TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 25535
Pakua: 3227


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 25535 / Pakua: 3227
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea. Hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka kwa lugha ya kiswahili hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasayansi kama kina Enstein, wasanii kama Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146), Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama. Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu Jabal amil 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa.” Kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Mwendelezo wa Sura Ya Thelathini Na Tatu: Surat Al-Ahzab.

وَمَن يَقْنُتْ مِنكُنَّ لِلَّـهِ وَرَسُولِهِ وَتَعْمَلْ صَالِحًا نُّؤْتِهَا أَجْرَهَا مَرَّتَيْنِ وَأَعْتَدْنَا لَهَا رِزْقًا كَرِيمًا ﴿٣١﴾

31. Na yeyote katika nyinyi atakayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake na akatenda wema, tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki yenye heshima.

يَا نِسَاءَ النَّبِيِّ لَسْتُنَّ كَأَحَدٍ مِّنَ النِّسَاءِ إِنِ اتَّقَيْتُنَّ فَلَا تَخْضَعْنَ بِالْقَوْلِ فَيَطْمَعَ الَّذِي فِي قَلْبِهِ مَرَضٌ وَقُلْنَ قَوْلًا مَّعْرُوفًا ﴿٣٢﴾

32. Enyi wake wa Mtume! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine kama mtamcha Mwenyezi Mungu. Basi msilegeze sauti, asije akaingia tamaa mwenye maradhi moyoni mwake. Na semeni maneno mema.

وَقَرْنَ فِي بُيُوتِكُنَّ وَلَا تَبَرَّجْنَ تَبَرُّجَ الْجَاهِلِيَّةِ الْأُولَىٰ وَأَقِمْنَ الصَّلَاةَ وَآتِينَ الزَّكَاةَ وَأَطِعْنَ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ إِنَّمَا يُرِيدُ اللَّـهُ لِيُذْهِبَ عَنكُمُ الرِّجْسَ أَهْلَ الْبَيْتِ وَيُطَهِّرَكُمْ تَطْهِيرًا ﴿٣٣﴾

33. Na kaeni majumbani mwenu wala msidhihirishe mapambo kwa madhihirisho ya kijahiliya ya zamani.Na simamisheni Swala, na toeni Zaka, na mtiini Mwenyezi Mungu. Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.

وَاذْكُرْنَ مَا يُتْلَىٰ فِي بُيُوتِكُنَّ مِنْ آيَاتِ اللَّـهِ وَالْحِكْمَةِ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ لَطِيفًا خَبِيرًا ﴿٣٤﴾

34. Na kumbukeni yanayosomwa majumbani mwenu katika Aya za Mwenyezi Mungu na hikima. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole, Mwingi wa habari.

UTWAHARA WA AHLUL BAYT

Aya 31-34

MAANA

Na yeyote katika nyinyi atakayemtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake na akatenda wema, tutampa malipo yake mara mbili, na tutamwandalia riziki yenye heshima.

Kama ambavyo adhabu itakuwa mara mbili kwa atakayejasiri kufanya maasi katika wake wa Mtume, vile vile thawabu zitakuwa mara mbili zaidi kwa atakayemuogopa Mwenyezi Mungu na akamcha.

Enyi wake wa Mtume! Nyinyi si kama yeyote katika wanawake wengine kama mtamcha Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawaambia wake wa Mtume kuwa nyinyi mko zaidi ya wanawake wengine kiheshima na utukufu, ikiwa mtamcha Mwenyezi Mungu kwa kauli na vitendo. Vinginevyo basi mtakuwa hamna muungano wowote na Mtume.

Al-Hafidh, Muhammad bin Ahmad Al-Kalabiy anasema katika kitabu Attas-hil: “Walipata fadhila juu ya wanawake wote isipokuwa Fatima bint Muhammad, Maryam bint Imran na Asiya bint Muzahim.”

Basi msilegeze sauti asije akaingia tamaa mwenye maradhi moyoni mwake. Na semeni maneno mema na kaeni majumbani mwenu wala msidhihirishe mapambo kwa madhihirisho ya kijahiliya ya zamani.

Zama za Mtume zilikuwa ni bora kuliko zama nyingine, lakini bado Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwahadharisha wake wa Mtume wasilainishe mazungumzo na wanaume na wasitoke majumbani wakiwa wanajionyesha vipambo vyao.

Ikumbukwe kuwa wake wa Mtume walikuwa wakijistahi na kustahiwa kwa hali ya juu isiyokuwa na shaka yoyote. Sasa je, vipi kwenye zama zetu hizi ambapo mwanamke amechomoka nyumbani kwake hadi kwenye mabwawa ya kuogelea na kwenye majumba ya sinema na akaweza kuwa uchi kwa kutumia mfumo wa kustarehe?

