UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH0%

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH Mwandishi:
: Abdul Kareem J. Nkusui
Kundi: Tarehe

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH

Mwandishi: Dr. As'ad Waheed Alqasim
: Abdul Kareem J. Nkusui
Kundi:

Matembeleo: 8245
Pakua: 1630

Maelezo zaidi:

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 13 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 8245 / Pakua: 1630
Kiwango Kiwango Kiwango
UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYYAH

Mwandishi:
Swahili

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA

SEHEMU YA TANO

NDOA YA MUDA

Ndoa ya muda ambayo inajulikama vile vile kama ndoa ya "Mut'a," nayo ni mwanamke kuozesha nafsi yake kwa mwanamme kwa mahari maalumu na kwa muda maalumu, kwa kufunga ndoa iliyotimiza masharti Sahih ya kishariah. Tamko lake ni mwanamke kumwambia mwanaume baada ya maafikiano na maridhiano juu ya mahari na muda: "Zawwajtuka nafsi bimahri qadruhu kadha ilal-ajalil-maalum" (Nimekuoza nafsi yangu kwa mahari kadha kwa muda maalumu), na muda unabainishwa wazi. Na jibu la mwanaume linakuwa haraka "Qabiltu" (Nimekubali).

Na wakala unajuzu katika ndoa hii kama ilivyo katika mikataba mingine. Na kwa kukamilika masharti ya ndoa, mwanamke anakuwa ni mke wa mwanaume na mwanaume anakuwa ni mume wake hadi mwisho wa muda uliopangwa katika ndoa. Na wanaweza kuongeza muda mwingine, na ni wajibu kwa mke akae 'Iddah baada ya kumalizika muda kwa tohara mbili (hedhi mbili) kama anapatwa na hedhi, vinginevyo ni kwa muda wa siku arobaini na tano. Na mtoto wa mut'a awe ni mvulana au binti ananasibishwa kwa baba yake.

Na Waislamu pamoja na khitilafu za madhehebu yao wanaafikiana na aina hii ya ndoa, ndoa hii ni katika mambo yalioanza tangu mwanzo wa Uislamu na kwayo imeteremka Ayah:

فَمَا اسْتَمْتَعْتُم بِهِ مِنْهُنَّ فَآتُوهُنَّ أُجُورَهُنَّ فَرِيضَةً ﴿٢٤﴾

"Kwa mlio jifurahisha nao miongoni mwao basi wapeni mahari yao .” (An-Nisaa 04:24)

Na wamefasiri wengi wa wafasiri wa Ahl as-Sunnah Al-Istimtai katika Ayah hii kwa ndoa ya Mut'a na Ibn 'Abbas na 'Ubay bin Kaab na Sa'id bin Jubair walikuwa wanasoma Ayah hii "Fama-stamta'atum bihii minhunna ilaa ajalim-musammaa fa'tuuhunna ujuurahunna."[226]

Amesema Ibn Kathir katika tafsiri yake akielezea hilo "na jambo ambalo liko mbali sana, ni hawa kuamini kupotoshwa kwa Qur'an, hivyo ni lazima kwa lililokusudiwa na wala sio kusoma"[227] na kuteremka Ayah hii katika ndoa ya Mut'a ni katika ambayo hayapasi kuwa ni maudhui ya mjadala, bali mjadala ni kuwa Ayah hii ni Mansukh au sio Mansukh? yaani imeharamishwa baada ya kuhalalishwa kwake au imebakia katika hali yake?

Mwanzo tunaeleza baadhi ya yaliopokewa katika Hadith zinazothibitisha ndoa ya Mut'a, kuwa ni ya kisheria katika Uislamu miongoni mwa aliyopokea Bukhari katika Sahih yake.

Kutoka kwa 'Abdillah amesema tulikuwa tukipigana vita pamoja na Nabii(s.a.w.w) na hatukuwa na wanawake basi tukasema Je tufanye ponyeto (tujichue wenyewe)? Akatukataza hilo, akaturuhusu baada ya hapo kuoa mke kwa kumpa nguo - kisha akasema: "Enyi mlioamini msiharamishe mazuri aliyo wahalalishia Allah (s.w.t)."[228]

Na Hadith ifuatayo inathibitisha bila ya shaka yoyote kwamba Mtume amefariki bila ya kuharamisha ndoa ya Mut'a na kwamba aliyekataza ni mtu mwingine baada ya kufariki kwa Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) . Amesema Ayah ya Mut'a imeteremka katika Kitabu cha Allah (s.w.t) na haikuteremka Ayah ya Qur'an ya kuiharamisha na kuikataza mpaka akafariki, Mtu (fulani) akasema kwa maoni yake aliyoyataka.[229]

Na 'mtu' anaye ashiriwa katika Hadith iliyotangulia, si mwingine isipokuwa ni 'Umar al-Khattab, ambaye imethibitika kuwa yeye ndiye aliyeharamisha ndoa hii kama ilivyokuja katika Sharh ya Al-Baari katika Sahih Bukhari - angalia maelezo yake chini kwa tarjuma ya Kiingereza.

Na imekuja katika Sahih Bukhari vile vile katika Babu al-Tamattu' 'alaa ‘ahdi rasulilah(s.a.w.w) : ametusimulia Musa bin Isma’il, ametusimulia Hamaam kutoka kwa Qatadah amesema, amesimulia Mutarifu kutoka kwa Imran amesema: Tulifanya Mut'a wakati wa Mtume wa Allah(s.a.w.w) na Qur'ani ilishuka (juu ya hilo), na mtu (fulani) akasema kwa maoni yake anayoyataka.[230]

Ni uwazi ulioje wa vipi mtarjum alivyopiga chenga kwa kuifanya kwake kuwa ni mahsusi kwa Tamattu iliyopokewa katika riwayah ya Imran kuwa ni Haji-Tamattu na wala sio Mut'a ya wanawake. Vyovyote iwavyo kilicho muhimu kwetu ni kile kilichopokewa katika Sahih Bukhari tu, na kuashiria kwetu katika tarjuma haikuwa isipokuwa ni kudhihirisha alicho kinukuu mtarjum kutoka sharh ya Al-Baary katika Sahih Bukhari, na hasa kwa mwanamme asiyejulikana katika riwayah. Na yanatiwa nguvu kwa aliyo mwanamme asiyejulikana katika riwayah. Na yanatiwa nguvu kwa aliyo yapokea Muslim katika Sahih yake kwa Isnad ya Ibnun-Nadhar amesema: “Ibn ‘Abbas alikuwa anaamrisha Mut’a na Ibn Zubeir alikuwa anaikataza basi nikaeleza hilo kwa Jabir.”

