• Anza
  • Iliyopita
  • 21 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 21053 / Pakua: 4216
Kiwango Kiwango Kiwango
MAISHA YA ABU DHARR

MAISHA YA ABU DHARR

Mwandishi:
Swahili

5

MAISHA YA ABU DHARR

Kwa mujibu wa hadithi ya Mtukufu Mtume, Abu Dharr aliona ndoa ni jambo la muhimu. Alioa lakini kwake ndoa kamwe haikuwa na maana ya starehe na furaha. Alidhani kwamba ndoa ilikuwa ni jina la kufuata Hadith ya Mtukufu Mtume. Inaeleweka kwamba alifuatana na mke wake popote alipokwenda.

Kwa kuwa mke wake alitoka Afrika, wakati fulani watu walisema, "wewe unaye mke mweusi?" Alijibu, "Nafikiri ni bora zaidi kuwa na mke mweusi na mwenye sura mbaya kuliko mke wenye sura inayopendeza na watu wanitembelee kwa sababu tu ya uzuri wa sura ya mke wangu." Abu Dharr alikuwa anamjali sana mkewe.

Ukarimu si tu ndio mojawapo ya sifa bora sana, lakini ni kiini cha ubinadamu. Jinsi mtu anavyozidi kutambua kanuni za Uislamu ndivyo anayozidi kujaa moyo wa huruma.

Naim Bin Qanat Riyath anasema, "Siku moja nilikwenda kumtembelea Abu Dharr na nikamwambia kwamba ninampenda na ninamdharau wakati huo huo." Abu Dharr akasema, "Inawezekanaje hali hizi mbili zije pamoja?" Nilisema, "Nimekuwa nikiwaua watoto wangu. Sasa nimetambua kwamba hicho ni kitendo kiovu. Kwa hiyo, kila mara ninapofikiria kuja kwako kukuuliza kuhusu vipi nitaokolewa na kusamehewa, hisia hizi kubwa zinapanda pamoja. Nilipofikiria kwamba ingekuwa bora kama ungeniambia kuhusu ufumbuzi wake hisia za mapenzi zilipanda juu sana, lakini nilipofikiria kwamba ningeumia daima milele endapo ungetangaza kwamba dhambi hiyo haisameheki, chuki dhidi yako ilizidi kuongezeka. Sasa nimekuja kutaka kutafuta ufumbuzi wa tatizo hili."

Abu Dharr alisema, Sawa! Niambie endapo umefanya yote haya mnamo siku za ujahilia au baada ya kuingia kwenye Uislamu?

Nilisema, "Wakati wa ujahilia." Abu Dharr akasema, "Dhambi yako imesamehewa. Uislamu ni ukombozi wa uchafu wa aina hiyo yote na dhambi zote."

Niliposikia hivi niliridhika. Baadae nilitaka kuondoka akasema, "Ngoja!" Na nilifuata maelekezo yake.

"Baadaye alimwambia mkewe kwa alama alete chakula ambaye alikwenda ndani na akarudi akiwa na chakula. Abu Dharr alisema, "Naim, Bismillah (maana yake kula katika jina la Mwenyezi Mungu).

Kabla sijaanza kula nilimwambia tule wote. Akasema, "Mimi nimo kwenye Swaumu." Aliposema hivi akaanza kuswali. Mimi nikaanza kula na nilipokaribia kumaliza, naye akamaliza Swala na akaanza kula.

Nilisema, "kusema uongo ni dhambi kubwa katika Uislamu na hata kama nikimdhania mtu fulani kuwa ni mwongo inawezekana kwamba anaweza kuwa mwongo, lakini nikufikirie vipi wewe?"

Abu Dharr alisema, "Umekaa muda mrefu na mimi. Jambo gani limekufanya unifikirie mimi kuwa ni mwongo?" Nikasema, "Muda mfupi uiliopita uliniambia kwamba unafunga Swaumu na sasa unakula na mimi."

Aliniambia, "Sijakuambia uongo. Nimefunga Swaumu na wakati huo huo ninakula na wewe."

Akasema, Mtukufu Mtume amesema kwamba yeyote anayefunga Swaumu terehe 13, 14, na 15 ya mwezi huu wa Shabani, kwa namna nyingine ni sawa kama amefunga Swaumu ya mwezi mzima. Kwa maneno mengine, atapata thawabu ya kufunga Swaumu ya siku thelathini yaani kila Saumu ya siku moja inabeba uzito wa Swaumu ya siku kumi. Kwa kuwa nimefunga Swaumu katika siku hizi ninayo haki ya kusema kwamba ninafunga Swaumu ya mwezi mzima." (Musnad Ahmad bin Hanbal na Hayatul Qulubi-Allamah Majlis).

Alamah Bayhaqi pia amesimulia tukio la aina hiyo hiyo. Muhtasari wake ni kama ifuatavyo:

Siku moja Abu Dharr na Abdullah bin Shafiq Uqaili walikwenda nyumbani kwa mtu kama wageni. Abu Dharr alikwisha sema kwamba yeye anafunga Saumu na chakula kilipoletwa alianza kula. Abdullah alidokeza, "Wewe unafunga Saumu." Abu Dharr alisema, "Ninaikumbuka Swaumu yangu. Sijaisahau Saumu yangu. Kila mara nipo makini kufunga Swaumu katika hizo siku tatu za kila mwezi ambazo huitwa "Ayyam al-Beydh." na kwa mujibu wa hadithi ya Mtukufu Mtume(s.a.w.w) , uelewe kwamba mimi ninafunga Saumu (Sunan Bayhaqi).

SURA YA SITA

Shahidi Thalit Allamah Nurullah Shustari ameandika: Abu Dharr alikuwa mmoja wa masahaba mashuhuri sana na anahesabiwa miongoni mwa masahaba wa mwanzo kabisa walioingia kwenye Uislamu. Katika kuukubali Uislamu alikuwa mtu wa tatu, hivyo kwamba, aliingia kwenye Uislamu baada ya mama wa Waumini Khadijahtul Kubra na Amiri wa Waumini Ali. Kwa mujibu wa mwandishi wa kitabu cha 'Isti'ab' alikuwa na sifa ya juu katika ujuzi, kushikilia maadili, uchaji Mungu na kuwa mkweli, miongoni mwa masahaba wote. Ali amesema kwamba, Abu Dharr alifanikiwa nafasi hiyo katika kupata na kuelewa mafundisho ya kidini ambayo hakuna mwingine ambaye angeyafikia. Mtukufu Mtume alikuwa anasema, "Abu Dharr yu kama Mtume Isa katika umma wangu. Abu Dharr anashikilia maadili kama alivyofanya Mtume Isa."

Kwa mujibu wa hadithi, mtu anayetaka kuona mfano wa Mtume Isa amuone Abu Dharr. Shaykh Saduq katika kitabu chake Uyumul Akhbar al-Ridha ameandika kwamba Imamu Ali al-Ridha amesema kutoka kwa mamlaka ya wahenga wake kwamba kwa mujibu wa Hadith ya Mtume, "Abu Dharr ni mtu mkweli wa umma huu."

Ali anasema kwamba Abu Dharr ndiye mtu peke yake asiye jali kamwe kushutumiwa kwa sababu ya Mwenyezi Mungu maamrisho na maagizo yake, ni kwamba, yeye alisema lolote ambalo ni haki na atatekeleza kwa vitendo, na wala hatajali vitisho vyovyote kuhusu jambo hili, ama kuogopeshwa na uwezo wa serikali.

Wanavyuoni wameandika kwamba Abu Dharr alitoa kiapo cha uaminifu kwa Mtume kwa ahadi kwamba katika imani ya Mwenyezi Mungu hangejali mtu yeyote anaye mshutumu na kwamba angesema ukweli hata ungelikuwa na athari ya aina yoyote ile.

Ukweli na ujasiri ni sifa ambazo hata watu mashuhuri sana hushindwa kushikilia. Mtukufu Mtume ameitabiri sifa hii ya Abu Dharr na akasema kwamba Abu Dharr angetoa mchango mkubwa katika jambo hili na ataendelea kushikilia hata katika mateso makali ambayo angeyavumulia.

Mtume alisema: "Hapana mtu mkweli zaidi ya Abu Dharr kati ya utando wa anga na ardhi ." [3] .

Katika ufafanuzi wa hadithi hii Allamah Subaiti ameandika: "Mtukufu Mtume aliwahutubia masahaba wake alisema: "Enyi masahaba wangu! Ni nani miongoni mwenu ambaye atakutana na mimi mnamo siku ya Hesabu katika hali hiyo hiyo ambayo nitamwacha nayo hapa duniani? "

Waliposikia hivi, kila mmoja wao alinyamanza kimya isipokuwa Abu Dharr aliyesema kuwa mtu huyo ni yeye. Mtukufu Mtume akasema: "Bila shaka! umesema kweli ."

Baada ya hapo, aliongeza, "Enyi masahaba wangu! kumbukeni ninayowaambieni. Hakuna mtu kati ya mbingu na dunia ambaye ni mkweli zaidi kuliko Abu Dharr ."[4] .

Allamah Majlis ameandika maelezo baada ya kunukuu hadithi hiyo hapo juu kwenye kitabu chake (Hayatul Qulub).

Bin Babwayh ameeleza kupitia mamlaka ya kuaminika kwamba mtu fulani alimuuliza Imamu al-Sadiq endapo Abu Dharr alikuwa bora zaidi ya Ahlul -Bait wa Mtukufu Mtume au vinginevyo. Imamu Alisema, "Mwaka mmoja una miezi mingapi?" Alijibu, "Kumi na miwili." Imamu akasema, "Miongoni mwa miezi hiyo mingapi

inaheshimika na kutakaswa?" Akasema, "Miezi minne," Imamu aliuliza, "Mwezi wa Ramadhani umejumuishwa katika miezi hii minne?" Akasema, "Hapana." Imamu aliuliza, "Mwezi wa Ramadhani ni bora zaidi au miezi hiyo ni bora zaidi."

Akajibu, Mwezi wa Ramadhani ni bora zaidi." Imamu Akasema, "Ndivyo ilivyo na sisi, Ahlul-Bait. Huwezi kumlinganisha yeyote na sisi."

Siku moja Abu Dharr alikuwa ameketi katika kundi la watu ambao walikuwa wanaeleza maadili ya taifa hili. Abu Dharr alisema, "Ali ni bora kuliko wote katika taifa hili, na yeye ni mpaka wa Pepo na Jahanamu, ni Siddiq na Farooq wa Umma na utibitisho wa ujuzi wa mambo ya dini wa taifa hili." Waliposikia maelezo haya kutoka kwake wanafiki hao waligeuza nyuso zao na kutazama upande mwingine na kukanusha tamko lake na kumwita muongo. Haraka Abu Amamah alinyanyuka na akaenda kwa Mtukufu Mtume na kumwambia alichosema Abu Dharr, na jinsi kundi hilo lilivyokataa kukubali. Mtukufu Mtume akasema, "Hapana mtu kati ya ardhi na mbingu ambaye ni mkweli kuliko Abu Dharr."

Kitabu hiki hiki kimeeleza kupitia mamlaka nyingine kwamba mtu mmoja alimuuliza Imamu Jafar al-Saqiq endapo hadhithi hiyo ilikuwa sahihi ambamo Mtukufu Mtume ametangaza hivyo. Imamu alisema, "Ndio." Akasema, "Kama ndio hivyo, Mtukufu Mtume, Ali, Imamu Hasan, na Imamu Husein na nafasi yao ni ipi?"

Imamu akajibu, "Sisi ni kama mwezi wa Ramadhani ambao ndani mwake upo usiku huo ambao ibada yake ni sawa na ile ya miezi elfu moja ambapo masahaba ni sawa na mwezi unao heshimika

ikilinganishwa na miezi mingine, na hapana mtu anayeweza kulinganishwa na sisi, Ahlul-Bait."

Ni dhahiri kama mwanga wa mchana kutoka kwenye hadithi hiyo hapo juu ya Mtukufu Mtume kwamba Abu Dharr alikuwa hana wa kumlinganisha naye katika ukweli.

Maelezo na ufafanuzi wa hadithi hii hii kama yalivyotolewa na Subaiti inaeleza kwamba Abu Dharr ataondoka hapa duniani akiwa katika hali ile ile ambayo Mtume alimwacha nayo, na atamuona akiwa katika hali hiyo hiyo huko Peponi.

Kama hadithi hii ikitazamwa kwa umakini zaidi, msimamo imara wa Abu Dharr kwenye njia ambayo iliimarishwa na Mtukufu Mtume unadhihirisha uadilifu wake. Wanavyuo wanakubaliana kwenye mtazamo huu kwamba Abu Dharr hakutetereka hata nchi moja kutoka katika njia ya Mtukufu Mtume. Baada ya Mtume, hata sabaha kama Salman alilazimishwa kutoa kiapo cha utii na siku moja alipigwa sana ndani ya msikiti hadi shingo yake ikavimba. Lakini Abu Dharr kamwe hakunyamaza.

