AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18352
Pakua: 2872

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18352 / Pakua: 2872
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

KIMEANDIKWA NA: ALI IBN AL - HUSAYN IMAM ZAYNUL AL - ABIDIN (A.S)

KIMETAFSIRIWA NA: SHEIKH HAROON PINGILI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu

Tunamshukuru Allah (s.w.t) na baraka za Mtukufu Mtume(s.a.w.w) na Ahlul Bayt(a.s) kwa kutujaalia kuweza kufanikia juhudi zetu hizi katika kuchapisha kitabu hiki "Sahifatul Kamillah Al-Sajadia".

Kitabu kilochopo mikononi mwako ni tafsiri ya kitabu cha Kiarabu, kiitwacho "As-Sahifatul Kamillah Al-Sajadia" kilichoandikwa na Imamu wa Nne Al-Imam Zainul Abdeen(a.s) . Ndani ya Kitabu hiki Imam(a.s) ameelezea Du'a mbali mbali.

Sababu iliyoifanya Mission yetu isimamie kazi hii ni kama zile za mwanzo, ambayo zinatokana na maombi ya Maulamaa wengi katika Afrika Mashariki kututaka tukifanyie tarjuma kitabu hiki kiingie kwenye lugha ya Kiswahili.

Tunamshukuru Shaikh Harun Pingili kwa kutukubalia ombi letu na kuifanya kazi hii kwa moyo mmoja, na vile vile Bilal Muslim Mission of Scandinavia kutukubalia kukichapisha kitabu hiki.

Tunamshukuru Mwenyezi Mungu tena kwani vitabu vyetu vya mwanzo vimependwa mno na wasomaji na hivyo kutupa ari ya kuchapisha hiki ulichonacho mkononi na kitakachofuatia Insha-Allah.

Mission inatoa shukurani zake za dhati kwa wale wote ambao kwa juhudi zao kitabu hiki kinawafikia wasomaji wetu mikononi na waliosaidia kwa njia moja au nyingine katika tarjuma na uchapishaji wa kitabu hiki. Tunamuomba Mwenyezi Mungu (s.w.t) awalipe malipo mema hapo Duniani na baadaye huko, Akhera.

Wa Ma Tawfeeq Illa Billah

Bilal Muslim Mission of Tanzania

UTANGULIZI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Utangulizi Na: Allamah Sayyid Muhammad Rizvi

Du'a, Sala, kwa maana ya mawasiliano na Allah (s.w.t), ni sehemu ya maumbile ya Mwanadamu. Mara nyingi, umuhimu wa Du'a upo dhahiri, na hata hivyo, katika nyakati zingine, dhiki na majanga humpelekea mwanadamu kujutia na kuomba msaada kutoka kwa Allah (s.w.t). Utafiti wa Kisayansi wa hivi karibuni uliofanyika mwaka 1999, katika Hospitali ya Maradhi ya Moyo Jijini Kansas U.S.A, umethibitisha kupona kwa njia ya Sala kwa Wagonjwa wenye kusali (bila ya wao wala daktari wao kufahamu) walionekana kupona maradhi yao kwa kupimwa na vyombo 35 vya vipimo vya afya ukilinganisha na Wagonjwa Wasiosali.. Allah (s.w.t) amesema wazi wazi kuwa wakati wote milango yake ipo wazi na kwamba (Allah) yupo karibu na (mja wake) mwanadamu wakati wote kuliko alivyo yeye Mwanadamu na mshipa wa shingo yake. Qur'an tukufu inasema: "Na Mwenyezi Mungu ana Majina mazuri mazuri, muombeni kwayo". (7:180) katika Aya nyingine Mwenyezi Mungu ansema: "Na Mola wenu anasema: "Niombeni nitakujibuni: Kwa hakika wale wajivunao kufanya ibada yangu, bila shaka wataingia Jahanamu, wadhalilike." (40:60) Ingawaje inaruhusiwa kuomba (du'a) kwa Allah (s.w.t) kwa njia yeyote tuipendayo, Mtume na Maimamu wa Ahlul Bayt(a.s) pia wametuongoza katika jambo hili. Miongoni mwa miongozo ya hekima ya Maimamu ni as-Sahifah as-Sajjadiyya ya Imamu 'Ali ibnul Husayn(a.s) . Imam 'Ali ibnul Husayn anafahamika na Waislamu wote kuwa ni Kiongozi Mkuu wa Imani ya Kiroho. Hii inaelezewa kwa majina yake maarufu: Zaynul 'Abidin kiongozi (mtukufu) wa Wachamungu na Sayyidus Sajidin, kiongozi wa wale wanaosujudu chini na kuabudu.

Kitabu chake cha as-Sahifah as-Sajjadiyya ni kitabu chenye mpangilio madhubuti wa Sala na Du'a. na kinajumuisha vipengele vyote anavyopambana navyo mwanadamu katika maisha yake, Matatizo ya Afya hadi Utajiri, furaha hadi upweke na unyonge; matukio ya mafanikio na mahitajio, siku za wiki hadi siku kuu maalum n.k. Mwanachuoni maarufu wa Ki-Sunni wa Misri (Egypt) Shaykh at-Tantawi al-Jawhari ameandika yafuatayo kuhusiana na Kitabu cha Sahifah. "Nimekisoma kitabu hiki kwa makini, NimezisomaDu'a zake na Munajjat kwa jicho la utafiti, nimeshangazwa na mantiki na falsafa lliyomo ndani yake. Nimevutiwa mno kwa ubora na mtiririko wa maandishi (tungo) haya. Ninashangaa ni vipi Waislamu kwa muda mrefu wamekuwa hawajui (jahili) kuhusu hazina hii tukufu. Wamekuwa katika usingizi mzito kwa karne nyingi. Hawakuweza hata kuzinduka na kutambua kuwa Allah (s.w.t) amewapatia Hazina hii kubwa ya Elimu. Tungo za Kitabu hiki zaweza kuwekwa katika mitazamo miwili mikubwa; kwanza ni kutafuta Elimu na mwongozo ili kujitenga mbali na madhambi na vitendo viovu wakati ambapo mtazamo mwingine ni kufuata na kuyatenda matendo mema ya kiroho ambayo tunaweza kusema matendo haya yaliyojaa maarifa na mwongozo mwema ni Hazina ya ajabu na ni siri iliyojaa Hekima. Mikakati yote hii inapatikana katika sehemu ya mwanzo ya Kitabu na sehemu ya pili imejaa sifa za Allah (s.w.t), Uumbaji wa viumbe na miujiza ya Allah (s.w.t). "Je hii haishangazi? Je hii sio siri ambayo hawa Watukufu wanaweka dhahiri siri nyingi kwa kusoma na kuiweka wazi Elimu ya Waislamu ambao wanaonekana hawajui kitu? Na huu ni ukweli kwamba mambo ya Wanadamu yamegawika katika sehemu mbili kubwa. Kwanza ni yale yanayohusiana na kujitenga (kuwa mbali) na vitendo viovu na pili ni yale matendo mema pamoja na kutambua kuwepo kwa Allah ambayo ni muhimu kwa utakaso binafsi na ukamilifu wa roho" (At-Tantawi Ad'iyyatu 'Ali Zayni 'l-'Abidin katika jarida la Huda 'l-Islam la Misri (Egypt)). Nina uhakika kwa kukisoma hiki kitabu kikubwa kutoka kwa Ahlul Bayt, sio tu utapata njia sahihi ya kuwasiliana na Allah, lakini pia kitakuweka karibu na Itikadi sahihi kuhusu uwezo na rehema ya Allah (s.w.t). Hatimaye utatambua kuwa maarifa (Elimu) sahihi ya Allah inapatikana tu kwa kupitia mafundisho sahihi ya Maimamu wa Ahlul Bayt wa Mtume. Allah, subhanah wa Taala, wakati wote yupo tayari kutusikiliza na Imam Zaynul Abidin(a.s) ametuwekea njia sahihi ya kuwasiliana na Allah. Hivyo huhitajii kwenda kwa mshauri yeyote au mganga wa kienyeji ambao kwao utatoa pesa ili kusikiliza matatizo yako; Allah (s.w.t) wakati wote yupo tayari kukusikiliza, bila muda maalum wala malipo yoyote!

