• Anza
  • Iliyopita
  • 9 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 13969 / Pakua: 2345
Kiwango Kiwango Kiwango
USUULID DIIN

USUULID DIIN

Mwandishi:
Swahili

6

USUULID DIIN

MAREJEO YA KIAMA

UWEZEKANO WA KUWEPO MAREJEO NA DALILI ZAKE

Tumetaja kwenye utangulizi wa kijitabu hiki ya kuwa sisi tunaishi na suala la marejeo kwa ukamilifu wake ndani ya jengo la itikadi na ndani ya maeneo yake maalumu.

Na tumeashiria sehemu hiyo ya kuwa Imani ya marejeo ni hatua itokanayo na Imani ya ule msingi mkubwa, na tunakusudia Imani ya Mwenyezi Mungu mtukufu muumba wa ulimwengu na muanzilishi wa kuwepo kwa ulimwengu na walimwengu na ni sababu ya juu kabisa ambayo sababu zote hurejea kwake, pasina kuwepo sababu ya kuwepo kwake au sababu ya kusaidizana nae katika kuanzisha kuwepo kwa ulimwngu.

Na inapothibiti Imani kama hii iliyo thabiti na madhubuti ya kumuamini Mwenyezi Mungu na kwamba yeye ndiye chanzo cha viumbe na chanzo cha ulimwengu na kwamba madda ni moja kati ya viumbe vyake hata kama watadhania na kuamini kuwa ni ya tangu na tangu kama wasemavyo baadhi ya wanafikra wa kimadda (materialists)[154] , hakutakuwa na kizuwizi mbele ya mwanadamu kitakacho mzuwia kuamini kuwepo kwa marejeo na ufufuo na kukubali uwezekano wa kutokea na kuwa si muhali kutokea kwake.

Hakika akili kumuamini mfanyaji wa kwanza inajifungulia njia ya kuamini uwezo wa mfanyaji huyo wa kuweza kufanya kitendo chake kwa mara ya pili na kwa mara elfu kadha, na kwamba jambo hilo ni miongoni mwa mambo ya badaha , yaani ya wazi kwenye akili yasiyo hitaji ufafanuzi wala dalili na ushahidi zaidi, na inatosha kutoa mfano juu ya jambo hilo kwa kumuangalia mtu alie weza kuunda kitu fulani, kwa mfano mashine itumiayo nguvu za umeme yenye uwezo mkubwa, hakika uwezo wa mtu huyo wa kuweza kutengenza tena kitu kile halitakuwa ni jambo la kusitasita au kulitilia shaka, madamu tumekinaika kuwa yeye ndie muundaji wa kitu kile kwa mara ya kwanza.

Hakika muundaji wa gari lau kama atasambaratisha gari lile na kuliweka kwenye vipande tofauti vidogo vidogo maelfu kwa maelfu, kisha akasema kuwa anaweza kuliunda na kulirudisha gari lile ikiwa limeungwa kama ilivyo kuwa, hakuna mtu yeyote ulimwenguni atakae jitokeza na kumtaka atoe dalili juu ya uwezo huo, na haitafanyika hivyo isipokuwa ni kwa sababu mfanyaji wa kitu kwa mara ya mwanzo ana uwezo wa kukifanya kwa mara ya pili na ya tatu na kwa mara mia kadha na kwa mara milioni na kwa njia hii ya utoaji ushahidi juu ya uwezekano wa kurejea na kwa mujibu wa utaratibu huu wa kupanda kwenye ngazi ya akida, Qur'ani tukufu imetoa dalili juu ya ubadaha (uwazi wa akilini) wa marejeo baada ya kifo (yaani ni suala lisilo hitaji dalili).

Na hebu tutoe baadhi ya aya hizo tukufu ambazo zilihusika na kuweka wazi ukweli huu na kufafanua uwezekano wake kwa kila mwenye akili na ufahamu na uelevu. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu:

"Na wakasema, tutakapo kuwa mifupa na mapande yaliyo sagikasagika, je sisi tutafufuliwa kwa maumbile mapya? Sema kuweni mawe au chuma au kiumbe kingine ambacho kinaone-kana kikubwa au kigumu kwenye nyoyo (fikra) zenu. Hapo watasema, ni nani atakae turudisha (kwenye hali yetu ya mwzanzo)? Sema ambae alikuumbeni kwa mara ya mwanzo . "Suratu-Israai:49-51".

