• Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18910 / Pakua: 2149
Kiwango Kiwango Kiwango
MAISHA YA ABU DHARR

MAISHA YA ABU DHARR

Mwandishi:
Swahili

MAISHA YA ABU DHARR

KIMEANDIKWA NA: KIKUNDI CHA WANACHUONI ISLAMIC SEMINARY PUBLICATIONS

KIMETARJUMIWA NA: AL-AKH SALMAN SHOU

KIMEHARIRIWA NA: USTADH ABDALLAH MOHAMED

NENO LA MCHAPISHAJI

Kitabu kilichoko mikononi mwako, ni tarjuma ya kitabu cha Kiingereza, kwa jina la: "Abu Dharr"

Kitabu hiki kinahusu maisha ya Sahaba mkubwa na mashuhuri; Abu Dharr (Jundab bin Junadah). Abu Dharr alikuwa mtu wa tano kuingia kwenye Uislamu na upanga wake ulikuwa unafaa sana katika kuendeleza Uislamu. Aliona mikengeuko mingi katika Uislamu tangu kuanza kwake, na baada ya kifo cha Mtukufu Mtume mambo hayakuwa mazuri. Alishuhudia mitafaruku mingi wakati wa makhalifa watatu wa mwanzo kiasi kwamba hakuweza kuvumilia, na alianza kukemea maovu yanayofanywa na makhalifa wazi wazi na kwa ujasiri mkubwa sana mpaka ikafikia Khalifa wa tatu kuchukua hatua za kumhamisha na kumpeleka jangwani ambako aliishi maisha ya dhiki mpaka kifo kikamkuta huko.

Kwa bahati mbaya sana wanahistoria wengi wa Kiislamu na wasio wa Kiislamu hawakuzungumza habari zake kwa kina na kama inavyostahiki kuwa. Kwa hakika Abu Dharr pamoja na Masahaba wengine kama vile Amar bin Yasir, Mikidadi, Salman Farsy, halikadhalika na ami yake Mtukufu Mtume, mzee Abu Twalib na mke wa Mtume Bibi Khadija, alikuwa ni madhulumu wa historia.

Tumekiona kitabu hiki ni chenye manufaa sana, hususan wakati huu wa maendeleo makubwa ya elimu katika nyanja zote, ambapo uwongo, ngano za kale na upotoshaji wa historia ni mambo ambayo hayana nafasi tena katika akili za watu. Kutokana na ukweli huo,

Taasisi yetu ya 'Al-Itrah Foundation' imeona ikitoe kitabu hiki kwa luhga ya Kiswahili, kwa madhumuni yake yale yale ya kuwahudumia Waislamu, hususan wazungumzaji wa Kiswahili.

Tunamshukuru ndugu yetu, Salman Shou kwa kukubali jukumu hili la kukifanyia tarjuma kitabu hiki. Vile vile tunawashukuru wale wote walioshiriki kwa njia moja au nyingine hadi kufanikisha kuchapishwa kwa kitabu hiki.

Ni matumaini yetu kwamba kitabu hiki kitakuwa ni mwanga kwa wasomaji wetu na kuzidisha upeo wao wa elimu katika dini.

KUHUSU WACHAPISHAJI

Leo hii akili yenye hadhari inaona kiakili mabadiliko ya maisha ya mwanadamu. Sayansi na teknolojia na mafanikio yao ya kushangaza yanaonekana yamefika kwenye kilele chao. Mahitaji ya kidunia hisia kali za matamanio ya mamlaka na ukubwa, ni mambo ambayo yamemwelekeza mwanadamu kwenye muflisi wa maadili mema. Katika hali hii ya kukatisha tamaa, mtu analazimika kutulia na kukadiria upya hatari zinazoweza kuwa tishio kwa mwanadamu kwa ujumla. Mwanadamu kwa mara nyingine tena ameelekeza macho yake kwa Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu kwani sasa ametambua kwamba ufumbuzi wa matatizo yake na hatima ya ukombozi wake ni mambo yaliyomo katika kufuata na kutekeleza.

Kuhama huku kutoka kwenye fikra ya mambo ya kidunia na kwenda kwenye mambo ya kiroho ni hali inayoafikiana kikamilifu na malengo na madhumuni ya seminari ya Kiislamu. Miongozo ya kidini, iliyo sambamba na maendeleo ya wakati uliopo, yanatoa kimbilio linalohi-tajiwa sana na akili inayosumbuliwa na yenye wasi wasi. ni matokeo ya ongezeko la utambuzi, kwamba imeeleweka kwamba siri ya kuishi maisha ya uadilifu hapa duniani kuelekeza kwenye furaha kamili ya milele ya maisha ya Peponi. Huu ni ujumbe wa Uislamu kwa ulimwengu wote.

Jumuiya yetu ya Kiislamu inataka kunyanyua juu mwenge wa mwongozo wa kiroho na kusaidia kwa moyo wote kutangaza urithi wa kiroho wa mwanadamu. Inaonyesha njia ya maisha kwa mujibu wa Quran katika utukufu wake ulio safi kabisa. Inaonyesha hayo tu yenye mamlaka na yaliyothabiti. Uenezi wake umebuniwa kwa jinsi inayoweza kukidhi mahitaji ya kiroho katika wakati uliopo.

Itahudumia kama chemchem ya kudumu kwa wale wenye kiu ya ujuzi. Seminari ya Kiislamu ni taasisi ya kimataifa ambayo inajaribu kuleta udugu wa Kislamu. Inapata mchango mzuri sana kutoka kwa wanachuo, kama nyongeza ya kuwa na msaada wa kimataifa kwa ajili ya kutimiza lengo lake kubwa. Inayo vituo; Asia, Afrika, Ulaya, Amerika, Canada na Mashariki ya mbali.

MPENDWA MSOMAJI

Kitabu hiki kimechapishwa na Seminari ya Kiislamu. Uenezi wake umebuniwa kwa ajili ya kuhudumia mahitaji ya kiroho katika kipindi hiki ukiwa na msisitizo mahsusi kusafisha akili na fikra ya Muislamu. Juhudi kubwa sana zimefanywa na Seminari kuweka katika machapisho yake yale ambayo yanaaminika na thabiti kweli katika Uislamu.

Unaombwa kwa ukarimu kukisoma kitabu hiki kwa moyo ambao umekusudiwa. Pia unaombwa uwe huru kuwasilisha kwetu maoni yako ambayo yatathaminiwa sana kuhusu uenezi wetu.

