TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 25532
Pakua: 3223


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 32 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 25532 / Pakua: 3223
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA Juzuu 21

Mwandishi:
Swahili

19

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ ﴿١٠٠﴾

100. Ewe Mola wangu! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ ﴿١٠١﴾

101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole.

فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّـهُ مِنَ الصَّابِرِينَ ﴿١٠٢﴾

102. Basi alipofika makamo ya kuhangaika pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa. Utanikuta mimi, Inshallah, katika wanaosubiri.

فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ ﴿١٠٣﴾

103. Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.

وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ ﴿١٠٤﴾

104. Tulimwita: Ewe Ibrahim!

قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١٠٥﴾

105. Umekwishaisadikisha ndoto. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

إِنَّ هَـٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ ﴿١٠٦﴾

106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.

وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ ﴿١٠٧﴾

107. Na tukamfidia kwa dhabihu adhimu.

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ﴿١٠٨﴾

108. Na tukamwachia kwa walio baadaye.

سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ ﴿١٠٩﴾

109. Amani kwa Ibrahim.

كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١١٠﴾

110. Hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١١﴾

111. Hakika yeye ni katika waja wetu waumini.

وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ ﴿١١٢﴾

112. Na tukambashiria Is-haq, Nabii miongoni mwa watu wema.

وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ ﴿١١٣﴾

113. Na tukambarikia yeye na Is-haq na miongoni mwa dhuriya zao yuko mwema na mwenye kudhulumu nafsi yake waziwazi.

NIMEONA USINGIZINI KUWA NINAKUCHINJA

Aya 100 – 113

MAANA

Ewe Mola wangu! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.

Ibrahim alifikia uzee sana, wala hakuruzukiwa mtoto. Akamuomba Mola wake ampe kizazi cha waumini na warithi wema.

Basi tukambashiria mwana aliye mpole ambaye ni Ismail, hilo halina shaka, kwa ushahidi wa Qur’an. Ufafanuzi utakuja baada ya tafsiri ya Aya hizi tulizo nazo.

Basi alipofika makamo ya kuhangaika pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchin- ja. Basi angalia, waonaje?

Yaani alipofikia Ismail umri wa kuhangaika pamoja na baba yake. Ibrahim aliota kuwa anamchinja mwanawe. Kafahamu kutokana na ndoto hii kuwa amchinje au amlete machinjioni mwanawe. Na fahamu ya manabii ni yakini. Ndio maana akaamua kuitekeleza ndoto yake. Akampa habari mwanawe na kumtaka maoni yake.

Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyoamrishwa.

Alimjibu bila ya kusita kuwa mimi sina maoni wala amri yoyote kwenye amri ya Mwenyezi Mungu na amri yako. Nichinje tu maisha yangu hayana thamani yoyote mbele ya radhi za Mwenyezi Mungu na rdhi zako. Nikate kichwa na bado wewe utakuwa unanihurumia, maadamu unatekeleza radhi za Mwenyezi Mungu na kuitikia mwito wake.

Kisha Ismail akawa anampoza baba yake na kumwambia:Utanikuta mimi, Inshallah, katika wanaosubiri na kuwa mvumilivu kuweza kukabili kuchinjwa.

Basi wote wawili walipojisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji, tulimwita: Ewe Ibrahim! Umekwishaisadikisha ndoto. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

Ismail aliponyoosha shingo yake na Ibrahim akapeleka kisu chake, kila mmoja wao akimwachia Mungu, ulikuja mlingano kutoka amri ya juu kwamba hii ndio tafsiri ya ndoto yako - azimio la kujitolea kwako kuchinja kwa ajili ya ikhalasi ya Mwenyezi Mungu na Ismail kutekeleza amri ya Mwenyezi Mungu kwa moyo safi. Kwa hiyo kuchinja halikuwa ndio lengo.

Unaweza kuuliza : Ikiwa lengo halikuwa kuchinja, basi kulikuwa na haja gani ya kuamrishwa?

Jibu : baadhi wanasema kuwa lengo la hilo ni kudhihirisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa watu na vizazi vitakvyokuja, utukufu wa Ibrahim na mwanawe Ismail walivyojitolea muhanga na ikhlasi yao.

Wawe ni sehemu ya kutukuzwa na tukufu hadi ufufuo. Wengine wakasema ni kwa ajili ya kuugeuza wivu wa Sara kwa Hajar, mama wa Ismail na kuzuia ugumu wake kwa Ibrahim.

