HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU

 HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU 33%

 HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU Mwandishi:
: HEMEDI LUBUMBA SELEMANI
Kundi: Tarehe

HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU
  • Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 10376 / Pakua: 4832
Kiwango Kiwango Kiwango
 HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU

HISTORIA NA SIRA ZA VIONGOZI WAONGOFU

Mwandishi:
Swahili

HISTORIA NA SIRA YA VIONGOZI WAONGOFU

MTUNZI: JOPO LA WAANDISHI WA VITABU VYA KIADA

MTARJUMI: HEMEDI LUBUMBA SELEMANI

Utangulizi

Hamna shaka kuwa historia ya mwanadamu ndio chemchemu na chanzo cha maarifa, chanzo ambacho mataifa yanakihitaji katika safari yake yenye kuendelea. Na ndio chanzo pekee chenye uwezo wa kuhuisha na kulisukuma taifa mbele na kulipa sifa na hadhi maalum huku kikilifunganisha taifa hilo na mizizi yake ya ustaarabu ambayo hulizuwia taifa dhidi ya mmong'onyoko.

Qur'ani imemhimiza kila mwanadamu ikamtaka azame ndani ya his- toria ya mwanadamu na azingatie yaliyomo ili awaidhike na kuongoka, hivyo Mwenyezi Mungu akasema:

"Je, hawatembei katika ardhi ili wapate nyoyo za kufahamia au masikio ya kusikilizia? "[1]

Baada ya Mwenyezi Mungu kutoa historia ya Adi, Thamudi, Firauni, watu wa miji iliyopinduliwa na watu wa Nuh akasema:

"Ili tuifanye ukumbusho kwenu na sikio lisikialo lisikie ."[2]

Historia ya ujumbe mbalimbali wa Mwenyezi Mungu imejaa masomo na mazingatio, masomo ambayo yameonyesha jinsi manabii watukufu walivyojali mataifa yao ili kuyaokoa toka kwenye matatizo mbalimbali.

Pia ujumbe huo umeonyesha lengo na mwelekeo wake wenye kujaa nuru na manufaa. Kwa ajili hiyo sera ya Mtukufu Mtume(s.a.w.w ) na kizazi chake huwa ni tafsiri ya kivitendo ya misingi na sheria za kiislamu.

Hivyo kusoma sera yao na historia ya maisha yao ni chanzo muhimu cha kuifahamu Qur'ani na Sunna, na ni chemchemu ya maarifa ya wanadamu wote, kwa sababu ni ujumbe wa Mwenyezi Mungu alioutuma kwa wanadamu huku Nabii wa mwisho na mawasii wake wateule wakiwa ni viongozi wa wanadamu wote bila kubagua.

Tumeona ni vizuri tuweke silabasi kwa ajili ya kusoma historia ya kiislamu kwa kufuata hatua moja baada ya nyingine, kwani masomo ya historia ya nukuu hutangulia kabla ya masomo ya uchambuzi.

Na kwa kuwa umma wote umekongamana juu ya wema na utakaso wa viongozi wa ujumbe wa Mwenyezi Mungu basi inafaa tuingize historia ya maisha yao ndani ya maisha ya wanafunzi, kwani Qur’ani imetamka wazi kuhusu umaasumu na utakaso wao ili wawe ni kiigizo chema kwa yule anayetarajia fadhila za Mwenyezi Mungu na malipo mema ya Siku ya Kiyama.

LENGO LA SILABASI YA KITABU HIKI

Kitabu “Masomo ya utangulizi katika historia na sera ya viongozi wema” kimetungwa ili kiwe hatua ya mwanzo ya kuelekea kwenye masomo mbalimbali ya lengo la kina zaidi, huku kikitegemea kufikia lengo hilo kwa kutumia wepesi wa ibara, usalama wa nukuu na vyanzo vyenye kukubalika ili kitoe picha ya wazi isiyokuwa na utata, shaka au hisia ambazo huenda zikamchanganya msomaji wa sera na historia mwanzoni tu mwa safari yake hii.

Masomo haya sitini yataanza kuzungumzia historia na sera kwa mtazamo wa Qur’ani, kisha yatatoa maisha binafsi na ya kijamii ya kila mmoja kati ya maasumina kumi na wanne(a.s ) , na mwisho yataishia kwenye uwanja kati ya viwanja vya urithi wao wenye kunukia manukato.

Mwisho kabisa tutatoa faida ya maisha yao ya ujumbe huku tukionyesha mavuno ambayo yamepatikana ndani ya karne tatu bali ni zaidi ya karne kumi na nne za mapambano yenye kuendelea kwa ajili ya kuuokoa umma wa kiislamu na jamii ya wanadamu toka kwenye yale yaliyowapata na waliyonasa ndani yake.

Na ili yawe maandalizi mema yenye kuunea na mapinduzi ya kiulimwengu ambayo yanamsubiri kiongozi wake wa kiroho, Imam angojewaye Al-Mahdi(a.s ) ambaye Mwenyezi Mungu aliwaahidi watu wa mataifa yote, ili aje kuunganisha nguvu na kuzifanya vizuri hali zao huku akiwaokoa wanadamu toka kwenye upotevu na kutimiza matarajio ya manabii na akitimiza wema wa ubinadamu, wema ambao bado binadamu anaendelea kuutolea juhudi zake usiku na mchana.

Hivyo mafunzo ya historia yamegawanywa katika sera binafsi na sera ya kijamii, huku yakiwa hayana uchambuzi wa matukio ya kihistoria wala kuzama sana ndani ya matukio makuu ya kihistoria, hiyo ni ili baadaye yafuatiwe na masomo mapana zaidi kuliko mafunzo haya.

Pia tumejiepusha na urudiaji huku tukikomea kwenye historia ya ujumbe wenyewe na yale yaliyopita katika mzunguko na vipindi vya ujumbe na kwenye matokeo yaliyopatikana ndani ya karne zilizopita ambazo ziliupitia Uislamu na waislamu.

Mada hizi zimetimia kwa kufuata uchambuzi wa kielimu dhidi ya matukio yaliyosajiliwa ndani ya vitabu vya historia au yaliyogunduliwa na watafiti. Katika hali zote mbili tumejaribu kutegemea juhudi za wale waliotutangulia, ambazo ni masomo ya waandishi na watafiti ili kupata matunda ya juhudi zao na kuunganisha kati ya watu wa zamani na kizazi cha sasa.

Pia ili tuwafunze vijana dharura ya kupitia rejea za kutegemewa za zamani na za sasa bila kudhulumu haki za waliyotangulia bali ili zionekane juhudi zao na jinsi walivyochangia katika uwanja wa elimu na maarifa ya jamii, na ili kuijua nafasi waliyonayo katika kunukuu urithi na kuvipelekea vizazi vyenye kufuata.

Waandishi wa zama hizi tutakaowataja ni Sheikh Baqir Sharifu Al- Qarashiy, Sayyid Murtaza Al-Askariy, marehemu Sheikh Asad Haydar, mashahidi wawili: Sayyid Muhammad Baqir As-Sadri na Sayyid Muhamad Baqir Al-Hakim. Kisha Sayyid Jafar Murtaza Al- Amiliy, Sheikh Muhammad Had Al-Yusufiy Al-Gharawiy na wengine ambao tumegusia vitabu vyao mwishoni mwa kila mada ambayo tumenukuu toka kwao.

Ni wajibu wetu kusema: Kitabu hiki ni mjumuisho wa mada mbalim- bali na utunzi unaolenga mafunzo ambayo yamezagaa ndani ya vitabu maalumu vilivyoteuliwa kufundisha sera ya kizazi cha Mtume (s.a.w.w.) ili iwe ni mali kwa mtafiti, mwanafunzi, mhutubu, mubali- hghiina, mlezi na mlelewa ili ajiandae na masomo ya juu zaidi katika historia ya Uislamu kwa ajili ya kupambana mapambano ya kielimu dhidi ya matukio ya kihistoria na kijamii, na ili tuzame ndani huku tukipata mafunzo toka humo ili yawe ni mazingatio kwa msomaji na mawaidha kwa mwenye mazingatio, insha’allah.

Kutokana na maelezo yaliyopita, kwa muhtasari tunatoa matokeo yafuatayo:

Kwanza : Katika hatua hii mwalimu anapofundisha historia asitege- mee kukutana na mafunzo ya kihistoria yenye mtiririko wa kuungana na kufuatana kwa maana iliyozoeleka. Kwa kuanzia jografia na histo- ria ya Bara la Uarabu, kisha utume wa Mtukufu Mtume(s.a.w.w ) na dola yake, kisha dola ya makhalifa ambao walitawala kwa utaratibu maalumu. Hiyo ni kwa sababu sisi hatukusudii isipokuwa kusoma sera ya viongozi wema maasumina ambao ni lazima kuwaiga ili mwanafunzi afuate nyayo zao, awafuate na kuongoka kwa uongozi wao na sera yao katika maisha yake binafsi na ya kijamii.

Pili : Mwanafunzi anaweza kupata mafunzo muhimu ya kihistoria kupitia njia ya kutoa hatua za maisha ya kila mmoja kati ya maasumina kumi na wanne kwa kiwango kinachonasibiana na hatua ya mwanzo ya utangulizi ambayo imeishia kugusia nafasi na sehemu ya kizazi cha Mtume katika historia na harakati za Uislamu, kwa kuanzia nafasi yao maalumu ya kipekee aliyowapa Mwenyezi Mungu na kumalizia hali halisi ya kihistoria ambayo imetoa harakati zao na mwenendo wao muda wa karne tatu na zaidi.

Tatu : Kwanza hakika mafunzo ya historia ya Bara la Uarabu hayaingii yote katika historia ya Uislamu isipokuwa huwa kama utan- gulizi tu. Pili hutumiwa katika sehemu ya uchambuzi, jambo ambalo hatulikusudii katika hatua hii ya masomo haya. Zaidi ya hapo ni kuwa maelezo ya kizazi cha Mtume(s.a.w.w ) kama vile kauli za Imam Ali(a.s ) toka kwa Mtume(s.a.w.w ) na maelezo ya Zahra(a.s ) ndani ya hotuba yake mashuhuri aliyoitoa baada ya kifo cha Mtume(s.a.w.w ) yameelezea vizuri hali ya waarabu kabla ya Uislamu. Na pia imeunganisha kati ya yaliyopita na yaliyopo ambayo aliyatimiza Mtume(s.a.w.w ) , na majukumu makubwa yaliyofuatia yaliyopo juu ya wais- lamu ambao walitolewa na Uislamu toka kwenye shimo la ujinga mpaka kwenye nuru ya mwanga wa Uislamu.

Nne : Hakika anayemaliza kusoma kitabu hiki inampasa azalishe mafunzo ambayo yatampa njia ya kufikia malengo yanayokusudiwa katika kusoma historia ndani ya hatua zote mbili, na wala asitosheke na haya yaliyopo kwenye masomo ya hatua ya utangulizi.

Hatutaki kurudia mafunzo mara juu juu au mara nyingine kwa upana na undani zaidi, kwa ajili hiyo tunategemea waheshimiwa walimu wetu watazingatia malengo ya masomo kabla ya kuhoji silabasi ya kitabu. Na watatilia maanani silabasi ya kitabu kabla ya kuzama ndani ya vipengele vidogo vidogo vya historia ambavyo tumeviteua kwa ajili ya hatua hii. Pia watazingatia kikomo cha wakati na dharura ya kupangilia mafunzo kulingana na ubora ambao ni lazima kuzingatiwa katika silabasi ya mafunzo. Na kwa kuwa hiki si kitabu cha ziada bali kimeandaliwa kama kitabu cha kiada basi walimu watafundisha kulingana na silabasi ya mafunzo iliyopangwa.

Hatuna budi kusema kuwa kitabu hiki kilichapishwa mwanzo kwa jina la: ‘Dondoo za sera za viongozi wema’. Lakini baada ya kupi- tia upya mafunzo ya kitabu, kilibadilishwa jina na kuitwa:

‘Masomo ya utangulizi katika historia na sera ya viongozi wema’.

Mwisho tunatoa shukurani za dhati kwa ndugu zetu kamati ya elimu katika taasisi ya kimataifa inayosimamia vituo vya elimu na shule za kiislamu kwa msaada na juhudi walizozitoa.

Tunamuomba Mwenyezi Mungu ampe uongofu na nguvu, hakika Yeye ndiye kiongozi bora na Mwenye kunusuru. Pia tunatoa shukuranu za dhati kwa mwandishi wa kitabu hiki Ustadh Sayyid Mundhir Al-Hakim (heshima yake idumu).

Jopo la kamati ya waandishi wa vitabu vya kiada.

