TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 19963
Pakua: 2226


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 19963 / Pakua: 2226
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

Mwandishi:
Swahili

13

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

Sura Ya Arubaini Na Mbili: Surat Ash-Shura. Ina Aya 53.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

حم ﴿١﴾

1. Haa Mim.

عسق ﴿٢﴾

2. A’yn Siin Qaaf.

كَذَٰلِكَ يُوحِي إِلَيْكَ وَإِلَى الَّذِينَ مِن قَبْلِكَ اللَّـهُ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿٣﴾

3. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na Mwenye hikima anavyokuletea Wahyi wewe na walio kabla yako.

لَهُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ وَهُوَ الْعَلِيُّ الْعَظِيمُ ﴿٤﴾

4. Ni vyake vilivyomo mbinguni, na vilivyomo ardhini. Na Yeye ndiye Mtukufu, Mkuu.

تَكَادُ السَّمَاوَاتُ يَتَفَطَّرْنَ مِن فَوْقِهِنَّ وَالْمَلَائِكَةُ يُسَبِّحُونَ بِحَمْدِ رَبِّهِمْ وَيَسْتَغْفِرُونَ لِمَن فِي الْأَرْضِ أَلَا إِنَّ اللَّـهَ هُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿٥﴾

5. Zinakaribia mbingu kutatuka juu yao. Na Malaika wakimsabihi Mola wao kwa kumhimidi na wakiwaombea maghufira waliomo kwenye ardhi. Ehe! Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu.

وَالَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ اللَّـهُ حَفِيظٌ عَلَيْهِمْ وَمَا أَنتَ عَلَيْهِم بِوَكِيلٍ ﴿٦﴾

6. Na wale waliowafanya mawalii wengine badala yake Yeye, Mwenyezi Mungu ni Mwangalizi juu yao; wala wewe si wakili juu yao.

وَكَذَٰلِكَ أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لِّتُنذِرَ أُمَّ الْقُرَىٰ وَمَنْ حَوْلَهَا وَتُنذِرَ يَوْمَ الْجَمْعِ لَا رَيْبَ فِيهِ فَرِيقٌ فِي الْجَنَّةِ وَفَرِيقٌ فِي السَّعِيرِ ﴿٧﴾

7. Na namna hivi tumekupa wahyi Qur’an kwa kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa miji na walio pembezoni mwake. Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.

وَلَوْ شَاءَ اللَّـهُ لَجَعَلَهُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَلَـٰكِن يُدْخِلُ مَن يَشَاءُ فِي رَحْمَتِهِ وَالظَّالِمُونَ مَا لَهُم مِّن وَلِيٍّ وَلَا نَصِيرٍ ﴿٨﴾

8. Na Mwenyezi Mungu angelipenda angewafanya umma mmoja. Lakini anamwingiza katika rehema yake amtakaye. Na madhalimu hawana walii wala msaidizi.

HIVYO NDIVYO MWENYEZI MUNGU ANAVYOKULETEA

Aya 1 – 8

MAANA

Haa Mim. A’yn Siin Qaaf.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1). Baadhi ya wafasiri wamesema kuwa ni majina ya Sura hii kubainisha ubora wake juu ya Sura za Hamim nyingine.

Razi amesema: kuzungumzia mianzio hii kunatia dhiki na ni kufungua mlango wa porojo. Lilio bora ni kuachia ujuzi wake kwa Mwenyezi Mungu

Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu Mwenye nguvu na Mwenye hikima anavyokuletea Wahyi wewe na walio kabla yako.

Mwenye nguvu na uweza ambaye anapanga mambo kulingana na kipimo chake na hekima, ameleta wahyi kwako wewe Muhammad na kwa mitume wengine waliokuwa kabla yako.

Ni vyake vilivyomo mbinguni, na vilivyomo ardhini. Na Yeye ndiye Mtukufu, Mkuu.

Yeye peke yake ndiye mfalme wa ulimwengu na viliomo ndani yake, bila ya kuweko mwengine yoyote.

Zinakaribia mbingu kutatuka juu yao.

Makusudio ya mbingu ni sayari za juu; na juu yao ni juu ya hizo mbingu. Maana ni kuwa sayari ambazo zimepandana juu ya nyingine zinakurubia kupasuka kutokana na kauli ya anayesema kuwa Mwenyezi Mungu ana washirika. Mfano wake ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

تَكَادُ السَّمَاوَاتُ يَتَفَطَّرْنَ مِنْهُ وَتَنشَقُّ الْأَرْضُ وَتَخِرُّ الْجِبَالُ هَدًّا ﴿٩٠﴾ أَن دَعَوْا لِلرَّحْمَـٰنِ وَلَدًا ﴿٩١﴾

“Zinakurubia mbingu kutatuka kwa hilo na ardhi kupasuka na milima kuanguka vipande vipande, kwa kudai kwao kuwa Mwingi wa rehema ana mwana.” Juz. 16 (19:90-91).

Na Malaika wakimsabihi Mola wao kwa kumhimidi.

Lau kama Mwenyezi Mungu angelikuwa na washirika, Malaika wasingelimsabihi kwa kumsifu Mwenyezi Mungu ambaye hakuna Mola mwingine isipokuwa Yeye. Imam Ali(a.s ) anasema:“Lau kama Mola wako angelikuwa na mshirika, wangelikujia mitume wake na ungeliona athari za ufalme wake na usultani wake na ungelivijua vitendo vyake na sifa zake.”

Na Malaikawakiwaombea maghufira waliomo kwenye ardhi, waumini na wenye kutubia; kama ilivyoelezwa katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

رَبَّنَا وَسِعْتَ كُلَّ شَيْءٍ رَّحْمَةً وَعِلْمًا فَاغْفِرْ لِلَّذِينَ تَابُوا وَاتَّبَعُوا سَبِيلَكَ ﴿٧﴾

“Na wanawaombea msamaha walio amini. Mola wetu! Umekienea kila kitu kwa rehema na ujuzi. Basi wasamehe ambao wametubu na wakaifuata Njia yako.” Juz. 24 (40:7).

