TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Juzuu 23

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 26545
Pakua: 2657


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 30 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 26545 / Pakua: 2657
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU Juzuu 23

Mwandishi:
Swahili

3

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

وَاذْكُرْ أَخَا عَادٍ إِذْ أَنذَرَ قَوْمَهُ بِالْأَحْقَافِ وَقَدْ خَلَتِ النُّذُرُ مِن بَيْنِ يَدَيْهِ وَمِنْ خَلْفِهِ أَلَّا تَعْبُدُوا إِلَّا اللَّـهَ إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿٢١﴾

21. Na mtaje ndugu wa kina A’di, alipowaonya watu wake kwenye vilima vya mchanga. Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake: kuwa msimwabudu isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ninawahofia na adhabu ya siku iliyo kuu.

قَالُوا أَجِئْتَنَا لِتَأْفِكَنَا عَنْ آلِهَتِنَا فَأْتِنَا بِمَا تَعِدُنَا إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿٢٢﴾

22. Wakasema: Je, umetujia ili ututenge mbali na miungu yetu? Basi tuletee hayo unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

قَالَ إِنَّمَا الْعِلْمُ عِندَ اللَّـهِ وَأُبَلِّغُكُم مَّا أُرْسِلْتُ بِهِ وَلَـٰكِنِّي أَرَاكُمْ قَوْمًا تَجْهَلُونَ ﴿٢٣﴾

23. Akasema: Hakika ujuzi uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Mimi ninawafikishia niliyotumwa, lakini ninawaona kuwa nyinyi ni watu mnaofanya ujinga.

فَلَمَّا رَأَوْهُ عَارِضًا مُّسْتَقْبِلَ أَوْدِيَتِهِمْ قَالُوا هَـٰذَا عَارِضٌ مُّمْطِرُنَا بَلْ هُوَ مَا اسْتَعْجَلْتُم بِهِ رِيحٌ فِيهَا عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٢٤﴾

24. Basi walipoliona wingu likielekea kwenye mabonde yao, walisema: Wingu hili ni la kutunyeshea mvua! Kumbe, haya ni hayo mliyoyahimiza, ni upepo ndani yake imo adhabu chungu!

تُدَمِّرُ كُلَّ شَيْءٍ بِأَمْرِ رَبِّهَا فَأَصْبَحُوا لَا يُرَىٰ إِلَّا مَسَاكِنُهُمْ كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْقَوْمَ الْمُجْرِمِينَ ﴿٢٥﴾

25. Unaangamiza kila kitu kwa amri ya Mola wake. Wakawa hawaonekani ila nyumba zao tu. Hivyo ndivyo tunavyowalipa watu wakosefu.

وَلَقَدْ مَكَّنَّاهُمْ فِيمَا إِن مَّكَّنَّاكُمْ فِيهِ وَجَعَلْنَا لَهُمْ سَمْعًا وَأَبْصَارًا وَأَفْئِدَةً فَمَا أَغْنَىٰ عَنْهُمْ سَمْعُهُمْ وَلَا أَبْصَارُهُمْ وَلَا أَفْئِدَتُهُم مِّن شَيْءٍ إِذْ كَانُوا يَجْحَدُونَ بِآيَاتِ اللَّـهِ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُوا بِهِ يَسْتَهْزِئُونَ ﴿٢٦﴾

26. Na hakika tuliwamakinisha, sio kama tulivyowamakinisha nyinyi, Na tuliwapa masikio, na macho, na nyoyo; na hayakuwafaa kitu masikio yao, wala macho yao, wala nyoyo zao, Kwani hao walikuwa wakizikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, na yakawazunguka yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.

وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا مَا حَوْلَكُم مِّنَ الْقُرَىٰ وَصَرَّفْنَا الْآيَاتِ لَعَلَّهُمْ يَرْجِعُونَ ﴿٢٧﴾

27. Na hakika tuliiangamiza miji ilio jirani zenu, na tuliziainisha Ishara ili wapate kurejea.

فَلَوْلَا نَصَرَهُمُ الَّذِينَ اتَّخَذُوا مِن دُونِ اللَّـهِ قُرْبَانًا آلِهَةً بَلْ ضَلُّوا عَنْهُمْ وَذَٰلِكَ إِفْكُهُمْ وَمَا كَانُوا يَفْتَرُونَ ﴿٢٨﴾

28. Basi mbona wale waliowashika badala ya Mwenyezi Mungu, kuwa wawakurubishe, hawakuwanusuru? Bali waliwapotea! Na hivyo ndio uwongo wao na waliyokuwa wakiyazua.

HUD

Aya 21 -28

MAANA

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amekitaja kisa cha Hud, katika Juz. 8 (7:65-72), Juz. 12 (11:50 -60), Juz. 19 (26: 123-140) na katika Juzuu nyinginezo zilizopita na zitakazofuatia. Kwa hiyo hapa tutaja kwa ufupi tu, kwa kutegemea yaliyokwishapita.

Na mtaje ndugu wa kina A’di, alipowaonya watu wake kwenye vilima vya mchanga.

Ewe Muhammad! Watajie watu wako kisa cha Hud na watu wake, ili wapate mawaidha na mazingatio. Walikuwa ni waarabu kama watu wako, walikuwa na nguvu zaidi na mali, na nyumba zao zilikuwa karibu na mji wako, kwa vile waliishi kwenye vichuguu vya mchanga – sehemu ya Yemen iliyoshikana na Hijaz; kama ilivyosemekana.

Na kwa yakini waonyaji wengi walitokea kabla yake na baada yake.

Makusudio ya waonyaji ni mitume. Maana ni kuwa waambie ewe Muhammad, kuwa vile vile Hud hakuwa Mtume wa mwanzo wala wa mwisho, bali Mwenyezi Mungu alituma mitume wengi kabla ya Hud na baada yake. Na alikuwa akiwaonya watu wake kwa maneno yale yale ya kila Nabii:

Kuwa msimwabudu isipokuwa Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ninawahofia na adhabu ya siku iliyo kuu, ikiwa mtabakia na upotevu na shirki mliyo nayo.

Wakasema: Je, umetujia ili ututenge mbali na miungu yetu? Basi tuletee hayo unayotuahidi ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli.