1425 A.H.

SOMO LA KWANZA

HATUA YA MWANZO KUELEKEA KWENYE MASOMO YA SERA NA HISTORIA YA UISLAMU

KWANZA: SERA NA LENGO LA KUISOMA

1- Sera Kiistilahi

Sera ya mwanadamu ni njia yake na mwenendo wake katika maisha, hivyo sera ya Mtume na kizazi chake ni njia na mwenendo wao katika maisha. Sera hii inaonekana katika kauli zao, matendo yao na misimamo yao dhidi ya matukio na mambo mbalimbali ambayo yalitokea katika zama zao na wakaishi nayo kipindi cha karne tatu na miongo minne.

Yaani tangu uanze utume wa Mtukufu Mtume(s.a.w.w ) mpaka mwisho wa ghaiba ndogo ya Imam wa kumi na mbili Muhammad bin Hasan Al-Askariy, Al-Mahdi hoja mwenye kungojewa.

2- Jinsi Qur’ani Ilivyotilia Umuhimu Sera

Hakika Qur’ani imetilia umuhimu sera kwa kubainisha sera ya man- abii na watu wema. Ikataka tufuate sera yao na kujifunza kupitia sera ya wale waliopita huku tukiwaidhika na sera yao. Pia imetuhimiza kujali sera ya hitimisho la manabii na bwana wa mitume, Muhammad bin Abdullah(s.a.w.w ) ikataka tumuige[3] baada ya kumwambia: “Na kwa hakika wewe unaongoza kwenye njia iliyonyooka.”[4]

Kisha akawaamrisha waislamu wote kukazania yote yanayotoka kwa yule asiyetamka la matamanio yake akasema: “Na anachokupeni Mtume basi kipokeeni, na anachokukatazeni basi jiepusheni .”[5]

Kisha akatuelekeza kwa kizazi cha Mtume, ambao Mwenyezi Mungu kawaondolea uchafu na kuwatakasa kabisa[6] . Akahimiza kushikamana na wakweli na kufuata mwenendo wao, hivyo Mwenyezi Mungu akasema: “Enyi mlioamini, mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli .”[7]

3 - Lengo La Kusoma Sera

Hakika kumfuata Mtume wa Mwenyezi Mungu na kizazi chake kitakasifu ni kufuata njia iliyonyooka inayofikisha kwenye wema na ushindi kwa sababu ni njia inayokuepusha na upotovu na ghadhabu za Mwenyezi Mungu. Na ndio njia ya manabii ambao Mwenyezi Mungu aliwaneemesha kwa neema ya uongofu wake unaowapeleka kwenye haki[8] . Ndiyo maana akaamrisha kuwafuata, Mwenyezi Mungu akasema: “Hao ndio ambao Mwenyezi Mungu amewaongoza, basi fuata mwongozo wao .”[9]

Pia kwa ajili hiyo ndiyo maana sera ya yule hitimisho la manabii na sera ya mawasii wake watakasifu imekuwa ni chanzo kati ya vyanzo vya sheria ya kiislamu, na ni chemchemu ya maarifa na elimu ya kiis- lamu na ni sawa na Kitabu cha Mwenyezi Mungu cha milele, kama ilivyoelezea kuhusu hilo Hadithi ya vizito viwili iliyo mutawatir[10] .

Zaidi ya hapo ni kuwa sera yao - Amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao wote kwa ujumlaina faida kubwa katika kufahamu makusudio ya Kitabu kitakatifu na tafsiri ya Aya zake tukufu.

Pia sera yao hutubainishia jinsi ya kutekeleza mafunzo ya juu ya kiislamu katika maisha ya mwanadamu anayeishi katika maisha haya. Kwa hiyo tunafahamu kuwa kusoma sera yao kwa namna sahihi kutatupa silabasi muhimu katika malezi ya kiislamu na njia sahihi ya kujifunza mwenendo sahihi katika maisha.

PILI: MAHUSIANO KATI YA HISTORIA YA UISLAMU NA SERA

HISTORIA

Historia ni mkusanyiko wa matukio na uzoefu wa wanadamu waliopita ukilinganisha na zama tunazoishi hivi sasa.

HISTORIA YA UISLAMU

Hakika historia ya Uislamu ni historia ya dini ya milele ya kiislamu, tangu ulipodhihiri, kuenea kwake na harakati zake katika maisha. Pia inakusanya historia ya walioibeba dini na kuihami ambao walikesha wakihudumia na kulinda dini dhidi ya vitimbi vya maadui wake.

Hivyo hakika sera ya bwana wa mitume na sera ya kizazi chake kitakasifu ambacho kilipewa jukumu la kufikisha dini, kutekeleza na kuilinda, inakuwa ni sehemu isiyogawika ndani ya historia yenyewe ya Uislamu (yaani ndio historia yenyewe ya Uislamu).

Kwa sababu wao walizama ndani ya Uislamu na wakaihami sheria, wakatoa nafsi zao na maisha yao kwa ajili ya Uislamu. Hivyo misimamo yao ya kidini ndio Uislamu wenyewe na harakati zao ndio harakati za Uislamu wenyewe. Wao hudhihirisha kimatendo mafunzo halisi ya Uislamu na huyaelezea maelezo halisi. Hivyo historia yao ndio historia ya Uislamu katika hatua zake zote na mambo yake yote, wala siyo historia ya mtu fulani kati ya waislamu.

VYAVZO VYA HISTORIA YA UISLAMU NA SERA YA MTUME (S.A.W.W)

Hakika chanzo muhimu cha historia ya Uislamu na historia na sera ya manabii hasa historia na sera ya nabii wa mwisho(s.a.w.w) ni Kitabu cha milele cha Mwenyezi Mungu, Qur’ani yake ya muujiza ambayo: “Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa na Mwenye hekima, Mwenye kuhimidiwa.”[11]

Ama vitabu vya sera, historia, tafsiri na Hadithi ambavyo viliandikwa baada ya kupita karne moja au zaidi tangu kufariki kwa Mtume(s.a.w.w) vyenyewe ni vyanzo vya daraja la pili.

Hakika vyanzo hivi vilivyokuja nyuma vimejumuisha ukweli huku pembeni yake vikiwa vimejaza visa vya uongo, Hadithi na habari za uzushi zilizowekwa kupitia ndimi za maswahaba au wanafunzi wa maswahaba.

Kwa ajili hiyo vyanzo hivi vinahitajia kipimo makini ili kupembua habari sahihi na kuzitenganisha na habari zilizochomekwa. Pia inatakiwa kuzipima na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna sahihi ya Mtume na akili salama ili ziwe ni mwongozo kwa watafuta ukweli.

ZAMA ZA HISTORIA YA UISLAMU

Historia ya Uislamu inaanzia pale alipopewa utume Mtukufu Mtume, tarehe ishirini na saba mfungo kumi (Rajabu) miaka kumi na tatu kabla ya hijra ya Mtume(s.a.w.w) , muda ambao maisha ya Uislamu wa kudumu yalianza na yakaendelea kuchanja mbuga ndani ya jamii ya kiarabu na mwanadamu chini ya mkono wa Mtukufu Mtume Muhammad bin Abdullah.

Uislamu ulikuwa ni mapinduzi ya Mwenyezi Mungu yenye mabadi- liko katika kila kitu, hivyo yalianzia Makka tukufu na kuishia kwenye kuasisi dola ya kiislamu iliyobarikiwa huko Madina na Bara la Arabu. Baada ya jihadi kubwa chini ya uongozi wa Mwenyezi Mungu Mwenye busara matunda yake yalionekana ndani ya muda mfupi, kinyume na historia nyingi za wito wa mabadiliko.

Zama hizi ambazo Mtume Muhammad(s.a.w.w) alianzisha mapinduzi haya yaliyobarikiwa tunaweza kuziita ni zama za Mtume Muhammad(s.a.w.w) , nazo ni zama za kufikisha Uislamu.

Ama zama zilizofuatia zenyewe ni zama za mawasii waliousiwa mapinduzi na dola ya Mtume. Hizi tunaweza kuziita zama za Maimam maasumina au zama za Maimam viongozi wema. Zama zote mbili zinagawanyika katika vipindi na nyakati mbili.

A) ZAMA ZA MTUME (S.A.W.W)

Zama za Nabii zina vipindi viwili tofauti navyo ni: Kipindi cha Makka na kipindi cha Madina. Kipindi cha kwanza kinaanzia pale ali- poruhusiwa kutangaza utume huko Makka na kinakomea pale alipohama toka Makka kuelekea Madina (Yathirib) katika usiku wa mwanzo wa mfunguo sita mwaka wa kumi na tatu tangu kupewa utume.

Kipindi cha pili kinaanzia pale alipofika Madina tarehe kumi na mbili ya mfungo sita ndani ya mwaka huo huo, na kinakomea pale alipofariki Mtume(s.a.w.w) tarehe ishirini na nane mfunguo tano mwaka wa kumi na moja tangu kuhamia Madina.

Katika kipindi cha Makka Mtume alitengeneza nguvu kali, alijenga Uislamu kiimani na kisheria kwa ajili ya maisha, hivyo ni kipindi cha kutengeneza umma wa kiislamu na kuanzisha kundi la waumini wenye kuamini Uislamu.

Ama kipindi cha Madina kinajitofautisha kwa kuasisiwa dola ya kiislamu, nayo ndiyo jengo la kwanza la kisiasa lenye sura ya dola ya kiislamu iliyojengeka katika kutekeleza sheria ya kiislamu ndani ya maisha. Katika vipindi vyote viwili wahyi wa Mwenyezi Mungu ndiyo uliokuwa ukimuelekeza yeye Mtume kama kiongozi wa umma wa kiislamu kupitia Aya za Qur’ani ambayo iliteremka ndani ya muda wa miaka ishirina na tatu.

Qur’ani imetuhifadhia matukio ya vipindi vyote viwili kupitia Aya zake. Hivyo tunaweza kuijua historia ya zama hizi iwapo tu tutajua kwa usahihi utaratibu wa kushuka Aya za Qur’ani tukufu. Hivyo tunaweza kugawa kipindi cha Makka katika vipindi viwili vifuatavyo:

Kipindi cha kuwalingania watu mahsusi na kuandaa mbegu za mwanzo za kundi la waumini. Muda wa kipindi hiki unakadiriwa ni miaka mitatu mpaka mitano.

Kipindi cha kuwalingania watu wote au kipindi cha kutangaza na kuanza mapambano dhidi ya shirki na ukafiri. Muda wa kipindi hiki unakadiriwa ni miaka mitatu mpaka minne.

Kipindi cha uhamishoni, nacho ni kipindi cha kuendeleza mkondo wa Uislamu. Kipindi hiki kimekusanya hijra tatu zenye kufuatana nazo ni: Kuhama kuelekea Uhabeshi (Ethiopia ya sasa), kisha kuelekea Taif na kisha kuelekea Madina.

Pia tunaweza kugawa kipindi cha Madina katika vipindi viwili tofauti navyo ni: Kipindi cha kuasisiwa dola ya kiislamu na kuihami ndani ya nusu ya kwanza ya kipindi cha Madina kuanzia hijra na kumalizikia vita vya Handaki au Ahzab.

Kipindi cha ufunguzi na kuendeleza mapinduzi ya kiislamu na kupan- ua wigo wa dola ya kiislamu. Hii ni kuanzia suluhu ya Hudaybiya mpaka mwaka wa Hijja ya mwisho ya kuaga, nayo ni nusu ya pili ya kipindi cha Madina.

B) ZAMA ZA MAIMAM WEMA

Hakika harakati za mageuzi ziliienea jamii ya kijahiliya hivyo kutokana na zilivyokuwa fikra, mafunzo, mila, na desturi za kijahiliya ni kuwa mapinduzi ya kiislamu na dola mpya ya Mtume(s.a.w.w) vilikuwa vinahitajia usia wa kiitikadi. Hiyo ni kwa sababu njia mbele ya harakati ilikuwa bado ndefu huku ikiendela kipindi chote cha vita nzito vya kiroho kati ya Uislamu na ujahiliya.

Kipindi kilichochukuliwa na mapinduzi, kisha dola ya Mtume hakikuwa kinatosha kung’oa mizizi yote ya ujahiliya na athari zake. Na hilo ni kama ilivyothibitisha historia ya matukio ambayo yalitokea baada tu ya kifo cha Mtume(s.a.w.w) .

Kwani baada ya Mtume(s.a.w.w) utawala wa kiislamu ulibakia ni mpira unaochezewa na watoto wa kizazi cha Umayya ambao kabla ya hapo walikuwa wamesimama kidete dhidi ya Uislamu kuanzia mwanzo mpaka sekunde ya mwisho[12] .

Kuanzia hapo Mtume kiongozi aliainisha Maimam kumi na wawili maasumina kwa amri toka kwa Mwenyezi Mungu. Ambao ni mawasii wenye uwezo watakaoshika nafasi yake ili kulinda mapinduzi yake, ujumbe wake, umma wake, na dola yake baada yake. Hivyo baada yake walisimamia jukumu la kutetea sheria ya Mwenyezi Mungu na dola ya bwana wa mitume na umma wa hitimisho la manabii.

