TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Juzuu 24

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE12%

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Mwandishi:
: HASANI MWALUPA
Kundi: Qurani tukufu

Juzuu 1 Juzuu 2 Juzuu 3 Juzuu 4 Juzuu 5 Juzuu 6 Juzuu 7 Juzuu 8 Juzuu 12 Juzuu 13 Juzuu 14 Juzuu 15 Juzuu 16 Juzuu 17 Juzuu 18 Juzuu 19 Juzuu 20 Juzuu 21 Juzuu 22 Juzuu 23 Juzuu 24
  • Anza
  • Iliyopita
  • 30 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 28951 / Pakua: 5121
Kiwango Kiwango Kiwango
TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE Juzuu 24

Mwandishi:
Swahili

1

9

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Sura Ya Sitini Na Tatu: Surat Al- Munafiqun. Imeshuka Madina. Ina Aya 11.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

ذَا جَاءَكَ الْمُنَافِقُونَ قَالُوا نَشْهَدُ إِنَّكَ لَرَسُولُ اللَّـهِ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ إِنَّكَ لَرَسُولُهُ وَاللَّـهُ يَشْهَدُ إِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَكَاذِبُونَ ﴿١﴾

1. Wanapokujia wanafiki huse­ma: Tunashuhudia ya kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa hakika wewe ni Mtume wake. Na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa hakika wanafiki ni waongo.

اتَّخَذُوا أَيْمَانَهُمْ جُنَّةً فَصَدُّوا عَن سَبِيلِ اللَّـهِ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿٢﴾

2. Wamevifanya viapo vyao ni kinga, na wao wakajizuia kuifuata Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika ni mabaya waliyokuwa wakiyafanya.

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ آمَنُوا ثُمَّ كَفَرُوا فَطُبِعَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمْ فَهُمْ لَا يَفْقَهُونَ ﴿٣﴾

3. Hayo ni kwa sababu ya kuwa waliamini, kisha wakakufuru; kwa hivyo umepigwa muhuri juu ya nyoyo zao nao hawafahamu.

وَإِذَا رَأَيْتَهُمْ تُعْجِبُكَ أَجْسَامُهُمْ وَإِن يَقُولُوا تَسْمَعْ لِقَوْلِهِمْ كَأَنَّهُمْ خُشُبٌ مُّسَنَّدَةٌ يَحْسَبُونَ كُلَّ صَيْحَةٍ عَلَيْهِمْ هُمُ الْعَدُوُّ فَاحْذَرْهُمْ قَاتَلَهُمُ اللَّـهُ أَنَّىٰ يُؤْفَكُونَ ﴿٤﴾

4. Na unapowaona, miili yao inakupendeza, na wakisema, unasikiliza usemi wao. Kama kwamba wao ni magogo yaliy­oegemezwa. Wao hudhania kila ukelele ni kwa ajili yao. Hao ni maadui; jihadhari nao.

وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْا يَسْتَغْفِرْ لَكُمْ رَسُولُ اللَّـهِ لَوَّوْا رُءُوسَهُمْ وَرَأَيْتَهُمْ يَصُدُّونَ وَهُم مُّسْتَكْبِرُونَ ﴿٥﴾

5. Na wanapoambiwa: Njooni ili Mtume wa Mwenyezi Mungu awaombee maghufira, huvigeuza vichwa vyao, na unawaona wanageuka nao wamejaa kiburi.

سَوَاءٌ عَلَيْهِمْ أَسْتَغْفَرْتَ لَهُمْ أَمْ لَمْ تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ لَن يَغْفِرَ اللَّـهُ لَهُمْ إِنَّ اللَّـهَ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴿٦﴾

6. Ni sawa kwao, ukiwatakia maghufira au usiwatakie maghufura, Mwenyezi Mungu hatawaghufiria. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu mafasiki.

HAO NI MAADUI JIHADHARI NAO

Aya 1-6

MAANA

Qur’an imewasifia maswahaba na jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu na ikawasifia kwa nguvu daraja zao na vyeo vyao. Vile vile imezungumzia aina za wanafiki katika sura kadhaa na jinsi walivyong’ang’ania kuufanyia vitimbi Uislamu na manabii wake. Masimulizi kuhusiana na wanafiki hayana ukomo, kwa sababu uwongo wao na mbinu zao chafu hazina mpaka.

Kwa hiyo si ajabu kukaririka masimulizi yao, na Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwahusisha na sura kamili katika Kitabu chake na kuwasi­fia kwa sifa mbaya; miongoni mwazo ni hizi zifuatazo:-

Wanapokujia wanafiki husema: Tunashuhudia ya kuwa wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu anajua kuwa hakika wewe ni Mtume wake.

Walidhamiria kumkufuru Mwenyezi Mungu na kumfanyia uadui Nabii wake mtukufu, wakadhihirisha mapenzi na imani kwake na kwa risala yake.

Na Mwenyezi Mungu anashuhudia ya kuwa hakika wanafiki ni waongo.

Makusudio ya kushuhudia kwake Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni kujua. Maana ni kuwa wanafiki wanasema kwa ndimi zao yale yasiyo nyoyoni mwao; na Mwenyezi Mungu anajua wanayoyaficha na wanayoyadhi­hirisha naye anawangojea tu.

Vile vile Nabii anajua hakika yao, lakini ameamrishwa kuwachukulia kwa dhahiri na sio kwa uhalisia; akasema: “Nimeamriwa kupigana na watu mpaka waseme: Lailahaillallah Muhammadur-rasurullah. (Hapana Mola isipokuwa Mwenyezi Mungu) wakishasema basi imehifadhika nami damu zao na mali zao, isipokuwa kwa haki yake, na hisabu yao iko kwa Mwenyezi Mungu.”

Ufasaha zaidi niliousoma kuhusiana na maudhui haya ni kauli ya Imam Ali(a.s ) :“Ulimi wa mumin uko nyuma ya moyo wake na moyo wa mnafiki uko nyuma ya ulimi wake.” Yaani ulimi wa mumin unafuata moyo wake, hasemi isipokuwa analoliamini. Lakini mnafiki moyo wake unafuata ulimi wake na ulimi wake unazunguka na hawaa yake na malengo yake. Natija ya hayo ni kuwa mnafiki hana moyo isipokuwa hawa na matamanio.

Wamevifanya viapo vyao ni kinga, na wao wakajizuia kuifuata Njia ya Mwenyezi Mungu.

Mara nyingi njama za wanafiki zilikuwa zikifichuka, nao kila walipokuwa wakizungumza wanafanya kiapo ndio kinga yao kuzuia kughadhibikiwa na Mtume(s.a.w. w ) na kuficha njama zao dhidi ya Mtume na upinzani wao kwa risala yake.

Hakika ni mabaya waliyokuwa wakiyafanya ya vitimbi, hadaa na kuwa vigeugeu.

Hayo ni kwa sababu ya kuwa waliamini, kisha wakakufuru; kwa hivyo umepigwa muhuri juu ya nyoyo zao nao hawafahamu lolote.

Makusudio ya waliamini ni kuwa walijulikana na watu kwamba wameami­ni. Vinginevyo ni kuwa wao hawakuwahi kuamini hata chembe. Na makusudio ya wakakufuru ni kujulikana kuwa kumbe walidhihirisha imani na wakaficha ukafiri. Ama makusudio ya kupigwa muhuri juu ya nyoyo zao ni kuwa hawaongoki kwenye heri baada ya kupofushwa na hawaa na upotevu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 5 (4:137).

Na unapowaona, miili yao inakupendeza , Wana mandhari mazuri na hisia mbaya. Kwa ibara ya Imam Ali(a.s ) :“Nyoyo zao zina maradhi na nyuso zao ni safi.”

Na wakisema, unasikiliza usemi wao , kwa sababu wanazungumza maneno ya wenye ikhlasi na wanaizungumzia dunia kwa maneno ya wenye zuhudi.

Kama kwamba wao ni magogo yaliyoegemezwa . Ni mfano wa magogo, lakini wanakula na kunywa. Kila mwenye kupofu­ka na uongofu, basi ni maiti hai.

Wao hudhania kila ukelele ni kwa ajili yao. Hao ni maadui; jihadhari nao.

Wana roho za woga wa kufichuka siri zao, hawasikii sauti ila wanadhani ni sauti ya adhabu itakayowanyakuwa bila ya kujua. Woga huu ume­wazidishia lawama na uadui kwenu enyi wenye ikhlasi, basi jihadharini na njama zao na msiwape fursa kadiri mtakavyoweza.

Mwenyezi Mungu awaangamizilie mbali! Vipi wanageuzwa?

Hii ni shutuma kwa tamko la kuduia na kushangaa. Maana ni kuwa wao wamelaaniwa kwa vile wameiacha haki kwa inadi na jeuri.

Kila sifa walizosifiwa wanafiki wakati wa Mtume(s.a.w. w ) ni sura iliyoko kwa vibaraka wa leo wanaokula njama na maadui wa Mwenyezi Mungu na wa nchi kwa kuufanyia vitimbi uma wao.

Hakuna hatia kubwa kama kuufanyia hiyana uma, na hakuna fedheha kama mtu kumuuza mtu mwenzake.

Na wanapoambiwa: Njooni ili Mtume wa Mwenyezi Mungu awaombee maghufira, huvigeuza vichwa vyao, na unawaona wanageuka nao wamejaa kiburi.

Mtu akiwanasihi na kuwaambia tubieni mliyo nayo na Mwenyezi Mungu atawaghufiria, basi wao wanag’ang’ania batili na kuipinga haki, waki­inamisha vichwa vyao kwa dharau na kiburi. Kwa vile wao ni wakubwa kuliko wanayoyahitajia kwa Mtume; kama wanavyodai.

Ni sawa kwao, ukiwatakia maghufira au usiwatakie maghufira, Mwenyezi Mungu hatawaghufiria.

Hakuna faida ya kuwataka watengenee; kwa hiyo hakuna haja ya kuwatakia maghufira.

Ni kweli Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira mwenye kurehemu, hilo halina shaka, na rehema ya Mwenyezi Mungu ni yenye kuenea katika kila kitu, isipokuwa kwa mwenye kuikataa na akaifanyia kiburi. Kwa hiyo itakuwa si huruma kumfanyia yule anayeona kuwa haihitajii huruma yako.

Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu mafasiki , maadamu wanang’ang’ania ufuska.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 10 (9: 80).

هُمُ الَّذِينَ يَقُولُونَ لَا تُنفِقُوا عَلَىٰ مَنْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ حَتَّىٰ يَنفَضُّوا وَلِلَّـهِ خَزَائِنُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَفْقَهُونَ ﴿٧﴾

7. Hao ndio wanaosema: Msitoe kwa ajili ya walioko kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, ili wawaondokee. Na hazina za mbingu na ardhi ni za Mwenyezi Mungu, lakini wanafiki hawafahamu.

يَقُولُونَ لَئِن رَّجَعْنَا إِلَى الْمَدِينَةِ لَيُخْرِجَنَّ الْأَعَزُّ مِنْهَا الْأَذَلَّ وَلِلَّـهِ الْعِزَّةُ وَلِرَسُولِهِ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَعْلَمُونَ ﴿٨﴾

8. Wanasema: Tukirejea Madina mwenye utukufu zaidi bila ya shaka atamfukuza aliye mnyonge. Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye utukufu Yeye, na Mtume wake, na Waumini. Lakini wanafiki hawajui.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّـهِ وَمَن يَفْعَلْ ذَٰلِكَ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ ﴿٩﴾

9. Enyi mlioamini! Zisiwa­shughulishe mali zenu, wala watoto wenu, kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Na wenye kufanya hayo ndio wenye hasara.

وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَىٰ أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ ﴿١٠﴾

10. Na toeni katika tulichowapa kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti, kisha aseme: Mola wangu! Mbona hukuni­akhirishia muda kidogo nika­toa sadaka, na kuwa katika watu wema?

وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّـهُ نَفْسًا إِذَا جَاءَ أَجَلُهَا وَاللَّـهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١١﴾

11. Wala Mwenyezi Mungu hata­iakhirisha nafsi yoyote inapofika ajali yake; na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda.

MWENYE NGUVU ATAMFUKUZA MNYONGE

Aya 7 – 11

MAANA

Hao ndio wanaosema: Msitoe kwa ajili ya walioko kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, ili wawaondokee.

Wanaosema ni wanafiki na walioko kwa Mtume ni wahajiri walio mafukara. Matajiri wa Kianswar walikuwa wakiwasaidia hawa, ndio wanafiki wakawaambia matajiri msitoe mali zenu kwa muhajiri yoyote ili wapate kuona vibaya waweze kuondoka. Ndio Mwenyezi Mungu (s.w.t) akawarudi kwa kuwaambia:

Na hazina za mbingu na ardhi ni za Mwenyezi Mungu, lakini wanafiki hawafahamu.

Mnawaamuru ubahili wale waliomwamini Mwenyezi Mungu na wakafanya juhudi katika njia yake, na hali Mwenyezi Mungu ndiye muumba wa viumbe na ndiye anayevimiliki pamoja na mali zao na ndiye mwenye kuviruzuku! Yeye anaweza kuwatajirisha waumini kwa fadhila yake, lakini nyinyi hamjui.

Wanasema: Tukirejea Madina mwenye utukufu zaidi bila ya shaka atamfukuza aliye mnyonge.

Wafasiri wamesimulia kisa cha Aya hii kinachohusiana na kiongozi wa wanafiki Abdallah bin Ubayya na vita vya Bani Mustaliq.

Hawa walikuwa ni sehemu ya Khuza’a na walikuwa wakiishi karibu na Makka. Waliona kuwa Uislamu utakuwa na nguvu katika Bara Arabu, hivyo wakajiandaa kupigana vita na Mtume(s.a.w.w) wakiongozwa na kiongozi wao Harith bin Abu Dhirar. Mtume(s.a.w.w) alipojua hilo akaharakisha kuwatokea na jeshi lake kabla ya wao kufika Madina.

Ibn Ubayya naye akatoka pamoja na jeshi la waislamu kwa tamaa ya ngawira. Basi Mwenyezi Mungu akampa ushindi Mtume wake dhidi ya maadui zake, wakapata mali nyingi ya ngawira. Mtume(s.a.w.w)

akawaongezea mafukara wahajiri katika ngawira ili kupunguza pengo baina ya mafukara na matajiri. Ibn Ubayya akaona vibaya, akawa anawa­chochea Answar; miongoni mwa aliyoyasema ni: “Tukirejea Madina mwenye utukufu zaidi bila ya shaka atamfukuza aliye mnyonge.”

Mtukufu anajikusudia yeye mwenyewe na mnyonge anamkusudia Mtume(s.a.w.w) . Ndio ikashuka Aya hii na Ibn Ubayya akafedheka. Wafasiri wengi wamesema kuwa Ibn Ubayya alisema neno hili la kufuru kutokana na mzozo uliotokea baina ya mmoja wa wafuasi wake na mfanyakazi wa Umar bin Al-Khattab.

Abdallah bin Ubayya alikuwa na mtoto mwema aliyekuwa akiitwa Abdallah pia. Alipojua kuhusu baba yake, alimwendea Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) na kumwambia: “Umekwishajua alivyofanya baba yangu. Ukiwa unataka kumuua basi niamuru mimi nimuue, ili nisije nikashindwa kujizuia kumuona aliyemuua baba yangu, nikamuua mumin kwa sababu ya kafiri, nikaingia motoni.”

Mtume(s.a.w.w) akamjibu:“Tutamuhurumia baba yako na tutaishi naye kwa wema muda ule atakaobakia nasi.”

Na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye utukufu -Yeye, na Mtume wake, na Waumini.

Hii ni kumrudi Ibn Ubayya aliyejisifu kuwa mtukufu zaidi. Utukufu wa Mwenyezi Mungu (s.w.t) ni kuwa yeye ndiye mtukufu zaidi kwa waja wake, utukufu wa Mtume ni dini yake kushinda dini nyingine zote na kuwashinda maadui zake, na utukufu wa waumini ni kushinda haki na watu wake.

Lakini wanafiki hawajui kwamba utukufu ni kwa imani na takua. Enyi mlioamini! Zisiwashghulishe mali zenu, wala watoto wenu, kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Na wenye kufanya hayo ndio wenye hasara.

Mwenye kuitaamali Aya hii na ile iliyo kabla yake ataona kuwa makusudio ya kumkumbuka Mwenyezi Mungu hapa ni jihadi.

Kwa sababu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwanza ametaja utukufu wake, wa Mtume na wa waumini; kisha akawakataza na kuwahadharisha waumini, dunia isiwasahaulishe kumkumbuka Mwenyezi Mungu na akajaalia natija ya hayo ni hizaya na udhalili duniani na Akhera.

Hakuna mwenye shaka kwamba hizaya na udhalili ni natija ya kuipenda dunia na kuhofia jihadi na mauti. Hakuna linalosadikisha hakika hii kuliko maisha ya waislamu na waarabu hivi sasa jinsi yalivyo.

Na toeni katika tulichowapa kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti, kisha aseme: Mola wangu! Mbona hukuniakhirishia muda kidogo nikatoa sadaka, na kuwa katika watu wema?

Makusudio ya kufikiwa na mauti ni kudhihiri alama zake na utangulizi wake. Maana ni kuwa chukueni fursa ya kutoa kile alichowapa Mwenyezi Mungu. Na mwenye kupuuza akangoja mpaka siku zake za mwisho mwisho atauma vidole kwa kujuta na kumnyenyekea Mwenyezi Mungu ampe muda kidogo, lakini wapi! Yaliyopita hayarudi.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (14:44).

Wala Mwenyezi Mungu hataiakhirisha nafsi yoyote inapofika ajali yake; na Mwenyezi Mungu ana habari za mnayoyatenda.

Ajali imekwishaamriwa haiwahi wala haichelewi. Mwenye kupoteza fursa hana jingine isipokuwa hasara na majuto. Umetangulia mfano wake katika Juz. 4 (3:145) kifungu cha ‘Ajali haina kinga.’ Na Juz. 8 (7:34).

MWISHO WA SURA YA SITINI NA TATU: SURAT AL- MUNAFIQUN

10

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA ISHIRINI NA NNE

Sura Ya Sitini Na Nne: Surat At – Taghabun. Imeshuka Madina Ina Aya 18.

بِسْمِ اللَّهِ الرَّحْمَٰنِ الرَّحِيمِ

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa rehema Mwenye kurehemu.

يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ ﴿١﴾

1. Vinamsabihi vilivyo katika mbingu na vilivyo katika ardhi, Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake. Na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu

هُوَ الَّذِي خَلَقَكُمْ فَمِنكُمْ كَافِرٌ وَمِنكُم مُّؤْمِنٌ وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ بَصِيرٌ ﴿٢﴾

2. Yeye ndiye Aliyewaumba. Miongoni mwenu yupo aliye kafiri, na yupo aliye Muumini. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ بِالْحَقِّ وَصَوَّرَكُمْ فَأَحْسَنَ صُوَرَكُمْ وَإِلَيْهِ الْمَصِيرُ ﴿٣﴾

3. Ameziumba mbingu na ardhi kwa haki, na akawapa sura, na akazifanya nzuri sura zenu Na marejeo ni kwake.

يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَيَعْلَمُ مَا تُسِرُّونَ وَمَا تُعْلِنُونَ وَاللَّـهُ عَلِيمٌ بِذَاتِ الصُّدُورِ ﴿٤﴾

4. Anajua vilivyomo mbinguni na ardhini, na anajua mnayoy­afanya siri na mnayoy­atangaza. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani.

أَلَمْ يَأْتِكُمْ نَبَأُ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَبْلُ فَذَاقُوا وَبَالَ أَمْرِهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ ﴿٥﴾

5. Kwani haikuwajia habari ya waliokufuru kabla, wakaonja ubaya wa mambo yao? Na wao wana adhabu iliyo chungu.

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُ كَانَت تَّأْتِيهِمْ رُسُلُهُم بِالْبَيِّنَاتِ فَقَالُوا أَبَشَرٌ يَهْدُونَنَا فَكَفَرُوا وَتَوَلَّوا وَّاسْتَغْنَى اللَّـهُ وَاللَّـهُ غَنِيٌّ حَمِيدٌ ﴿٦﴾

6. Hayo ni kwa kuwa walikuwa wakiwajia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, nao wakase­ma: Hivi binadamu ndio atuongoze? Basi wakakufuru, na wakageuka upande. Mwenyezi Mungu si muhitaji. Na Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, naye ni Msifiwa.

MIONGONI MWENU KUNA KAFIRI NA MUUMIN

Aya 1 – 6

MAANA

Vinamsabihi vilivyo katika mbingu na vilivyo katika ardhi.

Baadhi ya viumbe vinamsabihi kwa lugha ya maneno na vingine kwa lugha ya hali. Umetangulia mfano wake katika Juzuu hii tuliyonayo, mwanzo wa sura 62.Ufalme ni wake, humpa amtakaye na humvua amtakaye.

Na sifa njema ni zake. Kwa utukufu wa ihsani yake na uangavu wa dalili zake.Na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu bila ya nyenzo wala kufikiria, bali ni kwa neno ‘kuwa.’

Yeye ndiye Aliyewaumba. Miongoni mwenu yupo aliye kafiri, na yupo aliye Muumini. Na Mwenyezi Mungu anayaona mnayoyatenda.

Mtu katika mtazamo wa kiislamu ni kwa uhuru wake na utashi wake. Hakuna utu bila ya uhuru. Anayo hiyari ya kuchagua imani hata kama wazazi wake ni makafiri, na ana hiyari ya kuchgua ukafiri hata kama wazazi wake ni waumini; wala haifai kabisa yeyote kumlazimisha mwingine - hakuna kulazimishana katika dini; vinginevyo taklifa, hisabu na thawabu zitakuwa ni batili.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kumpa mja wake uhuru, unaomfanya kuwa mtu, akamwamuru kufuata imani na kufanya heri na akamkataza ukafiri na kufanya shari, akamwekea dalili za uzuri wa aliyomwamrisha na ubaya wa aliyomkataza; kutokana na akili yake na maumbile yake. Wakaamini baadhi ya watu na wakakufuru waliokufuru; na kila mmoja atapata thawabu au adhabu kulingana na imani na matendo yake.

Ameziumba mbingu na ardhi kwa haki,

Yaani kwa hikima ya hali ya juu; wala hakuna chochote katika ulimwengu huu kilichoko kwa mchezo, wala hakuna tofauti baina ya kusema kuwa vitu vimepatikana kwa sadfa na kusema kuwa kila kitu, hata nidhamu, kimejileta chenyewe.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 14 (16:3).

Na akawapa sura, na akazifanya nzuri sura zenu.

Msanii anaweza kutengeneza sura ya chochote na kwa ufundi na ustadi wa hali ya juu, lakini kazi yake kubwa inakuwa ni kupamba na kuweka shepu tu; sawa na mjengaji anayeweka jiwe juu ya jiwe jingine, lakini nyenzo za ujenzi na kutengeneza sura inatoka kwa anayekiambia kitu kuwa na kikawa.

Mwenyezi Mungu aliiumba mada ya mtu kwa neno ‘kuwa’ akaitia sura zaidi kuliko viumbe vingine. Umetangulia mfano wake katika Juz. 18 (23:14)

Na marejeo ni kwake awambie mliyokuwa mkiyafanya, na mwenye kuepushwa na moto atakuwa amefuzu.

