AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU 0%

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU Mwandishi:
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi: Imam Ali bin Husein (A.S)

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi: Ali ibn al - Husayn Imam Zaynul al - Abidin (a.s.)
: Sheikh Haruna Pingili
Kundi:

Matembeleo: 18341
Pakua: 2865

Maelezo zaidi:

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU
Tafuta ndani ya kitabu
  • Anza
  • Iliyopita
  • 16 /
  • Inayofuata
  • Mwisho
  •  
  • Pakua HTML
  • Pakua Word
  • Pakua PDF
  • Matembeleo: 18341 / Pakua: 2865
Kiwango Kiwango Kiwango
AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

Mwandishi:
Swahili

6

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 31

DU'A ZAKE (A.S) KATIKA KUIELEZEA TOBA NA KUIOMBA

Oh Allah! Oh yule ambaye hazi sifa za wenye kumsifu kumsifia. Oh we ambaye hayamvuki matarajio ya watarajiao. Oh we ambaye kwake hayapotei malipo ya watenda mema. Oh we ambaye yeye ndiye mwisho wa hofu ya wachapa ibada. Oh we ambaye ni upeo wa woga wa wachamungu. Hiki ni kituo cha aliyepitiwa na madhambi mkono kwa mkono. Hatamu za makosa zimemwongoza na shetani amemtawala. Amezembea kutekeleza uliyomwamrisha kwa kupuuza. Na akajipa uliyomkataza ajiepushe nayo katika hali ya kudanganyika akiwa kama asiyejua uwezo wako juu yake, au akiwa kama mfano wa akanushaye ubora wa ihisani yako kwake! Mpaka jicho la uongofu litakapo mfungukia. Viwingu vya upofu vitakapomtanduka atahesabu vile ambavyo ameidhulumu nafsi yake. Na atatafakari katika yale amemkhalifu bwana wake. Hivyo ataona ukubwa wa maasi yake kuwa ni mkubwa na uzito wa kumkhalifu kwake kuwa ni mzito. Kwa hiyo ataelekea upande wako akikutumainia, akikuonea haya. ataelekeza maombi yake kwa kukuamini atakuwa amejitengeneza upya kwako kwa tamaa zake akiwa na yakini. Amekukusudia moja kwa moja kwa hofu na unyofu, tamaa zake zimeepukana na yote ya kufanyiwa tamaa bali ni wewe tu.

Kwa hiyo amesimama mbele yako akijitetea ameyaelekeza macho yake chini mnyenyekevu, ameinamisha kichwa chake kwa ajili ya utukufu wako mwenye kujidhalilisha. Akudhihirishia siri zake ambazo wewe wazijua vizuri mno kuliko yeye hali ya unyenyekevu. Atakuwa amezihesabu dhambi zake kwa unyenyekevu hali wewe wazijua vizuri mno idadi yake. Atakuomba sana msaada kwa lakutisha ambalo ameangukia humo katika elimu yako Na kwa ajili ya baya lililomfedhehesha katika hukumu yako miongoni mwa dhambi ambazo starehe zake zimetumba mgongo na kutokomea ambazo matokeo ya ubaya wake yamethibiti na kulazimu. Hato kanusha Oh! Mola wangu uadilifu wako endapo utamwadhibu wala hatouzingatia msamaha wako kuwa ni jambo kubwa endapo utamsamehe na kumuhurumia kwa sababu wewe ni bwana mkarimu ambaye hadogeshwi na msamaha wa dhambi kubwa. Oh Allah ! mimi ni huyoo! Nimekujia hali nikiwa mtii wa amri yako kwa kuwa umeamuru kuomba DU'A kwa hiyo nakuomba kutekeleza ahadi yako kwa uliyoahidi kujibu kwa vile wasema: (niombeni nitakujibuni). Oh Allah! mrehemu Muhammad na Aliy zake, kutana na mimi kwa msamaha wako kama nilivyokutana na wewe kwa kukiri kwangu. Niinuwe kutokana na mweleka wa dhambi kama nilivyojitupa chini kwako, nisitiri kwa sitara yako kama vile ulivyoacha kunifanyia haraka malipizi. Oh Allah! Iimarishe nia yangu katika utii wako upe nguvu ufahamu wangu katika ibada yako, nipe tawfiki katika matendo mema ambayo yataniosha uchafu wa makosa. Nifishe nikiwa katika mila yako na mila ya Nabiy wako Muhammad amani imfikie Oh Allah!, Hakika mimi natubu kwako katika kikao changu hiki kuwa nitaacha madhambi yangu makubwa na madogo.

Maovu yangu ya ndani na nje kupotoka kwangu kulikotangulia na kwa hivi sasa toba ya mtu asiyeweza fanya maasi wala hana dhamira ya kurejea kwenye makosa. Na kwa hakika umekwisha sema ewee Mola wangu katika kitabu chako thabiti kuwa hakika wewe waikubali toba ya waja wako na wasamehe maovu. Na unawapenda wanaotubu basi ikubali toba yangu kama ulivyoahidi na nisamehe maovu yangu kama ulivyochukua dhamana. Na niwajibishie mapenzi yako kama ulivyoweka sharti, sharti yangu kwako Oh bwana wangu sitorudi kwenye machukio yako na dhamana yangu nitoayo ni kuwa sitorudi kwenye yalaumiwayo na wewe. Na ahadi yangu ni kwamba nitayahama maasi yako yote. Oh Allah! hakika wewe wajua zaidi niliyoyatenda. Basi nighofirie uliyoyajua niepushe kwa uwezo wako na nielekeze kwenye ambayo wayapenda. Oh Allah ! na dhidi yangu kuna haki daiwa nimezihifadhi, na haki daiwa nimezisahau zote hizo zi jichoni mwako ambalo halilali. Na elimu yako ambayo haisahau wafidie wenye haki na nipunguzie mzigo wake, nifanyie wepesi uzito wake, nilinde nisiikurubie iliyo mfano wake. Oh Allah! kwa hakika sina uwezo wa kutekeleza toba yangu isipokuwa kwa kulindwa na wewe wala kujiziwiya na makosa isipokuwa kwa uwezo wako nipe uwezo wa kutosha. Nipe ulinzi wako wenye kuzuiya. Oh Allah! mja yeyote ametubu kwako naye katika elimu yako ya ghaibu ataitanguwa toba yake, na atarejea katika dhambi zake na makosa yake. Kwa hakika mimi najilinda kwako nisiwe kama vile, ifanye toba yangu hii toba sihitajii baada yake toba yeyote. Iwe toba iwajibishayo kufuta yaliyotangulia, na ya salama kwa yaliyobaki. Ewe Mola! Hakika mimi nakuomba msamaha kwa sababu ya ujinga wangu. Nakuomba usitilie manani vitendo vyangu viovu, niunganishe kwenye kivuli cha rehma yako kwa ihsani, nisitiri kwa sitara ya afya yako kwa fadhila zako. Oh Allahl kwa hakika mimi ninatubu kwako kutokana na kila kilichokwenda.

