TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 25743
Pakua: 3337


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 25743 / Pakua: 3337
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

26

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini Na Tisa: Surat Az-Zumar. Imeshuka Makka ina Aya 75 isipokuwa Aya tatu.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

تَنزِيلُ الْكِتَابِ مِنَ اللَّـهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ ﴿١﴾

1. Mteremsho wa Kitabu hiki umetokana na Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

إِنَّا أَنزَلْنَا إِلَيْكَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ فَاعْبُدِ اللَّـهَ مُخْلِصًا لَّهُ الدِّينَ ﴿٢﴾

2. Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu hiki kwa Haki. Basi muabudu Mwenyezi Mungu ukimsafia Dini Yeye.

أَلَا لِلَّـهِ الدِّينُ الْخَالِصُ وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ إِنَّ اللَّـهَ يَحْكُمُ بَيْنَهُمْ فِي مَا هُمْ فِيهِ يَخْتَلِفُونَ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي مَنْ هُوَ كَاذِبٌ كَفَّارٌ ﴿٣﴾

3. Ehe! Dini halisi ni ya Mwenyezi Mungu. Na wale wanaowafanya wenginewe kuwa ni walinzi badala yake, (husema): Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika wanayohitalifiana. Hakika Mwenyezi Mungu hamwongozi aliye mwongo, kafiri.

لَّوْ أَرَادَ اللَّـهُ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا لَّاصْطَفَىٰ مِمَّا يَخْلُقُ مَا يَشَاءُ سُبْحَانَهُ هُوَ اللَّـهُ الْوَاحِدُ الْقَهَّارُ ﴿٤﴾

4. Lau kuwa Mwenyezi Mungu angelitaka kujifanyia mwana, basi bila ya shaka angeli teua amtakaye katika aliowaumba. Ametakasika na hayo! Yeye ni Mmoja, Mtenza nguvu.

DINI SAFI NI YA MWENYEZI MUNGU TU!

Aya 1-4

MAANA

Mteremsho wa Kitabu hiki umetokana na Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

Qur’an inatoka kwa Mwenyezi Mungu ambaye ameumba viumbe kwa uweza wake na akaupangilia kwa hekima yake.

Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu hiki kwa Haki. Basi muabudu Mwenyezi Mungu ukimsafia Dini Yeye.

Inaweza kusemwa kuwa : Nabii(s.a.w. w ) ana yakini kuwa Qur’an imetoka kwa Mwenye nguvu Mwenye hekima na kwamba yeye anamwabudu Mwenyezi Mungu kwa kumsafia dini; sasa kuna haja gani ya amri na habari hii?

Jibu : Nabii(s.a.w. w ) aliudhiwa sana na akavumilia mengi, ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akamwambia kwamba wewe unalingania kwenye haki; na mwenye kulingania kwenye mazingira kama yako hana budi kujitolea nafsi yake na mali yake. Vile vile wewe unamfanyia ikhlasi Mwenyezi.

Mungu katika kauli na vitendo vyako vyote; na mwenye kumfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu hukumbana na mengi kutoka kwa maadui zake.

Kwa maneno mengine ni kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu: “Tumekuteremshia Kitabu,” sio kutoa habari; wala kauli yake: “ Basi muabudu Mwenyezi Mungu,” sio amri; bali ni ushahidi wa utukufu wa mtume na kumpoza kutokana na anayokumbana nayo kutoka kwa maadui zake.

Ehe! Dini halisi ni ya Mwenyezi Mungu, isiyokuwa na doa, lakini dini iliyo na madoadoa ya ria na hawa, basi ni ya shetani, siyo ya Mwenyezi Mungu. Dini safi ya namna hii haiwi ila kwa yule aliyeifanya ndio mfano wake wa juu, akajitolea nafsi yake na manufaa yake yote, na wala sio kujitolea kwa manufaa yake na masilahi yake.

Na wale wanaowafanya wenginewe kuwa ni walinzi badala yake, (husema): Sisi hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewarudia washirikina na kuwaelezea kuwa wao wanawafanya wengine kuwa waungu ili wawaombee kwake. Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:18).

Hakika Mwenyezi Mungu atahukumu baina yao katika wanayohitalifiana.

Washirikiana hawatofutiani; isipokuwa wanatofutiana na wanaompwekesha Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu atahukumu baina ya makun- di haya mawili – ampe neema mwenye kumpwekesha na ampe adhabu mwenye kumshirikisha.

Hakika Mwenyezi Mungu hamwongozi aliye mwongo kafiri.

Hakika yeye Mwenyezi Mungu Mtukufu anamwongoza mwenye kufuata njia ya uongofu, anampoteza mwenye kuchagua njia ya upotevu, anamwangamiza mwenye kujitia kwenye maangamivu na anamwokoa mwenye kuchukua hadhari na akajiepusha na maangamizi

Lau kuwa Mwenyezi Mungu angelitaka kujifanyia mwana, basi bila ya shaka angeliteua amtakaye katika aliowaumba.