Yaani wewe Hud unataka tuache kuabudu masanamu na tuabudu Mungu mmoja, si ni jambo la ajabu hili! Tena unatuhofisha na adhabu, si utuletee haraka basi ikiwa vitisho vyako ni vya kweli?

Akasema: Hakika ujuzi uko kwa Mwenyezi Mungu tu. Mimi ninawafikishia niliyotumwa, lakini ninawaona kuwa nyinyi ni watu mnaofanya ujinga.

Mola wangu ameniamarisha niwaonye na adhabu, basi nikatii amri, nikawaonya. Ama kuwa lini itatokea adhabu hiyo, ni ya aina gani au ikoje, anaiujua Mwenyezi Mungu tu, mimi sijui lolote katika hayo. Isipokuwa nina uhakika kabisa kuwa nyinyi ni watu mliozama kwenye ujinga na upotevu.

Basi walipoliona wingu likielekea kwenye mabonde yao, walisema: Wingu hili ni la kutunyeshea mvua!

Waliidhania adhabu kuwa ni mawingu, wakafurahi kuwa watanyeshewa mvua, Kwa hiyo wakabashiriana kupata rutuba na mavuno.

Basi Hud akawaambia au hali halisi ikaonyesha:

Kumbe, haya ni hayo mliyoyahimiza, ni upepo ndani yake imo adhabu chungu! Unaangamiza kila kitu kwa amri ya Mola wake.

Wakaona mawingu angani ambayo dhahiri yake ni rehema na undani wake ni adhabu, wakadanganyika na dhahiri na wakaghafilika na yanayojificha yanayokuja ghafla. Basi adhabu ikawanyakua wakiwa wamelewa amani na matamanio. Huu ndio mwisho wa mwenye kuyatii matamanio yake.

Wakawa hawaonekani ila nyumba zao tu amabazo zimekuwa ni makaburi ya miili yao. Mwenye akili ni yule anayepata mawaidha na mfano wa watu hawa, akahofia mashiko ya Mwenyezi Mungu wakati wa nema na raha na akatarajia rehema yake wakati wa shida na karaha.

Hivyo ndivyo tunavyowalipa watu wakosefu duniani na Akhera au Akhera peke yake kulingana na inavyotaka hikima yake.

Na hakika tuliwamakinisha, sio kama tulivyowamakinisha nyinyi.

Tuliwaangamiza akina A’d walipoasi na kupetuka mipaka, na tulikuwa tumewapa nguvu na mali kwa namna ambayo hatukuwapa nyinyi mfano wake enyi vigogo wa kikuraishi. Hivi hamuogopi kuwapata yaliyowapata A’d na wengineo katika uma zilizopita?

Na tuliwapa masikio, na macho, na nyoyo; kama tulivyowapa nyinyi,na hayakuwafaa kitu masikio yao, wala macho yao, wala nyoyo zao, kwa sababu hawakunufaika nayo, bali walikuwa kama wendawazimu, viziwi, mabubu na vipofu kwenye ukumbusho na hadhari.

Basi enyi watu wa Makka msighurike na masikio, macho na akili zenu. Kwani yote hayo hayawatafaa kitu itakaposhuka adhabu.

Kwani hao walikuwa wakizikataa Ishara za Mwenyezi Mungu, na yakawazunguka yale waliyokuwa wakiyafanyia stihizai.

Waliipinga haki pamoja na dalili zake na wakaidharau na watu wake. Wakaingia kwenye uovu na upotevu; malipo yao yakawa ni maangamizi na kuvunjika.

Na hakika tuliiangamiza miji ilio jirani zenu, na tuliziainisha Ishara ili wapate kurejea.

Maneno yanaelekezwa kwa washirikina wa Makka. Makusudio ya miji ni watu wa miji hiyo ambao ni akina A’d na Thamud na wanaopakana nao.

Kuzianisha Ishara ni kuwabainishia aina za dalili na mawaidha, na walihadharishwa kwa kauli na vitendo ili wawaidhike na wakome, lakini wakakataa isipokuwa ukafiri, basi ikawathibitikia adhabu na wakabomolewa kabisa.

Basi mbona wale waliowashika badala ya Mwenyezi Mungu, kuwa wawakurubishe, kwa Mwenyezi Mungu,hawakuwanusuru? Bali waliwapotea! Na hivyo ndio uwongo wao na waliyokuwa wakiyazua.

‘Hivyo’ ni hivyo kutookoa masanamu na kwamba hayamsaidii aliyekuwa akiyaabudu wakati wa dhiki. Maana ni kuwa kauli ya washirikina kuwa sanamu ni muombezi wetu mbele ya Mwenyezi Mungu na muokozi wetu, ni uzushi.

وَإِذْ صَرَفْنَا إِلَيْكَ نَفَرًا مِّنَ الْجِنِّ يَسْتَمِعُونَ الْقُرْآنَ فَلَمَّا حَضَرُوهُ قَالُوا أَنصِتُوا فَلَمَّا قُضِيَ وَلَّوْا إِلَىٰ قَوْمِهِم مُّنذِرِينَ ﴿٢٩﴾

29. Na tulipokuletea kundi la majini kusikiliza Qur'an. Basi walipoihudhuria walisema: Nyamazeni! Na ilipomalizwa, walirudi kwa kaumu yao kwenda kuwaonya.

قَالُوا يَا قَوْمَنَا إِنَّا سَمِعْنَا كِتَابًا أُنزِلَ مِن بَعْدِ مُوسَىٰ مُصَدِّقًا لِّمَا بَيْنَ يَدَيْهِ يَهْدِي إِلَى الْحَقِّ وَإِلَىٰ طَرِيقٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿٣٠﴾

30. Wakasema: Enyi kaumu yetu! Sisi tumesikia Kitabu kilichoteremshwa baada ya Musa, kinachosadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinachoongoza kwenye Haki na kwenye Njia iliyonyooka.

يَا قَوْمَنَا أَجِيبُوا دَاعِيَ اللَّـهِ وَآمِنُوا بِهِ يَغْفِرْ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمْ وَيُجِرْكُم مِّنْ عَذَابٍ أَلِيمٍ ﴿٣١﴾

31. Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mwenye kuitia kwa Mwenyezi Mungu, na mumwamini, Mwenyezi Mungu atawasamehe, na atawakinga na adhabu chungu.

