HADITHI THAQALAINI

HADITHI THAQALAINI0%

HADITHI THAQALAINI Mwandishi:
: Sheikh Salimu Ng'ang'amwega
Kundi: Mtume (S.A.W.W)

HADITHI THAQALAINI

Mwandishi: Sayyid Muhsin Al-Kharraaziy
: Sheikh Salimu Ng'ang'amwega
Kundi:

Matembeleo: 2994
Pakua: 1862

Maelezo zaidi:

Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 5 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 2994 / Pakua: 1862
Kiwango Kiwango Kiwango
HADITHI THAQALAINI

HADITHI THAQALAINI

Mwandishi:
Swahili

HADITHU AL-THAQALAINI

HADITHI YA VIZITO VIWILI

UTANGLIZI

KUAMBATANA NA HEKIMA YA MWENYEZI MUNGU

Baada ya hayo, jua ya kwamba hekima ya Mwenyezi Mungu inamlazimu yeye kuwaongoza watu katika kuyafikia yaliyo mema na yenye maslahi kwao, humu duniani na huko akhera, ili waweze kuupata ukamilifu unaoambatana na lengo la maumbile yao, ambao ni, kumjua Mwenyezi Mungu na kuupata ukurubifu wake.

Uongofu wake unapatikana kwa njia ya wahyi na kuviteremsha vitabu vitukufu na kwa kuwatuma manabii na marasuli na kuwateua mawasii. Huu uon-gofu umeendelea kupatikana tangu alipoumbwa Nabii Adam(a.s) na wala watu hawakuwahi kutouhitajia kamwe katika zama mojawapo, kwani akili zao hazikuyajua maslahi yao yote (yanayowafaa) ya humu duniani na huko akhera, bali daima walikuwa ni wenye kuuhitajia msaada wa Mwenyezi Mungu kwa kupitia wahyi na mitume watukufu. Nao wahyi hautengamani na Mtume bali vyote viwili ni kama mapacha, vina-shirikiana katika kuwafikishia watu uongofu wao.

Basi kila Mtume alikuwa na wahyi na kila wahyi ulikuwa na Mtume. Naam, kuteuliwe kwa mitume (manabii) na wajumbe (marasuli) kulipo khitimishwa, Kitabu kitukufu kilichokuwa kimeteremshwa na Mwenyezi Mungu kilibaki mikononi mwa wasii, kwani watu walikuwa ni wenye kukihitajia daima Kitabu hiki pamoja na mfafanuzi wa yaliyomo ndani yake, ambaye ni mwalimu na mlezi na mtakasaji.

Hili ni jambo lenye uhakika linaloungwa mkono na kila mwenye akili safi, pamoja na riwaya (hadithi) zilizo mutawatir (nyingi).

Mwenyezi Mungu (s.w.t) kwa kuonyesha mshangao kutokana na kukanusha kwa makafiri amesema:

وَكَيْفَ تَكْفُرُونَ وَأَنتُمْ تُتْلَىٰ عَلَيْكُمْ آيَاتُ اللَّـهِ وَفِيكُمْ رَسُولُهُ وَمَن يَعْتَصِم بِاللَّـهِ فَقَدْ هُدِيَ إِلَىٰ صِرَاطٍ مُّسْتَقِيمٍ ﴿١٠١﴾

"Na mnakanushaje, hali nyinyi mnasomewa aya za Mwenyezi Mungu na Mtume wake yuko pamoja nanyi? Na mwenye kushikamana Mwenyezi Mungu (sawa sawa) basi yeye amekwisha ongozwa katika njia iliyo-nyooka".( Quran, 3:101).

Yaani, mnakufuruje na kukanusha ilhali aya za Mwenyezi Mungu zasomwa mbele yenu na mjumbe (Rasuli) wake, naye yu pamojo nanyi anawapa mawa-idha na kuwakataza mabaya. Na Mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu kwa hakika atakuwa amepata uongofu bila shaka. Kwa hivyo tunaona wazi kuwa aya tukufu inatuthibitishia kuwa kufuru na upotofu havipatikani vinapokuwepo vitu viwili, navyo ni:

kwanza : Aya zinazosomwa, nazo ni Qurani tukufu.

Pili : kuwepo kwa Mtume(s.a.w.w) .

Mwenye kuvikhalifu hivi viwili basi amekwisha-potea na kutoka kwenye njia iliyonyooka, kinyume cha mwenye kushikamana na Mwenyezi Mungu kwa kuzipokea aya na kumfuata Mtume(s.a.w.w) . Basi huyo amekwishaongoka na kuipata njia iliyonyooka.

Kufuatana na msingi huu wa haki Mtume(s.a.w.w) alitaka kuubainishia umma wa kiislamu njia ya sawa ili wasipotee baada ya kufa kwake, bali waifwate njia iliyonyooka. Na hii ndio sababu hasa ya kuwaongoza katika kukifuata Kitabu cha Mwenyezi Mungu na katika kuwafuata Ahlulbait(a.s) , ili kwamba sababu za uongofu na saada yao ya dunia na akhera zidumu kuendelea. Mtume(s.a.w.w) aliwabainishia kwa njia tofauti tofauti na katika sehemu na nyakati zilizonasibiana na maudhui.

Miongoni mwazo ni; hadithuth thaqalain (Hadithi ya vizito viwili) iliyo maarufu na yenye kuafikiana ma-dhehebu ya kishia na kisunni. Mtume(s.a.w.w) kwa maneno yoliyoko kwenye hadithi hii alitaka kuuongoza umma katika mustakbali wao hadi siku ya kiyama.

HADITHU AL-THAQALAINI

Hakuna shaka kuwa hii hadithi inayopatikana kwenye vitaba vya madheheba yote inaelezea kwa uwazi kwamba Mtume(s.a.w.w) hakuupuuza umma wa kiislamu na kuuacha hivi hivi bila ya mwongozo, bali aliwaelezea cheo kitukufu cha Quran na kizazi chake kitoharifu, na kuuwajibishia umma kushika-mana navyo. Kisha akawadhaminia washikanao navyo kuwa hawatapote, na kisha akasisitizia kuwa kamwe havitatengana hadi vitakaporudi kwake huko hodhini mwa kauthar. Kwa maneno haya alibainisha wazi kabisa kutotengana na kutofarikiana kwa kizazi kutokana na Quran, na kutotengana kwa Qurani kuto-kana na kizazi chake. Kisha akauainsishia umma wa kiislamu maregeleo yao katika mambo ya kielemu na katika mambo ya kisiasa.

