TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 25563
Pakua: 3251


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 25563 / Pakua: 3251
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

14

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

إِنَّ أَصْحَابَ الْجَنَّةِ الْيَوْمَ فِي شُغُلٍ فَاكِهُونَ ﴿٥٥﴾

55. Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi.

هُمْ وَأَزْوَاجُهُمْ فِي ظِلَالٍ عَلَى الْأَرَائِكِ مُتَّكِئُونَ ﴿٥٦﴾

56. Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fahari.

لَهُمْ فِيهَا فَاكِهَةٌ وَلَهُم مَّا يَدَّعُونَ ﴿٥٧﴾

57. Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakachokitaka.

سَلَامٌ قَوْلًا مِّن رَّبٍّ رَّحِيمٍ ﴿٥٨﴾

58. Salaam! Ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mwenye kurehemu.

وَامْتَازُوا الْيَوْمَ أَيُّهَا الْمُجْرِمُونَ ﴿٥٩﴾

59. Na jitengeni leo enyi wakosefu.

أَلَمْ أَعْهَدْ إِلَيْكُمْ يَا بَنِي آدَمَ أَن لَّا تَعْبُدُوا الشَّيْطَانَ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ ﴿٦٠﴾

60. Je, sikuagana nanyi, enyi wanadamu, kuwa msimuabudu Shet’ani? Hakika yeye ni adui dhahiri kwenu.

وَأَنِ اعْبُدُونِي هَـٰذَا صِرَاطٌ مُّسْتَقِيمٌ ﴿٦١﴾

61. Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia iliyonyooka.

وَلَقَدْ أَضَلَّ مِنكُمْ جِبِلًّا كَثِيرًا أَفَلَمْ تَكُونُوا تَعْقِلُونَ ﴿٦٢﴾

62. Na hakika yeye amewapoteza viumbe wengi miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkim- tia akili?

هَـٰذِهِ جَهَنَّمُ الَّتِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿٦٣﴾

63. Hii ndiyo Jahannamu mliyokuwa mkiahidiwa.

اصْلَوْهَا الْيَوْمَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ ﴿٦٤﴾

64. Ingieni leo kwa vile mlivyokuwa mkikufuru.

الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَىٰ أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُم بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ ﴿٦٥﴾

65. Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyokuwa wakiyachuma.

وَلَوْ نَشَاءُ لَطَمَسْنَا عَلَىٰ أَعْيُنِهِمْ فَاسْتَبَقُوا الصِّرَاطَ فَأَنَّىٰ يُبْصِرُونَ ﴿٦٦﴾

66. Na lau tungelipenda tungeliyafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wangeionaje?

وَلَوْ نَشَاءُ لَمَسَخْنَاهُمْ عَلَىٰ مَكَانَتِهِمْ فَمَا اسْتَطَاعُوا مُضِيًّا وَلَا يَرْجِعُونَ ﴿٦٧﴾

67. Na lau tungelitaka tungewageuza hapo hapo walipo, basi wasingeweza kwenda wala kurudi.

وَمَن نُّعَمِّرْهُ نُنَكِّسْهُ فِي الْخَلْقِ أَفَلَا يَعْقِلُونَ ﴿٦٨﴾

68. Na tunayempa umri tunampindua katika umbo. Basi je! hawatii akilini?

WATU WA PEPONI NA WATU WA MOTONI

Aya 55 – 68

MAANA

Hakika watu wa Peponi leo wamo shughulini, wamefurahi. Wao na wake zao wamo katika vivuli wameegemea juu ya viti vya fahari. Watapata humo kila namna ya matunda na watapata kila watakachokitaka.

Anachotamani mtu zaidi ni siha, amani, utulivu wa moyo kutokana na tabu na mihangaiko na kupata kuburudika na chakula na kinywaji, maskani, mavazi, kustarehe na wanawake na kuwa na bustani yenye miti na mito. Haya yote yanapatikana Peponi.

Zaidi ya hayo ni Salaam! Ndiyo kauli itokayo kwa Mola Mwenye kurehemu.

Salaam ya Mwenyezi Mungu ni amani na rehema. Na radhi yake ndio ukomo wa wema na neema. Ndio maana Imam Ali(a.s ) akasema:“Kila neema isiyokuwa Pepo ni upuzi na kila balaa isiyokuwa moto ni faraja.”

Na jitengeni leo enyi wakosefu.

Wakosefu walikuwa duniani wakijionyesha ni watu wema, wakivaa nguo za utawa na kuchanganyika na watu wa takua na wa heri. Hali halisi haikuwa ikijulikana na watu wengi. Ama leo – siku ya hukumu na malipo, Mwenyezi Mungu atawaweka mbali na watu wema na kuwaambia, ingieni motoni pamoja na watakaoingia:

يُعْرَفُ الْمُجْرِمُونَ بِسِيمَاهُمْ فَيُؤْخَذُ بِالنَّوَاصِي وَالْأَقْدَامِ ﴿٤١﴾

“Watajulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele za utosi na kwa miguu” (55:41).

Je, sikuagana nanyi, enyi wanadamu, kuwa msimuabudu Shet’ani? Hakika yeye ni adui dhahiri kwenu.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwahadharisha waja kutokana na shetani na wasiwasi wake na akwakataza wasimtii; akawaongoza kwenye njia ya heri na uongofu. Lakini wengi wamemtii Shetani na kumuasi Mwingi wa rehe- ma. Hili ameliashiria kwa kusema:

Na ya kwamba mniabudu Mimi? Hii ndiyo Njia iliyonyooka.