Sayyid Muhammad Rizvi

NENO LA WACHAPAJI

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu.

Allah (s.w.t) ameumba uhai na umauti kwa makusudio maalum Amelielezea hilo kwa njia ya vitabu vinavyobainisha wazi wazi kati ya matendo mema na maovu. Maelezo fasaha na yenye mtiririko mzuri yanatuthibitishia kuwa kila mmoja wetu na wa kila rika na jamii tofauti anaweza kukielewa kitabu hiki kwa urahisi. Imani ya Dini imemuweka mwanadamu katika upeo wa juu ambao haulinganishwi na zama za Kijahiliyya. Kwa kuujua uwezo wa Allah (s.w.t) huwapelekea watu kuwa na matumaini na furaha katika maisha ya hapa Ulimwenguni na Akhera. Katika mada hii Quran tukufu inasema: "Ambao ni wale walioamini na zikatulia nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Sikilizeni! Kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu nyoyo hutulia" Al-Raad:28. Hapana yeyote mwenye kuujua udhaifu wa mwanadamu na mapenzi ya Allah (s.w.t); atashindwa kubadilika kwa mafunzo yaliyomo katika Sahifa. Ndani yake tunapata mafunzo ya kiroho ya Kiislam au mafundisho ya kina na mapana ya Dini ya Kiislamu yanayohusu matendo na ukweli katika maisha na mahusiano kati ya mwanadamu na Allah (s.w.t) ambayo yameandikwa katika lugha za Kimataifa kwa kuweka misingi imara ya kiroho kwa ukamilifu. Kwa Niaba yetu sote tunatoa shukurani zetu za dhati kwa Mtukufu Allah (s.w.t) na kwa mwandishi wa kitabu hiki kitukufu kilichotuwezesha kuandika tafsiri ya pili na tunaungana na kufurahia kazi ngumu ya tafsiri yake ya Kiswahili pamoja na Mzee wetu Ayatullah Allamah Sayyid Saeed Akhtar Rizvi wa Bilal Mission of Tanzania. Tunamuomba Allah (s.w.t) ambariki na amlipe kwa kazi yake kubwa aliyoifanya katika nyanja hii; pamoja na wale waliotoa mchango wao wa hali na mali Mission na Mwandishi pia wanatoa shukurani zao za dhati kwa wale wote waliotoa mchango wao katika kazi hii. Tunaweka kalamu yetu chini kwa kumalizia na methali ya Kiswahili isemayo, "Fuata nyuki ule asali."

DIBAJI KUHUSIANA NA USHUHUDA - THABITI WA SAHIFA

Kwa Jina la Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema - Mwenye Kurehemu

Mtukufu Sayyed Najmu Deen Bahausharafu Abul-Hasan Muhammad bin Ahmad bin Ali bin Muhammad bin Umar bin Yahya Al-Alawi Al-Husayn - Mungu amrehemu - alituhadithia Alisema: Alitupa khabari Shaikh heri zimfikiye Abu Abdilahi Muhammad bin Ahmad bin Shahriyar muweka hazina wa hazina ya Amiyrul Muuminen Maulana Aliy bin Abiy Taalib alayhis-salaam katika mwezi wa Rabi-u-Awal (mwezi wa tatu A.H.) mwaka wa 516 mwezi May - June wakati Sahifa ilikuwa inasomwa mbele yake nami nasikia.

Alisema nimeisikia kutoka kwa Shaikh ikisomwa mbele yake Shaikh Swaduqu Abiy Mansoor Muhammad bin Muhammad ibun Ahmad bin Abdil-Aziz Al-Ukbari mwadilifu Mungu amreheu kutoka kwa Abil-Mufazzali Muhammad bin Abdilahi ibnil-Mutalib Ashaybaanee. Alisema: Sharifu Abu Abdilahi Jaafar bin Muhammad ibun Jaafar ibunil Hasani ibin Jaafar ibunil Hasan Ibunil Hasan ibun Ameril-muumineena Aliy ibn Abiy Taalib amani juu yake ametuhadithia. Amesema: Ametuhadithia Abdulahi ibin Umar ibin Khataab Azaya mwaka wa mia mbili sitini na tano 265 (878-9) Amesema: Ametuhadithia mjomba wangu Ali bin Anuumani Al-Aalamu. Amesema: Ametuhadithia Umairi bin Mutawakili Athaqafiyu Al-Balakhiyu naye... kutoka kwa baba yake Mutawakili bin Haroon. Alisema nimekutana na Yahya bin zaid bin Aliy Alayhi-salaam naye akiwa yu aelekea khurasani baada ya kuuliwa baba yake nilimsalimia. Aliniuliza umetoka wapi? Nikasema kutoka Hajji. Aliniuliza kuhusu Ahli wake na watoto wa ami yake huko Madina na alisisitiza swali kuhusu Jaafar bin Muhammad amani iwe juu yake.Nilimuelezea khabari zake na khabari zao na huzuni walionayo kuhusu baba yao Zaid bin Aliy amani iwe juu yake. Aliniambia: Ami yangu Muhammad bin Aliy amani iwe juu yake alimshauri baba yangu asitoke na alimjulisha kuwa endapo atatoka na kuiacha Madina mambo yatavyomuwia. Je ulipata kukutana na mtoto wa ami yangu Jaafar bin Muhammad amani iwe juu yake? Nikamwambia ndio. Akasema je ulipata kumsikia anasema chochote kunihusu? Nikasema ndio.

