TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA15%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 28399 / Pakua: 5248
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

1

12

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini na Sita: Surat Yasin. Imeshuka Makka isipokuwa Aya moja. Ina Aya 83.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

يس ﴿١﴾

1. Yasin.

وَالْقُرْآنِ الْحَكِيمِ ﴿٢﴾

2. Naapa kwa Qur’an yenye hekima.

إِنَّكَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿٣﴾

3. Hakika wewe bila shaka ni miongoni mwa waliotumwa.

عَلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٤﴾

4. Juu ya njia iliyonyooka.

تَنزِيلَ الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ ﴿٥﴾

26. Ni uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

لِتُنذِرَ قَوْمًا مَّا أُنذِرَ آبَاؤُهُمْ فَهُمْ غَافِلُونَ ﴿٦﴾

6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi ni wenye kughafilika.

لَقَدْ حَقَّ الْقَوْلُ عَلَىٰ أَكْثَرِهِمْ فَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿٧﴾

7. Imekwishathibiti kauli juu ya wengi wao, kwa hiyo hawaamini.

إِنَّا جَعَلْنَا فِي أَعْنَاقِهِمْ أَغْلَالًا فَهِيَ إِلَى الْأَذْقَانِ فَهُم مُّقْمَحُونَ ﴿٨﴾

8. Hakika tumeweka minyororo shingoni mwao, nayo inafika videvuni, kwa hiyo vichwa vyao viko juu.

وَجَعَلْنَا مِن بَيْنِ أَيْدِيهِمْ سَدًّا وَمِنْ خَلْفِهِمْ سَدًّا فَأَغْشَيْنَاهُمْ فَهُمْ لَا يُبْصِرُونَ ﴿٩﴾

9. Na tumeweka kizuizi mbele yao na kizuizi nyuma yao na tumewafunika, kwa hiyo hawaoni.

وَسَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَأَنذَرْتَهُمْ أَمْ لَمْ تُنذِرْهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ﴿١٠﴾

10. Ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.

إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ اتَّبَعَ الذِّكْرَ وَخَشِيَ الرَّحْمَـٰنَ بِالْغَيْبِ فَبَشِّرْهُ بِمَغْفِرَةٍ وَأَجْرٍ كَرِيمٍ ﴿١١﴾

11. Hakika unamuonya yule tu anayefuata ukumbusho na akamcha Mwingi wa rehema kwa ghaibu. Basi mbashirie maghufira na ujira wa heshima.

إِنَّا نَحْنُ نُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَنَكْتُبُ مَا قَدَّمُوا وَآثَارَهُمْ وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ فِي إِمَامٍ مُّبِينٍ ﴿١٢﴾

12. Hakika sisi tunawahuisha wafu na tunayaandika wanayoyatanguliza na athari zao. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari linalobainisha.

WEWE NI KATIKA MITUME

Aya 1 – 12

MAANA

Yasin

Wafasiri wengi wamesema kuwa tamko hili lina maana kama mianzo mingine ya Sura yenye herufi za mkato; kama ilivyo katika Juz.1 (2:1). Ama kauli yake Mwenyezi Mungu: “Amani kwa Ilyasin” (37:130), makusudio yake ni Ilyas.

Naapa kwa Qur’an yenye hekima. Hakika wewe bila shaka ni miongoni mwa waliotumwa juu ya njia iliyonyooka.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameapa, kwa Qur’an yenye hekima, kwamba Muhammad(s.a.w.w) yuko kwenye dini ya ya sawasawa. Kuapa kwa Mwenyezi Mungu kwa Qur’an pamoja na kuisifu kuwa ina hekima, kunaashiria kwenye utukufu wa Qur’an na ukuu wake na kwamba ni dalili yenye nguvu zaidi juu ya ukweli wa Muhammad(s.a.w.w) katika mwito wake.

Ama kujisifu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa nguvu na rehema, katika kauli yake:

Ni uteremsho wa Mwenye nguvu Mwenye kurehemu, ni ishara kuwa anawachukulia waasi kwa namna ya Mwenye uwezo na anawahurumia waumini na wenye kutubia.

Imam Ali(a.s) anasema:“Ghadhabu haimshughulishi (asiwe) na rehema, wala rehema haimshughulishi (asiwe) na mateso.”

MDUNDO WA NDANI KATIKA QUR’AN

Mnamo mwaka 1959 Mustafa Mahmud, Mmisri, alitunga kitabu Allahu wal-insan (Mungu na mtu). Katika kitabu hicho alikana Mungu na ufufuo, nami nikamjibu kwa kutunga kitabu Allahu wal-Aqli (Mungu na Akili).

Kisha nikafuatilia makala zake na tungo zake. Nikasoma makala yake katika jarida linaloitwa Ruzil-yusf la tarehe 10-4-1967 akikiri kuweko ufufuo. Hayo nimeyaashiria katika Juz. 1 (2:28 – 29) kifungu cha ‘Ufufuo.’

Mustafa Mahmud ni mwana fasihi, mwenye akili inayogundua undani na siri za lugha. Ushahidi wa hayo ni aliyoyaandika kuhusu Qur’an katika jarida la Sabahul-khayr la tarehe 1-1-1970 kwa anuani ya “Usanifu wa Qur’an” Tunadokoa machache katika makala hiyo, kama yafuatavyo:

“Sijui niseme nini kuelezea hisia niliyoipata katika ibara ya kwanza ya Qur’an... Basi matamshi yake yalikuwa yakiingia kwenye nafsi yangu, kama kwamba ni kiumbe hai chenye maisha ya aina ya peke yake... Nikagundua simulizi za mdundo wa kindani katika ibara za Qur’an Hii ni siri ya ndani sana katika mpangilio wa Qur’an...

Yenyewe sio mashairi wala nathari au lugha ya mjazo; isipokuwa ni ubainifu maalum wa maneno yaliyoundwa kwa njia inayogundua mdundo wa kindani. Mdundo uliozoeleka unakuja kutoka nje na kufika masikioni, na sio ndani bali unatokana na mahadhi, wizani na kina.

Mdundo wa Qur’an hauna wizani wala kina au mahadhi, lakini pamoja na hayo, unashuka kwa kila herufi yake... kutoka wapi na vipi, hiyo ndiyo siri katika siri za Qur’an zisizofanana na mfumo wowote wa kifasihi. Inashangaza na wala hatuwezi kuujua mfumo wake. Ni mfumo wa kipekee haujapatakina katika kila kilichoandikwa kwa lugha ya kiarabu ya zamani na ya sasa. Haiwezekani kuuiga mfumo huu.”

Ndio haiwezekani kuuiga. Na hapa ndio inapatikana siri ya muujiza wa Qur’an. Baada ya mwandishi huyu kuleta ushahidi mwingi wa hakika hii katika maneno ya Mwenyezi Mungu na Aya zake, aliendelea kusema:

“Na sio mdundo wa kindani tu ndio kitu cha aina yake katika Qur’an, bali kuna sifa nyingine inayokutambulisha kuwa hii ni sanaa ya muumba sio ya muumbwa... Hebu isikilize Qur’an ikisifia mfungamano wa maingiliano ya kijinsia baina ya mume na mke, kwa tamako laini na la heshima, jambo ambalo huwezi kulipata kwenye lugha yoyote: “Alipomkurubia [5] 1 alishika mimba nyepesi.” Juz. 9 (7:189).

Tamko hili taghashaha alimfunika (kwa maana ya kumkurubia) linamchanganya mume na mke kama vinavyochanganyika vivuli viwili au kama rangi inavyofunika rangi nyingine. Tamko hili la ajabu linalofahamisha muingiliano mkamilifu wa mume na mke, ni ukomo wa ibara.

Hakika Qur’an ina hali ya kipekee na ya ajabu, inayoleta unyenyekevu katika nafsi na kuathiri moyo, pale tu matamshi yake yanapogusa masikio, kabla ya akili kuanza kuyafanyia kazi. Na ikianza kufanya uchambuzi na kutaamali, inagundua vitu vipya vinavyomzidisha unyenyekevu. Lakini hii ni hatua ya pili; inaweza kutokea na isitokee, inaweza kugundua siri za Aya na inaweza isigundue, na inaweza kuleta busara au isilete, lakini unyenyekevu upo.”

Hii nayo ni aina mojawapo ya muujiza wa Qur’an. Mwandishi huyu wa kitabu Allahu wal insan alimaliza makala yake ndefu kwa kusema: “Hakika Qur’an ni matamshi na maana kutoka kwa Mwenyezi Mungu ambaye amekizunguuka kila kitu kwa ujuzi.”

Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, basi ni wenye kughafilika.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kutaja kuwa Muhammad(s.a.w.w) ni Mtume wa haki na kwamba Qur’an imetoka kwake, sasa anabainisha umuhimu wa Qur’an kuwa inakataza aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu, kwenye masikio ya waarabu, walioghafilika na Mwenyezi Mungu na haki, bila ya kufikiwa na muonyaji kabla ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) .

Huko nyuma kwenye Juzuu hii, kwenye kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na hakuna uma wowote ila alipita humo muonyaji (35:24),” tumesema kuwa makusudio ya muonyaji hapo ni kila linalosimamia hoja, iwe ni akili au nakili na kwamba makusudio ya muonyaji kwenye Aya hii tuliyo nayo ni Mtume hasa.

Imekwishathibiti kauli juu ya wengi wao, kwa hiyo hawaamini.

Makusudio ya kauli hapa ni kiaga cha adhabu, na wengi wao ni hao maba- ba zao; yaani mababa za waarabu waliokuwa wakati wa Muhammad(s.a.w.w) , waliokufa kwenye ushirikina. Ni wachache sana waliokuwa kwenye dini ya Tawhid. Tazama Juz. 15 (17:105–111) kifungu ‘Wanyoofu.’

Hakika tumeweka minyororo shingoni mwao, nayo inafika videvuni, kwa hiyo vichwa vyao viko juu.

Mikono ikifungwa kwa minyororo mpaka shingoni kichwa huinuka juu, na aliyefungwa anakuwa hawezi kugeuka kuume wala kushoto au kuangalia mbele; atakuwa anaangalia juu tu.

Na tumeweka kizuizi mbele yao na kizuizi nyuma yao na tumewafunika, kwa hiyo hawaoni.

Siku ya Kiyama Mwenyezi Mungu atawaweka kwenye vizuizi viwili vya moto. Kimoja mbele yao na kingine nyuma yao, hawawezi kwenda mbele wala kurudi nyuma; wala hawezi kuona mbingu, kwa sababu vizuizi viwili vimefunika macho yao.

Sio mbali kuwa hiki ni kinaya cha ukali na uchungu wa adhabu. Kwa vyovyote iwavyo, adhabu haihusiki na washirikina tu, bali itaenea kwa kila mwenye hatia na dhalimu.

Imam Ali(a.s) anasema:“Ama watu wa maasia atawaweka mahali pa baya, atawafunga mikono kwa minyororo hadi videvuni, utosi utafungwa na nyayo, na atawavisha kanzu za lami na nguo za moto. Watu wake watafungiwa mlango katika Moto mkali wenye kuvuma.”

Umetangulia mfano wake katika Juzuu hii (34:33).

Ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye hawataamini.

Ni sawa kwao ewe Muhammad, uwape mawawidha au usiwape, basi hakika wao, hawatafanya lolote isipokuwa kwa hawaa zao na masilahi yao. Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:6).

Hakika unamuonya yule tu anayefuata ukumbusho na akamcha Mwingi wa rehema kwa ghaibu. Basi mbashirie maghufira na ujira wa heshima.

Anayekusikiliza ni yule anayeitafuta haki kwa ajili ya haki na kwenda nayo kwa matokeo yoyote yatakayokuwa. Umetangulia mfano wake katika Juzuu hii (35: 18).