Allamah Subaiti ameandika: "Abu Dharr alikuwa mmojawapo wa wafuasi wa Mtukufu Mtume ambao walishika njia yao na walisimama imara kuhusu agano lao walilofanya na Mwenyezi Mungu. Ali mtu Mtukufu Mtume kwa uaminifu, alifuata nyayo zake na kuiga mwenendo wake. Hakuachana na Imamu Ali hata kidogo, alimfuata hdi mwisho na akapata faida ya nuru ya ujuzi wake.

Allamah Majlis ameandika: "Bin Babwayh anaeleza kupitia kwa mamlaka ya kuaminika kutoka kwa Imamu Ja'far al-Sadiq kwamba siku moja Abu Dharr alikuwa anapita karibu na Mtume wakati Jibril alikuwa anazungumza naye katika faragha katika

umbile la 'Dahyah Kalbi.' Abu Dharr alirudi nyuma kwa kudhani kwamba Dahyah Kalbi alikuwa anazungumza na Mtume kwenye faragha. Aliporudi Jibril alimwambia Mtume, "Ewe Muhammad! Abu Dharr alikuja muda mfupi uliopita na akarudi bila kunisalimia. Amini kwamba endapo angenisalimia, hakika ningejibu salamu yake. Ewe Muhammad! Abu Dharr anayo dua yake ambayo inajulikana kwa watu wa Peponi. Tazama! Nitakapoandoka kwenda mbinguzi muulize kuhusu taarifa hii. Akasema, "Vema."

Jibril alipoondoka na Abu Dharr akarudi kwa Mtume, Mtume akasema; "Ewe Abu Dharr! Kwa nini hukutusalimia ulipokuja hapa muda mfupi uliopita? Abu Dharr alijibu, Nilipokuja, Dahyah Kalbi alikuwa ameketi na wewe na mlikuwa na mazungumzo. Nilidhani mnazungumza kuhusu mambo fulani ya siri na mimi sikuona vema kuingilia kati.

Kwa hiyo nikarudi. Mtukufu Mtume akasema, "Huyo hakuwa Dahyah Kalbi lakini huyo alikuwa Jibrili aliyenijia katika umbile la Dahyah Kalbi. Ewe Abu Dharr! Alikuwa ananiambia kwamba endapo ungemsalimia naye angejibu salamu yako. Pia aliniambia kwamba unayo dua ambayo inajulikana sana miongoni mwa watu wa Peponi." Abu Dharr aliondoka akiwa na haya sana na akaonyesha kujutia kitendo chake.

Halafu Mtukufu Mtume akasema, "Ewe Abu Dharr! Niambie dua unayosoma na ambalo linazungumziwa sana mbinguni" Abu Dharr akamwambia Mtume "Dua hiyo ni hii ifuatayo: Allahumma inni Asalukal Amna wal Imana bika wat tasdiqa bi nabiyyika wal 'Aafiyata min jami'il blaa'i' washukra 'alal 'afiyat wal ghina'an shirarin naasi."[5]

Zipo hadithi nyingi sana upande wa madhehebu ya Shia na Suni ambamo maagizo maalum yametolewa kuwapenda masahaba wanne. Wanavyuo wanasema kwamba masahaba hao wane ni Ali, Abu Dharr, Miqdad na Salman.

Umar Kashi ameandika kwenye Rijal yake, Abu Jafar Qummi kwenye Khasail, Abdullah Humayri kwenye Qurbul Asnad, Shaykh Mufid kwenye Iktisas, Ayashi kwenye maelezo yake, Sadiqu kwenye Uyun Akhbar al-Riza, Abdul Barr kwenye Istiab, Bin Sad kwenye Tabaqat na mwandishi wa Usudul Ghabah kwenye kitabu chake:

Mtukufu Mtume(s.a.w.w) amesema kwamba Mwenyezi Mungu amemuagiza kuwaweka masahaba wangu wanne kuwa marafiki zangu na niwapende, na pia nimeambiwa kwamba Yeye pia amewafanya marafiki masahaba hao majina yao ni haya: Ali bin Abi Talib, Abu Dharr Al-Ghifari, Miqdad bin Al-Aswad na Salman Farsi[6] .

Hadithi inasema kwamba hao masahaba wanne ni Salman, Abu Dharr, Miqdad na Ammar. Wanachuo wanafikiria kwamba hawa masahaba wanne ambao Pepo na wakazi wa Pepo wanawapenda sana. Inasimuliwa kwenye hadithi kwamba ambapo mtangazaji atatangaza mnamo siku ya Hukumu, "Wako wapi hao masahaba wa Muhammad bin Abdullah ambao hawakuvunja ahadi yao ya kuwapenda Ahlul Bait al-Risalah, lakini walikuwa imara kuendelea nayo?" Salman, Miqdadi, na Abu Dharr watasimama.

Allamah Nuri ameandika kwa kumnukuu Raudhatul Waidhin cha Shaykh Shahia Muhammad bin Ahmad bin Ali bin Fital Naishapuri

kwamba Imamu Muhammad al-Baqir amesema, zimo daraja kumi za imani. Miqdad amepata daraja nane, Abu Dharr amepata daraja tisa na Salman amepata zote kumi.

Dhamana ya udugu inakumbusha hilo tukio la kihistoria ambalo Mtukufu Mtume aliasisi udugu katika jozi moja ya masahaba wake kabla na baada ya kuhamia Madina.

Kabla ya Hijiriya aliasisi dhamana ya udugu baina ya kila masahaba wawili ili kwamba waweze kuhurumiana kwenye udugu huu alifikiria mfanano wa tabia wa masahaba wawili. Aliwafanya hao masahaba wawili kuwa ndugu wa kila mmoja kwa kua tabia zao zilikuwa zinafanana na kulingana kwa mwenendo. Kwa njia hii alitangaza udugu kati ya Abu Bakr na Umar, Talhah na Zubayr, Uthman na Abdur Rahman bin Auf, Hamza na Zayd bin Harith, Salman na Abu Dharr na Ali na yeye Mtume.

Halafu baada ya miezi mitano au minane, baada ya Hijiriya, Mtume(s.a.w.w) kwa mara nyingine aliasisi dhamana ya udugu kwa njia ile ile. Ilikuwa muhimu kuanzisha udugu baina ya wahamiaji na wenyeji wa Madina kwa lengo la kujenga misingi ya kuhurumiana baina yao. Mtume alianzisha udugu miongoni mwa masahaba hamsini.

Allamah Sahibli Nomani ameandika: "Kwenye himaya ya Uislamu yapo maadili na tabia safi sana. Ilikuwa ilizingatiwa kwamba masahaba ambao walipewa dhamana ya udugu baina yao walikuwa na mfanano wa upendeleo. Muungano huu wa upendeleo baina ya mwalimu na mwanafunzi ni muhimu kwa lengo la usilimishaji wa ujuzi. Baada ya kuuliza kupima ilionekana kwamba muungano huu wa upendeleo wa hao wawili waliofanywa ndugu ulizingatiwa na tunapoona kwamba ni kama vile haiwezekani kuamua kikamilifu na

kwa usahihi mienendo na upendeleo wa mamia ya watu kwa muda mfupi hivyo, lazima ikubalike kwamba uamuzi wa Mtukufu Mtume ulikuwa mfano wa sifa maalumu ya Utume[7] .

Juu ya hayo, hili pia linafaa kukumbukwa kwamba Mtume hakupata mtu mwenye upendeleo unaofanana na ule wa Ali ama miongoni mwa Muhajirina (wahamiaji au Ansari). Ali akasema, "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu umeniunganisha na nani?" Akasema, "Wewe ni ndugu yangu hapa duniani na baada ya hapa duniani (Peponi)" Ndio maana ya Ali alitangaza mara kwa mara kwenye mimbari ya Msikiti wa Kufa, "Mimi ni mja wa Mwenyezi Mungu na ndugu yake Mtume wa Mwenyezi Mungu."[8]

Mtukufu Mtume pia alisema kuhusu Salman, "Salman ni mmoja wetu sisi Ahlul Bait ."

Kwa maoni yangu hii pia ni mojawapo ya sifa bora za Abu Dharr kwamba mtu mwenye uamuzi ulio komaa kama Mtukufu Mtume alimtangaza kuwa ndugu yake Salman. Allamah Subaiti amenukuu usemi wa Saleh al-Ahwal ambaye alimsikia Imamu Jafar al-Sadiq akisema kwamba Mtukufu Mtume alianzisha dhamana ya udugu baina ya Salman na Abu Dharr na alimwambia Abu Dharr asije akampinga Salman.[9]

Hadith ya Abu Dharr ni ya juu sana hivyo kwamba aya za Quran Tukufu zimeteremshwa kwa ajili ya kumsifu yeye. Moja ya Aya hizo ni kama ilivyonukuliwa hapa chini:

"Hakika wale walioamini na wakatenda mema mashukio yao yatakuwa kwenye Pepo ya Firdausi ." (Surah 18:107).

Imamu Jafar al-Sadiq anasema kwamba Aya hii imeteremshwa kuhusu Abu Dharr, Miqdadi, Ammar na Salman.

Kwa mujibu wa hadithi, Mtume alisema kwamba Mwenyezi Mungu alimuamuru ampende Salman, Abu Dharr, Miqdadi na Ammar na akaongeza zaidi kwamba yeye mwenyewe aliwafanya hao marafiki zake. Kwa mujibu wa hadithi nyingine Mtume alisema: "Pepo inayo shauku na watu hawa. "[10] .

Allamah Gilani ameandika kwamba heshima ya Abu Dharr na hadhi yake ni hali zilizoongezeka sana siku hadi siku katika mazingira ya Mtume, hivyo kwamba, Mtukufu Mtume alipokwenda kwenye Vita ya Zaat al-Ruqa1 alimfanya yeye kuwa mtemi wa Madina, na si yeye tu kuwa mtemi lakini kwa ajili yake wakati fulani Ghifari wengine pia walipata cheo hiki. Mathalani, Mtukufu Mtume alimteua Saya' bin Urfah al-Ghifari kama Mtemi wa Madina wakati wa Vita ya Daumatul jandal, (Zaadul Ma'ad).

Ilikuwa kawaida ya huko Arabuni kwamba wakati wowote ilipotokea mtu anapanda ngamia alimfanya mtu wake maalumu kuwa 'sanjari' wake. Sanjari alipoketi nyuma, alikuwa akishika hatamu kwa kuzungusha kiunoni. Kwa mujibu wa hadith hii ya hawaida Mtukufu Mtume pia alimfanya mtu kuwa Sanjari wake.

Wakati wa hija ya mwisho, Sanjari wake alikuwa Fazal bin Abbas bin Abdul Muttalib.

Masahaba waliona kuwa ni heshima kuwa Sanjari. Sanjari wa Mtume aliitwa'Radifun Nabi.' Wasomi wanasema kwamba Mtume zaidi alimpa heshima hii Abu Dharr. Mtume alikuwa na desturi ya kupanda wanyama wengine wadogo.

Punda pia mara nyingi walitumika kumbeba Mtume. Alikuwa na tabia ya kumruhusu Abu Dharr kukaa nyuma yake na waliendelea na safari huku wanazungumza. (Tabaqat Ibn Sa'd).

Shah Walyullah Dehlavi, anapoelezea ghasia kwenye Uislamu, ameandika kuhusu tukio la Harrah. Abu Dawudi amemnukuu Abu Dharr ambaye alisema, "Siku moja niliketi nyuma ya Mtukufu Mtume tukiwa tumepanda punda.

Tulipokuwa nje ya Madina- sehemu isiyokaliwa na watu, aliniuliza hali yangu ingekuwaje wakati njaa itakapoikumba Madina, na ningeshindwa kuvumilia kabla ya kufika msikitini baada ya kutoka kitandani mwangu." Nikasema, "Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanajua zaidi."

Akasema, "Ewe Abu Dharr! Usije ukaenda kuomba wakati huo." Halafu akasema, "Hali yako itakuwaje ambapo bei ya kaburi italingana na ile ya mtumwa kwa sababu ya kiasi kikubwa cha vifo?" Nikasema. "Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanajua zaidi." Akasema, "Ewe Abu Dharr! Jizoeze uvumilivu."

6

MAISHA YA ABU DHARR

Halafu aliuliza tena, "Ewe Abu Dharr! Hali yako itakuwaje ambapo patatokea mauaji ya haliaiki hapa Madina hivyo kwamba mawe na

mchanga vitaloa damu?" Nikajibu, "Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wanajua zaidi." Alisema, "Wakati huo utatakiwa ukae nyumbani kwako."