Akasema:”Tulifanya Mut’a pamoja na Mtume wa Allah(s.aw.w) na alipotawala ‘Umar akasema: “Hakika Allah (s.w.t) anahalaisha kwa Mtume wake anayoyataka, basi timizeni Hijja na Umra na acheni kuoa hawa wanawake, sitoletewa mwanamme aliyeoza mwanamke kwa mwanamme isipokuwa nitampiga kwa mawe.”[231]

Na katika Sahih Tirmidhi kutoka kwa 'Abdallah bin 'Umar aliulizwa na mtu kutoka katika watu wa Sham juu ya Mut'a ya wanawake, akasema: "Ni halali", akasema: "Hakika baba yako alikwishaikataza." Ibn 'Umar akasema: "Unaonaje kama baba yangu amekataza na Mtume(s.a.w.w) ameifanya, utaacha Sunnah na kufuata kauli ya baba yangu?"[232]

Vile vile katika Sahih Muslim kumepokewa: "Kisha wakataja Mut'a, akasema kweli tulifanya Mut'a wakati wa Mtume wa Allah(s.a.w.w) , Abubakr na 'Umar."[233]

Na imekuwa mashuhuri kwa hibril-ummah 'Abdallah bin 'Abbas (r.a.) kwa rai yake kuwa Mut'a haikufutwa kama anavyopokea hayo Al- Zamakh'shariy katika Tafsiri yake Al-Kashaaf, ambapo ananukuu kutoka kwa Ibni 'Abbas kwamba Ayah ya Mut'a ni katika Muhkamaati, na vile vile katika Sahih Bukhari kuna yanayotilia mkazo hayo.

Amesema: "Nilimsikia Ibn 'Abbas anaulizwa kuhusu mtumwa wake akamwambia: 'hakika hiyo ni katika hali ngumu na wanawake wakiwa ni wachache au mfano wa hayo?’. Ibn Abbas akasema: “Ndiyo.” [234] 9 Pamoja na uwazi wa dalili hizo ni kama vile uwazi wa jua katikati ya mchana kuhusu kuendelea uhalali wa ndoa ya Mut’a.

Watu wengi katika Ahl as-Sunnah wako kinyume na hayo, lakini Ayah ambayo ni maalumu katika ndoa hii wanadai kuwa imefutwa na wamehitilafiana kuhusu Ayah iliyo ifuta, kati yao wanasema imefutwa na Ayah iliyopo katika Qur'an, na kati yao wanasema iliyofuta ni riwayah zilizopo kati ya Hadith. Tunajibu rai zote mbili kwa Hadith zilizothibiti ambazo zimetangulia, na ambazo zinaonyesha kufariki kwa Mtume(s.a.w.w) bila ya kukataza, na wale waliosema iliyofuta ni Ayah katika Qur'an nayo ni:

وَالَّذِينَ هُمْ لِفُرُوجِهِمْ حَافِظُونَ ﴿٥﴾ إِلَّا عَلَىٰ أَزْوَاجِهِمْ أَوْ مَا مَلَكَتْ أَيْمَانُهُمْ فَإِنَّهُمْ غَيْرُ مَلُومِينَ ﴿٦﴾

"Na wale ambao wanahifadhi tupu zao isipokuwa kwa wake zao au iliyowamiliki mikono yao ya kuume .”(Al-Mu’minun 23:5-6).

Inatosha kujibu rai yao hii kwa kutazama katika Ayah hii ambayo wanadai kuwa imefuta Ayah ya Mut'a, Ayah hii ni Makki (yaani imeshuka Makkah) na Ayah ya Mut'a ni Madani (yaani imeshuka Madina) na hukumu ya kisheria ya ndoa ya Mut'a ni madani (yaani imeshuka baada ya Ayah ya (na ambao wanahifadhi tupu zao...) na Ayah iliyotangulia haifuti inayokuja baada yake.

Ama aliyesema iliyofuta ni Hadith zilizopokewa kwa Mtume(s.a.w.w) , hakika Hadith hizo wanazozidai kuwa zimefuta, zinapingana zenyewe kwa zenyewe, baadhi yake zinasema imefutwa katika Khaibar na nyingine katika Autasi, ya tatu inasema ni katika siku ya Fath Makkah, na ya nne katika vita vya Tabuk na ya tano ni katika Umrah ya Qadhaa, ya sita ni katika Hajjat tul-Wida'a.

Kugongana na kupingana kwa riwayah hizo sio kwengine ila ni kuonyesha dalili ya kutokuwa ni Sahih, hayo ni pamoja na kuongezea kuwa riwayah hizo. Haziepukani na kuwa kwake ni Hadith za Ahaad, ambazo hazifai kuwa ni zenye kufuta hukumu ambayo imeletwa na Qur'an, na Shariah yake imethibiti kwa kongamano la Waislamu wote, kwa sababu Naasikhi haipatikani kwa habari ya mtu mmoja kwa ijmai, na Ayah haifutwi isipokuwa na Ayah kwa dalili ya kauli ya Allah (s.w.t):

مَا نَنسَخْ مِنْ آيَةٍ أَوْ نُنسِهَا نَأْتِ بِخَيْرٍ مِّنْهَا أَوْ مِثْلِهَا ﴿١٠٦﴾

"Hatufuti Ayah au kuisahaulisha isipokuwa tutaleta iliyo bora zaidi au mfano wake .”(Al-Baqarah 02:106)

Na ambacho kinaweza kuwa ni kisingizio cha ijtihad ya 'Umar katika kuharamisha ndoa ya Mut'a ni kwamba, mmoja wa Waislamu jina lake ni 'Amr bin Harith alitumia vibaya Shariah hii, hivyo akachokoza hasira za 'Umar na ikampelekea kuharamisha huku. Na dalili kuhusu haya ni riwayah ambayo ameipokea Muslim katika Sahih yake kutoka kwa Ja'abir: "Tulikuwa tunafanya mut'a kwa kutoa kiasi cha tende na unga wakati wa Mtume(s.a.w.w) na Abubakr na Umar, mpaka alipokataza kutokana na jambo la 'Amr bin Hurayth.[235]

Na ameitoa Tabarani na Tha'alabi katika tafsiri zao kwa isnad ya Al- Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) amesema: "Kama asingekataza 'Umar Mut’a, basi asingezini isipokuwa mwovu.”[236]

Na katika riwayah nyingine isipokuwa wachache.