Kinyume na utashi wako au kimekuwa mbali na mapenzi yako kutoka mawazo ya moyoni mwangu, mtizamo wa macho yangu na hekaya za ulimi wangu.Toba ambayo kila kiungo cha mwili wangu kitabaki salama bila malipizi yako na kitakuwa na amani bila ya woga wa yale wayaogopayo wakiukaji miongoni mwa machungu ya adhabu zako. Oh Allah! Uhurumie upweke wangu mbele yako, na kupondekana kwa moyo wangu kutokana na kukuogopa wewe. Nakutetemea kwa viungo vya mwili wangu kwa ajili ya haiba yako. Ewe Bwana wangu! Dhambi zangu zimeniweka weko la kudharauliwa uwanjani pako. Nikinyamaza hakuna atakayenisemea na nikiomba Shafaa sikuwa miongoni mwa wenye haki ya kupata Shafaa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake Ufanye ukarimu wako kwa mwombezi wa makosa yangu. Yarejelee maouvu yangu kwa msamaha wako. Usinilipe malipo ninayostahiki katika adhabu zako. Ni kunjuliye juu yangu ihisani zako ni viringishe sitara yako. Nitendee kitendo cha mtu mwenye enzi wakati mtumwa dhalili amnyenyekeapo na akamuhurumia. Au tendo la mtu tajiri fakiri anapomnyenyekea naye akamtajirisha. Oh Allah! Sina wakunilinda dhidi yako hivyo basi naomba Enzi yako inilinde. Sina mwombezi kwako hivyo basi fadhila zako ziwe ndiyo mwombezi wangu. Makosa yangu yamenitia hofu wacha msamaha wako unipe amani. Siyo yote niliyotamka kwa ujinga wangu kwa sababu ya ufuatiliaji wangu mbaya wala sikusahau yaliyopita miongoni mwa matendo yangu yastahiliyo kulaumiwa.

Lakini ili mbingu zako zisikie na waliomo humo na ardhi yako na waliomo juu yake niliyokudhihirishia miongoni mwa majuto. Na nimekimbilia kwako kutubu. Huwenda baadhi yao kwa Rehema Zako watanirehemu kwa sababu ya ubaya wa kikao changu. Au mtu ashikwe na huruma juu yangu kwa sababu ya ubaya wa hali yangu. Huenda nikapata kutoka kwake DU'A ambayo sikilizwa mno kwako kuliko Duwa yangu. Au ombezi lenye nguvu mno kwako kuliko ombezi langu. Humo utakuwa uwokovu wangu epukana na ghadhabu zako. Na kufuzu kwangu kwa ridhaa zako

Oh Allah! Ikiwa kujuta ni toba ya kukubaliwa kwako, basi mimi ni mjutaji mno wa wajutaji wote. Na ikiwa kuacha kukuasi ndio kurejea kwako, basi mimi ni mrejea wa kwanza kwako kuliko warejeao wote. Na ikiwa kuomba ghofira ni sababu ya kupunguziwa dhambi, basi mimi ni miongoni mwa wakuombao ghofira. Oh Allah! Kama ulivyoamrisha toba na ukachukuwa dhamana msalie Muhammad na Aali zake ikubali toba yangu. Wala usinirudishe Rudisho la kutofanikiwa Rehma zako. Hakika wewe ni mwingi wa kupokea toba ya watenda dhambi. Na mwenye Rehma sana kwa wakosaji wanaorejea kwako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake. Na kama vile umetuongoza kwa sababu yake mrehemu Muhammad na Aali zake. Kama ulivyotuokowa kwa sababu yake mrehemu Muhammad na Aali Zake Rehema itakayotuombea siku ya Kiyama na siku ya kukuhitajia. Hakika wewe ni muweza wa kila kutu na ni rahisi kwako.

DUA YA 32

DU'A ZAKE BAADA YA KUMALIZA SALA ZA USIKU

Oh Allah! mmiliki wa ufalme wa kudumu wa melele. Utawala usioshindika bila ya askari wala wasaidizi. Na enzi ya kubaki miaka nenda miaka rudi zama nenda zama rudi siku nenda siku rudi. Yana Enzi mamlaka yako Enzi isiyo na mpaka wa mwanzo wala mwisho. Ufalme wako umekuwa wa juu zaidi vimeporomoka vitu bila ya kuufikia muhula wake. Sifa zenye uwezo wambali za wenye kusifu hazitoweza kukufikia kile kidogo mno ulichojitengea kwa ajili yako. Kwako sifa zimepotoka. Zimeshindwa kukufikia sifa. Mawazo yame DU'A mbele ya utukufu wako. Kwa ajili hiyo wewe ni wa Daima hutoweki. Nami ni Mja dhaifu wa matendo mwenye matumaini makubwa kabisa. Sababu za kuwasiliana zimeponyoka toka mikononi mwangu isipokuwa zilizo wasilishwa na Rehma zako. Hamana za matumaini zimenikatika isipokuwa ni ishikiliayo katika msamaha wako. Kimekuwa kidogo mno niwezacho kukihesabu katika utii wangu kwako. Yamekithiri dhidi yangu maasi yangu kwako haitokuwia dhiki kumsamehe mja wako japo afanye maovu basi nisamehe Oh Allah!

Elimu yako ya chunga kazi zilizojificha kila kilicho sitirika kimefichuka mbele ya utambuzi wako. Hayafichiki kwako mambo madogo sana na viroja vya siri kabisa havifichiki kwako. Adui yako amenishinda nguvu adui ambaye alikuomba umbakishe ili anipotoshe na ulimbakisha. Alikuomba umpe muhla wa kubakia mpaka siku ya hukumu ili anipoteze ulimpa muhula. Hivyo basi amenitupa chini ingawaje nimekimbilia kwako kutokana na madhambi madogo madogo angamizi na amali kubwa ziuwazo mpaka nilipotenda maasi yako na kwa ubaya wa juhudi yangu nimewajibika chuki yako. Amegeuza toka kwangu ugwe ya udanganyifu wake. Akakutana na mimi kwa neno lake la kufuru. Akajitenga na mimi. Akatumba mgongo anikimbia. Kwa hiyo akanitupa kwenye jangwa la ghadhabu zako peke yangu. Amenitoa nje na kuniweka kwenye uwanja wa malipizi ya kisasi chako nikiwa mwenye kufukuzwa. Hakuna mwombezi atakayeniombea kwako wala mlinzi atakayenifanya niwe na amani kwako. Wala hakuna ngome itakayonificha wewe usinione. Wala hapana kimbilio niwezalo kukimbilia kukukimbia wewe. Hivyo hiki ni kikao cha ajilindae na wewe nani mahali pa mtu akutambuaye. Basi fadhila zako zisinijie finyu, wala usikose kunifika msamaha wako wala nisiwe miongoni mwa waja wako wasio fanikiwa mno katika waja wako waliotubu. Wala nisiwe miongoni mwa wakata tamaa miongoni mwa wajao kwako wakiwa na matumaini. Nisamehe hakika wewe mghofiri bora miongoni mwa wenye kughofiri. Oh Allah! Hakika umeniamrisha nikaacha. Umenikataza nikafanya. Mawazo mabaya yamenifanyia majaribu kufanya mabaya nikazembea. Wala siwezi kutolea ushahidi funga yangu mchana. Wala siwezi kuomba kimbilio kwa ajili ya sala yangu ya Tahajudi usiku wala Sunnah hainipi sifa kwa kuihuisha.

Isipokuwa faradhi zako ambazo atakayezembea atahiliki siwezi kutaka wasila kwako kwa fadhila za sala za naafila hali yakuwa mengi nimeghafilika kuyatenda miongoni mwa nyadhifa za faradhi zako na nimevuka mipaka yako. Na kukiuka sehemu takatifu. Madhambi makubwa nimeyatenda ingawa afya yako ilikuwa kwangu ndio sitara kwa kuepukana na fedheha yake. Haya ni makazi ya mwenye kujionea haya binafsi mbele yako, na ameikasirikia nafsi yake, na ameridhika na wewe. Kwa hiyo akutana na wewe kwa moyo mnyenyekevu. Shingo iliyoinama chini. Mgongo mzito kwa makosa. Amesimama akibabaika kati ya kukupenda na kukuogopa. Na wewe ni bora wa aliowatumainia. Na umwenye haki mno kati ya alio waogopa na kuwa hofu. Basi nipe ewe Bwana wangu niliokutumainia. Nipe Nipe amani kwa niliyojihadhari nayo nihurumie kwa huruma za Rehema yako hakika wewe u mkarimu mno miongoni mwa wenye kuombwa. Oh Allah! kwa vile umenisitiri kwa afya yako. Na umenikinga kwa fadhila zako katika makazi yenye mwisho mbele ya marika nipe kimbilio la kujiepusha na fedheha za makazi ya kubaki milele waliko simama mashahidi. Miongoni mwa malaika walioletwa karibu na mitume waheshimiwa na watu waliokufa mashahidi na watu wema. Miongoni mwa jirani nilikuwa na mficha maovu yangu. Na ndugu watumbo moja nilikuwa namwonea haya siri zangu. Sikuwa na waamini kunisitiri Oh Rabi! Nimekuamini wewe Oh! Mola wangu, katika kunighofiria. Na wewe ni bora mno wa kuaminiwa. Na u mtowaji mno kuliko wote waombwao u mwema mno kuliko wote wanaoombwa Rehema, hivyo ni Rehemu. Ewe Mola wewe ndiwe uliye nifanya nitoke kwenye asili ya maji duni. Kutoka kiuno chenye mifupa miembamba na mapito ya shida.

