AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18385
Pakua: 2892

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18385 / Pakua: 2892
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

4

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 20

DU'A ZAKE KATIKA TABIA NJEMA NA VITENDO VYA KURIDHISHA

Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Ifanye iymani yangu ifikiye daraja kamilifu ya iymanni. Na ifanye yakini yangu iwe yakini bora. Na ifikishe nia yangu kwenye nia nzuri mno. Ewe Mola kwa huruma zako ikamilishe nia yangu. Ifanye yakini yangu iwe sahihi kwa yale uliyonayo. rekebisha kwa uwezo wako kilicho haribika kwangu. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Niepushe na hima inishughulishayo na kunirudisha nyuma. Nitumikishe katika ambayo utaniuliza kesho. Ziache siku zangu zitumike kwa yale tu ambayo kwa ajili yake uliniumba. Nitosheleze unipanulie riziki yako, usinipe mtihani wa kutokuwa na shukrani. Nipe enzi usinitihani kwa kunifanya niwe na kibri. Nifanye niwe nakuabudia wewe usiiharibu ibada yangu kwa kujisifu. Ipitishe mikononi mwangu kheri kwa watu usiifute kwa masimbulizi yangu kwao. Nipe tabia njema za hali ya juu kabisa. Nilinde na kujifaharisha. Ewe Mola wangu mrehemu Muhammad na Aliy zake. Wala usinipandishe daraja kwa watu ila uwe umeniteremshia nafsini mwangu mfano wake, usinifanyie utukufu wa wazi isipokuwa uwe umenifanyia udhalili wa ndani ya nafsi yangu kwa kadiri ile ile. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Na unistareheshe kwa mwongozo mwema ambao sitoubadilisha. Na njia ya haki ambayo sitopotoka na nia ongofu ambayo sitokuwa na mashaka nayo. Nipe maisha ikiwa maisha yangu yatakuwa zawadi ya bure kukutii wewe. Na endapo maisha yangu yatakuwa malisho mema ya shetani nichukuwa kwako kabla haijatangulia chuki yako kwangu au kabla haijachukuwa nafasi ghadhabu zako juu yangu. Ewe Mola usiiache sifa ambayo kwayo nitaaibishwa isipokuwa utakuwa umeirekebisha. Au aibu nalaumiwa kwayo ila itakuwa umeirekebisha. Wala daraja bora linakasoro uwe umelikamilisha.

Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nibadilishie bughudha ya watu wenye chuki kwa upendo. Na nibadilishie husda ya mafedhuli iwe mapenzi, na dhana ya watu wema iwe uaminifu, na uadui wa makaraba uwe urafiki, na kutojaliwa na watu wa tumbo moja kuwe wema, na kutupiliwa mbali na ndugu wa karibu kuwa ni msaada, na upendo wa wabembe uwe upendo uliorekebika upendo sahihi, na kukataliwa na wenzi kuwe heshima na urafiki. Uchungu wa kuwaogopa wadhalimu uwe utamu wa uaminifu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Unijaalie niwe na mkono wa juu dhidi ya wanaonidhulumu, na ulimi wa juu dhidi ya wanaonigomba, ushindi kwa anayemng'ang'ania kunikaidi. Nipe mbinu dhidi ya anayenifanyia vitimbi, na uwezo dhidi ya anayenikandamiza na kumkanusha anayenikebehhi, nipe usalama kwa anayenikamia, nipe taufiki ya kumtii anayeniweka sawa. Kumfuata anayeniongoza. Ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake. Niweke sawa ili nimpinge anayenighushi kwa nasaha, mlipe anayejitenga na mimi kwa wema umlipe mwenye kuninyima kwa kutoa bure, umlipe mwenye kujitenga na mimi kwa mawasiliano, nimpinge mwenye kunisengenya kwa kunitaja vyema, na niwezeshe kushukuru yaliyomema na kuyafumbia macho maovu, ewe Mola mrehemu Muhammad na Ali zake, nipambe kwa mapambo ya watu wema nivishe pambo la wachamungu kwa kueneza uadilifu. Kujizuiya na ghadhabu, kuuzima moto wa chuki, kuwaleta pamoja watu waliotawanyika, kusuluhisha mizozo ya wasiopatana, kueneza mema, kusitiri aibu, kuwa na tabia ya upole, kushusha bawa chini, mwendo mwema, uvumilivu, uzuri wa mwenendo, na kuharakia maadili, kuchagua fadhila, kuacha kuaibisha, kumfadhili asiyestahiki, kusema yaliyo haki japo ni machungu, kuudogesha wema japo uwe mwingi, kwa kauli yangu au kwa kitendo changu, nakuikithirisha shari japo iwe ndogo kwa kauli yangu au kitendo changu. Nikamilishie hayo mimi kwa kudumisha utii, na kujiambatanisha na jamaa na kuwakataa wazushi na watumiao rai zao za kubuni. Ewe Mola mrehemu Muhammad na aliy zake. Na jaalia riziki yangu iwe riziki ya wasaa mno kwangu endapo nitakuwa mtu mzima. Na mwenye nguvu sana katika nguvu zako nitakapoishiwa nguvu. Usinipe mtihani wakuwa mvivu katika ibada yako. Wala kuwa kipofu wakutoiona njia yako, wala kujihusisha na linalopingana na mapenzi yako, wala kujiunga na ambaye amejitenga na wewe, wala kujitenga na aliyejiambatanisha na wewe.