Baada ya riwayah zote hizi ambazo zinathibitisha hukumu ya ndoa ya Mut'a, na Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) kutoikataza, na kubaki kwake halali hadi alipoharamisha 'Umar wakati wa ukhalifa wake, hatupati ufumbuzi wa tatizo hili, isipokuwa 'Umar amefanya ijtihad kwa rai yake kwa ajili ya maslahi aliyoyaona - kwa mtazamo wake - kwa Waislamu katika wakati wake na siku zake, yaliyo sababisha kuzuia kufanya Mut'a.

Kuzuia huko ni kwa kijamii na wala sio kwa kidini kwa ajili ya maslahi ya muda, kwa sababu 'Umar ana cheo kikubwa na alikuwa na daraja kitawala, hawezi kuharamisha alichokihalalisha Allah (s.w.t) au kuingiza kitu katika dini naye anajua kuwa halali ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni halali hadi siku ya Qiyamah, na haramu ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) ni haramu hadi siku ya Qiyamah.

Hivyo ni lazima makusudio yake ya kukataza yawe ya muda na ni kuharamisha kwa kijamii na wala siyo kwa kidini. Na msimamo wake huu mkali katika jambo la ndoa ya Mut'a sio wa kwanza katika aina yake kwani amejulikana kwa ukali na ugumu katika mambo yake yote. Anafanya ijtihad katika hilo kwa kutaka kupata maslahi bora zaidi - kwa mtazamo wake - kwa ajili ya Uislamu na kusimamisha Shariah. Na miongoni mwa mifano katika ijtihad ya 'Umar katika hukumu na ukali wake, ni amri yake kwa Waislamu kusali Sala ya Ramadhani (tarawih) katika jamaa baada ya kuwa inasaliwa furada (mmoja mmoja) wakati wa Mtume wa Allah(s.a.w.w) .

Kutoka kwa Abu Huraira: "Hakika Mtume wa Allah (s.a.w.w.) amesema mwenye kusali Sunnah ya Ramadhani kwa imani na kutaka thawabu anasamehewa yaliyo tangulia katika dhambi zake." Ibnu Shihab amesema: "Mtume wa Allah(s.a.w.w) amefariki na watu wanafanya hivyo, kisha mambo yalikuwa vivyo hivyo katika zama za Abubakr na mwanzo wa zama za 'Umar (r.a.)."

Akasema (Ibn Shihab): "Nilitoka pamoja na 'Umar Al-Khattab usiku wa mwezi wa Ramadhani kwenda msikitini basi tukakuta watu wametapakaa na wametawanyika, kila mtu anasali peke yake na mtu anasali na kundi linasali nyuma yake, 'Umar akasema mimi naona kama nitawakusanya hawa kwa msomaji mmoja ingekuwa ni bora.

Kisha akaazimia, akawakusanya kwa 'Ubay bin Ka'ab, kisha nilitoka pamoja naye usiku mwingine na watu wanasali kwa sala ya msomaji wao, 'Umar akasema: "Bida'a nzuri ni hii na wale wanaolala (wakasali usiku) ni bora kuliko wanaoisali (sasa), amekusudia mwisho wa usiku na watu walikuwa wanasali mwanzo wa usiku.”[237]

Vile vile amefanya ijtihadi katika Sunnah hiyo ambayo imeitwa sala ya tarawih kwa kuongeza idadi ya raka'a zake hadi kufikia ishirini. Kutoka kwa 'Abdurahman kwamba amempa habari kwamba yeye alimwuliza 'Aisha Sala ya Mtume wa Allah(s.a.w.w) ilikuwaje katika mwezi wa Ramadhani?" Akasema: "Mtume wa Allah(s.a.w.w) hakuwa anazidisha katika Ramadhani wala katika mwezi mwingine zaidi ya raka'a kumi na moja."[238]

Lakini baadhi ya walioishi wakati wa khalifa na walio kuja baada yake baadhi ya muhadithin wajinga, waliona ni jambo kubwa mno kuwa ameharamisha alichokihalalisha Allah (s.w.t) na wakalazimika kutoa kisingizio kwa ajili ya hilo. Hivyo hawakupata isipokuwa madai ya nasikh kutoka kwa Nabii baada ya kuhalalishwa, basi wakagongana mgongano huo na kauli zao zikapingana mpingano huo.

Tazama riwayah ifuatayo ili uone upeo wa mgongano na mgawanyiko ambao tunauzungumzia, na mshangao ni kwamba wazushi wa riwayah hiyo wameinasibisha kwa Al-Imam ‘Ali ibn Abi Talib(a.s) na watoto wake.

Kutoka kwa Zuhri kutoka kwa Hassan na 'Abdillah watoto wa Muhammad bin 'Ali kutoka kwa baba yao: Hakika Al-Imam 'Ali ibn Abi Talib(a.s) aliambiwa kuwa Ibn 'Abbas haoni ubaya wa Mut'a ya wanawake, akasema: 'Hakika Mtume wa Allah(s.a.w.w) ameikataza siku ya Khaibar, pamoja na nyama ya punda wa nyumbani', na baadhi ya watu wakasema na kama atafanya hila hadi akafanya Mut'a basi ndoa itakuwa ni batil na baadhi yao wamesema: "Ndoa inajuzu na sharti litakuwa batili."[239]

Kama hawa wangefahamu sababu ya khalifa kukataza Mut'a hilo lingewatosha kutokana na mgawanyiko na kutokuendelea.

Hakika mtazamo wa ndoa ya Mut'a uliotangulia ulikuwa ni kwa pande mbili; kidini na kihistoria. Ama mtazamo katika upande wa tabia ya kijamii kuhalalishwa kwake kumekuja kuwa ni rehema kwa wanaadamu na ruhusa kwa walio wengi, na hasa wanaosafiri kwa kutafuta elimu au biashara au wanaopigana jihadi au wanajeshi pamoja na kushindwa kwao kuoa ndoa ya daima, kwa vile mara nyingi kuna vipengele na vitu ambavyo haviendani na hali ya wasafiri, hasa ambao wako katika umri wa ujana na mchemko wa shahawa.

