AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18495
Pakua: 2954

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18495 / Pakua: 2954
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

2

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 5

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE KWA AJILI YAKE MWENYEWE (A.S) NA KWA WALIO CHINI YA WILAYA YAKE

Ewee! ambaye maajabu ya utukufu wake hayatokwisha. Mrehemu Muhamadi na Ali zake tuzuwiye kupotoka katika utukufu wako. O we ambaye muda wa ufalme wake hautakoma. Mrehemu Muhammad na Aali zake zikomboe shingo zetu na lipizi zako. Oh! wee ambaye hazishi hazina za rehma zake mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utupe sehemu katika rehema zako, Oh wee ambaye macho yanashindwa kumwona. Mrehemu Muhammad na Aali zake, tusogeze karibu yako. Oh! wee ambaye unakuwa mdogo ukubwa wa kila kikubwa mbele yake. Mrehemu Muhammad na Aali zake utupe heshima. Oh, wee ambaye mbele yake hujitokeza kila kilichojificha. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Usitufedheheshe mbele yako. Ewe Mola! tuonndolee haja ya hiba ya watowao hiba kupitia hiba zako. Tutosheleze tusisumbuliwe na kitwea cha wajitengao nasi kwa mawasiliano yako ili tusimsihi yeyote pamoja na kuwa wewe watupa bure. Wala tusione kitwe kutokana na yeyote ikiwa fadhila zako twazipata. Ewee Mola! Mrehemu Muhammad na Aali wake. Na utupangie wala usipanguwe dhidi yetu. Tupe ushauri kwa faida yetu wala si kinyume chake. Mzunguko wa neema udumishe kwetu wala usiuelekeze kwingine. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na utulinde sisi kuwa dhidi yako. Na utulinde kupitia wewe mwenyewe.

Utuongoze kuelekea kwako wala usituweke mbali na wewe. Kwa hakika umlindaye huwa salama. Na umwongozaye hujuwa. Umwekaye karibu nawe hupata ngawira. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Na tukinge na makali ya mabadiliko ya wakati, na shari ya windo la shetani. Na ukali wa udhalimu wa kisultani Ewe Mola kwa hakika wajitoshao wajitosha kwa fadhila za uwezo wako. Msalie Muhammad na Aali zake kwa hakika hutowa watowao kupitia wingi wa utajiri wako. Mrehemu Muhammad na Aali zake na utupe, huongoka waongokao kwa nuru ya uso wako, msalie Muhammad na Aali wake na tuongoze. Ewe Mola hakika uliyemfanya rafiki hakumdhuru kutelekezwa na watelekezaji. Na uliyempa hapungukiwi kwa kunyimwa na wanyimaji. Na uliyemwongoza haumpotezi upotovu wa wapotovu. Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utuzuiye (tusidhuriwe na waja wako) kwa nguvu zako. Tutosheleze tusimhitaji mwingine mbali na wewe kwa kuungwa mkono na wewe. Tupitishe njia za haki kwa mwongozo wako. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia usalama wa nyoyo zetu kwa kukumbuka utukufu wako. Na nafasi ya wazi ya miili yetu iwe twakushukuru neema zako. Na ujaaliye mtiririko wa ndimi zetu uwe katika kusifu ihisani zako. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Tujaalie tuwe miongoni mwa wahitaji wako wanaowaita watu kuja kwako na viongozi wako waongozao kuelekea kwako. Na tuwe miongoni mwa watu makhsusi uliowafanya wawe makhsusi kwako. Ewe mwenye kurehemu mno kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA 6

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE A.S. NYAKATI ZA ASUBUHI NA JIONI