Zama zao zimegawanyika katika vipindi viwili tofauti navyo ni: Kipindi cha kuonekana na kipindi cha ghaibu. Kipindi cha kuonekana kinaanzia pale alipofariki Mtume(s.a.w.w) na kinakomea mwaka 260 A.H. Pale alipofariki Imam wa kumi na moja kati yao naye ni Hasan Al-Askariy.

Ama kipindi cha ghaibu ni kipindi cha kutoonekana Imam wa kumi na mbili kati yao naye ni maasumu wa kumi na wane. Hujja bin Al- Hasan Al-Mahdi(a.s) mwenye kungojewa. Ambaye uimamu wake umefungana na ghaibu yake.

KIPINDI CHA GHAIBU NACHO KINA VIPINDI VIWILI:

Cha kwanza : Kipindi cha ghaibu fupi ambacho kilifikia muda wa miongo saba. Yaani kuanzia mwaka 260 mpaka 329 A.H.

Cha pili : Kipindi cha ghaibu ndefu ambacho kilifuata baada ya fupi ikiwa ni mwishoni mwa muongo wa tatu karne ya nne baada ya kufariki balozi wake wa nne mwaka 329 A.H. Nacho kinaendelea mpaka leo.

MUHTASARI

Sera ya Mtukufu Mtume(s.a.w.w) na sera ya kizazi chake kitakasifu ni chanzo muhimu kati ya vyanzo vya maarifa na sheria ya kiislamu. Huzingatiwa pia kuwa ni nyenzo kati ya nyenzo za kufikia wema na mafanikio, kwa sababu kuwafuata wao ni mfano halisi wa kufuata njia ya Mwenyezi Mungu iliyonyooka.

Historia ya kiislamu ndio historia ya Uislamu na ndio historia ya watetezi ambao walizama ndani na kujitoa muhanga kila dakika ya maisha yao katika njia ya Uislamu. Nao ni Mtukufu Mtume(s.a.w.w) na kizazi chake kitakasifu kilichotakasika dhidi ya kila aina ya uchafu na kila aina ya dosari.

Qur’ani ndio chanzo muhimu cha historia na sera ya Mtume(s.a.w.w) na historia ya kiislamu. Kwa ajili hiyo vyanzo vyote vingine vya sera na historia vinapimwa kwa Qur’ani, kwa sababu vyanzo vingine vimekosa sifa ya “kumdiriki Mtume(s.a.w.w) ”, “kudiriki yote, umakini, na kutoegemea” kwenye maslahi ya makundi na madhehebu ambayo yalizuka baada ya zama za Mtume(s.a.w.w) .

Zama za Mtume wa mwisho(s.a.w.w) huchukuliwa kama mwanzo wa zama za historia ya kiislamu kisha hufuatiwa na zama za Maimam wema(a.s) .

SOMO LA PILI: MUHAMMAD BIN ABDULLAH (S.A.W.W) NI UTABIRI WA MANABII (A.S)

MWENENDO WA UTABIRI

Ni mwenendo wa Mwenyezi Mungu na ni rehema na amani kutoka Kwake kuwapa habari waja Wake za kuja kwa Mtume atakayemtuma kwao muda ujao. Hivyo manabii waliotangulia walikuwa wakim- bashiri Nabii atakayekuja baada yao.

Qur’ani imeashiria jinsi Yahya alivyobashiri unabii wa Isa (Al Imran: 39). Pia imeashiria jinsi Isa alivyobashiri unabii wa Muhammad (As-Swaf: 6). Hivyo manabii wote msitari wao ni mmoja kwani aliyetangulia humbashiri atakayemfuata, na huyu aliyefuata humwamini aliyetangulia. Mwenendo huu wa kubashiri umetamkwa na Qur’ani katika Sura ya tatu Aya ya themanini na moja. Zaidi ya hapo ni ushahidi na mifano halisi utakayoiona hapa mbele:

1. Qur’ani imeelezea utabiri wa Ibrahim kipenzi juu ya utume wa Nabii wa mwisho kwa ulimi wa dua akisema:

رَبَّنَا وَابْعَثْ فِيهِمْ رَسُولًا مِنْهُمْ يَتْلُو عَلَيْهِمْ آيَاتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ الْكِتَابَ وَالْحِكْمَةَ وَيُزَكِّيهِمْ إِنَّكَ أَنْتَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ { 129 }.

“Ewe Mola wetu, wapelekee mtume katika wao awasomee Aya zako na kuwafunza kitabu na hekima na kuwatakasa. Hakika wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima.” (Al-Baqarah: 129).

Qur’ani imeeleza wazi kuwa utabiri wa Nabii Muhammad ulikuwemo ndani ya vitabu viwili: Taurati na Injili, na laiti kama utabiri huo usingekuwemo ndani ya vitabu hivyo basi watu wa vitabu hivyo wangeupinga waziwazi, Mwenyezi Mungu anasema:

الَّذِينَ يَتَّبِعُونَ الرَّسُولَ النَّبِيَّ الْأُمِّيَّ الَّذِي يَجِدُونَهُ مَكْتُوبًا عِنْدَهُمْ فِي التَّوْرَاةِ وَالْإِنْجِيلِ يَأْمُرُهُمْ بِالْمَعْرُوفِ وَيَنْهَاهُمْ عَنِ الْمُنْكَرِ وَيُحِلُّ لَهُمُ الطَّيِّبَاتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيْهِمُ الْخَبَائِثَ وَيَضَعُ عَنْهُمْ إِصْرَهُمْ وَالْأَغْلَالَ الَّتِي كَانَتْ عَلَيْهِمْ {157}.

“Ambao wanamfuata mtume, nabii aliyeko Makka ambaye wanamuona ameandikwa kwao katika Taurati na Injili, ambaye anawaamrisha mema na anawakataza yaliyo mabaya, na kuwahalalishia vizuri na kuwaharamishia maovu, na kuwaondolea mizigo yao na minyororo iliyokuwa juu yao.” (Al-A’araf: 157).

Aya ya sita ya Surat Swaffu imeelezea waziwazi kuwa Isa(a.s ) alisadikisha Taurati na akambashiri Mtume atakayekuja baada yake jina lake Ahmad. Kama inavyoashiria kauli ya Mwenyezi Mungu:

وَإِذْ قَالَ عِيسَى ابْنُ مَرْيَمَ يَا بَنِي إِسْرَائِيلَ إِنِّي رَسُولُ اللَّهِ إِلَيْكُمْ مُصَدِّقًا لِمَا بَيْنَ يَدَيَّ مِنَ التَّوْرَاةِ وَمُبَشِّرًا بِرَسُولٍ يَأْتِي مِنْ بَعْدِي اسْمُهُ أَحْمَدُ فَلَمَّا جَاءَهُمْ بِالْبَيِّنَاتِ قَالُوا هَٰذَا سِحْرٌ مُبِينٌ {6}.

“Na aliposema Isa bin Mariam: Enyi wana wa Israeli, hakika mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nimethibitisha yaliyokuwa kabla yangu katika Taurati, na ni mwenye kutoa habari njema ya mtume atakayekuja baada yangu, jina lake ni Ahmad, lakini alipowaletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhahiri” (As-Swaff: 6).

AHLUL-KITAB WAMNGOJEA NABII WA MWISHO

Manabii waliyotangulia hawakuishia tu kutoa sifa kuu za nabii aliyetabiriwa, bali zaidi ya hapo walitaja baadhi ya alama ambazo wale wanaopewa utabiri wanaweza kumjua vizuri.

Alama hizo ni kama vile sehemu atakayozaliwa, atakayohamia na sifa mahsusi za wakati atakaopewa utume. Pia alama za kipekee alizonazo mwilini, tabia na sheria zake za kipekee. Bali Qur’ani imeeleza kuwa walikuwa wanamjua kama wanavyowajua watoto zao (Al-An’am: 20).

Kutokana na utabiri huo wakafuatilia kivitendo na mwisho wakagun- dua sehemu atakayohamia na kusimamisha dola yake. Hapo wakafanya makazi yao na kuanza kuiombea nusra dini yake dhidi ya makafiri (Al-Baqarah: 89), na kuomba ushindi kupitia Mtume wa Mwenyezi Mungu dhidi ya Ausi na Khazraji.

Hivyo habari hizi zikaenea kwa wengine kupitia mapadri na wasomi wao, zikazagaa Madina zikafika hadi Makka. Wakampa habari Abdul Muttalib[13] na Abu Talib[14] huku wakiwahadharisha na vitimbi vya mayahudi.

Hivyo baada ya Mtume kutangaza utume wake, ujumbe wa makuraishi ulikwenda kwa mayahudi wa Madina kwa lengo la kuthibitisha ukweli wa madai ya unabii waliousikia toka kwa Muhammad, wakachukua baadhi ya mambo waliyomtahini nayo Mtume,[15] na hatimaye ukabainika ukweli wa madai yake.

Baadhi ya Ahlul-Kitabi na wengineo walimwamini Nabii Muhammad kwa kufuata alama hizi ambazo walizifahamu hata bila ya kumuom- ba muujiza wowote mahsusi (Al-Maidah: 83). Mpaka leo baadhi ya nakala za Taurati na Injili zimehifadhi baadhi ya utabiri huo.[16]

Na hivyo ndivyo ulivyofuatana utabiri wa unabii wa nabii wa mwisho Muhammad kabla ya kuzaliwa kwake. Kisha ukanukuliwa wakati wa uhai wake kabla ya kukabidhiwa unabii. Ulienea utabiri aliouelezea padri Buhayra kisha ushahidi wa Waraqa bin Nawfal juu ya utume wa Muhammad, ushahidi uliotokana na utabiri.[17]

Imam Ali(a.s ) ameelezea hali hiyo kwa kusema: “Mwenyezi Mungu hajawaacha viumbe wake bila ya nabii aliyetumwa au kitabu kilichoteremshwa, au hoja ya lazima, au njia ya wazi iliyonyooka. Mitume ambao uchache wa idadi yao au wingi wa wapingaji havikumzuwia aliyetangulia kumtaja atakayekuja baada yake, au aliyepita kutambulishwa na aliye kabla yake. Kwa mwenendo huo karne zikapita…Mpaka Mwenyezi Mungu alipomleta Muhammad Mtume wa Mwenyezi Mungu ili kutekeleza utaratibu Wake na kutimiza unabii wake, huku ahadi yake ikiwa imechukuliwa kwa manabii waliyotangulia na alama zake zikiwa ni mashuhuri……..[18]

SIFA ZA NABII MUHAMMAD (S.A.W.W)

Ibnu Saad amepokea toka kwa Sahlu mtumwa wa Utayba ambaye alikuwa mkiristo wa Mar’yasi na alikuwa ni yatima aliyelelewa na mama yake mzazi na ami yake, pia alikuwa msomaji wa Injili, alisema kuwa: “Nikachukua kitabu cha ami yangu nikawa nakisoma mpaka iliponipita karatasi, hivyo nikataka kujua ni kipi kilichoandikwa katika karatasi iliyonipita. Nikaigusa kwa mkono wangu na pindi nilipoangalia nikakuta vitini vya karatasi vimeshikana hapo nikaviachanisha nikakuta ndani yake sifa za Muhammad:

Yeye si mfupi, si mrefu, mweupe, kati ya mabega yake kuna muhuri, mara nyingi hukaa mkao wa ihtibau, hapokei sadaka, anapanda punda na ngamia, anakamua mbuzi, anavaa kanzu chakavu, na atakayefanya hivyo basi kajiepusha na kiburi na yeye hufanya hivyo, na yeye anatokana na kizazi cha Ismail na jina lake ni Ahmad .”

Sahlu akasema: “Nilipofika hapa katika kumtaja Muhammad ami yangu akaja na alipoiona karatasi alinipiga na kusema: “Kwa nini umefungua karatasi hii na kusoma?” Nikasema: Humu mna sifa za nabii Ahmad. Akasema: “Yeye bado hajakuja.”[19]

MUHTASARI

Matukio ya kihistoria yanaonyesha kuwa mwenendo wa manabii ni wa kiukamilifu wenye lengo moja na njia moja. Pia mwenendo wa Mwenyezi Mungu ni manabii waliyopo kuwabashiri watakaochukua nafasi zao katika unabii. Ikiwa ni huruma toka kwa Mwenyezi Mungu dhidi ya mzigo walio nao wanadamu katika kuamini na kukubali na ni kumrahisishia nabii anayefuata kazi ya uhubiri na ulinganio.

Na kwa kuwa Uislamu na Mtume Muhammad vina umuhimu mkub- wa katika historia ya binadamu, na ukizingatia kuwa Uislamu ni dini inayohusu kila kitu na ndiyo dini ya mwisho huku Mtume(s.a.w.w ) akiwa ndiyo mtume wa mwisho, basi Uislamu huo ulibashiriwa tangu zamani na hilo limeelezwa na Qur’ani tukufu.