Kwani hali yao haiepukani na mambo mawili, ima subira na kubana nafsi ambako kunasababisha matatizo ambayo yanaleta maradhi ya kudumu na magonjwa ya kinafsi yenye kuangamiza, na mengineyo katika madhara ambayo hayafichikani kwa yeyote, na ima kutumbukia katika zinaa ambayo imejaza dunia kwa ufisadi na madhara. Na imepokewa kutoka kwa Ibn 'Abbas kuhusu suala hilo; " Mut'a haikuwa isipokuwa ni rehema ya Allah (s.w.t) ameuhurumia ‘Ummah wa Muhammed na kama sio kukataza kwake (yaani ‘Umar) asingezini isipokuwa mwovu.”[240]

Na katika yanayotia mkazo dharura ya kitabia na kijamii kwa kuhalalisha aina hii ya ndoa ya muda, ni ambayo baadhi ya Waislamu wametoa Fatwa katika wakati ambao tunao kwa kuruhusu ndoa ya aina nyingine inayomrahisishia msafiri peke yake kutatua matatizo yake katika hali ya kutoweza kuoa ndoa ya daima, na sifa ya ndoa hii ni ya muda kwa upande wa wanaume na ni ya daima kwa upande wa wanawake. Na aliyo kusudia mume katika nafsi yake bila ya yeyote kujua unapomalizika muda, anamshitusha mke wake masikini kwa kumpa talaka.

Hivyo aina hii ya ndoa wameipa jina la "Ndoa kwa nia ya talaka (kuachika)," pamoja na kutambua wale waliozua kuwa huo ni uongo kwa mke na ni udanganyifu na hakuna dalili juu ya hilo katika Kitabu wala Sunnah ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) lakini wao wanafanya kwa hoja ya kuwa madhara yake yatabaki yamefichikana kuliko ufisadi wa zinaa. Yote ni kwa kuwa wao wameamini kubatilika kwa ndoa ya Mut'a ambao uhalali wake umekuja katika Kitabu kitukufu na Sunnah za Mtume na kwa kufanya hivyo watakuwa wamebadilisha bida'a walioizua na hukumu ya Allah (s.w.t). "Je mnabadilisha ambacho ni duni kwa kile kilicho bora." Fala haula wala Quwata illa billahi.

Mut'atul Hajj

Mtume amekwisha ifundisha na akaamuru kutokana na kauli ya Allah (s.w.t) Mtukufu: “Basi atakayefanya umrah ya hijja, hiyo ni kwa ambaye familia yake haiko karibu na Msikiti Mtakatifu wa Makkah.” (Al-Baqarah 02:196)

Na makusudio ya hayo ni 'Umrah katika miezi ya hijja kabla ya hijja, nayo ni faradhi kwa ambaye familia yake iko mbali na Makkah. Na imeitwa Tamattu ya hijja kwa yale yaliyomo humo katika kujifurahisha, (yaani raha ya kuhalalishiwa makatazo ya Ihraam katika muda uliopo baina ya Ihraam mbili - Ihraam ya umrah Tamattu na Ihraam ya hijja. Na hayo ni ambayo 'Umar aliyachukia pia, na akayakataza pamoja na kuwa Mtume(s.a.w.w) alifariki bila ya kukataza.

Kutoka kwa Sa'id bin Mussayib amesema: "Ali(a.s) alikhitilafiana na 'Uthman na wao wako katika kuhirimia 'Umrah Tamattu. 'Ali(a.s) akasema: 'Hataki isipokuwa kukataza jambo alilolifanya Nabii(s.a.w.w) .' 'Ali(a.s) alipoona hivyo akahirimia zote mbili."[241]

Kutoka kwa Al-Hakim amesema: "Niliwaona 'Ali(a.s) na 'Uthman , na (huku) 'Uthman anakataza Mut'a na kuunganisha baina yake, 'Ali(a.s) alipoona akapaza sauti kwa vyote viwili: " Labayka bi umrati wa hajjati. " Akasema: 'Sikuwa ni mwenye kuacha Sunnah ya Nabii kwa kauli ya yeyote.”[242]

Ama udhr wa 'Uthman katika rai yake hiyo ni kwa kuwa yeye alikubali sharti kabla ya kupewa bay'a ya kuwa khalifa, Abdulrahman bin 'Auf alitoa sharti kwa wosia kutoka kwa 'Umar, ahukumu kwa Kitabu cha Allah (s.w.t)

Sunnah za Nabii wake na kwa mwenendo wa masheikh wawili kama ilivyo tangulia katika sehemu iliyo tangulia. Na imepokewa kwa tawatur kauli ya 'Umar: "Mut'a mbili zilizo kuwepo wakati wa Mtume wa Allah(s.a.w.w) mimi nazikataza” [243] 18 na anakusudia kwa kauli yako hiyo Mut’a ya wanawake na Mu’ta ya Hijja.

Na maneno ya 'Umar yanadhihirisha uamuzi wa hukumu hizo ni wake,na wala sio wa mwengine, kwani yeye anakiri kuwa Mut'a mbili zilizokuwa katika wakati wa Nabii(s.a.w.w) .

Na hakunasibisha kukataza kwake kwa Mtume bali amekataza yeye mwenyewe kwa kauli yake "na mimi nakataza" na Allah (s.w.t) amrehemu aliyesema kuhusu Hadith ya mwisho kuhusu 'Umar "Tumekubali ushahidi wake lakini hatujakubali kuharamisha kwake."

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA

SEHEMU YA SITA

TAQIYYAH

Taqiyyah ni mwanadamu kuficha ukweli wa imani yake, ili kujihifadhi katika sehemu za hatari anapohisi kuwa kuna hatari kwa nafsi yake au mali yake, kwa sababu ya kutangaza itikadi (imani) yake au kujidhihirisha nayo. Na kumepatikana baadhi ya watu wanaotuhumu Shi'a kwa itikadi (imani) yao ya Taqiyyah kwa ujahili wao wa kutojua maana yake, nafasi yake na makusudio yake. Na kama wangefanya uchunguzi katika jambo (hili) na kufahamu hukumu, wangejua kuwa Taqiyyah ambayo wanaisema Shi'a haiwahusu wao tu, wala sio wao peke yao wanaosema hivyo, bali ni jambo la dharura la kiakili.