Sifa njema ni za Mungu ambaye ameumba usiku na mchana kwa nguvu zake. Na amezipambanuwa kwa uwezo wake. Na amekifanyia kila kimoja kati ya hivi viwili mpaka wenye kikomo na muda ulio na mwisho. Hukiingiza kila kimoja ndani ya mwenzake. Na humwingiza mwenzake ndani.yake. Kwa mpango kutokana na yeye, kwa ajili ya waja kwa vile awalishavyo na kwa hivyo ndivyo awakuzavyo. Amewaumbia usiku ili wapumzike humo kutokana na harakati za taabu na juhudi zenye kuchosha. Na ameufanya (usiku) kuwa vazi ili wajisitiri kwa mapumziko humo kwa kulala, iwe kwao kiburudisho na nguvu mpya na waifanyie kwa huo usiku furaha na matamanio. Na amewaumbia mchana uwezeshao kuona ili wazifikie fadhila zake. Na iwe sababu ya kuipata rizki yake. Na wazunguke kwa uhuru katika ardhi yake wakitafuta kipato cha mwenye haraka ya dunia yake na kufanikiwa ya baadaye katika maisha ya akhera. Kwa yote hayo awawekea sawa hali yao na kuuzifanyia mtihani khabari zao, ili awaangalie wakoje wakati wa utii wake na mahali mwa wajibu zake. Na sehemu za hukumu zake.(Ili awalipe waliotenda maovu kulingana na waliyotenda. Na awalipe waliotenda mema wema.) Ewe Mola! sifa zote njema ni zako. Kwa kutukunjulia asubuhi, na kutufanya tufurahie mwanga wa mchana. Na umetufanya tuone jinsi ya kuitafuta chakula na umetulinda na maafa. Tumekuwa asubuhi na vimekuwa vitu vyote pamoja ni vyako. Mbingu, ardhi na ulicho kitawanya kwa kila mmoja wao chenye kutulia na chenye kufanya harakati kikazi na chenye kusafiri na kirukacho juu kabisa angani na kijifichacho chini ya ardhi twapambazukiwa na asubuhi katika ushiko wako. Twazingirwa na ufalme wako na mamlaka yako. Tumo ndani ya utashi wako. Tunakwenda hapo na pale kwa amri yako. Tunageuka geuka ndani ya mpango wako.Hatumiliki letu jambo ila ulilolipitisha, wala hatulimiliki jambo la kheri isipokuwa ulilotoa. Na hii siku mpya imekuja, itakuwa shahidi madhubuti kwetu, tukifanya mema itatuaga iondokapo kwa sifa njema. Na tufanyapo maovu itatuacha kwa lawama. Ewe! Mola msalie Muhammad na Aali wake. Na utupe uzuri wa kusuhubiana naye na utulinde na kutengana naye vibaya, kwa kutenda yasiyofaa au kutenda dhambi yeyote ile ndogo au kubwa. Tufanye tuwe na matendo mema mengi humo na tuepushe na matendo maovu humo. Na jaza kwa ajili yetu kati ya ncha zake mbili sifa njema na shukrani, ujira na akiba, fadhila na ihsani. Ewe Mola wepesisha mizigo yetu kwa waandishi watukufu, na lijaze mema yetu katika sahifa zetu (karatasi za hesabu) usitudharaulishe kwako kwa matendo yetu maovu. Ewe Mola tujaaliye hadhi toka kwa waja wako katika kila sehemu ya shukurani zako. Na ushahidi wa kweli miongoni mwa malaika wako.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Utuhifadhi mbele yetu na nyuma yetu kuliani kwetu na kushotoni kwetu na pande zetu zoote, hifadhi inayotulinda na kukuasi wewe, yenye kutuongoza kwenye utii wako, yenye kutekeleza upendo wako. Ewe Mola! msalie Muhammad na Aali zake. Na utukubalie katika siku yetu hii na usiku wetu huu na katika siku zetu zoote kuitenda kheri na kuihama shari na kuishukuru neema na kuzifuata sunnah na kujiepusha na bidaa, na tuwe wenye kuamrisha mema na kukemea maovu. Kuulinda Uislamu na kuutweza ubatili na kuudhalilisha ili kuinusuru haki na kuipa nguvu kumwongoza aliyepotoka kumsaidia mnyonge kumkomboa aliyekatika taabu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Na ifanye (siku) kuwa ya baraka mno kuliko siku ya baraka tuijuayo na mwenzi bora kuliko mwenzi yeyote tumepata kuwa naye na wakati uwe ni wakati bora kuliko wakati wowote tumepata kuwa chini ya kivuli chake. Na utufanye tuwe wenye kuridhiwa mno miongoni mwa waliopitiwa na usiku na mchana katika jumla ya viumbe wako. Wenye kushukuru sana kati yao kwa mema uliowapa miongoni mwa neema zako. Watekelezaji kwa uthabiti mno wa sheria uliowawekea miongoni mwa sheria zako. Na wenye kujizuia sana na uliyo yahadharisha miongoni mwa makatazo yako. Ewe Mola mimi nakufanya shahidi nawe nishahidi tosha. Na ninazifanya mbingu zako na ardhi zako na uliowafanya kuwa wakazi wa mbingu na ardhi kuwa mashahidi miongoni mwa malaika wako na viumbe wako wengine. Katika siku yangu hii saa yangu hii usiku wangu huu na kikazi changu hiki. Hakika mimi nashuhudia kuwa hakika wewe ni Mungu ambaye hapana Mungu mwingine isipokuwa ni wewe! mwenye kuidhibiti adala uko mwadilifu katika hukumu mwenye huruma kwa waja-u-Mfalme wa Wafalme mwenye huruma kwa viumbe. Yakuwa Muhammad ni mja wako na ni mjumbe wako mteule wako miongoni mwa viumbe wako. Umembebesha risala yako na ameitekeleza. Ulimuamuru kuitowa nasaha kwa umma wake na aliunasihi. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Zaidi ya vile ulivyomsalia yeyote katika viumbe wako. Umpe kwa niaba yetu kilicho bora ulichompa yeyote katika waja wako. Na umlipe kwa niaba yetu kilicho bora na hheshima zaidi kuliko ulichomlipa yeyote miongoni mwa Manabiy wako kwa niaba ya umma wake. Hakika wewe ndiye mtowaji kwa wingi na msamehevu wa makubwa nawe u mwenye huruma zaidi kuliko mwenye huruma yeyote. Msalie Muhammad na Aali zake wema waliotahirika wateule waheshimiwa.

DUA YA 7

NA ILIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S) ANAPOTOKEWA NA JAMBO SUMBUFU AU KUSHUKIWA NA TAABU NA WAKATI WA KUKERWA

Oh! we ambaye kwake hufunguka mafundo ya mambo yachukizayo. Ee! wee ambaye kwake makali ya shida huwa butu. Ee we! ambaye huombwa njia ya kutoka kuelekea kwenye burudisho la faraja. Magumu yamekuwa dhalili mbele ya nguvu zako. Kwa huruma zako sababu zimepatikana. Kwa nguvu zako hukumu zimepita. Kwa utashi wako vitu vimekwenda kama ilivyotakiwa. Kwa utashi wako bila ya kauli yako vimewajibika. Kwa utashi wako vimejiziwiya bila ya kutumia katazo lako, wewe ndiye wa kuombwa wakati wa jambo litishalo. Na ndio kimbilio la wakati wa shida haiondoki isipokuwa ile shida ulioiondowa. Haitoki isipokuwa uliyoitowa, yameniteremkia ewe Mola wangu ambayo uzito wake umenielemea.Juu yangu kumeshuka jambo ambalo uzito wake umenishinda. Kwa nguvu zako umeshusha juu yangu kwa mamlaka yako umeelekeza kwangu.

Hakuna wa kuondowa ulichokileta, wala kuziwiya ulichokielekeza, wala wakufunguwa ulicho funga, wala wakufunga ulichokifunguwa, wala wa kufanya kiwe chepesi ulichokifanya kigumu, wala wakumsaidia uliyemwacha. Msalie Muhammad na Aali zake, na nifungulie ewe Mola wangu mlango wa faraja kwa rehma zako, niondolee mamlaka yatishayo kwa nguvu zako. Unipe mtazamo mzuri kwa malalamiko yangu. Unionjeshe utamu wa matendo kwa niliyoomba. Na unipe kutoka kwako rehmah na faraja njema. Na nijaalie mwanya wa kupenya kutoka kwako. Usinifanye nijishughulishe na mengine na kuacha wajibu wako. Na kuifanya sunnah yako. Nimezikika na yaliyo nishukia Ee Mola wangu nimejawa na huzuni kwa kuyabeba yaliyo niteremkia.Wewe ndiye mwenye uwezo wa kuondoa yaliyo nifika na kuyaweka mbali niliyoangukia, nifanyie hivyo ingawaje sistahiki kwako hivyo Ewee! bwana wa arshi tukufu.