"Na mwanadamu anasema:"Ikiwa nitakufa je nitatolewa tena nikiwa hai"? Je mwanadamu hakumbuki ya kuwa sisi tumemu-umba hapo kabla na hakuwa ni chochote ".Suratu Maryam:66.

"Siku ambayo tutaikunja mbingu kama ukunjaji wa kurasa (karatasi) zilizo andikwa, kama tulivyo kianzisha kiumbe cha kwanza tutakirudisha (hivyo). Ni ahadi juu yetu hakika sisi ni wenye kufanya hivyo ". Suratul-ambiyaa: 104.

"Mwenyezi Mungu huwaanzi-sha viumbe kisha atawarudisha kisha mtarudishwa kwake ". "Suratu-Al-ruum:11".

"Na watasema:Tutakapo kuwa mifupa na mapande yaliyo sagika sagika je sisi tutafufuliwa kwa maumbile mapya? Je hawa-kuona ya kuwa Mwenyezi Mungu alieumba mbingu na ardhi ni Mwenye uwezo wa kuumba mfano wao "."Suratul-Israai: 49-51.

"Hakika tulimuumba mwanadamu kutokana na chembe chembe za udongo, kisha tukamfanya kuwa ni mbengu za uzazi kwenye mahali madhubuti, kisha tukaumba kutokana na mbengu za uzazi pande la damu, na tukalifanya pande la damu kuwa pande la nyama, na pande la nyama tukaliumbia mifupa, na mifupa tukaivisha nyama kisha tukakiumba kiumbe kingine, ametakasika (Mwenyezi Mungu) mbora wa uumbaji, baadae hakika nyinyi mtafishwa, kisha nyinyi siku ya kiama mtafufuli-wa". "Suratul-muuminuuna :12-16.

"Sisi tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadiki? Je mmeyaona maji ya uzazi myatoayo? Je nyinyi ndio myaumbayo au sisi ndio wenye kuyaumba? Sisi tumekikadiria kifo kati yenu, nasi si wenye kushindwa kuleta viumbe mfano wenu na kukuumbeni kwenye umbo msilolijua, na hakika mnajua umbo la kwanza (kuumbwa kwenu) kwanini hamkumbuki"? "Suratul-Waaqia:57-62.

"Je anadhani mwanadamu ya kuwa ataachwa hivi hivi? Je hakuwa ni mbegu ya uzazi ya manii yatokayo kwa kuchupa, kisha akawa pande la damu na (Mwenyezi Mungu) akamuumba na kumuweka kwenye umbo la sawa, na akamfanya namna mbili mwanamume na mwanamke. Je (alie kufanya hivyo) hakuwa ni muweza wa kuwahuisha na kuwarudisha kwenye uhai walio kufa? "Suratul-qiyama:36-40".

"Je hawakuona ya kuwa Mwenyezi Mungu ambae ameumba mbingu na ardhi na hakuchoshwa na kuwaumba kwao ni Mwenye uwezo wa kuwahuisha walio kufa ? Naam hakika yeye ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu" "Suratu-Ahqaafi:33".

"Je hatukukuumbeni kutokana na maji yaliyo dhalili na tukayaweka mahali pa utulivu hadi muda maalumu na tukakadi-riya (wakati wa kutoka mtoto). Na si ni wazuri kabisa wa kukadiria. Ole wao siku hiyo wanaokadhibisha"! "Suratul-mursalat:20 -24".

"Je mwanadamu hakuona ya kuwa sisi tumemuumba kutokana na maji ya uzazi, na ghafla ana kuwa ni adui wa wazi, na akatupigia mfano na kasahau kuumbwa kwake akasema: "Nani ataihuisha mifupa ikiwa imeharibika na kusambaa"? Sema ataihuisha yule amabae aliiumba kwa mara ya mwanzo, nae ni mjuzi wa kila kitu."Suratul Yaasin 77-79".

