TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA15%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 27888 / Pakua: 4988
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

1

2

3

22

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini Na Nane: Surat Saad. Imeshuka Makka, Ina aya 88

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

ص وَالْقُرْآنِ ذِي الذِّكْرِ ﴿١﴾

1. Swaad. Naapa kwa Qur’an yenye ukumbusho.

بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا فِي عِزَّةٍ وَشِقَاقٍ ﴿٢﴾

2. Lakini waliokufuru wamo katika majivuno na upinzani.

كَمْ أَهْلَكْنَا مِن قَبْلِهِم مِّن قَرْنٍ فَنَادَوا وَّلَاتَ حِينَ مَنَاصٍ ﴿٣﴾

3. Vizazi vingapi tumeviangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwishapita.

وَعَجِبُوا أَن جَاءَهُم مُّنذِرٌ مِّنْهُمْ وَقَالَ الْكَافِرُونَ هَـٰذَا سَاحِرٌ كَذَّابٌ ﴿٤﴾

4. Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anayetokana na wao. Na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.

أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ﴿٥﴾

5. Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili kweli ni jambo la ajabu.

وَانطَلَقَ الْمَلَأُ مِنْهُمْ أَنِ امْشُوا وَاصْبِرُوا عَلَىٰ آلِهَتِكُمْ إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ يُرَادُ ﴿٦﴾

6. Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililopangwa.

مَا سَمِعْنَا بِهَـٰذَا فِي الْمِلَّةِ الْآخِرَةِ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا اخْتِلَاقٌ ﴿٧﴾

7. Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.

أَأُنزِلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ مِّن ذِكْرِي بَل لَّمَّا يَذُوقُوا عَذَابِ ﴿٨﴾

8. Ati yeye ndiye aliyeteremshiwa mawaidha kati yetu?” Bali wao wana shaka na mawaidha yangu; bali hawajaionja adhabu yangu.

أَمْ عِندَهُمْ خَزَائِنُ رَحْمَةِ رَبِّكَ الْعَزِيزِ الْوَهَّابِ ﴿٩﴾

9. Au wanazo wao hazina za rehema za Mola wako, Mwenye nguvu, Mpaji?

أَمْ لَهُم مُّلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَلْيَرْتَقُوا فِي الْأَسْبَابِ ﴿١٠﴾

10. Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake? Basi na wazipande sababu zote.

جُندٌ مَّا هُنَالِكَ مَهْزُومٌ مِّنَ الْأَحْزَابِ ﴿١١﴾

11. Ni jeshi litakaloshindwa miongoni mwa makundi yatayoshindwa.

NAAPA KWA QUR’AN YENYE MAWAIDHA

Aya 1 – 11

MAANA

Swaad.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1).

Naapa kwa Qur’an yenye ukumbusho, Lakini waliokufuru wamo katika majivuno na upinzani.

Jawabu la kiapo linakadiriwa kuwa ni ‘Hakika hiyo ni haki.’ Makuraishi walikadhibisha Qur’an ambayo ina kheri yao na enzi yao. Ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akaapa kwa Qur’an yenyewe kwamba hiyo ni haki kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kwamba hakuna sababu ya kukadhibisha huku isipokuwa kiburi cha wakadhibishaji, kuikimbia kwao haki na uadui wao kwa Muhammad(s.a.w. w ) .

Kuapa kwake Mwenyezi Mungu kwa Qur’an kunaashiria kwamba hiyo Qur’an kushinda kwake kunafahamishwa na ufasaha wake na ukweli wake unafahamishwa na mafunzo yake. Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawahadharisha makuraishi na kuwakumbusha maangamizi ya waliotangulia pale walipowakadhibisha mitume, kwa kusema:

Vizazi vingapi tumeviangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwishapita.

Wa mwanzo walijizuia na haki na kuwafanya watu wa haki ni mahasimu wao; sawa na mlivyofanya nyinyi. Walipojiwa na adhabu wakaanza kurudi nyuma na kunyenyekea, lakini muda ulikwishapita tena. Kwa hiyo bora muamini sasa kabla ya kupita muda mkajuta ambapo majuto hayatafaa kitu tena.

KUMWIGA MWENYE KUMPWEKESHA MUNGU NA KUMWIGA MSHIRIKINA

Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anayetokana na wao.

Muhammad(s.a.w. w ) ni Mkuraishi, hilo halina shaka, lakini si katika vigogo wala mataghuti wao, vipi awe ni miongoni mwao? Lau angelikuwa mion- goni mwao angewafanya watu watumwa wake na akawa na hazina au nyumba ya dhahabu. Tazama Juz. 15 (17: 90) kifungu cha ‘Kupenda mali’ na Juz. 18 (25:7) kifungu cha ‘Mantiki ya watu wa pesa ni benki na ardhi.’

Na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo.

Kwa nini ni muongo?

Jibu ni:

Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili kweli ni jambo la ajabu.

Ajabu kwa hawa sio kuwa Muhammad(s.a.w. w ) anapinga shirki na kuweko waungu wengi, ingawaje hilo wanaliwaza, lakini ajabu hasa ni Muhammad(s.a.w. w ) kutoka kwenye maigizo yao na mazowea yao waliyoyarithi tangu jadi na jadi. Wao hasa wanatetea kuiga kwa mababa na mababu zao kuwa ndio dini na msingi; sio kuwa wanatetea masanamu kwa kuwa ni masanamu. Wanatetea masanamu kwa vile ni turathi na urithi kutoka kwa wakale wao:

إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَىٰ أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَىٰ آثَارِهِم مُّقْتَدُونَ ﴿٢٣﴾

“Kwa hakika tuliwakuta baba zetu juu ya mila na hakika sisi tunafuata nyayo zao.” (43:23).

Imani ya wajinga hawa ni sawa na imani ya washirikina, kwa sababu chimbuko la imani mbili ni moja nalo ni kuiga. Tofuati ni kuwa kumuiga mwenye kumpwekesha Mungu ni sahihi na kwenye kukubalika kwa sababu kuna msingi wa hali halisi; kama, kwa mfano, nikikuambia:

“Mwenye nadharia ya mvutano ni Newton na mwenye nadhariya ya uwiyano ni Einstein” Lakini kuiga kwa washirikina ni upotevu.

Na mwenye kuiga hivyo atabeba majukumu na atawajibishwa ila akiwa hana ajualo; kama mnyama. Kwa sababu kumshirikisha Mwenyezi Mungu hakuna msingi wowote kwake.

Kwa maneno mengine ni kuwa fikra itakuwa ni ya kweli ikiwa inatokana na uhalisi wa hali; iwe imetokana na elimu au kuiga. Tazama Juz.2 (2:168-170). Kifungu: ‘Kufuata na msingi wa itikadi.’

Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililopangwa. Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu.

Makusudio ya wakubwa wao ni vigogo wa kikuraishi. Kudumu kwenye miungu ni kudumu kuiabudu. Jambo lililopangwa ni kudumu kwenye ibada ya masanamu. Mila ya mwisho ni itikadi ya utatu ya kimasihi (kikiristo). Washirikina waliita ya mwisho kwa vile ndiyo dini ya mwisho kujitokeza wakati wao.

Kwenye Tafsir Tabariy na nyinginezo imeelezwa kuwa wazee wa kikuraishi walimwendea Abu Twalib na kumwambia: “Mwana wa nduguyo na aachane na miungu yetu nasi tutamwacha na Mungu wake anayemwabudu. Abu Twalib alipomwambia hilo Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alisema:

“Ninawataka neno moja tu waliseme, basi waarabu na waajemi watawafuata.” Wakasema tutakukubalia hilo na mengine kumi, ni lipi hilo? Akasema: “Hapana mola isipokuwa Mwenyezi Mungu. (Lailaha illa llah)” wakaondoka zao huku wakisema: “Hivi miungu yote ameifanya kuwa mmoja!”

Riwaya hii inaafikiana na dhahiri ya Aya na inasaidiwa na hali halisi ya washirikina na nafasi ya mzee aliyelemewa.

Ati yeye ndiye aliyeteremshiwa mawaidha kati yetu?

Mwenyezi Mungu atamchagua vipi Muhammad na hali hana jaha wala mali?

Bali wao wana shaka na mawaidha yangu,

Wao ni washirikina. Kwa sababu miongoni mwao kuna waliompinga Muhammad(s.a.w. w ) kwa hasadi na wengine wakampinga kwa kulinda masilahi yao.

Bali hawajaionja adhabu yangu.

Wakishaionja shaka itawaondokea na “wataficha majuto” Juz. 11 (10:54).

Au wanazo wao hazina za rehema za Mola wako, Mwenye nguvu, Mpaji?

Makusudio ya hazina za rehema hapa ni utume tu, au utume na neema nyinginezo za Mwenyezi Mungu na hisani yake. Maana ni kuwa kwa nini washirikina wanalalamikia na kupinga rehema ya Mwenyezi Mungu ya kumchagua kwake kuwa mjumbe kwa walimwengu? Je ni kwa kuwa wao wanamiliki hiyari hii badala ya Mwenyezi Mungu?

Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake?

Mmliki wa ulimwengu ni yule anayemiliki utume, kuutoa na kumuenzi nao amtakye. Na washirikina hawamiliki chochote kwa Mwenyezi Mungu kuweza kumpa utume mtu mkubwa kati ya miji miwili.

Kuna jambo moja ambalo wanaweza kwalo kumiliki mbingu na ardhi nalo ni Basi nawazipande sababu zote.

Makusudio ya sababu ni njia na nyenzo. Maana ni kuwa utume anauhukumu ambaye anamiliki ulimwengu na viliomo ndani yake. Basi vigogo wa kikuraishi wakitaka kumchagua kwa utume yule wanayemtaka, kabla ya chochote nawamiliki nyenzo za kufikia kwenye umiliki huu ikiwa wanaweza. Changamoto hii ni ubainifu wa kutosha kabisa.

Ni jeshi litakaloshindwa miongoni mwa makundi yatayoshindwa.

Wale waliokupiga vita, ewe Muhammad, si chochote, watashindwa mbele ya mwito pamoja na wingi wa majeshi na vikosi vyao.

كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ ذُو الْأَوْتَادِ ﴿١٢﴾

12. Walikadhibisha kabla yao kaumu ya Nuh, na kina A’adi na Firauni mwenye vigingi.

وَثَمُودُ وَقَوْمُ لُوطٍ وَأَصْحَابُ الْأَيْكَةِ أُولَـٰئِكَ الْأَحْزَابُ ﴿١٣﴾

13. Na Thamud na kaumu ya Lut na watu wa mwituni. Hayo ndiyo makundi.

إِن كُلٌّ إِلَّا كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ عِقَابِ ﴿١٤﴾

14. Wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahili adhabu yangu.

وَمَا يَنظُرُ هَـٰؤُلَاءِ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً مَّا لَهَا مِن فَوَاقٍ ﴿١٥﴾

15. Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.

وَقَالُوا رَبَّنَا عَجِّل لَّنَا قِطَّنَا قَبْلَ يَوْمِ الْحِسَابِ ﴿١٦﴾

16. Na wao husema: Mola wetu Tuletee upesi sehemu yetu kabla ya Siku ya Hisabu.

اصْبِرْ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَاذْكُرْ عَبْدَنَا دَاوُودَ ذَا الْأَيْدِ إِنَّهُ أَوَّابٌ ﴿١٧﴾

17. Subiri kwa wayasemayo, Na umkumbuke mja wetu Daud. Mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia.

إِنَّا سَخَّرْنَا الْجِبَالَ مَعَهُ يُسَبِّحْنَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِشْرَاقِ ﴿١٨﴾

18. Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi

وَالطَّيْرَ مَحْشُورَةً كُلٌّ لَّهُ أَوَّابٌ ﴿١٩﴾

19. Na pia ndege waliokusanywa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.

وَشَدَدْنَا مُلْكَهُ وَآتَيْنَاهُ الْحِكْمَةَ وَفَصْلَ الْخِطَابِ ﴿٢٠﴾

20. Na tukautia nguvu ufalme wake. Na tukampa hikima na kukata hukumu.

SUBIRI JUU YA HAYO WANAYOSEMA

Aya 12 – 20

MAANA

Walikadhibisha kabla yao kaumu ya Nuh, na kina A’adi na Firauni mwenye vigingi Na Thamud na kaumu ya Lut na watu wa mwituni.

Wote hawa waliwakanusha mitume; baadhi yao wakaangamizwa kwa tufani; kama vile watu wa Nuh, wengine kwa kuzama baharini, kama Firauni.

Kuwa na vigingi ni kinaya cha kujikita ufalme wake kama linavyokitwa hema na vigingi kwenye ardhi.

“Basi Thamud waliangamizwa kwa balaa kubwa (la ukelele wa adhabu). Ama A’d waliangamizwa kwa upepo mkali usiozuilika” (69:5-6).

Kaumu ya Lut majumba yao yalipinduliwa juu chini. Tazama Juz. 12 (11:82). Watu wa mwituni Mwenyezi Mungu aliwaadhibu adhabu chungu. Tazama Juz.14 (15:78) na Juz. 19 (26:176).

Hayo ndiyo makundi. Wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahili adhabu yangu.

Mwenyezi Mungu aliviadhibu vikosi vya shetani kwa sababu ya madhambi yao; ikiwa ni malipo ya yale waliyoyafanya. Je, wanaomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) hawahofii kuwafika yaliyowafika hao.

Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda.

Hawa ni waliomkadhibisha Muhammad(s.a.w.w) . Maana ni; wanangoja nini kwa Mungu baada ya kukukadhibisha ewe Muhammad na hali Mwenyezi Mungu, kwa neno moja tu anaweza kuwapelekea adhabu itayowafyeka katika muda ambao hawataweza kuusia wala kurudi kwa watu wao.

Na wao husema: Mola wetu! Tuletee upesi sehemu yetu kabla ya Siku ya Hisabu.

Yaani sehemu yetu ya adhabu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwatishia na adhabu ya Jahannam kupitia kwa Mtume wake mtukufu, lakini wao wakasema kwa madharau kuwa ikiwa ni kweli basi anangoja nini mpaka siku ya Kiyama? Basi na iwe duniani sio akhera.

Subiri kwa wayasemayo, kuwa wewe ni mwongo na mengineyo ya uzushi. Kwani mwisho wa mambo yao ni hasara na kusalimu amri.

Mtume(s.a.w.w) alisubiri na kuvumilia adha ya washirikina kwa muda wa mika 13 na vitimbi vya wanafiki kwa miaka kadhaa huko Madina. Alivumilia muda huu mrefu akiwa na mategemeo ya mustkabali hata kama utachelewa. Hazikupita siku Muhammad(s.a.w.w) akashinda kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, na akaudhihirisha uislamu kuliko dini zote, wajapochukia washirikina.

Na umkumbuke mja wetu Daud.

Hili ni jina la kiebrania lenye maana ya mpendwa (mahboob). Yeye alikuwa mfalme wa pili wa Kiyahudi, wa kwanza alikuwa Talut:

إِنَّ اللَّـهَ قَدْ بَعَثَ لَكُمْ طَالُوتَ مَلِكًا ﴿٢٤٧﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu amewachagulia Talut kuwa mfalme.” Juz. 2 (2:247).

Tawrat imemwita Talut huyu kwa jina la Shaul (Saulo). Imeelezwa kwenye Kamusi ya Kitabu kitakatifu’ kwamba Shaul ndiye mfalme wa kwanza wa waisrail na kwamba Daud alipigana katika jeshi lake. Razi anasema kuwa Mwenyezi Mungu amemsifu Daud kwa sifa nyingi. Kisha akazifafanua kwenye kurasa nne. Tutazifupiliza kwenye mistari ifuatayo: Mwenyezi Mungu alimwambia Muhammad(s.a.w.w) :

Subiri kwa wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daud.

Hii ni karama kwa Daud.

Mwenye nguvu; yaani mwenye nguvu ya kumtii Mwenyezi Mungu.

Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia; yaani akiyarudisha mambo yote kwa Mwenyezi Mungu.

Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye. Na pia ndege waliokusanywa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake.

Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَا جِبَالُ أَوِّبِي مَعَهُ وَالطَّيْرَ ﴿١٠﴾

“Enyi milima sabihini pamoja naye na ndege” Juz. 22 (34:10).

وَسَخَّرْنَا مَعَ دَاوُودَ الْجِبَالَ يُسَبِّحْنَ وَالطَّيْرَ ﴿٧٩﴾

“Na tuliidhalilisha milima na ndege pamoja na Daud ikisabihi.” Juz. 17: (21:79).

Kwa maelezo zaid kuhusu Daud rejea huko.

Na tukautia nguvu ufalme wake.

Na tukampa hikima.

Ambayo ni kukiweka kitu mahali pake. Kwa ibara ya Razi ni elimu na kuitumia. Imeitwa hivyo kwa sababu hekima ni kupanga mambo na kuyaweka sawa.

Na kukata hukumu.

Razi anasema ni uwezo wa kudhibiti maana na kuyatolea tafsiri ya upeo wa juu. Hivi ni zaidi ya tunavyofahamu kuwa kukata hukumu ni elimu ya kuhukumu, kwa uadilifu, mambo ya wanaoteta.

Hivi ndivyo Qur’an ilivyomsifu Daud kwa sifa bora za ukamilifu, lakini Tawrat imemsifu kwa sifa mbaya mbaya; kama dhulma, ufuska, hadaa na kunyanyag’anya wanawake; kiasi amabacho waliochangia kuweka kamusi ya Kitabu Kitakatifu wakasema katika ukurasa 365, chapa ya mwezi Machi 1967, ninanukuu: “Mara nyingine Daud aliweza kufanya mambo ya kufedhehesha na ya aibu.”

23

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

وَهَلْ أَتَاكَ نَبَأُ الْخَصْمِ إِذْ تَسَوَّرُوا الْمِحْرَابَ ﴿٢١﴾

21. Na je, imekufikia habari ya wagombanao walipopindukia ukuta kuingia mihrabu.

إِذْ دَخَلُوا عَلَىٰ دَاوُودَ فَفَزِعَ مِنْهُمْ قَالُوا لَا تَخَفْ خَصْمَانِ بَغَىٰ بَعْضُنَا عَلَىٰ بَعْضٍ فَاحْكُم بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَلَا تُشْطِطْ وَاهْدِنَا إِلَىٰ سَوَاءِ الصِّرَاطِ ﴿٢٢﴾

22. Walipomuingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Ni mahasimu wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoze kwenye njia iliyo sawa.

إِنَّ هَـٰذَا أَخِي لَهُ تِسْعٌ وَتِسْعُونَ نَعْجَةً وَلِيَ نَعْجَةٌ وَاحِدَةٌ فَقَالَ أَكْفِلْنِيهَا وَعَزَّنِي فِي الْخِطَابِ ﴿٢٣﴾

23. Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisini na tisa; na mimi nina kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo! Na amenishinda kwa maneno.

قَالَ لَقَدْ ظَلَمَكَ بِسُؤَالِ نَعْجَتِكَ إِلَىٰ نِعَاجِهِ وَإِنَّ كَثِيرًا مِّنَ الْخُلَطَاءِ لَيَبْغِي بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَقَلِيلٌ مَّا هُمْ وَظَنَّ دَاوُودُ أَنَّمَا فَتَنَّاهُ فَاسْتَغْفَرَ رَبَّهُ وَخَرَّ رَاكِعًا وَأَنَابَ ﴿٢٤﴾

24. Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao. Isipokuwa walioamini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daud akaona kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba maghufira Mola wake na akaanguka kunyenyekea na kutubia.

فَغَفَرْنَا لَهُ ذَٰلِكَ وَإِنَّ لَهُ عِندَنَا لَزُلْفَىٰ وَحُسْنَ مَآبٍ ﴿٢٥﴾

25. Basi tukamghufiria kwa hayo. Naye kwa hakika anao ukuruba na marejeo mazuri kwetu.

KONDOO 99 KWA KONDOO 1

Aya 21 – 25

TAFSIRI NA HADITH ZA KIISRAIL

Baadhi ya wafasiri, wakifafanua Aya hii, wamemnasibishia Nabii Daud mambo ambayo si laiki hata ya mtu wa kawaida mwenye murua na haya; sikwambii tena mtume aliye maasumu. Wakataja kisa kirefu kutoka katika Biblia kitabu cha 2 Samweli: 11 na 12, kutoka agano la kale ambalo mahala pake pamechukuliwa na hukumu ya Qur’an. Nukuu za agano lenyewe kuhusiana na hilo haziingiliki akili.

