TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI15%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 22113 / Pakua: 3996
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea. Hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka kwa lugha ya kiswahili hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasayansi kama kina Enstein, wasanii kama Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146), Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama. Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu Jabal amil 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa.” Kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

Mwendelezo wa Sura Ya Thelathini Na Tisa: Surat Az-Zumar.

فَمَنْ أَظْلَمُ مِمَّن كَذَبَ عَلَى اللَّـهِ وَكَذَّبَ بِالصِّدْقِ إِذْ جَاءَهُ أَلَيْسَ فِي جَهَنَّمَ مَثْوًى لِّلْكَافِرِينَ ﴿٣٢﴾

32. Basi ni nani dhalimu zaidi kuliko yule anayemzulia uwongo Mwenyezi Mungu, na kuikadhibisha kweli imfikiapo? Je! Siyo katika Jahannamu makazi ya makafiri?

وَالَّذِي جَاءَ بِالصِّدْقِ وَصَدَّقَ بِهِ أُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُتَّقُونَ ﴿٣٣﴾

33. Na aliyeleta ukweli na aliyeusadikisha, hao ndio wenye takua.

لَهُم مَّا يَشَاءُونَ عِندَ رَبِّهِمْ ذَٰلِكَ جَزَاءُ الْمُحْسِنِينَ ﴿٣٤﴾

34. Watapata watakachotaka kwa Mola wao. Hayo ndiyo malipo ya watendao mema.

لِيُكَفِّرَ اللَّـهُ عَنْهُمْ أَسْوَأَ الَّذِي عَمِلُوا وَيَجْزِيَهُمْ أَجْرَهُم بِأَحْسَنِ الَّذِي كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٣٥﴾

35. Ili Mwenyezi Mungu awafutie uovu zaidi walioufanya na awalipe ujira wao kwa wema zaidi ya waliokuwa wakiufanya.

أَلَيْسَ اللَّـهُ بِكَافٍ عَبْدَهُ وَيُخَوِّفُونَكَ بِالَّذِينَ مِن دُونِهِ وَمَن يُضْلِلِ اللَّـهُ فَمَا لَهُ مِنْ هَادٍ ﴿٣٦﴾

36. Je! Mwenyezi Mungu si wa kumtoshea mja wake? Na wanakutishia kwa wasiokuwa Yeye! Na anayepotezwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumwongoza.

وَمَن يَهْدِ اللَّـهُ فَمَا لَهُ مِن مُّضِلٍّ أَلَيْسَ اللَّـهُ بِعَزِيزٍ ذِي انتِقَامٍ ﴿٣٧﴾

37. Na anayeongozwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumpoteza. Je! Mwenyezi Mungu si Mwenye nguvu anayeweza kulipiza.

JE, MWENYEZI MUNGU SI WA KUMTOSHEA MJA WAKE?

Aya 32 – 37

MAANA

Basi ni nani dhalimu zaidi kuliko yule anayemzulia uwongo Mwenyezi Mungu, akamfanyia washirika au mtoto?

Kauli mbaya zaidi ni uwongo na uwongo mbaya zaidi ni kumzulia Mwenyezi Mungu na Mtume wake.

Na kuikadhibisha kweli imfikiapo kutoka kwa Mwenyezi Mungu kupitia ulimi wa Mtume wake.

Hivi ndivyo walivyo watu wa masilahi na manufaa, mahali popote na wakati wowote, wanaukana ukweli na kuusadikisha uwongo. Kwa sababu masilahi yao yanakuwa kwa uzushi na ubatilifu. Miongoni mwa niliyoyasoma kuhusiana na haya ni kuwa uwongo mkubwa zaidi ni kusema mwongo: “Mwenyezi Mungu anajua kuwa mimi ni mkweli.”

Je! Siyo katika Jahannamu makazi ya makafiri ? Bila shaka ndio makazi yao na makazi ya kila taghuti muovu.

Na aliyeleta ukweli na aliyeusadikisha, hao ndio wenye takua.

Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alikuja na ukweli kutoka kwa Mwenyezi Mungu na waislamu wakausadikihsa. Hao mbele ya Mwenyezi Mungu ndio watu wema ikiwa watayaogopa aliyoyakataza; vinginevyo kusadikisha bila matendo hakuna maana yoyote.

Watapata watakachotaka kwa Mola wao. Hayo ndiyo malipo ya watendao mema.

Yaani wale wanaogopa aliyoyaharamisha Mwenyezi Mungu. Kwa sababu bado mazungumzo yanawahusu wao. Mwenyezi Mungu hakuanisha malipo, bali amewaachia vile watakavyo.

Ili Mwenyezi Mungu awafutie uovu zaidi walioufanya na awalipe ujira wao kwa wema zaidi ya waliokuwa wakiufanya.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasamehe madhambi yote, makubwa na madogo, kwa yule mwenye kutubia, akaamini na akatenda mema; na atawalipa wale wanaomtii na kushukuru neema zake kwa wema mkubwa kuliko vile walivyokuwa wakitii na kushukuru.

Je! Mwenyezi Mungu si wa kumtoshea mja wake? Na wanakutishia kwa wasio kuwa Yeye!

Makusudio ya mja wake hapa ni Muhammad(s.a.w. w ) . Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamkinga na shari ya anayemkusudia shari. Makusudio ya wale wasiokuwa yeye ni masanamu. Kundi la wafasiri wamesema: “Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alipoyataja masanamu kwa ubaya, makuraishi walisema: Muhammad asipokoma kuwataja vibaya miungu wetu, basi tutamshtakia kwao apatwe na majanga.”

Ndipo Mwenyezi Mungu akateremsha Aya hii. Hili haliko mbali na akili za wajinga na wapumbavu. Hakuna mwenye shaka kuwa Mwenyezi Mungu anamtoshea na kumkinga mja wake na mtume wake.

Na anayepotezwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumwongoza. Na anayeongozwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumpoteza.

Wakati tukifasiri Aya ya 23 ya Sura hii tuliyo nayo, kwenye Juz. 23, na kwengineko, tulisema kuwa: Mwenyezi Mungu, anampoteza yule mwenye kufuata njia ya upotevu kwa hiyari yake, na anamwongoza mwenye kuchagua uongofu kwa hiyari yake na akafuata njia yake.

Je! Mwenyezi Mungu si Mwenye nguvu anayeweza kulipiza anayekufuru na akadhulumu kwa hiyari yake tena baada ya kupewa hoja?

وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ اللَّـهُ قُلْ أَفَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ إِنْ أَرَادَنِيَ اللَّـهُ بِضُرٍّ هَلْ هُنَّ كَاشِفَاتُ ضُرِّهِ أَوْ أَرَادَنِي بِرَحْمَةٍ هَلْ هُنَّ مُمْسِكَاتُ رَحْمَتِهِ قُلْ حَسْبِيَ اللَّـهُ عَلَيْهِ يَتَوَكَّلُ الْمُتَوَكِّلُونَ ﴿٣٨﴾

38. Na ukiwauliza: Ni nani aliyeziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu. Sema: Je! Mnawaonaje wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa Mwenyezi Mungu akitaka kunidhuru, wao wanaweza kuniondolea dhara yake? Au akitaka kunirehemu, je, wao wanaweza kuzuia rehema yake? Sema: Tosha yangu ni Mwenyezi Mungu. Kwake wategemee wanaotegemea.

قُلْ يَا قَوْمِ اعْمَلُوا عَلَىٰ مَكَانَتِكُمْ إِنِّي عَامِلٌ فَسَوْفَ تَعْلَمُونَ ﴿٣٩﴾

39. Sema: Enyi watu wangu! Fanyeni muwezavyo, mimi pia nafanya. Basi punde mtajua.

مَن يَأْتِيهِ عَذَابٌ يُخْزِيهِ وَيَحِلُّ عَلَيْهِ عَذَابٌ مُّقِيمٌ ﴿٤٠﴾

40. Ni nani itakayemfikia adhabu ya kumhizi, na itakayemshukia adhabu ya kuendelea.

إِنَّا أَنزَلْنَا عَلَيْكَ الْكِتَابَ لِلنَّاسِ بِالْحَقِّ فَمَنِ اهْتَدَىٰ فَلِنَفْسِهِ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيْهَا وَمَا أَنتَ عَلَيْهِم بِوَكِيلٍ ﴿٤١﴾

41. Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu kwa ajili ya watu wote kwa Haki. Basi mwenye kuongoka ni kwa nafsi yake, na mwenye kupotoka bila ya shaka amepotoka kwa nafsi yake. Na wewe si mlinzi juu yao.

اللَّـهُ يَتَوَفَّى الْأَنفُسَ حِينَ مَوْتِهَا وَالَّتِي لَمْ تَمُتْ فِي مَنَامِهَا فَيُمْسِكُ الَّتِي قَضَىٰ عَلَيْهَا الْمَوْتَ وَيُرْسِلُ الْأُخْرَىٰ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ ﴿٤٢﴾

42. Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinapokufa. Na zile zisizokufa wakati wa kulala kwake. Huzishika zilizohuku- miwa kufa, na huzirudisha nyengine mpaka ufike wakati uliowekwa. Hakika katika hayo bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri.

أَمِ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ شُفَعَاءَ قُلْ أَوَلَوْ كَانُوا لَا يَمْلِكُونَ شَيْئًا وَلَا يَعْقِلُونَ ﴿٤٣﴾

43. Au ndio wamejifanyia waombezi badala ya Mwenyezi Mungu? Sema: Ingawa hawana mamlaka juu ya kitu chochote, wala hawatambui?

قُل لِّلَّـهِ الشَّفَاعَةُ جَمِيعًا لَّهُ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ثُمَّ إِلَيْهِ تُرْجَعُونَ ﴿٤٤﴾

44. Sema: Uombezi wote uko kwa Mwenyezi Mungu. Ni wake Yeye ufalme wa mbingu na ardhi. Kisha mtarejeshwa kwake.

وَإِذَا ذُكِرَ اللَّـهُ وَحْدَهُ اشْمَأَزَّتْ قُلُوبُ الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِالْآخِرَةِ وَإِذَا ذُكِرَ الَّذِينَ مِن دُونِهِ إِذَا هُمْ يَسْتَبْشِرُونَ ﴿٤٥﴾

45. Na anapotajwa Mwenyezi Mungu peke yake nyoyo za wasioiamini Akhera huchafuka. Na wanapotajwa walio kinyume naye basi wao hufurahi.

SEMA, TOSHA YANGU NI MWENYEZI MUNGU

Aya 38 – 45

MAANA

Na ukiwauliza: Ni nani aliyeziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Mwenyezi Mungu.