Haya, pamoja na kuwa hadithi haionyeshi kuwa mambo haya yanahusu zama fulani makhsusi, bali inanyesha kuwa ni wajibu unaoendelea juu ya waislamu wote katika kila pembezoni mwa ardhi na katika kila wakati na zama.

Kutokana na haya, na yatakayokuja tunatambua ya kwamba uchunguzi na kufikiria kwa makini kuihusu hadithi hii ni kitu chenye faida kubwa kwetu na kwa ndugu zetu waislamu ambako kutaondosha dhana mbaya zinazosababisha kukhitilafiana na kufarikiana.

1

HADITHI THAQALAINI

SEHEMU YA KWANZA

MATAMSHI YA HADITHI KAMA YALIVYO KUJA VITABUNI

1) KATIKA HIJJA YA MWISHO

a) "Huenda nikaitwa (na Mola wangu) nami nikajibu, nami ninaacha kati yenu viwili vizito, Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu na Aiyetukuka, ambacho ni kamba iliyonyooshwa toka binguni hadi ardhi. Na kizazi changu (ambao ni) Ahlubaiti wangu. Hakika Mjuzi wa (yote) yaliyofichika na yaliyodhahiri amenijulisha kuwa havitatengana kamwe mpaka vitakaponijia huko hodhini (mwa kauthar) basi angalieni vile mtakavyovitendea baada yangu ".[1]

b) "Hakika mimi ninaacha kati yenu ambavyo mkivichukua (na kushikamana navyo) kamwe ha mtopotea baada yangu, navyo ni vizito viwili, kimoja kati yavyo ni kikuu kuliko kinginecho".

Na katika hijja ya mwisho katika sehemu iitwayo Ghadir khum aliongeza maneno haya (kwa kusema):

c) "Basi angalieni mtakavyo vifanyia baada yangu, kwani, kamwe havitotengana hadi vitakaponija kwenye hodhi", kisha akasema, "Hakika Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu na Aliyetukuka ni Bwana wangu, nami ni bwana wa kila muumini". Kisha akaushikia mkono wa Ali na kusema "Ambaye mimi ni bwana wake, basi huyu Ali ni bwana wake ".[2]

2) KATIKA GHADIR KHUM

"Nakukumbusheni Mwenyezi Mungu katika Ahlu-baiti wangu, nakukumbusheni Mwenyezi Mungu katika Ahlubaiti wangu, nakukumbusheni Mwenyezi Mungu katika Ahlubaiti wangu ".[3]

3) KATIKA HOTUBA YA MWISHO SIKU ALIYOAGA DUNIA

Katika siku aliyoaga dunia na kurudi kwa Mola wake alisema katika hotuba yake ya mwisho:

a) "Hakika mimi ninaacha mambo mawili kati yenu, mkishikamana nayo hamtapotea kamwe baada yangu Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu Aliyetukuka, na kizazi changu (ambao ni) Ahlubaiti wangu, kwani mjuzi wa yaliyoficha na yaliyodhahiri Amenijulisha kwamba (Mambo haya mawili) hayato-tengana kamwe mpaka yatakaponijia katika hodhi (ya kauthar) kama hivi viwili - (akavishikanisha vidole vyake viwili vya shahada) - na wala sisemi kama hivi viwili (akakishikanisha kidole cha shahada na kidole cha kati) basi shikamaneni nayo (mawili) na wala msiwatangulie (Ahlubaiti wangu) msije mkapotea ".[4]

b) "Nimekwishaviacha kati yenu ambavyo mkishi-kamana navyo hamtapotea kamwe baada yangu, Kitabu cha Mwenyezi Mungu kilicho mikononi mwenu, mnakisoma asubuhi na jioni, na ndani yake kuna yale mnayokutana nayo na yale mnayodai. Kwa hivyo msishindane wala msihusudiane wala msichukiane, na kueni ndugu kama alivyokuamrisheni Mwenyezi Mungu kisha nawa usieni kizazi changu (ambao ni) Ahulbaiti wangu".[5]

c) "Basi misivitangulie (vizito viwili) msije mka-angamia na wala msivifunze kwani vina elimu zaidi kuwaliko nyinyi ".[6]

d) "Basi msiwatangulie Ahlubaiti wangu kwa kauli msije mkaangamia na wala msibaki nyuma yao msije mkapotea kwani mfano wao kati yeni ni mfano wa safina ya Nuhu(a.s) aliyeipanda aliokoka na aliye-baki nyuma (bila kungia) aliangamia. Na mfano wao kati yenu ni mfano wa mlango wa Hitta (msamaha) katika wana wa Israeli, aliyeuingia alisamehewa. Tambueni kuwa Ahlubaiti wangu ni amani kwa umma wangu, basi watakapoondoka Ahlubaiti wangu (ardhini) kitawajia umma wangu kile walichoahidiwa (yaani kiyama); Tambueni kuwa Mwenyezi Mungu Amewa-hifadhi hawa kutokana na upotofu na kuwatakasa kutokana na machafu na kuwachagua juu ya walimwengu wote. Tambueni kuwa Mwenyezi Mungu Amewajibisha kuwapenda wao (na Ameamuru kuwa wapendwe).[7]

e) "Hakika mimi ninaacha kati yenu Viwili vizito Kitabu cha Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na kizazi changu(ambao ni) Ahlubaiti wangu. Tambueni kuwa viwili hivi, ndivyo makhalifa wawili baada yangu na havitatengana kamwe, baada yangu mpaka vitakapo-nijia huko hodhini (mwa kauthar) ".[8]

f) "Hakika mimi ninaacha kati yao makhalifa wawili, Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Ahlubaiti wangu, navyo havitoachana kamwe mpake vitakapo-nijia hodhini."[9]

g) "Hakika mimi ninaacha kati yenu makhalifa wawili, Kitabu cha Mwenyezi Mungu (ambacho) ni kamba (ya Mwenyezi Mungu) iliyonyooshwa baina ya mbingu na ardhi, na kizazi changu (ambao ni) Ahlubaiti wangu, nao (makhalifa wawili) hawato-tengana kamwe hadi watokapo nijia hodhini (mwa kauthar). "[10]

h) "Kwa hakika Mjuzi wa yaliyofichika na yaliyo-dhahiri amenijulisha kuwa havitatengana kamwe mpaka vitakaponijia kwenye hodhi. Basi niliviombea haya kwa Mola wangu, kwa hivyo msivitangulie msije mkaangania na wala msibaki nyuma msije mkaangamia, na wala msiwafunze (Ahlubait wangu) kwani wao wanajua zaidi yenu. Ambaye mimi ni bwana wake basi Ali ni bwana wake. Ewe Allah mpende ampendaye (Ali) na mfanyie uadui amfamyiae uadui ."[11]