"Je alie umba mbingu na ardhi si mwenye uwezo wa kuumba viumbe mfano wao? Naam, na yeye ndie Mwingi wa kuumba na Mjuzi"."Suratu-Yaasin 81".

Je tulichoka kwa kuumba kwa mara ya kwanza? (Hata tushindwe kuumba umbo la pili). Basi wao wako kwenye shaka juu ya umbo jipya". "Suratu-Qaf:15".

"Hakika kuumba mbingu na ardhi ni kukubwa zaidi (na kugumu) kuliko kuwaumba watu, lakini watu wengi hawajui".

"Enyi watu ikiwa mko kwenye shaka kuhusu ufufuo, hakika sisi tumekuumbeni kutokana na udongo kisha mbegu za uzazi kisha pande la damu kisha pande la nyama lenye umbile (kamili), na lisilo na umbile (kamili), ili tukubainishieni. Nasi tunavithibi-tisha kwenye mifuko ya uzazi tuvitakavyo hadi muda uliowekwa kisha tunakutoweni mkiwa watoto, kisha tunakuleeni ilimfikie kuwa wakubwa, na kuna wanao kufa na kuna warudishwao kwenye umri dhalili, ili asijue chochote baada yu kuwa alikuwa akijua mambo".

Na unaiona ardhi ikiwa imetulia kimya na tunaposhusha juu yake maji inataharuki na kukuwa na kuotesha kila aina ya mimea iliyo mizuri. Hayo ni kwa sababu Mwenyezi Mungu ndie haki na kwamba yeye anawahuisha wafu na kwamba yeye ni Mwenye uwezo juu ya kila kitu, na kwamba kiama kitakuja hapana shaka ndani yake, na hakika Mwenyezi Mungu atawafufua waliomo makaburini. "Suratul-Hajji:5-7.

"Hakika mmetujia kama tulivyo waumba kwa mara ya mwanzo bali mlidhani ya kuwa hatukukuwekeeni miadi hii". "Suratul-kahfu:48".

Kwa hivyo inatudhihirikia wazi kuwa "hakika Mwenyezi Mungu ambae ameumba mbingu na ardhi ni mwenye uwezo wa kuumba viumbe mfano wa hivyo" kama alivyo kiumba kiumbe cha mwanzo atakirudisha hivyo hivyo. Na kwamba uumbaji wa pili hautatofautiana na uumbaji wa mwanzo tunao ufahamu kwa kuushuhudia kwa macho yetu. Na kuwa alieipa mbegu ya uzazi uwezekano na nguvu ya kukua hadi kufikia kuwa pande la damu kisha kuwa pande la nyama kisha kuwa mtoto na kuwa kijana hadi kuwa mzee, ni Mwenye uwezo wa kuifanya tena kazi ya uu mbaji na kuvifufua na kuvihuisha na kuvirudisha kama vilivyo kuwa.

Kwa hivyo ataihuisha mifupa nayo ikiwa imebadilika na kuwa mchanga kama alivyo iumba hapo kabla na haikuwa ni chochote. Na hilo si la ajabu maadamu yeye Mwenyezi Mungu "ndiye ambae aliviumba vitu kwa mara ya mwanzo", nae ndie ambae ameiumba mbingu na ardhi na hakuchoshwa na kuviu-mba na ni mwingi wa kuumba na mjuzi".

Ametakasika yule ambae ufalme wa kila kitu umo kwenye miliki yake" "Ametakasika mola wa walimwengu". Na hii ndio mantiki ya akili na maumbile na dhamiri, vikiwa vime epukana na aina yoyote ya shaka na dhana.