Ewe Mola nifanye niwe narukia kwako wakati wa dharura. Nakuomba wakati wa haja, nanyenyekea kwako wakati wa shida, usinipe mtihani wa kuomba msaada kwa mwingine mbali na wewe nikiwa nimedharurika wala kunyenyekea kwa ombi kwa mwingine mbali na wewe niwapo fakiri, wala kunyenyekea kwa ambaye ni chini yako nikiwa na woga. Kwa kufanya hivyo nitastahiki kutupiliwa mbali na wewe na kukabiliwa na zuio lako na kutumbiwa mgongo na wewe. Ewe mwingi mno wa kurehemu kuliko wanaorehemu wote. Ewe Mola fanya anachonitupia shetani moyoni miongoni mwa tamaa, dhana, na husda iwe ni kumbusho la utukufu wako kuitafakari nguvu yako, na iwe ni onyo dhidi ya adui wako. Nayafanye ayapitishayo ulimini mwangu miongoni mwa tamko baya au kebbehi au ushahidi batili, au kumsengenye muumini asiyekuwapo au kumtusi aliyopo na yaliyomfano wa hayo iwe ni tamko la kukuhimidi wewe. Na kuzama katika kukusifu wewe na juhudi katika kukuenzi wewe na shukrani kwa ajili ya neema zako. Nakutambua ihisani yako, na kuhesabu huruma yako. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nisidhulumiwe hali wewe ni muweza wakunilinda, wala nisidhulumu nawe waweza kunizuia, usiache nipotee hali waweza kuniongoza, usinniache niwe masikini na hali kwako kuna yakunitosheleza. Nisivuke mipaka haki kwako ndio utajiri wangu. Ewe Mola, nimekuja kwenye msamaha wako, naelekea msamaha wako. Ninashauku na kufumbiwa macho kwako ninaithibati na fadhila zako, sina kinachoweza kuwajibisha msamaha wako kwangu, wala katika kazi yangu hakuna ninachoweza kustahiki msamaha wako, sina chochote baada ya kujihukumia mwenyewe dhidi ya nafsi yangu kinifaacho ila fadhila zako, mrehemu Muhammad na Ali zake, nipe fadhila zako. Ewe Mola, nitamkishe uongofu, nipe mwongozo wa uchamungu, niwafikishe fanaka katika ambacho ni safi mno, nitumikishe kwa ambalo lakuridhiwa ewe Mola nipitishe njia ya mfano bora. Yafanye maisha yangu katika mila yako kufa na kupona. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nifanye wakufurahiya iktiswadi (yaani uwekevu), nifanye niwe miongonni mwa watu wa sawa miongoni mwa waongofu, miongoni mwa waja wema, niruzuku kuwa mwenye kufaulu marejeo na usalama wa mawindo.

Ewe Mola, chukuwa kwa ajili yako kutoka nafsini mwangu kitachoitakasa, nabakisha kwa ajili ya nafsi yangu kutoka nafsi yangu kitakachoifanya iwe njema kwa kuwa nafsi yangu ni yenye kuangamia isipokuwa ukiilinda. Ewe Mola, wewe ndio kifao changu ni huzunikapo wewe ndio kimbilio langu ninyimwapo kwako ndio mahali pa kuomba msaada nikiwa katika taabu. Na kwako kuna badali ya yaliyopotea na marekebisho kwa kilichoharibika. Na mabadiliko kwa ulichokikaa, nihurumie kwa kunipa afya kabla ya balaa. Na mali kabla ya kuomba, na kabla ya kupotea uongofu, nitosheleze nisipatwe na mzigo wa aibu kwa waja, unipe amani siku ya marejeo, nipe mwongozo mwema, ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nilinde kwa rehma yako, nilishe kwa neema zako, nisawazishe kwa ukarimu wako, nitibu kwa wema wako, nifunike kwa kivuli chako, nienezee ridhaa zako.

Niwafikishe ili nifikie jambo lenye mwongozo mno endapo mambo yatachanganyika mbele yangu, nifikie kwenye kazi iliyo safi mno endapo kazi zitashabihiyana, nifikie kwenye itikadi iridhiwayo endapo itikadi zitapingana, ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake, nivishe taji la kuridhika. Nipe malezi mema, nipe mwongozo sahihi, usinipe mtihani kwa kuwa na nafasi, unipe maisha mema, usiyafanye maisha yangu kuwa ya taabu na shida, usiirudishe DU'A yangu kwangu kwa kuikataa. Kwa hakika mimi sikufanyii yeyote kuwa dhidi yako, wala simwombi yeyote pamoja na wewe nikimfanya kuwa yu sawa na wewe, ewe Mola msalie Muhammad na Aliy wake. Niziwie ili nisiwe mfujaji, ilinde riziki yangu na uharibifu, zidisha mali zangu kwa kuzibariki, niwafikishe njia ya mwongozo kwa wema wa niyatumiayo, ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Niepushe na mzigo wa kuchuma, na unipe bila ya hesabu, kutafuta kusiniziwie kufanya ibada yako, nisibebe mzigo wa matokeo mabaya ya uchumaji. Ewe Mola nipe niyatafutayo kwa uwezo wako, nipe kimbilio safi kwa nguvu zako kwa nihofiayo, ewe Mola msalie Muhammad na Aliy zake uhifadhi uso wangu kwa kuwa na nafasi bora ya maisha, usiidhalilishe heshima yangu kwa ufakiri ili nisije waomba riziki uliowaruzuku au niwaombe kipawa watu washari katika viumbe wako. Kwa hiyo nitakuwa katika fitna ya kumsifu atakaye nipa na kuingia katika balaa la kumlaumu atakaye nikatalia.

Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aliy zake. Na wewe siwawo ndio Bwana wa utoaji na uzuiaji. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Alali zake. Na unipe siha katika ibada, nijihusishe na zuhud, na elimu katika matendo, na kujiepusha katika kipimo. Ewe Mola hitimisha muda wangu kwa msamaha wako. Nayathibitishie matarajio ya Rehma zako matazamio yangu. Wepesisha njia zangu kufikia Ridhaa zako. Amali zifanye nzuri katika hali zote. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Nizinduwe kukukumbuka nyakati za mghafala. Nitumikishe katika utii wako siku za Raha. Nifanyie njia nyeupe na rahisi kuelekea mapenzi yako. Nikamilishie kwayo kheri ya dunia na Akhera. E Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Kwa ubora ule uliomrehemu yeyote katika viumbe vyako kabla yake. Na ule ambao utamrehemu yeyote baada yake. Tupe mema hapa duniani na mema akhera. Na unilinde kwa rehema zako na adhabu za mto