Jawabu lao hili linatokana na ufahamu wa kimaumbile aliowaumbia watu Mwenyezi Mungu. Kwa sababu hakuna tafsiri ya kupatikana ulimwengu isipokuwa kuweko Mwenyezi Mungu. Lakini walahidi wanasema: “Sisi hatuamini isipokuwa kwa kujaribu.” Ama maumbile hayo ni maneno ya upuzi. Nasi kwa upande wetu tunawauliza: ikiwa hamuamini isipokuwa majaribio, basi tuonyesheni majaribio yaliyowafahamisha kuwa hakuna Mungu.

Sisi hatuna shaka kuwa mwenye kupinga maumbile haya au kupinga mantiki yake, ndio ameupinga ubinadamu na kupinga yaliyo na thamani zaidi ndani ya binadamu; ukiwemo utashi na uwezo.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (29:66) na (31:25).

Sema: Je! Mnawaonaje wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu, ikiwa Mwenyezi Mungu akitaka kunidhuru, wao wanaweza kuniondolea dhara yake? Au akitaka kunirehemu, je, wao wanaweza kuzuia rehema yake?

Washirikina walimtishia Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa masanamu, ndio Mwenyezi Mungu akamwamrisha mtume wake awaambie kuwa masanamu yana uwezo gani kwangu na kwa mwengine? Je, yanaweza kunikinga ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kunidhuru? Au yanaweza kuzuia heri anazonitakia Mwenyezi Mungu? Hapana! Masanamu hayawezi kujikinga hata hayo yenyewe ikiwa binadamu anataka kuyavunja kwa shoka au kuyakanyaga kwa kiatu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:17) na Juz. 11 (10:107).

Sema: Tosha yangu ni Mwenyezi Mungu. Kwake wategemee wanaotegemea.

Ewe Muhammad! Mwambie anayekadhibisha risala yako kuwa mimi nataka msaada kwa Mwenyezi Mungu na kumtaka mwongozo; naye kwangu ni tosha kabisa! Na yeyote mwenye dhiki basi akimbilie kwake. Yeye ana tosha kuwa walii na msaidizi.

Sema: Enyi watu wangu! Fanyeni muwezavyo, mimi pia nafanya. Basi punde mtajua Ni nani itakayemfikia adhabu ya kumhizi, na itakayemshukia adhabu ya kuendelea.

Yaani kila mtu abaki kama alivyo, kisha tungoje mwisho utakuwaje. Bila shaka itakuwa ni hasara na moto kwenu nyinyi na baraka na neema kwetu sisi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:104) na Juz. 11 (10:93).

Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu kwa ajili ya watu wote kwa haki.

Basi fikisha bishara na maonyo, kwa niaba ya Mola wako, kwa kutumia Aya zake; wala usimwachie yoyote udhuru.

Basi mwenye kuongoka ni kwa nafsi yake, na mwenye kupotoka bila ya shaka amepotoka kwa nafsi yake. Na wewe si mlinzi juu yao.

Kila mtu ana majukumu yake na hisabu yake kwa muumba wake, wewe huna majukumu yoyote kwake baada ya kumfikishia na kumpa nasaha.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:104) na Juz. 11 (10:108).

Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinapokufa.

Wanaoamini maada wanasema: Mtu ni huu mwili tu, wala hakuna kitu kingine nyuma yake. Tazama kifungu ‘Wanaoamini maada na maisha baada ya mauti’ katika Juz. 13 (13:5-7). Na ‘Pamoja na wanaoamini maada’ katika Juz. 14 (16:78-83).

Waumini wanasema: Mtu ni mwili na roho, na kwamba roho ndiyo inayouendesha mwili na kuupangilia kwa amri ya Mwenyezi Mungu Mtukufu. Mauti ni kukatika mfungamano wa roho na mwili na roho kwenda kwa Mola wake: “Ewe nafsi iliyotua! Rejea kwa Mola wako hali ya kuwa uradhi mwenye kuridhiwa” (89:27-28).

Na hii ndio maana ya kuwa ‘Mwenyezi Mungu huzipokea roho zinapoku- fa,’ ni kuwa anazishika wakati wa kufa miili.

Na zile zisizokufa wakati wa kulala kwake.

Usingizi ni aina ya mauti au ni mauti kimajazi. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

وَهُوَ الَّذِي يَتَوَفَّاكُم بِاللَّيْلِ ﴿٦٠﴾

“Naye ndiye anayewafisha usiku.” Juz. 7 (6:60).

Mwenye Majmaul-bayan anasema: “Inayokufa wakati wa kulala ni nafsi ya upambanuzi na akili ambayo inafarikiana na mwenye kulala, kwa hiyo hawi na akili. Ama ile inayokufa wakati wa mauti ni nafsi ya uhai ambayo inaondoka na pumzi na mwenye kulala huwa anapumua. Kwa hiyo tofauti baina ya kushikwa usingizini na kwisha kwenye mauti ni kuwa usingizi ni kutokuwa macho na mauti ni kutokuwa hai. Na kushikwa usingizini roho inakuwa mwilini na kushikwa kwenye mauti ni roho kuondoka mwilini.”

Huzishika zilizohukumiwa kufa, na huzirudisha nyengine mpaka ufike wakati uliowekwa. Hakika katika hayo bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaofikiri.

Mwenyezi Mungu kuzishika roho wakati wa kufa mwili na wakati wa kulala. Zile zilizohukumiwa kufa zinabaki kwake na zile nyingine anaziachia zirudi mpaka muda maalum.

Umar bin Al-Khattab alisema: “Ajabu ni kuwa mtu anaota ndoto inakuwa kama kuchukua kwa mkono na anaota ndoto nyingine, lakini haiwi kitu.” Imam Ali bin Abi Twalib akamwambia: “Hakika Mwenyezi Mungu anazifisha nafsi zote. Ile unayoiona iko mbele yake basi ni ya ukweli na unayoiona baada ya kuiachia basi ni ya uwongo.” Akastaajabu Umar kutokana na kauli ya Imam.

Haya ameyanukuu Sheikh Al-Maraghi katika tafsiri yake kutoka kwa Abi Hatim na Ibn Mardawayh.

Au ndio wamejifanyia waombezi badala ya Mwenyezi Mungu? Sema: Ingawa hawana mamlaka juu ya kitu chochote, wala hawatambui?

Masanamu hayatambui kitu, wala hayawezi kujikinga na madhara, lakini pamoja na hayo washirikina wanawatarajia wawaombee mbele ya Mwenyezi Mungu. Hivi ndivyo wanavyofanya wajinga. Muombezi bora zaidi kwa Mwenyezi Mungu kwa wale wenye madhambi ni toba na kurejea kwa Mwenyezi Mungu.

Sema: Uombezi wote uko kwa Mwenyezi Mungu.

Yaani hakuna yoyote anayemiliki uombezi wowote isipokuwa yule aliyemilikishwa na Mwenyezi Mungu:

قُلْ إِنَّ الْأَمْرَ كُلَّهُ لِلَّـهِ ﴿١٥٤﴾

“Hakika mambo yote ni ya Mwenyezi Mungu” Juz.4 (3:154).

Ni wake Yeye ufalme wa mbingu na ardhi. Kisha mtarejeshwa kwake.

Mfano wake ni

وَلِلَّـهِ مُلْكُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ﴿١٧﴾

“ Na ni wa Mwenyezi Mungu ufalme wa mbingu na vilivyomo baina yake.” Juz. 6 (5:17).

Na anapotajwa Mwenyezi Mungu peke yake nyoyo za wasioiamini Akhera huchafuka. Na wanapotajwa wenginewe asiye kuwa Yeye basi wao hufurahi.

Washirikina walipokuwa wakisikia kauli ya hapana mola ispokuwa Mwenyezi Mungu (Lailaha illa llah) wanakimbia, na wanaposikia kusifiwa masanamu wanafurahi.

Hivi ndivyo walivyo wabatilifu wa zamani na wa sasa. Haiwapumbazi isipokuwa batili wala haiwatishi isipokuwa haki. Kwenye Nahjulbalagha, amesema: “Ambaye inakuwa uzito kwake kuambiwa haki au kuonyeshwa uadilifu, basi kuyatumia mawili hayo inakuwa uzito zaidi.”

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

قُلِ اللَّـهُمَّ فَاطِرَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ عَالِمَ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ أَنتَ تَحْكُمُ بَيْنَ عِبَادِكَ فِي مَا كَانُوا فِيهِ يَخْتَلِفُونَ ﴿٤٦﴾

46. Sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Muumba wa mbingu na ardhi! Mjuzi wa yasiyoonekana na yanayoonekana! Wewe utahukumu baina ya waja wako katika waliyokuwa wakikhitalifiana.

وَلَوْ أَنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا مَا فِي الْأَرْضِ جَمِيعًا وَمِثْلَهُ مَعَهُ لَافْتَدَوْا بِهِ مِن سُوءِ الْعَذَابِ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَبَدَا لَهُم مِّنَ اللَّـهِ مَا لَمْ يَكُونُوا يَحْتَسِبُونَ ﴿٤٧﴾

47. Na lau kuwa waliodhulumu wangelikuwa na vyote viliomo duniani na pamoja navyo vingine kama hivyo, bila ya shaka wangelivitoa kujikomboa katika adhabu mbaya Siku ya Kiyama. Na yatawadhihirikia kwa Mwenyezi Mungu wasiyokuwa wakiyatazamia.

وَبَدَا لَهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ ﴿٤٨﴾

48. Na utawadhihirikia ubaya wa waliyoyachuma, na yatawazunguka waliyokuwa wakiyafanyia mzaha.

فَإِذَا مَسَّ الْإِنسَانَ ضُرٌّ دَعَانَا ثُمَّ إِذَا خَوَّلْنَاهُ نِعْمَةً مِّنَّا قَالَ إِنَّمَا أُوتِيتُهُ عَلَىٰ عِلْمٍ بَلْ هِيَ فِتْنَةٌ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٤٩﴾

49. Na dhara inapomgusa mtu hutuomba. Kisha tunapompa neema zitokazo kwetu, husema: Nimepewa haya kwa sababu ya ilimu. Sio! Huo ni mtihani! Lakini wengi wao hawajui.

قَدْ قَالَهَا الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ ﴿٥٠﴾

50. Walikwishayasema haya waliokuwa kabla yao, lakini hayakuwafaa waliyokuwa wakiyachuma.

فَأَصَابَهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَالَّذِينَ ظَلَمُوا مِنْ هَـٰؤُلَاءِ سَيُصِيبُهُمْ سَيِّئَاتُ مَا كَسَبُوا وَمَا هُم بِمُعْجِزِينَ ﴿٥١﴾

51. Basi ukawasibu ubaya wa waliyoyachuma. Na wale ambao wamedhulumu miongoni mwa hawa utawasibu ubaya wa waliyoyachuma. Nao si wenye kushinda.

أَوَلَمْ يَعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يُؤْمِنُونَ ﴿٥٢﴾

52. Je, hawajui kwamba Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na humkunjia? Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaoamini.