Ama mwenye shaka na kujitatiza kwenye ukweli huu ulio wazi hatumzingatii kuwa ni mwenye shaka kuhusu marejeo ili tuweze kuingia kwenye mazungumzo yenye kumuhusu, bali shaka yake hii inajulisha kutokuwa mkweli kwenye madai yake ya kuamini kuwa Mwenyezi Mungu ndie Muumbaji wa mwanzo, na wakati huo hatastahili kutaka zitolewe dalili kuhusu suala la marejeo au kudai kulipinga suala hilo au kutokinaika na suala hilo, bali inampasa atafute dalili za kuamini kwa uumbaji wa mwanzo, na muumbaji wa mwanzo, kwa kuzingatia kuwa marejeo -kama tulivyo tangulia kusema- ni kurudia kufanya kitu ambacho hapo kabla kilikwisha tengenezwa na kutokea, na Imani ya hayo yaliyo tangulia inapothibiti kwa kukinai na kwa yakini kutakuwa hakuna shaka kamwe katika kuthibiti marejeo.

Huenda kukawa na mwenye kutoa pingamizi kuhusiana na haya yaliyo tangulia na akasema: "Hakika kupinga kwetu suala la marejeo sio kupinga kuumba kwa Mwenyezi Mungu na kuviweka kwake viumbe, bali ni kusalimu amri juu ya hukumu ya akili katika hukumu yake kuwa ni muhali kurejea, baada ya mwanadamu kutokana na kifo chake kuwa ni kitu kilicho potea na kutoweka, na nijambo lililo wazi kuwa kilicho kwisha potea na kutoweka ni muhali kukirudisha, na sijambo la kiakili mtu mwenye akili kuamrishwa kuamini mambo yasiyo wezekana (yaliyo muhali).!

Huu ndio muhtasari na ufupi wa shub'ha ambayo wenye kuikubali ni wengi na waisemayo ni wenye kuhesabika, baada ya jambo hilo kuwatatiza na kuchanganya kati ya hili na lile au wakaghafilika kunako maana ya kweli ya kifo na marejeo.

Lau kama wenye shub'ha (shaka inayofanana na haki) hiyo wangetaka kuzama na kuliangalia kwa ndani, kidogo wangeweza kuelewa uwazi wa jambo hilo, kwani ingemuwia wazi ya kuwa kifo kilivyo, si kutoweka viungo vya mwanadamu, bali ni kuvitenganisha na kuvisambaza viungo vile, na baadhi ya watu walidhani ya kuwa mwili baada ya kuachana na kusambaa vinapotea na kutoweka haviwi tena, lakini ukweli ni kuwa viungo hivyo vipo vikiwa vimetawanyika na chembe zake kusambaa, na Mwenyezi Mungu anapotaka kuvirudisha atavikusanya kwa uwezo wake viungo hivi vilivyo sambaa na kuviunganisha na kuviweka kwenye hali yake ya mwanzo ukiwa ni mwili na roho na sifa zake, na hayo ndio marejeo (kiama).

Na tunaelekezwa na kuongozwa mwongozo bora kwenye maana hii na maneno yaliyo zungumzwa kwenye Qur'an tukufu kutokana na suali la Ibrahimul-Khalil(a.s) alipo muuliza Mola wake kwa kusema: "Nionyeshe vipi unawahuisha wafu"?

Na jawabu la Mwenyezi Mungu aliyetakasika kwa Ibrahim lilikuwa ni kauli yake "Chukua ndege wanne wakatekate" yaani Ibrahim awakatekate vipande vidogo vidogo na avichanganye vyote uchanganyaji ambao hauwezi kutofautisha wala kutengani-sha kati ya ndege wale,"Kisha weka juu ya kila mlima kati ya vipande hivyo kipande kimoja" yaani kipande kimoja kati ya vile alivyo vichanganya, kisha waite, watakujia wakitembea kwani Mwenyezi Mungu atapambanua viungo vya kila ndege kuvito-fautisha na ndege mwingine, na kukusanya kila kipande kuki-weka na chenzake vikijitenga na vinginevyo, na kuviwekea uhai wakati ndege anapo kamilika kwenye umbo lake maalumu.

Na mfano huu wa Qur'ani ulio makini na ulio wazi ya kuwa kifo ni sawa na kuvitenganisha viungo na sio kutoweka kama wadhaniavyo baadhi ya wapingaji.