Na hakika yeye amewapoteza viumbe wengi miongoni mwenu. Je, hamkuwa mkitia akili?

Kila mwenye kufuata njia ya walioangamia baada ya kuhadharishwa na kuonywa, basi huyo ni katika vipofu wa nuru ya akili na muongozo wake. Wala hakuna malipo ya mfano huu isipokuwa adhabu ambayo amaeiashiria Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kusema:

Hii ndiyo Jahannamu mliyokuwa mkiahidiwa, kupitia midomoni mwa mitume; mkaidharau na mkawadharau. BasiIngieni leo kwa vile mlivyokuwa mkikufuru, na huu ndio mwisho wa kila mpotevu na aliyepituka mipaka.

Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyokuwa wakiyachuma.

Kila kiungo cha muasi kesho kitatamka kumtolea ushahidi mtu wake yale maovu aliyoyafanya. Mkono utatoa ushahidi kwa ulivyopiga, kuiba, kuandika na kuashiria. Mguu kwa ulivyohangaika. Jicho kwa lililoona n.k.Unaweza kuuliza : Utachanganya vipi kauli hii ‘Tutaziba vinywa vyao’ na ile isemayo:

يَوْمَ تَشْهَدُ عَلَيْهِمْ أَلْسِنَتُهُمْ ﴿٢٤﴾

“Siku ambayo zitawashuhudia ndimi zao” Juz. 18 (24:24).

Ambapo ya kwanza imekanusha kutamka na hii ikathibitisha.

Jibu : Kesho waja watakuwa wana hali tofauti, wengine wataruhisiwa kuzungumza na wengine hawataruhusiwa:

يَوْمَ يَأْتِ لَا تَكَلَّمُ نَفْسٌ إِلَّا بِإِذْنِهِ ﴿١٠٥﴾

“Siku itakapofika, nafsi yoyote haitasema ila kwa idhini yake.” Juz. 13 (11:105).

Na lau tungelipenda tungeliyafutilia mbali macho yao, wakawa wanaiwania njia. Lakini wangeionaje? Na lau tungelitaka tungewageuza hapo hapo walipo, basi wasingeweza kwenda wala kurudi.

Makusudio ya kufutilia mbali macho yao ni kuwa kipofu. Maana ni lau Mwenyezi Mungu angelitaka kuwaadhibu wakosefu dunianai angeliwapofusha macho yao na wasingeweza kuongoka na angeliwageuza wakawa wameganda bila ya kuwa na harakati wala uhai.

Na tunayempa umri tunampindua katika umbo. Basi je! hawatii akilini?

Kupindua kitu ni kukifanya juu chini. Binadamu kila anavyoendelea kuwa na umri mrefu anarudi nyuma: anakuwa mdhaifu baada ya kuwa na nguvu.

Lengo la ubainifu huu ni kuashiria kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amempa maisha ya kutosha ili aongoke na afanye mambo mema. Na lau angelipewa umri zaidi ya kawaida, basi maradhi yangelimweka chini, na umri mrefu ungelikuwa ni balaa na shari:

أَوَلَمْ نُعَمِّرْكُم مَّا يَتَذَكَّرُ فِيهِ مَن تَذَكَّرَ وَجَاءَكُمُ النَّذِيرُ فَذُوقُوا فَمَا لِلظَّالِمِينَ مِن نَّصِيرٍ ﴿٣٧﴾

“Je, hatukuwapa umri wa kutosha kukumbuka mwenye kukumbuka, na akawajia mwonyaji? Basi onjeni Na madhalimu hawana wa kuwanusuru” Juz. 22 (35:37).

وَمَا عَلَّمْنَاهُ الشِّعْرَ وَمَا يَنبَغِي لَهُ إِنْ هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ وَقُرْآنٌ مُّبِينٌ ﴿٦٩﴾

69. Wala hatukumfundisha mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur’an inayobainisha.

لِّيُنذِرَ مَن كَانَ حَيًّا وَيَحِقَّ الْقَوْلُ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴿٧٠﴾

Ili imwonye aliye hai, na ihakikike kauli juu ya makafiri.

HATUKUMFUNDISHA MASHAIRI

Aya 69 – 70

MAANA

Maadui wa Mwenyezi Mungu walijaribu kwa nyenzo zote kumkadhibisha Muhammad(s.a.w. w ) . Miongoni mwazo ni kauli yao kuwa ni mwenda wazimu, lakini mmoja wao, Walid bin Al-Mughira, aliyekufa akiwa kafiri, akasema: “Hapana, hakika kauli yake – yaani Qur’an – ina utamu na ina mvuto na kwamba juu yake kuna matunda na chini yake kumejaa. Hakika iko juu na haishindwi” Basi wakabadilisha kumtusi na wazimu na kusema: “Huyu ni mchawi muongo” (38:4.) Ilipowabainikia kuwa wao ndio waongo wakasema ni kuhani anakosea na anapatia au ni malenga mwenye kutunga mashairi kwa mawazo.

Ilivyo hasa ni kuwa kutuhumu kwao kuwa Mtume(s.a.w. w ) ni mshairi kunafahamisha kwamba mashairi kwa waarabu si lazima yawe na vina na uzani, bali yana upana zaidi. Ni fani iliyo na uzuri wake; iwe na uzani au la. Hali ni hiyo hiyo hata kwa wanafalsafa wa kale.