UTAHUKUMU BAINA YAO

Aya 46 – 52

MAANA

Sema: Ewe Mwenyezi Mungu! Muumba wa mbingu na ardhi! Mjuzi wa yasiyoonekana na yanayoonekana! Wewe utahukumu baina ya waja wako katika waliyokuwa wakikhitalifiana.

Aya hii inafungamana na ile iliyotangulia: ‘Na wewe si mlinzi juu yao.’ Maana yake yako wazi. Kwa ufupi ni, sema ewe Muhammad, baada ya kufikisha ujumbe na kutoa nasaha: ewe Mwenyezi Mungu wewe ni muumba wa ulimwengu, Mfalme wa wafalme, Mjuzi wa yaliyoko kwangu na kwa wakadhibishaji. Hukumu ni yako peke yako katika kila kuhitalifiana na kuzozana baina ya waja wako kwenye maisha haya.

Na lau kuwa waliodhulumu wangelikuwa na vyote viliomo duniani na pamoja navyo vingine kama hivyo, bila ya shaka wangelivitoa kujikomboa katika adhabu mbaya Siku ya Kiyama. Na yatawadhi- hirikia kwa Mwenyezi Mungu wasiyokuwa wakiyatazamia.

Walikuwa wakipupia dunia na wakikusanya mali juu mali, wakiwa wameghafilika na kukutana na Mwenyezi Mungu na hisabu yake. Wakati watakaposimima mbele yake kwa ajili ya hisabu na kuwafunukia waliyokuwa wakiyapuuza, basi watauma mikono wakijuta. Lakini wapi!

Jahannam haiwezi kukombolewa. Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (3:91), Juz. 11 (10: 54) na Juz. 13 (13:18)

Na utawadhihirikia ubaya wa waliyoyachuma, na yatawazunguka waliyokuwa wakiyafanyia mzaha.

Walikuwa wanapoambiwa iogoponi siku ambayo mtarejeshwa kwa Mwenyezi Mungu, walikuwa wakiifanyia masikhara kauli hii na yule aliyeisema.

Lakini watakapohudhurishwa siku iliyoagwa, hapo ndio haki- ka itawadhihirikia na adhabu itawashukia kulingana na msimamo wao wa madharau na kumdharau yule aliyewaonya.

UDHURU MBAYA KULIKO DHAMBI

Na dhara inapomgusa mtu hutuomba. Kisha tunapompa neema zitokazo kwetu, husema: ‘Nimepewa haya kwa sababu ya ilimu.’

Makusudio ya mtu hapa ni kila mwenye sifa hiyo iliyotajwa ambaye anamtaka msaada Mwenyezi Mungu wakati wa shida na kumsahau wakati wa raha huku akisema kwa kujidai: ‘Neema hii ni kwa mipango na ufundi wangu.’

Wakati nikiandika maneno haya, nimekumbuka siasa ya Marekani aliyoitangaza Rusk, alipokuwa waziri wa mambo ya nchi za nje wa Marekani, alisema: “Hapana budi kwa Marekani kuonyesha umuhimu wake katika dunia nzima, ikiwemo anga yake, maji yake na pambizo zake zinazoizunguka.”

Anamaanisha kuwa ni lazima Amerika itawale dunia yote na vilivyomo ndani yake.

Tangazo hili lilikuwa mnamo mwaka 1966, kabla ya Marekani kupeleka chombo chake mwezini. Kwa hiyo ingelikuwa leo angeuanganisha mwezi na sayari nyinginezo.

Baada ya magazetu ya kimataifa kutangaza siasa hii ya kikoloni, aliyoitangaza waziri wa mambo ya nchi za nje wa Amerika, kibaraka mmoja aliandika makala ya kutetea siasa hii, kwa kusema:

“Marekani ndio dola kubwa kielimu na kiutajiri. Imeonyesha ushindi mkubwa katika uwanja wa elimu na viwanda. Kwa hiyo basi inayo haki ya kuingilia ulimwengu kwa sura mbalimbali, kutawala kila inachokitaka, kugeuza kanuni za nchi yoyote, vile inavyotaka, na kuielekeza kiuchumi, kuiwekea bajeti yake na kuipangia nchi hiyo itakachouza nje na itakochonunua.

Vile vile Marekani inayo haki ya kutumia siasa kwenye nchi yoyote kwa mfumo wowote, hata ikibidi kutumia nguvu, kwa mapinduzi ya kijeshi na kuunga mkono harakati za upinzani, ili kuleta utulivu.

Marekani inayo haki hii na zaidi, kwa sababu:

kwanza : Haki hii ni ya kielimu.

Pili : Marekani inamiliki silaha za maangamizi, na kila mwenye kumilki silaha hizi ana haki ya kutawala dunia nzima na vilivyomo ndani yake.”

Yote yaliyoandikwa kwenye makala hii kupitia mwandishi huyu ni ubainifu wa siasa halisi ya Marekani kama ilivyo. Mwenye kutaka kuhakikisha haya naangalie siasa ya Marekani katika Vietnam, Asia, Afrika na Latin Amerika.

Vile vile msimamo wake wa kiadui kwa nchi za kiarabu, jinsi inavyotoa msaada usiokuwa na mpaka kwa adui Israil na inavyopinga jaribio lolote la amani katika tatizo la Palestina na mahali popote penye tatizo mashariki na magaharibi.

Mzandiki huyu aliyejitolea kuitetea Marekani, kubariki siasa zake na kusema kuwa inayo haki ya kushibisha matamanio yake ya kiuadui, kwa kuwa eti inamiliki viwanda vya silaha, tunamuuliza hivi: Ikiwa elimu inaruhusu kuua, kubomoa na kupora, maana yake ni kuwa elimu ni ya shari sio ya heri na ni ya ufisadi wala sio ya utengenezaji?

Na kwamba mwenye elimu anayoruhusa kuitumia elimu yake kuiba, kudanganya na kuzua? Na mwizi atakuwa ni mwenye kushukuriwa na kulipwa; na kila anavyozidi kuwa hodari wa hatia na kuwa na ufisadi mwingi na upotevu basi atakuwa anastahiki heshima?

Ikiwa elimu inaboresha uadui, kwanini basi Marekani inainua nembo za haki za binadamu na kujaribu kila juhudi kuwakinaisha watu kwamba wao wanafanya ibada wana zuhudi na wanupiga vita ukomonisti kwa jina la imani ya Mungu na siku ya mwisho?

Zaidi ya hayo mzushi huyu mwenye dhambi amaesahau kuwa anafichua hiyana yake na upotevu wake, huku akiwa anatetea matamanio ya Marekani kwa mantiki yake ya kufedhehesha akitoa udhuru kwa yaliyo mabaya zaidi ya dhambi yake.

Sio! Huo ni mtihani!

Makusudio ya mtihani hapa ni neema. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamneemesha mja wake ili amjaribu kuwa atashukuru au atakufuru. Akishukuru humzidishia neema duniani na malipo akhera, na akikufuru basi Jahannam imeandaliwa makafiri.

Lakini wengi wao hawajui kuwa Mwenyezi Mungu anawapa mtihani waja wake ili vidhihirike vitendo vinavyostahiki thawabu na adhabu.

Walikwishayasema haya waliokuwa kabla yao, lakini hayakuwafaa waliyokuwa wakiyachuma.

Yaani haya ya kusema kuwa nimepewa kwa elimu yangu. Maana ni kuwa msemaji huyu mjinga ana wanaofanana naye katika historia, lakini mali haikuwazuia na ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake iliyotolewa kiaga. Tazama Juz. 20 (28:76-82).

Basi ukawasibu ubaya wa waliyoyachuma. Na wale ambao wamedhulumu miongoni mwa hawa - waliomkadhibisha Muhammad – utawasibu ubaya wa waliyoyachuma.

Mwenye kufanya wema atalipwa nao wala hatapata msaidizi asiyekuwa Mwenyezi Mungu. Hii imethibiti kwa wote bila ya kuvua wala kuhusika na uma zilizotangulia au zijazo. Ni desturi ya Mwenyezi Mungu, wala hutapata mabadiliko katika desturi ya Mwenyezi Mungu.

Nao si wenye kushinda.

Kwani inawezekana muumbwa kumshinda muumba wake?

Je, hawajui kwamba Mwenyezi Mungu humkunjulia riziki amtakaye na humkunjia? Hakika katika haya bila ya shaka zipo Ishara kwa watu wanaoamini.

Umetangulia mfano wake katika Juzuu zifuatazo: Juz.13 (13:27), Juz.15 (17:30), Juz.20 (28:82), Juz.21(29:62), Juz.21 (30:37) na Juz.22 (34:36,39).

Na tumezungumzia kwa ufafanuzi zaidi kuhusu suala hili katika Juzuu zifuatazo: Juz. 6 (5:64-66), kifungu cha ‘Riziki na ufisadi,’ Juz. 7 (5:100) kifungu ‘Je riziki ni bahati au majaliwa?’ Juz. 13 (13:26-29) kifungu ‘Mtu na riziki’ na Juz. 20 (29:56-63) kifungu ‘Riziki na kumtegemea Muumba si kiumbe.’

قُلْ يَا عِبَادِيَ الَّذِينَ أَسْرَفُوا عَلَىٰ أَنفُسِهِمْ لَا تَقْنَطُوا مِن رَّحْمَةِ اللَّـهِ إِنَّ اللَّـهَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ جَمِيعًا إِنَّهُ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿٥٣﴾

53. Sema: Enyi waja wangu waliozifanyia israfu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

وَأَنِيبُوا إِلَىٰ رَبِّكُمْ وَأَسْلِمُوا لَهُ مِن قَبْلِ أَن يَأْتِيَكُمُ الْعَذَابُ ثُمَّ لَا تُنصَرُونَ ﴿٥٤﴾

54. Na rejeeni kwa Mola wenu, na silimuni kwake, kabla ya kuwajia adhabu. Kisha hapo hamtanusuriwa.

وَاتَّبِعُوا أَحْسَنَ مَا أُنزِلَ إِلَيْكُم مِّن رَّبِّكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَكُمُ الْعَذَابُ بَغْتَةً وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ ﴿٥٥﴾

55. Na fuateni yaliyo bora zaidi katika yale yaliyoteremshwa kwenu kutoka kwa Mola wenu, kabla haijawajia adhabu kwa ghafla, na hali hamtambui.

أَن تَقُولَ نَفْسٌ يَا حَسْرَتَىٰ عَلَىٰ مَا فَرَّطتُ فِي جَنبِ اللَّـهِ وَإِن كُنتُ لَمِنَ السَّاخِرِينَ ﴿٥٦﴾

56. Isije ikasema nafsi: Ee masikitiko yangu kwa yale niliyopoteza upande wa Mwenyezi Mungu; na hakika nilikuwa miongoni mwa wanaofanya maskhara!