Anajua viliomo mbinguni na ardhini, na anajua mnayoyafanya siri na mnayoyatangaza. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa yaliomo vifuani. Maana yako wazi. Kwa ufupi ni kuwa Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.

Kwani haikuwajia habari ya walio kufuru kabla, wakaonja ubaya wa mambo yao? Na wao wana adhabu iliyo chungu.

Swali ni la kutahayariza, na maneno yanaelekezwa kwa washirikina waliomkufuru Muhammad(s.a.w. w ) na wakatangaza vita naye na mwito wake. Amewakumbusha Mwenyezi Mungu yaliyowapata waliokuwa kabla yao; kama vile kaumu ya Nuh, A’d na Thamud - waliwakadhibisha mitume yakawasibu maangamizi duniani na adhabu ya Akhera ni kali zaidi na ya kufedhesha.

Hayo ni kwa kuwa walikuwa wakiwajia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, nao wakasema: Hivi binadamu ndio atuongoze? Basi wakakufu­ru, na wakageuka upande.

‘Hayo’ ni ishara ya adhabu iliyowafika uma zilizopita kwa vile wali­wakadhibisha mitume. Waliwajia na dalili mkataa juu ya utume wao, lakini bado wao waling’ang’ania kufuru, si kwa lolote ila ni kuwa mitume ni watu kama wao watawaongozaje!

Hawajui kuwa uongozi unatokana na ilimu? Ajabu ni kuwa walipopewa mwito wa tawhid walisema ‘mtu kama sisi atuongoze?’ lakini hawakumwambia hivi aliyewaita kwenye ibada ya mawe, bali walimsikiliza na kumtii bila ya ubishi. Hili si la kushangaza, ndio tabia ya ujinga.

Kadiri nitakavyotia shaka, lakini siwezi kutia shaka kuwa wenye busara lau watahiyarishwa baina ya upofu pamoja na ilimu, na ujinga pamoja na uoni, basi wangelichagua upofu, kwa sababu hauwezi kulikaribisha la mbali wala kulibaidisha la karibu, wala hausawirishi weusi kuwa weupe au weupe kuwa weusi. Lakini ujinga unasawirisha uongofu kuwa ni upotevu, upotevu kuwa uongofu, haki kuwa batili na batili kuwa haki.

Mwenyezi Mungu si muhitaji. Na Mwenyezi Mungu ni Mkwasi, naye ni Msifiwa.

Kila kilichoko kinashuhudia kwa lugha ya maneno na lugha ya hali kuwa Mwenyezi Mungu hawahitajii viumbe na utiifu wao, mwenye kusifiwa katika sifa zake zote na vitendo vyake.

زَعَمَ الَّذِينَ كَفَرُوا أَن لَّن يُبْعَثُوا قُلْ بَلَىٰ وَرَبِّي لَتُبْعَثُنَّ ثُمَّ لَتُنَبَّؤُنَّ بِمَا عَمِلْتُمْ وَذَٰلِكَ عَلَى اللَّـهِ يَسِيرٌ ﴿٧﴾

7. Waliokufuru wanadai kuwa hawatafufuliwa. Sema: Kwani? Naapa kwa Mola wangu! Hapana shaka mtafu­fuliwa, na kisha hapana shaka mtaambiwa mliyoyatenda. Na hayo ni mepesi kwa Mwenyezi Mungu.

فَآمِنُوا بِاللَّـهِ وَرَسُولِهِ وَالنُّورِ الَّذِي أَنزَلْنَا وَاللَّـهُ بِمَا تَعْمَلُونَ خَبِيرٌ ﴿٨﴾

8. Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Nuru tuliyoiteremsha. Na Mwenyezi Mungu kwa mnay­oyatenda anazo habari.

يَوْمَ يَجْمَعُكُمْ لِيَوْمِ الْجَمْعِ ذَٰلِكَ يَوْمُ التَّغَابُنِ وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ وَيَعْمَلْ صَالِحًا يُكَفِّرْ عَنْهُ سَيِّئَاتِهِ وَيُدْخِلْهُ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا أَبَدًا ذَٰلِكَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ﴿٩﴾

9. Siku atakayowakusanya kwa ajili ya Siku ya Mkusanyiko; hiyo ni siku ya hasara. Na anayemwamini Mwenyezi Mungu na akatenda mema, atamfutia maovu yake, na atamuingiza katika Bustani zipitiwazo na mito chini yake, watadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa.

وَالَّذِينَ كَفَرُوا وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا أُولَـٰئِكَ أَصْحَابُ النَّارِ خَالِدِينَ فِيهَا وَبِئْسَ الْمَصِيرُ ﴿١٠﴾

10. Na waliokufuru na waka­ kadhibisha Ishara zetu, hao ni watu wa Motoni, watadumu humo milele. Na hayo ndiyo marudio mabaya.

مَا أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ إِلَّا بِإِذْنِ اللَّـهِ وَمَن يُؤْمِن بِاللَّـهِ يَهْدِ قَلْبَهُ وَاللَّـهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ ﴿١١﴾

11. Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu. Na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu huuongoza moyo wake. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

وَأَطِيعُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ فَإِن تَوَلَّيْتُمْ فَإِنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا الْبَلَاغُ الْمُبِينُ ﴿١٢﴾

12. Na mtiini Mwenyezi Mungu, na mtiini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha kwa uwazi tu.

اللَّـهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا هُوَ وَعَلَى اللَّـهِ فَلْيَتَوَكَّلِ الْمُؤْمِنُونَ ﴿١٣﴾

13. Mwenyezi Mungu, hapana mungu isipo kuwa Yeye. Na juu ya Mwenyezi Mungu nawategemee Waumini.

HII NI SIKU YA HASARA

Aya 7-13

MAANA

Waliokufuru wanadai kuwa hawatafufuliwa. Sema: Kwani? Naapa kwa Mola wangu! Hapana shaka mtafufuliwa, na kisha hapana shaka mtaambiwa mliyo yatenda. Na hayo ni mepesi kwa Mwenyezi Mungu.

Tumebainisha njia ya Qur’an katika ufufuo na kuzirudi shaka shaka za wakanushaji na kwamba mwenye kufanya kitu bila ya mali ghafi basi ni rahisi zaidi kwake kuvikusanya viungo baada ya kutawanyika kwake. Tumefafanua kwa mifumo mbali mbali katika kufasiri Aya za ufufuo; kama vile Juz. 11 (10:4) ‘Hisabu na malipo ni lazima.’

Unaweza kuuliza : Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) alitoa mwito wa ufufuo kwa kiapo wakampinga waabudu masanamu; na kimsingi ni kuwa ushahidi ni wa mwenye kudai na kiapo ni cha mwenye kupinga. Msingi huu ni wa kibinadamu uliokubaliwa na sharia zote. Kwa hiyo basi Mtume(s.a.w. w ) anatakiwa alete ushahidi, sio aape. Sasa je, kuna wajihi gani wa Mtume kuleta kiapo na alitakiwa alete hoja za kuwanyamazisha. Je ufufuo utathibitika kwa kuapa tu?

Jibu : Kwanza, Mwenyezi Mungu (s.w.t) anasimulia kuwa wakanushaji hapa walimwuliza Mtume kuhusu ufufuo kama wenye kuchunguza sio wenye kujadiliana; hawakusema:

مَن يُحْيِي الْعِظَامَ وَهِيَ رَمِيمٌ ﴿٧٨﴾

“Ni nani atakayeiuisha mifupa nayo imemung’unyika?” Juz. 23 (36:78).

Au kusema:

أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ﴿١٦﴾

“Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?” Juz. 23 (37:16).

Kwa kuwa, katika Aya tuliyo nayo, wakanushaji walitosheka na kuuliza tu, sio kushangaa na kujadiliana, basi Mwenyezi Mungu na Mtume wake wametosheka na kujibu tu pamoja na msisitizo wa kiapo.

Ndio maana pale waliposema: ‘Ni nani atakayeihuisha mifupa nayo imemung’unyika,” aliwaambia: “Ataihuisha yule Alieiumba mara ya kwanza. Na Yeye ni mjuzi wa kila jambo.” Jibu linakuja kulingana na swali.

Pili , wale waliokufuru pamoja na wanafiki walikuwa wakiamini kuwa Mtume(s.a.w. w ) hawatakii heri wala masilahi; isipokuwa anataka kujituku­za na kuwa juu yao; kama walivyoamini makafiri, hapo kabla, kwa Nabii Nuh:

فَقَالَ الْمَلَأُ الَّذِينَ كَفَرُوا مِن قَوْمِهِ مَا هَـٰذَا إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُكُمْ يُرِيدُ أَن يَتَفَضَّلَ عَلَيْكُمْ ﴿٢٤﴾

“Wakasema wale wakuu waliokufuru: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi, anataka kujipatia ubora juu yenu.” Juz. 18 (23:24).

Ndio akaapa Mtume kwamba mwito wake ni wa haki; akimaanisha kuwa hataki isipokuwa haki tu. Mfano wake ni kauli ya Shu’ayb kwa watu wake walipomdhania mabaya:

إِنْ أُرِيدُ إِلَّا الْإِصْلَاحَ مَا اسْتَطَعْتُ وَمَا تَوْفِيقِي إِلَّا بِاللَّـهِ ﴿٨٨﴾

“Sitaki ila kutengeneza kiasi ninavyoweza. Na tawfiki yangu haiko ila kwa Mwenyezi Mungu.” Juz. 12 (11:88).

Basi muaminini Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na Nuru tuliyoiteremsha.

Maadamu ufufuo ni haki na hisabu na malipo ni haki, basi ni juu ya kila mtu kumwamini Mwenyezi Mungu na Mtume wake na nuru; yaani Qur’an. Ameisifu kuwa ni nuru kwa vile inamtoa mtu kwenye giza la ujinga na kufuru kumpeleka kwenye nuru ya ilimu na imani na kumwongoza kwenye njia ya salama:

قَدْ جَاءَكُم مِّنَ اللَّـهِ نُورٌ وَكِتَابٌ مُّبِينٌ ﴿١٥﴾ سُبُلَ السَّلَامِ وَيُخْرِجُهُم مِّنَ الظُّلُمَاتِ إِلَى النُّورِ بِإِذْنِهِ وَيَهْدِيهِمْ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿١٦﴾

“Hakika imekwishawafikia nuru kutoka kwa Mwenyezi Mungu na Kitabu kinachobainisha. Mwenyezi Mungu huwaongoza kwacho wenye kufuata radhi yake katika njia za amani na huwatoa katika giza kuwapeleka kwen­ya nuru kwa amri yake, na huwaongoza katika njia iliyonyooka.” Juz.6 (5:15-16).

Na Mwenyezi Mungu kwa mnayoyatenda anazo habari. Siku atakayowakusanya kwa ajili ya Siku ya Mkusanyiko; hiyo ni siku ya hasara.

Neno ‘hasara,’ tumelifasiri kutokana na neno la kiarabu taghabun ambalo wafasiri wengi wamesema kuwa makusudio yake hapa ni kupunjana, ambapo siku ya Kiyama watu wa haki watawapunja watu wa batili, lakini tunavyofahamu sisi ni kuwa makusudio yake ni faida na hasara; ambapo wenye haki watapata faida na wabatilifu watapata hasara. Hata hivyo nati­ja ya maana zote mbili ni moja.

Mwenyezi Mungu anadhibiti kauli za waja wake, vitendo vyao, malengo yao na makusudio yao katika maisha ya dunia na kuyatumia siku ya Kiyama kwa hisabu.

Yakiwa ni heri basi ni heri na yakiwa ni shari basi ni shari. Siku ya mwisho imeitwa ya mkusanyiko kwa vile Mwenyezi Mungu atawakusanya viumbe kwa ajili ya hisabu na malipo.