DUA YA 8

DU'A ZAKE KATIKA KUJILINDA NA MAMBO YACHUKIZAYO NA TABIA MBAYA NA MATENDO YALAUMIWAYO

Ewe Mola najilinda na wewe dhidi ya uchochezi wa pupa na ukali wa ghadhabu na kuhemewa na husda na kudhofika kwa subira na uchache wa kutosheka na ukali wa tabia.Na uchochezi wa harara. Na kumilikiwa na msukumo wa tabia au jadhba. Na mgeuzo wa nia na kwenda kinyume na uongofu na sinzio la kughafilisha na kujikalifisha (yaani kujitwisha mambo zaidi ya uwezo) kuchaguwa batili na kuiacha haki. Na kujibakisha na kuendelea na madhambi na kuyadogesha maasi na kuukuza utii. Na kujifaharisha kwa matajiri na kuwadharau masikini na uangalizi mbaya kwa walio chini yetu. Na kutokuwa na shukrani kwa waliotutendea mema au tumsaidiye dhwalimu au kumtelekeza mwenye taabu au kujitakia yasiyo haki. Kwetu au tuongee kuhusu elimu bila ya elimu au kujihusisha na kumghushi yeyote na kujionea fahari matendo yetu. Na kuwa na matumaini marefu. Na tunajilinda na wewe kuwa na undani na kukidharau kidogo. Na kudhibitiwa na shetani. Au kuhujumiwa na wakati, au kudhulumiwa na mtawala. Na tunajilinda na wewe kufanya israfu na kuwa na kisichotosha. Na tunajilinda na wewe na masimango ya maadui. Na kukosa wenzi, na kuishi katika shida na kufa bila ya maandalizi. Na twajilinda na hasara kubwa mno na msiba mkubwa na twajilinda na mwisho mbaya, na kunyimwa thawabu na kufikwa na adhabu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake na unilinde na yote hayo kwa huruma yako na waumini wote wanaume na wanawake. Ewe! mwingi wa rehma kuliko wenye kurehemu wote.

DUA YA9

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIWA NA SHAUKU SANA YA KUOMBA MSAMAHA KWA MWENYE ENZI MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake, tufanye tuelekee kwenye toba uipendayo. Na ututoe tusiendelee kutenda uchukialo. Oh! Mola tusimamapo kati ya hali mbili ya upungufu iwe siku ya dini au dunia uiondoe hali ile ya upungufu haraka iishe. Na ujaalie kwangu toba iwe ya kubaki sana miongoni mwa mawili hayo. Na tuyakusudiapo mambo mawili moja la kuridhisha kutoka kwetu na la pili lakuchukiza toka kwetu. Tufanye tuelemee kwenye lile likuridhishalo toka kwetu. Dhoofisha nguvu zetu kwenye linalokuudhi na kutuchukia kwa ajili yake. Usiziache nafsi zetu kuchaguwa kwa sababu zenyewe huchaguwa batili isipokuwa ulizozipa taufiki. Na zenye kuamrisha mabaya isipokuwa ukirehemu. Ewe Mola kutokana na unyonge umetuumba, na umetujenga juu ya hali duni umetuanza (kutuumba) kutokana na maji hafifu. Hatuna uwezo isipokuwa kwa nguvu zako, wala nguvu hatuna isipokuwa kwa msaada wako. Tuwezeshe kwa kutufanikisha. Tuongoze kwenye njia ya sawa kwa mwongozo wako.

Ipofushe nguvu ya kuona ya nyoyo zetu dhidi ya yaendayo kinyume na mahaba yako. Usikijaalie chochote katika viungo vyetu vya mwili upenyo wa kwenye maasi yako. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aali zake. Na jaalia nong'ono za nyoyo zetu na harakati za viuongo vyetu na mitupo ya macho yetu na semi za ndimi zetu viwe kwa ajili ya mambo yawajibishayo thawabu zako. Ili tusije pitwa na jema twastahiki kwalo malipo yako. Na usitubakishie tendo baya ambalo tutastahiki kwa ajili yake adhabu yako.

DUA YA 10

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIOMBA KIMBILIO KWA MUNGU

Ewe Mola! Ukipenda tusamehe kwa fadhila zako na ukipenda utatuadhibu na hiyo itakuwa kwa uadilifu wako. Hivyo basi tufanyie wepesi msamaha wako kwa huruma yako. Tuepushe na adhabu yako kwa subira zako. Kwa kuwa hatuna uwezo kuukabili uadilifu wako. Wala hakuna atayeokoka bila ya msamaha wako. Ewe mwenye kujitosheleza kuliko matajiri wote. Tu hapa waja wako mbele yako. Nami ni fakiri kuliko mafakiri wote kwako. Urekebishe ufakiri wetu kwa wasaa wako. Usikate matumaini yetu kwa zuio lako, utakuwa umemdhalilisha mwenye kukuomba heri. Na umemnyima aliyekuomba fadhila zako. Kwa hiyo tugeukie kwa nani mbali na wewe, twende! Wapi kama si mlangoni kwako! Utakatifu ni wako, sisi ni wenye kudhikika ambao umewajibisha kuwakubalia. Ni wenye uovu uliowaahidi kuwaondolea uovu wao. Ni kitu chafanana sana na utashi wako. Na ni bora kulingana na utukufu wako, kumuhurumia aliye kuomba umuhurumie. Kumsaidia aliekuomba msaada uhurumie ungamo letu kwako. Tutosheleze tujitupapo mbele yako. Oh! Mola wetu hakika shetani ametusimanga, kwa kuwa tumemfuata katika kukuasi wewe. Mrehemu Muhammad na Aali zake usimwache atusimange baada ya kuwa tumemwacha kwa ajili yako. Tumemtelekeza na kuelekea kwako.

3

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 11

DU'A ZAKE KWA AJILI YA MWISHO MWEMA

Ewe! mwenye utajo wake ni heshima kwa wamtajao. Ewe! mwenye shukrani yake ni ufanisi kwa wenye kumshukuru. Owe! Mwenye utii wake ni uokovu kwa wenye kumtii. Mswaliye Muhammad na Aali zake. Zihangaishe nyoyo zetu katika kukutaja wewe na kuziweka mbali na utajo mwingine wote. Na zihangaishe ndimi zetu katika kukushukuru na ziwe mbali na shukuru zingine zote. Na viungo vyetu vya miili vihangaike kukutii wewe na kuwa mbali na utii mwingine wowote. Ukitupangia wakati wa faragh (usio na kazi) basi jaalia faragha iliyo salama. Tusifuatwe na lipizi baya, wala usituambatanishie humo na kuchoshwa, ili watuondokee waandishi wa maovu na nyaraka tupu zisizotaja chochote katika maovu yetu. Na warudi waandishi wa mema kutoka kwetu wakiwa na furaha na waliyoyaandika miongoni mwa mema yetu. Na ziishapo siku za maisha yetu na kumalizika kwa muda wa umri wetu. Na kutufikia wito wako ambao hapana budi utufikie na pia hapana budi kuujibu. Msalie Muhammad na Aali zake. Na jaalia mwisho wa matokeo ya hesabu ya waandishi wa mabaya yetu kuwa toba yenye kukubaliwa. Usitusimamishe na dhambi tuliyotenda baada yake, wala maasi tuliyoyafanya, wala usifichue sitara uliyotusitiri mbele ya mashahidi siku zitakapojaribiwa khabari za waja wako. Hakika wewe ni mpole kwa akuombaye na u mwenye kuitika kwa akuitaye.