Kutangaza ujumbe wa Uislamu ni kazi inayotaka ushirikiano wa watu wote. Seminari inakukaribisha katika kazi hii ikikubaliana kwa furaha na Aya ya Quran Tukufu.

"Sema; Mimi ninakunasihini kwa jambo moja tu ya kwamba msimame kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, wawili wawili na mmoja mmoja. " (34:46).

Mwenyezi Mungu na akurehemu. Wako katika Uislamu.

UTANGULIZI

Baada ya miaka kumi na tatu ya mfululizo wa mateso na mapambano, Mtume wa Uislamu aliondoka Makkah na kwenda Madina. Alihisi kwamba kipindi cha uvunjaji sheria na kutangazwa kwa siri kwa Uislamu kilikwisha na kwa msaada wa masahaba wake waaminifu na jasiri angeweza kujenga jumba kubwa la dola ya Kiislamu na kuweka msingi wa serikali ya kisiyasa kama anavyotaka Mwenyezi Mungu.

Mara tu baada ya kufika Madina, Mtukufu Mtume alijenga msikiti hapo. Alijenga nyumba yake iliyotazamana na msikiti, na alifanya mlango wake wa kuingia moja kwa moja msikitini. Hapakuwepo na mabadiliko ya maisha yake tangu mwanzo hadi mwisho. Tabia, mwenendo na maadili mema yalikuwa hivyo hata baada ya kuanzisha serikali ya Kiislamu katika Arabia yote.

Mfumo wa utawala mpya na dola mpya vilitokeza na kuanza kuwepo katikati ya dola mbili za wakati huo. Kwenye Serikali hii ya Kiislamu hapakuwepo na mtawala na mtawaliwa, hapakuwepo afisa na wa chini yake, na hapakuwepo na bwana na mtumwa. Wote walikuwa sawa mbele ya Mwenyezi Mungu.

Mwasisi wa mfumo huu mpaya wa utawala alitawafu na baada ya kunyang'anywa Ali urithi na kuundwa kwa vikundi vya kisiasa, mkengeuko wa kwanza ambao ulitikisa msingi wa Kiislamu ulitokeza kwenye jambo la Ukhalifa.

Mmojawapo wa masahaba waaminifu sana na jasiri sana wa Mtukufu Mtume alikuwa Abu Dharr. Alikuwa mtu wa tano kuingia kwenye Uislamu na upanga wake ulikuwa unafaa sana katika kuendeleza Uislamu. Aliona mikengeuko yote hii. Ali ambaye alikuwa mfano halisi wa wema na ukweli, alilazimika kuishi maisha ya upweke na

maadui wa Uislamu walipe na kwenye mfumo wa Ukhalifa na walikuwa wanauharibu Uislamu kwama mchwa.

Abu Dharr alisumbuliwa sana na kushtuka na aliona kwamba hali ya Uislamu ya siku za usoni ilikuwa ya wasi wasi na kuogopesha. Hata hivyo pia aliona kwamba kwa hali yoyote ile msafara wa Uislamu ulikuwa unaendelea kwenye njia yake, ingawa haki kuu ilikuwa, mpangilio wa Kiislamu hakuvunjika kabisa. Kwa hivyo, ingawa alihuzunika na kufadhaika, alinyamaza kimya!

Mfumo wa utawala wa Uthman ulipopata uwezo kamili wa serikali ya Kiislamu, haki za wafanya kazi na Waislamu wasio jiweza zilikiuka na wala riba, wanao shughulika na watumwa, matajiri na makabaila, ambao walifika kwenye baraza la Uthman na Muawiyah. Tofauti za matabaka na kuhodhi utajiri ni tabia zilizoanzishwa tena na Uislamu uliotishiwa na hatari kubwa. Njia na tabia za Mtukufu Mtume ziliachwa. Maelfu ya dinari zilitumika kujenga Ikulu ya Muawiyah iliyoitwa (Green Palace) ya mtawala wa Kiislamu na utaratibu wa mabaraza ya Kifalme ulianzishwa. Umari aliendesha maisha yake kama mtu wa kawaida na Abu Bakr naye aliishi hivyo hivyo, ili kuendesha maisha yake, alikuwa anafanya kazi ya kukamua mbuzi wa Myahudi ambapo kidani cha mke wa Uthman, Khalifa wa tatu kiligharimu thuluthi moja (1/3) ya pato la lililoletwa kutoka Afrika.

Akichukua nafuu isiyostahili ya kazi anayofanya baba yake, mtoto wa kiume wa mmojawapo wa maofisa wa ngazi ya juu sana katika utawala wa Umari alichukua farasi wa mtu kwa lazima. Kwa upande mwingine Uthman alimteua Marwan bin Hakam kama mshauri wake mtu ambaye alipewa adhabu ya uhamisho na Mtukufu Mtume na akampa zawadi ya kiunga cha Kheybar pamoja na malipo kutoka Afrika!

Abu Dharr alipochunguza shughuli hizi za kuaibisha hakuweza kuvumilia yote haya, aliamua kufanya upinzani dhidi ya mfumo huo wa kidikteta. Yalikuwa maasi ya kijasiri na ukakamavu ambayo yalisababisha nchi zote za Kiislamu kufanya uasi dhidi ya Uthman; mawimbi yake yanayo rindima bado yanaweza kuonekana kwenye jamii nyingi za binadamu.

1

MAISHA YA ABU DHARR

Abu Dharr alikuwa na shauku ya kuanzisha mfumo wa maadili ya Kiislamu, ambapo utawala wa Uthman ulikuwa unakiuka kwa kuhuisha utawala wa kitabaka. Abu Dharr aliona Uislamu kuwa ndio kimbilio la wasiojiweza, na mafakiri waliokuwa wanakandamizwa, na Uthman aliufanya utawala wake kuwa njia ya kuwafadhili jamii ya watu wakuu na wala riba.

Ugomvi huu baina ya Abu Dharr na Uthman uliendelea, hatimaye Abu Dharr alipoteza maisha yake kwa sababu hii.

Abu Dharr alimtambua Mwenyezi Mungu Mweza wa yote; kwa hiyo kamwe hakutetereka katika njia Yake hata kwa nukta moja. Aligeuka kuwa mtu bora katika kundi la Uislamu na ndio jambo ambalo linatosha kuonyesha umashuhuri wake.

