NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI Juzuu 2

NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI0%

NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: VITABU VYA HADITHI

NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI

Mwandishi: SAYYIDI SHARIFU RADHIY
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 7719
Pakua: 2905


Maelezo zaidi:

Juzuu 1 Juzuu 2
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 15 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 7719 / Pakua: 2905
Kiwango Kiwango Kiwango
NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI

NAHJULBALAGHAH JUZUU YA PILI Juzuu 2

Mwandishi:
Swahili

NAHJUL BALAGHA

JUZUU YA PILI

MTARJUMI: HARUNA PINGILI

70 - NA AMESEMA(A.S)

Na Amesema(a.s) - Ibn Sa’ad ameielezea ndani ya at-Tabaqat, Jz. 3, uk. 36, na Al’Qaaliy ndani ya Dhaylul’amali uk. 190, na Al’Isfahani ndani ya Maqatilu Talibiin uk.16, na Ibn Abdi Rabih ndani ya Al-Iqdul al-Farid Jz. 2, uk. 298, na wengine.

KATIKA MKESHA WA SIKU ALIYOSHAMBULIWA

“Nilipatwa na usingizi nikiwa nimekaa nikamuona Mtume wa Mungu(s.a.w.w) , nilimuuliza: ‘Ewe Mtume wa Mungu! Kupindama kulikoje na uadui ambao nimekabiliana navyo kutoka kwa umma wako!’ Akasema: ‘Wapatilize,’ Nikasema: ‘Mungu anibadilishie walio bora kuliko wao, na anibadilishe na aliye mbaya zaidi kwao kuliko mimi.[40]

Amesema Ar-Radhiy (r.a): Anakusudia kwa neno kupindama, na kwa neno mzozo, na huu ni ufasaha wa hali ya juu mno wa maneno.

71 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Al-Mufid ameielezea katika al-Irshad uk. 61, na ibn Da’abiy katika al-Ikhtiswas uk. 155, na Tabrasiy katika al-Ihtijaj Juz.1, uk. 254.

KATIKA KUWALAUMU WA-IRAQI:

“Ama baada! Enyi watu wa Iraqi, mko kama mwanamke mwenye mimba, ameshika mimba na alipotimiza upevu wa mimba akaporomosha mimba, na mumewe akafariki, kwa hiyo muda wake wa ujane ukawa mrefu, na akarithiwa na wa mbali kabisa[41] . Wallahi sijakujieni kwa hiyari; isipokuwa nilikujieni katika hali ya kusukumwa[42] .

Nimepata habari kuwa ninyi mwasema: ‘Ali anasema uwongo, Mungu (swt) akuangamizeni! Nani nimsemee uwongo? Nimuongopee Mungu? Mimi ni wa kwanza kumwamini! Au nimsemee uwongo nabii wake? Mimi ni wa kwanza kumsadiki yeye!

Hapana wallahi, lakini hiyo ni ibara ambayo mmeshindwa kuitambua maana yake[43] , hamkuwa wenye kustahiki nayo, Waylumah, ninakupimieni vipimo vya kiilimu na hikma, upimaji usio na thamani [44] ,4 lau angekuwa na chombo apime humo.” “ Na bila shaka mtajuwa habari zake baada ya muda ,” (38:88).

72 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Ameieleza ibn Qutayba katika Gharibul-Hadith, na Thaqafi katika al-Gharatu, na al- Qadhy al-Qadhwaiy katika as-Sahifatul-Alawiyah, uk. 3.

ALIWAELIMISHA WATU NAMNA YA KUMSALIA MTUME WA MUNGU

“Ewe Mola Wangu! mkunjuaji wa yakunjuliwayo na mhifadhi wa yahifadhiwayo, na muumba wa nyoyo katika maumbile yake ya asili, zenye taabu na mashaka na zenye maisha ya furaha, zijaalie sala zako za ziada na baraka zako zenye kuendelea juu ya Muhammad, mja wako na mjumbe wako, mhitimishaji wa yaliotangulia katika unabii[45] , na mfunguzi wa yaliojifunga[46] na mtangazaji wa haki kwa haki na mzuiaji wa mfuriko wa batili[47] na mvunjaji wa ukali wa upotovu[48] kama alivyobebeshwa akasimama kwa nguvu, akitekeleza amri Yako, mwenye kuharakia katika ridhaa Zako, si goigoi kwenda vitani, wala si dhaifu katika azimio, mwenye kufahamu wahyi Wako, mhifadhi wa wahyi Wako, mhifadhi wa amri Zako na mwenye kuzitekeleza, mpaka kupatikana haki, na akaiangaza njia kwa ababaikaye, na nyoyo zikaongozwa baada ya kuingia fitna na dhambi. Na alitekeleza dalili wazi za njia, na hukumu zenye nuru.

Hivyo yeye ni muaminifu Kwako mwenye kuaminiwa, na mhifadhi wa ilimu Yako iliyo mahsusi, na shahidi Wako Siku ya Hukumu[49] .

Yeye ni mtumishi Wako wa kweli, na Mtume wako kwa viumbe. Oh, Ewe Mola Wangu! Mpanulie nafasi katika kivuli chako[50] , na umlipe kheri ya ziada katika fadhila Zako. Umnyanyulie daraja jengo lake[51] , na ikirimu daraja yake Kwako[52] , mtimizie nuru yake, mlipe akutakalo ushahidi unaokubalika, na usemi unaoridhiwa, muadilifu wa mantiki, na hutba pambanuzi.

Oh Ewe Mola wangu! Kusanya kati yetu na yeye tuwe katika maisha baridi na neema tulivu ya kudumu[53] , na kutosheka na yatakiwayo, na ladha ya utashi, maisha ya raha, utulivu wa akili, na tunu za heshima.[54] ”.

73 - NA MIONGONI MWA MANENO YAKE (A.S)

Na Miongoni Mwa Maneno Yake(a.s) - Ibn Sa’ad ameieleza sehemu ya maneno haya katika Tabaqat, Jz. 1, na al-Baladhuliy kati- ka al-Ansab, uk. 361.