DUA YA 12

DU'A ZAKE KATIKA KUKIRI NA KUOMBA TOBA KWA MUNGU MTUKUFU

Ewe Mola! tabia tatu zaniziwiya kukuomba na moja yanihimiza nikuombe, iniziwiayo jambo umeamrisha na nikazembea kulifanya. Na katazo umenikataza nikaharakia kulitenda. Na neema ulinineemesha nayo nikashindwa kuishukuru. Na linihimizalo kukuomba ni fadhila zako kwa mwenye kuelekeza uso wake kwako. Na akaja kwa dhana nzuri kwako kwa kuwa ihsani zako zote ni fadhila. Na kwa sababu neema zako zote ni mwanzo mpya. Basi mimi huyu hapa Ewee! Mola wangu mwenye kusimama kwenye mlango wa enzi yako msimamo wa aliyesalim amri dhalili.Nikikuomba nikiwa na haya ombi la fakiri hohe hahe mnyonge. Mwenye kukiri kwako, sikusalimu amri wakati wa ihsani yako isipokuwa kwa kujiweka mbali na maasi yako. Sijapata kuwa katika hali zangu zote bila ya huruma zako. Je kutanifaa ewe Mola wangu kukiri kwangu kwako kwa maovu niliyotenda? Je kutaniokoa kutambua kwangu kwako kwa mabaya niliyotenda? Au utawajibisha makasiriko yako kwangu katika kikao changu hiki? Au chukio lako litaniambata wakati wa DU'A yangu? Utakatifu ni wako, sikati tamaa nawe hali umenifungulia mlango wa toba kwako. Bali nasema usemi wa mja mnyonge mwenyekujidhulumu nafsi yake, mwenye kuifanya haramu ya Mola wake kuwa kitu chepesi. Ambaye dhambi zake zimekuwa kubwa mno. Ambaye siku zake zimemtumbia mgongo na kutokomea. Mpaka aonapo muda wa kazi ya ibada umeisha. Na upeo wa umri umekwisha. Na akawa na yakini kuwa hana njia ya kujiepusha nawe, na hana kimbilio litalomweka mbali nawe.

Akugeukia kwa marejeo ya mara kwa mara, na kufanya toba kwako kwa ikhlaswi. Atasimama mbele yako kwa moyo safi kabisa. Na kukuomba kwa sauti dhalili ya chini, ameinama mbele yako na kujipinda hali ameinamisha kichwa chake chini, woga wake watetemesha miguu yake machozi yamtiririka mashavuni mwake. Akuomba akisema Ewe mwingi wa kurehemu kuliko wote! Ewe mwingi wa kurehemu wa wanaorejea kwake wakimwomba huruma. Ewee mwenye huruma mno kwa wenye kumzunguka waombao msamaha. Ewe ambaye msamaha wake ni mwingi kuliko malipizi yake. Ewe ambaye ridhaa yake ni nyingi sana kuliko makasiriko yake. Ewe yule ambaye amesifika kwa waja wake na njema saburi njema. Ewe ambaye amewazowesha waja wake kwa kukubali marejeo yao ya mara kwa mara. Oh! yule ambaye amewarekebisha waharibifu wao kwa njia ya tobah. Oh! yule ambaye ameridhika na madogo katika matendo yao. Oh! yule ambaye huwalipa mengi kwa machache yao. Oh! yule ambaye amechukuwa dhamana kwa ajili yao kuzikubali DU'A. Oh! yule ambaye amewaahidi mwenyewe binafsi kwa fadhila zake malipo mema. Mimi sio muasi zaidi kuliko waliokuasi na umewasamehe, wala mimi si mlaumiwa mno miongoni mwa walioomba udhuru kwako na umewakubalia, wala mimi si mdhalimu mno miongoni mwa waliotubu kwako na umepokea toba yao. Natubu kwako katika kikao changu hiki toba ya mwenye kujutia waliyompita. Mwenye kutambua yaliyomzunguka, mwenye haya sana kwa yaliyo mfika, ajua kuwa kuisamehe dhambi kubwa mno haliwi jambo kubwa kwako.

Na kuyafumbia macho madhambi makubwa kabbisa haiwi ngumu kwako. kuyavumilia makosa mabaya sana ya jinai hayakupi tabu. Na yakuwa mja wako mpendwa sana kwako ni mwenye kuacha kibri mbele yako. Na akajiepusha na kung'ang'ania, kashikamana na kuomba msamaha. Nami najitakasa kwako nisiwe na kibri na ninajilinda kwako nisiwe mwenye kung'ang'ania nakuomba msamaha kwa nililozembea. Naomba msaada kwa nililohemewa ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nipe yaliyowajibu wangu kwako, niondolee ninayostahiki kwako. Nitakase na wayaogopayo waovu. Wewe ni mwingi wa msamaha, mwenye kutumainiwa msamaha, wajulikana kuwa umvumilivu. Haja yangu haina pakuitafutia isipokuwa kwako. Wala dhambi zangu hazina wakuzisamehe asiyekuwa wewe. Je! lawezekana hilo? Sijihofu binafsi ila kwako, hakika wewe ni mstahiki wa taqwa na mstahiki wa msamaha.Mrehemu Muhammad na Aliy zake nikidhie haja yangu. Fanikisha ombi langu. Nisamehe dhambi zangu. Nipe dhamana ya woga wa nafsi yangu hayo ni mepesi kwako, aameen ewe bwana wa maumbile yote.