Nilimuuliza, "Itabidi nishike upanga wakati huo?" Alijibu, "Kama ukifanya hivyo utafikiriwa kuwa ni mshirika wao." Halafu nilimuuliza, "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Nifanye nini wakati huo?" Alisema, "Hata kama unaogopa kwamba mng'ao wa upanga utafanya macho yako yasione vizuri, funika uso wako tu kwa kipande cha nguo yako na usipigane, lakini nyamaza kimya."

Maelezo haya yapo ukurasa wa 176 kwenye Juzuu ya 5 ya Musnad Ahmad bin Hanbal iliyochapishwa Misri. Kwamba Mtukufu Mtume alikuwa na kawaida ya kumdokeza Abu Dharr siri zake na akasema kwamba alikuwa anamwamini sana. Abu Dharr naye pia, alikuwa mwangalifu sana kuficha siri zake. Wakati wowote alipoulizwa kuhusu Hadith, alisema, "Isipokuwa mambo yale ambayo Mtukufu Mtume ameniambia kuwa ni siri, nipo tayari kukueleza kila kitu. Unaweza kuniuliza chochote unachotaka."

SURA YA SABA

Zipo nasaha nyingi ambazo Mtume alimpa Abu Dharr. Hapa tunadokeza kuhusu chache miongoni mwazo. Muhammad Harun Zangipuri ameandika ka mujibu ya mamlaka ya 'Amali' ya Shaykh Tusi kwamba Mtume alimwambia Abu Dharr: "Ewe Abu Dharr! Muabudu Mwenyezi Mungu kama vile unamuona Yeye, na Yeye Anakuona wewe na hata kama humuoni wewe." Tambua kwamba kwanza kabisa ibada Yake ni kumtambua yaani kuelewa kwamba Yeye ni wa kwanza kabla ya chochote. Yeye hana mshirika. Yeye ni wa Milele hana mwisho.

Yeye ni Muumbaji wa vitu baina ya ardhi na mbingu. Yeye Ametakasika na yumo kila mahali. Yeye hahusiki na dosari yoyote, na ni Muumbaji wa vitu vyote.

Baada ya kuelewa Upweke wa Mwenyezi Mungu ni muhimu kukubali Utume wangu na kuamini, kwamba Mwenyezi Mungu amenituma kama mjumbe wa habari njema, mwonyaji na taa nyeye nuru ya mwongozo kuwaita watu kwa Mwenyezi Mungu.

Baada ya kukubali Utume wangu, ni wajibu na muhimu kuwapenda Ahlil-Bait wangu ambao Mwenyezi Mungu ameweatakasa kutokana na uovu wote.

Zingatia kwamba vimo vitu viwili vyenye neema: Afya njema na fursa ya kufanya ibada.

Vithamini vitu vitano kabla ya vitu vitano: Thamini ujana kabla hujazeeka, afya njema kabla ya kuugua maradhi, utajiri kabla ya umaskini, starehe kabla ya kazi na uhai kabla ya kifo. Ishi duniani kama mgeni au pitisha siku zako kama mpita njia.

Unapoamka asubuhi, usiwe na matumaini ya kuiona jioni, na baada ya kupitisha siku usiwe na tegemeo la kuiona asubuhi. Chukua nafuu ya afya yako njema (kwa ajili ya kuabudu kabla hujaugua na tumia maisha (katika njia ya Mwenyezi Mungu) kabla hujafa, kwa sababu hatujui watu watatuitaje kesho tukiwa hai au tumekufa; maana yake ni kwamba hatujui endapo kesho tutakuwa hai au hapana.

Uwe bahili kuhusu maisha yako kuliko pesa zako. Kwa maneno mengine, kama vile unavyotumia fedha zako kwa kujinyima na unajaribu hutaki kutumia kitu chochote isivyofaa kwa njia ile ile,

unatakiwa kuwa bahili kuhusu maisha yako na jaribu kutokufuja katika matendo ya uovu.

Mnamo siku ya Hesabu, Mwenyezi Mungu atawapia jicho baya kupita kiasi la kutoridhika hao Maulamaa ambao ujuzi wao haukuwanufaisha watu, au ambao wamepata ujuzi kwa lengo la kupata heshima ya kidunia bila kumnufaisha yeyote. Maulamaa wa aina hiyo, hawatanusa manukato ya Pepo.

Wakati wowote unapoulizwa kuhusu kitu ambacho hukijui, kiri ujinga wako wazi wazi. Tazama usitoe uamuzi kuhusu jambo usilolijua.

Siku inakuja ambapo baadhi ya wakazi wa Peponi watawaambia baadhi ya wakazi wa Jahanamu, "Kwa sababu gani tumeingia Peponi kwa sababu ya mafundisho yako na nasaha, lakini wewe umeingia Jahanamu?" Watajibu kwa kusema, "Tuliwaagiza wengine kufanya wema lakini sisi hatukufanya hivyo sisi."

Mwenyezi Mungu anazo haki nyingi juu yako. Ili iweze kuzitambua unatakiwa kuomba msamaha wake wakati wa kulala na unapoamka asubuhi.

Kifo kinakutafuta wewe na kinaweza kuja wakati wowote. Kwa hiyo, inatakiwa kufanya mambo mema na uharakie kufanya hivyo, na sikiliza! Mtu huvuna anachokipanda. Ngano huzaa ngano na shairi huzaa shairi. Usisahau adhabu ya matendo yako.

Watu wanaojihini ni makamanda na wanasheria ni viongozi, kuna manufaa yasiyo na mwisho kuwa karibu nao.

Muumini anafikiria dhambi kuwa mzigo mkubwa kama mlima. Anahisi kama vile anakandamizwa na mlima.

Lakini asiye muumini anafikiria dhambi kama inzi kwenye pua yake.

Usiangalie udogo wa dhambi lakini angalia unafanya dhambi hiyo kinyume cha matakwa ya nani.

Mtu ambaye ni muumini anao wasiwasi zaidi katika dunia hii kuliko ndege aliye nasa kwenye mtego wako. Anataka aondoke duniani haraka iwezekanavyo.

Si vema kuingilia katika kila jambo na unatakiwa kudhibiti ulimi wako kwa namna ile ile unavyo linda chakula chako.

Mwenyezi Mungu amezifanya Swala kuwa utulivu wa macho yako. Ewe Abu Dharr! Mtu mwenye njaa hula chakula hadi anashiba na mwenye kiu hunywa maji hadi anatosheka, lakini mimi sitosheki na Swala.

Almuradi unaswali, wewe ni kama vile unagonga mlango wa Mfalme kamili, unatakiwa utambue kwamba, kwa kugonga mlango huo mfululizo, hatimaye mlango huo hufunguka.

Usiifanye nyumba yako kama kaburi. Nyumba ambamo haisaliwi Swala imeenea giza kama kaburi. Unatakiwa kufanya mpango wa kuweka nuru kwenye kaburi lako kwa kusali ndani ya nyumba yako kwani unaposali ndani ya nyumba yako, unatia nuru kwenye kaburi lako.

Sala ni nguzo ya imani na sadaka hutakasa dhambi, lakini kudhibiti ulimi wako ni jambo la muhimu zaidi kuliko hayo mawili yaliyo tangulia kutajwa.

Mtu mwenye moyo mgumu hawezi kumkaribia Mwenyezi Mungu. Kwa hiyo, unatakiwa kuwa na moyo wa huruma.

Mkumbuke Mwenyezi Mungu Katika hali ya Khumul (faragha) Nilimuuliza yeye, "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Khumul ni nini?" akajibu, "Maana yake ni kumkumbuka mwenyezi Mungu katika faragha."

Mwenyezi Mungu anasema: "Mja wangu ni yule anayeniogopa. Nitamfanya mtu wa aina hii asiogope mnamo siku ya Hukumu, ikiwa ananiogopa Mimi. Hatakuwa na fadhaiko siku ya ufufuo badala yake atakuwa na amani."

Mwenye akili ni yule ambaye hunyenyekea na kufanya matendo kwa ajili ya kuingia Peponi; "Na asiye na msaada na mpumbavu ni yule anayefuata matamanio ya kidunia na hajali Pepo. Dunia na watu wa dunia wamelaaniwa. Ni vitu hivyo tu ambavyo vimetumika katika njia ya Mwenyezi Mungu, vinaweza kuwanufaisha watu wa dunia.

Mwenyezi Mungu alimfunulia ndugu yangu, Mtume Isa, "Ewe Isa! Usiipende dunia kwa sababu ni mahali pa marejeo. Kila mtu atarejea hapo na atatakiwa kutoa maelezo ya matendo yake hapo. Thawabu za matendo mazuri zitakuwa nzuri na adhabu itatolewa kwa matendo maovu.

Mwenyezi Mungu ataujaza busara moyo wa mtu anayejinyima. Ataupatia ulimi wake uwezo wa kujieleza kwa ufasaha, atamwonyesha maovu ya dunia na jinsi ya kuyaepuka na atamnyanyua kutoka hapa duniani kwa namna ambayo kwamba atafika kwenye nyumba ya amani (Darus-Salaam) kwa jinsi inayostahili.

Mwenyezi Mungu kamwe hakuamuru kukusanya utajiri. Badala yake Ameagiza Aabudiwe Yeye. Kwa hiyo, unatakiwa kuwa mchaji

Mungu, rukuu mbele Yake na uendelee kumuabudu Yeye hadi mwisho wa uhai wako.

Mimi huvaa nguo za kawaida, huketi kwenye ardhi na hupanda punda asiye na mito ya kukalia. Sikiliza! Unatakiwa kuwa mfuasi wangu na ufuate Sunna zangu. Mtu anayekataa Sunna zangu, hata hesabiwa miongoni mwa watu wangu.

Nawapongeza watu wanao hiji ni ambao hawajali mambo ya dunia na wanaielekea Pepo; ambao hukaa chini kwenye ardhi, na huifanya ardhi kuwa zulia na maji yake kuwa safi; watu ambao wanacho kitabu cha Mwenyezi mungu, Qurani Tukufu kuwa kigezo chao na maombi kuwa heshima yao, na hujitenga na dunia.

Bidhaa za dunia ni watoto na utajiri na bidhaa za Peponi ni matendo mema.

Muogope Mwenyezi Mungu na usiwajali watu. Watu watakuheshimu wewe pia ikiwa utamuogopa Mwenyezi Mungu.

Nyamaza kimya unapoona maiti imebebwa, au unapokuwa na maiti. Pia nyamaza mapigano yanapoendelea na pia unyamaze wakati Quran Tukufu inaposomwa.

Chumvi huhifadhi kila kitu kisioze, lakini chumvi ikiharibika, hakuna marekebisho (Hadith hii inahusu wanavyuo na maana yake ni kwamba imani huharibika pale ambapo wanavyuo kuwa waovu). Swala mbili fupi zikisaliwa kwa uaminifu na tafakuri ni bora zaidi kuliko Swala za usiku moja zilizosaliwa bila uaminifu.

Jiite na ujifanye unahesabiwa matendo yako mnamo Siku ya Hesabu. Kusali bila matendo mema ni sawa na kutupa mshale bila lengo.

Mtu anaposali angalipo porini, Mwenyezi Mungu huwaamuru Malaika kusimama katika safu na kusali nyuma yake na kusema Amin baada ya Swala yake alimuradi Adhan imeadhiniwa na Swala imekimiwa kabla ya Swala.

Endapo mtu anasali Swala bila ya wito huo uliotajwa hapo juu, malaika wawili tu kuamuriwa kushiriki katika Swala hiyo.

Kumkumbuka Mwenyezi Mungu miongoni mwa watu wazembe ni sawa na kupigana kwenye uwanja wa vita. Kuwa na watu wazuri ni bora zaidi kuliko kukaa katika upweke na upweke ni bora zaidi kuliko kuwa miongoni mwa watu wabaya.

Kila wakati fanya urafiki na waumini, kula na kunywa na watu wanao

jinyima.

Mwenyezi Mungu yu karibu na ulimi wa kila msemaji kila wakati.

Kwa hiyo mfikirie Mwenyezi Mungu unaposema.

Kwa uwongo inatosha kwamba mtu husema chochote asikiacho. Ni muhimu kudhibiti ulimi moja kwa moja.

Mwenyezi Mungu humpenda mtu anayeheshimu ujuzi, wanavyuo, Waislamu wakongwe, wafuasi wa Qurani Tukufu, na mtawala mwenye haki.

Zilinde na uzifuate amri za Mwenyezi Mungu. Naye atakulinda na utamuona Yeye yu mbele yako. Mkumbuke Yeye wakati wa furaha naye atakukumbuka wakati wa shida na atakukomboa kutoka humo. Kama unahitaji kitu, omba kutoka kwake tu. Hakuna atakaye kudhuru hata kama dunia yote itakuwa adui yako, almuradi Mwenyezi Mungu hana ugomvi na wewe. Hutaweza kunufaika hata kama watu wote kwa kuungana pamoja wanataka kukunufaisha

wewe isipokuwa Mwenyezi Mungu aridhie hivyo. Mwenyezi Mungu hukusaidia wewe ukiwa kwenye uvumilivu. Ni Yeye ndiye anayekuondolea maumivu yako. Kila mara kuna faraja baada ya shida.

