NAHJULBALAGHAH Juzuu 1

NAHJULBALAGHAH0%

NAHJULBALAGHAH Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: VITABU VYA HADITHI

NAHJULBALAGHAH

Mwandishi: SAYYIDI SHARIFU RADHIY
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 5455
Pakua: 1988


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 7 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 5455 / Pakua: 1988
Kiwango Kiwango Kiwango
NAHJULBALAGHAH

NAHJULBALAGHAH Juzuu 1

Mwandishi:
Swahili

NAHJUL-BALAGHAH

MAJMUA YA KHUTBA, AMRI, BARUA, RISALA, MAWAIDHA NA SEMI ZA

AMIRUL-MUUMININ ALI BIN ABU TALIB(a.s)

Mkusanyaji: Al-Sharif Al-Radhii

Kimetarjumiwa na: Sheikh Haroon Pingili

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu kilichoko mkononi mwako ni tarjumi kutoka lugha ya Kiarabu ya kitabu maarufu katika ulimwengu wa Kiislamu, Nahju 'l-Balaghah. Kitabu hiki kitachapishwa katika majalada mbali mbali, na hili ulilo nalo mkononi ni jalada la kwanza.

Nahju 'l-Balaghah ni mkusanyiko wa khutba, barua na maelekezo ya Imam Ali(a.s) . Mengi yamesemwa kuhusu ubora na ufasaha wa maneno yaliyomo katika khutba na harua hizo. Kwa ufupi, Nahju 'l-Balaghah ni kilele cha ufasaha.

Mbali na mawaidha yaliyomo humo, msomaji atafaidika na lugha iliyomo katika khutba na barua hizo, hususan kwa wasomaji wa Kiarabu.

Inasemekana kwamba baada ya Qur'ani Tukufu na maneno ya Mtukufu Mtume(s.a.w.w) , Nahju 'l-Balaghah ndiyo inayofuatia kwa ufasaha na ubora wa maneno.

Si rahisi kwa msomaji wa Kiswahili kupata ladha ileile aipatayo msomaji wa Kiarabu kutokana na ukweli kwamba lugha ya Kiarabu ni pana mno na msamiati wake ni mkubwa. Pamoja na hayo, mtarjumi wetu amejitahidi sana kuleta maana ya maneno ya Kiarabu kwenye lugha ya Kiswahili bila kupoteza maana yake.

Kwa vile kitabu hiki ni muhimu sana, tumeona ni bora tukichapishe katika lugha ya Kiswahili ili Waislamu na wasomaji wetu wazungumzao Kiswahili wapate kunufaika na yaliyomo humo. Hivyo, ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakkuwa ni chenye manufaa sana kwao na katika jamii yetu.

Tunamshukuru ndugu yetu, Sheikh Harun Pingili kwa kukubali jukumu hili kukitarjumi kitabu hiki. Vilevile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.

Mchapishaji

Al-Itrah Foundation

S. L. P. 19701

Dar-es-Salaam, Tanzania

DIBAJI

Kwa jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu. Kwanza yanipasa nimshukuru Mwenyezi Mungu Jalali, asiye kuwa na mithali, kwa neema zake za kila hali na kila mahali, hata nikaweza mimi mja mpungufu, kutimiza kazi hii tukufu ya kuipitia tarjuma hii ya Kiswahili ya Nahju 'l-Balaghah.

Nahju 'l-Balaghah ni jina la diwani mashuhuri yenye khutba, uweza wa kusema, na barua za Imam Alî bin Abu Talib(a.s) . Haya yote yamekusanywa na Sharîf Ar-Radhi. Diwani hii yenye khutba takriban 237, baru 79 na mithali 480 ilikamilika mwezi wa Rajab 400 A.H./1009 A.D. Maana ya NAHJ ni njia iliyo wazi, au barabara kuu; na maana ya Balaghah ni ufasaha (wa lugha) au ilimu ya usemaji, n.k. Kwa hivyo Nahju 'l-Balaghah yaani Barabara kuu ya ufasaha.

"Huyu Imam 'Ali ni nani? Ni vigumu mno kuzitaja sifa zake kwa ukamilifu. Yeye alikuwa mtaalamu, shujaa na khatibu kuliko wote. Uchamungu wake, mapenzi yake ya Mwenyezi Mungu, uaminifu wake na ushupavu wake wa kufuata dini ulikuwa wa darja ya juu kuliko mtu yeyote akichukia diplomasia (ujanja), na akipenda haki na insafu. Sera zake ni kama zilivyoamrishwa na Mwenyezi Mungu. Wataalamu wa Kiyahudi na wa Kikristo wakijaaliwa kujua daraja ya ilimu yake huisujudia ilimu hiyo isioweza kufananishwa.

Wafalme wa Ki-Rumi wangependa kuzitundika picha zake katika kasri zao, na maaskari wakubwa wa vita wangependelea kulichonga jina lake kwenye panga zao.

لآ فثي إ لاَّ عَلِيَّ وَ لآ سَيْفَ اِلاَّ ذُو الْفقار

"Hayuko kijana shujaa mfano wa 'Ali! wala hakuna upanga mfano wa Dh-ul-Faqar (upanga wa Imam 'Alî (a.s) aliorithi kwa Mtume) ."

Allama Mustafa Beck Najeeb wa al-Azhar, Cairo amesema:

خَرَجَ اِلَي الدُّ نْيَا وَ الثَّهَادَةُ مَكْتُوْبَهَّ عَلي جَبَيْنِهِ وَ خَرجَ مِنْهَا وَ الثَّهَادَةُ مَكْتُوْبَهَّ عَلي دَ لِكَ الجَبَيْنِ بضَرْبَهِ حُسَّا مٍ لَقدْ كَمَا عَلِمْنَا فِي الْكَعْبَهِ وَ ضُربَ كَمَ عَلِمْنَا فِي الْمَسْجِدِ قأَيَّه بَدَايَهٍ وَ نِهَايَهٍ اَثْْبَهَ بالْحَيَاةِ الّتي بَيْنَهُمَا مِنْ تِلْكَ الْبدَايَهٍ وَ تِلْكَ النَّهَايَهِ؟

"Imam 'Alî amekuja duniani na shahada imeandikwa kwenye kipaji chake; na ameondoka duniani na shahada vile vile imeandikwa kwenye hicho kipaji kwa dharba ya upanga. Kama tunavyojua amezaliwa ndani ya Ka'bah, na kama tujuavyo amepigwa dharba (ya upanga) msikitini. Ilioje ajabu? Mwanzo wake na mwisho wake kupata darja ya kifo cha kishahidi ."