Mpaka kwenye tumbo jembamba uliloli sitiri kwa mifuniko. Wani hamisha toka hali moja kwenda hali nyingine. Mpaka ulinimalizia kwenye umbo lililo kamilika. Ukaniweka viungo vya mwili, kama ulivyoaridhia katika kitabu chako (tone la Manii) kisha pande la Damu, kisha nyama, kisha mifupa, kisha uliivisha mifupa na nyama, kisha ulinifanya umbo jingine) kama ulivyopenda mpaka nilipohitaji riziki yako siku jitosha bila ya msaada wa fadhila zako. Ulinifanyia chakula chenye lishe kutoka fadhila ya chakula na kinywaji ulichomtunukia kijakazi wako ambaye tumbo lake ulifanya kuwa makazi yangu. Uliniweka chini ya tumbo lake la uzazi. Ewe Mola wangu! Lau ungeniwakilisha katika hali zile kwenye uwezo wangu au ungenifanya ni lazimike kutumia nguvu zangu. Uwezo ungekuwa haupo kwangu. Na nguvu zingekuwa mbali na mimi. Ulinipa lishe kwa fadhila zako lishe ya mtu mwema mwenye huruma. Wanitendea hayo kwa wema tu juu yangu mpaka kwenye mwisho wangu huu. Siyakosi mema yako. Mema yako haya niachi ningojee, pamoja na yote hayo 'ithibati' yangu haijaimarika. Kiasi cha kuwa niwe nina nafasi kwa ajili ya lile ambalo lina hadhi sana kwangu mbele yako.

Shetani ameshika barabara hatamu yangu kupitia dhana yangu mbaya. Na udhaifu wa yakini. Kwa hiyo mimi na nung'unika ubaya wa ujirani wake na mimi, na nafsi yangu kumtii yeye! Nakuomba hifadhi niepukane na utawala wake. Ninanyenyekea kwako ili niondolewe vitimbi vyake dhidi yangu. Sifa njema ni zako kwa sababu ya kuanza kwako Neema kubwa na kwa sababu ya Il-Hamu yako iwezeshayo kutambuwa ihsani na neema. Msaliye Muhammad na Aali Zake na unirahisishiye riziki yangu na unifanye niwe natosheka na makadirio yako kwangu. Unifanye ni ridhike na hisa yangu katika ulichonigawiya. Na ujaaliye kilicho toweka toka mwili wangu na umri wangu kiwe ni kwa ajili ya njia ya utii wako. Hakika wewe ni mbora wa watowao riziki.

Oh Allah! Hakika mimi najilinda nawe ili kuepukana na moto ulioutia makali dhidi ya watakaokuasi. Moto ambao umemuonya mwenye kugeuka mbali na ridhaa zako na moto ambao mwanga wake ni giza. Ambao nafuu yake ni machungu na umbali wake ni karibu. Kutokana na moto ambao baadhi yake yaila baadhi nyingine. Moto ambao waiacha mifupa imekwisha teketeza. Unawanywesha watu wake maji yachemkayo. Moto ambao haumwachii mwenye kukiri kwake. Hautomhurumia mwenye kuomba Rehema. Hauwezi kujipunguza makali kwa mwenye kuunyenyekea na kusalimu amri kwake. wapambana na wakazi wake kwa joto ililo nalo kwa mateso yaumizayo na ghadhabu kali mno. Najilinda kwako na nge wake walio midomo wazi. Na nyoka wake wenye meno yagege DU'A yo. Na kinywaji chake kinacho kata utumbo na nyoyo za wakazi wake na kuutowa ubongo wao. Nakuomba mwongozo kutoka kwako wa kile ambacho kitaweka mbali na huwo moto na kuufanya urudi nyuma. Oh Allah!

Mrehemu Muhammad na Aali Zake nipe kimbilio ili niepukane nao kwa fadhila za Rehema Zako. Nisamehe kujikwaa kwangu kwa uzuri wa msamaha wako. Wala usinitupe Ewe Mbora wa kutowa kimbilio. Oh Allah! Hakika wewe wahifadhi lichukizalo, Na watowa lililo zuri. Watenda upendalo, na U-muweza juu ya kila kitu. Oh Allah! mrehemu Muhammad na Aali Zake watajwapo watu wema. Na mrehemu Mhammad na Aali Zake kwa kadiri ya usiku na mchana unavyopishana kwa heri. Rehema ambazo ongezo lake halikatiki idadi yake haihesabiki. Rehema itakayojaza anga, na itajaaza ardhi na mbingu. O Allah! Mrehemu yeye mpaka aridhike O Allah! Mrehemu yeye na Aali Zake baada ya kuridhika. Rehema zisizo na mpaka wala mwisho OWEE Mwingi wa Kurehemu miongoni mwa wanaorehemu.

Dua ya 33

MIONGONI MWA DUWA ZAKE KATIKA ISTIKHARA

Oh Allah! Hakika mimi nakuomba ambalo ni zuri zaidi katika ujuzi wako. Msaliye Muhammad na Aali Zake na tuamuliye lililo zuri zaidi. Na tupe Il-Hamu ya maarifa ya kuchagua. Na ifanye iwe ni sababu ya kuridhiya uliyo yapitisha kwa ajili yetu na kusalimu amri kwa uliyotuhukumia tuondolee mashaka ya kusita sita tu imarishe kwa yakini ya watu wanyofu. Usitupatilize kwa kushindwa kutambua uliyo yachagua tusije tukadharau kadirio lako. Na tusije chukia mahali pa ridhaa zako na kuelemea kwenye ambalo li mbali na mwisho mwema na li karibu sana na kinyume cha afya njema.Tupendezeshe tukichukiacho katika Agizo lako. Na tusahilishiye tuonacho kuwa kigumu katika hukumu yako. Tufunulie kuwa wasikivu kwa uliletalo kwetu katika utashi wako mpaka iwe hatupendi kuchelewesha uliloliharakisha wala kuharakisha uliyolichelewesha. Wala tusichukie ulichopenda wala kuchaguwa ulichokichukia na tuhitimishiye kile chenye mwisho wenye sifa njema mno na matokeo yenye heshima zaidi hakika wewe unafisha chenye heshima na watowa kingi, watenda utakalo nawe u muweza wa kila kitu.

Dua ya 34

DU'A ZAKE AKIPATWA NA BALAA AU AMWONAPO MWENYE KUPATWA NA FEDHEHA, KWA AJILI YA DHAMBI

Oh Allah! Himidi ni yako kwa sababu ya kusitiri kwako baada ya kujuwa kwako. Na msamaha wako baada ya kuelewa kwako. Kila mmoja kati yetu amefanya aibu lakini hukumtangaza na amefanya tendo la utovu wa adabu na wala haukumfedhehesha. Na Alijisitiri kwa maovu wala haukumuonesha. Ni makatazo yako mangapi tumeyatenda! Amri yako umetuagiza na tumeikiuka; matendo maovu tumeyatenda. Makosa tumeyatenda. Ulikuwa ukiyaona na watazamaji wengine hawaoni.