Mwenye Tafsir Ruhul-bayani amesema: “Mashairi ya watu wa kale hayakuwa na uzani wala vina wala hivyo sio nguzo ya ushairi.” Fikra hii imeenea leo kwenye somo la fasihi na uchambuzi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewarudi wanaomtuhumu Mtume Mtukufu kuwa ni mshairi au kuhani kwenye Aya nyingi; miongoni mwazo ni:

إِنَّهُ لَقَوْلُ رَسُولٍ كَرِيمٍ ﴿٤٠﴾ وَمَا هُوَ بِقَوْلِ شَاعِرٍ قَلِيلًا مَّا تُؤْمِنُونَ ﴿٤١﴾ وَلَا بِقَوْلِ كَاهِنٍ قَلِيلًا مَّا تَذَكَّرُونَ ﴿٤٢﴾

“Kwa hakika hiyo ni kauli ya Mtume mwenye heshima. Wala si kauli ya mshairi. Ni machache mnayoamini, wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayokumbuka. (69:40 – 42).

فَذَكِّرْ فَمَا أَنتَ بِنِعْمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٍ وَلَا مَجْنُونٍ ﴿٢٩﴾ أَمْ يَقُولُونَ شَاعِرٌ ﴿٣٠﴾

Na wewe kwa neema ya Mola wako si kuhani wala mwendawazimu. Au wanasema ni mshairi (52:29 – 30).

Na wakisema:

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ﴿٣٦﴾

“Hivi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mshairi mwendawazimu?” (37:36).

“Bali huyo ni mshairi.” Juz. 17 (21:5). Aya hizi tulizo nazo:

Wala hatukumfundisha mashairi, wala hayatakikani kwake hayo. Haukuwa huu ila ni ukumbusho na Qur’an inayobainisha. Ili imwonye aliye hai, na ihakikike kauli juu ya makafiri.

Makusudio ya aliye hai hapa, ni yule ambaye akili yake iko hai kiuzingatiaji, kutaamali na kufungua moyo wake kwa haki na kheri. Na makusudio ya kauli hapa ni adhabu; sawa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَلَـٰكِنْ حَقَّتْ كَلِمَةُ الْعَذَابِ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴿٧١﴾

“Lakini limekwishahakika neno la adhabu juu ya makafiri.” (39:71).

Washirikina walisema kuwa Qur’an aliyokuja nayo Muhammad si chochote ila ni mashairi yanayoelezea fikra yake na mawazo yake; na wala sio wahyi kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawarudi, kwa kuwaambia, kuwa shairi linajikita zaidi kwenye fikra hawa na mapendeleo ya mshairi; anamtetea anayempenda hata kama hana haki na anapamabana na anayemchukia hata kama ana haki. Na Qur’an ni kauli yenye hadhi na ya upambanuzi, na wala si kauli ya hawa na mzaha.

Ni Kitabu cha itikadi na sharia, maadili na mawaidha, ndani yake mna ilimu na fikra. Sasa wapi na wapi ushairi na hayo.

Kama ingelikuwa Qur’an imetengenezwa na Muhammad(s.a.w.w) , angeliweka humo machungu yake na huzuni yake, maisha yake na maazimio; sawa na walivyo malenga.

Kilichobakia ni kudokeza kuwa; hata hivyo Mtume(s.a.w.w) alikuwa akithamini na akiheshimu ushairi, kama fani iliyo na athari nzuri katika kuelezea mapendeleo na matakwa ya watu na amani yao.

Kuna kauli mshuhuri aliyoisema: “Katika baadhi ya ubainifu kuna uchwi na katika baadhi ya mshairi kuna hekima.” Alikuwa akiwaombea tawfiki malenga wanaoipigania haki na watu wa haki.

Aliwahi kumvulia kashida yake Ka’ab bin Zuheir kwa kumtuza, pale alipomsifu kwa kaswida yake iliyo maarufu kwa jina la Burda (kashida); miongoni mwa beti zake ni:

Haki ni nuru rasuli, kwaye twaangaziwa, Upanga wenye makali, wa Mola umechomozwa.

Tazama Juz. 22 (36:4) kifungu cha ‘Mdundo wa ndani katika Qur’an’ na Juz. 19 (26:224).

15

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّا خَلَقْنَا لَهُم مِّمَّا عَمِلَتْ أَيْدِينَا أَنْعَامًا فَهُمْ لَهَا مَالِكُونَ ﴿٧١﴾

71. Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyofanya mikono yetu wanyamahowa, na wao ni wenye kuwamiliki.

وَذَلَّلْنَاهَا لَهُمْ فَمِنْهَا رَكُوبُهُمْ وَمِنْهَا يَأْكُلُونَ ﴿٧٢﴾

72. Na tumewatiisha kwao. Basi baadhi yao wako wanaowapanda, na baadhi yao wanawala.

وَلَهُمْ فِيهَا مَنَافِعُ وَمَشَارِبُ أَفَلَا يَشْكُرُونَ ﴿٧٣﴾

73. Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?

وَاتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ آلِهَةً لَّعَلَّهُمْ يُنصَرُونَ ﴿٧٤﴾

74. Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu wapate kusaidiwa!

لَا يَسْتَطِيعُونَ نَصْرَهُمْ وَهُمْ لَهُمْ جُندٌ مُّحْضَرُونَ ﴿٧٥﴾

75. Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio jeshi lao watakaohudhurishwa.