Na anayemwamini Mwenyezi Mungu na akatenda mema, atamfutia maovu yake, na atamuingiza katika Bustani zipitiwazo na mito chini yake, watadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa. Na waliokufuru na wakakadhibisha Ishara zetu, hao ni watu wa Motoni, watadumu humo milele. Na hayo ndiyo marudio mabaya.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kusema kuwa Yeye atawakusanya watu siku isiyo na shaka, sasa anasema kuwa watu siku hiyo watakuwa aina mbili:

Ya kwanza : ni wale waliomwamini Mwenyezi Mungu, mitume wake na vitabu vyake na wakajitayarisha kwa matendo mema duniani kwa ajili ya Akhera yao. Aina hii ya watu ndio watakaofuzu kesho kwa kupata maghufira ya Mwenyezi Mungu na radhi yake na kwa kupata neema isiyo na ukomo wala kupungua kiwango chake.

Aina ya pili , ni waliopotezwa na dunia wanaoitafuta kwa njia yoyote itakayokuwa; hawajali dini wala dhamiri au halali wala haramu. Aina hi ya watu ndio watakaopata hasara, makazi yao ni Jahannam ambayo ni marejeo mabaya kabisa.

Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.

Dhahiri ya Aya inafahamisha kuwa shari yoyote ya duniani ni kwa kadha na kadari yake Mwenyezi Mungu. Na hii inapingana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

وَمَا أَصَابَكُم مِّن مُّصِيبَةٍ فَبِمَا كَسَبَتْ أَيْدِيكُمْ وَيَعْفُو عَن كَثِيرٍ ﴿٣٠﴾

“Na misiba inayowasibu ni kwa sababu ya yaliyotendwa na mikono yenu. Naye anasamehe mengi.” Juz. 25 (42:30).

Hili tumelijibu kwa ufafanuzi katika Juz. 5 (4:78-79). Ufupi wa jawabu ni kuwa majanga ya kimaumbile; kama vile tetemeko la ardhi kahati nk, yananasibika na maumbile moja kwa moja na yanasabishwa Kwake Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa wasita; kwa vile Yeye ndiye Alieyaleta maumbe.

Hii ndio maana ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Mwenyezi Mungu.” Na msiba wowote ambao chimbuko lake ni kupuuza na ufisadi, linanasibika kwenye uchaguzi mbaya wa kupuuza na ufisadi. Hii ndio iliyokusudia na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Na misiba inayowasibu ni kwa sababu ya yaliyotendwa na mikono yenu.”

Na mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu huuongoza moyo wake.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anamchukulia mtu kwa vile inavyochagua nafsi yake. akijichagulia uongofu na heri na kufauata njia iliyonyoka, basi humshika mkono, kumsaidia na kumpatia thawabu za wenye kuongoka. Na akijichagulia upotevu na kuifuata njia yake, humwachilia mbali na kumtweza kisha anamtia kwenye adhabu ya moto.

Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.

Anamjua mwenye kujihurumia na anamuhurumia, na mwenye kujiangamiza kwa makusudi basi humwangamiza.

Na mtiini Mwenyezi Mungu, na mtiini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha kwa uwazi tu.

Wajibu wa Mtume ni kufikisha na wajibu wetu ni kusikiliza na kutii. Umetangulia mfano wake katika Aya kadha, ikiwemo ile iliyoko Juz. 7 (5:92).

Mwenyezi Mungu, hapana mungu isipokuwa Yeye. Na juu ya Mwenyezi Mungu nawategemee Waumini.

Anawatoshea wenye kumtegemea Yeye na ni walii wa wenye ikhlasi.

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ وَإِن تَعْفُوا وَتَصْفَحُوا وَتَغْفِرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ ﴿١٤﴾

14. Enyi mlioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui zenu. Basi tahadharini nao. Na mkisamehe, na mkapuuza, na mkaghufiria basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

إِنَّمَا أَمْوَالُكُمْ وَأَوْلَادُكُمْ فِتْنَةٌ وَاللَّـهُ عِندَهُ أَجْرٌ عَظِيمٌ ﴿١٥﴾

15. Hakika mali zenu na watoto wenu ni mtihani. Na kwa Mwenyezi Mungu kuna ujira mkubwa.

فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ وَاسْمَعُوا وَأَطِيعُوا وَأَنفِقُوا خَيْرًا لِّأَنفُسِكُمْ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفْسِهِ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الْمُفْلِحُونَ ﴿١٦﴾

16. Basi mcheni Mwenyezi Mungu vile muwezavyo, na sikieni, na tiini, na toeni, itakuwa heri kwa nafsi zenu. Na mwenye kuepushwa na uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu.

إِن تُقْرِضُوا اللَّـهَ قَرْضًا حَسَنًا يُضَاعِفْهُ لَكُمْ وَيَغْفِرْ لَكُمْ وَاللَّـهُ شَكُورٌ حَلِيمٌ ﴿١٧﴾

17. Mkimkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mzuri, atawazidishia maradufu, na atawaghufiria. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa shukrani, Mpole.

عَالِمُ الْغَيْبِ وَالشَّهَادَةِ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ ﴿١٨﴾

18. Mwenye kujua ghaibu na dhahiri. Mwenye nguvu, Mwenye hikima.

UADUI WA WAKE NA WATOTO

Aya 14 – 18

MAANA

Enyi mlioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui zenu. Basi tahadharini nao.

Katika vitabu vya tafsiri na Hadith kuna maelezo kuwa kuna watu waliosilimu Makka na wakataka kuhamia kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w. w ) , wake zao na watoto wao wakawazuia. Ndipo ikashuka Aya hii kuwahadharisha waumini wasiwatii baadhai ya wake zao na watoto.

Mara nyingi tumesema kuwa sababu ya kushuka haiihusishi Aya na tukio hilo, bali inaenea. Hiyo inakuwa ni sehemu tu miongoni mwa sehemu zake. Kwa hiyo basi kila mke asiyesaidiana na mumewe kwenye lile lilo na masilahi kwa pande zote mbili kidini na kidunia, basi huyo ni adui yake.

Pia mume atakuwa ni adui wa mke akiwa naye ni kikwazo kwa hilo. Vile vile kwa upande wa mtoto na mzazi bali mama na ndugu. Lolote linalofanywa na adui, akilifanya naye pi atakuwa ni adui, kwa hali yoyote itakavyokuwa.

Kwa mnasaba huu tunasema kuwa, kutoka mtu kwenye maisha ya useja kwenda kwenye maisha ya ndoa kunafanana na kwenda Akhera; itakuwa ni Peponi au motoni. Mara nyingi sana ni motoni sio kwenye neema. Kwani maisha ya familia wakati huu ni adhabu na Jahannam - mtoto hawezi kumridhia baba yake ila kwa kutiiwa yeye na kunyenyekewa, wala mke hamridhii mume ila awe yeye ndio mume na mume awe mke!

Na mkisamehe, na mkapuuza, na mkaghufiria basi hakika Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa maghufira, Mwenye kurehemu.

Hakuna tofauti baina ya msamaha, kupuuza na maghufira isipokuwa kwenye matamshi tu. Makusudio ya kuyachanganya matamko haya ni kiasi cha kusisitiza na kuhimiza tu.

Baada ya Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuhadharisha baadhi ya wake na wato­to kwa vile wanafanya wayafanyayo maadui akasema: Mkiwasamehe kwa kuwahurumia na kutumaini kurekebika kwao, basi Mwenyezi Mungu Mtukufu atawafanyia hivyo hivyo nanyi, kwa sababu Yeye humhurumia mwenye huruma na humsamehe mwenye kusamehe, lakini ni pale ikiwa kufanya hivyo ni vizuri; vinginevyo baadhi ya makosa haifai kuyasamehe kwa hali yoyote.

Aya inaashiria kwamba maisha ya famailia hayawezekani isipokuwa kwa subira na kusamehe. Na kwamba lau mtu atahisabu kila linalotoka kwa watoto wake basi mzozo usingemalizika na wangeliishi kwenye Jahannam.

Hakika mali zenu na watoto wenu ni mtihani. Na kwa Mwenyezi Mungu kuna ujira mkubwa.

Kila litakalokuvutia na kukuzuia na majukumu ya kidunia na akhera, hilo ni mtihani; iwe ni mali, mtoto, mke, cheo, usanii n.k. Mwenyezi Mungu (s.w.t) amehusisha kutaja mali na watoto, kwa sababu ndiyo mambo yanayoongoza kwenye majaribu. Kadiri ladha ya dunia itakavyokuwa kubwa, lakini yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ni bora na yenye kubaki. Umetangulia mfano wake katika Juz. 9 (8:28). Katika Tafsir Tabari na nyinginezo kuna maelezo haya: “Mtume(s.a.w. w )

alikuwa akihutubia, akaja Hasan na Husein wakiwa wamevaa kanzu nyekundu, wakijikunguwaa na kusimama. Basi Mtume akashuka akawachukua na kuwabeba mapajani mwake; kisha akasema: Amesema kweli Mwenyezi Mungu: Hakika mali zenu na watoto wenu ni mtihani. Nimewaona hawa na kukatisha mazungumzo yangu ili niwachukue. Kisha akaendelea na hutuba yake.

Basi mcheni Mwenyezi Mungu vile mwezavyo,

Fanyeni bidii kadiri mnavyoweza kuzichunga nafsi zenu na majaribio na mjiweke mbali na aliyoyaharimisha Mwenyezi Mungu wala msifanye chochote cha haramu kwa sababu ya mali au watoto.

Kuna mfasiri aliyesema kuwa kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu: “Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu ipasavyo kumcha.” Juz. 4 (3:102) ni ya mkazo zaidi na kauli yake hii hapa ‘Basi mcheni Mwenyezi Mungu vile mwezavyo,’ ni ya tahafifu; kisha akaongezea hapo kuwa kauli hii imeondoa hukumu ya kauli ile.

Sisi hatuoni tofauti yoyote baina ya Aya mbili hizi, kwa sababu wajibu wa mtu ni kujikinga na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu, kadiri atakavyoweza, wala yeye halazimiki na asichokiweza. Tazama Juz. 3 (2:286).

Na sikieni, na tiini, na toeni,

Sikieni mwito wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake na muuchunge kwa utiifu na takua, na toeni ziada ya mali yenu katika njia ya Mwenyezi Mungu. Hiyo itakuwa heri kwa nafsi zenu; yaani:

إِنْ أَحْسَنتُمْ أَحْسَنتُمْ لِأَنفُسِكُمْ وَإِنْ أَسَأْتُمْ فَلَهَا ﴿٧﴾

“Mkifanya uzuri mnajifanyia wenyewe na mkifanya ubaya mnajifanyia wenyewe.” Juz. 15 (17:7)

Na mwenye kuepushwa na uchoyo wa nafsi yake, basi hao ndio wenye kufaulu.

Kutoa mali na nafsi ni njia ya kufaulu na kuokoka na kuifanyia ubahili mali na nafsi ni njia ya hasara. Kwa sababu ubahili na uchoyo ni katika nguvu kubwa inayopelekea kujiingiza kwenye maovu.

Imetangulia kwa herufi zake katika Juzuu hii tuliyo nayo (59:9).

Mkimkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mzuri, atawazidishia maradufu, na atawaghufiria. Na Mwenyezi Mungu ni Mwingi wa shukrani, Mpole.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) anataka mkopo kwa waja wake na hali anazo hazina za mbingu na ardhi, anawazidishia malipo watiifu kwa hisani kutoka kwake, anawaghufiria wenye kutubia kwa kuwahurumia, anawashukuru wenye kufanya ihsani kwa kuwapa kingi kutokana na kichache walichotoa na anawapa muda waasi; kama kwamba amewasamehe. Umetangulia mfano wake katika Juz. 2 (2:245), Juz. 9 (5:12) na Juz. 27 (57:11).

Mwenye kujua ghaibu na dhaahiri hakifichiki kitu chochote kwake.Mwenye nguvu, isiyoshindwaMwenye hikima katika alivyoumba na kupangilia.