Na muweza wa kuyatangaza kuliko wawezao wote. Uislama uliotupa ni pazia mbali na macho yao. Na kiziwizi dhidi ya masikio yao. Ifanye aibu uliyotufichiya na mambo ya ndani uliyoyaficha yawe onyo kwetu. Na kemeo dhidi ya matendo mabaya na kutenda makosa. Na viwe kichocheo cha juhudi ya kufanya toba ifuatayo na njia yenye kuhimidiwa na usogeze wakati wa toba. Usitupatilize kwa kukusahau kwa hakika sisi twakuomba. Na twatubu kwa kuacha dhambii. Oh Allah! Na mrehemu mteule wako katika viumbe wako Muhammad na kizazi chake, wateule miongoni mwa viumbe wako wa Taharifu. Na tujaaliye sisi kuwa wasikivu na watii kwao kama ulivyoamrisha.

DUA YA 35

MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) KATIKA RIDHAA AWAANGALIAPO WANA WA DUNIA HII

Sifa njema ni za Allah kwa kuridhika na hukumu ya Allah Nimeshuhudia kuwa Mungu amegawa maisha ya waja wake kwa uadilifu. Amechukuwa jukumu la fadhili viumbe wake wote. Ewe Allah! Mrehem Muhammad na Aali zake. Usinifanyie kishawishi kwa uliyowapa viumbe wako. Wala usiwafanyiye kishawishi kwa uliyoninyima, ili nisije mwonea husuda kiumbe wako na kuyadharau maamuzi yako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake. Ipendezeshe nafsi yangu maamuzi yako. Kipanuwe kifuwa changu katika maeneo ya maamuzi yako. Nipe imani ili nikirikwa imani hiyo ya kuwa maamuzi yako hayafanyiki ila kwa kheri. Na ifanye shukurani yangu kwako juu ya ulichokiondoa kwangu iwe kubwa zaidi kuliko shukrani yangu kwako juu ya ulichonipa.

Unilinde nisije dhaniya kuwa kutokuwa na kitu kwa mtu ni kudunishwa au ni mdhaniye mwenye utajiri kuwa mwenye ubora (kwa Mungu). Kwa kuwa mbora ni yule aliye boreshwa na utii wako. Na mwenye enzi ni yule aliye enziwa na Ibada zako. Mswalie Muhammad na Aliy zake tupe starehe kwa mali isiyokwisha. Tupe nguvu kwa Enzi isiyotoweka. Tupe nafasi katika ufalme wa milele. Hakika wewe ni Mmoja peke yako kimbilio la milele. Haukuzaa wala haukuzaliwa, wala hakuna anayelingana na wewe.

DUA YA 36

DU'A ZAKE AANGALIAPO MAWINGU NA UMULIKAJI NA ASIKIAPO SAUTI YA RADI

Oh Allah! hakika hizi ni alama zako mbili na hawa ni wasaidizi wako wawili wa harakiao utii wako imma kwa Rehema yenye manufaa au kisasi kiumizacho. Usituteremshie kutoka kwa wawili hao mvua mbaya. Usituvishe toka kwa wawili hao vazi la balaa. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na ututeremshie manufaa ya mawingu haya na baraka zake. Na utuondolee adha yake na madhara yake. Usitufikishie maafa kutokana nao usitutumie uharibifu wowote katika maisha yetu. Oh Allah! Ikiwa umewapeleka hao kwa kisasi na umewatuma kwa makasiriko basi twakuomba kimbilio ili kuepukana na ghadhabu zako.

Tunakusihi utupe msamaha wako elemea kwa washirikina kwa ghadhabu. Tupa jiwe la ghadhabu zako kwa makafiri. Oh Allah! Ondoa ukame wa nchi yetu kwa maji yako. Ondoa ukorofi wa vifua vyetu kwa riziki yako. Usituzuie kwako kwa kutushughulisha na kingine mbali na wewe. Usitukatie sote sisi vitu vya wema wako, kwa kuwa tajiri ni yule uliyemtajirisha aliyesalimika ni yule uliyemlinda. Hakuna yeyote mwenye ulinzi bila ya wewe. Hapana yeyote awezaye kuzuia adhabu yako. Waamua utakalo kwa umtakaye. Wapitisha utakalo kwa umtakaye. Sifa njema ni zako kutulinda na balaa. shukrani ni zako kwa kutupa neema. Sifa njema zitakazo ziwacha nyuma sifa njema za wenye kusifu kwa sifa njema. Sifa njema zitakazojaa ardhi yake na mbingu yake. Hakika wewe mwenye huruma nyingi mpaji wa neema nyingi. Mpokeaji wa sifa kidogo mwenye kushukuru ihisani ndogo matenda mema mtenda mzuri mfadhili. Hapana muabudiwa ila wewe. Na kwako ndio Marejeo.

7

AL-SAHIFATU AL-KAAMILATU AL-SAJJAADIYYATU

DUA YA 37

DU'A ZAKE(A.S) ANAPOTAMBUWA KUSHINDWA KUTEKELEZA SHUKRANI IPASAVYO

Oh Allah! Hakika hakuna awezaye kufikia upeo wa kukushukuru isipokuwa atakuwa amepata hisani yako ambayo pia itamlazimu akushukuru. Wala hafikii kiwango cha kutosha katika kukutii japo afanye juhudi atakuwa chini ya haki yako kwa sababu ya uwingi wa fadhila zako. Kwa hiyo, mwenye shukrani zaidi miongoni mwa waja wako ashindwa kukushukuru ipasavyo. Na mcha mungu mno miongoni mwao yuko chini ya kiwango cha kukutii. Si wajibu kwa yeyote umsamehe kwa kuwa yu astahiki kusamehewa. Wala hana haki ya kuwa umridhiye kwa kustahiki umghofiriyae ni kwa sababu ya huruma zako. Na umridhiaye ni kwa sababu ya ukarimu wako. Waridhika na shukrani ndogo ulioshukuriwa. Walipa kiasi kikubwa kwa kadiri ndogo uliyotiiwa. Hata yaonekana kana kwamba. Shukurani ya waja wako ambayo umewajibisha malipo yao kwa ajili yake. Na umekithirisha malipo yao kwa sababu yake ni jambo wanamiliki uwezo wa kujizuia bila ya wewe na utawalipa na wala haikuwa sababu yake mkononi mwako ndio ukawalipa! Ukweli ni kuwa umemiliki Ewe Mola wangu! Mambo yao kabla ya waja wako hawajamiliki ibada yako. Uliandaa malipo mema kwa ajili yao kabla hawajaanza kukutii wewe. Hiyo ni kwa sababu sunnah yako ni kufadhili. Na tabia yako ni kufanya ihsani na njia yako ni kusamehe. Kwani kila kiumbe cha tambuwa kuwa wewe si dhalimu kwa uliyemwadhibu. Na chashuhudia kuwa unafanya ukarimu kwa uliyemsamehe, kila mmoja anakiri nafsini mwake kuwa hafanyi uliyowajibisha juu yake ipasavyo.