Muhtasari wa kisa chenyewe ni kuwa Daud alimtamani mke wa mmoja wa watumishi wake aliye pia mwanajeshi wake. Basi akamfanyia hila ya kumuua ili amchukue mkewe. Biblia inasema kuwa Mwenyezi Mungu alikasirika sana na kumkemea kwa kitendo kibaya alichokifanya; miongoni mwa aliyoyasema ni “…Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, nawe ukamtwaa mkewe awe wako… Basi sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau…Nitakuondokeshea uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako mbele ya jua hili. Maana wewe ulifanya jambo hili kwa siri; bali mimi nitalifanya jambo hili mbele ya Israil wote na mbele ya jua” (2 Samweli 12:9-12.).

Katika 1 Wafalme 1 imeelezwa kuwa jina la mke wa Uria ni Bath-sheba naye ndiye mama yake Suleiman bin Daud.

Daud azini kwa siri na Mwenyezi Mungu, badala ya kumpa adhabu ya hadd ya zina au kumlaumu na kumtaka atubie, badala ya kumfanyia hivyo, anamtia adabu kwa kuwavunjia heshima wakeze wawe uchi na wafanye machafu hadharani kweupe mchana kadmanasi!

Haya ndio maandiko matakatifu yanavyomsifu muumba kwa sifa za unyama. Mwenyezi Mungu Mtukufu ametakata kabisa na hayo wanayomsifu nayo. Huu ni mfano mmoja kati ya mifano kadhaa. Soma kuhusu kupigana miereka Mwenyezi Mungu na Ya’qub na kushindikana kupatikana mshindi, mpaka Ya’qub akalazimika kupiga mfupa wa paja wa Mwenyezi Mungu.

Vile vile soma yaliyoandikwa kwenye biblia, Kumbukumbu la Torat, 7, kwamba Mungu amewahalalishia Mayahudi kula mataifa yote, bila ya huruma. Baadhi ya wafasiri wametegemea Hadith hizi za kiisrail, katika kufasiri Aya za Qur’an yenye mawaidha, biashara na maonyo; ikiwemo hii tuliyo nayo. Kwa hiyo ni juu ya msomaji kuzikabili kauli zao na tafsiri zao kwa jicho la hadhari sana.

MAANA

Na je, imekufikia habari ya wagombanao walipopindukia ukuta kuingia mihrabu. Walipomuingilia Daudi, naye akawaogopa.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamsilmulia Nabii wake mtukufu kisa cha Daud, kwamba siku moja Daud alipokuwa amemwelekea Mola wake kwenye mswala wake, ghafla watu wawili wakajitokeza mbele yake ana kwa ana. Basi kushtukiza huku kulimshtua; tena kuingia kwao kwa njia isiyokuwa ya kawaida.

Hata hivyo kuingia kwao huko, kusikokuwa kwa kawaida, hakufahamishi lolote kuwa ni malaika; kama walivyolitolea dalili baadhi ya wafasiri. Kwa sababu hata binadamu pia anaweza kuingia nyumbani kwa njia isiyokuwa ya kawaida kutokana na sababu fulani. Pia Aya haikuashiria kuwa ni malai- ka. Kwa hiyo hakuna sababu ya kuleta taawili ya kuwa ni malaika.

Wakasema: Usiogope! Ni mahasimu wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuon- goze kwenye njia iliyo sawa.

Walipoona hofu iliyomjaa, haraka sana wakamtuliza na kusema, sisi tumekuja kwako kuhukumiwa, basi utuhukumu kwa uadilifu na utuongoze kwenye haki wala usikengeuke nayo. Kisha mmoja wao akasema:

Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisini na tisa; na mimi nina kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo! Na amenishinda kwa maneno.

Hapa hakuna haja yoyote ya kuleta taawili. Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa tukio hili lilitokea wakati wa zama za Nabii Daud; nalo lina mfano wake katika kila zama na kila wakati; hasa wakati wetu huu wa sasa. Kwa hiyo ni wajibu kuichukulia dhahiri yake na kuitumia.

Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake.

Daud aliyasema haya kabla ya kusikiliza ushahidi kutoka kwa mdai na kujibu mdaiwa.

Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao.

Hapa itabidi kuchukulia majazi neno washirikia, kuwa na maana ya wenye mabavu. Kwa sababu hakukua na ushirika wowote kati ya wale mahasimu wawili.

Isipokuwa walioamini na wakatenda mema. Na hao ni wachache.

Nguvu inakuwa ni ya haki ikiwa kwa watu wema, lakini ikiwa kwa waovu basi, bila shaka yoyote, itakuwa dhidi ya haki. Na watu wema ni wachache kwa idadi, lakini wana nguvu katika maadili yao na sifa zao.

Na Daud akaona kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba maghufira Mola wake na akaanguka kunyenyekea na kutubia

Baada ya Daud kutoa hukumu, alitanabahi kuwa amehukumu kabla ya kutaka dalili upande wa pili. Kwa hiyo akajuta na akamuomba msamaha Mwenyezi Mungu.

Basi tukamghufiria kwa hayo. Naye kwa hakika anao ukuruba na marejeo mazuri kwetu.

Mwenyezi Mungu alimsamehe Daud kwa vile alikuwa ni miongoni mwa waliotangulia kumtii Mwenyezi Mungu na kutaka radhi yake.

Katika kitabu Uyunil-akhbar, imeelezwa kuwa mtu mmoja alimuuliza Imam Ar-Ridha(a.s ) kuhusu kisa cha Daud na Uria na mkewe, Imam akapinga yanayonasibishiwa Daud. Muulizaji akauliza: Kosa lake lilikuwa nini ewe mwana wa Mtume wa Mwenyezi Mungu? Basi akajibu kwa jawabu refu, miongoni mwake ni: “Daud alifanya haraka kusema: “Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake,” bila ya kumuuliza yule mwingine unasemaje? Basi hilo likuwa ni kosa la rasimu ya mahakama, sio kosa la wanavyosema watu.

Kwani hukusikia Mwenyezi Mungu Mtukufu alivyomwambia Daud: “Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya uwe Khalifa ardhini.”

Unaweza kuuliza : Vipi Daud alihukumu bila ya ushahidi, na tunajua kuwa mitume wamehifadhiwa na makosa (ni maasumu).

Jibu : kuwa maasumu hakumaanishi kuwa na maumbile mengine yasiyokuwa ya kibinadamu, hapana! Maasumu ni mtu kama watu wengine. Maana ya isma ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamlinda wakati wowote; hata wakijaribu watu kumhadaa kwa mandhari ya uzuri, basi Mwenyezi Mungu mara moja humwongoza kwenye haki na uhakika, kabla ya kuiingia mtegoni. Na hivyo ndivyo ilivyomtokea Daud. Mwenye kondoo mmoja alijaribu kumhadaa kwa namna yake ya kutaka kuhurumiwa, lakini Mwenyezi Mungu alimpa ilhamu ya uhakika kabla ya kutoa hukumu, akafahamu na akatubia.

Mtume alitokewa na yaliyo karibu na haya na akakurubia kuhadaiwa lau si Mwenyezi Mungu kumwimarisha kwa kumwambia: “Hakika tumekuteremshia Kitabu kwa haki ili upate kuhukumu baina ya watu kwa alivyokufahamisha Mwenyezi Mungu; wala usiwe mtetezi wa wenye kufanya hiyana. Na muombe maghufira Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu. Wala usiwatetee wale ambao wamezihini nafsi zao...” Juz. 5 (4:105 – 107).

Na akasema Mwenyezi Mungu kumwambia Mtume wake Mtukukufu:

وَلَوْلَا أَن ثَبَّتْنَاكَ لَقَدْ كِدتَّ تَرْكَنُ إِلَيْهِمْ شَيْئًا قَلِيلًا ﴿٧٤﴾

“Lau sikukuweka imara ungelikurubia kuwaelekea kidogo.” Juz. 15 (17:74).

Kuna Hadith isemayo: “Mimi ni mtu kama nyinyi, isipokuwa ninapewa wahyi tu. Na nyinyi mnakuja kuamuliwa kwangu. Pengine mmoja wenu anaweza kuwa hodari wa kusema kuliko mwingine na nikahukumu kulingana na nilivyosikia.

Ikiwa mtu nitamuhukumia kumpatia kitu katika haki ya ndugu yake, basi ajue ninampatia kipande cha Moto.”

Ingawaje Hadith hii haingii moja kwa moja kwenye maudhui haya tuliyo nayo, lakini tunaweza kuiunganisha nayo. Ama toba ya manabii na kutaka kwao maghufira ya dhambi, hiyo ni aina ya ibada na unyenyekevu kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t). Hilo tumeliashiria mara kadhaa.

يَا دَاوُودُ إِنَّا جَعَلْنَاكَ خَلِيفَةً فِي الْأَرْضِ فَاحْكُم بَيْنَ النَّاسِ بِالْحَقِّ وَلَا تَتَّبِعِ الْهَوَىٰ فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ إِنَّ الَّذِينَ يَضِلُّونَ عَن سَبِيلِ اللَّـهِ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ بِمَا نَسُوا يَوْمَ الْحِسَابِ ﴿٢٦﴾

26. Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya uwe Khalifa ardhini. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio, yakakupoteza Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanaopotea Njia ya Mwenyezi Mungu, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.

وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاءَ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا بَاطِلًا ذَٰلِكَ ظَنُّ الَّذِينَ كَفَرُوا فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِنَ النَّارِ ﴿٢٧﴾

27. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo kati yake bure. Hiyo ni dhana ya waliokufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto.

أَمْ نَجْعَلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ كَالْمُفْسِدِينَ فِي الْأَرْضِ أَمْ نَجْعَلُ الْمُتَّقِينَ كَالْفُجَّارِ ﴿٢٨﴾

28. Je! Tuwafanye walioamini na wakatenda mema kama wafisadi katika ardhi? Au tuwafanye wenye takua kama waovu?

كِتَابٌ أَنزَلْنَاهُ إِلَيْكَ مُبَارَكٌ لِّيَدَّبَّرُوا آيَاتِهِ وَلِيَتَذَكَّرَ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٢٩﴾

29. Hiki ni Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.

TUMEKUFANYA UWE KHALIFA ARDHINI

Aya 26 – 29

MAANA

Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya uwe Khalifa ardhini.

Kila mtu aliyeko, au atakayekuweko, ardhini basi huyo ni khalifa wa Mwenyezi Mungu ardhini; kwa maana yakuwa ana majukumu mbele ya Mwenyezi Mungu ya kufanya mambo ya heri duniani na Akhera katika maisha haya.