Mwenyezi Mungu haangalii nyuso zenu au utajiri wenu; Yeye hutazama nia zenu na matendo yenu.

Sifa za muumini ni kuwa na amani, kuonyesha staha na kumkumbuka Mwenyezi Mungu katika hali yoyote ile. Aliyelaaniwa ni yule anayesema uwongo kwa watu kwa madhumuni ya kuchekesha tu.

Epukana na usengenyi kwa sababu hilo ni tendo ovu zaidi ya zinaa. Nikauliza, "Vipi Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?" Mtume alijibu, "Mzinzi akitubu, Mwenyezi Mungu hukubali toba yake lakini dhambi ya kuteta (kusenyenya) haisameheki hadi mtu ambaye ametetwa (amesengenywa) anaisamehe."

Mtu anayemtukana muumini ni mwovu na mtu anayepigana na muumini ni kafiri, na akimsengenya muumini maana yake ni kwamba anakula nyama ya anayemsengenya na kwa hivyo ni mwovu mkubwa; na mtu anaye linda mali ya muumini ni sawa kama vile analinda maisha yake."

Mimi nilisema, "ewe mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Kusengenya ni nani?" Akasema, "Kumtaja ndugu yako kwa mabaya yake ambayo hangependa kutajwa kwayo." Mimi nikasema, "Hata kama anazo sifa hizo?" Akasema, "Hiyo ni kusengenya, kwa kweli; lakini, kama ukimsingizia mambo asiyo kuwa nayo, hiyo ni usingiziaji ambao adhabu yake ni tofauti."

Mwenyezi Mungu atamzawadia thawabu ya kwenda Peponi endapo anamwondolea shida ndugu yake katika imani.

Qatat, hawataingia Peponi." niliuliza, "Ni nani hawa Qatat?" Alijibu, "Hawa ni wasengenyaji."

Mtetaji hataweza kukwepa adhabu ya Mwenyezi Mungu huko Akhera."

"Msaliti atakwenda Jahanamu." kutoa siri ya rafiki yako ni usaliti.

Endapo mtu anakufa kabla ya kuhisi toba baada ya kuonyesha majivuno hata mara moja tu, hatanusa harufu ya Pepo. Mtume mwenye mashati mawili, yeye atumie moja na la pili ampe ndugu yake ambaye hana shati.

Mtu anayeacha kuvaa nguo za gharama, pamoja na yeye kuwa tajiri, kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, huko Peponi atapewa majoho kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Kabla ya majilio ya Mahdi.[11] watatokea watu watakaovaa nguo za sufi wakati majira ya joto na baridi, kuonyesha ubora wao kwa watu wengine. Mwenyezi Mungu atawalaani.

Dunia hii ni jela kwa muumini na Pepo kwa kafiri. Nia yako katika hali yoyote lazima iwe uaminifu. Hata kula na kulala kwako ni mambo ambayo unatakiwa uyafanye kwa makusudio ya uamifu.

Kwa mujibu wa Hafidh Abu Naim, Kama inavyoelezwa kwenye kitabu chake, Huyatul Awlita Abu Dharr anasema: "Siku moja nilikwenda kwa Mtukufu Mtume alipokuwa amekaa msikitini. Nilikuwa hata bado sijaketi sawasawa, akiniambia, "Bado hujatoa heshima yako kwa msikiti."

Nilimuuliza, "Kitu gani hicho bwana wangu!" Alijibu, "Rakaa mbili za Swala. Ewe Abu Dharr! Unapoingia msikitini haraka sana lazima swali Swala ya raka mbili." Kufuatana na amri yake, mara moja nilisali Swala ya rakaa mbili.

Halafu niliuliza, "Nini msingi na dhamira ya Swala?" Alijibu, "Ni ibada bora kuliko zote."

Halafu niliuliza, "Ni amali gani iliyo bora kuliko zote." Alijibu, "kumwamini Mwenyezi Mungu na kupigana katika njia ya Mwenyezi Mungu hizi ni amali kuzidi zote."

Nikauliza, "Ewe bwana! Ni waumini gani ambao imani yao inafikiriwa kuwa kamili?" Alijibu, "Ni hao ambao matendo yao ni mema na tabia zao ni nzuri." akasema, "Ni hao ambao ndimi zao haziwasemi kwa ubaya na mikono yao haiwashambulii Waislamu wenzao" Niliuliza, "Ni mambo gani mtu anatakiwa ayaepuke?" Alijibu, "Kujinyima na kuepuka kufanya dhambi." Nikauliza. "Ni Swala zipi zilizo bora kuliko zote?" Alijibu, "Ni Swala zile ambazo dua ndefu hukaririwa katika Qunuti," Nikauliza, "Ewe bwana! Kufunga swaumu ni nini?" Akajibu, "Ni ibada ya faradhi ambayo thawabu yake ni kubwa sana" Niliuliza, "Ni jihadi ipi iliyo bora zaidi?" akajibu, "Ni hiyo ambayo miguu ya mnyama aliyepandwa hukatwa na aliyempanda mnyama huyo kuuawa." Niliuliza, "Ni sadaka ipi iliyo bora zaid?"

Alijibu, Ni sadaka ile iliyotolewa kutokana na malipo ya kazi ngumu." Niliuliza, "Ewe bwana ni Aya gani miongoni mwa zile zilizofunuliwa na Mwenyezi Mungu ni bora zaidi kuzidi zingine?" Alijibu, "Ayat al-Kursi (aya za kiti cha enzi) Nikasema, Ewe bwana! Nipe nasaha zako." Akasema, "Nina kushauri umwogope Mwenyezi Mungu kwa sababu huo ndio msingi wa amali njema."

Kariri Qurani Tukufu ambayo ni chanzo cha nuru kwako hapa duniani, na utajo wa upendeleo wako huko mbinguni. Usicheke sana, ukicheka sana moyo hukosa uhai na uso husinyaa. Uwe kimya kwa muda mrefu zaidi, kwani hali hii itakuepusha kwenye matatizo mengi.

Uwe kipenzi cha watu fukara na uwe nao.

Waangalie watu hao ambao kipato chao ni cha chini zaidi na usijilinganishe na watu ambao kiuchumi wapo juu zaidi.

Wafanyie wema ahali zako, hata kama wanakudharau. Usijali lawama yoyote endapo tendo lako ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu. Sema ukweli hata kama unauma.

Kwa kuwa Mtukufu Mtume alikuwa na uwezo wa kubashiri mara kwa mara alitamka matukio na matatizo ambayo yangempata Abu Dharr katika maisha yake ya baadaye.

Imeandikwa kwenye Musnadya Ahmad bin Hanbali kwamba siku moja Abu Dharr alikwenda msikitini na kulala baada ya mchoko wa mahubiri. Mtume alikwenda msikitini kumliwaza na akaona kwamba alikuwa amelala. Mtume alimwambia kwa ishara ya kidole gumba chake na alisema: "Ewe Abu Dharr! Utafanya nini utakapofukuzwa kwenye msikiti?" Abu Dharr alijibu, "Ewe bwana! Endapo hali inakuwa hiyo, nitachomoa upanga wangu na nitamkata kichwa chake mtu atakayefanya hivyo." Mtume akasema, "Ewe Abu Dharr! Usije ukafanya hivyo lakini uwe mvumilivu wakati huo; nenda popote utakapo pelekwa na uondoke uende huko utakapopelekwa."

Allamah Muhammad Baqir Majlis ameandika kwamba siku moja Mtume alimwambia Abu Dharr, "Ewe Abu Dharr! Utaishi maisha ya

upweke, na utakufa ukiwa peke yako. Utafufuka mnamo siku ya Ufufuo ukiwa peke yako. Utafariki dunia ukiwa peke yako katika nchi ya ugenini. Baadhi ya watu wa Iraq wataikafini maiti yako, wataivisha sanda, na kukuzika." (Anwarul Qulub).

Aidha ameandika kwamba siku moja Uthman na Abu Dharr walingia kwenye msikiti wa Mtume huku wakizungumza.

Hapo walimuona Mtume ameketi akiwa ameegemea kwenye mto. Wote wawili walikwenda kwake. Baada ya muda mfupi Uthman aliondoka hapo. Baadaye Mtume akasema, "Ewe Abu Dharr! Ulikuwa unazunguma nini na Uthman?" Abu Dharr alisema, "Tulikuwa tunazungumza kuhusu aya fulani ya Quran Tukufu." Mtume akasema, Ewe Abu Dharr! Haiko mbali siku ambapo wewe na Uthman mtatofautiana sana na wote nyinyi wawili mtakuwa wahasimu wakubwa. Wakati huo mmoja wenu atakandamizwa na mwingine atakuwa mkandamizaji. Abu Dharr! Usiache kusema kweli, hata kama ukifanyiwa udhalimu wa aina yoyote ile" (Hayatul Qulub).

Ilielekea zaidi kwamba aya iliyotajwa kwenye fungu la maneno hapo juu lilihusu suala la Zaka kwa sababu Allamah Subaiti akidokeza kwenye kitabu chake ameandika kwamba palitokea mazungumzo baina ya Uthman na Abu Dharr kuhusu suala la Zaka, ambalo lilisuluhishwa na Mtukufu Mtume (Hayatul Qulubi).

Waandishi wa historia na wahadithi wanakubaliana kwamba Abu Dharr alikuwa kwenye upeo wa uchaji Mungu. Alitumia maisha yake yote katika kuhubiri, na sababu ni kwamba alitoa kiapo cha utii kwa Mtukufu Mtume katika kipindi hicho hicho. alisema kwamba hangemjali mtu yeyote mwenye kumshutumu kwa sababu inayohusiana na amri za Mwenyezi Mungu. Hotuba zake ni nyingi sana, baadhi ya hizo zimeatajwa hapa chini:

Kwa mujibu wa maneno ya Allamah Turayhi, Abu Dharr amesema mara nyingi kwenye mahubiri yake, "Enyi watu! Hata kama migongo yenu itajikunja na miguu yenu kushindwa kufanya kazi kwa sababu ya kusali sana na huduma zingine za dini, haitawapeni manufaa isipokuwa muwapende Ahlul-Bait katika mioyo yenu. Kwa hiyo mnatakiwa kwanza, muwapenhe watu wa nyumba ya Muhammad kwenye nyoyo zenu (kwa maelezo zaidi kuhusu "kuwapenda Ndugu" [12]

Allamah Subaiti ameandika kwamba siku moja Abu Dharr aliita kwa sauti kwenye mlango wa Al-Kaaba, "Enyi ndugu zangu! Njooni karibu yangu na msikileze kwa uangalifu."

Waliposikia hivi watu walikusanyika karibu naye. Abu Dharr alisema, kila mmoja wenu hukusanya mahitaji kwa ajili ya safari yake na huanza safari yake baaada ya kukusanya mahitaji. Si rahisi kumuona mtu miongoni mwetu ambaye ataanza safari bila mahitaji. "Enyi ndugu zangu! Safari yenu kwenye siku ya Ufufuo ipo mbele yenu. Kwa hiyo, ni muhimu kwenu kukusanya mahitaji kwa ajili ya safari."

Watu wakasema, "Ewe ndugu hapana shaka kuhusu safari ya kwenye Ufufuo, lakini hatujui tuchukue mahitaji gani?" Abu Dharr akasema, "Jambo linalohitajiwa katika safari hii ni Hija ya kutembelea Kaabah. Mahitaji yake ni kufunga Swaumu wakati wa siku za joto sana na kusali Swala ya rakaa mbili ili kuondoa hofu ya kaburi kwenye usiku wa giza, "Enyi ndugu zangu! Fanyeni amali njema. Chunga ulimi wako usitamke maneno mabaya. Tumia utajiri wako katika kutoa Sadaka. Tumia siku za uhai wako katika kuitafuta Pepo, na tafuta njia za halali za kupata riziki. Ukipata dinari mbili, tumia moja kwa kumpa nduguyo na nyingine toa sadaka kwa ajili ya ustawi wa Pepo.

3

MAISHA YA ABU DHARR

Baada ya haya, Abu Dharr na Unais waliketi kwenye nafasi zao wakitazamana uso kwa uso na mtemi, Khafaf. Khafaf alisema kwa sauti ya upole lakini kali, "Ewe Abu Dharr! Ninayo Taarifa kwamba wewe umekuwa na msimamo wa kumuabudu Mwenyezi Mungu Ambaye haonekani. Watu mashuhuri wa kabila letu wamekasirika na msimamo wako huu. Wanasema kwamba Abu Dharr amewatukana miungu yao na anawaita hawana hekima yoyote.