ALIMWAMBIA MARWAN BIN AL-HAKAM HUKO BASRA

“Walisema: Marwan bin Al-Hakamu alitekwa siku ya Jamal na aliwasihi Hasan na Husain wamuombee kwa Amirul-Mu’minina(a.s) . Nao walisema naye kuhusu suala lake, naye (Amirul’Mu’minina) alimwacha huru. Walimwambia (wasemaji ni Hasan na Huseni): Akuba’i ewe Amirul- Mu’minina.Akasema(a.s) :

“Kwani hakunifanyia bai’a baada ya kuuliwa Uthman? Sina haja ya bai’a yake! Kwa kuwa huo ni mkono wa kiyahudi[55] , lau anifanyie bai’a kwa mkono wake angenisaliti kwa tako lake[56] . Ila tu yeye Marwan atakuwa na uamiri wa muda mfupi kama vile mbwa anavyoramba pua yake[57] . Na yeye ni baba wa maraisi wanne wa kaumu[58] .

Umma utapata siku nyekundu kutoka kwake na kwa wanawe.[59] ”.

74 - NA KATIKA USEMI WAKE(A.S)

WALIPOAZIMIA KUMFANYIA BAI’A UTHMAN

“Kwa kweli mnajua kuwa mimi ni mwenye haki nao (ukhalifa) zaidi kuliko mwingine yeyote asiye kuwa mimi; na wallahi nitamwachia (Uthman) maadamu kumwachia mambo ya waislamu yatakuwa katika amani na dhulma haitokuwa isipokuwa kwangu tu[60] , nikitaraji ujira wa hilo na fadhila zake, na kujiweka mbali na mnachoshindania na kujiweka kando na kuyafikia mapambo yake ambayo mnagombania.”

75 - NA MIONGONI MWA SEMI ZAKE (A.S)

Na Miongoni Mwa Semi Zake(a.s) - Ibn al-Athir ameieleza katika an-Nihayah katika mada ya Qirzu.

ALIPOPATA HABARI KUWA BANI UMAYYAH WANAMTUHUMU KUSHIRIKI DAMU YA UTHMAN

“Je Bani Umayyah kunijua kwao hakujawazuia kuniaibisha? Je kutangulia kwangu (kuukubali uislamu) hakujawaweka mbali wajinga na kunituhumu? Kwa kweli aliyowaonya Mungu amewaonya kwa ufasaha zaidi kuliko ulimi wangu, mimi ni mtoa hoja dhidi ya watokao nje ya dini, na ni hasimu wa wavunjao ahadi na wenye shaka[61] , na kwenye Kitabu cha Mungu.

Kwa Kitabu cha Mungu hupimwa yasiyo wazi[62] . Kulingana na yaliyo mioyoni waja watalipwa.” Anaikusudia kauli yake (s.w.t) “Hadhani khasmani ikh’taswamu fii Rabbihim” (22:19).

NAHJUL BALAGHA

JUZUU YA PILI

MTARJUMI: HARUNA PINGILI

76 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Ameyaeleza hayo al-Haraniy katika at-Tuhaf, uk. 150, na ibn Shakir katika Uyunul- Hikami wal mawa’idh, na Zamakhshari katika Rabiul-Abrar Jz. 1, uk. 231, na al-Hisriy katika Zuhurul-Adabi, Jz. 1, uk. 42.

KUHUSU ZUHUDI

“Mungu amrehemu mtu aliyeisikia hukumu akaihifadhi na kuielewa, na aitwapo kwenye mwongozo akausogelea[63] , na amfuata kiongozi (kwa kushika mkanda wake wa kiunoni) na akaokoka, akajihadhari na Mola wake Mlezi, na kuhofia dhambi zake, akatanguliza ikhlas na kutenda mema, akachuma na kupata hazina, na akajiepusha na yaliyohadharishwa. Na akalenga lengo, na kufanikiwa kupata kitu mbadala, akaukabili utashi wake, na kuyakadhibisha matumaini yake (bandia), na akaifanya subira kuwa ndio njia yake ya uwokovu, na taqwa kuwa ndio masurufu ya kifo chake. Akapita njia ya haki, kwa mwenendo wa kiadilifu, na akijiambatanisha na njia ya hali ya juu ya ukweli, na kuutumia vyema wakati wake, na kuuharakia mwisho (wake), na akaenda na akiba ya matendo mema.”.

77- NA MIONGONI MWA SEMI ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Semi Zake(a.s) - Al’Isfahaniy ameielzea usemi huu ndani ya ‘Al-Aghaaniy’ Juz. 11, uk. 29, na Al-Azhariy ndani ya ‘Tah’dhiibi-lughah’ Juz. 15, uk. 27.

KUWAHUSU BANI UMAYYAH

“Kwa kweli Bani Umayyah wananiruhusu kiasi kidogo cha mirathi ya Muhammad(s.a.w.w) . Wallahi endapo nitabaki nitawapuliza mpulizo wa muuza nyama apulizapo mnofu wa nyama ulioenea mchanga!”

Maelezo

Ar-Radhiy (r.a) amesema: Na yaelezwa kwa tamko nayo iko katika hali ya kugeuza, kwa sababu ukweli ni kama ilivyokuwa katika riwaya ya kwanza, sio kwa kuwa hilo halina maana, kwa hiyo hii yakusudiwa riwaya iliyogeuzwa.

Na kauli yake(a.s) (Layufawiqunaniy) yaani wananipa kutoka mali ya (Muhammad) kitu kidogo sawa na mkamo mmoja wa maziwa ya ngamia. Na wid-hamu at-taribatu: ni udongo, ni wingi wa neno wadhamatu, nacho ni kipande cha tumbo au cha ini kilichoanguka na kutapakaa vumbi hupulizwa.

78 - NA MIONGONI MWA SEMI ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Semi Zake(a.s) - Al-Jaahidhwu ameueleza mwisho wa du’a hii katika al-Miatu al-Mukhtaratu.

ALIKUWA AKIOMBA KWA DUA HII:

“Ewe Mungu wangu! Nisamehe ambayo wewe wayajua zaidi kuliko mimi, endapo nitarudia nirejelee kwa msamaha. Ewe Mungu Wangu! Nisamehe kwa niliyoyaahidi nafsini mwangu, na wala hukuuona utekelezaji wake kwangu[64] .

Ewe Mungu Wangu! nisamehe niliyojikurubisha nayo kwako kwa ulimi wangu, halafu moyo wangu ukawa kinyume nayo[65] . Ewe Mungu Wangu! nisamehe na mikonyezo, na maneno ya ovyo, na usahaulifu wa moyo na mtelezo wa ulimi.”

