VITABU VILIVYOPOKEA HADITHI ZILIZONAKILIWA MWENYE KITABU HIKI (1) Tafseer cha Thalabi; (430 A.H.)
(2) Tafseer Kash-shaaf; Zamakh-shari (528 A.H.)
(3) Tafseer cha Nishapuri
(4) Tafseer cha Muhammad bin Saaib Al-Kalbi
(5) Tafseer Libaabut Taaweet wa Maanil anzeel; Khazn
(6) Tafseer Madarikut Tanzeel wa Hakaaikut Taweel
(7) Tafseer Ad Darrul-Manthoor; Jalaalud-Deen Suyooti
(8) Saheeh Al-Bukhari
(9) Saheeh Muslim
(10) Sunan Ibnu Maajah Al-Qazwini
(11) Sunan Abi Yaala
(12) Sunan Ad-Daar Qutni
(13) Kanzul Ummal; Ali Muttaki Al Hanafi
(14) Mustadrak-Saheehain; Al-Hakim Nishapuri
(15) Muntakhab Kanzul Ummal; iliyoko pembezoni mwa kitabu cha Musnad cha Ahmad bin Hanbal
(16) Masabeehus-Sunna; Baghawi
(17) Musnad; Ahmed bin Hanbal
(18) Musnad; Abi Daud Al-Tayaalisi
(19) Musnad; Abi ya'laa Al-Moosali
(20) Al-Mujamul-Kabeer; Tabarani
(21) Usdul Ghabah fi Maarifatis Sahaba; Ibnul Atheer Ash-Shafii (630 A.H.)
(22) Is-aafur-Raaghibeen, Ibnu Sabbaan-Sahfii
(23) Al-Isteeab; Ibn Abdil-Bar Annamry; (463 A.H.)
(24) Al-Isaba fi Tamyeezis Sahaba; Ibnu Hajar Al-Askalani; (863 A.H.)
(25) Jaami Tirmiz
(26) Khasasi Ahmad bin Shueib Annasai Ash-Shafii; (303 A.H.)
(27) Tabakaat; Ibnu Saad
(28) Firdausul Akhbaar; Ad-Daylami
(29) Faraidus-Simtain; Ibrahim bin Muhammad Al-Hamwini Ash- Shafii
(30) Al-Fusoolul Muhimma; Ibnu Sabbagh-Al-Maliki
(31) Kunoozul Hakaik, Abdurrauuf Al-Manawi Ash-Shafii (1031 A.H.)
(32) Kifaayatut-Taalib, Al-Kanji Ash-Shafii
(33) Al-Kaukabud-Durri; Sayyid Muhammed Saleh Al-Tirmizi Al-Haanafi
(34) Al-Kuna; Al-Hakim
(35) Manaakib; Al-Muwaffak bin Ahmad Al-Khwarazmi Al-Hanafi (865 A.H.)
(36) Manaakib; Ibnu Maghazili Ash-Shafii (483 A.H.)
(37) Maktalul Husein (a.s.); Al-Muwaffak bin Ahmad Al-Khwarazmi Al-Hanafii
(38) Mawaddatul Kurba; Sayyid Ali Al-Hamdani Ash Shafii
(39) Al-Ikdul Fareed; Ibnu Abdi Rabbih
(40) Al-Gheelaaniyaat, Abi Bakr Ash-Shafii
(41) Arjahul Mataalib; Ubaidullah Amristary Al-Hanafii
(42) Al-Ithaaf Behubbil Ashraak Sheikh Abdullah Shabrawi As-Shafii
(43) Al-Alkaab; Ahmad bin Abdurrahman Shirazi
(44) Al-Bidaya Wannihaya; Ibnu Katheer Ad-damashki (774 A.H.)
(45) Tareekhul khulafa; Jalaalud-Deen Assuyooti; (911 A.H.)
(46) Tareekhul Kabeer; Ibnu Asaakir; (571 A.H.)