Ewe Abu Dharr! Tunakuheshimu lakini haimaanishi kwamba tupo tayari kustahamili miungu yetu kubezwa. Ninakuomba uache hoja ya mawazo yako ya sasa na urudi kwenye imani ya wahenga wako, au vinginevyo unatakiwa uieleze imani yako kwangu ili niweze kuelewa ukweli wa imani yako. Pia, ninakuhakikishia kwamba nitafikiria kuingia kwenye imani hiyo endapo utathibitisha kwamba imani yako haina shaka zaidi kuliko ya kwetu.

Abu Dharr naye alijibu, "Ewe mtemi wa kabila! Tunakuheshimu na kustahi chochote unacho sema. Lakini, wakati huo huo tunataka kueleza kwamba Mwenyezi Mungu, wa Pekee Ambaye tumeamua kumuabudu na Ambaye tunamwamini, ni huyu huyu ambaye ameumba dunia na mbingu, Ambaye huruzuku viumbe vyote, Ambaye kudhibiti maisha ya viumbe vyote vyenye uhai na Ambaye uwezo wake hauna mipaka.

Masanamu ambayo tumekuwa tunayaabudu hadi sasa, yametengenezwa na mikono yetu kwa kutumia patasi na nyundo. Akili inaweza kuamrisha kwamba yule ambaye ametengenezwa na mikono yetu anaweza kuwa muumbaji wetu, anaweza kuruzuku na tusikiliza dua zetu?

Mwanadamu ni kiumbe bora zaidi kuliko viumbe vya muumbo wote. Inawezekana yeye na heshima yake astahili kuinamisha kichwa chake mbele ya jiwe? Mtemi wangu! Tafadhali tafakari bila upendeleo kuhusu haya ninayosema. Masanamu hayana hata uwezo wa kufukuza adui yao.

Nisikilize, ewe mtemi! Wakati fulani nilikwenda kwa Manat na nikampa sadaka ya kikombe cha maziwa. Nilikuwa bado nipo eneo hilo ambapo mbweha alifika hapo na akanywa maziwa hayo yote na akamkojolea Manat. Tukio hili liliniathiri sana na nilifikiri kwa nini mungu anashindwa kujilinda mwenyewe?

Jambo hili lilinidhihirishia kwamba sanamu haliwezi kuwa mungu. Nina uhakika na kila mtu mwenye akili ataamini kwamba Muumbaji wa mbingu ni bora zaidi kuliko mbingu na muumbaji wa dunia ni bora zaidi kuliko ardhi. Kwa mujibu wa kanuni hii yenye mantiki, masanamu hayawezi kuwa ni bora kuzidi sisi, haina maana sisi kuyaabudu.

Ewe mtemi wangu! Nimekuja kwenye kweli kwamba Mwenyezi Mungu ni Peke Yake Ambaye ni Mumbaji na mwenye kuruzuku ulimwengu, na Muhammad Mustafa ambaye alipelekwa Makkah ni Mjumbe Wake.

"Anazo sifa nzuri kama hizo hivyo kwamba hakuna afananaye Naye hapa duniani. Quraishi ambao ni maadui zake wabaya wanakubali

ukweli wake na uwezo wake. hata wanapojua kuwa Muhammad ni mpinzani mkubwa wa miungu yao na dini yao, wamempatia jina la Sadiq na Amin, kama ambavyo, nimetambua hivi karibuni tu. Sikiliza! Uso wake unang'aa nuru na hekima inatiririka kutoka kwenye maneno yake."

Mara tu Abu Dharr alipomaliza hotuba yake, kelele kubwa ilitoka sehemu zote, "Jinsi gani maneno ya Abu Dharr yalivyo matamu! Kwa hiyo, miungu yetu haisikii na haisemi! Abu Dharr ameidhalilisha imani yetu na anaitukana miungu yetu!"

Kundi moja lilisema kwa pamoja, "Rafiki zangu! Msizungumze mambo yasiyo na mantiki. Kwa uaminifu tunasema kwamba lolote alilosema Abu Dharr linaonekana kuwa sahihi na akili inataka kwamba lazima tukubali ukweli. Tunao uhakika kwamba hatuwezi kupata mwongozo mzuri zaidi kuzidi yale ambayo Abu Dharr ametuletea."

Sauti nyingine ilitokeza: "Nchi ya Arabuni inahitaji muongozaji na inaonyesha kama vile hakuna mwongoaji bora zaidi kuliko huyu ambaye amedhihirishwa na Abu Dharr."

Halafu sauti nyingine ilitokeza, "Hotuba ya Abu Dharr ni ya maana sana." na baada ya hii sauti ya juu sana ilitokeza; kama vile ingetoboa masikio, Ewe Abu Dharr! Ninashahidilia kwamba hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu na ninakiri kuamba Muhammad ni Mtume Wake!"

Alipoona hivi, Khafaf, mtemi wa kabila, baada ya kufikiri sana alinyanyua kichwa chake na akawaambia watu wake: "Wapendwa watu wa kabila langu! Nisikilizeni kwa makini. Mmesikia yote hayo aliyoyasema Abu Dharr. Ni wajibu wetu kutafakari kuhusu hotuba

yake kwa uangalifu sana na kwa makini sana na tuweze kuona inayo kiasi gani cha ukweli.

Uamuzi wa haraka haufai. Si busara kutupilia mbali ushauri wa mtu bila kuchunguza. Rafiki zangu! Mnatambua kiasi cha machafuko yaliopo miongoni mwetu na jinsi uhalifu ulivyo zidi ambao sisi tunahusika. Matajiri wanawanyonya masikini na hakuna mipaka katika kufanya dhambi na maovu.

"Mimi nimeamua kwamba lazima nikubali na kuunga mkono yale anayoyasema Abu Dharr. Sasa ni juu yenu nyinyi kujiamulia wenyewe. Sikilizeni nyinyi nyote. Ninashahidilia kwamba hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu na Muhammad ni Mtume wake!"

Mara tu Khafaf alipotamka Kalimah (la ila ha illalah Muhammadan Rasulillah) palitokea kelele kubwa ndani ya kabila, Khafaf amekuwa Muislamu. Khafah ameingia Uislamu!"

Haikupita muda mrefu baada ya Khafaf kuingia kwenye Uislamu, hali ya kabila ilibadilika kabisa. Watu walio wengi walisilimu na kuwa Waislamu hapo hapo, ambapo wengine walingojea kukubali kuwa Waislamu mbele ya Mtukufu Mtume baada ya kuwasili huko Madina.

Kwa ufupi, kwa juhudi kubwa ya Abu Dharr watu wengi wa kabila la Ghifar walikubali kuwa Waislamu na palitokeza ukelele wa "Mungu Mkubwa! na "Mungu ndiye Mwenye Kusifiwa!" na jina la Mtukufu Mtume likaanza kutangazwa mchana na usiku.

Baada ya kujaza moyo wa Uislamu kwenye kabila la Ghifari na kuwasilimisha watu na kuingia kwenye Uislamu, Abu Dharr alielekeza umakini wake Asfan. Alipofika huko alianza kuhubiri Uislamu miongoni mwa watu. Kwa kuwa sehemu hii ilikuwa kwenye njia kuu iliyotumiwa mara nyingi na Quraishi na alijenga hisia dhidi yao kwa sababu ya mateso aliyofanyiwa nao alifanya zoezi la nidhamu kali katika kuwafanya kuwa Waislamu. Kundi la Quraishi lilipopita hapo, aliwaeleza habari ya Uislamu na kwa hiyo idadi kubwa ya Quraishi walikubali kuwa Waislamu.

SURA YA NNE

Abdul Hamid Jaudatus Sahar wa Misri ameandika, Uislamu ulienea Madina kama moto wa mbuga ya majani makavu." Kabila la Ghifar lilifurahishwa sana na hali hiyo. Waislamu walipongezana wao kwa wao kwamba makabila mawili ya Aus na Khazraj, ambao walikuwa wasemaji sana, wapiganaji wazuri sana na waunga mkono wazuri sana walikubali kuingia kwenye Uislamu, na pia kwa kuwa Mwenyezi Mungu alikwisha ridhika kuinyanyua dini Yake na alinuia kumsaidia Mtukufu Mtume na kutimiza ahadi yake.

Unais alikwenda kwa kaka yake Abu Dharr akiwa na habari za kufurahisha na akasema "Uislamu umeenea Madina na Aus na Khazraj wamekubali Uislamu!"

Abu Dharr akasema, "Mtume wa Mwenyezi Mungu atakwenda na kuhamia huko baada ya kipindi kifupi."

Unais alimwangalia kaka yake kwa mshangao na alisema, "Umepokea habari zozote za aina hiyo?"

Abu Dharr, "Hapana, wala sina taarifa yoyote kuhusu habari hizi, ama kujua kwamba watu wa Yathrib wamekuwa waumini."

Unais, "Vipi sasa ulijua kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu atahamia Yathrib?"

Abu Dharr, "Aliniambia siku hiyo hiyo nilipokutana naye, kwamba alitarajia kwenda kwenye mji wa mitende na nadhani sehemu hiyo ya Yathrib, Mtume alisema kweli."

Unais, "Inawezekana kwamba kabila lake litamruhusu aondoke hapo akiwa na Waislamu, ili kwamba baada ya matayarisho kamili awashambulie?"

Abu Dharr, "Wanaweza wakamruhusu au wasimruhusu, lakini baada ya kipindi kifupi atahamia huko. Kama mambo yalivyo, ni Mwenyezi Mungu tu ndiye anaye jua ni vipi na lini itatokea."

Abu Dharr alisilimisha kabila lake na kuingia kwenye Uislamu baada ya yeye kuwa muumini. Halafu akaelekeza shughuli hiyo Madina. tangu aliporudi kutoka Makkah hadi kuhama kwa Mtukufu Mtume, Abu Dharr alikuwa anashughulika na kuhubiri Uislamu na aliendelea kufanya juhudi kuipeleka dini ya Mungu kwa umma Mtukufu Mtume aliendelea kufanya kazi yake ya kuhubiri Uislamu na Quraishi waliendelea kufanya kazi yao ya kumtesa Mtume. Walimpa mateso makubwa sana hivyo kwamba hakuwa na uchaguzi mwingine isipokuwa kuondoka nyumbani kwake. Kwa ufupi, kwa amri ya Mwenyezi Mungu Jibril alimwambia aondoke Makkah baada ya kumwambia Ali alale kwenye kitanda cha Mtume.

Alifanya alivyoagizwa. Alimwambia alale kitandani pake na akaondoka, hivyo kwamba Quraishi hawangejua kama hayupo kitandani pake. Baada ya kukaa siku tatu kwenye pango la Hira aliondoka kwenda Madina.

Abu Dharr alikuwa anangojea uhamiaji Madina. Watu wa kabila lake pia walikuwa wanangojea na walikuwa wanauliza mara kwa mara habari za Mtukufu Mtume kwa mtu yeyote aliyetokea sehemu hiyo.

Kuanzia Makkah na baada ya kukaa kwa muda wa siku chache pangoni, Mtume aliondoka kwenda Madina. Kabila la Ghifar lilipopata taarifa kwamba alikuwa kati ya Makkah na Madina walifurahi sana. Abu Dharr alihisi wimbi la neema lilikuwa linakuja. Aliungana na kabila kungoja.

Watu walikusanyika na kumzunguka na walimuuliza kuhusu Mtume wa Mwenyezi Mungu, mwenendo wake na umbile lake alijibu, "Mtamuona baada ya muda si mrefu.

Yeye ni bora kuliko wote na anamzidi kila mtu kwa sifa." Watu walipongojea kwa kipindi kirefu, Abu Dharr alikuwa anaangalia njia, ili awe mtu wa kwanza kuwataarifu watu atakapo wasili Mtume na kutuliza nyoyo za watu na kuondoa hofu iliyokuwa inawaelemea kwa kungojea kwa kipindi kirefu hivyo.

Muda uliendelea kupita. Watu wa kabila la Ghifar walikuwa na shauku kubwa ya kumpokea Mtume. Abu Dharr alipotupa jicho aliona ngamia anakwenda hapo. Watu wote walikuwa wanaangalia macho ya Abu Dharr. Baada ya muda mfupi, Abu Dharr akasema kwa sauti ya kushangaa, "Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mtume anawasili!"

Allamah Subaiti ameandika, "Uso wa Mtukufu Mtume ulikuwa unatoa nuru. Kwa ufupi watu wote walimfuata Abu Dharr, huku wakisema kwa sauti moja, "Mtume wa Mwenyezi Mungu amekuja! Mtume wa Mwenyezi Mungu amekuja!" Abu Dharr alikwenda mbele haraka na akashika hatamu ya ngamia wake.

Watu walianza kusema, "Allahu Akbar." (Mwenyezi Mungu Mkubwa) huku wakimzunguka Mtume kwa hamu kubwa. Wanawake wote, vijana na vikongwe, wavulana na wasichana walikuwa wanashangilia kwa furaha kubwa. Mtume wa Mwenyezi Mungu amewasili! Mtume wa Mwenyezi Mungu amewasili!"