Na simamisheni Swala kwa sababu inakataza kujionyesha mapambo na mengineyo ya haramu.

Na toeni Zaka inayosafisha mali, kama Swala inavyosafisha nafsi.

Na mtiini Mwenyezi Mungu katika kila kitu, sio kwenye Swala tu na Zaka wala kwenye kuacha kudhihirisha mapambo au kulegeza sauti.

AHLUBAYT (WATU WA NYUMBA YA MTUME)

Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea ucha- fu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.

Makusudio ya uchafu hapa ni dhambi. Shia wametoa dalili ya isma ya watu wa nyumba ya Mtume kwa Aya hii na wakasema herufi Innama ambayo ki nahw ni chombo cha kudhibiti (adaatul haswr) inafahamisha kudhibiti utwahara wa dhambi kwa watu wa nyumba ya Mtume tu, sio wengineo; wala hakuna maana nyingine ya isma isipokuwa kutwaharika na dhambi.

Katika Sahih Muslim, sehemu ya pili ya Juzuu ya pili, Uk. 116 chapa ya 1348 AH, kuna Hadith hii, ninanukuu: “Aisha amesema: Mtume(s.a.w. w ) alitoka asubuhi na mapema akiwa amejifunika guo – Aina ya kitambaa cha Yemen – kilichofumwa kutokana na sufu nyeusi.

Basi akaja Hasan bin Ali akamwingiza, akaja Husein akamwingiza pamoja naye, tena akaja Fatima akamwingiza, kisha akaja Ali akamwingiza na akasema:“Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume na kuwatakasa kabisa kabisa.”

Kuna Hadith kama hiyo kisanadi, aliyoipokea Tirmidhiy katika Sahih yake, Imam Ahmad katika Musnad yake na wengineo katika maimau wa Hadith wa kisunni.

Katika Tafsir At-Twabariy imeandikwa: “Imepokewa kutoka kwa Abu said Al-Khudriy, Swahaba mtukufu na Ummu salama, mke wa Mtume(s.a.w. w ) , Amesema huyo mke wa Mtume: Iliposhuka Aya hii ‘Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, Mtume(s.a.w. w ) alimwita Ali, Fatima, Hassan na Hussein na akawafunika guo na akasema:“Ewe Mola wangu! Hawa ndio watu wa nyumba. Ewe Mola wangu! Waondolee uchafu na uwatakase kabisa kabisa.’

Ummu Salama akasema: “Mimi si katika wao?” Mtume akasema:“Wewe uko kwenye kheri.”

Kuna mfano wa Hadith hiyo katika Tafsir Al-bahrul- muhit ya Al-andalusi,Tas-hili ya Hafidh, Durrul manthur ya As-Suyuti na Tafsir nyinginezo.

Katika Juz. (2: 35 – 33) Kifungu cha ‘Ahlubayt’ Tumenukuu aliyoyasema Muhyi-ddni Ibnul-Arabiy katika Juzuu ya kwanza na ya pili ya Kitabu Futuhatil-Makkiyya kuhusiana na Aya hii. Sasa tunayanukuu aliyosema kuhusiana na Ahlul-bayt katika Juzuu ya nne ya Kitabu hicho Uk. 139 chapa Darul-kutubil-arabiyya al-kubra ya Misr, anasema: “Hakika mapenzi yetu kwa Mtume(s.a.w. w ) na watu wa nyumba yake ni sawa sawa.

Mwenye kuwachukia watu wa nyumba yake basi amemchukia Mtume(s.a.w. w ) , kwa sababu yeye ni mmoja wao, na mwenye kuwafanyia hiyana atakuwa amemfanyia hiyana Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) .”

Na kumbukeni yanayosomwa majumbani mwenu katika Aya za Mwenyezi Mungu na hikima. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole, Mwingi wa habari.

Makusudio ya hekima hapa ni sunna za Mtume kwa kulinganisha na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Aya zake. Maana ni kuwa enyi wake wa Mtume wa Mwenyezi Mungu! Shukuruni neema ya Mwenyezi Mungu juu yenu, pale alipowajaalia katika majumba ambayo ndani yake mnasikia Kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna za Mtume wake ambazo ni nuru ya akili na kiburudisho cha nyoyo.

Unaweza kuuliza : Mfumo wa Aya unafahamisha kuwa makusudio ni kutwaharishwa wake wa Mtume(s.a.w. w ) , vipi wafasiri na wasimulizi wa Hadith wamewatoa?

Jibu :Kwanza : mwenye Tafsir Al-manar akimnukuu ustadh wake Sheikh Muhammad Abduh, katika Juz.2 Uk. 451 chapa ya pili, anasema: “Hakika ni katika ada ya Qur’an kumgurisha mtu kutoka jambo moja hadi jingine, kisha inarudia utafiti wa kusudio moja mara kwa mara.”