Hii ni katika kukadiria muhali. Na kukadiria muhali sio muhali. Muhali wenyewe ni kuwa kutaka kuwa na mtoto ni kuwa na haja na kuhitajia, na Mwenyezi Mungu ni mwenye kujitosheleza na kila kitu, si muhitaji. Zaidi ya hayo ni kuwa kila mzazi anarithiwa na kila anayerithiwa huwa ametoweka. Kwa hiyo kila mzazi anatoweka; sasa Mwenyezi Mungu atakuwa- je mzazi?

Ametakasika na hayo! Yeye ni Mmoja, Mtenza nguvu, hana mshirika wala wakufanana naye wala hana mwenzahakuna chochote isipokuwa Yeye tu.

خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ يُكَوِّرُ اللَّيْلَ عَلَى النَّهَارِ وَيُكَوِّرُ النَّهَارَ عَلَى اللَّيْلِ وَسَخَّرَ الشَّمْسَ وَالْقَمَرَ كُلٌّ يَجْرِي لِأَجَلٍ مُّسَمًّى أَلَا هُوَ الْعَزِيزُ الْغَفَّارُ ﴿٥﴾

5. Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Huuzongazonga usiku kwenye mchana, na Huuzongazonga mchana kwenye usiku. Na amelitiisha Jua na Mwezi, kila kimoja kinapita mpaka muda uliotajwa. Ehe! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kughufiria.

خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ ثُمَّ جَعَلَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَأَنزَلَ لَكُم مِّنَ الْأَنْعَامِ ثَمَانِيَةَ أَزْوَاجٍ يَخْلُقُكُمْ فِي بُطُونِ أُمَّهَاتِكُمْ خَلْقًا مِّن بَعْدِ خَلْقٍ فِي ظُلُمَاتٍ ثَلَاثٍ ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبُّكُمْ لَهُ الْمُلْكُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ فَأَنَّىٰ تُصْرَفُونَ ﴿٦﴾

6. Amewaumba kutokana na nafsi moja, na katika hiyo akamjaalia mkewe. Na amewateremshia wanymahoa namna nane za madume na majike. Anawaumba katika matumbo ya mama zenu, umbo baada ya umbo, katika viza vitatu. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu. Ufalme ni wake. Hapana Mola isipokuwa Yeye. Basi nyinyi mnageuzwa wapi?

إِن تَكْفُرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَنِيٌّ عَنكُمْ وَلَا يَرْضَىٰ لِعِبَادِهِ الْكُفْرَ وَإِن تَشْكُرُوا يَرْضَهُ لَكُمْ وَلَا تَزِرُ وَازِرَةٌ وِزْرَ أُخْرَىٰ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّكُم مَّرْجِعُكُمْ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٧﴾

7. Mkikufuru basi Mwenyezi Mungu si mwenye haja nanyi. Wala haridhii kufuru kwa waja wake. Na mkishukuru atawaridhia. Wala hatabeba mbebaji mzigo wa mwingine. Kisha marejeo yenu ni kwa Mola wenu. Basi atawaambia mliyokuwa mkiyafanya. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

وَإِذَا مَسَّ الْإِنسَانَ ضُرٌّ دَعَا رَبَّهُ مُنِيبًا إِلَيْهِ ثُمَّ إِذَا خَوَّلَهُ نِعْمَةً مِّنْهُ نَسِيَ مَا كَانَ يَدْعُو إِلَيْهِ مِن قَبْلُ وَجَعَلَ لِلَّـهِ أَندَادًا لِّيُضِلَّ عَن سَبِيلِهِ قُلْ تَمَتَّعْ بِكُفْرِكَ قَلِيلًا إِنَّكَ مِنْ أَصْحَابِ النَّارِ ﴿٨﴾

8. Na dhara inapomfikia mtu humwomba Mola wake akielekea kwake. Kisha akimpa neema kutoka kwake, husahau yale aliyokuwa akimwitia zamani, na akamfanyia Mwenyezi Mungu washirika ili apoteze njia yake. Sema: Starehe na kufuru yako kidogo, kwani hakika wewe mi miongoni mwa watu wa Motoni.

HUUFUNIKA MCHANA JUU YA USIKU

Aya 5 – 8

LUGHA

Neno Huuzongazonga limefasiriwa kutokana na neno la kiarabu yukawwir, lenye maana ya kufunika kitu kilicho mviringo; kama mtu anavyozongazonga kitambaa kichwani kufanya kilemba.

