TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 19930
Pakua: 2211


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 29 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 19930 / Pakua: 2211
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI Juzuu 22

Mwandishi:
Swahili

17

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

Sura Ya Arubaini Na Tatu: Surat Az-Zukhruf. Ina aya 89 Imeshuka Makka. Imesemekana isipokuwa Aya moja haikushuka Makka

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu

حم ﴿١﴾

1. Haa-miim.

وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ ﴿٢﴾

2. Naapa kwa Kitabu kinachobainisha.

إِنَّا جَعَلْنَاهُ قُرْآنًا عَرَبِيًّا لَّعَلَّكُمْ تَعْقِلُونَ ﴿٣﴾

3. Hakika tumeifanya Qur’an kwa kiarabu ili mfahamu.

وَإِنَّهُ فِي أُمِّ الْكِتَابِ لَدَيْنَا لَعَلِيٌّ حَكِيمٌ ﴿٤﴾

4. Na hakika hiyo imo katika mama wa Kitabu kilichoko kwetu, ni tukufu na yenye hiki- ma.

أَفَنَضْرِبُ عَنكُمُ الذِّكْرَ صَفْحًا أَن كُنتُمْ قَوْمًا مُّسْرِفِينَ ﴿٥﴾

5. Je, tuache kuwakumbusha kwa kuwa ni watu mliopita mipaka?

وَكَمْ أَرْسَلْنَا مِن نَّبِيٍّ فِي الْأَوَّلِينَ ﴿٦﴾

6. Na manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!

وَمَا يَأْتِيهِم مِّن نَّبِيٍّ إِلَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ ﴿٧﴾

7. Na hakuwajia nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli.

فَأَهْلَكْنَا أَشَدَّ مِنْهُم بَطْشًا وَمَضَىٰ مَثَلُ الْأَوَّلِينَ ﴿٨﴾

8. Na tuliwaangamiza waliokuwa na nguvu kushinda wao, na mfano wa watu wa zamani umekwishapita.

وَلَئِن سَأَلْتَهُم مَّنْ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ لَيَقُولُنَّ خَلَقَهُنَّ الْعَزِيزُ الْعَلِيمُ ﴿٩﴾

9. Na ukiwauliza: Nani aliyeumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi.

الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ مَهْدًا وَجَعَلَ لَكُمْ فِيهَا سُبُلًا لَّعَلَّكُمْ تَهْتَدُونَ ﴿١٠﴾

10. Ambaye amewafanyia ardhi kuwa tandiko, na akawafanyia ndani yake njia mpate kuongoka.

وَالَّذِي نَزَّلَ مِنَ السَّمَاءِ مَاءً بِقَدَرٍ فَأَنشَرْنَا بِهِ بَلْدَةً مَّيْتًا كَذَٰلِكَ تُخْرَجُونَ ﴿١١﴾

11. Na ambaye ameteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyokufa. Na hivyo ndivyo mtakavyotolewa.

وَالَّذِي خَلَقَ الْأَزْوَاجَ كُلَّهَا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ الْفُلْكِ وَالْأَنْعَامِ مَا تَرْكَبُونَ ﴿١٢﴾

12. Na ambaye ameumba aina zote, na akawafanyia jahazi na wanyamahowa mnaowapanda.

لِتَسْتَوُوا عَلَىٰ ظُهُورِهِ ثُمَّ تَذْكُرُوا نِعْمَةَ رَبِّكُمْ إِذَا اسْتَوَيْتُمْ عَلَيْهِ وَتَقُولُوا سُبْحَانَ الَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَـٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُ مُقْرِنِينَ ﴿١٣﴾

13. Ili mkae vizuri migongoni mwao. Kisha mkumbuke neema za Mola wenu mnapokaa sawa sawa juu yao hao mnaowapanda na mseme: Ametakasika aliyemfanya huyu atutumikie, na tusingeliweza kufanya haya wenyewe.

وَإِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ ﴿١٤﴾

14. Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.

KITABU KINACHOBAINISHA

Aya 1 – 14

MAANA

Haa-miim.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:1).

Naapa kwa Kitabu kinachobainisha.

Hiki ni kiapo kutoka kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Qur’an ambayo ndani yake mna ubainifu wa uongofu na upotevu, na halali na haramu.

Hakika tumeifanya Qur’an kwa kiarabu ili mfahamu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 12 (12:2), Juz. 16 (20:113), Juz. 24 (41:3) na kwenye Juzuu hii tuliyo nayo (42:7). Tumekwishaizungumzia sana Aya hii, na hivi sasa hatuna la ziada.