Imam Ja’far As-Sadiq(a.s ) naye anasema:“Hakika Aya moja katika Qur’an inakuwa mwanzo wake kuna jambo na mwisho wake ni jambo jingine.”

Kwa hiyo basi haifai kutegemea mfumo wa Aya ya Qur’an yenye hekima kuwa ndio kawaida yake yote.

Pili : Lau tukichukulia kutegemea mfumo wa Aya, kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, ‘kuwaondolea na kuwatakasa,’ imekuja kwa dhamir (kum) ambayo huwa haitumiki kwa wanawake peke yao, kulingana na sarufi ya kiarabu (Nahw).

Tatu : Hakika wafasiri na wasimulizi wa Hadith tuliowataja wametegemea Hadith sahih katika kuwatoa wake wa Mtume. Na waislamu wote wameafikiana kuwa Hadith za Mtume ni Tafsiri na ubainifu wa Kitabu cha Mwenyezi Mungu.

إِنَّ الْمُسْلِمِينَ وَالْمُسْلِمَاتِ وَالْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ وَالْقَانِتِينَ وَالْقَانِتَاتِ وَالصَّادِقِينَ وَالصَّادِقَاتِ وَالصَّابِرِينَ وَالصَّابِرَاتِ وَالْخَاشِعِينَ وَالْخَاشِعَاتِ وَالْمُتَصَدِّقِينَ وَالْمُتَصَدِّقَاتِ وَالصَّائِمِينَ وَالصَّائِمَاتِ وَالْحَافِظِينَ فُرُوجَهُمْ وَالْحَافِظَاتِ وَالذَّاكِرِينَ اللَّـهَ كَثِيرًا وَالذَّاكِرَاتِ أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُم مَّغْفِرَةً وَأَجْرًا عَظِيمًا ﴿٣٥﴾

35. Hakika waislamu wanaume na waislamu wanawake, na waumini wanaume na waumini wanawake, na watiifu wanaume na watiifu wanawake, na wakweli wanaume na wakweli wanawake, na wanaume wanaosubiri na wanawake wanaosubiri, na wanyenyekevu wanaume na wanyenyekevu wanawake, na wanaotoa sadaka wanaume na wanaotoa sadaka wanawake, na wanaume wanaofunga na wanawake wanaofunga, na wanaume wanohifadhi tupu zao na wanawake wanohifadhi tupu, na wanaume wanomkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi na wanawake wanaomkumbuka Mwenyezi Mungu kwa wingi. Mwenyezi Mungu amewaandalia msamaha na malipo makubwa.

WANAUME NA WANAWAKE WANAOHIFADHI MIPAKA YA MWENYEZI MUNGU

Aya 35

MAANA

Uislamu ni kukiri umoja wa Mwenyezi Mungu na risala ya Muhammad. Imani ni kukiri kwa ulimi na kufanya kwa vitendo. Kuna Aya inayofahamisha tofauti ya Uislamu na imani:

قَالَتِ الْأَعْرَابُ آمَنَّا قُل لَّمْ تُؤْمِنُوا وَلَـٰكِن قُولُوا أَسْلَمْنَا وَلَمَّا يَدْخُلِ الْإِيمَانُ فِي ﴿١٤﴾

“Mabedui wamesema: Tumeamini, sema: Hamjaamini, lakini semeni tumesilimu. Kwani imani haijaiingia katika nyoyo zenu.” (49:14).

Makusudio ya utiifu hapa ni kutekeleza na kudumu kwenye utiifu. Ukweli ni ikhlasi. Kusubiri ni kuvumilia tabu na mashaka kwa ajili ya haki na kuinusuru. Kunyenyekea ni kujirudisha chini. Kutoa sadaka ni kutoa katika njia ya Mwenyezi Mungu. Saumu ni ile ile ya kawaida. Pia kuhifadhi tupu ni kule kwa kawaida. Ama kumtaja Mwenyezi Mungu kwa wingi ni kinaya cha kudumu kwenye Swala tano.

Mwenye kuwa na sifa zote hizi basi yeye mbele ya Mwenyezi Mungu atakuwa na cheo na malipo makubwa awe mwananmume au mwanamke.

Tazama Juz. 2 (2:228) na Juz. 5 (4:123 – 124) kifungu cha ‘Mwanamume na mwanamke.’

وَمَا كَانَ لِمُؤْمِنٍ وَلَا مُؤْمِنَةٍ إِذَا قَضَى اللَّـهُ وَرَسُولُهُ أَمْرًا أَن يَكُونَ لَهُمُ الْخِيَرَةُ مِنْ أَمْرِهِمْ وَمَن يَعْصِ اللَّـهَ وَرَسُولَهُ فَقَدْ ضَلَّ ضَلَالًا مُّبِينًا ﴿٣٦﴾

36. Haiwi kwa muumini mwanamume wala muumini mwanamke, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapoamua jambo, kuwa na hiyari katika jambo lao. Na yeyote mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi amepotea upotevu ulio wazi.

