MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN (A.S)

MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN (A.S)0%

MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN (A.S) Mwandishi:
: SHEIKH MUSABBAH SHA'ABANI
Kundi: Imam Husein (A.S)

  • Anza
  • Iliyopita
  • 7 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 8196 / Pakua: 1813
Kiwango Kiwango Kiwango
MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN (A.S)

MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN (A.S)

Mwandishi:
Swahili

,MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN(A.S)

KIMEANDIKWA NA: SAYYID ABDUL HUSAIN SHARAFUDDIN

MTARJUMI: MUSABBAH SHABAN

Mtukufu Mtume(s.a.w.w) Amesema:

1. "Ee Allah! Hawa (Ali, Fatima, Hasan na Husain) ndio AhlulBait wangu, basi watoharishe kwa tohari kamili."

2. "Husain anatokana na mimi na mimi ninatokana na Husain..."

3. "Hao (Hasan na Husain) ni maua yangu katika dunia."

4. "Ewe Mwanangu (Husain)! Mwili wako ni mwili wangu na damu yako ni damu yangu;"

5. (Ewe Husain), wewe u Sayyid, mwana wa Sayyid, na ndugu wa Sayyid; wewe u uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu) mwana wa uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu) na ndugu wa uthibitisho (wa Mwenyezi Mungu); na baba wa uthibitisho tisa ambao wa tisa wao ni Qaim wao ambaye atakuwa al-Mahdi.

6. "Hasan na Husain ni Masayidi wa Vijana wa Peponi."

7. "Ewe Mola wangu! Mpende yule ampendae Husain."

8. "Adhabu atakayoipewa yule mwuaji wa Husain huko Motoni itakuwa sawa na nusu (nzima) ya adhabu yote watakayoipewa wenye dhambi waulimwengu."

9. " Allah hujirafikisha na wale wajirafikishao na Husain yu adui wa wale walio maadui zake."

DIBAJI

Ahlul-Bayt(a.s) Assembly ya Tanzania (ABATA) ina furaha kutoa kitabu kama hicho cha Majlis kwa watu wazungumzao Kiswahili. Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi, Mwenyekiti wa ABATA, amekichagua kwa ajili ya madhumuni hiyo kitabu kiitwacho "Muqaddamah al-Majalis al-Fakhirah fi Ma'atim al-Itrah at Tahirah" kilichoandikwa na mwanachuoni mashuhuri wa dini na mtunzi, marehemu Allamah Sayyid Abdul Husain Sharafud-din al-Musawi, wa Jabal Amil (Lebanon).

Shaykh Musabah Shaban Mapinda, wa Dar-es-Salaam, kwa ushauri wa Mwenyekiti wa ABATA amefanya tarjuma ya kitabu hiki kutoka Kiarabu kwenda kwenye Kiswahili, knachoitwa "Maombolezo ya Kifo cha Imam Husain(a.s) ."

Hiki ni kitabu cha pili ambacho kinatolewa na Ahlul-Bayt(a.s) Assembly ya Tanzania; na tunayo furaha kubwa kwa kutoa kitabu cha Majlis ambacho ni cha kwanza katika lugha ya Kiswahili.

Allah Subhanahu wa Ta'ala atoe malipo yake kwa mtunzi, mfasir na wale wote ambao wamesaidia katika uchapishaji wake kwa njia yoyote.

Wa ma Tawfeeqi illa Billah

MAOBOLEZO YA KIFO CHA IMAM HUSEIN(A.S)

KIMEANDIKWA NA: SAYYID ABDUL HUSAIN SHARAFUDDIN

MAJLIS YA KWANZA

RUHUSA YA KULIA

Hapana shaka kwamba kuwalilia wafu Waumini ni jambo linalofaa katika Uislamu kutokana na dalili ya kitendo cha Mtume(s.a.w.w) kuhusu jambo hilo.

Mtume kulitenda tendo hili kumekaririka mara nyingi na pahala pengi kama ifuatavyo: Mara ya kwanza ni siku alipofariki ami yake na mlezi wake Bwana Abu Talib. Ya pili ni siku alipouawa kishahidi ami yake Mtume Bwana Hamza katika vita ya Uhud. Ya tatu siku alipopata Shahada (kuuawa) Bwana Jaafar Bin Abi Talib na Bwana Zaid Bin Harith na Bwana Abdallah Bin Ruwah, wote hawa waliuawa katika vita ya Muuta. Mara ya pile, ni siku alipofariki Bwana Ibrahim ambaye ni mtoto wake mwenyewe Mtume(s.a.w.w) .

Mtume(s.a.w.w) alimlilia mwanawe huyu kiasi ambacho kilimfanya Bwana Abdurahman bin Auf amwambie Mtume(s.a.w.w) : "Na wewe unalia Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu "?

Bwana Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe mwana wa Auf hiyo ni alama ya huruma ".

Kisha Mtume akaendelea kulia na akasema: "Hakika jicho Iinatoa machozi na moyo unahuzinika, wala hatusemi isipokuwa yale anayoyaridhia Mola wetu, na hakika sisi kutengana nawe ewe Ibrahim Wallahi tunahuzunika . "

Na mara ya tano, ni siku Mtume(s.a.w.w) alipozuru kaburi Ia mama yake Bibi Amina, alilia kiasi cha kuwaliza watu waliokuwa karibu yake.

Vitabu vinavyoashiria juu ya Mtume kuwalilia wafu ni vingi mno idadi yake siyo rahisi kuidhibiti.

Kadhalika mapokezi ya kauli ya Mtume(s.a.w.w) na kukiri kwake juu ya kufaa kulia kwa ajili ya wafu ni mengi. Mojawapo ni siku alipopata Shahada Bwana Jaafar bin Abi Talib (At-Tayyaar), Mtume(s.a.w.w) alikwenda kwa mkewe (Jaafar) Bibi Asmaa bint Umais ili kumpa faraja, naye Bibi Fatma aliingia pahala hapo huku analia na kusema: "Ewe Ami yangu". Basi Mtume(s.a.w.w) akasema:

"Na walie wenye kulia kuwalilia mashujaa mfano wa Jaafar ."

Siku nyingine aliyowakubalia watu kuwalilia wafu ni siku alipofariki Ruqaiya binti wa Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) , wanawake wakawa wanamlilia (Ruqaiya), basi Omar bin Al-Khatab akawa anawapiga kwa bakora yake, pamoja na kwamba Mtume alikwishawakubalia kulia, basi Mtume(s.a.w.w) akamwambia Omari: "Waache walie " kisha Mtume akasema: "Vyovyote iwavyo, huzuni itokayo Moyoni na jicho kulia, hayo ni kwa ajili ya huruma, ameyaweka Mwenyezi Mungu ".