79 - NA MIONGONI MWA MANENO YAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Maneno Yake(a.s) - Ibrahim ibn Hasan ibn Dizili ameieleza katika kitabu Swiffiin, na Saduq katika kitabu Uyunul-Akhbar ar-Ridha, Jz. uk. 138.

Aliwaambia baadhi ya sahaba zake alipokuwa ameazimia kufanya msafara kukabiliana na Khawarij. Na (mmoja wa sahaba zake) alimwambia: “Ewe Amirul-Mu’minina ukifanya safari katika wakati huu nahofia hautofanikiwa mradi wako kwa mujibu wa ilimu ya nyota.” Akasema(a.s) :

“Wadhani kuwa wewe unaelekeza saa ambazo mwenye kufanya safari katika saa hizo ataepushwa na jambo baya, na unahofisha saa ambazo mwenye kusafiri humo atakumbwa na jambo la madhara? Hivyo basi mwenye kukusadiki kwa hilo atakuwa ameikadhibisha Qur’ani, na atakuwa amejitosheleza hatohitaji kuomba msaada kwa Mungu ili kuyapata yapendwayo na kujikinga na makruhu; kwa kauli yako hii wamtaka atakeye itendea kazi amri yako akumiminie shukrani wewe sio Mola wake, kwa kuwa wewe - kwa dhana zako - ndiye uliye muongoza saa ambazo kwazo amepata manufaa, na ataepukana na madhana.”

Kisha Aliwaelekea Watu(a.s) Akasema:

“Enyi watu! Jihadharini na kujifunza elimu ya falaki isipokuwa kiasi cha kupata mwongozo, bara au baharini[66] , kwa kuwa hiyo (falaki) inaitia kwenye ukuhani, na mwanafalaki ni sawa na kuhani, na kuhani ni kama mchawi[67] , na mchawi ni sawa na kafiri na kafiri (marejeo yake) ni motoni. Safirini kwa jina la Mungu.”

80 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Baada Ya Vita Vya Jamal (Ngamia) Katika Kuwalaumu Wanawake

“Enyi watu, kwa hakika wanawake ni wapungufu wa imani[68] , wapungufu wa hisa, wapungufu wa akili. Ama kuhusu upungufu wao wa imani ni kule kubaki kwao bila sala na saumu siku zao za hedhi. Ama upungufu wao wa akili ni kule kuwa ushahidi wa wanawake wawili ni sawa na ushahidi wa mwanaume mmoja. Ama upungufu wao wa hisa ni kule kuwa mirathi zao ziko nusu ya mirathi za wanaume. “Hivyo basi zicheleeni shari za wanawake na jihadharini na walio wa kheri miongoni mwao, wala msiwape tamaa katika jema ili wasiwe na tama katika jambo la munkari.[69]

Sibti ibn Jauzi ameieleza katika at-Tadhkira uk. 85, na ameieleza baadhi yake Abu Talib al-Makki katika Fautul- Qulub, Jz. 1, uk. 282.

81- NA MIONGONI MWA MANENO YAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Maneno Yake(a.s) - Saduq ameieleza katika Ma’anil-Akhbar, uk. 251, na katika al-Khisal, Jz. 1, uk. 11, na al- Barkiy katika al-Mahasin, uk. 234.

KUHUSU ZUHUDI (KUTOTILIA MANANI RAHA YA DUNIA)

“Enyi watu! Zuhudi ni kupunguza matumaini[70] ,na kushukuru neema[71] , na kuogopa kujiingiza kwenye haramu[72] , na endapo hilo likiwa mbali kwenu basi haramu isiishinde subira zenu[73] ,wala msisahau shukrani kwenye neema, Mungu amemaliza udhuru kwenu [74] ,5 kwa hoja zilizo wazi, na vitabu vilivyo na udhuru wa wazi.”.

82 - NA MIONGONI MWA SEMI ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Semi Zake(a.s) Sharifu ar-Radhiy amesema: ‘Nasema: Mzingatiaji akizingatia kauli yake(a.s) : “Atakayeizingatia itampa mwanga” chini yake atakuta maana ya ajabu, na lengo la mbali, lisilofikiwa upeo wake wala hakifikiwi kina chake hasa hasa ikilinganishwa na kauli yake: “Atakayeikodolea macho itampofusha” kwani yeye atakuta tofauti wazi yenye mwanga na ajabu kubwa kati ya “Atakayeizingatia” na “Atakayeikodolea macho”. Salawatul-llahi wasalamuhu alayhi.’

KUHUSU DUNIA NA WATU WAKE

“Nieleze nini kuhusu dunia hii ambayo mwanzo wake ni taabu, na mwisho wake ni kuharibika. Ya halali yake yatakuwa na hesabu, na ya haramu yake yatakuwa na adhabu. Awaye tajiri humo (duniani) hukabiliwa na fitna. Na maskini humo yu ahuzunika. Mwenye kuipenda sana huikosa[75] ,na mwenye kuitupilia mbali humwelekea[76] .

Atakayeizingatia itampa mwanga, na atakayeikodolea macho itampofusha.[77] ”.

NAHJUL BALAGHA

JUZUU YA PILI

MTARJUMI: HARUNA PINGILI

83 - MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Ibn Shu’uba ameieleza katika ‘Tuhaful’uquli’ uk. 146; Na Al-Qaadhi Al-Qudhaiy katika mlango wa tatu wa kitabu ‘Dasturu maalimil’Hukm’ uk. 59; Na Abu Na’im katika ‘Al’hilya’ Juz. 1, uk. 77; Na Al-Amidiy katika ‘Ghurarul’hukam.’

NAYO NI MIONGONI MWA KHUTBA ZA AJABU, NA HUITWA ‘AL-GHARRAAU’:

“Ninamhimidi Allah (s.w.t) ambaye amekuwa na daraja ya juu kwa nguvu Zake[78] , na amekurubia kwa fadhila Zake[79] , Mtoaji wa kila faida na fadhila, na muondoaji wa kila kubwa na dhiki. Ninamhimidi kwa ajili ya huruma na ukarimu Wake, na uwingi wa neema Zake. Na ninamwamini kwa kuwa ni wa mwanzo Aliye dhahiri[80] , na ninamuomba mwongozo kwa kuwa yu karibu mwongozaji.