وَإِذْ تَقُولُ لِلَّذِي أَنْعَمَ اللَّـهُ عَلَيْهِ وَأَنْعَمْتَ عَلَيْهِ أَمْسِكْ عَلَيْكَ زَوْجَكَ وَاتَّقِ اللَّـهَ وَتُخْفِي فِي نَفْسِكَ مَا اللَّـهُ مُبْدِيهِ وَتَخْشَى النَّاسَ وَاللَّـهُ أَحَقُّ أَن تَخْشَاهُ فَلَمَّا قَضَىٰ زَيْدٌ مِّنْهَا وَطَرًا زَوَّجْنَاكَهَا لِكَيْ لَا يَكُونَ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ حَرَجٌ فِي أَزْوَاجِ أَدْعِيَائِهِمْ إِذَا قَضَوْا مِنْهُنَّ وَطَرًا وَكَانَ أَمْرُ اللَّـهِ مَفْعُولًا ﴿٣٧﴾

37. Na pale ulipomwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu amemneemsha nawe ukamneemesha: Shikamana na mkeo na mche Mwenyezi Mungu. Ukaficha katika nafsi yako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, na ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea. Basi Zayd alipokwisha haja naye, tulikuoza ili isiwe tabu kwa waumini kuoa wake wa watoto wao wa kupanga watakapokuwa wamekwisha haja nao. Na amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kutekelezwa.

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

مَّا كَانَ عَلَى النَّبِيِّ مِنْ حَرَجٍ فِيمَا فَرَضَ اللَّـهُ لَهُ سُنَّةَ اللَّـهِ فِي الَّذِينَ خَلَوْا مِن قَبْلُ وَكَانَ أَمْرُ اللَّـهِ قَدَرًا مَّقْدُورًا ﴿٣٨﴾

38. Hakuna ubaya kwa Nabii kufanya ambalo amefaradhiwa na Mwenyezi Mungu. Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu kwa waliopita zamani na amri ya Mwenyezi Mungu ni kadara iliyokwisha kadiriwa.

الَّذِينَ يُبَلِّغُونَ رِسَالَاتِ اللَّـهِ وَيَخْشَوْنَهُ وَلَا يَخْشَوْنَ أَحَدًا إِلَّا اللَّـهَ وَكَفَىٰ بِاللَّـهِ حَسِيبًا ﴿٣٩﴾

39. Ambao walifikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na kumwogopa yeye, wala hawamwogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye anayetosha kuhisabu.

مَّا كَانَ مُحَمَّدٌ أَبَا أَحَدٍ مِّن رِّجَالِكُمْ وَلَـٰكِن رَّسُولَ اللَّـهِ وَخَاتَمَ النَّبِيِّينَ وَكَانَ اللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمًا ﴿٤٠﴾

40. Hakuwa Muhammad ni baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na mwisho wa mitume. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

KISA CHA ZAINAB BINT JAHSH

Aya 36 – 40

JE, MTUME ALIMTAMANI ZAINAB BINT JAHSH?

Maneno yamekuwa mengi kuhusiana na Aya hizi, kutoka kwa wanaoutetea Uislamu na pia maadui zake. Hawa waliutuhumu utakatifu wa Mtume, wakasema kuwa Mtume alimtamani Zainab bint Jahsh As-Saadiyya binti wa shangazi yake Umayma, mke wa huria[1] wake Zayd bin Haritha, na kwamba hilo alilificha kwa kuhofia watu, sio kumuhofia Mwenyezi Mungu. Wakitumia kauli yake Mwenyezi Mungu:“Ukaficha katika nafsi yako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, na ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea.”

Watetezi wa Uislamu wakawajibu kwa kiuhakika na kimantiki, ingawaje wengine wamefuata njia inayoleta tuhuma. Lakini pamoja na hivyo sisi tutakuwa na msimamo usiopendelea, tukilazimiana na dhahiri ya tamko, hatutafanya taawili wala kutoka kwenye dalili za Aya, kisha tumwachie msomaji mwenye kuchunga haki ahukumu mwenyewe. Kabla ya kuanza kufasiri tutatanguliza yafuatayo: Zayd bin Haritha alikuwa mtumishi wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) .

Siku moja akaja baba yake kwa Mtume na akamtaka ama amwache huru mwanawe au amuuzie kwa bei yoyote anayotaka. Mtume wa huruma akamwacha huru kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na akampa hiyari ya kwenda na baba yake au abakie.

