TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Juzuu 24

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE0%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Mwandishi: Sheikh Muhammad Jawad Mughniyya
: HASANI MWALUPA
Kundi:

Matembeleo: 25959
Pakua: 3219


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 30 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 25959 / Pakua: 3219
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Juzuu 24

Mwandishi:
Swahili

23

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Sura Ya Sabini Na Nne: Surat Al- Muddathir. Imeshuka Makka Ina Aya 56.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu.

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ ﴿١﴾

1. Ewe uliyejigubika!

قُمْ فَأَنذِرْ ﴿٢﴾

2. Simama uonye!

وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ ﴿٣﴾

3. Na Mola wako mfanyie takbira!

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ ﴿٤﴾

4. Na nguo zako zitwaharishe.

وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ ﴿٥﴾

5. Na mabaya yaambae!

وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ ﴿٦﴾

6. Wala usitoe kwa kutaka kingi.

وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ ﴿٧﴾

7. Na kwa ajili ya Mola wako, fanya subira!

فَإِذَا نُقِرَ فِي النَّاقُورِ ﴿٨﴾

8. Basi litapopulizwa barugumu.

فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ ﴿٩﴾

9. Siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu.

عَلَى الْكَافِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ ﴿١٠﴾

10. Kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

EWE ULIYEJIGUBIKA

Aya 1 - 10

MAANA

Aya hizi zinaashiria wadhifa wa Muhammad(s.a.w.w) kama mjumbe wa haki kwa viumbe. Pia kuna ishara kuwa watu wote mbele ya Mwenyezi Mungu wako sawa; ufafanuzi ni kama ufufatavyo:­

Ewe uliyejigubika!

Huyo ni Mtume mtukufu(s.a.w.w) . Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemwita kwa sifa hii kwa sababu wakati huo alikuwa katika hali hiyo kutokana na sababu fulani; kama tulivyosema mwanzo wa Sura iliyopita.

Simama uonye!

Neno linaweza kuwa na maana moja ya kilugha, lakini maana hayo, mara nyingi, yanatofautiana kulingana na msemaji na anayeambiwa. Mfano neno ‘onya,’ maana yake katika kamusi za lugha lina maana ya kuhofisha na kuhadharisha.

Kwa mfano ukimuona mtu anachimba shimo njiani na kumwambia toa onyo, utakuwa unamaanisha atangaze na kuwaonya wapita njia wasiingie shimoni. Ukimwambia mwana fakihi katika kijiji: ‘onya.’ Utakuwa unamaanisha awafundishe watu wa hapo hukumu za dini na kuwahofisha kuzihalifu.

Ama kauli ya Mtukufu kwa Nabii wake; ‘simama uonye,’ Maana yake ni pambana na waasi wenye nguvu na kiburi kwa neno la haki na uwambie: nyinyi ni wapotevu wafisadi na mtajua kesho hizaya na udhalili utakaowapata, kama hamtarudi kuuacha upotevu wenu. Ukiwambia hivi uvumilie yatakayokupata kutoka kwao na umsabihi Mola wako na kumshukuru.

Tukiona jinsi Muhammad(s.a.w.w) alivyopambana na makuraishi wakiwa na nguvu na kauli na yeye hana chochote zaidi ya ikhlasi na imani, hapo ndio tunabainikiwa na yaliyomsibu kutoka kwao: walimpa sifa ya uchawi, uwongo, ushairi na hata wendawazimu. Walimshakizia watoto wamfanyie masikhara na kumtupia mawe; wakawaambia wanawake waweke miba kwenye njia atakayopita na wasafihi wamwekee uchafu na najisi njiani; hata kuna mmoja wao aliyewahi kumvua kilemba Mtume na kukifunga shingoni mwake. Fauka ya yote hayo makuraishi waliweka azimio la kumwekea vikwazo Mtume na watu wake na kumzuia asiwe na mahusiano na jamii.

Pamoja na yote hayo Nabii(s.a.w.w) alivumilia na kuendelea na mwito wake bila ya kujali hali ngumu waliyompa makuraishi, wakaunda vikosi na majeshi. Akavumilia, akawa imara na subira na kuitikia kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Ewe uliyejigubika! Simama uonye.”

Haya yanatuwekea wazi kuwa wadhifa wa Mtume ni kuonya pamoja na uvumilivu wa tabu na mashaka. Hili ndilo jambo la kwanza. Ama la pili, ni usawa baina ya watu, linalofa­hamika kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Na Mola wako mfanyie takbira!

Ukimwambia mtu wa kawaida: Mfanyie takbira Mwenyezi Mungu, tutafa­hamu kuwa unataka asema Allahf akbar; kama vile ukisema: mswalie Mtume.

Lakini kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kumwambia Nabii wake: ‘Na Mola wako mfanyie takbira, ina maana kubwa na nzito zaidi, ambayo ni: Ewe Muhammad(s.a.w.w) waambie usoni mwao wale wanoji­fanya majabari wenye kiburi kuwa enzi ni ya Mwenyezi Mungu na Yeye pekee ndiye mkubwa aliye juu, na kwamba nguvu, utukufu na utawala ni wa mmoja aliye pekee asiyekuwa na mshirika kutoka kwenye miungu wenu au nyinyi wenyewe au kutoka kwa wengine; na kwamba watu wote wako sawa katika kumwabudu Mwenyezi Mungu; hakuna tofauti baina ya mweusi na mweupe wala baina ya tajiri na fukara.