DUA YA 21

NA ALIKUWA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) AKIHUZUNISHWA NA JAMBO NA YA MUOGOPESHAPO MAKOSA

Ewe Mola! Ewe mwenye kumtosheleza mpweka dhaifu. Mlinzi wa jambo lihofiwalo. Makosa yamenitenga wala sina mwenzi nimekuwa dhaifu kwa ghadhabu zako hakuna wakunipa nguvu. Nimeikaribia hofu ya kukutana na wewe hakuna wakuituliza hofu yangu nani anipe amani kwako na wewe ndiye umeniogopesha? Hatowi kimbilio Ewe! Mola wangu ila Bwana mlezi kwa awaleao hatowi amani ila mshindi kwa mshindwa. Hakuna asaidiaye juu ya chenye kuombwa ila ni mwombaji. Na mkononi mwako Ewe! Mola wangu kuna sababu zote hizo. Kwako ndio kwa kukimbilia na ndio kimbilio msaliye Muhammad na Aali zake. Na nipe kimbilio kwa ajili ya kimbilio langu fanikisha ombi langu. Ewe Mola hakika wewe ukinigeuzia uso wako mtukufu mbali nami au ukiniziwiya fadhila zako kubwa, au kunikataza riziki yako. Au ukikata mbali namimi sababu yako sitoipata njia kufikia chochote katika matumaini yangu bila ya wewe. Wala sitoweza kuyapata yaliyo kwako kwa msaada wa mwingine. Mimi ni mja wako niko mashikoni mwako. Nyele zangu za mbele zi mikononi mwako. Sina amri pamoja na amri yako hukumu yako yatekelezeka kwangu. Maamuzi yako kwangu ni ya kiadilifu. Sina uwezo wakutoka nje ya mamlaka yako. Wala siwezi kuzikurubia nguvu zako wala siwezi kuelemeza upendo wako. si ufikii upendo wako. wala sitoyapata yaliyokwako isipokuwa kwa utii wako nakwa fadhila za rehema zako Oh! Mungu wangu! muda wote niko mjawako wa ngazi ya chini kabisa. Si miliki manufaa kwa ajili ya nafsi yangu wala madhara isipokuwa kwa njia yako.

Nashuhudia hilo mwenyewe binafsi. Natambua udhaifu wa nguvu zangu na uhaba wa mbinu zangu: Hivyo basi nipe ulilo niahadi. Nitimizie ulilonipa Mimi ni mja wako Masikini, mnyonge Dhaifu mwenye dhiki Dhalili, mwenye kudharauliwa, mnyonge fakiri. Aliyeshikwa na woga aombaye hifadhi, Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Ala mwenye kughafilika ihsani yako uliponipa mtihani. Wala kukata tamaa na jibu lako japo lije polepole sana kwangu. Sawa niwe katika neema au katika taabu. Shida au raha. Katika hali njema au katika balaa. Katika maafa au katika raha. Katika utajiri au hangaiko. Ufakiri au utajiri. Ewe Mola mrehemu Muhammadi na Aali zake. Na jaaliya kukusifu kwangu kwa sifa njema, kukuhimidi, na kukutukuza kuwe katika hali zangu zote. Ili niwe sifurahii ulionipa katika dunia. Wala nisihuzunikie ulionizuia humo. Upe moyo wangu kukuogopa wewe utumikishe mwili wangu kwa lile unalolikubali kutoka kwangu. Ishughulishe nafsi yangu katika utii wako kwa kila liingialo kwangu kiasi chakuwa nisikipende chochote kinachokukasirisha.

Wala nisichukie chochote kikufurahishacho. Ewe Mola msalie Muhammad na Aali zake. Ufanye moyo wangu uwe tupu ila kukupenda wewe. Na ushughulishe kukukumbuka wewe. Uhuishe kukuogopa na utishike na wewe upe nguvu kukusihi wewe. Uelemeze kwenye utii wako. Upitishe katika njia zipendwazo sana na wewe. Udhalilishe kupenda ulichonacho siku zote za uhai wangu. Kukuogopa wewe Duniani iwe ndio masurufu yangu. Safari yangu iwe kuielekea Rehma za kuingia kwangu kuwe katika maridhawa yako. Jaalia makazi yangu yawe katika jannah yako. Nipe nguvu za kubeba kila kitu ukipendacho. Jaalia kukimbia kwangu iwe kuja kwako na kupenda kwangu kile kilichokuwa kwako. Uvishe moyo wngu kuwaona watenda shari katika viumbe wako kuwa si wako kawaida. Nipe urafiki na wewe na marafiki zako na watu wako watii. Wala usimjaalie muwovu wala kafiri fadhila juu yangu, wala asiwe na mkono kwangu, wala ni siwee na haja kwake. Lakini jaalia utulivu wa moyo wangu, Raha ya nafsi yangu, kujitegemea, kwangu na kujitosheleza kwangu kwako. Na kwa viumbe wako wazuri mno. Ewe! Mola mrehemu Muhammad na Aali zake nifanye niwe rafiki kwao. Nifanye niwe msaidizi kwao. Nitunukie niwe na shauku ya upendo wako na kufanya mema kwa ajili yako yale uyapendayo na wayaridhiya. Hakika wewe ni muweza wa kila kitu. Na hayo kwako ni mepesi.

DUA YA 22

DU'A ZAKE(A.S) KATIKA SHIDANA JUHUDI NA MAMBO YANAPOKUWA MAGUMU

Oh! Allah Hakika umeniagiza jambo lihusulo nafsi yangu ambalo wewe wahusika nalo zaidi kuliko mimi. Uwezo wako juu yake na juu yangu ni mkubwa mno kuliko uwezo wangu. Hivyo basi nipe mimi ndani ya nafsi yangu linalokuridhisha kutoka kwangu na chukuwa kwa ajili ya nafsi yako ridhaa zake toka nafsini mwangu, katika hali ya afya njema. O Allah! Sina ustahimilivu katika juhudi wala sina subira katika balaa, sina nguvu za kuubeba mzigo wa ufakiri hivyo usikataze Riziki yangu, wala usiniwakilishe kwa viumbe wako ishughulikie haja yangu peke yako. Shikilia mwenyewe kunitosheleza. Niangalie nichunge, katika mambo yangu yote kwa kuwa wewe ukiwakilisha kwangu mwenyewe nitakuwa nimehemewa na sitofanya lenye maslahi. Kwa nafsi yangu. Endapo utaniwakilisha kwa viumbe wako watanikunjia uso, Ukinifanya nikimbilie kwa ndugu zangu wa karibu wataninyima. Na kama watanipa watanipa kidogo shingo pembeni. Na watanisimbulia saana mda mrefu na huku wakinilaumu sana. Hivyo basi kwa fadhila zako O Allah! Nitosheleze. Na utukufu wako ni nyanyuwe, kwa wasaa wako ikunjuwe mikono yangu. Nitosheleze kwa yaliyo kwako. O Allah! Msalie Muhammad na Aali Zake. Na uniweke mbali na husda nitenge mbali na dhambi nifanye niogope kutenda haram. Nisithubutu kutenda maasi. Fanya upendo wangu kwako na Ridhaa yangu iwe kwenye kinifikiacho kutoka kwako. Kibariki kwa ajili yangu, ulichoniruzuku. Na ulichonijaalia. Na ulichonineemesha.