Zayd akaathirika na Mtume kuliko kwenda na baba yake. Hapo baba yake, Haritha, akasema: “Enyi jamaa wa kikuraishi! Shuhudie kuwa huyu si mwanangu tena.” Mtume(s.a.w. w ) naye akasema:“Shuhudieni kuwa ni mwanangu.” Watu wakadhani kuwa Mtume amemfanya Zayd kuwa ni mwanawe wa kupanga, wakawa wanamwita Zayd bin Muhammad.

Waarabu kabla ya Uislamu walikuwa na desturi ya kumfanya mtoto wa kupanga ni sawa na mtoto wa kiuhakika hata kwenye mirathi na uharamu wa nasaba. Wenye akili wote wema na waovu wanaafikiana kuwa ada inayorithiwa kutoka jadi ni kama sharia na dini, haifai kwa yoyote kuihalifu kwa hali yoyote atakayokuwa.

Hekima yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ikataka kuiondoa ada hii, kwa vitendo sio kwa kauli tu, kwa kumuoza Zayd bin Haritha, ambaye jana alikuwa ni mtumwa asiyekuwa na uwezo wowote, mke mwenye hadhi ya kinasabu na uzuri. Hakuna anayemfikiria kumuoa isipokuwa mwinyi tu. Naye ni Zaynab bint Jahsh. Na mama yake ni Umayma bint Abdul Muttwalib, babu wa Mtume(s.a.w. w ) . Na kwamba Zayd amalize haja yake, ampe talaka kisha aolewe na Mtume(s.a.w. w ) .

Kwa sababu hilo litakuwa na nguvu na ufasaha zaidi wa kukataza desturi hiyo kwa upande mmoja. Na kwa upande mwingine mamwinyi wasione kigegezi kuwaoa waliotalikiwa na mahuria wao na walala hoi. Na zaidi ya hayo asiwe na madharau yule mwenye nasaba tukufu au walii wake kumuoza aliye chini yake kihadhi au kinasaba.

Mwenyezi Mungu akalipitisha hilo na akalikadiria, kama alivyoesema Mwenyezi Mungu (s.w.t):“Na amri ya Mwenyezi Mungu ni kadara iliyokwisha kadiriwa .” Mwenyezi Mungu (s.w.t) akampa wahyi Mtume wake mtukufu kwa kadhaa na kadari hiyo, akamwamrisha kumuoza Zaynaba kwa Zayd.

Basi Mtume akaja kumchumbia Zaynab kwa ajili ya huria wake Zayd na akaficha moyoni mwake yale aliyompa wahyi Mwenyezi Mungu kuwa amepitisha amuoe yeye baada ya Zayd. Aliuficha Mtume wahyi huu kwa sababu ulikuwa mzito kwa watu kutokana na kuwa mbali na desturi na mila zao. Kuficha huku ndiko alikokuashiria Mwenyezi Mungu kwa kauli yake: ‘Ukaficha katika nafsi yako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, na ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea.’

Hata hivyo Abdallah, kaka yake Zaynab, alikataa kumuoza dada yake kwa mtu ambaye si kufu yake naye mwenyewe pia akakataa kuolewa. Ndipo ikashuka kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu ‘Haiwi kwa mumin mwananamume wala mumin mwanamke, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapoamua jambo, kuwa na hiyari katika jambo lao.’ Basi hapo Zaynab na kaka yake wakainyenyekea hukumu ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na ikafungwa ndoa.

Baada ya kupita muda uhusiano wa ndoa ukawa una matatizo. Zayd akaenda kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu akitaka kumpa talaka Zaynab; hata hivyo akamkataza na akamwamrisha awe na subira, lakini amri ya Mwenyezi Mungu ni lazima ipite; ikawa talaka. Baada ya kwisha eda Mtume akamuoa na nidhamu ya mtoto wa kupanga ikavunjikilia mbali.

Kwa hiyo basi suala la Mtume kumuoa Zaynab si suala la matamanio na mapenzi; bali ni suala la amri ya Mwenyezi Mungu, kadha na kadari yake kwa nukuu ya Aya zilizo wazi ambazo wazushi wamejaribu kuzipotoa na kuziletea tafsiri ile wanayoitaka wao kulingana na hawa zao.

Hizi hapa nukuu zinazosema waziwazi: ‘Na amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kutekelezwa.’ ‘Na amri ya Mwenyezi Mungu ni kadara iliyokwisha kadiriwa.’ ‘Ukaficha katika nafsi yako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, na ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea.’

Makusdio ya amri ya Mwenyezi Mungu na yenye kukadiriwa na lile analolidhihirisha Mwenyezi Mungu ni jambo moja – Mtume kumuoa Zaynab ambako Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekutangaza waziwazi kwa kusema: ‘tulikuoza.’