(47) Tareekhul Kaamil; Ibnu Atheer Aljuzary; (606 A.H.)
(48) Tareekh Baghdad; Al-khateeb Al-Baghdad
(49) Tareekh Baghdad; Ibnu Najjar
(50) Tareekh Attabari Al-Kabeer; Abi Jaafar Ibnu Jareer: (310 A.H.)
(51) Tadhkiratu Khawaasil Umma: Sibt Ibni Jauzi Al-Hanafi (654 A.H.)
(52) Hilyatul Awliyaa; Abi Naeem Al-Isfahani (530 A.H.)
(53) Khulaasatul Manaakib
(54) Dhakairul Ukba; Muhibbuddeen At-Tabari (695 A.H.)
(55) Ar-Riyaadhun Nadhra; Muhibbuddeen At-Tabari Ash-Shafii
(56) Rashfatus-Saadi; Sayyid Shahaabud-Deen Abi Bakr Ash-Shafii
(57) Assawaikul Muhrika; Ibnu Hajar Al-Haytami Ash-Shafii
(58) Al-Masheekhatul Baghdaadiya; Al-Hafidh As-Salafi
(59) Nuzhatul Majalis; As-Safoori Ash-Shafii
(60) Wafayaat-ul-Aayaan; Ibnu Khallikan Ash-Shafii
(61) Yanaabee-ul-Mawaddah Shaikh Suleina Al-Kanduzi Al-Hanafii (1294 A.H.)
FAHARASA YA MANENO YALIYONENWA NA MTUKUFU MTUME WETU (S.A.W.W.) (1) Kauli ya Mtume (s.a.w.w.); hatavuka Sirati yeyote isipokuwa aliyeandikiwa ruhusa na Ali.
(2) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ni mgawaji wa Pepo na Moto
(3) Kauli yake (s.a.w.w.); kuangalia uso wa Ali ni Ibada
(4) Kauli yake (s.a.w.w.); mfano wa Ali katika Umma huu ni mfano wa Kaaba
(5) Kauli yake (s.a.w.w.); kumwangalia Ali ni Ibada
(6) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ni mlango wa elimu yangu na mwenye kuwaeleza umma wangu madhumuni ya kuletwa kwangu (duniani na Mungu).
(7) Kauli yake (s.a.w.w.); Kumwangalia Ali ni rehema, mapenzi na ibada
(8) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenyezi Mungu amemjalia ndugu yangu Ali kuwa sifa na vyeo visivyohisabika.
(9) Kauli yake (s.a.w.w.); Kumkumbuka na kumdhukuru Ali ni Ibada
(10) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali kwangu ni kama nilivyokuwa mimi kwa Mwenyezi Mungu.
(11) Kauli yake (s.a.w.w.); kwamba Ali ni mpole kwa Umma na mwenye subira mno.
(12) Kauli yake (s.a.w.w.); kwamba Ali anapendwa zaidi naye kuliko mtu yeyote.
(13) Kauli yake (s.a.w.w.); gao langu na la Ali katika uadilifu ni sawa.
(14) Kauli yake (s.a.w.w.); Mimi niko katika suluhu na yule atakayekuwa na watu wa hema hii.
(15) Masahaba walikuwa na sifa kumi na nane na katika hizo Ali alikuwa na sifa kumi na tatu ya pekee na kashirkiana nao katika tano zilizobaki.
(16) Kauli yake (s.a.w.w.); wewe kwangu kama alivyokuwa Harooni kwa Musa.
(17) Kauli yake (s.a.w.w.); ya kuonekana imani ya Ali kuwa mbora zaidi kuliko watu wote wa mbinguni na ardhini.
(18) Kauli ya Umar kwamba Ali amepewa sifa tatu ambazo ningalipata walau mojawapo ingalikuwa kwangu bora kuliko ngamia wekundu.