Sheikh Abbas Mahmud al-Aqqad - mwandishi maarufu wa Ki-masri amesema:

"Mtu yeyote ambaye amebobea katika lugha ya Ki-arabu atakubali tu kwamba Nahju 'l-Balaghah inafuata kwa ubora wake baada ya maneno ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Maneno ya 'Alî ni yenye maana na fikra nzito. Kwa hivyo Nahju 'l-Balaghah lazima isomwe kwa makini, na irejewe na idondolewe na wanafunzi na walimu. Ninapenda kutilia mkazo kwamba Nahju 'l-Balaghah iingizwe kwenye mukhtasar wa masomo na mafundisho (syllabi) ya vyuo vikuu vyote vya Masri na Beirut kwenye masomo ya kiwango cha juu ya lugha na falsafa."

Sheikh Muhammad 'Abdo - Mufti wa Masri na Profesa wa lugha ya Kiarabu na falsafa amesema:

تَحْتَ كَلاَمِ الْخَالِق وَ فَوْقَ كَلاَ مِ الْمَخْلُوق.

"Mtu yeyote hawezi kukataa kwamba 'Alî alikuwa Imamu wa makhatibu, mwalimu na kiongozi wa waandishi na wanafalsafa. Bila ya shaka khutba zake na maneno yake ni yenye kiwango cha juu kabisa kushinda maneno ya mtu ye yote isipokuwa maneno ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake:"

'Abd-ul-Masîh al-Antaqi - Mhariri wa Kikristo wa gazeti la Ki-masri Al- Ahram amesema:

'Alî alikuwa Imamu kwenye nyanja za vita, Imamu wa siasa, Imamu wa dini, Imamu wa falsafa, Imamu wa maadili, Imamu wa maandiko mbali mbali, na Imamu wa ilmu na hikma."

Profesa Muhammad Kamil, Cairo amesema:

فاِ دَا لَمْ يَكُنْ عَلِيّ نَبِيًّا فلَقدْ كَانَ خُلُقُهَ نَبَوتًّا.

"Ijapokuwa Imam 'Alî alikuwa si nabii, lakini khulqa yake ilikuwa ya kinabii ."

Shaykh Nasif al-Yazidi alipokuwa akimwaidhi mwanawe alimwambia: “Kama unataka mamlaka ya juu kabisa dhidi ya wenzako katika masomo, hikma, maandiko, inshaa n.k. basi hifadhi Qur'ani Tukufu na Nahju 'l- Balaghah”.

Amîn Nakhlah anasema: “Mtu yeyote anayetamani kuikata kiu yake (ya kiroho) kwa maneno ya 'Ali(a.s) lazima ausome kila ukurasa wa Nahju 'l- Balaghah kwa uangalifu.

Nahju 'l-Balaghah ni diwani ambayo humfanya kila mtu kuukubali ubingwa wa Imam 'Ali(a.s) . Hakuna kitabu kinachoweza kuishinda Nahju 'l- Balaghah isipokuwa Qur'ani Tukufu. Humo ndani ya Nahju 'l-Balaghah utazikuta lulu za maarifa zilizotungwa kwenye mikufu mizuri, utayakuta maua ya lugha ambayo huifanya akili ya binadamu inukie kwa harufu nzuri ya ushujaa na uungwana; vile vile humo utaikuta mito ya lugha safi ambayo ni mitamu na baridi zaidi kuliko mto wa al-Kauthar.

Imam 'Alî(a.s) anawaidhi juu ya maudhui mbali mbali, k.m. Kuumbwa kwa ardhi na mbingu, tawhîd, taqwa, malaika, zuhd, Qiyamah, kiburi, tamaa, vita vya Jamal, Siffin, Nahrawan, ibada, maarifa, tamaa, imani, insafu, n. k.

Katika mithali yake mashuhuri Imam 'Alî(a.s) anatuwaidhi sisi wanaadamu kutobaguwana kwa makabila.

"Watu kwa makamu ni sawa sawa

Baba ni Adamu na mama Hawa

Ukijia'dhimu kwa kuzaliwa

Maji na kinamu uliumbiwa

Fahamu na jua mwana Adamu"

Maneno haya ya Sayyidna 'Alî yamo katika msingi wa Qur'ani Tukufu. (Sh. 'Alî Muhsin al-Barwani).

Tunatumai wasomaji wetu watastafidi sana na tarjama hii ya Nahju 'l-Balaghah (kwa lugha ya Kiswahili) ambayo imefanywa kwa kifundi na ujuzi mkubwa. Mwenyezi Mungu atujaalie tawfiq ya Kutenda Kheri na atuepushe na kila shari.

Wa Billahi Tawfîq,

KUKHUSU NASABA YA AMIRUL-MU’MININA ALI(A.S) NA KUTAJA SEHEMU KIDOGO YA FADHAILI ZAKE

Yeye ni Abul’Hasan Ali bin Abi Taalibina jina lake Abdu Manaf bin Abdulmuttalib - na jina lake ni: Shaybatul’hamd bin Hashim-na jina lake ni Amr bin Abdu Manaf bin Qusayyi. Kuniya ambayo aghlabu hutumika kumuita ilikuwa: Abul’hasan.

Na mwanawe Hasan(a.s) katika zama za uhai wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alikuwa akimwita Abulhusayn, na Husayn(a.s) alikuwa akimwita Abulhasan, na wawili hao walikuwa wakimwita Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) baba yao, na alipokufa Nabii(s.a.w.w) ndipo walimwita baba yao baba.

Na Mtume wa Mwenyezi Mungu alimpa kunia ya: Abu Turab, hivyo ni kwa sababu siku moja alimkuta amelala usingizi kwenye mchanga, hali ikiwa ridaa-nguo-yake imemdondoka, na mchanga ukawa umemtapakaa mwilini mwake. Akamjia na akaketi karibu ya kichwa chake, na alimwamsha na akawa yuampangusa mchanga toka mgongoni huku akimwambia: “Kaa; kwa hakika wewe ni Abu Turab” na tokea hapo ikawa miongoni mwa kunia aipendayo mno katika kunia zake(a.s) . Alikuwa ana- furahi kuitwa kunia hii (Abuturab).

Na Bani Umayyah walikuwa wakiwaraghibisha makhatibu wao wamtukane kwa kunia hii wakiwa juu ya mimbari, na waliifanya kuwa ni upungufu fulani na ni dosari kwake; Basi ikawa kwake kama wamemvika pambo, kulingana na alivyosema Hasan Albasri (r.a). Jina lake la kwanza ambalo mama yake alimwita ni: Haidara, ikiwa ni jina la baba yake Asad bin Hashim - na Alhaidara ni: Simba, baba yake (yaani Abutalib) alimbadilisha jina hilo na akamwita Ali. Na kuna kauli isemayo kuwa: Haidara ni jina ambalo Makurayshi walikuwa wana mwita. Kauli ya kwanza ndio sahihi; kwa kuwa kuna habari yajulisha hivyo kutokana na yeye mwenyewe, siku alipomkabili Marhab ambaye alikuwa anajigamba kutafakhari akisema: “Ana lladhi sammatni ummi Marhaba” ndipo hapo Imam Ali(a.s) alimjibu na kumkabili: “Ana lladhi sammatni Haidara”.