Kama Mtume angelikuwa ameficha matamanio, waliyoyazusha wakuza mambo, basi Mwenyezi Mungu angeliyadhihirisha kutokana na kauli yake:‘Aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha.’

Zaidi ya hayo ni kuwa Zaynab alikuwa mikononi mwa Mtume (alikwa akimjua) na alikuwa akimtii zaidi kuliko viungo vyake. Kama angelikuwa anamtamani basi asingelingoja kwanza amuoze huria wake kisha amalize haja naye ndipo amuoe. Hasha! Bwana wa watu na majini hawezi kuwa na matamanio na hawa hizo. Yuko mbali kabisa na hayo.

Baada ya hayo ni kuwa Aya zote hizi zimekuja kwa maudhui moja, kwa hiyo zinaungana na kushikana; wala haiwezekani kwa hali yoyote kuzitenganisha na kuzigawa mafungu. Ama kuzichukua zote au kuziacha zote.

Mwenye kuchukua kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea,’ kuwa ni jumla iliyo peke yake na akaipuuza kauli yake: ‘aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha’ na ‘amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kutekelezwa,’ basi atakuwa ni katika wale wanaoipotosha haki kwa kuifanyia inadi na watu wake.

Kutokana na utangulizi huu, maana ya Aya yatakuwa yako wazi na pia makusudio yatakuwa yamejulikana. Kwa hiyo tutazipitia juu juu, tukiashiria mfuatano wa Aya kulingana na kisa cha ndoa ya kwanza hadi ya pili.

MAANA

Haiwi kwa mumin mwanamume wala mumin mwanamke, Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapoamua jambo, kuwa na hiyari katika jambo lao. Na yeyote mwenye kumuasi Mwenyezi Mungu na Mtume wake, basi amepotea upotevu ulio wazi.

Aya hii ilishuka pale Mtume(s.a.w. w ) alipomchumbia Zayanb bint Jahsh kwa ajili ya huria wake, Zayd bin Haritha. Zaynab akakataa yeye na kaka yake kwa vile Zayd sio kufu yake.

Maana ni kuwa ndoa hii ni amri ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na yeyote katika waumini hana hiyari mbele ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na atakayekataa basi atakuwa katika wapotevu wa kuangamia. Basi hapo Zaynab na kaka yake wakaridhia hukumu ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na ndoa ikakamilika.

Na pale ulipomwambia yule ambaye Mwenyezi Mungu amemneemsha nawe ukamneemesha.

Huyo ni Zayd bin Haritha. Mwenyezi Mungu alimneemesha kwa uislmu na usuhuba pamoja na Mtume naye Mtume akamneemessha kwa kumwacha huru.

Shikamana na mkeo na mche Mwenyezi Mungu.

Baada ya kupita muda, uhusiano wa ndoa baina ya Zaynab na Zayd ukawa sio mzuri. Akamwambia Mtume(s.a.w. w ) : “Nataka nimtaliki.” Mtume akamuusia kushikamana naye na amche Mwenyezi Mungu katika hali zote. Lakini Mtume alikuwa na hakika kuwa Zayd atakuja mwacha Zaynab kisha amuoe; isipokuwa hakulidhihirisha hilo kwa kuhofia lawama, ndio Mwenyezi Mungu akamwambia kwa kumwelekeza:

Ukaficha katika nafsi yako aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, na ukachelea watu na hali Mwenyezi Mungu ndiye mwenye haki zaidi ya kumchelea.

Makusudio ya aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha, ni ndoa ya Mtume kwa Zaynab baada ya kuachwa na Zayd. Mwenyezi Mungu aliidhihirisha kwa kauli yake:

Basi Zayd alipokwisha haja naye, tulikuoza.

Haya ndiyo aliyoyaficha Muhammad(s.a.w. w ) na akayadhihirisha Mwenyezi Mungu. sasa yako wapi hayo matamnio aliyoyaficha Muhammad katika nafsi yake. Kwanini Mwenyezi Mungu alinyamaza baada ya kusema: ‘Aliyotaka Mwenyezi Mungu kuyadhihirisha.’ Mtume alificha kujua kwake kuwa Zayd atamwacha Zaynab na amuoe yeye. Ni kuficha huku ndiko alikoambiwa na Mwenyezi Mungu kuwa mtu aliye kwenye nafasi yako hatilii umuhimu lawama za anayelaumu na kauli za wanaobobokwa.

Ili isiwe tabu kwa waumini kuoa wake wa watoto wao wa kupanga watakapokuwa wamekwisha haja nao. Na amri ya Mwenyezi Mungu ni yenye kutekelezwa.

Ndoa ya Mtume ilikuwa ni ubainifu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa waumini na kwa watu wote kuwa hakuna ubaya kuoa wake wa watoto wao wa kupanga ambao wamemaliza haja nao.