Nasi tunaongeza kwenye kauli mbili hizo, kuwa vile vile Mwenyezi Mungu (s.w.t.) alitaka kutoa mfano wa mumin wa haki, kwamba ni yule anayemtii Mwenyezi Mungu katika kila jambo, hata ikibidi kumchinja mwanawe aliye nyongo mkalia ini. Hili linaashiriwa na kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t):

Hakika haya ni majaribio yaliyo dhahiri.

Yaani azimio hili la kujitolea muhanga kwa hali na mali kwa kufuata amri ya Mwenyezi Mungu peke yake ndio uthibitisho wa kweli wa mumin na ndio msitari unaogawanya baina ya mumin wa kweli na yule mwenye kuleta njozi za kuwa ni mumin, kumbe si chochote.

Na tukamfidia kwa dhabihu adhimu.

Makusudio ya dhabihu hapa ni mnyama wa kuchinjwa. Inasemkana alikuwa kondoo, wengine wakasema ni mbuzi. Sisi hatuna majukumu ya kujua aina ya fidia ilivyokuwa, wala jambo hilo halina uhusiano wa mbali au karibu na maisha yetu.

La kushangaza zaidi ni kauli ya aliyesema kuwa alikuwa ni kondoo aliyelisha Peponi miaka arubaini na kwamba Ibrahim(a.s ) alimpa Ibilisi wengu na kordani zake. Ikiwa alichunga Peponi miaka arubaini, basi uzito wake utakuwaje?

Na tukamwachia kwa walio baadaye. Amani kwa Ibrahim. Hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema. Hakika yeye ni katika waja wetu walio waumini.

Zimetangulia Aya hizi kwa herufi zake kwenye sura hii Aya (78 – 81).

Na tukambashiria Is-haq, Nabii miongoni mwa watu wema. Na tukambarikia yeye na Is-haq.

Bishara hii kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa Ibrahim kupata mtoto wa pili, ni malipo ya subira yake na kumtoa mtoto wake kwa ajili ya kumtii Mwenyezi Mungu.

Katika Kamusi ya Kitabu kitakatifu imeandikwa kuwa Sara alimzaa Is-haq akiwa na mika 90 na Ibrahim akiwa na miaka mia, na kwamba maana ya neno Is-haq katika Lugha ya Kiebrania ni kucheka. Ama Hajar alimzaa Ismail na umri wa Ibrahim ni miaka 86.

Na miongoni mwa dhuriya zao yuko mwema na mwenye kudhulumu nafsi yake waziwazi.

Mwema katika kizazi hiki ni yule anayefuata mila ya Ibrahim na mwenye kujidhulumu ni yule aliyeiwacha mila hiyo.

JE, DHABIHU ALIKUWA ISMAIL AU IS-HAQ?

Baadhi wamesema kuwa mtoto wa Ibrahim aliyetakiwa kuchinjwa ni Is-haq na wala siye Ismail. Kauli hii haina rejea isipokuwa Hadith za kiisrail za Ka’bul-ahbar na hasadi ya mayahudi kwa watoto wa Ismail. Hili si la kushangaza kwa waisrail. Ama dalili za kuwa aliyetaka kuchinjwa ni Ismail ni kama zifuatazo:-

Kwanza : Kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Basi tukambashiria mwana aliye mpole. Basi alipofika makamo ya kuhangaika pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja,’ inafahamisha waziwazi kuwa aliyebashiriwa, aliyehangaika naye na aliyetaka kuchinjwa ni mtu mmoja tu ambaye ni mtoto wa kwanza wa Ibrahim. Na mtoto wa kwanza ni Ismail, kwa maafikano ya waislamu, wanaswara na wayahudi.

Biblia inasema: “Naye Abramu alikuwa mtu wa miaka themanini na sita, hapo Hajir alipomzalia Abramu Ishmael”

Mwanzo 16:16. Pia inasema: “Ndipo Ibrahim akaanguka kifudifidi akacheka, akasema moyoni, Je! Mtu wa umri wa miaka, kwake atazaliwa mtoto? Naye Sara mwenye umri wa miaka tisini atazaa? Tukiunganisha vifungu viwili hivi, maana yanayopatikana ni kuwa Ismail ni mkubwa wa Is-haq kwa mika 14.