Hakika sisi tunawahuisha wafu na tunayaandika wanayoyatanguliza na athari zao. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari linalobainisha.

Daftari linalobainisha ni kinaya cha elimu ya Mwenyezi Mungu. Maana ni kuwa, Mwenyezi Mungu atawafufua, na ameyahifadhi wanayoyafanya ya kheri na ya shari na athari walizoziacha za manufaa au madhara, na kwamba Yeye atamlipa kila mmoja alilolifanya, nao hawatadhulumiwa.

وَاضْرِبْ لَهُم مَّثَلًا أَصْحَابَ الْقَرْيَةِ إِذْ جَاءَهَا الْمُرْسَلُونَ ﴿١٣﴾

13. Na wapigie mfano wenyeji wa mji Mitume walipowafikia.

إِذْ أَرْسَلْنَا إِلَيْهِمُ اثْنَيْنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزْنَا بِثَالِثٍ فَقَالُوا إِنَّا إِلَيْكُم مُّرْسَلُونَ ﴿١٤﴾

14. Tulipowatuma wawili wakawakadhibisha. Basi tukawaongezea nguvu kwa (mwingine) wa tatu Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.

قَالُوا مَا أَنتُمْ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَمَا أَنزَلَ الرَّحْمَـٰنُ مِن شَيْءٍ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا تَكْذِبُونَ ﴿١٥﴾

15. Wakasema nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na mwingi wa rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.

قَالُوا رَبُّنَا يَعْلَمُ إِنَّا إِلَيْكُمْ لَمُرْسَلُونَ ﴿١٦﴾

16. Wakasema: Mola wetu anajua kwamba sisi tumetumwa kwenu.

وَمَا عَلَيْنَا إِلَّا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿١٧﴾

17. Wala si juu yetu ila kufikisha waziwazi.

قَالُوا إِنَّا تَطَيَّرْنَا بِكُمْ لَئِن لَّمْ تَنتَهُوا لَنَرْجُمَنَّكُمْ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿١٨﴾

18. Wakasema: Hakika sisi tunapata mkosi kwa ajili yenu. Kama hamtakoma basi hakika tutawapiga mawe na itawafika adhabu chungu kutoka kwetu.

قَالُوا طَائِرُكُم مَّعَكُمْ أَئِن ذُكِّرْتُم بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ مُّسْرِفُونَ ﴿١٩﴾

19. Wakasema: Mkosi wenu mnao wenyewe. Je, ni kwa kuwa mnakumbushwa? Bali nyinyi ni watu mnaopituka mipaka.

وَجَاءَ مِنْ أَقْصَى الْمَدِينَةِ رَجُلٌ يَسْعَىٰ قَالَ يَا قَوْمِ اتَّبِعُوا الْمُرْسَلِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na akaja mtu mbio kutoka upande wa mbali wa mjini akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni Mitume.

اتَّبِعُوا مَن لَّا يَسْأَلُكُمْ أَجْرًا وَهُم مُّهْتَدُونَ ﴿٢١﴾

21. Wafuateni wasiowaomba ujira nao wameongoka.

وَمَا لِيَ لَا أَعْبُدُ الَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٢٢﴾

22. Na kwa nini nisimwabudu yule aliyeniumba na kwake mtarejeshwa?

أَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِ آلِهَةً إِن يُرِدْنِ الرَّحْمَـٰنُ بِضُرٍّ لَّا تُغْنِ عَنِّي شَفَاعَتُهُمْ شَيْئًا وَلَا يُنقِذُونِ ﴿٢٣﴾

23. Je, nishike miungu mingine badala yake? Mwingi wa rehema akinitakia madhara, uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.

إِنِّي إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٢٤﴾

24. Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotofu ulio dhahiri.

إِنِّي آمَنتُ بِرَبِّكُمْ فَاسْمَعُونِ ﴿٢٥﴾

25. Hakika mimi nimemwamini Mola wenu, basi nisikilizeni.

قِيلَ ادْخُلِ الْجَنَّةَ قَالَ يَا لَيْتَ قَوْمِي يَعْلَمُونَ ﴿٢٦﴾

26. Ikasemwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti watu wangu wangejua.

بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ الْمُكْرَمِينَ ﴿٢٧﴾

27. Jinsi Mola wangu alivyonighufiria na akanifanya katika waheshimwa.

WAJUMBE WAWILIA WALIOWAONGEZEWA NGUVU KWA WA TATU

Aya 13 – 27

MAANA

Na wapigie mfano wenyeji wa mji Mitume walipowafikia.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume awaambie washirikina wa Kiarabu. Ama mji, wafasiri wengi wamesema ni Antiokia, lakini Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuelezea. Kwa sababu makusudio ya kupiga mfano ni kupata mawaidha na mazingatio, sio jina la mji na sehemu yake.

Dhana kubwa ni kuwa wafasiri wametegemea vitabu vya kinaswara; ambapo imeelezwa kwenye Matendo ya mitume 11:19 – 26, kwamba Barnaba na Sauli walikwenda Antiokia na kuwafundisha watu wengi. Na kwamba mitume ni wanafunzi 12 aliowachagua Bwana Masih(a.s) ili wamsaidie na wamwone atakapotoka kaburini, waelezee walimwengu; kama ilivyoelezwa kwenye Mathayo na Matendo ya mitume.

Barnaba alikuwa ni Mkupro (Cyprus) akaingia kwenye ukiristo katika zama za mitume na akawa ni mhubiri; kama ilivyoelezwa katika ‘Kamusi ya Kitabu kitakatifu’

Tulipowatuma wawili wakawakadhibisha. Basi tukawaongezea nguvu kwa (mwingine) wa tatu.

Katika tafsiri nyingi imeelezwa kuwa mitume walikuwa ni wanafunzi wa Isa(a.s ) na kwamba yeye ndiye aliyewatuma wawili mjini kisha akawaongezea nguvu kwa mwingine wa tatu.

Lakini neno mitume likitegemezwa kwa Mwenyezi Mungu, kama ilivyo katika neno ‘tulipowatuma’ na ‘tukawaongezea nguvu,’ huwa linafahamisha kuwa wao walitumwa kwa amri ya Mwenyezi Mungu moja kwa moja sio kwa kwa amri ya Isa(a. s ) .

Vyovyote iwavyo, la kuzingatia ni utendaji si majina. Zaidi ya hayo sisi hatutaulizwa mbele ya Mwenyezi Mungu, wala hilo halina uhusiano wowote na maisha yetu kwa karibu au mbali. Maana yaliyo wazi, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwatuma mitume watatu kwenye mji huo, watoe mwito wa haki.

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu. Wakasema; nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na mwingi wa rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.

Hii ndio nembo ya wapinzani siku zote. Tazama Juz. 13 ( 14:10), Juz. 15 (17:94), Juz. 17 (21:3), Juz. 18 (23:24) na Juz. 19 (26:154).

Wakasema: Mola wetu anajua kwamba sisi tumetumwa kwenu. Wala si juu yetu ila kufikisha waziwazi.

Baada ya mitume kusimamisha hoja za kusadikisha ukweli wao, waliwaambia wakadhibishaji kuwa sisi tumetumwa kwenu na Mwenyezi Mungu, akatupa ubainifu, kama mnavyouona, na tumetekeleza ujumbe wake, kama inavyotakikana. Basi si juu yetu tena hisabu yenu wala si juu yenu nyinyi hisabu yetu. Yeye ni mjuzi mwenye kuhisabu.

Wakasema: Hakika sisi tunapata mkosi kwa ajili yenu. Kama hamtakoma basi hakika tutawapiga mawe na itawafika adhabu chungu kutoka kwetu. Wakasema: Mkosi wenu mnao wenyewe. Je, ni kwa kuwa mnakumbushwa? Bali nyinyi ni watu mnaopituka mipaka.

Mkosi wenu mnao wenyewe; yaani hakuna mkosi, bali hizo ni dhana zenu tu. Kuna Hadith mashuhuri isemayo:“Hakuna kuambukiza, wala mkosi wala nyuni” Imam As-Sadiq(a.s ) anasema:“Mkosi unaufanya wewe, ukiupuuza utakupuuza, ukiutilia mkazo utakutilia mkazo na ukiufanya si chochote nao hautakuwa ni chochote”

Yaani hakuna kitu kama kisirani, ndege au mkosi; wala hauna athari yoyote kwa mtu; isipokuwa unaathiri nafsi ya mtu na mishipa yake, kwa vile anavyouwazia tu; kama mtoto anavyotishika na zimwi.

Maana ni kuwa wakadhibishaji waliwaambia mitume kuwa mmetuletea mkosi, kwa hiyo tunahofia tutagawanyika; sasa bora mnyamaze, la sivyo tutawanyamazisha kwa kuwapiga mawe na adhabu kali. Ndio Mitume wakawaambia, chimbuko la hofu ya mkosi linatokana na wasiwasi wenu nyinyi wenyewe, kwamba mwito wetu ni mkosi na shari; na hali yakuwa shari inatoka kwenu kwa kufanya shirki, ujahili na ufisadi.

Na akaja mtu mbio kutoka upande wa mbali wa mjini.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hakuashiria jina la mtu huyu, lakini wafasiri wengi wakasema jina lake ni Habib An-Najar, na kwamba nyumba yake ilikuwa kandoni mwa mji. Alikuwa mumin. Aliposikia kuwa watu wake wanaazimia kuwaua mitume, alifanya haraka kuja kuwaokoa na kuwasaidia.

Sijui wafasiri wamelitoa wapi jina hili. Mimi nimetafuta mpaka katika Biblia ukurasa wa yaliyomo na kamusi ya Kitabu kitakatifu pia sikulipata.

Vyovyote iwavyo, jina la huyo mtu halina mfungamano wowote na sisi. Wala hakuna linalotushughulisha isipokuwa lile lililofahamishwa na Aya. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu kuwa na imani na wema, kwa sababu alisema:

Enyi watu wangu! Wafuateni Mitume. Wafuateni wasiowaomba ujira nao wameongoka.

Aliwapa nasaha watu wake wakubali mwito wa Mitume wala wasiwapinge, kwa sababu ni kwa masilahi yao. Wanatoa mwito na hawataki malipo wala shukrani; wala uluwa au ufisadi katika ardhi.

Na kwa nini nisimwabudu yule aliyeniumba na kwake mtarejeshwa?

Kauli hii ni ya yule mumin anayetoa nasaha. Maana yake ni kuwa, ni kizuizi gani kitakachonizuia na ibada ya ambaye amenifanya niweko baada ya kutokuweko, kisha atatufufua sote baada ya mauti kwa ajili ya hisabu na malipo?

Hapa anawapinga watu wake walioacha ibada ya Mungu mmoja wa pekee. Anaendelea kuwagonga na kusema:

Je, nishike miungu mingine badala yake? Mwingi wa rehema akinitakia madhara, uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa. Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotofu ulio dhahiri.

Vipi niabaudu masanamu yasiyodhuru wala kunufaisha? Hayaokoi wala hayaombei? Nikifanya hivyo nitakuwa nimepotea, wala sitakuwa katika walioongoka. Hapana!

Hakika mimi nimemwamini Mola wenu, basi nisikilizeni.

Hawi jasiri wa maneno haya isipokuwa yule asiyeogopa mauti katika njia ya haki na kuinusuru. Kuna mapokezi yanayoeleza kuwa alipowajia watu wake na hakika hii, walimuua kwa kumpiga mawe na hakupata wa kumhami. Hili haliko mbali kulingana na sera ya mataghuti na wafisadi. Linalotia nguvu ukweli wa risala hii ni ile kauli ya washirikina kwa mitume: “Kama hamtakoma basi hakika tutawapiga mawe na itawafika adhabu chungu kutoka kwetu.”