Na hakika hiyo imo katika mama wa Kitabu kilichoko kwetu, ni tuku- fu na yenye hikima.

‘Hiyo’ ni hiyo Qur’an na mama ni asili. Hakuna mwenye shaka kwamba ilimu ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndio asili ya vitabu vyote mbinguni. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameisifu Qur’an kuwa ni tukufu kwa sababu inainua na kuwatukuza wanayoisikiliza na kuitumia. Tumeona jinsi ilivyowatoa waarabu kwenye ujinga wa wajinga kuwapeleka kwenye maendeleo na jinsi ilivyoeneza utawala wao na lugha mashariki ya ardhi na magharibi yake, pale walipohalalisha halali ya Qur’an na wakaharamisha haramu ya yake.

Vile vile Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ameisifu kuwa ina hikima kwa sababu imeweka sawa baina ya watu bila ya kubagua, ikatoa mwito wa kusameheana na ikahimiza kufanya kazi yenye manufaa na kusaidiana kwa masilahi ya watu wote.

Je, tuache kuwakumbusha kwa kuwa ni watu mliopita mipaka?

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuitaja Qur’an kwamba ni mtoa nasaha mwaminifu, sasa anawaambia wale walioikadhibisha katika washirikina wa kiarabu: Mnaonaje tuache kuwakumbusha Qur’an kwa vile tu nyinyi mmezipitishia kiasi nafsi zenu na mkazidhulumu kwa ujinga na upotevu? Bali nyinyi ndio mnafaa zaidi kukumbushwa kuliko wengineo.

Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani!

Ni wengi tu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsimulia Mtume wake habari za manabii kadhaa na akamwambia:

وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا رُسُلًا مِّن قَبْلِكَ مِنْهُم مَّن قَصَصْنَا عَلَيْكَ وَمِنْهُم مَّن لَّمْ نَقْصُصْ عَلَيْكَ ﴿٧٨﴾

“Na kwa hakika tuliwatuma Mitume kabla yako. Wengine katika hao tumekusimulia na wengine hatukukusimulia.” Juz. 24 (40:78).

Na hakuwajia nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli, kama walivyokukejeli wewe ewe Muhammad. Kwa hiyo lisikutie tabu hilo, si mageni hayo. Ni vita baina ya wapotevu na wanaolingania haki na uadilifu, kila mahali na kila wakati.

Na tuliwaangamiza waliokuwa na nguvu kushinda wao.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaangamiza mataghuti waliokuwa na nguvu katika umma zilizopita kwa kuwanusuru wema walio wanyonge.

Na mfano wa watu wa zamani umekwishapita.

Yaani tumekusimulia katika Qur’an hali ya waongo wa zamani na jinsi walivyoangamia, ili watu wako wapate funzo.

Na ukiwauliza: Nani aliyeumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (29:61), (31:25) na Juz. 24 (39:38)

Ambaye amewafanyia ardhi kuwa tandiko, na akawafanyia ndani yake njia mpate kuongoka. Na ambaye ameteremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyokufa. Na hivyo ndivyo mtakavyotolewa.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:99), Juz. 13 (13:3) na Juz. 16 (20:53).

Na ambaye ameumba aina zote.

Yaani aina zote za waanyama, mimea na vitu vigumu.

Na akawafanyia jahazi na wanyamahowa mnaowapanda.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwatajia neema ya maji na ardhi na kwamba wao wanakula, kuvaa na kunywa humo, sasa anawatajia neema ya mawasiliano. Ametaja jahazi na wanyama kwa njia ya mfano tu sio kuwa ndio hayo tu; kwa sababu magari na ndege hayakuwa maarufu wakati huo.

Ili mkae vizuri migongoni mwao.

Yaani migongoni mwa hao mnaowapanda.

Kisha mkumbuke neema za Mola wenu mnapokaa sawa sawa juu yao hao mnaowapanda na mseme: Ametakasika aliyemfanya huyu atutumikie, na tusingeliweza kufanya haya wenyewe. Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi.

Katika Nahjul-balagha amesema: “Ewe Mola wangu! Ninajilinda kwako na mashaka ya safari, na huzuni ya marejeo na ubaya wa mandhari katika watu wa nyumbani na mali.

Ewe Mola wangu! Hakika wewe ni mwenza safarini na wewe ndiwe wa kuachwa nyuma na familia. Wala hawezi kuyakusanya haya mawili isipokuwa wewe. Kwa sababu mwenye kuachwa nyuma hawezi kuwa mwenza na mwenza hawezi kuachwa nyuma.”

