TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Juzuu 23

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU12%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 30 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 29144 / Pakua: 4406
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Juzuu 23

Mwandishi:
Swahili

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

IMEANDIKWA NA: SHEIKH MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYA

IMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HASAN MWALUPA

IMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

IMEPANGWA KATIKA KOMPYUTA NA: UKHT PILI RAJABU

UTANGULIZI WA MCHAPISHAJI

Kitabu hiki kilichoko mikononi mwako hivi sasa ni juhudi ya miaka mingi sana ya watu waliojitolea kuona kazi hii imefanikiwa bila ya kumsahau Marhum Abu Muhammad wa London.

Kama lilivyo jina la Tafsiri ndivyo ilivyo Tafsiri yenyewe ambayo mwanachuoni huyu mahiri kabisa aliyeifafanua ni mtu aliyebobea katika fani zote ambazo mfasiri (Mfafanuzi) anatakiwa awe nazo.

Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya ameonesha cheche zake katika vitabu vingi alivyoviandika katika maudhui mbali mbalimbali na hivyo kujipatia wasomaji wengi sana.

Msomi huyu, mwenye fikra huru na anayetetea kile anachokiamini, ni mtu mwenye mawazo mapana na kuyaangalia mambo kwa undani sana, kipaumbele chake ni katika maslahi ya umma huu na amejaribu sana kwenda na wakati.

Sifa kubwa pekee ya mwanachuoni huyu ni kuwa yeye hakujihusisha sana na kung'ang'ania madhehebu fulani tu, labda hii yatokana na wadhifa wake wa ukadhi aliokuwa nao katika nchi ya Lebanon ambayo ina madhehebu mengi, ambapo sula la madhehebu ni nyeti nchini humo, hata hivyo yeye aliweza kuamua matatizo ya watu kwenye ofisi yake kulingana na madhehebu yao pale walipomwendea. Hiyo ilimsaidia sana hata kuweza kutoa kitabu kitwacho Al-Fiqh a'laa madhaahabil-khamsah (Fikhi ya madhehebu matano) yaani ya Hanafi, Maaliki, Shafi, Hambali na Shia (ambacho twataraji kitatoka kwa lugha ya kiswahili hivi karibuni Inshaallah).

Jambo lililotupa msukumo wa kukifasiri kitabu hiki kwa lugha ya Kiswahili ni zile faida nyingi atakazozipata msomaji na kujua mambo mengi na ya ajabu yaliyo mapya kwake ambayo si rahisi kuyapata kwa wafasiri wengine.

Msomaji atapata faida katika fani za Sayansi, Siasa, Historia, Mashairi, visa vizuri, na Saikolojia miongoni mwa mengine; ndiyo maana msomaji atashangaa kidogo anapoisoma Tafsiri hii atakapoona mwandishi amewataja na kuwanukuu watu kama kina Mfalme Edward, wanasayansi kama kina Enstein, wasanii kama Charlie Champlin (Mchekeshaji maarufu), na wengineo, hali inayoifanya tafsiri hii kuwa ni ya kipekee kabisa.

Mtindo alioutumia mwandishi ni sahali uliokusudiwa watu wa tabaka mbalimbali, wanavyuoni na watu wa kawaida.

Nia yetu ni kukigawanya kitabu hiki bure lakini tumelazimika kukiuza kwa bei nafuu ili kurudisha gharama za uchapishaji.

Mwisho: Shukrani kubwa iwaendee bila ya kuwataja watu waliojitolea usiku na mchana, jopo la wafasiri, wahariri, wachapaji, waliotupa moyo na kutoa maoni yao na walioisimamia ili kuhakikisha kwamba kitabu kimemfikia msomaji.

MAKOSA YA CHAPA

Sikumbuki kama nimewahi kusoma kitabu kilichotoka kupigwa chapa, cha zamani au cha sasa, bila ya kukuta makosa ya chapa, Nafikiri sitasoma kitabu kisichokuwa hivyo. Nimejaribu sana kuliepuka hilo katika tungo zangu, lakini sikufanikiwa.

Nilikuwa sifikirii kama ninaweza kuona makosa haya katika maandishi ya msahafu mtukufu, kama yale yaliyo katika baadhi ya chapa; kwa mfano neno yabswutu kwa swad, badala ya yabsutu kwa sin, na katika chapa ya Tafsir Arrazi ya Misr ya mwaka 1935, Sura ya (2:146), Imeandikwa La Ya'alamuun, (hawajui) badala ya Ya'alamuun (wanajua). Mfano wa makosa haya hausameheki.

Katika Tafsir Al-Manar, chapa ya Pili, sura (5:212), imeandikwa Fawqahum ila yawmil qiyama badala ya Fawqahum yawamal qiyama. Hatuwezi kusema kosa hili ni kubwa zaidi kuliko lile.

Lakini mkosaji atatuletea udhuru kwa msemo mashuhuri huko kwetu Jabal amil 'Makosa ya chapa.'

Katika Tafsiri Majmau chapa ya Urfan, Sura (46:15), imeandikwa: Hatta idha balagha arbai' na sanah badala ya: Hattaidha balagha ashuddahu arbai ' na sanah"

Kusema hivi sio kama ninajitetea kutokana na makosa ya chapa atakayoyakuta msomaji katika kitabu hiki, ijapokuwa naomba msamaha kama litatokea hili, lakini makusudio yangu hasa ni kumwambia yule atakayefungua macho yake kwenye makosa ya matamko na kuufungia macho uzuri wa maana.

Vilevile ninamwambia yule ambaye siku moja aliniambia: "Vitabu vyako vimejaa makosa ya chapa.” Kama kwamba hakuna kitu chochote katika vitabu hivyo isipokuwa makosa ya chapa tu. Wote hao ninawaambia: Mungu awasamehe na aniongoze mimi na nyinyi.

Vyovyote iwavyo, mimi ninaomba msamaha kutokana na makosa ya kifikra na ya chapa. Anasema Amirul Muminiin(a.s) :"Watu wote ni wapungufu wenye kuchanganyikiwa, isipokuwa yule aliyehifadhiwa na Mwenyezi Mungu." Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) ndiye mwenye jukumu la kunikubalia yale niliyoyapatia na kunisamehe niliyakosea, kwa jaha ya Mtume na kizazi chake, ziwashukie rehema na amani (Amin).

MUHAMMAD JAWAD MUGHNIYYAH

1

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

Sura Ya Arubaini Na Sita: Surat Al-Ahqaf. Imeshuka Makka. Ina Aya 35.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

حم ﴿١﴾

1. Haa miim.

تَنزِيلُ الْكِتَابِ مِنَ اللَّـهِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ ﴿٢﴾

2. Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hikima.

مَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَأَجَلٍ مُّسَمًّى وَالَّذِينَ كَفَرُوا عَمَّا أُنذِرُوا مُعْرِضُونَ ﴿٣﴾

3. Hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake ila kwa haki na kwa muda uliowekwa. Na wale waliokufuru wanayapuuza yale wanayoonywa.

قُلْ أَرَأَيْتُم مَّا تَدْعُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ أَرُونِي مَاذَا خَلَقُوا مِنَ الْأَرْضِ أَمْ لَهُمْ شِرْكٌ فِي السَّمَاوَاتِ ائْتُونِي بِكِتَابٍ مِّن قَبْلِ هَـٰذَا أَوْ أَثَارَةٍ مِّنْ عِلْمٍ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ﴿٤﴾

4. Sema: Je, mnawaona wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu? Nionyesheni wameumba nini katika ardhi; au wana shirika katika mbingu? Nileteeni Kitabu kilicho kuwa kabla ya hiki, au athari yoyote ya ilimu, ikiwa mnasema kweli.

وَمَنْ أَضَلُّ مِمَّن يَدْعُو مِن دُونِ اللَّـهِ مَن لَّا يَسْتَجِيبُ لَهُ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ وَهُمْ عَن دُعَائِهِمْ غَافِلُونَ ﴿٥﴾

5. Na ni nani mpotofu mkubwa kuliko yule anayeomba asiyekuwa Mwenyezi Mungu, ambaye hatamjibu mpaka Siku ya Kiyama, Na wala hawatambui maombi yao.

وَإِذَا حُشِرَ النَّاسُ كَانُوا لَهُمْ أَعْدَاءً وَكَانُوا بِعِبَادَتِهِمْ كَافِرِينَ ﴿٦﴾

6. Na watakapokusanywa watu watakuwa maadui zao, na wataikataa ibada yao.

IKO WAPI DALILI IKIWA NYINYI NI WA KWELI?

Aya 1-6

MAANA

Haamiim. Uteremsho wa Kitabu umetoka kwa Mwenyezi Mungu, Mwenye nguvu, Mwenye hikima.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juz. 25 (45:1) na Juz. 23 (39:1).

Hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake ila kwa haki na kwa muda uliowekwa.

Mwenyezi Mungu ni mwenye hekima, haumbi kitu ila kwa hikima, na ni muhali kuumba kwa mchezo. Ameuumba ulimwengu na yaliyomo ndani yake kwa hikima na malengo sahihi. Akauwekea muda maalum wa kwisha kwake; baada yake ni hisabu na malipo katika nyumba ya pili.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (30:8).

Na wale waliokufuru wanayapuuza yale wanayoonywa.

Mwenyezi Mungu anawahofisha wakosefu na siku ya Kiyama na vituko vyake, na akawawekea dalili wazi, lakini wakakataa isipokuwa inadi na jeuri.

Je, mnawaona wale mnaowaomba badala ya Mwenyezi Mungu? Nionyesheni wameumba nini katika ardhi; au wana shirika katika mbingu?

Maana ni kuwa nipeni habari enyi waabudu masanamu, ni jambo gani liliowafanya muyafanye masanamu ni miungu na kuyaabudu. Je, ni kwa kuwa yameumba kitu katika ardhi na mbinguni au yalishirikiana na Mwenyezi Mungu katika kuumba mbingu au sehemu yake?

Nileteeni Kitabu kilicho kuwa kabla ya hiki cha Qur’an; kama vile Tawrat, Injil n.k., kinachosema kuwa masanamu ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika kuumba kwake au kuwa yanaweza kuwaombea kwa Mungu au kuwa na utajo wowote.

Au athari yoyote ya ilimu, ikiwa mnasema kweli.

Ikiwa hamna dalili ya nukuu yoyote, je mnayo dalili ya kiakili kusadikisha myasemayo na kuyafanya sahihi mnayoyaabudu?

Umetangulia mfano wake katika Juz. 22 (35:40).

KUABUDU MASANAMU WAKATI MAENDELEO YA KUFIKA ANGANI

Unaweza kuuliza : Kwa nini Mwenyezi Mungu (s.w.t) ametilia umuhimu sana kuwarudi wenye kuabudu masanamu na mizimu kwenye Aya hii na nyinginezo, na hali hili sio jambo zito sana na liko wazi kabisa? Kuupinga uungu wa masanamu si ni jambo liliowazi; sawa na kuukanusha upofu na uoni na giza na nuru?