MWISHO WA SURA YA SITINI NA NNE: SURAT AT – TAGHABUN

5

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SABA

وَدَاوُودَ وَسُلَيْمَانَ إِذْ يَحْكُمَانِ فِي الْحَرْثِ إِذْ نَفَشَتْ فِيهِ غَنَمُ الْقَوْمِ وَكُنَّا لِحُكْمِهِمْ شَاهِدِينَ ﴿٧٨﴾

78. Na Daud na Suleiman walipohukumu juu ya shamba, walipolisha humo mbuzi wa watu usiku. Na sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao.

فَفَهَّمْنَاهَا سُلَيْمَانَ وَكُلًّا آتَيْنَا حُكْمًا وَعِلْمًا وَسَخَّرْنَا مَعَ دَاوُودَ الْجِبَالَ يُسَبِّحْنَ وَالطَّيْرَ وَكُنَّا فَاعِلِينَ ﴿٧٩﴾

79. Tukamfahamisha Suleiman na kila mmoja wao tukampa hukumu na elimu. Na tuliifanya milima na ndege kuwa pamoja na Daud imnyenyekee na imsabihi (Mwenyezi Mungu). Na sisi tulikuwa ni wenye kuifanya.

وَعَلَّمْنَاهُ صَنْعَةَ لَبُوسٍ لَّكُمْ لِتُحْصِنَكُم مِّن بَأْسِكُمْ فَهَلْ أَنتُمْ شَاكِرُونَ ﴿٨٠﴾

80. Na tukamfundisha kutengeneza mavazi ya vita ili kuwakinga katika mapigano yenu. Je, mtakuwa wenye kushukuru?

وَلِسُلَيْمَانَ الرِّيحَ عَاصِفَةً تَجْرِي بِأَمْرِهِ إِلَى الْأَرْضِ الَّتِي بَارَكْنَا فِيهَا وَكُنَّا بِكُلِّ شَيْءٍ عَالِمِينَ ﴿٨١﴾

81. Na upepo mkali kwa ajili ya Suleiman, wendao kwa amri yake, katika ardhi tuliyoibariki. Na sisi ndio tunaojua kila kitu.

وَمِنَ الشَّيَاطِينِ مَن يَغُوصُونَ لَهُ وَيَعْمَلُونَ عَمَلًا دُونَ ذَٰلِكَ وَكُنَّا لَهُمْ حَافِظِينَ ﴿٨٢﴾

82. Na katika mashetani kuna wanompigia mbizi na kufanya kazi nyinginezo; Nasi tulikuwa walinzi wao.

DAUD NA SULEIMAN

Aya 78 – 82

MAANA

Na Daud na Suleiman walipohukumu juu ya shamba, walipolisha humo mbuzi wa watu usiku. Na sisi tulikuwa wenye kushuhudia hukumu yao.

Kuna riwaya iliyo mashuhuri midomoni mwa wapokezi, kwamba watu wawili walikwenda kuamuliwa kwa Daud. Mmoja alikuwa na mimea na wa pili alikuwa na mifugo ya mbuzi na kondoo. Mwenye shamba akasema wanyama wa huyu bwana wamelisha kwenye mimea yangu usiku. Baada ya kumthibitikia hilo, Daud alitoa hukumu kuwa wanyama wawe wa mwenye shamba.

Suleiman alipojua hivyo akasema, ni vizuri mwenye shamba awachukue wanyama, anufaike nao lakini wasiwe wake kabisa, na mwenye wanyama achukue ardhi aishghulikie mpaka iwe kama ilivyokuwa kabla ya kuliwa. Kisha bada ya hapo kila mmoja achukue mali yake. Daud akapendezewa na hukumu ya mwanawe na akaitumia.

Dhahiri ya Aya inaafikiana na riwaya hii. Imethibiti kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) kwamba yeye amesema: “Linaloafikiana na Qur’an lichukueni na linalokhalifiana nalo liacheni.”

Unaweza kuuliza : Kila mmoja kati ya Daud na Suleiman ni Nabii na Nabii ni maasumu; hasa katika hukumu ya sharia na hukumu ya sawa, sasa je kuna wajihi gani wa kupingana hukumu mbili hizi?

Baadhi wamejibu kuwa kauli ya Daud ilikuwa ni upatanishi sio hukumu. Lakini ijulikane kuwa upatanishi unakuwa kwa baadhi ya mali sio yote na Daud hakumbakishia mfugaji hata mnyama mmoja.

Wengine wakasema kuwa kila mmoja kati ya manabii wawili hao alihukumu kwa ijitihadi yake. Kauli hii vile vile ina kasoro; kwamba Nabii anatumia ijitihadi kama ulama wengine na inajulikana kuwa rai ya ijtihadi inakuwa kwa kukosekana nukuu (Nass) na ilivyo ni kuwa kauli ya Nabii ni nukuu ya haki; na kwamba ijitihadi ina uwezekano wa kupatia na kukosea, jambo ambalo haliswihi kwa maasumu.

Jamaa wamesema kuwa hukumu ilikuwa kama alivyopitisha Daud; kisha ikabadilishwa (naskh), na kauli ya Suleiman[2]

Kauli hii ina nguvu zaidi kwa dalili ya kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

Tukamfahamisha Suleiman na kila mmoja wao tukampa hukumu na elimu.

Hapo Mwenyezi Mungu anashudia kuwa kila mmoja ni mjuzi wa hukumu. Kwa hiyo basi kauli yake Mwenyezi Mungu ‘Tukamfahamisha Suleiman’ ni kwamba yeye alimpelekea wahyi wa kubadilisha hukumu ya baba yake. Mafaqihi wametofautiana kuwa je mwenye mifugo atalipa kilichoharibiwa na wanyama wake?

Maliki na Shafi wamesema kuwa atalipa kilichoharibiwa usiku sio mchana. Abu Hanifa akasema halipi kwa hali yoyote; iwe usiku au mchana.

Jamaa katika mafaqihi wa kishia wamesema kama alivyosema Maliki na Shafi na wahakiki katika wao wakasema kuwa litakaloangaliwa ni hali ya uzembe wa mfugaji au la; sio hali ya kuwa usiku au mchana. Ikiwa mfugaji atazembea au kufanya makusudi, basi atalipa. Na ikiwa atajichunga na asipuuze, ikatokea bahati mbaya basi hatalipa.

Na tuliifanya milima na ndege kuwa pamoja na Daud imnyenyekee na imsabihi (Mwenyezi Mungu). Na sisi tulikuwa ni wenye kuifanya.

Imekuwa mashuhuri kuwa Daud alikuwa na sauti nyororo. Majaribio yamethibitisha kuwa wanyama wengi wanaburudika na aina fulani ya nyimbo na muziki [3] 2. Niliwahi kusoma kwenye gazeti kwamba nyoka aliwahi kutoka kwenye tundu yake ili astarehe na nyimbo za Ummu Kulthum, katika moja ya hafla yake. Nyimbo ilipokwisha akarudi sehemu yake.

Ama tasbibih ya mlima ni kwa njia ya majazi na kusifia zaidi tu; kama kusema: Amelichekesha na kuliliza jiwe. Au inawezekana ni kiuhakika hasa. Kwa sababu yule aliyeweza kuufanya moto kuwa baridi na salama kwa Ibrahim, ndiye anaweza pia kulifanya jabali litoe tasbih pamoja na Daud.

Angalia Aya 69 ya Sura hii tuliyo nayo.

Na tukamfundisha kutengeneza mavazi ya vita ili kuwakinga katika mapigano yenu. Je, mtakuwa wenye kushukuru?

Makusudio ya mavazi ya vita hapa ni deraya. Aya inaonyesha kuwa Daud ndiye mtu wa kwanza kutengeneza deraya.

Kuna riwaya inayoelezea kwamba sababu ya hilo ni kuwa Daud alikuwa ni mfalme wa Israil na alikuwa ana desturi ya kupita mitaani kujulia hali za watu, bila ya yeye kujulikana. Siku moja akakutana na mtu akamuuliza kuhusu sera za mfalme Daud.

Yule mtu akasema: Ana sera nzuri sana, kama asingekuwa anakula kwenye hazina ya serikali. Daud akaapa kuwa kuanzia siku hiyo hatakula kitu isipokuwa kilichotokana na mikono yake na jasho lake.

Alipojua Mwenyezi Mungu ikhlasi yake na ukweli wa nia yake, alimalainishia chuma na kumfundisha kutengeneza deraya.

Iwe sahihi riwaya hii au la, ni kwamba inaashria wajibu wa kufanya bidii kubwa kuchunga masilahi ya watu na mali zao. Kuna Hadith mutawatir kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu, Muhammad(s.a.w.w) , alifariki akiwa ameweka rahani deraya yake kwa sababu ya kukopa kiasi fulani cha shayir, huku zikiwa mali za Bara arabu zote ziko mikononi mwake.

Na upepo mkali kwa ajili ya Suleiman, wendao kwa amri yake, kati- ka ardhi tuliyoibariki. Na sisi ndio tunaojua kila kitu.

Dhahiri ya Aya hii inafahamisha kuwa upepo ulikuwa ukimchukua Suleiman kwa amri ya Mwenyezi Mungu. Wala hakuna haja ya kuleta taawili, maadamu akili inakubaliana na dhahiri hiyo.

Aya iliyo wazi zaidi ya hii ni ile isemayo: “Na Suleiman tukamtiishia upepo mwendo wake asubuhi ni mwezi mmoja na mwendo wake jioni yake ni mwezi mmoja.” (34:12) Yaani asubuhi unakwenda mwendo wa mwezi mmoja kwa kusafiri na ngamia na jioni vile vile.

Makusudio ya ardhi iliyobarikiwa ni ile iliyotajwa kwenye Aya ya 71 ya Sura hii.

Unaweza kuuliza : Hapa Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amesema upepo mkali na mahali pengine anasema: pole pole: “Na tukamtiishia upepo uendao polepole kwa amri yake.” (38:36). Je, kuna wajihi gani wa Aya zote mbili?

Jibu : Huwa mara unakwenda kwa kasi na mara nyingine polepole kulin- gana na amri yake; sawa na gari au ndege.

Na katika mashetani kuna wanompigia mbizi baharini na kumtolea lulu na marijani.

Makusudio ya mashetani hapa ni majini

Na kufanya kazi nyinginezo ; kama kujenga mihirabu na picha:

يَعْمَلُونَ لَهُ مَا يَشَاءُ مِن مَّحَارِيبَ وَتَمَاثِيلَ وَجِفَانٍ كَالْجَوَابِ وَقُدُورٍ رَّاسِيَاتٍ ﴿١٣﴾

“Wakimfanyia alipendalo, kama mihrabu na picha na masinia makubwa, kama hodhi na masufuria makubwa yasiyoondolewa mahali pake.” (34:13).

Nasi tulikuwa walinzi wao, kwamba wasitoroke na kufanya ukorofi. Hatuna la kuongeza zaidi ya ulivyothibisha wahyi kuwepo majini na kwamba wao walimtumikia Suleiman na akili hailikatai hilo. Kwa hiyo basi hakuna haja yoyote ya kuleta taawili na kuyazungusha maneno. Imam Ali(a.s) amesema:“Lau kama mtu angeliweza la kumfanya adumu ulimwenguni au kuhepa mauti, basi angelikuwa Suleiman ambaye alitiishiwa ufalme, majini watu, utume na heshima kuu.”