Na ninamuomba msaada kwa kuwa ni mshindi mwenye nguvu. Na ninamtegemea kwa kuwa ni mtoshelezaji, mnusuru. Na ninashuhudia kuwa Muhammad(s.a.w.w) ni mja Wake na Mtume Wake, amemtuma ili kutekeleza amri yake, na kumaliza udhuru wake[81] , na kutoa maonyo yake[82] .

“Nakuusieni! Enyi waja wa Mungu kumcha Mungu ambaye amekufanyiyeni mifano[83] , na amekuwekeeni wakati maalumu wa maisha, na amekuvikeni riyasha (yaani vazi)[84] ,na ameyafaharisha maisha yenu[85] na kuyaboresha, na amekuzungukeni kwa hesabu[86] ,na amekuandalieni malipo, na amekutunukieni neema nyingi na takrima kwa wasaa. Amekuonyeni kwa hoja za wazi bainifu.

Amekufanyeni kwa idadi, na amekuainishieni muda, ndani ya nyumba ya balaa na mtihani, na kwenye nyumba ya mazingatio ninyi ni wenye kufanyiwa mtihani humo, nanyi mtahesabiwa matendo yenu.”

KUTAHADHARISHWA NA DUNIA

“Kwa kweli dunia kinywaji chake kimetibuka, chanzo chake kina udongo na tope. Mandhari yake yanavutia, na yanaangamiza.

Ni yenye kudanganya na kutoweka, na ni mwanga utowekao haraka na kivuli kipitacho, na ni nguzo iliyoelemea upande, mpaka anayeichukia aanzapo kuifurahia, na mwenye kuichukia aanzapo kuwa na matumaini, punde yainua miguu yake na kuirudisha chini na kumnasa mwanadamu kwa kamba yake, na kumuuwa pale pale kwa mishale yake, na kumfunga mtu[87] , shingoni kamba ya kifo ikimuongoza kwenye malalo yaliobana (yaani kaburi), na marejeo ya upweke, na kuainisha mahali[88] - na thawabu za Aamali[89] .

Na hivyo hivyo waliokuja nyuma baada ya waliotangulia, kifo hakikomi kuziondoa nafsi, wala waliobakia hawakomi kutenda dhambi. Watafuatia mfano wao- (mfano wa waliotangulia katika matendo).

Wanapita kwa makundi mpaka upeo wa mwisho, na mwisho wa mambo, mpaka mambo yatakapokatika, dahari zitakapopita, na kukaribia kufufuka, Mungu atawatoa nje kutoka makaburini, na viota vya ndege, na maficho ya wanyama wakali, na katikati ya maangamizi.

Wataharakia kwenye amri Yake, wakienda haraka kuelekea maeneo yalioandaliwa kwa marejeo yao ya mwisho makundi kwa makundi, wakiwa kimya, hali wamesimama safu kwa safu, wakiwa katika kuonwa na Mungu wakiwa mahali mwitaji aweza kuwaita wamsikie.

Wakiwa na vazi la unyonge, wakifunikwa na unyenyekevu na udhalili, hila imekwisha, matumaini yamekatika, nyoyo zikiwa hazina furaha[90] , sauti zikiwa zimedhoofu, hafifu, na jasho limekuwa kama hatamu[91] , hofu imekuwa kubwa, na masikio yatakabiliwa na radi, kwa kelele ya sauti ya mfanya daawa, akiwaita kwenda kwenye upitishwaji wa maamuzi, na kupata malipo mbadala adhabu na kupata thawabu.[92] ”.

KUWATANABAHISHA VIUMBE

“Waja wenye kuumbwa kwa uwezo, na wamemilikiwa kwa kahari[93] , na mamlaka, na watakufa kwa kuhudhuriwa na Malaika wachukuaji roho[94] , na watawekwa kaburini, na hatimaye kuwa mifupa iliyochakaa, na watafufuliwa (kila mtu) pweke[95] , na watalipwa malipo, na watafanyiwa hisabu kila mtu na yake[96] walipewa muda wa kujiepusha[97] , na waliongozwa njia ya wazi[98] , na waliruhusiwa kuishi na muda wa kutafuta maridhawa, na wameondolewa giza la shaka, na wameachwa kwenye medani ya mashindano ya farasi[99] , na kuachwa wafikiri na kutafuta yahitajiwayo kwa mazingatio, kuwa na uvumilivu wa mtafutaji, anayejaribu kukipata kilichompotea, katika muda wa harakati za kazi kabla ya ajali.”

UBORA WA KUKUMBUSHA

“Mifano muwafaka ilioje na mawaidha yaponyayo! endapo yangeafikiana na nyoyo safi, na masikio sikivu, na rai zenye azma na akili thabiti!

“Mcheni Mungu uchaji wa mwenye kusikiliza na akanyenyekea, na atendapo ovu yu-atambua, na akiogopa hutenda yaliyo sawa, akiwa na hadhari huharakia kwenye mema, akiwa na yakini hufanya mema, akipewa mazingatio mara kadhaa huzingatia, akitahadharishwa hujihadhari, akikaripiwa hukaripika, aitwapo na wito wa mlinganiaji (kwa Mungu) hurejea kwake.

Arejeapo hutubu, na akifuata hufanya vizuri, akionyeshwa njia ya sawa huiona na yu aharakia akitafuta, na kuokoka mbio! na yuafaidika na mali, na kuwa na tabia njema, na kuyajenga marejeo, na akabeba masurufu mgongoni kwa ajili ya siku ya kuondoka kwake, na akaelekea njia aikusudiayo na hali ya haja yake, na mahali pa mahitaji yake, na kutanguliza mbele yake kwa ajili ya nyumba ya kubaki kwake.

Hivyo basi mcheni Mungu, enyi waja wa Mungu kwa upande wa lengo alilokuumbieni[100] , na mjihadhari upeo wa kujihadhari na ambayo amekuhadharisheni nafsi yake[101] , na kuweni wastahiki wa ambayo amekuandalieni[102] , kwa kutekeleza ya wajibu[103] , na kujihadhari na marejeo yake yanayotisha.”