MAANA

Ameumba mbingu na ardhi kwa Haki. Huuzongazonga usiku kwenye mchana, na Huuzongazonga mchana kwenye usiku.

Huko nyuma tumesema kuwa Mwenyezi Mungu ana vitabu viwili: Kitabu kinachotamka kwa mistari amabacho ni Qur’an na kitabu kilichonyamaza cha kuangaliwa, ambacho ni ulimwengu. Na kwamba yaliyomo katika kitabu hiki; kama vile umoja wenye kuthibiti na hekima iliyopangika, ni dalili mkataa ya umoja wa mwenye kuthibiti na hekima ya mwenye kupangalia. Ama sadfa, kama itatokea, basi hutokea kwenye kitu kimoja wala haikaririki mara nyingi kwenye kitu kimoja.

Mwenye Tafsir Adhilal akizungumzia Aya hii anasema: “Hakika ibara ya kuzongazonga inanilazimisha niangalie vizuri suala la ardhi kuwa ni mviringo, kwamba hiyo yenyewe inazunguka katika kulielekea jua. Kwa hiyo sehemu inayoeleka jua inafunikwa na mwanga na kuwa mchana, lakini sehemu hiyo haitulii kwa vile ardhi inazunguka.

Kila inavyozidi kuendelea ndio usiku nao unaanza kufunika sehemu iliyokuwa mchana. Kufunika huko kunakuwa kwa namna ya kuzongazonga. Kwa hiyo mchana unazongwazongwa na usiku na usiku nao unazongwazongwa”

Kwa hiyo neno kuzongazonga, haliko mbali kuwa linafahamisha mviringo. Ndio maana tunaungana na mwenye Dihilal aliposema ibara ya kuzongzonga inapelekea kuangalia kuwa ardhi ni mviringo. Mustafa Mahmud, katika gazeti la sabahulkhayr amesema kama alivyosema mwenye Dhilal, lakini hakumtaja. Sijui hii ni sadfa ya kuoana mawazo?

Umetangulia mfano wake katika Juzuu hii (36:37), lakini huko halikuja nen o kuzongazonga; bali tulipofafanua tuliashiria kuhusu mzunguko wa ardhi na kwamba upande uanaolelekea jua wakati wa kuzunguka unakuwa mchana na upande wa pili unakuwa usiku.

Na amelitiisha Jua na Mwezi, kila kimoja kinapita mpaka muda uliotajwa. Ehe! Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kughufiria.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (13:2), 21 (31:29) na 22 (35:13).

Amewaumba kutokana na nafsi moja, na katika hiyo akamjaalia mkewe.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (4:1) na Juz. 9 (7:143)

Na amewateremshia wanymahoa namna nane za madume na majike.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (6:143).

Anawaumba katika matumbo ya mama zenu, umbo baada ya umbo, katika viza vitatu. Huyo ndiye Mwenyezi Mungu Mola wenu. Ufalme ni wake. Hapana Mola isipokuwa Yeye. Basi nyinyi mnageuzwa wapi?

فَإِنَّا خَلَقْنَاكُم مِّن تُرَابٍ ثُمَّ مِن نُّطْفَةٍ ثُمَّ مِنْ عَلَقَةٍ ثُمَّ مِن مُّضْغَةٍ ﴿٥﴾

‘Umbo baada ya umbo’ ni ishara ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Hakika tuliwaumba kutokana na udongo kisha kutokana na pande la damu, kisha kutokana na pande la nyama” Juz. 17 (22:5).

Viza vitatu ni tumbo, tumbo la uzazi na fuko la mtoto. Kuendelea huku kutoka hali moja hadi nyingine ndani ya viza vitatu ni dalili mkataa ya kuweko mpangiliaji mwenye kutengeneza.

Ikiwa kukua huku kunatokana na maumbile moja kwa moja, basi maumbile ni katika usanii wa anayesema ‘kuwa ikawa’ Hili hawezi kupofuka nalo isipokuwa kipofu.

Imam Ali(a.s ) anasema:“Ewe kiumbe uliyembwa sawa sawa na mwenye kutunzwa kwenye viza vya tumbo la uzazi na tabaka za sitara! Umeanzishwa “Kutokana na asili ya udongo [9] .”

Na ukawekwa “mahali palipo madhubuti makini mpaka muda maalum,”[10] na muda maalum. Unataharaki tumboni ukiwa mchanga, huwezi kuita wala kusikia mwito.

Kisha ukatolewa kwenye makazi yako kwenda mahali ambapo hujapashuhudia wala hujui manufaa yake. Basi ni nani aliyekuongoza kutafuta chakula kutoka kwenye matiti ya mama yako na kukujulisha matakwa ya haja yako?”[11] .