وَأَيُّوبَ إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ أَنِّي مَسَّنِيَ الضُّرُّ وَأَنتَ أَرْحَمُ الرَّاحِمِينَ ﴿٨٣﴾

83. Na Ayyub aliopomlingania Mola wake: Hakika mimi imenigusa dhara, nawe ndiye unayerehemu zaidi kuliko wanaorehemu.

فَاسْتَجَبْنَا لَهُ فَكَشَفْنَا مَا بِهِ مِن ضُرٍّ وَآتَيْنَاهُ أَهْلَهُ وَمِثْلَهُم مَّعَهُمْ رَحْمَةً مِّنْ عِندِنَا وَذِكْرَىٰ لِلْعَابِدِينَ ﴿٨٤﴾

84. Basi tukamkubalia na tukamuondolea dhara na tukampa watu wake na mfano wao pamoja nao kuwa ni rehema itokayo kwetu na ukumbusho kwa wafanyao ibada.

وَإِسْمَاعِيلَ وَإِدْرِيسَ وَذَا الْكِفْلِ كُلٌّ مِّنَ الصَّابِرِينَ ﴿٨٥﴾

85. Na Isamil na Idris na Dhulkifl, wote walikuwa miongoni mwa wanaosubiri.

وَأَدْخَلْنَاهُمْ فِي رَحْمَتِنَا إِنَّهُم مِّنَ الصَّالِحِينَ ﴿٨٦﴾

86. Na tukawaingiza katika rehema yetu. Hakika wao ni katika watu wema.

وَذَا النُّونِ إِذ ذَّهَبَ مُغَاضِبًا فَظَنَّ أَن لَّن نَّقْدِرَ عَلَيْهِ فَنَادَىٰ فِي الظُّلُمَاتِ أَن لَّا إِلَـٰهَ إِلَّا أَنتَ سُبْحَانَكَ إِنِّي كُنتُ مِنَ الظَّالِمِينَ ﴿٨٧﴾

87. Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhabika na akadhani kuwa hatutamdhikisha. Basi aliita katika giza kwamba: Hapana Mola isipokuwa wewe, umetakasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.

فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَنَجَّيْنَاهُ مِنَ الْغَمِّ وَكَذَٰلِكَ نُنجِي الْمُؤْمِنِينَ ﴿٨٨﴾

88. Basi tukamkubalia na tukamwokoa kutokana na ghamu. Kama hivyo tunawaokoa wenye kuamini.

وَزَكَرِيَّا إِذْ نَادَىٰ رَبَّهُ رَبِّ لَا تَذَرْنِي فَرْدًا وَأَنتَ خَيْرُ الْوَارِثِينَ ﴿٨٩﴾

89. Na Zakaria alipomwita Mola wake: Ewe Mola wangu! Usiniwache peke yangu na wewe ndiye mbora wa wanaorithi.

فَاسْتَجَبْنَا لَهُ وَوَهَبْنَا لَهُ يَحْيَىٰ وَأَصْلَحْنَا لَهُ زَوْجَهُ إِنَّهُمْ كَانُوا يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَيَدْعُونَنَا رَغَبًا وَرَهَبًا وَكَانُوا لَنَا خَاشِعِينَ ﴿٩٠﴾

90. Basi tukamwitikia na tukampa Yahya na tukamponyeshea mkewe. Hakika wao walikuwa wepesi kufanya kheri na wakituomba kwa hofu na walikuwa wakitunyenyekea.

وَالَّتِي أَحْصَنَتْ فَرْجَهَا فَنَفَخْنَا فِيهَا مِن رُّوحِنَا وَجَعَلْنَاهَا وَابْنَهَا آيَةً لِّلْعَالَمِينَ ﴿٩١﴾

91. Na mwanamke aliyelinda tupu yake na tukampulizia katika roho yetu na tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni ishara kwa walimwengu.

NA AYYUB ALIOPOMLINGANIA MOLA WAKE

Aya 83 – 91

MAANA

Na Ayyub aliopomlingania Mola wake: Hakika mimi imenigusa dhara, nawe ndiye unayerehemu zaidi kuliko wanaorehemu. Basi tukamkubalia na tukamuondolea dhara.

Makusudio ya dhara ni madhara ya nafsi, kama vile maradhi, kutokana na neno la kiarabu dhurr.

Likisomwa dharr ndio linakuwa na maana ya madhara ya kila kitu. Wafasiri na wapokezi wengi wamepokea riwaya nyingi zinazomuhusu Ayyub. Tunalolifahamu sisi, kutokana na Aya zinazomzungumzia kwa uwazi na kwa ishara hapa na pia katika Sura Swad (38), ni kwamba Ayyub alikuwa na afya yake nzuri akiwa hana matatizo yoyote. Kisha mabalaa yakaanza kumwandama kila upande, akawa ni wa kupigiwa mifano.

Masaibu yalimpata yeye mwenyewe binafsi; akavumilia uvumilivu wa kiungwana; na akabakia na yakini yake na kumtegemea kwake Mwenyezi Mungu. Huzuni wala machungu hayakumfanya aache kumtii Mwenyezi Mungu. Lakini muda ulivyomzidi na machungu nayo yakazidi, alimshtakia

Mwenyezi Mungu mambo yake kwa maneno mawili tu: “Imenigusa dhara, nawe ndiye unayerehemu zaidi kuliko wanaorehemu,” na wala hakulalamika kwa kusema balaa gani hii iliyoniandama.

Ndipo Mwenyezi Mungu akamwitikia maombi yake na akamuondolea mabalaa na kumrudisha katika hali nzuri zaidi ya alivyokuwa.

Na tukampa watu wake na mfano wao pamoja nao kuwa ni rehema itokayo kwetu na ukumbusho kwa wafanyao ibada.

Mwenyezi Mungu alimruzuku watoto na wajukuu zaidi ya wale aliowakosa, ikiwa ni rehema na malipo ya uvumilivu wake; na pia kukumbusha kwamba mwenye kuwa na subra na uvumilivu kama wa Ayyub, basi mwisho wake utakuwa kama wa Ayyub. Mwenyezi Mungu amehusisha kuwataja wenye kuabudu kwa kuashiria kuwa Mwenyezi Mungu yuko pamoja na mwenye subra aliye na ikhlasi kwa kauli yake na vitendo vyake.

Huu ndio ujumla wa maelezo ya Aya zinazofungamana na Ayyub; bila ya kuingilia ufafanuzi walioutaja wapokezi na wasimulizi. Kwani huo hauam- batani na itikadi wala uhai kwa mbali wala karibu. Miongoni mwa njia za Qur’an ni kukitaja kisa kwa yale yaliyo na mazingatio yenye kunufaisha na mawaidha ya kukanya.

Na Isamil Na Idris Na Dhulkifl, wote walikuwa miongoni mwa wanao- subiri. Na tukawaingiza katika rehema yetu. Hakika wao ni katika watu wema.

Ismail alifanya subra ya kukubali kuchinjwa na akawa na uvumilivu wa kukaa katika nchi isiyokuwa na mimea wala kinywewa. Idris tumemueleza katika Juz. 16 (19:56).

Ama Dhulkifl wengi wamesema alikuwa Mtume; na baadhi wakasema alikuwa ni mja mwema tu na sio Mtume. Sisi tunaamini kwamba yeye ni miongoni mwa waliokuwa na subira na waja wema, kwa kufuata Qur’an ilivyosema, na wala hatutaulizwa zaidi ya hayo.

Na Dhun-Nun alipoondoka hali ameghadhabika na akadhani kuwa hatutamdhikisha. Basi aliita katika giza kwamba: Hapana Mola isipokuwa wewe, umetakasika. Hakika mimi nilikuwa miongoni mwa madhalimu.

Dhun-Nun ni Yunus. Maana ya neno ‘Nun” ni samaki. Mwenyezi Mungu anasema:

فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ ﴿٤٨﴾

“Na vumilia hukumu ya Mola wako wala usiwe kama sahibu wa samaki” (68:48).

Hali ameghadhibika ni kuwaghadhibikia watu wake. Neno kudhikishwa limefasiriwa kutokana na neno Naqdira alyh; kama lilivyotumika mahali pengine:

وَمَن قُدِرَ عَلَيْهِ رِزْقُهُ ﴿٧﴾

“Na yule ambaye imekuwa dhiki riziki yake” (65:7).

Makusudio ya katika giza hapa ni ndani ya tumbo la samaki.

Maana kwa ujumla ni: kumbuka ewe Muhammad habari ya Yunus alipowalingania watu wake, lakini hawakumwitikia mwito wake, akawaondokea kwa kuwakasirikia, akadhani kuwa hatutamdhikisha kwa kumzuia n.k. Alipomezwa na samaki akataka uokovu kutoka kwetu,basi tukamkubalia na tukamwokoa kutokana na ghamu. Kama hivyo tunawaokoa wenye kuamini.

Makusudio ya ghamu hapa ni tumbo la samaki; na kuokoka, ni kutolewa humo hadi kwenye nchi kavu. Umetangulia mfano wake katika Juz. 11 (10:98).

Na Zakaria alipomwita Mola wake: Ewe Mola wangu! Usiniwache peke yangu na wewe ndiye mbora wa wanaorithi. Basi tukamwitikia na tukampa Yahya na tukamponyeshea mkewe.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 ( 3: 38) na Juz. 16 (19:7).

Hakika wao walikuwa wepesi kufanya kheri na wakituomba kwa hofu na walikuwa wakitunyenyekea.

Wao ni Zakariya, mkewe na Yahya au wale Mitume waliotangulia kutajwa. Wote walifanya kheri kwa kutaka thawabu za Mwenyezi Mungu na kuhofia adhabu yake na walikuwa wakimfuata Mwenyezi Mungu katika kila jambo.

Na mwanamke aliyelinda tupu yake na tukampulizia katika roho yetu na tukamfanya yeye na mwanawe kuwa ni ishara kwa walimwengu.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 3 (3: 45) na Juz. 16 (19: 16).

6

TAFSIRI YA QURANI AL-KAASHIF JUZUU YA KUMI NA SABA

إِنَّ هَـٰذِهِ أُمَّتُكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّكُمْ فَاعْبُدُونِ ﴿٩٢﴾

92. Hakika umma wenu huu ni umma mmoja, na mimi ni Mola wenu kwa hivyo niabuduni.

وَتَقَطَّعُوا أَمْرَهُم بَيْنَهُمْ كُلٌّ إِلَيْنَا رَاجِعُونَ ﴿٩٣﴾

Na wakalivunja jambo lao baina yao. Wote watarejea kwetu.

فَمَن يَعْمَلْ مِنَ الصَّالِحَاتِ وَهُوَ مُؤْمِنٌ فَلَا كُفْرَانَ لِسَعْيِهِ وَإِنَّا لَهُ كَاتِبُونَ ﴿٩٤﴾

94. Na atendaye mema naye ni mumin, basi haitakataliwa bidii yake na hakika sisi tutamwandikia.

وَحَرَامٌ عَلَىٰ قَرْيَةٍ أَهْلَكْنَاهَا أَنَّهُمْ لَا يَرْجِعُونَ ﴿٩٥﴾

95. Na ni haramu kwa mji tuliouangamiza kwamba wao hawatarejea.

حَتَّىٰ إِذَا فُتِحَتْ يَأْجُوجُ وَمَأْجُوجُ وَهُم مِّن كُلِّ حَدَبٍ يَنسِلُونَ ﴿٩٦﴾

96. Mpaka watakapofunguliwa Juju na Majuju, wakawa wanateremka kutoka kila mlima.

وَاقْتَرَبَ الْوَعْدُ الْحَقُّ فَإِذَا هِيَ شَاخِصَةٌ أَبْصَارُ الَّذِينَ كَفَرُوا يَا وَيْلَنَا قَدْ كُنَّا فِي غَفْلَةٍ مِّنْ هَـٰذَا بَلْ كُنَّا ظَالِمِينَ ﴿٩٧﴾

97. Na miadi ya haki itakaribia, ndipo yatakapokodoka macho ya wale waliokufuru. Ole wetu! Hakika tulikuwa tumeghafilika na haya, bali tulikuwa ni wenye kudhulumu.

إِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ مِن دُونِ اللَّـهِ حَصَبُ جَهَنَّمَ أَنتُمْ لَهَا وَارِدُونَ ﴿٩٨﴾

98. Hakika nyinyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Jahannam, mtaifikia.

لَوْ كَانَ هَـٰؤُلَاءِ آلِهَةً مَّا وَرَدُوهَا وَكُلٌّ فِيهَا خَالِدُونَ ﴿٩٩﴾

99. Lau haya yangelikuwa ni miungu yasingeliingia na wote watadumu humo.

لَهُمْ فِيهَا زَفِيرٌ وَهُمْ فِيهَا لَا يَسْمَعُونَ ﴿١٠٠﴾

100. Lao humo ni kupiga mayowe na wala hawatasikika.

UMMA MMOJA

Aya 92 – 100:

MAANA

Hakika umma wenu huu ni umma mmoja, na mimi ni Mola wenu kwa hiyo niabuduni.

LUGHA

Maana ya neno umma ni watu wenye lugha moja na historia moja. Kisha neno hili likawa linatumika zaidi kwa maana ya dini na mila. Maana haya ndiyo yaliyokusudiwa hapa.

Umma wenu huu ni itikadi ya mitume ambayo ni tawhid pamoja na kufuata amri za Mwenyezi Mungu kwa kauli na vitendo. Msemo ‘wenu’ unaelekezwa kwa watu wote.

Maana ni kuwa enyi watu wote! Shikeni dini ya Tawhidi waliyokuwa nayo Mitume na mumwabudu Mungu mmoja aliye peke na mumfanyie ikhlasi katika kauli na vitendo.

Na wakalivunja jambo lao baina yao.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) aliwaamrisha wote wawe kwenye itikadi ya tawhidi, lakini wakagawanyika wakawa makundi ya wakana Mungu na washirikina. Hata wale wafuasi wa Mitume nao wanatukanana na kujitenga na wengine; bali hata wafuasi wa Mtume mmoja nao ni hivyo hivyo.

Wote watarejea kwetu.

Haya ni makemeo na hadhari kwa wale wanaofarikiana wakawa vikundi.

Na atendaye mema naye ni mumin, basi haitakataliwa bidii yake na hakika sisi tutamwandikia.

Imani pamoja na matendo mema ni njia ya Peponi na imani bila ya matendo haifai chochote. Hiyo ni kutokana na kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu:

لَا يَنفَعُ نَفْسًا إِيمَانُهَا لَمْ تَكُنْ آمَنَتْ مِن قَبْلُ أَوْ كَسَبَتْ فِي إِيمَانِهَا خَيْرًا ﴿١٥٨﴾

“Basi mtu haitamfaa imani yake ambaye hakuamini zamani, au hakuchuma kheri kwa imani yake.” Juz. 8 (6:158).

Ama matendo mema bila ya imani, humnufaisha mtendaji kwa namna moja au nyingine na huenda ikamfaa huko Akhera kwa kupunguziwa adhabu. Tumeyafafanua hayo katika Juz. 4 (3:158) kwenye kifungu ‘kafiri na amali njema’ Pia Umepita mfano wake katika Juz. 14 (16: 97)

Na ni haramu kwa mji tuliouangamiza kwamba wao hawatarejea.

Aya hii ni jawabu la swali la kukadiria, kwamba je, washirikina katika watu wa kijiji kilichoangamizwa na Mwenyezi Mungu kwa kufuru yao, watarudishwa tena kuwa hai na kuadhibiwa huko Akhera, kama walivyoadhibiwa duniani?

Ndio akajibu Mwenyezi Mungu (s.w.t) kuwa watu wote, kesho watarejea kwa Mwenyezi Mungu; hata wale walioangamizwa duniani kwa dhambi zao na ni muhali kukosa kurejea kwa Mwenyezi Mungu baada ya mauti; bali hakuna budi lazima watafufuliwa.

Swali la pili : je inafaa kuadhibiwa akhera baada ya kuadhibiwa duniani? Huko si ni kuadhibu mara mbili kwa kosa moja?

Jibu : Hapana! Kuadhibiwa kwao duniani kulikuwa ni kwa ajili ya kuwakadhibisha kwao Mitume waliowajia na miujuza; kama zinavyofahamisha Aya hizi zifuatazo na nyinginginezo mfano wake:

وَقَوْمَ نُوحٍ لَّمَّا كَذَّبُوا الرُّسُلَ أَغْرَقْنَاهُمْ ﴿٣٧﴾

“Na kaumu ya Nuh walipowakadhibisha Mitume tuliwagharikisha” (25:37)

كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ وَأَصْحَابُ الرَّسِّ وَثَمُودُ ﴿١٢﴾ وَعَادٌ وَفِرْعَوْنُ وَإِخْوَانُ لُوطٍ ﴿١٣﴾ وَأَصْحَابُ الْأَيْكَةِ وَقَوْمُ تُبَّعٍ كُلٌّ كَذَّبَ الرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ ﴿١٤﴾

“Kabla yao walikadhibisha kamu ya Nuh na watu wa Rassi na Thamud na A’d na Firauni na ndugu wa Lut na watu wa vichakani na kaumu ya Tubbai, wote waliwakadhibisha Mitume, kwa hiyo kiaga kikathibitika juu yao.” (50: 12-14).

Ama adhabu ya Akhera ni ya ukafiri wenyewe na madhambi mengineyo; kama dhulma n.k.

Kwa hiyo adhabu zinakuwa nyingi kutokana na dhambi kuwa aina nyingi, sio kwa dhambi moja.

Mpaka watakapofunguliwa Juju na Majuju, wakawa wanateremka kutoka kila mlima.

Katika Juz. 16 (18: 94) tuliwanukuu baadhi ya wafasiri wakisema kuwa Juju ni wa Tatars na Majuju ni Wamongoli. Vile vile tumesema huko kuwa ukuta wa Juju na Majuju hauko tena. Kwa hiyo basi makusudio ya kufunguliwa Juju na Majuju ni kuenea kwao katika mabara.

Vyovyote iwavyo sisi hatujawahi kusoma ya kutegemewa kuhusu Juju na Majuju, si katika tafsiri wala mahali penginepo. Kwa hiyo tutasimama kwenye dhahiri ya nukuu ya Qur’an tu na ufafanuzi tutawachia wengine.

Na miadi ya haki itakaribia, ndipo yatakapokodoka macho ya wale waliokufuru.

Makusudio ya miadi ya haki hapa ni Kiyama, hapo akili za waliokufuru zitapotea na macho yatatoka kutokana na vituko vya siku hiyo. Umetangulia mfano wake katika Juz. 13 (14: 42).

Ole wetu! Hakika tulikuwa tumeghafilika na haya, bali tulikuwa wenye kudhulumu.

Yaani watasema hivyo. Umetangulia mfano wake katika Juz. 8 (7:5) na katika juzuu na Sura hii tuliyo nayo Aya 14 na 46.

Hakika nyinyi na hayo mnayoyaabudu badala ya Mwenyezi Mungu ni kuni za Jahannam, mtaifikia.

Hapa wanaambiwa washirikina wa Makka. Makusudio ya mnayoyaabudu ni masanamu yao. Maana ni kuwa, enyi washirikina! Nyinyi na masanamu yenu mtakutana kwenye Jahannamu kesho. Kuna Hadithi isemayo: “Mtu yuko pamoja na anayempenda.”

Unaweza kuuliza : Kuna faida gani ya kutiwa masanamu kwenye Jahannamu na ni mawe yasiyokuwa na utambuzi wala hisiya?

Wafasiri wamejibu kuwa lengo ni kuwazidishia masikitiko wale wanaoyaabudu, kila watakapoyaona karibu nao. Lakini jawabu hili ni kiasi cha kuchukulia uzuri na hisia tu. Lilio bora ni kuicha Aya nyingine ijibu:

فَاتَّقُوا النَّارَ الَّتِي وَقُودُهَا النَّاسُ وَالْحِجَارَةُ ﴿٢٤﴾

“Basi uogopeni moto ambao kuni zake ni watu na mawe, uliowekewa makafiri.” Juz. 1 (2:24).

Kuna riwaya isemayo kuwa Ibn Az-Zab’ariy – mmoja wa washirkina wa kikuraishi na mshairi wao – aliingilia Aya hii kama mayahudi wanamwabudu Uzayr na wanaswara (wakristo) wanamwabudu Masihi na hawa wawili ni watu wa Peponi, kama anavyosema Muhammad, sasa vipi aseme kila kinachoabudiwa ni kuni?

Mtume akamjibu: Ni ujinga ulioje wako wewe kutojua lugha ya watu wako. Kwani huoni herufi ma (ambayo) ni ya visivyo na akili?

Zaidi ya hayo maneno yanawahusu washirikina wa kikurashi, kama tulivyotangulia kusema nao wanaabudu masanamu.

Lau haya yangelikuwa ni miungu yasingeliingia na wote watadumu humo.

Haya ni ishara ya masanamu. Maana ya Aya yako wazi, kwamba lau masanamu yangelikuwa miungu yasingeliiingia motoni. Ni kama kusema: Lau ungelikuwa mwaminifu usingelifanya khiyana, lakini umefanya khiyana kwahiyo wewe si mwaminifu. Mfano huu katika mantiki unaitwa kutoa dalili kwa kipimo cha kuvua (istithnaiyy).

Lao humo ni kupiga mayowe na wala hawatasikika.

Hapa anaambiwa kila mkosaji, awe mwislamu au kafiri. Humo ni humo ndani ya Jahannam. Maana ni kuwa kila mkosaji atakuwa katika Jahannam akilalama kwa machungu; hatasikia neno la upole wala huruma, bali atakayemuona atamtahayariza na kumsema:

وَقِيلَ لِلظَّالِمِينَ ذُوقُوا مَا كُنتُمْ تَكْسِبُونَ ﴿٢٤﴾

“Na wenye kudhulumu wataambiwa onjeni yale mliyokuwa mkiyachuma.” (39:24).

إِنَّ الَّذِينَ سَبَقَتْ لَهُم مِّنَّا الْحُسْنَىٰ أُولَـٰئِكَ عَنْهَا مُبْعَدُونَ ﴿١٠١﴾

101. Hakika wale ambao umewatangulia wema kutoka kwetu, hao watatenganishwa na hayo.

لَا يَسْمَعُونَ حَسِيسَهَا وَهُمْ فِي مَا اشْتَهَتْ أَنفُسُهُمْ خَالِدُونَ ﴿١٠٢﴾

102. Hawatasikia mvumo wake. Nao watudumu katika yale ambayo nafsi zao zinayatamani.

لَا يَحْزُنُهُمُ الْفَزَعُ الْأَكْبَرُ وَتَتَلَقَّاهُمُ الْمَلَائِكَةُ هَـٰذَا يَوْمُكُمُ الَّذِي كُنتُمْ تُوعَدُونَ ﴿١٠٣﴾

103. Hiyo fazaa kubwa haitawahuzunisha. Na Malaika watawapokea: Hii ndiyo siku yenu mliyokuwa mkiahidiwa.

يَوْمَ نَطْوِي السَّمَاءَ كَطَيِّ السِّجِلِّ لِلْكُتُبِ كَمَا بَدَأْنَا أَوَّلَ خَلْقٍ نُّعِيدُهُ وَعْدًا عَلَيْنَا إِنَّا كُنَّا فَاعِلِينَ ﴿١٠٤﴾

104. Siku tutakapozikunja mbingu mkunjo wa karatasi za vitabu. Kama tulivyoanza umbo la mwanzo tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu yetu. Hakika sisi ni wenye kufanya.