(19) Kauli ya Mtume (s.a.w.w.); Lau bahari ingaligeuka wino na miti kuwa kalamu isingaliwezekana kuandika sifa zote za Ali Bin Abi Talib (a.s.)
(20) Kauli yake (s.a.w.w.); Ewe Ali mkono wako utakuwa katika mkono wangu utapoingia Peponi nami.
(21) Kauli yake (s.a.w.w.); Huyu Ali ni ndugu yangu hapa duniani na kesho akhera.
(22) Kauli yake (s.a.w.w.); Hakuchuma mchumaji wa aina yeyote kama alivyokuwa nayo sifa Ali (a.s.)
(23) Kauli yake (s.a.w.w.); Hakuna sahaba yeyote aliyekuwa na sifa kama za Ali (a.s.)
(24) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenyezi Mungu amewaumba Malaika kutokana na nuru ya Ali (a.s.).
(25) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenyezi Mungu katika mbingu ya nne amemwumba malaika katika sura na mfano wa Ali (a.s.)
(26) Kauli yake Umar (R.A.) Ali tu ndiye mwenye ujuzi wa kuhukumu.
(27) Kauli yake (s.a.w.w.); kwamba Ali ni mjuzi zaidi wa kuhukumu kuliko watu wa Madina.
(28) Alikuwa Umar (R.A.) akiomba kwa Mwenyezi Mungu amwepushe kwenye dhiki wakati ambapo Ali hayupo.
(29) Kauli ya Umar (R.A.) kusema Ewe Mola wangu usinishushie dhiki yoyote ila akiwapo Ali (a.s.).
(30) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ndiye mwamuzi asiokuwa mfano na anavyoamua yeye ndiyo sawa.
(31) Uthibitisho wa Al-Kanji As-Shafiiy kuwa Ali ni mwenye elimu kuliko wote.
(32) Maamuzi ya Ali (a.s.) kuhusu mabedui wawili.
(33) Kauli ya Umar (R.A.) Ali ni bwana wangu na bwana wa kila mwenye kuamini na anayo mamlaka juu yetu sote.
(34) Kutia adabu na Umar (R.A.); mwenye kumbugudhi Ali.
(35) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali anatokana nami na mimi ninatokana na Ali.
(36) Kauli yake,(s.a.w.w.); kumwambia Buraydah usimbughudhi Ali (a.s.).
(37) Kauli yake (s.a.w.w.); Msimseme Ali.
(38) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ni (Bwana) mwenye mamlaka juu yenu baada yangu.
(39) Muhtasari wa kisa cha Ghadeer.
(40) Kauli ya Umar (R.A.): Nilimsikia Mtume (s.a.w.w.); akitaja sifa tatu za Ali (a.s.).
(41) Kisa cha kutekwa kwa Khaybar kwa mikono ya Ameerul Mumineen Ali (a.s.)
(42) Hadithi ya kisa cha Ghadeer kwa maelezo ya Umar (R.A.)
(43) Kauli yake (s.a.w.w.); kumwambia Ali (a.s.); wewe kwangu kama alivyokuwa Haruni kwa Musa.
(44) Kumwamrisha Ali kufikisha sura ya Bara-at kwa Makureshi wa Makka.
(45) Kisa cha kufungwa milango yote ifungukayo ndani ya Msikiti, na. ushindi wa Khaybar, na hadithi ya Ghadeer na hadithi ya Manzila.
(46) Kauli yake (s.a.w.w.); Laiti wangekusanyika watu wote kumpenda Ali (a.s.) asingaliumba Mwenyezi Mungu Moto (Jahanam).
(47) Kauli yake (s.a.w.w.); Ewe Ali, mwenye kukupenda wewe atakuwa pamoja na Mitume siku ya Qiyama.
(48) Mazungumzo ya Umar pamoja na Ibnu Abbasi kuhusu Khilafa (ukhalifa).