Ehe! Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwenye kurehemu.

Hamnyimi mwenye kuomba rehema na maghufira, vyovyote atakavyokuwa, lakini kwa sharti ya kufuata njia yake ambayo ni toba na ukweli wa nia.

Na wale waliowafanya mawalii wengine badala yake Yeye, Mwenyezi Mungu ni Mwangalizi juu yao. Wala wewe si wakili juu yao.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamwambia Mtume wake kuwa wewe ni mfikishaji unatoa bishara na kuonya tu, na Mwenyezi Mungu ndiye mwenye kuwadhibiti waja na matendo yao, kauli zao na makusudio yao na kuwahisabu nayo. Maana haya yamekaririka kwenye Aya kadhaa.

Hakuna mwenye shaka kuwa hakuna kulazimishwa katika imani, lakini anayevunja heshima ya watu niwajibu kumtia adabu na kumrudi, kwa sababu atakuwa amejivunjia heshima yeye mwenyewe. Na mwenye kuzaliwa Mwislamu kisha akartadi ni wajibu kumuua.

Vile vile Mwislamu akiacha swala au saumu kwa kupuuza atazinduliwaa na kuaziriwa, akiendelea atauawa baada ya kuzinduliwa mara ya nne. Kwa hiyo basi kauli hii ‘wala wewe si wakili juu yao’ itakuwa haihusiki kwenye masula haya au tuseme ilishuka wakati ambapo Mtume hakuwa na nguvu za kutia adabu.

Na namna hivi tumekupa wahyi Qur’an kwa kiarabu ili uwaonye watu wa Mama wa miji na walio pembezoni mwake.

Makusudio ya mama wa miji ni Makka. Yaani mwanzo kabisa utakavyoanza mwito wa Uislamu, ewe Muhammad, uanze na mji wako wa Makka na miji inayoizunguka, kisha ndio uueneze ulimwenguni pote; kama ilivyo miito mingine inaanzia alipozaliwa mtu kisha ndio aieneze kwengine. Tazama Juz.7 (6:92)

Na uhadharishe na Siku ya Mkutano, haina shaka hiyo. Kundi moja litakuwa Peponi, na kundi jengine Motoni.

Siku ya mkutano ni siku ya Kiyama ambayo Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameitolea shaka kutokea kwake, na kuwapambanua siku hiyo watu wa Peponi na wa Motoni. Imeitwa siku ya mkutano kwa vile viumbe watakusanyika siku hiyo kwa hisabu na malipo:

ذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّجْمُوعٌ لَّهُ النَّاسُ وَذَٰلِكَ يَوْمٌ مَّشْهُودٌ ﴿١٠٣﴾

“Hiyo ndiyo siku itakayokusanyiwa watu na hiyo ndiyo siku itakayoshuhudiwa.”

Juz. 12 (11:103).

Na Mwenyezi Mungu angelipenda angewafanya umma mmoja.

Lau Mwenyezi Mungu angeliwachukuwa watu kwenye dini moja kwa nguvu, sifa ya utu ingeliondoka; ambapo angelikuwa, katika hali hii, ni sawa na unyoya kwenye upepo. Umetangulia mfano wake katika Juz. 6 (5:48), Juz. 14 (16:93) na tumelizungumzia hilo kwa ufafanuzi katika Juz. 12 (12:118)

Lakini anamwingiza katika rehema yake amtakaye ambaye ni mumin, kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَالرَّسُولَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ ﴿١٣٢﴾

“Na mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume ili mpate kurehemiwa.” Juz. 4 (3:132).

Na madhalimu hawana walii wala msaidizi kwa sababu wamestahabu upofu kuliko uongofu kwa hiyo ikawanyakua adhabu ya kufedhesha kwa yale waliyokuwa wakiyachuma.

أَمِ اتَّخَذُوا مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءَ فَاللَّـهُ هُوَ الْوَلِيُّ وَهُوَ يُحْيِي الْمَوْتَىٰ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٩﴾

9. Au wamechukua mawalii wengine badala yake! Lakini Mwenyezi Mungu ndiye walii hasa. Na Yeye ndiye anayehuisha wafu. Na Yeye ni Muweza wa kila kitu.

وَمَا اخْتَلَفْتُمْ فِيهِ مِن شَيْءٍ فَحُكْمُهُ إِلَى اللَّـهِ ذَٰلِكُمُ اللَّـهُ رَبِّي عَلَيْهِ تَوَكَّلْتُ وَإِلَيْهِ أُنِيبُ ﴿١٠﴾

10. Na mkikhitalifiana katika jambo lolote, basi hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu. Huyo Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu ninayemtegemea na kwake Yeye narejea.

فَاطِرُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ جَعَلَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا وَمِنَ الْأَنْعَامِ أَزْوَاجًا يَذْرَؤُكُمْ فِيهِ لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ وَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ ﴿١١﴾

11. Muumba mbingu na ardhi. Amewajaalia mke na mume katika nafsi zenu, na katika wanyama howa dume na jike, anawazidisha namna hii. Hakuna chochote kama mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona.

لَهُ مَقَالِيدُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ يَبْسُطُ الرِّزْقَ لِمَن يَشَاءُ وَيَقْدِرُ إِنَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿١٢﴾

12. Yeye ndiye Mwenye funguo za mbingu na ardhi. Humkunjulia riziki amtakaye, na humpimia amtakaye. Hakika Yeye ni Mjuzi wa kila kitu.