Katika Tafsiri ya Zamakhshari na Tha’labi imesemwa: Watangulizi wa umma ni watatu, hawakukufuru hata kwa kupepesa jicho: Ali bin Abu Twalib, Mtu wa Yasin na Mumin wa watu wa Firauni.

Ikasemwa: Ingia Peponi!

Aliiuza nafsi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na thamani ya bei yake ikawa ni Pepo. Hiyo ni tosha kuwa ni thawabu na malipo.

Akasema: Laiti watu wangu wangejua jinsi Mola wangu alivyonighufiria na akanifanya katika waheshimiwa.

Hakusema hivi kwa kuwacheka watu, ingawaje walimkadhibisha, hapana! Watu wema hawawi hivi; bali alisema hivi kuwasikitikia na yaliyowapita, akitamani lau wangelijua kwamba yeye alikuwa akiwapa nasaha na kwamba zilikuwa ni njozi na ujinga kuwa yeye na mitume wana mikosi.

13

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

وَمَا أَنزَلْنَا عَلَىٰ قَوْمِهِ مِن بَعْدِهِ مِن جُندٍ مِّنَ السَّمَاءِ وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ ﴿٢٨﴾

28. Na hatakuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala sisi si wenye kuteremsha.

إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ خَامِدُونَ ﴿٢٩﴾

29. Hakuwi ila ukelele mmoja tu na mara wamezimia.

يَا حَسْرَةً عَلَى الْعِبَادِ مَا يَأْتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ ﴿٣٠﴾

30. Ni sikitiko kwa waja. Hawakufika mitume ila wanamfanyia stihizai.

أَلَمْ يَرَوْا كَمْ أَهْلَكْنَا قَبْلَهُم مِّنَ الْقُرُونِ أَنَّهُمْ إِلَيْهِمْ لَا يَرْجِعُونَ ﴿٣١﴾

31. Je, hawaoni umma ngapi tulizoziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei kwao.

وَإِن كُلٌّ لَّمَّا جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ ﴿٣٢﴾

32. Na hapana ila wote watahudhurishwa mbele yetu.

وَآيَةٌ لَّهُمُ الْأَرْضُ الْمَيْتَةُ أَحْيَيْنَاهَا وَأَخْرَجْنَا مِنْهَا حَبًّا فَمِنْهُ يَأْكُلُونَ ﴿٣٣﴾

33. Na ishara kwao ni ardhi iliyokufa, tunaifufua na tukatoa ndani yake nafaka wakaila.

وَجَعَلْنَا فِيهَا جَنَّاتٍ مِّن نَّخِيلٍ وَأَعْنَابٍ وَفَجَّرْنَا فِيهَا مِنَ الْعُيُونِ ﴿٣٤﴾

34. Na tukafanya ndani yake mabustani na mitende na mizabibu, na tukachimbua chemchem ndani yake.

لِيَأْكُلُوا مِن ثَمَرِهِ وَمَا عَمِلَتْهُ أَيْدِيهِمْ أَفَلَا يَشْكُرُونَ ﴿٣٥﴾

35. Ili wale katika matunda yake na hayakufanywa kwa kwa mikono yao, je hawashukuru?

سُبْحَانَ الَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّهَا مِمَّا تُنبِتُ الْأَرْضُ وَمِنْ أَنفُسِهِمْ وَمِمَّا لَا يَعْلَمُونَ ﴿٣٦﴾

36. Kutakata na mawi ni kwa ambaye ameumba jozi katika kila vinavyooteshwa na ardhi na katika nafsi zao na katika wasivyovijua.

NAWASIKITIKIA WAJA WANGU

Aya 28 – 36

MAANA

Na hatakuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala sisi si wenye kuteremsha. Hakuwi ila ukelele mmoja tu na mara wamezimia.

Kaumu yake, ni kaumu yake yule mumin aliyesema: ‘Wafuateni mitume.’ Makusudio ya jeshi la mbinguni ni malaika, na ukelele ni adhabu.

Maana ni kuwa kuangamia kwa wakadhibishaji ni jambo rahisi kwetu, lisilohitajia majeshi kutoka mbinguni. Bali ukelele mmoja tu, watakousikia, unawatosha kuyafanya majumba yao ni makaburi ya mili yao.

Ni sikitiko kwa waja. Hawakufika mitume ila wanamfanyia stihizai.

Kunga’ng’ania washirikina kukadhibisha mitume na kuwafanyia madharau ndiko kunakoleta masikitiko.

Unaweza kuuliza : Ni nani anayesikitika na hali tunajua kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) hamsikitikii yoyote?

Jibu : Masikitiko hapa ni kinaya cha mwendo wao mbaya na mwisho wao muovu ambao utawaletea masikitiko watakapoiona adhabu ya Jahannam na kujuta kwao walivyopoteza fursa katika maisha ya dunia.

Je, hawaoni umma ngapi tulizoziangamiza kabla yao?

Wanasikitika na kujuta kwa sababu hawakuchukua somo duniani kwa umma zilizowatangulia zilizoangamizwa na Mwenyezi Mungu walipowakadhibisha mitume.

Hakika hao hawarejei kwao.

Wafasiri wengi wa zamani na wapya, akiwemo Al-Maraghi na mwenye Dhilal, wamesema kuhusu maana ya jumla hii ni: Hawaoni wakadhibishaji kwamba tuliowaangamiza hawarudi tena duniani?

Lakini tafsiri hii inatakikana iangaliwe vizuri. Kwa sababu kukosa kurudi wafu daniani itakuwa ni hoja ya wakadhibishaji kuwa hakuna ufufuo; na wala si hoja juu yao.

Maana ya sawa – kwa tunavyodhania - ni kuwa je, hawakuona wakadhibishaji kwamba Mwenyezi Mungu amewangamiza waliopita wote na hakubaki yeyote wa kuweza kuwarudia wakadhibishaji kuwafahamisha habari ya wakadhibishaji wa mwanzo? Kinachofahamisha kuangamia kwao ni athari tu:

فَتِلْكَ بُيُوتُهُمْ خَاوِيَةً بِمَا ظَلَمُوا إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّقَوْمٍ يَعْلَمُونَ ﴿٥٢﴾

“Basi hizo nyumba zao ni tupu kwa sababu ya walivyodhulumu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa watu wanaojua.” Juz. 19 (27:52).

Jumla hii inafanana na kauli yake Mwenyezi Mungu iliyo katika Aya ya 50 ya sura hii tuliyo nayo:“Basi hawataweza kuusia, wala hawatarejea kwa watu wao”

Na hapana ila wote watahudhurishwa mbele yetu.

Watu wote kesho watasimamishwa mbele ya Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kuchukuliwa hisabau ya matendo yao, hilo ni lazima.

Na ishara kwao ni ardhi iliyokufa, tunaifufua na tukatoa ndani yake nafaka wakaila. Na tukafanya ndani yake mabustani na mitende na mizabibu, na tukachimbua chemchem ndani yake.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7(6:99), Juz. 13 (13:4) na Juz. 17 (22:5).

Ili wale katika matunda yake na hayakufanywa kwa mikono yao, je hawashukuru?

Neema za Mwenyezi Mungu hazihisabiki wala hazidhibitiki. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Na waliyofanya kwa mikono yao,’ inaashiria kuwa neema ya kweli ni mali ya halali iliyochumwa kwa jasho, lakini mali ya haramu ni moto:

أُولَـٰئِكَ مَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ إِلَّا النَّارَ ﴿١٧٤﴾

“Hao hawali matumboni mwao isipokuwa Moto” Juz. 2 (2:174),

إِنَّمَا يَأْكُلُونَ فِي بُطُونِهِمْ نَارًا ﴿١٠﴾

“Hakika wanakula moto matumboni mwao” Juz. 4 (4:10).

Kutakata na mawi ni kwa ambaye ameumba jozi katika kila vinavyooteshwa na ardhi na katika nafsi zao na katika wasivyovijua.

Ametakasika kutokana na shirk, na ametakata na kutukuka kukubwa ambaye ameumba aina za wanyama, ndege, mimea na binadamu. Pia vile ambavyo hatuvijui katika mbingu na ardhini. Kila aina katika aina hizo inahitalifiana kirangi na kiumbo. Nyingine zinatofauti na kiladha; kama vile mimea na wanadamu kutofautiana kiakhlaki.

Wataalamu wanasema hata vitu vikavu vigumu vinafungamana kutokana na vitu viwili: chanya na hasi, na lau si hivyo basi kusingepatikana vitu. Wala hakuna chimbuko la hayo isipokuwa Mjuzi mwenye hekima. Ama sadfa haina nafasi na hawezi kuuikimbilia ila mzembe mwenye kujikwaza.

وَآيَةٌ لَّهُمُ اللَّيْلُ نَسْلَخُ مِنْهُ النَّهَارَ فَإِذَا هُم مُّظْلِمُونَ ﴿٣٧﴾

37. Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.

وَالشَّمْسُ تَجْرِي لِمُسْتَقَرٍّ لَّهَا ذَٰلِكَ تَقْدِيرُ الْعَزِيزِ الْعَلِيمِ ﴿٣٨﴾

38. Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.

وَالْقَمَرَ قَدَّرْنَاهُ مَنَازِلَ حَتَّىٰ عَادَ كَالْعُرْجُونِ الْقَدِيمِ ﴿٣٩﴾

39. Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka ukarudi kuwa kama karara la zamani.

لَا الشَّمْسُ يَنبَغِي لَهَا أَن تُدْرِكَ الْقَمَرَ وَلَا اللَّيْلُ سَابِقُ النَّهَارِ وَكُلٌّ فِي فَلَكٍ يَسْبَحُونَ ﴿٤٠﴾

40. Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia.

وَآيَةٌ لَّهُمْ أَنَّا حَمَلْنَا ذُرِّيَّتَهُمْ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ﴿٤١﴾

41. Na ni Ishara kwao kwamba tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.

وَخَلَقْنَا لَهُم مِّن مِّثْلِهِ مَا يَرْكَبُونَ ﴿٤٢﴾

42. Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyovipanda.

وَإِن نَّشَأْ نُغْرِقْهُمْ فَلَا صَرِيخَ لَهُمْ وَلَا هُمْ يُنقَذُونَ ﴿٤٣﴾

43. Na tukitaka tunawagharikisha; wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi.

إِلَّا رَحْمَةً مِّنَّا وَمَتَاعًا إِلَىٰ حِينٍ ﴿٤٤﴾

44. Isipokuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.

KILA KITU KINA ISHARA

Aya 37 – 44

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja ishara za ulimwengu zinazofahamisha uweza wake na ukuu wake; kama ifutavyo:

Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.

Usiku unafuatana na mchana kutokana na kuwa ardhi ni tufe na kuwa inazunguka kama jiwe la kusagia. Wakati ardhi inapozunguka, upande ule unaolielekea jua unakuwa ni mchana na ule usiolieleka jua unakuwa ni usiku. Nao ukifikia kwenye jua unakuwa mchana na ule mwingine unakuwa usiku, na kuendelea namna hiyo.

Hali hiyo ndiyo aliyoitolea ibara Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwa ni kuvua. Na amekutegemeza kwake Yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa sababu ndiye mumba wa ulimwengu na msababishaji wa sababu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (3:27) na Juz. 15 (17:12).

Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.

Wafasiri wametofautiana katika makusudio ya neno Mustaqarrin lahaa, tulilolifasiri kwa maana ya kiwango chake. Razi ameishilia kwenye kauli nne, lakini zote ziko mbali na ufahamu. Ilivyo hasa ni kinaya cha kwenda kwa nidhamu na mpangilio.

Hilo linatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua’ Mwandishi wa kitabu Al-qur’an wal-ilmulhadith (Qur’an na sayansi) amenukuu wataalamu wa falaki wa kisasa wakisema: Jua linakwenda kwa kasi ya maili 12 kwa sekunde mbali ya kuwa hilo lenyewe linazunguka, na kwamba linatofautiana na mzunguuko wa ardhi.