Pili : Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Na tukambashiria Is-haq, Nabii miongoni mwa watu wema,’ ambapo bishara hii ilikuwa ni malipo ya utiifu wake Ibrahim kwa Mungu kumchinja mwanawe. Bila shaka malipo yanakuja baada ya kazi. Kwa hiyo Is-haq alipatikana baada ya Ismail.

Tatu : Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Tukampa bishara ya Is-haq na baada ya Is-haq, Ya’qub.” Juz. 12 (11: 71). Vipi Mwenyezi Mungu (s.w.t) atoe bishara ya Is-haq kumzaa Ya’qub kisha wakati huohuo aamr- ishwe achinjwe, kabla ya kupatikana Ya’qub?

Nne : Kama aliyetaka kuchinjwa alikuwa ni Is-haq basi ingelazimika kuchinja, kufanya sa’yi na kupiga vikuta vya shetani kuwe kwenye ardhi ya Sham alipokuwa Sara na mwanawe Is-haq na wala kusingekuwa Makka alipokuwepo Hajar na mwanawe Ismail.

وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ﴿١١٤﴾

114. Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Harun.

وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ﴿١١٥﴾

115. Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na tabu kubwa.

وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ﴿١١٦﴾

116. Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio washindi.

وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ ﴿١١٧﴾

117. Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.

وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ ﴿١١٨﴾

118. Na tukawaongoza kwenye njia Iliyonyooka.

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ ﴿١١٩﴾

119. Na tukawachia kwa walio baadaye.

سَلَامٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ﴿١٢٠﴾

120. Amani kwa Musa na Harun.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١٢١﴾

121. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٢٢﴾

122. Hakika hao ni katika waja wetu walio waumini.

وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٢٣﴾

123. Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٢٤﴾

124. Alipowaambia watu wake: Hamna takua?

أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ ﴿١٢٥﴾

125. Mnamwomba Baa’li na mnamwacha Mbora wa waumbaji.

اللَّـهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٢٦﴾

126. Mwenyezi Mungu, Mola wenu na Mola wa baba zenu wa zamani?

فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ﴿١٢٧﴾

127. Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa.

إِلَّا عِبَادَ اللَّـهِ الْمُخْلَصِينَ ﴿١٢٨﴾

128. Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa.

وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ﴿١٢٩﴾

129. Na tukamwachia kwa walio baadaye.

سَلَامٌ عَلَىٰ إِلْ يَاسِينَ ﴿١٣٠﴾

130. Amani kwa Ilyasin.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ﴿١٣١﴾

131. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema.

إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ﴿١٣٢﴾

132. Hakika yeye ni katika waja wetu walio waumini.

MUSA NA ILYAS

Aya 114 – 132

MAANA

Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Harun.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimfanyia hisani Musa na Harun kwa utume, utajo wa kudumu na kuwashinda maadui. Utume hauwi kwa bidii ya mtu au kazi yake; isipokuwa unatokana na uteuzi wa Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Mwenyezi Mungu ndiye Mjuzi zaidi wa kujua mahali anapoweka ujumbe wake.” Juz. 8 (6:124).

Ndio maana utume haufungamani na taklifa yoyote. Kwa hiyo mtu haambiwi kuwa Mtume; kama anavyoambiwa kuwa na takua.

Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na tabu kubwa.

Tabia ya mayahudi ni kukubali kila kitu kwa ajili ya mali; ikibidi hata udhalili na aibu. Hivi ndivyo ilivyowazungumzia historia yao.

Firauni aliwafanya watumwa na hawakufanya lolote mpaka Mwenyezi Mungu alipowapa msaada wa Musa kuwatoa kwenye tabu na shida na kupata faraja.

Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio washindi.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimwangamiza Firauni na askari wake, waisrail wakakomboka na utumwa na udhalili.

Na tukawapa wawili hao Kitabu kinachobainisha.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) alimteremshia Musa na Harun Tawrat ndani yake mkiwa na hukumu zilizo waziwazi.

Na tukawaongoza kwenye njia Iliyonyooka, njia ya haki na uadilifu.Na tukawachia kwa walio baadaye, utajo mzuri na sifa njema.Amani kwa Musa na Harun kutoka kwa Mwenyezi Mungu hapa duniani na akhera.

Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema. Hakika hao ni katika waja wetu walio waumini.

Yaani malipo ya wema ni wema tu. Yamepita maelezo kuhusu Musa na Harun katika Aya nyingi.

Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.