Mkikufuru basi Mwenyezi Mungu si mwenye haja nanyi

Hayamdhuru maasi ya mwenye kuasi, wala haumnufaishi utiifu wa mwenye kutii “lakini inamfikia takua kutoka kwenu” Juz. 17 (22:37); yaani anawaridhia mkiwa ninyi ni wenye takua;

Ashaira wanasema kuwa Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kutaka yote yanayokuwa; hata kufuru ya kafiri, zina ya mzinifu na uuaji wa mwenye kuua kwa dhulma; kwa vile Yeye ni muumba wa kila kitu. Lakini wakati huohuo anakataza kufuru, zina na kuua.

Almawafiq Juz. 8 Uk. 173. Kwa hiyo kukalifishwa lisilowezekana inajuzu kwa Ashaira. Kwa sababu Mwenyezi Mungu hawajibikiwi na kitu chochote wala hakuna kibaya kwake. Almawaqif Juz. 8 Uk. 200.

Hakuna kitu kilicho wazi zaidi kufahamisha ubatilifu wa fikra hii kuliko kauli yake Mwenyezi Mungu:

Wala haridhii kufuru kwa waja wake. Na mkishukuru atawaridhia.

Analoturidhia ni amani kwetu na rehema.

Wala hatabeba mbebaji mzigo wa mwingine.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 8 (6:164), 15 (17:15), 22 (35:18).

Kisha marejeo yenu ni kwa Mola wenu. Basi atawambia mliyokuwa mkiyafanya. Hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

Kwake Yeye Mwenyezi Mungu ndio marejeo ya viumbe na mikononi mwake ndio kuna malipo ya matendo na Yeye anajua siri zote na yale wanayoyakusudia.

Na dhara inapomfikia mtu humwomba Mola wake akielekea kwake. Kisha akimpa neema kutoka kwake, husahau yale aliyo kuwa akimwitia zamani, na akamfanyia Mwenyezi Mungu washirika ili apoteze njia yake.

Kumgusa ni kumpata, dhara ni tabu na maudhi na kuelekea kwake ni kurejea kwake. Maana ni kuwa mtu anapopatwa na shida ya nafsi yake au mali yake humkimbila Mwenyezi Mungu kwa kumnyenyekea, lakini shida ikimwondokea basi anasahau unyenyekevu aliokuwa nao.

Sema: Starehe na kufuru yako kidogo, kwani hakika wewe mi miongoni mwa watu wa Motoni.

Hili ni kemeo na kiaga kwa yule anayeamini wakati wa shida na kukufuru wakati wa raha. Hakuna mwenye shaka kwamba starehe ya dunia pamoja kufuru ina mwisho mbaya.

26

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

أَمَّنْ هُوَ قَانِتٌ آنَاءَ اللَّيْلِ سَاجِدًا وَقَائِمًا يَحْذَرُ الْآخِرَةَ وَيَرْجُو رَحْمَةَ رَبِّهِ قُلْ هَلْ يَسْتَوِي الَّذِينَ يَعْلَمُونَ وَالَّذِينَ لَا يَعْلَمُونَ إِنَّمَا يَتَذَكَّرُ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿٩﴾

9. Je, Afanyaye ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama akitahadhari na Akhera, na akitaraji rehema za Mola wake. Sema: Je, wanalingana sawa wale ambao wanajua na wale ambao hawajui? Hakika wanaokumbuka ni wenye akili tu.

قُلْ يَا عِبَادِ الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا رَبَّكُمْ لِلَّذِينَ أَحْسَنُوا فِي هَـٰذِهِ الدُّنْيَا حَسَنَةٌ وَأَرْضُ اللَّـهِ وَاسِعَةٌ إِنَّمَا يُوَفَّى الصَّابِرُونَ أَجْرَهُم بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴿١٠﴾

10. Sema: Enyi waja wangu ambao mmeamini! Mcheni Mola wenu. Wale ambao wamefanya wema katika dunia hii watapata wema. Na ardhi ya Mwenyezi Mungu ni pana. Hakika si mengineyo, wenye subira watapewa ujira wao bila ya hisabu.

قُلْ إِنِّي أُمِرْتُ أَنْ أَعْبُدَ اللَّـهَ مُخْلِصًا لَّهُ الدِّينَ ﴿١١﴾

11. Sema: Hakika mimi nimeamrishwa nimuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumsafia Yeye Dini.

وَأُمِرْتُ لِأَنْ أَكُونَ أَوَّلَ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٢﴾

12. Na nimeamrishwa niwe wa mwanzo wa Waislamu.

قُلْ إِنِّي أَخَافُ إِنْ عَصَيْتُ رَبِّي عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٣﴾