Yametangulia maelezo yanayoambatana na haya katika Juz. 13 (13:2).

Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka ukarudi kuwa kama karara la zamani.

Vituo hivi havibadiliki au kuondoka mahali pake, wala mwezi haupotei navyo. Wana falaki wanasema kuwa ni 28. Mwezi unashuka usiku kwenye kila kimoja na unajificha nyusiku mbili ikiwa mwezi utakuwa wa siku 30 na usiku mmoja ukiwa na siku 29.

Wakati huo unakuwa kama tawi la mtende kwa wembamba. Haya ndio makusudioya kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘karara.’ Yametangulia yanayofungamana na haya katika Juz.10 (9: 36 – 37) kifungu cha ‘miezi miandamo ndiyo miezi ya kimaumbile’

Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia.

Kila sayari ina njia yake maalum, ikizunguka humo kwa nidhamu na kwenda kwenye kituo chake kilichopangiwa mpaka atakapozikunja Mwenyezi Mungu kama karatasi. Kwenye Nahjul-balagh kuna maelezo haya: “Na akalifanya Jua lake – yaani jua na hizo sayari - kuwa ni ishara yenye kuonwa na mchana wake, na Mwezi wake kuwa unaufuta usiku wake; yaani mwangaza wa mwezi unazidi miangaza ya sayari nyinginezo. Basi akazipitisha katika njia yake ili upambanuke usiku na mchana kwazo na ili ijulikane idadi ya miaka na hisabu kwa makisio ya hizo mbili.

Miongoni mwa niliyoyasoma katika maudhui haya ni Hadith Qudsi aliyoitaja mwenye kitabu cha Al-asfar Jalada la tatu, maana yake ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amesema: Lau jua lingewekwa upande maalum, basi matajiri wangelijenga jengo refu kuzuia mwanga wa Jua usiwafikie mafukara, lakini ameliweka kwenye anga likizunguka na kwenda, ili fukara apate sehemu yake, sawa na anavyopata tajiri.

Na ni ishara kwao kwamba tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.

Kwao, ni kwao hao Binadamu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawakumbusha neema zake kuu kwao; miongoni mwazo ni kuwabeba kwenye majahazi wao na mizigo yao, wakitolewa huku na kupelekwa kule. Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (14:32) na Juz. 15 (17:66).

Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyovipanda.

Yaani mfano wa majahazi. Wafasiri wa kale walisema kuwa makusudio ya mfano wake ni ngamia, farasi, nyumbu na punda. Walisema haya wakati ambapo hakukuwa na ndege wala gari au chombo chote cha angani.

Na tukitaka tunawagharikisha hata kama wako katika manowari na meli.

Lengo ni kuwakumbusha neema ya kuokoka na kuangamia lau kama si rehema yake na usaidizi wake.Wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi, na kuangamia kadiri watakavyotaka usaidizi.

Isipokuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.

Yaani isipokuwa Mwenyezi Mungu akiwawahi kwa rehema yake na kuwaakhirisha hadi muda malum kulingana na ujuzi wake na hekima yake.

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ اتَّقُوا مَا بَيْنَ أَيْدِيكُمْ وَمَا خَلْفَكُمْ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿٤٥﴾

45. Na wanapoambiwa: Ogopeni yalioko mbele yenu na yaliyoko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa.

وَمَا تَأْتِيهِم مِّنْ آيَةٍ مِّنْ آيَاتِ رَبِّهِمْ إِلَّا كَانُوا عَنْهَا مُعْرِضِينَ ﴿٤٦﴾

46. Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao ila wao huwa ni wenye kuipuuza.

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ أَنفِقُوا مِمَّا رَزَقَكُمُ اللَّـهُ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا أَنُطْعِمُ مَن لَّوْ يَشَاءُ اللَّـهُ أَطْعَمَهُ إِنْ أَنتُمْ إِلَّا فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٤٧﴾

47. Na wanapoambiwa: Toeni katika aliyowapa Mwenyezi Mungu, waliokufuru huwaambia walioamini: Je! Tumlishe ambaye Mwenyezi Mungu angependa angelimlisha? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhahiri.

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٤٨﴾

48. Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?

مَا يَنظُرُونَ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً تَأْخُذُهُمْ وَهُمْ يَخِصِّمُونَ ﴿٤٩﴾

49. Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakaowachukua nao wanazozana.

فَلَا يَسْتَطِيعُونَ تَوْصِيَةً وَلَا إِلَىٰ أَهْلِهِمْ يَرْجِعُونَ ﴿٥٠﴾

50. Basi hawataweza kuusia, wala hawatarejea kwa watu wao.

وَنُفِخَ فِي الصُّورِ فَإِذَا هُم مِّنَ الْأَجْدَاثِ إِلَىٰ رَبِّهِمْ يَنسِلُونَ ﴿٥١﴾

51. Na itapulizwa Parapanda, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao.

قَالُوا يَا وَيْلَنَا مَن بَعَثَنَا مِن مَّرْقَدِنَا هَـٰذَا مَا وَعَدَ الرَّحْمَـٰنُ وَصَدَقَ الْمُرْسَلُونَ ﴿٥٢﴾

52. Watasema: Ole wetu! Nani aliyetufufua malaloni petu? Haya ndiyo aliyoyaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume.

إِن كَانَتْ إِلَّا صَيْحَةً وَاحِدَةً فَإِذَا هُمْ جَمِيعٌ لَّدَيْنَا مُحْضَرُونَ ﴿٥٣﴾

53. Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhuruishwa mbele yetu.

فَالْيَوْمَ لَا تُظْلَمُ نَفْسٌ شَيْئًا وَلَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ﴿٥٤﴾

54. Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyokuwa mkiyatenda.

OGOPENI YALIYO MBELE YENU

Aya 45 – 54

MAANA

Na wanapoambiwa: Ogopeni yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa.

Wanaoambiwa ni washirikina wa kiarabu. Makusudio ya yaliyo mbele yao ni kumuasi Mwenyezi Mungu na aliyoyaharamisha, na yaliyo nyuma yao ni adhabu ya hayo. Kwenye Nahjul-balagh imeelezwa: “Hakika Kiyama kimewazingira kwa nyuma yenu.” Maana ni kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewakataza kumuasi Mwenyezi Mungu na akwahadharisha na adhabu yake wakimuasi. Akawapa bishara ya rehema yake na thawabu zake wakimtii, lakini waligeuka nyuma.

Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao ila wao huwa ni wenye kuipuuza.

Kila alipowajia Mtume na muujiza wa dhahiri au hoja iliyo wazi, walimkadhibisha kwa jeuri na inadi. Umetangulia mfano wake katika Juz. 19 (26:5).

Na wanapoambiwa: Toeni katika aliyowapa Mwenyezi Mungu, waliokufuru huwaambia walioamini: Je! Tumlishe ambaye Mwenyezi Mungu angependa angelimlisha? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhahiri.

Wapenda anasa wana msingi na dini moja tu; kupupia utajiri wao na maslahi yao. Ndio mazungumzo yao na vitendo vyao. Wakiambiwa msifanye ufisadi, wanasema sisi ni watengenezaji. Wakiambiwa aminini kama walivyoamini watu, wanasema: Tuamini kama walivyoamini wapumbavu? Wakiambiwa msujudieni Mwingi wa rehema, wanasema: Ni nani huyo Mwingi wa rehema? Sisi tunasujudia pesa.

Na wakiamriwa kuwapatia wenye haja wanasema Mwenyezi Mungu amewahukumia kuwa mafukara na sisi tuwe matajiri. Hawajui au wamejitia kutojua kuwa ufukara unatokana na yanayofanywa ardhini sio yanayofanywa mbinguni; kama vile ufisadi, serikali za kidhalimu, za unayanyasaji na uporaji.

Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?

Mwenyezi Mungu na Mtume anapowahadharisha na mwisho mbaya, wanasema kwa dharau yatakuwa lini haya? Umetangulia mfano wake kati- ka Aya kadhaa.

Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakaowachukua nao wanazozana.

Yaani wakizozania mambo ya dunia yao. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu:

فَأَخَذْنَاهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ ﴿٩٥﴾

“Basi tuliwaachukua kwa ghafla hali hawatambui.” Juz. 9 (7:95).

Basi hawataweza kuusia, wala hawatarejea kwa watu wao.

Ukija ukelele wa adhabu hakuna yeyote atakayepata muda wa kuusia watu wake mambo muhimu, na akiwa mbali nao hataweza kurudi kwao.

Na itapulizwa Parapanda, mara watatoka makaburini wakikimbilia kwa Mola wao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (18:99).

Watasema: Ole wetu! Nani aliyetufufua malaloni petu?

Watastaajabu kwa kufufuliwa kwao baada ya mauti, na hapo mwanzo walikuwa wakimfanyia mzaha yule anayewaandalia na kuwamarisha kujianda nao. Baada ya kushuhudia watasema: Haya ndiyo aliyoyaahidi Mwingi wa Rehema na wakasema kweli Mitume kwamba Kiyama kitafika tu, bila ya shaka yoyote na kwamba Mwenyezi Mungu atawafufua walio makaburini.

Haitakuwa ila ukelele mmoja tu, mara wote watahudhurishwa mbele yetu.

Kuumba, mauti na ufufuo kwa Mwenyezi Mungu ni sawa, kunakuwa kwa neno moja tu:

مَّا خَلْقُكُمْ وَلَا بَعْثُكُمْ إِلَّا كَنَفْسٍ وَاحِدَةٍ ﴿٢٨﴾

“Hakukuwa kuumbwa kwenu wala kufufuliwa kwenu ila ni kama nafsi moja tu.” Juz. 21 (31:28).

Umetangulia mfano wake katika Aya 32 ya sura hii tuliyo nayo.

Basi leo nafsi yoyote haitadhulumiwa kitu, wala hamtalipwa ila yale mliyokuwa mkiyatenda.

Kauli nyingine yenye maana haya ni:

الْيَوْمَ تُجْزَىٰ كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ لَا ظُلْمَ الْيَوْمَ إِنَّ اللَّـهَ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴿١٧﴾

“Leo kila nafsi italipwa kwa iliyoyachuma. Hapana dhulma leo. Hakika Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kuhisabu” (40:17).

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini na Nne: Surat Saba. Imeshuka Makka. Ina Aya 54.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

الْحَمْدُ لِلَّـهِ الَّذِي لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَلَهُ الْحَمْدُ فِي الْآخِرَةِ وَهُوَ الْحَكِيمُ الْخَبِيرُ ﴿١﴾

1. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na sifa ni zake katika Akhera. Naye ni Mwenye hekima, Mwenye habari.

يَعْلَمُ مَا يَلِجُ فِي الْأَرْضِ وَمَا يَخْرُجُ مِنْهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ السَّمَاءِ وَمَا يَعْرُجُ فِيهَا وَهُوَ الرَّحِيمُ الْغَفُورُ ﴿٢﴾

2. Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo, na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda huko na Yeye ni Mwenye kurehemu, Mwingi wa maghufira.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَأْتِينَا السَّاعَةُ قُلْ بَلَىٰ وَرَبِّي لَتَأْتِيَنَّكُمْ عَالِمِ الْغَيْبِ لَا يَعْزُبُ عَنْهُ مِثْقَالُ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَلَا أَصْغَرُ مِن ذَٰلِكَ وَلَا أَكْبَرُ إِلَّا فِي كِتَابٍ مُّبِينٍ ﴿٣﴾

3. Na walisema wale ambao wamekufuru: Haitatufikia Saa. Sema: Ndio! Naapa kwa Mola wangu, itawafikia. Mjuzi wa ghaibu. Hapana kinachofichikana kwake hata chenye uzito wa chembe, si katika mbingu wala katika ardhi, wala kilicho kidogo katika hivyo wala kikubwa zaidi; ila vimo katika Kitabu chenye kubainisha.