Jibu : Kuyatukuza masanamu na kuyaabudu, kumekua ni sehemu ya maisha ya mtu kuanzia zama na Nuh(a.s ) mpaka zama za Muhammad(s.a.w. w ) , ambapo baina ya wawili hao kuna maelefu ya miaka; bali mpaka hivi sasa kwenye maendeleo ya kufika angani, bado masanamu yameenea mashariki mwa ardhi na magharibi yake.

Masanamu yaliyoko kwenye nyumba za ibada, siku hizi, kwenye njia panda na kwenye vilele vya milima. Pia mapicha kwenye kuta yaliyoenea huku na huko na kwenye vitabu vya kumbukumbu si ni aina ya kuabudu masanamu?

Umetukuka ukuu wa Muhammad(s.a.w. w ) katika kumtukuza mtu kwa kumsafisha na ibada ya masanamu yaliyotengenezwa na mikono yake. Mshairi anasema:

Namshangaa insani mchonga jiwe ambaye

Hulifanya rahamani Mungu aabudiwaye

Huku adhani moyoni hudhuru na kumfaaye

Si aabudu mikono ilochonga hilo jiwe

Hayo si ndio maono lau ataka ajuwe

Basi na iwe mikono ya kuabudu si jiwe

Ndiyo imechonga jiwe kama anavyoelewa

Na nani mpotofu mkubwa kuliko hao wanaowaomba, badala ya Mwenyezi Mungu, ambao hawatawaitikia mpaka Siku ya Kiyama.

Makusudio ya kusema ‘mpaka siku ya Kiyama,’ ni milele na kutowezekana kujibu kabisa. Maana ni kuwa hakuna mjinga aliyepotea zaidi kuliko yule anayeabudu kisichosikia anayeita wala kumjibu anayeomba.

Na wala hawatambui maombi yao.

Washirikina wanaabudu masanamu, lakini masanamu hayana habari nao, wala hayana hisia yoyote.

Na watakapokusanywa watu watakuwa maadui zao, na wataikataa ibada yao.

Vile vile siku ya Kiyama wakati watu watakapofufuliwa kwa hisabu na malipo, miungu ya washirikina itajitenga nao na kuwakataa. Tazama Juz.11 (10:28).

وَإِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِمْ آيَاتُنَا بَيِّنَاتٍ قَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلْحَقِّ لَمَّا جَاءَهُمْ هَـٰذَا سِحْرٌ مُّبِينٌ ﴿٧﴾

7. Na wanaposomewa Aya zetu zilizo wazi, wale waliokufuru husema juu ya haki inapowajia: Huu ni uchawi ulio wazi.

أَمْ يَقُولُونَ افْتَرَاهُ قُلْ إِنِ افْتَرَيْتُهُ فَلَا تَمْلِكُونَ لِي مِنَ اللَّـهِ شَيْئًا هُوَ أَعْلَمُ بِمَا تُفِيضُونَ فِيهِ كَفَىٰ بِهِ شَهِيدًا بَيْنِي وَبَيْنَكُمْ وَهُوَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ ﴿٨﴾

8. Au wanasema: Ameizua! Sema: Ikiwa nimeizua mimi, basi nyinyi hamwezi kunifaa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu. Yeye anajua zaidi hayo mnayoropokwa; anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi. Na Yeye ni Mwingi wa Maghufira, Mwenye kurehemu.

قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ وَمَا أَدْرِي مَا يُفْعَلُ بِي وَلَا بِكُمْ إِنْ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰ إِلَيَّ وَمَا أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿٩﴾

9. Sema, mimi si kioja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyofanywa mimi wala nyinyi. Mimi nafuata niliyopewa Wahyi tu, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji, mwenye kubainisha.

قُلْ أَرَأَيْتُمْ إِن كَانَ مِنْ عِندِ اللَّـهِ وَكَفَرْتُم بِهِ وَشَهِدَ شَاهِدٌ مِّن بَنِي إِسْرَائِيلَ عَلَىٰ مِثْلِهِ فَآمَنَ وَاسْتَكْبَرْتُمْ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الظَّالِمِينَ ﴿١٠﴾

10. Sema: Mwaonaje yakiwa haya ni kweli yametoka kwa Mwenyezi Mungu, nanyi mmeyakataa, na alishuhudia shahidi miongoni mwa Wana wa Israili juu ya mfano wa haya, na akaamini, na nyinyi mnafanya kiburi? Hakika Mwenyezi Mungu hawaongozi watu madhalimu.

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لِلَّذِينَ آمَنُوا لَوْ كَانَ خَيْرًا مَّا سَبَقُونَا إِلَيْهِ وَإِذْ لَمْ يَهْتَدُوا بِهِ فَسَيَقُولُونَ هَـٰذَا إِفْكٌ قَدِيمٌ ﴿١١﴾

11. Na wale ambao wamekufuru waliwaambia wale ambao wameamini: Lau hii ingelikuwa ni heri, wasingelitutangulia. Na walipokosa kuongoka kwayo basi wakasema: Huu ni uzushi wa zamani.

وَمِن قَبْلِهِ كِتَابُ مُوسَىٰ إِمَامًا وَرَحْمَةً وَهَـٰذَا كِتَابٌ مُّصَدِّقٌ لِّسَانًا عَرَبِيًّا لِّيُنذِرَ الَّذِينَ ظَلَمُوا وَبُشْرَىٰ لِلْمُحْسِنِينَ ﴿١٢﴾

12. Na kabla yake kilikuwapo Kitabu cha Musa, kuwa kiongozi na chenye rehema. Na hiki ni Kitabu chenye kusadikisha cha lugha ya kiarabu, ili kiwaonye wale waliodhulumu, na kiwe ni bishara kwa watendao mema.

AU WANASEMA WAMEYATUNGA?

Aya 7 – 12

MAANA

Na wanaposomewa Aya zetu zilizo wazi, wale waliokufuru husema juu ya haki inapowajia: Huu ni uchawi ulio wazi.

Makusudio ya ishara zetu na haki ni Qur’an. Maana ya zilizo wazi ni kuwa Aya za Qur’an ziko wazi hazikufunganafungana. Lakini pamoja na kuwa Qur’an iko wazi na kudhihiri dalili kuwa ni haki, bado wazushi, walio mataghuti na wapenda anasa wameipa sifa ya uchawi ulio waziwazi. Si kwa lolote ila ni kwa kuwa imewafanya wao kuwa sawa na watu wengine. Umetangulia mfano wa hayo katika Aya kadhaa huko nyuma.

Au wanasema: Ameizua! Sema: Ikiwa nimeizua mimi, basi nyinyi hamwezi kunifaa chochote mbele ya Mwenyezi Mungu.

Je, washirikina wanadai kuwa umeizua hii Qur’an ewe Muhammad(s.a.w. w ) ? Waambie: vipi nimzulie Mungu uwongo na hali mimi ndiye ninayemuhofia zaidi? Je, mtanikinga na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake ikiwa nitasema uwongo au kumzulia? Aliyasema haya Mtume kutegemea vile wanavyomjua yeye jinsi anavyochukia uwongo na tabia nyinginezo mbaya.

Yeye anajua zaidi hayo mnayoropokwa; anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi.

Hakifichiki kitu katika kauli zenu na vitendo vyenu nanyi mtahisabiwa navyo; na Mwenyezi Mungu ananijua mimi na nyinyi, kwa hiyo anashudia ukweli na uaminifu kwangu na anashuhudia uwongo na hiyana kwenu

Na Yeye ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Atawasamehe na kuwachanganya kwenye rehema yake ikiwa mtatubia na kurejea.

Sema: mimi si kioja miongoni mwa Mitume.

Mimi si wa kwanza kufikisha ujumbe wa Mungu. Wamenitangulia mitume na manabii wengi

Wala sijui nitakavyofanywa mimi wala nyinyi.

Mtume(s.a.w. w ) anajua hali yake na hali ya washirikina huko Akhera. Kwa sababu Mwenyezi Mungu alimpa habari ya hilo; kama zinavyoeleza Aya kadhaa; mbali ya kuwa ilimu hii ni katika nyenzo za utume. Zimekuja Hadith mutawatir, kwamba Mtume aliwabashiria pepo watu kadhaa.

Kwa hiyo basi Maana ya Aya ni kuwa Mtume hajui yatakayowatokea katika maisha ya duniani na atawatia mtihani gani Mwenyezi Mungu. Vile vile hajui kuwa Mwenyezi Mungu atawaadhibu hapa duniani au ataahirisha adhabu yao mpaka siku ya ufufuo.

Mimi nafuata niliyopewa Wahyi tu, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji mwenye kubainisha.

Sio kazi ya muonyaji kujua ilimu ya ghaibu; isipokuwa yeye anafikisha anayopewa wahyi na Mwenyezi Mungu kuhusiana na yale yatakayowatokea washirikina.

Ieleweke kuwa Aya hii ilishuka kabla ya kushuka Aya inayosema kuwa mwisho ni wa dini ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake, wajapochukia washirikina. Au pengine ni miongoni mwa mifumo ya kutoa mwito kwa hikima na mawaidha mazuri.

Sema: Mwaonaje yakiwa haya ni kweli yametoka kwa Mwenyezi Mungu, nanyi mmeyakataa, na alishuhudia shahidi miongoni mwa Wana wa Israili juu ya mfano wa haya, na akaamini, na nyinyi mnafanya kiburi? Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu madhalimu.

Sura hii tuliyo nayo imeshuka Makka isipokuwa Aya hii tuliyo nayo, ilishuka Madina kwa ajili ya Abdullah bin Salim, aliposilimu Madina. Yeye alikuwa mwanachuoni mkubwa wa Wana wa Israil. Haya ndiyo yaliyoelezwa kwenye tafsiri nyingi.

Maana ni sema ewe Muhammad kuwaambia wale wanaodai kuwa Qur’an ni uchawi uliozushwa, hebu niambieni itakuwaje hali yenu mbele ya Mwenyezi Mungu ikithibiti kuwa Qur’an ni haki na kweli na akaiamini mwana wa chuoni katika wana wa Israil; kama vile Abdullah bin Salam ambaye anatambua siri za wahyi na kushuudia kuwa mafunzo ya Qur’an ni kama mafunzo ya Tawrat iliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu kwa Musa? Basi mtakuwaje mkibaki na upotevu wenu na inada yenu? Je mjidhulumu kwa hiyari yenu na kujianika kwenye adhabu ya Mwenyezi Mungu?

Na wale ambao wamekufuru waliwaambia wale ambao wameamini: Lau hii ingelikuwa ni heri, wasingelitutangulia.