Akasema: Alisema nini kunihusu? Nikasema nimejitoa muhanga kwako sipendi nikukabili kwa yale niliyoyasikia kutoka kwake. Akasema wanitishia umauti? Lete ulichosikia. Nikasema nimemsikia akisema kwa hakika kabisa kuwa utauliwa na utasulubiwa kama alivyouliwa baba yako na alisulubiwa. Basi uso wake ulibadilika na akasema: (Mungu huyafuta apendayo na huyathibitisha na kwake ipo asli ya kitabu). Ewe! Mutawakilu hakika Mwenyezi Mungu mwenye enzi na ametukuka ameliunga mkono jambo hili kupitia kwetu na ametupa sisi elimu na upanga. Haya mawili yameunganishwa na sisi na wamepewa wana wa ami yetu khususan elimu tu peke yake. Nikasema nimejitoa kwako muhanga mimi naona watu wanaelemea sana kwa mwana wa ami yako Jaafar amani iwe juu yake kuliko kwako na kwa baba yake. Akasema: kwa hakika ami yangu Muhammad na mwanawe Jaafar amani iwe juu yao wamewaita watu kwenye uhai na sisi tumewaita kwenye umauti. Nikasema ewe mwana wa mjumbe wa Mungu je wao wanaelimu zaidi au ninyi? Aliinama punde kisha akainuwa kichwa chake na akasema: Sote tunaelimu isipokuwa wao wanayajua yoote tuyajuwayo nasi hatujuwi yote wayajuwayo. Kisha aliniambia: Je umeandika chochote kutoka kwa mwana wa ami yangu? Nikasema naam. Akasema nionyeshe, nikamtolea aina kadhaa za elimu na nikamtolea duwa nilizoandika kutoka kwake Abiy Abdilahi amani iwe juu yake. Na alinihadithia kuwa baba yake Muhammad bin Aliy amani iwafikie alimwandikia kwa imla na akampa khabari kuwa ni miongoni mwa DU'A za baba yake Aliy bin Husain amani ziwe juu yao ni miongoni mwa DU'A za Sahifa al-Kamila. Yahya aliiangalia mpaka mwisho wake na aliniambia: Je waniruhusu niinakili? Nikasema Ewe mwana wa mjumbe wa Mungu waomba ruhusa kile ambacho ni kutoka kwenu? Akasema hakika nitakutolea Sahifa ya DU'A kamili zile alizozihifadhi baba yangu kutoka kwa baba yake na kwa hakika baba yangu ameniusia kuilinda na kutompa asiyestahiki. Umairu alisema: Alisema baba yangu: Basi nilisimama na kumwendea nikabusu kichwa chake. Na nikamwambia naapa ewe mwana wa mjumbe wa Mungu hakika mimi nitafanya dini ya Mungu kupitia upendo wenu na kuwatii ninyi, nami nataraji anipe Mungu maisha ya faraja na umauti mwema kwa wilaya yenu (kuwa penda). Basi alitupa zile kurasa zangu nilizompa kwa mtoto alikuwa pamoja naye na akasema andika DU'A hii kwa hati bayana nzuri kisha nipe huenda nikaihifadhi kwani nilikuwa naiomba kutoka kwa Jafari Mungu amhifadhi naye alikuwa akiniziwiya nayo. Mutawakilu alisema: Nilijutia nililofanya sikujuwa la kufanya na Abu Abdilahi amani imfikiye hakuniambia kuwa nisimpe yeyote! Baadaye aliagiza kisanduku ambacho humo alitowa sahifa iliyofungwa na kupigwa muhuri akauangalia ule muhuri na akaubusu akalia akavunja na kufunguwa kufuli. Kisha aliikunjuwa ile sahifa na akaiweka kwenye macho yake na kuipitisha usoni kwake na akasema walahi ewe! Mutawakilu lau kama kwa ajili ya yale uliyoyasema miongoni mwa usemi wa mwana wa Amiy yangu yakuwa mimi nitauwawa na kusulubiwa nisingekupa hii sahifa ningeifanyia ubakhili. Lakini natambua kuwa usemi wake ni wa haki ameuchukua kutoka kwa baba zake na itatimia hivyo basi nimeogopa elimu kama hii iwafikie baniy Umayya wataificha katika kabati zao kwa ajili yao tu. Ichukue ihifadhi kwa niaba yangu na ungoje ukiwa nayo Mungu atapopitisha jambo langu na jambo la hawa watu na atapitisha.