Lau si kama shetani kuwahadaa na kuwaweka mbali na utii wako asingekuasi mwenye kukuasi lau asingewaonesha batili katika mfano wa haki asingepotea njia yako mpoteaji. Hivyo basi utukufu ni wako ubainifu ulioje wa ukarimu wako katika kumtendea anayekutii au anayekuasi. Wamridhia mtii hali yakuwa wewe ndiye uliyesimama kwa ajili yake. Ulimpa muda mfanya maasi hali yakuwa ulikuwa na uwezo wa kumuharakishia adhabu yake. Kila mmoja wao umempa asilopaswa kupewa. Umempa fadhila kila mmoja wao isio lingana na kazi yake. Lau ungemlipa mtii kulingana na kiwango cha utii wake. Angekaribia kukosa malipo yao mema. Na imtoke neema yako. Lakini kwa ukarimu wako umemlipa muda mfupi uishao kwa muda mrefu wakudumu. Na badali ya upeo wa karibu wakutoweka. Kwa upeo mrefu wakubaki milele kisha hukumfanyia kisasi kwa ajili ya aliyokula miongoni mwa riziki yako inayompa nguvu ya kukutii. Wala haukumdadisi kuhusu viungo vya mwili ambavyo matumizi yake imekuwa ndio sababu ya kuufikia msamaha wako. Ungemfanyia hivyo yangekwenda yote aliyotaabikia na yote aliyoyafanyia juhuudi. Ikiwa ni malipo ya kidogo mno miongoni mwa nufaisho lako na huruma yako. Na angebakia rehani mkononi mwako kuhusiana na neema zako zingine. Basi vipi atakuwa anastahiki kupata chochote katika thawabu zako hakika ni vipi? Hii ewe Mola wangu ndio hali ya aliyekutii na aliyefanya ibada kwa ajili yako. Vipi hali ya mwenye kuasi amri yako na kutenda katazo lako!

Wala haukumuharakishia adhabu yako ili aibadilishe hali yake katika kukuasi wewe na hali ya kurejea kwenye utii wako. Alikuwa anastahiki O Mola wangu! Pale mwanzo alipokuasi kila ulilowaandalia viumbe wako wote miongoni mwa adhabu zako. Kwa hiyo yote uliyoyachelewesha miongoni mwa adhabu na umemcheleweshea kumtia adabu. Ni kuiacha haki yako na kuridhia bila ya wajibu wako. Basi E Mola wangu! Ni nani mkarimu zaidi kuliko wewe? Nani mwenye hali mbaya zaidi kuliko aliyeangamia kwa kutokukujali wewe! Hapana ni Nani? U mwenye baraka mno haiwezekani usifike isipokuwa kwa ihsani, umkarimu mno haiwezekani uogopwe isipokuwa uadilifu. Huogopwi kuwa utamdhulumu aliye kuasi. Wala haiogopwi kuwa utaghafilika kumpa malipo aliyekuridhisha msaliye Muhammad na Aali Zake na unipe matumaini yangu. Nizidishiye mwongozo wako utakaonifikisha kufanikisha amali yangu. Hakika wewe mwenye huruma mkarimu.

DUA YA 38

DUWA ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA RADHI KWA KUWATENDEA VIBAYA WAJA WA MWENYEZI MUNGU KWA KUTOWAJIBIKA IPASAVYO KUHUSU HAKI ZAO NA KUIKOMBOA SHINGO YAKE IEPUKANE NA MOTO

Oh Allah! Mimi nakuomba msamaha kutokana na mdhulumiwa alidhulumiwa mahali mimi nipo na sikumsaidia. Na kutokana na wema nimetendewa sikuwa mwenye shukurani. Na mtenda maovu aliniomba msamaha sikumsamehe. Mwenye shida aliniomba sikumpa kipaombele kuliko nafsi yangu. Na haki ya mwenye haki iliyo nilazimu ya muumini sikuitekeleza. Na aibu ya muumini ilinidhihirikia na sikumsitiri. Na kila aina ya dhambi ilijitokeza mbele yangusikuihama. Nakuomba msamaha Ewe Mola wangu kwa yote haya na kwa yafananayo na haya. Msamaha wa kujuta ambao utakuwa onyo kwa yaliyo mfano wake hapo baadaye. Msaliye Muhammad na Aali zake na jaaliya kujuta kwangu juu ya yale niliyojiingiza katika mitelezo iwe azma ya kujiepusha na yanayojitokeza mbele yangu miongoni mwa maovu. Iwe toba itakayo niwajibishia mapenzi yako. Ewe mpenzi wa wafanyao toba.

DUA YA 39

DUWA ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA MSAMAHA NA REHEMA

Oh Allah! msaliye Muhammad na Aali zake.Yavunje matamanio yangu ya kila haramu. Uondowe uchu wangu wa kila tendo la dhambi. Niziwiye kumuudhi muumini yeyote Muislamu mwanaume na mwanamke. Oh Allah! mja yeyote amenitendea baya ulilo hadharisha kwake na amekiuka kwa kunitendea ulilo mgombeza na amekufa na aliyo nidhulurnu au nimemlalamikia akiwa hai. Msamehe aliyonitendea na umuwiye radhi kwa yale aliyenitumbiya mgongo. Msimsimamishe kumtaka aliyonitendea. Usimuumbue kwa aliyoyachuma kwangu. Na jaaliya niliyosamehe kwa kuwawia radhi na niliyojitolea miongoni mwa sadaka kwao iwe sadaka safi mno miongoni mwa sadaka za watoao sadaka. Na zawadi ya hali ya juu mno miongoni mwa zawadi za watafutao ukaribu na wewe. Nifidiye msamaha wangu kwao kwa msamaha wako. Na DU'A yangu kwao nipate rehema zako ili kila mmoja wetu apate hali njema kwa fadhila zako. Na ili aokoke kila mmoja wetu kwa huruma zako. Oh Allah!

mja yeyote katika waja wako amepata kutoka kwangu ovu au aliguswa na madhara kutoka kwangu au lisilofaa limemfika kupitia kwangu au kwa sababu yangu amedhulumiwa. Nimeshindwa kuwa mwangalifu wa haki yake au nimekwenda (kufa) na haki yake iliyo dhulumiwa. Mswalie Muhammad na Aali zake mridhishe kwa ajili yangu kutaka utajiri wako. Mpe haki yake kamili kutoka kwako kisha nilinde na liwajibishalo hukumu yako kwa ajilii yake. Na niepushe na lihukumiwalo na uadilifu wako. Kwa sababu nguvu zangu haziwezi kuhimili adhabu yako. Na kwa sababu uwezo wangu hauwezi kusimama mbele ya makasiriko yako. Kwa hakika ikiwa utanilipa kulingana na haki utanihilikisha. Na kama hautonikinga na rehema zako utaniangamiza. Oh Allah ! hakika mimi nakuomba Ewe Mola wangu ambacho kukitowa kwake hakukupunguzii (chochote).

Nakuomba kubeba ambalo uzito wake haukutopei. Nakuomba uipe nafsi yangu Ewe Mola wangu! Ambayo haukuiumba ili ujikinge na uovu au iwe ndio njia ya manufaa, bali umeiumba ili kuthibitisha uwezo wako kwa nyingine iliyo mfano wake na kwa sababu iwe ni hoja dhidi ya iliyo mfano wake. Nakuomba ubebe mizigo yangu ya dhambi ambayo uzito wake umenishinda nguvu kubeba. Naomba msaada kwako kwa ajili ya ambalo uzito wake umenielemea. Msaliye Muhammad na Aali zake uipe nafsi yangu ingawa imetenda maovu. Iwakilishe Rehma yako kubeba mzigo wangu (dhambi). Wangapi miongoni mwa watenda mabaya imewafika Rehma zako! Wadhalimu wangapi msamaha wako umewajumuisha. Mswaliye Muhammad na Aali Zake. Na nifanye mimi mfano wa ulio wainuwa kwa kuwastahmilia kutoka kwenye mweleka wa wakosefu. Na umemwokowa kwa tawfeeki yako kutoka kwenye hali mbaya ya waovu. Na akawa aliyeachwa huru na msamaha wako kutoka pingu za makasiriko yako.