Muhammad aliitikia mwito wa Mola na kuwaambia mataghuti mengi tu; miongoni mwayo ni: “Hakika nyinyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Jahannam, mtaifikia.” Juz. 17 (21:98).

Na nguo zako zitwaharishe.

Vile vile hii inafungamana na kulingania na kuonya. Hakuna anayetia shaka kuwa usafi wa mwili na nguo ni katika imani, lakini makusudio hapa ni zaidi ya hivyo; kwamba Mtume(s.a.w.w) atoe mwito wa usafi wa nje, kama vile uchafu, na usafi wa ndani, kama vile udanganyifu na hiyana, ria na unafiki, ujinga na kuhadaika na madhambi mengineyo.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) hayo ameyatolea ibara ya usafi wa nguo, kwa kutumia des­turi ya waarabu; wanaposema: Fulani ni msafi wa mapindo ya nguo yake, wakimaanisha kuwa ni msafi wa moyo na dhati.

Na mabaya yaambae!

Hii inakuwa ni tafsiri na ufafanuzi wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: ‘Na nguo zako zitwaharishe,’ kama ilivyosemekana. Pia imese­mekana makusudio ni ushirikina na kuabudu masanamu.

Wala usitoe kwa kutaka kingi.

Makusudio ya kutaka kingi hapa ni kujiona umefanya mengi. Maana ni kuwa Ewe Muhammad! umewafanyia watu mema mengi na fadhila nyin­gi, lakini usimsimbulie yeyote kwa hilo ukajiona kuwa umefanya mengi, ukasema mimi nimefanya hili ni kawafadhili lile. Kwani kila ulilojitolea ni fadhila yako kutoka kwa Mwenyezi Mungu. Kuna fadhila gani na tukufu zaidi kuliko kuafikiwa kufanya kheri?

Mara nyingi huko nyuma tumeeleza kuwa makatazo yanafaa hata ikiwa anayeambiwa hana azma ya kufanya hilo linalokatazwa, mbali ya kuwa amri za Mwenyezi Mungu na makatazo yake yanawahusu waja wake wote, hata wale wenye takua.

Imesemwa katika Nahjul-balagha: “Kutekeleza haja hakuwezi kuendelea ila kwa mambo matatu: Kwa kuifanya ndogo itakuwa kubwa, kwa kuificha itajitokeza na kwa kuiharakisha itasifika.”

Na kwa ajili ya Mola wako, fanya subira!

Mwenyezi Mungu hakumwamrisha Nabii wake mtukufu jambo lolote la taklifa ya kufikisha na utume ila analikutanisha na subira, kama ilivyose­mekana, kwa sababu ya kujua kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu maudhi atakayopambana nayo kutoka kwa wenye inadi.

Basi litapopulizwa barugumu; siku hiyo, basi, itakuwa siku ngumu; kwa makafiri haitakuwa nyepesi.

Ni kama mfano wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

فَإِذَا نُفِخَ فِي الصُّورِ ﴿١٠١﴾

“Basi itakapopuziwa parapanda, Juz. 18 (23:101).

Baada ya Mwenyezi Mungu kumwamuru Mtume wake kuwa na uvumilivu kutokana na adha ya wakadhibishaji, sasa anawahadharisha na Siku ya Kiyama ambayo itakuwa ngumu na kali sana kwao; itakuwa nzito isiyofu­atiwa na wepesi. Yametangulia makumi ya Aya kuhusiana na aliyoyaandaa Mwenyezi Mungu kwa wakosefu; yakiwemo chakula, kinywaji na adhabu kali.

ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا ﴿١١﴾

11. Niache peke yangu na niliye­ muumba.

وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا ﴿١٢﴾

12. Na nikamjaalia kuwa na mali mengi.

وَبَنِينَ شُهُودًا ﴿١٣﴾

13. Na wana wanaoonekana.

وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا ﴿١٤﴾

14. Na nikamtengenezea mipan­go.

ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ ﴿١٥﴾

15. Kisha anatumai nimzidishie!

كَلَّا إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا ﴿١٦﴾

16. Sivyo! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!

سَأُرْهِقُهُ صَعُودًا ﴿١٧﴾

17. Nitamtesa kwa mateso ya hali ya juu.

إِنَّهُ فَكَّرَ وَقَدَّرَ ﴿١٨﴾

18. Hakika yeye alifikiri na akapima.

فَقُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ ﴿١٩﴾

19. Basi amelaaniiwa! Vipi alivyopima!

ثُمَّ قُتِلَ كَيْفَ قَدَّرَ ﴿٢٠﴾

20. Tena amelaaniiwa! Vipi alivyo pima!

ثُمَّ نَظَرَ ﴿٢١﴾

21. Kisha akatazama.

ثُمَّ عَبَسَ وَبَسَرَ ﴿٢٢﴾

22. Kisha akakunja uso na aka­nuna.

ثُمَّ أَدْبَرَ وَاسْتَكْبَرَ ﴿٢٣﴾

23. Kisha akageuka, na akatak­abari.

فَقَالَ إِنْ هَـٰذَا إِلَّا سِحْرٌ يُؤْثَرُ ﴿٢٤﴾

24. Akasema: Haya si chochote ila ni uchawi ulionukuliwa.

إِنْ هَـٰذَا إِلَّا قَوْلُ الْبَشَرِ ﴿٢٥﴾

25. Haya si chochote ila ni kauli ya binadamu.

سَأُصْلِيهِ سَقَرَ ﴿٢٦﴾

26. Nitamtia kwenye Saqar.

وَمَا أَدْرَاكَ مَا سَقَرُ ﴿٢٧﴾

27. Na nini kitakujulisha ni nini Saqar?

لَا تُبْقِي وَلَا تَذَرُ ﴿٢٨﴾

28. Haubakishi wala hauachi.

لَوَّاحَةٌ لِّلْبَشَرِ ﴿٢٩﴾

29. Unababua ngozi.

عَلَيْهَا تِسْعَةَ عَشَرَ ﴿٣٠﴾

30. Juu yake wapo kumi na tisa.

وَمَا جَعَلْنَا أَصْحَابَ النَّارِ إِلَّا مَلَائِكَةً وَمَا جَعَلْنَا عِدَّتَهُمْ إِلَّا فِتْنَةً لِّلَّذِينَ كَفَرُوا لِيَسْتَيْقِنَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَيَزْدَادَ الَّذِينَ آمَنُوا إِيمَانًا وَلَا يَرْتَابَ الَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ وَالْمُؤْمِنُونَ وَلِيَقُولَ الَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ وَالْكَافِرُونَ مَاذَا أَرَادَ اللَّـهُ بِهَـٰذَا مَثَلًا كَذَٰلِكَ يُضِلُّ اللَّـهُ مَن يَشَاءُ وَيَهْدِي مَن يَشَاءُ وَمَا يَعْلَمُ جُنُودَ رَبِّكَ إِلَّا هُوَ وَمَا هِيَ إِلَّا ذِكْرَىٰ لِلْبَشَرِ ﴿٣١﴾

31. Na hatukuwafanya walinzi wa Moto ila Malaika, Wala hatukufanya idadi yao ila kuwa jaribio kwa wale waliokufuru. Ili wawe na yakini waliopewa Kitabu na wazidi imani wale walioamini, wala wasiwe na shaka wale waliopewa Kitabu na waumi­ni, na wapate kusema walio na maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu? Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humpoteza amtakaye na humwongoza amtakaye. Na hapana ajuae majeshi ya Mola wako ila Yeye. Na huo si chochote ila ni ukumbusho kwa watu.

NIACHE PEKE YANGU NA NILIYEMUUMBA

Aya 11 - 31

KISA KWA UFUPI

Walid bin Al-Mughira Al-Makhzumi, alikuwa ni miongoni mwa vigogo wa kikuraishi, akiwa na mali nyingi na watoto. Siku moja akamsikia Mtume akisoma Aya mojawapo ya Qur’an, akasema: “Hii sio maneno ya binadamu wala jinni. Wallah, hakika kauli yake ‧ yaani Qur’an ‧ ina utamu na ina mvuto na kwamba juu yake kuna matunda na chini yake kumejaa. Hakika iko juu na haishindwi.”

Basi makuraishi waliposikia hivi waka­hofia maneno ya Walid kama yakienea kwa watu, watamwamini Muhammad(s.a.w.w) . Wakamtaka Walid ampinge Mtume. Akasema nisemeje sasa? Niseme ni mwendawazimu, nani ataamini? Au niseme ni kuhani, naye hakuwahi kuwa kuhani kabisa.

Nikisema ni mshairi, yeye hajawahi kutamka shairi na nikisema ni mwongo, hakuna yeyote aliyewahi kusikia uwongo kwake. Kisha akafiria akaona ampe sifa ya uchawi na kwamba yeye ameichukua Qur’an kutoka kwa wachawi.

MAANA

Niache peke yangu na niliyemuumba.

Maneno yanaelekezwa kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) . Makusudio yake ni kumkemea na kumhadharisha Walid bin Mughira kwa maafikiano ya wafasiri. Maana ni kuwa niachie mimi huyo ewe Muhammad, usijishughulishe naye, wala na yale anayokuzulia. Mimi peke yangu ndiye nitakayempiga vita na kumpa adhabu.

Mwenyezi Mungu alifikia ghadhabu hii kwa Walid, kwa sababu yeye alip­ituka mipaka na uovu; akakufuru neema ya Mwenyezi Mungu na akaipin­ga haki na kuifanyia kiburi haki na watu wake. Kila mwenye kuipinga haki basi ni mlengwa wa ghadhabu hii na makemeo haya; kama vile Walid Bin Mughira, kwa vile sababu ya kushuka Aya haihusiki na aliyeteremshiwa tu, bali inaenea, kama tulivyosema mara nyingi.

Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:Na nikamjaalia kuwa na mali mengi, inaashiria kuwa linasobabisha na kuleta msukumo wa kufanya uovu ni utajiri na wingi wa mali. Aya kadhaa zianaashria hakika hii, ikiwemo Aya 11 ya sura iliyopita na pia kauli yake Mwenyezi Mungu akimsimulia muasi aliyojifaharisha kwa mtu mwema:

أَنَا أَكْثَرُ مِنكَ مَالًا ﴿٣٤﴾

“Mimi nimekushinda kwa mali” Juz. 15 (18:34).