Na Sehemu Hii Ya Khutba Kuwakumbusha Watu Neema Za Mungu

“Amekujaalieni masikio ili muweze kufahamu na kuyahifadhi aliyoyakusudia, na macho ili muweze kutandua tandabui ya giza giza, na viungo vya mwili vyenye kuwemo ndanimwe viungo vingine, na vyenye kulingana na umbo la mahali khusika katika muundo wa sura zake, na muda wa umri wao, na miili yenye kutekeleza manufaa yake, na nyoyo ambazo zimeshughulika kutafuta chakula chake, ndani ya neema zake zilizo funi- ka, na yawajibishayo upaji wake, na vizuizi vya afya yake[104] .

“Amekukadirieni umri aliousitiri mbali na (uelewa wenu) amekubakishieni mabaki ya athari za waliopita kabla yenu, ili iwe mwongozo kwenu, watu hao walistarehe na hisa zao kubwa, kwa nafasi bila ya kizuizi[105] .

Kifo kiliwachukua bila kufikia matumaini yao, (kifo) kiliwakata na kuwa’ngoa mbali nayo - matumaini - hawakujiandaa wakati miili iko salama, wala hawakuzingatia mwanzoni mwa umri wa ujana. Je wenye ngozi laini ya ujana wanangoja mpaka kupinda migongo kwa uzee!

Na ambao wana siha njema wanangoja kufikiwa na hali mbaya ya siha! Na walio na muda wa kubaki wanangoja mpaka uishe, pamoja na ukaribu wa kutoweka, na mbabaiko wa kutoweka, na kufikiwa na huzuni moyoni, na kusongwa na mate, na hofu ya mgonjwa na uchungu wa huzuni, na mbinyo wa mate.

Muda utafika wa kuomba nusra ya wajukuu na ndugu wa karibu, wapenzi na wenzi. Je! Ndugu wa karibu wamezuia, au vilio vimeleta nafuu!

Ameachwa mahali pa wafu amefungika, na kwenye malalo yaliyombana akiwa mpweke, wadudu wameirarua ngozi yake, na matukio yameuchakaza upya wake, na dhoruba itakuwa imefuta athari zake, na tukio litakuwa limefuta dalili zake, na miili itakuwa imehiliki baada ya kujaa kwake, na mifupa itakuwa imeoza baada ya nguvu zake, na nyoyo zitakuwa zimefungika kwa uzito wa mizigo (dhambi) yao, zitakuwa na yakini na habari zake zilizojificha, hazitotakiwa baada ya hapo kuzidisha Aamali zake njema[106] wala hazitoombwa kutubia kwa ajili ya ubaya wa kuteleza kwake![107] .

Je! Hamko wana wa kaumu hii, na mababa zao, ndugu na jamaa zao wa karibu? Mnafuata mifano yao na kuiga njia zao[108] na mwaenda njia zao, nyoyo ziko bado ngumu, zimeghafilika mbali na mwongozo wake, zaenda njia isiyokusudiwa! Kama kwamba mkusudiwa ni mwingine, kama kwamba mwongozo upo katika kukusanya dunia yake.”

HADHARI YA KITISHO CHA AS-SIIRAAT

“Na juweni kuwa mtapaswa kuvuka juu ya as-Siiraat nyayo zitateleza kiasi cha kumtupa mtu chini, na vitisho vya utelezi wake na mfululizo wa vitisho vyake.

Basi mcheni Mungu enyi waja wa Mungu uchaji wa mwenye akili, ambaye fikra zimeushughulisha moyo wake, na hofu imeutaabisha mwili wake, na sala ya tahadjudi imemfanya akeshe, na matumaini yamembakisha na kiu nusu ya mchana wa siku yake, (yaani anafunga mchana wake) na zuhudu imezuia matamanio yake, na dhikr ya Mungu imeufanya ulimi wake kuwa mwepesi, na ametanguliza hofu kwa ajili ya amani yake[109] akajiepusha njia zilizo kombo kwa kufuata iliyo sawa, kwa ajili ya iliyo sawa, yu afuata njia iliyonyooka zaidi ili kuifikia njia ihitajiwayo; wala geuzo la ghururi halikugeuza fikra yake, wala mkanganyiko wa mambo haukumfanya asijue ukweli.

Akiwa katika hali ya furaha kwa bishara ya kufaulu neema ya maisha mema, katika neema kubwa ya usingizi wake, na siku yake yenye amani mno.

Akiwa amevuka kivuko cha hii haraka (dunia) mwenye kuhimidiwa[110] , na akiwa ametanguliza masurufu ya baadaye akiwa na furaha, na ameharakia kutoka kwenye woga[111] na akakaza mwendo katika muda wa uhai[112] na akapenda kipaswacho, na kukiepuka kinachobidi, katika siku yake akaichunga kesho yake, na akaangalia yanayokuja mbele miongoni mwa a’amali, yaani akaangalia atakachokitanguliza miongoni mwa aamali.

Yatosha pepo kuwa ni malipo mema na mafanikio, na moto ni adhabu tosha na mateso, Mungu (s.w.t) ni mlipizaji tosha na mnusuru! Na Kitabu (Qur’ani)[113] ni hoja tosha na hasimu.

“Nakuusieni kumcha Mungu ambaye hakuacha udhuru kwa aliyoyaonya, na ametoa udhuru kwa onyo lake wazi[114] , amekutahadharisheni na adui aingiae vifuani kwa kificho[115] , na kupulizia masikioni kwa siri, kwa njia hiyo, amepotosha na kufanya uharibifu.

Atoa ahadi ya uwongo na kuyapamba maovu, na kudharau madhambi makubwa yaangamizayo, mpaka anapomporomosha kutoka daraja ya mwongozo mwenzi wake[116] , naye atastahiki rehani yake, atakuwa yuakanusha aliyokuwa akiyapamba, na kuyakuza aliyokuwa akiyadharau, na kuyatahadharisha aliyokuwa akiyafanya yako salama.”

MIONGONI MWAYO MAELEZO YA KUUMBWA MWANADAMU

“Au mwangalie mwanadamu ambaye Mungu amemuumba ndani ya giza la mfuko wa uzazi na mifuniko ya sitara, ikibubujikiwa na manii, kisha likafanyika pande la damu lisilo na sura, baada ya hapo mimba, halafu kitoto kichanga kinyonyacho, kisha mtoto, baada ya hapo kijana, kisha amemtunukia moyo wenye kumbukumbu, ulimi wa kunenea, na macho yakuonea, ili aweze kufahamu na kuzingatia, apate kuacha kutenda maovu akijiziwia (kwa nguvu za mazingatio) afikiapo utu uzima, na kufikia kimo chake cha kawaida, na umbo lake kufikia kimo chake.