Watu wengi walioitikia mwito wa Mtume(s.a.w. w ) , mwanzo mwanzo wa mwito wa Uislamu, walikuwa ni miongoni mwa wanyonge. Kwa hiyo mamwinyi wakaifanya hiyo ni sababu ya kuituhumu risala ya Mtume. Kwa sababu, wanavyodai, ni kuwa haki ni ile inayokubaliwa na vigogo, wala sio kuwa watu wajulikane kwa kuwa na haki. Kila wanalolilifanya matajiri ndio haki na wanalolilifanya wengine ni batili. Hayo ndiyo madai yao, lakini kila mwenye kuipinga haki itamshinda.

Ndio maana hazikupita siku mtumwa wa kihabeshi akapanda kwenye mgongo wa Al-Ka’aba akinadi Lailaha illallah Muhammadurrasulullah (Hakuna Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu, Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu). Na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) akayavunja masanamu na kuyatupa chini ya nyayo zake huku akisema: “Haki imefika na batili imeondoka, hakika batili ni yenye kuondoka.”

Katika Tafsir Arrazi, imeandikwa kuwa mjakazi wa Amru alisilimu na alikuwa akimpiga mpaka anachoka. Basi makafiri wakasema: “Kama Uislamu ungelikuwa ni kheri asingetutangulia majakazi wa Amru.” Lakini Amru mwenyewe alisilimu badaye, akapigana vita vya Roma na Fursi.

Na walipokosa kuongoka kwayo basi wakasema: Huu ni uzushi wa zamani.

Wanazungumziwa makafiri wa kikuraishi. ‘Kwayo’ ni hiyo Qur’an. Mataghuti waliisifu kuwa ya zamani, kwa vile, kwa madai yao, wanasema ni ngano za watu wa kale zilizopitwa na wakati.

Walisema hivi sio kwa lolote isipokuwa wao hawaamini isipokuwa masilahi yao na chumo lao tu, na Qur’an inapinga na kupiga vita hayo.

Na kabla yake kilikuwapo Kitabu cha Musa, kuwa kiongozi na chenye rehema. Na hiki ni Kitabu chenye kusadikisha cha lugha ya kiarabu, ili kiwaonye wale waliodhulumu, na kiwe ni bishara kwa watendao mema.

Qur’an ni kama Tawrat iliyomshukia Musa. Vitabu vyote hivyo viwili vinaongoza kwenye haki na ni rehema kwa mwenye kuviamini na avitumia kwa mujibu wake. Tawrat ilitoa habari za kuja Muhammad:

الَّذِي يَجِدُونَهُ مَكْتُوبًا عِندَهُمْ فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنجِيلِ يَأْمُرُهُم بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَاهُمْ عَنِ الْمُنكَرِ ﴿١٥٧﴾

“Ambaye wanamkuta ameandikwa kwao katika Tawrat na Injili, ambaye anawaamrisha mema na anawakatazamaovu.” Juz. 9 (7:157).

Vile vile Qur’an inaisadikisha Tawrat hii na inatamka kwa lugha yenu, enyi waarabu, ikimuonya na adhabu yule atakayefanya uovu na kumpa habari njema za thawabu yule mwenye kufanya wema. Basi vipi mara mnasema ni uchawi na mara nyingine ni ngano za watu wa kale; mbona hamyasemi hayo kwa Tawrat?

2

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

إِنَّ الَّذِينَ قَالُوا رَبُّنَا اللَّـهُ ثُمَّ اسْتَقَامُوا فَلَا خَوْفٌ عَلَيْهِمْ وَلَا هُمْ يَحْزَنُونَ ﴿١٣﴾

13. Hakika wale waliosema: Mola wetu ni Mwenyezi Mungu; kisha wakawa na msimamo, hawatakuwa na hofu, wala hawatahuzunika.

أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ الْجَنَّةِ خَالِدِينَ فِيهَا جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٤﴾

14. Hao ndio watu wa Peponi, watadumu humo, ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda.

وَوَصَّيْنَا الْإِنسَانَ بِوَالِدَيْهِ إِحْسَانًا حَمَلَتْهُ أُمُّهُ كُرْهًا وَوَضَعَتْهُ كُرْهًا وَحَمْلُهُ وَفِصَالُهُ ثَلَاثُونَ شَهْرًا حَتَّىٰ إِذَا بَلَغَ أَشُدَّهُ وَبَلَغَ أَرْبَعِينَ سَنَةً قَالَ رَبِّ أَوْزِعْنِي أَنْ أَشْكُرَ نِعْمَتَكَ الَّتِي أَنْعَمْتَ عَلَيَّ وَعَلَىٰ وَالِدَيَّ وَأَنْ أَعْمَلَ صَالِحًا تَرْضَاهُ وَأَصْلِحْ لِي فِي ذُرِّيَّتِي إِنِّي تُبْتُ إِلَيْكَ وَإِنِّي مِنَ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٥﴾

15. Na tumemuusia mtu awafanyie wema wazazi wake wawili. Mama yake amebeba mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu. Na kubeba mimba kwake na kumwachisha ziwa ni miezi thalathini. Hata anapofika kukomaa kwake, na akafikilia miaka arubaini. Husema: Mola wangu! Nizindue nishukuru neema yako uliyonineemesha na wazazi wangu, na nipate kutende mema unayoyaridhia. Na unitengenezee dhuriya zangu. Hakika mimi nimetubu kwako, na hakika mimi ni miongoni mwa Waislamu.

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ نَتَقَبَّلُ عَنْهُمْ أَحْسَنَ مَا عَمِلُوا وَنَتَجَاوَزُ عَن سَيِّئَاتِهِمْ فِي أَصْحَابِ الْجَنَّةِ وَعْدَ الصِّدْقِ الَّذِي كَانُوا يُوعَدُونَ ﴿١٦﴾

16. Hao ndio tunaowatakabalia bora ya vitendo walivyovitenda. Na tunayasamehe mabaya yao, watakuwa miongoni mwa watu wa Peponi. Miadi ya kweli hiyo waliyoahidiwa.

KUWAFANYIA WEMA WAZAZI WAWILI

Aya 13 – 16

MAANA

Hakika wale waliosema: Mola wetu ni Mwenyezi Mungu; kisha wakawa na msimamo, hawatakuwa na hofu, wala hawatahuzunika.

Katika Juz. 17 (21:103) Mwenyezi Mungu amesema:“Hiyo fazaa kubwa haitawahuzunisha. Na Malaika watawapokea: Hii ndiyo siku yenu mliyokuwa mkiahidiwa.”

Na katika Aya hii tuliyo nayo, anasema Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwa: hao ni wale walioshikamana na dini ya Mwenyezi Mungu kiitikadi, kikauli na kivitendo katika maisha ya duniani. Jumla hii imetajwa hivi ilivyo na tumeifafanua zaidi katika Juz. 21 (41:30).

Hao ndio watu wa Peponi, watadumu humo, ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda.

Hao ni wale walioamini na wakawa na msimamo. Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Kwa waliyokuwa wakiyatenda,’ ni msisitizo wa kuwa hakuna imani wala msimamo bila ya matendo.

Na tumemuusia mtu awafanyie wema wazazi wake wawili. Mama yake amebeba mimba yake kwa taabu, na akamzaa kwa taabu.

Yaani amepata matatizo mengi alipokuwa na mimba, wakati wa kumzaa na hata kwenye malezi pia. Kuna riwaya inayosema kuwa haki ya mama ni zaidi ya haki ya baba, kwa sababu alimbeba wakati ambapo hakuna yoyote wa kumbeba, akamkinga kwa masikio na macho na viungo vyote, akiwa na furaha. Akakubali awe na njaa, lakini mwanawe ashibe, awe na kiu lakini anywe, awe uchi lakini avae. Basi shukrani na wema ziwe kwa kiasi hicho.

Mwanzoni mtoto alikuwa akiona kuwa ni wajibu wake kuwasikiliza na kuwatii, wazazi wake, lakini sasa mtoto anaona kuwa ni lazima wazazi wake wamtii na kumnyenyekea mtoto na kusikiliza amri zake. Yametangulia maelezo ya kuwafanyia wema wazazi wawili katika Juz. 1(2:83), Juz. 5 (4:36), Juz. 8 (6:151) na Juz. 15 (17:23).

Na kubeba mimba kwake na kumwachisha ziwa ni miezi thalathini.

Tukiunganisha Aya hii na ile isemayo:

وَفِصَالُهُ فِي عَامَيْنِ ﴿١٤﴾

“Na kumwachisha ziwa miaka miwili.” Juz. 21 (31:14),

Inatubainikia kuwa uchache wa muda wa mimba ni miezi sita. Kwa sababu tukiondoa miaka miwili ya kunyonyesha inabakia miezi sita kwa uchache. Elimu ya utabibu ya kisasa imethibitisha nadharia hii.

Sheikh Al-Maraghi Almasri katika tafsiri yake anasema: “Wa kwanza kuvumbua hukumu hii ni Ali (K.W.).”

Na amepokea Muhammad bin Is-haq, mwenye kitabu cha As-Sira, kwamba mtu mmoja alimuoa mwanamke akamzalia mtoto wa mimba ya miezi sita kamili. Akamshitakia Uthman. Alipoletewa, akaamuru arujumiwe (apigwe kwa mawe).

Ali alipopata habari alimjia akamwambia:“Kwani husomi Qur’an? “ Uthman akasema, kwa nini nasoma. Akamwambia:“Hukusikia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na kubeba mimba kwake na kumwachisha ziwa ni miezi thalathini.” Na ile isemayo “Na kumwachisha ziwa miaka miwili.”

Kwa hiyo baada ya miaka miwili, hakuna kinachobaki ila miezi sita?” Uthman akasema: Wallah! Sikujua hivyo.

Hebu nileteeni huyo mwanamke. Basi wakamkuta amezaa. Akasema Muammar bin Abdallah: “Wallah! Hakuna kunguru kwa kunguru wala yai kwa yai lilifonana kuliko mtoto huyu alivyofanana na baba yake. “ Baba yake alipomuona, akasema: “Huyu ni mwanangu, wallah, sina shaka”

Hata anapofika kukomaa kwake na akafikilia miaka arubaini,

Anapofikia baleghe mtu kwa kutoa manii au kwa miaka [1] 1, na akawa ni mwenye akili, katika matumizi yake, basi anakuwa na yale waliyo nayo watu wazima na ni juu yake kutekeleza taklifa zote za sharia.

Hata hivyo wafasiri wamesema kuwa Aya hii inaashiria maudhui mengine ambayo ni kukomaa mtu akili na mwili, kwa dalili ya kuli yake Mwenyezi Mungu: ‘Na akafikia miaka arubaini,’ ambapo anafikia ukomo wa nguvu zake.

Vyovyote iwavyo miaka haitoshi kumfanya mtu kuwa na ukomavu wa akili ikiwa hakupitia uzoefu mwingi.

Sio mbali kuwa kutajwa miaka arubaini katika Aya ni kuashiria kuwa, aghalabu, mtu katika miaka hii anapitia majaribio yenye manufaa. Wafasiri na wanahistoria wanasema kuwa Mwenyezi Mungu hakumtuma Mtume ila baada ya kufikisha miaka arubaini, isipokuwa Isa na Yahya.