شَرَعَ لَكُم مِّنَ الدِّينِ مَا وَصَّىٰ بِهِ نُوحًا وَالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ وَمَا وَصَّيْنَا بِهِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَىٰ أَنْ أَقِيمُوا الدِّينَ وَلَا تَتَفَرَّقُوا فِيهِ كَبُرَ عَلَى الْمُشْرِكِينَ مَا تَدْعُوهُمْ إِلَيْهِ اللَّـهُ يَجْتَبِي إِلَيْهِ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي إِلَيْهِ مَن يُنِيبُ ﴿١٣﴾

13. Amewapa sharia ya Dini aliyomuusia Nuh na tuliyokupa wahyi wewe, na tuliyowausia Ibrahim na Musa na Isa, kwamba simamisheni Dini wala msifarikiane kwayo. Ni magumu kwa washirikina hayo unayowaitia. Mwenyezi Mungu humteua kwake amtakaye, Na humwongoa kwake aelekeaye.

وَمَا تَفَرَّقُوا إِلَّا مِن بَعْدِ مَا جَاءَهُمُ الْعِلْمُ بَغْيًا بَيْنَهُمْ وَلَوْلَا كَلِمَةٌ سَبَقَتْ مِن رَّبِّكَ إِلَىٰ أَجَلٍ مُّسَمًّى لَّقُضِيَ بَيْنَهُمْ وَإِنَّ الَّذِينَ أُورِثُوا الْكِتَابَ مِن بَعْدِهِمْ لَفِي شَكٍّ مِّنْهُ مُرِيبٍ ﴿١٤﴾

14. Na hawakufarikiana ila baada ya kuwajia ilimu kwa sababu ya uhasidi baina yao. Na lau si neno lililokwishatangulia kutoka kwa Mola wako mpaka muda uliowekwa, basi bila ya shaka palingelihukumiwa baina yao. Na hakika waliorithishwa Kitabu baada yao wanamtilia shaka inayowahangaisha.

SIMAMISHENI DINI WALA MSIFARIKIANE

Aya 9 – 14

MAANA

Au wamechukua mawalii wengine badala yake! Lakini Mwenyezi Mungu ndiye walii hasa. Na Yeye ndiye anayehuisha wafu. Na Yeye ni Muweza wa kila kitu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusema katika Aya ya 6: ‘Na wale waliowafanya mawalii wengine badala yake Yeye, Mwenyezi Mungu ni Mwangalizi juu yao,’ hapa amerudia tena kauli hii na kuzidisha kuwa Yeye peke yake ndiye Mwenye kunusuru, Mwenye kusaidia, Mwenye kuhuisha, Mwenye kufisha na Muweza wa kila kitu.

Amerudia pamoja na ziada hii ili kumpinga anayemfanyia washirika; kwamba asiyekuwa Yeye hawezi kuleta uhai wala mauti au kusaidia, kwa vile hawezi kila kitu.

Na mkikhitalifiana katika jambo lolote, basi hukumu yake iko kwa Mwenyezi Mungu.

Huyo Mwenyezi Mungu ndiye Mola wangu ninayemtegemea na kwake Yeye narejea.

Haya ni masimulizi ya maneno ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) akiwaambia watu wote kwamba kila kitu watakachikhitalifiana kuwa ni haki au batili, basi rejea ni Qur’an; kauli yake ni ya upambanuzi na hukumu yake ni ya uadilifu.

Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na kama mkipingana katika jambo, basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake mkiwa mwamwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho. Hilo ni bora zaidi na mwisho mzuri.” Juz. 5 (4:95).

Muumba mbingu na ardhi.

Ameziumba na akazipangilia, wala hakuna tofauti kwa Mwenyezi Mungu baina ya kuumba mbingu na ardhi na kuumba mdudu chungu. Amempangilia vizuri hivi, kama alivyoupangilia ulimwengu.

Amewajaalia mke na mume katika nafsi zenu, ili mpate utulivu:

وَمِنْ آيَاتِهِ أَنْ خَلَقَ لَكُم مِّنْ أَنفُسِكُمْ أَزْوَاجًا لِّتَسْكُنُوا إِلَيْهَا وَجَعَلَ بَيْنَكُم مَّوَدَّةً وَرَحْمَةً إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَاتٍ لِّقَوْمٍ يَتَفَكَّرُونَ ﴿٢١﴾

”Na katika ishara zake ni kuwaumbia wake kutokana na nafsi zenu ili mpate utulivu kwao. Na akajaalia mapenzi na huruma baina yenu. Hakika katika haya kuna ishara kwa watu wanaofikiri.” Juz. 21 (30:21).

Na katika wanyama howa dume na jike, anawazidisha namna hii.

Yaani Mwenyezi Mungu amewafanya watu na wanyama waume na wake ili wazidi kuwa wengi. Na kuzidi huku ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Hakuna chochote kama mfano wake, si katika dhati yake wala sifa zake, kwa vile Yeye ni zaidi ya kila kitu. Hakuna Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu mmoja Mwenye nguvu.Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona, anasikia kauli zote na kuona matendo yote.

Yeye ndiye Mwenye funguo za mbingu na ardhi. Humkunjulia riziki amtakaye, na humpimia amtakaye. Hakika Yeye ni Mjuzi wa kila kitu.

Riziki za mbinguni na ardhini ziko mikononi mwa Mwenyezi Mungu. Humpanulia amtakaye na humfinyia amtakaye kutokana na hekima yake inavyotaka. Hakuna mwenye shaka kwamba uchache wa mali pamoja na afya, amani, dini na utengenevu ni bora mara elfu kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na hofu, ugonjwa, ukafiri na ufisadi. Tumezungumzia rizi kwa anuani ya: ‘Riziki na ufisadi’ Juz. 6 (5:66), ‘Je, riziki ni bahati au majaliwa’ Juz. 7 (5:100) na ‘Mtu na riziki’ Juz. 13 (13:26).