أَوْ تَقُولَ لَوْ أَنَّ اللَّـهَ هَدَانِي لَكُنتُ مِنَ الْمُتَّقِينَ ﴿٥٧﴾

57. Au ikasema: Ingelikuwa Mwenyezi Mungu ameniongoa, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa wenye takua.

أَوْ تَقُولَ حِينَ تَرَى الْعَذَابَ لَوْ أَنَّ لِي كَرَّةً فَأَكُونَ مِنَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٥٨﴾

58. Au ikasema inapoona adhabu: Lau kuwa ningelipata kurudi, ningeli kuwa miongoni mwa wafanya mema.

بَلَىٰ قَدْ جَاءَتْكَ آيَاتِي فَكَذَّبْتَ بِهَا وَاسْتَكْبَرْتَ وَكُنتَ مِنَ الْكَافِرِينَ ﴿٥٩﴾

59. Wapi! zilikwishakujia Ishara zangu, nawe ukazikadhibisha, na ukajivuna, na ukawa miongoni mwa makafiri!

MWENYEZI MUNGU ANASAMEHE MADHAMBI YOTE

Aya 53 – 59

MAANA

Sema: Enyi waja wangu waliozifanyia israfu nafsi zao! Msikate tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu husamehe dhambi zote. Hakika Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Huu ni mwito wa wazi, kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kwa wale waliodhulumu nafsi zao kwa kufanya madhambi na maasi. Akaahidi msamaha kwa kila dhambi kadiri itakavyokuwa kubwa. Kwa hiyo amefungua mlango kwa yule mwenye kutaka kufuta maovu yake yeye mwenyewe na kutengeneza yaliyoharibika.

Kuna Hadith inayosema:“Hakika Mwenyezi Mungu hachoki mpaka mchoke. Mkiacha naye anaacha.” yaani mkiacha toba naye anaacha maghufira. Katika Hadith nyingine Mtume(s.a.w. w ) anasema:“Hakuna ninachopenda zaidi katika dunia na vilivyomo kuliko Aya hii.” Imekua mashuhuri kauli ya kuwa hii ni Aya yenye matarajio zaidi katika Qur’ani.

Miongoni mwa madhambi makubwa zaidi ni kukata tamaa na rehema ya Mwenyezi Mungu:

قَالَ وَمَن يَقْنَطُ مِن رَّحْمَةِ رَبِّهِ إِلَّا الضَّالُّونَ ﴿٥٦﴾

“Na ni nani anayekata tamaa na rehema ya Mola wake isipokuwa wale waliopotea.” Juz. 14 (15:56).

Tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi zaidi katika Juz. 5 (4:56). Pia tumeweka kifungu maalum cha toba ’Toba na umbile’ katika Juz. 4 (4:17-18).

Na rejeeni kwa Mola wenu, na silimuni kwake, kabla ya kuwajia adhabu. Kisha hapo hamtanusuriwa.

Chukueni fursa enyi wenye dhambi wala msiipoteze. Tubieni kwake na mumfanyie ikhlasi kwa kauli na vitendo.

Na fuateni yaliyo bora zaidi katika yale yaliyoteremshwa kwenu kutoka kwa Mola wenu, kabla haijawajia adhabu kwa ghafla, na hali hamtambui.

Hakuna kitu, katika alivyoviteremsha Mwenyezi Mungu kilicho bora zaidi ya kingine kwake. Kila alichokisema ni kizuri zaidi na adhimu. Ama kwa wenye dhambi basi kitu bora zaidi walichoteremshiwa ni mwito wa toba na kukubaliwa hata ikiwa dhambi ni kubwa kiasi gani. Na yasiyokuwa hayo ni kiaga na hadhari.

Kisha Mwenyezi Mungu (s.w.t) akabainisha matokeo ya atakayepuuza toba; kama ifuatavyo:

Isije ikasema nafsi: Ee masikitiko yangu kwa yale niliyopoteza upande wa Mwenyezi Mungu katika kumtii. Masikitiko ni miongoni mwa adhabu kubwa ya nafsi. Hasa ikiwa hakuna kimbilio wala pa kutokea.

Na hakika nilikuwa miongoni mwa wanaofanya maskhara!

Kesho mwenye madhambi atasema kwa majuto na masikitiko: Sikutosheka na kumwasi Mwenyezi Mungu na kupuuza toba mpaka nikawafanyia masihara wanaomtii Mwenyezi Mungu na wenye kuogopa adhabu yake.

Au ikasema: Ingelikuwa Mwenyezi Mungu ameniongoa, bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa wenye takua.

Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Watasema walioshirikisha: Lau angelitaka Mwenyezi Mungu tusingelishirikisha” Juz. 8 (6:148).

Au ikasema inapoona adhabu: Lau kuwa ningelipata kurudi, ningeli kuwa miongoni mwa wafanya mema.

Mfano wake ni:

قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ ﴿٩٩﴾ لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ ﴿١٠٠﴾

“Husema Mola wangu nirudishe ili nitende mema badala ya yale niliyoacha” Juz. 18 (23:99-100).

Wapi! Mambo hayako kama unavyotaka zilikwishakujia Ishara zangu, nawe ukazikadhibisha, na ukajivuna, na ukawa miongoni mwa makafiri!

Zilimjia ishara za Mwenyezi Mungu akazikanusha na akasema hazitoki kwa Mwenyezi Mungu. Akafanya kiburi na imani na akamkufuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake, kisha akakadhibisha na akasema: hakuna chochote kilichonijia kutoka kwa Mwenyezi Mungu kupitia kwa Mtume wake.

Kwa hiyo akachanganya maovu ya kufuru, uwongo na kiburi. Lau angelichukua fursa ya kutubia ingelikuwa hana haja na malalamiko yote haya; na angelikuwa kwenye raha bila ya kuwa na hizaya.

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿الشَّهْرُ الْحَرَامُ بِالشَّهْرِ الْحَرَامِ وَالْحُرُمَاتُ قِصَاصٌ فَمَنِ اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ فَاعْتَدُوا عَلَيْهِ بِمِثْلِ مَا اعْتَدَىٰ عَلَيْكُمْ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ ﴾

194.Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu; na vitu vitakatifu vina kisasi. Basi wanaowachokoza, pia nanyi wachokozeni kwa kadiri walivyowachokoza. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaomcha.

﴿وَأَنفِقُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ وَلَا تُلْقُوا بِأَيْدِيكُمْ إِلَى التَّهْلُكَةِ وَأَحْسِنُوا إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ﴾

195.Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamivu, na fanyeni wema. Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wafanyao wema.

MIEZI MITAKATIFU

Aya 194 - 195

MAANA

Mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu.

Miezi mitakatifu ni minne; mitatu inafuatana, nayo ni Dhul-Qaada, Dhul Hijja na Muharram (mfunguo pili, mfunguo tatu na mfunguo nne). Na mwezi mmoja uko pekee na ni (Rajab). Miezi hii imeitwa mitakatifu kwa sababu ya kuharamishwa kuuana ndani ya miezi hiyo. Katika wakati wa ujahiliya na wa Uislamu, ilikuwa mtu anaweza kukutana na mtu aliyemuua baba yake katika miezi hiyo na asimfanye chochote. Yameshatangulia maelezo kwamba Mtume na sahaba zake walitaka kufanya umra katika mwezi wa dhul-Qaada (mfunguo pili) mwaka wa sita (6 Hijriya), wakazuiwa na washirikina na wakatupiwa mishale na mawe; kisha waka-fanyiana suluhu kuwa Waislamu warudi mwaka utakaofutia. Lakini Waislamu wakaogopa washirikina wasije wakaanza kupigana katika mwezi mtakatifu; ndipo Mwenyezi Mungu akawapa idhini ya kupigana na washirikina na akabainisha kuwa lenye kukatazwa ni kuanza uadui wa kupigana na sio kujikinga. Kwa hivyo maana ya mwezi mtakatifu kwa mwezi mtakatifu ni kwamba mwenye kuihalalisha damu yenu enyi Waislamu katika mwezi huu, basi nanyi ihalalisheni damu yake katika mwezi huo huo.

Na vitu vitakatifu vina kisasi. Yaani mwenye kuvunja heshima ya Mwenyezi Mungu atalipizwa kisasi na atafanywa kama alivyofanya. Hiyo ndiyo asili kwa ujumla inayoondoa kila udhuru wa mwenye kuvunja heshima. Mwenye kuhalalilisha damu za watu, mali zao na heshima zao, naye atahalalishwa kwa kiasi kile alichowafanyia. Heshima kwa mtu mwingine inatokana na heshima ya Mwenyezi Mungu isipokuwa kama akivunja heshima ya mwingine. Hapo itakuja haki ambayo daima inakuwa juu na wala haikaliwi. Hapa ndipo tunapata tafsiri ya:

Anayechokoza pia nanyi mchokozeni kwa kadiri alivyo wachokoza. Sharti la kulipiza ni kuwa sawa na kosa la aliyeanza bila ya kuzidisha au kupunguza. Hicho ndio kisasi hasa kilivyo. Unaweza kuuliza: Mwenye kuchokoza , yeye ni mchokozi bila ya wasiwasi wowote, lakini mwenye kulipiza kisasi bila shaka siye mchokozi. Kwa hiyo kuna wajihi gani kwa Mwenyezi Mungu kusema:Mchokozeni

Jibu : Makusudio ya kuwafanyia uchokozi, sio uchokozi hasa kwa maana yake, isipokuwa makusudio ni malipo ya uchokozi uliofanywa kwa kipimo chake bila ya kudhulumu. Hayo ni mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu(s.w.t.):

"Na malipo ya ubaya ni ubaya ulio sawa na (ubaya) huo..." (42:40)

KUTOA KATIKA NJIA YA MWENYEZI MUNGU

Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu. Kutoa katika njia yake Mwenyezi Mungu kunakuwa ni kwa masilahi ya umma; kama vile shule, hospitali na nyumba za kulea mayatima. Vile vile jihadi, sadaka kwa mafukara na masikini na kuwalisha watu wa nyumbani. Bora zaidi ya kutoa ni kule kunakohusika na kutia nguvu na kuieneza dini, kuthibitisha haki na kuibatilisha batili.