Husema: Mola wangu! Nizindue nishukuru neema yako uliyonineemesha na wazazi wangu, na nipate kutenda mema unayoyaridhia.

Mwenye akili hutaka tawfiki na msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu, kuweza kutekeleza shukrani kwake kwa kumtii na kumnyenyekea.

Neema kubwa zaidi ni kuongozwa kwenye haki na kuitumia inavyotakikana. Ama kule kuweko mtu sio neema kwake wala kwa mwingine akiwa si nyenzo ya kufanya matendo mema.

Imetangulia Aya hii kwa herufi zake katika Juz. 19 (27:19).

Na unitengenezee dhuriya zangu.

Watoto ni mzigo mkubwa kwa wazazi, bali malezi yao na matakwa yao ni janga hasa. Lakini, maskini, baba anasahau taabu zote hizi ikiwa Mwenyezi Mungu atamneemesha kizazi chema, vinginevyo itakuwa ni majanga na masaibu makubwa.

Hakika mimi nimetubu kwako, na hakika mimi ni miongoni mwa Waislamu.

Hapa kuna ishara kuwa Mwenyezi Mungu hakubali toba ya mwenye dhambi wala haitikii dua yake ila akitubia dhambi zake na akawa na msimamo katika vitendo vyake na kauli yake.

Hao ndio tunaowatakabalia bora ya vitendo walivyovitenda.

Makusudio ya bora ya vitendo ni visivyokuwa vitendoviovu. Kwa vile vitendo viovu anavisamehe; kama alivyovyosema:Na tunayasamehe mabaya yao, kwa sababu wametubia na kufanya ikhlasi.Watakuwa miongoni mwa watu wa Peponi; yaani watakuwa pamoja nao.

Miadi ya kweli hiyo waliyoahidiwa, kuwa matendo yao yatakubaliwa, kusamehewa makosa yao na kuingia Peponi. Ahadi ya Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kweli na kauli yake ni haki.

وَالَّذِي قَالَ لِوَالِدَيْهِ أُفٍّ لَّكُمَا أَتَعِدَانِنِي أَنْ أُخْرَجَ وَقَدْ خَلَتِ الْقُرُونُ مِن قَبْلِي وَهُمَا يَسْتَغِيثَانِ اللَّـهَ وَيْلَكَ آمِنْ إِنَّ وَعْدَ اللَّـهِ حَقٌّ فَيَقُولُ مَا هَـٰذَا إِلَّا أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٧﴾

17. Na ambaye amewaambia, wazazi wake Ah! Nanyi! Je, mnanitisha kuwa nitafufuliwa, na hali vizazi vingi vimekwishapita kabla yangu! Na hao humwomba msaada Mwenyezi Mungu: Ole wako! Amini! Hakika miadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli. Na yeye husema: Hayakuwa haya ila ni ngano za watu wa kale.

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ حَقَّ عَلَيْهِمُ الْقَوْلُ فِي أُمَمٍ قَدْ خَلَتْ مِن قَبْلِهِم مِّنَ الْجِنِّ وَالْإِنسِ إِنَّهُمْ كَانُوا خَاسِرِينَ ﴿١٨﴾

18. Hao ndio ambao imehakikishwa kauli juu yao; kama mataifa yaliyokwishapita kabla yao miongoni mwa majini na watu. Hakika hao wamekuwa wenye kuhasirika.

وَلِكُلٍّ دَرَجَاتٌ مِّمَّا عَمِلُوا وَلِيُوَفِّيَهُمْ أَعْمَالَهُمْ وَهُمْ لَا يُظْلَمُونَ ﴿١٩﴾

19. Na wote watakuwa na daraja zao mbali mbali kwa waliyoyatenda, na ili awalipe kwa vitendo vyao, na hawatadhulumiwa.

وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَذْهَبْتُمْ طَيِّبَاتِكُمْ فِي حَيَاتِكُمُ الدُّنْيَا وَاسْتَمْتَعْتُم بِهَا فَالْيَوْمَ تُجْزَوْنَ عَذَابَ الْهُونِ بِمَا كُنتُمْ تَسْتَكْبِرُونَ فِي الْأَرْضِ بِغَيْرِ الْحَقِّ وَبِمَا كُنتُمْ تَفْسُقُونَ ﴿٢٠﴾

20. Na siku wale waliokufuru watakapoonyeshwa Moto: Nyinyi mlitwaa vitu vyenu vizuri katika maisha yenu ya dunia, na mkastarehe navyo. Basi leo mnalipwa adhabu ya fedheha kwa mlivyokuwa mkitakabari katika ardhi bila ya haki, na kwa mlivyokuwa mkifanya ufuska.

ALIYEWAAMBIA WAZAZI WAKE AKH!

Aya 17 – 20

MAANA

Na ambaye amewaambia, wazazi wake Ah! Nanyi! na akawaambia:Je, mnanitisha kuwa nitafufuliwa, na hali vizazi vingi vimekwishapita kabla yangu!

Ni nani mtoto huyu anayezungumziwa na Qur’an na kusema kuwa ni kafiri mwenye kuwaudhi wazazi wake?

Jibu : Mwenyezi Mungu hakumtaja mtu hasa. Dhahiri ya Aya inaonyesha kwamba makusudio yake ni kila mtoto anayeikanusha siku ya mwisho, naye akiwa na wazazi wanaojitahidi kumpa nasaha, kumwongoza na kumhadharisha na ghadhabu za Mwenyezi Mungu na adhabu yake, lakini bado anaona kusumbuliwa na kuwaambia: Poteleeni mbali! Vipi mtu ataweza kutoka kaburini na hali amekuwa mchanga? Je, ameshawahi kutokewa na hivyo mwingine asiyekuwa mimi katika zama zozote?

Aya hii inawaelekea vijana wengi wa kisasa, kama vile imewashukia wao. Lau kama watauliza na kujadiliana kwa kukusudia maarifa na kuongoka kwenye uhakika, basi itakuwa ni wajibu wetu tuwakaribishe na maswali na majadiliano yao; na tufanye bidii kubwa kadiri tunavyoweza ili tuwakinaishe, kwa kuifanyia kazi kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

لَتُبَيِّنُنَّهُ لِلنَّاسِ وَلَا تَكْتُمُونَهُ ﴿١٨٧﴾

“Lazima mtakibainisha kwa watu wala hamtakificha.” Juz. 4 (3:187).

Na pia kuwa wao wana haja zaidi ya kuongozwa na kubainishiwa.

Na hao wazazihumwomba msaada Mwenyezi Mungu na humwambia mtoto wao:Ole wako! Amini! Hakika miadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli.

Wanamwomba msaada Mwenyezi Mungu kutokana na kufuru ya mtoto wao na kumsisitiza kwamba ufufuo ni kweli. Mara nyingi mwito wa wazazi kwa mtoto unakuwa kama kawaida tu, lakini neno ‘humwomba msaada Mwenyezi Mungu,’ linaonyesha jinsi wanavyoona uchungu na masikitiko kwa kufuru ya mtoto wao aliyewaasi na ujeuri wake. Lakini pamoja na yote hayo anang’ng’nia upotevu na yeye husema:

Hayakuwa haya ila ni ngano za watu wa kale.

Anawajibu wazazi wake pamoja na huruma zao kwake na nasaha zao: Maneno yenu haya hayana maana yoyote ispokuwa porojo tu. Hivi ndivyo vijana wengi wa kileo wanavyowangalia baba zao na mama zao. Ajabu ni kuwa kijana lau atayasikia haya kutoka kwa kijana mwenzake asingelikuwa na msimamo huu wa dharau.

Hao ndio ambao imehakikishwa kauli juu yao kama mataifa yaliyok- wishapita kabla yao miongoni mwa majini na watu.

‘Hao,’ ni kila mwenye kuifanyia inadi haki na akapinga mwito wa wenye ikhlasi. Kuhakikishiwa kauli juu yao ni neno la adhabu. Hii ni desturi ya Mwenyezi Mungu katika uma zilizotangulia, wawe maji- ni au watu.

Hakika hao wamekuwa wenye kuhasirika, kwa vile waliuacha mwito wa haki na wakamzibia masikio mtoa nasaha aliyemwaminifu.

Na wote watakuwa na daraja zao mbali mbali kwa waliyoyatenda, na ili awalipe kwa vitendo vyao, na hawatadhulumiwa.

Daraja za watu, siku ya Kiyama, zitatofautiana kulingana na matendo yao yalivyokuwa duniani. Tafisiri wazi zaidi inayofafanua Aya hii, ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

يَوْمَ تَجِدُ كُلُّ نَفْسٍ مَّا عَمِلَتْ مِنْ خَيْرٍ مُّحْضَرًا وَمَا عَمِلَتْ مِن سُوءٍ ﴿٣٠﴾

“Siku ambayo kila nafsi itakuta heri iliyoitenda imehudhurishwa, na iliyoyatenda katika uovu.” Juz. 4 (3:30).

Na siku wale waliokufuru watakapoonyeshwa Moto; yaani watakapoadhibiwa, na Malaika wa adhabu watawaambia:

Nyinyi mlitwaa vitu vyenu vizuri katika maisha yenu ya dunia, na mkastarehe navyo.

Mlikusanya mamilioni ya pesa mlizozipora kisha mkazirundika, mkajijengea viwanda na majumba marefu kwa hisabu ya wanyonge, mkatumia yote kwenye raha na starehe, bila ya kuiwekea akiba siku hii ya leo.

Basi leo mnalipwa adhabu ya fedheha kwa mlivyokuwa mkitakabari katika ardhi bila ya haki, na kwa mlivyokuwa mkifanya ufuska.

Mlionyeshwa haki mkaifanyia kiburi, mkajitukuza na mkaijaza ardhi dhulma na ufisadi. Basi onjeni uchungu wa ubaya wenu kama mlivyoonja utamu wake jana.

Katika Tafsir ya Sheikh Al-Maraghi, kuna maelezo kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alipokuwa akitaka kusafiri, mtu wa mwisho kumuaga katika familia alikuwa ni Fatima, na mtu wa kwanza kumjulia hali, anaporudi safirini, alikuwa ni Fatima. Siku moja aliporudi kutoka katika vita alikwenda nyumbani kwa Fatima, kama desturi yake.

Akaona pazia ya sufu nzito mlangoni na akawaona Hasan Na Husein wamevishwa vikuku vya fedha, basi akarudi bila ya kuingia. Fatima akaona kuwa hakuingia kutokana na aliyoyaona. Basi akaiondoa ile pazia na vikukuu akavipeleka kwa baba yake naye akawapa masikini na akasema: “Hawa ndio watu wa nyumba yangu – akiwashiria Fatima na waliomo nyumbani mwake – wala sipendi wale vizuri vyao katika maisha yao ya dunia.”