Pia kuna siku lilipitishwa jeneza mbele ya Mtume(s.a.w.w) ili-hali kuna wanawake wanalia, Omar akawakemea, Mtume akamwambia Omar: "Waache walie ewe Omar kwani nafsi huhuzunika na jicho hutoa machozi ".

Mapokezi ya hadithi kuhusu jambo hili yako mengi kiasi ambacho hatuna nafasi ya kuyakamilisha yote, lakini itoshe kwamba Nabii Yaaqub bin Is-haq bin Ibrahim alimlilia mwanawe Yusufu pale Mwenyezi Mungu alipomuondosha Yusuf machoni pake na akasema (alipokuwa akilia): "Oh majonzi yangu kwa Yusufu! Na macho yake yakawa meupe kwa huzuni naye alikuwa amejawa na huzuni ." Qur'an 12:84.

Kutokana na kilio cha Yaaqub imefikia hadi kusemwa kwamba, "Hayakukauka macho yake (kwa kulia) tangu alipotengana na Yusuf(a.s) mpaka alipokuja kukutana naye, ukiwa umepita muda wa miaka themanini. [1]

Basi je palikuwa na nani aIiyebora mbele ya Mwenyezi Mungu katika zama hizo kuliko Nabii Yaaqub?

Imepokewa kutoka kwa Mtume(s.a.w.w) kwamba yeye Mtume alimuuliza Jibril(a.s) yalifikia kiasi gani majonzi ya Yaquub alipokuwa akimlilia mwanae"? Jibril akaseama: Yalifikia kiasi cha majonzi ya wanawake sabini waliopotelewa na watoto wao.

Mtume akasema: "Je alipata malipo kiasi gani?" Jibril akasema: "Alipata ujira wa mashahidi mia moja.. " [2]

Mimi nasema: "Basi ni mtu gani atakayechukizwa na madhehebu yetu sisi (Shia Ithnashari) katika suala Ia kulia tokana na huzuni, baada ya kuwa jambo hili limethibiti toka kwa Manabii. Ni nani anayechukizwa na mila ya Ibrahim? Hakuna, Isipokuwa yule anayeitia nafsi yake katika upumbavu. Qur'an, 2:130.

Kwa hakika sera ya Maimamu juu ya maombolezo na kulia iliendelea zama baada ya zama, na wakawaamuru wafuasi wao kudumisha mikusanyiko ya huzuni juu ya Imam Husein(a.s) .

Amesema Imam Jaafar As-Sadiq(a.s) : "Hakika Ali bin Husein(a.s) alimlilia baba yake maisha yake yote, hapakuwekwa chakula mbele yake ila hulia, na wala hakuletewa kinywaji isipokuwa hulia.

Kutokana na kulia kwake huko, mmoja wa wafuasi wake alimwambia: "Mimi niwefidia kwako, acha kulia hakika nachelea kwamba utakuwa miaongoni mwa wenye kuangamia kwa kulia sana".

Imam Ali bin Husein (Zainul Abidina) akajibu: "Hapana jambo lolote (linaloniliza sana) isipokuwa mimi nashitakia huzuni zangu kwa Mwenyezi Mungu nami nayajua yaliyoko kwa Mwenyezi Mungu ambayo ninyi hamuyajui ".

Na katika mapokezi mengine Imam Ali bin Husein alisema kumwambia mmoja katika wafuasi wake, "Ole wako hakika Yaaqub(a.s) alikuwa na watoto kumi na wawili, macho yake yalibadilika na kuwa meupe kwa ajili ya kulia sana (kumlilia Yusuf) na mgongo wake ulipinda kutokana na huzuni nyingi, hali yakuwa mwanawe yu hai hapa duniani, lakini mimi nalia sana kiasi hiki kwa sababu niliwaona na kuwashuhudia, baba yangu (Imam Husein), ndugu zangu, ami zangu na watu kumi na saba miongoni mwa watu wa nyumba yangu wakiwa wamenizunguka hali wamechinjwa!"

Pia Imam Ali bin Husein alikuwa kila anapochukuwa chombo ili anywe maji, hulia mpaka chombo kile akakijaza damu.

Akiulizwa kuhusu bali hiyo hujibu: "Basi ni kwa nini nisilie wakati ambapo baba yangu alinyimwa maji ambayo yalikuwa hayana kizuwizi chochote kwa wanyama.........?

Na imepokewa hadithi toka kwa Bwana Rayaan bin Shubaib amesema: "Nilingia nyumbani kwa Imam Ar-Ridha(a.s) katika siku ya kwanza ya Muharram, Imam akaniambia: "Ewe mwana wa Shubaib, hakika Mwezi wa Muharram (Mfungo nne) ni mwezi ambao watu wa zama za Jahiliya (kabla kuja Uislamu) walikuwa wakiharamisha dhulma na mauaji kutokana na utukufu wa Mwezi huu lakini watu wa Ummah huu (wa Kiislamu) hawakuheshimu Utukufu wa Mwezi huu wala heshima ya Mtume wao(s.a.w.w) , kwani walikiua kizazi chake ndani ya Mwezi wa Muharram, na wakawateka wanawake wa kizazi cha Mtume wao, na wakapora vyombo vyao, Ewe mwana wa Shubaib, ikiwa wewe utakuwa ni mwenye kulia, basi mlilie Husein(a.s) kwani yeye alichinjwa kama anayavyochinjwa kondoo, na aliuawa yeye pamoja na watu kumi na nane katika watu wa nyumba yake, ambao hawalinganishwi na ye yote hapa duniani kwa ubora, na kwa hakika Mbingu Saba zililia kwa kuuawa Husein".

Imepokewa hadithi toka kwa Abu Ammarah Al-Munshid amesema: "Hakutajwa Imam Husein(a.s) mbele ya Abu Abdillah As-Sadiq(a.s) katika siku yoyote isipokuwa (siku hiyo) hakuonekana kuwa na furaha mpaka usiku".

Na amesema Abu Ammarah, "Abu Abdillah as-Sadiq alikuwa akisema: Mauaji aliyouliwa Husein(a.s) ni jambo Ia kumpa mazingatio kila Muumini.

Na imepokewa kutoka kwa Imam Jaafar As-Sadiq(a.s) amesema: "Imam Husein(a.s) alisema, mimi nitauawa ili yapatikane mazingatio kutokana na mauaji hayo, hatanikumbuka (kwa kunitaja) Muumini yeyote bali atapata mazingatio.