Kuna habari zilizoenea kabla ya Mtume kukabidhiwa utume ambazo zilikuwa zimebeba wasifu kamili wa Mtume Muhammadin(s.a.w.w ) na mazingira yake, zikiwataka watu wamwamini na wajiepushe na upotovu kwa kumfuata yeye.

Habari hizi zilisaidia baadhi ya Ahlul-Kitabu na wengineo kuamini dini ya Mtume Muhammad(s.a.w.w ) bila ya kuomba muujiza wowote mahsusi.

SOMO LA TATU: MAZINGIRA SAFI

Mazingira yana mchango mkubwa katika malezi ya mwanadamu, humfanya awe mwema au humharibu. Mazingira tunayokusudia hapa ni wale watu wanaomzunguka mwanadamu ambao mwanadamu huyu hupokea kutoka kwao misingi ya maarifa yake na lugha yake. Wanadamu ambao kupitia kwao hujifunza elimu na maarifa mbalimbali na huongoka kupitia kwao, kwani huathirika kulingana na wanadamu wanaomzunguka, hivyo yeye huwaathiri na wao humwathiri.

Familia ndio mazingira ya mwanzo ambayo wanadamu hukulia ndani yake wakiwemo manabii na walinganiaji wa tawhidi ambao walisi-mama kidete kupiga vita shirki, maadili machafu na mila potovu. Hakika Mwenyezi Mungu aliwaumba na kuwalea katika familia za tauhidi zenye kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu.

Baba wa manabii Adam(a.s ) ndiye aliyefundishwa majina yote na Mwenyezi Mungu kabla hajaletwa aridhini. Na yeye ndiye wa kwanza kumtakasa Mwenyezi Mungu na ndiye wa kwanza aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu katika tauhidi. Hivyo kwa mwenendo huo wakafuata manabii wote, manabii ambao wamehitimishwa na Muhammad(s.a.w.w ) .

MAZINGIRA YA MTUME (S.A.W.W) KWA MUJIBU WA MAELEZO YA AHLUL-BAYT

Imam Ali(a.s ) ameelezea mazingira ya tauhidi ambayo Mtume(s.a.w.w ) alitokana nayo akasema: “Akamteua kutokana na mti wa manabii, shubaka yenye mwanga, nywele za utosi wa watukufu na kitovu cha Makka”[20] “….Mahala pake alipoishi (Mfuko wa uzazi) ndiyo mahala bora, na chimbuko lake ndio chimbuko bora katika machimbuko ya madini ya utukufu na busati la amani .”[21]

“Hivyo akamleta toka ndani ya madini yenye chimbuko bora na asili tukufu, toka ndani ya mti ambao alikusudia kuwatoa ndani yake manabii na kuteua waaminifu wake kutoka humo.”[22]

“Kila Mwenyezi Mungu alipokiongeza kizazi kwa kugawa makundi mawili basi alikiweka kizazi chake katika kundi bora, kundi ambalo mzinifu hakuchangia chochote wala hakupata fungu lolote.”[23]

Pindi Qur’ani ilipotaja kuteuliwa kwa ajili ya ulimwengu wote Adam, Nuh, kizazi cha Ibrahim na kizazi cha Imran Mwenyezi Mungu aliendelea kwa kusema:

ذُرِّيَّةً بَعْضُهَا مِنْ بَعْضٍ وَاللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ {34}.

“Kizazi cha wao kwa wao na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusikia, Mwenye kujua” (Al Imrani: 34).

Akamtaja kipekee mtume wake wa mwisho kwa kusema:

وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ. الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ وَتَقَلُّبَكَ فِي السَّاجِدِينَ {219}.

“Na umtegemee Mwenye nguvu, Mwenye rehema. Ambaye anakuona unaposimama. Na mageuko yako katika wale wanao- sujudu (Shu’araa: 217-219).”

Hivyo wote waliomtangulia Muhammad walikuwa wakisujudu na kunyenyekea kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na wala hawajamshirikisha na chochote hata sekunde moja.

Imam Jafar As-Swadiq(a.s ) amefafanua geuko hili kwa kusema: “Ndani ya mifupa ya migongo ya manabii kulikuwa na nabii baada ya nabii mpaka akamleta toka mifupa ya mgongo wa baba yake kutokana na ndoa na wala si kwa uzinzi, hali hii ni tokea kwa Adam .”[24]

Nabii mwenyewe(s.a.w.w ) kaelezea hali hiyo waziwazi kwa kusema: “Nilihamishwa toka ndani ya mifupa ya migongo mitakasifu mpaka kwenye kizazi kitakasifu katika hali ya ndoa wala si hali ya uzinzi .”[25]

Pia akasema: “Hakika Mwenyezi Mungu alimteua Ibrahim toka kizazi cha Adam akamfanya kipenzi. Akamteua Isma’il toka kizazi cha Ibrahim. Kisha akamteua Nazari toka kizazi cha Isma’il. Kisha akamteua Mudhira toka kizazi cha Nazari. Kisha akamteua Kinana toka kizazi cha Mudhar. Kisha akamteua Qurayshi toka kizazi cha Kinana. Kisha akateua kizazi cha Hashim toka kizazi cha Qurayshi. Kisha akateua kizazi cha Abdul Muttalib toka kizazi cha Hashim. Kisha akaniteua mimi toka kizazi cha Abdul Muttalib.”[26]

MAZINGIRA YA MTUME (S.A.W.W) KWA MUJIBU WA MAELEZO YA WANAHISTORIA

Wanahistoria wameeleza wazi kuwa Abdul Muttalib alikataa kuabudu masanamu. Akampwekesha Mwenyezi Mungu, akatekeleza nadhiri. Akaanzisha mienendo ambayo mingi kati ya hiyo imetajwa na Qur’ani huku ikiridhiwa na Mtume(s.a.w.w ) kupitia sunna yake.

Kati ya mienendo hiyo ni kutimiza nadhiri, fidia ya ngamia mia moja, kutooa maharimu na kutoyaendea majumba kwa nyuma. Pia kukata mkono wa mwizi, kukataza kuwauwa watoto wa kike, maapizano, kuharamisha pombe, kuharamisha zinaa na kutoa adhabu kwa mzinifu. Kuteua kwa bahati, kukataza kutufu uchi, kumkirimu mgeni, kutokutoa kitu wanapohiji isipokuwa toka kwenye mali waipendayo na kutukuza miezi mitukufu.

Walipokuja watu wa tembo maquraishi waliikimbia Haram, Abdul Muttalib akawaambia: “Naapa kwa Mwenyezi Mungu sitoki haramu natafuta ushindi kupitia njia nyingine.”

Maquraishi wakawa wakisema: “Abdul Muttalib ni Ibrahim wa pili. Al-Masuudiy amesema: “Abdul Muttalib alikuwa akiwausia wanawe kuunga undugu, kulisha chakula na akiwatamanisha na kuwahofisha kufanya na kuaacha kitendo cha mtu anayetaraji siku ya Kiyama na ufufuo.”[27]

Al-Shahrastaniy amesema: “Alikuwa akiwaamrisha wanawe waache dhuluma na ujeuri. Akiwahimiza juu ya maadili mema. Akiwakataza mambo duni. Katika usia wake alikuwa akisema: Hakika dhalimu hatotoka ndani ya dunia hii isipokuwa baada ya malipo ya kisasi na kufikiwa na adhabu.”

Hivyo alipofariki mtu mmoja dhalimu ambaye hakufikiwa na adhabu, watu wakaanza kumuuliza Abdul Muttalib kuhusu hilo. Akafikiri na kusema: Naapa kwa Mwenyezi Mungu hakika nyuma ya nyumba hii kuna nyumba nyingine ambayo ndani ya nyumba hiyo mwema hulipwa wema wake na muovu ataadhibiwa kwa uovu wake.”[28]

MTOTO WA VICHINJWA VIWILI

Imam Ali Ridha(a.s ) aliulizwa kuhusu maana ya kauli ya Mtume: “Mimi ni mtoto wa vichinjwa viwili .” Akajibu: “Hakika Abdul Muttalib alijining’iniza katika mlango wa Kaaba akamuomba Mwenyezi Mungu amruzuku watoto kumi. Akaweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu kuwa atamchinja mmoja kati ya hao iwapo tu Mwenyezi Mungu atajibu dua yake.

Hivyo walipofika watoto kumi akasema: Hakika Mwenyezi Mungu kanitekelezea ombi langu, basi ni lazima nitekeleze nadhiri kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Akawaingiza wanawe Kaaba na kuanza mchakato kati yao, na hatimaye mchakato huo ukaangukia kwa Abdullah baba wa Mtume(s.a.w.w ) na ndiye aliyekuwa kipenzi chake sana.

Akarudia mara ya pili mchakato huo ukaangukia tena kwa Abdullah. Akarudia kwa mara ya tatu mchakato ukaangukia kwa Abdullah. Ndipo alipomchukua na kuazimia kumchinja. Wakakusanyika maquraishi na kumkataza asifanye hivyo.”[29]

Imam Al-Baqir(a.s ) amesema: “Mchakato ukaangukia kwa Abdullah. Akazidisha majina kumi lakini bado mchakato ukamwan- gukia Abdullah. Akaendelea kuzidisha majina kumi kumi mpaka yakafika mia moja ndipo mchakato ulipoangukia kwa ngamia. Hapo Abdul-Muttalib akasema: ‘Sikumtendea haki Mola wangu,’ hivyo akarudia mara tatu na mara zote ukaangukia kwa ngamia. Akasema: ‘Sasa nimejua kuwa Mola Wangu kaniridhia.’ Ndipo alipochinja ngamia .”[30]

AMINA BINTI WAHAB

Baada ya miaka kumi tangu kuchimbwa Zamzamu na baada ya mwaka mmoja12 tangu Abdullah kufidiwa kwa ngamia Abdul Muttalib alitoka na mwanae Abdullah na kuenda nae katika nyumba ya Wahab bin Abdul Manafi bin Zahrat (wakati huo alikuwa ndio bwana wa kizazi cha Zahrah kinasaba na kisharaf). Hapo akamposa binti wa Wahabi, Amina kwa ajili ya Abdullah.

Amina alikuwa ndiye mwanamke bora kinasaba na kimaadili kwa maquraishi, hivyo Abdul Muttalib akamuozesha na kummilikisha Abdullah, Amina. Ndani ya nyumba ya Abdul Muttalib ndimo Abdullah alimomuingilia Amina na kupata ujauzito wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w ) .[31]

Imam Ali(a.s ) amesema: “Amina binti Wahabi aliona usingizini kuwa anaambiwa: Hakika aliyomo tumboni mwako ni bwana, hivyo ukimzaa mwite Muhammad.” Kisha Ali(a.s ) akasema: “Hivyo Mwenyezi Mungu alimpa jina kutoka ndani ya jina lake, kwani hakika Mwenyezi Mungu ni Mahmudu na huyu ni Muhammad.”[32]

Hakika Abdullah alipata umashuhuri mkubwa akawa ni mtu muhimu kwa watu, akawa ndiyo mazungumzo yao na kipenzi chao. Baada ya tukio la kisa cha fidia yake, kisa ambacho kilifanana na kisa cha babu yake Isma’il…… Mwenyezi Mungu akamjalia kukutana na binti bora kati ya mabinti wa kiquraishi……lakini hakumjalia kuishi nae muda mrefu. Kwani utafutaji ulimpeleka Sham akiwa na maquraishi kwa ajili ya biashara.

Alielekea Gaza huku akiwa amemuacha mke wake mja mzito, na alipokuwa akirudi alielekea Madina kwa lengo la kuwazuru wajomba zake na kuzidisha undugu, lakini mipango ya Mwenyezi Mungu haikumpa muda, hivyo akaugua huko na rafiki zake kulazimika kumwacha na kurudi huku wakiwa wamebeba habari za ugonjwa wake na kufikisha kwa baba yake Abdul Muttalib.

Abdul Muttalib akamtuma Al-Harithi ambaye ni mwanae mkubwa ili akamuuguze ndugu yake mpaka apone kisha arudi nae Makka. Isipokuwa mipango ya Mwenyezi Mungu ilikuwa ikimuharakisha Abdullah, hivyo Al-Harithi hakufika Madina isipokuwa baada ya siku nyingi tangu kufariki kwa ndugu yake.[33]

Hivyo akarudi kwa baba yake akiwa na moyo wa huzuni, mwenye kutetemeka huku akibeba habari za kifo cha mtoto kipenzi kati ya watoto wa baba yake. Hakika ni habari nzito kwa Abdul Muttalib lakini hazikuteteresha subira yake wala hazikudhoofisha uvumilivu wake.

MUHTASARI

Hakika Mwenyezi Mungu aliweka umuhimu maalumu kwa manabii wake, hivyo akawezesha wazaliwe toka ndani ya familia takasifu ili wawe na uwezo wa kuwasafisha watu dhidi ya shirki. Hivyo ndivyo alivyomteua nabii Muhammad(s.a. w.w ) . Hakika alihama toka mifupa ya migongo mitakasifu yenye imani na toka mapaja ya utawa mpaka dunia ilipopata sharafu kwa kuzaliwa kwake.