Kwa hivyo basi, kwenye jambo hili hakuna maana yoyote kati ya maana za kutowezekana na kuwa muhali wala shub'ha yoyote kati ya shub'ha zipingazo kwa kusema ni jambo lisilowezekana kiakili kama wanavyodai baadhi ya watu hao.

Kutokana na kuwa marejeo, kama tulivyo tangulia kusema, yana maana ya kurudi kwa watu wote, baada ya kufa kwa malengo ya kufanyiwa hesabu na kuhukumiwa, kisha kupewa thawabu (yaani malipo mema) na kuadhibiwa kutokana na matokeo ya hukumu ile "Na tutawafufua na hatutamuacha miongoni mwao yeyote" "Siku ambayo kila nafsi itayakuta iliyo yatenda kati ya mazuri yakiwa yameletwa mbele yake, na maovu aliyo yatenda".

Hakika marejeo haya ni lazima yatanguliwe na kumalizika kwa ulimwengu na vyote vilivyomo, vitu na wanadamu kiasi kwamba uhai utasimama kufanya kazi na vyote vilivyo hai kufariki "siku ambayo tutaikunja ardhi kama ukunjaji wa kurasa zenye maandishi" "siku ambayo ardhi itabadilishwa tofauti na ardhi hii, na mbingu (vile-vile)".

Je hilo linawezekana kiakili? Na je elimu ya kisasa inaweza kutuongezea na kutuelekeza kwenye uwezekano huu kutokana na kufungukiwa na nyanja mbali mbali na sehemu nyingi za ugunduzi wa vitu au habari zisizo julikana na kutoa habari za mambo yatakayo tokea siku za usoni?

Profesa Frank Allen anasema:

"Hakika kanuni za mwendo wa joto (dynamic law), zinajuli-sha kwamba vitu vitoavyo nguvu kwenye ulimwengu huu vinapotelewa na kuondokewa na joto lake taratibu, na kwamba vitu hivyo vinaelekea kwenye siku ambayo vitakuwa vyote kwenye siku hiyo, chini ya kiwango cha joto cha chini kabisa ambacho ni sifuri, na siku hiyo nguvu yote itakosekana na itakuwa ni muhali kuwepo uhai. Hakuna budi kutokea kwa hali hii ya kutoweka kwa nishati zote (energy) wakati kiwango cha joto cha vitu kitakapo-fikia chini ya sifuri kwa kupita kwa muda".

Naye Profesa Edward Luther Keel anasema:

"Kuna uhamaji wa joto wenye kuendelea kutoka kwenye vitu vya joto na kuhamia kwenye vitu vya baridi, na haiwezekani kutokea kinyume kwa nguvu za kidhati (ya kibinafsi) kiasi kwamba joto likarudi (lenyewe binafsi) na kuhama kutoka kwenye vitu baridi kwenda kwenye vitu vyenye joto. Na maana ya hayo ni kwamba ulimwengu unaelekea kwenye kiwango cha joto ambacho vitu vyote vitakuwa na kiwango cha joto kilicho sawa na ndani yake nguvu ya usaidizi. Na siku hiyo hakutakuwa na kazi ya kemia au maumbile, na hakutakuwa na athari ya uhai wenyewe kwenye ulimwengu huu".

Naye Profesa Claud M.Nathaway anasema:

"Sir (bwana) Isack Newton alikuja kufahamu ya kuwa nidhamu ya ulimwengu huu inaelekea kwenye kusimama (kuisha) na kuwa inakaribia kwenye hatua ya kiwango cha joto cha vitu vingine (vitoavyo nguvu) kuwa sawa na utafit i wa joto umeunga mkono rai hizi na umetusaidia kupambanua kati ya nishatiweza (energy potential) na isiyoweza, na imegundulika kwamba kunapo tokea mabadiliko yoyote ya joto hakika sehemu fulani ya nishatiweza, na kwamba hakuna uwezekano mwingine ila kuwa na mabadiliko haya kwenye maumbile kwa njia ya kinyume".