فَلَا يَحْزُنكَ قَوْلُهُمْ إِنَّا نَعْلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعْلِنُونَ ﴿٧٦﴾

76. Basi isikuhuzunishe kauli yao, hakika Sisi tunayajua wanayoyaweka siri na wanayoyatangaza.

MIKONO YA MWENYEZI MUNGU NDIO DESTURI YA ULIMWENGU NA MAUMBILE

Aya 71 – 76

MAANA

Je! Hawaoni kwamba tumewaumbia kutokana na iliyofanya mikono yetu wanyamahowa, na wao ni wenye kuwamiliki. Na tumewatiisha kwao. Basi baadhi yao wako wanaowapanda, na baadhi yao wanawala. Na wao wanapata kwao manufaa na vinywaji. Basi je, hawashukuru?

Wanyamahowa ni wanyama wa mifugo ambao ni ngamia, ngo’mbe, mbuzi na kondoo. Ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa waja wake; wanawala, wanakunywa maziwa yao, kutengenza majumba, samani, mavazi kutokana na ngozi, sufu na manyoya. Vile vile kuwabeba wao na mizigo yao kutoka sehemu moja hadi nyingine ambayo wangelifika kwa tabu.

Hilo amelikariri Mwenyezi Mungu (s.w.t) katika Aya kadhaa; kama vile Juz. 8 (6:142) na Juz. 14 (16:5- 8). Lengo ni kuhimiza Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kushukuriwa na kutiiwa. Hilo ameliashiria kwa kauli yake: “Basi je, hawashukuru?” Katika Nahjul-Balagha imeelezwa: “Hata kama Mwenyezi Mungu asingelitoa kiaga kwa kuasiwa kwake, bado ingelikuwa ni wajibu kutoasiwa kwa kushukuru neema zake.”

Makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Kutokana na iliy- ofanya mikono yetu,” ni sababu za kimaumbile. Kwa vile Mwenyezi Mungu sio mwili, mpaka isemwe kuwa ana mikono hasa.

Ibn Al- Arabi anasema katika Futuhat: “Watu wa Mwenyezi Mungu wanawagawanya viumbe kwenye namna mbili: Kuna namna inayopatikana kwa ulimwengu wa amri kwa sababu neno “kun” (kuwa) ni amri. Na aina nyingine inapatikana kwa mikono ya sababu, wanaita ulimwengu wa maumbile. Haya yamefafanuliwa katika Juz. 3 (2:255) kifungu cha ‘Mwenyezi Mungu na desturi ya maumbile.’

Na wameishika miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu wapate kusaidiwa! Hawataweza kuwasaidia. Bali hao ndio jeshi lao watakaohudhurishwa.

Yaani hao washirikina ndio jeshi la hayo masanamu. Maana ni kuwa masanamu hayawezi kuwanufaisha washirikina, lakini pamoja na hayo wao wanayalinda. Ni jambo la kushangaza sana kuwa mwenye akili anaabudu mawe yasiyodhuru wala kunufaisha.

La kushangaza sana ni kuwa wao wanayalinda yasiibwe au kuharibiwa na wakati huo huo wanayatarajia yawasaidie katika shida na kuwakurubisha kwa Mwenyezi Mungu. Hayo yenyewe hayawezi kujisaidia yatawasaidiaje wengine.

Zaidi ya hayo yote, waabudu masanamu walimwambia Mtume(s.a.w. w ) kuwa yeye ni mwendawazimu. Kwa nini? Kwa sababu yeye haabudu mawe. Wao ndio wenye akili kwa sababu wanaaabudu yale wanayoya- chonga. Jambo la kushangaza kabisa.

Basi isikuhuzunishe kauli yao kuwa wewe Muhammad ni mwendawazimu, au mshairi au ni kuhani.

Hakika Sisi tunayajua wanayoyaweka siri na wanayoyatangaza.

Walidhamiria chuki na kinyongo kwa Mtume(s.a.w. w ) na wakatangaza shutuma kwake na kwa mwito wake. Hakuna shaka kwamba Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa hilo na muweza wa kuwahisabu na kuwaadhibu. Basi hakuna haja ya huzuni na uchungu.

أَوَلَمْ يَرَ الْإِنسَانُ أَنَّا خَلَقْنَاهُ مِن نُّطْفَةٍ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٌ مُّبِينٌ ﴿٧٧﴾

77. Je, haoni mtu kuwa tumemuumba kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndiye mgomvi wa dhahiri!

وَضَرَبَ لَنَا مَثَلًا وَنَسِيَ خَلْقَهُ قَالَ مَن يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ ﴿٧٨﴾

78. Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: ‘Ni nani huyo atakayeihuisha mifupa nayo imemung’unyika?’

قُلْ يُحْيِيهَا الَّذِي أَنشَأَهَا أَوَّلَ مَرَّةٍ وَهُوَ بِكُلِّ خَلْقٍ عَلِيمٌ ﴿٧٩﴾

79. Sema: Ataihuisha aliyeiumba mara ya kwanza. Na Yeye ni Mjuzi wa kila uumbaji.

الَّذِي جَعَلَ لَكُم مِّنَ الشَّجَرِ الْأَخْضَرِ نَارًا فَإِذَا أَنتُم مِّنْهُ تُوقِدُونَ ﴿٨٠﴾

80. Yeye ambaye aliwajaalia moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa mnauwasha.

أَوَلَيْسَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يَخْلُقَ مِثْلَهُم بَلَىٰ وَهُوَ الْخَلَّاقُ الْعَلِيمُ ﴿٨١﴾

81. Kwani aliyeziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwa nini! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.