Familia ya Mtume Muhammad(s.a.w.w ) ilikuwa ni familia na damu yenye kuheshimika, kwani yeye ametokana na nabii Ibrahim(a.s ) . Pia ilikuwa ikijihusisha na kulinda Haram ya Makka na kuitetea dhidi ya maadui.

Babu wa Mtume Abdul Muttalib aliishi zama ambazo ujumbe wa Mwenyezi Mungu ulikuwa umetoweka huku nguvu za shirki zikiwa zimedhihiri na ufisadi na dhuluma vikishamiri, lakini pamoja na hayo yote alikuwa ni mwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu huku akilingania maadili mema, na njia hiyo ndiyo waliyopita watoto wake.

Abdul Muttalib alimjali sana mwanae Abdullah, hivyo akamwozesha mwanamke bora toka familia na damu yenye heshima. Lakini matak- wa ya Mwenyezi Mungu yalitaka Abdullah afariki kabla ya kuzaliwa mwanae Muhammad(s.a.w.w ) .

SOMO LA NNE: MAISHA YA NABII WA MWISHO

Hakika Mwenyezi Mungu alipenda asimamie malezi ya Muhammad(s.a.w.w ) amtoe mikononi mwa familia yake ili awe chini ya ulinzi wake ikiwa ni maandalizi ya kupata familia kubwa ambayo kiongozi wake atakuwa ni Muhammad.

Familia ambayo haitopendelea taifa wala lugha au rangi bali mbora wao ndani ya familia hiyo ni yule tu mwenye uchamungu. Hivyo Qur’ani imeelekeza maana hii kwa kusema: “Je hakukukuta ni yatima akakuhifadhi?” (Dhuha: 6). Mtume akaelezea kwa kusema: “Hakika Mola wangu alinilea akaboresha maadili yangu .”[34]

Hakika busara za Mwenyezi Mungu zilimnyima Muhammad(s.a.w.w ) mapenzi na huruma ya muda mfupi huku Mwenyezi Mungu akimpangia huruma na mapenzi ya muda mrefu usio na kikomo, kwani alimuhifadhi kwa babu yake kisha kwa ami yake, hivyo hao wawili wakawa wakimpendelea zaidi ya nafsi zao na zaidi ya watoto wao wa kuzaa.

Katika njia hiyo ya malezi wakatoa kila aina ya mapenzi na huruma kwa kiwango ambacho wazazi hawawezi kujitolea kwa watoto wao wa kuzaa.

Hilo ni miongoni mwa fadhila za Mwenyezi Mungu kwa Mtume(s.a.w.w ) bali hakika alimfanyia umuhimu maalumu pindi alipojitolea mwenyewe kumlinda na kumuhami kwa huruma yake, na hakika hakuna neema kubwa kama hii ambayo kaielezea Mwenyezi Mungu kwa kusema: “Na hakika fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yako ni kubwa .”[35]

KUZALIWA KWAKE: ZAMA, SEHEMU NA NAMNA

Alizaliwa(s.a.w.w) katika mji wa Makka ndani ya mwaka wa ndovu (tembo) mwezi wa mfungo sita.

Kwa Shia Imamiya ni mashuhuri kuwa alizaliwa alfajiri ya siku ya ijumaa ya terehe kumi na saba. Kwa wengine mashuhuri ni kuwa alizaliwa siku ya jumatatu terehe kumi na mbili wakati wa kuchomoza alfajiri au jua au wakati wa kukengeuka jua.

Lililo mashuhuri toka kwa Amina binti Wahabi kama alivyoelezea Ibnu Is’haqa ni kuwa: “Wakati Amina alipokuwa akielezea siku za mimba ya Mtume(s.a.w.w) alisema: Hakika Amina aliona nuru ikitoka mpaka akaona makasiri ya Basra kutokea ardhi ya Sham. Akaambiwa hakika wewe umembeba bwana wa umma huu, hivyo atakapotua aridhini sema: Namkinga kwa Mwenyezi Mungu mmoja dhidi ya shari ya kila hasidi, kisha mwite Muhammad.”[36]

Halima binti Dhuaybu As-Saadiyyah ameongeza kuwa: “Amina alisema: ‘Kisha naapa kwa Mwenyezi Mungu hakuna mimba niliyoona ni nyepesi kwangu na rahisi kama yake .”[37]

Al-Yaaqubiy amesema: “Alipozaliwa Muhammad(s.a.w.w) mashetani yalilaaniwa na nyota ziliporomoka, watu wakasema: Hakika hii ni alama ya Kiyama, watu wakapatwa na tetemeko la ardhi ambalo lilienea dunia nzima mpaka makanisa na mahekalu yakabomoka, na kikatoka sehemu yake kila kilichokuwa kikiabudiwa kinyume na Mwenyezi Mumgu.

Mambo ya kichawi yakaharibika na mashetani wao wakafungwa, kasri la Kisra likatetemeka hivyo yakaporomoka masharafu kumi na tatu na moto wa Farsi ukazimika.

Kabla ya hapo ulikuwa na muda wa miaka elfu bila kuzimika….Mtu kati ya Ahlul-kitabi alikwenda kwa maquraishi akiwemo Hisham bin Al-Mughirah, Al-Walid bin Al-Mughirah na Al-Utba bin Rabia akasema: “Usiku huu kazaliwa mtoto kwa ajili yenu[38] ……..ndani ya usiku huu kazaliwa nabii wa umma huu naye ni Ahmad wa mwisho……Kisha akatoa alama zinazomtambulisha.”[39]

KUNYONYA KWAKE

Maziwa ya mwanzo aliyonyonya baada ya maziwa ya mama yake mzazi yalikuwa ni ya Thuwaybah mjakazi wa Abu Lahabi bin Abdul Muttalib. Hiyo ilikuwa ni kabla hajanyonyeshwa na Halima binti Abu Dhuaybu As-Saadiyyah,[40] kwani watu wa Makka walikuwa wakiwanyonyesha watoto wao kwa wanawake wa vijijini kwa lengo la kutaka ufasaha.

Ushahidi juu ya hilo ni kauli yake mwenyewe(s.a.w.w) : “Mimi ndiye mfasaha kuliko wote wanaotamka kiarabu, zaidi ya hapo mimi ni mkurayshi na nimenyonyeshwa na watoto wa Saad .”

Alibakia(s.a.w.w) mikononi mwa Halima muda wa miaka miwili mpaka alipoacha kunyonya, ndipo Halima akamkabidhi kwa mama yake na kumpa habari za baraka zote alizoziona, hapo Amina akam- rudisha kwa Halima kisha baadae Halima akamrudisha kwa mama yake huku Mtume(s.a.w.w) akiwa na umri wa miaka mitano.[41]

MAJINA YAKE NA MAJINA YAKE YA HESHIMA

Muhammad bin Jubayri bin Mut’im amepokea toka kwa baba yake kuwa alimsikia Mtume(s.a.w.w) akisema: “Hakika mimi nina majina kadhaa: Mimi ni Muhammad, Ahmad na mfutaji, Mwenyezi Mungu atafuta ukafiri kupitia mimi. Na mimi ni mkusanyaji, Mwenyezi Mungu atakusanya watu chini ya nyayo zangu. Na mimi ndiye niliyefuata baadae hakuna mwingine yeyote baada yangu .”[42]

Jina lake la heshima lililo maarufu ni: Abu Qaasim. Imepokewa kutoka kwake kuwa alisema: “Jiiteni kwa jina langu lakini msijipe heshima kwa jina langu la heshima.”10 Pia inasemekana kuwa jina lake la heshima ndani ya Taurati ni: Baba wa wajane, na jina lake ni: Swahibul-Malhama.[43]

Al-Halbiy amesema: “Ni wazi kuwa majina yake yote yametokana na sifa za vitendo alivyotenda ambavyo vinalazimu sifa na ukamilifu, hivyo ndani ya kila sifa ana jina.”[44]

VIPINDI VYA MAISHA YAKE

Maisha ya Mtume(s.a.w.w) mwanzo yamegawanyika katika vipindi viwili tofauti:

Kipindi cha kwanza: Ni kuanzia alipozaliwa mpaka alipokabidhiwa unabii, nacho ni kipindi cha miaka arubaini.

Kipindi cha pili: Ni kuanzia alipokabidhiwa unabii mpaka alipofariki, nao ni muda wa miaka ishirini na tatu.

Katika vipindi vyote vya maisha yake, Muhammad bin Abdullah(s.a.w.w) alijulikana kwa maadili mema, kujitenga na vitendo vya shirki, kujitenga na unywaji pombe, kutokuhudhuria vikao vya upuuzi, kamari na zaidi ya hayo ambayo vijana wa zama hizo walikuwa wakivutiwa nayo. Kutokana na maadili yake mema alijulikana kwa jina la mwaminifu, hivyo maquraishi walipozozana kuhusu mtu atakayeweka jiwe jeusi waliangukia kwenye uamuzi wa Muhammad(s.a.w.w) huku wakikiri kuwa yeye ni mwaminifu asiyeyumba.

Wanahistoria wote wamekiri kuwa Muhammad(s.a.w.w) hakuwahi kuabudu sanamu na alikuwa akichukizwa na masanamu hayo. Alikuwa akihamia pango la Hira kila mwaka muda wa mwezi mzima……Pia alikuwa mbali na sifa za kijahiliya ambazo walikuwa nazo vijana wa kiarabu wa zama hizo. Bali alikuwa akikataza ibada ya masanamu pale anapopata fursa ya kufanya hivyo.

Kila kipindi kati ya vipindi vya maisha yake kimegawanyika sehemu nyingi, hivyo kipindi cha kwanza unaweza kukigawa sehemu tatu:

Sehemu ya kwanza: Ni kuanzia alipozaliwa mpaka aliposafiri safari yake ya kwanza ya Sham akiwa na ami yake Abu Talib. Kipindi hicho alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili.

Sehemu ya pili: Ni kuanzia pale aliporudi kutoka Sham mpaka alipomuoa Khadija. Kipindi hicho alikuwa na umri wa miaka ishirini na tano.

Sehemu ya tatu: Ni kuanzia alipooa mpaka alipokabidhiwa unabii akiwa na umri wa miaka arubaini.

Kipindi cha pili kimegawanyika zama mbili tofauti:

Zama za kwanza : Nazo ni zama za Makka ambazo zilichukua muda wa miaka kumi na tatu.

Zama za pili : Nazo ni zama za Madina[45] ambazo zilichukua muda wa miaka kumi.

MUHTSARI

Ni maarufu kuwa Mtume Muhammad(s.a.w.w) alizaliwa yatima. Na mama yake Amina binti Wahabi aliona baadhi ya alama zilizojulisha kuwa mwanae atakuwa na jambo kubwa na cheo cha juu.

Hakukuwa na kalenda maarufu ya kuhifadhi kumbukumbu za matukio, hivyo historia ya kuzaliwa Mtume(s.a.w.w) imehifadhiwa na tukio la kuhujumiwa kwa Kaaba, tukio ambalo hujulikana kwa jina la tukio la tembo. Qur’ani imeashiria tukio hili la kihistoria ndani ya Sura Al-Fiylu.

Ukoo wa Abdul Muttalib ulimjali sana Muhammad bin Abdullah(s.a.w.w) . Hilo lilidhihirika pale walipompeleka kunyonya kwa Bani Saad kwani baada ya maziwa ya mama yake walimpeleka kijijini ili akanyonye katika mazingira ya afya na ufasaha wa lugha.

Mtume ana majina mazuri, sifa nzuri na majina mazuri ya heshima. Maisha ya Mtume(s.a.w.w) yalichukua miaka sitini na tatu huku yakigawanyika vipindi viwili vikuu: Cha kwanza: Kuanzia alipozaliwa mpaka alipokabidhiwa unabii. Muda wake ni miaka arubaini. Cha pili: Kuanzia alipokabidhiwa unabii mpaka alipofariki. Muda wake ni miaka ishirini na tatu.