Naye Boltsman alitilia umuhimu uchunguzi wa kutaka kufahamu hali hii, na katika uchunguzi wake akatumia uwezo wake wote wa kugundua na vipimo vyake vya mahesabu, hadi akathibitisha kuwa kukosekana kwa nishati weza (energy potential) ambayo ina ashiriwa na kanuni ya pili ya mwendo joto ya joto (dynamic law of heat), si jambo lingine isipokuwa ni hali mahsusi katika matukio mengi ya jumla inayo ashiria kuwa mabadiliko yoyote au mgeuko wa kimaumbile hufuatiwa na hali ya kuzorota au kuwepo upungufu kwenye nidhamu ya ulimwe-ngu. Na katika hali ya joto kubadilika kwa nishati kutoka kwenye nishati weza na kuwa nishati isiyo weza, huchukuliwa kuwa ni ukosefu au upungufu wa nidhamu katika kiungo fulani au kwa ibara nyingine, ni kuzorota na kuharibika kwa jengo".

Naye Dr Muhammad Jamalud- din Afandi:

"Wataalamu wa sayari wote wanasisitiza ya kuwa jua, kama sayari nyingine yoyote ni lazima ipatwe na hali ya kuzidi kwa ghafla kwenye joto lake na ukubwa wake na miaka yake kwa kiwango ambacho akili haiwezi kukikubali, na wakati huo anga lake la nje litapanuka pamoja na vilivyomo ndani ya anga lake, navyo ni moto na moshi hadi kuufikia mwezi na kusababisha kasoro kwenye uwiano (nidhamu) wa jamii ya sayari zote. Na kila jua kwenye anga (mbinguni) ni lazima lipitie kwenye hali kama hizi kabla halijafikia kwenye uwiano wake wa daima, na jua letu kwa dhati yake halijapitia mzunguko huu bado.[155]

Amesema mwenyezi Mungu mtukufu:

"Basi ingoje siku ambapo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri " "Suratud- dukhan:10"

"(Itakuwa siku hiyo) wakati litakapo parama jicho, na mwezi utakapo patwa, na jua na mwezi kukusanywa, siku hiyo mtu atasema makimbilio yako wapi "? "Suratul-Qiyamah:7-10".

"Na ardhi na majabali yatabebwa na kupigwa pigo moja" "Suratul-Haaqqah:14". Kwa hivyo basi, siku ya marejeo na dalili zake na kila litufahamishalo kuhusu siku hiyo, kama vile kumali-zika kwa ulimwengu na kutoweka kwa uhai, ni siku ambayo inawezekana kutokea kwa hali yoyote, bali ni jambo la lazima na lisilo na shaka kwenye ufahamu wa kielimu ya kisasa.

Na elimu ya kisasa ikiwa imezidi kutupa matumaini ya ukweli huu basi hakika baadhi ya wanafalsafa wa zamani ambao elimu haikuwasaidia kwenye zama zao kuweza kufahamu ukweli, walishikilia na kuchukua kauli zisemazo kuwa ulimwengu utabakia kwenye hali yake ya hivi sasa bila kumalizika wala kuondoka, kwa kutoa ushahidi wa jua juu ya hayo, ambalo pamoja na kuwa lina umri mrefu sana, halijatokewa na mabadi-liko yoyote yanayoashiria kupungua au kuyayuka kwake na haya yana maana kwamba litabakia milele na milele, kwani lau kama lingekuwa limepangiwa kumalizika kungedhihiri kwenye jua hilo vitu vijulishavyo kumalizika huko kama upungufu au kubadilika au kuyayuka.

Ubatilifu wa madai haya unakuwa wazi kutokana na kufaha-mu uhakika ufuatao:

01- Hakika kanuni ya diynamic ya joto imetufahamisha ya kuwa joto halitadumu milele, na kwamba siku ya kumalizika kwake ambako kutapelekea kumalizika kwa ulimwengu bila shaka yoyote itakuja na kutokea kama tulivyo elezea kwa upana.