Abu Dharr ni mmojawapo wa wale viongozi na wakombozi wa uhuru ambapo mwanadamu anautaka leo hii. Hususan kwa vile utaratibu wa muda umefanyiza hali ya wasiwasi mkubwa katika ulimwengu wa uchumi na matatizo ya kiuchumi yanashughulikiwa kuwa ndio matatizo ya msingi zaidi ya maisha, maoni yake yamepata umuhimu mkubwa. Hali hiyo hiyo iliyoanzisha huko Syria na Madina kwa kuwakusanya mafakiri na wasiojiweza na kuwashawishi waasi dhidi ya wala riba na wanaohodhi utajiri, pia leo hii imejitokeza. Waislamu hapa duniani wanakumbuka maneno yake ya kuvutia, maoni sahihi na ho tuba kali. Inawezekana kwamba wanaweza kuona kwenye sehemu za mbali sana historia kwamba amewakusanya wanaokandamizwa na

wasiojiweza kwenye msikiti na ana chokonowa hisia zao dhidi ya wale waishio kwenye ikulu (majumba ya maraisi wa mataifa mbali mbali duniani) na utaratibu mchafu wa Uthman na kutangaza hadharani: "Watu hao wanao hodhi dhahabu na fedha na hawatumii katika njia ya Mwenyezi Mungu, wanapaswa kujua kwamba adhabu yao itakuwa mateso makali ." (Quran 9:34).

"Ewe Muawiyah! Endapo unajenga Ikulu hii kwa fedha yako mwenyewe ni ubadhilifu, na kama unajenga kwa kutumia hazina ya taifa, huko ni kuitwalia ."

"Ewe Uthman! Masikini wamekuwa masikini zaidi na matajiri wamekuwa matajiri zaidi. Yote haya yanasababishwa na wewe."

SURA YA KWANZA

Abu Dharr alikuwa mmojawapo wa hao masahaba wa Mtume wa Uislamu, Muhammad(s.a.w.w) ambao walikuwa wachaji Mungu na wapenda uhuru na walikuwa na tabia bora kwa mujibu wa maneno ya Mtukufu Mtume: Pepo na wakazi wa huko wanawataka haraka sana. Alifaidika kuwa na Mtume katima uhalisi wake.

Abu Dharr mwenyewe anasema: "Jina langu halisi ni Jundab bin Junadah, lakini baada ya kuingia kwenye Uislamu, Mtume alinipatia jina la 'Abdullah' na hili ndilo jina ninalolipenda hasa ."

Abu Dharr ilikuwa Kuniyah yake (kutokana na mtoto wake wa kwanza aliyeitwa Dhar).

Wanavyuoni wanakubaliana kwamba Abu Dharr alikuwa mtoto wa kiume wa Junadah bin Qays bin Saghir bin Hazam bin Ghafir na mama yake alikuwa Ramlah binti Wafiah Ghifariah. Alikuwa wa jamii ya Kiarabu na alikuwa wa kabila la Ghifar. Ndio sababu ya neno 'Ghifar; limeandikwa na jina lake.

Abdullah al-Subaiti ameandika: "Tunapoangalia wasifu wa Abu Dharr inaonekana kama vile ni nuru iliyopewa umbo la Binadamu. Alikuwa mfano halisi wa sifa za mtu mashuhuri. Alikuwa na sifa pekee ya akili, uelewa, busara na werevu." Kwa maneno ya Imamu Jafar Sadiq: "Wakati wote alikuwa katika tafakuri na Swala zake ziliegemezwa kwenye mawazo kuhusu Mungu ." (Sahih Muslim).

Mwandishi maarufu wa Misri Abdul Hamid Jaudatus Sahar, kwenye kitabu 'Al-Ishtiraki az-Zahid, ameandika: Wakati fulani ilitokea njaa kali. Watemi wa kabila la Ghifar walikusanyika kwa ajili ya kushauriana ili wapate ufumbuzi wa tatizo hilo kwa sababu ya ukame wa muda mrefu. Kwa hiyo hicho kilikuwa kipindi cha mateso makubwa. Wanyama walikonda na akiba kwenye maghala ilikwisha. Waliambizana wao kwa wao, 'Hatujui kwa nini Mungu wetu (Sanamu Manat) amekasirishwa na nini kutoka kwetu, ingawa tumeomba mvua, tumetoa sadaka ya ngamia na tumefanya kila linalowezekana ili atupendelee.

Msimu wa mvua sasa umekwisha. Hakuna hata dalili ya wingu angani. Hapajatokea mngurumo na rasha rasha ya mvua kipindi hiki, hakuna hata tone la mvua au manyunyu. Unafikiria nini? Tumekuwa wapotevu hivyo kwamba ghadhabu ya mungu wetu imetuangukia? Kwa nini ahisi amekosewa na sisi ambapo tumetoa sadaka nyingi kwa ajili ya kumfurahisha yeye?"

Watu walianza kutafakari juu ya jambo hili na kubadilishana mawazo. 'Binadamu hawezi kuingilia mipango ya Mbinguni. Hakuna

mtu yeyote anayeweza kuleta mawingu ya mvua kutoka angani. Anayeweza kufanya hivyo ni 'Manat' tu. Kwa hiyo hatuna njia nyingine isipokuwa sisi, wanaume na wanawake, twende Hija huku tunalia kwa huzuni na kusali na kumwombea kwa huzuni na kusali na kumwomba Manat atusamehe. Labda inawezekana akatusamehe na mvua ikaanza kunyesha na kuifanya ardhi kuwa kijani kibichi baada ya ukame, ili umasikini wetu ubadilike kuwa mafanikio, uchungu kuwa furaha na matatizo kuwa raha na starehe."

Kwa hiyo, kabila lote lilianza matayarisho ya safari ya kwenda kumuona Manat. Wale waliokuwa wamelala waliamka na kuweza kuweka mito ya kukalia juu ya migongo ya ngamia wao. Unais (ndugu yake Abu Dharr) naye pia alipanda ngamia wake na kumwendesha, ili aungane na msafara, karibu na Pwani ya bahari, Mushalsal na Qadid sehemu zilizomo kati ya Makkah na Madina, ambapo ndipo Manat alipo.

Unais alitazama huku na kule lakini hakumuona kaka yake. Alimbembeleza ngamia akakaa chini. alikimbia kuelekea nyumbani. Aliingia ndani huku akiita 'Jundab!

Mara tu Unais aliposikia hivyo, alikimbia kwenda huko. Alipofika hapo, alimuona mtu anasema, "Sifa zote zinastahiki kwake Mwenyezi Mungu. Ninamsifu Yeye na ninahitaji msaada Wake. Ninamwamini Yeye, ninamtegemea Yeye na ninashahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu na Hana mshirika."