SOMO LA TANO: TABIA NA MWONEKANO WA HITIMISHO LA MANABII (S.A.W.W)

NDANI YA QUR’ANI TUKUFU

Hakika Muhammad bin Abdullah alisifika kwa sifa nzuri na maadili bora ambayo yalimtofautisha na kila aliyeishi katika zama zake au kabla yake au aliyekuja baada yake, hivyo ndio maana akawa ni mbora wa manabii. Hakika ukamilifu wake umeelezwa wazi na Qur’ani kupitia maelezo yake matukufu. Qur’ani imeelea ukamilifu wa akili yake na ubora wa maadili yake kwa kusema: “Kwa neema ya Mola wako wewe si mwenda wazimu.* Na kwa hakika una malipo yasiyokatika.*Na bila shaka una tabia njema tukufu .”[46]

Utumwa wake kwa ajili ya Mwenyezi Mungu umeonyeshwa na kauli ya Mwenyezi Mungu: “Utukufu ni wake ambaye alimpeleka mja wake usiku kutoka msikiti mtukufu mpaka msikiti wa mbali .”[47]

Ama ukunjufu wa kifua chake umeashiriwa na Aya: “Je hatukuku- panulia kifua chako?”[48] Ama kumfuata kwake Mwenyezi Mungu katika kila kitu huku akimwogopa na kumnyenyekea yeye tu kumeelezwa na Aya: “Sifuati ila ninayofunuliwa kwa wahyi. Hakika mimi naogopa nikimwasi Mola wangu adhabu ya siku iliyo kuu .”[49] Ushahidi mwingine ni Aya: “Wale wanaofikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na kumwogopa yeye wala hawamwogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye atoshaye kuhesabu .”[50]

Ama huruma yake na upole wake kwa walimwengu huku akiwahangaikia watu ili kuwaongoza waelekee kwa Mwenyezi Mungu kumeelezwa na Aya: “Nasi hatukukutuma ila uwe rehema kwa walimwengu.[51] Na akasema: “Bila shaka amekufikieni Mtume kutoka miongoni mwenu, yanamhuzunisha yanayokutaabisheni, anakuhangaikieni, kwa waumini ni mpole, mwenye kuwaonea huruma.”[52] Na Aya isemayo: “Enyi watu wa kitabu, hakika amek- wisha kufikieni mtume wetu, anayekubainishieni mengi mliyokuwa mkiyaficha katika kitabu, na kusamehe mengi”[53] inaonyesha msamaha wake.

Ama Aya isemayo: “Sema: Hii ndiyo njia yangu ninalingania kwa Mwenyezi Mungu kwa ujuzi, mimi na wanaonifuata, na Mwenyezi Mungu ametakasika na kila upungufu wala mimi simo miongoni mwa washirikina[54] inaonyesha ufahamu wake na kudumu kwake katika njia ya uongofu wa Mola wake.

Pia hali hiyo inathibitishwa na Aya isemayo: “Sema: Na uite kwa Mola wako, bila shaka wewe uko juu ya mwongozo ulio sawa ”.[55] Na ile isemayo: “Basi tegemea kwa Mwenyezi Mungu hakika wewe uko juu ya haki iliyo wazi.”[56] Pia ile isemayo: “Yeye ndiye aliyemtuma mtume wake kwa mwongozo na kwa dini ya haki ili ishinde dini zote, ingawa washirikina wat- achukia.”[57] Zote hizo zinathibitisha hali hiyo.

Aya ifuatayo: “Ambao wanamfuata mtume, nabii aliyoko Makka, ambaye wanamwona ameandikwa kwao katika Taurati na Injili, ambaye anawaamrisha mema na anawakataza yaliyo mabaya na kuwahalalishia vizuri na kuwaharamishia maovu, na kuwaondolea mizigo yao na minyororo iliyokuwa juu yao.”[58] inathibitisha kutojifunza kwake toka kwa mtu yeyote huku akimkomboa mwanadamu dhidi ya kila aina minyororo.

Ama uadilifu na usawa wake katika maadili na mwenendo wake umeashiriwa na Aya isemayo: “Na hivyo tumekufanyeni umati bora ili muwe mashahidi juu ya watu, na Mtume awe shahidi juu yenu.”[59]

Aya ifuatayo: “Bila shaka mnao mfano mwema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, kwa mwenye kumwogopa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na kumtaja Mwenyezi Mungu sana.”[60]

Imethibitisha kuwa yeye ndiye mfano wa kuigwa katika ukamilifu wa mwanadamu. Ama utawala wake juu ya viumbe na cheo chake juu yao umethibitishwa na Aya isemayo: “Hakika kiongozi wenu hasa ni Mwenyezi Mungu na Mtume wake.”[61]

Aya ifuatayo: “Muhammad mtume wa mwenyezi Mungu na walio pamoja naye ni imara mbele ya makafiri na wenye kuhurumiana wao kwa wao[62] inathibitisha jinsi alivyo mkali dhidi ya wapinzani na makafiri.

Ama Aya ifuatayo: “Ewe Nabii, kwa hakika sisi tumekutuma shahidi na mtoaji wa habari nzuri na muonyaji. Na muhitaji kwa Mwenyezi Mungu kwa idhini yake na taa itoayo nuru.”[63] inathibitisha ufasaha wake, kuhusika kwake katika kila jukumu na kuwaongoza watu.

NDANI YA MAELEZO YA BWANA WA MAWASII (A.S)

Imam Ali(a.s ) amesema: “ ……Mpaka Mwenyezi Mungu alipomtuma Muhammad shahidi, mtoaji wa habari njema, mwonyaji, mbora wa viumbe kati ya watoto wote, na mbora wa viumbe watakasifu kati ya wakongwe wote, mtakasifu wa maadili kati ya watakasifu wote, na mbora wa ukarimu kati ya wakarimu wote .”[64]

“Akamteua kutokana na mti wa manabii, shubaku yenye mwanga, nywele za utosi wa watukufu…… na chemchemu ya hekima, tabibu maarufu kwa tiba yake, yuko tayari kwa dawa yake huku akifuatilia kwa hiyo dawa yake kila sehemu yenye mghafiliko na sehemu za shaka.”[65]

“Nakiri kuwa Muhammad ni mja Wake na Mtume Wake aliyemteua kati ya viumbe Wake, aliyeteuliwa kwa ajili ya kubainisha ukweli halisi, aliyeteuliwa mahsusi kwa ajili ya miujiza mitukufu na ujumbe mtakatifu, mwenye kubainisha alama za uongofu kupitia ujumbe huo, hivyo mwenye kujitenga naye yumo katika upotevu mkubwa.”[66]

“Hakika Mwenyezi Mungu alimtuma Muhammad huku ndani ya waarabu hakuna anayejua kusoma kitabu wala anayedai unabii, hivyo akawapeleka watu mpaka akawafikisha sehemu yao, huku akiwafikisha eneo la uokovu wao, hivyo njia yao ikanyooka na sifa zao zikatulia.”[67]

Hivyo akavuka kiwango katika kutoa nasaha, akafuata njia sahihi na kulingania hekima na mawaidha mazuri .”[68]

“Mwenye kutangaza haki kupitia haki, mwenye kuondoa mchemko wa batili, na mwenye kuangamiza ukali wa upotovu. Kama alivyobebeshwa ndivyo alivyoinuka huku akisimama kwa nguvu zote kupitia amri yake. Mwenye kuharakisha katika kupata ridhaa Zako huku akiwa haogopi kwenda vitani wala si dhaifu katika nia. Mwenye kuhifadhi ufunuo Wako, mwenye kulinda ahadi Yako huku akiendelea kutekeleza maamrisho Yako……..Hivyo yeye ni mwaminifu mwenye kuaminika na muhazini wa elimu Yako ya siri.”[69]

“Imam wa atakayemcha Mwenyezi Mungu na jicho la atakayeongoka.”[70]

“Hivyo akapambana katika njia ya Mwenyezi Mungu dhidi ya wale waliyomkimbia na dhidi ya wale waliyojitenga Naye……..[71] kwa ajili ya kutetea dini Yake, huku haumzuwii kufanya hivyo mkusanyiko wa wote wenye kumpinga na ule wa wenye kutaka kuzima nuru yake.”[72]

“Ilikuwa tukizidiwa na ukali wa vita tunajikinga kwa mtume, hivyo hakuna yeyote kati yetu aliyekuwa karibu na adui zaidi yake.”[73]

“Hivyo muige Mtume wako mbora wa watakasifu. Hakika katika kumuiga kuna kigezo chema kwa atakayeiga. Aliidokoa dunia na wala hakuitamani kabisa, hivyo yeye ndiye aliyeiacha dunia bila kuijali, na ndiye aliyeliacha tumbo tupu bila dunia…… Alipewa dunia yote akakataa kuipokea………..Alikuwa akila huku kakaa aridhini, alikaa mkao wa mtumwa huku akishona viatu vyake kwa mkono wake……..Alitoka duniani bila kustarehe na nayo, na alifika akhera akiwa salama, hivyo hakulimbikiza kitu mpaka alipofariki.”[74]

Imepokewa kutoka kwa Hasan bin Ali(a.s ) kuwa Hindu bin Abi Halati alitoa wasifu wa Mtume(s.a.w.w ) kwa kusema: “Huanza kumtolea salamu yule aliyekutana naye……..Daima alikuwa na huzuni, mwingi wa tafakuri muda wote, mwimgi wa ukimya, hazungumzi pasipo na haja ya kuzungumza, huzungumza yenye kutosheleza, hazungumzi yasiyo na maana wala yaliyo pungufu, si mwenye kun- yanyapaa wala si mwenye kudharau.”

Hivyo neema ndogo kwake ilikuwa kubwa, haikashifu neema yoyote. Wala dunia na kichache alichokipata havimkasirishi. Anapopewa haki hakuna anayefahamu, wala hakutenda jambo kwa ghadhabu mpaka atakapoimiliki……..Anapoghadhibika huacha na kuondoka, na anapofurahi hubana sauti yake bali alama ya kucheka kwake ni tabasamu lake.

NDANI YA DONDOO ZA SERA YAKE KIJAMII

Husein bin Ali(a.s ) amepokea Hadithi kutoka kwa baba yake Imam Ali(a.s ) inayozungumzia sera ya Mtume(s.a.w.w ) kijamii:

“Anapokuwa nyumbani kwake hugawa muda wake mafungu matatu: Fungu kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Fungu kwa ajili ya wakeze na fungu kwa ajili ya nafsi yake. Kisha fungu lake huligawa kwa ajili yake na kwa ajili ya kuhudumia jamii.

Mwenendo wake katika kuhudumia umma ulikuwa ni kuwatanguliza wale wenye ubora huku akigawa ubora wao kulingana na ubora wao katika dini.

Alikuwa akizuia ulimi wake isipokuwa katika yale yanayomuhusu huku akiwaunganisha pamoja bila kuwasambaratisha. Humheshimu mheshimiwa wa kila kundi huku akimtawalisha juu yao. Hujihadhari na kujilinda dhidi ya watu bila ya kupunguza bashasha yake wala tabia yake. Huwatafuta maswahaba zake wasipoonekana huku aki- ulizia matatizo ya watu.

Hulisifia jema na kulipa nguvu, na hulisifu kwa ubaya lile lililo baya huku akilishusha thamani. Jambo lake huwa wastani wala haghafiliki na kitu….Hapunguzi wala hazidishi huku aliye mbora mbele yake ni yule mwenye kuwanasihi sana waislam.

Na mwenye hadhi kubwa sana mbele yake ni yule mwenye kuwasaidia na kuwanusuru watu. Hakai wala hasimami ila akimtaja Mwenyezi Mungu. Humpa kila aliyekaa naye fungu lake, hivyo anapokaa na mtu humvumilia mpaka mtu yule aondoke mwenyewe.

Amwombaye haja yoyote humjibu kwa kumtekelezea haja yake na kwa kauli tamu. Kikao chake ni kikao cha heshima, ukweli na uaminifu. Muda wote alikuwa ni mwenye bashasha, mwenye tabia nyepesi, mpole, asiye mkali wala si mkavu wa tabia. Hakuwa mchekaji ovyo wala mtukanaji, hakuwa mwaibishaji au mwongeza chumvi katika kusifia.

Hujighafilisha na yale asiyoyapenda, hivyo alikuwa akinyamaza kwa sababu ya mambo manne: Kwa sababu ya busara, tahad- hari, ridhaa, na tafakari.”[75]

MUHTASARI

Mwenyezi Mungu katoa wasifu wa Mtume Wake Muhammad(s.a.w.w ) kwa kueleza sifa zake za ukamilifu wa kibinadamu, hivyo akamfanya mbora wa mitume, hitimisho lao, na kigezo chema amba- cho watakiiga wanadamu ili wanadamu hao wafikie kilele cha ukamilifu. Mwenyezi Mungu kawafafanulia waigaji sifa zake na maadili yake mazuri mema.

Kizazi chake ambacho ndio kijuacho zaidi yale yaliyomo nyumbani kimetoa wasifu wa mbora wao na mjumbe mwaminifu kupitia maneno yaliyo timilifu yaliyokusanya sifa zote. Huku maneno hayo yakitoa taswira ya ukamilifu na sifa ambazo zimemfanya awe ni kiigizo chema kwa wanaomfuata na bendera kwa wenye kuongoka.

Maelezo hayo yaliyonukuliwa kutoka kwa kizazi chake yametoa taswira ya adabu ya hali ya juu ya Mtume(s.a.w.w ) na sera yake binafsi na ya kijamii ya hali ya juu.

SOMO LA SITA: TABIA NA MWONEKANO WA HITIMISHO LA MANABII (S.A.W.W)

MSOMI ASIYEWAHI KUSOMA WALA KUANDIKA

Kati ya sifa za kipekee alizonazo Mtume wa mwisho(s.a.w .w ) ni kuwa yeye hakujifunza kusoma wala kuandika kutoka kwa mwalimu yeyote yule wa kibinadamu,[76] wala hakukulia katika mazingira ya kielimu bali alikuwa ndani ya jamii ya wajinga.