Jina la mama yake ni Faatima binti Asad bin Hashim bin Abdi Manaf bin Qusayyi, ni (mwana mama wa kwanza Hashimiya amezaa kwa Bwana wa kihashimii; Ali(a.s) alikuwa mdogo katika watoto wake (huyu mama), na Ja’far alikuwa mkubwa kuliko yeye kwa miaka kumi, na Aqiil alikuwa mkubwa kuliko yeye kwa miaka kumi, na Talib ni mkubwa kuliko Aqiil kwa miaka kumi, na Fatima binti Asad mama wa hao wote.

NAHJUL-BALAGHAH

JUZUU YA KWANZA

1. NA KATIKA KHUTBA ZAKE(a.s)

Ndani ya khutba hii anaelezea kuumbwa kwa ardhi, mbingu, na kuumbwa kwa Adam(a.s)

الحَمْدُ للهِ الَّذَي لاَ يَبْلُغُ مِدْحَتَهُ القَائِلُونَ، وَلاِ يُحْصِي نَعْمَاءَهُ العَادُّونَ، ولاَ يُؤَدِّي حَقَّهُ الُمجْتَهِدُونَ، الَّذِي لاَ يُدْركُهُ بُعْدُ الهِمَمِ، وَلاَ يَنَالُهُ غَوْصُ الفِطَنِ، الَّذِي لَيْسَ لِصِفَتِهِ حَدٌّ مَحْدُودٌ، وَلاَ نَعْتٌ مَوْجُودٌ، وَلا وَقْتٌ مَعْدُودٌ، وَلا أَجَلٌ مَمْدُودٌ فَطَرَ الخَلائِقَ بِقُدْرَتِهَ، وَنَشَرَ الرِّيَاحَ بِرَحْمَتِهِ، وَوَتَّدَ بِالصُّخُورِ مَيَدَانَ أَرْضِهِ.

Sifa zote njema zinamstahikia Mwenyezi Mungu ambaye ubora wa sifa zake hawa ufikii wasemaji. Ambaye neema zake wahasibu hawawezi kuzihisabu. Wenye juhudi hawawezi kutekeleza haki ya utii wake.Ambaye fahamu ya hali ya juu ya wenye akili haiwezi kumfikia kumtambua[1] , wala, utambuzi wa kina hauwezi kumuelewa[2] ambaye sifa zake hazina mpaka wenye kikomo[3] , wala hana sifa. Wala wakati uhisabiwao, wala muda uliowekwa[4] . Ameumba viumbe kwa uwezo wake, na ameutawanya upepo kwa rehema zake; kwa milima ameimarisha ardhi yake ili isiyumbe.

أَوَّلُ الدِّينِ مَعْرِفَتُهُ، وَكَمَالُ مَعْرِفَتِهِ التَّصْديقُ بِهِ، وَكَمَالُ التَّصْدِيقِ بِهِ تَوْحِيدُهُ، وَكَمَالُ تَوْحِيدِهِ الاخْلاصُ لَهُ، وَكَمَالُ الاخْلاصِ لَهُ نَفْيُ الصِّفَاتِ عَنْهُ، لِشَهَادَةِ كُلِّ صِفَة أَنَّها غَيْرُ المَوْصُوفِ، وَشَهَادَةِ كُلِّ مَوْصُوف أَنَّهُ غَيْرُ الصِّفَةِ، فَمَنْ وَصَفَ اللهَ سُبْحَانَهُ فَقَدْ قَرَنَهُ، وَمَنْ قَرَنَهُ فَقَدْ ثَنَّاهُ،وَمَنْ ثَنَّاهُ فَقَد جَزَّأَهُ، وَمَنْ جَزَّأَهُ فَقَدْ جَهِلَهُ، [وَمَنْ جَهِلَهُ فَقَدْ أشَارَ إِلَيْهِ]، وَمَنْ أشَارَ إِلَيْهِ فَقَدْ حَدَّهُ، وَمَنْ حَدَّهُ فَقَدْ عَدَّهُ.

La kwanza katika dini ni kumtambua yeye[5] , na ukamilifu wa kumtambua ni kumsadiki, na ukamilifu wa kumsadiki ni kumpwekesha[6] . Na ukamilifu wa kumpwekesha ni kumtakasa na ukamilifu wa kumtakasa ni kumuepusha mbali na sifa. Na mwenye kumsifu Mwenyezi Mungu swt. Atakuwa amemuambatanisha[7] , na mwenye kumuambatanisha amemfanya kuwa wawili[8] , na mwenye kumfanya kuwa wawili atakuwa amemfanya kuwa mwenye sehemu sehemu, na mwenye kumfanya kuwa mwenye sehemu sehemu atakuwa hamjui (s.w.t), na asiyemjua atakuwa amemuonyesha, na mwenye kumuonyesha atakuwa amemwekea mipaka [9] , na mwenye kumuwekea mipaka atakuwa amemuhesabu [10] .

وَمَنْ أشَارَ إِلَيْهِ فَقَدْ حَدَّهُ، وَمَنْ حَدَّهُ فَقَدْ عَدَّهُ، وَمَنْ قَالَ: «فِيمَ» فَقَدْ ضَمَّنَهُ، وَمَنْ قَالَ: «عَلاَمَ؟» فَقَدْ أَخْلَى مِنُهُ كائِنٌ لاَ عَنْ حَدَث، مَوْجُودٌ لاَ عَنْ عَدَم، مَعَ كُلِّ شَيْء لاَ بِمُقَارَنَة، وَغَيْرُ كُلِّ شيء لا بِمُزَايَلَة، فَاعِلٌ لا بِمَعْنَى الْحَرَكَاتِ وَالاْلةِ، بَصِيرٌ إذْ لاَ مَنْظُورَ إلَيْهِ مِنْ خَلْقِهِ، مُتَوَحِّدٌ إذْ لاَ سَكَنَ يَسْتَأْنِسُ بهِ وَلاَ يَسْتوْحِشُ لِفَقْدِهِ

Na mwenye kusema yuko ndani ya nini? Anakuwa amemwingiza (s.w.t) ndani ya kitu[11] . Na mwenye kusema yuko juu ya nini? Atakuwa amemtoa humo[12] . Amekuwa yupo sio kwa kutukia, yupo lakini sio kwa maana ya hakuwapo hapo kabla. Yuko pamoja na kila kitu si kwa mwambatano wa kimwili[13] . Yutafauti na kila kitu si utafauti wa kimwili, mtendaji sio kwa maana ya harakati za kimwili na vyombo, mwenye kuona pindi hakuna wakuonwa kati ya viumbe wake. Yu pweke pindi hakuna mkazi analiwazika naye wala haoni ukiwa kwa kukosekana kwake.