Wala msijitie, kwa mikono yenu, katika maangamivu

Mwenyezi Mungu ametumia neno mikono kwa maana ya mtu kujiingiza mwenyewe. Kama tukiangalia jumla hii peke yake tu bila ya kuangalia mfumo mzima wa maneno, ingelikuwa maana yake ni kuwa haijuzu kwa mtu kufanya lolote ambalo lina madhara na bila ya kuwako manufaa kwa ujumla. Lakini tukichunga mfumo wa maneno na kuja kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):"wala msijitie kwa mikono yenu katika maangamivu" baada ya kusema:"Na toeni katika njia ya Mwenyezi Mungu", basi maana yanakuwa, toeni katika mali zenu sio kwa ubahili wala ubadhirifu, kwa sababu yote hayo mawili yanaleta uangamivu. Kwa hivyo Aya kwa maana haya inakuwa kama ile Aya isemayo:

﴿ وَالَّذِينَ إِذَا أَنفَقُوا لَمْ يُسْرِفُوا وَلَمْ يَقْتُرُوا وَكَانَ بَيْنَ ذَٰلِكَ قَوَامًا ﴾

"Na wale ambao wanapotoa hawafanyi ubadhirifu wala ubahili, bali wanakuwa katikati ya hayo."( 25:67)

Inasemekana pia kwamba maana yake ni: Msijitie kwa mikono yenu kwenye maangamivu kwa kuacha kupigana jihadi na maadui wa dini na kutoa mali kwa ajili ya kuwaandaa wapigania jihadi, kwa sababu hilo litawaogopesha na atawaweza adui; muangamie na mdhalilike. Haya ndiyo yaliyothibitishwa na majaribio waliyoyapitia Waislamu. Wamekosa uhuru wao na heshima yao tangu walipoacha jihadi na kutoa mali kwa ajili ya kuinusuru haki na uadilifu. Hivyo akapata tamaa kila mnyang'anyaji na mnyakuzi; hata Wazayuni, vibaraka wa ukoloni, nao waliivamia Palestina mnamo 1948. Baada ya Waarabu kunyamaza na wasifanye jihadi. Baada ya miaka ishirini wakateka Sinai na ukanda wa Gaza Magharibi mwa mto Jordan; wakazikalia sehemu hizo kwa msaada wa Amerika, Uingereza na Ujerumani Magharibi. Wakawaua wanaume na kuwafukuza wanawake na watoto. Lau Waislamu wangefanya jihadi kabla yake, wangeliokoka na maangamizo haya na udhalili huu, na wala dola ya Israel isingekuwepo kabisa.Na fanyeni wema Kwa jihadi na kujitolea mali katika njia ya Mwenyezi Mungu na katika kila njia inayomridhisha Mungu na yenye sifa nzuri.

﴿ وَأَتِمُّوا الْحَجَّ وَالْعُمْرَةَ لِلَّـهِ فَإِنْ أُحْصِرْتُمْ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ وَلَا تَحْلِقُوا رُءُوسَكُمْ حَتَّىٰ يَبْلُغَ الْهَدْيُ مَحِلَّهُ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوْ بِهِ أَذًى مِّن رَّأْسِهِ فَفِدْيَةٌ مِّن صِيَامٍ أَوْ صَدَقَةٍ أَوْ نُسُكٍ فَإِذَا أَمِنتُمْ فَمَن تَمَتَّعَ بِالْعُمْرَةِ إِلَى الْحَجِّ فَمَا اسْتَيْسَرَ مِنَ الْهَدْيِ فَمَن لَّمْ يَجِدْ فَصِيَامُ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ فِي الْحَجِّ وَسَبْعَةٍ إِذَا رَجَعْتُمْ تِلْكَ عَشَرَةٌ كَامِلَةٌ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمْ يَكُنْ أَهْلُهُ حَاضِرِي الْمَسْجِدِ الْحَرَامِ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ ﴾

196.Na timizeni Hijja na Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Na kama mkizuiliwa, basi (chinjeni) wanyama walio wepesi kupatikana. Wala msinyoe vichwa vyenu mpaka wanyama hao wafike machinjioni mwao. Na ataka-yekuwa mgonjwa katika nyinyi au ana adha kichwani mwake, basi atoe fidia kwa kufunga au sadaka au kuchinja mnyama. Na mtakapokuwa salama, basi mwenye kujistarehesha kwa kufanya Umra, kisha akahiji, achinje mnyama aliye mwepesi kumpata. Na asiyepata, ni kufunga siku tatu katika Hijja na siku saba mtakaporudi; hizo ni siku kumi kamili. Hayo ni kwa yule ambaye watu wake hawako karibu na Msikiti Mtakatifu. Na mcheni Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

﴿ الْحَجُّ أَشْهُرٌ مَّعْلُومَاتٌ فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ الْحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي الْحَجِّ وَمَا تَفْعَلُوا مِنْ خَيْرٍ يَعْلَمْهُ اللَّـهُ وَتَزَوَّدُوا فَإِنَّ خَيْرَ الزَّادِ التَّقْوَىٰ وَاتَّقُونِ يَا أُولِي الْأَلْبَابِ﴾

197.Hijja ni miezi maalumu. Na anayejilazimisha kufanya Hijja katika miezi hiyo, basi hakuna kuchafua wala ufuska wala mabishano katika Hijja. Na heri yoyote mnayoifanya Mwenyezi Mungu anaijua. Na chukueni masurufu, na hakika masurufu bora ni takua; na nicheni Mimi, enyi wenye akili.

﴿ لَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ أَن تَبْتَغُوا فَضْلًا مِّن رَّبِّكُمْ فَإِذَا أَفَضْتُم مِّنْ عَرَفَاتٍ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ عِندَ الْمَشْعَرِ الْحَرَامِ وَاذْكُرُوهُ كَمَا هَدَاكُمْ وَإِن كُنتُم مِّن قَبْلِهِ لَمِنَ الضَّالِّينَ ﴾

198.Si vibaya kwenu kutafuta riziki ya Mola wenu. Na mtakapomiminika kutoka Arafa, mtajeni Mwenyezi Mungu katika Mash'aril- Haram: Na mkumbukeni kama alivyowaongoza, ijapokuwa zamani mlikuwa miongoni mwa waliopotea.

﴿ ثُمَّ أَفِيضُوا مِنْ حَيْثُ أَفَاضَ النَّاسُ وَاسْتَغْفِرُوا اللَّـهَ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴾

199.Kisha miminikeni kutoka mahali wanapomiminika watu (wote), na mumwombe Mwenyezi Mungu maghufira; hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kughufiria Mwenye kurehemu.

﴿ فَإِذَا قَضَيْتُم مَّنَاسِكَكُمْ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ كَذِكْرِكُمْ آبَاءَكُمْ أَوْ أَشَدَّ ذِكْرًا فَمِنَ النَّاسِ مَن يَقُولُ رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ﴾

200.Na mmalizapo kuzitimiza ibada zenu, basi mtajeni Mwenyezi Mungu kama mlivyokuwa mkiwataja baba zenu; bali mtajeni zaidi. Na kuna baadhi ya watu wasemao: Mola wetu! Tupe duniani; nao katika Akhera, hawana lolote.

﴿ وَمِنْهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا حَسَنَةً وَفِي الْآخِرَةِ حَسَنَةً وَقِنَا عَذَابَ النَّارِ ﴾

201.Na miongoni mwao kuna asemaye; Mola wetu! Tupe mema duniani na (tupe) mema Akhera, na utulinde na adhabu ya Moto.

﴿ أُولَـٰئِكَ لَهُمْ نَصِيبٌ مِّمَّا كَسَبُوا وَاللَّـهُ سَرِيعُ الْحِسَابِ ﴾

202.Hao ndio wenye fungu katika waliyoyachuma, na Mwenyezi Mungu ni Mwepesi wa kuhisabu.

﴿ وَاذْكُرُوا اللَّـهَ فِي أَيَّامٍ مَّعْدُودَاتٍ فَمَن تَعَجَّلَ فِي يَوْمَيْنِ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ وَمَن تَأَخَّرَ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ لِمَنِ اتَّقَىٰ وَاتَّقُوا اللَّـهَ وَاعْلَمُوا أَنَّكُمْ إِلَيْهِ تُحْشَرُونَ﴾

203.Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika siku zinazohisabiwa. Na mwenye kufanya haraka katika siku mbili, basi si dhambi juu yake; na mwenye kukawia pia si dhambi juu yake, kwa mwenye takua. Na mcheni Mwenyezi Mungu, na jueni kwamba nyinyi mtakusanywa Kwake.

TIMIZENI HIJJA NA UMRA

Aya 196 - 203

MAANA

Aya hizi zimeonyesha baadhi ya hukumu za Hijja, Mafaqihi wameweka vitabu maalumu vinavyohusu Hijja, nami nimetunga kitabu kwa jina Al- Hajj ala Madhahabil-Khamsa; kisha nikakiunganisha katika kitabu Al- Fiqh ala Madhahabil Khamsa wakati kiliporudiwa kuchapishwa kwa mara ya tatu. Vile vile nimeizungumza kwa urefu katika Juzuu ya pili ya kitabu Fiqh ul-Imam Jaffar Sadiq(a.s) Hijja imekuwa maarufu tangu zama za Nabii Ibrahim na Ismail(a.s) na iliendelea katika zama za ujahiliya; na Uislamu ukaithibitisha baada ya kuisafisha na mambo machafu, na kuongeza baadhi ya ibada.

Na timizeni Hijja na Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu.

Maana ya Hijja kilugha, ni kukusudia, na kisharia ni ibada maalum katika mahali na wakati maalum. Umra kilugha ni ziara yoyote; na kisheria ni ziara katika Al-Kaaba kwa namna maalum, Hijja ni wajibu katika Quran, Hadith na Ijami. Bali wajibu wake umethubutu kwa dhahiri ya dini. Na mwenye kuikanusha sio Mwislamu, sawa sawa na aliyekanusha wajibu wa Saumu na Swala. Shia Imamiyya na Shafii wamesema Umra ni wajibu, Hanafi na Malik wamesema ni Sunna. Kusema kwake Mwenyezi Mungu Kwa ajili ya Mwenyezi Mungu Yaani Hijini na fanyeni Umra kwa ajili ya Mwenyezi Mungu peke yake na sio kwa makusudio ya kidunia. Kwani Waarabu walikuwa wakikusudia kuhiji kwa ajili ya kukutana, kujifaharisha, kutafuta mahitaji na kuhudhuria soko. Ndipo Mwenyezi Mungu akaamrisha Hijja iwe ni kwa makusudio yake Yeye kwa ibada safi yenye kutakasika na makusudio yoyote mengine.

Na kama mkizuiliwa, basi (chinjeni) wanyama walio wepesi kupatikana.

Yaani ikiwa mmeherimia Hijja, kisha mkazuilika kukamilisha ibada kwa njia yake ya kisheria kutokana na maradhi au adui na mengineyo, basi ni juu yenu kuchinja mnyama atakayepatikana kwa urahisi; kwa uchache awe ni mbuzi, wastani ni ng’ombe na wa juu zaidi ni ngamia.

Wala msinyoe vichwa vyenu mpaka wanyama hao wafike machinjioni mwao.