MAJLIS YA PILl

RUHUSA YA KUOMBOLEZA

Hapana shaka kwamba ipo ruhusa ya kuomboleza vifo vya Waumini, na kwamba jambo hilo ni halali, na hapana dalili iliyo kinyume cha hivi.

Kwa hakika baba yetu Nabii Adam(a.s) aliomboleza kifo cha mwanawe Habil, na maombolezo yakawa yanaendelea mpaka leo kila inapotokea jambo la kifo katika kizazi cha wanaadamu bila upinzani.

Ama Mtume Muhammad(s.a.w.w) aliwaruhusu Masahaba wake kufanya maombolezo kwa wingi kutokana na huzuni, na pia aliruhusu kutaja mema ya waliofariki na kutoa sifa zao katika tabia nzuri na matendo mazuri.

Na wakati Mtume(s.a.w.w) alipofariki, Masahaba walishindana katika kutaja sifa zake walipokuwa wakiomboleza kifo chake.

Katika kifo hicho cha Mtume(s.a.w.w) Bibi Fatma bint wa Mtume(s.a.w.w) pia aliomboleza wazi wazi na kuonesha huzuni yake kwa kusoma beti za Kishairi. [3]

Kadhalika kifo cha Bwana Mtume kiliombolezwa na shangazi yake Mtume(s.a.w.w) Bibi Safia kama inavyoonesha katika Istiiab cha Ibnu Abdil-Bari. Pia lbnu ami yake Mtume Bwana Abu Sufian bin Harith Bin Abdil-Mutalib na Bwana Abu-Dhuarib AlHadh-li, Bwana Abul-Haithami At-Taihani, Ummu Ra-Ala AlQushairiyya na Bwana Amir bin At-Tufail na wengineo wote waliomboleza.[4]

Pamoja na maelezo haya, ili kumkinaisha mtu kuhusu suala la maombolezo yafaa sana kukiangalia na kukisoma kitabu kiitwacho Al Istiiab na pia At-Tabaqat cha Ibn Saad na Usudul Ghaaba na al-Isaba, kwani humo atakuta mambo mengi yanayohusu maomboIezo yaliyofanywa na Masahaba.

Katika Masahaba walioomboleza sana-sana kutokana na vifo ni Sahaba wa Kike Bibi Al-Khinsaa, ambaye aliomboleza vifo vya nduguze wawili, Mabwana Sakhr na Muawiya ambao walikuwa makafiri.

Bibi huyu alikuwa miongoni mwa watu wachamungu kiasi kwamba alitoa wanawe kwa ajili ya kutumikia Uislamu, na wote waliuawa katika njia ya kutumikia Uislamu, kitu ambacho Bibi huyu alikifurahia.

Lakini pamoja na yote hayo hakuacha kuomboleza mauti ya nduguze mpaka alipofariki na wala hakutokea mtu wa kumkemea kwa tendo hilo.

Kwa kifupi suala la kuomboleza ni mashuhuri katika kila zama na kila mahali baina ya Waislamu na wala hawapingani katika hilo.

Sisi tunatosheka na dalili ya kuhalalisha maombolezo yetu tuyafanyayo kama walivyopokea wapokezi wetu kutoka kwa Bwana Zaidi bin As-Shuhaam amesema: "Tulikuwa mbele ya Abu Abdullahi Al-Sadiq(a.s) huku tukiwa na kundi la watu kutoka Al-Kufah, mara akaingia Jaafar bin Af-Fan basi Imam Al- Sadiq akamkaribisha na akamsogeza karibu yake kisha akasema: "Ewe Jaafar nimepata habari kwamba wewe unasoma mashairi juu ya Imam Husein na unayasema vizuri, Jaafar bin Af-Fan akasema: "Ndiyo", Imam Jaafar akasema: "Hebu soma mashairi hayo, nikasoma".

Baada ya Mashairi hayo kusomwa katika hali ya kuomboleza mauaji ya Imam Husein(a.s) , Imam Jaafar Al-Sadiq(a.s) alilia na wakalia watu waliokuwa wamemzunguka kiasi ambacho machozi yalimtiririka usoni mwake hadi kwenye ndevu, kisha Imam akasema: "Ewe Jaafar WalIah wamekushuhudia Malaika Watukufu na wao wanasikiliza maneno yako unapoomboleza kwa ajili ya Imam Husein(a.s) , na kwa hakika wamelia kama tulivyolia sisi na zaidi ya hapo, na Mwenyezi Mungu Mtukufu amefaradhisha kwako Pepo katika muda huu na amekusamehe".

Kisha Imam Jaafar Al-Sadiq akasema kumwambia Jaafar bin Af-Fan, "Je. nikuongezee ubora kwa wenye kuomboleza mauaji ya Imam Husein(a.s) ", akasema Jaafar bin Afan: "Ndiyo Ewe Bwana wangu".

Akasema Imam Jaafar(a.s) : "Hapana yeyote yule atakayesoma Shairi la maombolezo ya Imam Husein(a.s) , na kwa maombolezo hayo akalia na akawaliza wengine isipokuwa Mwenyezi Mungu atamsamehe na kumuwajibishia kupata Pepo".

Imam Muhammad bin Idris As-Shafii (Imam Shafii) ni miongoni mwa watu waliombeleza mauaji ya Imam Husein(a.s) aliposoma mashairi ambayo tafsiri yake ni kama ifuatavyo:

Ulimwengu ulitingishika kwa ajili ya kuuawa kizazi cha Mtume Muhammad(s.a.w.w) , Milima migumu ilikuwa karibu kuyeyuka kwa ajili ya kuuawa kizazi cha Mtume Muhammad(s.a.w.w) , Milima migumu ilikuwa karibu kuyeyuka kwa ajili ya kuwahuzunikia wao (kizazi cha Mtume), Basi nani atanifikishia barua ya huzuni kwa Husein? Nitaomboleza kifo cha Husein japo nafsi za watu na nyoyo zitachukia. [5]

MAJLIS YA TATU YAH:

KUSOMWA HABARI ZA WALIOKWISHA PITA HAPO KALE

Hapana shaka kuwa, upo mkazo na umuhimu mkubwa kusoma na kueleza habari na sifa za Waumini waliokwisha fariki zamani, na pia kutaja matatizo na misiba iliyowafika katika maisha yao ya kueneza Uislamu. Kwani kuyataja mambo yao huwa sawa kama kuwataja wao katika hali ya uhai wao.