13. Sema: Hakika mimi ninahofia adhabu ya Siku Kubwa nikimuasi Mola wangu.

قُلِ اللَّـهَ أَعْبُدُ مُخْلِصًا لَّهُ دِينِي ﴿١٤﴾

14. Sema: Mwenyezi Mungu ninamuabudu kwa kumsafia Yeye Dini yangu.

فَاعْبُدُوا مَا شِئْتُم مِّن دُونِهِ قُلْ إِنَّ الْخَاسِرِينَ الَّذِينَ خَسِرُوا أَنفُسَهُمْ وَأَهْلِيهِمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ أَلَا ذَٰلِكَ هُوَ الْخُسْرَانُ الْمُبِينُ ﴿١٥﴾

15. Basi abuduni mpendacho badala yake. Sema: Hakika waliohasirika ni wale waliojihasiri nafsi zao na ahali zao Siku ya Kiyama. Ehe! hiyo ndiyo hasara iliyo dhahiri

لَهُم مِّن فَوْقِهِمْ ظُلَلٌ مِّنَ النَّارِ وَمِن تَحْتِهِمْ ظُلَلٌ ذَٰلِكَ يُخَوِّفُ اللَّـهُ بِهِ عِبَادَهُ يَا عِبَادِ فَاتَّقُونِ ﴿١٦﴾

16. Watakuwa na vivuli vya moto juu yao, na chini yao vivuli. Kwa hayo Mwenyezi Mungu anawahofisha waja wake. Enyi waja wangu! Nicheni.

HADHARI YA AKHERA NA MATARAJIO YA REHEMA YA MOLA

Aya 9 – 16

MAANA

Hata Manabi Wana Shauku Na Hofu

Je, Afanyae ibada nyakati za usiku kwa kusujudu na kusimama akitahadhari na Akhera, na akitaraji rehema za Mola wake.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja yule anayeamini wakati wa shida na kukufuru wakati wa raha, anafuatishia kumtaja yule anayeamini wakati wa shida na raha. Neema haimzidishii kitu isipokuwa imani, shukrani, kusujudu na kurukui wakati wa giza la usiku, watu wakiwa wamelala. Hafanyi kitu isipokuwa shauku ya thawabu za Mwenyezi Mungu na kuhofia adhabu yake.

Katika Aya hii kuna ishara kuwa mtu hafanyi ila kwa msukumo shauku na hofu, awe ni mwenye takua au muovu. Tofauti ni kuwa muovu anafanya na kuacha kwa shauku ya starehe za dunia na kuhofia tabu na machungu, lakini mwenye takua anafanya na kuacha kwa sahuku ya shamba la Akhera na neema zake na kuhofia adhabu yake na moto wake.

Hali hii iko hata kwa manabii walio maasumu ambao Mwenyezi Mungu Mtukufu amewasifu kwa kusema: “Wakituomba kwa shauku na hofu.” Juz. 17 (21:90).

Sema: Je, wanalingana sawa wale ambao wanajua na wale ambao hawajui? Hakika wanaokumbuka ni wenye akili tu.

Makusudio ya wanaojua hapa sio wale waliohifadhi sherehe na matini, wala sio wale waliogundua elektroni, mabomu ya masafa marefu na kupanda mwezini au kwenye Mars.

Hapana! Sio hao kabisa; isipokuwa makusudio ni wale wanaofanya kheri kwa binadamu wote na kuwakomboa wanaoadhibiwa ardhini na kuwaondoa watu kwenye tabu na mashaka.

Ama ulama wasiojali au wale ambao wameuza dini yao kwa mshetani na maibilisi kwa ajili ya kuwachapa watu na wakagundua silaha za maangamizi, hawa ni kama wanyama; bali wao wamepotea zaidi ya wanyama.

Hawawezi kuitambua hakika hii isipokuwa wale wenye akili na busara.

Sema: Enyi waja wangu ambao mmeamini! Mcheni Mola wenu, kwa sababu imani bila takua wala amali njema haina manufaa yoyote. Ndio maana baadhi ya maulama wamesema kuwa matendo mema ni sehemu ya kuamini haki.

Wale ambao wamefanya wema katika dunia hii watapata wema.

Haya ni maneno mapya hayaungani na yaliyotangulia. Maana yake ni kuwa mwenye kufanya hata chembe ya amali ya kheri ataiona.

Na ardhi ya Mwenyezi Mungu ni pana.

Kwa hiyo atayepata dhiki mjini kwake na akashindwa kutekeleza wajibu wake wa kidini au wa kidunia basi ahamie kwengine. Umetangulia mfano wake katika Juz. 5 (4:97).

Hakika si mengineyo, wenye subira watapewa ujira wao bila ya hisabu.

Yaani wenye kuvumilia shida kwa subira ya kiungwana na kukataa kusalimu amri kwenye ufukara na udhalili. Ama wale ambao wanawanyeyekea wenye nguvu na kuwa waoga mbele ya mataghuti, hao ndio waliohasirika duniani na akhera na huko ndiko kuhasrika waziwazi.