(49) Kauli ya Umar (R.A.) haukamiliki utukufu bila ya kumpenda Ali (a.s.).
(50) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenyezi Mungu amewaumba malaika kwa nuru ya uso wa Ali (a.s.).
(51) Kauli yake (s.a.w.w.); Hasan na Husain ni viongozi wa vijana wa Peponi.
(52) Kauli yake (s.a.w.w.); Mbora wa wanaume wenu ni Ali Bin Abi Talib.
(53) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ni mbora wa viumbe na mwenye kukataa hayo amekufuru.
(54) Kauli yake (s.a.w.w.); Mbora wa wote walio juu ya ardhi baada yangu ni Ali Bin Abi Talib (a.s.).
(55) Kauli ya Ibnu Umar, Ali ni katika Ahlu-Bait ambaye cheo chake hakikisiwi na mtu yeyote.
(56) Kauli yake (s.a.w.w.); Sisi Ahlul-Baiti hakisiwi mtu yeyote nasi.
(57) Kauli yake (s.a.w.w.); Huyu (anamkusudia Ali) ni Bwana (mwenye Mamlaka) wenu baada yangu humu duniani na Akhera.
(58) Kauli yake (s.a.w.w.); Hakika Ali anatokana nami na mimi ninatokana naye.
(59) Kauli yake (s.a.w.w.); kumwambia Ali, wewe ndugu yangu hapa duniani na kesho Akhera.
(60) Kauli yake (s.a.w.w.); mwenye kumwacha (asimfuata) Ali ameniacha mimi.
(61 ) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali wewe utakwenda Peponi.
(62) Kuhusu wale wanne wataoingia Peponi.
(63) Imani ya Ali (a.s.) kuwa na uzito zaidi kuliko mbingu na ardhi.
(64) Kauli ya Abdullah bin Umar kusema; Ali anayo mambo matatu, ninatamani niwe nao mojawapo.
(65) Kuonana kwa siri Ali (a.s.) na Mtume (s.a.w.w.); na Ali kutoa sadaka alivyoamrisha Mwenyezi Mungu.
(66) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenye kumpenda Ali Mwenyezi Mungu atamkubalia swala na saumu yake.
(67) Kauli yake (s.a.w.w.); kuwapenda Aali Muhamad (dhuriya wa Mtume) siku moja tu ni bora kuliko ibada ya mwaka mmoja.
(68) Kuzungumza Mwenyezi Mungu na Mtume (s.a.w.w.) usiku wa Miraji kwa lugha (sauti) ya Ali.
(69) Kauli yake (s.a.w.w.); Nalikuwa Mimi na Ali mbele ya Mwenyezi Mungu kabla ya kumwumba Adam (a.s.).
(70) Kauli yake (s.a.w.w.); Kumwambia Ali, 'wewe ni ndugu na waziri wangu'.
(71) Kauli yake (s.a.w.w.); Mwenye kupenda aishi maisha yangu na kufa kwangu) basi ampende na kumfuata Ali.
(72) Kauli yake (s.a.w.w.); kumwambia Aisha kwamba Ali ni Bwana wa Waarabu.
(73) Kauli ya Aisha kwamba Ali ni bora wa viumbe hatilii shaka juu ya jambo hilo ila kafiri.
(74) Kauli yake (s.a.w.w.); Ali ni bora wa viumbe.
(75) Kauli ya Aisha, "Hakumwumba Mwenyezi Mungu aliye mpenzi zaidi kwa Mtume (s.a.w.w.) kuliko Ali (a.s.).
(76) Kauli ya Aisha kwamba: Ali alikuwa mpenzi mno wa Mtume kuliko watu wote.
(77) Kauli ya Aisha, "Kwamba Ali ni karibu zaidi katika huba kwa Mtume (s.a.w.w.) kuliko watu wote.
(78) Kauli yake (s.a.w.w.); kumwangalia uso wa Ali (a.s.) ni ibada.