4) HUKO JUHFA

katika hotuba yake(s.a.w.w) huko Juhfa, Ghadir khum alisema;

"Je si mimi ninazitawala nafsi zenu zaidi ya mnav-yozitawala nyinyi nafsi zenu?" wakajibu "Ndiyo, ya Rasulallah" akasema "basi mimi nitawaulizeni kuhu-siana na vitu viwili (siku ya kiyama), Qurani (tukufu) na kizazi changu".[12]

SEHEMU YA NNE

MAANA YA HADITHI

Tunajifunza kutokana na hadithi hii tukufu mambo yafwatayo:

1- Mtume(s.a.w.w) aliwajulisha waislamu kifo chake.

Mtume Mtukufu(s.a.w.w) aliwajulisha waislamu kuhusu kifo chake. Hadithi nyingi zinaonyesha maana hii, kama vile kauli yake tukufu aliyoisema;

"Hakika mimi huenda nikaitwa (na Mola wangu) nami nikajibu. "

Na kauli yake:

"Hakika Mwenyezi Mungu, Mwenye Nguvu na Aliyetukuka ameniteremshia wahyi (kunijulisha) kuwa mimi nitafariki ".

Pamoja na kauli nyingi nyinginezo.

Hizi hadithi zinaonyesha kuwa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) alipozungumza maneno hayo alikua katika hali ya kubainisha wadhifa wa umma baada ya kufa kwake, ili usibaki katika hali ya kupuuzwa, jambo lisilomstahiki Mtume(s.a.w.w) kwani mfano wake, ambaye ni mwanzilishi wa uislamu, atawezaje kuridhia kuuacha uislamu na waislanu hivi tu, bila ya mwelekeo, baada ya kupitio mateso na misiba katika kuuasisi uislamu na serikali ya kiislamu? Kamwe, hekima ya Mwenyezi Mungu pamoja na elimu ya Mtume Mtukufu(s.a.w.w) haimruhusu yeye(s.a.w.w) kufanya vivyo.

2) Kutotengana kwa Qurani na kizazi cha Mtume(s.a.w.w)

Kuviacha vitu viwili (yaani Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi cha Mtume Mtukufu(s.a.w.w) katika umma ni sawa na kuvifanya kuwa makhalifa wake. Basi Quran na kizazi chake Mtume(s.a.w.w) ni makhalifa wawili wa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) katika ummu. Vinachukua cheo cha Mtume(s.a.w.w) vinapo-dumu kuwa pamoja na kutofarikiana, na hii ndio sababu tunaona kwenye hadithi nyingi Mtume(s.a.w.w) akiviita makhalifa, kama alivyopokea Ahmad katika kitabu chake cha Musnad kutoka kwa Zaid ibnu Thabit, aliyesema, "Mtume wa Mwenyezi Mungu alisema:

"Hakika mimi ninaacha kati yenu makhalifa wawili ".[13]

Vile vile imepokewa kutoka kwa Abu Sa'id Alkhidri ya kwamba alisema,"Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alihotubia na kusema:

"Enyi watu, hakika mimi nimeacha kati yenu vizito viwili, vikiwa (kama) makhalifa wawili ".[14]

Au kwa riwaya nyingine;

"Hakika mimi ninaviacha viwili vizito kuwa makh-alifa kati yenu ".[15]

Na kwenye riwaya nyingine alisema:

"kwa hakika nimeviacha viwili vizito kuwa makhalifa kati yenu ".[16]

Lengo la kukifanye kizazi chake(s.a.w.w) kuwa khalifa na kukiachia cheo chake si jengine ila tu, ni kukipa majukumu yake, na hii kwa njia nyingine inathibitisha uimamu na uongozi wa kizazi chake(s.a.w.w) juu ya umma wake.

Kwa hivyo basi, hadithi hii inatuthibitishia vilevile uongozi wao katika mambo ya kisiasa kama inavyo-thibitisha uongozi wao katika mambo ya kielimu na mengineo. Inatuthibitishia pia wajibu wa kuwafuata kiujumla, na wala haikushurutisha jambo lotote lile katika kuwafuata. Imetuthibitishia pia uharamu wa kuwatangulia au kubaki nyuma (yao).

Lakini, ni sikitiko kubwa kuona kuwa umma wa kiislamu uliwaacha na kuwapuuza Ahlulbait (Baada ya kuwa Mtume Mtukufu(s.a.w.w) ametilia mkazo sana.) na wala hawakujali haki zao, kwani hawaku-unyenyekea uimamu na uongozi wao, bali walifanya yale waliyoya fanya baada ya kuwa Mtume(s.a.w.w) amemteuwa na kumuainisha Imamu katika sehemu nyingi na hasa katika siku yake ya kuaga dunia.

Zaidi ya hayo hawakuchukuo hukumu na sheria za Mwenyezi Mungu na wala adabu na sunna za Mtume(s.a.w.w) walibaki bila kuziandika hadi baada ya nusu ya karne ya pili ya hijriya takriban, ali po kuja khalifa Umar ibnu Abdul Aziz na kuifuta sheria hii, kwa kuona kuwa hadithi tukufu zina potea. Ndipo maula-maa wa kisunni wakaanza kuandika hadithi za Mtume Mtukufu(s.a.w.w) ziilizobaki (kama vile Malik na Ahmad ibnu Hambal na Bukhari na wengineo (kwa utaratibu huo) baada ya kuzisahao nyingi kati ya hizo au baada ya kufariki kwa kwa waliokuwa wamezihifadhi. Baadhi ya wachunguzi wa hadithi wamesema ya kwamba "Hadithi wanazozitegemea (ndugu zetu masunni) katika kutoa hukumu za sheria hazizidi mia tano".