Katika nukuu ya Subaiti, Unais alimsikia mtu huyo akitangaza, "Enyi watu! Nimekuleteeni neema ya dunia hii na baada ya maisha haya. Semeni kwamba hapana mungu isipokuwa Allah ili muweze kupata ukombozi. Mimi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na nimekuja kwenu. Ninawaonya kuhusu adhabu ya siku ya Hukumu. Kumbukeni kwamba hakuna mtu atakayepata kuokolewa isipokuwa yule anayekuja mbele ya Mwenyezi Mungu kwa moyo wa unyenyekevu. Wala utajiri hautakuwa na manufaa kwake, ama watoto hawatawasaidieni. Mwogopeni Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu atakuwa mwema kwenu. Enyi watu! Nisikilizeni! Ninasema wazi kabisa kwamba mababu zetu walifanya upotovu kwa kuacha njia iliyonyooka na kuanza kuabudu masanamu haya na nyinyi mnafuata nyayo zao. Kumbukeni kwamba masanamu wala hayawezi kuwaumizeni ama kuwanufaisheni. Wala hayawezi kuwazuieni ama kuwaongozeni."

Unais aliposikia hotuba hii yenye ushawishi mkubwa alishangaa. Lakini katika kustajabu kwake aliona kwamba watu walikuwa wanasema mambo tofauti dhidi yake.

Aliposikia Mtume alisema, "Mitume hawasemi uongo. Ninaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu mbali na Yeye, kwamba nimetumwa kwenu kama mjumbe. Kwa jina la Mwenyezi Mungu mtakufa kama mnavyolala na mtafufuka kama mnavyoamka. mtaitwa kuhesabiwa matendo yenu. Halafu mtapewa Pepo au Jahanamu ya milele!"

Aliposema hivi watu walimuuliza Mtume, watafufukaje baada ya kuwa vumbi?

Wakati huu huu Mwenyezi Mungu aliteremsha Aya zifuatazo: "Sema: Kuweni hata mawe, na chuma. au umbo lolote mnaloliona kubwa katika vifua. Watasema: Nani atakayeturudisha tena? Sema: Yule aliye kuumbeni mara ya kwanza! Watakutikisia vichwa vyao, na watasema: Lini hayo? Sema: Asaa yakawa karibu! " (17:50-51).

Mara tu Mtume alipomaliza hotuba yake watu walinyanyuka. Wakati walipokuwa wanasambaa, mmoja wao alisema: "Huyu ni mtabiri?" Mwingine akasema, "Huyu ni mchawi."

Unais alimsikiliza Mtume na watu. Aliinamisha kichwa chake kwa muda fulani na akanong'ona: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu maneno yake ni matamu. Hayo aliyoyasema ni kweli na watu wanaompinga ni wapumbavu."

Halafu akapanda ngamia wake akaanza safari ya kuelekea kwao. Aliendelea kufikiria kuhusu Muhammad, Mtume wa Mwenyezi Mungu wakati wote wa safari yake, na alikuwa anashangaa kuhusu mazungumzo yake, hadi alipoonana na Abu Dharr.

Abu Dharr alipomuona Unais, alimuuliza kwa shauku kubwa, "Kuna taarifa gani? Uliona nini Makkah?"

Unais: "Wanasema kwamba mtu huyu ni mshairi, mchawi na mtabiri. Lakini nilipochunguza mazungumzo yake kulingana na wale wanaosema kuwa ni mshairi, niliona kwamba maneno yake si mashairi wala si utabiri kwani nimewahi kukutana na watabiri wengi, na mazungumzo yake si sawa na yale ya watabiri.

Abu Dharr: "Hufanya nini na husema nini?"

Unais: "Husema mambo ya ajabu."

Abu Dharr: "Huwezi kukumbuka chochote katika yale aliyosema."

Unais: "Kwa jina la Mwenyezi Mungu! Hotuba yake ilikuwa tamu sana lakini sikumbuki chochote zaidi ya yale ambayo nimekwisha kwambia, lakini nimemuona anasali karibu na Al-Ka'abah, na pia nimemuona kijana moja mwenye sura ya kupendeza ambaye haja-balekhe, akisali pamoja naye. Watu wanasema kwamba huyo ni binamu yake Ali. Pia niliona mwanamke anasali nyuma ya mtu huyu. Watu waliniambia huyo ni mke wake, Khadijah.

SURA YA PILI

Baada ya kumsikiliza kaka yake, Abu Dharr alisema, "Sijaridhishwa na ripoti yako. Nitakwenda huko mimi mwenyewe, nimuone na nimsikilize mimi binafsi."

Abu Dharr alifika Makkah, aliingia kwenye eneo la Ka'abah na akaanza kumtafuta Mtume, lakini wala hakumuona pale, ama kusikia akitajwa. Alikaa hapo hadi machweo ya jua. Ali aliwasili hapo na akapita karibu na pale alipoketi Abu Dharr. Alimuuliza, "Unaonekana kuwa msafiri. Ni kweli?"

Abu Dharr: "Ndio." Ali: "Njoo nifuate."

Ali alimchukua nyumbani kwake. Wote wawili walikuwa kimya wakati wanakwenda nyumbani kwa Ali. Abu Dharr hakumuuliza Ali kitu chochote hadi walipofika nyumbani. Ali alitayarisha mahali pa kulala na Abu Dharr akalala. Kesho yake asubuhi alikwenda tena Ka'abah kumtafuta Mtume. Wala hakumuuliza mtu yeyote ama mtu

yeyote kumwambia chochote. Abu Dharr aliendelea kungoja kwa hamu kubwa hadi mwisho wa siku. Ali alikwenda tena kwenye Al-Ka'abah kama kawaida yake na alipita mbele ya Abu Dharr: mara alipomuona Abu Dharr, alimuuliza: "Kwa nini hujaenda nyumbani hadi sasa?"

Abu Dharr: "Hapana."

Ali: "Vema! Sasa twende nifuate Mimi."

Wote walili walikuwa wanakwenda kimya Ali alipouliza, "kwa nini!

Umekuja hapa kwa sababu gani?"

Abu Dharr: "Ninaweza kukuambia sababu endapo hutamwambia mtu

mwingine."

Ali: "Sema wazi chochote unachotaka kusema. Sitamwambia mtu yeyote."

Abu Dharr: Nimekuja kumuona mtu baada ya kupata taarifa kwamba mtu huyu anajiita yeye Mtume. Nilimtuma kaka yangu azungumze naye. Aliporudi hakunipa taarifa ya kuridhisha. Sasa, nimeamua kumuona mtu huyu mimi mwenyewe."