Msemo unaelekezwa kwa wale waliozuilika ambao hawakuweza kutimiza Hijja au Umra. Wao hawatakuwa wametoka katika ihram yao (miko ya Hijja) mpaka wajue kwamba mnyama amefika mahali pake pa kuchinjwa. Na mahali pa kuchinja ni Mina ikiwa ni Hijja; na kama ni Umra basi ni Makka. Hayo ni itakapokuwa kizuizi ni maradhi. Ama ikiwa kizuizi ni adui, basi mahali pa kuchinja ni pale mahali palipotokea kizuizi. Kwa sababu Mtume(s.a.w.w) alichinja mnyama katika Hudaybiya, alipozuiliwa na washirikina kuzuru nyumba ya Mwenyezi Mungu tukufu (Al Kaaba).

Na atakayekuwa mgonjwa katika nyinyi au ana adha kichwani mwake, basi atoe fidia kwa kufunga au sadaka au kuchinja mnyama.

Yaani ikiwa mwenye kuhirimia atanyoa kichwa chake kwa dharura, basi ni juu yake kutoa kafara, atakuwa na hiyari baina ya kufunga siku tatu, kuwalisha masikini sitini au kuchinja mnyama; kwa uchache awe ni mbuzi.

Na mtakapokuwa salama, basi mwenye kujistarehesha kwa kufanya Umra kisha akahiji, achinje mnyama aliyemwepesi kupatikana.

Yaani mtu asiyekuwa na kizuizi, akafanya Umra kisha akahiji baadae katika mwaka huo huo, basi ni juu yake kuchinja mnyama. Hii ndiyo aina ya Hijja inayojulikana kwa jina la Haj Tamattui (Hijja ya starehe) ambayo ni wajibu kwa wasiokuwa watu wa Makka.

Imeitwa Hijja ya starehe, kwa sababu mwenye kuhiji baada ya kumaliza amali za Umra anatoka kwenye miko ya Umra mpaka aje ahirimie Hijja.

Na asiyepata, ni kufunga siku tatu katika Hijja na siku saba mtakaporudi; hizo ni siku kumi kamili.

Imam Jaffar Sadiq(a.s) amesema;Mwenye kufanya Hajj Tamattu, asipopata mnyama atafunga siku tatu katika Hijja; siku ya saba, ya nane na ya tisa katika Dhul-Hijja (mfungu tatu) wala hakuna sharti la Iqama na siku saba atafunga atakaporudi kwa watu wake. Hizo ni siku kumi kamili za kutosheleza mnyama.

Hayo ni kwa yule ambaye watu wake hawako karibu na msikiti mtakatifu.

Mwenye Majmaul Bayan amesema kuwa hayo yaliyotangulia kutajwa katika Tamattui ya Umra kisha Hijja, sio kwa watu wa Makka na walio karibu yake. Isipokuwa ni kwa ambaye hayuko Makka, yule ambaye yuko mbali na Makka kwa zaidi ya maili kumi na mbili (12) kwa kila upande. Mafaqihi wa Kishia Imamiya wamesema Hajj Tamattui ni wajibu kwa walio mbali na Makka, wala haijuzu kwa aliyembali na Makka kuhiji Hijja Qiran na Ifrad, kwani hizo ni wajibu kwa watu wa Makka na wa kando kando yake; na wao haijuzu kwao kuhiji Hajj Tamattui. Kwa ufafanuzi zaidi angalia vitabu vya Fiqh.

Hijja ni miezi maalumu.

Nayo ni kuanzia Shawwal, Dhul-qaad na kumi la mwanzo la Dhul-Hijja. (mfunguo mosi, mfunguo pili na mfunguo tatu) Mwenye kuhirimia kabla yake Hijja yake haitaswihi na mwenye kuhirimia ndani ya miezi hiyo itaswihi na ataleta amali zilizobakia.

Na anayejilazimisha Hija katika miezi hiyo, basi hakuna kuchafua wala ufuska wala mabishano katika Hijja.

Makusudio ya uchafuzi hapa ni kujamii. Mtu akimjamii mkewe na huku amehirimia Hijja, basi Hijja yake imeharibika, sawa sawa na aliyejamii au kula huku akiwa amefunga. Kwa hiyo atakamilisha Hijja yake, kisha aje alipe mwaka ujao; kama ilivyo kwa mwenye kuiharibu Saumu. Makusudio ya ufuska, ni uongo na kutukana. Ama kuhusu kubishana riwaya za Ahlul Bait zinasema, hilo ni kusema mtu; Hapana wallahi au Kwa nini, wallahi n.k.

Si vibaya kwenu kutafuta riziki ya Mola wenu.

Kwa vile wakati wa ujahilia watu walikuwa wakifanya biashara na kuchuma siku za Hijja, kukadhaniwa kuwa ni haramu, ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t.), akaondoa tuhuma hii na akabainisha kwamba kuchuma hakupingani na ikhlasi katika amali za Hijja.

Na mtakapomiminika kutoka Arafa, mtajeni Mwenyezi Mungu katika Masharil Haram.

Arafa ni mahali maalum. Kumiminika kutoka Arafa ni kuondoka, Masharil-Haram ndipo pale panajulikana kama Muzdalifa na kutua hapo ni wajibu; kama ilivyo kwa Arafa.

Kisha miminikeni kutoka mahali wamiminikapo watu (wote). Inasemekana kuwa Maquraish walikuwa hawatui Arafa pamoja na watu wengine kwa kiburi tu, ndipo Mwenyezi Mungu akamwamrisha Mtume wake kutua hapo na kutoka pamoja na watu ili abatilishe waliyokuwa wakiyafanya Maquraish.

Na mmalizapo kuzitimiza ibada zenu, basi mtajeni Mwenyezi Mungu zaidi.

Imepokuwa kutoka kwa Imam Baqir baba wa Imam Sadiq(a.s) kwamba watu walikuwa wanapomaliza Hijja wanakusanyika huko na kuwataja wazazi wao kwa fahari, ndipo Mwenyezi Mungu akawaamrisha kuliacha hilo na badala yake wamtaje Mwenyezi Mungu na jinsi alivyowaneemesha. Kwa sababu Yeye ndiye mwenye kuwaneemesha wao na mababa zao.

Na baadhi ya watu kuna asemaye: Mola wetu! Tupe duniani; nao katika akhera hawana lolote. Na miongoni mwao kuna asemaye: Mola wetu! Tupe mema duniani na (tupe) mema akhera, na utulinde na adhabu ya moto. Hao ndio wenye fungu katika waliyoyachuma, na Mwenyezi Mungu ni mwepesi wa kuhisabu.

Watu katika Hijja zao wako aina mbili. Aina ya kwanza ni yule asiyetaka lolote isipokuwa starehe ya dunia na hana makusudio yoyote isipokuwa dunia tu, na anapomwabudu Mwenyezi Mungu humwabudu kwa ajili ya dunia. Hawa ndio wenye kunyimwa neema ya Akhera. Ama aina ya pili ni yule anayetaka heri ya dunia na akhera na anafanya amali kwa ajili ya dunia yake na akhera yake. Huyu ndiye mwenye radhi mbele ya Mwenyezi Mungu kesho kwa kulipwa amali yake njema. Mwenye Tafsiri Rawhul Bayan amenukuu kutoka kwa Imam Ali bin Abi Twalib(a.s) kwamba wema katika dunia ni mwanamke mwema na katika akhera ni Hurulain. Ama adhabu ya moto makusudio yake ni mwanamke muovu.

Iwe ni sahih Hadith hiyo au la, lakini mimi najua kuna watu wanaohisi kwamba lau wao wangekuwa katika Jahanam kisha wakahiyarishwa kutoka katika Jahanam na warudi kwa wake zao waliokuwa nao duniani au wabaki Jahannam, basi wangelichagua kubaki katika Jahannam kuliko kuishi tena na wake zao hao.

Na mtajeni Mwenyezi Mungu katika siku zinazohisabiwa.

Makusudio yake ni siku tatu za Tashriq nazo ni; Tarehe kumi na moja, kumi na mbili na kumi na tatu katika mwezi wa Dhul-Hijja (mfungo tatu). Si wajibu kwa mwenye kuhiji kulala Mina usiku wa kumi na tatu, lakini kwa sharti ya kuwa atoke Mina siku ya kumi na mbili baada ya kupinduka jua na kabla ya Maghrib na awe hakuvunja mwiko wa kuwinda au kujamii. Kwa hali hiyo ndipo tunapopata tafsiri ya kauli yake Mwenyezi Mungu:

Na mwenye kufanya haraka katika siku mbili, basi si dhambi juu yake; na mwenye kukawia pia si dhambi juu yake kwa mwenye takua.

Yaani mwenye kuacha kuwinda na wanawake katika ihram yake. Ikiwa amevunja mwiko wa kulala na mke au kuwinda au alichelewa na jua siku ya kumi na mbili akiwa yuko Mina, basi itakuwa wajibu kwake kulala usiku wa kumi na tatu na kutupia mawe vikuta vitatu (shetani).

7

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA PILI

﴿ وَمِنَ النَّاسِ مَن يُعْجِبُكَ قَوْلُهُ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَيُشْهِدُ اللَّـهَ عَلَىٰ مَا فِي قَلْبِهِ وَهُوَ أَلَدُّ الْخِصَامِ ﴾

204.Na katika watu kuna ambaye kauli yake inakupendeza katika maisha ya duniani, naye humshuhudiza Mwenyezi Mungu kwa yaliyo moyoni mwake na hali ni hasimu mkubwa kabisa.

﴿ وَإِذَا تَوَلَّىٰ سَعَىٰ فِي الْأَرْضِ لِيُفْسِدَ فِيهَا وَيُهْلِكَ الْحَرْثَ وَالنَّسْلَ وَاللَّـهُ لَا يُحِبُّ الْفَسَادَ﴾

205.Na anapotawala hufanya bidii katika ardhi kufanya ufisadi, na huangamiza mimea na viumbe, na Mwenyezi Mungu hapendi ufisadi.

﴿ وَإِذَا قِيلَ لَهُ اتَّقِ اللَّـهَ أَخَذَتْهُ الْعِزَّةُ بِالْإِثْمِ فَحَسْبُهُ جَهَنَّمُ وَلَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴾

206.Na anapoambiwa. Mche Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kufanya dhambi. Basi Jahannam inamtosha, napo ni makao mabaya mno

﴿ وَمِنَ النَّاسِ مَن يَشْرِي نَفْسَهُ ابْتِغَاءَ مَرْضَاتِ اللَّـهِ وَاللَّـهُ رَءُوفٌ بِالْعِبَادِ ﴾

207.Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni mpole kwa waja.