6

ILI NIWE PAMOJA NA WAKWELI

UCHAMBUZI WA MADA

Madda muhimu katika uchambuzi: Imebakia madda moja muhimu ndani ya uchambuzi wote huu, madda ambayo inataka kuangaliwa kwa makini na kusomwa, na huenda hiyo pekee ndiyo kikwazo ambacho huwachemua wapinzani pale wanaposhinikizwa kwa hoja nzito. Utawaona wanashangaa na kutokuamini ya kuwa Masahaba wapatao laki moja walihudhuria kutawazwa kwa Imam Ali (kuwa Khalifa wa Mtume) na hatimaye hao hao Masahaba wakaafikiana wote kumkhalifu Imam Ali na kumpuuza na miongoni mwao wamo Masahaba wakubwa.

Hali hii (ya kushangazwa kwa wapinzani) imepata kunitokea mimi mwenyewe wakati nilipoingia kikamilifu ndani ya utafiti, sikuamini na haiwezekani kwa mtu yeyote kuamini pindi tukio hili linapoaridhiwa kama lilivyo, lakini wakati tunapolisoma tukio hili kwa pande zote basi kule kushangaa kunaondoka kwani hali halisi haiko kama tunavyoitazamia sisi au kama wanavyoiaridhi Masunni (ya kuwa) haiwezekani Masahaba laki moja wakaenda kinyume na amri ya Mtume, hivyo basi ilikuwaje mambo yakatokea kama yalivyotokea?

Kwanza Siyo kila aliyehuduria Baia ya Ghadir alikuwa akiishi Madina, bali ilikuwa kama ambavyo hali halisi ilivyokuwa kwamba kwa kiasi kikubwa itakuwa ni watu elfu tatu au Nne tu miongoni mwa Masahaba hao ndiyo waliokuwa wakiishi Madina.Na tutakapofahamu ya kwamba wengi wa hawa walikuwa ni watumwa na walioachwa huru na wanyonge ambao walimfikia Mtume (s.a.w.) kutoka sehemu mbali mbali na hapo Madina hawakuwa na uwenyeji wala jamaa (kwa mfano watu wa As-Safah) basi haitabakia isipokuwa nusu yao yaani watu elfu mbili tu, na hata hawa nao ni watiifu kwa viongozi wa makabila na muongozo wa kidugu ambao ndiyo wanaohusika nao na Mtume aliwakubalia (kuwa watiifu kwa viongozi wao) kwani ulipokuwa ukimfikia ujumbe wa kabila fulani, Mtume (s.a.w.) humtawalisha juu yao kiongozi wao, na kwa ajili hiyo ndiyo tumekuta katika Uislamu Istilahi ya kuitwa kwao kuwa ni Ahlul-Hilli wal-Iqdi, watu wanaotumainiwa kutowa maamuzi katika jamii au nchi.

Kadhalika tunapoutazama mkutano wa Saqifah ambao ulikutana mara tu baada ya kufariki Mtume (s.a.w.), tunawakuta waliohudhuria ambao waliuthibitisha uchaguzi wa Abubakar kuwa ni khalifa, idadi yao haizidi watu mia moja kwa makadirio ya juu, kwani katika Ansari ambao ndiyo wenyeji wa Madina hawakuhudhuria isipokuwa viongozi wao kama ambavyo Muhajirina ambao ni wenyeji wa Maka waliohama pamoja na Mtume (s.a.w.) hawakuhudhuria isipokuwa watu watatu au wanne wakiwakilisha Maquraishi. Hali hii itoshe basi kuwa ni dalili ya kupima ukubwa wa hiyo Saqifah ikoje, Saqifah ambayo ilikuwa haina nafasi ya kutosha, kwani haikuwa inakosa kuwa karibu katika kila nyurnba.

Kwa hiyo haikuwa uwanja wa maadhimisho wala siyo jumba la mikutano, na tunaposema kuwa watu mia moja walihudhuria hapo Saqifah bani Saida basi idadi hiyo sisi ndiyo tunaoizidisha ili tu, mwenye kutafiti aweze kufahamu kwamba wale Masahaba laki moja hawakuwepo wala hata hawakusikia mazungumzo yalivyofanyika ndani ya Saqifah isipokuwa baada ya muda mrefu kupita, .kwani hapo zamani hapakuwa na mawasiliano ya anga wala simu au Satellite.

Na baada ya mabwana wakubwa hawa kuafikiana juu ya Abubakar pamoja na upinzani wa bwana wa Kiansari Saad bin Ubbadah ambaye ni kiongozi wa kabila la Khazraj na mwanawe Qais, lakini wengi mno miongoni mwao (kama isemwavyo hii leo) walipitisha makubaliano hayo na kumpa Abubakar mkono wa Baia, wakati ambapo Waislamu wengi hawakuwepo hapo Saqifah, na baadhi yao walikuwa wameshughulika kumuandaa Mtume (s.a.w.) kwa mazishi au walihamanika kutokana na khabari za kifo chake, ambapo Umar bin Al-Khatab naye alikuwa amewatisha na kuwatia khofu iwapo watasema kuwa Mtume amefariki. Taz: Sahih BukhariJuz. 4 -195.

Zaidi ya hayo wengi wa Masahaba wa Mtume walikuwa amewateua wawemo ndani ya Jeshi la Usamaha na wengi wao walikuwa wameweka kambi mahala paitwapo Jorfi wakiwa tayari kwenda vitani na jeshi la Usamah hawakuwepo Mtume alipofariki wala hawakuhudhuria mkutano wa Saqifah. Basi je, inaingia akilini baada ya haya yaliyotokea kwamba mtu fulani katika kabila au ukoo kumpinga kiongozi wake kwa lile alilolipitisha na hasa inapokuwa hilo alilolipitisha lina ubora na utukufu mkubwa ambao kila kabila linaukimbilia? Ni nani ajuwaye ya kwamba huenda siku moja naye atawatawalia Waislamu wote, maadamu mwenye haki hiyo kisheria amekwisha tupwa mbali na mambo sasa yanakwenda kwa kushauriana wanabadilishana kwa kuachiana, basi ni kwa nini wasilifurahie hilo, na ni kwa nini wasiliunge mkono?

Pili Ikiwa wenye uwezo wa kuamua ni wakaazi wa Madina na wamepitisha jambo fulani, basi watu walio mbali katika sehemu mbali mbali za bara Arabu hawawezi kupinga na hali ya kuwa hawajui yanayopita wakati hawapo kwani vifaa vya mawasiliano kwa zama hizo vilikuwa ni vile vya kizamani kisha wao walikuwa wakifahamu kwamba wakazi wa Madina ndiyo waliokuwa wakiishi na Mtume wa Mwenyezi Mungu hivyo basi hao ndiyo wajuao mno mambo mapya miongoni mwa hukmu, kwani huenda ukashuka Wahyi wakati wowote au siku yoyote. Kisha kama kuna kiongozi wa kabila lolote lililo mbali na makao makuu basi jambo la Ukhalifa kwake si muhimu sana sana iwapo Abubakr atakuwa Khalifa au Ali au mtu mwingine yeyote, kwani watu wa Maka ndiyo wajuao zaidi utaifa wao, na cha muhimu kwao ni kubakia kwenye uongozi wa ukoo wake ambapo hakuna anayemkera katika uongozi huo.

Basi ni nani ajuwaye kwamba huenda baadhi ya watu waliulizia juu ya jambo hilo (la Ukhalifa) na walitaka kufahamu mambo yalivyokwenda lakini vyombo vya mtawala viliwanyamazisha sawa iwe kwa njia ya kuwapa tamaa ya mali au vyeo au vitisho, na huenda kisa cha Malik bin Nuwairah ambaye alikataa kutoa zaka kwa Abubakr ni utokea jambo hilo. Na yeyote mwenye kufuatilia matukio hayo yaliyotokea katika vita ya wanaokataa kutoa zaka katika zama za Abubakr atakuta kuna kupingana (kwa maelezo), wala hawezi kutosheka kwa maelezo yaliyoelezwa na baadhi .ya wanahistoria kwa lengo la kulinda heshima ya Masahaba na hasa wale watawala.

Tatu Kiini cha tatizo hili ni kule kushitukizwa ghafla kupatikana kwa Khalifa, hili ni jambo lililochangia mno kukubalika kwa kile ambacho leo kinaitwa kuwa "Hali halisi iliyopo". Kwani mkutano wa Saqifah ulifanyika ghafla kwa kuwashitukiza baadhi ya Mashaba ambao walikuwa wakimshughulikia Mtume (s.a.w.), na miongoni mwao alikuwa Imam Ali na Abbas na wengine miongoni mwa Bani Hashim, Miq-dad, Salman, Abu Dharri, Ammar, Zubair na wengineo wengi. Ama wale waliokuwa Saqifah walipotoka huko hali ya kuwa wakimshangilia Abubakr walielekea msikitini huku wakitoa mwito kwa watu wafanye baia ya jumla na watu wakaipokea baia hiyo kwa wingi watake wasitake kipindi hicho Imam Ali na wafuasi wake walikuwa hawajamaliza wajibu wao Mtukufu ambao tabia zao (mwenendo wao) mwema uliwalazimisha (wautimize) basi haikuwezekana kwao kumuacha Mtume (s.a.w.) bila ya kumkosha, kumvisha sanda, kumtayarisha na kumzika eti badala yake wakimbilie Saqifah kugombea Ukhalifa.

Walipomaliza wajibu wao huo, mambo yalikuwa yamekwisha kamilika kwa Abubakr na yeyote mwenye kwenda kinyume na baia hiyo akawa anahesabiwa kuwa ni miongoni mwa watu wenye fitna ambaye anabomoa umoja wa Waislamu, hivyo ni wajibu kwa Waislamu kumpinga au hata kumuuwa ikiwa itabidi, na ndiyo maana tunamuona Umar alimuonya Saad bin Ubbadah kuwa atauawa pale alipokataa kumbai Abubakr, Umar akasema, "Muuweni hakika yeye ni mtu wa fitna"[52] na baada ya hapo Umar aliwatishia wote waliobaki ndani ya nyumba ya Ali ya kuwa atachoma moto nyumba hiyo na wote waliomo humo. Tukishakufahamu vyema maoni ya Umar bin Al-Khatab kuhusu baia tutatambua mengi baada ya hapo miongoni mwa mambo yanayotatanisha.