Na aliyeachwa huru na wema wako toka kamba za uadilifu wako. Hakika wewe ufanyapo hayo Ewe Mola wangu! wamfanyia ambaye hakanushi kustahiki kwake adhabu yako wala haji takasi nafsi yake kutoka wajibikiwa na malipizi yako. Wamfanyia hivyo Ewe Mola Wangu! Ambaye hofu yake kwako ni nyingi kuliko tamaa yake kwako. Na yule ambaye kukata tamaa kuwa hatofanikiwa ni saana kuliko matumaini yake ya kuokoka. Sio kutokuwa na matumaini kwake ni kukata tamaa au matumaini yake yawe ni kughurika (kudanganyika). Bali ni kwa sababu ya uchache wa mema yake kati ya maovu yake na udhaifu wa hoja zake katika matendo yake yote. Na wewe Ewe Mola wangu, ni mstahiki wa kuwa asi danganyike mbele yako mkweli. Wala asikatishwe tamaa na wewe muovu kwa sababu wewe ni bwana mtukufu ambaye fadhila zake hamziwii yeyote. Wala hamfuatilii yeyote haki yake. Jina lako litukuzwe zaidi ya watukuzwao, yametakasika majina yako zaidi kuliko wote watajwao. Neema zako kwa viumbe wote zimewaenea; zako ni sifa njema kwa yote hayo Ewe Bwana wa Ulimwengu wote.

DUA YA 40

MIONGONI MWA DU'A ZAKE(A.S) AKITANGAZIWA KIFO CHA MTU AU AKUMBUKAPO UMAUTI

Oh Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Tutosheleze na matumaini marefu tupunguzie nayo kwa kazi ya ukweli ili tusitumainiye kuikamilisha saa baada ya saa. Wala kuikamilisha siku baada ya siku wala kukutana pumzi na pumzi nyingine. Wala kukutana hatuwa na hatua nyingine, Tusalimishe na udanganyifu wake tupe amani na shari yake. Uweke umauti mbele yetu dhahiri usijaaliye kumbukumbu yake kwetu kuwa ni ya mara moja na kupotea utujaaliye kuwa miongoni mwa watenda mema. Ili tuone kwa ajili yake kuja kwako kuna chelewa mpaka ifikiye tuuone umauti ni jambo tunalopendezwa nalo. Na tuone umauti ni mahali tulipopazowea tuna shauku napo na mlinzi wetu tumpendaye kuwa karibu naye. Ukiuleta kwetu na kututeremshia tufanye tuwe na furaha nao kama mgeni aliyekuja kututembelea. Tuweke katika raha naye ajapo usitufanye tuwe katika mashaka ya kumpokea kwake. Usitudhalilishe katika kumpokea kwake. Wala usitutweze kwa ziara yake. Mfanye kuwa mlango miongoni mwa milango ya ghofirani zako awe ufunguo miongoni mwa funguo za Rehma zako. Tufishe katika hali ya uongofu si katika hali ya upotovu tuwe watii si wenye kukirihishwa. Wenye kutubu si katika hali ya uasi wala wenye kung'ang'ania maasi. Ewe mwenye kudhamini malipo ya watendao mema. Na mrekebishaji wa matendo ya waharibifu.

DUA YA 41

DU'A ZAKE(A.S) KATIKA KUOMBA SITARA NA ULINZI

Oh Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Nitandikiye kitanda cha heshima yako nipeleke kwenye manyweo ya maji ya rehema zako. Nikalishe kati kati ya bustani yako usinipe mtihani wa kukataliwa na wewe. Usininyime kwa kutokukutumainia. Usinifuatilie niliyoyatenda. Wala usinifuatilie nilioyafanya. Usiyadhihirishe yaliyofichika na kwangu wala usiyafichuwe yaliyositirika kwangu. Usiyaweke matendo yangu katika mizani ya uadilifu. Usizitangaze habari zangu mbele ya macho ya kundi la watu. Wafiche lile ambalo kulitangaza ni aibu kwangu. Likunje mbali nao litakaloniaibisha mbele yako. Ipe heshima daraja yangu kwa ridhaa zako. Nikamilishiye heshima yangu kwa ghofirani zako. Nipange katika watu wa mkono wa kulia, niongoze katika mapito ya walio katika amani. Nifanye niwe katika kundi la waliofaulu. Visitawishe vikao vya watu wema kwa kunitumikisha. Aameen. Ewe Bwana wa ulimwengu.

Dua ya 42

DU'A YAKE(A.S) WAKATI WA KUHITIMISHA QUR'AN

Oh Allah! Hakika wewe umenisaidia kuihitimisha Qur'ani kitabu chako ambacho umekiteremsha kikiwa nuru na umekifanya mlinzi wa kila kitabu ulichokiteremsha. Na umekiboresha juu ya kila hadithi uliyoisimulia. Na ni kitenganishi kwacho umetenganisha kati ya halali yako na haramu yako. Qur'an ambayo kwayo umeiweka wazi sheria ya hukumu yako. Kitabu umekipambanuwa kwa waja wako upambanuzi wa wazi. Ni Wahyi ulio uteremsha uteremsho kwa Nabii wako Muhammad Rehma Zako zimfikie na ziwafikiye Aali zake. Umeifanya kuwa nuru ituongoze katika giza ya upotevu na ujinga kwa kuifuata. Kiponyesho kwa mwenye kuisikiliza kwa kuifahamu na kuisadiki. Ni mizani ya kiadilifu isiyopotoka ulimi wake na kuwa mbali na haki. Nuru ya uongofu ambayo Burhani yake haiwazimikii watizamaji wake. Na alama ya uokovu ambayo hapotei mwenye kufuata mafunzo yake. Wala haitomfikia mikono ya maangamizi mwenye kujiambatanisha na kishiko chake cha ulinzi. Oh Allah! Kwa vile umetusaidia kuisoma. Na umeturahisishia ugumu wa ndimi zetu kwa uzuri wa ibara yake hivyo basi tufanye tuwe miongoni mwa wanaoichunga haki ya kuichunga na wakutumikia kwa itikadi ya kusalimu amri ya aya zake zilizothabiti waombao kimbilio kwa kuzikubali zile aya mutashabih na zile ufafanuzi wake uko bayana. Oh Allah! Hakika wewe umeiteremsha kwa Nabii wako Muhammad Rehema za mungu zimfikiye yeye na Aali zake kwa ujumla.

Na umeturithisha sisi Elimu yake tukiwa wafasiri. Na umetuboresha juu ya wasioijuwa elimu yake. Umetupa nguvu juu yake ili utunyanyuwe juu ya wasio weza Ibada. Oh Allah! kama vile umezifanya nyoyo zetu kuwa zenye kuibeba. Na kwa rehema zako umetutambulisha utukufu na ubora wake. Basi msaliye Muhammad, muhubiri wake na Aali zake wahifadhi wa Qur'ani. Utujaalie kuwa miongoni mwa wanaotambuwa kuwa yatoka kwako. Ili isituzukiye shaka katika kuisadiki. Wala upotovu usitutikise na kututowa nje ya njia yake nyofu. Ewe Allah, mswaliye Muhammad na Aali Zake. Na tujaaliye sisi kuwa miongoni mwa wanaoshikamana na kamba yako, na wakimbiliao kutoka kwenye aya mutashabihati kwenda kwenye ngome yake madhubuti na kuketi kwenye kivuli cha bawa lake, na aongokaye na mwanga wake wa asubuhi. Aongokaye na kuchomoza kwa mng'aro wake. Anamulika kwa taa yake. Wala hatafuti uongofu katika kitu kingine.