Inatosha kuwa ni ushahidi wa hayo kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

كَلَّا إِنَّ الْإِنسَانَ لَيَطْغَىٰ ﴿٦﴾ أَن رَّآهُ اسْتَغْنَىٰ ﴿٧﴾

“Hakika mtu hupituka mipaka, kwa kujiona amejitosheleza.” (96:6-7).

Kwa kutegemea Aya hizi na nyingine zilizo mfano wake, inawezekana kusema, ijapokuwa ni kwa kubuni, kwamba asili ni kuwa kila tajiri ni muasi, mpaka ithibitike kinyume. Imelezwa kwenye Nahjul-balagha: “Ni uzuri ulioje wa matajiri kuwanyenyekea mafukara kwa kutaka yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu! Na uzuri zaidi kuliko huo ni maringo ya mafukara kwa matajiri kwa kumtegemea Mwenyezi Mungu.”

Kuna Hadith isemayo: “Heri zote ni za aliyesilimu na ikawa maisha yake ni kutosheka.. ewe Mwenyezi Mungu mruzuku Muhammad na kizazi cha Muhammad kujichunga na kutosheka.”

Na wana wanaoonekana , wakiwa pamoja naye wakishindana kumhudu­mia.Na nikamtengenezea mipango . Nimemsahilishia njia ya jaha na mali akiogelea kwenye neema atakavyo.

Kwa mnasaba huu tunaashiria kwamba neema za dunia hazifahamishi kuridhiwa na Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasema: “Hakika maisha ya dunia ni mchezo na upuzi tu.” Juz. 26 (47:36). Kwenye Hadith amesema: “ Lau dunia mbele ya Mwenyezi Mungu italinganishwa na kheri kwa ubawa wa mbu, basi kafiri asingekunywa hata tama moja la maji.”

Ilijitokeza dunia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, mbora wa viumbe wa Mwenyezi Mungu, akaikataa, lakini Walid, muovu wa viumbe wa Mwenyezi Mungu, ilikithiri mali yake,kisha anatumai nimzidishie ! Yaani ana tamaa ya kuzidishiwa mali yake ili azidi uovu na uadui.

Haiwezekani kuchanganyika wema na tamaa katika moyo mmoja. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) anasema: “Tamaa ni ufunguo wa kila maasi na ni msingi wa kila hatia na ni sababu ya kuanguka mambo mema.”

Sivyo! Kwani hakika yeye alikuwa akizifanyia inadi Aya zetu!

Tokomea mbali ewe mpinzani mwenye hiyana! Hivi una tamaa kwa Mungu na wewe unaifanyia inadi haki na kuizuia kwa kutangaza vita kwa watu wa haki? Wapokezi wanasema kuwa iliposhuka tu Aya hii Walid alibadilika kutoka kwenye enzi na kuwa dhalili, utajiri kuwa fukara, na akafa na hali mbaya.

Amesema kweli aliyoesema: “Hawakusema watu kwa jambo lolote kuwa lina heri ila kuna shari iliyofichwa na nyakati.” Hii ni duniani, ama malipo yake huko Akhera yanaelezwa na Aya hii:

Nitamtesa kwa mateso ya hali ya juu.

Hali ya juu inaweza kuwa ni ukali na mashaka na inaweza kuwa ni zaidi. Mfumo wa maneno unajulisha maana zote mbili na kwamba adhabu siku hiyo itazidi kiwango na kiaina, muda baada ya muda.

Hakika yeye alifikiri na akapima.

alifikiria kuhusu Qur’an na akaandaa kauli ya uzushi kwamba Qur’an ni uchawi ulionukuliwa, kama itakavyokuja mbele.

Basi amelaaniwa! Vipi alivyopima! Tena amelaaniwa! Vipi alivyopima!

Amelaaaniwa kisha akalaaniwa katika kufikiria kwake na kupanga kwake kauli, vitendo na makusudio yake yote. Hakuna kitu kinachofahamisha ufasaha zaidi kuliko kukaririka laana kwa waovu.

Kisha akatazama . Baadaa ya kufikiria aliinua jicho lake kwa vigogo wa kikuraishi,kisha akakunja uso , kwa kukunja nyusi zakena akanuna ; uso ukamuiva.

Kisha akageuka, na akatakabari.

Alihakikisha alipofikiria kuwa Qur’an ni haki isiyokuwa na shaka, lakini pamoja na hayo aliipinga na akaitukukiaakasema: “Haya si chochote ila ni uchawi ulionukuliwa. Haya si chochote ila kauli ya binaadamu ,” aliyoichukua Muhammad kutoka kwa makuhani wa kichawi.

Picha hii ya Walid iliyopigwa na Qur’an, ya kufikiri, kupima, kukunja uso na kununa, inatujulisha kuwa yeye alikuwa hana la kufanya katika kupanga uwongo kwenye jambo analoliamini kuwa ni haki na kweli.

Nitamtia kwenye Moto waSaqar . Atakayetiwa ni huyo huyo Walid. Saqar ni miongoni mwa majina ya Jahannam.Na nini kitakujuulisha ni nini huo Moto waSaqar ? Kwani umefika kikomo cha kutisha; miongoni mwayo ni kwamba huohaubakishi yeyote katika wakosefuwala hauachi aina yoyote ya adhabu ila inawashushia naunababua ngozi .