Ali: Umefika. Sasa ninakwenda pale alipo. Nifuate. Ingia popote nitakapoingia. Endapo nitaona hatari yoyote nitaanza kukiweka sawa kiatu changu, nikiwa nimesimama karibu na ukuta, na nikianza kufanya hivyo, wewe rudi."

2

MAISHA YA ABU DHARR

Abu Dharr anasema, "Ali alinipeleka hadi ndani ya nyumba. Niliona nuru katika umbo la mtu inaonekana hapo. Mara tu nilipo muona, nilivutiwa kwake na nikahisi ninataka kubusu miguu yake. Kwa hiyo, nilimsalimia Assalamu Alaykum." (Alikuwa mtu wa kwanza kumsalimia Mtume wa Uislamu kwa desturi ya Kiislamu, kabla ya kusilimu).

Alijibu salamu, akasema, "Waa Aliakum as Salam, wa rahmatullah

wa Barakatuh. Ndio Unataka nini?"

Nilijibu; "Nimekuja kuwako kwa moyo na imani."

Alinielekeza mambo fulani muhimu na akanitaka nikariri Kalimah

(Shahada) yaani (La ilaha illalah Muhammadun Rasulul lah) nilisoma

hivyo, na kwa hiyo nikaingia kwenye Uislamu.

Baada ya hapo, aliondoka kwenda Ka'abah. Alipofika hapo alipoona kundi kubwa la makafiri wa kabila la Quraishi, alisema kwa sauti kubwa, "Sikilizeni enyi Waquraishi nina shahidilia kwamba Mwenyezi Mungu ni Mmoja na Muhammad ni Mtume Wake."

Sauti hii iliwaogofya Quraishi na kuvunja sanamu lao la Lat na Uzza. Hisia za Quraishi kwamba heshima ya masanamu yao imeshushwa iliwatia wasiwasi sana.

Hatimaye watu walimzunguka Abu Dharr wakaanza kumpiga sana hadi akazirai. Ilibakia kidogo afe lakini Abbas bin Abd al-Mutalib alifika hapo ghafla. Alipoona kwamba mfuasi wa Muhammad alikaribia kufa, alilazimika kumlalia Abu Dharr.

Akasema: "Enyi watu! Nini kimewatokea ninyi? Munataka kumuua mtu mkubwa wa kabila la Bani Ghifar. Mmesahau kwamba nyinyi hufanya biashara na Bani Ghifar na huwa mnatembelea huko mara kwa mara. Hamliogopi kabila lake kabisa!"

Baada ya kusikia hayo, watu hao waliondoka hapo na Abu Dharr ambaye alikuwa anatoka damu, alinyanyuka na kwenda kwenye kisima cha zam zam.

Alihisi kiu sana kwa sababu ya majeraha makubwa na kutoka damu nyingi. kwa hiyo, kwanza alikunywa maji halafu akasafisha mwili

wake. Baada ya hapo alikwenda kwa Mtukufu Mtume huku akigumia. Mara tu Mtume alipomuona katika hali ile, alisikitika sana na akasema, "Abu Dharr! Umekula au kunywa chochote?"

Abu Dharr: "Bwana wangu! Nimeona nafuu kidogo baada ya kunywa

maji ya Zam zam."

Mtume: "Bila shaka maji hayo hutoa nafuu."

Baada ya hapo alimliwaza Abu Dharr na akampa chakula. Ingawa

Abu Dharr aliumia sana kwa sababu ya hotuba yake, bado hamasa ya

dini haikumruhusu aondoke kwenda kwao kimya kimya. Imani yake

ilimtaka awafanye Maquraishii waamini kwamba akili ya

mwanadamu hudharau ushirikina wa uchaji masanamu.

Aliondoka hapo akaenda kwenye eneo la Al-Ka'abah tena. Alisimama sehemu iliyoinuka na akaita kwa sauti ya ushupavu imara. "Enyi watu wa Quraishii! Nisikilizeni! Ninashahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu na ninashahidilia kwamba Muhammad ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu."

Waliposikia hivyo wale wapotovu ambao waliona misingi ya miungu yao inatikiswa na ambao walikasirishwa sana na hotuba yake ya mwanzo, kwa mara nyingine waligutushwa na wakawa katika hali ya wasiwasi na wakageuka kuelekea upande inakotoka sauti na haraka sana walikusanyika na kumzunguka yeye. Walikuwa wanapiga kelele "Muueni huyu Ghifari haraka iwezekanavyo kwani yeye nia yake ni kuwatukana miungu wetu."

Mkusanyiko wote ulisema kwa sauti moja, Mueni Abu Dharr." Kwa hiyo walimpiga Abu Dharr hadi akazirai.

Abbas bin Abdul Muttalib alipoona hivi alijitokeza mbele na kumlalia Abu Dharr kama ilivyofanya jana yake, na akasema; "Enyi Quraishi!

Nini kimewatokeeni kwamba mnamuua mtu wa kabila la Ghifari ingawa mnao uhusiano mzuri na kabila lake na biashara yenu inaendelea vizuri kwa msaada wa kabila lake. Msiendelee kumpiga."

Baada ya kusikia haya, watu wote waliondoka na kumwacha Abu Dharr akiwa amepoteza fahamu. Alipopata fahamu, alikwenda kwenye kisima cha Zam zam! na baada ya kunywa maji alisafisha mwili wake uliokuwa umetapakaa damu.

Abdullah Subaiti ameandika kwamba ingawa Abu Dharr aliteseka sana kwa majeraha lakini hata hivyo aliwalazimisha Quraishi kuwa na maoni kwa mujibu wa ho tuba zake kwamba Uislamu ulikwisha enea kwa watu na uliwavutia sana.

Kwa ufupi Abu Dharr alinyanyuka kutoka kwenye kisima cha Zamzam na kwenda kwa Mtukufu Mtume. Mtume alipomuona Abu Dharr katika hali hiyo alisema, "Ewe Abu Dharr! Ulikwenda wapi na kwa nini umekuwa katika hali hii?" Abu Dharr alijibu, "Nilekwenda kwenye Ka'abah tena. Nilitoa ho tuba tena na nikatapakaa damu kwa kipigo. Sasa nimekuja kwako baada ya kuoga maji ya Zam zam." Mtume akasema; "Ewe Abu Dharr! Sasa ninakuamuru urudi nchini kwako mara moja. Nisikilize! Utakapofika nyumbani kwako, mjomba wako tayari atakuwa amekufa. Kwani hana mrithi mwingine isipokuwa wewe, wewe utakuwa mrithi wake na kuwa mmiliki wa rasilimali yake. Nenda ukatumie mali hiyo kwa kutangaza Uislamu. Baada ya muda mfupi nitakwenda na kuhamia Madina mji wa mitende. Wewe endelea kufanya kazi huko hadi nitakapohamia huko." Abu Dharr alisema, "Ndio! Bwana wangu vyema sana. Nitaondoka hivi karibuni na kuendelea kutangaza Uislamu." Sahih Bukhari, Sura ya Uislamu na Abu Dharr, chapa ya Misri, 1312 Hijiriya.