KUUMBWA KWA ULIMWENGU:

أَنْشَأَ الخَلْقَ إنْشَاءً، وَابْتَدَأَهُ ابْتِدَاءً، بِلاَ رَوِيَّة أَجَالَهَا، وَلاَ تَجْرِبَة اسْتَفَادَهَا، وَلاَ حَرَكَة أَحْدَثَهَا، وَلاَ هَمَامَةِ نَفْس اظْطَرَبَ فِيهَا أَحَالَ الاْشياءَ لأوْقَاتِهَا، وَلاَمَ بَيْنَ مُخْتَلِفَاتِهَا، وَغَرَّزَ غَرائِزَهَا، وَأَلزَمَهَا أشْبَاحَهَا، عَالِماً بِهَا قَبْلَ ابْتِدَائِهَا، مُحِيطاً بِحُدُودِها وَانْتِهَائِهَا، عَارفاً بِقَرَائِنِها وَأَحْنَائِهَا

Alianza kuumba viumbe mwanzo, na kuvibuni kwa ubunifu, bila ya kupitisha fikra, wala kufaidika na uzoefu wowote, wala hakufanya harakati yeyote, wala kusumbuliwa na azma ya ndani ya nafsi, amevitoa viumbe (kutoka hakuna kitu na kuviingiza) kwenye ulimwengu wa kuwepo kwa wakati wake.

Akaviunganisha viumbe pamoja na tofauti zao. Akaweka silika zao, na akaziambatanisha hizo silika na wenyewe. Akiwa mjuzi (s.w.t) kabla hajabuni (viumbe) akiwa mwenye kuelewa kwa ukamilifu, mipaka yao na mwisho wao, akiwa mwenye kutambua utashi wao na sehemu zao nyingi.

ثُمَّ أَنْشَأَ ـ سُبْحَانَهُ ـ فَتْقَ الاْجْوَاءِ، وَشَقَّ الاْرْجَاءِ، وَسَكَائِكَ الَهوَاءِ، فأَجازَ فِيهَا مَاءً مُتَلاطِماً تَيَّارُهُ، مُتَراكِماً زَخَّارُهُ، حَمَلَهُ عَلَى مَتْنِ الرِّيحِ الْعَاصِفَةِ، وَالزَّعْزَعِ الْقَاصِفَةِ، فَأَمَرَها بِرَدِّهِ، وَسَلَّطَهَا عَلَى شَدِّهِ، وَقَرنَهَا إِلَى حَدِّهِ، الهَوَاءُ مِنْ تَحْتِها فَتِيقٌ، وَالمَاءُ مِنْ فَوْقِهَا دَفِيقٌ

Kisha aliumba (s.w.t) mwanya wa anga na eneo la mbingu na utando wa upepo, alimimina humo maji ambayo mawimbi yake yalikuwa makali na mawimbi yalilundikana moja juu ya jingine, aliyabebesha kwenye upepo uendao kwa kasi, na mtikisiko mkali, na kimbunga kinachovunja. Aliyaamrisha yamwage (mvua) aliufanya upepo uwe na uwezo wa kuzuia nguvu za mvua na kuijulisha mipaka yake. Upepo ulivuma chini hali maji yalibubujika kwa kasi kwa upande wa juu.

ثُمَّ أَنْشَأَ سُبْحَانَهُ رِيحاً اعْتَقَمَ مَهَبَّهَا، وَأَدَامَ مُرَبَّهَا، وَأَعْصَفَ مَجْرَاها، وَأَبْعَدَ مَنْشَاهَا، فَأَمَرَها بِتَصْفِيقِ المَاءِ الزَّخَّارِ، وَإِثَارَةِ مَوْجِ البِحَارِ، فَمَخَضَتْهُ مَخْضَ السِّقَاءِ، وَعَصَفَتْ بهِ عَصْفَهَا بِالفَضَاءِ.

Kisha (s.w.t) aliumba upepo ambao ulifanya mvumo wake uwe tasa. Yaani mvumo wa hewa ulifanywa usioweza kurutubisha kizazi, kwa kuwa kuna upepo urutubishao mimea na kuifanya itoe mazao. Na upepo huu uli- umbwa ili kuyatikisa maji tu. Na akadumisha kubaki kwake, mwendo wake ulishika kasi na akayatawanya kwa umbali na kwa upana.

تَرُدُّ أَوَّلَهُ عَلَى آخِرِهِ، وَسَاجِيَهُ عَلَى مَائِرِهِ، حَتَّى عَبَّ عُبَابُهُ، وَرَمَى بِالزَّبَدِ رُكَامُهُ، فَرَفَعَهُ فِي هَوَاء مُنْفَتِق، وَجَوٍّ مُنْفَهِق، فَسَوَّى مِنْهُ سَبْعَ سَموَات، جَعَلَ سُفْلاَهُنَّ مَوْجاً مَكْفُوفاً، وَعُلْيَاهُنَّ سَقْفاً مَحْفُوظاً، وَسَمْكاً مَرْفُوعاً، بِغَيْر عَمَد يَدْعَمُهَا، وَلا دِسَار يَنْظِمُها ثُمَّ زَيَّنَهَا بِزينَةِ الكَوَاكِبِ، وَضِياءِ الثَّوَاقِبِ، وَأَجْرَى فِيها سِرَاجاً مُسْتَطِيراً، وَقَمَراً مُنِيراً: في فَلَك دَائِر، وَسَقْف سَائِر، وَرَقِيم مَائِر.