Makusudio ya kubabua hapa ni kuiva, kama alivyosema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

كُلَّمَا نَضِجَتْ جُلُودُهُم بَدَّلْنَاهُمْ جُلُودًا غَيْرَهَا ﴿٥٦﴾

“Kila zitakapoiva ngozi zao, tutawabadilisha ngozi nyingine.” Juz. 5 (4:56).

Juu yake wapo kumi na tisa.

Yaani juu ya hiyo Saqar. Kumi na tisa ni walinzi wa Jahannam. Je, kumi na tisa ni idadi, au aina au ni viongozi? Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye zaidi.

Kuna riwaya isemayo kuwa Abu Jahl, aliwaambia makuraishi: ‘’Hamna maana ninyi! Hivi watu kumi katika nyinyi wanashindwa kumshika mmoja katika hao 19?”

Mmoja alieyitwa Abul-Mushid alisema: “Mimi peke yangu nitawatoshea na 17, nyinyi shikeni wawili tu.” Huyu alisema kwa madharau kama alivyosema Abu Jahl.

Na hatukuwafanya walinzi wa Moto ila Malaika.

Walinzi wa moto si katika aina ya binadamu; bali ni malaika wakali wenye nguvu; hakuna anayewazidi nguvu isipokuwa aliye pekee, Mwenye nguvu ambaye ameumba kila kitu.

Kama kwamba muulizaji ameuliza: Nini makusudio ya kutajwa idadi, jambo ambalo linafungua mlango wa madharau kwa wapinzani? Ndio aka­jibu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwamba kutaja kwake kuna faida tatu:

1.Wala hatukufanya idadi yao ila kuwa jaribio kwa wale waliokufuru.

Ndio! Mwenyezi Mungu anajua kwamba washirikina watakaposikia idadi watacheka na kufanya stihizai, lakini pamoja na hayo ametaja, kwa sababu haki inapaswa itangazwe, hata kama natija yake ni madharau ya wanaod­harau. Kwa maneno mengine ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawa­jaribu waja, naye ni mjuzi zaidi kuliko nafsi zao. Anawajaribu kwa raha na dhiki. Vile vile anasema haki ili vijitokeze vitendo vyao vinavyostahiki thawabu na adhabu.

Kutajwa idadi kumedhihirisha hakika ya washirikina ya kudharau ghaibu, hivyo wakastahiki ghadhabu na adhabu ya Mwenyezi Mungu; kama kulivyodhihirisha hakika ya waumini wakastahiki radhi za Mwenyezi Mungu na thawabu zake, kama yatakavyokuja maelezo. Zaidi ya hayo ni kuwa kutangaza Mtume neno la haki bila ya kuangalia yatakayompata kwa ajili yake, ni dalili mkataa kwamba hana jingine analolitaka isipokuwa kui­hakikisha haki na kuibatilisha batili.

2.Ili wawe na yakini waliopewa Kitabu.

Ulama wa kiyahudi na wa kinaswara wakati huo walishuhudia kwa imani na yakini kwamba walinzi idadi yao ni 19, kwa sababu hilo linaafikiana na waliyoyasoma katika Tawrat na Injil.

3.Na wazidi imani wale walioamini.

Wahyi wa mambo ya ghaibu unawazidisha makafiri upinzani na jeuri na waumini wanazidi imani. Imesemekana kuwa waumini huzidi yakini waki­ambiwa na watu wa Kitabu kuwa idadi imo kwenye vitabu vyao. Usawa ni kuwa kila Aya katika Aya zake Mwenyezi Mungu Mtukufu inawazidisha waumini yakini kwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake; ni sawa watu wa Kitabu wakubali au wapinge. Ni kweli kwamba kukubali kwao ni hoja kwa wapinzani.

Wala wasiwe na shaka wale waliopewa Kitabu na waumini.

Huu ni ufafanuzi na msisitizo wa yaliyokuwa kabla yake, kwa sababu kutokuweko shaka ni kuwa na yakini na kuzidi imani.

Na wapate kusema walio na maradhi katika nyoyo zao na makafiri: Mwenyezi Mungu amekusudia nini kwa mfano huu?

Vile vile huu ni ufafanuzi na msisitizo wa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Wala hatukufanya idadi yao ila kuwa jaribio kwa wale walioku­furu,” pamoja na kufafanua aina ya makafiri ambao ni wanafiki walio na maradhi katika nyoyo zao. Umetangulia mfano wake katika Juz. 1 (2:26).

Ndio kama hivyo Mwenyezi Mungu humpoteza amtakaye na humwongoza amtakaye.

Mwenye kufuata njia ya upotevu Mwenyezi Mungu humpoteza:

فَلَمَّا زَاغُوا أَزَاغَ اللَّـهُ قُلُوبَهُمْ ﴿٥﴾

“Walipopotoka, Mwenyezi Mungu alizipotoa nyoyo zao.” Juz. 28 (61:5).

فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ فَزَادَهُمُ اللَّـهُ مَرَضًا ﴿١٠﴾

“Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi.” Juz. 1 (2:10).