Amewapa sharia ya Dini aliyomuusia Nuh na tuliyokupa wahyi wewe, na tuliyowausia Ibrahim na Musa na Isa, kwamba simamisheni Dini wala msifarikiane kwayo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwatuma mitume wote kwa tamko la Tawhid, kuamini siku ya mwisho, kusimaisha Swala na kutoa Zaka. Vile vile kuharamisha dhulma, ghushi, uongo na zina. Pia kuharamisha kuoa mama, binti, dada na mengineyo ya misingi ya dini na sharia, lakini sio matawi ya dini ambayo yanatofautiana kulingana na wakati na masilahi; kama alivyoashiria Mwenyezi Mungu kwa kusema:

لِكُلٍّ جَعَلْنَا مِنكُمْ شِرْعَةً وَمِنْهَاجًا ﴿٤٨﴾

“Na kila (umma) katika nyinyi tumeujaalia sharia (yake) na njia” Juz. 6 (5:48).

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuhusisha kumtaja Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na Muhammad, kwa vile tu wao ni mitume ulul-azm, vinginevyo ni kuwa huyo anayeusiwa ni mmoja kwa mitume wote.

Ikiwa Mungu ni mmoja, dini ni moja na mwito ni mmoja, basi kuna haja gani ya uadui na kuchinjana katika dini? Kuna sababu gani ya vita vilivyosajiliwa na historia kwa herufi za fedheha na aibu?

Tumezungumza kwa ufafanuzi zaidi kuhusu mwito wa mitume na kwam- ba wao wako kwenye dini moja katika Juz. 3 (3:18–20) kifungu cha ‘Dini ya Mwenyezi Mungu ni uislamu’ na tukafuatishia kuzungumzia tofauti baina ya dini na madhehebu kwenye kifungu ‘Vikundi sabini na tatu.’

Vile vile tumezungumzia kwenye Juz.1(2:111) kifungu cha ‘Ualanguzi wa Pepo’ na tukafuatishia na kifungu cha: “Kila mmoja avutia kwake’

Ni magumu kwa washirikina hayo unayowaitia ewe Muhammad, kwa sababu kwanza, wewe si mfalme wala huna mali. Pili, wewe unalingania kwenye haki, wala hakuna kitu kizito zaidi kuliko hicho kwa watu wa matamanio na wabatilifu. Tatu, kuwa wewe umewaita mababa zao wajinga na wapotevu.

Mwenyezi Mungu humteua kwake amtakaye, na amekuchagua wewe ewe Muhammad kuwa ni mtu wa risala yake na akakuishilizia kwa mitume wote, ambapo huna kifani na yeyote kuanzia wa kwanza hadi wa mwisho.

Na humwongoa kwake aelekeaye.

Kila anayekimbilia kwa Mwenyezi Mungu kwa ukweli na ikhlasi basi Mwenyezi Mungu humwitikia na kumwongoza:

وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ يَهْدِ قَلْبَهُ ﴿١١﴾

“Na mwenye kumwamini Mwenyezi Mungu huuongoa moyo wake.” (64:11).

Na hawakufarikiana ila baada ya kuwajia ilimu kwa sababu ya uhasidi baina yao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 2 (2:213) na Juz. 3 (3:19)

Na lau si neno lililokwishatangulia kutoka kwa Mola wako mpaka muda uliowekwa, basi bila ya shaka palingelihukumiwa baina yao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:19), Juz. 12 (11:110), Juz. 16 (20:110) na Juz. 24 (41:45)

Na hakika waliorithishwa Kitabu baada yao wanamtilia shaka inayowahangaisha.

Makusudio ya waliorithishwa kitabu ni mayahudi na manaswara. Baada yao ni mtume au uma zilizotangulia na wanayemtilia shaka ni Muhammad kutokana na inavyofahamisha kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Mwenyezi Mungu humteua kwake amtakaye.’ Maana ni kuwa watu wa Kitabu walipinga aliyokuja nayo Muhammad(s.a.w. w ) pamoja na ushahidi wazi wa utume wake na ukweli wa risala yake.

14

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

فَلِذَٰلِكَ فَادْعُ وَاسْتَقِمْ كَمَا أُمِرْتَ وَلَا تَتَّبِعْ أَهْوَاءَهُمْ وَقُلْ آمَنتُ بِمَا أَنزَلَ اللَّـهُ مِن كِتَابٍ وَأُمِرْتُ لِأَعْدِلَ بَيْنَكُمُ اللَّـهُ رَبُّنَا وَرَبُّكُمْ لَنَا أَعْمَالُنَا وَلَكُمْ أَعْمَالُكُمْ لَا حُجَّةَ بَيْنَنَا وَبَيْنَكُمُ اللَّـهُ يَجْمَعُ بَيْنَنَا وَإِلَيْهِ الْمَصِيرُ ﴿١٥﴾

15. Basi kwa hiyo waite! Nawe simama sawa sawa kama ulivyoamrishwa, wala usifuate matamanio yao. Na sema: Naamini aliyoteremsha Mwenyezi Mungu katika Kitabu. Na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu. Mwenyezi Mungu ni Mola wetu, na Mola wenu. Vitendo vyetu ni kwa ajili yenu, na vitendo vyenu ni kwa ajili yenu. Hapana ugomvi baina yetu na yenu. Na Mwenyezi Mungu atatukusanya pamoja, na marejeo ni kwake.

وَالَّذِينَ يُحَاجُّونَ فِي اللَّـهِ مِن بَعْدِ مَا اسْتُجِيبَ لَهُ حُجَّتُهُمْ دَاحِضَةٌ عِندَ رَبِّهِمْ وَعَلَيْهِمْ غَضَبٌ وَلَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ﴿١٦﴾

16. Na wanaohojiana juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kukubaliwa. Hoja zao ni batili mbele ya Mola wao, na juu yao ipo ghadhabu, na itakuwa kwao adhabu kali.