Wafasiri wanasema kwamba Ilyas ni mmoja wa manabii wa Bani Israil na kwamba nasabu yake inakomea kwa Harun. Kwenye Tafsiri nyingi imeelezwa kuwa Ilyas huyu ndiye Idris aliyetajwa kwenye Juz. 16 (19:56) na Juz. 17 (21:85).

Katika Kamusi ya Kitabu kitakatifu imeelezwa kuwa neno Iliy ni la kiebrania lenye maana ya Mungu wangu na neno la Kigiriki lenye maana hii ni Ilyas. Pia mara nyingine hutumika katika lugha ya Kiarabu.

Alipowaambia watu wake: Hamna takua?

Aliwaongoza watu wake kwenye tawhidi na kuwahadharisha na shirki, kama walivyofanya mitume wengine.

Mnamwomba Baa’li na mnamwacha Mbora wa waumbaji, Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?

Baa’ali ni jina la sanamu, kama unavyofahamisha mfumo wa Aya. Kwenye Kamusi ya Kitabu kitakatifu imeandikwa: “Baa’ali ni jina la Kikanaa’ni na maana yake ni Mola wa ahadi.”

Watu wa Ilyas waliabudu Baa’al, kama walivyoabudu masanamu waliokuwa kabla yao; ndio akawalingania kwenye tawhid; kama alivyofanya Nuh, Ibrahim, Musa na mitume wengineo.

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa. Yaani walokadhibisha mwito wake, watahudhurishwa Siku ya Kiyama kwa ajili ya hisabu na adhabu.

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliosafishwa ambao waliitika mwito wa Ilyas. Hakika wao wataokoka na adhabu na wana wao malipo mema.

Na tukamwachia kwa walio baadaye utajo mwema.

Amani kwa Ilyasin. Kwa hakika hivyo ndivyo tunavyowalipa watendao mema. Hakika yeye ni katika waja wetu walio waumini.

Kundi la wafasiri wamesema kuwa jina la baba yake Ilyas ni Yasin na kwamba makusudio ya Ilyasin ni Ilyas hasa, kwa sababu mtoto ni katika watu wa baba.

Vyoyvote iwavyo, makusudio ya Ilyasin hapa ni Ilyas kutokana na mfumo wa mtiririko wa Aya. Kwani Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwenye Aya za nyuma amamtaja Nuh kisha akasema: ‘Amani kwa Nuh,’ akamtaja Ibrahim, akasema: ‘Amani kwa Ibrahim.

Vile vile alipomtaja Musa na Harun. Kisha alipomtaja Ilyas kuwa ni katika Mitume alifuatishia kwa kusema: ‘Amani kwa Ilyasin’ ikajulikna kwamba makusudio ni Ilyas tu.

20

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٣٣﴾

133. Na hakika Lut bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ﴿١٣٤﴾

134. Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote.

إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ﴿١٣٥﴾

135. Isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma.

ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ ﴿١٣٦﴾

136. Kisha tukawaangamiza wale wengine.

وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ ﴿١٣٧﴾

137. Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi.

وَبِاللَّيْلِ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ﴿١٣٨﴾

138. Na usiku. Basi je! Hamtii akilini?

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٣٩﴾

139. Na hakika Yunus bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ﴿١٤٠﴾

140. Alipokimbia katika jahazi lililosheheni.

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ ﴿١٤١﴾

141. Wakapiga kura, akawa katika walioshindwa.

فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ ﴿١٤٢﴾

142. Basi samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulau- miwa.

فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ ﴿١٤٣﴾

143. Na lau asingelikuwa ni katika wanaomtakasa (Mwenyezi Mungu),

لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ﴿١٤٤﴾

144. Bila ya shaka angelikaa tumboni mwake mpaka siku ya kufufuliwa.

فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ ﴿١٤٥﴾

145. Kisha tulimtupa ufukweni patupu, hali ya kuwa mgonjwa.

وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ ﴿١٤٦﴾

136. Na tukamuoteshea mmea wa mung’unye.

وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ ﴿١٤٧﴾

147. Na tulimtuma kwa watu elfu mia moja (laki moja) au zaidi.

فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ ﴿١٤٨﴾

148. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

LUT NA YUNUS

Aya 133 – 148

MAANA

Na hakika Lut bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume. Tulipomwokoa yeye na ahali zake wote; isipokuwa mwanamke mkongwe katika wale waliobakia nyuma. Kisha tukawaangamiza wale wengine.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:80-84), Juz. 12 (11:77 – 83) na Juz. 20 (29:28 – 35).

