalili na usafihi kumshtakia ambaye haondoi dhara. Imam Ali(a.s) anasema:“Allah Allah! Na kumshatakia ambaye hawezi kuondoa mashaka yenu, wala hawezi kupunguza kwa rai yake yale mliyokwishayapitisha”

Na ninajua kwa Mwenyezi yale msiyoyajua.

Yaa’qub ameteseka kwa kumkosa Yusuf, lakini wakati huo huo bado anamtegemea Mwenyezi Mungu na kumwekea dhana nzuri wala hakati tamaaa na rehema yake huku akiamini kuwa mwisho wa subra ni faraja (baada ya dhiki faraja); kama ilivyofahamisha kauli yake kuwaambia wanawe “Wala msikate tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu.”

Tukiunganisha kumtegemea kwake Mwenyezi Mungu katika ndoto ya Yusuf udogoni mwake natija ni kuwa Yaa’qub ana matumaini ya uhai wa Yusuf hadi atakapokuwa mkubwa, lakini hajui yuko wapi na ana hali gani, Yuko utumwani au kwenye uhuru, Huo ndio ulikuwa wasiwasi wake.

HAKUNA KUNGOJA MEMA YAJE YENYEWE WALA MABAYA

Enyi wanangu! Nendeni mkamtafute Yusuf na nduguye wala msikate tamaaa na faraja ya Mwenyezi Mungu. Hakika hawakati tamaa na faraja ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri.

Nendeni mkatafute wala msikate tama, Amekutanisha matumaini na kutenda. Maana yake ni kuwa. Ikiwa hakutakuwa na matendo basi Aya itakwenda kinyume; na uvivu utaambatana na kukata tamaa na yatakuwa matarajio bila ya kufanya kitu ni ujinga na upumbavu. Neno tafuteni linawajibisha kutenda kwa hisia zote dhahiri na batini.

Ndivyo alivyo mwenye akili akitokewa na janga lolote anajitahidi kuondoa visababishi vyake, ni sawa viwe ni ufisadi au uzembe.

Na anapopatwa na mazuri huhofia asijisahau akapetuka mpaka kwa utajiri au cheo kikamletea kiburi. Kwa hiyo hujikinga kwa takua:

فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩٩﴾

“Hawaaminishi hila ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara.” Juz. 9 (7:99).

Kwa ufupi ni kuwa mwenye kutaraji mabaya ni yule asemaye hakuna faida ya kujisumbua, na mvivu ni yule mwenye kutaraji mazuri yaje yenyewe.


6

7

8

9

10

11

12

13