Basi hiyo ni amana yangu kwako mpaka uifikishe kwa wana wawili wa Amiy yangu Muhammad na Ibrahim wana wawili wa Abdilahi bin Hassan bin Hassan amani iwafikie. Kwa sababu wao ndio watakaoshika jambo hili baada yangu.Mutawakilu akasema: Niliipokea sahifa. Na alipouliwa Yahya bin Zaid nilikwenda Madina nikakutana na Aba Abdilah, amani imfikie. Nilimsimulia zile khabari kumuhusu Yahya alilia sana na huzuni kumuhusu ilikithiri na akasema: Mungu mrehemu mwana wa Amiy yangu na amkutanishe na baba zake na babu zake. Wallahi ewe Mutawakilu halikunizuwia kumpa ile DU'A yeye isipokuwa lile alilolihofia kuhusu sahifa ya baba yake, basi iwapi sahifa? Nikasema: Ni hii.Aliifungua na akasema: Wallahi hizi ni hati za Amiy yangu Zaid na ni DU'A ya babu yangu Aliy bin Hussain amani iwafikie. Kisha alimwambia mwanawe: Simama ewe Ismael niletee ile DU'A ambayo nilikuamuru uihifadhi kwa moyo na kuilinda Ismael alisimama na aliitowa ile sahifa kama ile aliyo mkabidhi Yahya bin Zaid Abu Abdilahi aliibusu na aliiweka machoni kwake na akasema huu ni mwandiko wa baba yangu na aliiandika kwa imla aliyoifanya babu yangu amani iwe juu yao mimi nikiwa naona. Nikasema ewee mwana wa Mtume wa Mungu waonaje nikiilinganisha na sahifa ya Zaidi na Yahya? Aliniruhusu kufanya hivyo na alisema: Nakuona wafaa kwa hilo.Nikazichunguza naona kuwa zi kitu kimoja sikuipata hata herufi moja inatofautiana na zilizo kwenye sahifa nyingine. Kisha nilimwomba ruhusa Aba Abdilah amani iwe juu yake ili niwape sahifa watoto wawili wa Abdilahi bin Husain. Akasema (hakika Mungu anakuamrisheni kuzifikisha amana kwa wenyewe) ndio wape hao wawili.Nilipoinuka ili kukutana nao aliniambia: bakia mahali pako. Kisha alituma waitwe Mohammad na Ibraheem, na akasema huu ni urithi wa mwana wa Amiy yenu Yahya kutoka kwa baba yake amempeni ninyi khususan na kuwaacha ndugu zake. Nasi tunakuwekeeni sharti. Wakasema sema kwani kauli yako yakubalika. Akasema musitoke nayo sahifa hii nje ya Madina.Wakasema: Kwanini iwe hivyo? Akasema: Kwa hakika mwana wa Amiy yenu aliihofia jambo nami nalihofia kwenu. Wakasema kwa hakika aliihofia alipojua kuwa atauwawa. Akasema Abu Abdilah amani imwendee; na ninyi musijiaminishe, kwa kweli najua kuwa ninyi mutapinga kama alivyopinga na mutauwawa kama alivyouwawa. Walisimama huku wakisema hapana hila wala nguvu ila kwa kuwezeshwa na Mungu aliye na enzi ya juu mno mtukufu.Walipokwisha toka akaniambia Abuu Abdilahi amani imfikiye: Ewe Mutawilu: vipi Yahya alikwambia kuwa hakika Amiy yangu Mohammad bin Aliy na mwanawe Jaafar wanawaita watu kwenye uhai nasi tunawaita kwenye umauti? Nikasema ndio Mungu akuweke katika islahi aliniambia hivyo mwana wa ami yako Yahya. Akasema Mungu amrehemu Yahya, hakika baba yangu alinihadithia naye alihadithiwa na baba yake naye toka kwa babu yake toka kwa Aliy amani juu yake kuwa mjumbe wa Mungu(s.a.w.w) alisinzia kidogo akiwa juu ya membari yake akaona akiwa katika usingizi wake kuwa watu wanaruka ruka juu ya membari yake kama ngedere na kuwafanya watu warudi kinyume nyume.Mtume wa Mungu alikaa sawasawa(s.a.w.w) hali ikiwa huzuni imetanda usoni kwake. Jibrilu (a.s) alimjia na aya hii: (Hatukuifanya njozi tuliyokuonyesha isipokuwa ni mtihani kwa watu na mti ulio laaniwa katika Qur'an na tunawahofisha lakini haiwazidishii ila kuvuka mipaka kukubwa) Awakusudia Baniy Umayya kwa tamko la mti uliolaaniwa katika Qur'an.

Akasema ewe Jibril watakuwa katika muda wangu na katika wakati wangu? Akasema la hapana lakini kinu cha Uislamu kitazunguka toka kuhama kwako na kubaki miaka kumi baada ya hapo kinu cha Uislam kitazunguka mpaka miaka thelathini na tano toka kuhama kwako. Baada ya hapo kitabaki miaka mitano kisha hapana budi kutakuwa na maongozi potovu ya kuwa katika muhimili wake kisha kutakuwa na ufalme wa mafirauni. Akasema na Mungu mtukufu aliteresha aya ya Qur'an kuhusiana na hayo: (Kwa hakika tumeiteremsha usiku wa maazimio kitu gani kitakujulisha usiku wa maazimio nini usiku wa maazimio ni bora kuliko miezi elfu). Watamiliki Baniy Umayya wakati ambao hautakuwa na usiku wa maazimio. Akas.ema Mwenyezi Mungu mtukufu alimjulisha Nabiy wake(s.a.w.w) utawala wa umaa huu na mamlaka yao muda wote huu. Hata lau milima ingerefuka kupita kiasi wangejirefusha na wao hata kushinda mirima mpaka Mungu mtukufu aidhinishe kutoweka ufalme wao na wao katika wakati huo wote wamepandisha bendera ya chuki na bughudha dhidi yetu sisi Ahla Bayt. Mungu alimpasha khabari Nabiy wake yale watakayopambana nayo Ahli Bayt wa Muhammad na wapenzi wao na Shia wao toka kwao (Baniy Umayya) katika siku za ufalme wao. Akasema: Mungu ameteremsha kuhusu hawa watu: (huwaoni ambao wameibadilisha neema ya Mungu kwa kukufuru na kuwafanya watu wao kubaki katika maangamizi wataunguwa katika jahannam na ni makazi mabaya mno.) Na neema ya Mungu ni Muhammad na Ahli Bayt wake kuwapenda wao ni iymani yaingiza peponi na kuwachukia ni ukafiri na unafiki uingizao motoni.Mtume wa Mungu aliiweka siri hiyo kwa Aliy na kwa Ahli Bayt wake. Akasema: Kisha Abu Abdilahi amani iwe juu yake alisema: Hajatokea wala hatotokea kati yetu Ahli Bayt yeyote mpaka siku ya kusimama na kujitokeza kwa qaim wetu Imamu Mehdi ili aziwiye dhulma au kuifanya haki itekelezeke ila atagongana na balaa na itakuwa kujitokeza kwake ndio sababu ya kuzidisha uadui na msiba juu yetu na Shia wetu. Mutawakilu bin Haroon alisema: kisha Abu Abdilahi aliniandikia DU'A kwa njia ya imla nazo zikiwa katika milango 75 imenipotea kutokana nazo milango kumi na moja na nimehifadhi miongoni mwa DU'A hizo milango sitini na kitu. Ametuhadithia Abul-Fazzal amesema: Na amenihadithia Muhammad bin Al-Hassan Ibun Ruzbih Abu Bakr Al-madaini mwandishi ni mkazi wa Arrah'ba alitusimulia akiwa nyumbani mwake. Amesema: Amenihadithia Mohammad bin Ahmad bin Muslim Al-Mutaharyu, amesema: amenihadithia baba yangu kuutoka kwa Umairi bin Mutawakili Al-Balkhiyi toka kwa baba yake Al-Mutawakilu bin Haroon. Alisema: Nilikutana na Yahya bin Zain bin Aliy amani iwe juu yao na aliitaja hadithi kikamilifu mpaka ile njozi ya Nabiy(s.a.w.w) ambayo Jaafar bin Muhammad aliitaja toka kwa baba zake amani iwafikie. Na katika riwaya ya Almutahari imetajwa milango nayo ni:

1. Kumuhimidi Mungu mwenye enzi na ametukuka.

2. Sala kwa Muhammad na Ali wake.

3. Sala kwa wabeba arshi (kitanda.)

4. Sala kwa wanomsadiki Mtume.

5. DU'A kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wamuhusuo.

6. DU'A ya kila asubuhi na jioni.

7. DU'A yake kwa ajili ya mambo yanayotisha na muhimu.

8. DU'A yake kwa ajili ya kujikinga.

9. DU'A yake kwa ajili ya ayapendayo.

10. DU'A yake kwa kutaka Mungu awe ndio kimbilio lake.

11. DU'A yake kwa ajili ya mwisho mwema.

12. DU'A yake kwa ajili ya kukiri.

13. DU'A yake kwa ajili ya mahitaji.

14. DU'A yake kwa ajili ya matendo ya dhuluma.

15. DU'A yake wakati wa ugonjwa.

16. DU'A yake kutaka ufumbuzi.

17. DU'A yake dhidi ya shetani.

18. DU'A kwa kujihadhari na hatari.

19. DU'A yake kuomba maji.

20. DU'A yake kwa ajili ya kuwa na tabia njema.

21. DU'A yake akihuzunishwa na jambo.

22. DU'A yake wakati wa shida.

23. DU'A yake kwa ajili ya afya njema.

24. DU'A yake kwa ajili ya wazazi wake wawili.

25. DU'A zake kwa ajili ya watoto wake.

26. DU'A yake kwa ajili ya majirani zake na rafiki zake.

27. DU'A yake kwa ajili ya walinda mipaka.

28. DU'A yake katika mfadhaiko.

29. DU'A yake inapokuwa haba riziki.

30. DU'A zake ili kupata msaada wa kulipa deni.

31. DU'A yake kwa ajili ya toba.

32. DU'A yake katika sala za usiku.

33. DU'A yake katika kumwomba Mungu amchagulie lililobora (istikhara)

34. DU'A yake apatwapo na balaa au aona balaa ya nyemelea

kumfedhehesha kwa dhambi.

35. DU'A yake kuonyesha ridha kwenye maamuzi ya Mola.

36. DU'A yake asikiapo radu.

37. DU'A yake katika kuonyesha shukurani.

38. DU'A yake kuomba udhuru.

39. DU'A yake kuomba msamaha.

40. DU'A yake akumbukapo umauti.

41. DU'A yake kuomba kusitiriwa na hifadhi.

42. DU'A yake wakati wa kuhitimisha Qur'an.

43. DU'A yake anapouona mwezi mwandamo.

44. DU'A yake uingiapo mwezi wa Ramadhani.

45. DU'A yake kuuaga mwezi wa Ramadhani.

46. DU'A yake kwa ajili ya Iddi ya Fitri na Ijumaa.

47. DU'A yake siku ya Arafat.

48. DU'A yake siku ya uzhiya (kuchinja) na siku ya Ijumaa.

49. DU'A yake kujikinga na vitimbi vya maadui.

50. DU'A yake wakati wa hofu.

51. DU'A yake katika kumwomba Mungu sana na unyenyekevu.

52. DU'A yake katika kuomba kwa bidii.

53. DU'A yake katika kujidhalilisha (mbele ya Mungu).

54. DU'A yake ili kuondoa maudhi.

Ama milango iliobaki ni kwa matamko ya Abiy Abdilahi Al-Hasaniy rehma za Mungu zimfikie.

Ametuhadithia Abu Abdilah Jaafar bin Mohammad Al-Hasaniy, amesema: Ametuhadithia Abdulahi bin Umairi bin Khataab Azzayatu. Amesema: Amenihadithia mjomba wangu Aliy bin Annuumani Al-Halam.

Amesema: Amenihadithia umairu bin Mutawakilu Athaqafiyu Al-Balakhiyu kutoka kwa baba yake Mutawakilu bin Haroon. amesema amenifanyia imlaa bwana wangu Aswadiqu Abu Abdilahi Jaafar bin Muhammad.

Amesema: Babu yangu Aliy bin Husain alimfanyia imla mbele ya macho yangu baba yangu Muhammad bin Aliy, juu ya wote amani ya Mungu iwafikie.

1

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA KWANZA

Na Alikuwa(a.s) Akianza Kuomba Du'a Huanza Kumhimidi Mungu Mtukufu Na Kumsifu Husema Hivi:

Sifa Njema Zote Ni Zake Mwenyezi Mungu. Ambaye ni wa mwanzo bila ya chanzo kilikuwa kabla yake, na wa mwisho bila ya cha mwisho kitakuwa baada yake: Ambaye yameshindwa kumwona macho ya watazamaji, yameshindwa kumuainisha mawazo ya wasifiaji. Kwa uwezo wake alianza kuumba viumbe. Aliwabuni (viumbe) kwa utashi wake wa kubuni, Kisha aliwapitisha njia ya utashi wake. Na aliwatuma katika njia ya upendo wake. Hawana uwezo wa kuchelewesha alichowatangulizia. Wala hawawezi kutanguliza alichowacheleweshea. Na ameifanyia kila roho miongoni mwao lishe ijulikanayo iliyogawanywa kutoka kwenye ruzuku yake. Mpunguzaji hawezi kumpunguzia aliye mzidishia. Wala mzidishaji hawezi kumzidishia aliempunguzia.

Kisha akaipigia kila nafsi muda wenye kikomo. Na akaisimamishia kila nafsi muda wenye mpaka. Yanatembea kuuelekea, kupitia siku za umri wake. Anaufikia kupitia miaka ya muda wake. Mpaka afikapo hatua ya mwisho, na kutimiliza hesabu za umri wake. Mungu humshika na kumpeleka kwenye thawabu zake nyingi au kwenye adhabu yake aliyo muhadharisha nayo. Ili awalipe ambao wamefanya vibaya waliyotenda, na awalipe wema ambao wamefanya mema. Ikiwa ni uadilifu kutokana naye. Yametakasika majina yake. Neema zake zimejitokeza!