Akanusha kwa kiburi, aingiwa na ghururi na kubabaika bila kujali. Aijaza ndoo kubwa ya matamanio yake, afanya juhudi kukamilisha utashi wa dunia yake, katika matamanio yake, akienda na yanayomdhihirikia katika utashi wake. Kisha hakuogopa uovu wowote, wala kutishika wala kuwa na wasiwasi. Alikufa ndani ya maovu yake hali yukijana aliyeghurika. Aliishi akiwa makosani kwa muda mfupi. Hakufaidika na thawabu mbadala. Wala hakutekeleza wajibu wowote. Maradhi mabaya yalimkabili akiwa bado na ukaidi wake katika njia ya furaha yake kubwa, na alipitisha usiku akiwa kama amelewa[117] .

Alikesha akiwa katika shida ya majonzi na machungu, kufikiwa na uchungu na magonjwa, kati ya ndugu na ndugu wa damu, na baba mwenye huruma, na mama anayelia akisema: ole wangu mwenye huzuni, dada apigaye kifua akiwa amefadhaika; na mtu yu katika sakarati ya mauti anataabika na shida ya kukatisha tamaa, na mvuto wa kuchukiza, na msukumo wa sakarati ya mauti.

Kisha yuatiwa ndani ya sanda akiwa mublisa[118] mwenye kukata tamaa ya rehema ya Mungu avutwa kwa urahisi[119] , kisha kutiwa ndani ya jeneza akiwa mwenye machovu ya kutupwa, na aliyekondeshwa na ugonjwa.

Akibebwa na wasaidizi vijana, na ndugu wasaidizi wambeba wakimpeleka kwenye nyumba yake ya upweke na na watu huacha kumzuru[120] , na mahali pa upweke, mpaka wanaporudi waliokuwa wakimsindikiza na akarejea wenye huzuni, atakalishwa shimoni mwake akisemeshwa[121] kwa faragha maswali ya kuduwaza, na mtihani wa kujikwaa.

Na balaa kubwa mno huko ni kuingia maji ya moto na kuteseka na Jahannam, na kutokota kwa moto, na ukali wa sauti ya moto, hakuna muda wa mapumziko, wala wa raha, wala nguvu ya kuzuia wala kifo cha kutuliza, wala usingizi wa kuliwaza, atakuwa kati ya aina mbalimbali za maiti[122] , na adhabu za kila wakati na saa zote! Hakika tunajilinda na Mungu.

Enyi waja wa Mungu! Wako wapi ambao walipewa umri mrefu na kuneemeshwa! Walijulishwa na wakafahamu, na walipewa muda na wakaupoteza bure[123] , walikuwa salama na wakasahau, walipewa muda mrefu wa maisha, waliumbwa kwa sura nzuri, walitahadharishwa machungu, waliahidiwa makubwa! Jihadharini na dhambi zinazoangamiza, na aibu zikasirishazo.

Enyi wenye macho na masikio na afya na mali! Je kuna upenyo! Au epuko, au kimbilio, au marejeo (yaani kurejea hapa duniani) au hapana? “Basi mpaka lini mwaibadilisha haki kwa batili?” (6:95) “Vipi mwaondolewa mbali na ibada ya Mwenyezi Mungu.” (40:62)

Au mwaghurika na nini! Hali ikiwa mmoja wenu hisa yake ya ardhi yenye urefu na upana ni kadiri ya urefu wake, mwenye kugusishwa shavu lake na mchanga (yaani maiti azikwapo ni sunna shavu lake ligusishwe mchanga kwa kuiondoa sanda aliyovikwa eneo la shavu lake).

Enyi waja wa Mungu! ni hivi sasa hali kamba haijakaza shingoni[124] , na roho zimeachwa katika wakati wa kutaka mwongozo, hali miili iko na raha, na ukumbi wa kujikusanya[125] , na muda wa maisha upo na mwanzo wa muda wa utashi [126] ,49 kuna nafasi ya kufanya toba, na nafasi ya wakati wa haja kabla ya shida, dhiki, hofu, na kubanwa, na kabla ya kuja mauti yanayongojewa na kabla ya shiko la Mwenye nguvu Muweza (s.w.t).”.

NAHJUL BALAGHA

JUZUU YA PILI

MTARJUMI: HARUNA PINGILI

84 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

KATIKA KUMUELEZEA AMRU IBNUL-A’AS

“Namshangaa ibn An-Nabighah! eti asema akiwa kati ya watu wa Syria (Sham) kuwa mimi ni mtu wa mzaha, na kuwa mimi ni mtu wa mchezo mwingi, najishughulisha na mieleka na kupigana na watu. Amesema batili na ametamka akiwa na dhambi.

Angalieni, (maneno ya uovu mno ni uwongo) naye yuasema na yuadanganya, anaahidi na yuaenda kinyume, anaomba kwa kung’ang’ania[127] na akiombwa yuafanya ubakhili, anavunja ahadi, na anaukata udugu. Awapo vitani yeye ni mkemeaji na muamrishaji!.

Hapo ni ikiwa panga hazijachukua nafasi yake, na zikichukua nafasi yake, ujanja wake mkubwa ni kuwaonyesha maadui zake utupu wake. Ama mimi wallahi kukumbuka mauti kwanizuia kufanya mzaha, na kwa kweli yeye kimzuiacho kusema kweli ni kuisahau akhera, kwa hakika yeye hakumpa bai’a Muawiya mpaka alipompa sharti ya kupewa kitu.[128] ”.

85 - MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - al-Wasitiy ameitaja katika Uyunul-Hikami wal Mawa’idhy, na Ibn Sibt Jauziy katika Tadhkiratul-Khawa’is uk. 131.

KATIKA KUMWADHIMISHA MWENYEZI MUNGU NA KUMTUKUZA

“Na ninashuhudia kuwa hapana apasaye kuabudiwa isipokuwa Allah swt. peke Yake, hana mshirika, ni wa milele (bila mwanzo) alikuwa yupo wakati hapakuwa na kitu kingine, na ataendelea kuwepo baada ya kutoweka kwa kila kitu, Yeye hana kikomo. Dhana haiambui kumpata na sifa, wala nyoyo haziwezi kumuelewa kwa aina, wala hapatwi na ufanywaji wa sehemu sehemu wala kufanywa kwa mfano kwamba hii ni baadhi ya sehemu ya Mungu. Hazungukwi na uoni wa macho na wa nyoyo.[129] ”.