SURA YA TATU

Baada ya kuingia kwenye Uislamu, Abu Dharr aliondoka Makkah kwenda nchini kwake. Abdullah Subaiti ameandika kwamba Abu Dharr alipoondoka, alikuwa anabubujika imani, kamili, na alikuwa na furaha sana. Alifurahia sana kwamba Mwenyezi Mungu, alimwongoza kwenye imani ambayo imekubaliwa na waliotakasika na dhamira imeridhika nayo na akili inakaribisha kwa ukamilifu.

Aliendelea na safari hadi nchini kwake. Mtu wa kwanza kumsalimia alikuwa kaka yake Unais na pia alikuwa mtu wa kwanza kupata mwamko wa imani yake. Unais alikwenda kubusu miguu ya kaka yake na kusema, "Ewe ndugu yangu! Umepitisha siku nyingi sana Makkah sasa niambie ulichopata huko."

Abu Dharr alisema, "Unais! Nimefanya uamuzi wenye busara. Niliamua baada ya kutafakari sana kwamba lazima nikubali imani ya Muhammad! Ewe Unais! siwezi kukuambia kwamba nilipokutana na Muhammad na kumtazama uso wake, nilihisi kama vile kifua changu kilikuwa kinaongezeka. Moyo wangu ulijaa furaha na akili yangu ililewa imani. Mara nikakariri kalimah-shahada na kukubali Utume wake nilimwomba alifundishe vipengele vya imani. Kwa hiyo alinieleza kanuni za Uislamu. Ewe Unais ninakuomba kwa kweli na kwa moyo safi na nia njema uinamishe kichwa chako kwa unyenyekevu mbele ya Mwenyezi Mungu na uache kuabudu miungu hii iliyotengenezwa na mikono ya watu yenye asili ya mawe."

Aliposikia hivi, Unais alikaa chini huku akiwa ameinamisha kichwa chake na kuanza kufikiri. Alipatwa na hali kama vile umelewa. Unais alikumbuka mambo hayo yote aliyo yaona huko Makkah. Baada ya muda fulani alisema, "Ewe Ndugu! Akili yangu imethibitisha ukweli

wako na mantiki yangu inanieleza nikutii wewe. kwa hiyo sikiliza! Ninashahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu na ninakiri kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu."

Abu Dharr alifurahi sana kuona Unais anaikubali imani. Alimwambia: "Sasa twende kwa mama yetu." Wote wawili walikwenda kwa mama yao. Baada ya kumuamkia mama yao, Abu Dharr akasema, "Mama yangu mpendwa! Nakuomba unisamehe! Nimekuwa mbali na wewe kwa kipindi kirefu sana. Lakini, nimepata kitu cha nadra ambacho hakuna mtu aliye nacho hapa."

Mama Akamuuliza, "Kitu hicho ni kipi ambacho kinakubainisha wewe?" Abu Dharr alisema, "Hii ni tunu ya imani mama. Nilikutana na mtu huko Makkah ambaye uso wake uling'aa nuru ya uadilifu, hana wa kumlinganisha kwa uzuri wa tabia yake na ukarimu wake. "Yeye husema kweli tupu. Yeye husema kilicho sahihi. Hutenda haki. Maneno yake yanayo busara. Mama! Maadui zake pia humwita mkweli na mwaminifu. Huwaita watu wamwelekee Mwenyezi Mungu ambaye ni muumba wa mbinguni na ardhi na mpangiliaji wa kuweza kudumu kwa ulimwengu huu.

"Nimekubali kumuamini mtu huyu kwa kuvutiwa na mwelekeo wake, maneno yake na semi zake, na Unais pia amekuwa Muislamu. Tumekubali Upweke wa Mwenyezi Mungu na Utume wa Muhammad."

Mama yake Abu Dharr akasema: "Mwanangu, endapo ndio hivyo, mimi pia nina shahidilia kwamba hapana mungu ila Mwenyezi Mungu, na kukiri kwamba Muhammad ni Mtume wa Mwenyezi Mungu."

Abu Dharr alitiwa moyo baada ya kaka yake na mama yake kuingia kwenye Uislamu na sasa alianza kutafakari jinsi ya kuwashawishi

watu wa kabila lake na kuwavuta waelekee kwenye njia iliyonyooka. Baada ya kufikiri sana Abu Dharr alitoka nje ya nyumba yake. Mama na kaka yake pia walikuwa naye. Baada ya kusafiri mwendo mfupi walipiga hema lao karibu na mahema ya watu wa kabila lao.

Usiku uliingia. Wasafiri hawa waliochoka walikuwa wamelala kwenye mahema yao walipohisi kwamba watu wengi wa kabila hilo waliokuwa pale walikuwa wanasimuliana hadithi wao kwa wao na kuelezea matukio mbali mbali. Walikuwa katika mazungumzo mfululizo.

Abu Dharr alipojaribu kusikiliza kwa siri walikuwa wanasema nini, alisikia kwamba walikuwa wanamsema yeye. Baada ya hapo watu waliondoka kutoka kwenye mahema yao na kwenda kwenye hema la Abu Dharr, akamwambia kaka yake, Unais, "Watu wa kabila letu wamekuja karibu na hema letu. Nenda nje ukawaone."

Unais alitoka nje mara moja. Aliwaona vijana wa kabila hilo walikuwa karibu na hema. Walikwenda karibu na hema ili wajue endapo Unais na Abu Dharr walikuwa hapo. Walimsalimia. Baada ya Unais kujibu salamu yao, aliwauliza sababu ya wao kutembelea hapo. Wakasema, "Tumekuja tu kukuona wewe na Abu Dharr."

Unais alirudi ndani na akamwambia Abu Dharr, "Vijana wa kabila letu wamekuja kutaka kujua hali ya safari."

Abu Dharr alisema, "Waambie waingie ndani. Nitazungumza nao. Inawezekana labda nikawasilimisha waanze kumuabudu Mwenyezi Mungu, Aliye Pekee."