"LA YUS'ALU AMMA YAF'ALLU' (Haulizwi atendayo) "WA HUM YUS' ALUNA" (Wao ndio wataulizwao). Sifa njema zote ni za Mungu ambaye lau angewaficha waja wake utambuzi wa Himidi yake, juu ya aliyowafanyia majaribu kwa neema zake zenye kufuatana, na amewakithirishia neema zake za wazi, wangezitumia neema zake, bila ya kumhimidi! Na wangejitanua katika riziki yake bila ya kumshukuru.

Na wangekuwa hivyo wangetoka nje ya mipaka ya ubinadamu na kuingia kwenye mipaka ya unyama na wangekuwa kama alivyo waelezea katika kitabu chake thabiti:

"IN HUM ILA KAL AN AAMI BAL HUM ADWAllU SABIILA" (Hakika wao ni kama wanyama, bali wao ni wapotovu mno wa njaa). Sifa njema ni za Mungu juu ya ujuzi aliotupa kumtambua yeye binafsi, na ametupa ilhamu ya kumshukuru. Ametufungulia milango ya elimu ya kutambua kuwa yeye ndiye Bwana. Na ametuelekeza tuwe wanyofu kwake katika kumpwekesha. Ametuepusha na upotovu na kuwa na mashaka katika amri yake. Sifa njema ambazo kwazo tutapata maisha marefu miongoni mwa viumbe wake walio muhimidi, na kwazo tumpite aliye tangulia kwenye ridhaa yake na msamaha' wake. Sifa njema ambazo zitatuangazia giza la BARZAKH na iturahisishie njia ya kufufuliwa. Ienzi mafikio yetu kwenye kisimamo cha mashahidi

'YAUMA TUJ'ZA KULU NAFSIN BIMA KASABAT WA HUM LAA YUDH'LAMUUN"

(Siku ambayo kila nafsi italipwa ilichotenda nao hawato dhulumiwa). "YAUMA LA YUGHNIIMAULA AN MAUL.4 SHA-I-AN WALA HUM YUN SWARUN"

(Siku ambayo Bwana hatomfaa chochote mtetezi wake nao hawatopata usaidizi) Sifa njema itatunyanyuwa juu mpaka juu zaidi ya walio juu) "FIKITABINMARQUMI. YASH'A HADU HUL-MUQARABUN"

(Katika kitabu kilicho andikwa. Wakishuhudia walio sogezwa karibu.) Sifa njema ambayo macho yetu yatapata utulivu pindi macho yatafanywa kiwi na kwayo sura zetu zitafanywa ziwe nyeupe pindi ngozi zitafanywa nyeusi. Sifa njema ambazo kwazo tutaachwa huru, kutoka moto mkali wa Mungu natuingiye kwenye karama ya ujirani wa Mungu. Sifa njema ambazo kwazo tutasongamana na Malaika wake walio kurubishwa, na tuungwe kwayo na Manabii wake waliotumwa.

Katika nyumba ya kudumu haitoweki, na mahali pa ukarimu wake ambao haubadiliki. Sifa njema ni za Mungu ambaye ametuchagulia maumbile mazuri.Na ametutunukia riziki muwafaka.Ametupa ubora kuvitawalia viumbe vyote. Viumbe wake wote wako chini ya utii wetu kwa Qudra yake waja kwenye kututii kwa enzi yake. Sifa njema ni zake Mungu ambaye amefunga kwa ajili yetu mlango wa mahitaji isipokuwa kwake. Kwa hiyo vipi tutaweza kumsifu? Au lini tutaweza kutekeleza shukrani zake Lahasha! Lini? Na sifa njema ni za Mungu ambaye ameunganisha katika sisi viungo vya mwili vyenye kupanuka, na ametujaalia viungo vya kushika. Ametustarehesha kwa roho ya maisha. Ametuunganishia kuwa imara viungo vya kazi. Na ametupa lishe maridhawa. Ametutosheleza kwa fadhila zake ili tusiwe na haja.

Ametumilikisha kwa wema wake. Kisha ametupa amri ili kututihani utiii wetu. Na ametukataza ili ajuwe shukrani zetu. Tumehalifu njia ya amri yake. Tumeparamia migongo ya makaripio yake! Hata hivyo hakutuharakishia adhabu yake, wala hakutuharakishia kisasi chake. Bali alikwenda nasi pole pole kwa huruma yake ikiwa ni takrima. Alitungoja turejee kwa huruma yake, ni upole (wake). Sifa njema ni za Mungu ambaye ametuonyesha jinsi ya kufana toba ambayo hatungefaulu isipokuwa kwa fadhila zake. Lau hatungeweza kuhesabu fadhila zake isipokuwa haya majaribu yake kwetu yamekuwa mema kwetu. Hisani zake kwetu ni kubwa mno. Fadhila zake kwetu ni za kutosha. Si kama hivi ulikuwa mwendo wake katika toba kwa waliokuwa kabla yetu. Ametuondolea lisilokuwa katika uwezo wetu. Hajatukalifisha isipokuwa lililo kwenye uwezo wetu hajatulazimisha jambo ila ni jepesi. Hajamwachia yeyote kati yetu udhuru wala hoja. Basi mwenye kuangamia kati yetu ni yule mwenye kuhiliki japo hataki.

Na mwenye heri kati yetu ni yule mwenye kumronga yeye. Na sifa njema ni za Mungu kwa kila aliye mhimidi malaika wake wa karibu naye. Na viumbe wake walio na heshima sana kwake, na wenye kumridhisha mno miongoni mwa wanao muhimidi. Sifa njema zilizo bora kuliko zote kama ubora wa Mola wetu juu ya viumbe wake wote. Kisha zake ni sifa njema mahali pa kila neema yake juu yetu na juu ya waja wake wote waliopita na waliobaki kwa idadi ya yaliyo zungukwa na elimu yake, toka vitu vyote. Na mahali pa kila moja miongoni mwazo idadi yake ni zaidi na zaidi milele mpaka siku ya Qiyama. Sifa njema isiokuwa na mwisho. Idadi yake haihesabiki. Mwisho wake haufikiwi. Muda wake hauna mwisho. Sifa njema itakuwa kiungo cha utii wake na msamaha wake, na ni sababu ya maridhawa yake. Na njia ya kwenye msamaha wake. Na njia ya kwenye pepo yake. Na mlinzi wa malipizi yake. Na ni usalama kwa ghadhabu yake. Usaidizi wa utii wake. Kizuizi cha maasi yake. Ni msaada wa kutekeleza haki yake na wajibu wake. Sifa njema ambazo zitatupa furaha miongoni mwa wenye furaha katika mawalii wake. Na kwayo tutakuwa katika daraja ya waliouliwa kwa upanga wa maadui wake. Hakika yeye ni mpendwa msifika.