لِّيَجْزِيَ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ لَهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ ﴿٤﴾

4. Ili awalipe wale ambao wameamini na wakatenda mema. Hao watapata maghufira na riziki yenye heshima.

وَالَّذِينَ سَعَوْا فِي آيَاتِنَا مُعَاجِزِينَ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ عَذَابٌ مِّن رِّجْزٍ أَلِيمٌ ﴿٥﴾

5. Na wale ambao wamehangaika kuzipinga ishara zetu wakiona watashinda, hao watapata adhabu mbaya yenye uchungu.

وَيَرَى الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ الَّذِي أُنزِلَ إِلَيْكَ مِن رَّبِّكَ هُوَ الْحَقَّ وَيَهْدِي إِلَىٰ صِرَاطِ الْعَزِيزِ الْحَمِيدِ ﴿٦﴾

6. Na wale ambao wamepewa ilimu wanaona kuwa uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako ni haki na huongoza kwenye njia ya Mwenye nguvu, Mwenye kusifiwa.

SIFA NJEMA ZOTE NI ZA MWENYEZI MUNGU

Aya 1 – 6

MAANA

Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na sifa ni zake katika Akhera. Naye ni Mwenye hekima, Mwenye habari.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye kustahiki kusifiwa kwa sifa njema katika nyumba mbili. Ni mmliki wa ulimwengu na mpangiliaji wake kwa vyote vilivyomo ndani yake, kulingana na elimu yake na hekima yake.

Kwenye Nahjul-Balagha, imesemwa: “Tunamsifu kwa ukubwa wa hisani yake na wema wa dalili yake na ziada ya fahila zake na neema zake. Sifa ambazo ni haki yake (sisi) kuzitekeleza na kulipa shukrani zake na kujikurubisha kwenye thawabu zake na kutaka ziada ya wema wake.”

Anayajua yanayoingia katika ardhi na yanayotoka humo na yanayoteremka kutoka mbinguni na yanayopanda huko na Yeye ni Mwenye kurehemu, Mwingi wa maghufira.

Maana ya Aya hii yamekaririka katika Aya kadhaa; ikiwemo Juz. 7 (6:59) na Juz. Juz. 11 (10:61). Ufupisho wake ni kuwa Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Na walisema wale ambao wamekufuru: Haitatufikia saa ya Kiyama. Sema: Ndio! Naapa kwa Mola wangu, itawafikia.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11(10:53).

Mjuzi wa ghaibu. Hapana kinachofichikana kwake hata chenye uzito wa chembe, si katika mbingu wala katika ardhi, wala kilicho kidogo katika hivyo wala kikubwa zaidi; ila vimo katika Kitabu chenye kubainisha.

Kitabu chenye kubainisha ni kinaya cha kuhifadhi. Maana ni kuwa hakuna anayejua wakati wa Kiyama isipokuwa Mwenyezi Mungu peke yake. Tazama Juz. 9 (7:187).

Ili awalipe wale ambao wameamini na wakatenda mema. Hao watapata maghufira na riziki yenye heshima. Na wale ambao wamehangaika kuzipinga ishara zetu wakiona watashinda, hao watapata adhabu mbaya yenye uchungu.

Huu ni ubainifu wa hekima ya ufufuo, ambayo ni kulipwa mema waliofanya wema na wale waliofanya uovu walipwe kwa uovu wao. Tazama Juz. 11 (10:3-4). Kifungu cha “Hisabu na malipo ni lazima.”

Na wale ambao wamepewa ilimu wanaona kuwa uliyoteremshiwa kutoka kwa Mola wako ni haki na huongoza kwenye njia ya Mwenye nguvu, Mwenye kusifiwa.

Makusudio ya wale waliopewa ilimu ni kila mwenye ilimu aliye na insafu, wakati wowote na mahali potepote. Na makusudio ya uliyoteremshiwa ni Qur’an. Maana ni kuwa yeyote mwenye ilimu atakayeisoma Qur’an kiusahihi, lazima ataishia kuwa ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu; kwa sababu iko sawasawa kwenye itikadi yake, sharia yake na mafunzo yake yote.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا هَلْ نَدُلُّكُمْ عَلَىٰ رَجُلٍ يُنَبِّئُكُمْ إِذَا مُزِّقْتُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ إِنَّكُمْ لَفِي خَلْقٍ جَدِيدٍ ﴿٧﴾

7. Na wale ambao wamekufuru walisema: Je, tuwajulishe mtu anayewaambia mtakapocham- buliwa mapande mapande mtakuwa katika umbo jipya?

أَفْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا أَم بِهِ جِنَّةٌ بَلِ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ فِي الْعَذَابِ وَالضَّلَالِ الْبَعِيدِ ﴿٨﴾

8. Amemzulia Mwenyezi Mungu au ana wazimu? Bali wale ambao hawaamini akhera wamo adhabuni na upotofu wa mbali.

أَفَلَمْ يَرَوْا إِلَىٰ مَا بَيْنَ أَيْدِيهِمْ وَمَا خَلْفَهُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِن نَّشَأْ نَخْسِفْ بِهِمُ الْأَرْضَ أَوْ نُسْقِطْ عَلَيْهِمْ كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً لِّكُلِّ عَبْدٍ مُّنِيبٍ ﴿٩﴾

9. Je, hawaoni yaliyo mbele yao na nyuma yao ya mbingu na ardhi. Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini, au tungeliwateremshia vipande vya mbingu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mja aliyetubia.

WANAOPINGA SIKU YA MWISHO

Aya 7 – 9

MAANA

Na wale ambao wamekufuru walisema: Je, tuwajulishe mtu anayewaambia mtakapochambuliwa mapande mapande mtakuwa katika umbo jipya? Amemzulia Mwenyezi Mungu au ana wazimu?

Hivi ndivyo washirikina walivyomwambia Muhammad, ni muongo au mwendawazimu – Mungu apishie mbali. Kwa nini walisema neno la ukafiri kama hilo? Ni Kwa sababu Mtume aliwaambia kuwa mtu atafu- fuliwa baada ya mauti. Hawana dalili yoyote ya kupinga kwao huku isipokuwa kushangaa tu; kama walivyosema:

أَجَعَلَ الْآلِهَةَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا إِنَّ هَـٰذَا لَشَيْءٌ عُجَابٌ ﴿٥﴾

“Amewafanya miungu wote kuwa ni mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu.” (38: 5).

Hali yao hii, kama inavyonekana, inategemea vile wanavyofikiria. Maana yake ni kupinga hali halisi kwa fikra na mawazo; pamoja na kuwa fikra haiwi ya kweli ila ikiwa inaakisi hali halisi na kwamba yeyote anayeikum- batia nadharia yoyote hana budi kutafuta dalili ya ukweli wake kwa kuweko uhalisi unaoitafsiri, na haifai kukana uhalisi kwa fikra isiyokuwa na msingi wowote.

Katika hili Imam Ali(a.s) anaashiria kwa kusema:“Watu wanajulikana kwa haki, wala haki haijulikani kwa watu.”

Bali wale ambao hawaamini akhera wamo adhabuni na upotofu wa mbali.

Hao ni wajinga na wapotevu, kwa sababu wameipima haki na uhalisi kwa fikra zao na mawazo yao; na walitakiwa wapime fikra zao kwa haki na uhalisi.

Je, hawaoni yaliyo mbele yao na nyuma yao ya mbingu na ardhi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawaambia wakadhibishaji: Kuna ajabu gani ya kufufuliwa kwenu baada ya mauti:

أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُم ﴿٨١﴾

“Kwani aliyeziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao?” (36:81).

Je, umbile hili halifahamishi umoja wake na ukamilifu wa uweza wake; ukiwemo kuwarudisha watu baada ya mauti?

Tumelizungumzia hilo mara nyingi. Tazama Juz. 1 (2:28 -29), Juz. 5 (4:85 – 87) na Juz. 11 (10:3–4).

Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini, au tungeliwateremshia vipande vya mbingu. Hakika katika hayo kuna ishara kwa kila mja aliyetubia.

Hayo ni ishara ya kuumba mbingu na ardhi. Kwa sabubu hilo, kwa mwenye akili, linafahamisha ukuu wa Mwenyezi Mungu na uweza wake wa kuipa uhai mifupa iliyochakafuka. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu:

‘Tungelipenda tungeliwadidimiza ardhini,’ ni karipio na makemeo kwa yule anayepinga siku ya mwisho, kwamba anaweza kumezwa na ardhi au kupigwa na kimondo kutoka mbinguni, kimuunguze.

وَلَقَدْ آتَيْنَا دَاوُودَ مِنَّا فَضْلًا يَا جِبَالُ أَوِّبِي مَعَهُ وَالطَّيْرَ وَأَلَنَّا لَهُ الْحَدِيدَ ﴿١٠﴾

10. Na kwa hakika tulimpa Daud fadhila kutoka kwetu. Enyi milima sabihini pamoja naye na ndege. Na tukamlainishia chuma.

أَنِ اعْمَلْ سَابِغَاتٍ وَقَدِّرْ فِي السَّرْدِ وَاعْمَلُوا صَالِحًا إِنِّي بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿١١﴾

11. Kwamba utengeneze nguo za chuma pana na kadiria sawa katika kuunganisha. Na tendeni mema. Hakika ninayaona mnayotenda.

وَلِسُلَيْمَانَ الرِّيحَ غُدُوُّهَا شَهْرٌ وَرَوَاحُهَا شَهْرٌ وَأَسَلْنَا لَهُ عَيْنَ الْقِطْرِ وَمِنَ الْجِنِّ مَن يَعْمَلُ بَيْنَ يَدَيْهِ بِإِذْنِ رَبِّهِ وَمَن يَزِغْ مِنْهُمْ عَنْ أَمْرِنَا نُذِقْهُ مِنْ عَذَابِ السَّعِيرِ ﴿١٢﴾

12. Na kwa Suleiman upepo. Safari yake ya asubuhi ni mwendo wa mwezi mmoja na safari yake ya jioni ni mwendo wa mwezi mmoja. Na tukamtiririshia chemchem ya shaba. Na katika majini kuna waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mola wake. Na anayejitenga na amri katika wao tunamwonjesha adhabu ya moto unaowaka.

يَعْمَلُونَ لَهُ مَا يَشَاءُ مِن مَّحَارِيبَ وَتَمَاثِيلَ وَجِفَانٍ كَالْجَوَابِ وَقُدُورٍ رَّاسِيَاتٍ اعْمَلُوا آلَ دَاوُودَ شُكْرًا وَقَلِيلٌ مِّنْ عِبَادِيَ الشَّكُورُ ﴿١٣﴾

13. Wakimfanyia alipendalo, kama mihrabu na masanamu na sinia kubwa kama mahodhi, na masufuria makubwa yasiyoondoka mahali pake. Fanyeni amali enyi watu wa Daud kwa kushukuru. Ni wachache katika waja wangu wanaoshukuru.

فَلَمَّا قَضَيْنَا عَلَيْهِ الْمَوْتَ مَا دَلَّهُمْ عَلَىٰ مَوْتِهِ إِلَّا دَابَّةُ الْأَرْضِ تَأْكُلُ مِنسَأَتَهُ فَلَمَّا خَرَّ تَبَيَّنَتِ الْجِنُّ أَن لَّوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ الْغَيْبَ مَا لَبِثُوا فِي الْعَذَابِ الْمُهِينِ ﴿١٤﴾

14. Tulipomkidhia mauti, hapana aliyewajulisha mauti yake ila mnyama wa ardhi aliyekula fimbo yake. Alipoanguka majini walitambua lau kuwa wangelijua ya ghaibu wasingelikaa katika adhabu ya kufedhehesha.