وَمَن لَّا يُجِبْ دَاعِيَ اللَّـهِ فَلَيْسَ بِمُعْجِزٍ فِي الْأَرْضِ وَلَيْسَ لَهُ مِن دُونِهِ أَوْلِيَاءُ أُولَـٰئِكَ فِي ضَلَالٍ مُّبِينٍ ﴿٣٢﴾

32. Na asiyemwitikia mwitaji wa Mwenyezi Mungu basi hatashinda katika ardhi, wala hatakuwa na walinzi mbele yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhahiri.

MAJINI WANASIKILZA QUR’AN

Aya 29 – 32

MAANA

Na tulipokuletea kundi la majini kusikiliza Qur’an. Basi walipoihudhuria walisema: Nyamazeni! Na ilipomalizwa, walirudi kwa kaumu yao kwenda kuwaonya.

Miongoni mwa wadhifa wa akili ni kuhukumu uwezekeano wa kuweko kitu au kutokuweko. Ikihukumu uwezekano wa kuweko, basi inakimbilia kuthibitisha kuweko kwake kwa kutumia nyenzo, zinazoafikiana na maumbile ya kitu kinachotakiwa kuthibitishwa, kwa hisia na majaribio.

Kikiwa ni katika mambo ya kiakili, basi njia yake itakuwa ni akili. Na kikiwa ni katika mamabo ya ghaibu –sio kuweko Mungu – basi njia yake itakuwa ni wahyi tu. Ukielezea basi itakuwa ni lazima kukubaliana nao.

Hakuna mwenye shaka kwamba akili haikatai kuweko viumbe vilivyo mbali nasi na vinavyotofautiana na tunayoyajua na tuliyoyazoea. Bali tuna uhakika kuwa tusiyoyajua ni mengi zaidi kuliko tunayoyajua; miongoni mwa hayo ni majini. Mwenyezi Mungu (s.w.t) ameyataja katika Aya kadhaa; kama vile:

وَأَنَّا مِنَّا الصَّالِحُونَ وَمِنَّا دُونَ ذَٰلِكَ ﴿١١﴾

“Na hakika katika sisi wako wema na wengine katika sisi ni kinyume na hayo.” (72:11).

Mwenyezi Mungu alipeleka kundi katika hao wema kwa Mtume Mtukufu(s.a.w. w ) , wakamsikia akisoma Qur’an, wakaanza kuambiana: ‘Hebu nyamazeni na mzingatie maana yake.’ Basi wakanyamaza na kusikiliza kwa makini. Wakaona uongofu na nuru, wakamwamini Muhammad(s.a.w. w ) . Mtume alipomaliza kusoma walirudi haraka kwa watu wao kuwaonya na kuwapa bishara ya Uislamu.

Wakasema: Enyi kaumu yetu! Sisi tumesikia Kitabu kilichoteremshwa baada ya Musa, kinachosadikisha yaliyo kuwa kabla yake, na kinachoongoza kwenye Haki na kwenye Njia iliyonyooka

Waliwaambia watu wao kuwa tumesikia Kitabu kutoka kwa Muhammad(s.a.w. w ) kinachofanana na kile alichoteremshiwa Musa, nacho kinasadikisha yale waliyokuja nayo manabii, ya kuamini tawhid na ufufuo. Vile vile kinaongoza kwenye usawa na kufanya heri:

فَقَالُوا إِنَّا سَمِعْنَا قُرْآنًا عَجَبًا ﴿١﴾ يَهْدِي إِلَى الرُّشْدِ فَآمَنَّا بِهِ وَلَن نُّشْرِكَ بِرَبِّنَا أَحَدًا ﴿٢﴾

“Wakasema: hakika tumesikia Qur’an ya ajabu. Inaongoza kwenye uwongofu kwa hiyo tumeiamini na hatutamshirikisha yeyote na Mola wetu.” (72:1-2).

Ikiwa sisi hatujawaona majini walioathirika na Qur’an na kuiamini, lakini tumewaona wataalamau na watu wenye akili wengi wakiathirika na matamshi ya Qur’an kwa kiasi cha kusikia matamshi yake tu; tena wakaamini imani isiyokuwa na shaka kuwa inatoka kwa Mwenye hekima Mjuzi.

Enyi kaumu yetu! Muitikieni Mwenye kuitia kwa Mwenyezi Mungu, na mumwamini, Mwenyezi Mungu atawasamehe, na atawakinga na adhabu chungu.

Itikieni mwito wa haki na mumfuate anayeutoa mwito huo; Mwenyezi Mungu atawasamehe dhambi zenu na atawaingiza katika rehema yake na kuwaokoa na ghadhabu yake na adhabu yake.

Na asiyemwitikia mwitaji wa Mwenyezi Mungu basi hatashinda katika ardhi, wala hatakuwa na walinzi mbele yake. Hao wamo katika upotovu ulio dhahiri.

Hakuna kumkimbia Mwenyezi Mungu isipokuwa kwake tu wala hakuna kuokoka na adhabu yake isipokuwa kwa ikhlasi na matendo mema.

Hao wamo katika upotevu ulio dhahiri.

‘Hao’ ni hao wasioitikia mwito wa Mwenyezi Mungu, na asiyemwitikia atakuwa ameiacha njia ya haki na uongofu.

أَوَلَمْ يَرَوْا أَنَّ اللَّـهَ الَّذِي خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَلَمْ يَعْيَ بِخَلْقِهِنَّ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ بَلَىٰ إِنَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿٣٣﴾

33. Je, hawaoni ya kwamba Mwenyezi Mungu, aliyeziumba mbingu na ardhi, na hakuchoka kwa kuziumba, kuwa ni Muweza wa kuwafufua wafu? Kwa nini? Hakika Yeye ni Muweza wa kila kitu.

وَيَوْمَ يُعْرَضُ الَّذِينَ كَفَرُوا عَلَى النَّارِ أَلَيْسَ هَـٰذَا بِالْحَقِّ قَالُوا بَلَىٰ وَرَبِّنَا قَالَ فَذُوقُوا الْعَذَابَ بِمَا كُنتُمْ تَكْفُرُونَ ﴿٣٤﴾

34. Na siku makafiri watakapoonyeshwa Moto, Je, haya si kweli? Watasema: Kwani? Tunaapa kwa Mola wetu! Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya mliyokuwa mkikataa.