NA SEHEMU YAKE NYINGINE (YA KHUTBA) KUIELEZEA PEPO

“Tabaka zinazo zidiana, na daraja zinazo tafautiana, neema zake hazikati- ki, atakayedumu humo hatozeeka, wala mkazi wake hatokuwa fakiri.”.

86 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Ad-Dainuriy ameitaja katika al-Akhbar at-Twiwalu uk. 145; na ibn Shu’ba katika Tuhaful- Uqul uk. 100, na al-Barqi katika al-Mahasimu uk. 233.

KUHUSU WAADHI WA KUJIANDAA KWA AJILI YA ULIMWENGU MWINGINE NA KUFUATA AMRI ZA MUNGU

“Amezijua siri, na habari ndani ya dhamiri, yuakizunguka kila kitu, na mwenye kukishinda kila kitu, na mwenye nguvu juu ya kila kitu. Basi mtendaji miongoni mwenu na atende ndani ya muda wa (uhai) wake kabla ya kukabiliwa na ajali yake. Na atende wakati wa wasaa kabla ya kushughulishwa kwake, na wakati wa nafasi yake kabla hajashikwa koo[130] .

Ajiandae kwa ajili ya nafsi yake na safari yake, na aandae masurufu kutoka kwenye nyumba ya kituo chake (cha muda) kwa ajili ya nyumba ya kudumu kwake.

Mkumbukeni Mungu swt. enyi watu, kwa aliyokutakeni ndani ya Kitabu chake kuyazingatia, na haki Zake alizozihifadhi humo, kwa kuwa Mungu (s.w.t) hajakuumbeni bure, na wala hajawaacheni bila ya faida, wala hajawaacha katika ujinga wala upofu. Amepandisha daraja ya athari zenu, na amejua amali zenu, na ameamua ajali zenu.

Na amekuteremshieni Kitabu kinachobainisha kila kitu, na amemrefushia umri nabii Wake kwa zama ndefu, kiasi cha kumkamilishia yeye na ninyi ujumbe - aliouteremsha Kitabuni mwake - ambao ni dini Yake ambayo ameiridhia nafsini Mwake; na amebainisha kwenu - kupitia ulimi wake - matendo mema na mabaya, makatazo Yake na amri Zake, na ameweka mbele yenu hoja Yake na kuondoa udhuru kwenu, amekukemeeni na kuwaonya na adhabu kali. Hivyo basi zidirikini siku zenu zilizobaki, na zifanyeni nafsi zenu zivumilie humo. Kwa kuwa ni chache katika siku nyingi ambazo mnakuwa katika mghafala, na kutotilia manani mawaidha, msiuachie muda, utawawekeni katika njia ya madhalimu, na msijipendekeze, kwa kuwa kujipendekeza kutawasukumeni kwenye maasi.

Enyi waja wa Mungu! Kwa kweli mnasihi mzuri mno wa nafsi yake katika watu ni yule mtii mno wa Mola Wake[131] ; Na kwa kweli mwenye kuighushi mno nafsi yake ni muasi sana wa Mola Wake[132] ; na mwenye kupunjwa ni yule ambaye ameipunja nafsi yake, na mwenye kutamani mfano wa hali ileile[133] ni yule ambaye dini yake iko salama, na mwenye furaha ni mweye kuwaidhika na mtu mwingine, na dhalili ni mwenye kuhadaika na utashi wa nafsi yake na kughurika kwake. Jueni kwamba kuwepo kwa kiasi kidogo cha riya’a[134] - ni ushirikina, na kukaa na watu wanaofuata matamanio ya nafsi zao - hawaa - yaliyoko nje ya maadili ya kisharia - kunasahaulisha imani, na ni mahudhurio ya Shetani.

Jiepusheni na uwongo, kwa kuwa ukando na imani. Mkweli yu ukingoni mwa wokovu na heshima, na muongo yuko katika kilele cha kuanguka na kudharauliwa. Msihusudiane, kwa kuwa husuda huila imani kama moto ulavyo kuni.

Msibughudhiane, kwa kuwa huko ni kwenye kufuta imani[135] ; na jueni kwa mba kuwa na matumaini mno - kunaisahaulisha akili na kumbukumbu[136] . Basi yakidhibisheni matumaini kwa kuwa ni ghururi, na mwenye nayo ameghurika.”

87 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - Zamakhshari ameieleza katika Rabiul-Abrar mlango wa al-izzu

wa sharaf.

KUHUSU AMPENDAYE MUNGU MTUKUFU

“Enyi waja wa Mungu! Kwa kweli miongoni mwa waja wapendwao mno na Mungu ni mja ambaye Mungu amemsaidia kupambana na nafsi yake, akawa yuaifanya huzuni ni shi’aru yake - vazi la ndani[137] , na amevaa joho la hofu, kwa hiyo taa ya mwongozo ikaangaza moyoni mwake, na aka andaa takrima kwa ajili ya siku yake atakayofikia, kwa hivyo akasogeza kwa ajili yake kilicho mbali, na akapoza makali ya shida[138] , ameangalia akatambua, akakumbuka na akakithirisha[139] .

Alipoza kiu kwa maji baridi aliyorahisishiwa maendeo yake, akanywa na kutosheka. Akapita njia iliyosawa, akiwa amevua vazi la matamanio, na kujiepusha na mahangaiko ya moyo, isipokuwa hangaiko moja pekee amebaki nalo[140] , kwa hiyo akawa ametoka na kuwa mbali na sifa za upofu, na mbali na kushirikiana na watu wa matamanio, hivyo akawa miongoni mwa funguo za milango ya uongofu, na vifungio vya milango ya kuangamia.

Ameiona njia yake na akaipita njia hiyo, na akaijua miongozo yake, akaivuka bahari yenye maji mengi iangamizayo, na akashikamana na kishiko kwa umadhubuti, na miongoni mwa kamba iliyo ngumu mno, kwa hiyo yeye kwenye yakini yu kama mwanga wa jua, ameisimamisha nafsi yake kwa ajili ya Mungu (s.w.t) katika mambo ya hali ya juu kabisa; kwa kulikabili kila limfikalo, na kuchukua kila hatua ihitajiwayo kwa hilo, na kulirudisha kila tawi kwenye shina lake[141] .