Na kwa hivyo sunna (hadithi) za Mtume Mtukufu(s.a.w.w) kwa ndugu zetu masunni zilikuwa hazijaku-sanywa wala hawakuzijua kabla ya nusu ya karne ya pili, na hali ya kuwa sunna kamili ilikuwa pamoja na Ahlul bait(a.s) tangu kuaga dunia kwa Mtume(s.a.w.w) .

Kwa hivyo basi, nini sababu ya kuiacha na kuipuuza elimu ya Ahlulbait, ilhali walikuwa wakina-kili sunna ya Mtume(s.a.w.w) kama ilivyo kuwa, kwa ukamilifu.

Almuhaqqiqul wahiid (Muhakiki wa aina yake) Seyyid Burujurdi (r.a) amesema ya kwamba, "Kuna hadithi nyingi zilizopokelewa kutoka kwa Ahlul bait(a.s) zisemazo kuwa wana kitabu kilichoandikwa kwa imla[17] ya Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) na kwa khati za Imam Ali bin Abi Talib(a.s) , ambacho ndani yake kuna Sunna zote za Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) na yote aliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu kuyafikisha kwa umma wake, katika mafunzo na hukumu za kidini."

Kisha alitaja baadhi ya riwaya hizi zenye kuonyesha kuwepo kwa kitabu kwa imla ya Mtume(s.a.w.w) na kwa hati ya Ali(a.s) na kusema, "Inadhihiri kutokana na hadithi hizi mambo yafwatayo ".

Kwanza : Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) hakuuacha umma baada yake bure, bila ya Imamu wa kuwaongoza, wala bayana ya kutosha, bali aliwachagulia Maimamu, watukufu, waongozao na kuihifadhi dini, kisha akawapa mafunzo yanayomhusu Mwenyezi Mungu, faradhi za kidini, sunna na adabu, halali na haramu, hekima na athari, na yote wanayoyahitajia watu hadi siku ya kiama, hata ikiwa mtu atamkwaruza mwenzake amewaelezea ni kiwango gani cha faini (dia) kinachofaa kutolewa. Wala hakumruhusu yeyote kuhukumu au katoa fatwa kwa kutumia rai na maoni yake au kwa kutumia Qiyas (kufananisha hukumu za sheria kama wafanyavyo ndugu zetu masunni) kwani hakuna maudhiu au jambo lolote lisilokuwa na hukumu thabiti itokayo kwa Mwenyezi Mungu, Aliye Mjuzi Mwenye Hekima, bali Mtume(s.a.w.w) alimju-lisha Imam Ali Ibnu Abi Talib (a.s) sheria na hukumu zote na kumuamuru kuwa aziandike na kuzihifadhi. Na kuwakabidhi Maimamu(a.s) katika kizazi chake.

Basi Ali(a.s) aliandika kwa hati yake (tukufu) na kuwakabidhi waliokusudiwa (yaani Maimamu).

Pili : Mtume(s.a.w.w) alimwamuru Imam Ali Ibnu Abi Talib(a.s) peke yake kuandika na wala hakuna yeyote mwengine katika zama zake aliyejua aliyokuwa ameandika. Kisha alimwusia kuwa kitabu hiki kiwe mikononi mwa Maimamu kumi na wawili baada yake.

Basi inauwajibikia umma wote wa kiislamu kuchukua elimu inayo husu halali na haramu, na yote wanayohitajia katika dini yao kutoka kwake Ali(a.s) na Maimamu watokanao na kizazi chake, kwani wao ndio wasiri wa Mtume(s.a.w.w) na ndio hazina ya elimu yake na wahifadhio dini yake.

Tatu : Kitabu hiki kilikuwa mikononi mwao Maimamu(a.s) .

Imam Muhammad Baqir(a.s) na Imam Ja'afar Swadiq(a.s) waliwaonyesha baadhi ya maswahaba wao na wengineo katika wafuasi wa dhehebu la kisunni, ili kuitimiza hoja, na ili kuwaon-dolea shaka mioyoni mwao".

Katika sehemu nyingine Seyyid Burujurdi anaendelea kusema: "Basi inawajibika kuchukua hadithi katoka kwao, kwani zinaaminika zaidi kuliko za wengineo ".[18]

3) Wajibu wa Kushikamana na Quran na kizazi kitukufu (a.s)

Hadithi hii inatufunza ya kwamba ni wajibu kwa waislamu kushikamana na Qurani tukufu na kizazi, vyote viwiti kwa pamoja. Kwa hivyo basi kushikamana na kimoja na kukiacha kingine ni kosa kwani maagizo ya hadithi ni kushikamana na vyoze viwili.

Basi watu wameamrishwa kushikamana na Qurani kama walivyoamwrishwa kushikamana na kizazi cha Mtume Mtukufu(s.a.w.w) . Katika baadhi ya riwaya imepokewa kuwa alisema:

"Nimeacha kati yenu ambacho mkishikamana nacho hamtapotea kamwe baada yangu, Kitabu cha Mwenyezi Mungu kilicho kati yenu, mnakisoma asubuhi na jioni. Ndani nwake mna yote mnayokutana nayo na yote mnayodai "[19]

Kurejeshwa kwenye Qurani kunaonyesha kuwa inabayana na ufafanuzi wa kutosha, na hii si kutokana na jambo jengine, ila tu ni kwa kuwa, maana dhahiri ya maneno yake ni hoja, kwa hivyo maana ya dhahiri ya maneno yake na aya zake za Muhkamat (zilizo dhahiri) ni nuru na uongofu. Naam, ufafanuzi wa lazima unaachiwa Mtume(s.a.w.w) na kizazi chake kitukufu, kwani Qurani tukufu, haikutoa maelezo yote kuhusu swala, zaka, hijja na mambo mengineo.