DAUD NA SULEIMAN

Aya 10 – 14

MAANA

Na kwa hakika tulimpa Daud fadhila kutoka kwetu. Enyi milima sabihini pamoja naye na ndege. Na tukamlainishia chuma.

Katika Juz. 6 (4:163) Mwenyezi Mungu anasema: “Na Daud tukamapa Zaburi,” kwenye Juz. 19 (27:15) anasema: “Na hakika tulimpa Daud na Suleiman elimu” na kwenye Aya hii tuliyo nayo anaseama kuwa amempa neema ya sauti nzuri ambayo ilikuwa inakurubia kwenda sambamba na sauti ya milima na ndege.

Katika Juz. 17 (21:79) tulisema kuwa inawezekana kuwa tasbihi ya milima na ndege ni tasbihi halisi hasa pamoja na Daud, Kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu. Kuna msemaji aliyesema kuwa makusudio ya kusabihi milima na ndege pamoja na Suleimani ni kuwa ilikuwa ikimfanya asabihi; alipokuwa akiiona husema: “Subhana man khalaqa wa swawwara...” (Kutakasika ni kwa aliyeumba na akatia sura...).

Pia Mwenyezi Mungu alimneeemesha Daud kwa kukifanya chuma vile anavyotaka yeye bila ya kukitia motoni au kukigonga na nyundo. Inawezekana kuwa Mwenyezi Mungu alimfahamisha sababu na nyenzo za kukilainisha chuma.

Kwamba utengeneze nguo za chuma pana na kadiria sawa katika kuunganisha.

Mwenyezi Mungu Mtukufu anamwambia Daud atengeneze deraya kutokana na chuma na atengeneze vizuri kuzuia panga mishale na mikuki na ziwe pana kwa namna ambayo mvaaji haitamzuia na harakati zozote.

Na tendeni mema. Hakika ninayaona mnayotenda.

Maneno yanaelekezwa kwa Daud na kizazi chake. Mwenyezi Mungu anawaamrisha wafanye mema na kuwa ameayaandalia malipo na thawabu. Umetangulia mfano wa Aya mbili hizi katika Juz. 17 (21:79 – 80).

Na kwa Suleiman upepo. Safari yake ya asubuhi ni mwendo wa mwezi mmoja na safari yake ya jioni ni mwendo wa mwezi mmoja.

Dhahiri ya Aya inaonyesha kuwa upepo ulikuwa ukimchukua Suleiman, anakotaka, kwa amri ya Mungu na kwamba masafa ya mwezi mzima kwa ngamia au kutembea kwa miguu alikuwa akienda kwa asubuhi moja na vile vile jioni.

Na tukamtiririshia chemchemi ya shaba.

Makusudio ya kumtiririshia hapa ni kumyeyushia. Yaani Mwenyezi Mungu Mtukufu alimyeyushia chuma Suleimani kama alivyomyeyushia baba yake Daud. Inawezekana kuwa Mwenyezi Mungu alimuongoza kwenye sababu za kuyeyusha.

Na katika majini kuna waliofanya kazi mbele yake kwa idhini ya Mola wake. Na anayejitenga na amri katika wao tunamwonjesha adhabu ya moto unaowaka. Wakimfanyia alipendalo, kama mihrabu na masanamu na sinia kubwa kama mahodhi, na masufuria makubwa yasiyoondoka mahali pake.

Imetangulia pamoja na tafsiri yake katika Juz. 17 (21:82).

Fanyeni amali enyi watu wa Daud kwa kushukuru. Ni wachache katika waja wangu wanaoshukuru.

Ibn Al-arabi ameitaja Aya hii katika Futuhat Juz. 4, akasema: Shukrani ni kuiona neema kuwa imetoka kwa Mungu si kwa mwingine. Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimpa wahyi Musa akamwambia: Nishukuru kwa haki ya kushukuru. Akasema Musa: “Ni nani anayeweza hilo ewe Mola?” Akamwambia: “Ikiwa unaona neema imetokana na mimi basi umenishukuru.”

Tulipomkidhia mauti, hapana aliyewajulisha mauti yake ila mnyama wa ardhi aliyekula fimbo yake. Alipoanguka majini walitambua lau kuwa wangelijua ya ghaibu wasingelikaa katika adhabu ya kufedhehesha.

Aliyekidhiwa na mauti ni Suleiman. Mnyama wa ardhi ni mchwa anayekula miti. Maana ni kuwa Suleimani alifikiwa na mauti akiwa ameegemea fimbo yake; akabakia hivyo mpaka muda aliotaka Mwenyezi Mungu, majini na watu wakimwangalia na kumdhania kuwa yuko hai, mpaka pale mchwa walipokula fimbo yake kwa ndani, ikavunjika na Suleiman akaanguka; hapo wote wakajua kuwa amekufa; ikadhihirika kwa watu kuwa majini hawajui ghaibu. Kwa sababu lau wangelijua basi wasingelikuwa katika utumishi wa Suleiman akiwa ni maiti.

Ikiwa baadhi ya yaliyo katika Aya hii yanaonekana, kwa kawaida, ni vigumu kutokea, lakini kiakili inakubalika kutokea. Ndio maana tunayasadiki na kuyakubali; tukiwa tunaamini msingi wa wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwenda kwa Mtume(s.a.w. w ) wake mtukufu.

Tazama Juz. 3 (3:45 – 51) kifungu cha “Lisilowezekana kiakili na kidesturi.”

KUPINGA FIKRA YA KIDINI

Kutoka na kutajwa majini na mambo yasiyo ya kawaida katika Aya hii, ni vizuri tutaje yaliyoelezwa kwenye kitabu kilichotoka hivi karibuni, kina- choitwa Naqdu lfikri ddiniy. (Kupinga fikra ya kidini).

Hivi sasa tuko katika mwezi wa Novemba 1969. Yamezungumzwa mengi kuhusu kitabu hicho na mtungaji wake. Mwenye kusoma kitabu hicho mara moja atamhukumu mtungaji wake kuwa ana shaka na wasiwasi na dini zote. Hilo amelisema waziwazi kwenye Uk. 29, 77 na nyinginezo.

Lakini mwenye kukifuatilia kitabu na kuchukua dhahiri yake, ataona kuwa yaliyopelekea shaka na wasiwasi huu ni mambo yafutayo:

Kwanza : Kujaribu baadhi ya waumini kulazimisha kuoanisha nukuu za Qur’an na ugunduzi wa kisayansi, na kuzama sana kuleta taawili iliyo mbali na matamshi. Mtunzi wa kitabu hicho amelitolea ushahidi mwingi hilo, yakiwemo yale aliyoyanukuu katika Uk. 37, kwamba ugunduzi wa chembe za mwanga unafahamisha kuweko malaika na majini.

Mtungaji akielezea kauli hii alisema: “Sijui kuna uhusiano gani baina ya nadharia ya mwanga na kuweko majini.”

Pili : Mazoweya na nembo za kidini zilizoganda haziendani na maendeleo ya karne ya ishirini; kama anavyodai mwandishi.

Tatu: Baadhi ya wakuu wa dini kuunga mkono ukabaila na ukoloni kwa kutumia jina na Uislamu au Ukristo. Kitabu kimejaa ushahidi wa hilo; kama vile kwenye uk. 23: “Dini huko ulaya ilikuwa rafiki mkubwa wa serikali za kikabaila, hali ambayo inaendelea hadi sasa katika miji mbalimbali, hasa ndani ya miji ya kiarabu na nje, na vile dini inavyoungana moja kwa moja na ukoloni mambo leo unaongozwa na Marekani.”

Mtungaji aliongeza katika kupinga kitabu “Almasihiyya wal Islamu fi Lubnan” (Ukiristo na Uislmu Lebanon) ambacho ni mkusanyiko wa mihadhara ya Lebanon ya mwaka 1965, iliyotolewa na wakuu wa kidini wane: mmoja wa kisunni, mwengine wa kishia na wawili wa kikiristo.

Na wengine wane wa wasiokuwa na dini yoyote, lakini walizungungumza kwa niaba ya dini. Wote wakamwahidi Mwenyezi Mungu kuwa watafanya bidii ya kudumu kuondoa pingamizi zinazowekwa baina ya Uislamu na ukiristo.

Miongoni mwa aliyoyasema mtungaji huyu, katika kuwarudi wale waliotoa ahadi, ni yale yaliyo katika ukurasa wa 64, wa Kitabu chake hicho: “Lengo la kwanza la mihadhara na ahadi hizo ni wakristo kuunga mkono serkali ya Lebanon, kwa vile inawanufaisha wao zaidi kuliko waislamu walio na ufukara sana.

Baadhi ya waislamu nao wanaikubali serikali na kuungana na wakiristo, na kuaiachia serikali usimamizi wote wa kisiasa, kijamii na kiuchumi, si kwa lolote ila ni kwa kuwa wanapata manufaa fulani na faida kutoka serikalini. Kiasi ambacho maovu ya serikali yamesahaulika na kuelekea kwenye nembo ya mshikamano wa wakiristo na waislamu.”

Dalili mkataa kuwa malengo ni masilahi sio mshikamano wa kidini, mwandishi anaiweka wazi kwenye Uk. 60, katika kitabu chake, akisema: “Hakika Uislamu hauikubali Biblia, utatu, mhanga, kusulubiwa Bwana Masih, kuzikwa kwake na kutoka kwake kaburini n.k. Kama ambavyo wakiristo nao hawaikubali Qur’an wala utume wa Muhammad(s.a.w. w ) n.k. Sasa hawa wahadhiri na ahadi zao wataondoa vipi pingamizi hizi? Usawa hasa ni kufahamiana na kuelewena Walebanoni kwa uzalendo wao tu na misingi ya ushirikiano kwa masilahi yao, lakini dini aachiwe hiyari kila mtu kulingana na alivyokinai na mazoweya yake.”

Kutokana na kauli ya mwandishi huyu na wengineo wengi, katika kupinga fikra ya dini, inatubainikia kuwa siri ya upinzani wao, kama tulivyodokeza mwanzoni, imetokana na wakuu wa dini kuukumbatia ukoloni, udhalimu na ukandamizaji na kuupamba kwa jina la dini.

Lau wakuu wote wa dini wangeifanyia ikhlasi, wakaifahamisha kwa ufahamu sahihi na wakaibanisha kama alivyoiteremsha Isa na Muhammad na wasiiuze kwa thamani ndogo, basi wapinzani au washambulizi wa kulipwa wasingelipata mwanya wa kuituhumu au kuwa na shaka na dini ya kiislamu wala ya kikiristo.

Lakini jambo la kuvunja moyo ni kuwa watu wamelitumia jina la dini kwa uzushi na wengine wakasimama kuiharibu na kuingiza shaka baada ya kulipwa na maadui wa Mwenyezi Mungu; ndio ikawa radiamali hii kuto- ka kwa mwandishi huyu wa kitabu ‘Kupinga fikra ya dini’ na wengineo. Inasemekana pia mwandishi huyu ni katika wanaolipwa.

Hata hivyo, kwani dini itakuwa imekosea nini ikituhumiwa na wazushi na wenye upendeleo? Ilitakikana mwandishi aangalie ushahidi mwingi ulio katika Kitabu cha Mwenyezi Mungu na suna za Mtume wake na pia katika historia ya Uislamu kuwa dini ni nguvu inayomwelekeza mtu kwenye maisha bora na kwamaba iko mbali na kila jambo lisiloingilika akilini na kugongana na hakika ya maisha.