Kisha aliuamrisha upepo kuyanyanyua maji yalio kwenye kina, na kuongeza kasi ya mawimbi ya bahari. Yakatikisa mtikiso kama ule ufanywao kwa kinywaji cha maziwa. Na kuvuma nayo angani. (Anakusudia kueleza kuwa upepo ukivuma angani anga ambazo ziko tupu huwa mvumo wake mkali kwa sababu ya kutozuilika na kitu chochote, na upepo huu ulivuma na maji mengi mvumo mkali sana). Wayarudisha ya mwanzo nyuma na yaliyotulia kuyapeleka kwa yaliyo kwenye mtikisiko, mpaka yakainuka mwinuko. Na sehemu ya chini ilijaa povu. Baadaye Mungu (s.w.t) aliinua povu lile juu ya upepo ulio wazi kutoka humo aliumba mbingu Saba. Na sehemu ya mawimbi ya chini aliyazuia na kuwa kituo, na ya juu kuwa kama dari inayo zuia na jumba lililoinuka bila ya nguzo zenye kulikinga, wala misumari inayo imarisha, kisha alizipamba (mbingu) kwa mapambo ya nyota na mianga yenye nuru. Na alipitisha humo jua lenye taa yenye kuenea mwanga wake. Na mwezi wenye nuru katika sayari zinazozunguka. Na dari inayokwenda, na ubao uendao[14] .

KUUMBA MALAIKA

ثُمَّ فَتَقَ مَا بَيْنَ السَّمواتِ العُلاَ، فَمَلاَهُنَّ أَطْواراً مِنْ مَلائِكَتِهِ : مِنْهُمْ سُجُودٌ لاَيَرْكَعُونَ، وَرُكُوعٌ لاَ يَنْتَصِبُونَ، وَصَافُّونَ لاَ يَتَزَايَلُونَ، وَمُسَبِّحُونَ لاَ يَسْأَمُونَ، لاَ يَغْشَاهُمْ نَوْمُ العُيُونِ، وَلاَ سَهْوُ العُقُولِ، وَلاَ فَتْرَةُ الاَبْدَانِ، ولاَ غَفْلَةُ النِّسْيَانِ.

Kisha aliumba mwanya kati ya mbingu za juu na kuzijaza malaika wake wenye daraja tofauti[15] .Mabingwa wa ibada, miongoni mwao kuna ambao wamesujudu na wala hawarukuu, na kuna waliorukuu na wala hawasimami, kuna waliosimama katika safu na wala hawatawanyiki kuna wanaosabihi na wala hawachoki, hawasinzii, wala hapitiwi, wala hawanyong’onyei, wala kughafilika kwa kusahau.

وَمِنْهُمْ أُمَنَاءُ عَلَى وَحْيِهِ، وأَلسِنَةٌ إِلَى رُسُلِهِ، وَمُخْتَلِفُونَ بِقَضَائِهِ وَأَمْرهِ وَمِنْهُمُ الحَفَظَةُ لِعِبَادِهِ، وَالسَّدَنَةُ لاِبْوَابِ جِنَانِهِ

b. Miongoni mwao kuna waaminifu wa wahyi wa Mungu, na ni ndimi zitamkazo ndani ya vinywa vya mitume Wake, na wanaopokezana kwa hukumu na amri zake (kupitia wao Mungu hupitisha hukumu kwa amtakae kwa apendacho).

وَمِنْهُمُ الثَّابِتَةُ في الاْرَضِينَ السُّفْلَى أَقْدَامُهُمْ، وَالمَارِقَةُ مِنَ السَّماءِ العُلْيَا أَعْنَاقُهُمْ، والخَارجَةُ مِنَ الاَقْطَارِ أَرْكَانُهُمْ، وَالمُنَاسِبَةُ لِقَوَائِمِ العَرْشِ أَكْتَافُهُمْ، نَاكِسَةٌ دُونَهُ أَبْصارُهُمْ، مُتَلَفِّعُونَ تَحْتَهُ بِأَجْنِحَتِهِمْ، مَضْرُوبَةٌ بَيْنَهُمْ وَبَيْنَ مِنْ دُونَهُمْ حُجُبُ العِزَّةِ، وَأسْتَارُ القُدْرَةِ، لاَ يَتَوَهَّمُونَ رَبَّهُمْ بالتَّصْوِيرِ، وَلاَ يُجْرُونَ عَلَيْهِ صِفَاتِ المَصْنُوعِينَ، وَلاَ يَحُدُّونَهُ بِالاْماكِنِ، وَلاَ يُشِيرُونَ إِلَيْهِ بِالنَّظَائِرِ

c. Malaika wahifadhi wa waja Wake (s.w.t), kana kwamba wao ni nguvu iliyowekwa ndani ya miili ya wanadamu na nafsini mwao. Na miongoni mwao wamo ambao miguu yao imeimarika katika ardhi ya chini, na shingo zao zimechomoza kwenye mbingu ya juu, na nguzo zao zimezidi kwenye peo (horizon), na mabega yamelingana na nguzo za Arshi, wenye kuinamisha macho yao mbali na Arshi, wenye kuizingira kwa mbawa zao, imepigwa pazia ya utukufu kati yao na wasiokuwa wao na stara ya uwezo, hawamfanyii taswira Mola wao, wala hawampitishii sifa za viumbe, wala hawamuwekei mipaka ya mahali, wala hawamuashirii kwa mifano.

KUUMBWA KWA ADAM(A.S)

ثُمَّ جَمَعَ سُبْحَانَهُ مِنْ حَزْنِ الاْرْضِ وَسَهْلِهَا، وَعَذْبِهَا وَسَبَخِهَا، تُرْبَةً سَنَّهَا بالمَاءِ حَتَّى خَلَصَتْ، وَلاَطَهَا بِالبَلَّةِ حَتَّى لَزَبَتْ، فَجَبَلَ مِنْها صُورَةً ذَاتَ أَحْنَاء وَوُصُول، وَأَعْضَاء وَفُصُول: أَجْمَدَهَا حَتَّى اسْتَمْسَكَتْ، وَأَصْلَدَهَا حَتَّى صَلْصَلَتْ، لِوَقْت مَعْدُود، وَأجَل مَعْلُوم.

Kisha (s.w.t) alikusanya aina za udongo: Ngumu, laini, tamu, chachu, udongo ambao aliumwagia maji mpaka ukalowana, na aliukanda kwa unyevunyevu mpaka ukaganda, kutoka humo aliumba sura yenye pande tofauti, na viungo tanzu, sehemu ya pingili aliigandisha na ikashikamana, akaifanya kuwa ngumu mpaka ikawa ngumu, kiasi cha kusikika sauti, kwa wakati uliowekwa kwa muda ujulikanao.

ثُمَّ نَفَخَ فِيها مِنْ رُوحِهِ فَمَثُلَتْ إِنْساناً ذَا أَذْهَان يُجيلُهَا، وَفِكَر يَتَصَرَّفُ بِهَا، وَجَوَارِحَ يَخْتَدِمُهَا، وَأَدَوَات يُقَلِّبُهَا، وَمَعْرِفَة يَفْرُقُ بِهَا بَيْنَ الحَقِّ وَالبَاطِلِ، والاَذْوَاقِ والَمشَامِّ، وَالاْلوَانِ وَالاْجْنَاس، مَعْجُوناً بطِينَةِ الاْلوَانِ الُمخْتَلِفَةِ، وَالاَشْبَاهِ المُؤْتَلِفَةِ، وَالاْضْدَادِ المُتَعَادِيَةِ، والاَخْلاطِ المُتَبَايِنَةِ، مِنَ الحَرِّ والبَرْدِ، وَالبَلَّةِ وَالْجُمُودِ، وَالْمَساءَةِ وَالسُّرُورِ.