Baada ya hapo watu wa kabila la Aslam walisema, "Pia na sisi tumekuwa Waislamu kama walivyo fanya ndugu zetu wa kabila la Ghifar." Mtume wa Mwenyezi Mungu alifurahi sana na alinyanyua mikono yake kuelekea mbinguni aliomba, "Ee Mola wa ulimwengu! Wasamehe kabila la Ghifari na uwaweke kabila la Aslam salama."

Baada ya hapo Mtukufu Mtume aliteremka kwenye ngamia na akaanza kukariri Quran. Sauti yake iliingia kwenye nyoyo za watu. Halafu akaanza kuhubiri. Watu walikwenda mbele kwa makundi na kutoa kiapo cha utii kwake. Abu Dharr alisimama kwa maringo karibu na Mtume akiwa amefurahi kupita kiasi.

Watu wa kabila la Ghifari walijitokeza mbele na wakasema, "Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Abu Dharr alitufundisha yote yale uliyomwambia. Tukasilimu na kuwa Waislamu na tukakiri kwamba wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu."

Baada ya hapo watu walifurahi sana na walikuwa wanaangalia uso wa Mtume mara kwa mara. Abdul Hamid Jaudatus Sahar ameandika, "Watu walianza kuangalia uso wa Mtume kwa makini, waliona kwamba alikuwa mtu mwenye uso unao ng'aa midomo inayo tabasamu na tabia njema kuhusu umbo lake, hakuwa mwembamba au aliye konda ama mnene. Alikuwa na sura nzuri ya kupendeza.

Macho yalikuwa makubwa na meusi, kope za macho zilikuwa ndefu, nyusi zake nyeusi zilizojikunja mfano wa tao, nywele nyeusi, shingo

ndefu na ndevu nyingi. Alikuwa Mtukufu wakati ametulia na alikuwa anatia moyo kwa heshima wakati anasema. Mazungumzo yake yalikuwa matamu. Wala hakuwa mkimya au msemaji. Alikuwa na sura ya kupendeza sana akiwa mbali na mzuri sana akiwa karibu.

Saizi ya umbile lake ilikuwa ya kati, wala hakuwa mrefu sana kiasi cha kutokupendeza kumwangalia, ama mfupi sana kiasi cha kufikiriwa kuwa mtu duni.

Baada ya hapo Mtukufu Mtume aliondoka kwenda Madina na Abu Dharr aliendela kuishi na kabila lake."

Kutoka hapo, Mtukufu Mtume aliondoka kuelekea Madina. Alipofika Madina, watu walimkaribisha kwa moyo mkunjufu. Mara tu baada ya kufika, alianza kuhubiri ujumbe wa Uislamu. Abu Dharr ambaye hakuweza kumsindikiza Mtukufu Mtume huko Madina aliishi mjini kwake kwa kipindi kirefu sana hivyo, vita kuu tatu za Kiislamu (Ghazawat) vita vya Badr, mwaka wa 2, Hijiriya, Uhud mwaka wa 3 Hijiriya, na Ahzab mwaka wa 5 Hijiriya zilipiganwa hadi mwisho.

Baada ya vita ya Ahzab, aya ya Quran Tukufu ilimlazimisha Abu Dharr kuondoka kwenda Madina. Siku moja alikuwa anashughulika na dua baada ya Swala ya jioni kwenye msikiti wa mjini kwake, ambapo alisikia mtu anasoma kwa sauti Aya (61:10)

"Enyi mlio amini! Nikuonyesheni biashara itakayokuokoeni na adhabu iliyo chungu ."(61:10)

Baada ya kutafakari maana ya Aya hii alipata shauku ya Jihadi na akamwambia Unais, "Nitaondoka kwenda Yathrib kesho."

Unais: "Sawa! Nenda. Mwenyezi Mungu na akufikishe huko Salama!"

Abu Dharr, "Sitarudi. Nitatumia maisha yangu yote katika kumtu-mikia Mtukufu Mtume."

Unais, "Ewe ndugu yangu! Umekuwa muumini wa kweli na imani imepenya kwenye moyo na roho yako. Kabila lako na watu wako hapa wanakutaka sana. Patakuwepo pengo kubwa sana ukiondoka hapa. Nadhani ungeacha mpango wa kwenda Madina na uishi hapa hadi mwisho wa uhai wako."

Abu Dharr; "Mtukufu Mtume ni bora zaidi kuliko watu hawa. Chochote ambacho kimetekelezwa kinatosha. Mtukufu Mtume alipigana Badr, Mimi sikuwa naye. Akapigana huko Uhud Mimi si kuwepo. Hadi lini nitaendelea kulitumikia kabila langu na nikose baraka za kufa shahidi. Yote hayo ambayo yamefanyika mpaka sasa yanatosha. Sasa sitakata tama hata kwa dakika moja kuhusu uamuzi wangu wa kwenda Yathrib."

Unais, "Pendekezo langu ni kwamba wewe uendelee kuishi hapa nyumbani kama kawaida. Mtukufu Mtume atakuita yeye mwenyewe atakapokuhitaji. Wewe angalia walikuwepo watu wengi waliokuwa katika miji ya kwao na waliondoka kwenda Madina baada ya kuitwa na Mtukufu Mtume."

Abu Dharr akasema: "muda wa kungojea umepita. Endapo Mtume hajaniita mimi pia nina wajibu. Sitaendelea kungoja, nitakwenda huko bila kuitwa."

Unais: "Vema! Lakini usifanye haraka. Chukua mahitaji ya muhimu kwa safari."

Abu Dharr; "Sihitaji chochote. Vipande vya mikate mikavu vinanitosha."

Abu Dharr aliondoka nyumbani kwake na kuelekea Madina. Alipofika huko alipata heshima ya kukutana na Mtume na akawa naye.

Alikuwa na desturi ya kulala kwenye msikiti wa Mtume usiku na wakati wa mchana alikutana na watu. Alikula chakula pamoja na Mtume na akaiga maisha yake ya kidunia kwa uchaji Mungu na uadilifu. Alifanya bidii sana kujifunza hadithi za Mtume na kuzihifadhi katika kumbu kumbu.

Baada ya kuifika Madina Abu Dharr aliugua kwa sababu ya mabadiliko ya hali ya hewa. Mtume alipata taarifa ya ugonjwa wake. Akaenda kumuona Abu Dharr na akamwambia; "Abu Dharr! Unatakiwa uishi nje ya Madina kwa muda fulani sehemu ambayo ngamia, kondoo na mbuzi wa taifa huchungwa na uzingatie kwamba usile chochote isipokuwa maziwa wakati wote utakapo kuwa kule."

Mara tu baada ya kupokea amri ya Mtume, Abu Dharr aliondoka kwenda mahali hapo alipoambiwa akiwa na mkewe.

Ugonjwa ulikuwa mkali sana kwa kipindi cha siku kadhaa lakini, ulipungua pole pole akapata afya nzuri hadi akaweza kutimiza tendo la ndoa na mke wake. Sasa, palijitokeza tatizo la upatikanaji wa maji kwa ajili ya josho kubwa la kuondoa janaba kabla ya Swala. Hadi hapo alikuwa hajajua Tayamamu. Kwa hiyo alikuwa hajui la kufanya kwa muda fulani. Hatimaye akili yake ilimwongoza na akaenda kumuona Mtume kwa mwendo wa haraka sana wa ngamia. Mara tu

Mtume alipomuona Abu Dharr alitabasamu na alisema kabla Abu Dharr hajasema, "Abu Dharr! Usiwe na wasiwasi. Maji yametayarishwa kwa ajili yako hapa na sasa hivi. kwa hiyo, msichana aliyekuwa mtumishi wa Mtume alitayarisha maji na Abu Dharr akaoga. Baadaye alikwenda kwa Mtukufu Mtume na aka fundishwa jinsi ya kutumia udongo kwa ajili ya kuchukua Wudhu (Tayamamu)- (Musnad Ahmad bin Hanbal).

Abu Dharr alikuwa anaendesha maisha yake ambapo Vita ya Tabuk ilitokea mnamo mwaka wa 9 Hijiriya. Waandishi wa historia wanasema kwamba Mtume alijua kwamba Wakristo wa Syria walifanya uamuzi thabiti wa kushambulia Madina na wapiganaji elfu arobaini kutoka kwa Harcules, Mfalme wa Roma. Kwa hiyo, Mtume aliamua kuondoka kwenda Syria kama hatua ya tahadhari akiwa na wapiganaji kati ya elfu thelathini hadi arobaini. Alimteua Ali kuwa mbadala wake Madina. Baada ya kutayarisha jeshi lake aliondoka Madina.

Baada ya kuondoka Mtume wanafiki walianza kumdhihaki Ali kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu alimwacha ili kupunguza mzigo wake mwenyewe. Katika kuwathibitishia kwamba wanafiki ni waongo aliamua kwenda kwa Mtume.

Kwa kufuatana na Mtume mahali paitwapo Jaraf na akamtaarifu kuhusu dhihaka ya wanafiki.

Mtume akasema, "Wanafiki ni waongo. Nimekuja hapa baada ya kukufanya wewe kuwa kaimu wangu. Ewe Ali hufurahikii cheo chako cha juu zaidi. Uhusiano wako na mimi ni sawa na uhusiano aliokuwa nao Harun na Musa ila tofauti moja tu ni kwamba hapatakuwepo na Mtume baada yangu. Maana yake ni kwamba Musa alipokwenda kwenye Mlima wa Tur alimteua Harun kuwa kaimu (wakili) wake na yeye (Mtukufu Mtume) alifanya namna hiyo hiyo."

Aliposikia hivi Ali alirudi Madina na Mtume aliendelea na safari ya kwenda Tabuk sehemu iliyokuwa kwenye mpaka wa iliyokuwa Falme ya Roma katika urefu wa vituo kumi kutoka Madina na Dameski. Alipofika Tabuk, alikaa hapo kwa muda wa siku kumi. Wakati wa kuwepo yeye hapo, alimtuma Sariys (jeshi la Uislamu linaloongozwa na mtu mwingine na si Mtume) sehemu zote, na alisisitiza kuwaita watu waingie kwenye Uislamu. Hakuna jeshi lililofika hapo kutoka Roma kwa madhumuni ya vita. Kwa hiyo, alilazimika kurudi Madina.

Wakati wa safari hiyo, siku moja usiku wanafiki walitaka kumuua wakati anapita kwenye bonde la Aqaba Zi Fata, kwa kumuogofya ngamia wake, ambaye angeweza kumwangusha chini, lakini Hudhayfah bin Yaman na Ammar bin Yasir walimwokoa. Baada ya Mtukufu Mtume kuvuka bonde, alimwambia Huzayfah bin Yaman majina ya wanafiki waliotaka kumuua kwenye giza, na akamuamuru kuwa majina hayo iwe siri yake. Masahaba maarufu walikuwemo kwenye orodha hiyo.[1] Kwa mujibu wa Tahzibut Tahzib, watu hao walijaribu kupata majina hayo kutoka kwa Hudhayfah lakini hakufichua.

Hatimaye mmoja wapo wa masahaba hao alikiri mwenyewe, "Uniambie ama usiniambie, kwa jina la Mwenyezi Mungu, mimi nilikuwa miongoni mwa wanafiki hao!" Kwa ufupi, Mtume alirudi Madina wakati wa mwezi wa Ramadhani.

Wakati wa kuondoka kutoka Madina kwa madhumuni ya Vita ya Tabuk, Abu Dharr alikuwa naye. Lakini kwa kuwa ngamia wake alikuwa dhaifu na kukonda, hakuweza kuwa katika msafara. Abu Dharr, hata hivyo, alibaki nyuma ya msafara kwa umbali wa muda wa safari ya siku tatu.

Alijitahidi sana kuwa karibu na Mtume lakini alishindwa. Alihuzunika sana alipotambua kwamba haingewezekana yeye kuwa ndani ya msafara.

Kwa mujibu wa maelezo mengine, alipobaki nyuma, watu fulani walimwambia Mtume kwamba ilikuwa vigumu sana Abu Dharr kuwa naye. Aliposikia hivi, Mtume akasema, "Mwacheni huyo hivyo alivyo. Atafika Inshallah. Kwa hiyo msafara uliendelea na Abu Dharr alizidi kubaki nyuma akiwa amefadhaika na wasi wasi.

4

MAISHA YA ABU DHARR

Wakati mwingine alifikiria kurudi Madina na halafu tena alishawishika kuendelea na safari hadi Tabuk kwa jinsi yoyote ile kwa sababu kuwa nyuma ya Mtume ni hali ambayo ilimtesa sana.

Aliendesha ngamia wake kwa msisimko mkubwa lakini hakuweza kwenda haraka kwa sababu ya udhaifu wake.