Ummah hunufaika kutokana na utukufu walioupata zinapotajwa sifa zao, pia tabia njema walizokuwa nazo na vitendo vyao vizuri huunufaisha Ummah wa Kiislamu.

Iwapo Ummah utatoa umuhimu wa kusimulia historia ya viongozi wao walio wema ndiyo nafasi bora ya kulinda Utukufu wake na huwa ni muongozo mzuri kwa kizazi kitakachofuata.

Kwa hakika mwendo wa vizazi vya tangu hapo zamani na vile vilivofuatia baadaye, upo katika mtiririko wa kutaja na kukumbuka ubora wa watu waliokufa na misiba iliyowafika kwa njia mbali-mbali, ikiwa ni pamoja na kuyakumbuka hayo kwa njia za uandishi, khutba na utunzi wa mashairi.

Maamuzi sahihi ya akili pamoja na mapokezi sahihi ni vitu ambavyo kimsingi vinatoa mwelekeo wa kuboresha hifadhi ya masimulizi ya watu waliopita.

Kadhalika misingi ya maendeleo na maarifa inalazimisha kuweko kumbukumbu za athari za zamani zenye manufaa kwa jamii.

Ukweli ulivyo ni kwamba uhifadhi wa athari hizo huzifanya roho za watu watukufu ziendelee kuwa hai, na kutokana na kumbukumbu zao hutokea mashindano kwa walio hai ili kujaribu kuzifikia sifa zao na wema wao (Hakika katika kutaja habari za watu waliopita kuna kumbukumbu yenye mazingatio kwa wenye akili). Qur'an 12:111

Angalia kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna ya Mtume wake(s.a.w.w) vimeweka wazi sifa za Manabii na matatizo yaliowapata. Pia vimeonyesha bayana jinsi maadui was Mwenyezi Mungu na Manabii wake walivyofedheheka.

Na lau kama si Qur'an na Sunna ya Mtume tusingefahamu Utukufu wa Manabii wa Mwenyezi Mungu, wala tusingejua uovu wa maadui wa Mwenyezi Mungu.

Basi ni vipi hatufahamu kwamba, lau si Qur'an na Sunna kusimamia maelezo ya mafunzo na miongozo ya Mwenyezi Mungu kwa Manabii na waja wa Mwenyezi Mungu, na pia mafunzo ya kuwausia subira kutokana na kero na usumbufu walioupata katika kupigania haki, tungejuaje vituko vya kina Namruda dhidi ya Nabii Ibrahim, na Firaun dhidi ya Musa na wengineo?

Ifahamike wazi kwamba kauli zitolewazo kuharamisha kusomwa na kutajwa ubora wa watu watukufu, na kutaja matatizo yao na misiba iliyowafika ni lazima ziende sambamba na kuharamisha Qur'an na Sunna ya Mtume visisomwe.

Kadhalika ni lazima kauli hizo kama zitakubalika, basi hakutakuwa tena na haja ya somo la historia wala (Ilmu-R-rijal).

Na hakuna mwenye kuridhia upumbavu huu katika nafsi yake akachagua upofu wakati anatambua haki iko wapi.

(Tunajilinda kwa Mwenyezi Mungu kutokana na ujinga uliopita kiasi).

Ili kuthibitisha kwamba kuyataja mema ya waliopita ni tendo lililoanza tangu hapo kabla, tunasoma ndani ya vitabu vya historia juu ya matokeo ya mwaka wa arobaini Hijriya kama ifuatavyo:

Alipofariki Imam Ali(a.s) alisimama mwanawe Imam Hasan(a.s) akasema: "Hakika leo mumemuuwa mtu ambaye hajakuweko kabl yake wakumfananisha naye miongoni mwenu, na hatapatikana ye yote baadaye wa kufananishwa naye .[6]

MAJLIS YA NNE

VIKAO KWA AJILI YA KUHUZUNIKIA WAFU

Hapana shaka kwamba Mtume(s.a.w.w) alihuzunika huzuni nyingi kwa ajili ya kufiwa na Ami yake Bwana Abu Talib na Bibi Khadija Ummul-Muuminina(a.s) , kwani wawili hawa walifariki ndani ya mwaka mmoja, na Mutume akauita mwaka huo kuwa ni mwaka wa "huzuni".

Kipindi hiki cha msiba huu mkubwa, Bwana Mtume(s.a.w.w) alipunguza kutoka, ikawa muda mrefu hukaa nyumbani, na ikawa Maquraishi wanapomhujumu huomboleza kwa kusema: "Ewe Ammi yangu imekuwa mapema mno kukukosa ." [7]

Na zimethibiti habari kwamba Mtume alifanya kikao ndani ya Msikiti kwa ajili ya kuwahuzunikia Ibn Ammi yake Jaafar na Zaid pamoja na ibn Ruwaha waliouawa katika vita ya Muuta.

Vile vile imethibiti kuwa yeye Bwana Mtume alihuzunika sana na haikuonekana huzuni namna hiyo kwa Mtume baada ya kuuawa wasomaji wake wa Qur'an, na alifanya Qunut kuwaombea msamaha kwa muda wa mwezi mmoja, na pia akawa huwaapiza katika Qunut hiyo waliowauwa.

Kwa hiyo basi kutokana na dalili hizi utakuta zinatoa maamuzi ya kutia nguvu kuwekwa vikao kwa ajili ya kuonesha huzuni kwa kuwakosa watu wema na wenye kumbukumbu nzuri na ukarimu.

Kwani katika kuwapambanua na makundi mengine, huwa na sababu ya kuwahamasisha watu ili waweze kutokea miongoni mwao wenye mfano kama huo. Pia jambo hilo dhahiri yake ni kuwapa haki yao wanayostahiki baada ya kufa kwao, na hupelekea kuwapata watu wengi watakaoiga mienendo yao.

Ama tukija upande wa kufanya vikao kwa ajili ya kumbukumbu ya Masaibu yaliyowapata Maimamu katika njia ya kuleta amani na sul-hu kwa Ummah, jambo hili hufanya nafsi kuwa na imani na uongofu na kuzifanya nyoyo kuwafuata Maimamu, japo zimekwisha kupita siku nyingi na matukio hayo yalitokea sehemu za mbali.

Na maneno ya wanaolaumu mambo haya, wakasema kwamba haifal kufanya vikao kwa ajili ya kuhuzunikia maiti hasa unapokuwa umepita muda mrefu, hayana maana tunapoizingatia misiba iliyotupata kutokana na mambo waliyofanyiwa watu wa nyumba ya Mtume(s.a.w.w) , kiasi ambacho ukweli maneno yao hayaturudishi nyuma katika kuwahuzunikia watu wa nyumba ya Mtume japo ni muda mrefu umepita, na wala hayaondoi huzuni iliyotokana na misiba hiyo, na wala hayazimi joto la huzuni muda wote.