Hayo ndio maana ya ukhalifa ardhini kwa hali yoyote ile; isipokuwa watu wanatofautiana kulingana na majukumu yenyewe; ambapo kila mmoja anatakiwa atekeleze kulingana na uwezo na wadhifa wake.

Kwa kuwa wadhifa wa manabii ni kutoa bishara na hadhari, ili watu wasiwe na hoja mbele ya Mwenyezi Mungu, basi imekuwa ni wajibu kwao kuwahukumu watu kwa haki na wengine wawasikilize wao.

Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio, kwa sababu unabii uko hivyo kimaumbile.

Kwa maneno mengine ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) anamchagulia wahyi wake yule anayeiamini haki na kuitumia na inakuwa ni muhali kwake kukosea.

Yakakupoteza Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanaopotea Njia ya Mwenyezi Mungu, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu.

Muovu zaidi katika watu ni yule mwenye kumhalifu Mola wake na akafuata matamanio yake. Kuna Hadith isemayo: “Hakika ninalolihofia zaidi kwenu ni hawaa na tamaa nyingi. Hawaa inaipinga haki na tamaa nyingi inasahauliza akhera.”

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo kati yake bure.

Lau katika kuumbwa mbingu na ardhi kungelikua na chembe ya mchezo au hivi hivi tu, basi ulimwengu usingeendelea na nidhamu kwa mamilioni ya miaka.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:191).

Hiyo ni dhana ya waliokufuru. Ole wao waliokufuru kwa Moto.

Hiyo inaashiria kuwa hakuna tofauti kati ya aneyepinga kuweko Mwenyezi Mungu kabisa na yule anayekubali, lakini akapinga kuweko hekima katika kuumba kwake. Kwa sababu dalili zake ni wazi na alama zake ziko kweupe.

Imam Ali(a.s ) anasema:“Amekadiria aliyoumba akapangilia makadirio yake; akapangilia akafanya kwa uangalifu mipangilio yake; akaelekeza kwa maelekezo yake, lakini hakupetuka mpaka wa cheo chake wala hakupunguza ukomo wa lengo lake.”

Je! Tuwafanye walioamini na wakatenda mema kama wafisadi katika ardhi? Au tuwafanye wenye takua kama waovu?

Tofauti baina ya mwema na mfisadi na baina ya mwenye takua na muovu ni sawa na tofauti baina ya kipofu na mwenye kuona. Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (5:100) na Juz. 7 (6:50).

Katika kitabu Ahkamul-qur’an cha Kadhi Abi Bakri, ambaye ni maarufu kwa jina la Ibnul-arabiy, amesema: “Aya hii iliwashukia bani Hashim; na kwamba walioamini na kuwa na takua ni Ali bin Abi Twalib, ndugu yake Ja’far, Ubayda bin Tufayl, Al-harth bin Tufayl, Ummu ayman na wengineo, na kwamba wafisadi na waovu ni Bani Abd Shams.

Hiki ni Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.

Hapa anaambiwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) . Kitabu ni Qur’an, nayo ina baraka kwa kila mwenye kuiamini, ni dawa ya ukafiri na hulka mbaya na ni uokovu wa shirki na maangamizi. Kwenye Nahjul-Balagha imeelezwa:“Itakeni nasaha kwa nafsi zenu na mzituhumu rai zenu kwayo na mtake uokofu wa hawa zenu ndani yake.”

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

وَمَا يَسْتَوِي الْبَحْرَانِ هَـٰذَا عَذْبٌ فُرَاتٌ سَائِغٌ شَرَابُهُ وَهَـٰذَا مِلْحٌ أُجَاجٌ وَمِن كُلٍّ تَأْكُلُونَ لَحْمًا طَرِيًّا وَتَسْتَخْرِجُونَ حِلْيَةً تَلْبَسُونَهَا وَتَرَى الْفُلْكَ فِيهِ مَوَاخِرَ لِتَبْتَغُوا مِن فَضْلِهِ وَلَعَلَّكُمْ تَشْكُرُونَ ﴿١٢﴾

12. Na bahari mbili haziwi sawa; hii ni tamu mno, kinywaji chake kinateremka uzuri, na hii ni chumvi sana. Na kutokana na zote, mnakula nyama freshi. Na mnatoa humo mapambo mnayoyavaa. Na unaona vyombo vikikata maji humo, ili mtafute fadhila yake na mpate kushukuru.

يُولِجُ اللَّيْلَ فِي النَّهَارِ وَيُولِجُ النَّهَارَ فِي اللَّيْلِ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي لِأَجَلٍ مُّسَمًّى ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ لَهُ الْمُلْكُ وَالَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِهِ مَا يَمْلِكُونَ مِن قِطْمِيرٍ ﴿١٣﴾

13. Anauingiza usiku katika mchana na anauingiza mchana katika usiku. Na amelitiisha Jua na Mwezi, kila kimoja kinaendelea mpaka muda uliotajwa. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wenu, ufalme ni wake. Na wale mnaowaomba badala yake hawamiliki hata utando wa kokwa ya tende.

إِن تَدْعُوهُمْ لَا يَسْمَعُوا دُعَاءَكُمْ وَلَوْ سَمِعُوا مَا اسْتَجَابُوا لَكُمْ وَيَوْمَ الْقِيَامَةِ يَكْفُرُونَ بِشِرْكِكُمْ وَلَا يُنَبِّئُكَ مِثْلُ خَبِيرٍ ﴿١٤﴾

14. Mkiwaomba, hawasikii maombi yenu. Na wakisikia hawajibu. Na siku ya Kiyama watakataa shirki yenu. Na hapana atakayekuambia kama Yeye mwenye habari.

يَا أَيُّهَا النَّاسُ أَنتُمُ الْفُقَرَاءُ إِلَى اللَّـهِ وَاللَّـهُ هُوَ الْغَنِيُّ الْحَمِيدُ ﴿١٥﴾

15. Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha, Msifiwa.

إِن يَشَأْ يُذْهِبْكُمْ وَيَأْتِ بِخَلْقٍ جَدِيدٍ ﴿١٦﴾

16. Akitaka atawaondoa na alete viumbe wapya.

وَمَا ذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ بِعَزِيزٍ ﴿١٧﴾

17. Na hilo kwa Mwenyezi Mungu si gumu.

وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ وَإِن تَدْعُ مُثْقَلَةٌ إِلَىٰ حِمْلِهَا لَا يُحْمَلْ مِنْهُ شَيْءٌ وَلَوْ كَانَ ذَا قُرْبَىٰ إِنَّمَا تُنذِرُ الَّذِينَ يَخْشَوْنَ رَبَّهُم بِالْغَيْبِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَمَن تَزَكَّىٰ فَإِنَّمَا يَتَزَكَّىٰ لِنَفْسِهِ وَإِلَى اللَّـهِ الْمَصِيرُ ﴿١٨﴾

18. Wala mbebaji hatabeba mzigo wa mwingine. Na kama aliyelemewa akiomba achukuliwe mzigo wake, hautachukuliwa hata kidogo, ingawa ana ujamaa. Hakika unawaonya wale tu wanaomcha Mola wao kwa ghaibu na wakasimamisha Swala. Na anayejitakasa, basi anajitakasa kwa ajili ya nafsi yake. Na marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu.

BAHARI MBILI HAZIWI SAWA

Aya 12 – 18:

MAANA

Na bahari mbili haziwi sawa; hii ni tamu mno, kinywaji chake kinateremka uzuri, na hii ni chumvi sana.

Aya hii ni miongoni mwa Aya za kilimwengu, inayoashiria aina za maji tamu na chumvi. Kutofautiana huku, hata kukitegemezwa moja kwa moja kwenye sababu zake za kimaumbile, lakini bado sababu hizo zinakomea kwa muumba wa ulimwengu na mbunifu wake.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 19 (25:53).

Na kutokana na zote, hizo bahari mbili,mnakula nyama freshi [4] ; kama samaki.

Na mnatoa humo mapambo mnayoyavaa. Na unaona vyombo vikikata maji humo, ili mtafute fadhila yake na mpate kushukuru.

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 14 (16:13).

Anauingiza usiku katika mchana na anauingiza mchana katika usiku.

Sayari zinazunguka na nyingine zinazunguka kando kando ya nyingine, na kupatikana vipindi. Wakati mwingine mchana unachukuliwa kutoka kwenye usiku na kipindi kingine usiku unachukuliwa kutoka mchana. Nidhamu hii ya hali ya juu inayoendela katika mamilioni ya miaka ni dalili mkataa wa kuweko mpangiliaji mwenye hekima wa ulimwengu huu; sawa na kinavyofahamaisha chombo kinachotekeleza kazi iliyotakiwa, kuwa kuna aliyekitengeneza na kukipangilia vizuri.

Sadfa inakuwa ni batili katika hukumu ya kukaririka; yaani sadfa haiwezi kukaririka.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (3:27).

Na amelitiisha Jua na Mwezi, kila kimoja kinaendelea mpaka muda uliotajwa.

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 13: (13:2).

Huyo ndiye Mwenyezi Mungu, Mola wenu, ufalme ni wake. Na wale mnaowaomba badala yake hawamiliki hata utando wa kokwa ya tende.

Utando wa kokwa ya tende ni kinaya cha vitu vilivyo duni zaidi. Maana ni kuwa mambo haya ya kustaajabisha yaliyo dhahiri mnayoyaona katika ulimwengu huu, ni katika matengenezo ya Mwenyezi Mungu, na wale manowabudu na kuwatarajia badala ya Mwenyezi Mungu, hawana wala hawezi chochote.

Mkiwaomba, wakiwa hawana hisia wala utambuzi, kama vile mawe na miti,hawasikii maombi yenu. Na wakisikia , wakiwa ni watu, majini au malaika,hawajibu, kwa vile wao wenyewe hawawezi kujinufaisha wala kujizuilia na madhara, itakuwaje waweze kuwasaidia wengine.

Na siku ya Kiyama watakataa shirki yenu.

Watajitenga na ushirikina na upotevu.

Na hapana atakayekuambia kama Yeye mwenye habari ya mwisho wa hawa wanaokadhibisha utume wako, na wengineo katika waasi, ewe Muhammad.

Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujitosha, Msifiwa.

Mahitaji ya muumbwa kwa muumba wake hayakatiki milele; kama mahitaji ya sababu kwa msababishi wake.