DUA YA 13

DU'A ZAKE KUMWOMBA HAJA MUNGU MTUKUFU

Oh Allah. Ewe! mwisho wa maombi ya haja zote. Ewe! ambaye kupitia kwake mahitaji hupatikana. Ewe! ambaye hauzi neema zake kwa thamani. Oh! yule ambaye hakipaki tope akitowacho kwa masimbulizi. Ewe! yule ambaye hutosheka kwa kupitia kwake hatosheki mtoshekaji bila ya yeye. Ewe yule ambaye hutakiwa na hauwi utashi kando na yeye. Ewe yule ambaye hazina zake hazimalizwi na maombi. Ewe yule ambaye sababu hazibadilishi hikima yake. Oh! yule ambaye hazishi kwake haja za wahitaji. Oh! yule ambaye hayampi dhiki maombi ya waombao, umesifika kwake kutokuwa muhitaji toka kwa viumbe wako. Wewe wastahiki kuwa uwahitajii wao, umewahusisha na ufakiri wao ndio wahitaji kwako. Hivyo basi mwenye kujaribu kuziba pengo lake kupitia kwako. Na akusudia kujiondolea ufakiri kwa njia yako. Atakuwa ametafuta mahitaji yake mahali pafaapo. Na atakuwa ameyaleta mahitaji yake katika njia zake. Na mwenye kuelekeza mahitaji yake kwa yeyote miongoni mwa viumbe wako au kuifanya sababu ya kufanikiwa kwake kando na wewe atakuwa amejiweka kwenye hatari ya kunyimwa. Na atakuwa amestahiki kwako kukosa ihsani. Oh! Allah ninahaja kwako. Juhudi yangu imeshindwa, mbinu zangu zimeshindwa kuifikia nafsi yangu imenishawishi kuifikisha haja yangu kwa awezaye kuifikisha kwako. Wala hajitoshi katika mahitaji yako kando na wewe, na huku ni kuteleza miongoni mwa mtelezo wa watenda makosa na ni kujikwaa wanako jikwaa watenda madhambi. Kisha nilizinduka kwa kumbusho lako kwangu kutokana na mghafala wangu. Nimeinuka kwa taufiki yako kutoka kwenye mtelezo wangu.

Nimeimarika kwa imarisho lako na kujitoa kwenye telezo langu. Nasema subhana Rabiy (utakatifu ni wa Mola wangu), vipi muhitaji amwomba muhitaji mwingine? Ni vipi asiyekuwa na kitu amwomba asiyekuwa na kitu mwingine! Hivyo nimekuja kwako ewe Mola wangu kwa upendo, nimeyaelekeza matumaini yangu juu yako kwa kukuamini. Na nimejua kuwa mengi nikuombayo ni kitu kidogo mbele ya utajiri wako. Mazito nikuombayo ni kidogo kulinganisha na wasaa wako. Na ukarimu wako hautakuwa mdogo kwa sababu ya ombi la yeyote. Na kwa hakika mkono wako kwa utowaji uko juu kuliko kila mkono. Ewee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake, nichukuwe kwa ukarimu wako kwa kunifadhili. Na usinichukuwe kulingana na uadilifu wako si kwa ninavyostahiki. Mimi si wa kwanza kukusihi miongoni mwa aliokusihi umempa hali ilikuwa astahiki kunyimwa. Na wala si kuwa mwombaji wa kwanza katika aliyekuomba na ukamfadhili hali ya kuwa alikuwa apaswa kunyimwa. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Na nikubalie ombi langu kwa wito wangu kuwa karibu. Uhurumie unyenyekevu wangu, isikilize sauti yangu, usiyakate matumaini yangu, usikate kiungo changu na wewe. Usinielekeze kwa haja yangu hii au nyingine kwa mtu mwingine. Nitilie manani ili kufanikisha ombi langu, na kidhi haja yangu ili kukipata nilichokiomba kabla sijatoka hapa niliposimama, kwa kunirahisishia kwako mimi magumu. Na uzuri wa kunikadiria kwako katika mambo yote. Mrehemu Muhammad na Jamiy yake, rehema ya kudumu na yenye kukuwa, kuendelea kusiko katika. Muda wake uwe hauna mwisho. Fanya hivyo iwe ni msaada kwangu, na iwe ndio sababu ya kufanikiwa ombi langu.Wewe ni mwenye wasaa mkarimu na miongoni mwa haja zangu ewe bwana wangu ni fulani na fulani (hapo utafanya sijda na kuisema haja yaneyewe badala fulani fulani). (Useme haya ukiwa ndani ya sijda):- Fadhila zake zimenipa raha. Ihsani yako imenionyesha njia. Nakuomba kwako na kwa Muhammad na Aliy wake ziwafikie rehma zako usinirudishe kinyume na matumaini yangu.

DUA YA 14

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AKIFANYIWA UCHOKOZI NA AONAPO ASIYOYAPENDA TOKA KWA WADHALIMU

Ewe! ambaye hazifichiki kwake habari za waliolemewa. Oh! wee ambaye kuhusu visa vyao ahitajii ushahidi. Oh! wee ambaye msaada wake upo karibu na wadhulumiwa. Ewe! ambaye msaada wake uko mbali na wadhalimu. Unajua ewe Mola wangu alivyoniumbua (fulani bin fulani) uliyomhadharisha na amekiuka kwangu uliyomkataza. Akionyesha hali ya kutokuwa na shukrani kwa neema zako kwake. Akidanganyika na uliyomkataza. Ewe Mola! mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mchukue aliyenidhulumu adui yangu kwa nguvu zako. Dugisha makali yake dhidi yangu kwa uwezo wako. Mshughulishe na aliyonayo, na ashindwe kumfikia amfanyiaye uadui ewe Mola! msalie Muhammad na Aliy zake, usimwachie anidhulumu. Nipe msaada mwema dhidi yake, nilinde na mfano wa vitendo vyake, usiniweke katika hali kama yake, ewe Mola! wangu mswalie Muhammad na Aliy zake. Na unisaidie dhidi yake msaada wa papo kwa papo, uwe kitulizo cha ghadhabu yangu kwake na kumaliza makasiriko yangu kumwelekea 'yeye. Ee Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Nifidie msamaha wako kwa dhulma yake kwangu. Nibadilishie uovu wa matendo yake kwangu iwe rehma zako kwangu. Kila chukizo kubwa liko chini kuliko ghadhabu zako. Na kila afa si sawa kulinganisha na ghadhabu zako. Ewe! Mola wangu kama ulivyonifanya nichukie kudhulumiwa, basi nilinde nisidhulumu. Ewe Mola sitolalamika kwa yeyote mbali na wewe. Na sitoomba msaada kwa hakimu ambaye si wewe. Vipi nithubutu hivyo! msalie Muhammad na Aliy zake. Iunganishe DU'A yangu na jibu, yakutanishe malalamiko yangu na mabadiliko. Ewe Mola wangu, usinifanyie majaribu ya kukata tamaa na insaafu yako. Wala usimfanyie yeye majaribu ya kujiona yuko salama na makatazo yako, asijeendelea kunidhulumu. Na kunizuia nisipate haki yangu. Mtambulishe haraka ulivyomuahidi mtenda dhulma. Na nijulishe mimi ahadi yako kuwajibu wenye kuzidiwa.

Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake, unipe taufiki ya kukubali uliyoniamulia kwa faida yangu na kinyume chake, nifanye niridhie uliyochukua kwa ajili yangu na uliyoyacbukuwa kutoka kwangu.Niongoze kwenye lililo sawa, na nitumikishe kwa lililo salama. Ewe Mola ikiwa ni bora kwangu uonavyo ni kuahirisha kuchukua kwa ajili yangu na kuacha kulipiza kisasi kwa aliyenidhulumu mpaka siku ya maamuzi na mkusanyiko wa magonvi! basi msalie Muhammad na Aliy zake.Nipe nguvu kutoka kwako kwa nia ya kweli na subira ya kudumu, nilinde na utashi mbaya na pupa ya wachoyo. Nifanyie picha ya mfano moyoni mwangu wa ulicho nihifadhia miongoni mwa thawabu zako na ulilomwandalia mgomvi wangu miongoni mwa malipo yako na adhabu yako. Fanya hilo iwe ndiyo sababu ya kukinai kwangu uliyohukumu na ithbati kwangu kwa uliyoyachagua. Ameen Oh! bwana wa malimwengu hakika wewe u mwenye fadhila kubwa na wewe u muweza wa kila kitu.

DUA YA 15

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE (A.S.) AKIWA MGONJWA AU AKISUMBULIWA NA JAMBO AU KUPATWA NA BALAA

Oh! Mola wangu sifa njema ni zako kwa vile nipo katika hali ya salama ya kiwiliwili changu. Sifa njema ni zako kwa kuwa ndio sababu ya uele kiwili wili changu. Sijui ewe Mola wangu ni ipi katika hali mbili hizi unastahiki kushukuriwa zaidi? Na upi katika nyakati mbili hizi uliobora kukuhimidi? Je ni wakati wa siha njema ambao umenipendezesha humo riziki zako nzuri, na umenipa uzima humo nitake radhi zako na fadhila zako. Kwayo umenipa nguvu kwa yale uliyonipa taufiki katika utii wako? Au wakati wa uele ambao humo umenichuja. Na neema ambazo umenitunukia? Ili kufanya wepesi yaliyonitopea juu ya mgongo wangu miongoni mwa makosa na kunitakasa maovu niliyozama ndani yake. Na kuniongoza kwenye toba na ukumbusho wa kuondoa matendo yasiyofaa kwa njia ya neema za hapo nyuma. Na kwa yote hayo yale waliyoniandikia malaika wawili waandishi wa matendo yangu mema ambayo moyo haukuweza kuyafikiria wala ulimi haukuweza kutamka wala kiungo cha mwili hakijatenda bali ni ufadhili mtupu toka kwako kwa ajili yangu.

Na hisani miongoni mwa matendo yako ya hisani kwangu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nipendezeshe uliyoyaridhia kwangu. Nifanyie wepesi uliyoniteremshia, nitakase uchafu nilioutanguliza. Nifutie shari niliyoitanguliza. Nionyeshe utamu wa afya njema, nionjeshe hali poa ya usalama. Na jaalia kutoka kwangu kwenye uele iwe kuelekea kwangu kwenye msamaha wako. Na mgeuko wangu toka kwenye kulemewa kwangu uwe ndio mwelekeo wangu kwenye kufumbiwa macho kwako. Epuko langu toka kwenye dhiki yangu liwe kuelekea kwenye burudisho lako. Usalama wangu toka kwenye shida hii uwe kuelekea faraja yako. Hakika wewe ni msifika kwa ihsani mwingi wa ihsani na huruma. Mpaji mkarimu mwenye utukufu na wema.

DUA YA 16

DU'A ZAKE AOMBAPO KUJITOA KWENYE DHAMBI ZAKE AU AKINYENYEKEA KUOMBA MSAMAHA WA DOSARI ZAKE

Oh! wee ambaye kwa rehma zake wanaomba msaada watenda dhambi. Oh! wee ambaye kwa kukumbuka ihsani yake hukimbilia wenye dhiki. Oh! wee ambaye kwa kumwogopa hulia wakosaji. Oh! wee faraja ya kila mpweka mgeni, Oh! we mfariji wa kila mwenye huzuni. Oh! wee msaada wa kila aliyetelekezwa mpweka. Oh! we msaidizi wa kila muhitaji aliyefukuzwa. Wewe ndiye ambaye umeeneza kwa kila kitu rehma na elimu. Na wewe ndiye ambaye umemfanyia kila kiumbe awe na hisa katika neema zako. Nawe ndiye ambaye msamaha wake uko juu zaidi kuliko adhabu zake. Wewe ndiye ambaye zatiririka rehma zake mbele ya ghadhabu zake. Na wewe ndiye ambaye upaji wake zaidi kuliko nyimo lake. Na wewe ndiye ambaye viumbe wote wamefunikwa na rehema zake, wewe ndiye ambaye hapendi malipo toka kwa aliyempa. Wewe ndiye ambaye hazidishi adhabu ya aliyemuasi. Mimi ewe! Mola wangu ni mja wako ambaye uliyemuamuru kukuomba. Akasema: Labeika na niko chini ya utumishi wako. Ni hapa ewe! bwana wangu nimejitupa mbele yako. Mimi ndiye yule ambaye makosa yameuzidi uwezo wa mgongo wake. Mimi ni yule ambaye madhambi yamemaliza umri wake. Na mimi ni yule ambaye kwa ujinga wake amekuasi, hali ukiwa haukustahiki hivyo toka kwake. Je! ewe Mola wangu utamrehemu akuombaye ili nikithirishe DU'A? Au utamsamehe mwenye kukulilia ili nifanye haraka kulia. Au wewe ni mwenye kumfumbia macho mwenye kutia mchanga uso wake kwa ajili yako akijidhalilisha? Au wewe ni mwenye kumtosheleza mwenye kushitakia kwako ufakiri wake akiwa na matumaini! Ewe Mola wangu usimvunje moyo ambaye asiye mpata mpaji mwingine mbali nawewe.