02- Hakika wachunguzi wametoa habari za kutokea kwa milipuko mingi juu ya anga la jua kwa kiwango cha masafa makubwa sana na mapengo yamedhihiri katika sehemu zilizoto-kea milipuko hiyo ambayo haiwezi kufasiri isipokuwa kwa kusema kuwa ni kulika (kuisha) kwa sayari ya jua

03- Wataalamu wa sayari kusisitiza kwa hali ya kupanuka anga la nje la jua hadi kufikia kwenye mwezi, kiasi kwamba uwiano wa sayari zote unaingiwa na kasoro, kama tulivyo tangu-lia kusema.

Na maana ya yote hayo ni kuwa kumalizika kwa ulimwengu ni jambo la lazima, hakuna makimbilio, na kwamba kauli ya kubakia milele kwa jua ni kauli isiyo kuwa na dalili yoyote.

Ama dalili ya wale wasemao ya kuwa hakuna marejeo kwa kutumia kanuni ya kuwa "Madda haimaliziki" ili kuyafanya sahihi madai yao, ni dalili yenye kupingwa kwa hali yoyote ile kwa sababu kauli isemayo kutomalizika kwa madda, imekuwa ni miongoni mwa kauli za zamani, ambazo elimu imezivuka na kusema kuwa itamalizika. Na sawa mada imemalizika au haikumalizika, kwani mas'ala haya hayana mahusiano yoyote na maudhui ya bahthi yetu, kwa sababu marejeo ni mabadiliko kwenye sura ya madda na sio kumalizika kwake.

Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu "Siku itakayo badili-shwa ardhi isiwe ardhi hii na mbingu hii" na ni tofauti kubwa iliyopo kati ya kubadilika na kumalizika.

Na muhtasari wa kauli ni kuwa:

"Hakika kiama kitakuja, hakuna shaka ndanyi yake, na Mwenyezi Mungu atawafufua waliomo makaburini".

"Na hakika wale ambao hutia shaka kuhusu kiama wako kwenye upotevu wa mbali na siku kitakapo simama kiama siku hiyo watapata hasara wenye kubatilisha ( kuwepo kwa kiyama)".

Na kiyama hicho kitakuja "pindi ardhi itakapofikia kileleni mwa utamaduni wake na mwanadamu kufikia mwisho wa maendeleo yake, na ardhi kuchukua mapambo yake, na mwana-damu kudhania ya kuwa anakihukumu kila kitu na akawa ni mwenye uwezo wa kufanya kila kitu, basi yeye akawa ana hukumu na kutawala suala la mvua, na kupandikiza au kulima kwenye ardhi yenye changalawe, na kwenye jangwa na kuhami-sha nyoyo na macho kutoka kwa wafu na kuwawekea watu walio hai, na akawa anasafiri kwenye sayari na anapasua chembe chembe za atom, na anahamisha majabali. Hakika Mwenyezi Mungu anatuahidi kwa kutuonya.

Hadi ardhi itakapo pambwa na kuwa vitu vya kuvutia na watu wake kudhania kuwa ni wenye uwezo juu yake, itawajia amri yetu usiku na mchana na tutawafanya kuwa kama mavuno kana kwamba hayakuwa ni mimea siku ya jana.

Na katika aya hii kuna uzuri (jamala) na siri (fumbo). Mwenyezi Mungu anasema, hakika kiama kitakuja usiku au mchana, na hakuna tafsiri ya maneno hayo isipokuwa ardhi iwe kama tufe la duara, nusu yake ni usiku na nusu nyingine ni mchana, basi kitakapo kuja kiama, nacho kitakuja ghafla,"na hakikuwa kiyama isipokuwa ni kama kupepesua jicho au karibu zaidi ya hivyo", nusu ya wakazi wake watakuwa kwenye usiku na nusu ya pili watakuwa kwenye mchana.

Kisha Qur'ani inatufikisha kwenye alama ya mwisho kati ya alama za kiama nayo ni kupulizwa kwa balagumu na kusimama kwa kiama.

Na matukio ya kiama yanayo simuliwa na Qur'an ni ya kutisha, kwa kuyasikia damu huganda kwenye mishipa kwamba jua litapatwa na mwezi kushikwa na majabali yatang'oka na nyota zitatawanyika, na mabahari yatapasuka, na ardhi itat ete-meka na viumbe hai vyote ardhini na mbinguni vitapiga kelele.