Je hawaioni hadithi iliyoandikwa na Imam Ahmad bin Hambal katika Musnad yake kwamba, Imam Ali(a.s) alipokuwa akienda Siffin, alipofika Nainawa akawa anasema: "Kuwa na subira Ee Abu Abdillah kuwa na subira Ee Abu Abdillah katika kingo za mto Furat ".

Akaulizwa Imam Ali(a.s) maana ya kusema hivyo, naye akajibu kwa kusema: "Siku moja niliingia kwa Mtume(s.a.w.w) nikamkuta analia, basi nikamuuliza sababu ya kulia kwake akasema: "Hivi punde Jibril alisimama mbele yangu akaniambia kwamba hakika Husein atauawa katika kingo za mto wa Furat, akasema Jibril: Je nikunusishe udongo wa sehemu hiyo? Nikamwambia ndiyo, basi akanyoosha mkono wake akachota gao moja la udongo akanipa ". [8]

Na imepokewa kutoka kwa Bibi Aisha UmmuI-Muuminina kwamba siku moja Husein bin Ali(a.s) aliingia nyumbani kwa Mtume(s.a.w.w) hali ya kuwa Mtume anapokeya Wahyi, basi Jibril akasema: "Hakika Ummah wako wataingia katika fitna baada yako na watamuuwa mwanao huyu (Husein a.s), na (Jibril a.s) akanyoosha mkono wake akachukua udongo mweupe na akasema katika ardhi ya udongo huu atauawa mwanao ."

Basi Jibril alipoondoka Mtume wa Mwenyezi Mungu alitoka nje hadi kwa Sahaba zake wakiwemo Abubakar na Umar and Ali na Hudhaifa, Ammar na Abudhar, hali ya kuwa analia, basi wote wakamwambia: "Kitu gani kinakuliza Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?"

Mtume akasema: "JibriI ameniambia kwamba mwanangu Husein atauawa katika ardhi ya AT-TAF na ameniletea udongo huu akasema kuwa, katika udongo huu ndipo yatakapokuwa malazi yake".

Basi mtu wa kwanza kumlilia Imam Husein katika Ummah huu na wa kwanza kupewa udongo wa malazi ya Imam Husein(a.s) na wa kwanza kuunusa na wa kwanza kuwasomea watu mauaji ya Imam Husein(a.s) katika ardhi ya AT-TAF ni Mtume wa Mwenyezi Mungu(s.a.w.w) .

Na ni yeye Mtume(s.a.w.w) ndiye wa kwanza aliyewasikilizisha masahaba zake hadith ya mauaji ya Imam Husein(a.s) .

Basi hapana shaka kwamba Masahaba walimliwaza Mtume(s.a.w.w) kutokana na huzuni hiyo na kilio chake (Hakika mnacho kiigizo chema kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa yule anayemtaraji Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho, na yeyote mwenye kupinga basi hakika Mwenyezi Mungu ni mkwasi Mtukufu). Qur'an 33:21

MAJLIS YA TANO

KUMTOLEA SADAKA MAITI

Hapana shaka kwamba, ni jambo zuri kuwatolea sadaka maiti wa Waumini kwani jambo hilo alilifanya Mtume(s.a.w.w) na akaamuru lifanywe.

Ndani ya sahihi mbili (Bukhari na Muslim) imepokewa toka kwa Bibi Aisha amesema: "Sikupata kumuonea wivu mwanamke ye yote miongoni mwa wakeze Mtume kuliko nilivyomuonea wivu Bibi Khadija ambaye hata sikuwahi kumuona, lakini Mtume alikuwa akimtaja sana (Khadija) na wakati mwingine alikuwa akichinja kondoo na kumkatakata vipande vipande kisha huvipeleka kwa jamaa za Khadija kuwa ni sadaka, basi wakati mwingine nilimuambia Mtume(s.a.w.w) , "Kama kwamba katika Dunia hii hakupata kuweko mwanamke isipokuwa Khadija, basi Mtume husema hakika alikuwa ni mwanamke wa pekee bora (katika wake nilioowa) na wala hajakuwepo wa mfano wake na kwake yeye Khadija nilipata watoto". [9]

Hadithi hii inatuonyesha kwamba ni jambo zuri kutowa sadaka kwa marafiki au jamaa wa maiti.

Naye Imam Muslim ameandika kwamba, mtu mmoja alifika kwa Mtume(s.a.w.w) akasema: "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu hakika mama yangu amefariki na wala hakuacha usia, je, atapata malipo iwapo nitamtolea sadaka? Mtume akasema: "Ndiyo ". [10]

KUZALIWA KWA AL-IMAM HUSEIN BIN ALI(A.S)

Al-Imam Husein(a.s) amezaliwa tarehe tano Mwezi wa Shaaban Mwaka wa nne Hijiriyah.

Baada ya kuzaliwa kwake alishuka Jibril(a.s) akiwa na kundi la Malaika wapatao Elfu Moja, wakampongeza Mtume(s.a.w.w) .

Mtume(s.a.w.w) alifurahi sana kwa kuzaliwa kijana huyu, na akawa amempa jina Ia Husein.

Imepokewa kutoka kwa Ummul-Fadhl mkewe Bwana Abbas Bin Abdil-Mutalib amesema; "Niliota ndoto kabla Husein hajazaliwa, nikaona kama kwamba kipande cha nyama ya mwili wa Mtume kimewekwa mapajani mwangu basi nikamsimulia jambo hilo Mtume wa Mwenyezi Mungu, Mtume akasema: "Naona kuna kheri iwapo ndoto yako itakuwa ya kweli, kwani Fatma atazaa mtoto wa kiume nami nitakupa wewe umlee".

Anaendelea kusimulia Ummul-Fadhli anasema: "Basi mambo yakawa kama alivyosema Mtume(s.a.w.w) na akanipa Husein nimlee".

Siku moja nikaja naye kwa Mtume(s.a.w.w) , wakati Mtume(s.a.w.w) akiwa anambusu Husein, alikojoa na likaruka tone la mkojo kwenye nguo ya Mtume(s.a.w.w) nikamshika Husein (a.s) ili kuepusha asizikojolee nguo za Mtume(s.a.w.w) , Husein(a.s) akalia, Mtume akasema katika hali ya kama mwenye kukemea, "Tulia ewe Ummul-Fadhli, nguo yangu itafuliwa lakini umemuumiza mwanangu ."