Baadaye alipulizia humo roho, akawa mtu mwenye akili imsukumayo, na fikra aitumikishayo, na viungo vya mwili avitumiavyo, na ala zimsaidiazo kubadilisha hali yake, na maarifa ambayo kwayo anatofautisha kati ya haki na batili, akiwa na uwezo wa kuonja, na kunusa, kupambanua rangi, na jinsi yenye mchanganyiko wa udongo wa rangi tofauti, na vitu vyenye kufanana na kuafikiana, vitu vilivyo kinyume na visivyoafikiana. Aina tofauti za mchanganyiko: kama vile joto, baridi, hali ya chepe, ugumu, chuki, furaha.

وَاسْتَأْدَى اللهُ سُبْحَانَهُ المَلائكَةَ وَدِيعَتَهُ لَدَيْهِمْ، وَعَهْدَ وَصِيَّتِهِ إِلَيْهمْ، في الاْذْعَانِ بالسُّجُودِ لَهُ، وَالخُنُوعِ لِتَكْرِمَتِهِ، فَقَالَ عزَّمِن قائِل: (اسْجُدُوا لاِدَمَ فَسَجَدُوا إِلاَّ إِبْلِيسَ) وَقَبِيلَهُ، اعْتَرَتْهُمُ الحَمِيَّةُ، وَغَلَبَتْ عَلَيْهِمُ الشِّقْوَةُ، وَتَعَزَّزُوا بِخِلْقَةِ النَّارِ، وَاسْتَوْهَنُوا خَلْقَ الصَّلْصَالِ، فَأَعْطَاهُ اللهُ تَعالَى النَّظِرَةَ اسْتِحْقَاقاً لِلسُّخْطَةِ، وَاسْتِتْماماً لِلْبَلِيَّةِ، وَإِنْجَازاً لِلْعِدَةِ، فَقَالَ: (إنَّكَ مِنَ المُنْظَرِينَ إِلَى يَوْمِ الْوَقْتِ الْمَعْلُومِ)

Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwataka malaika watekeleze ahadi aliyowekeana nao, na kutimiza agizo lake la kuwataka wamsujudie Adamu, na kunyenyekea ili kumpa heshima, akasema (s.w.t): “Msujudiyeni Adamu, wote walisujudu isipokuwa iblisi ”. Quran 2:34. Yeye alijiona, akazidiwa na uovu, akajitukuza na kufanya kibri kwa sababu ya kuumbwa kutokana na moto. Alikebehi asili ya umbo la Adamu, yaani udongo. Mwenyezi Mungu Mtukufu alimpa (Ibilisi) muda ili ghadhabu ithibiti kwake. Na kukamilisha mtihani ( kwa mwanadamu) na kutekeleza ahadi, akasema: “Basi kwa hakika umekwisha kuwa mingoni mwa waliopewa muhula mpaka ya siku ya wakati maalum ” (15:38, 38:81).

ثُمَّ أَسْكَنَ سُبْحَانَهُ آدَمَ دَاراً أرْغَدَ فِيهَاعَيْشَهُ، وَآمَنَ فِيهَا مَحَلَّتَهُ، وَحَذَّرَهُ إِبْلِيسَ وَعَدَاوَتَهُ، فَاغْتَرَّهُ عَدُوُّهُ نَفَاسَةً عَلَيْهِ بِدَارِ الْمُقَامِ، وَمُرَافَقَةِ الاْبْرَارِ، فَبَاعَ الْيَقِينَ بِشَكِّهِ، وَالعَزِيمَةَ بِوَهْنِهِ، وَاسْتَبْدَلَ بِالْجَذَلِ وَجَلاً، وَبِالاْغْتِرَارِ نَدَماً ثُمَّ بَسَطَ اللهُ سُبْحَانَهُ لَهُ في تَوْبَتِهِ، وَلَقَّاهُ كَلِمَةَ رَحْمَتِهِ، وَوَعَدَهُ المَرَدَّ إِلَى جَنَّتِهِ، فَأَهْبَطَهُ إِلَى دَارِ الَبَلِيَّةِ، وَتَنَاسُلِ الذُّرِّيَّةِ

Baadaye Mwezi Mungu Mtukufu alimuweka Adamu peponi ambapo aliyafanya maisha yake yakuridhisha, na kubaki kwa amani. Alimtahadharisha na Ibilisi na uadui wake. Adui yake (ambae ni Ibilisi) alimghuri. Akimwonea wivu kubaki kwake milele Peponi akiwa na watendao mema. Akauza yakini kwa shaka yake, na azma kwa unyonge wake, na furaha aliibadilisha kwa woga. Na kuhadaika ikawa ni majuto. Kisha Mwenyezi Mungu Mtukufu alimpa Adamu fursa ya kutubia. Alimfundisha neno la rehema Zake. Na alimuahidi kumrudisha kwenye Pepo yake. Alimteremsha duniani kwenye makazi ya mtihani, nyumba ya majaribu, na kuzaa watoto.

KUTEULIWA KWA MANABII(A.S)

وَاصْطَفى سُبْحَانَهُ مِنْ وَلَدَهِ أَنْبيَاءَ أَخَذَ عَلَى الْوَحْيِ مِيثَاقَهُمْ، وَعَلَى تَبْليغِ الرِّسَالَةِ أَمَانَتَهُمْ، لَمَّا بَدَّلَ أَكْثَرُ خَلْقِهِ عَهْدَ اللهِ إِلَيْهِمْ، فَجَهِلُوا حَقَّهُ، واتَّخَذُوا الاْنْدَادَ مَعَهُ، وَاجْتَالَتْهُمُ الشَّيَاطِينُ عَنْ مَعْرفَتِهِ، وَاقتَطَعَتْهُمْ عَنْ عِبَادَتِهِ.

Mwezi Mungu Mtukufu aliwateua manabii katika kizazi chake - watoto wa Adamu(a.s) - akachukuwa kwao ahadi kwa ajili ya wahyi, na kuchukuwa dhamana kwao kwa ajili ya kuifikisha risala - Ujumbe - lakini wengi katika viumbe Wake walivyobadili ahadi ya Mungu walipotosha agizo lake (s.w.t) kwao wakapuuza haki yake wakamfanyia washirika pamoja naye. Shetani aliwapotosha mbali na kumtambua Yeye. Na aliwaweka mbali na ibada yake.