Unais alitoka nje na akawaambia, "Ingieni ndani kwani kaka Abu Dharr anawaiteni."

Wote walikwenda kwa Abu Dharr. Mmojawao akasema, "Ewe Abu Dharr! Hatujakuona kwa kipindi kirefu na matokeo yake ni kwamba tunasikitika sana."

Abu Dharr akasema, "Wapendwa wangu vijana! Moyo wangu unayo mapenzi makubwa sana kwenu, na ninawahurumieni."

Mtu mmoja: "Abu Dharr! Ulikuwa wapi kwa muda mrefu hivi? Tumeshindwa kukuona kwa kipindi kirefu."

Abu Dharr: "Nilikwenda Makkah. Nilirudi siku chache zilizopita." Mtu wa pili: "Tunafurahi kwamba ulikwenda Makkah."

Abu Dharr: "Kama mambo yalivyo, nilikwenda Makkah, lakini sikutoa sadaka kwa Hubal wala sikuwasujudia Lat na Uzza. Vijana wangu! Kwa nini nifanye yote haya ambapo ninafahamu kwamba masanamu haya wala hayana uhai, ama kuweza kuumiza au kumnufaisha yeyote? Wala hayawezi kuona ama kusikia, ama kuzuia janga linaloweza kuwapata.

"Sikilizeni! Mimi nimekimbilia kwa Mwenyezi Mungu katika matendo yangu na mambo yangu yote. hakika Yeye ni Peke yake, hana mfano wala mshirika, na ninakiri kwa Mwenyezi Mungu ambaye ni Yeye peke yake anapaswa kuabudiwa, Yeye ni Muumbaji wa kila kitu na mwezeshaji wa kila kiumbe.

Ninawaomba njooni kwangu tuwe pamoja katika mpango wetu wa utekelezaji na mshahidilie Upweke wa Mwenyezi Mungu kama sisi" Waliposikia hivi, watu wote walianza kutetemeka. Mmoja wao

alisema kwa mshangao, "Ewe Abu Dharr! Unasema nini?" Abu Dharr: "Sikilizeni kwa yale ninayowaambieni ingawa siwezi kumuona Mwenyezi Mungu kwa macho yangu bado ninaweza kumuona Yeye kwa jicho langu la kiroho na sikilizeni! Inawezekanaje kitu chochote kinachotengenezwa na mikono ya mwanadamu kiwe na thamani ya kuabudiwa na binadamu? Si busara kuabudu masanamu yaliyotengenezwa kwa mawe na miti, na kuyaomba ili yatutimizie haja zetu.

"Watu wa kabila langu! mnajua kwamba masanamu haya hayana uwezo wowote. Wala hayawezi kuzuia uovu, ama kuwa na nguvu ya kupata manufaa?"

Baada ya kusikia ushawishi huu wa Abu Dharr, watu walianza kunong'onezana wao kwa wao.

Mmoja wao alisema; "Nimekwisha waambieni kwamba huko Makkah, mtu amejitokeza, anajiita yeye ni Mtume na anawaita watu kumwabudu Mwenyezi Mungu Mmoja. Abu Dharr amekutana na mtu huyu, na mahubiri ya mtu huyu yamesisimua sana hivyo kwamba fikra zozote anazozitoa Abu Dharr ni za mtu huyo."

Mtu mwingine akasema; "Hali ni mbaya sana. Sasa tupo hatarini ambayo inatujia kupitia kwa Abu Dharr na mahubiri yake. Tunadhani kwamba endapo ataendelea kuhubiri namna hii, tofauti zitajitokeza kwenye kabila letu na maisha yetu yataharibika. Ni vema twende kwa mtemi wetu Khafaf, tumwelekeze hatari zote zinazoweza kujitokeza, na tumsisitizie na alipatie jambo hili kipaumbele ili tuweze kukabiliana nalo."

Vijana wa kabila la Ghifari waliondoka nyumbani kwa Abu Dharr na walikwenda kumwona Khafaf. Wakati wapo njiani walibadilishana

mawazo wao kwa wao. Mmoja wao alisema, "Abu Dharr ameanzisha ghasia kubwa."

Mwingine akasema, "Itakuwa aibu kubwa sana kwetu kama tutaifumbia macho dhambi hii kubwa ya Abu Dharr. Anaifanyia ufisadi dini yetu waziwazi na kukebehi miungu yetu." Mtu wa tatu akasema, "Ni wajibu wetu kumfukuza kutoka kwenye kabila letu bila kuchelewa hata kidogo, kwa sababu kama tukichelewa kumtenga katika kipindi kifupi tu, atawaelemea vijana wetu, wanawake zetu, watumwa wetu na kuwatia mawazo yake maovu akilini mwao. Endapo inatokea hivyo, tutapata hasara kubwa sana."

Mtu wa nne akasema, "Maoni yako ni sahihi. Lakini, nani atamfunga paka kengele? Huyu ni mtu mashuhuri wa kabila na ni mzee wa kaya. Ninaona kwamba hata Unais anayo mawazo haya haya, na yeye pia ni mtu mwenye kuheshimiwa."

Mtu wa tano akasema, "Hakuna haja ya wasi wasi. Njooni tukamtaarifu Khafaf. Tunao uhakika kwamba Khafaf na watu wengine waungwana wa kabila ndio watakao mfukuza kutoka kwenye kabila."

Mtu wa sita akasema, "Ninatafakari kuhusu mawazo yao. Sina uhakika kama wataweza kuwabadili. Inawezekana kwamba wao ndio watakao badilika na kwenda kwenye njia iliyo nyooka tusijisumbue, lakini na tutafakari kuhusu dini yao. Nisikilizeni! Ninaona kuna ukweli kwenye imani yao. Hata hivyo karibu tutafika kwa mtemi Khafaf. Baada ya mazungumzo yetu na yeye, tunategemea kufikia uamuzi wenye msimamo."

Kwa ufupi, wakizungumza pamoja, watu hawa walifika nyumbani kwa mtemi wa kabila la Ghifar na wakamwambia, "Tumetoka kwa Abu Dharr kuja kwako."

Khafaf: "Abu Dharr amerudi kutoka safari yake ya kutoka Makkah?" Mtu mmoja akasema, "Bwana, Abu Dharr ameasi. Aliwabeza miungu wetu. Anasema kwamba yupo mtu ameteuliwa kuwa Mtume. Kazi yake ni kuwaita watu waende kumuabudu Mungu Mmoja na pia kufundisha mambo mazuri. Abu Dharr haridhiki bila kukubali utume wa mtu huyu na kuendelea na msimamo huo, lakini wakati wote anahubiri kwa watu na kuwaita wote wengine waende kwa Mtume huyo na Mungu wake.