Na mwenye kufuata njia ya uongofu Mwenyezi Mungu humuongoza: “Na ambao wameongoka anawazidishia uongofu.” Juz. 26: (47:17).

Umetangulia mfano wake katika Juz. 22 (35:8).

Na hapana ajuae majeshi ya Mola wako ila Yeye.

Askari wa Mwenyezi Mungu sio wale 19 tu, viumbe wote wanatii matak­wa hata wanyama, wadudu, ndege, upepo, matetemeko, matufani na men­gineyo ambayo hakuna anayejua isipokuwa mwanzishaji wa viumbe na mrudishaji.

Na huo si chochote ila ni ukumbusho kwa watu.

Huo ni huo moto wa Saqar. aliyoumba Mwenyezi Mungu (s.w.t) na kuwa­hadharisha nao ili wayaogope maasi kwa ndani na nje.

24

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

كَلَّا وَالْقَمَرِ ﴿٣٢﴾

32. Sivyo! Naapa kwa mwezi!

وَاللَّيْلِ إِذْ أَدْبَرَ ﴿٣٣﴾

33. Na kwa usiku unapokucha!

وَالصُّبْحِ إِذَا أَسْفَرَ ﴿٣٤﴾

34. Na kwa asubuhi inapopam­bazuka!

إِنَّهَا لَإِحْدَى الْكُبَرِ ﴿٣٥﴾

35. Hakika huo ni mojawapo ya mambo makubwa!

نَذِيرًا لِّلْبَشَرِ ﴿٣٦﴾

36. Ni onyo kwa watu.

لِمَن شَاءَ مِنكُمْ أَن يَتَقَدَّمَ أَوْ يَتَأَخَّرَ ﴿٣٧﴾

37. Kwa anayetaka miongoni mwenu kwenda mbele au kurudi nyuma.

كُلُّ نَفْسٍ بِمَا كَسَبَتْ رَهِينَةٌ ﴿٣٨﴾

38. Kila nafsi iko kwenye rahani kwa iliyoyachuma.

إِلَّا أَصْحَابَ الْيَمِينِ ﴿٣٩﴾

39. Isipokuwa watu wa kuliani.

فِي جَنَّاتٍ يَتَسَاءَلُونَ ﴿٤٠﴾

40. Watakua katika mabustani wakiulizana.

عَنِ الْمُجْرِمِينَ ﴿٤١﴾

41. Kuhusiana na wakosefu.

مَا سَلَكَكُمْ فِي سَقَرَ ﴿٤٢﴾

42. Ni kipi kilichowapeleka Motoni?

قَالُوا لَمْ نَكُ مِنَ الْمُصَلِّينَ ﴿٤٣﴾

43. Watasema: Hatukuwa mion­goni mwa waliokuwa wak­iswali.

وَلَمْ نَكُ نُطْعِمُ الْمِسْكِينَ ﴿٤٤﴾

44. Wala hatukuwa tukiwalisha masikini.

وَكُنَّا نَخُوضُ مَعَ الْخَائِضِينَ ﴿٤٥﴾

45. Na tulikuwa tukijiingiza pamoja na wanaojiingiza.

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ الدِّينِ ﴿٤٦﴾

46. Na tulikuwa tukikadhibisha siku ya hukumu.

حَتَّىٰ أَتَانَا الْيَقِينُ ﴿٤٧﴾

47. Mpaka ikatujia yakini.

وَكُنَّا نُكَذِّبُ بِيَوْمِ الدِّينِ ﴿٤٦﴾

46. Basi hautawafaa uombezi wa waombezi.

حَتَّىٰ أَتَانَا الْيَقِينُ ﴿٤٧﴾

47. Basi wana nini wanapuuza ukumbusho huu?

فَمَا تَنفَعُهُمْ شَفَاعَةُ الشَّافِعِينَ ﴿٤٨﴾

48. Kama kwamba wao ni punda waliotimuliwa.

فَمَا لَهُمْ عَنِ التَّذْكِرَةِ مُعْرِضِينَ ﴿٤٩﴾

49. Basi wana nini hata wanapuuza onyo hili?

كَأَنَّهُمْ حُمُرٌ مُّسْتَنفِرَةٌ ﴿٥٠﴾

50. Kama kwamba wao ni mapunda walio timuliwa,

فَرَّتْ مِن قَسْوَرَةٍ ﴿٥١﴾

51. Wanaomkimbia simba!

بَلْ يُرِيدُ كُلُّ امْرِئٍ مِّنْهُمْ أَن يُؤْتَىٰ صُحُفًا مُّنَشَّرَةً ﴿٥٢﴾

52. Bali kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizo­funuliwa.

كَلَّا بَل لَّا يَخَافُونَ الْآخِرَةَ ﴿٥٣﴾

53. Sivyo! Bali hawaiogopi Akhera.

كَلَّا إِنَّهُ تَذْكِرَةٌ ﴿٥٤﴾

54. Sivyo! Kwa hakika hiyo ni ukumbusho.

فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ ﴿٥٥﴾

55. Basi atakaye ataukumbuka.

وَمَا يَذْكُرُونَ إِلَّا أَن يَشَاءَ اللَّـهُ هُوَ أَهْلُ التَّقْوَىٰ وَأَهْلُ الْمَغْفِرَةِ ﴿٥٦﴾

56. Na hawatakumbuka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu.

TUKIJIINGIZA PAMOJA NA WANAOJIINGIZA

Aya 32 – 56

MAANA

Na hawatakumbuka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu.