Maajabu ni yale yaliyoandikwa katika Biblia Mwanzo, (19:30 – 37), kwamba Lut alikuwa na mabinti wawili, wakamlewesha pombe baba yao, kisha akawaingilia, kila mmoja akazaa mtoto wa kiume.

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi na usiku. Basi je! Hamtii akilini?

Waarabu walikuwa wakisafiri kutoka Hijaz kwenda Sham kwa ajili ya biashara na mengineyo. Njia yao ilikuwa ikipitia ardhi ya kaumu ya Lut. Kwa hiyo walikuwa wakipitia huko asubuhi na jioni wanapokwenda na kurudi safari yao.

Walikuwa wakiona athari ya maangamizi, Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawahadharisha washirikina wa kiarabu waliomkadhibisha Muhammad(s.a.w. w ) , kwa kuwaambia kuwa hampati mazingatio kwa majumba ya kaumu ya Lut yalivyokuwa matupu? Hamhofii kuwafika yaliyowafika wao?

Na hakika Yunus bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.

Yunus huyu ndiye aliyetajwa katika Juz. 17 (21: 87): “Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhabika” na ndiye aliyetajwa katika (68:48): “Wala usiwe kama mmezwa na samaki.”

Mfasiri mmoja amesema: “Yunus ni katika watu wa mji wa Neinawa ambao ulikuwa ni mji mkuu wa Waashwar (Assyrian) na kwamba ulikuwa mashuhuri sana kwenye karne kadhaa. Ulikuwa kwenye ukanda wa mashariki wa mto Dijla (Tigris) na wakazi wake walikuwa wakiabudu Ashtar au Ashtarut (Ashrot au Asterot) ambaye alikuwa akiabudiwa na watu wengi sana wa zamani[8] .”

Alipokimbia katika jahazi liliosheheni. Wakapiga kura, akawa katika walioshindwa.

Yunus aliwalingania watu wake kwenye ibada ya Mwenyezi Mungu, lakini hawakumwitikia. Basi akaona dhiki sana moyoni mwake, akaamua kuhama kwa hasira. Alifika ufukweni akaona jahazi limesheheni watu na mizigo akawaomba ajiunge nao kwenye msafara.

Walipofika katikati ya bahari jahazi likataka kuzama; wakona lazima wamtupe mmoja wao baharini ili wapate kuokoka. Ndipo wakamua kupiga kura, iliyomuangukia Yunus, naye akaamua kujitupa baharini.Basi samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa, kwa vile hakuvumilia adha ya watu wake kama walivyovumilia manabii wengine.

Na lau asingelikuwa ni katika wanaomtakasa (Mwenyezi Mungu), Bila ya shaka angelikaa tumboni mwake mpaka siku ya kufufuliwa.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amebainisha aina ya kutakasa huko (tasbihi) pale aliposema:

فَنَادَىٰ فِي الظُّلُمَاتِ أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾

“Basi aliita katika giza (yaani katika tumbo la samaki) kwamba hapana Mola isipokuwa wewe. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu” Juz. 17 (21:87).

Basi Mwenyezi Mungu akamkubalia mwito wake na akamtoa kwenye jela yake inayotembea baharini. Lau sikukimbilia kwa Mwenyezi Mungu kwa ikhlasi, angelibakia ndani ya jela maisha mpaka Kiyama.

Kisha tulimtupa ufukweni patupu, hali yakuwa mgonjwa. Na tukamuoteshea mmea wa mung’unye.

Wanasema alitoka tumboni mwa samaki akiwa kama kifaranga kisicho na manyoya kikiwa mbungani peke yake. Ndipo Mwenyezi Mungu akamuoteshea mmung’unye ili ajisitiri na majani yake.

Na tulimtuma kwa watu elfu mia moja (laki moja) au zaidi. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.

Mwenyezi Mungu alimtuma kwa watu hao, mwanzoni, wakampinga. Alipowaacha kwa kukasirika, walihofia wasifikwe na balaa na adhabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Basi wakamwamini Mwenyezi Mungu na wakamtaka msamaha na rehema. Akawasamehe na maangamizi. Yunus akawarudia na wakafurahi kwa kufika kwake naye akafurahi kwa imani yao.

Tazama Juz. 11 (10:98 – 100) kifungu cha ‘Kisa’ na Juz. 17 (21:87).

فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ ﴿١٤٩﴾

149. Basi waulize: Ati Mola wako ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wana watoto wa kiume?

أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ ﴿١٥٠﴾

150. Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ ﴿١٥١﴾

151. Ehe! Hakika wao kwa kujitenga kwao wanasema.

وَلَدَ اللَّـهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ﴿١٥٢﴾

152. Mwenyezi Mungu amezaa! Na hakika bila ya shaka hao ni waongo!

أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ ﴿١٥٣﴾

153. Je, amechagua watoto wa kike kuliko wa kiume?

مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ﴿١٥٤﴾

154. Mna nini? Vipi mnahukumu?

أَفَلَا تَذَكَّرُونَ ﴿١٥٥﴾

155. Hamkumbuki?

أَمْ لَكُمْ سُلْطَانٌ مُّبِينٌ ﴿١٥٦﴾

156. Au mnayo hoja iliyo wazi? Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.

فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿١٥٧﴾

157. Na wameweka nasaba baina yake na majini.

وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ﴿١٥٨﴾

158. Na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

سُبْحَانَ اللَّـهِ عَمَّا يَصِفُونَ ﴿١٥٩﴾

159. Ametakasika Mwenyezi Mungu na yale wanayomsifu.

إِلَّا عِبَادَ اللَّـهِ الْمُخْلَصِينَ ﴿١٦٠﴾

160. Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliotakaswa.

ATI MOLA WAKO ANA WATOTO WA KIKE NA WAO WANA WATOTO WA KIUME?

Aya 149 – 160

MAANA

Basi waulize: Ati Mola wako ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wana watoto wa kiume? Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?

Qur’an ni hoja ya kihistoria isiyokubali shaka wala mjadala. Nayo imeeleza kuwa baadhi ya makabila yalikuwa yakisema kuwa Mwenyezi Mungu amewafanya Malaika kuwa ni wanawake; kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawarudi kuwa huko ni kuvurumisha na kupofuka na haki, kwa sababu wao hawajui chochote kuhusiana na Malaika.

Katika maana ya hayo ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na wamewafanya Malaika ambao ni waja wa Mwingi wa rehema kuwa wanawake. Je, wameshuhudia kuumbwa kwao?” (43:19) Vile vile katika Juz. 15 (17:40).

Ehe! Hakika wao kwa kujitenga kwao wanasema: Mwenyezi Mungu amezaa! Na hakika bila ya shaka hao ni waongo!

Neno kujitenga tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu ifk, ambalo mara nyingi hutumika kwa maana ya uzushi, lakini hapa limekuja kwa maana ya kujitenga ambayo pia ni miongoni mwa maana yake; kama lilivyotumika katika Aya isemayo:

قَالُوا أَجِئْتَنَا لِتَأْفِكَنَا عَنْ آلِهَتِنَا ﴿٢٢﴾

“Je, umetujia ili ututenge na miungu yetu?” (46:22).

Kwa hiyo maana yake hapa ni kuwa wao kwa sababu ya kujitenga na Tawhid na kuifuata shirki walisema kuwa Mwenyezi Mungu ana mtoto. Hakuna mwenye shaka kuwa wao ni waongo katika kauli hii.

Je, amechagua watoto wa kike kuliko wa kiume?

Yaani Mungu achague wa kike tu na wa kiume awachie nyinyi; kama mnavyodai. “Na wamemfanyia Mwenyezi Mungu mabinti. Ametakata na hayo! Na hali wao hupata wanavyovitamani.

Na mmoja wao akibashiriwa msichana uso wake unasawijika naye amejaa chuki.” Juz. 14 (16: 56 -57).

Mna nini? Vipi mnahukumu yaliyo mbali na macho na akili zenu?Hamkumbuki mkakoma na shirki na kauli za uzushi,na hali Mwenyezi Mungu amewakumbusha na akawahadharisha kupitia kwa Mtume wake mwenye amana ya wahyi wake?

Au mnayo hoja iliyo wazi? Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.

Onyesheni hoja ya kiakili au ya kinukuu kuwa Mwenyezi Mungu ame- wafanya Malaika ni wanawake.

Na wameweka nasaba baina yake na majini.

Wametofautiana wafasiri kuhusu maana ya Aya hii. Tunavyofahamu sisi, kutokana na dhahiri yake ni kuwa washrikina walimnasibishia Mwenyezi Mungu mtukufu mahusiano ya uzazi na majini, kama walivyomnasibishia Malaika.