KAULI ZAO ZINAKUPENDEZA

Aya 204 – 207

MAANA

Baadhi ya wafasiri wapya wamejaza kurasa kwa maneno matamu katika kufasiri Aya hizi, lakini hawakuzidisha chochote zaidi ya kuwagawanya watu kwenye wema na uovu. Kwa dhahiri haya yanajulikana na wote, hayahitaji ubainifu wowote, sikwambii tafsiri ndefu tena. Unaweza kuuliza; Ikiwa kugawanyika watu kunajulikana na wote, basi kubainisha kunakuwa ni maelezo ambayo tayari yameshaelezwa na kufafanua lililofafanuliwa na yapasa kuyachukulia maneno ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) vizuri? Jibu: Inawezekana kuwa makusudio ni kuongoza na kuelekeza kwamba mwenye akili anatakikana kutohadaliwa kwa mambo ya nje wala asimwamini mwenye kutegeneza maneno matamu. Kwa sababu wafisadi ni mabingwa wa kazi hiyo na kazi ya ria. Kwa hivyo ni juu yetu kutomtegemea yeyote isipokuwa baada ya kufanya majaribio na kupatikana dalili ya ukweli wake na usafi wake.

Hiyo ndiyo asili ya ujumla inayoenea katika hukumu nyingi za dini na za kidunia; kama kuchagua Hakimu, Kadhi, Naibu, Kadhi, Mufti na kila anayesimamia masilahi ya Umma. Ajabu ya maajabu ni kutakiwa shahada ya kielimu tu kwa mwenye kujitokeza kwa kazi muhimu ya mji au nchi na inayogusa maisha ya watu. Lakini haulizwi uaminifu wake na tabia yake, pamoja na kuwa hayo ndio msingi. Wengi wenye shahada wanazitumia kuwa ni zana za kuibia.

Na katika watu kuna ambaye kauli yake inakupendeza hapa duniani, naye humshuhudia Mwenyezi Mungu kwa yaliyomo moyoni mwake, na hali ni hasimu mkubwa kabisa.

Yaani wanadhihihirisha mapenzi na heri na hali wao ndio maadui zaidi wa heri na watu wa heri.

Na anapotawala hufanya bidii katika ardhi kufanya ufisadi.

Wamehitaliafiana wafasiri kuhusu neno Tawalla. Je makusudio ni kuondoka na maana yake kuwa ni, anapoondoka kwa yule aliyemdanganya, huhangaika katika ardhi kwa ufisadi. Au kwamba makusudio ni kutawala na usultani, na maana yawe, na atakapokuwa mtawala atafanya wanayoyafanya watawala waovu ya kuangamiza mimea na viumbe? Mwenye Tafsir Al manar amenakili kutoka kwa Ustadha wake Sheikh Muhammad Abduh kwamba ameyapa nguvu maana ya utawala kwa kuunganisha na kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.):

"Na anapoambiwa mche Mwenyezi Mungu, hupandwa na mori wa kufanya dhambi."

Kwa maana ya kuwa mtawala mkaidi anakuwa na kiburi kuongozwa kwenye maslahi au kupewa tahadhari ya mambo ya ufisadi, yeye hujiona yuko juu ya haki; kama vile alivyo juu ya watu wake anaowatawala, basi itawezekanaje kwa mtu kumwambia amwogope Mwenyezi Mungu.

Na huangamiza mimea na viumbe.

Mimea ni kilimo na viumbe ni wanyama. Makusudio ni maslahi yote ya kiuchumi katika kilimo, viwanda na ufugaji, mali ghafi, na mengineyo yanayohusika na uhai wa watu na maisha yao. Mwenyezi Mungu amehusisha kutaja kilimo na ufugaji kwa vile viwanda wakati huo havikuwa na umuhimu wowote kama ilivyo sasa. Uharamu wa mambo hayo kwa mtazamo wa Uislamu ni sawa na uharamu wa kumwaga damu; na mwenye kukusudia ubaya katika vitu hivyo, ndio amekusudia ubaya wa utu hasa; hata kama vitu hivyo ni milki ya adui anayepiga vita Waislamu. Mtume(s.a.w.w) amekataza kukata miti, kuharibu mimea na majengo na kutia sumu miji ya washirikina siku za vita, n.k. Lau tunailinganisha sharia ya Kiislamu na mambo yanayofanywa leo na dola za kikoloni na vita vyao vya silaha za kemikali kwenye mimea, watu na wanyama, na kuitia sumu anga kwa mabomu ya Atomic na kuyatupa kwa wanawake na watoto, lau hayo yote tunayaunganisha na Uislamu, basi tutajua huruma, uadilifu na utu wa Uislamu na unyama wa dola za Magharibi na jinsi zilivyopetuka mipaka katika dhulma na unyang'anyi.

Na Mwenyezi Mungu (s.w.t.) hapendi ufisadi.

Hakuna uharibifu mkubwa zaidi kuliko kuzusha vita na kutumia silaha zenye kubomoa ili kuwatawala watu na kuwanyang'anya chakula na matunda ya jasho lao.

Na anapoambiwa mche Mwenyezi Mungu hupandwa na mori wa kufanya dhambi.

Mtu mwema wenye ikhlasi anakubali masahihisho na nasaha, bali huzitafuta na kuzikaribisha, kwa sababu yeye hana lengo jengine zaidi ya haki, wala hatafuti sifa; kwa sababu amali yake ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) sio umashuhuri.

Imam Amirul Muminin(a.s) anasema katika maneno anayowasifu wanaomcha Mwenyezi Mungu:"Hawaridhii na amali zao chache wala hawakioni kingi kilicho kingi; wao wanajituhumu na wao ni wenye kunyenyekea katika amali zao."

Katika hotuba yake siku za ukhalifa wake alisema: "Mtu hata kama ana cheo kikubwa katika haki na fadhila kubwa katika dini hawezi kuwa hahitajii kusaidiwa katika aliyobebeshwa na Mungu katika haki zake; wala si mwenye kutaka kujitukuza; wala mtu hata kama nafsi zinamfanya mdogo na kudharauliwa na macho sio kuwa hawezi kusaidia au kusaidiwa... Wala msinidhanie kuwa mimi ni mzito katika haki nitakayoambiwa, kwani mwenye kuifanya nzito haki atakayoambiwa au uadilifu atakaoonyeshwa, basi kwake kuitumia haki na uadilifu ni kuzito zaidi."

Hivyo ndivyo anavyotakikana mwanachuoni mwenye ikhlasi ya kweli. Ama mnafiki mwenye hiana, haki inakuwa nzito juu yake kwa sababu itamfedhehesha; na hununua sifa kwa thamani kubwa ili azibe upungufu wake na uovu wake.

Na katika watu yuko auzaye nafsi yake kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu.

Yaani baadhi ya waumini wanaikabili Jihadi na wanapenda mauti kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. sawa na wale wengine wanaopenda uhai. Hawana lengo jengine isipokuwa kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu na thawabu Zake. Razi katika kutafsiri Aya hii anasema kuhusu sababu za kushuka kwake kuwa kuna riwaya tatu; Mojawapo ni kwamba Aya hii imeshuka kwa sababu ya Ali bin Abi Twalib(a.s) alipolala kwenye kitanda cha Mtume wakati wa Hijra, alisimama Jibril kichwani mwake, Mikail miguuni mwake na Jibril: Pongezi! Pongezi! ewe Ali akisema: Mwenyezi Mungu anajionea fahari kwako, mbele ya Malalika( [7] ).

﴿ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً وَلَا تَتَّبِعُوا خُطُوَاتِ الشَّيْطَانِ إِنَّهُ لَكُمْ عَدُوٌّ مُّبِينٌ﴾

208.Enyi mlioamini! Ingieni katika usalama nyote, wala msifuate nyayo za Shetani. Kwa hakika yeye kwenu ni adui wa wazi.

﴿ فَإِن زَلَلْتُم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْكُمُ الْبَيِّنَاتُ فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

209.Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu, basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima.

﴿ هَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا أَن يَأْتِيَهُمُ اللَّـهُ فِي ظُلَلٍ مِّنَ الْغَمَامِ وَالْمَلَائِكَةُ وَقُضِيَ الْأَمْرُ وَإِلَى اللَّـهِ تُرْجَعُ الْأُمُورُ ﴾

210.Hawangoji ila kuwafikia (adhabu ya) Mwenyezi Mungu katika vivuli vya mawingu na Malaika, na liishe jambo; na mambo yote hurudishwa kwa Mwenyezi Mungu.

INGIENI KATIKA USALAMA NYOTE

Aya 208 - 210

MAANA

Enyi Mlioamini! Ingieni katika usalama nyote.

Imesemekana kuwa makusudio ya neno Silmi hapa ni Uislamu, na kwamba msemo unawaelekea wanafiki ambao wameificha kufuru na kudhihirisha Uislamu. Na imesemekana kuwa msemo unawaelekea wenye kumwamini Mwenyezi Mungu katika Ahlul Kitab ambao hawakusilimu. Na ikasemekana kuwa unawaelekea Waislamu wote kwa hivyo maana yake yanakuwa ni kumtii Mwenyezi Mungu na kumnyenyekea katika hukumu Zake zote sio baadhi. Na pia imesemekana maana yake ni suluhu kwa maana kuwa ingieni katika suluhu nyote. Tuonavyo sisi ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amemwamrisha mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu, kwa imani sahihi kuingia katika lile ambalo lina salama yake ya dunia na akhera. Na njia ya usalama inajulikana na wote, nayo ni kusaidiana, kuungana, na kuacha vita na uhasama. Vile vile kuyashinda matamanio na kuwa na ikhlasi katika kauli na vitendo.

Makusudio ya maneno hayo yanatiliwa nguvu na kauli yake Mwenyezi Mungu:Wala msifuate nyayo za shetani. Kwa hakika yeye kwenu ni adui wa wazi, Aliyoileta mara tu, baada ya kusema.Ingieni katika usalama nyote. Hapo Mwenyezi Mungu amezingatia kuwa nyayo za shetani kinyume chake ni usalama; na amemweka mtu mbele ya mambo mawili tu, hakuna la tatu; Ama kuingia katika usalama au kufuata nyayo za shetani ambazo ndio dhati ya uovu, ugomvi, shari na ufisadi.

Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu, basi jueni ya kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuamrisha kuingia katika usalama na kukataza kufuatwa nyayo za shetani, amemhadharisha yule atakayehalifu amri yake na makatazo yake na akatishia kwa kusema: "Basi jueni kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima." Mwenye nguvu, hashindwi katika amri Yake wala hakimzuwii chochote kwa alilokusudia kulifanya. Mwenye hekima, humlipa mema mtiifu na humwadhibu mwasi. Razi anasema: "Huo ndio ukomo wa kiaga kwa sababu ni kuhofisha bila ya kutaja adhabu. Huenda mzazi akamwambia mtoto wake: "Ukiniasi basi wewe wanijua na wajua uwezo wangu kwako", basi maneno hayo yanakuwa ni makemeo ya ufasaha zaidi kuliko kutaja kipigo na mengineyo.

Hawangoji ila kuwafikia (adhabu ya) Mwenyezi Mungu katika vivuli vya mawingu na Malaika. Maana kwa ujumla ni kwamba wale wenye kukadhibisha na wakaasi watajiwa na adhabu kwa ghafla wala hawataokoka. Aya iko katika mwelekeo wa Aya inayosema:

﴿ فَهَلْ يَنظُرُونَ إِلَّا السَّاعَةَ أَن تَأْتِيَهُم بَغْتَةً ﴾

"Na hawangoji ila saa ya Kiyama kiwajie kwa ghafla...?" (47:18).