Sema: Hakika mimi nimeamrishwa nimuabudu Mwenyezi Mungu kwa kumsafia Yeye Dini.

Hakuna tofauti baina ya Nabii na mwenginewe. Yeye anaamrishwa kum- fanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu katika kauli na matendo yake yote; kama binadamu mwingine.

Na nimeamrishwa niwe wa mwanzo wa Waislamu.

Mtume(s.a.w. w ) aliwapa watu mwito wa uislamu baada ya kutangulia yeye mwenyewe kwenye Uislamu, kwa sababu anafanya anayoyasema wala hasemi asiyoyafanya.

Sema: Hakika mimi ninahofia adhabu ya Siku Kubwa nikimuasi Mola wangu.

Muhammad(s.a.w. w ) anamhofia Mwenyezi Mungu kwa sababu Yeye hawezi kumwepuka Mwenyezi Mungu wala hana hoja naye, bali yeye ni hoja ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake wote.

Utukufu zaidi kwa Muhammad(s.a.w. w ) ni kwamba yeye ni mtiifu kwa Mola wake, mwenye kumfanayia ikhlasi na mtangulizi wa mambo ya heri, akipata wahyi kutoka kwa Mola wake na akiutekeleza unavyotakikana:

قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ وَمَا أَدْرِي مَا يُفْعَلُ بِي وَلَا بِكُمْ إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ وَمَا أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٩﴾

“Sema: mimi si kioja katika mitume; wala sijui nitakavyofanywa wala nyinyi; sifuati ila niliyopewa wahyi na mimi si lolote ila ni muonyaji, mwenye kubainisha.” (46:9).

Sema: Mwenyezi Mungu ninamuabudu kwa kumsafiia Yeye Dini yangu.

Mara nyingine Muhammad(s.a.w. w ) anasisitiza, kwa amri ya Mwenyezi Mungu, kwamba Yeye ni mja mwenye kuamriwa. Mustshriq mmoja wa kingereza, Jeb Hamilton, mwalimu katika chuo kikuu cha Oxford, katika kitabu “Modern trends in Islam” anasema: “Qur’an inakataa fikra ya kuingiliwa kati, baina ya Mwenyezi Mungu na mtu. Unamweka mtu moja kwa moja mbele ya Mola wake bila ya kuweko wa katikati kiroho au kiutu.” Na hii ni tofuati kubwa inayoshindia Uislamu dini nyingine.

Basi abuduni mpendacho badala yake.

Huu ni ufasaha wa hali ya juu kuelezea hasira za Mwenyezi Mungu na makemeo kwa yule anayemfanya muabudia asiyekuwa Mwenyezi Mungu.

Sema: Hakika waliohasirika ni wale waliojihasiri nafsi zao na ahali zao Siku ya Kiyama. Ehe! hiyo ndiyo hasara iliyo dhahiri.

Wamezihasiri nafsi zao kwa sababu wamejiingiza kwenye Jahannam, marejeo mabaya kabisa, na wamewahasiri watu wao kwa sababu atakayekuwa mshirikina katika wao ataangamia. Na mumin ni adui wa mwenye kushirikisha duniani na akhera.

Watakuwa na vivuli vya moto juu yao, na chini yao vivuli.

Yaani adhabu ya kuungua itawazunguka kila mahali.

Kwa hayo Mwenyezi Mungu anawahofisha waja wake. Enyi waja wangu! Nicheni.

Mwenyezi Mungu amewabainishia adhabu ya akhera ili waweze kujiepusha nayo wakiwa duniani kwa kufanya utiifu na ikhlasi. Vinginevyo wataionja tu.

Msemaji mmoja alisema kuwa Pepo ni ladha za kiroho na moto ni machungu ya kinafsi na kwamba yote yaliyoelezwa kwenye Qur’an katika sifa za kihisia ni aina ya kupiga mfano na kuleta karibu kwenye akili. Kwa vile mabedui wanapenda sana asali, maziwa, pombe na wanawake mahurilaini. Msemaji wa maneno haya ametolea dalili kauli yake, kwa Aya hii tuliyo nayo: “Kwa hayo Mwenyezi Mungu anawahofisha waja wake.”

Kwamba inavyofahamika ni kuwa Mwenyezi Mungu ametaja matamshi ya adhabu kwa ajili ya kuhofisha tu, wala hakuna hakika[12]

Tunajibu : kila tamko lililokuja katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na sunna za Mtume wake ni wajibu kuchukulia dhahiri yake, ila ikiwa halingiliki akilini; na hapo tutalitumia kimajazi yanayokwenda na tamko lenyewe.