Khafaf aliposikia, alisema, "inasikitisha kuona kwamba Abu Dharr, anawaacha miungu wote, na kutangaza kumuabudu Mungu Mmoja. Ni uovu mkubwa sana na kutia kinyaa.

Ninaona kwamba jambo hili litachochea vurugu kubwa katika kabila letu, na matokeo yake kabila litaangamia. Enyi vijana wangu! Msifanye haraka lakini nipeni, muda wa kutafakari kuhusu jambo hili la Abu Dharr."

Baada ya vijana hao kuondoka na kurudi makwao, Khafaf mtemi wa kabila, alianza kufikiri kwa nini wote walikuwa wanasema kwa kumpinga Abu Dharr. Aliendelea kutafakari usiku wote akiwa kitandani kwake. Hali ilimkanganya sana na hakuweza kufanya msimamo hasa. Lakini akili yake ilikuwa na fikra nzito kuhusu maneno yaliyosemwa na Abu Dharr. Saa nyingi zilipita bila kupata usingizi, na alikuwa anafumba macho yake.

Mtemi Khafaf pia alikumbuka hotuba ya mwanafalsafa wa Kiarabu, Qays bin Saidah, pale sokoni. Alisema kwamba Muumbaji wa ulimwengu bila shaka ni Mmoja na ni Yeye tu ndiye anaye stahiki kuabudiwa. Aliunga mkono kikamilifu maoni ya Abu Dharr kwenye hayo mahubri yake ya kusifika na pia alitamka kwamba fikra za Warqa bin Naufal, Zayd binAmr, Uthman bin Hoverath na Abdallah bin Hajash kuelekea kwenye imani ya Abu Dharr.

Alikuwa katika hali hii ya kustaajabisha ambapo akili yake ilimuongoza na akajisemea mwenyewe, 'Naam! Abu Dharr yu sahihi kwa sababu Qays bin Saida amemuunga mkono na ninao uhakika kwamba Qays hawezi akashindwa kuelewa wala kukubali itikadi yoyote ya uongo. Bila shaka, lazima atakuwepo muongozaji wa dunia hii, na lazima pawepo na nguvu yenye uwezo wa kuendesha mpangilio wote wa ulimwengu na ni dhahiri kwamba miungu wetu wa mawe na miti hawana kabisa uwezo kama huu. Ee Mungu wa Abu Dharr! Tuongoze na utukomboe kutoka kwenye uovu huu na utuweke kwenye njia ya haki."

Wakati ambapo Khafaf alikuwa anafanya uamuzi wake muhimu, siku ilipambazuka hadi jua lilionekana angani pamoja na kuenea kwa mwanga wa jua, pia habari zilizidi kuenea kwamba Abu Dharr, kaka yake na mama yake wote wamerudi kutoka Makkah na wamemuabudu Mungu Mmoja tu.

Pamoja na kuenea habari hizi hasira ilichochewa. Watu walianza kumlaani Abu Dharr na kusema, 'Amepata kichaa na hawezi kuelewa kwamba haya masanamu yetu hutuponya maradhi, yanatupatia riziki na kutulinda. Abu Dharr ni mtu wa ajabu ambaye anatuita twende kwa mungu asiyeonekana! Inaonyesha kama vile Abu Dharr anataka kuanzisha vurumai na matatizo miongoni mwa vijana wetu na kuwapotosha watoto wetu na wanawake wetu. Hakika mtu huyu ni muongo na madai yake si sahihi. Lazima afukuzwe kutoka kwenye kabila."

Mmojawao akasema, "Kwa nini! Unawezaje kuelezea wazo la kumfukuza mtu huyu? Itafanyikaje? Hapana , kamwe! Haiwezekani kutokea. Huyu ni mtu jasiri katika kabila letu."

Baada ya mazungumzo haya watu hao waliamua kutaka wasikilizwe na wazee kuhusu suala hili. Kufuatana na uamuzi wao, waliwaendea

wazee wao kushughulikia jambo hili. Wazee wao waliamua kulipeleka jambo hili la Abu Dharr kwa mtemi. Kwa hiyo, wote walikwenda kwa Khafaf.

Mtemi wa kabila alimtuma mtumwa wake haraka aende kumwita Abu Dharr. Mtumwa huyo alipofika nyumbani kwa Abu Dharr alisema, "Abu Dharr! Wewe na Unais mnaitwa na Mtemi."

Abu Dharr akajibu kwamba alikuwa tayari kwenda kwa mtemi. Mtumwa alipoondoka, Abu Dharr alichukua upanga wake na kuhifadhi kwenye mkanda na alimwambia kaka yake, Unais, "Njoo; twende kwa Khafaf!"

Unais: "Ewe kaka! Nimesikia mambo mabaya yanazungumzwa na watu kuhusu wewe. Nina hofu huu mkutano wetu unaweza usiwe na manufaa, jambo lisilotegemewa linaweza kutokea badala ya mategemeo yetu."

Abu Dharr: "Hapana, siyo. Namjua Khafaf vizuri sana. Ni mtu mwenye hekima. Mwenyezi Mungu amempa hekima. Ni mtu mwenye akili sana miongoni mwa kabila letu."

Ndugu hawa wawili waliendelea kuzungumza hadi wakafika kwa Khafaf. Hapo waliona kwamba watu maarufu wa kabila hilo walikuwa wamekaa kumzunguka Khafaf. Akawaamkia wote Abu Dharr akasema, "Salaamu Alaykum " (Amani iwe kwenu).

Waliposikia maamkizi ya Abu Dharr kwa jinsi ya Kiislamu, wazee wa kabila hilo walikasirika na walisema kwa hasira; "Salamu gani hii ambayo hatujawahi kuisikia kamwe." Halafu mmojawao akasema "Inasikitisha. Hatujui Abu Dharr anakoelekea."

Mtu mwingine akasema, "Hebu mtazame. Amekaa na upanga wake, na hana heshima kwa mtemi." Mtu wa tatu akasema, maneno yako ni sahihi. Lakini, huyu ni mpanda farasi wa kabila letu na watu jasiri wakati wote huwa tayari kwa lolote."

Abu Dharr akasema, "Silikizeni! Ninawaheshimu nyinyi kwa sababu ni watu maarufu wa kabila letu, ambao mnastahili kujivuniwa na kuwaenzi. Salaamu niliyo wapeni ni Salamu ya Kiislamu."