Matakwa ya binadamu na Shariah ya Kiislamu na kila mwanadamu analazimika kutetea nafsi yake na kuhifadhi maisha yake, navyo ni vitu vitukufu mno kwake na anavyo vipenda zaidi. Ni kweli wakati mwingine inakuwa rahisi kuvitoa katika njia ya utukufu na kuhifadhi heshima na kulinda haki.

Lakini katika yasiyokuwa makusudio haya na malengo matukufu, kufanya israf kwayo na kujitumbukiza katika sehemu za hatari ni ujinga na upumbavu, akili hairidhii wala Shariah. Na Uislamu umemruhusu Mwislamu katika sehemu za hofu, kuficha haki na kuifanyia kazi kwa siri mpaka dola ya haki inusurike katika dola ya batili. Kulingana na kauli yake Allah (s.w.t):

"isipokuwa mkiogopa kwao madhara .”(Ali-Imran 03:28)

Na kauli yake:

"isipokuwa aliye lazimishwa na moyo wake umetulizana kwa imani ". (An-Nahl 16:106).

Na kisa cha 'Ammar na wazazi wake na mateso ya washirikina kwao na baadhi ya Masahaba kwa kuwataka wakubali ushirikina na kudhihirisha kwao ukafiri ni mashuhuri. Na katika kufanya Taqiyyah kuna hukumu tatu:-

1. Wajibu: na hiyo ni ikiwa kuiacha kunasababisha kuangamia nafsi bila ya faida.

2. Ruhusa: ikiwa kuiacha kwake na kudhihirisha haki ni kuipa haki nguvu basi ana hiari kuitoa mhanga nafsi yake.

3. Haramu: na hiyo ni ikiwa kufanya Taqiyyah kunasababisha kueneza batili na kudhalilisha haki na kuihuisha dhulma na ujeuri.

Na ni maarufu kwa wafuasi wa madhehebu ya Shi'a Ithna-'Ashariyyah, na Maimamu wao wamepata balaa na kila aina ya dhiki katika uhuru wao katika zama zote ambazo madhehebu yoyote au 'Ummah wowote ule haujapata. Hivyo walilazimika katika wakati mwingi wa zama zao kutumia Taqiyyah kwa kuwaficha wanao wakhalifu kwa yale ambayo yangeleta madhara katika dini na dunia, na kwa sababu hii wamejulikana sana kwa Taqiyyah kuliko wasiokuwa wao.

Mwisho

Tumekwisha bainisha katika sehemu za utafiti huu yaliyo muhimu zaidi, ambayo kumetokea hitilafu baina ya Sunni na Shi'a, na tukabainisha njia ya sawa humo kwa kueleza dalili nyingi na hoja ambazo nyingine zimechukuliwa katika Sahih Bukhari.

Nayo ni ambayo inazingatiwa kuwa ni Kitabu muhimu cha marejeo na kinachoaminika kwa Ahl as-Sunnah baada ya Kitabu cha Allah (s.w.t), na haikuwa kuandika kwetu kurasa hizi kwa njia hii ambayo pengine inawaumiza baadhi ya watu, isipokuwa ni wasila (njia).

Tumelazimika kuitumia baada ya waongo kuvuka mpaka kwa upeo wa uongo na upotovu; wamekwisha turushia (sisi Mashi'a) tuhuma, na uongo mbaya zaidi miongoni mwa tuhuma hizo ni ushirikina, umajusi, unasara na uyahudi; mpaka wametoa Fatwa juu ya ukafiri wetu.

Na Mawahhabi wamechukua jukumu la mwelekeo huu mwovu ambao umesababisha kuzuka fitina hii kubwa baina ya Waislamu, na kuwapoteza wasiojua miongoni mwao kwa kutumia kila njia isiyokuwa ya kisheria miongoni mwa uongo na udanganyifu katika mambo ili kufikia malengo yao ya kutenganisha 'Ummah na kuwaridhisha mabwana zao ambao kumewakasirisha kuona Uislamu unameremeta na kuamka tena kutoka katika usingizi wake wa upotofu.

Vinginevyo kwa nini hatukuona aina hii ya fitina inakua na kumea isipokuwa baada ya kufaulu kwa mapinduzi matukufu ya Kiislamu nchini Iran? Mapinduzi hayo ambayo yametikisa utawala wa madhalimu na madikteta na ambayo Waislamu wote walipata matumaini, pamoja na tofauti zao za madhehebu. Baada ya kheri na matumaini ya kuchukua hatamu za haraka, katika njia ya kuwarejesha Waislamu katika nguvu na utukufu wao baada ya kuwa dhalili, 'Ummah zinageuzwa geuzwa kama chakula kinavyogeuzwa geuzwa juu ya sahani.

Maadui wa Uislamu walipokosa njia yenye mafanikio katika kuwaweka mbali Waislamu na mapinduzi haya, wamejaribu kutia shaka katika itikadi ya watu wake baada ya kushindwa vibaya sana kuvunjika hayo kwa Helikopta zao ambazo Allah (s.w.t) aliuwezesha mchanga wa jangwani kuziharibu na kuzisambaratisha, na kuharibu mbinu zao katika vita vyao ambavyo walipanga kupitia mamluki wao mtiifu ambaye walimvalisha vazi la utaifa hakuvuna isipokuwa hasara na fedheha katika mwito wake mwovu wa utaifa.

Amesema Sheikh mwanajihadi Abdulhamid Kishki, katika mazungumzo yake ya kujibu kauli ya mwovu huyo mwenye kuajiriwa: "Kwamba watu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wao ni Wafursi tu, hawajui Uislam wala Qur'an ambayo imeteremka kwa Waarabu na lugha yao, hivyo wao wanajua zaidi kuliko watu wengine wasio kuwa Waarabu kwa kusema kuwa Shi'a wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni Waislamu wenye kumpwekesha Allah (s.w.t) na Uislamu wao umekuwa mzuri tangu walipoingia katika Uislamu katika zama za 'Umar."[244]

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alishabashiri tangu karne ya kumi na nne, watu hawa ambao walipokea Uislamu na kuupeleka katika taifa hili la Kiislamu lililopo sasa, katika Hadith ambayo ameitoa Bukhari katika Sahih yake.