Vile vile kufafanua daraja za mafunzo yake na mambo yanayohusiana na akhlaq na jamii na mengi-neyo yote, ni jukumu lililo mikononi mwa kizazi kitoharifu(a.s) . Kwa vyovote vile, haijuzu kuacha kuirejelea Qurani kwa kudai kuwa umeshi kamana na kizazi cha Mtume(s.a.w.w) , kwani kizazi chenyewe kimeifanya Quran tukufu kuwa ndio kipimio cha haki, zinapo hitilafiana riwaya na hadithi za Mtume(s.a.w.w) na pia na kime kuwa kikiirejelea Qurani katika kupambanua baina ya hadithi zilizodhaifu na zilizosahihi. Kisha kizazi kitukufu kilitilia mkazo kuwa watu wairejelee Qurani na kuitegemea, na kuwahimiza katika mambo mengi yenye uhusiano na Qurani, kama vile kuisoma Qurani na kuizingatia. Kuhusiana na haya, yatutosha kauli yake Amirul muuminin Ali (a.s) aliyosema:

"Tambueni kuwa hii Qurani ni mtoaji nasaha asiye hadaa, na mwongozaji asiyepoteza, na mzungumzaji asiyedanganya. Hakuna anayeketi karibu na hii Qurani, ila tu husimama akiwa na ziyada (katika jambo) na upungufu (katika jambo). Ziada katika uongofu na upungufu katika upofu (na upotofu). Tambueni, kuwa, hakuna mwenye haja, (na ufukara) baada ya kuwa na Quran, na hakuna mwenye utajiri kabla ya kuwa na Qurani. Basi jitibuni kwayo kutokana na maradhi yenu, na itegemeeni katika shida zenu, kwani ndani yake kuna tiba ya ugonjwa mkuu zaidi, nao ni ukafiri, unafiki udanganyifu na upotofu. Basi, muombeni Mwenyezi Mungu kwayo na mumuelekee kwa kuipenda, na wala msiwaombe viumbe vyake kwayo. Hakika waja hawakumwelekea Mwenyezi Mungu kwa njia bora mfano wake (Qurani).

"Na jueni kuwa Qurani ni mtetezi atakaye kubaliwa utetezi wake (siku ye kiyama) na mzungumzaji anayesadikiwa. Na (Jueni) kuwa atakayetetewa nayo siku ya kiyama atakubaliwa (na Mwenyezi Mungu) na ambaye Qurani itashuhudia maovu yake (mbele ya Mwenyezi Mungu) siku ya kiyama itasadikiwa (na kukubaliwa) ".[20]

Vile vile yatutosha kauli yake Imam wetu Ja'afar Sadiq(a.s) aliyosema:

"Vitu vitatu vitashitaki kwa Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu na Aliyetukuka, (siku ya kiyama), msikiti ulioharibika ambao watu wake hawaswali ndani yake, na mwana chuoni katikati ya wajinga (wasiotaka kusoma) na Msahafu uliotundikwa, uliojaa mavumbi, usiosomwa ".[21]

Na kauli yake(a.s) nyingine:

Haikika ndani mwa hii Qurani kuna nuru ya uon-gofu, na taa (zinazowaka) na kuondosha kiza, basi na atembeze mtembezaji macho yake na ayafungue ili kuupokea mwangaza (wake) kwani tafakari ndio uhai wa moyo wenye busara (na ayatembeze macho) kama yule anayetaka nuru yake atembeavyo gizani"[22]

Tambueni kuwa mwenye kutosheka tu nakuwataja Ahlul bait(a.s) bila ya kufwata maagizo na makatazo ya Qurani na mwelekezo wake, basi atakua hajachukua kutoka kwa Ahlulbait(a.s) kikamilifu, kwani wao hawaridhishwi kamwe na mtu kuiacha na kuipuuza Qurani.

Vile vile haifai kutosheka na Qurani pekee, kwani ufafanuzi kuihusu Quran kiupana pamoja na hukumu na elimu za Qurani zote ziko kwao, Ahlul bait(a.s) .

Haya ni pamoja na haja iliyoko ya kuwepo kwao katika kuimarisha uadilifu, malezi bora, utakaso na kuondoa kuhitilafiana (baina ya waislamu) pamoja na mambo mengineo katika ulimwengu.

Kushikamana na Qurani bila ya kushikamana na Ahlulbait sio kushikamana kikamilifu na Qurani, kwani aya za Qurani zenyewe zinatuele keza katika kuwatawalisha juu ya mambo yetu yote na kuwatii na inatuelekeza katika wajibu wa kuwapenda, kwani kila moja wapo (Qurani na Ahlulbait) - kama ilivyo katika baadhi ya hadithi - inaifafanua nyengine na kuafikiana nayo.[23]

Kwa hivyo basi, la wajibu ni kushikamana na vyote viwili, na hili ndilo jambo lililotiliwa mkazo katika hadithuth thaqalain, isemayo:

"Mkishikamana navyo (vizito viwili) hamtapotea kamwe baada yangu " pamoja na riwaya nyingi nyinginezo.

4) Sababu ya kuiita Qurani na kizazi vizito viwili (Thaqalain)

kuiita Qurani na Ahlul bait kuwa ni vizito viwili (Thaqalain) huenda ikawa ni kwa lengo la kutaka kuonyesha kuwa ni vitu vyenye thamani na utukufu sana. Hata hadithi yenyewe yaelezea binafsi kuhusu utukufu wa Quran na cheo kitukufu cha Ahlul bait(a.s) .

Imenakiliwa kutoka kwenye kitabu cha Abaqatul Anwar kutoka kwa Ibnul Athir ya kwamba ameandika kwenye kitabu chake cha Annihaya kuwa "chochote kilicho hatari na chenye thamani huitwa "thaqal" (kizito). Basi ameviita vizito viwili (Thaqalain) ili kuonyesha utukufu wa cheo cha vitu hivi viwili na kwa hivyo neno kizito lafaa kusomwa kwa kutamta fatha mbili (Juu ya herufi mbili za mwanzo - yaani - (Thaqal)".

Qurani ni tukufu zaidi ya Kitabu chochote kilichoteremshwa na Mwenyezi Mungu, nayo ni muujiza wa milele, itaendelea kuwepo madamu jua lipo. Nayo ni ufunuo (wahyi) usiopatwa na ubatilifu kabla yake wala baada yake, na ni nuru na uongofu.

Vile vile, kizazi, hakina mfano katika sifa, elimu na fadhila tukufu. Kama ilivyo makosa kuwalinganisha Mitume watukufu(a.s) na watu wa kawaida, vile vile ni makosa kuwalinganisha Ahlul bait(a.s) na watu wengineo wa kawaida, kwani wao ni mahujja[24] wa Mwenyezi Mungu juu ya viumbe vyake na wao ni hazina ya elimu yake.