Hakika hii wanakubaliana nayo wataalamu wengi wa mashariki na wa magharibi wasiokuwa waislamu. Tazama Juz. 1 (2:1-5) kifungu cha ‘Qur’an na Sayansi,’ Juz. 9 (8:24) kifungu cha ‘Dini na maisha,’ na Juz. 15 (17:9-12) kifungu cha ‘Uislamu ni dini ya maumbile.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

لَقَدْ كَانَ لِسَبَإٍ فِي مَسْكَنِهِمْ آيَةٌ جَنَّتَانِ عَن يَمِينٍ وَشِمَالٍ كُلُوا مِن رِّزْقِ رَبِّكُمْ وَاشْكُرُوا لَهُ بَلْدَةٌ طَيِّبَةٌ وَرَبٌّ غَفُورٌ ﴿١٥﴾

15. Hakika ilikuwa ishara kwa wasabaa katika maskani yaobustani mbili, kulia na kushoto. Kuleni katika riziki ya Mola wenu na mumshukuru. Mji mzuri na Mola mwenye maghufira.

فَأَعْرَضُوا فَأَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ سَيْلَ الْعَرِمِ وَبَدَّلْنَاهُم بِجَنَّتَيْهِمْ جَنَّتَيْنِ ذَوَاتَيْ أُكُلٍ خَمْطٍ وَأَثْلٍ وَشَيْءٍ مِّن سِدْرٍ قَلِيلٍ ﴿١٦﴾

16. Lakini wakaacha, basi tukawapelekea mafuriko makubwa na tukawabadilishia bustani zao kwa bustani nyingine mbili zenye matunda makali na mivinje na miti michache ya kunazi.

ذَٰلِكَ جَزَيْنَاهُم بِمَا كَفَرُوا وَهَلْ نُجَازِي إِلَّا الْكَفُورَ ﴿١٧﴾

17. Hayo tuliwalipa kwa vile walikufuru, nasi kwani tunamwadhibu isipokuwa anayekufuru?

وَجَعَلْنَا بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ الْقُرَى الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا قُرًى ظَاهِرَةً وَقَدَّرْنَا فِيهَا السَّيْرَ سِيرُوا فِيهَا لَيَالِيَ وَأَيَّامًا آمِنِينَ ﴿١٨﴾

18. Na baina yao na miji mingine tuliyoibariki, tuliweka miji iliyo dhahiri na tukaweka humo vituo vya safari: Nendeni humo usiku na mchana kwa amani.

فَقَالُوا رَبَّنَا بَاعِدْ بَيْنَ أَسْفَارِنَا وَظَلَمُوا أَنفُسَهُمْ فَجَعَلْنَاهُمْ أَحَادِيثَ وَمَزَّقْنَاهُمْ كُلَّ مُمَزَّقٍ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّكُلِّ صَبَّارٍ شَكُورٍ ﴿١٩﴾

19. Wakasema: Mola wetu, weka mwendo mrefu baina ya safari zetu. Na wakazidhulumu nafsi zao. Basi tukawafanya ni masimulizi na tukawatawanyatawanya. Hakika katika hayo, bila shaka kuna ishara kwa kila aliye na subira sana mwenye kushukuru.

وَلَقَدْ صَدَّقَ عَلَيْهِمْ إِبْلِيسُ ظَنَّهُ فَاتَّبَعُوهُ إِلَّا فَرِيقًا مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢٠﴾

20. Na hakika Ibilisi alisadikisha dhana yake juu yao. Na walimfuata isipokuwa kundi la waumini.

وَمَا كَانَ لَهُ عَلَيْهِم مِّن سُلْطَانٍ إِلَّا لِنَعْلَمَ مَن يُؤْمِنُ بِالْآخِرَةِ مِمَّنْ هُوَ مِنْهَا فِي شَكٍّ وَرَبُّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ حَفِيظٌ ﴿٢١﴾

21. Naye hakuwa na mamlaka yoyote juu yao, ila ni kwa sababu tujue ni nani mwenye kuamini Akhera na nani anayetilia shaka. Na Mola wako ni mwenye kuhifadhi kila kitu.

SABAA

Aya 15 – 21

LUGHA

Sabaa ni jina la kabila la waarabu, lililotokana na jina la baba ambaye kizazi chao kinatokana naye.

KISA KWA UFUPI

Katika Tarikh almas’ud imeelezwa kuwa mfalme wa kwanza wa Yemen alikuwa ni Sabaa bin Yashjab bin Ya’arab bin Qahtan. Jina lake hasa lilikuwa ni Abdu Shams. Aliitwa Sabaa kutokana na kuchukua kwake mateka[2] . Ardhi ya Sabaa ilikuwa ndio ardhi yenye rutuba na utajiri zaidi katika Yemen.

Kabla yake, ardhi hiyo, ilikuwa ikikumbwa na mafuriko yaliyoangamiza mimea na majengo. Basi akawakusanya wataalamu wa zama hizo kutafuta suluhisho la tatizo hilo. Wakaafikiana kujengwe ukuta baina ya milima miwili na kuweka mlango wa kuyafungulia maji kwa kiasi wanachokitaka.

Ukuta huu ulijulikana kwa jina la mji wa Maaribu uliokuwa karibu na ukuta. Kadiri siku zilivyoendelea kupita ndivyo maji nayo yalivyoongezeka, ukuta ukaharibika na maji yakavunja majumba na mashamba. Watu wakagura na wakatawanyika sehemu kadhaa za nchi. Hapa ndipo ilipochukuliwa mithali: ‘Mikono ya sabaa imetawanyika.’

Katika Tafsir At-Tabari na Majmaul-Bayan imeelezwa kuwa mtu mmoja alimuuliza Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) kuhusu Sabaa, akasema: ‘Kulikuwa na mtu mmoja mwarabu aliyekuwa na watoto kumi, sita katika wao walikwenda upande wa Yemen na wane wakaenda upande wa Sham.

Waliokwenda upande wa Yemen ni: Kinda, Himyar, Azd, Ash’ar, Madh-hij na Anmar, miongoni mwao ni Khath’am na Bujayla. Ama wale waliokwenda upande wa Sham ni: Amila, Judham, Lakhmu na Ghassan.

Katika Tafsir Al-Ma raghi imeelezwa kuwa watafiti walikuwa wakitilia shaka jambo hili la ukuta, mpaka mgunduzi wa kifaransa Arno alipoweza kufika Maarib mnamo mwaka 1843 na akaona athari yake na kuweza kuchora picha iliyosambazwa kwenye magazeti ya ufaransa mwaka 1874. Baadaye Halevi na Glazr, wakatembelea sehemu hiyo, wakaafikiana na aliyoyasema.

MAANA

Hakika ilikuwa ishara kwa wasabaa katika maskani yaobustani mbili, kulia na kushoto. Kuleni katika riziki ya Mola wenu na mumshukuru. Mji mzuri na Mola mwenye maghufira.

Ishara ni dalili na alama ya neema za Mwenyezi Mungu zilizo nyingi katika mji huo. Bustani mbili kulia na kushoto, ni kinaya cha rutuba na mazao mengi yaliyopatikana kila pembe ya mji huo. Kila aliyepita ardhi ya Sabaa aliweza kuona mazao mengi kulia na kushoto.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaamrisha watu wa Sabaa, kupitia kwa manabii na Mitume wake, kuwa waneemeke na kheri zake na wamshukuru na wampwekeshe.

Lakini wakaacha, basi tukawapelekea mafuriko makubwa na tukawabadilishia bustani zao kwa bustani nyingine mbili zenye matunda makali na mivinje na miti michache ya mikunazi.

Neema ya Mwenyezi Mungu waliitumia kwa kumuuasi. Akawahadharisha kupitia Mitume wake, lakini halikuwafaa onyo wala kuzingatia mawaidha. Basi Mwenyezi Mungu akawapelekea mafuriko yaliyobomoa ukuta na kuharibu mimea. Mwenyezi Mungu akabadilisha bustani za matunda na konde za mazao kwa miti isiyoshibisha; kama vile: mikwaju, mikunazi na mingineyo inayomea jangwani ambayo wanakula wanyama wenye njaa au mtu aliyeishiwa kabisa.

Hayo tuliwalipa kwa vile walikufuru, nasi kwani tunamwadhibu isipokuwa anayekufuru?

Aliwalipa ufukara, ambao ni malipo ya kufedhehesha zaidi. Kuna Hadith isemayo: “Ufukara unakurubia kuwa ni ukafiri.” Nyingine inasema: “Ufukara unasawijisha uso duniani na akhera.” Imam Ali(a.s) alimwambia mwanawe Muhammad Al-Hanafiya: “Hakika ufukara unapunguza dini –yaani unampeleka mtu kumwasi Mwenyezi Mungu – unazubaisha akili na unaita mateso.”

Na baina yao na miji mingine tuliyoibariki, tuliweka miji iliyo dhahiri na tukaweka humo vituo vya safari: Nendeni humo usiku na mchana kwa amani.

Baina yao ni watu wa Sabaa. Makusudio ya miji ni Sham – kama walivyosema wafasiri-ambao Mwenyezi Mungu aliubariki kwa maji, miti, rutuba na matunda. Iliyodhahiri maana yake ni kuwa karibu ikijitokeza na kuonana.

Kuweka vituo vya safari baina ya mji mmoja na mwengine; kiasi ambacho msafiri anakuwa kwenye mji mmoja asubuhi na jioni anakuwa kwenye mji mwingine. Aya inausifia mji wa Sabaa kabla ya kuharibika. Maana yake ni kuwa miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu na fadhila zake ni kuwa anayetaka kusafiri anakuwa kwenye amani ya nafsi yake na mali yake na hakuwa na haja ya kuchukua masurufu ya safari au kuhofia kiu wala njaa.

Lakini wakachoka na neema wakasema: Mola wetu weka mwendo mrefu baina ya safari zetu.

Yaani weka mbuga na nyika ili tutafute usafiri na tuchukue masurufu ya safari; sawa na walivyofanya wana wa israil walipochoka na Manna na Salwa na kumwambia Musa: “Basi tuombee

Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi miongoni mwa mboga zake, na matango yake na ngano yake na adesi zake na vitunguu vyake. Akasema: ‘Mnabadili vitu duni kwa vile vilivyo bora?” Juz.1(2:61).

Na wakazidhulumu nafsi zao kwa kupituka mipaka na kukufuru neema. Basi tukawafanya ni masimulizi na tukawatawanyatawanya. Hakika katika hayo, bila shaka kuna ishara kwa kila aliye na subira sana mwenye kushukuru.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwatawanya ardhini mpaka wakawa ni historia kwa vizazi na mazingatio kwa mwenye kuvumilia shida na akushukuru wakati wa raha.

Na hakika Ibilisi alisadikisha dhana yake juu yao. Na walimfuata isipokuwa kundi la waumini. Naye hakuwa na mamlaka yoyote juu yao.

Shetani aliwahadaa wamuasi Mwenyezi Mungu; wakamsikiliza na kumtii wale waliopetuka mipaka na kukufuru na wakamwasi wale walioamini na kuwa na takua. Aya hii inaashiria kauli ya Ibilisi aliposema:

وَلَأُغْوِيَنَّهُمْ أَجْمَعِينَ ﴿٣٩﴾ إِلَّا عِبَادَكَ مِنْهُمُ الْمُخْلَصِينَ ﴿٤٠﴾ قَالَ هَـٰذَا صِرَاطٌ عَلَيَّ مُسْتَقِيمٌ ﴿٤١﴾ إِنَّ عِبَادِي لَيْسَ لَكَ عَلَيْهِمْ سُلْطَانٌ إِلَّا مَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْغَاوِينَ ﴿٤٢﴾

“Na nitawapoteza wote; isipokuwa waja wako waliosafishwa. Akasema (Mwenyezi Mungu): Hii ni njia juu yangu mimi iliyonyooka. Hakika waja wangu hutakuwa na mamlaka nao, isipokuwa wale wapotofu waliokufua- ta.” Juz. 14 (15:39 – 42).