Kutoka kwa Thaur kutoka kwa Abu Huraira amesema: "Tulikuwa tumekaa kwa Mtume(s.a.w.w) , basi akateremshiwa Surah al-Jumuah (na wengine miongoni mwao bado hawajajiunga nao) akasema: 'Nilisema nani hawa ewe Mtume wa Allah(s.a.w.w) hakumjibu hadi akauliza mara tatu na alikuwepo pamoja nasi Salman Al-Farsi akaweka mkono wake juu ya Salman, kisha akasema kama imani ingekuwa kwenye sayari basi wangeifikia wanaume au mwanamume katika hawa."[245]

Na Allah (s.w.t) ameashiria katika Kitabu chake kitukufu juu ya watu hawa kwa kauli Yake: "Ninyi ndiyo mnalinganiwa ili mtoe katika njia ya Allah (s.w.t) miongoni mwenu kuna wanaofanya ubakhili na anaefanya ubakhili hakika anafanya ubakhili kwa nafsi yake na Allah (s.w.t) ni tajiri na nyinyi ni mafakiri na kama mtakataa ataleta watu wengine, kisha hawatakuwa mfano wenu."[246]

Kutoka kwa Abu Huraira: "Hakika Mtume(s.a.w.w) alisoma Ayah hii (na kama mtakataa ataleta watu wengine kisha hawatakuwa mfano wenu)." Wakasema: "Ewe Mtume wa Allah(s.a.w.w) nani hao ambao kama tutakataa wataletwa baada yetu kisha hawatakuwa mfano wetu?" Basi akapiga juu ya paja la Salman kisha akasema: "Huyu na watu wake na kama dini ingekuwa katika sayari basi wangeifikia wanaume kutoka Farsi (Jamhuri ya Kiislamu ya Iran)."[247]

Lakini maadui wa Uislamu hawakukata tamaa baada ya kushindwa kwao katika uwanja wa mapambano na bado wanazo nafasi nyingine wanazopigana na huu ndiyo Uwahhabi umeshika nafasi ile ile.

Lakini kwa mara hii ni kwa silaha tofauti, wameshawavalisha askari wao vazi la Uislamu huenda ukawa unang'ara zaidi kuliko vazi la utaifa ambao umegeuka kuwa majivu katika upande wao wa mashariki.

Hila mpya kwa masikitiko makubwa imewakumba baadhi ya watu wasiojua, na wengi wametumbukia katika mtego wa fitina hii, ambayo hawajui itawapeleka wapi! "siku ambayo haitafaa mali wala watoto isipokuwa yule atakaye mwendea Allah kwa moyo safi."

Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) alishatahadharisha hadhari kubwa kutokutumbukia kwenye moto wa fitina hii, kama wangekuwa wanajua Sunnah zake katika Hadith nyingi ambazo amebainisha humo hata wale watakao isababisha kama ilivyo katika Hadith aliyoitoa Bukhari katika Sahih kutoka kwa Naf'i kutoka kwa Ibn 'Umar amesema:”

Mtume(s.a.w.w) alisema: "Ewe Allah! Tubariki sisi katika Sham. Ewe Allah! Tubariki sisi katika Yemen." Wakasema: "Na katika Najd?" Akasema: "Ewe Allah! Tubariki sisi katika Sham. Ewe Allah! Tubariki sisi katika Yemen." Wakasema: "Ewe Mtume wa Allah! Na katika Najd?" Alisema mara tatu: "Huko kuna tetemeko na fitina na huko kutachomoza upembe wa Shetani.”[248]

Na kundi lililokusudiwa katika Hadith iliyotangulia hatuoni isipokuwa linaafikiana na kundi la Mawahhabi ambalo muasisi wake ni Muhammad bin Abdul-Wahhab amezaliwa katika moja ya vijiji vya Najd kinachoitwa Uyainah. Kundi hili ambalo limekuwa ni tezi la kansa katika jamii ya Kiislamu na kukua kwake na kuendelea kwa juhudi zake za kubomoa katika njia ya kurejea Uislamu mtukufu; kwa hakika si lingine isipokuwa ni fitina nyuma yake umesimama ukoloni mwovu kama ambavyo historia yake inaonyesha hivyo na unalenga kwenye:-

1. Kubomoa shakhsiyyati (watu muhimu) za kidini kwa kuzuia watu kuwa karibu yao na kuwa karibu na athari na misingi yao.

2. Kutoa Uislamu kwa sura ya dini kavu isiyo na maendeleo ambayo haikubali kutekelezeka katika zama mbali mbali.

3. Kutengeneza vikundi na hitilafu katika safu za Waislamu kwa kuzuia umoja na udugu wao.

Na wameichukulia Tawhid kuwa ni uwanja wa malengo yao maovu kwa kutuhumu madhebu mengine kwa ushirikina kwa kudai kwamba tawassul kwa Manabii na watu wema ni chanzo cha ushirikina, wakapinga kwa hilo yaliyo pokewa kutoka kwa Mtume wa Allah (s.a.w.w.) kwa tawatur kwa kuruhusu hilo.

Na yanatutosha aliyoyatoa Bukhari katika Sahih yake juu Tawassul ya 'Umar kwa 'Abbas. Kutoka kwa Anas: "Hakika 'Umar al-Khattab alikuwa wakipatwa na ukame akimwomba 'Abbas bin 'Abdul-Muttalib awaombee mvua akasema: "

Ewe Allah (s.w.t) hakika sisi tulikuwa tuna-tawasali kwako kupitia kwa Nabii(s.a.w.w) wetu na unatunyesheleza, na hakika sisi tuna-tawasali kwako kupitia kwa Ami wa Nabii wetu basi tunyesheleze akasema: 'Basi wanateremshiwa mvua.'"[249]

Bali inatosha kwa kuwajibu Mawahhabi kwa kauli yake alama zao[250] ni kunyoa (wanawake vipara). Kama alivyopokea hayo Bukhari katika Sahih yake, hakika hakufanya hayo yeyote miongoni mwa wazushi isipokuwa wao kama ilivyo julikana hivyo katika historia yao.[251]

Na katika Hadith nyingine Nabii alibainisha maelekezo yake ya kinabii kwa watu katika yaliyo " wajib kuyafanya wakati zinapotokea fitna " kama hizi; anasema watu walikuwa wanamwuliza Mtume wa Allah(s.a.w.w) kuhusu kheri na nilikuwa namwuliza kuhusu shari kwa kuogopa isije ikanifika.