Nijaaliye katika hali zangu zote mwenye kuhifadhiwa mwenye kulindwa. Mwenye kusitiriwa mwenye kuzuiliwa. Mwenye kukingwa kupewa kimbilio. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Nifanye nitekeleze yote ulionilazimisha na uliyoyafaradhisha juu yangu kukuelekea wewe. Katika namna moja miongoni mwa aina zako za kukutii. Au kwa ajili ya kiumbe miongoni mwa viumbe wako. Japo mwili wangu uwe dhaifu kwa hilo na kudhoofu kwa hilo nguvu zangu. Uwezo wangu ukashindwa kulifikia hilo na mali yangu yakawa kidogo na hata kilichomkononi mwangu. Sawa niwe nakumbuka au nasahau. Mola wangu ni miongoni mwa uliyo yadhibiti hisabu yake dhidi yangu. Wakati mimi binafsi nimeghafilika. Ni jaaliye kutekeleza kwa wingi wa utoaji wako na kwa ukubwa wa ulichonacho. Kwa kuwa wewe unawasaa mno na ni mkarimu. Ili kwangu kisibakie kitu ambacho wataka kunifuatilia hesabu yake miongoni mwa maovu yangu siku nitakutana na wewe o Mola wangu! Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Niruzuku upendo wa kutenda mema kwa ajili yako ili itengenee kheri yangu. Nijuwe ukweli wa hilo moyoni mwangu. Na kujinyima starehe ya dunia kuwe ndio mshindi. Nitende mazuri kwa shauku kabisa niwe katika usalama wakutotenda matendo maovu kwa kitisho na woga.

Nipe mwanga uniwezeshao kutembea kati ya watu. Utakao niwezesha kupata mwongozo gizani. Ning'arishe kwa mwanga huo shaka na mambo yanapokuwa si dhahiri. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na uniruzuku kuogopa mayonzi ya kitisho. Na niruzuku kuwa na shauku ya thawabu iliyoahidiwa kiasi kwamba ni ipate ladha ya yale nikuombayo. Na niyapate majonzi ya kile nikiombeacho kimbilio kwako. Oh Allah! Wajua fika kitakachoweka sawa mambo ya dunia yangu na Akhera yangu. Hivyo basi kuwa na upendeleo kwenye mahitaji yangu. Oh Allah! mrehemu Muhammad na Aali Zake. Uniruzuku haki ninaposhindwa kukushukuru ipasavyo kwa ajili ya Neema zako ulizonineemesha. Nikiwa katika nafasi nzuri na katika matatizo. Katika siha njema na katika ugonjwa kiasi kwamba niwe natambua mwenyewe. Faraja ya maridhawa na utulivu wa nafsi kwa yaliyo wajibu kwako ambayo yazukayo katika hali ya hofu na amani. Hali ya ridhaa na ya makasiriko ya madhara na manufaa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake.

Na uniruzuku usalama wa kifua kuepukana na husuda. Ili nisimhusudu yeyote katika ujumbe wako juu ya kitu chochote miongoni mwa fadhila zako. Kiasi kwamba nisione neema katika neema zako kwa yeyote miongoni mwa viumbe wako kwa yeyote miongoni mwa viumbe wako sawa iwe katika dini au dunia katika hali njema ya maisha au uchamungu. Sawa iwe wasaa au Raha. Isipokuwa niwe natarajia kwa ajili ya nafsi yangu yaliyo bora ya hayo kwako kutoka kwako peke yako huna mshirika. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na uniruzuku kujilinda na makosa na niogope kuteleza hapa duniani na Akhera. Katika hali ya ridhaa na ghadhabu kwa kiasi isiwe sawa kwangu liingialo kati ya hayo mawili. Nitende utii wako nichaguwe ridhaa zako na kuacha yasiyokuwa hayo mawili. Kwa marafiki na maadui. Ili hata aduwi wangu awe katika amani mbali na dhulma yangu na maovu yangu. Na akate tamaa rafiki yangu na elemeo langu na kupinda kwenye matamanio yangu. Na ni jaalie niwe miongoni mwa wakuombao kwa unyofu katika raha ombi la wakuombao katika hali ya unyofu wamedharurika kukuomba. Hakika wewe wastahiki sifa njema u mtukufu.

DUA YA 23

NA MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) AMWOMBAPO MUNGU HALI NJEMA NA ANAPOISHUKURU

Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Nivishe afya yako. Niviringishe afya yako. Niweke kwenye ngome ya afya yako. Nipe heshma kwa afya yako. Nitosheleze kwa afya yako.Nipe sadaka kwa afya yako. Nitunukiye afya yako Nitandikiye afya yako. Niwekee sawa afya yako. Usinitenge mbali na afya yako. Duniani na Akhera. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake nipe afya. Afya ya kutosha iponyeshayo, ya hali ya juu ikuayo. Afya izalishayo mwilini mwangu afya njema. Afya njema duniani na akhera. Nifanye niwajibike kwa siha na amani. Na usalama katika Dini yangu na Mungu wangu. Na ufahamu moyoni mwangu. Na uwezo wa kuyapitisha mambo yangu na kukuogopa wewe. Na kukuhofia wewe. Niwe na nguvu juu ya uliyoniamrisha katika kukutii. Na kujiepusha na uliyo nikataza miongoni mwa maasi yako. Oh Allah! Nifadhili kwa kufanya hija na umra na kuzuru kaburi la Mtume wako, Rehema zako na baraka zako zimfikie na ziwafikiye watu wa nyumba ya Mtume wako. Milele pindi unibakishapo katika mwaka wangu huu na katika kila mwaka. Naijaalie iwe yenye kukubaliwa yenye kushukuriwa. Yenye kutajwa mbele yako. Yenye kuhifadhiwa kwako. Utamkishe ulimi wangu shukrani yako, kukukumbuka wewe na kukusifu kwa sifa njema. Ukunjuwe moyo wangu kwa mwongozo wa dini yako. Na unipe mimi na kizazi changu ulinzi dhidi ya shetani aliyelaaniwa. Na shari ya chuki na uharibifu na jicho baya. Na shari ya kila shetani muasi. Na shari ya kila mtawala mkaidi Na shari ya kila mkwasi mtumikiwa. Na shari ya kila dhaifu na mwenye nguvu.

Na shari ya kila mdogo na mkubwa, na shari ya kila wakaribu na wa mbali na shari ya kila mwenye kufanya uaduwi kwa Mtume wako na watu wanyumbani mwake miongoni mwa jini au mtu. Na shari ya kila kiumbe kitambaacho ambacho wewe umezishika nyele zake mbele ya kichwa. Hakika wewe uko juu ya njia ilinyooka. Oh Allah! Mrehemu Muammad na Aali zake. Endapo yeyote atanitakia uovu niondolee naye mbali. Niondolee mbali vitimbi vitmbi vyake. Ikinge mbali na mimi shari na virudishe vitimbi vyake kooni kwake.