Hakuna ubaya kwa Nabii kufanya ambalo amefaradhiwa na Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwamrisha Mtume wake kumuoa mtalaka wa mwanawe wa kupanga, ili kubatilisha desturi hiyo ya kijahilia. Mtume akaitikia amri ya Mwenyezi Mungu.

Kwa hiyo Mtume au mwingine hana lawama kumuoa mtalaka wa mtoto wake wa kupanga, hata kama watu watamlaumu na kumtia kasoro, madamu Mwenyezi Mungu amemuhalalishia.

Huo ndio mwendo wa Mwenyezi Mungu kwa waliopita zamani na amri ya Mwenyezi Mungu ni kadara iliyokwisha kadiriwa. Ambao walifikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na kumwogopa yeye, wala hawamwogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ndiye anayetosha kuhisabu.

Makusudio ya wale waliopita na wale waliofikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu, ni mitume waliotangulia. Maana ni kuwa hakuna Nabii yeyote ila Mwenyezi Mungu alimtuma kulingania haki na kukataza batili, kama vile desturi na maigizo ambayo Mwenyezi Mungu hakuyateremshia dalili yoyote.

Mtume alifikisha ujumbe wa Mola wake kwa uaminifu na kwa ikhlasi, hakulegeza wala hakubabaisha na hakumwogopa yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, alipata tabu nyingi sana katika hilo.

Wako waliofanana nawe ewe Muhammad katika mitume waliopita. Hisabu ya wakadhibishaji na wenye inadi ni kwa Mwenyezi Mungu tu peke yake.Hakuwa Muhammad (s.a.w. w ) ni baba wa yeyote katika wanaume wenu kwa nasaba wala kwa kuzaa, kuweza kumzuia kumuoa mtalaka wa Zayd bin Haritha.

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alizaa watoto wane wa kiume, wa tatu kutokana na Khadija; nao ni: Qasim, Twayyib, na Twahir. Imesemekana kuwa ni wawili, kwamba Twahir ndiye huyo huyo Twayyib. Na mmoja aliyetokana na Maria Qibtiya ambaye ni Ibrahim. Wote walikufa utotoni.

Ama Hasan na Husein ni watoto wa binti yake Fatima aliyewazaa na Ali(a.s ) , lakini Mtume aliwazingatia kama wanawe, pale aliposema:“Wanangu hawa wawili ni maimamu wakisimama au wakikaa.” Pia alisema:“Watoto wa binti wote wananasibiana na baba yao; isipokuwa watoto wa Fatima, mimi ni baba yao.” Tazama Juz. 7 (6:84 – 90).

Bali ni Mtume wa Mwenyezi Mungu

Na Mtume si baba, ingawaje anawashughulikia sana waumini na kuwahu- rumia kuliko baba zao.

Na mwisho wa mitume, hakuna Nabii mwingine baada ya Muhammad(s.a.w. w ) wala sharia nyingine baada ya sharia ya kiislamu.

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu, ukiwemo ujuzi wa kujua pale atakapouweka ujumbe wake na kuuishiliza kwa Muhammad(s.a.w. w ) .

KWA NINI UTUME ULIISHIA KWA MUHAMMAD?

Waislamu wote wameafikiana kwa kauli moja kwamba hakuna wahyi kwa yeyote baada ya Muhammad(s.a.w. w ) Mwenye kulipinga hilo basi si mwislamu, mwenye kudai utume baada ya Muhammad ni wajibu kuawa na mwenye kutaka dalili ya atakayedai utume huu, kwa kutaraji kumsadiki, basi ni kafiri.

Katika Tafsiri ya Isamil Haqiy, Ruhul-bayan, imeelezwa:“Lau angekuja Nabii baada ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w. w ) angelikuwa Ali bin Abi Twalib, kwa sababu yeye yuko kwenye daraja ya Haruna kwa Musa.”

Unaweza kuuliza : Kwa nini utume umeishilia kwa Muhammad(s.a.w. w ) ?

Jibu : lengo la kwanza na la mwisho la kutumwa Nabii ni kufikisha kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa waja wake. Hakuna kitu chochote alichotaka Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwafikishia waja wake ila kimo kwenye Qur’an Tukufu. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:“Na tumekuteremshia Kitabu hiki kubainisha kila kitu.” Juz. 14 (16:89).Na akasema: “Hatukupuuza Kitabuni kitu chochote.” Juz. 7 (6: 38).

Yaani kitu chochote kinachoamabatana na wadhifa wa mitume na kuhusika kwao katika kuwaongoza viumbe na kuwaelekeza kwenye masilahi yao yanayodhamini ufanisi katika nyumba mbili (duniani na akhera).