فَاصْبِرْ كَمَا صَبَرَ أُولُو الْعَزْمِ مِنَ الرُّسُلِ وَلَا تَسْتَعْجِل لَّهُمْ كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَ مَا يُوعَدُونَ لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا سَاعَةً مِّن نَّهَارٍ بَلَاغٌ فَهَلْ يُهْلَكُ إِلَّا الْقَوْمُ الْفَاسِقُونَ ﴿٣٥﴾

35. Basi subiri, kama walivyosubiri Mitume wenye azma, Wala usiwahimizie. Siku watakayoyaona waliyoahidiwa, itakuwa kama kwamba hawakukaa ila saa moja ya mchana. Huu ndio ufikisho! Kwani huangamizwa isipokuwa walio watu mafasiki?

JE, HAYA SI KWELI?

Aya 33 – 35

MAANA

Je, hawaoni ya kwamba Mwenyezi Mungu, aliyeziumba mbingu na ardhi, na hakuchoka kwa kuziumba, kuwa ni Muweza wa kuwafufua wafu? Kwa nini? Hakika Yeye ni Muweza wa kila kitu.

Ulimwengu huu wa ajabu unajulisha uweza wa muumba na ukuu wake. Vile vile unajulisha, tena kwa njia bora, kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu ana uwezo wa kuwafufa wafu. Kwa vile sabu inayoleta mambo hayo mawili ni moja, ambayo ni uweza wa mwenye kukiambia kitu ‘kuwa’ na kikawa. Imam Ali(a . s) anasema:“Namshangaa anayekanusha ufufuo wa pili na hali anaona ufufuo wa kwanza!”

Maana ya Aya hii yametangulia katika makumi ya Aya na yatakuja mengine mengi; miongoni mwayo ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Je, tulichoka kwa umbo la kwanza?” (50:15). Basi tutachoka vipi na umbo la pili?

Na siku makafiri watakapoonyeshwa Moto, yaani watakapoadhibiwa na kuaambiwa:Je, haya, mliyokuwa mkiyakanusha hapo mwanzo,si kweli? Watasema: Kwani? Tunaapa kwa Mola wetu! ni kweli.

Walikanusha duniani ambapo kunawadhuru kukana na wamekubali Akhera ambapo hakuwanufaishi chochote kukiri kwao.

Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu mlikuwa mkikataa; bali mliwadharau wale walioamini hisabu ya Mwenyezi Mungu na adhabu yake. Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:Na ungeliona watakaposimamishwa mbele ya Mola wao, Akasema: Je, si kweli haya? Watasema: Kwa nini? Tunaapa kwa Mola wetu. Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyakataa.” Juz. 7 (6:30).

Basi subiri, kama walivyosubiri Mitume wenye azma,

Kwenye tafsiri nyingi imeelezwa kuwa mitume wenye azma (Ululu-azm) ni watano: Nuh, Ibrahim, Musa, Isa na Muhammad. Kila mmoja wao alikuwa na sharia mahususi aliyoiwajibisha Mwenyezi Mungu kutumiwa na viumbe wote wakati wake mpaka afike mtume mwingine kati ya hao watano.

Akija anafuta sharia ya yule aliyemtangulia katika wale watano, mpaka kufikia sharia ya Muhammad(s.a.w. w ) , Bwana wa mitume na mwisho wa manabii. Hiyo haiwezi kufutwa hadi siku ya kiyama. Ama manabii wengine wasiokuwa hao ululu-azm, walikuwa wakitumia sharia ya waliyemtangulia katika hao watano.

Kuna riwaya za Ahlul-bayt zinazozungumzia hili na kuashirwa na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

شَرَعَ لَكُم مِّنَ الدِّينِ مَا وَصَّىٰ بِهِ نُوحًا وَالَّذِي أَوْحَيْنَا إِلَيْكَ وَمَا وَصَّيْنَا بِهِ إِبْرَاهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَى ﴿١٣﴾

“Amewapa sharia ya Dini aliyomuusia Nuhu na tuliyokupa wahyi wewe, na tuliyowausia Ibrahim na Musa na Isa,” Juz. 25 (42:13).

Ambapo amewahusu kuwataja hao watano na kutaja neno sharia. Na ‘wewe’ ni wewe Muhammad.

Wala usiwahimizie adhabu. Siku watakayoyaona waliyoahidiwa itakuwa kama kwamba hawakukaa ulimwenguni ila saa moja ya mchana.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w. w ) , na wanaoambiwa ni wale walioikanusha risala yake. Makusudio ya yale mliyoahidiwa ni adhabu ya Jahannam. Maana ni kuwa usifanye haraka ewe Muhammad(s.a.w. w ) ya kutaka wale waliokufuru waadhibiwe, kwa sababu itawapata tu huko Akhera. Huku kukaa kwao duniani hata kukirefuka, lakini watapoiona adhabu wataona kama kwamba ni kitambo kidogo tu.

Mfano wa Aya hii ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

مَتَاعٌ قَلِيلٌ ثُمَّ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَبِئْسَ الْمِهَادُ ﴿١٩٧﴾

“Ni starehe ndogo. Kisha makazi yao ni Jahannam ni mahali pabaya pa kushukia.”

Juz. 4 (3:197).

Imam Ali(a . s) anasema:“Hakika dunia ni starehe za siku kidogo, zinaondoka kama yanavyoondoka mangati au kama yanavyopotea mawingu.”

Huu ndio ufikisho!

Yaani Qur’an ni ufikisho wa risala za Mwenyezi Mungu Mtukufu, nayo ni hoja tosha ya mawaidha yake na ni ponyo kwa anayetaka mwongozo na uongofu.

Kwani huangamizwa wengine isipokuwa walio watu mafasiki?

Hapana!

إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ ﴿٥١﴾ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿٥٢﴾

“Hakika wenye takua watakuwa katika mahali pa amani. Katika mabustani na chemchem.”

Juz. (44:51-52).