Na weka mbele yake boma ili ufanye macho yake yasinione na umfanye Asisikiye utajo wangu uufunge moyo wake usihihisi. Uzimishe ulimi wake dhidi yangu kiziwiye kichwa chake. Utweze utukufu wake. ivunje jeuri yake. Idhalilishe shingo yake. Haribu kibri chake, niweke katika amani na madhara yake yote na shari yake. Na masingizio yake, masengenyo yake na uchokozi wake. Husuda yake na uaduwi wake. Mtego wake na mawindo yake. Waenda kwa miguu wake na wapanda farasi wake. Hakika wewe muweza na mwenye nguvu.

DUA YA 24

DU'A ZAKE(A.S) KWA AJILI YA WAZEE WAKE(A.S)

Oh Allah! Mrehemu Muhammad mja wako na mjumbe wako na warehemu Ahlul-Bayt wake watakatifu. Na uwahusishe kwa ajili yao peke yao kwa fadhila zako na rehema zako na baraka zako na amani yako. Wahusishe Oh Allah! wazazi wangu wawili kwa heshima mbele yako na Rehema kutoka kwako. Oh! We mwenye kurehemu sana miongoni mwa wanaorehemu Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na unifundishe kwa hamu elimu ya mambo ambayo ni wajibu wangu kwao. Na unikusanyie Elimu ya yote hayo kikamilifu. Kisha nitumikishe kwa yale unifundishayo kwa Il-ham. Niwafikishe kutekeleza elimu uliyonipa ili yasinipite matumizi ya kitu ulichonifundisha. Wala viungo vyangu visiwe vizito kutekeleza uliyonifundisha kwa njia ya Il-hamu. Oh Allah! Mrenemu Muhammad na Aali zake.

Kama ulivyotupa heshima kupitia kwake. Na mrehemu Muhammada na Aali zake kama ulivyowajibisha juu yetu haki juu ya viumbe kwa sababu yake. Oh Allah! Nifanye natishika nao (wazazi wawili) kitisho cha mtu mbele ya mtawala mshari nifanye niwe mwema kwao kama wema wa mama mwenye huruma. Na ufanye utii wangu na wema wangu kwao kuwa ni kitulizo cha macho yangu sana kuliko usingizi wa mwenye usingizi mzito. Na yawe baridi mno kwenye kifua changu kuliko kinywaji cha mwenye kiu kali. Ili niliweke walipendalo mbele kuliko nilipendelealo.Na niitangulize ridhaa yao mbele ya ridhaa yangu. Na niuone wema wao kwangu kuwa ni mkubwa japo uwe kidogo. Na niuone wema wangu kwao ni mdogo sana japo uwe mwingi. Oh Allah! Irudishe sauti yangu chini mbele yao. Yafanye maneno yangu kwao kuwa maneno yanayokubalika. Ifanye tabia yangu kuwa ya upole mbele yao. Ufanye moyo wangu laini kwao nifanye niwe mwenzi mwama, mwenye kuwahurumia.

Oh Allah! Washukuru kwa malezi yangu na walipe mema kwa kunipa mimi heshima. Na wahifadhi kama walivyokuwa wananihifadhi nilipokuwa mdogo. Oh Allah! Na kwa aina yoyote ya maudhi yaliwagusa kutoka kwangu na mambo yachukizayo yaliwafika kutoka kwangu. Au haki yao iliopuuzwa na mimi basi fanya iwe ni sababu ya kupunguza dhambi zao. Na kupanda kwao daraja yao. Na kuzidi kwa mema mengi sana. Oh Allah! Neno lolote liwalo walilonikosea au hawakuwa waadilifu kwangu katika tendo waliipoteza haki yangu. Au walizembea kutekeleza wajibu wao kwangu. Nawazawadia na kuwapa wao kama tulizo nakusihi kuwaondolea malipizi dhidi yao kwani mimi siwashitaki kwa ajili yangu. Wala siwaoni kuwa wamefanya goi goi katika kunitendea wema. Wala si chukii jinsi walivyo yapeleka mambo yangu. Ewe Mola wao wanahaki juu yangu zaidi hisani yao ndiyo ya kwanza zaidi kunifikia. Huruma yao ni kubwa mno kwangu kuliko niwezavyo kuwa fuaatilia kwa uadilifu. Au niwalipe kulingana nao. Uwapi basi Ewe Mola wangu urefu wa shughuli yao kunilea? Iwapi basi taabu kubwa ya kunilinda kwao mimi?

Kuwapi kujinyima kwao wenyewe ili wanipe mimi kwa wingi baada yao? Haiwezekani! Hawawezi kupata haki yao kamili kutoka kwangu. Wala siwezi kutekeleza yaliyowajibu juu yangu kwao. Wala siwezi kukamilisha wajibu wangu kwao kuwahudumiya. Hivyo basi mrehemu Muhammad na Aali zake. Na nisaidie Ewe mbora wa waombwa msaada. Na nifanikishe Ewe mbora wa waombwao mwongozo wake. Usinifanye niwe miongoni mwa wasio wathamini baba zao na mama zao (siku ambayo kila nafsi italipwa ilichochuma nao hawatodhulumiwa). Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake na dhuria zake. Uwatengee wazazi wangu wawili fadhila makhsusi uliyowatengea wazazi wa waja wako waumini na mama zao. Ewe Mwingi wa Kurehemu! Oh Allah! Usinisahaulishe kuwa kumbuka. Baada ya sala zangu. Nawakati wowote ule katika nyakati za usiku. Na katika kila saa miongoni mwa saa za mchana wangu. Oh Allah! Msaliye Muhammad na Aali zake. Ni ghofiriye kwa sababu ya DU'A yangu kwao. Na waghofiriye wao kwa wema wao kwangu ghofira ya sawa sana. Waridhiye kwa maombezi yangu kwa ajili yao ridhaa za yakini kabisa. Kwa ukarimu wako wafikishe makazi ya salama. Oh Allah! Na endapo ghofira zako zimetangulia kuwafika basi zifanye ziwe mwombezi wangu na ikiwa ghofira zako zimenifikia mwanzo. Nifanye niwe mwombezi wao. Ili tuweze kukutana pamoja kwa huruma zako. Katika nyumba ya heshima yako na mahali pa msamaha wako na rehema zako. Kwa hakika wewe ni mwenye fadhila nyingi na huruma ya kale. Na wewe ni mwenye Rehema sana kuliko wenye kurehemu wote

5

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 25

DU'A ZAKE(A.S) KWA AJILI YA WATOTO WAKE(A.S)

Oh Allah! Nihurumie kwa kubaki watoto wangu, na kuwa kwao wema kwangu, na kwa kufurahikiwa nao kwangu, Mola wangu. Refusha umri wako kwa ajili yangu wazidishie muda wao kwa ajili yangu mlee kwa ajili yangu mdogo miongoni mwako. Mpe nguvu aliyedhaifu miongoni mwao vipe siha kwa ajili yangu viwili wili vyao, miili yao na dini yao natabia zao. Wape afya nafsini mwao, viungo vya miili yao na kwa kila chenye umuhimu kwangu katika mambo yao. Nitiririshie juu ya mikono yangu riziki zao. Na wafanye wawe wema, wacha mungu watambuzi. Wasikivu watii kwao na kwa mawalii wako wana wapenda na kufuata ushauri wao. Na kwa maaduwi zako wote wana wapinga vikali ameen.