Hakuna yeyote aliyepinga ukweli huu uliyoelezwa na Qur’ani tukufu, bali alikuwa ndani ya jamii ambayo watu wake walikuwa ni wajinga sana kuliko watu wa jamii nyingine yoyote ile, lakini pamoja na hali hiyo alileta Kitabu kinacholingania elimu na maarifa, kikiamsha fikra na akili huku kikiwa kimekusanya aina zote za maarifa.

Hakika Mtume(s.a.w.w ) alianza kuwafunza watu Kitabu na hekima[77] kwa silabasi nzuri sana mpaka akaibua ustaarabu wa kipekee ambao ulizamisha Magharibi na Mashariki kupitia elimu na maarifa yake, na bado mpaka leo nuru yake inang’aa, hivyo yeye Mtume(s.a.w.w ) ni mtu asiyewahi kusoma wala kuandika lakini alikuwa aking’oa ujinga, ujahili na ibada za masanamu huku akiwa amewaletea wanadamu dini ya hadhi ya juu na sheria ya kimataifa ambayo itawafaa wanadamu muda wote wa maisha yao.

Hivyo kupitia elimu, maarifa yake, maneno yake timilifu, ubora wa akili yake, mafunzo yake na silabasi yake ya malezi yeye mwenyewe huwa ni muujiza, kwa sababu hiyo Mwenyezi Mungu akasema:

“Basi mwaminini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake nabii asiyewahi kuandika wala kusoma, ambaye anamwamini Mwenyezi Mungu na maneno yake, na mfuateni ili mpate kuongoka.”[78]

Hakika Mwenyezi Mungu alimfundisha yale aliyokuwa hayajui na akamfunza kitabu na hekima mpaka akawa nuru, taa yenye kuangaza, dalili, shahidi, mtume wa wazi, mshauri nasaha mwaminifu, mkum- bushaji, mwenye kutoa habari njema na mwenye kuonya.[79]

Yeye ndiye aliyemkunjua kifua kwa ajili yake, akamwandaa kupokea ufunuo na kutekeleza jukumu la kuongoza katika jamii ambayo ilikuwa imetawaliwa na ubaguzi, chuki na majivuno ya kijahiliya. Hivyo akawa ni kiongozi bora wa hali ya juu aliyetambuliwa na wanadamu katika uhubiri, malezi na mafunzo.

MWISLAMU WA KWANZA NA MBORA WA WANAIBADA

Hakika kilele cha mwanzo ambacho ni lazima kwa kila mwanadamu akifikie ili ajiandae kuteuliwa na kuchaguliwa na Mwenyezi Mungu ni unyenyekevu kamili kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Muumba wa ulimwengu. Pia kujisalimisha kiukamilifu mbele ya nguvu Zake tuku- fu na hekima zake kamilifu. Pia utumwa wa hiari uliotimia mbele ya Mwenyezi Mungu mmoja wa pekee aliye tegemeo.

Hakika Qur’ani tukufu imemtolea ushahidi nabii huyu aliyewapita manabii wote katika kila kitu, ikasema: “Na mimi ni wa kwanza wa waliojisalimisha.”[80]

Hakika hicho ni kilele cha ukamilifu ambacho alikifikia mja huyu mkweli katika ibada zake, na akawa kawapita watu wote kwa ujumla. Hakika unyenyekevu wake wa kweli ulidhihirika katika matendo na kauli zake, hivyo akasema: “Kitulizo cha macho yangu ni Swala.”[81]

Hakika Swala ilipendezeshwa kwake kama yalivyopendezeshwa maji kwa mtu mwenye kiu, hivyo anywapo maji hukata kiu, lakini Mtume(s.a.w.w ) hakukatwa kiu na Swala, kwani daima aliusubiri kwa hamu muda wa Swala huku shauku ya kusimama mbele ya Mola wake ikiongezeka. Alikuwa akimwambia mwadhini wake: “Tupe raha ewe Bilal”[82] .

Imepokewa kuwa alikuwa akizungumza na familia yake na wao wakimzungumzisha lakini unapoingia wakati wa Swala huwa kama vile hawajui na hawamjui.[83] Kipindi anaposali kifua chake hutoa sauti ya kutetemeka kama sauti ya mchemko wa chungu huku akilia kutokana na kumwogopa Mwenyezi Mungu mtukufu hadi msala wake unalowana[84] .

Hivyo alikuwa akisali mpaka nyayo zake zinatoa harufu. Watu humwambia unafanya hivyo ilihali Mwenyezi Mungu ame- shakusamehe madhambi yako yaliyotangulia na yaliyofuatia. Hujibu: “Hivi haifai nikawa mja mwenye kushukuru?”[85]

Alikuwa akifunga mwezi wa Shabani na Ranadhani na siku tatu ndani ya kila mwezi,[86] huku akibadilika rangi uingiapo mwezi wa Ramadhani, Swala zake huongezeka huku akinyenyekea katika dua.[87]

Linapoingia kumi la mwisho la Ramadhani hujitenga na kuwahama wakeze huku akiupitisha usiku akiwa faragha kwa ajili ya ibada.[88]

Alikuwa akisema: “Dua ndiyo roho ya ibada, silaha ya muumini, nguzo ya dini na nuru ya mbingu na ardhi .”[89]

Daima alikuwa katika mawasiliano na Mwenyezi Mungu, akijifunga kwake kwa unyenyekevu na dua katika kazi yoyote ile kubwa au ndogo, bali alikuwa akimwomba Mwenyezi Mungu msamaha na kutubu kila siku mara sabini bila ya kuwa na dhambi yoyote.[90]

Hakuamka usingizini ila ni mnyenyekevu mwenye kusujudu.[91]

Alikuwa akimhimidi Mwenyezi Mungu kila siku mara mia tatu sitini akisema: “Kila sifa njema ni ya Mwenyezi Mungu Mola wa ulimwengu wote, na ni nyingi katika kila hali.”

Daima alikuwa akisoma Qur’ani huku akiwa ni mwenye kushughulishwa sana na usomaji huo. Imani isiyo na mipaka kwa Mwenyezi Mungu:

Mwenyezi Mungu amemhimiza Mtume Wake(s.a.w.w) awe na imani isiyo na mipaka na Mola Wake kwa kusema: “Je, Mwenyezi Mungu hamtoshei mja wake?”[92]

Pia alisema: “Na umtegemee Mwenye nguvu, Mwenye rehema.* Ambaye anakuona unaposimama.* Na mageuko yako katika wale wanaosujudu.”[93]

Imepokewa kutoka kwa Jabir (r.a) kuwa: “Tulikuwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w ) tukafika kwenye mti wenye kivuli tukamwachia mti huo. Ghafla akatokea mtu kati ya mushrikina huku upanga wa Mtume(s.a.w.w ) ukiwa umetungikwa kwenye mti, ndipo mushrik yule alipouchukua upanga ule na kumwambia Mtume(s.a.w.w ) : “Je unaniogopa? “ Mtume akajibu: “Hapana.” Mushriku akasema: “Nani atakuzuwia dhidi yangu?” Mtume akajibu: “Mwenyezi Mungu.” Hapo upanga ukadondoka toka mikononi mwa mushriku.

Ndipo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipouchukua na kusema: “Na wewe ni nani atakayekuzuwia dhidi yangu?” Akajibu: ‘Mbora wa wachukuaji.” Mtume akasema: “Je unakiri kuwa hapana mola wa haki isipokuwa Allah na kwamba hakika mimi ni Mtume wa Allah?” Mushriku akajibu: “Hapana, isipokuwa ninakuahidi kuwa sitokupiga vita, wala sitokuwa pamoja na watu wanaokupiga vita.

Hapo Mtume akamwachia, na mushriku akaenda kwa jamaa zake na kuwaambia: “Nimewajia toka kwa mbora wa watu.”[94]

USHUJAA WA HALI YA JUU

Mwenyezi Mungu ameeleza sifa za Mtume Wake(s.a.w.w ) kwa kusema: “Wale wanaofikisha ujumbe wa Mwenyezi Mungu na kumwogopa Yeye wala hawamwogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye atoshaye kuh- esabu.”[95]

Imam Ali(a.s ) ambaye mashujaa wa kiarabu waliinamisha vichwa mbele yake ametupa wasifu makini kuhusu ushujaa wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w ) akasema: “Pindi vita vinapokuwa vikali na kundi moja likalizidi kundi lingine basi tulikuwa tukijikinga kwa Mtume, hivyo hakuna yeyote anayekuwa karibu sana na maadui kuliko yeye.”[96]

Mikidad ameelezea msimamo wa Mtume(s.a.w.w ) siku ya Uhud baada ya watu kutawanyika huku wakimwacha Mtume(s.a.w.w ) peke yake, Mikidad amesema: “Naapa kwa yule aliyemtuma kwa haki, ukimwona Mtume(s.a.w.w ) kainua mguu wake shibri moja basi ujue yuko mbele ya adui huku kundi la jamaa wa adui likiwa limemvamia na muda huo huo likitawanyika kwa kumkimbia, utamwona kasimama akirusha upinde au akirusha jiwe mpaka mawe yawaenee.”[97]

UTAWA USIYOKUWA NA MFANO

Mwenyezi Mungu amesema kumwambia Mtume Wake(s.a.w.w ) kuwa: “Wala usivikodolee macho yako tulivyowastarehesha watu wengi miongoni mwao, ni mapambo ya maisha ya dunia, ili tuwajaribu kwa hayo, na riziki ya Mola Wako ni bora mno na iendeleayo.”[98]

Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu alikuwa mkweli katika kuiacha dunia na mapambo yake. Aliiacha dunia mpaka ikapokewa toka kwa Abu Umamah toka kwa Mtume(s.a.w.w ) kuwa alisema: “Mola Wangu alinitunukia akataka aifanye Makka yote iwe dhahabu kwa ajili yangu, nikasema: Hapana Mola Wangu! lakini napenda niwe nashiba siku moja na kushinda na njaa siku nyingine……..Kwani nitakapokuwa na njaa nitakunyenyekea na kukukumbuka, na nitakaposhiba nitakushukuru na kukuhimidi”.[99]

Akalala juu ya changarawe na alipoamka zilikuwa zimeathiri ubavu wake. Akaambiwa: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu tungekuwekea kizuwizi.” Akajibu: “Mimi nina nini na hii dunia, kwani mimi si chochote ndani ya dunia hii isipokuwa ni kama msafiri aliyejipumzisha chini ya mti wa kivuli na baada ya mapumziko ataon- doka na kuuacha ule mti.”

Ibnu Abbas amesema: “Mtume(s.a.w.w ) alikuwa akilala njaa siku zenye kufuatana, huku familia yake ikiwa haipati chakula cha usiku. Mara nyingi mkate wao ulikuwa ni mkate wa shairi.”

Aisha amesema: “Familia ya Muhammad haikula milo miwili ndani ya siku moja isipokuwa mlo mmoja ulikuwa ni tende tu.”[100]

Akamwambia mtoto wa dada yake Urwah: “Hakika sisi tulikuwa tukiutazama mwezi mwandamo, kisha mwezi mwandamo mwingine hadi miezi miandamo mitatu katika miezi miwili huku ndani ya muda wote huo haujawashwa moto katika nyumba za Mtume(s.a.w.w ) .”

Urwah akamuuliza: “Ewe mama mdogo; alikuwa akiwalisha nini usiku?” Akajibu: “Vyeusi viwili: Tende na maji. Isipokuwa Mtume alikuwa na jirani yake wa kianswari aliyekuwa na mifugo, hivyo alikuwa akimpa Mtume wa Mwenyezi Mungu maziwa yake na Mtume anatupa sisi.”[101]

Pia amesema: “Mtume(s.a.w.w ) alifariki huku ngao yake ikiwa imewekwa rehani kwa yahudi kwa thamani ya vibaba thelathini vya shairi.”[102]

Imepokewa toka kwa Anas bin Malik kuwa: “Fatima(a .s) alimpelekea Mtume(s.a.w.w ) kipande cha mkate. Mtume akasema: “Ewe Fatima, kipande hiki cha nini? “Akajibu: “Ni kipande cha mkate kwani roho yangu haijaridhika mpaka nikuletee kipande hiki.” Mtume akasema: “Hakika hiki ni chakula cha kwanza kilichoingia ndani ya kinywa cha baba yako tangu siku tatu zilizopita.”[103]

Hii ni sura fupi na halisi ya utawa wa Mtume(s.a.w.w ) na jinsi alivyoipa mgongo dunia mpaka akafariki.

MUHTASARI

Mtume wa Mwenyezi Mungu Muhammad bin Abdullah hakujifunza mikononi mwa mwanadamu yeyote, lakini alikuja na Kitabu cha kie- limu na kimaarifa cha kimataifa ambacho kimewataka wanadamu wote katika zama zote walete mfano wake.