Ni taa ya giza jingi, mfichuaji wa upofu, ni ufunguo wa yaliyofumbika, mzuiaji wa shida, mwongozaji wa jangwani, akisema yuafahamisha, akinyamaza husalimika.

Amekuwa na ikhlasi kwa Mungu naye akamfanya makh’susi kwa ajili Yake, hivyo yeye ni chimbuko la dini Yake, na vigingi vya ardhi Yake. Amejiambatanisha binafsi na uadilifu, na ukawa uadilifu wake wa kwanza kujiondolea utashi wa kibinafsi.

Anaielezea haki na anaitendea kazi, haachi lengo la kheri ila atalikusudia, wala padhaniwapo kheri ila atapaendea. Amekishika Kitabu hatamu zake[142] nacho ndio kiongozi wake na Imamu wake. Anashuka pale ambapo kinapoifikisha mizigo yake[143] , na anateremka mahali pake pakufikia.”

SIFA ZA MTU FAASIQI

“Na mwingine amejiita mwanachuo hali akiwa si mwanachuo[144] , amedondoa dhana za kijahili kutoka kwa majaahili, na upotovu kutoka wapotovu, na amewategea watu mtego uliotengenezwa kwa kamba ya udanganyifu, na maneno ya uwongo; anakichukuwa Kitabu-Qur’an - kwa maoni yake; na ukweli ameupindisha kulingana na utashi wake binafsi.

Anawafanya watu wajione wako salama watendapo makosa ya jinai, na hulichukua kosa kubwa kama ni kitu chepesi, anasema: ‘Nasita kwenye mambo yasiyo wazi,’ na humo yuajiingiza; na anasema: ‘najiepusha mbali na bid’a,’ na punde amejiingiza humo. Hivyo basi sura yake ni ya mtu, na moyo ni moyo wa mnyama, hajui mlango wa uongofu ili aufuate, wala mlango wa upotofu ili aufunge akiwa mbali nao, na huo ni umauti wa walio hai. “Basi mpaka lini mwaibadilisha haki kwa batili?” (6:95) “Vipi mwaondolewa mbali na ibada ya Mwenyezi Mungu.” (40:62).

Na alama zipo[145] , Na aya ziko wazi, na minara imesimamishwa[146] ,mnapotezewa wapi! na vipi mnakuwa vipovu na kati yenu kuna itrah ya Nabii wenu![147] Nao ndio hatamu za ukweli[148] , na ni alama ya dini, na ndimi za ukweli! Hivyo wawekeni daraja nzuri mno ya Qur’an[149] , na muwaendee mwendo wa ngamia walio na kiu[150] . “Enyi watu! Chukueni kutoka kwa Khatamun-Nabiyina - hitimisho la Manabii(s.a.w.w) : (Kwa hakika hufa afaye katika sisi na wala si mfu[151] , na huoza aliyeoza katika sisi wala hakuoza) hivyo basi msiseme msiyoyatambua, kwa hakika ukweli mwingi upo katika myakanushayo[152] .

Kubalini udhuru wa msiye na hoja dhidi yake - naye ndimi - je sikuifanyia kazi kwenu thiq’lu kubwa![153] Na ninaiacha kwenu thiq’lu ndogo? Na nikasimika katika nyinyi bendera ya imani, na nimekusimasheni kwenye mipaka ya halali na haramu, na nikakuvisheni afya kutokana na uadilifu wangu, na nimekukukunjulieni mema kwa kauli yangu na vitendo vyangu, na nimekuonyesheni tabia njema za hali ya juu kutoka kwangu mimi mwenyewe binafsi. Hivyo msitumie rai katika ambayo hakifikiwi kina chake na macho, wala fikra haziingii.[154]

Na Sehemu Ya Khutba Hii Kuwahusu Bani Umayyah:

“Mpaka atadhania mwenye kudhani kuwa dunia imefungwa aqal, kwa Bani Umayyah, yawapa kheri zake[155] , na kuwaongoza kwenye chemchemi safi za manyweo yake, na wala ummah huu hautaondolewa mjeledi wala upanga wake, na atakuwa ameongopa adhaniaye hivyo. Bali hilo ni tone la maisha ya ladha[156] (watalila kwa muda kisha watalitema lote).”.

88 - NA MIONGONI MWA KHUTBA ZAKE(A.S)

Na Miongoni Mwa Khutba Zake(a.s) - al-Kailaniy ameieleza katika ar-Raudhwa uk.62, na Sheikh al-Mufiidu katika ar-Rishadu uk.173, na Ibn Athir amezitafsiri (hadith) ghariib katika an-Nihaya mada ya Azalu.

KATIKA KUELEZEA MAKOSA WALIYONAYO WATU

“Amma ba’ad. Kwa kweli Mungu hakupata kumuangamiza dhalimu wa zama fulani katu isipokuwa baada ya kumpa fursa na raha, wala hakuuganga mfupa wa yeyote katika wana umma isipokuwa baada ya dhiki na shida, na hakuwakabili kwa misiba na shida juu yao hata kwa kiasi kidogo kuliko ambacho kitawafikeni au tayari kimewafikeni, kinatosha kuwa somo. Wala sio kila mwenye moyo ni mwerevu, wala sio kila sikio ni sikivu, wala sio kila aangaliaye ni mwenye kuona.

Ajabu ilioje! Nitakuwaje nisistaajabishwe na makosa ya vikundi hivi kwa tafauti za hoja zao katika dini yao! Hawafuati athari ya Nabii (wao) wala hawaongoki na matendo ya waswii, wala hawaamini ghaibu, wala hawajiepushi na jambo la aibu, wanatenda katika mambo yanayoshakiwa, na wanakwenda na matamanio.

Kwa wao jema ni lile wanalolipenda wao, na ovu kwao ni walikataalo[157] , kimbilio lao katika matatizo ni kwao wenyewe binafsi, mategemeo yao katika mambo yanayoshakiwa ni rai zao. Kama kwamba kila mmoja ni imamu wa nafsi yake[158] , amejiamulia ayadhaniayo kuwa ndiyo tegemeo, na ni sababu thabiti.”.