Usimtelekeze asiyeweza kujitosheleza kando yako na mwingine yeyote. Ewe Mola wangu mrehemu Muhammad na Aliy zake. Usinitumpie hali nimekuelekea. Usininyime hali nimekuomba, usinipige kofi la uso kwa kunikatalia hali nimesimama mbele yako. Wewe ndiye uliyejisifu nafsi yako kwa rehema. Basi mswalie Muhammad na Aliy zake nirehemu. Wewe ndiye uliyejiita mwenyewe kuwa umsamehevu, basi nisamehe. Waona ewe Mola wangu mbubujiko wa machozi kwa kukuogopa, yote hayo ni haya nionayo kwa ubaya wa matendo yangu. Kwa ajili hiyo imezima sauti yangu kukulilia. Umebutuka ulimi wangu sinong'oni nisalipo. Ewe Mola wangu yako ni sifa njema aibu ngapi umenisitiri hukunifedhehi dhambi ngapi umezifunika kwa ajili yangu hukunifanya niwe mashuhuri kwazo. Makosa mangapi nimeyatenda wala hukunichania pazia la sitara, wala haukunibandika utepe wa chuki ya fedheha yake, wala haukudhihirisha aibu yake kwa atafutaye aibu zangu miongoni mwa majirani wangu na wenye husda ya neema zako kwangu. Hata hivyo hayakuniziwiya yote hayo nimepita kwenye maovu uliyoyajuwa kwangu. Hivyo basi ni nani mjinga zaidi wa mwongozo wake ewe Mola wangu kuliko mimi?

Nani mwenye kughafilika mno na hadhi yake kuliko mimi? Nani yu mbali sana na kuirekibisha nafsi yake kuliko mimi? Kwa kuwa naitumia riziki yako uliyoniruzuku katika mambo uliyonikataza miongoni mwa maasi yako. Nani aliyezama mbali sana katika mambo ya batili na mwenye kuyaendea maovu kuliko mimi? Nisimamapo kati ya wito wako na wito wa shetani huufuata wito wake bila kuwa niko kipofu katika kumjua wala sifanyi hivyo kwa kuwa kuna usahaulifu katika kumtambua. Hali yakuwa ninayakini kuwa mwisho wa wito wako ni peponi. Na mwisho wa wito wake ni motoni, utakatifu ni wako. Ajabu iliyoje juu ya ushahidi ni ubebao dhidi yangu mwenyewe. Na hesabu toka yaliyojificha katika mambo yangu? Ajabu kubwa kuliko hiyo ni ule upole wako kwangu na kwenda kwa utaratibu bila kuniharakishia. Hiyo si kwamba ninayo heshima kwako; bali ni uvumilivu wako kwangu, na ni fadhila zako juu yangu.Ili nijiepushe na maasi yako ya kukasirishayo, nipate mwanya wa kujing'oa toka maovu yangu yaniaibishayo. Kwa sababu kunisamehe wapendezwa sana kuliko kuniadhibu. Bali mimi ewe! Mola wangu ninadhambi nyingi sana na nyayo mbaya sana na matendo ya ovyo mno. Najitumbukiza vibaya sana katika batili. Niko dhaifu mno kuwa macho katika utii wako.

Ni mchache mno wakuzindukana na makamio yako na kuyachunga. Kwa kiasi cha kuweza kuzidhibiti aibu zangu. Au kuweza kuzikumbuka dhambi zangu kwa hayo nailaumu nafsi yangu tu nikiwa na tamaa ya huruma yako ambayo kwayo ndiyo kurekebika kwa mambo ya wenye dhambi. Na kutaraji rehma zako ambazo kwazo ndiyo ukombozi wa shingo za wakosaji. Oh! Mola hii ni shingo yangu imeshikwa utumwa na dhambi, msalie Muhammad na Aliy zake. Ikomboe kwa msamaha wako. Huu mgongo wangu umetopewa na makosa. Msalie Muhammad na Ali zake, uupunguzie uzito wake kwa huruma yako. Ewe Mola wangu lau ningekulilia mpaka zidondoke mbone za macho yangu na niliye mpaka ikatike sauti yangu. Na nisimame kwa ajili yako mpaka zifure nyayo zangu, na nirukuu kwa ajili yako mpaka ung'oke mgongo wangu, na nisujudu kwa ajili yako mpaka macho yangu yang'oke, na nile mchanga wa ardhini umri wangu wote, na ninywe maji yenye jivu mpaka mwisho wa umri wangu, na niwe na kutaja muda wote huo mpaka ulimi wangu uwe butu nisiinuwe uso wangu vyote hivyo nikikuonea haya isingewajibika kufutiwa ovu moja miongoni mwa maovu yangu. Ingawaje ulikuwa wanisamehe inapobidi nipate msamaha wako, na wanisamehe ninapostahiki msamaha wako. Kwani hilo haliwi wajibu kwa ajili yangu kwa kustahiqi wala silipati hilo kwa kuwa ni wajibu. Kwa kuwa malipo yangu toka kwako toka nilipokuasi kwa mara ya kwanza ilikuwa ni moto. Hivyo basi endapo utaniadhibu wewe sidhwalimu kwangu. Oh! Mola wangu kwa vile ulisitiri aibu yangu wala haukunifedhehi, ulinivumilia kwa ukarimu wako wala haukuniharakia. Ulinifanyia huruma kwa fadhila zako hukuibadilisha neema zako kwangu wala hukuyaboronga matendo yako mema kwangu. Hurumia unyenyekevu wangu wa muda mrefu. Na ukali wa umasikini wangu. Hali yangu mbaya. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Nilinde na maasi, nifanye niwe mtii, niruzuku kurejea kwako mara kwa mara, nisafishe kwa toba, nipe nguvu kwa kunilinda, nirekebishe kwa afya, nionjeshe utamu wa msamaha, nijaalie niwe niliye kombolewa kwa msamaha wako na niliyekombolewa utumwa kwa rehma zako, niandikie dhamana ya kutokasirikiwa nawe, nipe bishara ya haraka si ya baadaye bishara niitambuayo, itambulishe kwa alama nitaibainisha nayo. Hilo halikupi dhiki katika wasaa wako, wala halikusumbui katika nguvu zako, wala haliuzidi upole wako, wala haikuchokeshi katika hiba zako tukufu ambazo zimeonyeshwa na aya zako. Hakika wewe wafanya ulitakalo na wahukumu upendalo. Hakika wewe nimuweza wa kila kitu.