Ewe Mola! Kwa hiyo Qur'an umemweka Muhammad kuwa alama ya kukujuwa wewe. Na kupitia Ahlul-Bayt wake umeweka wazi njia za ridhaa zako. Msaliye Muhammad na Aali Zake na ifanye Qur'ani kwetu kuwa njia za kwenye daraja la utukufu. Na iwe ngazi tuipandayo kwenda mahali pa salama. Na iwe sababu tutakayolipwa uokovu kwenye uwanja wa kiyama. Na njia ambayo kwayo tutazifikia neema za nyumba ya kudumu. Ewe Allah! Msaliye Muhammad na Aali Zake. Kwa Qur'ani tupunguziye uzito wa dhana utupe sifa njema za watu wema na tufanye tufate athari za waliosimama kwa ajili yako nyakati za usiku na mwisho wa mchana. Ili ututakase na kila uchafu kwa utakaso wake. Utufanye tufate athari ya walioangaza kwa nuru yake. Wala matumaini hayakuwa zuiya kutenda kazi iliyowatenge mbali kwa vitimbi vya udanganyifu wake. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Ali Zake. Rekebisha kwa Qur'an upungufu wetu tusiwe mafakiri. Kwa Qur'ani tusukumiye maisha ya raha na wasaa wa riziki. Tuepushe kwayo na tabia mbaya na mwenendo duni. Tuhifadhi kwa Qur'ani tusiingiye ndani ya shimo la maangamizi kufuru na mwendo wa kinafiki.

Ili iwe mwongozo uelekezao kwenye maridhawa yako na bustani zako siku ya kiyama. Na iwe kwetu mlinzi hapa duniani dhidi ya makasiriko yako na kukiuka mipaka yako. Na iwe kwa yale uliyonayo kwa kuhalalisha halali yake na kuharamisha haramu yake shahidi. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake na kwa Qur'ani urahisishe umauti nafsini mwetu wakati wa kufa. Na usumbufu wa kukokotwa (Roho) Uuguaji. Na taabu ya mauguzi, na mfuatano wa kutatarika. (Ifikapo roho kooni na itasemwa: Mganga ni nani?) Atajitokeza Malaika wa umauti ili aichukue toka nyuma ya pazia ya mambo yasiyojulikana. Na kuitupa toka upinde wa umauti kwa mshale wa kuachwa peka na kuwa changanyiya sumu iuwayo kwenye kikombe chenye mwonjo wa sumu wakati msafara wa kuelekea akhera ukitusogelea. Kazi zitakuwa ukosi wa shingo makaburi yatakuwa ndio kimbilio mpaka wakati wa siku ya kukutana. Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali zake. Na utubariki wakati wa kuingia nyumba ya kuoza na makazi ya muda mrefu kati ya tabaka za udongo. Yajaaliye makaburi baada ya kuiaga dunia yawe mafikio yetu mema tupanulie mbano wa mwana ndani zetu kwa rehema zako Usitufedheheshe mbele ya walio hudhudhiria siku ya Kiyama kwa sababu ya madhambi yetu ya angamizayo. Kwa Qur'ani irehemu hali yetu duni katika kikao cha kuletwa mbele yako Kwa Qur'ani zithibitishe nyayo zetu zisiteleze wakati daraja la Jehannam litakapoyumba yumba.

Kwayo ing'arishe giza ya makaburi yetu kabla ya kufufuka. Utuokowe kwa Qur'ani na kila taabu ya siku ya Kiyama na shida za kutisha siku ya maafa. Zing'arishe nyuso zetu siku ambayo nyuso za wadhalimu zitakuwa nyeusi siku ya kuhasirika na majuto. Utujaaliye upendo ndani ya nyoyo za waumini. Usiyafanye maisha kwetu kuwa ya shida. Ewe Allah! mrehemu Muhammad mja wako na mjumbe wako kwa vile ameifikisha risala yako na alitekeleza amri yako. Aliwanasihi waja wako Ewe Allah! Mjaaliye Nabii wetu Rehema Zako ziwe juu yake, na juu ya Aali zake - Awe karibu mno na wewe siku ya kiyama miongoni mwa Manabii watakaokuwa karibu ya kikao. Na mwenye uwezo mkubwa sana kwako wakuombea. Mwenye Enzi kubwa miongoni mwao kwako. Mwenye cheo kikubwa mno mbele yako. Oh Allah! Mrehemu Muhammad na Aali wa Muhammad. Itukuze nyumba yake, Bur'hani yake itukuze, Mizani yake ipe uzito, ya kubali maombezi yake usogeze karibu wasila wake, ufanye uwe mweupe uso wake, ikamilishe nuru yake iinue daraja yake. Tufanye sisi tuishi na sunna yake, tufishe tukiwa katika mila yake, tupeleke tufikishe kwenye njia yake. Tupitishe njia yake. Tujaaliye tuwe miongoni mwa watu watii wake.

Tufufuwe katika kikundi chake tuelekeze kwenye dimbwi lake, tunyweshe kwa bilauri yake. Rehemu Muhammad na Aali zake. Rehema ambayo utamfikisha nayo kwenye ubora asio uwazia miongoni mwa kheri na fadhila zako, na heshima zako. Hakika wewe ni mwenye Rehma kubwa na fadhila tukufu. Oh! Allah mlipe kwa aliyoyafikisha katika jumbe zako. Na amefikisha aya zako, amepigana jihadi katika njia yako malipo yaliyo bora umepata kumlipa yeyote miongoni mwa Malaika wako wa karibu na Manabii wako walio Mursali wateule. Amani imfikie yeye na iwafikiye watoto wake watakatifu wema, na rehema za Mungu na baraka zake.

DUA YA 43

MIONGONI MWA DU'A ZAKE AUONAPO MWEZI MWANDAMO

Ewe Kiumbe mtii. Mwenye mwendo wa haraka usiochoka. Wenye kurudia rudia katika mafikio yalio kadiriwa. Wenye kupita katika mviringo uliopangwa. Na mwamini ambaye kwa kukutumia wewe ameangaza nuru kwenye giza na ameangaza kupitia wewe weusi na amekufanya alama katika alama za ufalme wake. Na alama miongoni mwa alama za mamlaka yake. Na amekufanya mnyenyekevu kwa kuzidi na kupunguwa. Kuchomoza na kuzama, kung'ara na kupatwa uko mtii kwake kwa yote hayo. Na kwenye utashi wake uko haraka ajabu ilioje mpango wake katika mambo yako. Werevu ulioje aliofanya katika kazi yako. Amekufanya kuwa ndio mwanzo wa mwezi mpya na hali mpya. Na mwomba Mungu Bwana wangu na Bwana wako, Muumba wangu na Muumba wako. Muweka vikomo wangu na muweka vikomo wako. Mfanya taswira wangu na mfanya tasweira wako. Amrehemu Muhammad na watoto wake. Na akufanye wewe uwe mwezi mwandamo wenye baraka isiyo futwa na kupitiwa na usiku. Na usafi usiochafuliwa na dhambi. Mwandamo wenye amani bila ya maafa na salama bila maovu. Mwandamo wenye heri bila ya ndege mbaya na ufanisi bila ya shida. Mwandamo wenye urahisi usiochanganyika na ugumu.

Na wenye heri isio changanyika na shari. Mwanadamo wa amani na imani neema na hisani. Salama na Uislamu. Ewe Mola mrehemu Muhammad na Aali zake. Na tujaalie sisi kuwa wenye kuridhika mno miongoni mwa waliochomozea nao. Na wasafi mno miongoni mwa waliouangalia. Na waliobahatika mno katika wale waliokuabudu katika huwo. Utukubalie humo toba utulinde utulinde humo na matendo yasiyofaa utuhifadhi humo tuwe hatujihusishi na kukuasi wewe. Utugawiye humo kushukuru neema zako. Na utuvalishe humo kwa sitara ya afya njema. Tukamilishiye neema zako kwa ukamilifu wa utii wako. Kwa hakika wewe mwenye huruma msifika wa sifa njema. Na Rehema za Allah zimfikiye Muhammad na Aali zake wema waliotahirika.