Sheikh Muhammad Abduh anaielezea kauli hiyo ya Imam Ali(a.s) , kwa kusema:“Mwanzo wa maneno haya umepokewa kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w) na akayatimiza Amirul-muminin kwa kusema Wala hawezi kuyakusanya…mpaka mwisho. Dhati ya Mwenyezi Mungu iko sawa mahali pote na wakati wote. Kwa hiyo kuwa safarini na kuwa mjini kwake ni sawa.”

وَجَعَلُوا لَهُ مِنْ عِبَادِهِ جُزْءًا إِنَّ الْإِنسَانَ لَكَفُورٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾

15. Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanadamu ni mwenye kukufuru waziwazi.

أَمِ اتَّخَذَ مِمَّا يَخْلُقُ بَنَاتٍ وَأَصْفَاكُم بِالْبَنِينَ ﴿١٦﴾

16. Au amejichukulia watoto wa kike katika vile alivyoviumba, na akawachagulia nyinyi watoto wa kiume?

وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِمَا ضَرَبَ لِلرَّحْمَـٰنِ مَثَلًا ظَلَّ وَجْهُهُ مُسْوَدًّا وَهُوَ كَظِيمٌ ﴿١٧﴾

17. Na mmoja wao akibashiriwa kwa yale aliyompigia mfano Mwingi wa rehema, uso wake husawijika naye amejaa chuki.

أَوَمَن يُنَشَّأُ فِي الْحِلْيَةِ وَهُوَ فِي الْخِصَامِ غَيْرُ مُبِينٍ ﴿١٨﴾

18. Ati aliyelelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema bayana?

وَجَعَلُوا الْمَلَائِكَةَ الَّذِينَ هُمْ عِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ إِنَاثًا أَشَهِدُوا خَلْقَهُمْ سَتُكْتَبُ شَهَادَتُهُمْ وَيُسْأَلُونَ ﴿١٩﴾

19. Na wakawafanya malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wataulizwa!

وَقَالُوا لَوْ شَاءَ الرَّحْمَـٰنُ مَا عَبَدْنَاهُم مَّا لَهُم بِذَٰلِكَ مِنْ عِلْمٍ إِنْ هُمْ إِلَّا يَخْرُصُونَ ﴿٢٠﴾

20. Na husema: Angelipenda Mwingi wa Rehema tusingeliwaabudu. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!

أَمْ آتَيْنَاهُمْ كِتَابًا مِّن قَبْلِهِ فَهُم بِهِ مُسْتَمْسِكُونَ ﴿٢١﴾

21. Au tuliwapa Kitabu kabla ya hiki, wakawa wameshikamana nacho?

بَلْ قَالُوا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَىٰ أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَىٰ آثَارِهِم مُّهْتَدُونَ ﴿٢٢﴾

22. Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu juu ya desturi na tunaongoza nyayo zao.

وَكَذَٰلِكَ مَا أَرْسَلْنَا مِن قَبْلِكَ فِي قَرْيَةٍ مِّن نَّذِيرٍ إِلَّا قَالَ مُتْرَفُوهَا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءَنَا عَلَىٰ أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَىٰ آثَارِهِم مُّقْتَدُونَ ﴿٢٣﴾

23. Na kadhalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila wapenda anasa wake walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu juu ya desturi na tunafuata nyayo zao.

قَالَ أَوَلَوْ جِئْتُكُم بِأَهْدَىٰ مِمَّا وَجَدتُّمْ عَلَيْهِ آبَاءَكُمْ قَالُوا إِنَّا بِمَا أُرْسِلْتُم بِهِ كَافِرُونَ ﴿٢٤﴾

24. Akasema: Hata nikiwaletea yenye muongozo bora kuliko mliowakuta nayo baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa hayo mliyotumwa nayo.

فَانتَقَمْنَا مِنْهُمْ فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُكَذِّبِينَ ﴿٢٥﴾

25. Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa waliokadhibisha!

AU AMEJICHUKULIA WATOTO WANAWAKE

Aya 15 – 25

MAANA

Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanadamu ni mwenye kukufuru waziwazi. Au amejichukulia watoto wakike katika vile alivyoviumba, na akawachagulia nyinyi watoto wa kiume?