Kwa hakika Umar anaona kuwa baia inatosha kusihi pale mmoja miongoni mwa Waislamu anapowahi, basi hapo inakuwa ni lazima kwa wengine kumfuata na yeyote atakayeasi miongoni mwao huyo atakuwa ametoka nje ya mshikamano ya Waislamu na ni wajibu kumuuwa. Basi hebu na tumsikilize yeye mwenyewe hasa kuhusu baia, kama alivyoeleza Bukhar ndani ya Sahih yake juzuu ya nane ukurasa wa ishirini na nane, Babu Rajmi Al-Hubla Minaz-Zinaa Idha-Ah-Sanat amesema: akisimulia yale yaliyotokea ndani ya Saqifah. "Basi fujo ikazidi na sauti zikapaa mpaka nikatishika kuwa kutatokea kuhitilafiana, nikasema, Ewe Abubakr kunjua mkono wako, Abubakar akakunjua mkono wake nikambai nao muhajirina wakambai[53] Ansari (nao wakambai) na tukamruka Saad bin Ubbadah, akasema msemaji miongoni mwao, "Mmemuuwa Saad bin Ubbadah" Mimi nikasema:

"Mwenyezi Mungu amuuwe Saad bin Ubbadah" Umar akasema: "Wallahi sisi hatujakutana na jambo gumu katika yote tuliyohudhuria kuliko kumbai Abubakar, tulichelea kuwa hawa jamaa tukiwaacha bila kupitisha baia, basi watambai mtu miongoni mwao baada yetu, hivyo imma tuwape madaraka, jambo ambalo hatulikubali, au tuwapinge itokee uharibifu, (naonya) yeyote atakayetoa baia bila ya kushauriana na Waislamu asifuatwe yeye wala yule aliyembai ili asiuawe. Basi jambo lililovyo kwa Umar siyo uchaguzi wala hiyari wala mashauriano, bali inatosha pale Mwislamu mmoja anapoiwahi baia hiyo iwe ni hoja kwa wengine na ndiyo maana alimwambia Abubakr, "Kunjua mkono wako Ewe Abubakar," na Abubakr naye akakunjua mkono wake akambai bila ya mashauriano tena haraka haraka kwa kuchelea kutanguliwa na mwingine na kwa hakika Umar amekwisha ieleza rai hii pale aliposema:

"Tulichelea lau tutawaacha watu hawa bila ya kuipitisha baia, watambai mtu miongoni mwao baia yetu (Umar aliwachelea Maansar wasimtangulie wakambai mtu miongoni mwao), na kinachomuongezea ufafanuzi zaidi ni pale anaposema: "Basi imma tuwape Baia jambo ambalo hatulikubali na au tuwapinge patokee uharibifu."[54]

Na ili tuwe waadilifu katika maamuzi na wenye kuchunguza kwa undani, inatupasa tukiri kwamba Umar bin Al-Khatab alibadilisha mtazamo wake kuhusu baia mwishoni mwa uhai wake na hilo ni pale mtu mmoja alipomjia Umar mbele ya Abdur-Rahman bin 'Auf katika Hijja yake ya mwisho aliyohiji, yule mtu akamwambia: "Ewe Amirul-Muuminina unayo habari kuwa fulani anasema, bila shaka Umar akifa hakika nitambai fulani kwani wallahi baia ya Abubakar haikuwa isipokuwa kwa kushitukiza tu na ilitimia". Umar alikasirika na kwa ajili hii alisimama akawahutubia watu alipokuwa akirudi Madina, miongoni mwa aliyoyasema katika khutba yake ni haya yafuatayo:

"Kwa hakika nimepata habari kwamba kuna asemaye miongoni mwenu kuwa, Wallahi lau Umar atakufa nitambai fulani, basi na asijidanganye mmoja wenu kusema kuwa baia ya Abubakar ilikuwa hivyo lakini Mwenyezi Mungu aliikinga shari yake.."[55] Kisha Anasema: "Yeyote mwenye kumbai mtu bila mashauriano kutoka kwa Waislamu, basi huyo asipewe baia yeye wala huyo aliyembai kuhofia asije uwawa.[56]

Basi laiti Umar angekuwa na mtazamo huu siku ya Saqifah na asiwalazimishe Waislamu kumbai Abubakr ambako kulikuwa kwa kushitukiza, na Mwenyezi Mungu aliikinga shari yake kama alivyoshuhudia yeye mwenyewe, lakini imekuwaje Umari awe na rai hii mpya katika mtazamo huu mpya, hakika atakuwa amejihukumia kifo yeye mwenyewe na rafiki yake (Abubakr) kwa kuwa kwenye mtazamo wake mpya anasema: "Yeyote mwenye kumbai mtu bila ya mashauriano toka kwa Waislamu basi asipewe Baia yeye wala huyo aliyembai ili asije uwawa."

Imebakia juu yetu kufahamu ni kwa nini Umar alibadilisha maoni yake mwishoni mwa uhai wake pamoja na kwamba yeye anafahamu mno kuliko mwingine ya kuwa mtazamo wake mpya unatengua baia ya Abubakar iliyotimia bila ya mashauriano toka kwa Waislamu na ilikuwa ni baia ya kushitukiza? Pia mtazamo wake huu mpya unatengua baia yake yeye aliyopewa, kwani aliupata ukhalifa kwa tamko la Abubakar wakati wa kufa bila ya makubaliano kutoka kwa Waislamu, kiasi baadhi ya masahaba walikwenda kwa Abubakar wakamkemea kwa kuwatawalishia mtu msusuavu tena mgumu wa tabia.[57] Na Umar alipotoka ili awasomee watu maandiko ya Abubakr kuna mtu alimuuliza: "Ewe Baba Hafs kuna nini ndani ya waraka huo?" Umar akasema, Sijuwi, lakini mimi nitakuwa wa kwanza kusikiliza na kutii." yule mtu akasema: "Lakini Wallahi mimi najua kilichomo, wewe ulimtawalisha (Abubakar) kipindi cha mwanzo naye amekutawalisha kipindi hiki".

Taz: Al-Imam Was-Siyasah cha Ibnu Qutaibah Juz. 1 uk. 25Mlango unaohusu maradhi ya Abubakri na kumtawalisha kwake Umar. Kauli hii inafanana na kauli ya Imam Ali kumwambia Umar pale alipomuona anawalazimisha watu kwa nguvu wambai Abubakr akasema "Nifanye jambo ambalo wewe utakuwa na hisa (wanitaka) leo nilikazanie jambo lake ili kesho akurudishie"? Taz: Al-Imamah Was-Siyasah cha ibnu Qutaiba Juz. 1 uk. 18. Cha muhimu ni kufahamu ni kwa nini Umar alibadilisha mtazamo wake kuhusu Baia?

Mimi ninakurubia kuamini kwamba, wakati alipowasikia baadhi ya Masahaba wanataka kumbai Ali bin Abi Talib baada ya kufa Umar jambo ambalo yeye Umar kamwe hakubaliani nalo, kwa kuwa yeye ndiye aliyezipinga maagizo ya Mtume yaliyobayana, na akapinga Mtume (s.a.w.) asiwaandikie yale maandiko[58] kwa kuwa yeye alilifahamu lengo lake kiasi kwamba akamtuhumu Mtume kuwa anaweweseka na akawatisha watu wasiseme kuwa Mtume amekufa[59] yote hayo ni kwa sababu wasije wakawahi kumbai Ali. Umar alitilia mkazo baia ya Abubakr na akawalazimisha watu kwa nguvu waikubali baia hiyo na kisha kumuonya kila atayepinga kuwa atamuua[60] ili tu kumtenga mbali Ali na ukhalifa.

Hivi itawezekana Umar aridhie aseme msemaji kwamba fulani atapewa baia lau Umar atakufa? Hasa pale msemaji huyu ambaye jina lake limebakia kuwa halijulikani na hapana shaka kuwa alikuwa miongoni mwa Masahaba wakubwa? Msemaji huyu alitumia hoja ya kitendo alichokitenda Umar mwenyewe alipombai Abubakar pale anaposema: "Wallahi Baia ya Abubakr haikuwa isipokuwa ya kushitukiza na ikatimia", yaani pamoja na kuwa ilitokea kwa kuwashitukiza Waislamu na bila kupata ushauri wao lakini ilitimia na likawa jambo lililothibitika, kwa hiyo ilifaa kwa Umar kulifanya kwa Abubakr kwa nini isifae kwake kulifanya yeye mwenyewe kwa njia ile ile kwa mwingine? Na hapa tunaona kwamba ibn Abbas na Abdur-Rahman bin Auf na Umar bin Khatab wanakwepa kulitaja jina la huyu msemaji kama ambavyo wanakwepa kulitaja jina la mtu anayetaka kupewa baia msemaji huyu. Na ilipokuwa wawili hawa wanao umuhimu mkubwa kwa Waislamu, tunamuona Umar alikasirika kwa usemi huu na haraka katika Ijumaa ya kwanza aliwahutubia watu na akaieleza maudhui ya Ukhalifa itakavyokuwa baada yake na akawaonesha maoni yake mapya kuhusiana na Ukhalifa, ili azuwie njia ya huyu anayetaka kurudisha ile ghafla iliyokwisha tokea kwani njia hiyo itamnufaisha mgomvi wake, kwani kwa kupitia uchunguzi tumefahamu kuwa usemi huo haukuwa ni maoni ya fulani tu peke yake, bali ulikuwa ndiyo mtazamo wa Masahaba wengi, na ndiyo maana Bukhari anasema: "Umar alichukia na kisha akasema bila shaka apendapo Mwenyezi Mungu mimi nitasimama usiku huu miongoni mwa watu niwaonye hawa ambao wanataka kuwapora mambo yao..." [61]

Basi kubadilisha kwa Umar mtazamo wake kuhusu Baia ilikuwa ni kuwapinga hawa ambao wanataka kuwapokonya watu mambo yao na wambai Ali, na hili ni jambo ambalo Umar hakubaliani nalo kwani yeye anaitakidi kuwa Ukhalifa ni miongoni mwa mambo ya watu na siyo haki ya Ali bin abi Talib, na itikadi hii itapokuwa ni sahihi, basi ni kwa nini yeye Umar aliruhusu kuwapokonya watu mambo yao baada ya kufariki Mtume (s.a.w.) na haraka haraka akambai Abubakar bila ya makubaliano na Waislamu. Na msimamo wa Abu Hafs (Umar) dhidi ya Abul-Hasan (Ali) unaeleweka na ni mashuhuri mno, nao ni kumtenga Ali kwenye utawala kwa kutumia njia yoyote inayowezekana.

Na matokeo haya hatukuyafahamu kutokana na hotuba yake (Umar) iliyotangulia hapo kabla peke yake, lakini yeyote mwenye kufuatilia historia atafahamu kuwa Umar bin Al-Khatab alikuwa ndiye mtawala mtendaji hata katika Ukhalifa wa Abubakr na ndiyo maana tunamuona Abubakr anamuomba Usamah bin Zaid amuachie Umar bin Al-Khatab ili amsaidie kuhusu suala la Ukhalifa kama alivyoeleza hilo Ibn Saad ndani ya Tabaqat yake na pia wanahistoria wengi walioelezea jeshi la Usamah - pamoja na hayo tunamuona Ali bin Abi Talib anabakia mbali na majukumu, hawakumpa cheo chochote wala utawala wowote wala kumpa uamiri wa jeshi lolote lile na wala hawakumuamini kuwa mweka hazina na yote haya ni kwa kipindi cha Ukhalifa wa Abubakr, Umar na Uthman, nasi sote twamjua Ali bin Abi Talib ni nani.