اللَّـهُ الَّذِي أَنزَلَ الْكِتَابَ بِالْحَقِّ وَالْمِيزَانَ وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّ السَّاعَةَ قَرِيبٌ ﴿١٧﴾

17. Mwenyezi Mungu ndiye aliyeteremsha Kitabu kwa Haki na Mizani. Na nini kitakujulisha pengine Saa ipo karibu.

يَسْتَعْجِلُ بِهَا الَّذِينَ لَا يُؤْمِنُونَ بِهَا وَالَّذِينَ آمَنُوا مُشْفِقُونَ مِنْهَا وَيَعْلَمُونَ أَنَّهَا الْحَقُّ أَلَا إِنَّ الَّذِينَ يُمَارُونَ فِي السَّاعَةِ لَفِي ضَلَالٍ بَعِيدٍ ﴿١٨﴾

18. Wasioamini huihimiza hiyo Saa ifike upesi, lakini wanaoamini wanaiogopa, na wanajua kwamba hakika hiyo ni kweli. Ehe! Hakika hao wanaobishana katika hiyo Saa wamo katika upotofu wa mbali kabisa.

KUWA NA MSIMAMO KAMA ULIVYOAMRISHWA

Aya 15 – 18

MAANA

Basi kwa hiyo waite! Nawe simama sawa sawa kama ulivyoamrishwa,

‘Hiyo’ ni hiyo dini. Maana ni kuwa ewe Muhammad! Lingania kwenye dini safi aliyowausia Mwenyezi Mungu (s.w.t) mitume wote; na uwe imara kwenye hiyo dini na kwenye mwito wake. Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 12 (11:113). Huko tumezungumzia kusimama na sawa sawa (msimamo) na mafungu yake.

Wala usifuate matamanio yao.

Nabii ni maasumu anafuata anayopewa wahyi, wala hafuati matamanio ya wengine. Mara nyingi tumesema kuwa kukataza kitu hakufahamishi kuwa kinaweza kutokea kwa anayekatazwa, na kwamba aliye juu anaweza kumkataza yeyote anachotaka. Jumla hii Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 6 (5:48).

Na sema: Naamini aliyoteremsha Mwenyezi Mungu katika Kitabu. Na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu. Mwenyezi Mungu ni Mola wetu, na Mola wenu. Vitendo vyetu ni kwa ajili yenu, na vitendo vyenu ni kwa ajili yenu. Hapana ugomvi baina yetu na yenu. Na Mwenyezi Mungu atatukusanya pamoja, na marejeo ni kwake.

Ewe Muhammad! Tangaza imani yako kwa watu katika vitabu vyote alivyoviteremsha Mwenyezi Mungu kwa vyovyote iwavyo; na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mola wa wote. Wewe unahukumu kwa uadilifu ukichunga haki ya mdhulumiwa kutoka kwa dhalimu, unachukua kisasi cha mnyonge kutoka kwa dhaifu hata kama ni ndugu. Vile vile utangaze kwamba kila mtu ana majukumu ya matendo yake mbele ya Mwenyezi Mungu yeye peke yake, huna ugomvi na mtu yeyote na kwamba marejeo ni kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu ailipe kila nafsi ilichokichuma.

Kwa njia hii iliyo sawa na mantiki yaliyo salama, utaweza kusimamisha hoja kwa maadui zako na hawatabaki na vijisababu vyovyote.

Na wanaohojiana juu ya Mwenyezi Mungu baada ya kukubaliwa. Hoja zao ni batili mbele ya Mola wao, na juu yao ipo ghadhabu, na itakuwa kwao adhabu kali.

Watu wa Kitabu walikuwa wakibishana na waislamu na wakijaribu kuwatoa kwenye dini yao baada ya Mwenyezi Mungu kuwaongoza kwenye Uislamu. Kuna mapokezi katika Tafsir At-Tabari kwamba mayahudi na wanaswara walikuwa wakiwaambia waislmu: “Kitabu chetu kimekuja kabla ya chenu na Mtume wetu ni kabla ya wenu, kwa hiyo sisi ni bora kuliko nyinyi.”

Haya si mageni katika ubishi wa maadui wa haki na dini, lakini hoja yao ni batili, kwa sababu ubora unakuwa kwa matendo sio kwa wakati na kutangulia; vinginevyo angelikuwa ibilisi ni bora kuliko Adam (a.s.), kwa vile amemtangulia.

Vyovyote iwavyo, mwisho wa ubishi wa batili ni maangamivu na hasara dunini na Akhera.

Mwenyezi Mungu ndiye aliyeteremsha Kitabu kwa Haki na Mizani.

Makusudio ya Kitabu ni Qur’an na mizani ni uadilifu. Maana ni kuwa kushuka kwake ni haki, kila kilichomo ndani yake ni haki na inakubali kila lilio haki. Maana ya kushuka kwake kwa uadilifu ni kuwa inahukumu baina ya watu kwa uadilifu. Uadilifu unahitaji pande mbele kinyume cha haki; yaani haki ni kwa ujumla. Kwa hiyo kila uadilifu ni haki, lakini sio kila haki ni uadilifu. Jua ni haki liko, lakini sio uadlifu.

Na nini kitakujulisha pengine Saa ya Kiyamaipo karibu.

Hili ni jawabu la kauli ya wanaofanya stihizai wakiuliza: Kiyama kitakuwa lini? Kuhusu ukaribu wake ni kuwa kila kinachokuja kiko karibu na mwenye kufa kiyama chake kimeanza.

Wasioamini huihimiza hiyo Saa ifike upesi kwa stihzai.

Mara ngapi anayehimiza jambo likimfika hutamani angelikuwa mbali nalo kwa umbali wa mashariki na magharibi.

Lakini wanaoamini wanaiogopa, na wanajua kwamba hakika hiyo ni kweli.