Oh Allah! Ipe nguvu mikono yangu kupitia wao kupitia wao unyoshe mgongo wangu uliotopewa. Iongeze Idadi yangu. Kupitia wao yapambe maudhurio yangu. Kupitia wao huisha utajo wangu. Kupitia wao nitosheleze nikiwa sipo. Kupitia wao nisaidiye Haja zangu. Wafanye wanipende wanielekee wanyofu watii kwangu. Wasiwe waasi wala watovu wa heshima wasiwe wafanyao kinyume wala wakosaji. Nisaidiye malezi yao kuwa adabisha na kuwafanya wawe wema. Unipe mimi pamoja na wao kutoka kwa watoto wa kiume. Hivyo ni kheri kwangu uwajaalie wawe msaada kwangu juu ya niliyokuomba. Nilinde mimi na kizazi changu na shetani mlaaniwa. Kwa kuwa wewe umetuumba, umetuamuru na umetukataza. Na umetupendezesha malipo kwa uliyotuamuru, na kutuogopesha adhabu yake. Umetufanyia aduwi anatushauri vibaya umemuwezesha kwetu juu ya ambayo hukutuwezesha sisi juu yake. Umemuwezesha kuketi vifuwani mwetu na kumpitisha ndani ya mishipa yetu ya damu. Haghafiliki tughafilikapo. Hasahau tunaposahau! Anatufanya tuone tuko salama na adhabu yako. Na yu atuogopesha na mwingine asiyekuwa wewe. Tukusudiapo kutenda yasiyofaa anatushajiisha. Na tukusudiapo kufanya tendo jema atuvunja moyo. Anatupinga kwa vishawishi. Hutuwekea mashaka. Akitupa ahadi hudanganya akitupa matumaini atatufanyia kinyume chake. Kama hautotuondolea vitimbi vyake atatupoteza. Kama hautotulinda na maovu yake atatutekelezesha.

Oh Allah! Ushinde uwezo wake kwetu kwa uwezo wako. Ili umzuiye mbali nasi kwa wingi wa DU'A zetu kwako. Mpaka tuwe miongoni mwa waliohifadhiwa na wewe mbali na vitimbi vyake. Oh Allah! Nipe mimi niliyoyaomba yote. Na kidhi haja zangu. Usiniziwiye itikio hali ulikwishachukuwa dhamana yake kwa ajili yangu usiizibe duwa yangu kwako hali uliniamuru nikuombe. Kuwa mwema kwangu kwa kila kitakachoniweka sawa katika dunia yangu na akhera yangu. Nikumbukacho na ni nachosahau. Ninachodhihirisha na ninachokificha. Nilichokitangaza au kukifanya siri nifanye kwa yote hayo kwa maombi yangu kwako kuwa miongoni mwa watu wema. Walio fanikiwa kwa kukuomba wewe wasio zuiliwa kwa kutegemea juu yako waliokingwa kwa kuomba kinga kwako waliopata faida kwa kufanya biashara na wewe. Waliopewa kimbilio kwa enzi yako. Waliopewa riziki nyingi ya halali kwa fadhila zako zenye wasaa na upaji, na ukarimu. Walioepushwa na dhulma kwa uadilifu wako. Waliowekwa mbali na balaa kwa rehma zako. Waliotajirishwa baada ya ufakiri kwa utajiri wako. Waliohifadhiwa mbali na dhambi kuteleza, na makosa kwa kukuogopa wewe. Waliofanikishwa kwa mema, mwongozo, na umakini kwa kukutii wewe. Waliokingwa kati yao na dhambi kwa uwezo wako. Walioacha maasi yako yote. Wakazi jirani na wewe. Oh Allah! Tupe yote hayo kwa kufanikishwa na wewe na kwa huruma yako. Tuepushe na adhabu ya moto. Uwape Waislamu wote wanaume na Waislamu wanawake wote.

Waumini wanaume na waumini wanawake. Kama yale niliyokuomba kwa ajili ya nafsi yangu na kwa watoto wangu. Kwa haraka ya hapa duniani na baadaye akhera. Hakika wewe ukaribu na mwenye uwezo wa kujibu. Msikilizaji mjuzi. Mwenye kughofiria mwenye kusamehe mpole mwenye huruma. Na tupe sisi mema duniani na mema akhera na tulinde na adhabu ya moto.

Dua ya 26

DU'A ZAKE(A.S) KWA AJILI YA MAJIRANI ZAKE NA MARAFIKI ZAKE AWATAJAPO

Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Nitumikishe kwa majirani zangu na marafiki zangu waitambuayo haki yetu na wapiganao na maaduwi zetu kwa utumishi ulio bora. Wafanikieshe. Kutekeleza sunnah 'yako. Nakuchukuwa adabu zako nzuri. Katika kuwatendea kwa upole wanyonge wao. Na kurekibisha dosari yao. Kuwatembelea wagonjwa wao. Kumwongoza atakayemwongozo. Kumpa nasaha mwenye kuwataka ushauri. kumpokea msafiri wao anaporudi. Kuwafichia siri zao. Kusitiri aibu yao. Kumsaidia mdhulumiwa wao. Kushirikiana nao vizuri katika matumizi ya vyombo. Nakuwapa yaliyo wajibu kwao kabla hawajaomba Nijaalie Oh Allah! Nimlipe mema muovu wao Nitupilie mbali kwa uvumilivu maovu ya dhalimu wao. Kuwadhania dhana njema wote. Niwatendee wema wote. Nirudishe macho yangu chini kujizuia na tamaa. Niteremshe upande wangu kwao kwa unyenyekevu. Niwe mpole kwa waliokumbwa na balaa miongoni mwao kuwa hurumia. Niwafurahishe wakiwa hawapo kwa upendo Nipende wabakiye na Neema kwa nia njema wape ambalo niwapalo jamaa zangu. Niwachungiye ambalo niwachungialo Marafiki zangu mahsusi. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Niruzuku kwa kadiri hiyo hiyo toka kwao. Nijaaliye hadhi ya kutosha katika waliyonayo wazidishiye utambuzi katika haki yangu, Na elimu ya ubora wangu. Ili wafanikiwe kupitia mimi na nifanikiwe kupitia wao. Ameen, E! Bwana wa Ulimwengu wote.