Yatatokea haya wakati wa kupulizwa parapanda la mwanzo. Na likipulizwa kwa mara ya pili watafufuka wote na kuanza hesabu.[156]

"Na kitabu kitawekwa, na utawaona waovu wakiyaogopa yaliyomo ndani yake, na wakisema:"Ole wetu kina nini kitabu hiki hakiachi jambo dogo wala kubwa isipokuwa hulihesabu". Na watayakuta mambo waliyo yatenda yakiwemo, na Mola wako hamdhulumu yeyote ". (Suratul-kahfu :49).

"Na kitabu kitawekwa na wataletwa manabii na mashahidi na itatolewa hukumu kati yao kwa haki, na wao hawatadhulumi-wa. Na itapewa kila nafsi malipo ya matendo iliyo yatenda, na yeye ni Mjuzi zaidi wa mambo wayafanyayo ". "Surat-uz-zumar: 69-70".

AMESEMA KWELI MWENYEZI MUNGU ALIE TUKUKA NA ALIE ADHIM

SHARTI YA KUCHAPA

Sharti ya kuchapa au kusambaza ni kutaja rejeo hili. haki zote zimehifadhiwa na Taasisi ya Al-Hasanain Taasisi ya Imamu Husein(a.s)

Site ya Al-Imaamaini Al-Hassanaini(a.s) ya usambazaji wa utamaduni wa Kiislamu na mafunzo ya Kidini.

MWISHO WA KITABU

YALIYOMO

USUULID DIIN 1

UIMAMU 1

UTANGULIZI 1

UIMAMU KWA MAANA YAKE YA UJUMLA 3

DALILI YA KUTEULIWA KWA IMAMU 12

DALILI YA KWANZA: 12

DALILI YA PILI: 14

HADITHI YA TATU: 16

MAIMAMU (REHMA NA AMANI ZIWE JUU YAO) 20

IMAMU WA KWANZA 21

ALI BIN ABI TWALIB(a.s) 21

USUULID DIIN 23

UIMAMU 23

IMAMU WA PILI 23

HASSAN BIN ALI(a.s) 23

IMAMU WA TATU 24

HUSSEN BIN ALY(a.s) 24

IMAMU WA NNE 26

ALI BIN HUSSEN(a.s) 26

IMAMU WA TANO 27

MUHAMMAD BIN ALI(a.s) 27

IMAM WA SITA 28

JAAFAR BIN MUHAMMAD(a.s) 28

IMAM WA SABA 30

MUSSA BIN JAAFAR(a.s) 30

IMAMU WA NANE 31

ALI BIN MUSSA(a.s) 31

USUULID DIIN 33

UIMAMU 33

IMAM WA TISA 33

MUHAMMAD BIN ALI(a.s) 33

IMAMU WA KUMI 34

ALI BIN MUHAMMAD(a.s) 34

IMAMU WA KUMI NA MOJA 35

ASSAN BIN ALI(a.s) 35

IMAMU WA KUMI NA MBILI 36

MUHAMMAD BIN HASSAN(a.s) 36

MAHDI MTARAJIWA KATI YA TASWAWWUR NA TASDIQ 39

KUMFAHAMU NA KUMSADIKI 39

UTANGULIZI 39

MUHAMMAD HASSAN AALU-YAASIN 40

USUULID DIIN 43

UIMAMU 43

SEHEMU YA KWANZA 43

SEHEMU YA PILI 48

MAHDI NI NANI? 48

USUULID DIIN 58

UIMAMU 58

SEHEMU YA TATU 58

NYONGEZA 65

BARUA YA SHEKH AL-KASAM 65

JAWABU LA BARUA 67

USUULID DIIN 69

MAREJEO YA KIAMA 69

MAREJEO YA KIAMA 69

UTANGULIZI 69

MAREJEO NI LAZIMA 72

USUULID DIIN 81

MAREJEO YA KIAMA 81

UWEZEKANO WA KUWEPO MAREJEO NA DALILI ZAKE 81

SHARTI YA KUCHAPA 88

MWISHO WA KITABU 88

YALIYOMO 89