Wala hakuna nyenzo ya kuthibitisha hakika hii ila kwa majaribio yasiyokubali shaka wala mjadala; yaani wataalamu wanatakikana waisome Qur’an kwa ukamilifu kuanzia alifu yake mpaka yee yake, kisha wailinganishe na vitabu vingine vya dini. Tuna hakika kabisa kuwa wataishia kwenye mambo mawili:

Kwanza : kwamba Qur’an kwa ufasaha wake, itikadi yake na sharia yake ni zaidi ya vitabu vyote vya kidini.

Pili : ndani ya Qur’an watakuta misingi na misimamo yote ambayo inaona na haja za watu, masilahi yao na maendeleo yao hadi siku ya Kiyama.

Hakuna maendelo yoyote ya kielemu au mapinduzi yoyote ya uhuru, ila Qur’an inayatolea mwito na kuyabariki. Na hakuna sharia yoyote anayoihitajia binadamu katika historia ila wataalam wanaweza kuitoa kutoka katika moja ya misingi ya Qur’an na misingi yake.

Mwenyezi Mungu na Mtume wake wamemruhusu kila mwenye uwezo na maandalizi kutoa tanzu katika mizizi ya Qur’an na kutoa hukumu iliyo na heri na masilahi kwa watu kwa namna fulani. Maana yake ni kuwa hukumu ya mujtahidi mwadilifu ni hukumu ya Qur’an na ya Mtume. Ndio maana kuna Hadith isemayo kuwa kuipinga hukumu yake ni kama kuipinga hukumu ya Mwenyezi Mungu.

Vile vile hii inamanisha kuwa Mtume yuko kwa kuweko Qur’an ambayo haingiliwi na batili mbele yake wala nyuma yake. Amepatia Ibn Al-arabiy aliposema: “Mwenye kuhifadhi Qur’an ameuunganisha utume mbavuni mwake” lakini kwa sharti ya kuizingatia na kuiamini kwa imani safi.

Zaidi ya hayo, Muhammad ni mtu aliyepewa wahyi; kama Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na mitume wengineo, lakini Mwenyezi Mungu amemuhusu kwa ambayo hakumuhusu nayo yeyote katika mitume. Pamoja na kuwa Mwenyezi Mungu alimpa kila Mtume ubora wote, kwa sababu utume ni mama wa ubora wote, lakini ubora una daraja. Kuna mbora na mbora zaidi, mkamilifu na mkamilifu zaidi, mjuzi na mjuzi zaidi na mkarimu na mkarimu zaidi. Mwenyezi Mungu anasema: “Na hakika tumewafadhilisha baadhi ya manabii kuliko wengine.” Juz. 15 (17:55).

Mwenyezi Mungu amemuhusu Muhammad(s.a.w. w ) kwa sifa na daraja ya hali ya juu; kiasi ambacho hakuna zaidi yake isipokuwa Mwenyezi Mungu na sifa za Mwenyezi Mungu. Miongoni mwa sifa hizo ni kukamilishwa wahyi ulioteremshwa kwake kukamilika katika pande zote. Dalili ya hilo ni hii Qur’an ambayo ni ubainifu wa kila kitu ambacho kinaingia katika wadhifa wa mitume. Basi wapi na wapi hiyo na vitabu vingine? Haya nawalete wapinzani kimoja tu kilicho na ubainifu wa kila kitu.

Bwana wa mitume na wa mwisho wao aliashiria haya kwa kusema:“Hakika mfano wangu na mfano wa manabii walikokuwa kabla yangu, ni kama mfano wa mtu aliyejenga jengo akalijenga vizuri na akalipamba; ispokuwa sehemu ya tofali moja. Ikawa watu wanapoliona wanastaajabu huku wakisema: “Mbona huweki hili tofali? Basi mimi ndio tofali hilo na mimi ni mwisho wa mitume.”

Tutaishiliza jawabu, kwa yale tuliyoyasema kwenye kitabu Imamatu Ali wal-aql (Uimamu wa Ali na akili): Mtu akisema: “Kwa nini Muhammad(s.a.w. w ) akawa ndiye mwisho wa mitume?

Tutamjibu kuwa Muhammad na dini ya Muhammad ina sifa zote za ukamilifu na imefikia kikomo; sawa na jua lilivyofikia kikomo cha nuru.

Hakuna nyota yoyote wala umeme wowote unaoweza kujaza nuru ulimwenguni kote zaidi ya jua. Kadhalika hakuna Nabii atakayeleta kheri kwa watu baada ya Muhammad(s.a.w. w ) . Maudhui haya yanaungana na tuliyoyaandika kwa anuani ya ‘Dini na maisha’ katika Juz. 9 (8:24), Juz. 15 (17: 9) na Juz. 21 (30:30).