MWISHO WA SURA YA ARUBAINI NA SITA: SURAT AL-AHQAF

4

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA TATU

Sura Ya Arubaini Na Saba: Surat Muhammad. Ina Aya 38. Aya zote au nyingi zimeshuka Madina.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

الَّذِينَ كَفَرُوا وَصَدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ أَضَلَّ أَعْمَالَهُمْ ﴿١﴾

1. Wale waliokufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu, Yeye atavipotoa vitendo vyao.

وَالَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَآمَنُوا بِمَا نُزِّلَ عَلَىٰ مُحَمَّدٍ وَهُوَ الْحَقُّ مِن رَّبِّهِمْ كَفَّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ وَأَصْلَحَ بَالَهُمْ ﴿٢﴾

2. Na wale walioamini, na wakatenda mema, na wakaamini aliyoteremshiwa Muhammad - nayo ni Haki iliyotoka kwa Mola wao - atawafutia maovu yao na ataitengeneza hali yao.

ذَٰلِكَ بِأَنَّ الَّذِينَ كَفَرُوا اتَّبَعُوا الْبَاطِلَ وَأَنَّ الَّذِينَ آمَنُوا اتَّبَعُوا الْحَقَّ مِن رَّبِّهِمْ كَذَٰلِكَ يَضْرِبُ اللَّـهُ لِلنَّاسِ أَمْثَالَهُمْ ﴿٣﴾

3. Hayo ni kwa sababu wale waliokufuru wamefuata upotovu, na walioamini wamefuata Haki iliyotoka kwa Mola wao. Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowapigia watu mifano yao.

فَإِذَا لَقِيتُمُ الَّذِينَ كَفَرُوا فَضَرْبَ الرِّقَابِ حَتَّىٰ إِذَا أَثْخَنتُمُوهُمْ فَشُدُّوا الْوَثَاقَ فَإِمَّا مَنًّا بَعْدُ وَإِمَّا فِدَاءً حَتَّىٰ تَضَعَ الْحَرْبُ أَوْزَارَهَا ذَٰلِكَ وَلَوْ يَشَاءُ اللَّـهُ لَانتَصَرَ مِنْهُمْ وَلَـٰكِن لِّيَبْلُوَ بَعْضَكُم بِبَعْضٍ وَالَّذِينَ قُتِلُوا فِي سَبِيلِ اللَّـهِ فَلَن يُضِلَّ أَعْمَالَهُمْ ﴿٤﴾

4. Basi mnapokutana na waliokufuru wapigeni shingo, mpaka mkiwadhoofisha wafungeni pingu. Tena waachilieni kwa hisani au wajikomboe, mpaka vita vitue mizigo yake. Ndio hivyo. Na lau angelitaka Mwenyezi Mungu angeliwashinda mwenyewe, lakini haya ni kwa sababu awatie katika mitihani nyinyi kwa nyinyi. Na waliouliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu hatazipoteza amali zao.

سَيَهْدِيهِمْ وَيُصْلِحُ بَالَهُمْ ﴿٥﴾

5. Atawaongoza na awatengezee hali yao.

وَيُدْخِلُهُمُ الْجَنَّةَ عَرَّفَهَا لَهُمْ ﴿٦﴾

6. Na atawaingiza katika Pepo aliyowajulisha.

AMININI TULIYOMTEREMSHIA MUHAMMAD

Aya 1 – 6

MAANAA

Wale waliokufuru na wakazuilia njia ya Mwenyezi Mungu, Yeye atavipotoa vitendo vyao.

Neno ‘kuzuilia’ tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu ‘swaddu’ lenye maana ya kupinga na pia lina maana ya kuzuuilia. Likifasiriwa kwa maana ya kwanza, itakuwa kukufuru na kupinga ni kwa maana moja na uungan- ishi utakuwa ni wa kitafsiri. Ikiwa litafasiriwa ‘kuzuiliwa’ maana yake itakuwa wao hawakuamini na pia wamewazuia watu wengine wasiamini. Hii ndio dhahiri inayofahamishwa na Aya.‘Kuvipotoa vitendo vyao,’ ni kuvibatilisha; kama kwamba havikuwaokoa.

Maana ni kuwa mwenye kuupinga Uislamu na akawazuia watu wengine wasiuamini, Mwenyezi Mungu hatamkubalia chochote. Kwa sababu Uislamu ni sharti la msingi la thawabu za Akhera. Mwenyezi Mungu Mtukufu anasema:

وَمَا مَنَعَهُمْ أَن تُقْبَلَ مِنْهُمْ نَفَقَاتُهُمْ إِلَّا أَنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّـهِ وَبِرَسُولِهِ ﴿٥٤﴾

“Na hawakuzuiliwa kukubaliwa michango yao, ila ni kwamba wao wamemkufuru Mwenyezi Mungu na Mtume wake.” Juz. 10 (9:54).

Na wale walioamini, na wakatenda mema, na wakaamini aliyoteremshiwa Muhammad - nayo ni Haki iliyotoka kwa Mola wao - atawafutia maovu yao na ataitengeneza hali yao.

Neno hali hapa tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu ‘bal’ ambalo pia lina maana ya moyo.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusema kuwa hatawakubalia makafiri, sasa anasema kuwa mwenye kufanya amali njema akiwa anamwamini Mwenyezi Mungu na Qur’an isiyo na shaka, atamkubalia na atamsamehe dhambi zake akitubia na pia atamtengenezea vizuri mambo yake duniani kwa tawfiki na heri na Akhera atamtia Peponi.

Hayo ni kwa sababu wale waliokufuru wamefuata upotovu, na walioamini wamefuata Haki iliyotoka kwa Mola wao.

‘Hayo’ ni hayo ya thawabu za watenda mema na adhabu ya watenda uovu. Maana ni kuwa haki ina wenyewe na batili ina wenyewe. Na Mwenyezi Mungu (s.w.t) atamlipa kila mmoja stahiki yake, hakika yeye ana habari ya wanayoyafanya.

Hivyo ndivyo Mwenyezi Mungu anavyowapigia watu mifano yao akibainisha thawabu za mtenda mema na mfano wa watenda mema wenzake, ili awe na yakini ya wema wake na uongofu wake na kumbainishia muovu mfano wa adhabu ya waovu wenzake, ili aweze kujikanya na kuongoka.

Basi mnapokutana na waliokufuru wapigeni shingo mpaka mkiwadhoofisha wafungeni pingu. Tena waachilieni kwa hisani au wajikomboe, mpaka vita vitue mizigo yake.