DUA YA 2

NA ILIKUWA KATIKA DU'A YAKE(A.S) BAADA YA KUMUHIMIDI MUNGU KAMA HIVI: HUANZA KUMTAKIA REHMA MJUMBE WA MUNGU(S.A.W.W)

Sifa njema ni zake Mungu ambaye amekuwa na huruma kwetu kupitia Nabiy wake Muhammad(s.a.w.w) mbali na umma zilizopita na vizazi vilivyopita. Kwa uwezo wake ambao haushindwi kitu japo kiwe kikubwa mno. Wala haupitwi na kitu japo kiwe chepesi, au chenye hila nyingi, janja. Na alihitimisha kwetu kwa wote waumba na kutufanya tuwe mashahidi kwa wanaopinga. Kwa wema wake ametufanya tuwe wengi kwa walio wadogo. Ewe Mola mrehemu Muhammad mwaminifu wako juu ya wahyi wako (ufunuo) mteule wako kati ya viumbe wako mwenye kujitoa wakfu katika waja wako. Imamu wa rehema. Kiongozi wa mema. Funguo wa baraka. Aliye jitaabisha nafsi yake kwa ajili ya mambo yako. Amejitoa mwili wake kuyakabili yachukizayo kwa ajili yako. Alijionyesha kwenye uadui wa wazi toka kwa ndugu zake kwa kuwaita kwako. Amepigana na famili yake kwa ajili ya ridhaa yako. Amejikata na kujiweka mbali na watu wa ukoo wake ili kuihuisha dini yako. Aliwaweka mbali na ndugu wa karibu kwa upinzani wao. Aliwasogelea walio mbali kwa kuitikia kwao wito wako. Aliwafanya marafiki watu wa mbali kwa ajili yako. Na aliwafanya maadui kwa ajili yako watu wa karibu. Alijibidisha nafsi yake kuifikisha risala yako.

Aliichosha nafsi yake kuwalingania watu kwenye dini yako. Alijishughulisha kwa kutoa nasaha kwa watu waliostahiki wito wako. Alihamia ugenini mahali mbali na maeneo ya vipandwa vyake na maweko ya miguu yake mbali na alipozaliwa mbali na maeneo yafurahishayo nafsi yake. Akitaka kuienzi dini yako na kuomba msaada dhidi ya makafiri wasiokuamini wewe. Mpaka yalitimia aliyojaribu kuyafanya dhidi ya maadui wako. Na yalifanikiwa aliyoyapanga kwa ajili ya wapenzi wako. Aliibuka na ushindi kwa msaada wako akiwa na nguvu kwa nusura yako pamoja na udhaifu wake. Aliwapiga wakiwa ndani ya miji yao.

Aliwahujumu ndani ya makazi yao mpa amri yako ilishinda neno lako likawa juu kabisa ingawaje washirikiina walichukia. Ewe Mwenye enzi Mungu mwinuwe kwa kuwa ametaabika kwa ajili yako, afikie daraja la juu kabisa katika jannah zako ili asilingane kwa daraja. Ili asiwe rika katika daraja wala malaika waliokaribu wasimkurubie hata Nabiy mursalu. Umtambulishe katika Ali wake waliotakaswa na umma wake walio waumini kuwa watakuwa na uombezi mwema zaidi ya vile ulivyo muahidi. Ewee mtekelezaji wa ahadi mtimizaji wa qauli. Ewee! mwenye uwezo wa kubadilisha maovu kwa mema mengi hakika wewe ndio mwenye fadhila tukufu mno.

DUA YA 3

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KWA MALAIKA WABEBAO ARSHI NA KWA KILA MALAIKA

Ewe Mola na kwa wabeba arshi yako ambao hawalegei kukusabihi wala hawachoki kukutakasa, wala hawafifii kukuabudu wewe hawazembei kufanya bidii katika amri yako. Na wala hawaghafiliki kuwa na nguvu ya mapenzi yako. Na Israafil malaika wa baragumu amesimama tayari angoja idhini yako tu na amri yako ili awazinduwe kwa pulizo waliotupwa chini makaburini. Na Mikail mwenye hadhi kwako na nafasi ya daraja la juu katika kukutii wewe. Na Jibril atambulikaye kwa uaminifu kufikisha wahyi (ufunuo) wako, mwenye kutiiwa na wakazi wa mbingu yako mwenye kuheshimiwa mbele yako na mwenye kusogezwa karibu na wewe. Na roho ambaye yuna ngazi ya juu miongoni mwa malaika wa hijabu, na roho ambaye ni amri yako, Ewe Mola warehemu na wale malaika walio chini yao miongoni mwa wakazi wa mbingu zako ambao ni miongoni mwa waamini wao kwa risala yako (jumbe) ambao hawachoshwi na hali ya kudumu wala hawaishiwi nguvu kwa kazi ngumu wala hawalegei. Wala hawasumbuliwi na matamanio ili waache kuku takasa wewe. Hawakatishwi na wakati wa usahaulifu katika kukutukuza. Wanyenyekevu wa macho hawathubutu kuinua macho yao kukuangalia videvu vyao viko chini ambao utashi wao umekuwa mrefu kwa yaliyo kwako. Wamerukwa na akili kwa upendo wa kuzitaja neema zako. Wanyenyekevu mbele ya utukufu wako na utukufu wa ukubwa wako. Wasemao waangaliapo jehanam ikiunguruma kwa ajili ya wanaokuasi, utakasifu ni wako hatujakuabudu ipasavyo kukuabudu wewe. Hivyo basi uwarehemu na rawhaniyyeena miongoni mwa malaika wako na wale wenye ukaribu kwako.Na wale wapelekao mambo yaliyo ghaibu kwa mitume wako na walioaminiwa kwa wahyi wako.Na kabila za malaika uliowafanya mahsusi kwa ajili yako na uliowaepusha na haja ya chakula na kinywaji kwa kukutakasa wewe uliowafanya waishi ndani ya tabaka za mbingu zako. Na ambao watasimama kwenye mipaka ya mbingu iteremkapo amri kwa kutimia ahadi yako.