DUA YA 44

MIONGONI MWA DU'A ZAKE UINGIAPO MWEZI WA RAMADHANI

Utukubalie humo toba utulinde litulinde humo na matendo yasiyofaa utuhifadhi humo tuwe hatujihusishi na kukuasi wewe. Utugawiye humo kushukuru Neema zako. Na utuvalishe humo kwa sitara ya afya njema. Tukamilishiye Neemza zako kwa ukamilifu wa utii wako. Kwa hakika wewe mwenye huruma msifika wa sifa njema. Na Rehema za Allah zimfikie Muhammad na Aali zake wema waliotahirika. Sifa njema ni za Allah ambaye ametuongoza kwenye sifa zake na kutujaalia sisi kuwa wastahiki wake. Ili tuwe wenye kushukuru ihsani zake. Ili atulipe kwa hilo malipo ya watu wema. Sifa njema ni za Allah ambaye ametupendelea kwa dini yake. Na ametuhusisha na mila yake na ametuelekeza katika njia za hissani zake. Ili tuzipate kwa upaji wake tuzifikie radhi zake. Himidi ambayo ataikubali kutoka kwetu, na ataridhika nayo. Sifa njema ni za Mungu ambaye amejaalia miongoni mwa njia hizo mwezi wake.

Mwezi wa Ramadhani mwezi waswiyam mwezi wa Uislamu. Mwezi wa usafi na ni mwezi wa mchekecho. Mwezi wa kusimama kwa ajili ya Sala. Mwezi ambao Qur'ani iliteremshwa humo ili iwe mwongozo kwa watu na ni ubainifu katika mwongozo na kitenganishi. Amebainisha ubora wake kwa kulinganisha na miezi mingine. Kwa kuwa ameujaalia matakatifu mengi na mengi yaliyo bora na mashuhuri. Hivyo basi ameharamisha humo ambayo aliyoyahalalisha katika miezi mingine ili kuuadhimisha. Ameziwia humo malaji na vinywaji ili kuupa heshima. Ameujaalia wakati bainifu, haruhusu Mtukufu Mwenye Enzi utangulizwe kabla ya wakati wake. Wala hakubali ucheleweshwe. Kisha ameuboresha usiku mmoja miongoni mwa usiku wake kwa daraja ya sawa na miezi elfu moja. Na ameuita Laylatul-qadri (Malaika na Arruhu huteremka usiku huo kwa idhini ya bwana wao na kila amri). Amani yenye baraka ya kudumu mpaka kuchomoza kwa alfajiri kwa amtakaye katika waja wake kwa aliyohukumu kulingana na maamuzi yake. Ewe Allah mrehemu Muhammad na Aali zake. Tupe Ilhamu ya kutambuwa ubora wao, na kutukuza heshima yake. Na kuchunga uliyoyazuiya. Tusaidie kutekeleza funga yake kwa kuvizuia viungo vya mwili visikuasi na kuvitumia humo (mwezini) kwa yakuridhishayo.

Kwa kiasi kwamba hatusikilizi kwa masikio yetu maongezi ya ovyo. Na tusiharakie kwa macho yetu kwenye upuuzi; na kwa kiasi kwamba hatunyoshi mikono yetu kwenye ambayo yamehadharishwa. Wala tusipige hatua kwa miguu yetu kuyaelekea yaliyokatazwa. Hata tusishibishe tumbo zetu isipokuwa iliyohalalishia, ndimi zetu zisitamke isipokuwa yale yaliyo mfano. Wala tusijibebeshe isipokuwa yanayosogeza karibu na thawabu zako wala tusijishughulishe isipokuwa na yale tu yanayozuia adhabu yako. Kisha yote hayo yaepushe na riya ya wapendao kusifiwa na yaepushe na kusikika kwa wapendao umashuhuri. Tusimshirikishe (kwenye matendo hayo yote) yeyote asiyekuwa wewe. Tusitaraji kwayo mradi usiokuwa wewe. Ewe Allah! mrehemu Muhammad na Aali zake na tujaalie humo kuhudhuria nyakati za Sala tano. Kwa mipaka yake uliyoiweka na wajibu uliowajibishia na nyadhifa zake ulizoziweka na nyakati zake ulizoweka. Na katika sala tuweke weko la waliofanya sawa mahali mwake, wenye kuhifadhi nguzo zake, watekelezao kwa wakati wake. Kama alivyofanya mja wako na mjumbe wako. Rehma zako zimfikie yeye na Aali zake.

Katika rukuu na katika Sijida na fadhaili zake zote kwa ukamilifu wa Twahara na wa sawa kabisa. Na unyenyekevu uliobayana na wa uhakika. Na tupe taufiki ndani yake ili tuunganishe udugu kwa mema na kujitolea. Na kuwa pamoja na majirani wetu kwa kuwafadhili. Tuziepushe mali zetu na madai na zitakase kwa kutoa zaka. Tumwendeee aliye tuwekea upasi na tumtendee uadilifu aliye tudhulumu. Tumsalimishe mwenye kutufanyia uadui isipokuwa yule afanyiwaye uadui kwa ajili yako kwa kuwa yeye ndiye adui ambaye hatutamfanya rafiki na ni kundi ambalo hatutalitakasa na tujikurubishe kwako humo kwa amali safi ambayo kwayo utatutakasa nayo na kutuweka mbali na dhambi. Utuhifadhi humo na kuzirudia aibu ili asikuletee malaika yeyote isipokuwa machache tuyaletayo katika milango ya utii wako na aina za ukaribu kwako. Ewe Allah hakika mimi nakuomba kwa haki ya mwezi huu. Na kwa haki ya walio abudu kwa ajili yako humo toka mwanzo wake mpaka wakati wa kwisha kwake, miongoni mwa Malaika uliyemsogeza karibu au Nabii uliyemtuma au mja mwema umemchagua makhsusi. Umrehemu Muhammad na Aali zake na utuandamishiye kwa yale uliyo waahidi wapenzi wako miongoni mwa karama zako. Twajibishiye humo uliowa wajibishia watu waliokwenda mbali sana katika kukutii.

Tuweke katika daraja la walio stahiki ngazi ya juu kwa rehema zako. Ewe Allah mrehemu Muhammad na Aali zake tuepushe na kupotoka katika kukupwekesha. Na kutofanya ipasavyo katika kukutukuza. Na kuwa na shaka katika Dini yako na kutoiona njia yako na mghafala wa heshima yako. Tuepushe na kudanganywa na adui yako shetani aliyewekwa kando na rehema zako.

Ewe Allah, mrehemu Muhammad na aali zake, tuelemeapo upande katika huu mwezi tuweke sawa. Tukienda kombo humo tuweke sawa. endapo adui wako shetani atatudhibiti tuokoe. Ewe Mola ujaze kwa Ibada zetu kwako zipambe nyakati zake kwa utii wetu kwako. Tusaidie katika nyakati zake za mchana kuufunga na usiku wake. Utusaidie kutekeleza sala na kukuomba wewe na kukunyenyekea kujidhalilisha mbele yako. Ili mchana wake usiwe shahidi dhidi yetu kwa mghafala wala usiku wake kwa kuzembea. Ewe Allah tujaaliye katika miezi mingine na mchana hivyo hivyo kwa kadiri utupavyo uzima. Tufanye tuwe miongoni mwa waja wako wema (ambao watarithi Janna ya Firdausi humo watabaki milele). ( Na wale ambao wanatoa wakitoacho hali ya kuwa nyoyo zao zaogopa kuwa watarejea kwa Mola wao) na miongoni mwa ambao (wanaharakia katika mambo ya kheri nao kwayo ni wenye kushinda). Ewe Allah! Mrehemu Muhammad na Aali Zake katika kila wakati na muda wote na hali zote kwa idadi uliomrehemu. Na zaidi ya yote hayo kwa ziyada ambayo hawezi kuihesabu asiyekuwa wewe! Hakika wawe ni mtendaji wa utakalo.