Hakuna tamshi katika matamshi ya sifa za Pepo na Moto yaliyotajwa na Qur’an, linalokataliwa na akili. Kwa hiyo ni wajibu kubakia tamko kwenye dhahiri yake, bila ya kuweko haja ya kuleta taawili.

Maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Kwa hayo Mwenyezi Mungu anawahofisha waja wake,” ni kuwa anawabainishia uhakika wa mambo, ili wachukue hadhari na wajiepushe na sababu zitakazopelekea hilo. Aya iliyotaja sifa za Moto ndio inayofahamisha maana haya:

إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقٌّ تَخَاصُمُ أَهْلِ النَّارِ ﴿٦٤﴾

“Hakika hayo ya kuhasimiana watu wa Motoni ni kweli.” (38:64).

Ama kauli ya kuwa huruma ya Mwenyezi Mungu haiafikiani na adhabu ya ya Moto kwa kiumbe huyu masikini aliye dhaifu, tunaijibu hivi:

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewandalia adhabu kali na chungu wale wanofanya ufisadi katika ardhi wakamwaga damu, kuwafanya waja wa Mungu kuwa watumwa wao, wakaangamiza watu kwa silaha za maangamizi na kuwaua kwa maelfu ndani ya dakika. Jahannam, pamoja na sifa zake zote, haitoshi kuwa ni malipo kwa hawa; bali wamehurumiwa pia. Amani imshukie yule aliyesema: “Ghadhabu haimshughulishi (asiwe) na huruma, wala huruma haimshughulishi (asiwe) na mateso.”

Tazama kifungu cha ‘Jahannam na silaha za maangamizi’ katika Juz.13 (14:46-52).

وَالَّذِينَ اجْتَنَبُوا الطَّاغُوتَ أَن يَعْبُدُوهَا وَأَنَابُوا إِلَى اللَّـهِ لَهُمُ الْبُشْرَىٰ فَبَشِّرْ عِبَادِ ﴿١٧﴾

17. Na wale wanaojiepusha na kuabudu taghut, na wakarejea kwa Mwenyezi Mungu, watapata bishara njema. Basi wabashirie waja wangu.

الَّذِينَ يَسْتَمِعُونَ الْقَوْلَ فَيَتَّبِعُونَ أَحْسَنَهُ أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ هَدَاهُمُ اللَّـهُ وَأُولَـٰئِكَ هُمْ أُولُو الْأَلْبَابِ ﴿١٨﴾

18. Ambao husikiliza maneno, wakafuata mazuri yake zaidi. Hao ndio aliowaongoza Mwenyezi Mungu, na hao ndio wenye akili.

أَفَمَنْ حَقَّ عَلَيْهِ كَلِمَةُ الْعَذَابِ أَفَأَنتَ تُنقِذُ مَن فِي النَّارِ ﴿١٩﴾

19. Je, Yule mwenye kustahili hukumu ya adhabu, Je, wewe unaweza kumwokoa aliyomo Motoni?.

لَـٰكِنِ الَّذِينَ اتَّقَوْا رَبَّهُمْ لَهُمْ غُرَفٌ مِّن فَوْقِهَا غُرَفٌ مَّبْنِيَّةٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَعْدَ اللَّـهِ لَا يُخْلِفُ اللَّـهُ الْمِيعَادَ ﴿٢٠﴾

20. Lakini waliomcha Mola wao watapata ghorofa zilizojengwa juu ya ghorofa; chini yake hupita mito. Ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu havunji ahadi yake.

أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّـهَ أَنزَلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً فَسَلَكَهُ يَنَابِيعَ فِي الْأَرْضِ ثُمَّ يُخْرِجُ بِهِ زَرْعًا مُّخْتَلِفًا أَلْوَانُهُ ثُمَّ يَهِيجُ فَتَرَاهُ مُصْفَرًّا ثُمَّ يَجْعَلُهُ حُطَامًا إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَذِكْرَىٰ لِأُولِي الْأَلْبَابِ ﴿٢١﴾

21. Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka mbinguni. Kisha akayapitisha yakawa chem-chem katika ardhi? Kisha kwa maji hayo akatoa mimea yenye rangi mbali mbali. Kisha hunyauka ukaiona imekuwa kimanjano kisha huifanya imevunjikavunjika. Bila ya shaka katika hayo kuna ukumbusho kwa wenye akili.

WANAOSIKILIZA MANENO WAKAFUATA MAZURI YAKE

Aya 17 – 21

MAANA

Na wale wanaojiepusha na kuabudu taghut, na wakarejea kwa Mwenyezi Mungu, watapata bishara njema. Basi wabashirie waja wangu.