Ila ni kwa sababu tujue ni nani mwenye kuamini Akhera na nani anayetilia shaka.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawajua zaidi waja wake kuliko wao wenyewe, lakini anawajaribu kwa raha na dhiki na kwa matamanio na hawaa, ili awadhihirishe ulimwenguni na yaonekane makusudio yao na vitendo vyao ambavyo vinastahiki thawabu na adhabu.

Maana ya Aya hii yamekaririka mara nyingi, ikiwemo Juz. 4 (3: 140).

Na Mola wako ni mwenye kuhifadhi kila kitu.

Hakimpotei chochote kilichomo mbinguni wala ardhini. Kuna Hadith isemayo: “Mche Mwenyezi Mungu kama kwamba wewe unamuona; ukiwa humuoni basi Yeye anakuona.”

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِ اللَّـهِ لَا يَمْلِكُونَ مِثْقَالَ ذَرَّةٍ فِي السَّمَاوَاتِ وَلَا فِي الْأَرْضِ وَمَا لَهُمْ فِيهِمَا مِن شِرْكٍ وَمَا لَهُ مِنْهُم مِّن ظَهِيرٍ ﴿٢٢﴾

22. Sema: Waombeni hao mnaodai kuwa ni badala ya Mwenyezi Mungu. Hawamiliki hata chembe katika mbingu wala ardhini. Wala hawana ushirika wowote humo. Wala hawana msaidizi miongoni mwao.

وَلَا تَنفَعُ الشَّفَاعَةُ عِندَهُ إِلَّا لِمَنْ أَذِنَ لَهُ حَتَّىٰ إِذَا فُزِّعَ عَن قُلُوبِهِمْ قَالُوا مَاذَا قَالَ رَبُّكُمْ قَالُوا الْحَقَّ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْكَبِيرُ ﴿٢٣﴾

23. Wala hautafaa uombezi mbele yake ila kwa yule aliyempa idhini. Hata itakapoondolewa fazaa kwenye nyoyo zao, watasema: Kasema nini Mola wenu? Watasema: Haki, naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ وَإِنَّا أَوْ إِيَّاكُمْ لَعَلَىٰ هُدًى أَوْ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٢٤﴾

24. Sema: Ni nani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini? Sema, ni Mwenyezi Mungu! Na hakika sisi au nyinyi bila shaka tuko kwenye uongofu au upotofu ulio wazi.

قُل لَّا تُسْأَلُونَ عَمَّا أَجْرَمْنَا وَلَا نُسْأَلُ عَمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢٥﴾

25. Sema: Nyinyi hamtaulizwa kwa makosa tuliyoyafanya wala sisi hatutaulizwa kwa mnayoyatenda.

قُلْ يَجْمَعُ بَيْنَنَا رَبُّنَا ثُمَّ يَفْتَحُ بَيْنَنَا بِالْحَقِّ وَهُوَ الْفَتَّاحُ الْعَلِيمُ ﴿٢٦﴾

26. Sema: Mola wetu atatukusanya kisha atatuhukumu kwa haki, naye ndiye Hakimu, Mjuzi.

قُلْ أَرُونِيَ الَّذِينَ أَلْحَقْتُم بِهِ شُرَكَاءَ كَلَّا بَلْ هُوَ اللَّـهُ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٢٧﴾

27. Sema: Nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika. Hapana! Bali Yeye ni Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا كَافَّةً لِّلنَّاسِ بَشِيرًا وَنَذِيرًا وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٢٨﴾

28. Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mtoaji bishara na muonyaji, lakini watu wengi hawajui.

وَيَقُولُونَ مَتَىٰ هَـٰذَا الْوَعْدُ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٢٩﴾

29. Na wanasema: Ni lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?

قُل لَّكُم مِّيعَادُ يَوْمٍ لَّا تَسْتَأْخِرُونَ عَنْهُ سَاعَةً وَلَا تَسْتَقْدِمُونَ ﴿٣٠﴾

30. Sema: Mna miadi ya siku ambayo hamtaakhirisha saa wala hamtaitangulia.

SEMA WAITENI MNAODAI KUWA NI WAUNGU

Aya 22 – 30

MAANA

Sema: Waombeni hao mnaodai kuwa ni badala ya Mwenyezi Mungu.

Washirikina waliabudu Malaika na masanamu, Mtume(s.a.w. w ) akawakataza lakini hawakusikia, akawaambia kwa amri ya Mwenyezi Mungu: iko wapi dalili ya mnaowafanya kuwa ni miungu? Waombeni manufaa au kukinga madhara, muone kuwa wanasikia na kuwajibu?

Lengo la matakwa haya ni kusimamisha hoja isiyoshindwa. Ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا ﴿٥٦﴾

“Sema:“Waombeni hao mnaodai badala Yake hawawezi kuwaondolea madhara wala kuyabadilisha.” Juz. 25 (17:56).

Hawamiliki hata chembe katika mbingu wala ardhini. Wala hawana ushirika wowote humo. Wala hawana msaidizi miongoni mwao.

Maneno yanaelekezwa kwa washirikina. Hata chembe ni kinaya cha kuwa hawamiliki hata kitu kilicho kidogo na duni. Maana ni kuwa hana mshirika wala msaidizi.

Wala hautafaa uombezi mbele yake ila kwa yule aliyempa idhini.

Hii ni kuwarudi washirikina na kauli yao:

مَا نَعْبُدُهُمْ إِلَّا لِيُقَرِّبُونَا إِلَى اللَّـهِ زُلْفَىٰ ...﴿٣﴾

“Hatuwaabudu ila wapate kutujongeza tu kumkaribia Mwenyezi Mungu.” (39:3).

Kwa maelezo zaidi Tazama Juz. 1 (47 – 48) kifungu cha ‘Shufaa.’

Hata itakapoondolewa fazaa kwenye nyoyo zao, watasema: Kasema nini Mola wenu? Watasema: Haki, naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

Wafasiri wametofautiana kuhusu watakaoondolewa fazaa, watakaouliza na wataoulizwa.

Kauli yenye nguvu zaidi ni watakaoondolewa fazaa ni wote walioko mbinguni na ardhini; kwamba fazaa itawaenea wote isipokuwa atakaowataka Mwenyezi Mungu; kama ilivyoelezwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu:

وَيَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَفَزِعَ مَن فِي السَّمَاوَاتِ وَمَن فِي الْأَرْضِ إِلَّا مَن شَاءَ اللَّـهُ وَكُلٌّ أَتَوْهُ دَاخِرِينَ ﴿٨٧﴾

“Na siku itakapopuziwa parapanda, watafazaika waliomo mbinguni na waliomo ardhini, ila amtakaye Mwenyezi Mungu. Na wote watamfikia hali ya kuwa ni wanyonge.” Juz. 20 (27:87).

Mara kwa mara tumesema kuwa Qur’an inajifasiri yenyewe. Kwa hiyo maana yanakuwa kwamba wakati wa Kiyama, wa mbinguni na wa ardhini watagawanyika mafungu mawili: Kuna kundi litakalokuwa na fazaa kubwa na kundi jingine litakuwa na amani. Hawa ndio walioashiriwa na kauli ya Mwenyezi Mungu: “Ila amtakaye Mwenyezi Mungu.” Kundi la kwanza ikitulia fazaa yake, watauliza kundil la pili: Mola wenu amesema nini na mwisho wetu ni upi? Watakoulizwa watajibu kuwa Mwenyezi Mungu amesema haki naye ndiye aliye juu, Mkubwa.

Jibu hili kwa ujumla linaashiria kuwa Mwenyezi Mungu hana mshirika wala msaidizi. Pia hakuna atakayeombea kwake isipokuwa aliyempa idhini.

Sema: Ni nani anayewaruzuku kutoka mbinguni na ardhini?

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume(s.a.w. w ) awaambie washirikina. Riziki ya kutoka mbinguni ni mvua na mwangaza na riziki ya ardhini ni mazao ya porini na yanayopandwa.

Sema : ni Mwenyezi Mungu, siyo masanamu au Malaika, wala sio Isa au Uzayr. Kwa vile hili ndio jibu pekee, ndio maana Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake mtukufu awajibie walioulizwa.

Na hakika sisi au nyinyi bila shaka tuko kwenye uongofu au upotofu ulio wazi.

Nabii ana uhakika kwamba yeye yuko kwenye uongofu na kwamba washirikina wako kwenye upotevu, lakini walipoukataa uwongofu na haki ndio akatumia mfumo huu wa hekima na kuwaambia kuwa mja wetu atakuwa kwenye haki na mwingine kwenye upotevu, basi zirudieni akili zenu muone ni nani aliye kwenye usawa?

Huu ndio mfumo wa Mtume wa uwongofu na rehema, kuongezea kuwa mwenye haki anajiamini hata wakimhalifu watu wote wa ardhini.

Sema: Nyinyi hamtaulizwa kwa makosa tuliyoyafanya wala sisi hatutaulizwa kwa mnayoyatenda.

Huu ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t):

وَإِن كَذَّبُوكَ فَقُل لِّي عَمَلِي وَلَكُمْ عَمَلُكُمْ أَنتُم بَرِيئُونَ مِمَّا أَعْمَلُ وَأَنَا بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٤١﴾

“Na kama wakikukadhibisha, basi sema: Mimi nina amali yangu na nyinyi mna amali yenu. Nyinyi hamna jukumu kwa ninayoyatenda, na mimi sina jukumu kwa mnayoyatenda.” Juz. 11 (10:41).

Sema: Mola wetu atatukusanya kisha atatuhukumu kwa haki, naye ndiye Hakimu, Mjuzi.

Siku ya mwisho ina majina mengi; miongoni mwayo ni siku ya mkusanyiko. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

يَوْمَ يَجْمَعُكُمْ لِيَوْمِ الْجَمْعِ ﴿٩﴾

“Siku atakayowakusanya kwa ajili ya Siku ya mkusanyiko” (64:9).

Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) atatukusanya sisi na na nyinyi ili tuangalie hisabu, malipo na matendo. Hapo pazia litafunuka na mtajua kundi gani ndio lililoelekea njia ya kunyooka.

Sema: Nionyesheni wale mliowaunganisha naye kuwa washirika.

Hapa kuna manaeno ya kukadiria kuwa nionyesheni dalili ya kuwa masanamu ni washirika wa Mwenyezi Mungu au watawajongeza kwa Mwenyezi Mungu.Hapana! Yeye hana mshirika wala msaidizi wala wa kuombea mbele yake isipokuwa aliyempa idhini.

Bali Yeye ni Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

Hakuna enzi wala nguvu isipokuwa kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Ama dalili za hekima yake na utukufu wake zinajitokeza katika kuumba ulimwengu na maajabu yake.

Na hatukukutuma ila kwa watu wote, uwe mtoaji bishara na muonyaji, lakini watu wengi hawajui.

Tazama Juz. 7 (6:92) na Juzuu hii tuliyo nayo (33:40) Kifungu cha ‘Kwanini utume umeishilia kwa Muhammad(s.a.w. w ) ?’

Na wanasema: Ni lini ahadi hii, ikiwa mnasema kweli?”

Imetangulia neno kwa neno katika Juz. 11 (10:48).

Sema: Mna miadi ya siku ambayo hamtaakhirisha saa wala hamtaitangulia.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu Mtukufu ameahidi ufufuo, hisabu na malipo, naye bila shaka, ni mwenye kutekelza miadi yake, lakini kwa wakati alioupanga yeye ambaye hekima yake imetukuka, hatanguliwi wala hacheleweshwi. Basi yasiwahade mliyo nayo enyi washirikina, kwa sababu yatakwisha tu, muda mfupi au mrefu, kisha marejeo yenu nyote ni kwa Mwenyezi Mungu awajulishe yale mliyokuwa mkiyafanya.


4

5

6

7

8

9

10

11

12

13