Ummul-Fadlili anasema: "Nikamuacha Husein mapajani kwa Mtume na nikasimama kwenda kumletea Mtume(s.a.w.w) maji aisafishe nguo yake.

Basi nikaleta maji na nikamkuta Mtume(s.a.w.w) analia, nikamwambia unalia nini ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu?

Mtume(s.a.w.w) akasema: "Hakika Jibril amenijia na kuniambia kwamba Ummati wangu watamuuwa mwanangu huyu basi ole wao, Mwenyezi Mungu asiwafikishie shufaa (maombezi) yangu siku ya Qiyama watu watakaomuuwa ."

Al-Imam Husein(a.s) alipotimiza mwaka mmoja tangu kuzaliwa kwake, walimshukia Mtume(s.a.w.w) Malaika kumi na wawili, nyuso zao nyekundu huku wanalia na wakawa wanamuambia Mtume(s.a.w.w) kwamba: "Hakika mwanao yatampata masaibu yaIiyompata Habil kutoka kwa Qabil, na kwa ajili hiyo atapewa malipo mema kama alivyopewa Habil, na atakayemuuwa atakuwa na dhambi sawa na dhambi za Qabil.

Hapakubakia Malaika huko Mbinguni ila wote walikuwa wakishuka na kuja kumpa pole na kumuomba awe mvumilivu na pia walikuwa wanamfahamisha malipo atakayolipwa Imam Husein(a.s) , si hivyo tu, bali walikuwa wanamuonyesha udongo wa mahali atakapouawa, na Mtume(s.a.w.w) akawa husema: "Ewe Mwenyezi Mungu mpinge atakayempinga na Umlaani atakaye muuwa... "

Alipotimia Imam Husein umri wa miaka miwili Mtume alitoka kufanya safari na katika safari yake hiyo alisimama mahali fulani, basi aliamua kutoendelea na safari yake na mara macho yake yakawa yanabubujika machozi, akaulizwa sababu gani iliyomfanya alie. Mtume(s.a.w.w) akasema: "Jibril ananieleza kuhusu ardhi iliyoko kando ya mto Furat iitwayo "KARBALA" mahala ambapo atauawa mwanangu Husein, sasa hivi ni kama nauona uwanja wa mapambano baina yake na adui zake, pia kama kwamba napaona mahala atapozikwa.

Kisha baadaye Bwana Mtume(s.a.w.w) aliamua kurudi hali ya kuwa mwenye huzuni na majonzi, akapanda katika Mimbari na akatoa khutba huku Hasan na Husein(a.s) wakiwa mikononi mwake.

Alipoteremka kwenye Mimbari akaweka mkono wake wa kulia juu ya kichwa cha Imam Hasan na nikono wa kushoto akauweka kichwani kwa Imam Husein(a.s) akanyanyua kichwa chake mbinguni akasema: "Ewe Mwenyezi Mungu hakika mimi Muhammad Mja wako na ni Nabii wako na hawa wawili (Hasan na Husein) ni watu bora katika familia yangu na ni wabora katika kizazi changu na atakuwa mbora mtu atakayewafuata hawa katika Ummati wangu, na hakika Jibril ameniambia kwamba mwanangu huyu atapingwa na atauawa. Ewe Mola mpe baraka nyingi atakapouawa na umfanye awe miongoni mwa Mabwana wa Mashahidi. Ewe Mwenyezi Mungu usimbariki atakayemuuwa na atakayempinga."

Basi baada ya maneno hayo watu wakaangua kilio Msikitini, kisha Mtume akatoa tena khutba nyingine fupi hali yakuwa rangi imembadilika na macho yake yanatoka machozi akasema, "Enyi watu hakika mimi ninawaachia vizito viwili, Kitabu cha Mwenyezi Mungu Mtukufu na Kizazi changu watu wa Nyumba yangu, na hakika viwili hivyo havitatengana mpaka vinifikie katika Haudh, fahamuni kwamba hakika mimi ninavisubiri viwili hivyo, na kwa hakika siwatakeni jambo lolote isipokuwa ni lile aliloniamuru Mola wangu. "Muwapende jamaa zangu". (Kizazi Changu).

Mtume akaendelea kusema: "Fahamuni ya kwamba (siku ya Qiyama) yatanijia makundi matatu katika Ummah huu.

Kundi Ia kwanza litakuwa Ia watu weusi sana, wamezingirwa na Malaika, kisha watasimama mbele yangu nami nitasema: "Ni kina nani nyie"?

"Watashindwa kunitambua, nao watasema: "Sisi ni watu wa Tauhidi mongoni mwa Waarabu.

Basi mimi nitawaambia, "Mimi ndiye Ahmad Nabii wa Waarabu na wasio Waarabu".

Kisha wao watasema: "Sisi ni katika ummati wako".

Nami nitawaambia: "Basi ni vipi mulinifuata katika kizazi changu na katika Kitabu cha Mola Wangu".

Watanijibu: "Ama kitabu tulikipuuza na kizazi chako tulikiangamiza kwa kuwauwa".

Basi nitageuza uso wangu, nao watarudi wakiwa na kiu kali hali ya kuwa nyuso zao ni nyeusi.

Kisha litanijia kundi jingine jeusi mao kuliko lile la mwanzo nami nitawaambia: "Vipi mulinifuata katika vizito viwili, kile kikubwa na kile kidogo, yaani Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Kizazi changu"?

Basi hao watasema: "Ama kile kikubwa (Qur'an) tulikipinga, na ama kile kidogo tulikinyanyasa na kukitawanya ovyo ovyo".

Basi nitawaambia niondokeeni mbele yangu hapo wataondoka hali wakiwa na kiu kali makoo yamewakauka na nyuso zao nyeusi.

Baadaye litanijia kundi jingine Ia watu ambao nyuso zao zinangara kwa nuru.

Basi nami nitawauliza, "Ni kina nani ninyi?"

Watasema: "Sisi ndiyo watu wa neno Ia Tauhidi na Uchamungu, sisi ni Ummati wa Muhammad Mteule, nasi ndiyo bora katika watu wa haki, tulikilinda vema Kitabu cha Mola wetu, tukaihalalisha halali iliyohalalishwa na Kitabu na tukaiharamisha haramu iliyoharamishwa na Kitabu, na tuliwapenda kizazi cha Nabii wetu".

Basi nitawaambia: "Furahini hakika mimi ndiye Nabii wenu Muhammad(s.a.w.w) na hakika ninyi duniani muliishi kama hivyo mlivyontajia."