Kupitia Kitabu hicho Mtume(s.a.w.w) aliweza kumtoa mwanadamu toka jamii ya kijinga mpaka jamii ya kielimu iliyokamilika yenye kustaarabika, huku akihimiza usiku na mchana juu ya utafutaji wa elimu na maarifa mbalimbali.

Hivyo kupitia Kitabu hicho aliasisi dola kubwa na kujenga ustaarabu wa pekee ambao mfano wake hau- jashuhudiwa na mwanadamu.

Mtume(s.a.w.w ) alibeba maana kamili ya ibada kwa Mwenyezi Mungu Muumba, hivyo alikuwa na mahusiano ya karibu sana na Mola Wake Mtukufu, mahusiano ambayo yalitokana na ujuzi, mapenzi, utashi, na moyo mkunjufu, hivyo akawa ni kiigizo chema katika swala yake, funga, dua na uombaji msamaha, kiigizo ambacho kinamchorea mwanadamu njia ya ukamilifu kuelekea kwa Muumba, Mjuzi.

Mtume(s.a.w.w ) alianza harakati akiwa amebeba jukumu kubwa huku akimtegemea Mwenyezi Mungu katika kila harakati na kila jambo, hivyo akawa ni shujaa, jasiri na mkakamavu katika kulingania njia ya Mwenyezi Mungu.

Mtume(s.a.w.w ) aliishi mbali na ladha za dunia na starehe zake, hivyo alikuwa ni sehemu ya mafakiri na masikini, akishirikiana nao katika taabu zao huku akitarajia rehema za Mola Wake, mnyenyekevu Kwake, mwenye kujitenga na kila ujeuri utokanao na starehe za dunia na furaha za mapambo yake.

SOMO LA SABA: TABIA NA MWONEKANO WA HITIMISHO LA MANABII (S.A.W.W)

UKARIMU

Ibnu Abbas amesema: “Mtume(s.a.w.w ) alikuwa mkarimu sana kati- ka mambo ya kheri, ukarimu wake ulikuwa ukiongezeka zaidi ndani ya mwezi wa Ramadhani……Alikuwa akikutana na Jibril ndani ya kila mwezi wa Ramadhani kila mwaka, hivyo akikutana na Jibril huwa mkarimu sana kuliko upepo uvumao.”[104]

Jaabir amesema: “Mtume(s.a.w.w ) hakuombwa chochote akajibu hapana.”[105]

Imepokewa kuwa Mtume(s.a.w.w ) alikwenda kwa muuza nguo aka- nunua kanzu kwa dirhamu nne akatoka huku kaivaa. Ghafla akatokea mtu kati ya answari na kusema: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, nivishe kanzu, hakika Mwenyezi Mungu atakuvisha nguo kati ya nguo za Peponi.”

Hapo Mtume(s.a.w.w ) akavua kanzu na kumvisha. Kisha Mtume(s.a.w.w ) akarudi dukani na kununua tena kanzu kwa dirhamu nne huku akibakiwa na dirhamu mbili. Ghafla akatokea kijakazi njiani huku akilia. Mtume akamuuliza: “Kitu gani kinakuliza?” Akjajibu: “Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu mabwana zangu wamenipa dirhamu mbili nikanunulie unga lakini zimepotea.” Basi hapo Mtume(s.a.w.w ) akatoa dirhamu mbili na kumpa.

Kijakazi yule akasema: “Nahofia watanipiga.”

Mtume(s.a.w.w ) akaenda naye kwa mabwana zake, kisha Mtume(s.a.w.w ) akawatolea salamu. Wakaijua sauti yake, kisha akatoa mara ya pili, kisha mara ya tatu. Ndipo walipomjibu salamu yake. Mtume akasema: “Je mlisikia salamu yangu ya mwanzo?” Wakajibu: “Ndio, lakini tulipenda utusalimie zaidi, je ni jambo gani lililokusumbua?”

Mtume(s.a.w.w ) akajibu: “Nilimuonea huruma kijakazi huyu msije mkampiga.” Hapo bwana wake akasema: “Yeye yuko huru katika njia ya Mwenyezi Mungu, hivyo utaondoka naye.”

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu akawabashiria heri na pepo kwa kusema: “Hakika Mwenyezi Mungu ametia baraka katika dirhamu kumi, kamvisha kanzu Mtume wake na mtu kati ya answari, na akam- pa uhuru mtumwa, ninamhimidi Mwenyezi Mungu, hakika Yeye ndiye aliyeturuzuku haya kwa uwezo Wake.”[106]

Alikuwa akiwaachia watumwa wote huru uingiapo mwezi wa Ramadhani huku akimpa kila mwombaji.[107]

UPOLE NA USAMEHEVU

Zaid bin Aslam amesema: “Tulipata habari kuwa Abdullah bin Salama alikuwa akisema: “Hakika sifa za Mtume wa Mwenyezi Mungu ndani ya Taurati ni: Ewe nabii hakika tumekutuma uwe shahidi, mbashiri, mwonyaji na kinga kwa wasiojua kusoma na kuandika. Wewe ni mja Wangu na Mtume Wangu, nimekuita jina la Al- Mutawakkil (Mwenye kunitegemea).

Si mkali wala si mshupavu wa moyo. Si mpiga kelele masokoni wala halipi ubaya kwa ubaya lakini husamehe. Sitomfisha mpaka ninyooshe dini iliyopinda na watu waseme: Hapana Mola wa haki isipokuwa Allah, hivyo kupitia yeye Mwenyezi Mungu afungue macho yasiyoona, masikio yasiyosikia na nyoyo zilizoziba.” Maneno hayo yalipomfikia Kaaby akasema: “Amesema kweli Abdullah bin Salama.”

Imepokewa toka kwa Aisha kuwa: “Hakika Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w ) hakulipiza kisasi dhidi ya jambo lolote alilotendewa binafsi isipokuwa linapovunja utukufu wa Mwenyezi Mungu. Hivyo hakukipiga kitu chochote kwa mkono wake isipokuwa akipige katika njia ya Mwenyezi Mungu. Hakuna chochote alichoombwa akanyima isipokuwa aombwe jambo la dhambi. Hakika alikuwa mbali na jambo lolote la dhambi.”[108]

Ubaydu bin Umayr amesema: “Hakuna jambo lolote alilofanyiwa Mtume(s.a.w.w ) lisilolazimu adhabu kisheria isipokuwa alisamehe.”[109]

Anas amesema: “Nilimhudumia Mtume wa Mwenyezi Mungu muda wa miaka kumi, ndani ya muda wote huo hakuwahi kunifyonza na nilipofanya jambo lolote hakuniambia: Kwa nini umefanya hivi? Na nilipoacha jambo lolote hakuwahi kuniuliza: Kwa nini umeacha?”[110]

Alikuja bedui na kuvuta nguo ya Mtume(s.a.w.w ) kwa nguvu mpaka upinde wa nguo ukamuumiza Mtume shingoni, kisha bedui yule akasema: “Ewe Muhammad amrisha nipewe sehemu ya mali ya Mwenyezi Mungu iliyopo kwako.”

Mtume(s.a.w.w ) akamgeukia huku akitabasamu, kisha akaamrisha apewe.

Hakika Mtume alifahamika kwa usamehevu na upole muda wote wa maisha yake…….Hivyo alimsamehe Wahshiyu muuaji wa ami yake Hamza……Alimsamehe mwanamke wa kiyahudi aliyempa nyama ya mbuzi yenye sumu. Pia alimsamehe Abu Suf’yani huku akifanya kitendo cha kuingia nyumbani mwa Abu Suf’yani ni usalama dhidi ya kuuawa. Aliwasamehe maquraishi ambao walimpiga vita kwa kila aina ya nyenzo waliyokuwa nayo……huku akiwa katika kilele cha uwezo na nguvu lakini anawaombea heri kwa kusema: “Ewe Mola Wangu! waongoze jamaa zangu, hakika wao hawajui…….Nendeni hakika nyinyi ni watu mlioachiwa huru.”

Qur’ani imeweka bayana usamehevu wa Mtukufu Mtume(s.a.w.w ) ikaelezea hilo kwa kusema:

Basi kwa sababu ya rehema ya Mwenyezi Mungu umekuwa mpole kwao na kama ungekuwa mkali mshupavu wa moyo wangekukimbia. Basi wasamehe na uwaombee msamaha na ushauriane nao katika mambo .”[111]

Na ikasema tena: “Bila shaka amekufikieni Mtume kutoka miongoni mwenu, yanamuhuzunisha yanayokutaabisheni, anakuhangaikieni, kwa waumini ni mpole, mwenye kurehemu .”[112]

Kwa usamehevu huu mkubwa Mtume(s.a.w.w) aliweza kukonga nyoyo ngumu kakamavu na kuzifanya zimzunguke na kuamini utume wake wa kudumu.

Haya: Imepokewa kutoka kwa Abu Saad Al-Khidriy kuwa: “Mtume(s.a.w.w) alikuwa na haya sana kuliko mtawa katika utawa wake, hivyo iwapo akichukizwa na jambo hufahamika kupitia uso wake.”[113]

Imepokewa kutoka kwa Ali(a.s) kuwa: “Iwapo Mtume(s.a.w.w) kaombwa kutenda jambo na akataka kulitenda basi husema: Ndio. Na iwapo hataki kulitenda hunyamaza kimya, wala hakuwa anasema hapana akataapo kutenda jambo.”[114]

UNYENYEKEVU

Imepokewa kutoka kwa Yahya bin Abi Kathiri kuwa Mtume(s.a.w.w) alisema: “Ninakula kama alavyo mtumwa, nakaa kama akaavyo mtumwa, hakika mimi ni mtumwa.”[115]

Siku moja Mtume(s.a.w.w) alimsemesha mtu, basi mtu huyo akatetemeka, hapo Mtume(s.a.w.w) akasema: “Tulia, hakika mimi si malaika isipokuwa mimi ni mtoto wa mwanamke wa kikurayshi ambaye alikuwa akila nyama kavu tu.”[116]

Imepokewa kutoka kwa Abu Amamah kuwa: “Mtume alitujia huku anatembelea fimbo basi tukasimama, hapo Mtume(s.a.w.w) akasema: Msisimame kama wanavyosimama waajemi kwani baadhi yao huwatukuza wengine.”14Alikuwa akiwatania maswahaba zake isipokuwa hatamki ila la kweli.[117]

Pia alikuwa akiwatolea watoto salamu.[118] Alishirikiana na swahaba zake katika kujenga msikiti.[119]

Akachimba handaki,[120] na mara nyingi alikuwa akiomba ushauri toka kwa maswahaba zake, japokuwa yeye ndiye aliyekuwa na akili bora kuliko watu wote.[121]

Mara nyingi alikuwa akisema: “Ewe Mola Wangu nipe uhai katika hali ya umaskini na unifishe nikiwa masikini. Hakika muovu wa kutupa ni yule anayekusanyikiwa na ufakiri wa dunia na adhabu ya Akhera.”[122]

Hii ni sura fupi sana kuhusu sifa za shakhsia ya Mtume(s.a.w.w) , na hizi ni baadhi tu ya tabia zake binafsi na za kijamii.

Pia kuna sura nyingi nzuri kuhusu mwenendo wake na sera yake kiutawala, kisiasa, kijeshi, kiuchumi na kifamilia, mwenendo ambao unahitaji masomo ya ndani zaidi ili kufuata na kuuiga, hivyo masomo hayo tunayaacha kwa ajili ya muhula ujao.

Hivyo ndivyo zilivyotubainikia sifa za pekee za Mtume Muhammad(s.a.w.w) ambazo tunaweza kuzifupisha katika maneno yafuatayo:

Usafi wa familia, ulinzi wa Mwenyezi Mungu daima, tabia za hali ya juu, nafasi ya juu ya kijamii, maadili mema, ufasaha wa lugha, maisha mepesi, kujiepusha na kila aina ya shirki na kila aina ya mila potovu, kufikia kilele katika ibada ya Mwenyezi Mungu na unyenyekevu kwa ajili ya haki katika hali yoyote ile.

MUHTASARI

Hakika Mtume(s.a.w.w) alikuwa mkarimu sana, hivyo alikuwa akieneza upendo, ukarimu, wema na mali kwa watu wote, huku akitoa msamaha, huruma na ulaini kwao. Ili awaokoe toka kwenye ujinga wao na apate kuwaunganisha pamoja wawe kitu kimoja.

Mtume(s.a.w.w) alikuwa anaishi na waislam kama mmoja wao huku haya zikimtukuza kwa kumpa haiba na heshima, huku unyenyekevu ukimzidishia heshima na utukufu. Hivyo alikuwa akiwahurumia wadogo na kuwaheshimu wakubwa. Alikuwa akisikia ushauri wa mnasihi ilihali yeye ni mwenye akili zitokazo mbinguni kwa njia ya ufunuo.


3

4

5

6