إِنَّمَا أَمْرُهُ إِذَا أَرَادَ شَيْئًا أَن يَقُولَ لَهُ كُن فَيَكُونُ ﴿٨٢﴾

82. Hakika amri yake anapotaka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kinakuwa.

فَسُبْحَانَ الَّذِي بِيَدِهِ مَلَكُوتُ كُلِّ شَيْءٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٨٣﴾

83. Basi Ametakata na mawi yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake mtarejeshwa.

AKASEMA NI NANI ATAKAYEIHUISHA MIFUPA?

Aya 77 – 83

MAANA

Je, haoni mtu kuwa tumemuumba kutokana na tone la manii? Kisha sasa yeye ndiye mgomvi wa dhahiri!

Jana alikuwa ni tone la manii, lakini alipokuwa, kwa uweza wa Mwenyezi Mungu, ni kiumbe aliye sawasawa mwenye ufahamu, alisahau asili yake na kuanza kumchokoza Mola wake kwa uasi na maneno mabaya.

Na akatupigia mfano, na akasahau kuumbwa kwake, akasema: ‘Ni nani huyo atakayeihuisha mifupa nayo imemung’unyika?’

Anayepiga mfano ni yule anayekana ufufuo. Anapiga mfano wa kutowezekana ufufuo kwa kusema, vipi vitaweza kuungana viungo vya mifupa na kuwa na uhai tena baada ya kuchakafuka na kuwa mchanga unaotawanyika huku na huko? Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamrudi mwenye mfano huu kwa kusema kuwa unastaajabu nini na kukana ufufuo kwa kupiga mfano na unasahahu nafsi yako? Hujui kwamba Mwenyezi Mungu amekuumba kwa mchanga kisha kwa tone la manii? Mwenyezi Mungu amekuleta baada ya kuwa hauko; vile vile basi ana uwezo wa kukurudisha baada ya kuwa mifupa iliyomung’unyika.

Sema: Ataihuisha aliyeiumba mara ya kwanza. Na Yeye ni Mjuzi wa kila uumbaji.

Yaani sema ewe Muhammad kumwambia mpinzani: Kuna ajabu gani kwa mifupa iliyochakaa kupata uhai? Yule ambaye amelifanya tone la manii liweze kusikia, kuona, kuwa na fahamu na ubainifu, ndiye atakayeweza kuirudisha mifupa ilivyokuwa. Umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa; miongoni mwazo ni: Juz. 15 (17:49).

Yeye ambaye aliwajaalia moto kutokana na mti wa kijani nanyi mkawa mnauwasha.

Mfano huu unaweka wazi fikra ya ufufuo. Ubainifu wa hilo ni kwamba wenye kupinga wameweka mbali fikra ya ufufuo si kwa lolote isipokuwa kwa kudhani kuwa vitu haviwezi kugeuka kuwa kinyume chake.

Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawajibu kuwa fikra hii ni dhana na njozi tu. Kwa sababu mageuko haya yanatokea waziwazi mkiyaona asubuhi na jioni, lakini hamatanabahi.

Mti mbichi unageuka kuwa kuni na ardhi kame inapata uhai na kumea miti mbalimbali ikipata maji. Sasa vipi mnakana kupata uhai mifupa na mnakubali kupata uhai ardhi iliyokufa na miti kugeuka kuwa moto. Yote haya ni mamaoja tu – kugeuka kitu kutoka kilivyo na kuwa kinyume chake.

Kwani aliyeziumba mbingu na ardhi hawezi kuwaumba mfano wao? Kwa nini! Naye ndiye Muumbaji Mkuu, Mjuzi.

Mwenye kuuleta ulimwengu bila ya kutokana na chochote ni rahisi kuleta mfano wake kufanya mfano wake saa yoyote anayotaka. Umetangulia mfano wake katika Juz. 15 (17:99).

Hakika amri yake anapotaka kitu ni kukiambia tu: Kuwa! Na kinakuwa.

Alianza kuumba kwa neno ’Kuwa’ na atarudisha kwa neno hilo hilo.

Basi Ametakata na mawi yule ambaye mkononi mwake umo Ufalme wa kila kitu; na kwake mtarejeshwa.

Ametakasika Mola wetu na shirk na Yeye peke yake ndiye mwanzishi na mrudishaji.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA SITA: SURAT YASIN

16

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Sura Ya Thelathini Na Saba: Surat As-Saffat. Imeshuka Makka ina Aya 182.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

وَالصَّافَّاتِ صَفًّا ﴿١﴾

1. Naapa kwa wanaojipanga safu-safu.

فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا ﴿٢﴾

2. Na kwa wenye kuzuia sana.

فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا ﴿٣﴾

3. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

إِنَّ إِلَـٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ ﴿٤﴾

4. Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ ﴿٥﴾

5. Mola wa mbingu na ardhi, na vilivyomo kati yake, na ni Mola wa mashariki zote.

إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ ﴿٦﴾

6. Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya dunia (karibu) kwa pambo la nyota.

وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ ﴿٧﴾

7. Na kuilinda na kila shetani muasi.

لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ ﴿٨﴾

8. Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

دُحُورًا وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ ﴿٩﴾

9. Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ ﴿١٠﴾

10. Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfuatia kimondo kinachong’ara.