فَبَعَثَ فِيهمْ رُسُلَهُ، وَوَاتَرَ إِلَيْهِمْ أَنْبِياءَهُ، لِيَسْتَأْدُوهُمْ مِيثَاقَ فِطْرَتِهِ، وَيُذَكِّرُوهُمْ مَنْسِيَّ نِعْمَتِهِ، وَيَحْتَجُّوا عَلَيْهِمْ بَالتَّبْلِيغِ، وَيُثِيرُوا لَهُمْ دَفَائِنَ الْعُقُولِ، وَيُرُوهُمْ آيَاتِ الْمَقْدِرَةِ: مِنْ سَقْف فَوْقَهُمْ مَرْفُوع، وَمِهَاد تَحْتَهُمْ مَوْضُوع، وَمَعَايِشَ تُحْيِيهِمْ، وَآجَال تُفْنِيهمْ، وَأَوْصَاب تُهْرِمُهُمْ، وَأَحْدَاث تَتَابَعُ عَلَيْهِمْ.

Aliwatuma kwao Mitume wake, aliwapeleka manabii wake kwao kwa vipindi: Ili watekeleze ahadi ya kuumba kwao, na wakumbushe neema zake zilizosahauliwa, na ili watoe hoja kwao kwa kufikisha ujumbe. Ili kuamsha vipaji vya hikima vilivyofichikana. Na kuwaonesha alama za uwezo wake wa kila kitu kama vile mbingu zilizoinuliwa na ardhi iliotandikwa chini yao, na sababu za maisha zinazowapa uhai, na ajali zinazowamaliza, na taabu zinazowazeesha na matukio yanayofululiza kwao.

وَلَمْ يُخْلِ اللهُ سُبْحَانَهُ خَلْقَهُ مِنْ نَبِيٍّ مُرْسَل، أَوْ كِتَاب مُنْزَل، أَوْ حُجَّة لاَزِمَة، أَوْ مَحَجَّة قَائِمَة، رُسُلٌ لا تُقَصِّرُ بِهِمْ قِلَّةُ عَدَدِهِمْ، وَلاَ كَثْرَةُ المُكَذِّبِينَ لَهُمْ: مِنْ سَابِق سُمِّيَ لَهُ مَنْ بَعْدَهُ، أَوْ غَابِر عَرَّفَهُ مَنْ قَبْلَهُ عَلَى ذْلِكَ نَسَلَتِ القُرُونُ، وَمَضَتِ الدُّهُورُ، وَسَلَفَتِ الاْباءُ، وَخَلَفَتِ الاْبْنَاءُ.

Mwenyezi Mungu Mtukufu hakuwaacha viumbe wake bila ya nabii mwenye kutumwa, au bila ya Kitabu kilichoteremshwa, au bila ya hoja ya lazima, au bila ya njia iliyonyooka. Hawa wajumbe, hawakujihisi kuwa wachache kwa udogo wa idadi yao wala kwa ukubwa wa idadi ya wanaowakadhibisha. Miongoni mwao aliyetangulia humtaja anayefuata baada yake au mfuasi aliyetambulishwa na mtangulizi wake. Kwa utaratibu huo karne baada ya karne zilipita, vilizaliwa vizazi. Miaka ikapita, mababa walipita na watoto walichukua nafasi.

KUTUMWA KWA MUHAMMAD (s.a.w.w)

إِلَى أَنْ بَعَثَ اللهُ سُبْحَانَهُ مُحَمَّداً(صلى الله عليه وآله) لاِنْجَازِ عِدَتِهِ وَتَمامِ نُبُوَّتِهِ، مَأْخُوذاً عَلَى النَّبِيِّينَ مِيثَاقُهُ، مَشْهُورَةً سِمَاتُهُ، كَرِيماً مِيلادُهُ

Hali iliendelea hivyo mpaka Allah (s.w.t) alipomtuma Muhammad(s.a.w.w) , mjumbe Wake ili kutimiza idadi Yake, na kukamilisha unabii Wake. Akiwa mwenye kuchukua ahadi Yake kutoka kwa manabii, alama zake(s.a.w.w) zilikuwa mashuhuri, uzao wake ni wa heshima.

وَأهْلُ الاْرْضِ يَوْمَئِذ مِلَلٌ مُتَفَرِّقَةٌ، وَأَهْوَاءٌ مُنْتَشِرَةٌ، وَطَرَائِقُ مُتَشَتِّتَةٌ، بَيْنَ مُشَبِّه للهِ بِخَلْقِهِ، أَوْ مُلْحِد في اسْمِهِ، أَوْ مُشِير إِلَى غَيْرهِ

Watu wa dunia hii wakati huo walikuwa kwenye itikadi zinazotofautiana, tamaa za nafsi zimeenea, na njia zikiwa tofauti, wakiwemo waliomshabihisha Mungu (s.w.t.) na viumbe Wake au wenye kupotosha jina lake (s.w.t) au wenye kumshirikisha na viumbe.

فَهَدَاهُمْ بهِ مِنَ الضَّلاَلَةِ، وَأَنْقَذَهُمْ بمَكانِهِ مِنَ الجَهَالَةِ ثُمَّ اخْتَارَ سُبْحَانَهُ لِمحَمَّد صلى الله عليه لِقَاءَهُ، وَرَضِيَ لَهُ مَا عِنْدَهُ، فَأَكْرَمَهُ عَنْ دَارِالدُّنْيَا، وَرَغِبَ بِهَ عَنْ مُقَارَنَةِ البَلْوَى، فَقَبَضَهُ إِلَيْهِ كَرِيماً.

Mwenyezi Mungu Mtukufu aliwaongoza kupitia kwake kutokana na upotovu, na kwa nafasi yake(s.a.w.w) aliwaokoa mbali na ujahili. Kisha Mwenyezi Mungu Mtukufu alimhitari Muhamamd(s.a.w.w) kukutana naye na alimridhia ili awe karibu Yake (s.w.t), na alimzidishia heshima kwa kumwondoa duniani mahali pa majaribu, kwa hiyo alimchukuwa Kwake(s.a.w.w) kwa heshima.

وَخَلَّفَ فِيكُمْ مَا خَلَّفَتِ الاْنْبيَاءُ في أُمَمِها، إذْ لَم يَتْرُكُوهُمْ هَمَلاً، بِغَيْر طَريق واضِح، ولاَعَلَم قَائِم

Na aliacha kwenu ambayo manabii waliacha katika Umma zao[16] . Kwani hawakuwaacha wamepuuzwa, bila ya kuwaeleza njia iliyowazi, wala watakayoongoka kwayo.