Ibn Al-arabi anasema katika Kitabu Futahitul- Makkiya: “Mtu ana pande mbili: upande mmoja anamuhitajia Mwenyezi Mungu na upande mwingine anajitosheleza na ulimwengu. Kwa hiyo yeye ni dhalili muhitaji kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na mwenye kujitosheleza kwa yule anayetosheka naye.”

Akitaka atawaondoa na alete viumbe wapya. Na hilo, la kuwamaliza waasi na kuwaleta watiifu,kwa Mwenyezi Mungu si gumu.

Lau Mwenyezi Mungu (s.w.t) akitaka lolote linakuwa tu, kwa sababu Yeye ni Muweza wa kila kitu.

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 13 (14: 19 – 20). Vile vile Umetangulia mfano wake katika Juz. 5 (4:133) na Juz. 8 (6:133).

Wala mbebaji hatabeba mzigo wa mwingine.

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 8 (6:164).

Kila mwenye dhambi atahisabiwa na kuadhibiwa kwa madhambi yake tu, lakini Taurat imeeleza kinyume: “Bwana ni mpole... mwenye kuwapatiliza wana kwa uovu wa baba zao...” (Hesabu 14:18).

Na kama aliyelemewa akiomba achukuliwe mzigo wake, hautachukuliwa hata kidogo, ingawa ana ujamaa.

Aliyelemewa ni yule mwenye mzigo wa madhambi. Maana ni kuwa siku hiyo hakutafaa kunyenyekea wala kuomba msaada kwa ndugu au mpenzi, kwa sababu kila mtu atajishughulikia mwenyewe:

يَوْمَ يَفِرُّ الْمَرْءُ مِنْ أَخِيهِ ﴿٣٤﴾ وَأُمِّهِ وَأَبِيهِ ﴿٣٥﴾ وَصَاحِبَتِهِ وَبَنِيهِ ﴿٣٦﴾ لِكُلِّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ يَوْمَئِذٍ شَأْنٌ يُغْنِيهِ ﴿٣٧﴾

“Siku ambayo mtu atamkimbia nduguye na mama yake na baba yake na mkewe na wanawe. Kila mtu siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha.” (80:34 – 37).

Hakika unawaonya wale tu wanaomcha Mola wao kwa ghaibu na wakasimamisha Swala.

Wanaoitikia mwito wako, ewe Muhammad ni wale tu wanaomwogopa Mwenyezi Mungu na kutarajia thawabu zake. Ama wale wasiomwamini wala kuamini siku ya mwisho, maonyo na nasaha haziwafai chochote.

Na anayejitakasa, basi anajitakasa kwa ajili ya nafsi yake.

Hii ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu:

مَّنْ عَمِلَ صَالِحًا فَلِنَفْسِهِ وَمَنْ أَسَاءَ فَعَلَيْهَا وَمَا رَبُّكَ بِظَلَّامٍ لِّلْعَبِيدِ ﴿٤٦﴾

“Mwenye kutenda mema ni kwa ajili ya nafsi yake na mwenye kutenda uovu ni juu yake. Na Mola wako si Mwenye kuwadhululumu waja” (41:46)

Katika Nahju-Balagha imeelezwa: “Ihisabu nafsi yako, kwani nafsi nyingine ina wa kuihisabu asiyekuwa wewe.”

Na marejeo ni kwa Mwenyezi Mungu, Ampe thawabu mwenye kuamini na akatenda mema na amwadhibu mwenye kufanya ufisadi na uovu.

وَمَا يَسْتَوِي الْأَعْمَىٰ وَالْبَصِيرُ ﴿١٩﴾

19. Hawi sawa kipofu na mwenye kuona.

وَلَا الظُّلُمَاتُ وَلَا النُّورُ ﴿٢٠﴾

20. Wala giza na nuru.

وَلَا الظِّلُّ وَلَا الْحَرُورُ ﴿٢١﴾

21. Wala kivuli na joto.

وَمَا يَسْتَوِي الْأَحْيَاءُ وَلَا الْأَمْوَاتُ إِنَّ اللَّـهَ يُسْمِعُ مَن يَشَاءُ وَمَا أَنتَ بِمُسْمِعٍ مَّن فِي الْقُبُورِ ﴿٢٢﴾

22. Na hawawi sawa walio hai na walio maiti. Hakika Mwenyezi Mungu humsikilizisha amtakaye. Wala wewe si wa kuwasikilizisha walio makaburini.

إِنْ أَنتَ إِلَّا نَذِيرٌ ﴿٢٣﴾

23. Hukuwa wewe ila ni mwonyaji

إِنَّا أَرْسَلْنَاكَ بِالْحَقِّ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَإِن مِّنْ أُمَّةٍ إِلَّا خَلَا فِيهَا نَذِيرٌ ﴿٢٤﴾

24. Hakika sisi tumekutuma kwa haki, uwe mbashiri na mwonyaji. Na hakuna umma wowote ila alipita humo muonyaji.

وَإِن يُكَذِّبُوكَ فَقَدْ كَذَّبَ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ جَاءَتْهُمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ وَبِالزُّبُرِ وَبِالْكِتَابِ الْمُنِيرِ ﴿٢٥﴾

25. Na kama wakikukadhibisha, basi hakika wamekadhibisha wale waliokuwa kabla yako. Waliwajia Mitume wao kwa dalili wazi wazi na kwa maandiko na kwa kitabu chenye nuru.

ثُمَّ أَخَذْتُ الَّذِينَ كَفَرُوا فَكَيْفَ كَانَ نَكِيرِ ﴿٢٦﴾

26. Kisha nikawakamata wale waliokufuru; basi je, kulikuwaje kukanya kwangu?

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَأَخْرَجْنَا بِهِ ثَمَرَاتٍ مُّخْتَلِفًا أَلْوَانُهَا وَمِنَ الْجِبَالِ جُدَدٌ بِيضٌ وَحُمْرٌ مُّخْتَلِفٌ أَلْوَانُهَا وَغَرَابِيبُ سُودٌ ﴿٢٧﴾

27. Je, huoni kuwa tumeteremsha kutoka mawinguni maji kutoka mbinguni na kwayo tumetoa matunda yenye kuhitalifiana rangi. Na katika milima imo mistari myeupe na myekundu yenye rangi mbalimbali na myeusi.

وَمِنَ النَّاسِ وَالدَّوَابِّ وَالْأَنْعَامِ مُخْتَلِفٌ أَلْوَانُهُ كَذَٰلِكَ إِنَّمَا يَخْشَى اللَّـهَ مِنْ عِبَادِهِ الْعُلَمَاءُ إِنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ غَفُورٌ ﴿٢٨﴾

28. Na katika watu na wanyama na wanyama howa pia rangi zao zinahitalifiana. Hakika si mengineyo wanaomcha Mwenyezi Mungu, katika waja wake ni wale wajuzi Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye maghufira.

HAWI SAWA KIPOFU NA MWENYE KUONA

Aya 19 – 28

MAANA

Hawi sawa kipofu na mwenye kuona, wala giza na nuru, wala kivuli na joto. Na hawawi sawa walio hai na walio maiti.

Makusudio ya kipofu ni yule mwenye kuacha njia ya haki na ya uongofu; kinyume chake ni mwenye kuona. Giza ni ujinga na upotevu, na nuru ni elimu na uongofu. Kivuli ni neema na joto ni moto wa Jahannam. Ama walio hai ni wale walio na nyoyo zinazosikia mazuri na zikayafuata; kinyume chao ni wafu.

Maana ni kuwa hawi sawa, mbele ya Mwenyezi Mungu na kihali halisi ilivyo, mwenye kuamini akafanya matendo mema na yule mwenye kukufuru akafanya ufisadi. Bali tofauti baina yao ni sawa na tofauti baina ya kipofu na mwenye macho, mwanga na giza, kivuli na joto na mauti na uhai.

Hakika Mwenyezi Mungu humsikilizisha amtakaye. Wala wewe si wa kuwasikilizisha walio makaburini. Hukuwa wewe ila ni mwonyaji.

Maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu yanaathiri na kufanya kazi katika nafsi za wale wanaotafuta haki kwa ajili ya haki na kuisikiliza kwa ajili ya kutaka kuifanyia kazi.

Ama wale ambao hakuna linalowashtua isipokuwa masilahi yao wala hawafanyi lolote isipokuwa masilahi, wao hawasikilizi maneno yake Mwenyezi Mungu Mtukufu, wala Yeye, ambaye imetukuka hekima yake, hawasukumi kwenye uongofu. Vinginevyo zitabatilika thawabu na adhabu.

Hakika sisi tumekutuma kwa haki, uwe mbashiri na mwonyaji.

Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad (s.a.w.), kwa hoja za kutosheleza, kulingania kwenye haki na kuwa shahidi kwa viumbe. Basi akafikisha ujumbe kwa ukamilifu na akawa ni rehema kwa viumbe wote, hasa waarabu; pale alipowatoa kwenye ujinga wa wajinga na kuwapeleka kwenye nuru ya Uislamu na karama yake.

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 11 (10:42) na Juz.20 (27:80).

KILA UMMA UNA MTUME

Na hakuna uma wowote ila alipita humo muonyaji.

Katika Qur’an kuna Aya zinazofahamisha waziwazi kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametuma Mtume kwa kila umma; miongoni mwa Aya hizo ni hizi zifuatazo:

Aya hii tuliyo nayo.

فَكَيْفَ إِذَا جِئْنَا مِن كُلِّ أُمَّةٍ بِشَهِيدٍ ﴿٤١﴾

“Basi itakuwaje tutakapowaletea kila umma shahidi.” Juz. 5 (4:41).

وَلَقَدْ بَعَثْنَا فِي كُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولًا ﴿٣٦﴾

“Na kwa hakika tulimtuma Mtume kwa kila umma.” Juz. 14 (16:36).

وَلِكُلِّ أُمَّةٍ رَّسُولٌ ﴿٤٧﴾

“Na kila Umma una Mtume.” Juz. 11 (10:47).

Kuongezea kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

فَوَرَبِّكَ لَنَسْأَلَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٩٢﴾

“Naapa kwa Mola wako tutawauliza wote Juz. 14 (15:92)

Na pia kauli yake:

أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى ﴿٣٦﴾

“Hivi anadhani mtu kuwa ataachwa bure?” (75:36)

Sio mbali kuwa makusudio ya mjumbe, muonyaji na shahidi ni kila linalosimamia hoja na kukata nyudhuru, liwe limetoka kwa Nabii, Mtume, Kitabu cha dini, kiongozi mwema au hukumu ya akili ya kimsingi, isiyopingika na wenye akili salama na umbile la Mwenyezi Mungu alilowaumbia watu; kama ubaya wa dhulma na hiyana, na uzuri wa uadilifu na uaminifu n.k. Wala hatujui umma ulioishi kwa vurugu bila nidhamu na kumwachia kila mtu afanye atakavyo bila ya kumhisabu kwa kauli na vitendo.