Makusudio ya Tghut hapa ni masanamu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawabashiria wale walioacha shirki wakatubia na wakamtii Mwenyezi Mungu

Ambao husikiliza maneno, wakafuata mazuri yake zaidi. Hao ndio aliowaongoza Mwenyezi Mungu, na hao ndio wenye akili.

Makusudio ya maneno mazuri sio uzuri wa matamshi na ufasaha wake; isipokuwa ni yale yanayonufaisha duniani na akhera – yakiwa yana madhara basi ni mabaya. Ama maneno yasiyodhuru wala kunufaisha, basi hayo hayawezi kusifiwa kwa ubaya wala kwa uzuri.

Kauli ya Mwenyezi Mungu ni nzuri zaidi kuliko kauli yoyote, wala hakuna kitu bora kuliko kinachotoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, iwe kauli au vitendo. Kwa sababu vitu kutoka kwake ni sawa.

Wale wanaosikiliza maneno ya Mwenyezi Mungu na wakayafanyia kazi ndio walioongoka, mbele ya Mwenyezi Mungu, kwenye maarifa mazuri zaidi na ndio wanaochukua kiini cha maneno sio maganda.

Imam Ali(a.s ) anasema:“Kithirisheni kumtaja Mungu kwa kuwa ni utajo mzuri zaidi, na yafanyieni shauku ambayo (s.w.t) amewaahidi wachamungu, kwa kuwa ahadi yake ni ahadi ya kweli mno, na fuateni mwongozo wa Nabii wenu kwa kuwa huo ni mwongozo bora zaidi, na fanyeni kwa mwenendo wake kwa kuwa ni mwenendo mwongofu bora mno, na jifundisheni Qur’an kwa kuwa hiyo ni maongezi mazuri zaidi, na jitahidini kuifahamu kwa kuwa ni chanuo la nyoyo.”

Je, Yule mwenye kustahili hukumu ya adhabu ni sawa na yule aliyeokolewa na adhabu ya Mwenyezi Mungu.

Je, wewe Muhammad unaweza kumwokoa aliyomo Motoni?

Hapana! Hakuna wasila wowote wa kuokoka na adhabu ya Mwenyezi Mungu ila matendo mema na msamaha wa Mwenyezi Mungu, iliyotukuka hekima yake. Hapana mwenye shaka kwamba mwenye kuzama katika upotevu, Mwenyezi Mungu hatamwangalia: “Hao hawatakuwa na sehemu yoyote akhera, wala Mwenyezi Mungu hatasema nao wala hatawatazama siku ya Kiyama, wala hatawatakasa, nao watapata adhabu iumizayo. Juz. 3 (3:77).

Lakini waliomcha Mola wao watapata ghorofa zilizojengwa juu ya ghorofa; chini yake hupita mito. Ndiyo ahadi ya Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu havunji ahadi yake.

Hii ndio ahadi ya Qur’an – kukutanisha bishara na onyo, ahadi na kiaga, kuwataja wenye takua na thawabu zao na kuwataja mataghuti na adhabu yao. Hawa wana vivuli vya moto na wale wana ghorofa za pepo. Hii ni ahadi yake Mwenyezi Mungu Mtukufu; na ninani mkweli wa maneno zaidi ya Mwenyezi Mungu?

Je! Huoni kwamba Mwenyezi Mungu ameteremsha maji kutoka mbinguni. Kisha akayapitisha yakawa chemchem katika ardhi?

Mvua inashuka kutoka mbinguni na kutirizika juu aya ardhi, kisha maji yananyonywa ndani ya ardhi, yanakuwa chemchem na kuwanufaisha watu. Je, hii yote ni sadfa au ni mipangilio ya Mjuzi Mwenye hekima?

Kisha kwa maji hayo akatoa mimea yenye rangi mbali mbali.

Je, mimea hii yenye rangi na ladha tofauti imetengenezwa na maumbile asili au ni kwa msaada wa Aliyetengeneza hayo maumbile asili na yaliyo ndani yake?

Kisha hunyauka ukaiona imekuwa kimanjano.

Baadae mimea hunyauka na kuwa manjano inapokomaa; kisha huifanya imevunjikavunjika.

Baada ya kukauka.

Bila ya shaka katika hayo kuna ukumbusho kwa wenye akili.

Katika kuteremshwa mvua, kuoteshwa mimea, kuwa kijani kisha kuwa njano, kisha kuvunjikavunjika kulingana na hekima na masilahi. Yote hayo ni ukumbusho wa muumbaji na mwanzilishaji.

Ikiwa haya yote yametokana na maji na mchanga, basi ni nani aliyeyaleta hayo maji, mchanga na ulimwengu kwa ujumla?

Tazama: Kifungu ‘Uhai umetoka wapi?’ katika Juz. 7 (6:95 – 99) na kifungu ‘Roho inatokana na amri ya Mola wangu’ katika Juz. 15 (17:62 – 85).