Aya hii ni miongoni mwa mama wa Aya na katika Aya zilizo wazi wazi na maudhui yake ya vita ni muhimu. Kwa hiyo kwanza tutafsiri misamiati yake kisha tubainishe maana yanayopatikana:

Makusudio ya kukutana ni kupamabana na maadui wa Uislamu katika vita. Kupiga shingo ni kinaya cha kuua; iwe ni kwa kukata shingo au vinginevyo. Mwenyezi Mungu amehusisha kutaja shingo kwa vile ni katika viungo muhimu. Kuwadhoofisha ni kuwaua sana na kuwakamata.

Kufunga pingu ni kuwafunga imara au kutia jela ili wasikimbie wakawarudishia mpira nyinyi. Kuwachilia kwa hisani ni kuwaachilia kwa fidia au bila ya kutoa fidia. Kutua vita mizio yake ni adui kusalimu amri na kutupa silaha. Kwa sababu mizigo ya vita ni silaha.

Maana ya Aya kwa ujumla ni maadui wa dini waking’ang’ania kufuru na mkapambana nao kwa vita, basi wapigeni ili isiwashike huruma na mpambane nao kwa uimara mpaka muwakamate.

Mkishawakamata basi muwazuie barabara ili wasiwaponyoke wasije wakawageukia. Baada ya hapo mwenye hiyari atakuwa ni Mtume au naibu wake, kuwaachia mateka kwa fidia au bila fidia kulingana na masilahi yalivyo wakati huo.

Ilivyo hasa maana ya Aya hii na ile simayo:

مَا كَانَ لِنَبِيٍّ أَن يَكُونَ لَهُ أَسْرَىٰ حَتَّىٰ يُثْخِنَ فِي الْأَرْضِ ﴿٦٧﴾

“Haimfalii Nabii yoyote kuwa na mateka mpaka awe ameshinda sawasawa katika ardhi.”

Juz. 10 (8:67),

Ni moja tu; yaani hakuna mateka ila baada ya kuwashinda vitani.

Ndio hivyo. Na lau angelitaka Mwenyezi Mungu angeliwashinda mwenyewe, lakini haya ni kwa sababu awatie katika mitihani nyinyi kwa nyinyi.

‘Ndio hivyo,’ ni ishara ya aliyoyabainisha Mwenyezi Mungu – kupigana na maaduia wa Mwenyezi Mungu na kuwachukua mateka. Maana ni kuwa lau Mwenyezi Mungu angelitaka kuwatesa maadui zake katika dunia bila ya vita angeliweza kuwaangamiza kwa askari wa kutoka mbinguni, lakini Mwenyezi Mungu amewaamuru waumini kupigana jihadi na kuwajaribu kwa makafiri, ili vidhihirike vitendo vya yule mwenye kustahiki thawabu na adhabu.

Na waliouliwa katika njia ya Mwenyezi Mungu hatazipoteza amali zao.

Mwenyezi Mungu anapigana vita na mwenye kumuasi kwa kumtumia mwenye kumtii. Akiuliwa mtiifu, damu yake haiendi bure. Vipi isiwe hivyo na hali atakuwa shahidi wa njia ya Mwenyezi Mungu na kwa ajili yake? Ni nani anayemtekelezea Mwenyezi Mungu kuliko yule aliyemafanyia ikhlasi na akafanya kwa ajili yake?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amebainisha ujira wa waliofanya kwa ajili yake kwa kusema: “Hatapoteza amali zao,” bali itawarudia wao heri. Hiyo ni kwa kuwaAtawaongoza peponi kwenye mashukio yao, sawa na walivyokuwa wakiongoka kwenye nyumba zao za dunianina awatengezee hali yao, siku ile mtu atakapomkimbia ndugu yake na mama yake na wanawe.

Na atawaingiza katika Pepo aliyowajulisha mito yake, matunda yake, makasri yake, mahurilaini wake na mengineyo yanayotamaniwa na nafsi na yale yanayoburudisha macho.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِن تَنصُرُوا اللَّـهَ يَنصُرْكُمْ وَيُثَبِّتْ أَقْدَامَكُمْ ﴿٧﴾

7. Enyi mlioamini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu naye atawanusuru ataithibitisha miguu yenu.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا فَتَعْسًا لَّهُمْ وَأَضَلَّ أَعْمَالَهُمْ ﴿٨﴾

8. Na waliokufuru, basi kwao ni maangamizo, na atavipoteza vitendo vyao,

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَرِهُوا مَا أَنزَلَ اللَّـهُ فَأَحْبَطَ أَعْمَالَهُمْ ﴿٩﴾

9. Hayo ni kwa sababu waliyachukia aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, basi akaviangusha vitendo vyao.

أَفَلَمْ يَسِيرُوا فِي الْأَرْضِ فَيَنظُرُوا كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ دَمَّرَ اللَّـهُ عَلَيْهِمْ وَلِلْكَافِرِينَ أَمْثَالُهَا ﴿١٠﴾

10. Je, hawatembei katika ardhi wakaona ulikuwaje mwisho wa waliokuwa kabla yao? Mwenyezi Mungu aliwaangamiza. Na kwa makafiri hawa itakuwa mfano wa hayo.

ذَٰلِكَ بِأَنَّ اللَّـهَ مَوْلَى الَّذِينَ آمَنُوا وَأَنَّ الْكَافِرِينَ لَا مَوْلَىٰ لَهُمْ ﴿١١﴾

11. Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa walioamini. Na makafiri hawana mlinzi.

إِنَّ اللَّـهَ يُدْخِلُ الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ وَالَّذِينَ كَفَرُوا يَتَمَتَّعُونَ وَيَأْكُلُونَ كَمَا تَأْكُلُ الْأَنْعَامُ وَالنَّارُ مَثْوًى لَّهُمْ ﴿١٢﴾

12. Hakika Mwenyezi Mungu atawaingiza ambao wameamini na wakatenda mema katika Bustani zipitiwazo na mito chini yake. Na ambao wamekufuru hujifurahisha na hula kama walavyo wanyama, na Moto ndio makazi yao.