Ndio! Kwa sababu wanaijua hakika yake kama vile wamekiona, ndio maana wakakihofia. Miongoni mwa aliyoyasema Imam Ali(a.s ) kuhusiana nacho ni: “Hofu imewachoma kama mshale.

Mtu akiwaangalia anawadhania ni wagonjwa, lakini jamaa hawana ugonjwa wowote. Wanasema: wamechanganyikiwa! Ndio kuna jambo kubwa limewafanya wachanganyikiwe.”

Kuna mshairi mmoja alitunga kuhusiana na maana haya: ref nguzo pg 518. Wanaambiwa ni wagonjwa wala sivyo, Au wamechanganyikiwa kamwe sivyo, Hofu imekuwa sawa na matarajio, Si kikomo cha hofu wala matamanio,

Ehe! Hakika hao wanaobishana katika hiyo Saa wamo katika upotofu wa mbali kabisa.

Upotevu wa mbali ni kuzama kabisa kwenye upotevu, kwa sababu wanakanusha ufufuo wa mwisho na hali wao wameona ufufuo wa kwanza.

اللَّـهُ لَطِيفٌ بِعِبَادِهِ يَرْزُقُ مَن يَشَاءُ وَهُوَ الْقَوِيُّ الْعَزِيزُ ﴿١٩﴾

19. Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake. Humruzuku ampendaye. Naye ni Mwenye nguvu, Mwenye kushinda.

مَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الْآخِرَةِ نَزِدْ لَهُ فِي حَرْثِهِ وَمَن كَانَ يُرِيدُ حَرْثَ الدُّنْيَا نُؤْتِهِ مِنْهَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِن نَّصِيبٍ ﴿٢٠﴾

20. Mwenye kutaka mavuno ya Akhera tutamzidishia katika mavuno yake, na mwenye kutaka mavuno ya duniani tutampa katika hayo, lakini katika Akhera hana fungu.

أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ شَرَعُوا لَهُم مِّنَ الدِّينِ مَا لَمْ يَأْذَن بِهِ اللَّـهُ وَلَوْلَا كَلِمَةُ الْفَصْلِ لَقُضِيَ بَيْنَهُمْ وَإِنَّ الظَّالِمِينَ لَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢١﴾

21. Au wana washirika waliowawekea dini asiyoitolea idhini Mwenyezi Mungu? Na lau lisingekuwako neno la kupambanua basi wangelikatiwa hukumu baina yao. Na hakika wenye kudhulumu watapata adhabu chungu.

تَرَى الظَّالِمِينَ مُشْفِقِينَ مِمَّا كَسَبُوا وَهُوَ وَاقِعٌ بِهِمْ وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ فِي رَوْضَاتِ الْجَنَّاتِ لَهُم مَّا يَشَاءُونَ عِندَ رَبِّهِمْ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَضْلُ الْكَبِيرُ ﴿٢٢﴾

22. Utawaona hao madhalimu wanavyokuwa na hofu kwa sababu ya waliyoyachuma, nayo yatawafika tu. Na walioamini na wakatenda mema watakuwamo katika mabustani ya Peponi. Humo watapata wayatakayo kwa Mola wao. Hiyo ndiyo fadhila kubwa.

MWENYEZI MUNGU NI MPOLE KWA WAJA WAKE

Aya 19 – 22

MAANA

Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake. Humruzuku ampendaye. Naye ni Mwenye nguvu, Mwenye kushinda.

Katika Aya hii Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametaja kuwa Yeye ni mpole Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu na Mwenye kushinda. Makusudio ya upole ni kufanya wema. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

إِنَّهُ هُوَ الْبَرُّ الرَّحِيمُ ﴿٢٨﴾

“Hakika Yeye ndiye mwema Mwenye kurehemu.” (52:28).

Maana ya kuruzuku ni kuwa Mwenyezi Mungu anampa mtu nguvu zote za maandalizi ya kufanya kazi ya kupata riziki na kumuongoza kwenye njia yake, kuongezea kuwa kheri zote zilizo ardhini na mbinguni ameziten- geneza Yeye kwa ufadhili wake. Ama kuwa na nguvu na kushinda ni kuwa Yeye hashindwi na lolote wala hakuna kitu asichokiweza ardhini au mbinguni.

Mwenye kutaka mavuno ya Akhera tutamzidishia katika mavuno yake, na mwenye kutaka mavuno ya duniani tutampa katika hayo, lakini katika Akhera hana fungu.

Mwenye kuitumikia Akhera atapata malipo ya aliyoyafanya na Mwenyezi Mungu atamzidishia ziada nyingi tu, na hatapunguziwa kitu duniani.

Hakuna mwenye shaka kwamba kufanya bidii kwa ajili ya maisha ni katika kuitumikia Akhera vile vile, lakini mwenye kuitumikia dunia peke yake na kuiacha Akhera, atastarehe siku kidogo tu, kisha atahamia kwenye adhabu ya daima. Watakokuwa na hali mbaya zaidi ni wale wanaoifanyia biashara dini na kuitafuta dunia kwa kazi ya Akhera kiunafiki na ria.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:145), Juz. 15 (17; 18-19).

Au wana washirika waliowawekea dini asiyoitolea idhini Mwenyezi Mungu?

Ni swali la kukana na kutahayariza. Makusudio ya washirika ni mashetani watu na majini. Kuwawekea ni kuwadanganya na kuwapambia pambia. Maana ni kuwa, kwa nini wakosefu wanaitumikia dunia na kuisahau Akhera? Je, ni kwa kuwa wana mashetani wanaowazuia nayo kwa kuwatia wasiwasi na mambo yasiyokuwa kwenye dini?

Kisha Mwenyezi Mungu amewatishia kwa kusema:Na lau lisingekuwako neno la kupambanua basi wangelikatiwa hukumu baina yao. Na hakika wenye kudhulumu watapata adhabu chungu.