Basi hapo nitawanywesha maji kutoka ndani ya Haudhi langu (alilonipa Mwenyezi Mungu) nao watarejea bali ya kuwa kiu imewakatika tena watakuwa na furaha, na baadaye wataingia peponi waishi humo milele na milele.

KUTHIBITI UIMAM KWA HUSEIN(A.S)

Ulithibiti Uimamu kwa Imam Husein(a.s) baada ya kufariki kwa nduguye Al-Imam Hasan bin Ali bin Abi Talib(a.s) na hapo ikawa ni faradhi kwa viumbe wote kumtii Imam Husein(a.s) .

Na Uimamu wake ulikuwa ni kwa mujibu wa kauli ya baba yake na babu yake(a.s) na pia usia wa nduguye Imam Hasan(a.s) .

Imam Hasan na Imam Husein(a.s) wao ni Mabwana wa vijana wa peponi kwa mujibu wa Mwenyewe Mtume wa Mwenyezi Mungu ambaye ni babu yao.

Miongoni mwa ubora waliokuwa nao Imam Hasan na Imam Husein(a.s) , baada ya kuwa ni wajukuu wa Mtume(s.a.w.w) na vipenzi vyake katika watu wa nyumba yake, pia ni miongoni mwa watu aliotokanao kwenda kuapizana na wakristo wa Najran pale iliposhuka aya ya 61 Sura ya Tatu:

"Basi watakaokuhoji kuhusu Nabii Issa, baada ya kukufikia ujuzi (wa-jambo hili) basi waambie njooni tuwaite watoto wetu na watoto wenu na wanawake wetu na wanawake wenu na sisi wenyewe na ninyi, kisha tuapizane tuombe laana ya Mwenyezi Mungu iwashukie waongo ".

Aya hii inaitwa aya ya Mubahala, na sababu ya kushuka kwake, ni pale viongozi wa Kikristo kutoka Najran walipokuja Madina katika mwaka wa tisa Hijiriya kumjadili Bwana Mtume(s.a.w.w) kuhusu Nabii Isa(a.s) Mtume akawajibu kwamba; "Hakika mfano wa Isa mbele ya Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam ".

Wakristo hao waliendelea kumjadili Mtume(s.a.w.w) hata baada ya jibu hili, ndipo Mwenyezi Mungu aliposhusha aya hii ya 61 Sura ya Tatu, Mtume akaambiwa kama wataendelea kumhoji, basi awaambie waje waapizane kama ilivyoashiria aya hiyo.

Kutokana na uzito wa suala la kuapizana baina ya Mtume(s.a.w.w) na Wakristo hao, ilibidi Bwana Mtume(s.a.w.w) kwa upande wa Waislamu atoke na watu ambao pia watakuwa na uzito wa kukabili maapizano hayo.

Ndipo alipowachukua Hasan na Husein kama wawakilishi wa watoto wa Kiislamu, na Bi Fatma(a.s) kama muwakilishi upande wa wanawake wa Kiislamu na yeye Mtume(s.a.w.w) na Imam Ali(a.s) wakawa ndiyo nafsi za Waislamu.

Kwa mujibu wa uwakilishi wa Imam Hasan na Imam Husein(a.s) katika tukio hili unadhihiri ubora na utukufu wa vijana hawa wawili ndani ya Uislamu, na inamuwajibikia kila Muislamu kuitambua heshima yao na daraja waliyopewa na Mwenyezi Mungu, kama ambavyo Kiongozi Mkuu wa Wakristo hao kutoka Najran alivyokiri ubora na utukufu uliomo ndani ya nyumba ya Mtume(s.a.w.w) siku hiyo ya mapinzano akasema: Hakika mimi naziona nyuso za watu ambao lau watamuomba Mwenyezi Mungu auondoe mlima mahala ulipo atauondoa, hivyo basi musiapizane nao mtaangmia na hatabakia Mkristo yeyote ulimwenguni baada ya leo".

Pia miongoni mwa hoja zilizowazi kuhusiana na utukufu walio kuwa nao Imam Hasan na Imam Husein ni kuteremka aya zinazothibitisha kuwa wao ni katika watu watakaoingia Peponi hali ya kuwa bado wakiwa ni vijana wadogo, na jambo hili linapatikana katika Surat Ad-Dahr kuanzia aya ya saba mpaka aya ya kumi na mbili.

Kabla ya kuzitaja aya hizo ni bora kukisimulia kisa cha kushuka aya hizo japo kwa mukhtasar.

Imepokewa kwa Ibn Abbas kwamba, Hasan na Husein(a.s) waliugua. Basi Mtume na baadhi ya watu wakenda kuwaona, watu hao wakamwambia Imam Ali(a.s) "Lau utaweka nadhiri itakuwa bora ".

Imam Ali, Bi Fatma(a.s) na Mjakazi wao aliyekuwa akiitwa Fiza, wakaweka nadhiri ya kufunga siku tatu ikiwa Hasan na Husein watapona.

Vijana hawa wawili walipona na ikawa kipindi cha kutekeleza ile nadhiri kimefika, lakini ndani ya Nyumba hamkuwa na kitu.

Hivyo Imam Ali(a.s) alikwenda kwa Myahudi mmoja aliyekuwa akiitwa Sham-uun na akakopa vibaba vitatu vya shayiri.

Bi Fatma(a.s) akaisaga shayiri hiyo na akaoka mikate mitano kwa ajili ya kufuturu kulingana na idadi yao katika nyumba yao.

Chakula hicho kilipowekwa ili waanze kula, alibisha hodi mgeni na akawatolea salam akasema:

"Asalaam Alaikum enyi watu wa Nyumba ya Mtume, mimi ni Masikini wa Kiislamu naomba munipe chakula, nanyi Mwenyezi Mungu atakulisheni chakula cha Peponi ".[11]

Basi wakamuonea huruma wakampa chakula chote, nao wakanywa maji kisha wakalala.

Asubuhi wakaamka na saumu na jioni mwana Fatma aliandaa tena mikate na ilipowekwa tayari kufuturu alibisha hodi yatima na kuomba chakula, wakampa na wao wakanywa maji kisha wakalala.

Asubuhi waliamka na saumu, kisha jioni Bi Fatma alioka tena mikate mitano kwa ajili ya kufuturu.

Walipoketi kufuturu alibisha hodi mtu aliyekuwa mateka akaomba chakula wakampa mikate yote kisha wakanywa maji wakalala.