DUA YA 27

DU'A ZAKE(A.S) KWA WATU WA MPAKANI

Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Uimarishe mstari wa mbele wa Waislamu kwa uwezo wako. Wape nguvu walinzi wake kwa nguvu zako. Kithirisha wapewacho kwa utajiri wako Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Zidisha idadi yao. Nowa silaha zao. Ilinde nchi yao. Yalinde mapambano yao. Unganisha mkusanyiko wao. Pangilia mambo yao. Fululiza posho lao. Peke yako chukuwa jukumu la kuwatosheleza posho lao. Waunge mkono kwa ushindi wasaidie kuwa na subira. Wape werevu kwenye vitimbi. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Watambulishe wasio yajuwa Wafundishe wasiyoyajua Waoneshe wasiyoyaona

Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Wasahaulishe wakati wa kutanapo na aduwi. Kuikumbuka Dunia yao babaishi danganyifu. Futa toka mioyoni mwao fikra ya mali ipendezayo sana. Na ifanye Jannah iwe mbele ya macho yao. Waoneshe baadhi ya uliyowaandalia humo machoni mwao. Miongoni mwa makazi ya kudumu. Nyumba za heshima. Huri warembo. Mito ibubujikayo kwa aina aina za vinywaji. Miti iliyojiangika karibu ikiwa na sampuli tofauti za matunda. Ili yeyote miongoni mwao asiwe na wazo la kutumba mgongo, Wala asijishauri kumkimbia mpinzani wake. Oh Allah! Kwa hayo mshinde aduwi yao. Mkate makucha yake kutoka kwao, waweke mbali na silaha zao. Ondoa uthabiti wa mioyoyao. Waweke mbali na akiba yao. Watundu waze katika njia zao. Wapotoshe toka kwenye mwelekeo wao. Wakatie msaada. Wapunguze idadi. Wajaze woga mioyoni mwao. Igandishe mikono yao isiweze kukunjuka, zifunge ndimi zao zisiongee, watawanye walio nyuma yao. Wape funzo walio nyuma yao. Zikate tamaa za watakaokuja baada yao. Kwa kuwa dhalilisha. Oh Allah! Yafanye tasa matumbo ya wanawake wao. Vikaushe viuno vya wanaume wao Kikate kizazi cha wanyama wao Usiiruhusu mbigu yao kunyesha Wala mmea katika ardhi yao Kwa kufanya hayo uupe nguvu ujasiri wa Uislamu. Boresha kwa hayo ngome za nyumba zao. Kwa hayo wazidishiye mali zao. Waweke mbali na kupambana nao kwa ajili ya ibada yako na mbali na kulumbana nao ili wapate muda wa kujitenga wakiwa na wewe. Ili asiabudiwe ardhini asiyekuwa wewe wala paji lau uso la yeyote miongoni mwao lisisuguliwe kwenye mchanga kwa ajili ya yeyote mbali na wewe. Oh Allah! Wapeleke washambulizi kutoka kila upande wa Waislamu kwa washirikina waliomuka bala wao. Na uwaongezee msaada wa malaika kutoka kwako kwa daraja. 111 wawatimuwe mpaka mwisho wa nchi kwa kuwa uwa katika ardhi yako na kuwateka au wakubali kuwa wewe ndiye Allah ambaye hapana miungu isipokuwa wewe tu, peke yako huna mshirika. Oh Allah ! Waingize kwa hilo maadui zako katika maeneo ya nchi za India, Urumi, Uturuki, Khazars, Abyssinia, Uhabeshi, Noubah Zanji na Daylamite. Na umma zingine za washirikina ambao majina yao na sifa zao zafichika lakini ni ambao umejua hesabu yao kwa maarifa yako. Na umewaona kwa uwezo wako. Oh Allah ! Washughulishe washirikina wao kwa wao ili wasiifikie mipaka ya Waislamu wazuiye kwa kuwa punguza kutoka upungufu wao.

Wazuie kwa mgawanyiko utakaowafanya washindwe kujikusanya dhidi yao. Oh Allah ! Ondoa usalama mioyoni mwao na ondoa nguvu milini mwao, iziwie mioyo yao isiweze kuwa na mbinu, dhoofisha viungo vyao wasiweze kupambana na wanaume. Wafanye wawe waoga kiasi cha kuwa hawawezi kupambana na mashujaa, watumie askari kutoka miongoni mwa malaika wako kwa ukali kutoka ukali wako. Kama ulivyofanya siku ya badri uikate mizizi yao kwa hilo, kwa hilo uiondoe miba yao na uitawanye idadi yao. Oh Allah ! changanya maji yao maradhi yakuambukiza na vyakula vyao na maradhi, iangamize miji yao kwa kuifuta kabisa. Na wahangaishe kwa kutupiwa, wazuiye kwa ukame. Na ijaalie rizki yao kwenye ardhi yenye ukuba mno miongoni mwa ardhi zako, ardhi iliyo mbali sana nao, wazuie wao kwenye ngome zake (ardhi) wape njaa ya mara kwa mara na ugonjwa uumizao. Oh Allah! Na mshambuliaji yeyote akiwashambulia kutoka watu wa mila yako, au mpambanaji akipambana kutoka wafuasi wa sunnah yako, ili dini yako iwe juu. Na kundi lako liwe ndilo kundi lenye nguvu mno. Na hadhi yako iwe kamili. Mpe nafuu, mpangie mambo, mpe mafanikio, mchagulie wenzi, umpe nguvu mgongo wake, mzidishiye nafaka, umstareheshe kwa uzima na nguvu. Umzimishie joto la shauku, mpe kimbilio kutokana na huzuni ya upeka. Msahaulishe kuwakumbuka mke na watoto, mpitishie kuchagua nia njema mpe afya.