Sivyo! Komeni enyi washirikina kucheza na moto na kuwadharau walinzi wake.

Naapa kwa mwezi na kwa usiku unapokucha na kwa asubuhi inapopambazuka. Hakika huo ni mojawapo ya mambo makubwa.

Baada ya Mwenyezi Mungu kuwakemea wapinzani, sasa anaapa kwa mwezi, usiku na mchana kwamba Moto ni kweli isiyokuwa na shaka na ni adhabu ambayo haina mfano na hakuna adhabu nyingine inayoishinda hiyo. Kuapa kwa maumbile haya ni kuashiria kuwa wenye busara wanap­ata dalili ya mtengenezaji kutokana na ubunifu wa utengenezaji, na kwam­ba mwenye kufanya kitu bila ya chochote, anaweza kuipa uhai mifupa iliyochakaa.

Ni onyo kwa watu, kwa anayetaka miongoni mwenu kwenda mbele au kurudi nyuma.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amewahadharisha waja na moto na akawafa­hamisha njia yake na kuwambia jichagulieni wenyewe kuundea au kuwa mbali nao. amejitoa lawamani Mwenye kuonya.

Kila nafsi iko kwenye rahani kwa iliyoyachuma.

Hii ni sababu ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: Kwa anayetaka kwenda mbele au kurudi nyuma. Maana ni kuwa jichagulieni wenyewe, nyinyi mmefungika kwenye rahani ya mliyoyafanya na mna deni la mliyoyatanguliza; ikiwa ni heri basi mtalipwa heri na ikiwa ni shari basi ni shari. Umetangulia mfano wake katika Juz. 21 (30:44).

Isipokuwa watu wa kuliani.

Qur’an inawaita watu wa upande wa kulia wale wanaomcha Mungu na wakosefu inawaita watu wa upande wa kushoto, Tazama Juz. 27 (56: 8-9, 38-41).

Maana ni kuwa hakuna mtu yeyote ila nafsi yake inakuwa ni mateka wa matendo yake; isipokuwa wenye takua, wao wamelipa madeni yao na wamezifungua nafasi zao kwa matendo yao mema, na malipo yao ni Bustani za milele zinazopitiwa na mito.

Watakua katika mabustani wakiulizana kuhusiana na wakosefu: Ni kipi kilichowapeleka Motoni.

Baada ya kutulia watu wa Peponi wataulizana wenyewe kwa wenyewe: Wako wapi wakosefu waliokuwa wakitupa tabu?

Mwenyezi Mungu (s.w.t) atawaonyesha walipo katika Jahannam, ili wazi­di furaha, kama yalivyoeleza baadhi ya mapokezi.

Atawauliza kwa kuwatahayariza: ni jambo gani lililowapeleka kwenye makazi haya?Watasema kwa lugha ya hali au ya maneno:Hatukuwa miongoni mwa waliokuwa wakiswali . Yaani hatukuacha machafu na maovu duniani. Tafsiri hii tumeichukua katika kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ ﴿٤٥﴾

“Hakika Swala inakataza machafu na maovu.” Juz. 21 (29:45)

Wala hatukuwa tukiwalisha masikini, bali tulilimbikiza mali bila ya kuyatoa katika njia ya Mwenyezi Mungu.Na tulikuwa tukijiingiza pamoja na wanaojiingiza.

Makusudio ya kujiingiza hapa ni kupiga porojo. Maana ni kuwa tukidha­rau kila jambo isipokuwa upuzi na mchezo na tukijiingiza kila mahali isipokuwa kwenye haki na kheri.

Na tulikuwa tukikadhibisha siku ya hukumu, mpaka ikatujia yakini, yaani mauti.

Neno hukumu tumelifasiri kutokana neno Din. Sheikh Abdul-Qadir Al-Maghribi anasema: “Siku ya Kiyama imeitwa hivyo kwa sababu ndani yake mna malipo, hisabu na hukumu. Yote haya ni katika maana ya neno din. Vile vile inaitwa siku ya ufufuo, kuhukumiwa watu, mlipaji na hakimu.

Wamesema Ali bin Abi Twalib ni hakimu wa umma huu baada ya Nabii; yaani baada ya Nabii(s.a.w.w) yeye alikuwa na aina ya pekee ya kuhukumu baina ya mahasimu. ( kwa kutumia neno din kwa maana ya hukumu)”

Basi hautawafaa uombezi wa waombezi

Hakuna muombezi atakayefaa wala udhuru utakaokubalika, isipokuwa toba na matendo mema.

Basi wana nini wanapuuza ukumbusho huu; kama kwamba wao ni punda waliotimuliwa, wanaomkimbia simba.

Wanaambiwa washirikina, makusudio ya ukumbusho ni Qur’an na punda ni wa mwituni. Maana ni kuwa wananini hawa wanakimbia uongofu na haki kama wanaokimbia mauti?

Bali kila mmoja katika wao anataka apewe nyaraka zilizofunuliwa.