WANAOJIPANGA SAFU

Aya 1 – 10

MAANA

Naapa kwa wanaojipanga safu-safu. Na kwa wenye kuzuia sana. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

Wametofautiana wafasiri katika maana ya wanaojipanga safu, wenye kuzuia na wenye kusoma ukumbusho. Kuna waliosema kuwa ni Malaika.

Wengine wakasema ni waumini wanaokaa safu katika Swala ya jamaa na katika jihadi. Na wenye kuzuia ni makatazo ya Qur’an na Aya zake. Na wenye kusoma ni wasomaji wa Qur’an kwenye Swala na kwengineko.

Sio mbali kuwa makusudio ni aina tatu alizozitaja Imam Ali(a.s ) katika khutba ya kwanza kwenye Nahjul-Balagha, katika wasifu wa Malaika: “Miongoni mwao kuna ambao wamesujudu na wala hawarukui, na kuna waliorukuu na wala hawasimami, kuna waliosimama katika safu na wala hawatawanyiki.” Aliposema: ‘Kuna waliosimama katika safu na wala hawatawanyiki’ inawezekana kuwa ni ishara ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Naapa kwa wanao jipanga safu-safu.”

Kisha Imam Ali(a.s ) akaendelea kusema: “ Miongoni mwao kuna waaminifu wa wahyi wa Mungu, na ni ndimi zitamkazo kwa mitume Wake;” yaani wanaoshuka na wahyi kwa mitume wake; kama vile Jibril(a.s ) . Kauli hii nayo ina uwezekano wa kuwa ni ishara ya kauli ya Mwenyezi Mungu: “Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.” Kwa sababu wao wanasoma Kitabu cha Mwenyezi Mungu wakati wanapofikisha kwa Mitume.

Akaendelea kusema: “Na miongoni mwao kuna wahifadhi wa waja wake.” Sheikh Muhammad Abduh, katika kuwaelezea hawa, anasema: “Kama kwamba wao ni nguvu inayotiwa katika miili ya binadamu na katika nafsi zao; akiwahifadhi Mwenyezi Mungu binadamu wasiangamie kwa Malaika. Na lau si hivyo, maangamizi yangelikuwa yanamwandama mtu zaidi kuliko amani.”

Sheikh, katika kuleta picha hii, anakusudia kurahisisha kufahamu jinsi Malaika wanavyohifadhi waja; akisema: “Kama kwamba wao.”

Kwa hiyo basi inawezekana hilo linaashiria kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na kwa wenye kuzuia sana,” ikiwa tutasema kuwa kuzia hapa maana yake ni kuzuia udhia kwa waja.

Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja. Mola wa mbingu na ardhi, na vilivyomo kati yake, na ni Mola wa mashariki zote.

Makusudio ya mashariki[6] zote ni mashariki ya Jua kwa kuangalia kwamba kila siku linatokeza mashariki na kutua magharibi. Mwenyezi Mungu amekata kuwa Yeye ni mmoja hana mshirika katika kuumba na kupangilia.

MWENYEZI MUNGU NA KUAPA NA VIUMBE VYAKE

Unaweza kuuliza : Kwa nini Mwenyezi Mungu ameapa kwa Malaika?

Wafasiri wamejibu kuwa Mwenyezi Mungu ameapa kwa Malaika kujulisha ukuu wa daraja na umuhimu wao. Hili ndio jawabu lao kwa kila alichoapia Mwenyezi Mungu; iwe ni wakati, mahali au chochote kilichoko juu au chini. Hata hivyo mwenye Dhilal ameunganisha kuapa huku na kauli ya watu wa jahiliya waliosema kuwa Malaika ni mabinti wa Mungu; kama alivyosema Mwenyezi Mungu:

أَفَأَصْفَاكُمْ رَبُّكُم بِالْبَنِينَ وَاتَّخَذَ مِنَ الْمَلَائِكَةِ إِنَاثًا إِنَّكُمْ لَتَقُولُونَ قَوْلًا عَظِيمًا ﴿٤٠﴾

“Je, Mola wenu amewachagulia waototo wa kiume na yeye akajichukulia watoto wa kike katika Malaika? Hakika nyinyi mnasema kauli kubwa.” Juz. 15 (17:40).

Akasema mwenye Dhilal: Lengo la kuapa kwa Malaika ni kuwarudi wenye kuamini upotofu huu alioita Mwenyezi Mungu ‘kauli kubwa.’

Tuanavyo sisi ni kuwa Mwenyezi Mungu anaapa na kitu chochote kile kwa lengo moja tu – kuwa kila kilichopo kwa asili yake kinafahamisha kuwa Mwenyezi Mungu ni mmoja hana mshirika.

Hakuna mwenye shaka kuwa Malaika wanaopanga safu na wasiopanga safu wanamwabudu Mwenyezi Mungu na kumtii kwa ujuzi na yakini na kwa utumishi wao. Kwa hiyo kujua kwao hivi ni dalili mkataa kuwa Yeye ni mmoja hana mshirika katika kuuumba umiliki na upangiliaji; sawa na kujua wataalamu hakika ya maudhui waliyoyagundua na kuyafanyia majaribio.

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya dunia (karibu) kwa pambo la nyota.