DUA YA 17

DU'A ZAKE(A.S) AMTAJAPO SHETANI HUJILINDA NAYE NA HUJILINDA NA UADUI WAKE NA VITIMBI VYAKE

Ewe Mola kwa hakika twajilinda kwako na mvuto wa shetani maluuni na vitimbi vyake na mitego yake. Na kuwa na matumaini ya ahadi zake.Udanganyifu wake na mawindo yake na asijipe tamaa nafsini mwake ya kutupoteza mbali na utii wako. Na kutotweza kwa sababu ya kukuasi tusije yaona kuwa ni mazuri aliyotufanya tuyaone mazuri. Na yasije onekana mazito kwetu aliyoyachukiza kwetu. Ewe Mola mtupe mbali nasi kwa njia ya ibada yako. Mtupe chini kwa upendo wetu wa kudumu kwako. Weka kati yetu na yeye kiziwizi asichoweza kukiondoa. Na kinga madhubuti hawezi ikiuka. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Mshughulishe awe mbali na sisi kwa baadhi ya maadui wako. Utulinde naye kwa uzuri wa uangalizi wako. Tufanye atusumbuliwi na khiyana yake, tugeuzie mgongo wake. Ukate kabisa ufuatilio wake kwetu. Ewe Mola msalie Muhammad na Ali zake. Tufurahishe kwa kutupa uongofu mfano wa upotovu wake. Tuzidishie uchamungu dhidi ya ushawishi wake. Tupitishe katika uchaji mungu kinyume na njia yake ya maangamio.

Ewe Mola usimjalie upenyo mioyoni mwetu. Usimfanyie makazi kwa yale tuliyonayo. Ewe Mola tutambulishe njia potovu atufanyiazo. Na tuitambuapo tulinde nayo tuonyeshe cha kumrubuni nacho. Tupe ilhamu ili kujiweka tayari naye tuamshe ili tutokane na sinzio la mghafala wa kumtegemea yeye. Ufanye uzuri msaada wako kwetu dhidi yake. Ewe Mola zinyweshe nyoyo zetu kuyakanusha matendo yake. Tufanyie upole kwa kutangua hila zake. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Yageuze mamlaka yake mbali nasi, kata matumaini yake kwetu, mziwie uchu wake kwetu, Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake.Wajaalie baba zetu, mama zetu, watoto wetu, ahli zetu, ndugu zetu wa karibu na majirani zetu miongoni mwa waumini wanaume na waumini wanawake katika ulinzi madhubuti dhidi yake. Na ngome yenye hifadhi na pango lenye kizuizi. Wavishe dhidi yake kinga iwalindayo, wape silaha dhidi yake silaha kali kali Ewe Mola waeneze hayo wenye kushuhudia kuwa wewe ndiyo Rabbu. Na akakutengea wewe umoja. Na amfanyiaye uadui (shetani) kwa ajili yako kwa hakika ya uja. Na akuomba msaada dhidi yake kwa maarifa ya elimu za kiungu.

Ewe Mola! fungua aliyoyafunga na rarua aliyoyashona. Haribu aliyoyapanga, mvunje moyo anapoazimia, yaharibu aliyoyafanya. Ewe Mola lishindishe jeshi lake, batilisha vitimbi vyake, bomoa pango lake, isuguwe pua yake chini ya ardhi. Ewe Mola! tuweke sisi katika ngazi ya maadui zake tutoe tusiwe katika idadi ya marafiki zake ili tusimtii anapotushawishi. Tusimwitikie atuitapo, tumpe amri mwenye kutii amri yetu amfanyie uadui, na tumuwaidhi ili asimfuate mwenye kufuata karipio letu. Ewe Mola! mrehemu Muhammad mwisho wa manabiy na bwana wa mitume na warehemu ahli bayt wake wema na wasafi. Na utulinde sisi na ahali zetu, ndugu zetu na jumla ya waumini wanaume na waumini wanawake, yale tuliyojilinda nayo. Na ututakase kwa yale tuliyokuomba ututakase nayo kwa hofu yake. Tusikilize tuliyokuomba na utupe tuliyoghafilika kuyaomba, ulinde na tuliyoyasahau. Kwa yote hayo tufanye tuwe katika daraja za watu wema na ngazi za waumini - Aameen ewe Mola wa ulimwengu wote.

DUA YA 18

LINDWA NA JAMBO ANALOLIHOFIA AU KUHARAKISHIWA AYATAKAYO

Oh! Mola sifa njema ni zako kwa uzuri wa utekelezaji wako. Kwa kuniondolea mitihani yako, usiijaalie hadhi yangu katika rehma zako ile ulioniharakishia katika afya yako nisije kuwa duni kwa niliyo nikiyapenda. Na mwingine awe na maisha mema kwa yale niliyoyachukia. Ikiwa hali njema niliyo nayo mchana wote au usiku wote kwa afya hii itafuatiwa na balaa isiyokoma na mzigo wa dhambi ambao usiotoweka.! Bora nitangulizie ambacho ungekichelewesha na nicheleweshee ambacho ungenitangulizia. Kwa kuwa ambacho mwisho wake ni kuteketea hakina wingi. Na ambacho matokeo yake ni kubakia hakina udogo. Msalie Muhammad na Aliy zake.

DUA YA 19

DU'A ZAKE(A.S) KUOMBA MAJI WAKATI WA UKAME

Oh! Mola tupe maji kwa kutuletea mvua. Tukunjulie rehma zako kwa mvua yako nyingi kutoka mawingu yasukumwayo kwenye mimea ya ardhi yako muwafaka kwa kuotesha katika zoni zote. Wahurumie waja wako kwa kuivisha matunda. Irudishie uhai nchi yako kwa kutungika maua. Wafanye malaika wako waheshimiwa waandishi kuwa mashahidi kwa mvua yenye manufaa toka kwako. Wingi wake uwe wa daima, mbubujiko wake uwe wa wasaa, mvua nyingi ya haraka, kwayo uirudishie uhai iliyonyauka, ukilete kwayo kinachokuja, kwayo ulete chakula nyingi, mawingu yenye kurundikana yenye kutosheleza, katika tabaka za mawingu yatoayo sauti mvua inyeshayo sio ile isiyo simama kuwe na umulikaji wenye matunda. Oh! Mola tupe mvua, yenye kusaidia, iletayo mazao yenye rutuba, yenye kuenea, nyingi, yakutosha inayotengeneza upya kilichovunjika. Oh! Mola tupe mvua, itakayofanya mawe ya mlimani yaporomoke itakayojaza visima, itakayoifanya mito itiririke, itakayootesha miti, itakayofanya bei za vitu irudi chini katika nchi zote, itakayo tia uzima wanyama na viumbe vingine, itakayotukamilishia chakula yakufaa, itakayotuoteshea mimea, itakayoongeza mtiririko wa maziwa katika chuchu za wanyama, itakayo tuongezea nguvu kwenye nguvu zetu. Ewe Mola usijaalie kivuli chake juu yetu kuwa upepo uunguzao, wala usiifanye baridi yake kwetu ya kukata, usiufanye mbubujiko wake kwetu kuwa ni pigo la mawe, wala usiyafanye maji yake kwetu kuwa ya chumvi. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Turuzuku miongoni mwa baraka za mbingu na ardhi. Hakika wewe u muweza wa kila kitu.