KITABU CHA MWENYEZI MUNGU NA SUNNAH

كِتَابَ رَبِّكُمْ [فِيكُمْ:] مُبَيِّناً حَلاَلَهُ وَحَرامَهُ، وَفَرَائِضَهُ وَفَضَائِلَهُ، وَنَاسِخَهُ وَمَنْسُوخَهُ، وَرُخَصَهُ وَعَزَائِمَهُ، وَخَاصَّهُ وَعَامَّهُ، وَعِبَرَهُ وَأَمْثَالَهُ، وَمُرْسَلَهُ وَمَحْدُودَهُ، وَمُحْكَمَهُ وَمُتَشَابِهَهُ، مُفَسِّراً جُمَلَهُ، وَمُبَيِّناً غَوَامِضَهُ

Amekuachieni Kitabu cha Mwenyezi Mungu, Mola wenu: kibainishacho halali yake na haramu yake[17] . Faradhi zake na fadhila zake. Batilisho (nasikh) zake na zilizobatilishwa (mansukh) zake, ruhusa zake na azma zake, hukumu ambazo ni makhsusi, na ambazo zipo katika sura ya jumla, na ambazo zina mafunzo ndani yake na mithali, ndefu na fupi, thabiti zake na mutashabih zake: zilizo wazi na ambazo ni ngumu kueleweka maana yake, zenye kufasiri aya zilizokuja kwa maana ya jumla, na zenye kubainisha maana zake ngumu.

بَيْنَ مَأْخُوذ مِيثَاقُ عِلْمِهِ، وَمُوَسَّع عَلَى العِبَادِ في جَهْلِهِ، وَبَيْنَ مُثْبَت في الكِتابِ فَرْضُهُ، وَمَعْلُوم في السُّنَّهِ نَسْخُهُ، وَوَاجب في السُّنَّةِ أَخْذُهُ، وَمُرَخَّص في الكِتابِ تَرْكُهُ.

Humo kuna aya ambazo kuzijua ni lazima, na kuna ambazo watu wanaruhusiwa kutozijua. Na ambazo imethibiti Kitabuni faradhi yake, na zajulikana kutenguliwa katika sunnah, na ambazo ni wajibu katika sunnah kuzitekeleza, na ambazo katika kitabu zaruhusiwa kuziacha.

وَبَيْنَ وَاجِب بِوَقْتِهِ، وَزَائِل في مُسْتَقْبَلِهِ، وَمُبَايَنٌ بَيْنَ مَحَارِمِهِ، مِنْ كَبير أَوْعَدَ عَلَيْهِ نِيرَانَهُ، أَوْ صَغِير أَرْصَدَ لَهُ غُفْرَانَهُ، وَبَيْنَ مَقْبُول في أَدْنَاهُ، ومُوَسَّع في أَقْصَاهُ

Na kuna ambazo ni wajibu kwa wakati wake, na wenye kuondoka wakati ujao, uharamu wake pia watofautiana, kuna ambazo ni kubwa ametishia kwa (kosa hilo) moto wake, au ndogo zenye ghofrani yake, na kati ya yanayokubalika uchache wake na yenye wasaa katika umbali wake. Kuna ambazo uchache wake wakubaliwa (kwa Mungu) na zenye uwezekano wa kutanuliwa (hukumu yake)[18] .

NDANI YA KHUTBA HII AELEZEA HIJJA

وَفَرَضَ عَلَيْكُمْ حَجَّ بَيْتِهِ الحَرَامِ، الَّذِي جَعَلَهُ قِبْلَةً لِلاْنَامِ، يَرِدُونَهُ وُرُودَ الاَنْعَامِ، وَيأْلَهُونَ إِلَيْهِ وُلُوهَ الحَمَامِ

Na amewajibisha juu yenu kuhiji nyumba yake tukufu, ambayo ameifanya Qibla kwa wanadamu, wanaiendea kama wanyama walazimikapo kuyaendea manyweo ya maji wanayahamanikia uhamanikaji wa njiwa.

جَعَلَهُ سُبْحَانَهُ عَلاَمَةً لِتَوَاضُعِهمْ لِعَظَمَتِهِ، وَإِذْعَانِهِمْ لِعِزَّتِهِ، وَاخْتَارَ مِنْ خَلْقِهِ سُمَّاعاً أَجَابُوا إِلَيْهِ دَعْوَتَهُ، وَصَدَّقُوا كَلِمَتِهُ، وَوَقَفُوا مَوَاقِفَ أَنْبِيَائِهِ، وَتَشَبَّهُوا بمَلاَئِكَتِهِ المُطِيفِينَ بِعَرْشِهِ، يُحْرِزُونَ الاْرْبَاحَ فِي مَتْجَرِ عِبَادَتِهِ، وَيَتَبَادَرُونَ عِنْدَهُ مَوْعِدَ مَغْفِرَتِهِ

Mwenyezi Mungu Mtukufu ameifanya (Kaaba) iwe ndio alama ya unyenyekevu wao kuunyenyekea utukufu Wake, na utii wao kwa enzi Yake. Amechagua kutoka kwa viumbe Wake watiifu walioitikia wito wake. Na wamesadikisha neno Lake. Na wakasimama msimamo wa manabii Wake. Wakashabihiana na malaika wake wazungukao Arshi Yake. Wanafaidika na biashara ya ibada yake. Wakiharakia kwenye ahadi ya msamaha Wake.

جَعَلَهُ سُبْحَانَهُ لِلاِسْلامِ عَلَماً، وَلِلْعَائِذِينَ حَرَماً، فَرَضَ حَجَّهُ، وَأَوْجَبَ حَقَّهُ، وَكَتَبَ عَلَيْكُمْ وِفَادَتَهُ، فَقَالَ سُبْحَانَهُ: (وَللهِ عَلَى النَّاسِ حِجُّ الْبَيْتِ مَنِ اسْتَطَاعَ إِلَيْهِ سَبِيلاً وَمَنْ كَفَرَ فَإِنَّ اللهَ غَنِيٌّ عَنِ العَالَمينَ.

Mungu (s.w.t.) ameifanya (nyumba hii) kuwa ni alama ya Uislamu na ni lengo la heshima kwa wanaojikinga nayo.

Amefaradhisha haki yake, na kulazimisha kuihiji. Na amefanya faradhi juu yenu kuiendea aliposema (s.w.t.): “Na kwa ajili ya Mwenyezi Mungu imewajibikia watu wahiji kwenye Nyumba hiyo, kwa yule awazae njia ya kwendea. Na atakayekanusha basi Mwenyezi Mungu si mhitaji kwa walimwengu. (3:97).