Makusudio ya mbingu ni anga ya juu na dunia ni dunia yetu sisi binadamu[7] , sio ulimwengu wote. Makusudio ya nyota ni zile zilizo kwenye anga iliyo karibu zaidi na sisi. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amejaalia nyota, jinsi ziliyvo na mwanga wake katika anga yetu, kuwa ni pambo na urembo; mbali ya manufaa na faida zake:

وَهُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ النُّجُومَ لِتَهْتَدُوا بِهَا فِي ظُلُمَاتِ الْبَرِّ وَالْبَحْرِ ﴿٩٧﴾

“Na yeye ndiye aliyewafanyia nyota ili muongoke kwazo katika viza vya bara na baharini. Juz. 7 (6:97).

Na kuilinda na kila shetani muasi wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande, wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu. Isipokuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfuatia kimondo kinacho ng’ara.

Misamiati ya Aya hii iko wazi, isipokuwa miwili-Shetani asi na viumbe watukufu. Mwenyezi Mungu na Mtume wake wameinyamazia, hawaku- tubainishia. Nasi hatuwezi kufasiri bila ya ujuzi. Kwa hiyo tunasema kuwa Aya hizi ni katika zinazotatiza kwetu, lakini inawezekana kuwa ziko wazi kwa wenzetu.

Sio mbali kuwa sababu ya kunyamazia ni kuwa kumjua shetani huyu na kiumbe mtukufu hakuna uhusiano na maisha yetu au kuwa fahamu zetu zinashindwa kufahamu uhakika wake. Na mwenye elimu kadiri atakavyojitahidi, lakini hawezi kujua kila kitu; bali hawezi hata kujua kitu chochote katika vinavyomzunguka uhakika wake hasa kilivyo.

Kujua kwetu misamiati ya Aya; kama kimondo kinachong’ara, adhabu ya kudumu, kunyakua na kufuatiwa, hakuwezi kutosha kufasiri makusudio ya Aya kwa ujumla wake, maadamu hatujui uhakika wa shetani asi na viumbe watukufu.

Baadhi ya wafasiri wamesema makusudio ya shetani asi ni shetani jini. Wengine wakasema ni binaadamu ambaye hafikiri ukuu na utukufu wa nyota na kufahamisha kwake kuweko Mwenyezi Mungu. Masufi wanase- ma: Makusudio ya shetani ni picha na nguvu ya kuwazia. Yote hiyo ni kutupia kwa mbali. Ni afadhali kunyamaza kuliko kusema bila ya kujua. Mwenyezi Mungu anasema:

وَمَا أُوتِيتُم مِّنَ الْعِلْمِ إِلَّا قَلِيلًا ﴿٨٥﴾

“Nanyi hamkupewa katika elimu ila kidogo tu.” Juz. 15 (17:85).

فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ ﴿١١﴾

11. Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.

بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ ﴿١٢﴾

12. Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ ﴿١٣﴾

13. Na wanapokumbushwa hawakumbuki.

وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ ﴿١٤﴾

14. Na wanapoona Ishara, wanafanya maskhara.

وَقَالُوا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

15. Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio dhahiri.

أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ﴿١٦﴾

16. Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ ﴿١٧﴾

17. Hata baba zetu wa zamani?

قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ ﴿١٨﴾

18. Sema: Naam! Na hali nyinyi ni madhalili.

فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ ﴿١٩﴾

19. Na hakika ni ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَـٰذَا يَوْمُ الدِّينِ ﴿٢٠﴾

20. Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

هَـٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ﴿٢١﴾

21. Hii ndiyo Siku ya upambanuzi mliyokuwa mkiikadhibisha.

احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ ﴿٢٢﴾

22. Wakusanyeni waliodhulumu, na wenzao, na hao waliokuwa wakiwaabudu,

مِن دُونِ اللَّـهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ ﴿٢٣﴾

23. Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

وَقِفُوهُمْ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ ﴿٢٤﴾

24. Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa.

مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ ﴿٢٥﴾

25. Mna nini? Mbona hamsaidiani?

بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ ﴿٢٦﴾

26. Bali leo, watasalimu amri.

BALI UNASTAAJABU, NA WAO WANAFANYA MASKHARA

Aya 11 – 26

MAANA

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tuliowaumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unaonata.

Waulize ewe Muhammad, wale wanaokana ufufuo kuwa kuumba mbingu na ardhi bila ya nyenzo yoyote ni kugumu au kumrudisha mtu kwenye uhai baada ya kufa kwake, na hali Mwenyezi Mungu amemuumba kwa udongo tu uanonata?

Hakika yule ambaye ameuumba ulimwengu bila ya nyenzo yoyote, inakuwa wepesi zaidi kurudisha viungo vya mtu kwenye uhai.

لَخَلْقُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ أَكْبَرُ مِنْ خَلْقِ النَّاسِ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَ النَّاسِ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٥٧﴾

“Hakika kuumba mbingu na ardhi ni kukubwa zaidi kuliko kuwaumba watu, lakini watu wengi hawajui.” (40:57)

Unaweza kuuliza : Kwenye Juz.15 (18: 22) Mwenyezi Mungu anasema: “Wala usiulize habari zao kwa yeyote yule.” Kuna njia gani ya kuafikiana Aya mbili hizi?

Jibu : maudhui ya Aya ile yanahusiana na watu wa pango; ambapo Mwenyezi Mungu alimkataza Nabii wake mtukufu kutomuuliza yeyote kuhusiana na wao, baada ya kumweleza habari zao. Na hii tuliyo nayo inahusiana na washirikina tu. Na makusudio ni kuwatahayariza na kuwapa hoja.