Makusudio ya fungu hapa ni mtoto, kwa sababu ni sehemu ya mzazi wake. Ama kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Watoto wa kike katika vile alivyoviumba, inaonyesha dalili ya uharibifu wa madai yao kuwa Mwenyezi Mungu ana mtoto, kwa sababu muumbwa hawezi kuwa ni sehemu ya aliyeumba; kama ambavyo nyumba haiwezi kuwa ni sehemu ya mjenzi.

Washirikina hawakutosheka na uzushi huu, mpaka wakamhusisha Mwenyezi Mungu na wale watoto wasiowapenda wao.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:100), Juz. 15 (17:40) na Juz. 23 (37:149-153).

Na mmoja wao akibashiriwa kwa yale aliyompigia mfano Mwingi wa rehema, uso wake husawijika naye amejaa chuki.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwasifu washirikina na ukafiri ulio waziwazi, sasa anawashutumu wale wanaohuzunika na kukasirika wakipata wasichana, wakati huohuo wanamzulia Mwenyezi Mungu na kusema kuwa ana watoto wasichana.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 14 (16:58).

Ati aliyelelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema bayana?

Ewe mshirikina mjinga! Unamnasibishia Mwenyezi Mungu wanawake wanojipamba, na kama ukihojiwa kwenye hilo utashindwa na hoja na dalili? Wafasiri wamesema wamemnasibishia Mwenyezi Mungu wanawake ambao hawawezi hoja na kubishana Dhahiri ya Aya inarudia kwenye tafsiri hii.

Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao?

Vipi wanajasiri washirikina kusema kuwa Malaika ni mabinti wa Mwenyezi Mungu. Je, walikuwako kwa Mwenyezi Mungu wakati akiwaumba Malaika au aliwapa habari ya hilo? Amesema kweli aliyesema: “Mtu amesema uwongo juu aliye mfano wake, juu ya Mola wake, juu ya Mitume wake na Malaika wake, vile vile amesema uwongo juu ya nafsi yake.”

Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ ﴿١٥٠﴾

“Au tumewaumba malaika kuwa ni wanawake na wao wakashuhudia? Juz. 23 (37:150).

Ushahidi wao utaandikwa na wataulizwa!

Kwa Mwenyezi Mungu hakufichiki chochote, Yeye anajua uzushi wao kwake na kwa Malaika wake na kesho atawauliza na kuwahisabu

Na husema: Angelipenda Mwingi wa Rehema tusingeliwaabudu.

Wanadai kuwa Mwenyezi Mungu yuko radhi wao kuabudu Malaika na masanamu; vinginevyo angeliwazuia kwa nguvu. Wamesahau kama Mwenyezi Mungu angelifanya hivyo, mtu angelikuwa sawa na mawe, asingelistahiki thawabu wala adhabu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (6:148).

Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uwongo tu!

Wamenasibisha shirki yao na upotevu wao kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu! Hawajui kuwa Yeye, ambaye imetukuka enzi yake, anaamrisha na anakataza kitaklifa na kimongozo, akaacha utekelezaji uwe kwa matakwa ya aliyekalifishwa, ili yadhihiri matendo yake yatakayomfanya astahiki thawabu au adhabu.

Au tuliwapa Kitabu kabla ya hiki, wakawa wameshikamana nacho?

Hapana! Hawana dalili ya akili wala ya nakili kwa madaia yao, isipokuwa dalili hii:

Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu juu ya desturi na tunaongoza nyayo zao.

Kwa hiyo kuwaiga mababa ndio kimbilio la kwnza na la mwisho. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameisimulia kauli yao hii katika Aya kadha; miongoni mwazo ni: Juz. 2 (2:170), Juz. 7 (5:104), Juz.17 (21:53), Juz.21 (31:21) na nyinginezo. Tumeweka kifungu kuhusu kuiga na mafungu yake katika Juz. 2 (2:170).

Na kadhalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila wapenda anasa wake walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu juu ya des- turi na tunafuata nyayo zao.

Haya ndio mantiki ya wanaotaka manufaa yao tu, tangu walipoanza kupatikana hadi siku ya mwisho. Tazama kifungu ‘Fikra ya mataghuti’ katika Juz. 13 (13:30-31), Juz. 15 (17:16-21) na kifungu ‘Mantiki ya watu wa pesa ni benki na ardhi.’ katika Juz. 18 (25:7-16).

Akasema: Hata nikiwaletea yenye muongozo bora kuliko mliowaku- ta nayo baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa hayo mliyotumwa nayo.