Kuna riwaya isemayo kuwa washirikina walimwambia Mtume wa Mwenyezi Mungu: “Hatutakuamini mpaka umteremshie kila mmoja wetu waraka usemao fulani bin fulani mfuate Muhammad(s.a.w.w) .”

Iwe sawa riwaya hii au la, lakini inafasiri dhahiri ya Aya. Hilo linatiliwa nguvu na Aya isemayo:

وَلَن نُّؤْمِنَ لِرُقِيِّكَ حَتَّىٰ تُنَزِّلَ عَلَيْنَا كِتَابًا نَّقْرَؤُهُ ﴿٩٣﴾

“Na hatutaamini kupaa kwako mpaka ututeremshie Kitabu tukisome.” Juz. 15 (17:93).

Lakini wao hawawezi kuamini hata kama wangeliitikiwa matakwa yao, kama ilivyoliweka wazi hilo kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَلَوْ نَزَّلْنَا عَلَيْكَ كِتَابًا فِي قِرْطَاسٍ فَلَمَسُوهُ بِأَيْدِيهِمْ لَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا إِنْ هَـٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ﴿٧﴾

“Na lau tungelikuteremshia maandishi katika karatasi na wakayagusa kwa mikono yao, bila shaka wale waliokufuru wangelisema: Haya si chochote ila ni uchawi dhahiri.” Juz. 7 (6:7).

Siri katika hilo ni kupupia kwao masilahi yao na mambo yao na wala sio hasadi, kama walivyosema baadhi ya wafasiri. Dalili ya hayo tuliyoyasema ni kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu iliyokuja moja kwa moja:Sivyo! Bali hawaiogopi Akhera . kwa sababu wao hawajui isipokuwa maisha ya dunia wala hawategemei isipokuwa anasa zake na starehe. Ama ubinadamu, haki na heri kwao ni maneno yasiyokuwa na maana.

Sivyo! Kwa hakika hiyo ni ukumbusho.

Mara nyingine tena Mwenyezi Mungu (s.w.t) anawakemea wakadhibisha­ji na kuwabainishia kuwa hii Qur’an ni mawaidha kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwenda kwa waja wake na wala sio kauli ya mchawi wala mshairi.

Basi atakaye ataukumbuka.

Yaani atanufaika na hukumu zake na mawaidha yake.

Na hawatakumbuka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu.

Unaweza kuuliza : Kauli yake Mwenyezi Mungu: ‘atakaye ataukumbuka,’ inaonyesha kuwa mtu ana hiyari ya uhuru wake na utashi wake. Na kauli hii ‘Hawatakumbuka isipokuwa atake Mwenyezi Mungu,’ inaonyesha kuwa mtu hana hiyari, anaendeshwa na hana uhuru wala utashi; sasa ni vipi mgongano huu?

Jibu : Makusudio ya matakwa ya kwanza, ni kwamba Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemwachia mtu hiyari ya kujichagulia imani au ukafiri. Na makusudio ya ya matakwa ya pili ni kuwa mpinzani anayekana hawezi kuamini mpaka Mwenyezi Mungu amlazimishe kwa nguvu. Kwa hiyo maana ya kauli mbili ni kuwa Mwenyezi Mungu amemwamchia mtu hiyari ya kuamini au kukufuru; kama isemwavyo kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَقُلِ الْحَقُّ مِن رَّبِّكُمْ فَمَن شَاءَ فَلْيُؤْمِن وَمَن شَاءَ فَلْيَكْفُرْ ﴿٢٩﴾

“Sema hii ni kweli itokayo kwa Mola wenu, basi atakaye aamini na atakaye akufuru.”

Juz. 15 (18:29).

Lakini mpinzani mwenye inadi hawezi, kwa hali yoyote ile, ila akifany­ishwa kwa nguvu na Mwenyezi Mungu; na hili haliwezi kuwa kabisa, kwa vile linapingana na uadilifu wa Mwenyezi Mungu na hikima yake. Kwa sababu uadilifu wake Mwenyezi Mungu Mtukufu na desturi yake kwa waja wake, ni kuwabainishia njia ya heri na kuwahimiza na kuwabinishia njia ya shari na kuwahadharisha nayo.

Kwa hiyo kila mmoja anakuwa na hiyari yeye mwenyewe ya mwishilio wake; vinginevyo thawabu na adhabu zitakua hazina maana yoyote.

Hili linaungwa mkono na kauli yake Mwenyezi Mungu iliyokuja moja kwa moja:

Takua ni kwake na maghufira ni yake.

Yaani yeye Mwenyezi Mungu ambaye imetukuka hikima yake, ndiye anayestahiki kutiiwa katika maamrisho yake na makatazo yake, na kuogopewa kwa ghadhabu yake na adhabu yake. Vile vile yeye ndiye mwenye kuwahurumia waja na kuwasamehe wanao­tubia na kurejea.

Kwa mnaeno machache na ya uwazi zaidi ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) amemuumba mtu akiwa na hiyari, mwenye akili na utashi, akamto­fautisha na mnyama kwa hilo; kwa hiyo akamkalifisha utiifu na msimamo. Kama angelitaka Mwenyezi Mungu angelimuondolea utashi wa akili na kumfanya kama mnyama au chini yake zaidi.

MWISHO WA SURA YA SABINI NA NNE: SURAT AL- MUDDATHIR