وَكَأَيِّن مِّن قَرْيَةٍ هِيَ أَشَدُّ قُوَّةً مِّن قَرْيَتِكَ الَّتِي أَخْرَجَتْكَ أَهْلَكْنَاهُمْ فَلَا نَاصِرَ لَهُمْ ﴿١٣﴾

13. Na miji mingapi iliyo kuwa na nguvu zaidi kuliko mji wako huu uliokutoa; nao tuliwateketeza na wala hawakuwa na wa kuwanusuru.

أَفَمَن كَانَ عَلَىٰ بَيِّنَةٍ مِّن رَّبِّهِ كَمَن زُيِّنَ لَهُ سُوءُ عَمَلِهِ وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُم ﴿١٤﴾

14. Je, mwenye kuwa na dalili kutoka kwa Mola wake ni kama aliyepambiwa uovu wa vitendo vyake, na wakafuata hawa zao?

MKIMNUSURU MWENYEZI MUNGU ATAWANUSURU

Aya 7 – 14

MAANA

Enyi mlioamini! Mkimnusuru Mwenyezi Mungu naye atawanusuru ataithibitisha miguu yenu.

Kuithibitisha miguu ni kinaya cha uimara. Aya hii ni dalili wazi kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) yuko pamoja na watu wa haki na uadilifu; anawasaidia na kuwashika mkono. Maana ya Aya hii yako kwenye Aya nyingi; kama vile:

فَإِنَّ حِزْبَ اللَّـهِ هُمُ الْغَالِبُونَ ﴿٥٦﴾

“Basi kundi la Mwenyezi Mungu ndio watakaoshinda.” Juz. 6 (5:56).

إِنَّ اللَّـهَ مَعَ الَّذِينَ اتَّقَوا وَّالَّذِينَ هُم مُّحْسِنُونَ ﴿١٢٨﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu yuko pamoja na wenye uchamungu Na wale ambao wanatenda mema” Juz. 14 (16:128),

إِنَّ اللَّـهَ يُدَافِعُ عَنِ الَّذِينَ آمَنُوا ﴿٣٨﴾ وَلَيَنصُرَنَّ اللَّـهُ مَن يَنصُرُهُ إِنَّ اللَّـهَ لَقَوِيٌّ عَزِيزٌ ﴿٤٠﴾

“Hakika Mwenyezi Mungu huwakinga walioamini. Na hakika Mwenyezi Mungu humnusuru yule anayemnusuru Yeye. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mtukufu.” Juz. 17 (22:38,40).

Nusra inayotoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) iko namna nyingi; miongoni mwazo ni hizi zifutazo:

• Kuwashinda maadui kwa vita na nguvu ya silaha; kama alivyowashinda Mtume wa Mwenyezi Mungu vigogo wa kikuraishi na dhulma yao na wengineo.

• Kushinda kwa adhabu itokayo mbinguni; kama vile kimbunga tufani n.k.

• Kushinda kwa nguvu ya hoja na dalili katika mijadala.

• Kushinda kwa shani na utajo wa kudumu duniani.

• Nusra ya Akhera siku ile zitakosawijika nyuso.

وَتَرَى الْمُجْرِمِينَ يَوْمَئِذٍ مُّقَرَّنِينَ فِي الْأَصْفَادِ ﴿٤٩﴾

“Na utawaona wahalifu siku hiyo wamefungwa katika minyororo.” Juz. 13 (14:49).

Kwa vile katika Aya tuliyo nayo nusra haikufungwa na sifa ya aina yoyote, basi inatubainikia kuwa makusudio ya nusura katika Aya hii ni nusra yoyote. Hakuna mwenye shaka kuwa itakuwa tu, hata kama ni huko Akhera kusiko na shaka. Kwa hiyo basi hakuna nafasi ya kutaaradhi au kuuliza kuwa vipi Mwenyezi Mungu amewaahidi wenye haki nusra yake, lakini historia imejaa dhulma na ujeuri waaliofanyiwa wema na wenye ikhlasi.

Yametangulia maelezo kuhusu maudhui haya katika Juz. 17 (22:38) kifungu cha “Mwenyezi Mungu huwakinga walioamini.”

DOLA YA KIISLAMU

Kwa mnasaba wa Aya hii tutadokeza yafuatayo: Kuna vikundi siku hizi vinadai kusimamisha dola ya Kiislamu. Ni mwislamu gani leo, mwenye ikhlasi ya Mwenyezi Mungu anayekataa Uislamu uwe na serkali yake inayotekeleza hukumu za Qur’an na waislamu wawe na umoja utakaowaokoa na utengano?

Lakini tujiulize: Je, dola hii itapatikana kwa kiasi tu cha kusimamisha bendera na kuinua nembo? Au kwa kuweko vilemba vingi kwenye vichwa vya wajinga na wenye undani?

Je, inawezekana kuwaunganisha Waislamu milioni 700 walioenea mashariki na magharibi mwa ardhi huku wakiwa na makabila, madhehebu na siasa mbalimbali; hawa wameukumbatia ujamaa, wale ubepari na wengine wakiwa na siasa zisizofungamana na upande wowote?

Kama itapatikana dola hiyo ya waarabu au wasiokuwa waarabu je, itaweza kukabili majukumu yake na kutatua matatizo ya waislamu katika nchi nyingine. Kisha je, dola hii ni ya kisunni au kishia au ya wote wawili?

Majibu ya maswali haya tuwachie wataalamu wenye ikhlasi[2] .

Hakika waislamu wamepatwa na udhalili mwingi na kushindwa. Kule kushindwa mnamo tarehe 5 June inatosha kuwa ni udhalili na utwevu. Sababu ya kwanza na ya mwisho ya kushindwa huko ni utengano. Dawa pekee ya hilo ni maarufu kwa wote – kusimama safu moja dhidi ya maadui wenye ushirikiano waliojipanga na kujitokeza kwenye vita vya mwezi June.

Mwenye kumfanyia ikhlasi Mwenyezi Mungu na akataka kuwanasihi waislamu kwa ukweli kabisa basi na afanye juhudi zake zote kwa ajili ya kuwasaidia waislamu kujikomboa na nguvu ya ufisadi ya ndani na nje.

Wakishajikomboa na kuwa na uhuru kamili, hapo ndipo wenye ikhlasi wanaweza kufikiria serikali ya kiislamu au nyingine yenye kuridhiwa na Mwenyezi Mungu na yenye masilahi kwa waislamu.