Tunalolifahamu kutokana na kauli yao hii ni kuwa wao wanaikataa haki popote na vyovyote iwavyo; hata kama ingelitoka kwa mababa zao, na kwamba wao hawaamini chochote isipokuwa manufaa na chumo lao tu.

Ama kujiingiza kwenye desturi ya mababa ni visingizio tu, wakihofia kujulikana uhakika wao na watu. Tumewawona wengi wakiwabeza mababa zao, si kwa lolote ila kuwa wanagongana na masilahi na mapendeleo yao. Hakuna malipo kwa mwenye kuipinga haki isipokuwa kumtumilia nguvu:

Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa waliokadhibisha!

Bila shaka ni fedheha na moto wa Jahannam.

18

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA MBILI

وَإِذْ قَالَ إِبْرَاهِيمُ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ إِنَّنِي بَرَاءٌ مِّمَّا تَعْبُدُونَ ﴿٢٦﴾

26. Na pale Ibrahim alipomwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyaabudu.

إِلَّا الَّذِي فَطَرَنِي فَإِنَّهُ سَيَهْدِينِ ﴿٢٧﴾

27. Isipokuwa yule aliyeniumba, kwani Yeye ataniongoza.

وَجَعَلَهَا كَلِمَةً بَاقِيَةً فِي عَقِبِهِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢٨﴾

28. Na akalifanya liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee.

بَلْ مَتَّعْتُ هَـٰؤُلَاءِ وَآبَاءَهُمْ حَتَّىٰ جَاءَهُمُ الْحَقُّ وَرَسُولٌ مُّبِينٌ ﴿٢٩﴾

29. Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume anayebainisha.

وَلَمَّا جَاءَهُمُ الْحَقُّ قَالُوا هَـٰذَا سِحْرٌ وَإِنَّا بِهِ كَافِرُونَ ﴿٣٠﴾

30. Na ilipowafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.

وَقَالُوا لَوْلَا نُزِّلَ هَـٰذَا الْقُرْآنُ عَلَىٰ رَجُلٍ مِّنَ الْقَرْيَتَيْنِ عَظِيمٍ ﴿٣١﴾

31. Na walisema: Kwa nini Qur’an hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?

أَهُمْ يَقْسِمُونَ رَحْمَتَ رَبِّكَ نَحْنُ قَسَمْنَا بَيْنَهُم مَّعِيشَتَهُمْ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَرَفَعْنَا بَعْضَهُمْ فَوْقَ بَعْضٍ دَرَجَاتٍ لِّيَتَّخِذَ بَعْضُهُم بَعْضًا سُخْرِيًّا وَرَحْمَتُ رَبِّكَ خَيْرٌ مِّمَّا يَجْمَعُونَ ﴿٣٢﴾

32. Kwani wao ndio wanaogawa rehema za Mola wako? Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawainua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wengine wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayoyakusanya.

وَلَوْلَا أَن يَكُونَ النَّاسُ أُمَّةً وَاحِدَةً لَّجَعَلْنَا لِمَن يَكْفُرُ بِالرَّحْمَـٰنِ لِبُيُوتِهِمْ سُقُفًا مِّن فِضَّةٍ وَمَعَارِجَ عَلَيْهَا يَظْهَرُونَ ﴿٣٣﴾

33. Na lau isingekuwa watu watakuwa kundi moja tungeliwajaalia wanaomkufuru Mwingi wa rehema nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazopandia.

وَلِبُيُوتِهِمْ أَبْوَابًا وَسُرُرًا عَلَيْهَا يَتَّكِئُونَ ﴿٣٤﴾

34. Na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyoegemea juu yake.

وَزُخْرُفًا وَإِن كُلُّ ذَٰلِكَ لَمَّا مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَالْآخِرَةُ عِندَ رَبِّكَ لِلْمُتَّقِينَ ﴿٣٥﴾

35. Na mapambo. Na hayo yote si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu, na Akhera iliyoko kwa Mola wako ni ya wenye takua.

JE, WANAIGAWA REHEMA YA MOLA WAO?

Aya 26 – 35

MAANA

Na pale Ibrahim alipomwambia baba yake na kaumu yake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayoyaabudu, isipokuwa yule aliyeniumba, kwani Yeye ataniongoza.

Kaumu ya Ibrahim, akiwemo baba yake, kama inayvofahamisha dhahiri ya Aya, walikuwa wakiabudu masanamu. Basi akawakataza na akatangaza kujitenga nayo, na kwamba yeye anamwabudu aliyemuumba na atamuongoza kwenye lile lililo na heri na masilahi naye.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 7 (6:73), Juz. 16 (19: 41-44), Juz. 17 (21:51-56), Juz. 19 (26:69-82) na Juz. 23 (37:83-85).