وَلَقَدْ كَتَبْنَا فِي الزَّبُورِ مِن بَعْدِ الذِّكْرِ أَنَّ الْأَرْضَ يَرِثُهَا عِبَادِيَ الصَّالِحُونَ ﴿١٠٥﴾

105. Na hakika tulikwishaandika katika Zaburi baada ya ukumbusho kuwa Ardhi watairithi waja wangu walio wema.

إِنَّ فِي هَـٰذَا لَبَلَاغًا لِّقَوْمٍ عَابِدِينَ ﴿١٠٦﴾

106. Hakika katika haya kuna ujumbe kwa wafanyao ibada.

وَمَا أَرْسَلْنَاكَ إِلَّا رَحْمَةً لِّلْعَالَمِينَ ﴿١٠٧﴾

107. Na hatukukutuma ila uwe ni rehema kwa walimwengu.

ARDHI WATARITHI WAJA WANGU WALIO WEMA

Aya 101 – 107

MAANA

Hakika wale ambao umewatangulia wema kutoka kwetu, hao watatenganishwa na hayo.

Mwenyezi Mungu aliwaahidi wenye takua kuamiliana nao kwa wema. Miongoni mwa wema huo ni kuokoka na moto.

Hawatasikia mvumo wake.

Hii ni kusisitiza watakavyokuwa mbali nao.

Nao watudumu katika yale ambayo nafsi zao zinayatamani.

Watasalimika na adhabu ya Mwenyezi Mungu wakineemeshwa kwenye Pepo yake.

Hiyo fazaa kubwa haitawahuzunisha, sikwambii ndogo tena.

Kwani fazaa zina daraja, kuanzia machungu ya kukata roho, upweke wa kaburini, kisha kutoka makaburini kwa ajili ya hisabu hadi kuingia Jahannam.

Na Malaika watawapokea: Hii ndiyo siku yenu mliyokuwa mkiahidiwa.

Malaika watawapokea kwa takrima na kuwaambia kuwa Mwenyezi Mungu amewakusanya kwenye siku hii aliyowaahidi kwa ufalme wa daima na neema isiyokatika. Aya hizi tatu zinafupilizwa na neno:

هَلْ جَزَاءُ الْإِحْسَانِ إِلَّا الْإِحْسَانُ ﴿٦٠﴾

“Je, malipo ya hisani si ni hisani tu.” (55:60)

Au neno:

لِّلَّذِينَ أَحْسَنُوا الْحُسْنَىٰ وَزِيَادَةٌ ﴿٢٦﴾

“Kwa wafanyao wema ni wema.” Juz.11 (10:26).

Siku tutakapozikunja mbingu mkunjo wa karatasi za vitabu.

Makusudio ya vitabu hapa ni maandishi ya matamko yanayoayaandikwa kwenye karatasi. Maana ni kuwa Mwenyezi Mungu (s.w.t) atazikunja sayari, siku ya Kiyama, pamoja na ukubwa na wingi wake; kama inavyokunjwa karatasi yenye maandishi; kiasi ambacho kila sayari itafanana na herufi au neno lilo kwenye karatasi.

Kama tulivyoanza umbo la mwanzo tutalirudisha tena. Ni ahadi iliyo juu yetu. Hakika sisi ni wenye kufanya.

Mwenyezi Mungu (s.w.t) amefananisha ufufuo na kuumba kwa kwanza; kwamba, kama kulivyowezekana kwa kwanza, basi kwa pili pia kuunawezekana. Si muhali kwa Mwenyezi Mungu kutekeleza ahadi yake.

Hilo halimshindi Mwenyezi Mungu; kwani mwenye kuumba ulimwengu basi hawezi kushindwa kuurudisha tena baada ya kuharibika na kutawanyika:

وَهُوَ الَّذِي يَبْدَأُ الْخَلْقَ ثُمَّ يُعِيدُهُ وَهُوَ أَهْوَنُ عَلَيْهِ ﴿٢٧﴾

“Na Yeye ndiye anayeanzisha uumbaji, kisha ataurudisha. Na hilo ni jepesi zaidi kwake” (30:27).

TENA MAHDI ANAYENGOJEWA

Na hakika tulikwishaandika katika Zaburi baada ya ukumbusho kuwa Ardhi watairithi waja wangu walio wema.

Zaburi ni kitabu cha Daud na ukumbusho ni vitabu vya mbinguni vilivyotangulia; kama vile vitabu vya Ibrahim na Musa. Maana yake ni kuwa utawala wa dunia, ingawaje hivi sasa uko mikononi mwa mataghuti waovu, lakini Mwenyezi Mungu atauhamisha uende kwa walio wema. Hilo halina budi. Hapo amani na uadilifu utaenea ardhini na watu wote wataneemeka na kheri za Ardhi na baraka zake.

Kuna Hadithi nyingi zenye maana ya Aya hii; miongoni mwazo ni ile aliy- oipokea Abu Daud katika Kitabu cha Sunan, ambacho ni mojawapo ya Sahihi sita: “Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu:

Lau haitabakia katika dunia isipokuwa siku moja tu, basi Mwenyezi Mungu angeliirefusha siku hiyo mpaka amtume mtu kutoka katika watu wa nyumba yangu (Ahlu bayt) jina lake linafanana na jina langu, na jina la baba yake ni kama la baba yangu, ataijaza ardhi uadilifu baada ya kujazwa dhulma na jeuri” [4] .

Kanuni ya maisha hailikatai hilo, bali inalithibitisha na kulisisitiza. Ikiwa nguvu hivi sasa ziko mikononi mwa unyama wenye kudhuru wa umoja wa mataifa, baraza la usalama n.k. basi hakuna litakalozuia, siku moja kugeuka nguvu hiyo kutoka mikononi mwa madhalimu waovu hadi kwa watu wa haki na uadilifu; bali maumbile yanapenda kujikomboa na dhulma.

Pia kuna misingi isemayo: “Kila kilicho katika ardhi kina harakati, kama ilivyo na harakati ardhi na kwamba kudumu hali ni muhali.” Yote hayo yanapelekea kuwa hatimaye nguvu zitakuwa mikononi mwa wema wanao- faa.

Hakika katika haya kuna ujumbe kwa wafanyao ibada.

Haya ni haya ya kuwa ardhi itarithiwa na waja wema; hata kama ni baada ya muda. Makusudio ya wafanyao ibada hapa ni wale wanaopata mawaidha kwa kuzingatia na kunufaika na maonyo.

Na hatukukutuma ila uwe ni rehema kwa walimwengu.

Maneno yanaelekezwa kwa Muhammad(s.a.w.w) . Risala yake ni rehema kwa wa mwanzo na wa mwisho. Huko nyuma tumeeleza mara nyingi kuhusu misingi ya risala hiyo na mafunzo yake.

Inatosha, kuthibitisha hilo, kauli za mwenye risala hiyo; kama vile: “Hakumwamini Mwenyezi Mungu yule ambaye watu hawamwamini. Likikuhuzunisha ovu na likakufurahisha jema, basi wewe ni mumin.”

Ni kwa hisia hizi ndio uadilifu utasimama, amani kuenea na maisha kuwa bora. Tumezungumzia kwa ufafanuzi kuhusu hilo katika Juz. 7 (6:92).

قُلْ إِنَّمَا يُوحَىٰ إِلَيَّ أَنَّمَا إِلَـٰهُكُمْ إِلَـٰهٌ وَاحِدٌ فَهَلْ أَنتُم مُّسْلِمُونَ ﴿١٠٨﴾

108. Sema: Hakika umeletwa wahyi kwangu ya kwamba hakika Mungu wenu ni Mungu mmoja tu. Je nyinyi mmesilimu?

فَإِن تَوَلَّوْا فَقُلْ آذَنتُكُمْ عَلَىٰ سَوَاءٍ وَإِنْ أَدْرِي أَقَرِيبٌ أَم بَعِيدٌ مَّا تُوعَدُونَ ﴿١٠٩﴾

109. Kama wakikataa, basi sema: Nimewatangazia sawasawa. Wala sijui yako karibu au mbali hayo mliyoahidiwa.

إِنَّهُ يَعْلَمُ الْجَهْرَ مِنَ الْقَوْلِ وَيَعْلَمُ مَا تَكْتُمُونَ ﴿١١٠﴾

110. Hakika Yeye anajua kauli ya dhahiri na anajua mnayoyaficha.

وَإِنْ أَدْرِي لَعَلَّهُ فِتْنَةٌ لَّكُمْ وَمَتَاعٌ إِلَىٰ حِينٍ ﴿١١١﴾

111. Wala sijui pengine huu ni mtihani tu kwenu na starehe mpaka muda kidogo.

قَالَ رَبِّ احْكُم بِالْحَقِّ وَرَبُّنَا الرَّحْمَـٰنُ الْمُسْتَعَانُ عَلَىٰ مَا تَصِفُونَ ﴿١١٢﴾

Akasema: Mola wangu! Hukumu kwa haki. Na Mola wetu ni Mwingi wa rehema aombwaye msaada juu ya mnayoyasifia.

HAKIKA MUNGU WENU NI MMOJA TU

Aya 108 – 112

MAANA

Sema: Hakika umeletwa wahyi kwangu ya kwamba hakika Mungu wenu ni Mungu mmoja tu. Je nyinyi mmesilimu?

Mwenyezi Mungu alimwarisha Mtume wake awaambie washirikina kuwa Mwenyezi Mungu ameniletea wahyi kwamba Yeye ni mmoja tu hana mshirika katika kuumba kwake na wala katika ujuzi wake.

Ulimwengu huu na maajabu yake na kanuni zake unashuhudia kwa uwazi juu ya umoja, uweza na ukuu wake Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Basi kwa nini hamuamini na kufuata amri yake? Kwanini mnadanganyika kuacha kumwabudu Yeye na kwenda kuabudu mawe yasiyodhuru wala kunufaisha?

Kama wakikataa, basi sema: Nimewatangazia sawasawa.

Baada ya kuwalazimu hoja ya kufikisha na maonyo, Mwenyezi Mungu alimwamrisha Mtume wake mtukufu awaambie kuwa nimekishatekeleza wajibu wangu na nikafikisha risala ya Mola wangu. Kwa hiyo haukubaki udhuru wowote kwenu.

Wala sijui yako karibu au mbali hayo mliyoahidiwa.

Mimi nina yakini na adhabu yenu, kwa sababu Mwenyezi Mungu ameiahadi na kuwahadhirisha nayo, na ahadi yake Mwenyezi Mungu ni ya kweli na adhabu yake pia ni kali zaidi, lakini sijui itakuwa lini. Ni sawa iwe karibu au mbali, lakini ina wakati wake. Ngojeni nami niko pamoja nanyi katika wenye kungojea.

Hakika Yeye anajua kauli ya dhahiri na anajua mnayoyaficha.

Umetangulia mfano wake katika Juz. 16 (20:7).

Wala sijui pengine huu ni mtihani tu kwenu na starehe mpaka muda kidogo.

Sijui kuna hekima gani ya kupewa kwenu muda na kucheleweshewa adhabu. Je Mwenyezi Mungu (s.w.t.) ametaka kumdhirisha kila mmoja hakika yake, aweze kutubia mwema na aendelee mouvu au ametaka mustarehe siku zilizobakia kwenye umri wenu? Mwenyezi Mungu ndiye ajuaye.

Akasema (Muhammad): Mola wangu! Hukumu kwa haki.

Yaani idhihirishe haki na uwanusuru watu wake kwa wale wanaoipinga.

Na Mola wetu ni Mwingi wa rehema aombwaye msaada juu ya mnayoyasema kuwa masanamu yenu ni miungu na madai yenu kwangu kuwa ni mzushi.

Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Wewe ni mtukufu kwa kila anayekuzulia. Wema ni wa yule anayekufuata, akachukua athari yako na akamwambia mzushi, kama vile ulivyosema wewe:

Na Mola wetu ni Mwingi wa rehema aombwaye msaada juu ya mnayoyasifia.

MWISHO WA SURA YA ISHIRINI NA MMOJA


4

5

6

7

8

9

10

11

12

13

14

15

16