Hekima Yake Mwenyezi Mungu Mtukufu imetaka kuiahirisha adhabu ya wakosefu hadi siku ya ufufuo; vinginevyo angelimpatiliza kwa adhabu kila mkosefu mwenye dhambi.

Utawaona hao madhalimu wanavyokuwa na hofu kwa sababu ya waliyoyachuma, nayo yatawafika tu. Na walioamini na wakatenda mema watakuwamo katika mabustani ya Peponi. Humo watapata wayatakayo kwa Mola wao. Hiyo ndiyo fadhila kubwa.

Kesho itapita hisabu kwa matendo yote. Mwenye kutenda mema atakuwa katika amani na Pepo, humo atapata kila analolipenda na kulitaka; na mwenye kufanya maovu atakuwa katika hofu ya hasira za Mwenyezi Mungu na adhabu yake. Adhabu hiyo itamfika tu, ikiwa ni malipo kwa iliyochuma mikono yake.

NITII UTAKUWA MFANO WANGU

Hapo mwanzoni nilikuwa nikizitilia shaka Hadith mbili nilizokuwa nikizisikia mara kwa mara masikioni mangu: Ya kwanza ni Hadith Qudsi isemayo:“Ewe mja wangu nitii utakuwa mfano wangu, utakiambia kitu kuwa na kinakuwa.” Na nyingine ni ya Mtume isemayo: “Hakika Mwenyezi Mungu ana waja wakitaka naye hutaka.”

Nilikuwa nikitilia shaka mategemezi ya Hadith mbili hizi, kwa vile sikuzionea athari yoyote katika maisha haya. Kisha nikagundua, wakati nikifasiri Aya za Qur’an yenye hekima, kuwa maudhui ya Hadith hizi ni ya Akhera si ya dunia, basi shaka yangu ikaniondokea na nikawa na yakini kuwa Hadith mbili hizi ni tafsiri na ubainifu wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Na walioamini na wakatenda mema watakuwamo katika mabustani ya Peponi. Humo watapata wayatakayo kwa Mola wao.’

Na mfano wa Aya hiyo.

ذَٰلِكَ الَّذِي يُبَشِّرُ اللَّـهُ عِبَادَهُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ قُل لَّا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ أَجْرًا إِلَّا الْمَوَدَّةَ فِي الْقُرْبَىٰ وَمَن يَقْتَرِفْ حَسَنَةً نَّزِدْ لَهُ فِيهَا حُسْنًا إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ شَكُورٌ ﴿٢٣﴾

23. Hayo ndiyo aliyowabashiria Mwenyezi Mungu waja wake walioamini na wakatenda mema. Sema: kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu. Na anayefanya wema tutamzidishia wema. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwingi wa shukrani.

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَىٰ عَلَى اللَّـهِ كَذِبًا فَإِن يَشَإِ اللَّـهُ يَخْتِمْ عَلَىٰ قَلْبِكَ وَيَمْحُ اللَّـهُ الْبَاطِلَ وَيُحِقُّ الْحَقَّ بِكَلِمَاتِهِ إِنَّهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٢٤﴾

24. Au wanasema: Amemzulia Mwenyezi Mungu uwongo? Mwenyezi Mungu akipenda atapiga muhuri juu ya moyo wako. Na Mwenyezi Mungu anaifuta batili na anaithibitisha Haki kwa maneno yake. Hakika Yeye anayajua yaliyomo vifuani.

وَهُوَ الَّذِي يَقْبَلُ التَّوْبَةَ عَنْ عِبَادِهِ وَيَعْفُو عَنِ السَّيِّئَاتِ وَيَعْلَمُ مَا تَفْعَلُونَ ﴿٢٥﴾

25. Naye ndiye anayepokea toba kwa waja wake, na anasamehe makosa. Na anayajua mnayoyatenda.

وَيَسْتَجِيبُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَيَزِيدُهُم مِّن فَضْلِهِ وَالْكَافِرُونَ لَهُمْ عَذَابٌ شَدِيدٌ ﴿٢٦﴾

26. Na anawaitikia walioamini na wakatenda mema, na anawazidishia fadhila zake. Na makafiri watakuwa na adhabu kali.

NI NANI HAO NDUGU?

Aya 23 – 26

MAANA

Hayo ndiyo aliyowabashiria Mwenyezi Mungu waja wake walioamini na wakatenda mema.

‘Hayo’ ni hayo ya fadhila kubwa ambayo Mwenyezi Mungu amewaandalia wenye takua huko Akhera. Ameyaeleza kwenye kitabu kuwa ni bishara ili nyoyo zao zitulie.

Sema: Kwa haya siwaombi malipo yoyote kwenu isipokuwa mapenzi katika ndugu.

Katika tafsiri ya Al-Bahrul-muhit ya Abu Hayan Al-Andalusi na Ruhul-bayani ya Ismail Haqqi, kuna maelezo haya: “Iliposhuka Aya hii, Mtume(s.a.w. w ) aliulizwa: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu: ni kina nani hao ndugu zako tuliowajibishiwa kuwapenda?Akasema: Ali, Fatima, Hasan na Husein.”

Ibn Al-arabi anasema katika Futuhati, kwa anuani ya ‘La takhunullah war-rasul’ (msimfanyie hiyana Mwenyezi Mungu na Mtume): “Mtume wa Mwenyezi Mungu ametutaka tuwapende akraba wake na watu wa nyumba yake (Ahlbayt) na yeye pia anaingia, kwa vile pendo la Ahlu Bayt haligawanyiki.

Kwa sababu mwenye kuwafanyia hiyana watu wa nyumba ya Mtume ndio amemfanyia hiyana Mtume. Na haishii hapo, kwa sababu mwenye kumfanyia hiyana Mtume wa Mwenyezi Mungu ndio amemfanyia hiyana Mwenyezi Mungu.”