Amirul muuminin Ali ibnu Abi Talib(a.s) katika maneno yake mafupi, (yaliyoko kwenye kitabu cha Nahjul balagha) kuhusu Ahlul bait(a.s) kwa kusema:

"Wao ni wasiri wake (Mwenyezi Mungu) na maficho (sanduku) ya mambo yake, na chemchemi ya elima yake na marejeo ya hekima zake, pango za vitabu vyake na milima ya dini yake. Kwa kupitia kwao amenyoosha kupinda kwa mgongo wa dini na kuondosha kutetemeka kwa viungo vyake (dini) Hakuna katika umma huu anayeweza kulinginanishwa nao, na kamwe hawezi kusawazishwa nao yule ana yetawaliwa na fadhila zao. Wao ndio msingi wa dini na nguzo ya imani. Aliyewatangulia (na kupita mipaka) yampasa kuwarejelea, na aliyebaki nyuma yampasa kuwafikia. Wana sifa zote za kustahiki uwalii (uongozi) na wao ndio wenye wasia (wa Mtume(s.a.w.w) na urithi (wake). Huu ndio wakati ambao haki imemrudia mwenyewe (anayeistahiki) na kunakiliwa hadi kwenye mahala pake."[25]

Huenda mtu akadai, kama alivyosema Zamakhshari, kuwa neno thaqalain limetumiwa kwenye hadithi kwa lengo la kuvifananisha vizito viwili na majini (yaani) kama wanavyoitwa (watu na majini) thaqalain (ndani ya Qurani) kumaanisha dunia, vile vile thaqalain (Quran na Ahlul bait) limetumika kumaanisha dini.[26]

Na huenda ikawa makusudio ya kutumia neno hili thaqalain, ni kuonyesha kuwa kutenda na kushikamana na vizito viwili na kutii na kuchunga haki zao na kuviangalia ni jambo zito. (Hii ni) kama walivyofasiri baadhi ya wajuzi wa lugha ya kiarabu, na wajuzi wa hadithi tukufu kama alivyo nukuu Alhamwini kutoka kwa Ibnul Abbas, ya kwamba, "Aliulizwa maana ya kauli ya Mtume(s.a.w.w) "Hakika mimi ninaacha kati yenu thaqalain (vizito viwili)?" akasema: "kwa kuwa kushikamana navyo nikuzito (Thaqiil) ".[27]

Na katika riwaya nyingine vile vile kutoka kwake, amesema, "kwa kuwa kushikamana navyo na kutenda kufwatana navyo ni kuzito (thaqiil)."[28]

Maneno haya vile vile yametajwa katika kitabu cha Abaqatu; Anwar kama ilivyopokewa kutoka kwa Al-azhari kwenye kitabu cha Tahdhibul lugha na kwenye vitabu vingine pia.[29]

Kwa hivyo basi, kufuatana na kauli hii neno (Thiqlu) lenye kasra - lina maana ya mzigo mzito au mojawapo ya vitu vizito, lakini hii ni kinyume cha maana dhahiri ya hadithi, kwa kuwa (ikifasiriwa vivyo) itakuwa ina sifia hali ya hivi vitu viwili, na ilhali dhahiri ya hadithi inawajibisha hii kuwa sifa ya vitu vivyo (wala siyo sifa ya hali yavyo) kwa kuwa vyenyewe ni vizuri na vyenye utukufu na cheo.

5) Maana ya Al-itrah (kizazi).

"Al-itra" (kizazi) kama ilivyotajwa katika Annihaya na katika vitabu vinginevyo ni jamaa wa karibu wanaomhusu mtu.

Kwa hivyo basi neno hili haliwa kusanyi wasio kuwa jamaa wa karibu wanaomhusu mtu, mbali na wasio kuwa jamaa wa karibu, bali kinacho kusudiwa hapa kufuatana na mnasaba wa hukumu na maudhui[30] sio yeyote yule, katika jamaa wa karibu kwani sifa zao zilizotajwa kwenye hadithi- kama kuwafanya kuwa ni sawa na Quran tukufu na mizani ya haki na uongofuhazitusaidii katika kulitumikisha neno hili kuwakusanya wote. Kwa hivyo basi wanaokusudiwa - kama ilivyo tajwa waziwazi kwenye riwaya chungu nzima - ni Ahlul bait waliotajwa katika Qurani tukufu kuwa wametoharishwa (kutokana na madhambi) nao ni Maimamu Maasumu waliowatoharifu.

Ibnu Abil Hadid amesema kuwa "Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alishabainisha kuwa ninani kizazi chake (itrah) aliposema".

"Hakika mimi ninaacha kati yenu thaqalain (vizito viwili) " kisha akasema;

"Na kizazi changu (ambao ni) Ahlubaiti wangu " (yaani watu wa nyumba yangu). Kisha akabainisha katika sehemu nyingine kuwa ni nani Ahlubaiti wake, alipowakusanya chini ya shuka, ilipoteremka aya

"Hakika Mwenyezi Mungu Anataka kakuondoleeni uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakasenikabisa kabisa" na kusema;

"Ewe Allah, hawa ndio Ahlubait wangu, basi waondolee uchafu ".[31]

Aljurjani Ash-shafii; (Aliyefariki katika mwaka wa 365 H.) amepokea kutoka kwa Abu Said ya kwamba alisema, "Hii aya - ayatut tat-hir' - (aya ya kutakaswa kwa Ahlulbait), iliteremshwa kuwahusu watu watano Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) Ali, Fatima, Hasa n na Husein(a.s) "[32]

Adh-dhahabi katika Talkhisul mustadrak amepokea kutoka kwa Ummu Salama ya kwamba alisema:

"Hakika Mwenyezi Mungu Anataka kukuondoleeni uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na (anataka) kukutakaseni kabisa kabisa ". iliteremka nyumbani kwangu. Basi Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) akawatumania Ali, Fatima, Hasan na Husein(a.s) , na kusema: "Ewe Allah hawa ndio Ahlubaiti wangu ". Ummu Salama akamwambia (Mtume(s.a.w.w) "Ya Rasulallah, Je, mimi si katika Ahlulbait?" akamjibu "Hakika wewe u katika kheri, na hawa ndio Ahlubaiti wangu. Ewe Allah Ahlubati wangu ndio wenye haki zaidi ". [33]

Na kuna riwaya nyingi nyinginezo zinazoonyesha kuwa Ahlul bait katika ayatut tathir wanao kusudiwa ni watu makhsusi.

Na hivyo ndivyo ilivyo pia katika riwaya zinazoifasiri "ayatul mubahala" (aya ya kuapizana kwa Mtume(s.a.w.w) na wakristo wa Najran) ambazo vile vile zinaelezea kuwa makusudio hasa ya Ahlul bait ni akina nani.