Unaweza kuuliza : Je, hii haipingani na kauli yake Mwenyezi Mungu, iliyo katika Juzuu hii: “Wala hatukuwatumia muonyaji kabla yako.” (34:44). Ambapo Aya tuliyo nayo inathibitisha kuwa kila kaumu ina muonyaji na ya pili inakataa kuwa kaumu ya Muhammad(s.a.w. w ) ilikuwa na muonyaji kabla yake?

Jibu : Muonyaji katika Aya tuliyo nayo inachanganya kila muonyaji awe mtume au la. Ama katika Aya ya pili inahusuiana na Mtume. Kwa hiyo hakuna kupingana baina ya Aya mbili na maana ni kuwa kaumu ya Muhammad(s.a.w. w ) hawakujiwa na Mtume kabla ya kutumwa yeye, lakini walijiwa na muonyaji wa akili na maumbile; nayo ni muonyaji tosha wa kuwapa hoja; hasa katika kuabudu kwao mawe.

Ndio maana Mtume(s.a.w. w ) alikuwa akiwajadili kwa mantiki ya akili na kuwaambia:

قُلْ أَتَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ مَا لَا يَمْلِكُ لَكُمْ ضَرًّا وَلَا نَفْعًا وَاللَّـهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٧٦﴾

“Sema: Je, mnamwabudu badala ya Mwenyezi Mungu, ambaye hawezi kuwadhuru wala kuwanufaisha? Juz. 6 (5:76).

Na kama wakikukadhibisha, basi hakika wamekadhibisha wale waliokuwa kabla yako. Waliwajia Mitume wao kwa dalili wazi wazi na kwa maandiko na kwa kitabu chenye nuru.

Makusudio ya maandiko hapa ni hikima na mawaidha. Kitabu chenye nuru ni Tawrat iliyoteremshwa kwa Musa, Injil iliyoteremshwa kwa Isa na vitabu vinginevyo vilivyotermshwa kabla ya Mtume wa mwisho. Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:184).

Kisha nikawakamata wale waliokufuru; basi je, kulikuwaje kukanya kwangu?

Makusudio ya kukanya hapa ni adhabu. Yaani Mwenyezi Mungu aliwakanya kwa kauli na vitendo. Umetangulia mfano wake katika Juz. 17 (22:44) na Juzuu hii tuliyo nayo (34:45).

Je, huoni kuwa tumeteremsha kutoka mawinguni maji kutoka mbinguni na kwayo tumetoa matunda yenye kuhitalifiana rangi na ladha yake na harufu yake.

Hakuna mwenye shaka kwamba kutoafautiana huku kunatokana na sababu za kimaumbile, lakini zote hizi zinaishia kwa muumba wa hayo maumbile. Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (13:4) katika kifungu cha ‘Sayyid Afghani na wanaomkana Mungu.’

Na katika milima imo mistari myeupe na myekundu yenye rangi mbalimbali na myeusi.

Anasema, mkuu wa wasemaji, kwamba Yeye amefanya kwenye majabali njia; kuna nyeupe, nyekundu na nyingine ni nyeusi. Kila moja katika njia hizo tatu inatofautiana rangi.

Mazingatio katika kutofautiana huku ni kufahamisha juu ya uweza wa Mwenyezi Mungu na matakwa yake; sawa na tofauti ya matunda.

Na katika watu na wanyama na wanyama howa pia rangi zao zinahitalifiana.

Kuunganisha wanyama na wanyama hoa, ni katika kuunganisha maalum kwenye ujumla, kwa sababu neno lililotumika kwa wanyama, Dawab, lina maana ya wanaotemebea ardhini, wakiwemo wanyama howa (mifugo) ambao ni ngamia, ng’ombe, kondoo na mbuzi.

Maana ni kuwa kutofautiana rangi za watu na kutofautiana wanyama, kunafahamisha uweza wa Mwenyezi Mungu; sawa na kutofautiana matunda na njia.

Hakika si mwengineyo wanaomcha Mwenyezi Mungu, katika waja wake ni wale wajuzi.

Makusudio ya wenye ujuzi hapa ni wale walioamini kwa kujua, sio kwa kuiga, na wakaujua utukufu wake kwa dalili na hoja.

Hakuna mwenye shaka kwamba mwenye kujua uweza wa asiyeshindwa na kitu wala kupitwa na kitu, hawezi kuacha kumuogopa; ndio maana wanaomjua Mwenyezi Mungu ndio wanaohofia zaidi hasira za Mwenyezi Mungu na ndio walio na matarajio zaidi ya fadhila na msamaha wake.

Sisi ni katika wale wanaoamini kuwa hakuna imani ya kweli bila ya takua wala hakuna takua bila ya mwamko. Ndio maana Mtume mtukufu(s.a.w. w ) akasema: “Ubora wa mjuzi juu ya mwenye kuabudu ni ubora wa mwezi usiku kwenye nyota.” Pia kuna Hadith mashuhuri ya Mtume(s.a.w. w ) :“Usingizi wa mwenye ujuzi ni bora kuliko ibada ya mjinga.”

Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye maghufira.

Mwenye nguvu katika kuwawaadhibu wenye kupituka mipaka na kufanya dhulma, na ni mwenye maghufira kwa mwenye kutubia na kurejea.

11

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

إِنَّ الَّذِينَ يَتْلُونَ كِتَابَ اللَّـهِ وَأَقَامُوا الصَّلَاةَ وَأَنفَقُوا مِمَّا رَزَقْنَاهُمْ سِرًّا وَعَلَانِيَةً يَرْجُونَ تِجَارَةً لَّن تَبُورَ ﴿٢٩﴾

29. Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na wakasimamisha Swala, na wakatoa kwa siri na kwa uwazi katika tuliyowapa, wanataraji biashara isiyoangamia.

لِيُوَفِّيَهُمْ أُجُورَهُمْ وَيَزِيدَهُم مِّن فَضْلِهِ إِنَّهُ غَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٣٠﴾

30. Ili awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fadhila zake. Hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye shukrani.

وَالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ مِنَ الْكِتَابِ هُوَ الْحَقُّ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ إِنَّ اللَّـهَ بِعِبَادِهِ لَخَبِيرٌ بَصِيرٌ ﴿٣١﴾

31. Na yale tuliyokupa wahyi kutoka Kitabuni ni haki yenye kusadikisha yaliyokuwa kabla yake. Hakika Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni Mwenye habari, Mwenye kuona.

ثُمَّ أَوْرَثْنَا الْكِتَابَ الَّذِينَ اصْطَفَيْنَا مِنْ عِبَادِنَا فَمِنْهُمْ ظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ وَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ وَمِنْهُمْ سَابِقٌ بِالْخَيْرَاتِ بِإِذْنِ اللَّـهِ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَضْلُ الْكَبِيرُ ﴿٣٢﴾

32. Kisha tumewarithisha Kitabu wale ambao tumewachagua katika waja wetu. Kati yao yupo aliyejidhulumu nafsi yake, na yupo wa katikati, na yupo aliyetangulia katika mambo ya kheri, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Hiyo ndiyo fadhila kuu.

جَنَّاتُ عَدْنٍ يَدْخُلُونَهَا يُحَلَّوْنَ فِيهَا مِنْ أَسَاوِرَ مِن ذَهَبٍ وَلُؤْلُؤًا وَلِبَاسُهُمْ فِيهَا حَرِيرٌ ﴿٣٣﴾

33. Mabustani ya milele watayaingia. Humo watavikwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na mavazi yao humo ni hariri.

وَقَالُوا الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي أَذْهَبَ عَنَّا الْحَزَنَ إِنَّ رَبَّنَا لَغَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٣٤﴾

34. Na watasema: Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu (Alhamdu lillah) ambaye ametuondoloea huzuni. Hakika Mola wetu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye shukrani.

الَّذِي أَحَلَّنَا دَارَ الْمُقَامَةِ مِن فَضْلِهِ لَا يَمَسُّنَا فِيهَا نَصَبٌ وَلَا يَمَسُّنَا فِيهَا لُغُوبٌ ﴿٣٥﴾

35. Ambaye ametuweka katika nyumba ya kukaa, humo haitugusi tabu wala humo hakutugusi kuchoka.

ALIYEJIDHULUMU, ALIYE KATIKATI, NA ALIYETANGULIA KWENYE KHERI

Aya 29 – 35

MAANA

Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu, na wakasi- mamisha Swala, na wakatoa kwa siri na kwa uwazi katika tuliyowapa, wanataraji biashara isiyoangamia.

Makusudio ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu ni Qur’an Tukufu. Kusoma ni kuzingatia maana yake na kuyatumia. Kwa sababu kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Hakika wale wanaosoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu.... ‘iliyokuja baada ya kauli yake: ‘Hakika si mengineyo wanaomcha Mwenyezi Mungu, katika waja wake ni wale wajuzi.’ Inaashiria hivyo.

Katika Nahjul-Balagha kuna maelezo:“... Katika zama hizo hakutakuwa na kitu kisichokuwa na thamani zaidi kuliko kusomwa Qur’an inavyopaswa kusomwa kwake. Wala hakutakuwa na kitu kilicho na thamni zaidi kuliko Qur’an kutowekwa mahali pake.”

Maana ya Aya ni kuwa wale ambao wanazingatia Qur’an na wakatumia hukumu zake, wakikusudia radhi ya Mwenyezi Mungu, basi watakuwa wamepata faida kwenye biashara yao na watakuwa ni wenye kufuzu.

Amesema tena kwenye Nahjul-Balagha:“ Na wameuza machache kati- ka dunia hii isiyodumu kwa mengi ya akhera isiyoisha.”

Ili awalipe ujira wao kwa ukamilifu, na awazidishie kutokana na fad- hila zake. Hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye shukrani.

Waliamini na wakamfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu, kwa kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu, thawabu zake, msamaha wake na rehema zake, na wakapata waliyoyataka.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (2:274) na Juz. 13 (13:22).

Na yale tuliyokupa wahyi kutoka Kitabuni ni haki.