Cha kushangaza kuliko yote haya ni kuwa, sisi tunasoma ndani ya vitabu vya historia kwamba kifo kilipomfikia Umar alisikitika kwamba lau Abu Ubaidah bin Al-Jarrah au Salim Huru wa Abu Hudhaifah wangekuwa hai angewatawalisha baada yake. Lakini hapana shaka Umar alikumbuka kuwa hapo kabla alikwisha badilisha mtazamo wake juu ya baia kama hii na akaiona kuwa ni ya kushitukiza na ni kupokonya mambo ya Waislamu, basi hapana budi kwake aweke njia mpya kuhusu baia ili kati kwa kati asije yeyote akafaulu kumbai amuonaye kuwa anafaa na kuwalazimisha watu kumfuata kama alivyofanya yeye kwa Abubakr na kama alivyofanya Abubakar kwake Umar au kama atakavyofanya fulani ambaye anangoja kufa kwa Umar ili ambai jamaa yake.Basi hili haliwezekani baada ya Umar kuwa ameuhukumia Ukhalifa kuwa ni jambo lililofanyika ghafla na kuwa linataka kuwa ni jambo la kupora, na haiwezekani pia kwake kuliacha jambo hili liwe la makubaliano baina ya Waislamu. Na ule mkutano wa Saqifah uliofuatia kufariki kwa Mtume (s.a.w.) yeye Umar alihudhuria na akajionea mwenyewe hitilafu iliyotokea ambayo karibu zitoke roho za watu na damu imwagike.

Basi baadaye alitoa fikra ya watu wa mashauriano au (tuseme) watu sita ambao peke yao ndiyo wenye haki ya kumchagua Khalifa na Muislamu mwingine yeyote hana haki ya kushirikiana nao katika jambo hilo, na Umar alikuwa akitambua kwamba tofauti baina ya watu hawa sita haiwezi kuepukwa, ndiyo maana aliusia ikiwa watatofautiana basi wawe kwenye upande alioko Abdur-Rahman bin Auf hata kama itapelekea kuwauwa watu watatu ambao watamkhalifu Abdur-Rahman bin Auf wakati watakapogawika watu hawa sita makundi mawili, na hilo ni muhali kwani Umar anafahamu kwamba Saad bin Abi Waqas ambaye ni ibn Ammi ya Abdur-Rahman bin Auf na wawili hawa ni ukoo wa Bani Zuhrah, na alifahamu pia kwamba Saad hampendi Ali na moyoni mwake kulikuwa na chuki kwani Ali ndiye aliyewauwa wajomba zake wa ukoo wa Abdis-Shams, kama ambavyo Umar alikuwa akifahamu kwamba Abdur-Rahman bin Auf ni shemeji wa Uthman kwani mkewe aliyekuwa akiitwa Ummu Kul-thum ni dada wa Uthman. Si hivyo tu kadhalika alifahamu kuwa Tal-hah akimpenda Uthman kutokana na mahusiano yaliyokuwepo baina yao kufuatana na maelezo ya baadhi ya wapokezi wa khabari, na hakika ilitosha kwa Tal-hah kumpenda Uthman kutokana na kumpinga kwake Ali kwani yeye Tal-hah ni katika ukoo wa Bani Taym, na kulikuwa na chuki fulani baina ya Bani Hashim na Bani Taym kutokana na Ukhalifa wa Abubakar.

Taz: Shark Najul-Balaghah ya Muhammad Abdoh, Juz. 1 uk. 88.

Umar alikuwa akiyajuwa yote hayo na kwa ajili hii ndiyo maana akawachagua hawa peke yao. Umar aliwachagua hawa watu sita na wote wakiwa ni Maquraish na wote ni kutoka katika Muhajirina na hakuna yeyote kati yao ambaye ni kutoka miongoni mwa Ansar na wote hawa kila mmoja wao akiwakilisha na kuongoza kabila lenye umuhimu wake na athari yake.

1. Ali bin Abi Talib, kiongozi wa Bani Hashim.

2. Uthman bin Affan kiongozi wa Bani Umayyah

3. Abdur-Rahman bin Auf, kiongozi wa Bani Zuhrah

4. Saad bin Abi Waqqas, yeye ni kutoka katika Bani Zuhrah na wajomba zake ni Bani Umayyah.

5. Tal-ha bin Ubaidullah, Bwana wa Bani Taym.

6. Zubair bin Al-Awwan, yeye ni mtoto wa Safiyyah ambaye ni shangazi yake Mtume na ni mume wa As-maa binti Abubakr.

Basi hawa ndiyo wenye kutoa maamuzi, na hukmu yao ikubaliwe na Waislam wote, sawa sawa wakiwa ni wakaazi wa Madina (Makao Makuu ya Ukhalifa) au wengineo katika ulimwengu wote wa Kiislamu na ni wajibu wa Waislamu yeyote atakayetoka miongoni mwao akawa kinyume cha maamuzi yao basi damu yake imwagwe (auawe). Na hili ndilo jambo pekee tulilokuwa tunataka kulisogeza katika akili ya msomaji kuhusiana na kunyamaziwa kwa tamko la Ghadir katika maelezo yaliyotangulia.

Na ikiwa Umar anaufahamu undani, mapenzi na mtazamo wa watu hawa sita, basi bila shaka yeye alikuwa kisha mpendekeza Uthman bin Affan kuwa Khalifah au alikuwa anajua kuwa wengi miongoni mwa hawa sita hawamkubali Ali, vinginevyo ni kwa nini na ni kwa haki gani Umar anatilia nguvu upande wa Abdur-Rahman bin Auf dhidi ya Ali bin Abi Talib wakati ambapo Waislamu tangu hapo zamani na mpaka leo wamekuwa wakishindana juu ya ubora wa Ali na Abubakar na hatujamsikia yeyote akimlinganisha Ali na Abdur-Rahman bin Auf.

Na hapa hapana budi nisimame kidogo ili niwaulize Masunni ambao wanatetea msingi wa mashauriano na pia (niwaulize) watu wenye fikra iliyohuru wote kwa ujumla, nawauliza wote hawa, ni vipi mnaafiki baina ya mashauriano kwa maana yake ya Kiislamu na baina ya fikra hii ambayo kama itajulisha kitu fulani basi haitajulisha isipokuwa ni maoni ya ki-dikteta, kwani yeye Umar ndiye aliyewachagua watu hawa sita na siyo Waislamu, na iwapo kuufikia kwake Ukhalifa lilikuwa ni jambo la ghafla, basi ni kwa haki ipi anawalazimisha Waislamu wakubali mmoja wa hawa sita?

Kinachojitokeza kwetu ni kwamba Umar anauona Ukhalifa kuwa ni haki ya Muhajirina peke yao na mwingine yeyote hana haki ya kuwakorofisha kwenye jambo hili, bali zaidi ya hivi ni kuwa Umar anaitakidi kama anavyoitakidi Abubakar kwamba Ukhalifa ni milki ya Maquraish, bali wamo pia wasiokuwa Waarabu, hivyo basi haistahiki kwa Sal-man Al-Farisi wala Ammar bin Yasir wala Bilal wa Uhabeshi wala Suhayb Mrumi, wala Abu Dharri Al-Ghifari wala maelfu ya Masahaba ambao siyo Maquraish (haistahiki kwao) kujitokeza kwa ajili ya Ukhalifa. Na haya siyo madai ya hivi hivi tu sivyo kabisa, bali hiyo ndiyo itikadi yao ambayo historia na wataalamu wa hadithi wameisajili kutoka vinywani mwao (kina Abubakar na Umar) na hebu tuirudie khutba yenyewe ambayo Bukhari na Muslim wameieleza ndani ya Sahih zao:

Umar bin Al-Khatab anasema:

"Nilitaka kusema, na nilikuwa nimetunga vizuri usemi ambao ulinifurahisha nikitaka niutamke mbele ya Abubakr na nilikuwa nikimzunguka karibu. Basi nilipotaka kusema Abubakr akasema, tulia (ewe Umar), na sikupenda kumkasirisha. Abubakar akazungumza, na alikuwa mpole mno kuliko mimi na mtulivu mno, Wallahi hakuacha neno lolote katika maneno nilioyaandaa isipokuwa aliyasema vizuri zaidi mpaka aliponyamaza kisha akasema, nilichokieleza kwenu katika wema ninyi ndiyo mnaostahiki (akiwaambia Maansari) na wala jambo hili halitatambulika isipokuwa kwa upande huu wa Maquraish. Taz: Sahih Bukhar Babul-Wasiyyah.

Kwa hiyo inatubainikia wazi- kwamba Abubakr na Umar hawaamini mashauriano na hiyari, na baadhi ya wanahistoria wanasema kwamba Abubakar alitoa hoja dhidi ya Maansar kwa hadithi ya Mtume (s.a.w.) isemayo kuwa "Ukhalifa uko kwa Maquraish" Na hadithi hiyo hapana shaka ni sahihi (kama walivyoitaja Bukhar na Muslim na Sahih zote kwa Masunni na Mashia) Mtume (s.a.w.) amesema: "Makhalifa baada yangu ni kumi na wawili na wote ni kutoka kwa Maquraishi" na hadithi iliyo wazi zaidi kuliko hii ni ile kauli ya Mtume (s.a.w.) aliposema:

"Jambo hili (la Ukhalifa) halitakoma kwa Maquraish muda wote hata wakibakia watu wawili"[62] pia kauli yake isemayo "Watu ni wafuasi wa Maquraishi katika kheri na shari[63].

Basi ikiwa Waislamu wote wanaziamini hadithi hizi, ni vipi mtu aseme kuwa Mtume aliliwacha suala la Ukhalifa liwe la mashauriano baina ya Waislamu wamchague wamtakaye? Na haiwezekani kwetu sisi kukwepa kupingana huku, isipokuwa tutakapoyachukua maneno ya Maimamu wa nyumba ya Mtume na wafuasi wao na baadhi ya wanachuoni wa Kisunni ambao wanasisitiza kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu aliwataja Makhalifa na akawabainisha kwa idadi yao na majina yao, na hapo ndipo utakapoweza pia kuufahamu msimamo wa Umar na kuuthibiti Ukhalifa kwa Maquraish na huyu Umar ni mtu aliyefahamika kwa Ijtihadi yake dhidi ya maagizo ya Mtume hata katika uhai wake mwenyewe Mtume (s.a.w.), kwani matukio ya Sul-hu ya Hudaybiyah[64] kuwasalia wanafiki,[65] msiba wa siku ya Al-Khamis,[66] na kuzuwiya kwake kubashiria watu pepo[67] ni ushahidi mkubwa wa haya tuyasemayo.