Kusema kwake: ‘Kwani Yeye ataniongoza,’ kunaonyesha yakini yake na kumtegemea kwake Mwenyezi Mungu. Hivi ndivyo anavyokuwa kila mwenye kuitafuta haki na mwongozo kwa nia safi. Anaamini kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja naye, atamtosha na atamwongoza. Hiyo inatokana na kauli zake Mwenyezi Mungu Mtukufu zifuatazo:-

وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ ﴿٣٦﴾

“Na jueni kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wenye takua.” Juz. 10 (9:36).

إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الصَّابِرِينَ ﴿١٥٣﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wanaosubiri” Juz.2 (2:153).

وَإِنَّ اللَّـهَ لَمَعَ الْمُحْسِنِينَ ﴿٦٩﴾

“Na hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wema” Juz. 21 (29:69).

Na akalifanya liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake.

Alilolifanya ni hilo neno la Tawhid, likiashiriwa na kauli yake: ‘Hakika mimi najitenga mbali na hayo mnayoyaabudu.’

Makusudio ya kulifanya ni kuliusia; kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na Ibrahim akawausia haya wanawe na Yaqub: Enyi wanangu! Hakika Mwenyezi Mungu amewachagulia dini; basi msife ila nanyi ni waislamu.” Juz. 1 (2:131).

Ili warejee.

Hii ndio sababu yake Ibrahim kuwazuia wanawe; kwa maana ya kuwa aliwausia neno la Tawhid, ili walijue. Na kama mmoja wao akishirikisha au akijaribu basi akumbuke wasia wa baba yake na aambiwe kuwa wewe umehalifu wasia wa Ibrahim.

Na hilo lilitokea hasa: “Sema: amesem kweli Mwenyezi Mungu. Basi fuateni mila ya Ibrahim aliyeshikamana na haki; wala hakuwa katika washirikina.” Ni mila ya baba yenu Ibrahim. Yeye aliwaita waislamu zamani. Juz. 4 (3:95) Juz. 17 (22:78).

KWA NINI ALI KARRAMALLAHU WAJHAH

Mwaka 1389 nilifunga Ramadhan tukufu Dubai kwa mwaliko kutoka huko. Vijana wakawa wananiuliza maswali mengi; miongoni mwayo ni: Kwa nini wanapotajwa maswahaba sunni wanasema: Radhiallah a’nhu (Mwenyezi Mungu awe Radhi naye) na Shia anapotajwa Imam wanasema : Alyhis salaam (Amani ishuke juu yake).

Nikajibu kuwa wote wamechukua kutoka kwenye Qur’an:

رَّضِيَ اللَّـهُ عَنْهُمْ وَرَضُوا عَنْهُ ﴿١١٩﴾

“Awe radhi nao Mwenyezi Mungu na wao wawe radhi naye” Juz. 7 (5:119).

قُلِ الْحَمْدُ لِلَّـهِ وَسَلَامٌ عَلَىٰ عِبَادِهِ الَّذِينَ اصْطَفَى ﴿٥٩﴾

“Sema: Sifa njema ni za Mwenyezi Mungu (Alhamdu lillah) na amani ishuke juu ya waja wake aliowateua” Juz. 19 (27:59).

Kwa hiyo Shia wamechukua hii na Sunni wakachukua ile.

Nilipofikia kufasiri kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Ili warejee,’ nikasoma kwenye Tafsir Ruhul-bayan ya Sheikh Ismail Haqqi, katika ulama wa kisunni, ninamnukuu: “Wamesema baadhi katika kutukuzwa uso wa Ali bin Abu Twalib, kwa kusemwa: Karramallahu wajhah (Mwenyezi Mungu autukuze uso wake), kwamba imenukuliwa kutoka kwa mama yake, Fatima bint Asad, kwamba yeye (Fatma) alipokuwa akitaka kusujudia sanamu, Ali akimzuia akiwa tumboni.”

Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume anayebainisha.

Hawa ni washirikina wa kiquraishi, ambao ni kizazi cha Ibrahim(a.s ) . Makusudio ya haki hapa ni Qur’an na Mtume ni Muhammad(s.a.w.w) . Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemsifu kuwa anabainisha, kwa sababu risala yake iko wazi dalili na muujiza wake umemziba mdomo kila mpingaji.