Makusudio ya Kitabu ni Qur’an ikiwa inachukua dalili na hoja za ukweli wake na uhakika wake; ambazo ni hukumu zake na mafundisho yake yanayoipa kipaumbele imani ya uadilifu wa Mwenyezi Mungu na umoja wake na heshima ya mtu na uhuru wake.

Yenye kusadikisha yaliyokuwa kabla yake katika vitabu na sharia zinazosimama kwenye misingi hii – misingi ya kumwamini Mwenyezi Mungu na utu.

Hakika Mwenyezi Mungu kwa waja wake ni Mwenye habari, Mwenye kuona yale yaliyo na masilahi kwao na yaliyo na ufisadi. Anawaamrisha lile na kuwakataza hili. Lakini Waislamu wameacha yaliyoamrishwa na Qur’an na wakafanya waliyokatazwa nayo. Wamesadikisha aliyoyasema Mtume mtukufu(s.a.w. w ) aliposema:“Utakuja wakati kwa umma wangu watakataza mema na kuamrisha maovu.” Kwa hiyo si ajabu kusalitika na viumbe waovu.

Kisha tumewarithisha Kitabu wale ambao tumewachagua katika waja wetu.

Makusudio ya Kitab ni Qur’an, hilo halina shaka yoyote; isipokuwa wafasiri wametofautiana katika makusudio ya waliochaguliwa. Wengi wakasema ni umma wa Muhammad(s.a.w. w ) .

Tuonavyo sisi ni Muhammad(s.a.w. w ) , Ahlu bayti wake, maswahaba wake na maulama wa umma wake wanaokwenda na sera yake na wakatumia sunna yake. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hawezi kuwachagua isipokuwa wenye takua walio wema.

Qur’an Tukufu imelitumia neno hili kwa maana haya katika Aya kadhaa; miongoni mwazo ni:

إِنَّ اللَّـهَ اصْطَفَىٰ آدَمَ وَنُوحًا وَآلَ إِبْرَاهِيمَ وَآلَ عِمْرَانَ عَلَى الْعَالَمِينَ ﴿٣٣﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu alimchagua Adam na Nuh na watoto wa Ibrahim na watoto wa Imran juu ya walimwengu wote.” Juz. 3 (3:33).

Ama dhamiri katikakati yao yupo aliyejidhulumu nafsi yake, na yupo wa katikati, na yupo aliyetangulia katika mambo ya kheri, kwa idhini ya Mwenyezi Mungu, inarudia neno waja wetu, kwa vile ndilo lililo karibu.

Mwenye kujidhulumu ni yule ambaye maovu yake yamekuwa makubwa kuliko mema yake. Aliyetangulia katika heri ni ambaye mema yake yamekuwa makubwa kuliko maovu yake; hasa yule ambaye hana maovu. Aliye katikati ni ambaye mema yake na maovu yake yamekuwa sawa.

Hiyo ndiyo fadhila kuu. Mabustani ya milele watayaingia. Humo watavikwa vikuku vya dhahabu, na lulu, na mavazi yao humo ni hariri.

‘Hiyo’ ni hiyo hali ya kurithi na kuchaguliwa. Mabustani ya milele na kuendelea, ni ubainifu wa hiyo fadhila kuu ambayo ameifanya ni malipo ya wale aliowachagua.

Dhahabu, lulu na hariri ni ibara nyingine ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَفِيهَا مَا تَشْتَهِيهِ الْأَنفُسُ وَتَلَذُّ الْأَعْيُنُ ﴿٧١﴾

“Humo vitakuwemo ambavyo nafsi inavipenda na macho yanavifurahia.” (43:71).

Kuna Hadith kuwa bedui mmoja alimuuliza Mtume: “Je, Peponi kuna samai, yaani nyimbo? Mtume(s.a.w. w ) akasema: “Ndio.”

Na watasema:, sifa njema ni za Mwenyezi Mungu (Alhamdu lillah) ambaye ametuondoloea huzuni. Hakika Mola wetu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye shukrani. Ambaye ametuweka katika nyumba ya kukaa, humo haitugusi tabu wala humo hakutugusi kuchoka.

Watamshukuru Mwenyezi Mungu na kumsifu kwa kuwandolea hofu na kuokoka na moto na adhabu. Pia kuondokana na tabu na mashaka na kudumu kwenye neema na shangwe.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا لَهُمْ نَارُ جَهَنَّمَ لَا يُقْضَىٰ عَلَيْهِمْ فَيَمُوتُوا وَلَا يُخَفَّفُ عَنْهُم مِّنْ عَذَابِهَا كَذَٰلِكَ نَجْزِي كُلَّ كَفُورٍ ﴿٣٦﴾

36. Na wale ambao wamekufuru watakuwa na moto wa Jahannam, hawahukumiwi wakafa wala hawatapunguziwa adhabu yake. Hivyo ndivyo tunavyomlipa kila mwenye kuzidi ukafiri.

وَهُمْ يَصْطَرِخُونَ فِيهَا رَبَّنَا أَخْرِجْنَا نَعْمَلْ صَالِحًا غَيْرَ الَّذِي كُنَّا نَعْمَلُ أَوَلَمْ نُعَمِّرْكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَاءَكُمُ النَّذِيرُ فَذُوقُوا فَمَا لِلظَّالِمِينَ مِن نَّصِيرٍ ﴿٣٧﴾

37. Na humo watapiga makelele: Mola wetu! Tutoe tufanye mema, sio yale tuliyokuwa tukiyafanya. Je, hatukuwapa umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka, na akawajia mwonyaji? Basi onjeni! Na madhalimu hawana wa kuwanusuru.

إِنَّ اللَّـهَ عَالِمُ غَيْبِ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٣٨﴾

38. Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa siri za mbingu na ardhi. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

هُوَ الَّذِي جَعَلَكُمْ خَلَائِفَ فِي الْأَرْضِ فَمَن كَفَرَ فَعَلَيْهِ كُفْرُهُ وَلَا يَزِيدُ الْكَافِرِينَ كُفْرُهُمْ عِندَ رَبِّهِمْ إِلَّا مَقْتًا وَلَا يَزِيدُ الْكَافِرِينَ كُفْرُهُمْ إِلَّا خَسَارًا ﴿٣٩﴾

39. Yeye ndiye aliyewafanya nyinyi makhalifa katika ardhi. Na anayekufuru, basi kufuru yake ni juu yake; na kufuru za makafiri haziwazidishii kwa Mola wao ila kuchukiwa. Wala kufuru za makafiri haziwazidishii ila hasara.

HAWAHUKUMIWI WAKAFA

Aya 36 – 39

MAANA

Na wale ambao wamekufuru watakuwa na moto wa Jahannam, hawahukumiwi wakafa wala hawatapunguziwa adhabu yake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja aina nyingi ya adhabu kwa waasi; miongoni mwazo ni aina hii: Uchungu wa adhabu, kudumu kwake na kuendelea kwake. Hakuna mauti ya kumaliza adhabu wala sababu ya kupelekea kupunguziwa adhabu.

Hivyo ndivyo tunavyomlipa kila mwenye kuzidi ukafiri.

Ni malipo yanayolingana na kosa lake. Umetangulia mfano wake katika Juz. 5 (4:56 – 57).

Na humo watapiga makelele: Mola wetu! Tutoe tufanye mema, sio yale tuliyokuwa tukiyafanya.

Watapiga kelele na kutaka usaidizi, lakini hakuna wa kuwaokoa. Watatubia, lakini baada ya kupita muda. Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (23:99 – 100,107).

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema:

وَلَوْ رُدُّوا لَعَادُوا لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿٢٨﴾

“Na kama wangelirudishwa, bila shaka wangeyarudia yale waliyokatazwa na hakika wao ni waongo.” Juz. 7 (6:28).

Watapiga kelele na kutaka usaidizi, lakini hakuna wa kuwaokoa. Na watataka kutubia, lakini baada ya kupita muda. Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (23: 99-100, 107).

Je, hatukuwapa umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka, na akawajia mwonyaji?

Wanamtaka Mwenyezi Mungu awaruidishe duniani ili wawahi yale yaliyowapita katika imani na matendo mema.

Mwenyezi Mungu naye anawajibu kuwa mlikuwako duniani hapo mwanzo, mkakaa muda mwingi, akawajia mbashiri na muonyaji, mkafahamishwa njia ya uwongofu, lakini mkakataa.

Basi onjeni adhabu, hivi sasa, kutokana na vile mlivyokuwa mkikufuru.Na madhalimu hawana wa kuwanusuru, kwa sababu wao ndio waliojidhulumu wenyewe kwa uchaguzi wao mbaya. Kwani Mwenyezi Mungu aliwapa hoja na ubainifu.

Kwa hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa siri za mbingu na ardhi. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

Anajua siri na dhahiri, na yanayofichikana machoni ardhini na mbinguni, wala hakuna chochote kilichokuwa na kitakachokuwa kinachofichikana kwake.

Yeye ndiye aliyewafanya nyinyi makhalifa katika ardhi. Na anayekufuru, basi kufuru yake ni juu yake; na kufuru za makafiri haziwazidishii kwa Mola wao ila kuchukiwa. Wala kufuru za makafiri haziwazidishii ila hasara.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameumba ardhi katika muundo wa kuweza kuishi watu, wakirithishana vizazi na vizazi. Akawapa akili na uwezo wa kuweza kuitumia kadiri wanavyotaka. Akawaamrisha wamwabudu Yeye peke yake bila ya kumshirikisha na jambo; akawawekea mipaka na kuwakataza wasiikiuke.

Mwenye kusikiliza na akawa na utii basi atapata malipo mema na mwenye kupinga basi atapata adhabu ya moto itakayozidi, na kuzidi kila wanavyozidisha uasi na kupituka mipaka. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema:

إِنَّمَا نُمْلِي لَهُمْ لِيَزْدَادُوا إِثْمًا ﴿١٧٨﴾

“Hakika tunawapa muda ili wazidi katika dhambi.” Juz. 4 (3:178).

قُلْ أَرَأَيْتُمْ شُرَكَاءَكُمُ الَّذِينَ تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَرُونِي مَاذَا خَلَقُوا مِنَ الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ أَمْ آتَيْنَاهُمْ كِتَابًا فَهُمْ عَلَىٰ بَيِّنَتٍ مِّنْهُ بَلْ إِن يَعِدُ الظَّالِمُونَ بَعْضُهُم بَعْضًا إِلَّا غُرُورًا ﴿٤٠﴾

40. Sema mnaona hawa washirika wenu mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu, nionyesheni wameumba nini katika ardhi? Au wana ushirika wowote katika mbingu? Au tumewapa Kitabu, nao kwa hicho, wakawa na hoja, lakini madhalimu hawaahidiani wao kwa wao ila udanganyifu.