Ishara yetu hii inatiliwa nguvu na kauli ya Imam Ali(a . s) :“Hakika uzushi wenye kutatiza ni maangamizi na katika utawala wa Mungu kuna hifadhi ya mambo yenu basi upeni utiifu wenu au Mwenyezi Mungu atawaondolea utawala wa kiislamu.”

Ikiwa utawala wa kiisalamu uliwaondokea wahenga kwa sababu ya utengano wao, je utaweza kuturudia sisi tuliotengana zaidi.

Unaweza kuuliza : Je, ni kweli yanayosemwa kuwa chimbuko la fikra ya dola ya kiislamu ni uzayuni ili kuitakasa dola yake ya kidini na ya kibaguzi? Ili waweze kusema kuwa hata waislamu nao pia wanataka dola ya kidini?

Jibu : Hakika dini ya kiyahudi ni dini ya uadui wa maisha na ubinadamu. Kwa sababu, katika itikadi yao, Mwenyezi Mungu ni Mungu wa kikabila, hajishughulishi na walimwengu wengine wote isipokuwa Israil peke yake, na kwamba watu wengine wote wameumbwa kuwatumikia wao; kama ilivyoelezwa katika kitabu Alkanzul marsud cha Dkt. Yussuf Hanna Naasrullah na kitabu Albaqau lilyahud cha mzayuni Rose Marine.

Ama Uislamu ni dini ya maisha, huruma na ubaindamu kwa ujumla. Hakuna kitu kinachofahamisha hivyo zaidi kuliko Aya na Hadithi zinazotangaza waziwazi kuwa uislamu unaongoza kwenye usawa zaidi na kwamba unatilia mkazo kwenye akili na maumbile na ni wajibu kuitikia mwito wa Mwenyezi Mungu na Mtume, kwa sababu ni mwito wa maisha bora.

Maana ni kuwa Uislamu ni dini ya kilimwengu ya kiakili; yaani unajishughulisha na mtu kama mtu wa namna yeyote, hata kama ni myahudi, kwa sharti ya kutomfanyia uadui nduguye mtu.

Sasa haya ni wapi kwa wapi na dini ya Mayahudi waliojiita taifa teule la Mwenyezi Mungu?

Na waliokufuru, basi kwao ni maangamizo, hawataona isipokuwa hizaya na maangamizina atavipoteza vitendo vyao, haitawarudia heri yoyote.

Hayo ni kwa sababu waliyachukia aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, basi akaviangusha vitendo vyao.

Walimchukia Mtume(s.a.w. w ) na Qur’an si kwa lolote ila ni kwa vile aliwatakia haki na wao wanaichukia, basi wakawa ni wenye hasara. Kupotea na kuanguka kuna maana moja, nako ni kupotea na kutofaa amali. Mwenyezi Mungu amekariri ili kuashiria kuwa kuikufuru Qur’an na kuichukia ni kupotea amali.

Je, hawatembei katika ardhi wakaona ulikuwaje mwisho wa waliokuwa kabla yao?

Jinsi washirikina walivyokadhibisha risala ya Muhammad(s.a.w. w ) , huku wakiona athari ya waliopita na wakisikia kuwa Mwenyezi Mungu aliwaadhibu walipowakadhibisha mitume?

Aya hii imetangulia kwa herufi zake katika Aya kadhaa.

Mwenyezi Mungu aliwaangamiza wao, watoto wao, wake zao na mali zao.

Na kwa makafiri hawa itakuwa mfano wa hayo.

Hukumu ya Mwenyezi Mungu kwa mataghuti ni moja – ikiwa atawaangamiza wa mwanzo kwa sababu ya uasi wao, basi wengine pia atawaangamiza kwa sababu hiyo hiyo.

Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ni Mlinzi wa walioamini. Na makafiri hawana mlinzi.

‘Hayo’ ni hayo ya kuangamizwa. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu aliwaangamiza makafiri wakiwa hawana wa kuwasaidia, lakini waumini, msimamizi wao ni Mwenyezi Mungu, akiwakinga na kuwaaneemesha.

Hakika Mwenyezi Mungu atawaingiza ambao wameamini na wakatenda mema katika Bustani zipitiwazo na mito chini yake.

Maana yako wazi na imekwishatangulia katika Aya kadhaa huko nyuma.

Na ambao wamekufuru hujifurahisha na hula kama walavyo wanyama, na Moto ndio makazi yao.

Wao ni sawa na wanyama, wanakula tu na wala hawafikirii chochote. Kwa hiyo mwisho wao ni Jahannam makazi mabaya kabisa.

Imam Ali(a . s) anasema:“Mimi sikuumbwa ili nijishughulishe na kula vizuri. kama mnyama aliyefungwa ambaye hamu yake ni lishe yake tu, au asiyefungwa ambaye shughuli yake kuu ni kuchakura majaa kwa ajili ya lishe yake na kucheza nayo anavyotaka.”

Na miji mingapi iliyo kuwa na nguvu zaidi kuliko mji wako huu uliokutoa; nao tuliwateketeza na wala hawakuwa na wa kuwanusuru.

Hili ni karipio kwa wale waliopanga njama za kumuua Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) , akalazimika kuuhama mji wake wa Makka na kuelekea Madina. Tazama Juz. 9 (8:30).

Katika Tafsir Attabariy, imepokewa kutoka kwa Ibn Abbas, kwamba Mtume alipotaka kuutoka mji wa Makka alisema: ‘’Wewe ni mji wa Mwenyezi Mungu unaopendeza zaidi kwa Mwenyezi Mungu. Na wewe ni mji wa Mwenyezi Mungu unaopendeza zaidi kwangu. Lau sikuwa washirikina wamenitoa nisingelikutoka.’’ Ndipo Mwenyezi Mungu (s.w.t) akateremsha Aya hii.

Je, mwenye kuwa na dalili kutoka kwa Mola wake ni kama aliyepambiwa uovu wa vitendo vyake, na wakafuata hawaa zao?

Yule mwenye kuichukua haki kutoka katika chimbuko lake na akawa na busara, hayuko sawa mbele ya Mwenyezi Mungu na yule anayeipima haki kwa hawaa yake na malengo yake, huku akijiona kuwa yeye ndiye mtu mwenye matendo mema zaidi kuliko wengine.