Wahifadhi wa mvua na watawanyaji wa mawingu ambaye kwa sauti ya karipio lake husikika muungurumo wa radu. Na mrindimo wa mawingu unapoelea kuelekea kwenye umeme sauti ya muwako itajitokeza. Na mpelekaji wa theluji na baridi na wateremkao na matone ya mvua yateremkapo na walinzi wa hazina za upendo. Mawakala wa ulinzi wa mirima isije poromoka. Na wale uliowajulisha uzito wa maji na vipimo vilivyomo katika mvuwa kubwa na wingi wake. Na malaika ambao ni wajumbe wako kwa wana ardhi kwa mambo yachukizayo na yashukayo miongoni mwa balaa na raha ipendwayo. Na malaika watukufu waandishi na malaika wa mauti na wasaidizi wake. Na Munkari na Nakiiri. Na Ruman mtahini wa kaburini na wazunguka Baitul-maamur na Maliki malaika mlinzi wa moto na Rizwan malaika walinzi wa jannah. Na ambao (hawamuasi Mungu aliyowaamrisha na wafanya wanayo amriwa). Na ambao husema (salamu iwe juu yenu kwa vile mulivumilia neema ni nyumba ya mwisho). Na Mazabaniya ambao wakiambiwa: (Mchukuweni mtupeni kisha mchomeni katika jehannam) watamharakia upesi sana hawatompa muda.Na yule ambaye tumeshindwa kumtaja na hatukujua mahali pake kwako na kwa jambo gani umemuwakilisha.Na malaika wakazi wa hewani na ardhini na majini, na wale uliowawakilisha kwa viumbe.Warehemu siku ambayo kila nafsi itakuja ikiwa na msukumaji na shahid. Uwarehemu kwa rehema zitakazo wazidishia heshima juu ya heshima zako na kuwazidishia usafi juu ya usafi wao. O Mola ukiwarehemu malaika wako na wajumbe wako na kuwafikishia (maombi yetu ya) rehma kwao (twakuomba) uwarehemu kwa kauli njema uliotufungulia kwa ajili yao. Wewe ni mpaji mkarimu.

Dua ya 4

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE AMANI IMFIKIE KATIKA KUWA TAKIA REHMA WAFUWASI WA MITUME NA WALIO WASADIKI MITUME

Ewe Mola na kwa ajili ya wafuasi wa mitume na waliowasadiki bila kuonekana miongoni mwa wana wa ardhini wanapokabiliwa na upinzani wa wale wanaowapinga kwa kuwafanya waongo. Na kuwaonea shauku mitume kwa njia ya iymani ya hakika. Ulituma katika kila muda na zama uliwatuma mitume wakiwa na dalili kwa ajili ya watu. Tokea Nabiy Adam mpaka zama za Muhammad (s.a.w.) miongoni mwa maimamu waongofu na viongozi wa wachamungu wote amani iwafikie. wakumbuke kwa msamaha na ridhaa. Ewe Mola khususan kwa swahaba wake Muhammad waliokuwa wema katika usuhuba. Waliokuwa na majaribu mema katika kumsaidia na kumhami. Walimwitikia kwa haraka alipowasikilizishia hoja za ujumbe wake. Walitengana na wake, na watoto ili kulidhihirisha neno lake. Waliwapiga vita mababa na watoto ili kuuthibitisha unabiy wake kupitia kwake walishinda. Waliozingirwa na upendo wake watarajia biashara ambayo haitokuwa na hasara katika upendo wake. Na wale waliotengwa na jamaa zao pale tu waliposhikamana naye, na ukiraba kwao ulikwisha ili tu wakitulia chini ya kivuli cha ukaribu wake. Hivyo basi ewe Mola usiwasahau kwa yale waliyoyaacha kwa ajili yako na katika wewe waridhishe kwa ridhaa zako. Kwa ajili ya faida ya viumbe wamejitoa kwako. Walipokuwa na mjumbe wako walikuwa walinganiaji wako kwa ajili yako, waonyeshe ridhaa yako kwa kuhama nyumba za watu wao kwa ajili yake na kutoka kwao nje ya maisha ya wasaa na kwenda kwenye maisha ya dhiki. Wale ambao kwa kudhulumiwa kwao umewazidishia ili kuienzi dini yako. Ewe Mola wape taabeena waliotenda mema kwa kufuata nyayo za masahaba.Wanasema: (Ee! Mola wetu tusamehe sisi na ndugu zetu waliotutangulia kwa iymani) malipo yako yaliyomema kwa waliokwenda njia yao waliochagua mwendo wao na walikwenda kwa utaratibu wao hawakugeuzwa upande na shaka katika utambuzi wao. Na wala hawakuingiwa na shaka katika kufuata nyayo zao na kuongoka na mwongozi wa nuru yao.Waendesha dini yao hali ya kuwahami na kuwasaidia.Wanaongoka kwa mwongozo wao, wanawafikiana nao. Wala hawawatuhumu kwa yale waliowapa. Ewe Mola wape rehma taabeena toka siku yetu hii mpaka siku ya malipo na rehma iwafikie wake zao na kizazi chao na wale waliokutii miongoni mwao. Rehma ambayo itawalinda wasikuasi na itawapatia nafasi katika maeneo ya janna yako.

Na itawakinga na makidi ya shetani. Na itawasaidia kwa yale waliokuomba msaada kwa ajili yake miongoni mwa wema. Na itawalinda na matukio ya ghafla ya usiku na mchana isipokuwa tukio lijalo kwa wema. Kwazo utawaimarisha kuwa na iymani ya matarajio mema kwako na kutumai yale uliyonayo. Na watokane na tuhuma kwa ajili ya yale yaliyomo mikononi mwa waja. Ili uwarejeshe kwenye upendo wako na kukuogopa wewe. Washawishhi waache kupigania wingi wa mapato ya haraka. Na uwapendezeshe kufanya mema kwa ajili ya baadaye na kujiandaa kwa yatakayojitokeza baada ya umauti. Na uwafanyie wepesi kila tatizo litakalo wafika siku nyoyo zitokapo nje ya viwili wili vyake. Na uwaepushe na yaletayo fitna miongoni mwa yaliyo hadharishwa, kutupwa motoni na kubaki milele humo.Uwafanye wawe katika amani miongoni mwa makazi ya wachamungu.