Kwa ajili ya wao kujinyima kwa muda huo wa siku tatu mfulululizo ndipo ziliposhuka aya zifuatazo katika Sura Ad-Dahr "Wanaotekeleza nadhiri (zao) wanaiogopa siku ambayo shari yake itaenea na wanawalisha chakula masikini na yatima na mateka hali wao pia wanakitaka chakula hicho. (nao husema watoapo chakula hicho) tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mwenyezi Mungu, hatutaki kwenu malipo wala shukurani. Hakika tunaogopa kwa Mola wetu siku hiyo yenye taabu na shida. Basi Mwenyezi Mungu atawalinda na shari ya siku hiyo na kuwakutanisha na neema na furaha. Na atawalipa kwa kuwapa Bustani (Pepo) na (Mavazi) ya hariri kutokana na kusubiri kwao.

Zaidi ya hayo ni kwamba Bwana Mtume(s.a.w.w) alidhihirisha wazi Uimamu wao kwa Ummah wake pale aliposema: "Wanangu hawa (Hasan na Husein) ni Maimamu wawe wima au wawe wamekaa ".

Mlolongo wa uimamu wa Maimamu wetu umekuja kwa kila mmoja kumbainisha atakayechukua nafasi ya Imam anayeondoka.

Na jambo hili Ia kubainisha Imamu anayefuata IiIianzia kwa mwenyewe Bwana Mtume(s.a.w.w) kumbainisha Imam Ali(a.s) katika bonde Ia Khum pale alipokuwa akitoka katika Hija ya mwisho. (Mwenye kutaka ziada kuhusu jambo la Uimamu wa Ali bin Abi Talib(a.s) atizame vitabu vya hadithi za Mtume na vitabu vya Historia vinavyotegemewa usahihi wake atalikuta liko wazi). Naye Imam Ali(a.s) alimbainisha Imam Hasan kuwa ndiye atakaye chukua nafasi yake, naye Imam Hasan alimbainisha nduguye Husein(a.s) kuwa ndiyo Imam wa haki baada yake.

Lakini kwa bahati mbaya sana siyo Imam Ali wala Imam Hasan na Husein(a.s) aliyepata fursa ya kuongoza Ummah kama ilivyotarajiwa.

Na hii ilitokana na hali iliyowasibu watukufu hawa baada ya Mtume kuondoka.

Tukimuangalia Imam Husein unakuta matatizo yaliyomkuta ni kama yale yaliyomkuta baba yake hata akasema lmamu Ali kama ifuatavyo: "Nikawa nafikiri baina ya kuwa niupate (Ukhalifa) kwa kuuvuta kwa nguvu au nivumilie uvumilivu wa vipofu wasiojua kitu" Mpaka alifikia kusema, "Basi nikaamua kuvumilia hali ya kuwa jichoni mwangu mna mchanga, na katika koo langu mna dukuduku, nauona urithi wangu umechukuliwa kwa nguvu".

Kwa mwendo kama huu, ndivyo alivyofanya Imam Hasan(a.s) katika siku za uhasama wa Bani Umayya, pindi Mu'awiya bin Abi Sufiyan alipotwaa madaraka ya Ukhalifa kwa nguvu.

Lakini ifahamike wazi sera ya Maimamu wetu kuwa ni sera ya Mtume(s.a.w.w) kwani taabu ilimpata Mtume mwanzo wa kubashiria Uislamu, hakupata utulivu kila alipokuwa akiwaita watu kwenye Uislamu.

Kwa hiyo hali ya Mawasii wake baada yake ni kama ilivyokuwa kwake Mtume(s.a.w.w) hasa itakapokumbukwa kwamba, Maquraishi walipata kumtenga Bwana Mtume(s.a.w.w) na baadaye akalazimika kujificha pangoni wakati akihama Makkah kwenda Madina.

Hali ya matatizo na usumbufu, kama ilivyowapata Manabii ndivyo ilivyokuwa kwa Maimamu.

Muawiyyah bin Abi Sufiyani alipofariki na hali ya vita ikawa imemalizika, hali ambayo ilikuwa ikimzuia Imam Husein(a.s)

kujitangaza Uimamu wake wazi wazi, kipindi hiki walitokea watu wa kumsaidia Imam Husein(a.s) katika kufikisha Ujumbe wa Mwenyezi Mungu, Imam Husein(a.s) alisimama na kujiandaa kufikisha na kusimamia Dini ya Mwenyezi Mungu (s.w.t).

Ili kuanza utekelezaji wa kazi hii, ilimbidi Imam Husein asafiri kutoka Madina kwenda Makkah na hatimaye aelekee Iraq kutokana na wito wa watu wa Al-Kufa waliomtaka aende huko ili akawasaidie na kuwaokoa dhidi ya watawala dhalimu.

Kabla yeye Imam Husein(a.s) kuelekea huko, alimtanguliza Ibn ammi yake Bwana Muslim Bin Aqiil ili akaanze kuwalingania

Dini ya Mwenyezi Mungu na kuchukua kwao baia (kiapo cha utii) kwa niaba ya Imamu Husein(a.s) kwamba watakuwa naye katika Jihadi ya kutetea neno Ia Mwenyezi Mungu, na kuiokoa Dini na Waislamu kutokana na wanafiki waliokuwa wamewakalia Waislainu kwa mabavu.

Muslim Bin Aqiil alipofika huko, watu hao walimpokea na kumuahidi kumsaidia. Lakini haukupita muda mrefu watu hao wakatangua kiapo chao kwa Muslim Bin Aqiil na wakamuacha akauawa mbele yao kifo cha dhulma akiwa ugenini, lakini pia alikufa akiwa ni shahidi.

Na wao hao hao waliomuita Imam Husein wakatoka hapo Al-Kufa kumfuata Imam Husein kwenda kumpiga vita, na wakamtendea mambo ambayo hawakuyatenda Khawarij (Kundi lililomuasi Imamu Ali(a.s) .

Wahinsonga Imam Husein(a.s) , wakamzuia asirudi Makkah wala Madina, wakaweka vizuizi baina yake na maji ya mto Furat mpaka wakamuua hali akiwa na kiu, na wakamdhulumu hali akiwa katika Jihadi, mwenye subira akitaraji radhi za Mola wake.

Hakika ilitenguliwa baia yake na heshima yake ilivunjwa na wala ahadi alizoahidiwa hazikutekelezwa na wakapora mali zake, wakawashika mateka familia yake, wakakidhulumu kizazi cha Mtume(s.a.w.w) hali ya kuwa kimekosa ni mahali gani kitakwenda, njia zote zimefungua.

Kizazi cha Mtume(s.a.w.w) kikawa na huzuni isiyokifani.