Alipogundua hivi, aliteremka kutoka kwenye ngamia na akachukua mzigo wake wote na kubeba mgongoni mwake na akaendelea na safari kwa mguu. Ulikua msimu wa joto kali. Kwa hiyo, ni jambo linalojulikana kwa wasafiri kiasi cha ukali wa kiu ambayo ingempata.

Alikuwa anatembea na mzigo mgongoni mwake wakati ambapo kiu ilikaribia kumwelemea. Tayari alikwisha choka na wakati huo kiu ilifanya hali yake kua mbaya zaidi. Abu Dharr akiwa na kiu kali, alitafuta maji huku na kule akaona maji ya mvua yaliyokuwa kwenye dimbwi. Akafika kwenye dimbwi la maji ambapo alikuwa na kiu sana, na alitaka kunywa maji yaliyojaa kwenye kiganja chake, ambapo ghafla, aliwaza kwamba maji hayo yalikuwa baridi sana na haikuwa vema yeye kunywa maji hayo kabla ya Mtukufu Mtume. kwa hiyo, baada ya fikra hii kuingia akilini mwake akayamwaga maji hayo na akajaza maji hayo kwenye gudulia.

Abu Dharr alikuwa peke yake huku akiwa na kiu kali sana na gudulia lililojaa maji hadi akafika kwenye mipaka ya Tabuk.

Mara tu alipofika kwenye mipaka ya Tabuk, Waislamu walimuona na wakamtaarifu Mtume kuhusu kuwasili kwa msafiri aliyedhikika. Mara moja alisema, huyu ni sahaba wangu, Abu Dharr. Kimbieni, enyi masahaba wangu, na mleteni kwangu. Waliposikia hivyo, masahaba walikwenda haraka kwa Abu Dharr na wakamfikisha kwa Mtume.

Baada ya Mtume kuuliza kuhusu afya yake, akasema, "Ewe Abu Dharr, unayo maji. Kwa nini basi unakiu kali namna hii?"

Abu Dharr; "Bwana wangu, kama unavyoona, maji yapo, lakini siwezi kunywa."

Mtume; "Kwa sababu gani?"

Abu Dharr; "Bwana wangu! Nilipokuwa njiani. Kuja hapa niliona maji karibu na kilima, lakini dhamiri yangu haikuniruhusu kunywa maji haya kwa ajili yako. Mimi nitayaonja baada ya wewe kunywa."

Aliposikia hivi Mtume alisema; "Ewe Abu Dharr! Mwenyezi Mungu Atakuhurumia. Utaishi peke yako na utaondoka hapa duniani peke yako. Utafufuka peke yako mnamo Siku ya Hukumu. Utaingia Peponi peke yako na kundi la watu wa Iraq watapata furaha kamili kwa sababu yako, ni kwamba watakuosha watakuvika sanda na kusalia maiti yako."

Tukio hili si tu linaonyesha mapenzi makubwa ya Abu Dharr kwa Mtume lakini kupitia kwenye tukio hili Mtukufu Mtume kwa wazi kabisa alitabiri matatizo na majanga ambayo yangemfika Abu Dharr katika maisha yake. Ni dhahiri kutoka katika maneno ya mwanachuo wa madhehebu ya Shia yangemtokea Abu Dharr. Amenukuu tukio kutoka kwa Bin Babway kutoka kwa Abbas kwamba siku moja Mtume(s.a.w.w) alikuwa ameketi ndani ya msikiti wa Quba na masahaba wake wengi walikuwa wamemzunguka.

Alisema, "Mtu ambaye atakuwa wa kwanza kuingia kwenye lango la Msikiti huu, atakuwa ametoka kwenye kundi la watu wa Peponi." Baada ya muda mfupi Abu Dharr aliingia kupitia kwenye lango hilo. Alikuwa wa kwanza ambaye alitoka nje akiwa peke yake. Mtukufu Mtume akasema hapo hapo, "Ewe Abu Dharr! Wewe unatoka kwenye watu wa Peponi." Aliendelea kusema, wewe utafukuzwa Makkah kwa sababu ya kuwapenda watu wa Nyumba yangu. Utaishi ugenini na utakufa katika hali ya upweke. Kundi la watu wa Iraq wataneemeka kwa kushughulikia maziko yako na utakuwa pamoja na mimi Peponi."

SURA YA TANO

Historia inashuhudia kwamba Abu Dharr alielimika sana baada ya kuwa Muislam hivyo kwamba hapakuwepo wa kumlinganisha naye miongoni mwa masahaba. Alipata utakaso ulio bora wa imani na unyofu wa moyo hivyo kwamba alihakikisha kwamba yeye ni nguzo ya nuru kwa watu wenye utambuzi. Alizirutubisha akili za watu kwa ushauri, baada ya kuja kwa Uislamu, aliwafundisha watu masomo ya usawa na upendo na aliwafundisha jinsi ya kumtii Mwenyezi Mungu na Mtukufu Mtume.

Maisha yake ya Kiislamu yaliheshimika sana hivyo kwamba hapakuwepo na mtu wa kulingana naye miongoni mwa waumini. Abdulah Subaiti ameandika kwamba Abu Dharr alijipatia sifa sana miongoni mwa masahaba hao ambao walifanya vizuri kuzidi wengine katika uchaji Mungu, kujihini, kumuabudu Mwenyezi Mungu, ukweli,

uimara wa imani na hakuna wa kumfananisha katika kujisalimisha kwa Radhi ya Mwenyezi Mungu. Wakati wa uhai wa Mtume(s.a.w.w) chakula chake cha kila siku kilikuwa kilo tatu za tende na aliendelea hivyo hadi mwisho wa maisha yake.

Anaendelea kuandika Abdullah Subaiti kwamba Abu Dharr alinyanyuliwa juu sana katika maadili na tabia yake hiyo kwamba Mtukufu Mtume alimjumuisha kwenye kundi la Ahlul-bait (watu wa Nyumba ya Mtume) kama alivyo mjumuisha Salman Farsi. Hafiz Abu Naim anasema kwamba Abu Dharr alikuwa msalihina, mtu mchaji Mungu, na alikuwa na moyo ulioridhika. Alikuwa mtu wa nne katika msululu wa kukubali Uislamu. Aliacha maovu yote hata kabla ya kuanza kutekeleza sharia ya Kiislamu. Hili lilikuwa lengo lake alilolihifadhi, kukataa kuwatii watawala dhalimu. Alikuwa imara katika kuvumilia maumivu na huzuni. Alijipatia sifa ya juu katika kuhifadhi hadithi na nasaha za Mtukufu Mtume.

Abu Naim ameandika kwamba Abu Dharr alitoa huduma kubwa kwa Mtukufu Mtume na alipata ujuzi wa vipengele vya imani na utekelezaji akiwa naye, na alijiepusha na maovu. Sifa yake maalum ilikuwa kuuliza maswali kwa Mtukufu Mtume. Alijifunza kuhifadhi maana na fahamu zilizotolewa na yeye (Mtume) na alikuwa na shauku sana kuhusu jambo hili. Kwa ufupi, kwa kadiri alivyoweza, hakuridhika na kuuliza maswali tu lakini pia alikusanya hazina kubwa ya ujuzi wa Kiislamu kwa ajili ya wafuasi wa Uislamu.

Kitendo kingine maarufu cha maisha yake ni kwamba alifuata nyayo za Mtukufu Mtume alizozitilia maanani na kuzithibitisha, na ambazo aliziamuru zifuatwe.

Akaambatana na Imamu Ali baada ya Mtukufu Mtume na hakumkana hata kidogo. Alimfuata na alipata manufaa kutokana na ujuzi mkubwa

wa Imamu Ali. Abu Dharr alihifadhi akilini anasa za mwili, ukarimu, maadili mema na tabia njema za Imamu Ali. Ndio sababu Mtume(s.a.w.w) alisema, "Abu Dharr ni Mtu mkweli zaidi katika taifa hili."

Mahali pengine alisema, "Abu Dharr yu kama Mtume Isa katika ibada ya kujinyima anasa za mwili." Kwa mujibu wa hadithi alisema, "Mtu anayetaka kuona mfano wa maisha na staha ya Isa amwangalie Abu Dharr."

Ni dhahiri kwamba ibada ya dini kama alivyofanya Abu Dharr, haikuwekewa mpaka kwenye Swala peke yake. Alikuwa hodari kiutendaji katika aina zote za ibada. Ni jambo lisilo na upinzani kwamba, kutafakari kuwepo kwa Mwenyezi Mungu na muumbo wake, pia ni ibada kubwa. Abu Dharr alifanikiwa katika ibada hii pia.

Waandishi wa historia na hadithi wanakubaliana kwa pamoja kwamba Abu Dharr alipata kiwango kikubwa cha ujuzi na hii ilikuwa kwa sababu alipata ujuzi kwa moyo ulio nyooka wakati anafuatana na Mtukufu Mtume. Alimuuliza maswali Mtume kila wakati na alijifunza na kuhifadhi majibu yake. Alikuwa na uzoefu mkubwa wa ujuzi wakati anafuatana na Mtume. Mwandishi wa Kitabu Darayatus Rafiah anasema kwamba Abu Dharr alihesabiwa katika safu ya wanachuo wakubwa na washikilia maadili na alikuwa na daraja la pekee la kitaalam. Alikuwa sahaba mwandamizi wa Mtume alikuwa miongoni mwa watu hao waliotimiza agano lao na Mwenyezi Mungu yaani, watu hao walitimiza ahadi ambayo waliahidiana Naye kuhusu wao kuwa wafuasi wa imani iliyokamilika, na alikuwa mmojawapo wa wale watu wanne ambao waumini wote wanawajibika kuwapenda.

Allamah Manazir Ahsan Gilani ametoa maelezo mafupi kuhusu utaalamu wa juu wa Abu Dharr, ameandika, Soma tamko la Ali,

mbora wa majaji miongoni mwa masahaba, na lango la Ujuzi na uhitimishe mwenyewe kwamba anaposema, "Abu Dharr alikuwa na shauku na hamu kubwa ya kupata ujuzi;" anasema jambo lililo sahihi.

Je! Hivi ushahidi huu wa Iman Ali, hauhalalishi madai ya Abu Dharr? Wakati mwingine Abu Dharr mwenyewe alikuwa akisema kwa shauku kubwa, "Tumetenganishwa na Mtukufu Mtume wakati ambapo hakuna hata mmoja wetu ambaye anaweza kujitegemea mwenyewe, kwa sababu bado hatujajua mambo fulani maalum."[2]

Allamah Gilani ameandika kuhusu ujuzi wa Abu Dharr, "Mtu mmoja alimuuliza Imamu Ali, alimfikiriaje Abu Dharr. Akamjibu kwamba wa'aa ilman ajaza fike, yaani 'Yeye, Abu Dharr alihifadhi ujuzi ambao ulimuemea.'

Umesoma na kuona jinsi alivyo kuwa mwepesi kukubali fikira, na wewe mwenyewe unaweza kukisia kutokana na matukio. Ndio maana kila mara alikuwa tayari kutekeleza kwa mujibu wa vile alivyosikia kutoka kwa Mtukufu Mtume. Kama vile alivyo jaribu kusikia kutoka kwa Mtukufu Mtume, kutoka kwa Mtukufu Mtume alitaka kutekeleza kwa vitendo bila kusita hata kidogo. Ilikuwa utashi wa dhati kuona kwamba tendo lake liliendana kwa ukamilifu na ujuzi.

Abu Dharr alinuia sana na alikuwa imara kuhusu kipengele hiki hivyo kwamba hakujali kamwe mamlaka yenye uwezo mkubwa kuliko zote hapa duniani kama ingekuwa kipingamizi chake. Hotuba na ushawishi hazikuweza kumtikisa kutokana na msimamo wake aliokuwa nao.

Akajivunia sifa hii wakati mwingine alisema, "Enyi watu! Mnaona siku ya Hukumu, mimi nitakuwa karibu sana na Mtume(s.a.w.w) na

kundi lake, kwa sababu nimemsikia akisema kwamba atakayekuwa karibu sana naye mnamo siku ya Hukumu atakuwa mtu ambaye ataondoka katika dunia hii katika hali ile ile ambayo alimwacha. Ninaapa kwa jina la Mwenyezi Mungu kwamba sasa hapana yeyote aliye achwa miongoni mwenu ambaye yumo katika hali ile ya wakati wa uhai wa Mtukufu Mtume isipokuwa mimi na sijanajisiwa na kitu chochote kipya. (Tabaqat bin Sad na Musnad ya Ahmad bin Hanbal).

Hili halikuwa dai la haki peke yake tu, lakini pia kiongozi wa dunia na Mtume wa mwisho alishuhudia hivyo.