Maana ni kuwa vigogo wa kiquraishi walimshirikisha Mwenyezi Mungu na wakaupinga wasia wa baba yao Ibrahim(a.s ) wa Tawhid, lakini Mwenyezi Mungu akawapa muda na akawaneemesha fadhila zake, lakini iliwatamalaki ghururi wakapituka mipaka, mpaka alipowajia Mtume kutokana na wao wenyewe na Kitabu cha Mwenyezi Mungu kinachowapa mwito wa Tawhid ambayo ni mila ya baba yao Ibrahim.

Na ilipowafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa.

Waliikataa Qur’an na wakasema ni uchawi uliozushwa na wakamkataa Mtume wakasema:

يَا أَيُّهَا الَّذِي نُزِّلَ عَلَيْهِ الذِّكْرُ إِنَّكَ لَمَجْنُونٌ ﴿٦﴾ لَّوْ مَا تَأْتِينَا بِالْمَلَائِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿٧﴾

“Ewe uliyeteremshiwa ukumbusho! Wewe ni mwendawazimu. Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?” Juz. 14 (15:6-7).

Na walisema tena: Kwa nini Qur’an hii haikuteremshwa kwa mtu mkubwa katika miji miwili hii?

Muhammad ni fukara ati anasema: Nimeteremshiwa Qur’an si ajabu hii! Mwenyezi Mungu anaweza kumchagulia risala yake mtu mkubwa; kama vile Walid bin Al-Mughira wa Makka na Urwa bin Mas’ud Athaqafi wa Taif. Mmoja wa hawa ndio angefaa kuteremshiwa Qur’an.

Hivi ndivyo walivyoipinga risala ya Muhammad(s.a.w. w ) ; si kwa lolote ila ni kwa vile hamiliki pesa wala ardhi. Hawajui kuwa mali inamilikiwa na mwema au muovu na mumin au kafiri. Lakini risala ni wakfu wa aliye kufu na na aliyesafi kati ya wasafi.

Hakuna tofauti mbele ya Mwenyezi Mungu (s.w.t.) baina ya anayepinga utume wa Muhammad kwa sababu ya ufukara wake na yule anayemtukuza na kumweshimu tajiri kwa sababu ya mali yake na utajiri wake na kumdharau fukara kwa sababu ya ufukara wake. Hakuna tofauti kabisa baina ya hawa wawili; hata mmoja wao akitamka shahada mbili. Isipokuwa tu, atakayetamka duniani atachukuliwa kama mwislamu, lakini huko Akhera atakuwa pamoja na wapinzani na washirikina.

Kwani wao ndio wanaogawa rehema za Mola wako?

Makusudio ya rehema hapa ni utume. Maana ni kuwa, je jambo la utume liko mikononi mwa wapenda anasa, ndio wachague wanayemtaka na wamzuie wasiyemtaka? Kwani utume ni udiwani au ubunge? Hapana! Utume unatoka kwa Mwenyezi Mungu na Mtume anafanya kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ndiye msemaji wake na mbainifu wake.

Sasa wapenda anasa ndio wasemaji rasmi wa Mwenyezi Mungu? Je, wao wanaweza kumruhusu mtu awe msemaji wao rasmi bila ya idhini yao? Vipi wanamfanyia Mwenyezi Mungu ambayo wao hawawezi kujifanyia?

Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawainua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi; kwa hivyo baadhi yao wanawafanya wengine wawatumikie. Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayoyakusanya.

Mwenyezi Mungu humruzuku amtakaye, hilo halina shaka, lakini Yeye vile vile ametaka kutoruzuku hivi hivi isipokuwa kwa sababu:

هُوَ الَّذِي جَعَلَ لَكُمُ الْأَرْضَ ذَلُولًا فَامْشُوا فِي مَنَاكِبِهَا وَكُلُوا مِن رِّزْقِهِ ﴿١٥﴾

“Yeye ndiye aliyeidhaliisha ardhi kwa ajili yenu, basi tembeeni katika pande zake na kuleni katika riziki zake.” (67:15).

Sababu hizi za riziki au mahangaiko katika ardhi yako aina nyingi; miongoni mwazo ni; viwanda, kilimo, biashara, utumishi, kama ilivyosema Qur’an: ‘Baadhi yao wanawafanya wengine wawatumikie,’ kama watumishi wa serikali, viwandani, madukani au hospitalini nk. Katika ufahamu wa watu nikuwa bosi yuko juu zaidi ya wengine, lakini mbele ya Mwenyezi Mungu mtukufu na na aliye juu zaidi ni yule mwenye takua zaidi.