Na lishe jambo; na mambo yote hurudishwa kwa Mwenyezi Mungu. Mauti ambayo hapana budi nayo, yakija na Kiyama kikija, kila kitu kitakuwa kimekwisha na hapatabakia mbele ya wenye makosa isipokuwa hisabu na mateso.

SIRI NA MATUKIO YA GHAFLA

Hakuna yeyote ajuaye yatakayomtokea mbele na siri ya wakati, heri au shari. Hawezi kuyajua hayo vyovyote atakavyokuwa na elimu au imani:

"Na nafsi yoyote haijui itachuma nini kesho." (31:34)

Mara nyingi mtu hujiwa na heri kwa ghafla wakati yeye anatazamia kupata shari; na hujiwa ghafla na shari wakati anapotazamia heri. Hakuna kitu kinachotia uchungu kama hicho cha kupata shari wakati wa kutazamia heri; kama vile ambavyo hakuna kitu kitamu kama kupata heri wakati wa kutazamia shari. Mwenye akili hawezi kughurika na alivyo navyo, bali hufikiria mzunguko wa zama; kama vile ambavyo hakati tamaa na lolote linalompata; kwani dunia inageuka milele; ndio maana ikasemwa; "Kudumu hali ni muhali na faraja inakuja kutokana na dhiki." Imam Ali(a.s) anasema:"Baada ya dhiki ni faraja. Anaendelea kusema Imam:"Hakika Musa bin Imran alitoka kuwatafutia watu wake moto akasemeshwa na Mwenyezi Mungu na akarudi akiwa Mtume." Mwenyezi Mungu anasema:

﴿ إِنَّهُ لَا يَيْأَسُ مِن رَّوْحِ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْكَافِرُونَ ﴾

"...Hawakati tamaa ya rehema ya Mwenyezi Mungu isipokuwa watu makafiri." (12:87).

Na amesema tena:

﴿ فَلَا يَأْمَنُ مَكْرَ اللَّـهِ إِلَّا الْقَوْمُ الْخَاسِرُونَ ﴾

... Hawajiaminishi na mipango ya Mwenyezi Mungu ila watu wenye hasara." (7:99).

Imeelezwa katika vitabu vya Historia na Sera kwamba Ibn Ziyat alikuwa waziri na mtu wa kutegemewa na Mu'utasim, naye alikuwa ni katika mataghuti wa hali ya juu na dhalimu mkubwa. Alitengeneza tanuri la chuma alilolijaza misumari yenye ncha pambizoni mwake. Anapomkasirikia mtu humtupa ndani, kila anavyojitingisha ndivyo misumari inavyomwingia mwilini mwake. Mutawakkil alipotawala alimshika Ibn Ziyat na akamfunga kwa chuma mikononi mwake na miguuni mwake kisha akamtupa katika tanuri hilo, na baadaye akafa. Kabla ya kufa alisikika akiimba shairi hili: Sifazake tulia, hebu nenda pole pole, Kigeugeu dunia, huenda nyuma na mbele.

﴿ سَلْ بَنِي إِسْرَائِيلَ كَمْ آتَيْنَاهُم مِّنْ آيَةٍ بَيِّنَةٍ وَمَن يُبَدِّلْ نِعْمَةَ اللَّـهِ مِن بَعْدِ مَا جَاءَتْهُ فَإِنَّ اللَّـهَ شَدِيدُ الْعِقَابِ﴾

211.Waulize wana wa Israil, ishara ngapi zilizo wazi tulizowapa? Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia, basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mkali wa kuadhibu.

﴿ زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُوا الْحَيَاةُ الدُّنْيَا وَيَسْخَرُونَ مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا وَالَّذِينَ اتَّقَوْا فَوْقَهُمْ يَوْمَ الْقِيَامَةِ وَاللَّـهُ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ بِغَيْرِ حِسَابٍ ﴾

212.Wamepambiwa makafiri maisha ya duniani, na wanawafanyia maskhara wale walioamini. Na wale wenye takua watakuwa juu yao Siku ya Kiyama. Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hisabu

WAULIZE WANAWA ISRAIL

Aya 211 – 212

MAANA

Waulize wana wa Israil, ishara ngapi zilizo wazi tulizowapa?

Makusudio ya waulize hapa sio swali hasa la kihakika, kwa sababu Mtume(s.a.w.w) anajua hali zao, wala makusudio sio kuelezea hali waliyokuwa nayo; kama ilivyo katika Aya ya 49 na inayofuatia. Isipokuwa makusudio hasa ni kuwa Waislamu wazingatie na wapate funzo na hali ya Waisrail. Njia ya kupata funzo ni kuwa Waisrail walijiwa na Mtume Musa(a.s) kwa miujiza na hoja ambayo ni mkono kuwa mweupe, fimbo kugeuka nyoka na kupasuka bahari. Vile vile kufunikwa na wingu, kuteremshiwa Manna na Salwa na jabali kutoka maji. Pamoja na hayo yote waliasi na kukhalifu, ndipo Mwenyezi Mungu akawaadhibu kwa madhila na utwevu katika dunia na adhabu iumizayo katika Akhera. Na Waislamu nao wamejiwa na Muhammad(s.a.w.w) kwa miujiza na hoja zinazofahamisha ukweli wa Utume wake na kuswihi sharia yake; naye akawafikilizia habari kutoka kwa Mwenyezi Mungu kuwa waaingie katika Uislamu wote, kwani humo watapata heri na utengeneo wao; kama wakiasi kama walivyofanya Waisrail, basi yatawapata yaliyowapata Waisrail.

Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia, basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu.

Makusudio ya neema hapa ni dalili za haki, kwani hizo ni katika neema kubwa. Kwa sababu ndani yake mna uongofu na kuokoka na kuhiliki na upotevu. Makusudio ya kuzibadilisha ni kuziasi na kuziharibu. Kwa hiyo kauli yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.)Na anayezibadilisha neema za Mwenyezi Mungu baada ya kumfikia ni sawa na kauli yake:

﴿ فَإِن زَلَلْتُم مِّن بَعْدِ مَا جَاءَتْكُمُ الْبَيِّنَاتُ﴾

"Na kama mkiteleza baada ya kuwafikia ubainifu..." (2:209).

Vile vile kusema kwake:

﴿فَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ عَزِيزٌ حَكِيمٌ ﴾

"Basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkali wa kuadhibu" (2:209) ni sawa na kusema Kwamba:Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu Mwenye hekima."

Maana ni moja na lengo ni moja.

HAPANA IMANI BILA TAKUA (UCHA MUNGU)

Wamepambiwa makafiri maisha ya duniani.

Hapana tofauti kati ya mwenye kukanusha kuwapo Mwenyezi Mungu na yule mwenye kuamini kinadharia tu, lakini matendo yakawa ni tofauti. Hapana tofauti kati ya wawili hao. Kwa sababu kila mmoja ameathiriwa na dunia na vipambo vyake, ameathirika na kitu cha sasa hivi kuliko cha muda ujao; heri na manufaa ameyapima kwa kiwango cha manufaa yake, wala hakupima na mambo aliyoharamisha Mwenyezi Mungu wala na msimamo wa kibinadamu. Mimi kila ninavyozidi kuzama katika tafsiri ya Qur'an na kuangalia kwa undani Aya zake, basi huwa na yakini zaidi kwamba imani bila ya ucha Mungu haina maana yoyote; na kwamba kila anayeiangalia dunia kuwa ndio makusudio yake yote, basi atakuwa ameiweka mbali sharia ya haki na dini, atake asitake.

Imekuja Hadith Mutawatir kutoka kwa Mtume Mtukufu akisema: "Dunia na akhera zina madhara" yaani zinadhuriana kuhujumu moja yao nikuiacha nyingine( [8] ).

Imam Ali(a.s) anasema: "Hakika dunia na Akhera ni maadui wawili wanaotofautiana, na ni njia mbili tofauti. Mwenye kuipenda dunia ataichukia akhera na kuwa adui yake; zote mbili ni kama Mashariki na Magharibi, mwenye kutembea kati yao huwa mbali na nyingine kila anapokaribia moja wapo.

" Na wanawafanyia maskhara wale walioamini.

Ni kawaida wale wanaozichezea Hoja za Mwenyezi Mungu na hukumu zake wakihalalisha damu na mali ya haramu kuwadharau na kuwachezea wale wanaojilinda na maharamisho na kuvumilia tabu na mashaka kwa ajili ya kumridhisha Mungu.

Na wale wenye takua watakuwa juu yao siku ya Kiyama.

Amesema wenye takua wala hakusema wale walioamini, kwa sababu imani bila takua si lolote; kama tulivyobainisha. Maana yako wazi ni kuwa makafiri wakiwadharau waumini hivi sasa, basi mambo yatabadilika kesho. Mwenyezi Mungu anasema:

﴿قَالَ الَّذِينَ أُوتُوا الْعِلْمَ إِنَّ الْخِزْيَ الْيَوْمَ وَالسُّوءَ عَلَى الْكَافِرِينَ ﴾

"...Watasema walio pewa ilimu: Hakika hizaya na ubaya leo itawafika makafiri." (16:27).

﴿فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ﴾

"Basi leo wale ambao wameamini wanawacheka makafiri." (83:34)

Na Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye bila hisabu.

Riziki ni mbili ya dunia na riziki ya Akhera. Riziki ya dunia inajulikana na riziki ya Akhera, ni neema isiyokatika na isiyokuwa na chembe ya huzuni au hofu. hataipata yeyote isipokuwa kwa imani na amali njema: Anasema Mwenyezi Mungu:

﴿وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ هُمْ فِيهَا خَالِدُونَ ﴾

"Na wale walioamini na kutenda mema, hao ndio watu wa Peponi, humo watakaa milele." (2:82).

Kila mtu anaweza kupata riziki duniani, awe ni kafiri au Mumin, mwema au mwovu, na anayehangaika au asiyehan-gaika; kama vile urithi, zawadi, wasiya, n.k. Vile vile inaweza kupatikana kwa njia ya halali, au haramu, kama vile kunyang'anya, kughushi na utapeli. Mwenye Tafsir Al-Manar amenakili kutoka kwa mwalimu wake Sheikh Muhammad Abduh kwamba, amesema wakati wa kutafsiri Aya hii, kwamba riziki bila ya kuhangaika inaweza ikapatikana kwa baadhi ya watu. Ama kwa Umma ni muhali kujitosheleza isipoku-wa kwa kuhangaika na kufanya kazi. Huo ni ukweli ulio wazi kabisa.


3

4

5

6

7

8

9

10

11

12

13