Allamah Subaiti amesema kwamba mifano ya uadilifu iliyowekwa na Abu Dharr inastahili pongezi. Msimulizi anasema, "Nilipomuona Abu Dharr amejifunika blanketi na amekaa kwenye kona ya msikiti, nilimuuliza kwa nini alikuwa amekaa peke yake hapo? Alisema kwamba alimsikia Mtukufu Mtume anasema, "Ni vizuri kukaa kwenye kona peke yako kuliko kuketi katikati ya kundi la watu wabaya na ni vema kuketi na watu wenye maadili mema kuliko kuketi peke yako. Kimya ni kizuri kuliko kusema jambo baya na kusema jambo zuri ni vema kuliko kunyamaza kimya."

Abu Dharr alisema kwamba Mtukufu Mtume amemwambia mengi kuhusu maelekezo ya maadili mema. Yapo Saba:

Fanya urafiki na watu masikini na jaribu kuwa nao karibu.

Ili uweze kuboresha hali yako waangalie watu wenye hali ya chini

kuzidi wewe na usijilinganishe na watu wenye hali nzuri kuzidi yako.

Usimwombe mtu yeyote msaada wa mambo ya kidunia na ujenge tabia ya kuridhika.

Wahurumie ndugu zako na wasaidie wanapohitaji msaada. Usisite kusema kweli hata kama dunia itakugeukia wewe.

Usijali shutuma za Kafiri kuhusu Mwenyezi Mungu.

Kila mara sema. "La hawla wa la quwwata illa billah." (Hapana mweza isipokuwa Mwenyezi Mungu). Kwa maneno mengine, 'Mwenyezi Mungu ni Uwezo Usiowezwa.

Abu Dharr anasema, baada ya kusema mambo haya, Mtume alisema huku anashika kifua changu, "Ewe Abu Dharr hakuna busara nzuri zaidi kama kupanga mambo vizuri, hakuna uchaji Mungu ulio bora zaidi kama kujizuia na hapana kitu kizuri zaidi kama maadili mema."

Allamah Gihani alikinukuu Musnad ya Ahmad bin Hanbal anataja madili mawili tu miongoni mwa maadili haya yaliyotajwa hapo juu, ambayo yanaendana na kufanya urafiki na watu maskini na kuwatazama watu wenye hali ya chini kuzidi ya kwako, na halafu ameandika: "Kwa kweli, haya ndio marekebisho mazuri kuliko yote dhidi ya maradhi ya kupenda utajiri na kupenda anasa za dunia. idhaniwe kwamba yupo mtu ambaye analo shati la Muislamu na suruali ndefu kuvaa, mkate wa ngano na nyama ya kondoo kwa ajili ya chakula, na nyumba ya udongo wa mfinyazi iliyo pangwa vizuri na safi kuishi humo. Sasa, endapo mtu huyu anajilinganisha na mtu ambaye hana kitu isipokuwa nguo iliyo duni. Mkate wa shayiri nyumba iliyoezekwa kwa mabua, atamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hali yake nzuri zaidi na hatateseka kisaikolojia, mateso ambayo angeyapata endapo angejilinganisha na mtu tajiri mwenye nguo za gharama zadi na chakula kizuri. Njia hii ndio bora zaidi kupata kujitosheleza kidunia na manufaa mengineyo ya kidunia.

Lakini wangapi miongoni mwetu wanatekeleza hivi leo? Hata ninaweza kwamba mtu hatapata matatizo yoyote endapo anafuata kanuni hii. Hii peke yake ndio kanuni ya muhimu kwa ajili ya dunia hii na kwa ajili ya Peponi, ambayo imeelezewa katika sentenso ifuatayo" ya Sheikh Sa'd, bingwa wa mashairi wa Iran.

"Nilikuwa nalilia jozi ya viatu hadi nilipo muona mtu asiyekuwa na miguu." Baada ya kupenda utajiri sehemu nyingine ya kupenda dunia ni kupenda daraja na uwezo. Hii inayo hatari zaidi na ni sababu ya uovu wa mpangilio wa dunia. Uharibifu unaendelezwa duniani na watumwa wa utajiri ni pungufu zaid kuliko ule unaosababishwa na watu wenye uroho wa cheo na uwezo.

Sababu halisi ya maradhi haya ni kwamba mtu anapohisi ubora wake katika fani fulani, husahau uwezo wa yule ambaye amemboresha, na hujifikiria yeye ni matokeo ya hivi hivi tu. Halafu hajaribu kuwafanya watu wengine, wako karibu naye, watambue umuhimu wake ambao amejipachika mwenyewe. Akiwa na hitimisho la fikra hii, hutayarisha mipango kwa mujibu wa uwezo wa akili yake. Ni mara chache sana kuonekana kwamba mtumwa wa ulafi na uchoyo ashindwe kufanya kila awezalo kwa lengo la kutimiza kusudio lake. Hujaza akili yake unafiki na wakati wote hubakia kuwepo kwake kupitia njia za halali na mbaya sana. Ubora ambao Abu Dharr alipata au alikaribia kupata, ulikuwa ule wa uchaji Mungu. Palikuwepo hofu kwamba hali ile ingemfanya kuwa na majivuno na kupenda makuu, ambayo baadaye tamaa ya hadhi na heshima huvuruga amani ya hapa duniani na Peponi. Kwa hiyo Mtume alizuia hiyo mapema na akamwambia Abu Dharr, siku moja kwa maneno ya wazi.

Mwenyezi Mungu alisema: "Enyi waja wangu! Wote nyinyi mnazo dhambi isipokuwa hao ambao nimewapa kinga. Kwa hiyo wote lazima msali mkiomba msamaha kwa utaratibu unaokubalika. Nitawasameheni.

Nitasamehe dhambi za mtu anayeniona Mimi kuwa ninao uwezo wa kutosha kumkomboa kutoka kwenye dhambi zake na kwamba ninawaokoa, na kwa mtu aliyeomba msamaha wa dhambi zake kupitia kwenye uwezo Wangu.

Enyi waja wangu! Nyote nyinyi ni wapotovu isipokuwa hao Ninawaonyesha njia iliyonyooka. kwa hiyo lazima mniombe Mimi ili niwaongoze. Wote nyinyi ni masikini na wahitaji isipokuwa wale Ninao wafanya matajiri.

Niombeni Mimi kwa ajili ya riziki yenu na kumbukeni kwamba endapo nyinyi wote walio hai na wafu, wazee na vijana, waovu na waadilifu, muungwana na kujizuia msiombe chochote kutoka kwangu hapataongezeka chochote kwenye milki Yangu. Na endapo wote nyinyi wafu na walio hai, wazee na vijana, waovu na waadilifu mnakusanyika pamoja na kuniomba Mimi niwatimizie mahitaji yenu na kuwatosheleza mahitaji yenu, hapatatokea upinzani wowote kwenye himaya yangu usiolingana hata na wingi wa maji yaliyochukuliwa na ncha ya sindano mtu anapoitumbukiza baharini. Hii ni kwa sababu Mimi ni Mkarimu, msamehevu, Mkuu, Anayetukuzwa na Aliyeko kila mahali.

Mtu yeyote anaweza kujivunia kuwepo kwake au mafanikio yake na utulivu wake baada ya kuamini ukweli wa Utulivu wa Mungu na Ufahari ambao unauona katika hali hii? Hivi mtu yeyote anaweza kuwa na kiburi hata kwa sekunde moja baada ya hapa? Mtu yeyote anayemwamini Mwenyezi Mungu anaweza kuchochea uhaini hapa duniani kwa ajili ya kituo chake cha maisha, heshima, kujionyesha na hudumu baada ya hao? Nani mwenye wazimu anayeweza kujivunia uchaji Mungu wake ambapo kila mmoja wetu ana dhambi?

Pale ambapo utajiri wa watu matajiri upo kwenye udhabiti na mamlaka ya Mwenyezi Mungu; yeyoye huyo anayeonyesha pesa si mpumbavu huyu? Endapo ni sahihi kwamba makubwa na madogo yetu hayawezi hata kwa kuungana kuongeza hata nukta moja upana wa himaya ya Mungu, mtu ambaye ni vumbi la kujaa kiganja tu atajivunia nini? Inapokuwa hii ni hali ya uhuru wake kutokana na utashi hata katika mambo ya mwongozo na ukomavu wa akili anafikiria upendeleo na uwezo a Mwenyezi Mungu kuwa ndio wakala halisi, ni katika misingi gani mhudumu wa dini au mrekebishaji atafikia juhudi zake zitastahili kuthaminiwa?

Ambapo kila kitu ni mali yake na sisi ni masikini na wahitaji, kwa nini basi kiburi hiki na kwa nini ufidhuli huu na majigambo haya?

Hizi zilikuwa amri na hotuba ambazo ziliiingiza maadili ya Mtume Isa kwenye moyo wa Abu Dharr. Hata hivyo, hali ilikuwa hiyo na hata zaidi ya Mtume alivyokuwa na desturi ya kuchokonoa tabia ya kujinyima ya Abu Dharr.

Lakini tunatakiwa kutazamna kwa makini zaidi wa upande huo wa mafundisho yake na nasaha ambamo humo ndimo Uislamu umesimama na kutofautiana na dini zingine zote.

Lazima utajihisi unataka kujaribu kufikiria kwamba kama haya yalikuwa mafundisho ya Mtukufu Mtume, kwa nini Uislamu ulipinga maisha ya utawa na kuyafikiria kuwa ni bidaa zilizoendakezwa na watawa na wahudumu wa kanisa? Nitajaribu kuelekeza usikivu wako kwenye jibu la swali hili. kwa ujumla kujizuia na uchaji mungu maana yake ni kuondoka mijini na kwenda milimani na misituni kuabudu Mwenyezi Mungu katika hali ya upweke. Abu Dharr anaeleza ifuatavyo:

Mtukufu Mtume alimwabia kwamba pia ni jambo zuri kuondoa mawe njiani, kuwasaidia wasiojiweza pia ni hisani na hata lendo la ndoa na mkeo ni kitendo cha fadhila. (Musnad Ahmad bin Hanbal)

Nilimuuliza Mtukufu Mtume kwa mshangao, pia ni sadaka kufanya tendo la ndoa na mke wa mtu, ingawa anatosheleza tamaa yake kwa tendo hili? Endapo mwanamume anatosheleza tamaa yake, pia atapata fidia kwa tendo hilo? Mtume alisema, "Vema, niambie, haitakuwa dhambi endapo ungetosheleza tamaa kwa kufanya kitendo kisicho halali na kilicho haramishwa?" Nilijibu, "Bila shaka."

Akasema, "Nyinyi watu mnafikiria kuhusu dhambi lakini si matendo mema. Kwa kawaida watu wanaoishi maisha ya kushikilia maadili kuacha kufanya kazi ili wajipatie riziki na baadaye pale ambapo mahitaji ya kidunia yanapowabana sana wanaanza kuomba."

"Siku moja Mtume(s.a.w.w) aliniita na akasema, "Unaweza kutoa kiapo cha uaminifu kwamba baada ya hapo patakuwepo Pepo tu inakungojea wewe." Nikajibu, "Ndio" Halafu nikanyosha mkono wangu. Mtukufu Mtume akasema, Ninataka useme kwamba hutaomba kitu chochote kutoka kwa mtu yeyote?" Nikajibu "Sawa" akasema, "hata ule mjeledi unaoanguka kutoka kwenye farasi wako. unatakiwa uteremke chini na kuchukua wewe mwenyewe."

Abu Dharr anasema kwamba Mtukufu Mtume alimwambia, "Usifikirie wema wowote na upendeleo kuwa ni kitu kisichokuwa na thamani na kidogo. Endapo hunacho kitu cha kumpa ndugu yako Muisilamu, angalau ni muhimu ukutane naye huku unatabasamau."

Abu Dharr anasema, "Mpendwa wangu (yaani Mtume) ameniusia kwamba niendelee kuonyesha wema kwa ndugu zangu, hata kama siwezi kutimiza kikamilifu, (Musnad Ahmad bin Hanbal) kwa sababu

ni vigumu sana. Hata hivyo mtu anatakiwa kuwafanyia wema watu wote kadiri iwezekanavyo."

Tabia ya Abu Dharr inadhihiri ambapo tunaona kwamba kila mara yupo na watu fukara na wenye kuhitaji. Alikuwa makini sana kuhusu mafundisho ya Mtume na hakuna miongoni mwa masahaba wenye mioyo migumu ambao hawakuathiriwa na maadili ya Mtume. Alikuwa muungaji mkono madhubuti wa Imamu Ali hivyo kwamba alichota tabia ya kiwango cha juu cha desturi njema za Mtume.

Agizo la Mtume lilikuwa: "Wape watumwa wako na watumishi wako chakula unachokula wewe, na wape nguo unazovaa wewe." (Musnad ya Ahmad bin Hanbal) Na Abu Dharr alifuata utaratibu huo huo. Kila siku aliwapa watumwa wake na watumwa wasichana chakula alichokula yeye na aliwapa nguo alizovaa yeye.


3

4

5

6

7

8

9

10

11