إِنَّ أَكْرَمَكُمْ عِندَ اللَّـهِ أَتْقَاكُمْ إِنَّ اللَّـهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ ﴿١٣﴾

“Hakika aliye mtukufu zaidi kati yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ni aliye na takua zaidi katika nyinyi” (49:13)

“Na Pepo ambayo upana wake ni mbingu na ardhi, imeandaliwa wenye takua.”

Kwenye Nahjul-balagha Imam Ali(a.s ) anasema:

“Alikuwa na njaa Mtume katika dunia pamoja na umahasusi wake – yaani umahasusi mbele ya Mola wake-na alijiweka mbali na vivutio vya dunia pamoja na kuwa karibu navyo. Basi naatazame mwenye akili, je, Mwenyezi Mungu amemtukuza Muhammad kwa hilo au amemtweza? Akisema amemtweza – basi Wallahil-adhim – atakuwa muongo (anayesema hivyo) na akisema amemtukuza basi naajue kwamba Mwenyezi Mungu amemtweza mwenginewe aliyemkunjulia dunia.”

Unaweza kuuliza : utaifanyaje kauli: ‘Sisi tumewagawanyia baina yao maisha yao katika uhai wa duniani, na tukawainua baadhi yao juu ya wengine kwa daraja nyingi’ inayoonyesha wazi kuwa Mwenyezi Mungu ndiye anayefukarisha na kutajirisha, na anayemfanya huyu ni mfanyikazi na yule ni mfanyiwa kazi?

Jibu : kauli yake hii Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kusimulia hali halisi waliyo nayo watu na ameyategemeza hayo kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa sababu kutofautiana kunatokana na sababu zake za kimaumbile moja kwa moja na zinatoka kwake kwa kupitia kwengine, kwa vile Yeye ndiye muumba wa ulimwengu.

Maana haya yanafahamishwa na kauli yake Mwenyezi Mungu mwisho wa Aya: ‘Na rehema za Mwenyezi Mungu ni bora kuliko hayo wanayoyakusanya.’ Ambapo kukusanya mali amekutegemeza kwa watu.

Hapa ndio zinaafikiana Aya zinazoamrisha kuhangaikia riziki na zile zilizoitegemeza rizi kwa Mwenyezi Mungu moja kwa moja. Katika Juzuu hii tuliyo, kwenye (42:27), tumeashiria kwamba Mwenyezi Mungu mara nyingine anawapa baadhi ya waja wake tawfiki na kuwaruzuku kingi kutokana na kichache.

Na lau isingekuwa watu watakuwa kundi moja tungeliwajaalia wanaomkufuru Mwingi wa rehema nyumba zao zina dari ya fedha, na ngazi zao pia wanazopandia na milango ya nyumba zao na vitanda wanavyoegemea juu yake na mapambo.

Yaani ngazi, milango na vitanda vyote vinatokana na madini ya fedha. Aya inamjibu anayesema kuwa ufukara hauendani na utume, eti kwa sababu ufukara ni hulka pungufu.

Ufupi wa jawabu ni kuwa dunia, mbele ya Mwenyezi Mungu, hailingani hata na bawa la mbu, na Akhera ni bora mbele ya Mola wako na ni yenye kubaki, lakini watu wanaathirika na dunia kuliko Akhera na wanakwenda nayo popote wanapoelekea. Lau si hivyo basi Mwenyezi Mungu angeliwapa makafiri nyumba zenye sakafu za fedha na pia milango, ngazi na samani. Na angeliwazidishia mapambo ya dunia kwa kuidharau. Mtaalamu mmoja alisema: “Watu wamepondokea dunia, lakini Mwenyezi Mungu hakulifanya hilo, je ingelikuwaje lau angelifanya. Aya hii inafahamisha kwamba Mwenyezi Mungu anawachukulia upole waja wake na kuwafanyia yale yatakayowakurubisha kwake na kuwaweka mbali na maasi. Kwa uchache kabisa ni kuwa hawafanyii yatakayowahadaa kwenye maasi.

Lakini hayo si chochote ila ni starehe ya maisha ya dunia tu.

Yaani neema za dunia, kwa vyovyote itakavyokuwa basi itaisha tu. Katika Aya nyingine dunia imeitwa upuzi, mchezo na ghururi. Na Akhera iliyoko kwa Mola wako ni ya wenye takua ambao wamemfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu katika kauli zao na vitendo vyao.