Kuna tafsiri iliyonukuliwa kutoka kwa Mujahid na Muqatil kwamba Kinana na Khuzaa walisema kuwa Mwenyezi Mungu alitaka uchumba kwa mabwana wa kijini nao wakamuoza binti wao wa ukoo wa kilodi, na ndio akazaa naye Malaika!

Na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.

Vipi atakuwa na nasaba na majini na hali wao wanajua kuwa Mungu ndiye aliyewaumba na kwamba wao watafufuliwa na kuulizwa yale waliyokuwa wakiyafanya.

Ametakasika Mwenyezi Mungu na yale wanayomsifu, na ametukuka sana na wanayoyasema wenye kufananiza na wapinzani

Isipokuwa waja wa Mwenyezi Mungu waliotakaswa, kwani hakika wao wanamtakasa na shirki na kuwa na mtoto na wanamtakasa kwa kauli na vitendo na yeye Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawalipa kwa imani yao na ikhlasi yao kwa yale mema waliyoyafanya.

21

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MOJA

فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ ﴿١٦١﴾

161. Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu.

مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَاتِنِينَ ﴿١٦٢﴾

162. Hamuwezi kuwapoteza.

إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ الْجَحِيمِ ﴿١٦٣﴾

163. Isipokuwa yule atakayeingia Motoni.

وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ﴿١٦٤﴾

164. Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalum.

وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ﴿١٦٥﴾

165. Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.

وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ ﴿١٦٦﴾

166. Na hakika sisi ndio wenye kusabihi.

وَإِن كَانُوا لَيَقُولُونَ ﴿١٦٧﴾

Na hakika wao walikuwa wakisema.

لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ ﴿١٦٨﴾

168. Tungelikuwa na kumbukumbu ya wa zamani.

لَكُنَّا عِبَادَ اللَّـهِ الْمُخْلَصِينَ ﴿١٦٩﴾

169. Bila shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu waliotakaswa.

فَكَفَرُوا بِهِ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ ﴿١٧٠﴾

180. Lakini waliikataa. Basi watakuja jua.

NYINYI NA MNAOWAABUDU

Aya 161 – 170

MAANA

Basi hakika nyinyi na mnaowaabudu hamuwezi kuwapoteza; isipokuwa yule atakayeingia Motoni.

Wanaambiwa washirikina. Maana ni kuwa, enyi washirikina! Hakuna atakayeitikia upotevu wenu na ibada yenu ya masanamu isipokuwa wale walioacha njia ya uongofu inayopelekea radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu zake na akafuata njia ya upotevu, inayokomea kwenye hasira za Mwenyezi Mungu na adhabu yake.

Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalum.

Haya ni maneno ya Malaika wakiwarudi washirikina waliosema kuwa Malaika ni mabinti wa Mwenyezi Mungu na washirikina wakachaguliwa watoto wa kiume.

Maana ni kuwa sisi sote ni waja wa Mwenyezi Mungu tunamtakasa kwa sifa njema zake. Na kila mmoja katika sisi ana wadhifa wake wa kiiibada haupetuki.

Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu. Na hakika sisi ndio wenye kusabihi.

Miongoni mwetu wako waliosimama safu kwa ibada na wengine hawachoki na dhikri na tasbihi. Kuna Hadith inayosema: “Katika wao kuna waliorukui hawasimami na miongoni mwao wapo waliosujudi hawainui vichwa vyao.”

Na hakika wao walikuwa wakisema: Tungelikuwa na kumbukumbu ya wa zamani, bila shaka tungelikuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu waliotakaswa.

Waliokuwa wakisema ni washirikina wa kiarabu ambao walimfanya Mwenyezi kuwa ana mabinti Malaika na wakamfanyia nasaba baina yake na majini. Maana ni kuwa washirikina walikuwa wakisema kabla ya kuja Muhammad(s.a.w. w ) na Qur’an, kwamba lau kitawajia kitabu kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa haki, watakiamini na watamwabudu Mwenyezi Mungu kwa kumtakasia Yeye dini.

Lakini yalipowajia yale waliyokuwa wakiyatamani walizidi jeuri na kuikimbia haki. Ndio akaishiria Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa kusema:

Lakini waliikataa. Basi watakuja jua, itakavyokuwa adhabu.

وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ ﴿١٧١﴾

171. Na bila ya shaka neno letu lilikwishatangulia kwa waja wetu waliotumwa.

إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ ﴿١٧٢﴾

172. Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.

وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ ﴿١٧٣﴾

173. Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda.

فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ﴿١٧٤﴾

174. Basi waache kwa muda.

وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ﴿١٧٥﴾

175. Na uwaone, nao wataona.

أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ ﴿١٧٦﴾

176. Je, wanaihimiza adhabu yetu?

فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ ﴿١٧٧﴾

177. Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.

وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ﴿١٧٨﴾

178. Na waache kwa muda.

وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ﴿١٧٩﴾

179. Na uone, nao wataona.

سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ﴿١٨٠﴾

180. Ametakasika Mola Wako, Mola Mwenye enzi, na yale wanayomsifu.

وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ ﴿١٨١﴾

181. Na Salamu juu ya Mitume.

وَالْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٨٢﴾

182. Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu wote.

JESHI LETU NDILO LITAKALOSHINDA

Aya 171 – 182

MAANA

Na bila ya shaka neno letu lilikwishatangulia kwa waja wetu waliotumwa. Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakaonusuriwa.

Na kwamba jeshi letu ndilo litakaloshinda duniani kwa hoja na dalili. Imam Ali(a.s ) anasema:“Si mshindi mwenye kushinda kwa dhambi na mwenye kushinda kwa shari ndiye aliyeshindwa. Ama huko Akhera hakuna hila wala nguvu kwa wabatilifu.”

Ar-razi anasema: “Ushindi unaweza kuwa kwa hoja na unaweza kuwa kwa dola na utawala na pia unaweza kuwa kwa kudumu na kuwa imara kwenye haki.

Kwa hiyo mumin hata kama wakati mwingine anashindwa, kwa sababu ya udhaifu na hali ya dunia, lakini bado yeye ndiye anayekuwa mshindi. Si lazima kusemwa kuwa Mitume waliuawa na waumini wengi wakashindwa.”

Kauli ya Razi, kuwa ushindi unaweza kuwa kwa uimara kwenye haki, inaweza kuthibitishwa na ukakamavu wa waarabu leo, kukataa kwao kujisalimisha na azma yao ya kumzuia adui, kwa namna yoyote itakavyokuwa dunia na pamoja na kuonekana kuwa ukoloni na uzayuni unawashinda.

Yametangulia maelezo ya jinsi Mwenyezi Mungu Mtukufu anavyowalinda wale walioamini katika Juz. 17 (22:38).

Basi waache kwa muda na uwaone, nao wataona.

Anaambiwa Muhammad(s.a.w. w ) aachane na washirikina kisha angoje kidogo atawaona watakavyosalimu amri wakiwa wanyonge. Na kweli haya yalitokea pamoja na majeshi yao makubwa na vikosi vingi dhidi ya Mtume.

Je, wanaihimiza adhabu yetu?

Hili ni jawabu la kauli ya washirikina waliposema: Tuletee uliyotuahidi. Maana ya jawabu ni kuwa vipi mnahimiza adhabu ya Mwenyezi Mungu na hali mnajua kuwa ikiwashukia hamtaiweza wala hamtaweza kuikimbia.

Basi itakaposhuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walioonywa.

Makusudio ya uwanajani kwao ni majumbani mwao na asubuhi ni siku ya adhabu. Maana ni kuwa siku atakayowaadhibu Mwenyezi Mungu baada ya kuwaonya itakuwa mbaya sana kwao.

Na waache kwa muda na uone, nao wataona.

Mwenyezi Mungu amelikariri kwa kutia msisitizo wa kutekeleza ahadi yake na kwamba itakuwa tu.

Ametakasika Mola Wako, Mola Mwenye enzi, na yale wanayomsifu. Na Salamu juu ya Mitume. Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola wa walimwengu wote.

Mwenyezi Mungu ameishiliza Sura hii kwa kujitakasa na yale yasiokuwa laiki ya ukuu wake, kwa vile kwenye Sura hii amewazungumzia washirikina.

Akajisifu kwa enzi kwa vile Yeye ni muweza wa kila kitu na akajisifu kwa sifa njema kwa sababu yeye ndiye mwenye kunemesha mwenye fadhila. Na salamu kwa mitume, kwa sababu wao walitekeleza amana kwa ikhlasi na wakaibeba. Kwa hiyo basi hakuna enzi wala sifa ila kwa yule aliyemuenzi Mwenyezi Mungu na akamtii.

MWISHO WA SURA YA THELATHINI NA SABA: SURAT AS-SAFFAT