إِنَّ اللَّـهَ يُمْسِكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ أَن تَزُولَا وَلَئِن زَالَتَا إِنْ أَمْسَكَهُمَا مِنْ أَحَدٍ مِّن بَعْدِهِ إِنَّهُ كَانَ حَلِيمًا غَفُورًا ﴿٤١﴾

41. Kwa hakika Mwenyezi Mungu huzuia mbingu na ardhi zisiondoke. Na zikiondoka hapana yeyote wa kuzizuia isipokuwa Yeye. Hakika Yeye ni Mpole, Mwingi wa maghufira.

وَأَقْسَمُوا بِاللَّـهِ جَهْدَ أَيْمَانِهِمْ لَئِن جَاءَهُمْ نَذِيرٌ لَّيَكُونُنَّ أَهْدَىٰ مِنْ إِحْدَى الْأُمَمِ فَلَمَّا جَاءَهُمْ نَذِيرٌ مَّا زَادَهُمْ إِلَّا نُفُورًا ﴿٤٢﴾

42. Na waliapa kwa ukomo wa kuapa kwao, kwamba akiwafikia mwonyaji bila ya shaka watakuwa waongofu zaidi kuliko taifa jingine lolote. Lakini alipowajia muonyaji hakuwazidishia ila kukimbia.

اسْتِكْبَارًا فِي الْأَرْضِ وَمَكْرَ السَّيِّئِ وَلَا يَحِيقُ الْمَكْرُ السَّيِّئُ إِلَّا بِأَهْلِهِ فَهَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا سُنَّتَ الْأَوَّلِينَ فَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّـهِ تَبْدِيلًا وَلَن تَجِدَ لِسُنَّتِ اللَّـهِ تَحْوِيلًا ﴿٤٣﴾

43. Kwa kutakabari kwao katika ardhi na kufanya vitimbi viovu. Na vitimbi viovu havimpati ila mwenyewe. Basi hawangoji ila desturi ya wa zamani. Hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu wala hutapata mageuzi katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

ANAZIZUIA MBINGU NA ARDHI

Aya 40 – 43

MAANA

Katika Aya hii ya kwanza hapa, Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewapa hoja tatu washirikina:

Sema mnaona hawa washirika wenu mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu, nionyesheni wameumba nini katika ardhi?

Niambieni enyi washirikina! Ni jambo gani lililowafanya mumfanye Mwenyezi Mungu ana washirika? Je, ardhini kuna kitu chochote kinachofahamisha kuwa kimetengenezwa na wengi? Hapana! Vitu vyote vina- julisha kuweko Mungu mmoja tu, na mpangilio wake ni ushahidi wa utukufu wake na hekima yake.

Au wana ushirika wowote katika mbingu?

Yaani hao mnaowaabudu wana athari yoyote mbinguni kujulisha kuwa wao ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika kuumba?

Au tumewapa Kitabu, nao kwa hicho, wakawa na hoja.

Tuliowapa ni hao washirikina sio washirika wanaoabudiwa. Maana ni kuwa au mumewafanya washirika wa Mungu hao mnaowabudu kwa kutegemea Kitabu kilichoteremshwa au Nabii aliyetumwa? Kwa ujumla ni kuwa hakuna hoja yoyote ya kiakili na kinakili kwa wanavyovishirikisha; bali wao wanamangamanga tu.

Lakini madhalimu hawaahidiani wao kwa wao ila udanganyifu.

Makusudio ya udanganyifu hapa ni ubatilifu. Viongozi wa washirikina walikuwa wakiwaambi wafuasi wao kuwa masanamu yatawaombea kesho. Hakuna mwenye shaka kuwa ahadi hii ni uwongo, uzushi na ubatilifu.

Kwa hakika Mwenyezi Mungu huzuia mbingu na ardhi zisiondoke. Na zikiondoka hapana yeyote wa kuzizuia isipokuwa Yeye. Hakika Yeye ni Mpole, Mwingi wa maghufira.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amezizuwia sayari kwa nguvu ya mvutano; sawa na anavyowazuia ndege angani kwa mbawa zao. Mwenyezi Mungu ametegemeza kwake, kwa sababu yeye ni muumba wa ulimwengu na msababishi wa sababu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 17 (22:65).

Na waliapa kwa ukomo wa kuapa kwao, kwamba akiwafikia mwonyaji bila ya shaka watakuwa waongofu zaidi kuliko taifa jingine lolote.

Walioapa ni washirikina. Katika Bahrul-Muhit imesemwa kuwa watakuwa waongofu ambao hawana mfano. Makuraishi walikuwa wakiwapinga Mayahudi kwa kupotoka kwao na dini yao na kuwaua mitume wao. Wakaapa viapo vya nguvu kwamba akiwajia Mtume kutoka kwa kwa Mwenyezi Mungu watakuwa watiifu zaidi.

Lakini alipowajia muonyaji hakuwazidishia ila kukimbia kwa kutak- abari kwao katika ardhi na kufanya vitimbi viovu.

Hatimaye mjumbe wa Mwenyezi Mungu aliwajia na hoja na ubainifu, lakini wao walimkadhibisha na wakamkimbia na wakamfanyia kiburi yeye na mwito wake. Vile vile walimfanyia vitimbi yeye na wafuasi wake na wakawazuia watu kuamini utume wake. Hata hivyo mwisho walishindwa na wakasalimu amri wakiwa dhalili na wanyonge.

Na vitimbi viovu havimpati ila mwenyewe.

Vitimbi viovu ni kumdhamiria ubaya ndugu yako na kumpangia njama, bila ya yeye kujua, ili atumbukie. Hata hivyo, akiwa hajui yaliyodhamiri- wa na kupangwa, basi Mwenyezi Mungu anajua na atamlipa mpanga njama malipo ya muongo mwenye hadaa na balaa litamrudia yeye.

Basi hawangoji ila desturi ya wa zamani. Hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu, wala hutapata mageuzi katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

Desturi ya wa zamani ni desturi ya Mwenyezi Mungu kwa watu wa zamani ambayo ni kuangamia waliowakadhibisha mitume wa Mwenyezi Mungu. Maana ni je, hawajui wanaomkadhibisha Mtume wetu Muhammad, kwamba Mwenyezi Mungu aliangamiza kaumu ya Nuh, A’ad, Thamud na mfano wao waliowakadhibisha mitume? Na kwamba hii ni desturi yake Mwenyezi Mungu isiyobadilika wala kugeuka? Je, hawapati funzo kwa wengine?

أَوَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ وَكَانُوا أَشَدَّ مِنْهُمْ قُوَّةً وَمَا كَانَ اللَّـهُ لِيُعْجِزَهُ مِن شَيْءٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ إِنَّهُ كَانَ عَلِيمًا قَدِيرًا ﴿٤٤﴾

44. Je, hawakusafiri katika ardhi wakaona vipi ulikuwa mwisho wa waliokuwa kabla yao? Nao walikuwa na nguvu zaidi kuliko wao. Na hakuna kitu kiwezacho kumshinda Mwenyezi Mungu mbinguni wala ardhini. Hakika Yeye ni Mwenye kujua, Mwenye kuweza.

وَلَوْ يُؤَاخِذُ اللَّـهُ النَّاسَ بِمَا كَسَبُوا مَا تَرَكَ عَلَىٰ ظَهْرِهَا مِن دَابَّةٍ وَلَـٰكِن يُؤَخِّرُهُمْ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى فَإِذَا جَاءَ أَجَلُهُمْ فَإِنَّ اللَّـهَ كَانَ بِعِبَادِهِ بَصِيرًا ﴿٤٥﴾

45. Na lau Mwenyezi Mungu angeliwachukulia watu kwa waliyoyachuma, basi asingeliwacha katika ardhi hata mnyama mmoja, lakini yeye anawaakhirisha mpaka muda maalum. Ukifika muda wao basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake.

ASINGELIMUACHA HATA MNYAMA MMOJA

Aya 44 – 45

MAANA

Je, hawakusafiri katika ardhi wakaona vipi ulikuwa mwisho wa waliokuwa kabla yao? Nao walikuwa na nguvu zaidi kuliko wao.

Aya hii inaungana na ile ya kabla yake. Ile inasema kuwa desturi ya Mwenyezi Mungu kwa waliowakadhibisha hapo mwanzo ni kuangamizwa na kung’olewa kabisa, na hii inawambia wale wanaomkadhibisha Muhammad(s.a.w. w ) kuwa athari ile ya waliokadhibisha kabla yenu iko wazi na wala sio mbali na nyinyi. Hebu safirini kidogo katika ardhi muone. Pengine mnaweza kuzingatia na mkapata funzo. Umetangulia mfano wake katika Juz. 17 ( 22:46).

Na hakuna kitu kiwezacho kumshinda Mwenyezi Mungu mbinguni wala ardhini. Hakika Yeye ni Mwenye kujua, Mwenye kuweza.

Hampiti aliyepo wala hamshindi mwenye kukimbia. Kila kitu kinanyenyekea uweza wake na kinanyenyekea ukuu wake. Katika baadhi ya tafsiri imeelezwa kuwa viumbe wote wanahusika na dhambi; hata wanyama, ndege na chembe chembe. Kwa sababu Mwenyezi Mungu anawateremshia adhabu, na akiiteremsha inawaenea wote; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَاتَّقُوا فِتْنَةً لَّا تُصِيبَنَّ الَّذِينَ ظَلَمُوا مِنكُمْ خَاصَّةً ﴿٢٥﴾

“Na jikingeni na fitna ambayo haitawasibu wale waliodhulumu miongoni mwenu peke yao”

Juz. 9 (8:25).

Na lau Mwenyezi Mungu angeliwachukulia watu kwa waliyoyachuma, basi asingeliwacha katika ardhi hata mnyma mmoja, lakini yeye anawaakhirisha mpaka muda maalum. Ukifika muda wao basi haki- ka Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaona waja wake.

Jambo linalofahamisha zaidi maudhi ya mtu kwa muumba wake, ni kuwa yeye anakula riziki yake na anamwabudi mwingine. Hii peke yake inatosha kuadhibiwa. Lakini kila kitu, mbele ya Mwenyezi Mungu, kina muda maalum.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA TANO: SURAT FATIR


6

7

8

9

10

11

12

13