Mwambatanishie usalama mwepushe na woga, mpe ushujaa, mpe nguvu, msaidie kwa kumpa ushindi. Mfundishe sera njema na sunnah, mweke sawa katika kuhukumu. Mwondolee riyaa, mwepushe na kupenda kusifiwa, na ifanye fikra yake, kumbukumbu yake, safari yake, na kaa yake iwe katika wewe na kwa ajili yako. Asimamapo safu kwa adui yake na adui yako waonyeshe mbele ya macho yake kuwa ni wadogo. Udogeshe umuhimu wao moyoni mwake zamu ya ushindi dhidi yao iwe yake, wala usiifanye zamu ya ushindi kuwa yao, lakini endapo utamuhitimishia na heri na kumwamulia kupata shahadat. Acha iwe baada ya kumng'owa adui yako kwa kumuuwa na baada ya kutekwa kumewachujusha. Na baada ya kuwa mipaka ya Waislamu iko salama. Na baada ya kuwa adui yako amekwisha tumba mgongo akimbia.

Oh Allah! Muislamu yeyote akimwacha mpiganaji au askari mlinzi katika nyumba yake akatunza alivyoviacha nyuma yake. au akamsaidia kwa sehemu ya mali yake au kumsaidia kwa vyombo au kumnowa kwa ajili ya vita au kumwagizia mbele ya uso wake DU'A au kumhifadhia heshima nyuma yake. Mpe malipo mfano wa malipo yake uzito kwa uzito. Na mfano kwa mfano, mpe malipo ya kitendo chake malipo ya haraka ambayo ataharakia kunufaika na alichokitanguliza na kufurahia alichokileta mpaka wakati uishiye kwenye yale uliyompa miongoni mwa fadhila zako. Na uliyomwandalia kutokana na ukarimu wako. Oh Allah ! Muislamu yeyote atilia manani suala la Uislamu na kumuhuzunisha ushirikiano wa washirikina dhidi yao. Kwa hiyo akawa na nia ya kwenda vitani au akusudia jihadi. "Lakini udhaifu ukamzuia au umasikini umemchelewesha au tukio la bahati mbaya likamzuia au amezukiwa na jambo kinyume na utashi wake. Basi andika jina lake miongoni mwa wachamungu wajibisha kwake thawabu za wapiganaji jihadi. Na mweke katika daraja ya mashahidi na watu wema. Oh Allah ! Mrehemu Muhammad mja wako na Mjumbe wako na Ali wake Muhammad Rehma ya hali ya juu. Juu ya rehma na maamkizi Rehma haina mwisho wala idadi yake haikatiki kama Rehma zako zilizokamili mno miongoni mwa zilizopita kwa yeyote miongoni mwa mawalii wako. Hakika wewe mwema mwenye kuhimidiwa, mwanzilishi na mwenye kurudisha mtekelezaji wa utakalo.

DUA YA 28

DU'A ZAKE ANAPOKIMBILIA KWA ALLAH

Oh Allah! Nimekuwa mnyofu kwa kukata mawasiliano na kingine chochote isipokuwa kwako, mzima na kwa yote nimeelekea juu yako. Nimeugeuza uso wangu toka kwa ambaye yu ahitajia au ni yako. Nimeacha maombi kwa asiyejiweza bila ya fadhila zako. Nimeona kuwa muhitaji kumwomba muhitaji kama yeye ni upuuzi wa maoni yake. Na ni upotovu wa akili yake, ni wangapi nimewaona ewe Mola wangu miongoni mwa watu.! Wameomba utukufu kwa asiyekuwa wewe wakadhalilika, walitaka mali kwa mwingine ambaye si wewe wamekuwa masikini, walijaribu kupanda wakaanguka. Kwa kuona mifano yao humsahihisha mwerevu. Uangalifu wake umemfanikisha, uchaguzi wake umemwongoza kwenye njia ya sawa. Hivyo basi wewe ewe bwana wangu mbali na mwombaji yeyote ndio mahali pa maombi yangu. Ndio mfadhili wa haja yangu mbali na mwingine yeyote ambaye maombi hufanywa kwake. Wewe tu wahusika pekee kwa wito wangu kabla ya mwombaji mwingine yeyote.

Hakuna ashirikishwaye na wewe katika matumaini yangu. Wala yeyote hawafikiani na wewe katika DU'A zangu. Wala hapana yeyote ajiungaye na wewe katika hili. Kwako wewe tu ndiyo maombi yangu. Wako ewe Mola wangu, ni umoja wa idadi, na miliki ya uwezo wa milele, na ubora wa uwezo na nguvu, na daraja ya utukufu wa juu kabisa, na yeyote ambaye si wewe ni wakuhurumiwa maishani mwake, mwenye kuhemewa katika mambo yake. Mwenye kushindishwa na hali yake mambo yake tofauti, zabadilika sifa zake, hivyo basi uko juu mbali na kufanana na vitu au kitu kuwa dhidi yako. Umetukuka huwi mfano wa chochote na dhidi yeyote kwako. Utakatifu ni wako hapana miungu isipokuwa ni wewe.

DUA YA 30

DU'A ZAKE(A.S) KWA AJILI YA KUOMBA MSAADA WA KULIPA DENI

Oh Allah ! Mrehemu Muhammad na Aliy zake. Nikombowe kutokana na deni ambalo lachakaza uso wangu laichanganya akili yangu, latawanya fikra yangu ili kulipa shughuli yangu inakuwa ndefu, na ninajikinga kwako Ewe bwana wangu kutokana na woge wa deni na fikra zake. Mshughuliko wa deni na mkesho wake msalie Muhammad na Aliy zake, nilinde nayo. Naomba hifadhi kwako ewe, Mola wangu ili niepukane na dhila yake maishani na kufuatiliwa kwake baada ya kufa. Mrehemu Muhammad na Aliy zake. Na unipe hifadhi niepukane nalo kwa kunipanulia fadhila au kwa kufululiziwa utoshelezi wako.

Oh Allah ! Mrehemu Muhammad na Aliy zake, nizuwie kufanya israfu na kutumia zaidi ya haja. Niweke sawa katika kutoa kwa ukarimu na wastani. Nifundishe uzuri wa kukadiria, nikamate kwa upole wako nisifuje, ipitishe rizki yangu kwa njia ya halali, uelekeze utowaji wangu kwenye milango ya wema. Niepushe na mali itakayonisababishia majivuno au kunifanya niwe jeuri au itakayonifikisha kwenye kukiuka mipaka. Oh Allah ! nipendezeshe kusuhubiana na mafakiri nisaidie katika kusuhubiana nao kuwa na saburi njema. Uniondoleapo mafao ya dunia ya mpito nihifadhiye nayo katika hazina zako za kudumu.Jaalia uliyonitunukia miongoni mwa mabomoko yake na vifaa vyake ulivyo harakisha kunipa, viwe ni njia ya kuufikia ujirani wako na kiungo cha ukaribu wako' na ni sababu ya kuifikia janna yako kwa hakika wewe ni mwenye fadhila kubwa na wewe ni mpaji mkarimu.