Basi haishangazi kwa Umar kufanya Ij-tihad baada ya kufariki Mtume dhidi ya hadithi inayohusu Ukhalifa, haoni ulazima wa kukubali agizo linalomuhusu Ali bin Abi Talib ambaye ni Quraish, mdogo kwa umri. Ni yeye aliyeidhibiti haki ya kumchagua Khalifa kwa Maquraish peke yao, na ni yeye ambaye alilazimisha peke yake kuchagua watu sita miongoni mwa watukufu wa Kiquraishi kabla hajafa ili ikubaliane kati ya hadithi ya Mtume (s.a.w.) na vile aonavyo yeye juu ya haki ya Maquraishi peke yao kuhusika na Ukhalifa. Huenda kumuingiza Ali katika kundi hilo hali yakuwa akifahamu kwamba wao hawatamchagua, ni udhibiti wake kwa Umma ili amlazimishe Ali kuingia pamoja nao ndani ya mchezo wa Kisiasa kama wanavyouita leo hii na ili pasibakie kwa Ali na wafuasi wake na wapenzi wake ambao walikuwa wakidai kuwa yeye ndiye wa mwanzo (pasibakie kwao) hoja yeyote. Lakini Imam Ali aliyazungumza yote hayo katika hotuba yake mbele ya watu wote akasema kuhusu jambo hilo:

"Nilivumilia muda wote wa taabu na majaribu mpaka alivyoondoka akauweka (Ukhalifa) chini ya maamuzi ya kikundi cha watu sita akidhania kuwa mimi nafanana nao oh! hayawi sawa ya Mungu na mashauriano! Toka lini nikatiliwa mashaka na wa kwanza miongoni mwao mpaka imebidi nilinganishwe na watu kama hawa! lakini nilitua walipotua na niliruka waliporuka (yaani, niliishi nao kwa hekima).

Nne: Hakika Imam Ali (a.s.) alitoa hoja dhidi yao kwa kila namna lakini bila mafanikio, na je, Imam Ali aombe baia ya watu ambao walimgeuzia nyuso zao na nyoyo zao zikawaelekea wengine imma kwa husuda dhidi yake kutokana na yale aliyompa Mwenyezi Mungu miongoni mwa fadhila zake, na imma kwa chuki dhidi yake kwani yeye ndiye aliyewaua mabwana zao, akawabomoa mashujaa wao, akawakatisha tamaa, akawadhalilisha na kuvunja ujeuri wao kwa upanga wake na ushujaa wake mpaka wakasilimu na kujisalimisha hali ya kuwa Imam Ali akiwa ni Mtukufu akimtetea mwana wa ammi yake (Mtume s.a.w.) na alipokuwa akifanya hayo haikumzuwia kuyatenda kwa ajili ya Mwenyezi Mungu lawama ya mwenye kulaumu na wala hakurudi nyuma kwenye azma yake kutokana na tamaa ya dunia. Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.) naye alikuwa akiyajua vema hayo na kila tukio alikuwa akitilia mkazo fadhaila za nduguye na mwana wa ammi yake ili kuwafanya wampende. Mtume alikuwa akisema "Kumpenda Ali ni (dalili ya) imani na kumchukia (ni dalili ya) unafiki"[68] Na pia husema "Ali anatokana nami, nami natokana na Ali."[69] Na alikuwa akisema: "Ali ni mtawala wa kila muumini baada yangu"[70] na husema kuwa, "Ali ni mlango wa mji wa elimu yangu na ni baba wa wanangu."[71] Pia Mtume alikuwa akisema, "Ali ni Bwana wa Waislamu na ni Imamu wa wachamungu na ni kiongozi wa waumini wenye kutowa mwanga na nuru."[72]

Lakini inasikitisha kwamba yote hayo hayakuwazidishia isipokuwa chuki na husuda na kwa ajili hiyo Mtume alimuita Ali kabla ya kufariki akamkumbatia kisha akalia na akamwambia: "Ewe Ali bila shaka mimi nafahamu kwamba ndani ya nyoyo za jamaa hawa kuna shinikizo la chuki dhidi yako, na hapo baadaye watakudhihirishia baada yangu mimi, iwapo watakupa baia kubali vinginevyo basi subiri mpaka hapo utapokutana nami hali ya kuwa mwenye kudhulumiwa". Taz: Ar-Riyadun-Naz-Rah Fi Manaqibil-Asharah cha Tabari Babu Fadail Ali ibn Abi Talib. Basi ikiwa Abul-Hasan (a.s.) ilimlazimu kuvumilia baada ya baia ya Abubakr, hilo ni kutokana na usia wa Mtume kwake yeye na ndani ya hilo muna hekima ambayo iko wazi.

Tano: Zaidi ya yote hayo yaliyotangulia ni kwamba, Muislamu ataposoma Qur'an Tukufu na kuzizingatia aya zake, atafahamu kwa kupitia masimulizi yake kuhusu mambo ambayo yaliwafika watu na mataifa yaliyopita kwamba, kwao yalitokea mengi kuliko yale yaliyotokea kwetu sisi. Basi mwangalie huyu Qabil anamuuwa nduguye Habil kwa dhulma na uadui tu, na huyu hapa Nuh ambaye ni babu wa Manabii, baada ya miaka elfu moja ya jihadi hakuna aliyemfuata katika watu wake isipokuwa wachache tu, isitoshe mkewe na mwanawe walikuwa miongoni mwa makafiri.

Mtazame Nabii Lut haikupatikana katika kitongoji chake isipokuwa nyumba moja tu ya Waumini. Nao Mafirauni ambao walikuwa wenye kiburi katika nchi wakawafanya watu kuwa watumwa, hapakuwepo miongoni mwao isipokuwa Muumini mmoja anayeficha imani yake. Hawa hapa nduguze Yusuf watoto wa Yaaqub nao ni kikundi, wanakula njama kumuuwa ndugu yao mdogo asiye na kosa lolote lakini (wanafanya hivyo) kwa kumhusudu kwa kuwa yeye ni kipenzi kwa baba yao. Watazame wana wa Israel ambao Mwenyezi Mungu aliwaokoa kupitia kwa Musa na akawapasulia bahari na kumuangamiza adui yao Firauni na askari wake bila ya kuwakalifisha taabu yoyote ya vita, basi mara walipotoka baharini na nyayo zao hata hazijakauka, wakawafikia watu wanaoabudia sanamu (wana wa Israel) wakasema:

"Ewe Musa tutengenezee Mungu kama wao walivyo na Miungu, Musa akawaambia hakika ninyi ni watu msiojua." Na alipokwenda kwenye ahadi ya Mola wake na kumuacha nduguye Harun, walifanya njama dhidi yake karibu wamuuwe, wakamkufuru Mwenyezi Mungu, na wakamuabudia ndama kisha baadaye waliwauwa Manabii wa Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu anasema: "Kila walipokufikieni Mitume kwa yale ambayo nafsi zenu haziyapendi mlijivuna, kundi moja mlilipinga na kundi jingine mkaliua".(Qur'an, 2:87)

Huyu hapa naye Bwana wetu Yahya bin Zakariya naye ni Nabii na Mtawa miongoni mwa watu wema anauwawa na kichwa chake anazawadiwa mtu muovu miongoni mwa waovu wa Kibani Israel. Mayahudi na Wakristo nao walikula njama kumuua na kumsulubu bwana wetu Isa. Nao ummati wa Muhammad wanaandaa jeshi la kiasi ya watu elfu thelathini ili kumuuwa kipenzi cha Mtume wa Mwenyezi Mungu na Bwana wa vijana wa peponi ambaye hawakuwa pamoja naye isipokuwa watu Sabini miongoni mwa wafuasi wake, wakawauwa wote ikiwa ni pamoja na mwanawe mchanga. La ajabu ni lipi baada ya yote haya? Lipi litashangaza baada ya kauli ya Mtume kuwaambia Masahaba wake yakuwa: "Mutafuata nyendo za wale waliokuwa kabla yenu shubiri baada ya shubiri na dhiraa baada ya dhiraa mpaka hata wakiingia kwenye shimo la kenge nanyi mutaingia". wakasema, "Wadhani kuwa hao ni Mayahudi na Wakristo"? Mtume akasema, "Ni kina nani basi (kama si hao)"?

Taz: Sahih BukharJuz. 4 uk. 144 na Juz. 8 uk. 151. Ni kipi cha ajabu basi, nasi twasoma ndani ya Bukhar na Muslim kauli ya Mtume (s.a.w.) isemayo: "Siku ya Kiyama Masahaba wangu watapelekwa upande wa kushoto nami nitasema wanapelekwa wapi? Patasemwa Wallahi Motoni, nitasema, Ewe Mola wangu Masahaba wangu hao, patasemwa, Hakika wewe hujuwi waliyoyazusha baada yako, nitasema atengwe mbali aliyebadilisha baada yangu, na sitamuona anaokoka miongoni mwao isipokuwa kikundi kidogo kama cha ngamia waliotelekezwa".

Tax: Sahih Bukhar Juz. 7 uk. 209 na Sahih Muslim Babul-Haudh. Basi lipi la ajabu baada ya kauli yake Mtume (s.a.w.) aliposema: "Umati wangu utagawanyika makundi sabini na tatu na yote yataingia motoni isipokuwa kundi moja". Taz: Sunan Ibn Majah Kitabul-Fitan Juz. 2 hadith Na. 3993, Ahmad Juz. 3 uk. 120, Sunan Tirmidhi Kitabul-Iman. Amesema kweli Mwenyezi Mungu Mtukufu Mola mwenye nguvu na Utukufu, mjuzi wa undani wa nyoyo pale aliposema: "Na watu wengi hawataamini japo utapupia" (Qur'an, 12:103)

"Bali amewajia na ukweli na wengi wao wanaichukia kweli" (Qur'an,23:70)

"Bila shaka tumekujieni na ukweli lakini wengi wenu hawaupendi ukweli" (Qur'an 43:78)

"Fahamuni ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni ya kweli lakini wengi wao hawafahamu" (Qur'an, 10:55)

"Wanakuridhisheni kwa vinywa vyao na nyoyo zao zinakataa, na wengi wao ni mafasiki (Qur'an, 9:8)

"Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mwenye fadhila juu ya watu, lakini watu wengi hawashukuru" (Qur'an, 10:60)

"Wanaitambua Neema ya Mwenyezi Mungu kisha wanaipinga na wengi wanakataa ila kukufuru tu" (Qur'an, 25:50)

"Na wengi wao hawawezi kumuamini Mwenyezi Mungu ila hali ya kuwa wanamshirikisha" (Qur'an, 12:106)

"Bali wengi wao hawaijuwi haki basi wao wanapinga" (Qur'an, 21:24)

"Hivi mwashangazwa na mazungumzo haya na mnacheka wala hamlii hali ya kuwa ninyi mmeghafilika (mmejisahau)" (Qur'an, 53:61


3

4

5

6

7

8

9

10

11

12

13

14

15

16