Muslim amepokea kwa isnadi yake, kwamba "ayatul mubahala[34] ilipoteremka Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alimwita Ali, Fatima, Hasan na Husein(a.s) na kusema.

"Ewe Allah hawa ndio Ahlu baiti wangu, Jamaa wangu (wa nyumbani) ".[35]

Na ndio sababu imetajwa kwenye kitabu cha Abaqatul Anwar kukiri kwa maulama wa dhehebu la kisunni kuwa hadithuth thaqalain inazungumza kuhusu Maimamu watokanao na Ahlulbait (wala haiwahusu watu wengine).

Miongoni mwa maulama hawa ni Alhakim Attirmidhi, aliyesema kuwa, "Basi kauli ya Mtume wa Mwenyezi, Mungu(s.a.w.w) kuwa

"Havitatengana kamwe mpaka vitakaponijia huko kwenye hodhi (ya kauthar)" na kauli yake kuwa: "Mkishikamana nacho hamtapotea kamwe", inawa-husu Maimamu. Basi wao ni maseyyid (mabwana) na wala haiwahusu wengine ".[36]

Na miongoni mwao ni Sibtu Ibnil Jauzi, alipoitaja hii hadithi katika Tadhkiratul khawass, chini ya unwani ya "Tunayoyataja kuwahusu Maimamu ".[37]

Na miongoni mwao ni Alkanji Ash-shafii katikakifaya tut Talib (baada ya kuitaja riwaya ya Zaid Ibnu Arqam na tafsiri yake ya Ahlulbait, kuwa ni wale walioharanmishiwa kula sadaka) alisema kuwa - "Hii tafsiri ya Zaid kuwahusu Ahlul bait hairidhishi, kwani amesema "Ahlulbait ni wale ambao wameharamishiwa kula sadaka baada yake - (yaani baadaye Mtume sawa) - ilhali kuharamishiwa kwao sadaka sio tu baada ya kufariki kwa Mtume(s.a.w.w) , bali hata katika uhai wake. Vile vile kuharamishwa huku hakuwahusu tu waliotajwa (katika hadithi) bali kunawahusu hata Bani Muttalib". mpaka akafikia kusema, "Bali lililo sahihi ni kuwa Ahlul bait ni Ali, Fatima, Hasan na Husein(a.s) kama alivyopokea Muslim kwa isnadi yake kutoka kwa Bibi Aisha (aliyeseme).

"Siku moja asubuhi, Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) alitoka akiwa amejifinika kwa shuka iliyoshonwa kwa sufi nyeusi; Hasan ibnu Ali akamjia, (Mtume) akamwingiza (ndani ya shuka). Kisha akaja Husein, akamwingiza (pia). Kisha akaja Fatima, akamwingiza (pia). Kisha akaja Ali, akamwingiza (vile vile): Kisha akasema "Hakika Mwenyezi Mungu (Anataka) kukuondoleeni uchafu enyi watu wa nyumba (ya Mtume) na (Anataka) kukutakaseni kabisa kabisa ".

Na hii ni dalili ya kuonyesha kuwa Ahlulbait ni wale ambao Mwenyezi Mungu Aliwaita kwa kauli yake Ahlulbait ambao Mtume(s.a.w.w) aliwaingiza ndani ya shuka".[38]

Kuna maulamaa wengine wengi waliokiri (kuwa Ahlulbait katika hadithuth thaqalain ni Maimanu Maasumin), walio tajwa, majina yao pamoja na maneno yao (yaani maulamaa) kwenye kitabu cha Abaqatul Anwar.[39]

Haya, bila ya kutaja riwaya nyingi zilizo mutawatir[40] katika vitabu vyetu zinazohusiana na mlango huu, ambazo miongoni mwazo ni riwaya aliyoipokea Ibnu Babaweihi katika kitabu cha "Uyunu Akhbarir Ridha(a.s) " kutoka kwa Imam Ja'afar Swadiq(a.s) kutoka kwa babu zake watukufu(a.s) kutoka kwa babu yake, (ambaye ni) Imam Husein(a.s) ya kwamba alisema",

"Amirul muminin Ali(a.s) aliulizwa maana ya kauli yake Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) (aliyosema) "Hakika mimi ninaacha kati yenu vizito viwili, Kitabu cha Mwenyezi Mungu na (itrah) kizazi changu ". Ni nani itrah (kizazi)? Akasema: "Ni mimi, Hasan, Husein na Maimamu tisa, wa tisa kati yao ndiye Mahdi na Qaim, (kamwe) hawa tengani na Kitabu cha Mwenyezi Mungu, nacho hakitengani nao, hadi watakapomjia Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenye hodhi yake (ya kauthar) ". [41]

Kwa hivyo ni wazi kuwa "itrah" (kizazi) ni Ahlul bait, nao ni Maimamu watoharifu na maasumin[42] watukufu(a.s) .

6) Quran na Ahulbait ndio kamba ya Mwenyezi Mungu

Qurani ni kamba ya Mwenyezi Mungu kama Asemavyo Mwenyezi Mungu:

"Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote, wala msitengane ".

Kuna riwaya nying zinazoshuhudia jambo hili. Miongoni mwazo, ni riwaya aliyoipokea Abu Said Alkhidri kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) ya kwamba alisema:"Huenda nikaitwa na (Mola wangu) nami nikajibu, nami ninaacha kati yenu vizito viwili, Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu. Kitabu cha Mwenyezi Mungu ni kamba iliyonyooshwa kutoka mbinguni hadi ardhini nacho Kizazi changu ni Ahlubait wangu (watu wa karibu wa nyumbani kwangu). Naye Mwingi wa huruma Aliyemjuzi wa yote amenijulisha kwamba havitotengana kamwe mpaka vitakaponijia kwenye hodhi (ya kauthar). Basi angalieni mtakavyo-vitendea baada yangu".[43]

Vile vile kamba ya Mwenyezi Mungu inawaku-sanya Ahlulbait (a.s), kwa kuwa wamefanywa kuwa sawa na Quran katika hadithuth thaqalain, na kwa kuwa wameteuliwa na Mwenyezi Mungu kuwaongoza watu. Basi kushikamana nao ni sawa na kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu ambayo inatuzuia na kupotoka na kuangamia.