Baadhi ya wafasiri wamenukuu riwaya katika mategemezi yake Muawiya kuwa maana ya Aya hii ni, sema ewe Muhammad kuwaambia makuraishi kuwa msiniudhi na ndugu zangu.

Katika Tafsir Gharaibul-Furqani ya Nidhamuddin Al-Hasan bin Muhammad An-naysaburi, amesema: “Imepokewa kwa Sai’d bin Jubayr, kuwa iliposhuka Aya hii walisema: Ni nani hao ambao Mwenyezi Mungu amewajibisha kuwapenda? Akasema: Ali, Fatima na watoto wao wawili. Hapana shaka kwamba hii ni fahari kubwa na utukufu uliokamilika.

Hiyo inatiliwa nguvu na riwaya kuwa Ali siku moja alimshtakia Mtume husuda ya watu kwake. Mtume akamwambia: “Kwani huridhii kuwa wane wa wane! Wa kwanza atakayeingia Peponi ni mimi na wewe na Hasan na Husein, na wake wetu wakiwa kuumeni kwetu na kushotoni kwetu na dhuria wetu wakiwa nyuma ya wake wetu.”

Imepokewa kutoka kwa Mtume amesema: “Pepo imeharamishiwa mwenye kuwadhulumu watu wa nyumba yangu na akaniudhi kwa kizazi changu.” Na alikuwa akisema: “Fatima ni sehemu yangu linaniudhi lile linalomuudhi.”Imethibiti kwa nukuu mutawatir kwamba yeye alikuwa akimpenda Ali, Hasan na Hussein na akatuwajibishia kuwapenda.

Ni utukufu kwa watu wa Mtume kuishilizwa tashahhud kwa kutajwa wao na kuswalia katika kila swala. Na akasema: mfano wa watu wa nyumba yangu ni kama Safina ya Nuh, mwenye kuipanda aliokoka na aliyeiacha aliangamia.” Mwisho wa kunukuu.

Na anayefanya wema tutamzidishia wema.

Mfano wake ni:

مَن جَاءَ بِالْحَسَنَةِ فَلَهُ عَشْرُ أَمْثَالِهَا ﴿١٦٠﴾

“Mwenye kufanya vizuri atalipwa mfano wake mara kumi.” Juz. 8 (6:160).

Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira Mwingi wa shukrani; yaani anawapa thawabu wenye kushukuru.Au wanasema: Amemzulia Mwenyezi Mungu uwongo? Mwenyezi Mungu akipenda atapiga muhuri juu ya moyo wako.

Wazushi wanasema kuwa wewe Muhammad unamzulia Mwenyezi Mungu kwa kudai kwako utume na hawajui kwamba Mwenyezi Mungu amekuhifadhi na makosa na hatia. Na hata kama ungejaribu – kukisia muhali sio muhali – basi Mwenyezi Mungu angelipiga muhuri moyo wako na kukuzuia kwa nguvu.

Na Mwenyezi Mungu anaifuta batili na anaithibitisha Haki kwa maneno yake.

Wewe Muhammad uko kwenye haki na maadui zako wako kwenye ubatilifu; na Mwenyezi Mungu ataiondoa batili na ataithibitisha haki kwa dalili na ubainifu ulio wazi aliokuunga mkono nao Mwenyezi Mungu na kulifanya neno lako liko juu na neno la maadui wako liko chini pamoja na wingi wao na wanavyokuduilia wewe na Uislamu.

Hakika Yeye anayajua yaliyomo vifuani.

Anayajua yanayofichwa na nyoyo zilizo vifuani na atawalipa wenye nyoyo hizo wanayostahiki iwe ni thawabu au adhabu.

Naye ndiye anayepokea toba kwa waja wake, na anasamehe makosa.

Mwenye kufanya dhambi kisha akatubia, Mwenyezi Mungu humkubalia toba yake na humsamehe dhambi yake isipokuwa haki ya watu.

Vile vile akiwa na mema yaliyo sawa na maovu, yasiyohusika na haki za watu, basi Mwenyezi Mungu humsamehe maovu yote na kubakia kama mtu ambaye hakufanya wema wala uovu. Ikiwa mema yatayazidi maovu basi atabakiwa na yale yaliyozidi.

Haya yanasadikishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الْحَسَنَاتِ يُذْهِبْنَ السَّيِّئَاتِ ذَٰلِكَ ذِكْرَىٰ لِلذَّاكِرِينَ ﴿١١٤﴾

“Hakika mema huondoa maovu. Hiyo ni ukumbusho kwa wanaokumbuka.” Juz. 12 (11:114)

Pia kauli yake:

وَآخَرُونَ اعْتَرَفُوا بِذُنُوبِهِمْ خَلَطُوا عَمَلًا صَالِحًا وَآخَرَ سَيِّئًا عَسَى اللَّـهُ أَن يَتُوبَ عَلَيْهِمْ إِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٠٢﴾

“Na wengine wamekiri dhambi zao; wakachanganya vitendo vyema na vingine viovu. Huenda Mwenyezi Mungu akapokea toba zao.” Juz.11(9:102).

Na anayajua mnayoyatenda katika mema na maovu.

Ambaye mizani yake ya maovu itakuwa nzito atakuwa miongoni mwa waliohasirika na ambaye mizani yake ya wema itakuwa nzito basi atakuwa miongoni mwa wenye kufaulu.

Na anawaitikia walioamini na wakatenda mema, na anawazidishia fadhila zake. Na makafiri watakuwa na adhabu kali.

Yaani waumini wanasikia mwito wa Mwenyezi Mungu na kuuitikia, kwa hiyo naye anawalipa kutokana na kuitkia kwao na utiifu na anawazidishia ziada nyingi kutokana na fadhila zake. Na wakosefu hawataki mwito wa Mwenyezi Mungu, kwa hiyo anawadhibu adhabu kubwa kutokana na upinzani wao na uasi.