Nikasema:"Ewe Mtume wa Allah(s.a.w.w) ! Hakika sisi tulikuwa katika ujahili (ujinga) na shari, Allah (s.w.t) akatuletea kheri hii je baada ya kheri hii kuna shari?"

Akasema: "Ndiyo!"

Nikasema:"Je baada ya shari hiyo kuna kheri?"

Akasema: "Ndiyo na kuna dakhani (wanaoongoza bila ya uongofu)."

Nikasema:"Je dakhani ni nini?"

Akasema: "Ni watu wanaoongoza bila ya uongofu, baadhi yao utawajua na baadhi yao hutawajua."

Nikasema:"Je! baada ya kheri hiyo kuna shari?"

Akasema: "Ndiyo, wenye kulingania katika milango ya Jahannam atakaye waitikia watamtupia humo."

Nikasema:"Ewe Mtume wa Allah (s.a.w.w.)! Tupe sifa zao."

Akasema: "Wao ni katika kabila letu, wanazungumza lugha yetu."

Nikasema:"Unaniamuru nini kama hayo yatanifikia?"

Akasema: "Jilazimishe na jamaa ya Waislamu na Imam wao.

Nikasema:"Na kama hawatakuwa na jamaa wala Imam?"

Akasema: "Basi jitenge na kundi hilo lote hata kama ni kung'ang'ania shina la mti hadi mauti yakufikie na wewe uko hapo."[252]

Na Hadith ya hapo juu inabainisha wazi wajibu wa kujilazimisha kushikamana na jamaa ya Kiislamu na Imam wao, na kwamba katika hali ya mkanganyiko wa mambo kutofahamika na kutowezekana kujua uhakika wake.

Basi maelezo ya Nabii yanatuamuru kunyamaza na vile vile Hadith inabainisha kuwa walinganiaji katika milango ya Jahannam atakaye waitikia watamtupia humo sio katika Waajemi bali ni katika Waarabu, na haya yanatilia mkazo yaliokuja katika Hadith iliyotangulia (kutoka Najd).

Jambo hili lazima limfanye Mwislamu awe katika hali ya uangalifu sana na tahadhari kwa kufuata mwendo unao mpelekea kwenye usalama katika Sunnah ya Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) , na hasa pamoja na kuwepo makundi mengi ambayo idadi yake ni sabini na tatu, kila moja linadai kuwa kunukuu kwake Sunnah za Nabii(s.a.w.w) ni sahih na amekwishatupa habari ambaye hatamki kwa matamanio yake kuwa kundi moja tu ndilo Sahihi na mengine sio Sahih.

Hivi ndivyo zilivyo patikana tofauti na Ikhtilaf hadi Waislamu wakawa wanatahayari na wenye kushangaa kwa yote yanayotendeka pembezoni mwao, miongoni mwa zogo hili kubwa na fitina kubwa.

Na mimi sishangai tahayari hii na mshangao huu, kwani Nabii wa Uislam amekwisha ashiria kuhusu jambo hili kwa kauli yake: "Uislamu umeanza katika hali ya ugeni na utarejea kuwa mgeni kama ulivyoanza." Je, ugeni hauko katika Waislamu kumpiga vita yule ambaye ni Mwislamu halisi? Je, sio ugeni! Na mshangao zaidi kwa watoa mawaidha kusimama na vilemba vyao juu ya mimbar na kupaaza sauti na hali wakiwakufurisha ambao ni Waislamu halisi?

Ewe Mtume wa Allah(s.a.w.w) umesema kweli na hawa ndio Waislamu wanawapiga vita na kuwakufurisha Mashi'a (wafuasi wako) ambao wameshikamana na Sunnah zako kupitia katika njia ya viumbe watoharifu zaidi (Ahlul Bayt(a.s) baada yako. Hakika wao wanampiga vita huyu mwenye kurejea na watu wake wamekuwa wageni katika kundi la Waislamu na wamepotoshwa na kupelekwa katika njia ya wale ulio tahadharisha kuwa ndiyo machomozo ya upembe wa Shetani, tetemeko na fitina. Na ulishasema kuwa kundi katika 'Ummah wangu halitaacha kudhihirisha haki, hata wadhuru atakaye wakhalifu mpaka itakapokuja amri ya Allah (s.w.t.) kulingana na kauli ya Allah (s.w.t.):

لَقَدْ جِئْنَاكُم بِالْحَقِّ وَلَـٰكِنَّ أَكْثَرَكُمْ لِلْحَقِّ كَارِهُونَ ﴿٧٨﴾

"Tumekwisha wajieni kwa haki, lakini wengi wenu wanaichukia haki.”(Az-Zukhruf 43:78)

Na umekwisha mbashiri Mahdi wa Aali Muhammad mjukuu wako na wasii wako, Imam wa kumi na mbili (Al Imam Muhammad Mahdi Sahib az-Zamaan(a.s) ambaye atajaza dunia haki na uadilifu, baada ya kujazwa dhulma na jawr (ujeuri) na umetuamuru kuelekea kwake hata kama ni kwa kutembea juu ya theluji kwa kauli yako: "Hakika sisi ni Ahlul-Bayt; Allah (s.w.t) ametuchagulia akhera dhidi ya dunia, na hakika watu wa nyumba yangu watapata baada yangu tabu, shida na kufukuzwa katika nchi, mpaka watakuja watu, (kutoka hapa akaashiria kwa mkono wake upande wa mashariki) watu wenye bendera nyeusi, wataombwa haki, lakini hawataitoa watapigana, basi watanusurika na watapewa wayatakayo hawatakubal,i hadi wampe mwanamme katika watu wangu. Basi ataijaza dunia uadilifu kama ilivyojazwa dhuluma, basi atakaye fikiwa na huyo amwendee, hata kama ni kwa kutembea juu ya theluji.[253]

Mwisho wa ulingano wetu tunamwomba Allah (s.w.t), atuja'alie kuwa miongoni mwa ambao wanasikiliza kauli, wakafuata mazuri yake. Na shukurani njema ni za Allah (s.w.t) Mola wa viumbe, sala na salamu zimwendee Bwana wetu Mtume Muhammad Mustafa(s.a.w.w) na Ahlul Bayt zake watoharifu.