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

Wewe Muhammad unawastaajabu washirikina kwa jinsi walivyomfanya Mwenyezi Mungu kuwa na washirika, pamoja na dalili za umoja zilizo wazwazi. Nao vile vile wanakushangaa wewe; bali wanakufanyia maskhara. Kwa sababu dalili za ushirikina ziko wazi kulingana na ufahamu wao na wala sio dalili za tawhid.

Hii inafahamisha kuwa ndio makusudio ya kauli yake Mwenyezi Mungu: “Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili kweli ni jambo la ajabu. (38:5).

Ikiwa mtu atasema pamoja na yule mshairi: “Kila mtu dini yake anaitukuza, laitani usahihi ningejuzwa,” nasi tutajibu:

Kuna misingi na uhakika ulio wazi ambao hawawezi kutofautiana hata watu wawili; ambapo anaweza kuijua mjuzi na asiyekuwa mjuzi; mfano: Elimu ni bora kuliko ujinga, na utajiri ni bora kuliko ufukara.

Ikiwa wawili watatofautiana katika nadharia fulani, yule ambaye kauli yake itaishia kwenye misingi iliyo wazi basi huyo ndiye atakayekuwa na haki.

Na wanapokumbushwa hawakumbuki. Na wanapoona Ishara, wanafanya maskhara.

Kwa sababu mwenye kutii hawaa yake na kuiga mababa zake, huifumbia macho haki: Imam Ali(a.s ) anasema:“Yeyote anayeiacha haki, mazuri huwa mabaya kwake na mabaya huwa mazuri kwake, na hulewa ulevi wa upotevu.”

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi ulio dhahiri.

Haya wameyakari mara nyingi. Miongoni mwayo ni yale yaliyo katika Juz. 7 (6:7).

Ati tukishakufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa? Hata baba zetu wa zamani?

Maana yako wazi. umetangulia mfano wake katika Aya kadhaa; miongoni mwazo ni: Juz. 13 (13:5), Juz. 15 (17: 98), Juz. 18 (23: 82) na Juz. 20 (27:68)

Sema: Naam! Na hali nyinyi ni madhalili. Na hakika ni ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

Yaani sema ewe Muhammad, kuwaambia wale wanaopinga ufufuo: ndio, nyinyi mtafufuliwa kutoka kwenye makaburi yenu kwa neno moja tu kutoka kwa Mwenyezi Mungu na mtakusanywa kwake mkiwa madhalili na mtaiona adhabu mliyokuwa mkiikadhibisha kwa macho yenu.

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo. Hii ndiyo Siku ya upambanuzi -baina ya haki na batili -mliyokuwa mkiikadhibisha.

Haki inapowajia wanapokuwa na fursa ya kuifanyia kazi, wanasema huu ni uwongo na uchawi, hauamini ila mjinga mwenye kuhadaliwa. Na wakati ukipita ukaja wakati wa malipo na kuonja ubaya wa matendo yao, watasema: Ole wetu, sisi tulikuwa kwenye mghafala wa haya, tumejidhulumu wenyewe.

Hali hii mara nyingi inatokea. Mjinga anahangaikia litakalomdhuru, lakini anapopewa nasaha na mwenye akili na kumhadharisha na mwisho mbaya, yeye humdharau na anafura kichwa.

Yakimfika na kutokuwa na pa kukimbilia na kutambua kuwa amehasirika anahangaika na majuto na kusema: laitani nisingelikuwako.

Wakusanyeni waliodhulumu, na wenzao, na hao waliokuwa wakiwaabudu, badala ya Mwenyezi Mungu.

Aya inaashiria kugawanyika wakosefu; kwamba mshirikina atafufuliwa na washirikina wenzake mahali pamoja kwenye Jahannam wakiwa pamoja na masanamu waliyokuwa wakiyaabudu. Vile vile mwizi pamoja na wezi. Kila aina kwa aina yake; sawa na walivyokuwa duniani.

Waongozeni njia ya Jahannamu!

Ikishamalizika hisabu Malaika wataambiwa: Haya wapelekeni haraka kwenye moto mbaya.

Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:

Kabla ya Malaika kuwapeleka kwenye Jahannam watawazuia ili waulizwe yale waliyokuwa wakiyafanya. Katika badhi ya mapokezi imeelezwa kuwa siku hiyo mtu ataulizwa kuhusu alivyomaliza umri wake, mali yake alivyoipata na kuitumia na elimu yake alivyoifanyia kazi.

Ama kulinganisha baina ya Aya hii na ile isemayo:

فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُسْأَلُ عَن ذَنبِهِ إِنسٌ وَلَا جَانٌّ ﴿٣٩﴾

“Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.” (55:39)

Tumekuelezea mara nyingi. Kwa ufupi ni kuwa siku ya mwisho itakuwa na hali ya kuulizwa na ya kutoulizwa. Tazama juzuu hii tuliyo nayo (36:65).

Mna nini? Mbona hamsaidiani?

Yaani kesho wataambiwa wakosefu; kwa nini leo hamsaidiani na kule duniani mlikuwa na mshikamano dhidi ya haki na watu wake. Lengo la swali hili ni kutahayariza.

Bali leo, watasalimu amri.

Watafuata amri ya Mwenyezi Mungu na hawatakuwa na hila yoyote.