Katika Tafsiru Alaur Rahman' baada ya kuitaja aya hii,

"Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote "

Mwandishi amesema, "yaani jizuieni kutokana na kuanguka, kwa kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu mkiwa katika hali ya umoja, na (pia) kwa kushikamana na) kile ambacho amekijaalia kuwa ni chenye kuwahifadhi (na kuwazuia) kutokana na kuanguka kwenye upotofu. Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) ameshatu julisha kuwa ni nani wanaoitwa kamba, ambayo mwenye kushikamana nayo hapotei, katika kauli yake kwenye hadithuth thaqalain isemeyo:

"Ambavyo mkishi kamana navyo hamtapotea kam-we, (navyo ni) Kitaba cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu (ambao ni) Ahlubait wangu". Neno kamba limetumika katika (maana) kuonyesha kuwa kutoshi-kamana nayo kutamfanya mtu kuanguka kwenye upotofu mkubwa na kuangamia."[44]

Dalili nyingine inayo tuthibitishia kuwa neno kamba halikutumiwa makhsusi kwa Qurani, bali lime-wakusanya pia Ahlul bait, ni kuwa, Mtume(s.a.w.w) amekusanywa kwenye maana hii katika aya:

"Na mnakanushaje, hali nyinyi mnasomewa Aya za Mwenyezi Mungu, na Mtume wake yuko pamoja na nyiye? Na mwenye kumshika Mwenyezi Mungu sawa sawa basi yeye amekwishaongozwa katika njia iliyonyooka "

Katika aya hizi ni dhahiri kuwa kushikamana na aya za Mwenyezi Mungu na kumfwata Mtume(s.a.w.w) ni sawa na kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu, kama alivyosema Mwenyezi Mungu katika aya iliyotangulia, kwamba kushikamana navyo ni kushikama na Mwenyezi Mungu, kwa hivyo basi kama vile Mtume(s.a.w.w) ni mfano wa kamba ya Mwenyezi Mungu, vile vile kizazi chake kitukufu chenye kuchukua cheo chake (baada yake) ni mfano wa kamba ya Mwenyezi Mungu.

Haya pamoja na kuongezea riwaya nyingi zilizoe-lezea wazi wazi jambo hili. Miongoni mwazo ni riwaya iliyopokewa kwenye Abaqatul Anwar kutoka kwa Sheikh Suleiman Al-hanafi Alqanduzi katika tafsiri ya aya "Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote " alisema kuwa "Ath-tha'alabi amepokea kwa sanadi yake (silsila ya wapokezi) kutoka kwa Aban Ibnu Taghlib kutoka kwa Ja'afar Swadiq (R.a) ya kwamba alisema.

"Sisi ndio kamba ya Mwenyezi Mungu ambayo Mwenyezi Mungu Mwenye Nguvu na Aliyetukuka Amesema: "Na shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote na wala msiachane ".

Vile vile mwandishi wa Kitabul Manaqib ame-pokea kutoka kwa Said Ibnu Jubair (R.a) kutoka kwa Ibnul Abbas (r.a) ya kwamba alisema:

"Tulikuwa pamoja na Mtume(s.a.w.w) alipokuja bedui mmoja wa kiarabu na kumwambia "Ya Rasulallah, nilikusikia ukisema "Na shikamaneni na kamba ya Mwenyezi Mungu". Basi ni ipi kamba ya Mwenyezi Mungu ambayo tutashikamana nayo? Mtume(s.a.w.w) akaupigisha mkono wake kwenye mkono wa Ali na kusema " Shikamaneni na huyu, yeye adiye kamba ya Mwenyezi Mungu iliyoimara ".[45]

Na miongoni mwazo ni hadithi aliyoipokea Annumani kwa isnadi yake kutoka kwa Hariiz Ibnu Abdillah kutoka kwa Abu Abdillah Ja'afar Swadiq Ibnu Muhammad(a.s) kutoka kwa baba yake kutoka kwa babu zake(a.s) kutoka kwa Ali(a.s) ya kwamba alisema,

"Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) aliho tubia kwenye msikito wa Alkhiif - (Nayo ni hotuba mashuhuri katika hijjatul wida'a (hijja yake ya mwisho) - na kusema". Tambueni kuwa mimi ninaacha kati yenu vizito viw ili, kizito kikubwa na kizito kidogo. Kizito kikibwa ni Quran, na kizito kidogo ni kizazi changu (ambao ni) Ahlubaiti wangu. Navyo (viwili hivi) ni kamba iliyonyooshwa baina yenu na baina ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka na Mwenye Nguvu. Mkishikamana nayo hamtapotea kamwe. Sehemu moja yake iko mikononi mwa Mwenyezi Mungu na sehemu (nyingine) iko mikononi mwenu".[46]

Na miongono mwazo ni hadithi aliyoitaja Ibnu Abil Hadid, ya kwamba Mtume(s.a.w.w) alisema:

"Nemeacha kati yenu viwili vizito (kama) makhalifa (wawili) Kitabu cha Mwenyezi Mungu na kizazi changu (amboa ni) Ahlubait wangu, (hivi viwili) ni kamba mbili zilizonyooshwa toka binguni hadi ardhini, (na) havitatengana mpaka vitakapanijia huko hodhini (mwa kauthar).[47]

Kwa hivyo basi, la wajibu kufanya katika kuleta umoja na kuondosha utengano na ufarikiano, ni kushikamana na vizito viwili na kuzuia utengano kabisa, kwani hivi ndivyo vinavyoleta umoja, kama ilivyo kuwa katika zama za Mtume(s.a.w.w) umoja ulipatikana kwa kushikamana na Mtume wake(s.a.w.w) .

Yatupasa basi, sisi waislamu, kuamka kutoka usingizini na kushikamana na sababu muhimu na ya asili ya umoja wetu. Ndipo tutakuwa tumepata umoja wa kweli tulioamrishwa kuwa nao katika aya tukufu, na umoja huu utakuwa umeondoa umoja wa juu juu, hata ingawa ni umoja unaofaa, unaostahiki kuwepo.

Kisha kuiita Qurani na kizazi kwa jina la kamba ya Mwenyezi Mungu kunaonyesha wazi uhusiano mkubwa vilivyonao na Mwenyezi Mungu, kwa hivyo mwenye kushikamana navyo atakuwa kwa hakika ameshikamana na Mwenyezi Mungu. Na kunaonyesha pia kuwa kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu ndio njia ya pekee ya kujihifadhi kutokana na upotovu.