Wassalamu ‘alaykum wa Rahmatullahi wa Barakatuh

SHARTI YA KUCHAPA

Sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini.

MWISHO WA KITABU

YALIYOMO

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 1

KIMEANDIKWA NA: DR. ‘ASAD WAHID AL-QAASIM 1

KIMEATAFSIRIWA NA: ABDUL KARIM J. NKUSUI 1

KUHUSU MTUNGAJI 1

NENO LA MCHAPISHAJI 2

DIBAJI YA MTARJUM 3

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 4

KIMEANDIKWA NA: DR. ‘ASAD WAHID AL-QAASIM 4

KIMEATAFSIRIWA NA: ABDUL KARIM J. NKUSUI 4

NATOA ZAWADI YA KITABU HIKI 4

Je, Tunahitaji Kujifunza Namna Ya Kufikiri? 6

Dhana Nzuri Ya Moja Kwa Moja Kwa Maulamaa Walio Tangulia Mara Nyingine Inamwongoza Mtafiti Kwenye Upotovu 7

Wako wapi wao kati ya Maulamaa wajuzi ambao wametoa Fatwa juu ya Uislamu mzuri wa Shi’a? 8

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 9

KIMEANDIKWA NA: DR. ‘ASAD WAHID AL-QAASIM 9

KIMEATAFSIRIWA NA: ABDUL KARIM J. NKUSUI 9

UTANGULIZI 9

NI NANI SHI’A ITHNA-’ASHARIYYAH? 9

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 12

SEHEMU YA KWANZA: UIMAMU 12

Kwanza: Hoja Za Kuthibitisha Uimamu Wa Ahlul- Bayt (A.S.) 12

Hadith Ya ‘Ummu Salamah Katika Mapokezi Ya Bukhari 14

Uchunguzi Juu Ya Ayah Ya “Tat-Hiir” 16

Pili -Dalili Za Kuthibitisha Idadi Ya Maimamu Wa Ahlul Bayt (A.S.) Ni Kumi Na Mbili 18

Tatu-Hoja Za Kuthibitisha Kupewa Ukhalifa Al Imam ‘Ali Ibn Abi Talib (A.S.) 19

Kukhalifu Kwa Jamhuri Ya Waislamu Nasi (Pokezi) Za Uimamu 24

Kwanza- Baadhi Ya Masahaba Kumkataza Mtume Wa Allah (s.a.w.w) Kuandika Wosia 25

Pili- Baadhi Ya Masahaba Kukhalifu Jeshi La Usamah Na Kukosoa Kupewa Kwake Uongozi 28

Tatu -Matukio Ya Saqifah Na Bay’ia Ya Abubakr 29

Hasira (Ghadhabu) Ya Bibi Fatimah Az-Zahra(A.S) 32

Je, Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) Alidokeza Juu Ya Abubakr Kupewa Ukhalifa? 35

Je, Bi.Fatimah Az-Zahra (A.S.) Alikufa Kifo Cha Kijahiliyyah (Kikafiri)? 35

Nne: ‘Umar Kupewa Ukhalifa Na Bay’ia Yake 37

Tano-Shura Na Bayi’a Ya ‘Uthman Bin ‘Affan 38

Kuuliwa Kwa ‘Uthman Bin ‘Affan 39

Bai’a Ya Al-Imam ‘Ali Ibn Abi Talib(A.S) 41

Sita- Tukio La Jamal Na Kutoka Kwa ‘Aisha 41

Uzushi Wa ‘‘Abdallah Bin Saba’ 43

ORODHA YA WAPOKEZI WA UONGO WA SABA’100 45

MZUSHI WAKE NI SEIF BIN ‘AMRU AT-TAMIMIY ALIYEFARIKI MWAKA WA 170 HIJRIYYAH. WAPOKEZI WAKE:- 45

Saba: Vita Vya Siffin Na Uasi Wa Mu’awiyah Bin Abi Sufian 45

Nane-Kufa Shahid Kwa Al-Imam ‘Ali Ibn Abi Talib(A.S ) 48

Al Imam Hasan Ibn ‘Ali Ibn Abi Talib(a.s) Na Suluhu Ya Mu’awiyah Bin Abi Sufian 48

Tisa: Kufa Shahid Kwa Al-Imam Hasan Ibn ‘Ali Ibn Abi Talib(a.s) 49

Kumi: Thawrah (Mapambano) Ya Karbala Na Kufa Shahid Kwa Al Imam Hussein Ibn ‘Ali Ibn Abi Talib(a.s) 50

Shura Baina Ya Misingi Na Utekelezaji 53

1. Ukhalifa Wa Abubakr Ibn Abu Quhafa 54

2. Zama Za ‘Umar 54

3. Zama Za ‘Uthman Bin ‘‘Affan 54

4. Zama Za Mu’awiyah Bin Abi Sufian 54

5. Zama Za Yazid Bin Mu’awiyah Bin Abi Sufian 54

Mwisho Wa Utafiti Wa Uimamu 55

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 57

SEHEMU YA PILI 57

UADILIFU WA MASAHABA 57

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 66

SEHEMU YA TATU 66

SHI'A NA QUR'AN TUKUFU 66

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 71

SEHEMU YA NNE 71

SHI'A NA SUNNAH TUKUFU ZA NABII (S.A.W.W) 71

Kuondoa Shaka Kuhusu Uma'asum Wa Mtume Muhammad Mustafa (s.a.w.w) 72

Abu Huraira Na Wingi Wa Riwayah Zake Katika Hadith 79

Kisimamo Pamoja Na Bukhari Katika Sahih Yake 85

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 89

SEHEMU YA TANO 89

NDOA YA MUDA 89

Mut'atul Hajj 94

UKWELI WA SHIA ITHNA ASHARIYA 96

SEHEMU YA SITA 96

TAQIYYAH 96

Mwisho 96

SHARTI YA KUCHAPA 101

MWISHO WA KITABU 101

YALIYOMO 102